Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live

Breaking News: Kim Kardashian And Kanye West Welcome Baby Boy

$
0
0

Kim Kardashian has given birth to her second child with husband Kanye West.

The news was announced via a statement on her website kimkardashianwest.com

It read: "Kim Kardashian West and Kanye West welcomed the arrival of their son this morning. Mother and son are doing well."

Along with the statement was a picture of the couple holding hands.

It was initially reported that the expected delivery date was Christmas Day, December 25, but the baby has been born some three weeks earlier.


Katika Wabunge Vijana Ambao Wameweza Kurudi Tena Bungeni Kuwakilisha Majimbo yao..Unavutiwa zaidi na Mbunge Gani Kijana?

$
0
0
Wote ni wabunge vijana ambao wameweza kurudi tena bungeni kuwakilisha majimbo yao.
Unavutiwa zaidi na mbunge gani kijana?

Nafasi za Kazi
Bonyeza www.ajirayako.com

Breaking News: Moto wa Magufuli Watua Tanesco..Wafanyakazi Wasimamishwa Kazi Kutokana na Wizi

$
0
0
Kutoka shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuhusu kuwasimamisha kazi maofisa 7 waandamizi kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo wizi na ubadhirifu.
Akizungumza leo Dec 6, 2015 mbele ya waandishi wa habari Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba alisema…’Ukiacha kero zinazosababisha na Miundombinu TANESCO inachukua hatua madhubuti za kuwaadhibisha wafanyakazi wake wanaotoa huduma mbaya na kuwa kero kwa wateja baadhi ya kero ambazo zimekuwa zikilalamikiwa pamoja na lugha mbaya, wateja kudaiwa rushwa kabla ya kupewa huduma kucheleweshewa huduma, ubadhirifu‘ – Mramba

‘Shirika linapenda kuwahakikishia wateja wake kuwa tayari limeanza kuchukua hatua kali kwa wafanyakazi wanaobainika kujihusisha na mambo hayo’ – Mramba

Kwa mfano katika kipindi cha miezi miwili Shirika limewaachisha kazi maofisa 7 waandamizi kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo wizi na ubadhirifu.Miongoni mwao ni wale waliofikishwa mahakamani kule Kagera na kuripotiwa na vyombo vya habari jana.Walioachishwa kazi ni pamoja na wafanyakazi wa ngazi za Mameneja, wahandisi na wahasibu’ – Mramba
‘Shirika litaimarisha hatua hizo ambapo mfanyakazi yeyote atakayebainika analaghai wateja, anadai rushwa anatoa lugha chafu au huduma mbovu atawajibishwa mara moja na pale atakapobainika kuachishwa kazi‘Mramba

Nafasi za Ajira Kutoka Magazetini

Baraza Dogo la Rais John Magufuli Lazua Jambo...

$
0
0
Ahadi ya Rais John Magufuli kuwa ataunda Baraza dogo la Mawaziri imejenga shauku ya Watanzania kufahamu kiwango cha ukubwa au udogo wa baraza hilo ikilinganishwa na mabaraza yaliyoundwa na watangulizi wake baada ya kuapishwa, tangu Tanzania ipate Uhuru mwaka 1961.

Baraza hilo la Dk Magufuli ambalo Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema litatangazwa muda ukifika, tayari limechukua muda mrefu zaidi kuandaliwa, ikilinganishwa na mabaraza ya kwanza ya marais waliomtangulia tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini.

Changamoto inayomkabili Rais Magufuli ni kuunda baraza litakalokidhi matarajio yake na kauli mbiu yake ya “Hapa ni Kazi Tu” na matarajio ya Watanzania kwa upande mmoja na ahadi yake kwa upande mwingine, ya kuwa na baraza dogo.

Akilihutubia Bunge mjini Dodoma hivi karibuni na wakati akiwa katika mikutano yake ya kampeni za Uchaguzi Mkuu, Dk Magufuli aliahidi kuunda baraza dogo ikiwa ni njia za kudhibiti matumizi ya Serikali kwa nia ya kutafuta majawabu ya kero za wananchi kwa kasi inayostahili.

Kutokana na ahadi yake, jambo ambalo halitarajiwi ni Dk Magufuli kuteua mawaziri, idadi sawa na alioanza nao mtangulizi wake, Rais Jakaya Kikwete aliyevunja rekodi ya kuunda Baraza kubwa kuliko marais wote waliomtangulia tangu Uhuru.

Baraza hilo alilounda Kikwete mwaka 2005 baada ya kuingia madarakani, lilikuwa na mawaziri 60, kati yao 29 walikuwa mawaziri kamili na 31 naibu mawaziri.

Kinyume chake, Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, ndiyo iliyovunja rekodi ya kuwa na Baraza dogo la mawaziri 11 mwaka 1961.

Katika awamu ya pili mwaka 1985, Rais Ali Hassan Mwinyi alipoingia madarakani aliunda Baraza la Mawaziri lenye mawaziri 23 na manaibu wanane, jumla walikuwa 31.

Mwaka 1995, Rais Benjamin Mkapa alianza na mawaziri 27 na naibu mawaziri 10, jumla walikuwa 37 na aliowaita askari wa miamvuli.

Kauli ya wasomi

Wachambuzi wa masuala ya siasa na utawala wanapendekeza kuwa kutokana na mahitaji ya sasa na jitihada za kubana matumizi, Baraza lingefaa kutozidi mawaziri 20.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Benson Bana alisema ukubwa au udogo wa baraza unategemea na vipaumbele vya Rais katika kipindi chake cha uongozi kama vitakidhi mahitaji ya Watanzania.

“Haiwezekani kuwa na wizara 10 au chini ya hapo kutokana na ukubwa wa nchi na utendaji kazi wa Serikali kwa sasa, lakini sidhani kama kuna haja ya kuzidisha zaidi ya wizara 20,” alisema.

