Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Ujerumani Yamsifu Raid Magufuli Kwa Kupambana na Ufisadi Kwa Vitendo.....Yaahidi Kumpa Ushirikiano

$
0
0
Serikali ya Ujerumani imeeleza kufurahishwa na kasi ya kupambana na rushwa na ufisadi ya Rais John Magufuli na kuahidi kumpa ushirikiano katika masuala ya maendeleo.

Ujerumani inakuwa nchi ya kwanza ya kigeni kuvutiwa na kasi ya Rais Magufuli ambaye ameonekana kuelekeza nguvu katika si tu kupambana na maovu hayo tangu aapishwe Novemba 5, bali pia kuchochea maendeleo ya watu wenye kipato cha chini.

Aidha, Ujerumani imesema inasubiri kuona vipaumbele vya maendeleo vitakavyoainishwa na serikali ya Rais Magufuli ili iweze kuisaidia utekelezaji.

Pongezi hizo zilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani, Georg Schmidt.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara yake ya siku tano hapa nchini, Schmidt alisema katika kipindi cha mwezi mmoja tu, Dk. Magufuli ameweza kushughulikia masuala muhimu ya kijamii ikiwamo kuboresha huduma za afya na kuwashughulikia wakwepa kodi.

Kasi ya Rais Magufuli, alisema, itasaidia kuokoa fedha nyingi ambazo zitakapokusanywa zitachangia miradi mbalimbali ya maendeleo kama alivyofanya tayari kwenye afya na elimu.

Mkurugenzi huyo alisema ziara yake nchini ilikuwa na lengo la kuangalia hali ya maendeleo nchini baada ya uchaguzi, miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali yake pamoja na kukuza ushirikiano baina ya nchi mbili hizo.

Alisema ameshakutana na baadhi ya watendaji wa serikali, wabunge, wanaharakati, watendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na kuitembelea Mahakama ya Haki za Binadamu iliyopo mjini Arusha.

Alisema pia amekuja kuangalia fursa za kibiashara nchini kwa sababu wawekezaji wengi duniani huvutiwa kwenda kuwekeza kwenye mataifa mbalimbali iwapo nchi hiyo ina usalama wa kutosha.

Akizungumzia suala la Zanzibar, Schmidt aliwataka wananchi kuwa na subira wakati mazungumzo yakiendelea katika jitihada za kutatua mgogoro huo.

“Mazungumzo yanaendelea ya usuluhishi tunasisitiza utulivu, amani na tuna imani mwafaka mzuri utafikiwa,” alisema.
Alisema kwa sasa serikali ya Ujerumani itazielekeza fedha nyingi kwa serikali ya Tanzania ili kushughulikia wakimbizi kutoka Burundi wanaokimbia machafuko.

“Tuna jukumu na wajibu wa kushughulikia mgogoro wa Burundi na fedha zilizokuwa zinakwenda Burundi sasa zitaelekezwa Tanzania kwa kuwa wanapokea wakimbizi wengi zaidi,” alisema Schmidt.

Diamond Platnumz na Mama yake Wakaa Kikao Kizito..Kisa Zari

$
0
0
Supastaa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na mama’ke mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’ wamelazimika kukaa kikao kizito ili kupata muafaka wa mzazi mwenzake na staa huyo, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kurejea Bongo na kuishi katika nyumba moja na mkwewe huyo ambaye walipishana kauli hivi karibuni.

Hivi karibuni, Zari aliyekuwa akiishi na mama Diamond nyumbani kwake, Tegeta-Madale jijini Dar, walipishana kauli na mzazi huyo sambamba na ndugu zake hadi kufikia hatua mrembo huyo aliyezaa mtoto mmoja na Diamond (Tiffah) kurejea nyumbani kwake Afrika Kusini kupisha kile alichokiita ni ‘uswahili’.

Chanzo makini kimeeleza kuwa, baada ya kuona Diamond anampenda Zari na mapenzi yao ni motomoto, familia haikuwa na jinsi zaidi ya kukaa kikao kulijadili kwa kirefu suala hilo na kupata muafaka ambapo habari njema ni kwamba, mama Tiffah anatarajia kutua Bongo siku chache zijazo.
“Diamond si unajua ndiyo kichwa katika familia. Amewaita ndugu akawaeleza dhamira na mikakati yake na Zari hivyo wamekubaliana arejee Bongo,” kilisema chanzo hicho.
Alipoulizwa Diamond kuhusiana na suala hilo, hakutaka kufunguka kwa undani akidai ni mambo ya kifamilia.

“Kila kitu kipo sawa. Zari ataibuka na maisha yataendelea kama kawaida, haya mambo ya kifamilia bwana,” alisema Diamond.

Kabla ya kufikia muafaka huo, Zari aliripotiwa kuwa anakuja nchini Desemba 8, mwaka huu wakati mama Diamond akionekana kupinga lakini hatimaye muafaka umepatikana.

GPL

Haki Elimu Wamwanika Jakaya Kikwete..Wadai Katika Awamu Yake Elimu iliporomoka Kuliko Wakati Mwingine Wowote Katika Histolia ya Tanzania

$
0
0
TAASISI isiyo ya kiserikali ya HakiElimu leo imezindua ripoti iliyobainisha madudu yaliyofanywa katika utawala wa Awamu ya Nne chini ya Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete.

Ndani ya ripoti hiyo iliyobeba miaka 10 ya utawala wa Rais Kikwete sekta ya elimu, imeeleza kuwa katika uongozi wake, ubora wa kiwango cha elimu uliporomoka kuliko wakati mwingine wowote katika histolia ya Tanzania.

Katika ripoti hiyo ambayo iliandaliwa na jopo la wataalamu na wadau wa elimu mbalimbali ambao walifanya katika mwezi Julai na Agosti mwaka huu, pia imebaini utekelezaji hafifu wa ahadi zake alizokuwa akizitoa kwenye sera zake kuhusu uboreshaji wa sekta ya elimu.

Akichambua ripoti hiyo baada ya kuzinduliwa na Mwenyekiti wa Bodi HakiElimu, Martha Qorro, Mhadhili wa Chuo Kikuu Dar es Salaam Prof. Kitila Mkumbo amesema, katika utafiti huo pia walibaini kuwa, Rais Kikwete hakuongeza vitu vipya katika uongozi wake kuhusu sekta ya elimu bali aliendeleza yale aliyoachwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.

“Hakuwa na falsafa mpya katika sekta ya elimu bali alichokuwa anafanya ni kuyabeba kila anayoyapata kama yalivyo na kuanza kufanyia kazi.

“Mfano; alisema ataanzisha shule za kimataifa nchini lakini hizo hizo alizoziongeza ndio zipo hoi, hadi sasa shule zenye viwango vinavyokubalika nchini ni asilimia nne tu,” amesema Mkumbo.

Mkumbo amesema, alichofanikiwa Rais Kikwete katika uongozi wake ni kupanua fursa za elimu ambapo aliweza kuongeza miundombinu kwa kuongeza madarasa, matundu ya vyoo, kuongeza idadi ya walimu, vitabu, udahili, uwiano kati ya wasichana na wavulana wanaojiunga na shule ya msingi na sekondari lakini sio katika suala la ubora wa elimu.

“Mathalani, shule za msingi zimeongezeka kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 16,538 mwaka 2015 huku wanafunzi wa shule za msingi wakiongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,202,892, shule za sekondari zimeongezeka kutoka 1,745 mwaka 2005 hadi 4,753 mwaka 2015 huku idadi ya wanafunzi shule za sekondari zikiongezeka 524,325 mwaka 2001 hadi 1,804,056 mwaka 2015.

“Vyuo vya ufundi pia vimeongezeka kutoka 184 mwaka 2005 hadi 744 mwaka 2015 huku idadi ya wanafunzi katika vyuo ikiongezeka kutoka 40,059 hadi 145,511 mwaka 2015. Licha ya wanafunzi kuonekana kuwa wengi shuleni na vyuoni, tafiti mbalimbali zilizofanyika zinaonesha wanafunzi wengi hawajui kusoma wala kuandika,” amesema Mkumbo.

Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, John Kalage akisoma mapendekezo yaliyopo kwenye ripoti hiyo amesema kuwa, serikali iliyopo madarakani hivi sasa inatakiwa kuchukua maoni yaliyopendekezwa kwenye ripoti hiyo na kuyafanyia kazi ili kuboresha sekta ya elimu nchini.

Akitaja baadhi ya mapendekezo yaliyomo katika ripoti hiyo Kalage amesema, serikali ya Awamu ya Tano inatakiwa iwatazeme walimu kwa jicho lingine.

Ili elimu iwe bora lazima walimu pia wawe bora na sio bora walimu hivyo iunde bodi ya kuwachunguza walimu labla ya kuanza kazi kama ilivyo kwa madaktari baada ya kumaliza masomo.

Amesema mapendekezo mengine ni kuwajali walimu ili wapate moyo wa kufanya kazi hiyo kwa kuwajengea nyumba kwani ni asilimia 22 tu ya walimu ndio wamepewa nyumba na kuboresha mioundombinu katika mazingira wanayoishi. Kuboresha madarasa, vifaa vya kufundishia, ukaguzi kwa walimu na mazingira ya shule yaimarishwe.

“Ni kazi ya Rais John Magufuli sasa kuiboresha sekta ya elimu kwani hiyo ndio sekta muhimu na kubwa kuliko zote na ndiyo yenye bajeti kubwa kuliko zote lakini utendaji wake ni ziro sasa hiyo bajeti inaendaga wapi?

“Walimu mishahara haiboreshwi, wanafunzi wengi hawajui kusoma wanamaliza shule kichwani hakuna kitu,” amesema Kalage.

Watorosha Makontena Bandarini Bila Kulipia Ushuru Hawa Hapa...Majina Yatajwa

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) imetaja majina ya kampuni 43 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa na kufichuliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita.
Aidha, TRA imesema imesimamisha kazi watumishi wake 35 wanaofanya kazi katika ngazi mbalimbali, wakiwemo 27 waliokamatwa wiki hii katika Geti Namba Tano.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.
Alisema mbali na hilo walitakiwa kuwatambua wamiliki wa makontena hayo, bidhaa zilizokuwemo, kuwalipisha wahusika kodi iliyokwepwa pamoja na kuwachukulia hatua watumishi waliohusika na upotevu huo.
Dk. Mpango aliyataja makampuni hayo kuwa ni Lotai Steel Tanzania Ltd iliyokuwa na makontena 100, Tuff Tryes Centre Company 58, Binslum Tyres Company Ltd 33, Tifo Global Mart Company Limited 30, Ips Roofing Company Limited 20, Rushywheel Tyre Centre Co Ltd 12 na Kiungani Trading Co Ltd 10.

Makampuni mengine yaliyotajwa ni Homing International Limited (9), Red East Building Materials Company Ltd (7), Tybat Trading Co Limited (5), Zing Ent Ltd (4), Juma Kassem Abdul (3), Salum Link Tyres (3), Ally Masoud Dama (2), Cla Tokyo Limited (2), Farid Abdullah Salem (2), Salum Continental Co (2), Zuleha Abbas Ali (2) na Snow Leopard Building (2).
Wamiliki wengine wa makampuni ambayo yalikuwa na kontena moja moja ni Abdulaziz Mohamed Ally, Ahmed Saleh Tawred, Ali Amer, Ally Awes Alhamdany, Awadhi Salim Saleh, Fahed Abdallah Said, Hani Said, Hassan Husrin Suleyman, Humud Suleiman Humud, Kamil Hussein Ali na Libas Fashion.
Wengine ni Nassir Salehe Mazrui, Ngiloi Ulomi Enterprises Co Ltd, Omar Hussein Badawy, Said Ahmad Hamdan, Said Ahmed Said, Salumu Peculier Tyres, Sapato N. Kyando, Simbo Yonah Kimaro, Strauss International Co. Ltd na Swaleh Mohamed Swaleh.
Alisema kwa ujumla, makampuni hayo yalipitisha makontena 329 ambayo yaliondolewa kinyume cha taratibu kutoka ICD ya Azam inayomilikiwa na Said Salim Bakhresa And Company Limited.

Dk. Mpango alisema bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.

27 WALIOKAMATWA
Aidha, Dk. Mpango alisema watumishi 35 wa Mamlaka hiyo wanaofanya kazi katika vitengo mbalimbali wamesimamishwa kazi, wakiwemo 27 waliokamatwa wiki hii katika geti namba tano.
Alisema watumishi hao wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano huku akisisitiza kuwa mtumishi yoyote wa TRA atakayebainika kuhusika katika hujuma hiyo atachukuliwa hatua kali za kinidhamu kwa mujibu wa sheria na kanuni za kazi kulingana na makosa atakayokutwa nayo.
Alisema TRA inaendelea kupanga safu ya watumishi wake ili kuthibiti upotevu wa malipo ya kodi na kwamba wanapitia upya taratibu za utoaji leseni kwa Bandari Kavu ili kuondoa mianya na kuweka udhibiti katika uondoshaji wa mizigo katika bandari zote na bohari za forodha.

“Pamoja na hatua hizi, TRA inafuatilia kwa kina ili kubaini mawakala wote wa forodha walioshiriki katika upotevu wa makontena hayo na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafungia leseni pamoja na adhabu zingine kwa mujibu wa sheria,” alisema Dk. Mpango
Mwishoni mwa wiki iliyopita serikali ya awamu tano chini ya Rais John Magufuli ilibaini ukwepaji wa kodi kwa kutorosha makontena 329 ambayo yamenyima serikali kodi ya Sh. bilioni 80.
Rais Magufuli alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade huku Jeshi la Polisi likiwashikilia maofisa kadhaa waandamizi wa Mamlaka hiyo akiwemo Kamishina wa Forodha, Tiagi Masamaki.
Masamaki na wengine saba walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu jana.


NIPASHE

Kigogo wa Bandari Afariki Kwa Presha...Undani wa Kifo chake Waelezwa Hapa

$
0
0
WAKATI Rais John Magufuli akiwa kwenye zoezi la kutumbua majipu kwenye Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), mshtuko mkubwa umetokea kufuatia kigogo mwenye wadhifa wa Artsan One (TPA) jijini Dar, Elia Eliampenda Kimaro (51) kufariki dunia ghafla kwa shinikizo la damu (presha) akiwa nyumbani kwake, Mikwambe, Kigamboni, Dar.

Kimaro alifariki dunia Novemba 30, mwaka huu kwa uthibitisho wa daktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako marehemu alikimbizwa kwa ajili ya matibabu.

Kifo cha Kimaro kimetokea wakati kukiwa na sintofahamu kubwa miongoni mwa wafanyakazi wa mamlaka hiyo kuhusiana na utolewaji wa makontena 349 kinyemela na kuisababishia serikali kukosa mapato ya kiasi cha shilingi bilioni 80.

Taarifa kutoka ndani ya familia, marehemu alisumbuliwa na maradhi hayo kwa muda mrefu. Lakini ghafla alfajiri ya Novemba 30, hali yake ilibadilika na hivyo kukimbizwa Muhimbili ambako daktari alisema alishafariki dunia.

Mwandishi aliweza kufika msibani ambapo aliwashuhudia wafanyakazi wengi wa bandarini na TRA bandarini wakiwa hapo kwa ajili ya maandalizi ya mazishi.