Kauli hiyo imeshabihiana na aliyoitoa Mhadhiri wa Chuo kikuu cha Mzumbe, Profesa George Shumbusho kuwa kulingana na mahitaji ya wananchi kwa sasa, hakuna haja ya kuwa na wizara zaidi ya 22.

Alisema udogo wa baraza hilo utategemea na namna ambavyo Rais Magufuli atapunguza na kuunganisha wizara zisizokuwa na uzito.

“Kuna wizara ambazo hata zikipunguzwa hazina athari na zinaweza kuvunjwa au kuunganishwa kwa ufanisi zaidi,” alisema. Mapendekezo ya wachambuzi hao yanaenda sanjari na yale yaliyokuwa katika Rasimu ya Katiba Mpya ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ibara ya 93(2) ilikuwa imependekeza Baraza la Mawaziri lisizidishe watu 15.

Hata hivyo, pendekezo hilo lilitupiliwa mbali wakati wa kujadili rasimu hiyo katika Bunge la Katiba ambalo lilifanikisha kuanzishwa kwa Katiba Inayopendekezwa inayosubiri kupigiwa kura ya maoni.   

Nafasi za Kazi
Bonyeza www.ajirayako.com

Kiama cha Mtandao wa Matajiri Wauza Madawa ya Kulevya 'Unga' Kimefika....Sasa ni Pekua Pekua na Kumata tu

$
0
0
Siku za wauza unga sasa zinahesabika baada ya Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya kuvunjwa rasmi na chombo kingine kitakachokuwa na mamlaka ya kuchunguza, kukamata, kupekua, kuteketeza na kuwapeleka mahakama kikitarajiwa kuundwa hivi karibuni.

Hatua hiyo imekuja baada ya Sheria ya Dawa za Kulevya ya mwaka 1995 kufikia kikomo Septemba 14 na kutungwa kwa sheria mpya ya kupambana na dawa za kulevya ya mwaka 2015 iliyoanza kutumika Septemba 15, mwaka huu.

Machi mwaka huu, aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama wakati akisoma muswada wa Sheria ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya (the drug control and enforcement act, 2014) bungeni Dodoma, alisema Serikali inakusudia kuanzisha chombo kinachojitegemea chenye mamlaka ya kiutendaji ya kuchunguza, kupekua na kukamata watuhumiwa tofauti na ilivyokuwa tume ambayo haikuwa na mamlaka ya kudhibiti na kupambana na tatizo hilo.

Katika mapambano hayo dhidi ya dawa za kulevya tofauti na sheria inayotumika sasa, chombo hicho kitajikita katika maeneo muhimu ikiwamo; kudhibiti mbegu za mimea ya dawa za kulevya, kuongeza viwango vya faini na nyongeza ya kifungo badala ya kuwa mbadala wa kifungo, na kutoa adhabu kutokana na uzito wa kosa.

Mapendekezo yaliyotolewa na kwa mujibu wa Muswada huo, watakaobainika kufanya biashara ya dawa za kulevya watozwe faini ya Sh1 bilioni moja au kifungo kisichopungua miaka 30 jela.

Pia, atakayekutwa analima, kusambaza mbegu, kusafirisha, kuzalisha au kuingiza mimea inayozalisha dawa za kulevya kama bangi, mirungi na cocaine atatozwa faini isiyopungua Sh 20milioni, kifungo kisichozidi miaka 30 au vyote pamoja.

Akiwa kwenye mikutano ya kampeni, Rais John Magufuli alitangaza mapambano dhidi ya dawa za kulevya na alipozindua Bunge Novemba 20, aliwaomba Watanzania wamuombee katika mapambano hayo aliyoyasema kuwa ni magumu.

Wakati akihutubia Bunge mjini Dodoma, Rais Magufuli alisema dawa za kulevya ni janga kwa taifa na kundi linaloathirika zaidi ni vijana wa kiume na kike.

Aliongeza kusema kuwa familia nyingi zimeathirika na nguvu kazi ya taifa imepotea kutokana na matumizi ya dawa hizo za kulevya.

“Tutaushughulikia mtandao huo hususan wafanyabiashara wakubwa wanaojihusisha na dawa za kulevya bila ajizi,” alisema.

Hata hivyo, hadi sasa uundwaji wa chombo kipya haujakamilika hadi Rais atakapomteua kamishna wa kukiongoza.

Msemaji wa tume hiyo, Florence Mlay, alisema tume ipo katika hatua za mabadiliko kuelekea kuwa chombo kamili kutokana na sheria mpya ya mwaka 2015.

“Hiki chombo kitakuwa na mabadiliko na kitakuwa na majukumu makubwa zaidi tofauti na ilivyokuwa tume,” alisema.

Katika miaka ya 90, Serikali ilianzisha vitengo vya kudhibiti dawa za kulevya katika baadhi ya idara na taasisi zake ili kuimarisha jitihada za udhibiti wa dawa za kulevya nchini.

Taasisi hizo ni Jeshi la Polisi, Idara ya Usalama wa Taifa na Idara ya Ushuru wa Forodha. Pamoja na jitihada hizo, tatizo la dawa za kulevya limeendelea kukua, mwaka 1995, Bunge lilitunga Sheria ya Kuzuia Biashara Haramu ya Dawa za Kulevya Namba 9 ya Mwaka 1995 (Sura 95).

Sheria hiyo ilianzisha Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya ambayo ilianza kazi mwaka 1997, chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na mwenyekiti wa Tume ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumzia sheria mpya ya dawa za kulevya, Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Alfred Nzowa alisema katika sheria mpya, dawa za kulevya hazihifadhiwa kama ilivyo sasa bali zitaharibiwa baada ya kupata hati ya uthibitisho kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

“Tume haipo tena hii ni baada ya kuundwa kwa sheria mpya, lakini chombo kipya kitakachoundwa kitakuwa na meno zaidi ya tume na kitakuwa na vitengo hadi mikoani,” alisema.