Baadhi ya wafanyakazi hao, walisikika wakidai, marehemu alikuwa miongoni mwa vigogo waliokuwa wakichunguzwa kwa utolewaji wa makontena 349 siku chache zilizopita.

“Pia nasikia baada ya waziri mkuu (Kassim Majaliwa) kutoa mwongozo siku zile bandarini, watu wa usalama wa taifa walishamfuata hapa kwake mara kadhaa na kumhoji.

"Lakini pia, kuna madai kwamba, miamala yake ya kibenki nayo ilifuatiliwa na jamaa hao ambapo walikuta pesa nyingi,” alisikika akisema mmoja wa wafanyakazi hao ambaye alipogundua kuna waandishi wa habar alifunga kinywa.

Nao baadhi ya waendesha bodaboda wa eneo hilo, walionekana kushangazwa sana kufuatia taarifa za kifo cha kigogo huyo, wakidai siku moja kabla, walionana naye akiwa mzima wa afya.

Hata hivyo, walisema mara baada ya taarifa za kifo, walishangaa kuona magari yake ya kifahari yakiondolewa kutoka nyumbani kwake hapo:

“Labda waliyapeleka mahali ili kupata nafasi ya kuweka maturubai ya msiba. Si unajua majumba haya ya ghorofa, yana nafasi zaidi ya kwenda juu kuliko upana,” alisema mmoja wa bodaboda hao.

Mwendesha bodaboda mmoja alisema: “Mzee wa bandari alikuwa mtu poa sana. Hata madereva wa daladala zake wameumia. Unajua jamaa alikuwa na mkwanja wa maana. Hii nyumba ya hapa ‘cha mtoto’, ana nyumba nyingine Yombo (Dar), magari ndiyo usiseme. Yaani tumempoteza mtu muhimu sana.”

Marehemu Kimaro alizikwa Desemba 2, mwaka huu kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar. Ameacha mke na watoto wanne.

Credit: GPL

Nafasi za Ajira

Afisa TPA: Vigogo Walitumia "Vimemo" Kupitisha Makontena yao ya Ndugu zao na ya Wapendwa Wao

$
0
0

Afisa mmoja wa TPA amesema vigogo na watu wakubwa wenye ushawishi serikalini walitumia kampuni za mifukoni na vimemo kupitisha makontena yao bandarini.

Afisa huyo amesema vigogo hao walikuwa wakituma vimemo kwa wakubwa wa bandari na kuagiza kupitishwa kwa makontena yao, ya ndugu zao na ya wapendwa wao.

Ofisa huyo wa TPA aliongeza kuwa kutokana na nyadhifa za wakubwa hao,ilikuwa uamue ama upitishe ubaki kazini na uneemeke au ukatae kupitisha makontena hayo alafu upoteze kazi.

Orodha ya majina ya vigogo hao imekabidhiwa kwa waziri mkuu.

Hiki ndio kitakuwa moja ya kipimo cha Magufuli katika kupambana na mafisadi.

Hatutaraji watuhumiwa hawa kupewa msamaha kama alivyofanya kwa wakwepa kodi wakubwa.

UKAWA fuatilieni sakata hili na ikibidi majina ya vigogo hao muyaweke hadharani.

Nafasi za Ajira

Taarifa Sahihi Kuhusu Hotel ya Serena Kufungwa Kwa Amri ya Serikali Kwa Kosa la Kukwepa Kulipa Kodi

$
0
0
Serena Hotel
HOTELI ya kimataifa ya Serena jana ilikumbwa na msukosuko wa kuandamwa na waandishi wa habari baada ya kusambaa kwa tetesi kuwa imefungwa kwa amri ya serikali kwa kosa la kukwepa kulipa kodi.


Tetesi hizo zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii jana asubuhi, zikieleza kuwa maofisa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) wameifunga hoteli kufunga kwa kukwepa kuliko kodi serikalini.



Mbali ya kusambazwa kwa uvumi huo, zilitumwa pia picha zilizokuwa zikionyesha sehemu ya hoteli hiyo ikiwa imezungushwa uzio uliokuwa na rangi nyeupe na nyekundu ambao ni alama inayotumika kuonyesha kusitisha kwa huduma katika eneo hilo.



Tetesi hizo zilikwenda mbali zaidi kwa kueleza kuwa uongozi wa hoteli hiyo ulikuwa mbioni kubadilisha jina kwa lengo la kukwepa kulipa kodi.



Hata hivyo, mwandishi wetu baada ya kufika hotelini hapo kwa lengo la kufuatilia ukweli wa tetesi hizo alikuta shughuli za ukarabati wa sehemu ya kupokea wageni zikiendelea, huku wageni wakielekezwa kutumia mlango wa dharura ambako kumetengezwa sehemu ya muda ya kupokelea wageni.



Uongozi wa Hoteli ya Serena kupitia Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko, Seraphine Lusala, ulilazimika kutoa taarifa kwa vyombo vya habari ukikanusha kufungwa kwa hoteli hiyo na kusisitiza kuwa kinachoendelea hotelini hapo ni matengenezo.



“Si kweli kama hoteli imefungwa, tunafanya matengenezo na yalikuwa yafanyike tangu miaka mitatu iliyopita, kilichofanyika sasa ni kubadilisha eneo la mapokezi yaliyohamishiwa milango mingine na tumeanza na eneo hilo pamoja na sehemu ya mazoezi,” alisema Lusala.



Alisema matengenezo hayo yanalenga kuifanya hoteli hiyo kuwa ya kiwango cha juu zaidi na yatachukua miezi  10.



Lusala alisema awamu ya kwanza ya matengenezo itachukua miezi minne na miezi minne ijayo itahusu matengenezo sehemu ya vinywaji, chakula, eneo la uwanja na baadaye maeneo mengine ya wazi.


Nafasi za Kazi

Woman Forgets To Wear Skirt, Causes Chaos In SA

$
0
0
A young woman wearing only a white shirt and panties was seen at a taxi park in northern KwaZulu-Natal, South Africa.

According to SA's Daily Sun, the incident happened at Nquthu Taxi Rank on Tuesday evening.

Commuters, taxi men and passersby looked on in shock when the woman appeared. When she realised that people were staring, making catcalls, taking photos and laughing, she jumped into a taxi, took out a skirt from one of her bags and put on.

An eyewitness, Bongani Zondi said people first thought she was mentally unstable but later realised she was not.

"She looked fine. But it was the first time a thing like this has happened at our taxi rank. That's why people got excited and took pictures," Bongani said.

He added that the police were called to ease the situation and they took the woman away.

Chairman for Nguthu Taxi Association, Mthandeni Ndlovu who confirmed the incident said they were surprised to see a half-naked woman at their park.

"We know it is summer and people are allowed to wear anything that makes them feel cool. But in Nquthu, we are not familiar with half-naked people, because we are a rural area. Seeing that woman shocked us"


Death Has Forgotten Me, Now I Have Lost All Hope to Die....179-Year-Old Man Cries Out (Pictured)

$
0
0
An Indian man who claims to be born in 1835 is not only the oldest man in the world, but also the man who has lived the longest since the history of mankind (according to the Guinness World Records).

According to the information transmitted, Mahashta Mûrasi was born in Bangalore on January 6, 1835.

In 1903, he lived in Varanasi, where he worked until 1957, until his retirement at the already venerable age of 122.

According to WorldNewsDailyReport, all official documents to identify this man support his version.

"I have been alive for so long, that my great grand-children have been dead for years," says Mr Mûrasi. "In a way, death has forgotten me. And now I have lost all hope to die!"

Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Awaagiza Wakurugenzi Kuwaondoa Ombaomba Waliko Barabara za Jiji

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za jiji la Dar es Salaam, kuwaondoa ombaomba wote walioko katika barabara za jiji, kwani wanachangia uchafu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Sadiki alisema utekelezaji wa kauli ya Rais John Magufuli ya kutumia siku ya Desemba 9 mwaka huu kufanya usafi, utakwenda sambamba na kuwaondoa ombaomba hao, ambao wanachangia kuongeza uchafu.

“Siwezi kusema wao ni uchafu lakini mazingira yanayowazunguka katika maeneo wanayofanyia shughuli zao wanayachafua, wanajisaidia kwenye mifuko na kutupa ovyo,” alisema.

Alisema viongozi ambao wako katika maeneo ambayo ombaomba hao wanarudi, wahakikishe hawarudi mjini kwa sababu imekuwa ni tabia ya omba omba hao wanaporudishwa baada ya muda kurudi tena jijini.

Aidha, aliiagiza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kushirikiana na Jeshi la Polisi kuwaondoa wapigadebe katika vituo vya daladala kwani wamekuwa kero kwa abiria.

Nafasi za Kazi 
Bonyeza www.ajirayako.com

Rais Magufuli Amkalia Kooni Kigogo Aliyetaka Kuchukua Ufukwe wa Coco Beach na Kuwekeza...Amsema Kimafumbo

$
0
0
Akitumia lugha ya mafumbo na moja kwa moja alisema hata ukiwa na fedha hata ukiwa na uwezo wa kufoji documents jua serikali ipo tena ya Magufuli. 

Akauliza hivi wakazi milioni nne wa DSM wakiamua kuvamia na kutwaa eneo lao utaenda wapi? Kwanini msitafute maeneo sehemu nyingine na si hili la wanyonge wanapopumzikia? 


Nafasi za Kazi 
Bonyeza www.ajirayako.com

Siku 30 za Kuwa Madarakani Kama Rais , Magufuli Aokoa Sh1trilioni

$
0
0
 Rais John Magufuli leo ametimiza mwezi mmoja tangu alipoapishwa kushika wadhifa huo huku akiweka rekodi ya kuokoa kiasi cha Sh997.4 bilioni (karibu Sh 1trilioni) ambazo zilikuwa zitumike kwa matumuzi yasiyo ya lazima, na ukwepaji kodi.

Sh997.4 bilioni zilizookolewa zitaweza kutumika kununua magari ya wagonjwa, kujenga zahanati, kujenga barabara za lami, kununua madawati, kujenga vyumba vya madarasa, kuchimba visima, kununua mashine za uchunguzi wa magonjwa, magari ya wanafunzi, pikipiki kwa maofisa kilimo, mikopo ya elimu ya juu au kujenga viwanja vya michezo kadri Serikali itakavyoelekeza.

Dk Magufuli aliapishwa Novemba 5 katika hafla iliyofana na alianza kazi ya kutafuta na kuziba mianya ya upotevu wa fedha Novemba 6 alipotembelea Hazina. Katika mazungumzo ya watendaji wa wizara hiyo Rais Magufuli alipiga marufuku safari zote za nje na kwamba zitakuwa zinaruhusiwa kwa kibali maalumu.

Novemba 7 alitembelea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambako aliagiza mashine za MRI na CT-Scan zitengenezwe na aliagiza Sh3 bilioni zitolewe kugharimia matengenezo kati ya Sh7 bilioni zilizokuwa zinahitajika.

Novemba 19, Dk Magufuli aliwasilisha bungeni jina la Kassim Majaliwa, mbunge wa Ruangwa kwamba ndiye alimpendekeza kuwa Waziri Mkuu. Baada ya jina kupitishwa na Bunge, Novemba 20 Kassim Majaliwa aliapishwa.

Jioni alilihutubia Bunge akionyesha mwelekeo wa Serikali yake ya awamu ya tano. Katika hotuba hiyo iliyowasisimua wabunge na hata wananchi waliosikiliza kupitia televisheni na redio, Dk Magufuli aliahidi kupambana na mafisadi, kubana matumizi, kuhimiza utendaji kazi, kuinua uchumi na kulinda amani na utulivu.

Baada ya hapo Magufuli na Waziri Mkuu, Majaliwa wamekuwa wakitembelea maeneo muhimu kwa uchumi wa nchi kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bandari na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL)

Utendaji huo wa Serikali wa Magufuli ndani ya mwezi moja na kipindi kabla hajaunda baraza la mawaziri, umetazamwa na jamii kuwa ni mbinu ya kusafisha nchi na kutengeneza mazira safi ili mawaziri watakaoteuliwa wafuate kasi hiyo.

Fedha zilizookolewa

Kwa kuzingatia ripoti ya matumizi ya fedha za safari zilizolipwa kama nauli na posho kwa kipindi cha kati ya mwaka 2013 na 2015 kiasi hicho ni pamoja na Sh356.3 ambazo zingeweza kutumika kwa safari hizo. Dk Magufuli aliagiza kwamba baadhi ya shughuli zitafanywa na mabalozi wa Tanzania walioko nje.

Novemba 19 alipozindua Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano mjini Dodoma, Dk Magufuli aliagiza Sh225 milioni zilizokuwa zimekusanywa kwa ajili ya hafla ya wabunge, zipelekwe kununua vitanda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. Fedha hizo zilinunua vitanda 300, magodoro 300, mablanketi 1675, na viti vya magurudumu 30.

Pia, katika hotuba yake bungeni, Dk Magufuli alirejea uamuzi wake wa kufuta safari za nje kwa watendaji wa Serikali na kueleza safari hizo zimeigharimu Serikali Sh356.3bilioni ambazo zingeweza kujenga barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 400.

Novemba 23, Dk Magufuli alitangaza kufutwa kwa maadhimisho ya Siku ya Uhuru Desemba 9 na akaagiza Sh4 bilioni ambazo zingetumika zitumike kufanya upanuzi wa barabara ya Morocco kwenda Mwenge. Kazi hiyo imeanza.

Novemba 25, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alitangaza kufutwa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani na akaelekeza kwamba fedha zilizopangwa kwa ajili ya sherehe hizo zitumike kununua dawa za kufubaza makali ya ukimwi (ARVs).

Novemba 27, Waziri Mkuu Majaliwa alitembelea bandarini na kubaini makontena 349 ambayo yalitolewa bandarini bila kulipiwa ushuru na kuifanya Serikali kukosa mapato ya Sh80 bilioni.

Tayari wenye makontena hayo wameanza kulipia na jana  TRA ilitangaza kukusanya Sh6.3 bilioni kati ya hizo Sh80 bilioni. Katika ziara yake nyingine ya kushtukiza Desemba 3 Majaliwa alibaini makontena 2,431 yalitolewa bila kulipiwa kodi. Ikiwa makontena hayo yangelipiwa kodi viwango sawa na yale 349 Serikali ingepata Sh557.2 bilioni.

Desemba 3, Dk Magufuli alifanya mazungumzo na jumuiya ya wafanyabiashara nchini na akawataka wote ambao waliondoa mizigo yao bandarini bila kulipa kodi, wajitahidi kulipa katika kipindi cha siku saba kuanzia juzi vinginevyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Makontena ni shida

Desemba 1, makontena mengine tisa yalikamatwa na TRA eneo la Mbezi, Tangibovu yakiwa yametoroshwa bila kulipuiwa ushuru wa Sh58 milioni. Jumla ya Sh637.2 zimeokolewa kutokana na mkakati wa kukusanya fedha kutoka kwenye makontena 2,431 pamoja na 349 na hayo tisa.

Matumizi ya Sh 997.4 bilioni

Kwa muda mrefu, Serikali imekuwa ikikwama kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kutokana na kukosa fedha. Dk Magufuli alikiri juzi kuwa hakuna fedha za maendeleo zilizokuwa zimetolewa kwa wizara zote katika mwaka huu wa fedha wa 2015/16, lakini baada ya miezi sita juzi ndiyo zimetolewa Sh120 bilioni.