Alisema sheria hiyo mpya ya dawa za kulevya haijaathiri kitengo cha kupambana na dawa za kulevya kwa kuwa kimeundwa na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP).

Kesi 105 za dawa za kulevya

Akizungumzia kesi za dawa za kulevya nchini, Kamanda Nzowa alisema mpaka sasa bado kesi 105 zipo katika hatua ya kusikilizwa na watuhumiwa wengine wamehukumiwa.

Nzowa alitoa mfano wa Anna Mboya kuwa alikamatwa Novemba 2, 2011 na gramu 1,140 za dawa za kulevya aina ya cocaine na kuhukumiwa kwenda jela miaka 20 na kutozwa faini ya Sh 148.1 milioni.

Kesi nyingine ni ya raia wa Nigeria Chukwudi Okechukwu na wenzake watatu, Paul Ikechukwa Obi, Shoaib Muhammad Ayaz na Hycenth Stan ambao walihukumiwa jela miaka 30 kila mmoja na kulipa faini ya Sh9 bilioni. Chukwudi na wenzake walibeba kilo 81 za dawa za kulevya aina ya heroine.

Mtuhumiwa mwingine aliyehukumiwa hivi karibuni alitambulika kwa jina moja la Fred, alikamatwa na kilo 180 za heroine maeneo ya Mbezi Jogoo na kuhukumiwa jela miaka 20 na kulipa faini ya Sh15 bilioni.

Kamanda Nzowa alisema kukamatwa kwa watuhumiwa wa dawa za kulevya hakuna ujuzi bali ni taarifa zinazoletwa na wasamaria wema ndizo zinazosaidia.

“Mashine ya X-ray peke yake haisaidii chochote, lakini taarifa zinazotusaidia ni zile zinazoletwa na raia wema halafu sisi tunazithibitisha kwa mashine maalum ya poligrahic,” alisema.

Alisema mashine hiyo inawasaidia kugundua mtu kasema uongo au ukweli pindi anapopeleka taarifa katika kitengo hicho.

Wasamaria wema wakituambia, sisi tunaanza kazi mara moja, tunahakikisha kama taarifa ni za kweli kwa kutumia mashine hiyo, inatueleza kama mtu anasema kweli,” alisema.

Nafasi za Ajira
Bonyeza www.ajirayako.com    


Wakati Tanzania Tukiwa Tunashangilia Kusimamishwa Maofisa TRA, Kenya Wanafanya Hivi...

$
0
0
Kwa wanaofatilia siasa za kenya kulikua na skendo iliyokua inamuhusu waziri wa uhuru Anne Waiguru, huyu Anne Waiguru alikua ni waziri mtu mkubwa na maarufu serikalini.

Zimepotea 795 milion kshs ambazo ni kama 16 billion tz shs amewajibishwa na nyumbani kwake kumepekuliwa na maofisa wa kupambana na rushwa na kukuta mamilioni ya pesa kwenye mabunda, soon atafunguliwa mashtaka na kufungwa.

Juzi hapa Tanzania ufisadi wa escrow umetu cost zaidi 300 billions lakini hakuna hata mmoja aliyepekuliwa na wote wamerudi kua wabunge.

Tunatakiwa kuiga wakenya, sio tunatimua maofisa wa tra na muhimbili alafu tunaanza kujiisifu sana bado tuna safari ndefu kwenye hii vita dhidi ya ufisadi.

Sina nia ya kubeza anachofanya Magufuli, nampongeza ila tunapaswa kushinikiza yafanyike zaidi ya hapa na tumuunge mkono.


Kenya wana upinzani imara ndio maana kukitokea ubadhirifu kidogo tu wanaibana serikali hadi inawachukulia hatua wahusika.

Tusiwabeze wapinzani wa serikali tuwasapoti maana wao ndio wanaweza kuibana serikali kwa niaba yetu panapofanyika madudu kama haya

Mch. Gwajima Asifu Utendaji wa Magufuli

$
0
0
"Mhe Magufuli hayo unayo yafanya ndio watanzania tumekuwa tukiyapigia kelele miaka yote na tukaonekana wabaya. Tuko sambamba na wewe tunakuunga mkono safisha nchi.. usilegeze upanga wako wala usijali vitisho vyao. Tunakuombea ushujaa zaidi na roho ya Mungu iwe nawe"

Sehemu ya mahuburi yake leo Jumapili kanisani kwake

Nafasi za Kazi Kutoka Magazetini leo

Bonyeza www.ajirayako.com

Kanye West Ametumia zaidi ya Milioni 130 Kuuzuia Mkanda wa ‘Ngono’ Kusambaa, Mkanda Huo Umemuhusisha Nani?

$
0
0
Star  wa hip hop nchini Marekani, Kanye West, ameamua kutoa kiasi cha dola milioni 130, kwa ajili ya kuzuia mkanda wa ngono wenye picha zinazofanana na mke wake usiingie sokoni.

Kwa mujibu wa mtandao  wa US,  msanii huyo aliamua kafanya hivyo kwa kuwa ndani ya filamu hiyo kuna mrembo anafanana na mke wakewe Kim Kardashian.

Nimeona bora nifanye hivyo kwa kupunguza maneno ambayo yangejitokeza, ni filamu ambayo ina mambo mengi ndani yake, lakini inaweza kuharibu mwonekano wa familia yetu japokuwa hakuna mhusika ndani yetu,” alisema Kanye.

Nafasi za Kazi Kutoka Magazetini leo

Bonyeza www.ajirayako.com

Harmonize: ‘Directors’ wa Video Kutoka South Africa, Wanatuheshimu Sana Wasanii Kutoka Tanzania.

$
0
0
Chipukizi wa Bongo flava anayeunguruma poa na hit yake ‘Aiyola’, Harmonize amesema waongozaji wa video za muziki kutoka Afrika kusini huwa wanaonesha heshima ya hali ya juu wanapokutana na wasanii kutoka Tanzania.

Akifunguka mbele ya kipaza sauti cha Timesfm.co.tz, Mkali huyo ambaye jina lake halisi ni Rajab amedai sababu kubwa ya kupewa heshima ni kwa kuwa mziki wetu ni wa pili kwa ukubwa Barani Afrika ukiwatoa Nigeria.

“Labda mi niseme kitu kimoja” alisema “Directors wa kule(Afrika kusini) wanajua kabisa ili uweze kuhit Afrika mashariki ni lazima utusue Tanzania, na hilo liko wazi sisi ni wa pili kimuziki Afrika na tunaushindani mkubwa na Nigeria tu.

huduma huwa zinakuwa nzuri kiukweli, wanatu treat poa yani hadi unaona heshima unayopata” alimaliza.

Nafasi za Kazi Kutoka Magazetini leo

Bonyeza www.ajirayako.com

Rungu la TRA Yalishukia BAKWATA...Magari 82 Yaingizwa Kwa Jina lao Bila Kulipiwa Kodi..Watwangwa Barua Nzito

$
0
0
Rungu la TRA Yalishukia BAKWATA...Magari 82 Yaingizwa Kwa Jina lao Bila Kulipiwa Kodi..Watwaga Barua Nzito, Isome HApa chini:

Nafasi za Kazi Kutoka Magazetini leo
Bonyeza www.ajirayako.com

Katibu Mkuu Tamisemi Akagua Miundombinu ya Mfumo wa Mabasi Yaendayo Haraka

$
0
0
WATOA huduma katika kipindi cha mpito cha mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, kampuni ya UDA-RT wameihakikishia serikali na wananchi kuwa matayarisho yanaendelea vizuri tayari kwa huduma hiyo kuanza Januari 10 mwakani.


Ahadi hii ilitolewa wakati wa ziara iliyofanywa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jumanne Sagini, alipokuwa akikagua miundombinu katika mabasi yanayotarajiwa kutoa huduma hiyo.


Siku chache zilizopita, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliwataka wahusika wote wa mradi huo kuhakikisha unaanza mara moja ili kupunguza adha ya usafiri Dar es Salaam.

“Tulitaka kujiridhisha kama mabasi haya yako tayari kutoa huduma hii,” alisema Sagini mbele ya waandishi wa habari na kuwataka wahusika kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa haraka.

Mabasi 140 yanayomilikiwa na kampuni ya UDA-RT yatatumia mfumo wa kisasa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) wa ukusanyaji nauli, mifumo ya utoaji taarifa na maeneo maalum ya wazee na walemavu. 

Mwenyekiti wa UDA-RT, Robert Kisena aliwataka wananchi kujali mabasi hayo mara huduma itakapoanza.

“Wananchi wajali mabasi haya, madereva nao wana wajibu wa kuhakikisha magari haya yanadumu,” alisisitiza.

Alisema kuhujumu mabasi hayo mapya au miundombinu ya mradi huo ni sawa na wananchi kujihujumu wenyewe, kwani huduma hiyo ni kwa ajili yao. 

Alisema tayari kazi ya kufunga vifaa vinavyotakiwa katika mabasi hayo imeshakamilika kwa baadhi ya mabasi na inaendelea kwa mengine.

Msemaji wa UDA-RT, Said Mabruk alisema magari yote yanayotakiwa kuanza kwa huduma hiyo ya mpito yana madereva na walishapewa mafunzo na kwamba ni matumaini yao kuwa huduma itaanza kwa wakati uliopangwa.

Awamu ya kwanza inahusisha kilometa 20.9 za njia maalumu kutoka Kimara hadi Kivukoni, barabara ya Msimbazi kutoka Faya hadi Kariakoo- Gerezani na sehemu ya barabara ya Kawawa kutoka Magomeni hadi njia panda eneo la Morocco.

Tibaigana Afunguka...Huyu Ndiye Rais Niliyemtaka

$
0
0
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna mstaafu Alfred Tibaigana amesema Rais John Magufuli amepatikana wakati sahihi, kwa kuwa nchi inamhitaji kiongozi ambaye akitoa amri inatekelezwa mara moja.

Kauli ya Tibaigana inakuja takribani miezi 15 tangu aliposema anatamani kuiona Tanzania ikimpata rais dikteta kwa kuwa nchi haiwezi kupiga hatua iwapo mkuu wa nchi hataweza kukemea na kutoa amri watu wakatii.

Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti hili nyumbani kwake katika Kijiji cha Katare, wilayani Muleba Mkoa wa Kagera, hivi karibuni, Tibaigana alisema anaamini changamoto nyingi zinazowakabili Watanzania zitatatuliwa na Rais Magufuli.

Akitolea mfano utaratibu wa Rais Magufuli wa kufanya ziara za ghafla kwenye sekta mbalimbali za umma, Tibaigana alisema: “Watu hawafanyi kazi na viongozi ni waoga wa kutoa uamuzi, ziara ya Rais Magufuli (Hospitali ya) Muhimbili imesababisha hospitali nyingi kuboresha huduma, siyo lazima afike kila mahali akitoa kauli hatua ichukuliwe.”

Kamanda huyo mstaafu alisema hata uamuzi wa Rais Magufuli wa kufuta safari za nje kwa viongozi wa umma mpaka kwa kibali maalumu, umekuja wakati mwafaka kwa kuwa baadhi ya safari hazikuwa na masilahi kwa taifa.