Dk Magufuli hakusema Serikali imepata wapi fedha hizo, lakini huenda ni sehemu ya fedha ambazo ameokoa katika kipindi cha mwezi mmoja.

Kama fedha hizo zingeelekewa katika ujenzi wa barabara, na kwa kuzingatia kilomita moja inajengwa kwa Sh1 bilioni, fedha hizo zitaweza kujenga karibu au zaidi ya kilomita 1,000, ambao ni umbali kutoka Dar es Salaam hadi Kigoma au Dar es Salaam mpaka Tunduma.

Aidha, Sh997.4 bilioni zingeweza kununua magari 3,325 ya kubebea wagonjwa kwa gharama ya Sh300 milioni kwa kila moja na kuwezesha kila mkoa kupata magari 133 ya aina hiyo.

Pia, zahanati moja yenye vifaa vyote muhimu ujenzi wake unagharimu kati ya Sh600 milioni na Sh700 milioni. Hivyo, fedha hizo zingeweza kujenga zahanati 1,425 yaani kila mkoa ungepata zahanati 57.

Vilevile, wakati maelfu ya wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari wanasoma kwa kukaa chini kutokana na kukosa madawati, Sh997.4 bilioni zitaweza kutengeneza madawati yenye miguu ya chuma 33,249,142 kwa gharama ya Sh30,000 kwa kila moja na kuwezesha kila mkoa kupata madawati 1,329,966.

Pengine, fedha hizo zinaweza kujenga vyumba vya madarasa 132,996 kwa bei ya Sh7.5 milioni kwa darasa moja, hatua ambayo itawezesha kujengwa kwa vyumba vya madarasa 5,319 kila mkoa nchini.

Kipimo maarufu cha CT-Scan ambacho ufanyaji wake wa kazi unasuasa Muhimbili kwa muda mrefu, kinauzwa kwa wastani wa Sh900 milioni, hivyo, Sh997.4 bilioni zitaweza kununua mashine 1,108 ambazo zingesambazwa na kila mkoa ukapata mashine 44.

Gharama za kuchimba kisima kifupi ni kati Sh1 milioni na Sh3 milioni kulingana na jiografia ya eneo husika, hivyo Sh997.4 bilioni zitaweza kuchimba visima 332,491; kila mkoa ukapata visima 13,299.

Pia, kwa kuwa Serikali inahimiza uboreshaji wa sekta ya kilimo, Sh997.4 bilioni zitaweza kununua pikipiki 332,491 na kugawiwa kwa maofisa kilimo kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa kilimo vijijini na kila mkoa ungepata pikipiki 13,299.

Kama fedha hizo zitaelekezwa kwenye mikopo ya elimu ya juu, zitaweza kugharamia wanafunzi 249,368 wa mwaka wa kwanza kwa asilimia 100 kwa wastani wa Sh4 milioni kwa kila moja kwa ajili ya chakula, malazi na ada.

Imeandikwa na Fidelis Butahe, Joyce Mmasi na Peter Saramba

Wabunge: Magufuli Futa Wakuu wa Wilaya na Mikoa

$
0
0
BAADHI ya wabunge kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM)  kutoka mkoa wa Dodoma wamemshauri Rais John Magufuli kuondoa nafasi za Ukuu wa Mikoa na Wilaya na badala yake kazi hizo zifanywe na Makatibu tawala wa mikoa na Wakurugenzi wa halmashauri husika. 

Wakizungumza  kwa masharti ya kutokutaka kutajwa majina wabunge hao walisema hakuna sababu yoyote ya kuwepo kwa Mkuu wa Mkoa wala Mkuu wa wilaya kwani hawana kazi na badala yake ni kuiogezea mzigo serikali.
Mmoja wa wabunge kutoka kati ya majimbo ya Nyanda za juu kusini,alisema ili kudhiilisha kuwa wakuu wa mikoa na wilaya hawana kazi ni hivi tu ambavyo wanaonekana kukurupika kwa kuwawajibisha watumishi waliopo chini yao.

“Inasikitisha kuona wakuu wa Wilaya na Mikoa wanavyokurupuka kwa sasa kuwawajibisha watendaji ambao wapo chini yao kwa kuwanasa vibao ama kuwasweka rumande.
“Hapo utajiuliza muda wao walikuwa wapi hata hivyo ukiangalia vizuri utagundua wazi kuwa wakuu wa
Mikoa na Wilaya hawana kazi yoyote ya kufanya na badala yake watendaji wakuu ni Makatibu tawala wa Mikoa au wakurugenzi wa Halmashauri husika” amesema Mbunge huyo.
Wabunge wakipendekeza hayo baadhi ya watumishi katika halmasauri ya Dodoma,nao kwa masharti ya kutokutaka kutajwa majina wamesema kwamba kutokana na kasi ya utendaji wa Rais Magufuli sasa wanasiasa wanalazimisha kuingilia masuala ambayo ni ya kitaalam.
“Tunashangaa zaidi kuona wanasiasa kama vile wakuu wa wilaya na wakuu wa Mikoa wakiwakaripia watumishi ambao ni wanataaluma.

“Na pale wanasiasa wanaposhauriwa juu ya utendaji wao wanakuwa wakali wakali zaidi kwa sasa kilichobaki ni watumishi kukaa kimya ili wawasikilize wanasiasa lakini matokeo yake kazi zitalala” alisema Mtumishi huyo.

Yapo mambo mengine kwa sasa ambayo uwezi kuyafanya kutokana na kuhitajika kwa vitendea kazi,wakati mwingine unatakiwa kutoa tiba wakati huo hakina vifaa.
Watumishi hao wanalazimika kutoa yao ya moyoni kutokana na taarifa mbalimbali zinaziripotiwa kuwa wapo baadhi ya wakuu wa Wilaya na wakuu wa Mikoa ambao wanawazaba watumishi vibao na kuwashweka ndani watumishi.

Wakati huohuo baadhi ya wanasheria mkoani Dodoma wamewataka baadhi viongozi wa serikali kuacha kutumia madaraka yao vibaya kwa kuwadhibu baadhi ya watumishi wanaochelewa kazini kwani kufanya hivyo ni kosa.

Siku za hivi karibuni vyombo vya habari kumezagaa taarifa za baadhi ya viongozi ndani ya serikali wamedaiwa kutumia nyadhifa zao vibaya kwa kuwapiga au kuwasweka lumande watumishi wa ngazi ya chini pindi wanapobainika kuchelewa kufika kazini.
Wanasheria hao kwa kuweka weka sawa suala la wakuu wa mikoa na wilaya au kiongozi yotote kumpiga mtumishi walisema kwa kufanya hivyo ni kosa la jinai.

Wakizungumza na MwanaHalisi online mjini hapa juzi, bila kumlenga kiongozi yeyote, Wanasheria hao  walisema ni kosa kwa mtumishi wakiwemo viongozi kupigana katika sehemu za kazi.
Mmoja  wa mawakili  wa Kituo cha Sheria cha Goldmac Attorneys Advocates, Modester Mganga, alisema watumishi wote wa Idara za serikali wanapaswa kuzingatia sheria sehemu za kazi pamoja na utawala bora na si vinginevyo.

Alisema kuwa endapo kama ni kweli kuna mfanyakazi ambaye amefanyiwa vitendo hivyo vya kupigwa au kuwekwa rumande anayo haki ya kwenda kushitaki kwenye vyombo vya sheria kwa vile sheria za kazi ziko wazi kwamba zina kataza watumishi kupigana sehemu za kazi.

Haya Hapa Majina 43 ya Wamiliki wa Makontena 329 Ambayo Yalipitishwa Bandarini Bila Kulipiwa Ushuru

$
0
0
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) juzi  ilitaja majina ya kampuni 43 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa ushuru, na kufichuliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wiki iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi jijini Dar es Salaam, Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.

Alisema mbali na hilo walitakiwa kuwatambua wamiliki wa makontena hayo, bidhaa zilizokuwemo, kuwalipisha wahusika kodi iliyokwepwa pamoja na kuwachukulia hatua watumishi waliohusika na upotevu huo.

Dk. Mpango aliyataja majina ya makampuni na watu binafsi na idadi ya makontena waliyopitisha bila kulipia ushuru (katika mabado) kuwa ni:-
Lotai Steel Tanzania Ltd (100)
Tuff Tryes Centre Company Ltd (58)
Binslum Tyres Company Ltd (33)
Tifo Global Mart Tanzania Company Limited (30)
IPS Roofing Company Limited (20)
Rushywheel Tyre Centre Co Ltd (12)
Kiungani Trading Co Ltd (10)
Homing International Limited (9)
Red East Building Materials Company Ltd (7)
Tybat Trading Co Limited (5)
Zing Ent Ltd (4)
Juma Kassem Abdul (3)
Salum Link Tyres (3)
Ally Masoud Dama (2)
CLA Tokyo Limited (2)
Farid Abdullah Salem (2)
Salum Continental Co Ltd (2)
Zuleha Abbas Ali (2)
Issa Ali Salim (2)
Snow Leopard Building (2)
Abdulaziz Mohamed Ally
Ahmed Saleh Tawred
Ali Amer
Ally Alhamdany
Awadhi Salim Saleh
Faheed Abdallah Said
Hani Said
Hassan Hussein Suleyman
Hamud Suleiman Enterprise
Kamil Hussein Ali
Libas Fashion
Nassir Salehe Mazrui
Ngiloi Ulomi Enterprises Co Ltd
Omar Hussein Badaway
Said Ahmad Hamdan
Said Ahmed Said
Salumu Peculiar Tyres
Sapato N. Kyando
Simbo Yonah Kimaro
Strauss International Co. Ltd
Swaleh Mohamed Swaleh
Alisema kwa ujumla, makampuni hayo yalipitisha makontena 329 ambayo yaliondolewa kinyume cha taratibu kutoka ICD ya Azam inayomilikiwa na Said Salim Bakhresa And Company Limited.

Dk. Mpango alisema bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.

Ukimya wa Lowassa,Sumaye na Mbowe Kuhusu MAJIPU Yanayotumbuliwa na Magufuli Wazua Maswali

$
0
0
Ukimya wa wanasiasa walioongoza harakati za kupambana na ufisadi katika majukwaa ya kisiasa, wakati huu Serikali ikichukua hatua za wazi na haraka kukabiliana na ubadhirifu wa mali za umma, umeibua maswali kuhusu uzalendo kwa nchi yao.

Miongoni mwa wanasiasa waliohusishwa na maswali hayo ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe na mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa.

Akizungumzia sakata hilo jana, Mhadhiri Mwandamizi wa Masuala ya Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Benson Bana, alisema kama kweli ni wazalendo, ni vyema wale wote waliokuwa wakipinga ufisadi wajitokeze hadharani, kupongeza hatua zinazoendelea kuchukuliwa.

Profesa Bana alisema hali inavyoendelea nchini kwa sasa ni wazi kwamba Rais John Magufuli, anapaswa kuungwa mkono na wote waliokuwa wakipinga ufisadi na ubadhirifu serikalini. 
  
Ni wakati muafaka sasa wale wote waliokuwa wanapinga ufisadi wakiwemo wanasiasa, wajitokeze hadharani kumuunga mkono Rais wetu, kama kweli walisema hayo kwa uzalendo na uungwana,” alisisitiza Profesa Bana.

Alisema ni wakati sasa wa Sumaye, Lowasa, Mbowe na wengine waliokuwa mstari wa mbele kueleza umma ufisadi na ubadhirifu serikalini kwenye kampeni za kuwania urais mwaka 2015, wakajitokeza hadharani kupongeza kazi inayofanyika.

Pia aliwataka wote waliosema hawataunga mkono serikali iliyoko madarakani, kufuta mara moja kauli yao, kwani yanayoendelea kufanywa ni mambo mazuri kwa ajili ya ustawi wa Watanzania wote bila kujali itikadi zao.

Magufuli na Ilani ya Ukawa 
“Yapo maneno kwamba Rais Magufuli anatekeleza ilani za vyama vingine na si ya CCM, haya maneno yapuuzwe ni kukosa hoja, ilani za vyama vyote vya siasa vinavyojitambua, zinajibu maswali haya ya wananchi,” alisema Profesa Bana.

Akifafanua hilo, Profesa Bana alisema kuna maneno yanaendelea kuzunguka kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu au kwenye mitandao ya kijamii, kuwa Dk Magufuli anatekeleza ilani za vyama vingine vya siasa na kusisitiza hoja hiyo haina mashiko.

Alisema Dk Magufuli anatekeleza yale aliyoahidi kwenye kampeni alipokuwa akiwania nafasi hiyo, kwa kuwa yapo kwenye Ilani ya CCM, huku akisisitiza kuwa ilani za vyama vya siasa mwaka huu zilifanana kwa njia moja au nyingine.

“Sisi tulipata bahati ya kusoma na kuchambua ilani za vyama vitatu CCM, Chadema na ACT-Wazalendo, tulipopitia ilani za vyama hivyo na vingine vilivyoshiriki kwenye uchaguzi uliopita, tulibaini zote zinafanana,” alisema Profesa Bana.

Alisema kama kuna chama kinasema ilani inayotekelezwa ni yao, wangekuwa mstari wa kwanza kujitokeza hadharani kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kutekeleza hayo, lakini kukaa kimya kunazua maswali mengi. 
  
Wajuta kutompa kura 
Alisema ni vyema Rais apewe nafasi aendelee kutekeleza anayofanya kwa sababu anajibu maswali ya wananchi yaliyokuwa yakisubiriwa kwa muda mrefu na kwamba wapo baadhi ya wananchi wanajuta hivi leo kwa kutompigia kura.

Tunazungumza na watu mbalimbali wanatuambia wanajuta kumnyima kura Rais Magufuli, kwa sababu kama asingeshinda, nchi ingekosa kiongozi mzuri na mwenye kasi ya maendeleo kwa wote,” alisema Dk Bana.

Wapenda utajiri 
Mhadhiri mwingine wa chuo hicho, Profesa Kitila Mkumbo alitoa mwito kwa Watanzania wote kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kubadilisha mitazamo yao ya kupenda vya bure, bali wafanye kazi kwa bidii.
  
Profesa Mkumbo alisema juhudi zinazofanywa na Rais Magufuli, zitakuwa na tija zaidi iwapo Watanzania wote watamuunga mkono kwa kubadilisha mitazamo yao ya kupenda utajiri wa haraka haraka.

Jitihada za Rais Magufuli pekee hazitoshi, bali jamii yote ya Tanzania lazima ibadilike, tuache kufanya vitu kwa mazoea na kupenda vya bure na utajiri wa haraka haraka, bali tupende kufanya kazi kwa bidii,” alisema Profesa Mkumbo.

Alisema masuala ya ubadhirifu na ufisadi ni mambo sugu yanayosumbua nchi na hatua zilizoanzwa kuchukuliwa na Rais Magufuli ni nzuri kwani tofauti na serikali zilizopita, yeye anatekeleza kwa kasi zaidi.

Ubadhirifu ni tatizo sugu nchini, lilianza kufanyiwa kazi tangu enzi za Mwalimu Nyerere hadi Rais mstaafu Jakaya Kikwete, ila kwa awamu hii ya Rais Magufuli, yeye anatekeleza kwa kasi zaidi,” alisema Profesa Mkumbo.