“Safari zinatumia pesa nyingi na nyingine huwa siyo za lazima, kwa uzoefu wangu wa kukaa Serikalini hata baadhi ya wafanyakazi wa ndani hulipwa kama waajiriwa kwa kufanyiwa mipango na mabosi wao,’’ alisema.

Tibaigana ambaye aliwahi kugombea ubunge Jimbo la Muleba Kusini miaka mitano iliyopita kupitia CCM na kushindwa kwenye kura ya maoni, alipendekeza Bunge la 11 kufanyia marekebisho baadhi ya sheria ili ziwe kali kwa watu wanaohujumu uchumi.

Maagizo yatekelezwa

Kauli ya Tibaigana imekuja wakati Rais Magufuli ameanza kazi ya kutafuta na kuziba mianya ya upotevu wa fedha, alianzia Hazina na kupiga marufuku safari zote za nje kwa viongozi na kusema zitakuwa zinaruhusiwa kwa kibali maalumu.

Dk Magufuli pia aliamuru mashine za MRI na CT-Scan katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) zitengenezwe na kuagiza Sh3bilioni zitolewa kugharimia matengenezo kati ya Sh7bilioni zilizokuwa zinahitajika.

Vilevile, aliagiza Sh4bilioni zilizokuwa zitumike katika Maadhimisho ya Sherehe za Uhuru Desemba 9, kutumika kupanua barabara ya Morocco kwenda Mwenge, kazi ambayo utekelezaji wake unaendelea.

Rais huyo wa Awamu ya Tano na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa nyakati tofauti walitembelea maeneo muhimu kwa uchumi wa nchi kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bandari na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) na kuibua vitendo vya ufisadi na ukwepaji wa kodi.

Akizungumzia hali hiyo, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana anasema kinachoonekana ni uzembe au udhaifu kwa watumishi wa umma ambao mbali na kuwa wazito katika kutoa uamuzi, lakini ni wazito katika kutambua uzito wa tatizo.

Alisema lipo tatizo kubwa kwa viongozi wengi kukosa uwajibikaji licha ya dhamana kubwa walizopewa na kusema wakati umefika wa kuangalia upya mfumo wa uteuzi wa viongozi wa ngazi mbalimbali nchini.

“Hii ni dalili ya kuwa na viongozi wasiowajibika…maana haiwezekani mashine muhimu inaharibika na mkurugenzi na madaktari wake wanakaa kimya tu kama vile hakuna kilichotokea… hii inaonyesha kuwa tabia ya uwajibikaji haipo serikalini,” alisema Dk Bana.

Alisema kama ambavyo wafanyakazi wa Serikali wanaweza kudai mishahara kwa kugoma, kunapotokea kukosekana kwa vitendea kazi, watumie nguvu ileile kudai ili waweze kufanya kazi.

Alisema haiingii akilini kuona baadhi ya watendaji wa Serikali wakiwamo wakuu wa mikoa, wilaya na hata makatibu wakuu kukaa kimya licha ya Rais kuonyesha njia kipindi kifupi tangu ashike nafasi hiyo.

Profesa George Shumbusho wa Chuo Kikuu cha Mzumbe alisema uchapaji kazi wa viongozi katika eneo lolote unategemea na umakini na ufuatiliaji wa kiongozi mkuu.

“Baba katika familia akiamua mambo yaende yataenda tu… ni kawaida katika mabadiliko, binadamu kujaribu wakiona huna mchezo watafanya kazi wakiona ni nguvu ya soda mtarudi kule kule” alisema Profesa Shumbusho.

Alisema watendaji walio wengi walionekana kulala na kufanya kazi kwa mazoea kutokana na wakuu wao na akasema sasa wameanza kuamka kutokana na kasi ya mtendaji mpya na akasema kasi ya utendaji inaweza ikawa kubwa zaidi endapo rais naye ataendelea kuonyesha njia.     

Jakaya Kikwete Aibukia 'Sauzi' Magufuli Akitumbua Majipu Magogoni Aliyomwachia....

$
0
0
Wakati Rais John Magufuli akitimiza siku 31 akiwa amejifungia Ikulu kutatua kero za nchi bila kusafiri nje ya nchi, Rais mstaafu Jakaya Kikwete (pichani) ameendelea kujumuika katika hafla za kimataifa baada ya kuonekana nchini Afrika Kusini juzi akiwa mwalikwa wa Mkutano wa China na Afrika.

Tangu aingie madarakani Novemba 5, Rais Magufuli amepiga marufuku safari za nje kwa watendaji wa serikali bila ya kibali maalumu cha Ikulu.
Alifikia uamuzi huo baada ya kubainisha katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge la 11 mwezi uliopita kuwa safari za kimataifa zinatafuna mabilioni ya fedha za walipa kodi.

Rais Magufuli hajasafiri kwenda nje ya nchi mbali na kwenda Dodoma kwa ajili ya kumwapisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na kuzindua Bunge.
Picha zilizotumwa na Ofisi ya Makamu wa Rais jana, zilimwonyesha JK akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, aliyemwakilisha Rais Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na China, uliomalizika jana jijini Johannesburg.

JK ameonekana katika picha hizo akitembelea mabanda ya maonyesho ya mkutano huo ulioandaliwa na China ili kujadili mikakati ya ushirikiano baina yake na Afrika. 

Ni mara ya pili kwa Kikwete kwenda nje ya nchi tangu Rais Magufuli aingie madarakani. Novemba alionekana katika Jiji la Addis Ababa Ethiopia.