Mkuu wa Mkoa Wa Dar es Salaam Amsihi Yussuf Manji Akubali Kuachia Ufukwe wa Coco Beach Ili Uwanufaishe Watanzania Wote

$
0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadiki amemuomba mmiliki wa Kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na mfanyabiashara Yussuf Manji kutumia busara kukubali kuuachia ufukwe wa Coco jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Sadiki alisema Mahakama Kuu ya Tanzania, Kitengo cha Ardhi katika uamuzi wake imeiamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni ya Q Consult kwa ajili ya kampuni hiyo kuendeleza ufukwe huo hata hivyo Manispaa ya Kinondoni imekata rufaa.

“Kampuni ya Q Consult kwa busara tu iachane na kesi, ikubali kurudisha ufukwe huo chini ya mamlaka ya Kinondoni ili iweze kuuendeleza ufukwe huo kwa manufaa ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na sio kwa manufaa ya mtu mmoja kama anavyotaka mtu huyo,” alisema Sadiki.

Alisema wananchi wafahamu kuwa ufukwe huo wa Coco haujauzwa, kama watu wanavyodai na kwamba kesi hiyo iko mahakamani, ambapo Ofisi ya Manispaa ya Kinondoni kupitia Mwanasheria Mkuu wa Serikali wamekata rufaa.

Akielezea sakata hilo, Sadiki alisema kampuni ya Q Consult inayomilikiwa na Manji mwaka 2007 iliingia mkataba na Manispaa ya Kinondoni kuendeleza ufukwe huo.

Alisema, hata hivyo, baadaye Manispaa ya hiyo ilivunja mkataba huo baada ya Kampuni ya Q Consult kushindwa kutimiza masharti, jambo ambalo liliifanya kampuni hiyo kwenda mahakamani.

Mahakama Kuu ya Tanzania Kitengo cha Ardhi iliamuru Manispaa ya Kinondoni, kutekeleza mkataba wake na kampuni hiyo kwa ajili ya kuendeleza ufukwe huo.

“Kama nilivyosema kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali tumekata rufaa katika uamuzi huo kwasababu tunaamini haukuwa sahihi, hata hivyo mwekezaji huyo namshauri tu anaweza kufanya maamuzi akaachana na kesi hiyo na kuamua kurudisha ufukwe huo uendelee kutumiwa na Watanzania wote,” alisema Sadiki.

Kwa kampuni hiyo kushinda kesi hiyo, inamaanisha kuwa mwekezaji huyo endapo ataendeleza eneo hilo, wananchi hawatakuwa na fursa hiyo tena, kama wanavyoutumia sasa.

Sadiki alisema tayari serikali imefanya mazungumzo na moja na benki hapa nchini kwa ajili ya kupata mkopo, ambao utasaidia kuendeleza eneo hilo ili liendelee kubaki chini ya Manispaa ya Kinondoni na kutumiwa na watu wote.

Taarifa Sahihi Kutoka Kwa Prof Ibrahim Lipumba Kuhusu Tetesi ya Kuteuliwa Kwake na Magufuli Kuwa Mshauri wa Uchumi

$
0
0
Baada ya taarifa nyingi kusambaa hususani kwenye mitandao ya kijamii kwamba Rais John Magufuli amemchagua aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba kuwa mshauri wa masuala ya kiuchumi nchini.
Haya ndio majibu ya Prof. Lipumba, unaweza kuyapata kwa kubonyeza Play hapa chini:

Gazeti la Sweden Lamuandika Magufuli...Ladai John Magufuli Anawachonganisha na Marais Wenzake na Wapiga Kura Wao!

$
0
0
Dagens Nyheter ni gazeti kubwa kushinda yote nchini Sweden, ndio 'Daily News' lao kwa maana ya jina la gazeti.

Katika toleo lake la Ijumaa Desemba 4, habari za John Magufuli zimepamba pia gazeti hilo.

Amemwagiwa sifa, na ikaandikwa pia, kuwa Magufuli amewaweka katika wakati mgumu marais wenzake wa nchi jirani kwa vile wapiga kura wao wameonyesha wivu wao kwa Watanzania kupata Rais wa aina ya Magufuli.

Hata hivyo, kwenye gazeti hilo, imeandikwa pia, kuwa hata kabla ya kuingia milango ya Ikulu, Magufuli tayari ameshajipatia maadui wakiwamo wa ndani ya chama chake kwa hatua zake anazozichukua, hususan za kubana matumizi ya Serikali.

 Habari nzima  unaweza kuitazama kupitia Website ya Hilo gazeti kwa kubofya link hii hapa .Imeandikwa kwa lugha yao.


Tafsiri ya maelezo waliyoandika  kwa Kiingereza ni kama inavyosomeka hapa chini......

The newly elected President John Magufuli barely had time to move into Tanzania's presidential palace before he got his first enemies - the members of his own party CCM, which snuvats at the annual independence celebration. The money will instead go to a cleaning campaign.

The newly elected President John Magufuli barely had time to move into Tanzania's presidential palace before he got his first enemies - the members of his own party CCM, which snuvats at the annual independence celebration. The money will instead go to a cleaning campaign.

December 9 is the 54 years since the then Tanganyika gained independence from Britain, which is usually celebrated with pomp and circumstance in Tanzania's economic hub of Dar es Salaam. On vipl?ktaren sitting members of the party, CCM, who has ruled the country since then.

CCM's long hold on power has contributed to Tanzania is one of the world's poorest countries. Lately Tanzanians started playing with the idea that change is possible even in a system where the same party again and again win elections.

This year there will be no celebration, the newly elected President John pombe Magufuli declared on state television.

Instead, the money should be used for a national cleaning campaign. This year's Christmas card from the government has also been abolished in order to save money.

The budget for a grand opening celebration for the new parliament in the capital Dodoma were cut from the equivalent of 1.2 million SEK to 100 000 SEK. The surplus was used to buy new beds to the run-down hospital Muhumbili in Dar es Salaam, whose director was fired in the rebound after Magufuli made an impromptu visit.

Newspapers report on a delegation of 50 leaders who were off on a tour to the other countries of the British community. Magufuli shrank delegation to four people, which should have saved 2.4 million.

Civil servants and politicians forbidden to travel abroad on state funds and conferences will be held in the meeting rooms rather than in expensive resorts.

Magufuli, called the bulldozer because of its persistent road construction in his previous role as Minister, is now living up to his nickname in the more figurative sense, and voters in neighboring countries look with envy on development.

On social media spread nowadays continental success stories - that Muhammadu Buhari corruption fight in Nigeria, Malawi's former president Joyce Banda who sold the government plane and 60 Mercedes limousines or Namibia EX-PRESIDENT Hifikepunye Pohamba, who was awarded this year's Mo Ibrahim prize for good leadership.

Tanzania, one in all the years have had a big brother attitude to become a model harbors its own leaders in a difficult position where they have to feel ashamed or explain himself.

An Open Letter to President John Pombe Magufuli....Read Here

$
0
0

Dear Mr. President,

Like most Tanzanians, I applaud you for going after the tax evaders and corrupted government officials. It's about time.

However, to make Tanzanians more tax compliant and to reduce corruption, serious economic and political reforms must be implemented immediately.

I propose the following to your administration:

1. Reduce VAT to 10%. 
This will stimulate the economy by making goods and services affordable to low income earners.

2. Eliminate income tax for income below 1 million shillings a month for salaried workers and 4 million for traders.
This will increase spending power for poor consumers and help them afford to pay their bills. It will also make small traders more willing to pay taxes without reducing their capital. They can also be able to invest more in their businesses if they have extra income.