Kwenye utawala wake wa miaka 10, Rais mstaafu huyo alilaumiwa kusafiri mara nyingi nje ya nchi akiwa na msururu wa viongozi na wasaidizi wake hivyo kutumia gharama kubwa, lakini alijitetea kuwa huenda nje kutafuta fedha za maendeleo.

Wakati akihutubia Bunge mjini Dodoma mwezi uliopita Rais Magufuli alisema safari za nje ziliigharamu nchi Sh. bilioni 356 kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.

Alisema kati ya kiasi hicho karibu Shilingi bilioni 200 zilitumiwa kwa tiketi za ndege, kadhalika bilioni 68 zilitumiwa kwa mafunzo ya nje wakati bilioni 104 ziliishia kwenye mifuko ya vigogo na maofisa kwa ajili ya posho.

Rais Magufuli alisema mabilioni hayo ya safari yangejenga kilometa 400 za barabara kwa kiwango cha lami akitaja ile inayotoka Urambo Tabora hadi Kigoma mjini.

Katika kutimiza azma ya kupinga safari za nje , Rais Magufuli alikacha kwenda kwenye mkutano wa wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Madola, uliofanyika visiwa vya Malta wiki mbili zilizopita.

Aliagiza Balozi wa Tanzania jijini London Uingereza na maofisa wengine wanne kuiwakilisha nchi kwenye mkutano huo hatua iliyookoa karibu Shilingi milioni 700 ambazo zingegharamia safari hiyo.

Nafasi za Kazi 

Kasi ya Rais John Magufuli Yaibua Upya Sakata la Ubomoaji wa Jengo la Ghorofa 16 Ambalo liliamriwa Libomolewe Tangu 2013

$
0
0
Kasi ya utendaji wa Rais John Magufuli, imeibua upya sakata la ubomoaji wa jengo la ghorofa 16 ambalo serikali iliamuru libomolewe baada ya kutokidhi viwango lakini viongozi walionekana kulega lega katika utekelezaji wa agizo hilo.

Azma ya kubomolewa kwa jengo hilo lililopo mtaa wa Indira Ghand na Kisutu, kunafuatia tukio la Machi 29 mwaka 2013 baada kuporomoka kwa jengo pacha lililosababisha vifo vya watu 36, na kujeruhi wengine 18.
Hata hivyo, kazi ya kubomoa imeonekana ikisuasua kwa miaka mitatu kutokana na wakandarasi wanaopewa kazi hiyo kujitoa katika hatua ya mwisho wakitoa sababu mbalimbali.

Manispaa ya Ilala sasa imetangaza kufanya kazi hiyo haraka na tayari kampuni tatu za kimataifa zimejitokeza kufanya kazi hiyo.
Akizungumza na Nipashe, Ofisa Habari wa Manispaa ya Ilala, David Langa alisema Halmashauri hiyo ipo katika hatua ya mwisho ya kumpata mkandarasi wa kufanya kazi hiyo.

Alisema mpaka sasa katika zabuni iliyotangazwa kuna kampuni tatu zilizojitokeza kutaka kazi hiyo na wako katika hatua za mwisho mwisho kumpata mshidi wa zabuni hiyo.

“Kuna mambo mengi ya kuangalia kabla ya kubomoa jengo, lazima tujiridhishe athari zitakazojitokeza katika usalama wa watu, mazingira na mali zingine,” alisema Langa.
“Muda si mrefu tutataja jina la kampuni itakayopewa kazi, ” aliongeza Langa.

Jengo hilo linamilikiwa kwa pamoja kati ya Shirika la la Nyumba la Taifa (NHC) na Ali Raza Investment, awali lilitakiwa kuvunjwa na kampuni ya kichina ya CRJ lakini ilishindikana.

NJIA YA KUBOMOA

Mtaalam mmoja kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye hakutaka jina lake litajwe, alisema ubomoaji wa jengo la aina hiyo ni kazi ngumu na hapa nchini kuna kampuni na taasisi chache zenye uwezo wa kufanya kazi hiyo.

Alisema kuna aina mbalimbali za ubomoaji salama wa majengo ya aina hiyo, lakini ina gharama kubwa.
Mtaalam huyo alisema kinachotakiwa kufanyika ni kuhakikisha jengo hilo linaporomoshwa kwa kushuka chini na si vinginevyo kwa ajili ya kuepuka madhara.

Alizitaja njia hizo kuwa ni kubomoa kwa kuondoa ghorofa moja moja kutoka juu, lakini alionya njia hiyo ina hatari ya kukosea kisha sehemu ya ghorofa kuangukia makazi ya watu.
Alisema njia nyingine ni kutumia vyombo maalum vya kukatia na kuondoa vifusi.

“Kwa kutumia njia hii inakuwa rahisi kidogo, lakini mara nyingi kunahitajika vyombo na utaalamu wa hali ya juu ambao kwa nchi yetu ni vigumu kupata,” alisema mtaalam huyo.

Alitaja njia inayofaa na yenye madhara kidogo ni ubomoaji wa mabomu ambayo inapolipuka inaporomosha jengo kwa kulishusha chini.
Alisema mabomu hayo yanategwa kulingana na urefu wa jengo, kisha yanalipuliwa kufuata mtitiriko maalum ambao hautasababisha jengo kukatika na kuanguka.

“Mabomu haya yanategwa katika nguzo za kila ghorofa, halafu yanalipuliwa kuanzia juu kushuka chini, hivyo jengo litashuka chini na halitatawanyika,” alisema mtaalam huyo.

Hata hivyo alieleza kwamba njia hiyo inawezekana pale kazi hiyo itafanywa na vikosi vya Jeshi la Ulinzi au kampuni iliyothibitika inaweza kutumia utaalam huo.

HALI HALISI

Wakazi wanaoishi jirani na jengo hilo walisema kuchelewa kubomolewa inawazidishia hofu juu ya usalama wao na mali zao.
Hafidh Haroon alisema shughuli za biashara katika eneo hilo zimekuwa za mashaka kutokana na wasiwasi wa kuangukwa na jengo hilo.
“Tunafanya kazi zetu tukiwa na wasiwasi pengine linaweza kuanguka muda wowote tunaomba serikali kuingilia kati haraka kufanya kazi hiyo,” alisema Haroon.

Mwandishi wa gazeti hili alishuhudia majengo yaliyozunguka jengo hilo yakiwa hayana watu baada ya kuhama kunusuru maisha yao.
Hata hivyo baadhi ya maduka na huduma zingine za biashara zilizo jirani zilionekana kuendelea kutoa huduma kama kawaida.

Mara baada ya tukio hilo, la Machi 29, Aprili 5 mwaka 2013, aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka aliyeambatana na wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira walitembelea eneo hilo na kutoa siku 30 kwa mmiliki wa jengo hilo, Ally Raza kulibomoa baada ya kubainika kujengwa chini ya kiwango na sehemu isiyo zingatia mipango miji.

Kulingana na sheria ya Ardhi namba 4 ya mwaka 1999, kifungu cha 44 na 45 na pia kanuni za ardhi za 2001 inaelekeza mhusika aliyekiuka masharti ya uendelezaji anapaswa kupewa ilani ya kubomoa na akiendelea kukaidi amri analipa faini ya asilimia mbili.

Hata hivyo, mmiliki huyo alikimbilia mahakamani kufungua kesi ya kupinga kubomolewa, kesi ambayo iliisha kutolewa hukumu ya jengo hilo linapaswa kubomolewa.

Nafasi za Kazi Magazetini

Kati ya Makampuni yaliyokwepa Kodi Mbona Hatusikii Yanayomilikiwa na Lowassa?

$
0
0
Zile siasa chafu za nchi hii zinaelekea kujidhiirisha baada ya watanzania kushuhudia makampuni ya wakwepa kodi bila kutajwa kampuni hata moja yenye mahusiano na Lowassa. Kinyume chake kuna harufu ya uvundo inayowahusisha vigogo waliocheza mchezo wa kumchafua.

Ukweli utadhiirika kwamba alizamishwa kwente tope la ufisadi makusudi ili kukatiza safari yake ya "matumaini" na watu waoga wenye nia ya kuila nchi yetu bila kunawa na wenye hofu ya kulipiziwa kisasi

Nafasi za Kazi 

Habari ya Week Leak Kwamba Osama Bin Laden Bado Yupo Hai Yaishtua Dunia....

$
0
0
Kuna habari zimetolewa muda mfupi uliopita na shushushu nguli la Marekani Edward Snowden kupitia Weekleaks yake kuwa ana taarifa za uhakika kwamba Osama bin Laden yuko hai na anaishi kwa payroll ya Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA mjini Nassau katika visiwa vya Bahamas huko USA.

Kama habari hii ni ya kweli basi Marekani inatisha. Ebu wataalam wa mambo kama haya ingieni kazini mchimbe mtupe ukweli wa jambo hili maana inasemekana kuna picha za hivi karibuni zimethibitishwa kuwa ndiye na ni za kweli.
----------------------
From the Web:

Worldnewsdailyreport.com published an article recently in which they quoted Snowden saying that Osama was living in Bahamas and was on the payroll of CIA.

The article quotes him as saying - “I have documents showing that Bin Laden is still on the CIA’s payroll. He is still receiving more than $100,000 a month, which are being transferred through some front businesses and organizations, directly to his Nassau bank account. I am not certain where he is now, but in 2013, he was living quietly in his villa with five of his wives and many children."

The article further quotes him as follows - “Osama bin Laden was one of the CIA’s most efficient operatives for a long time. What kind of message would it send their other operatives if they were to let the SEALs kill him? They organized his fake death with the collaboration of the Pakistani Secret services, and he simply abandoned his cover. Since everyone believes he is dead, nobody’s looking for him, so it was pretty easy to disappear. Without the beard and the military jacket, nobody recognizes him.”

But the real catch is this - The website which published the article is a satire organisation. 

A disclaimer on their site reads as follows - WNDR assumes all responsibility for the satirical nature of its articles and for the fictional nature of their content. All characters appearing in the articles in this website – even those based on real people – are entirely fictional and any resemblance between them and any persons, living, dead, or undead is purely a miracle.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya Desemba 7, Ikiwemo ya Kukosekana Kwa Mawaziri Kwaokoa Mamilioni

Wafanyabiashara Mliokimbilia Ubunge Uwabebe Kwenye Mishe Zenu imekula Kwenu

$
0
0
Kama kuna walio na bahati mbaya naongelea wafanyabiashara walioamua kukimbilia bungeni kusaidika.

Hakika kwa speed hii kama kweli umefanikiwaa jiandae kutumikia jimbo kwa nguvu zote pls.

Misamaa ya kizembe na ya kijinga kama zamani haipo tena kwa hapakazi tu kwakweli. Jipangeni mnasaidiaje jimbo mrudi tena.

Nawatakia la kheri najua sio wote wenye mawazo hayo ila kama uliingia bungeni TRA na misaada yake ikubebe imekula kwenu

Nafasi za Ajira
Bonyeza www.ajirayako.com

Vanessa Mdee Anogesha Tamasha la Trust 'Divas Only' Jijini Mbeya

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Vanessa Mdee (Katikati) akiwajibika jukwaani mbele ya umati wa akina dada waliojitokeza kwenye Tamasha la “Divas Only Concert” ambalo lilifanyika katika ukumbi wa Mtenda, Sunset-Soweto jijini Mbeya. burudani hiyo ya nguvu iliandaliwa na chapa ya Trust toka shirika lisilokuwa la kiserikali la DKT International ambalo liliwakutanisha madiva kutoka sehemu mbalimbali wengi wao wakiwa ni wanafunzi wa vyuo vikuu vya jijini Mbeya kwa ajili ya kutoa elimu juu ya uzazi wa mpango.