3. Reduce income tax for businesses. High taxes, without fine-tuning the rates in times of economic slowdow/crisis is one of the reasons why 99% of businesses cheat the government of tax revenue. Economic hardship encourage civil servants to take bribes to pay for the high cost of living. It also encourage businesspeople to give bribe to make their products more competitive. 

4. Introduce civil service reforms. Productive civil servants should be paid more and promoted accordingly. Incompetent ones should be fired and corrupt ones should serve long prison sentences. The civil servants should not expect "life employment" if they are not competent. Competitive wages to the civil servants will also discourage corruption. 

5. Increase the minimum wage to at least 500,000 a month. Most Tanzanians cannot eat 3 meals a day, let alone send their children to a good school with the current wages. This wage should also cover domestic workers. They have long suffered from minimum wage exclusion. 

6. Reform the court sysyem. 
Too many poor Tanzanians are spending years behind prison for petty crimes. Please set people free if they have served over 3 years waiting for their cases to be heard. The judges should send them to clean government buildings, clear trash in the city or do something more productive instead. It will also reduce prison congestion. Prison facilities should also be improved. It is a real shame, in this day and age, not to provide enough toilets to prisoners. 

Judges should be not allowed to take a leave of absence for whatever reason other than health. Cases must be heard and judgement given in a reasonable time. It should not take 5 years to conclude a simple case. 

The judiciary must be, at all times, feel, look and function independent of government pressure/interference. Even though our constitution stipulates that independence, in reality, the government often ignores it if the courts makes decisions not in her favour. Tanzanians would like to see the government respect court decisions. This will show the world our maturity as a democratic nation.

Before you introduce special courts to deal with corrupted civil servants and tax evaders, reform the current system first. It is impossible at the moment to seek justice in the court of law. It is not only time consuming but the system is heavily corrupted. Not only do average citizens are denied justice, it also discourages investors' confidence. It takes too long to settle business disputes. 

7. Let more foreign nationals get visas on arrival. This will encourage more tourists to come to Tanzania hassle free.

8. Introduce a special visa for rich retirees. This will increase foreign revenue, employment and taxes.

9. Allow highly educated foreigners to work/immigrate to Tanzania for a fee. They will bring in much needed skills which are in short supply and capital. They will ask create employment.

10. Legalize dual citizenship. 

11. Direct the postal service administrators not to tax packaged goods meant for personal use (under 300, 000 value).
Impose lower taxes for imports through the postal services to encourage Internet businesses to flourish. This will make it possible for small traders to afford starting a business with little capital. They can import without filling a container.

12. Encourage domestic manufacturers to invest with confidence by introducing competitive tax rates and by reducing red tape. They should be able to get all the necessary permits and licenses faster and cheaper under one roof. 

13. Discourage luxurious imports by imposing higher taxes on them.

14. Since transportation network is still poor, many people depend on their cars for transportation. Currently, unrealistic tax rates just encourage corruption to take place. I suggest lowering car import tax to 25% for brand new cars regardless of engine capacity and 35% for used cars under 10 years old. This will let more Tanzanians afford to import more cars. You can then charge them more for road tax and make them pay for road worthy sticker as well. You can easily get 200,000 -1,000,000 per car, per year, depending on the engine size, for the duration of the car's usage.

15. Allow the people of Zanzabar and Tanganyika to choose their future destiny. I believe majority of Tanzanians believe in the union. However, we were not consulted. I believe the people are now mature enough to decide on their fate through a referendum. It is the right way, the democratic way to seek our consent.

Mr. President, I hope my suggestions will be of some use to your administration. I am sure other contributors will come forward and give you more suggestion and proposals. All we want, is a strong, stable and prosperous country. 

My very best wishes to your administration.

Sincerely,
Tokyo40

Kiama Cha Waliotorosha Makontena 2431 Kimekaribia.....Majina Yao Yameshatua Kwa Waziri Mkuu

$
0
0
Baada ya moto kuwawakia watumishi wa Mamlaka ya Mapato wanaotuhumiwa kujihusisha na ukwepaji kodi wa kifisadi kwenye Bandari Kavu (ICDS) na kupelekea wanane kati ya watuhumiwa 37 kufikishwa mahakamani, zamu ya Mamlaka ya Bandari inakaribia, imefahamika. 

Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam, waliohusika na kupitisha makontena 2,431 bila kulipiwa kodi wanakaribia kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria baada ya majina ya wahusika kutua mezani kwa Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa, kama alivyoagiza. 

Kuwasilishwa kwa majina hayo katika Ofisi ya Waziri Mkuu Majaliwa, kunafuatia ziara ya kushtukiza katika Bandari hiyo ambapo aligundua kuwapo kwa ufisadi huo. 

Katika ziara hiyo, Majaliwa alimtaka Kaimu Meneja wa Bandari, Hebel Mhanga kupeleka ofisini kwake majina ya watumishi wote waliohusika na ukwepaji huo wa kodi unaokadiriwa kufikia shilingi bilioni 600 ifikapo saa 11 jioni Alhamisi. 

Jana  Mwandishi wa Habari wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Irene Bwire, alithibitisha  kuwa majina hayo yameshamfikia Waziri Mkuu. 

“Ninachoweza kukwambia ni kwamba majina yamefika mezani kwake kama alivyoagiza lakini siwezi kukutajia majina ya wahusika... Waziri Mkuu ndiye mwenye mamlaka ya kuyataja hadharani iwapo ataamua kufanya hivyo,” alisema Irene. 

Kwenye ziara hiyo, Majaliwa alimpa Meneja huyo siku saba kuhakikisha kuwa mamlaka hiyo inabadilisha mfumo wa utozaji malipo kutoka kwenye mfumo wa ankara na kuwa wa malipo wa kielektroniki. 

Wakati huohuo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaban Mwinjaka, aliuonya uongozi wa Bandari kutofanya ujanja wa kuficha majina ya watu wakubwa waliohusika na upotevu wa makontena 2,431 yaliyotolewa bila kulipiwa ushuru. 

Mwinjaka alitoa onyo hilo baada ya uongozi huo kutekeleza agizo la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kupeleka majina ya watu hao ofisini kwake juzi. 

“Lazima uongozi wa Bandari ujihakiki kama watu wote waliohusika katika hujuma ile majina yao yamo kwenye orodha iliyopelekwa kwa Waziri Mkuu,” alisema katibu Mkuu huyo. 
“Hata akiwa papa lazima ajulikane na wasiwachukue watu wadogo wadogo peke yao maana itawagharimu.” 

Waziri Mkuu Majaliwa alifanya ziara nyingine ya kushtukiza bandarini katikati ya wiki kwa kukagua mfumo wa upokeaji na utoaji mizigo wa malipo baada ya kupewa taarifa kuna makontena 2,431 yalitolewa bandarini bila kulipiwa ushuru. 
Majaliwa, alikagua idara mbalimbali za mamlaka ya bandari na kuona ukaguzi wa mizigo unavyofanyika kwa kutumia Scanners. 

Katika ukaguzi huo, Majaliwa alieleza kuwa kwa mujibu wa taarifa ya ukaguzi wa bandari ya kuanzia Machi hadi Septemba 2014, makontena hayo yalipita bila kulipiwa kodi kupitia bandari kavu nne ambazo ni JEFAG, DICD, PMM na Azam huku watumishi 10 tu wa ngazi za chini ndio wakiwa wamesimamishwa kazi kutokana na makosa hayo. 

Ziara hiyo ilikuwa ya pili bandarini katika kipindi cha siku tano, baada ya ile ya awali kubaini upotevu wa makontena 349 bila kulipiwa ushuru, kitendo kilichosababisha awasimamishe kazi watumishi tisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Bandari, huku Rais John Magufuli akimsimamisha kazi kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade.
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images