Msanii Vanessa Mdee akitoa burudani kwa madiva wa jiji la Mbeya wakati wa Tamasha la Trust “Divas Only Concert” ambalo lilifanyika jijini humo katika ukumbi wa Mtenda Sunset uliopo Soweto lengo la Tamasha likiwa ni  kutoa elimu ya uzazi wa mpango kwa akina dada na mama wa jiji hilo.


Msanii Vanessa Mdee (katikati) akiwa pamoja na wanenguaji wake katika Tamasha la “Divas Only Concert” lililofanyika katika ukumbi wa Mtenda Sunset-Soweto jijini Mbeya mwishoni mwa wiki. Msanii huyo aliporomosha burudani ya nguvu kwa madiva lukuki waliofika kushuhudia tamasha hilo ambalo lililoandaliwa na chapa ya TRUST toka shirika lisilokua la kiserikali la DKT lengo la Tamasha likiwa ni kuwahamasiha kuamka kifikra na kutoa elimu ya uzazi wa mpango kwa wasichana na kina mama wa jiji hilo.


Baadhi ya akina dada waliohudhuria burudani iliyotolewa na mwanamuziki Vanessa Mdee jijini Mbeya kwenye hamasa ya matumizi ya uzazi wa mpango iliyodhaminiwa na chapa ya Trust toka shirika lisilokuwa la kiserikali la DKT International. Tamasha hilo lillilopewa jina la “Divas Only Concert” lilifanyika katika ukumbi wa Mtenda Sunset-Soweto jijjini Mbeya mwishoni mwa wiki.


Mbeya Desemba 2015 TRUST imeendelea kuzikonga nyoyo za mashabiki wake hususani wakina dada katika mfululizo wa matamasha ya kusisimua ya “Divas Only” ambapo kwa wikiendi hii ilikua ni zamu ya jiji la Mbeya baada ya Tamasha hilo kuzinduliwa rasmi jijini Dodoma mwishoni mwa wiki iliyopita. Kama ilivyo ada Tamasha hilo humshirikisha Diva wa nguvu na msanii wa muziki wa kizazi kipya Vanessa Mdee ambaye alizikonga nyoyo za mashabiki wake vilivyo. Tamasha hilo liliwavutia madiva kibao kutoka maeneo ya karibu pamoja na vyuo mbalimbali vya jijini Mbeya kama TECU, Mzumbe, CBE na TIA ambapo kiingilio cha Tamasha hilo kilipangwa kuwa Tsh. 10,000/= tu. Trust ni chapa ya njia za kisasa za uzazi wa mpango zenye kuaminika pamoja na bidhaa na huduma za maisha na urembo zinazotengenezwa kwa ajili ya wanawake. Trust ipo ili kuhamasisha madiva wajipange kwa ajili ya baadaye. Madiva wa Trust wanataka kufanya maamuzi na kupanga kwa ajili ya mafanikio; Trust ipo hapa kukusaidia wakati wa safari hii. “Kwa mara nyingine ilikuwa ni fursa nzuri ya kufurahi kwa muda tuliopata wa kukaa na Vanesaa na Madiva wa Trust wa jijini Mbeya na kufurahi na kuelimishana, tumejifunza kutoka kwa wataalamu mambo mengi  na njia nyingi bora, kwamfano  njia ya Kitanzi ni bora sana ina ufanisi wa zaidi ya asilimia 99.9 na pia ni bora sana kwakua aina nyingi hazina vichocheo  ”…alisema Sialouise Shayo Meneja Masoko Trust. Kama wewe ni Diva wa Trust ama unataka kujua Trust inahusu nini, njoo ukutane na Madiva wa Trust wengine pamoja na Vanessa Mdee katika Tamasha letu lingine jijini Mwanza Desemba 13, Malaika Beach Resort. Huwezi kufika? Tutafute kupitia ofisi zetu zinazopatikana Dodoma, Mbeya na Mwanza au kwa kupitia tovuti yetu (trustlife.co.tz) na ututembelee leo!

Gazeti la Mwanahalisi Latoa Majina Yaliyovuja Baraza la Mawaziri wa Magufuli

$
0
0
Wakati joto la kusubiri rais John Magufuli atangaze majina ya baraza lake la mawaziri likizidi kupanda, gazeti la Mwanahalisi limetoa baadhi ya majina yanayodaiwa kuvuja kutoka kwenye orodha hiyo.

Mmoja kati ya majina ambayo yamevuta usikivu wa wengi ni jina la aliyekuwa waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe ambaye alikuwa mmoja kati ya wagombea wa CCM waliokuwa wanatajwa kuwa chaguo la rais mstaafu, Jakaya Kikwete.

Kwa mujibu wa gazeti la Mwana Halisi, majina mengine yanayotajwa ni pamoja na January Makamba,Dk. Asha Rose Migiro,Ridhiwani Kikwete,Peter Serukamba na Mwigulu Nchemba.

Jina jingine lililotajwa kwenye orodha hiyo ni jina la aliyekuwa Makamo Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino (SAUT), Dk. Charles Kitima.

 Dk. Kitima anadaiwa kuwa mmoja kati ya watu waliomuamini sana Dk. Magufuli wakati akiwa Waziri wa Ujenzi na hata kumualika kuwa mgeni rasmi kwenye mahafari ya chuo hicho.

NB: Majina  haya  ni  kwa  mujibu  wa  gazeti  la  Mwanahalisi ambalo limedai kuyapata baada ya kuvuja. Rais Bado hajatangaza baraza lake la mawaziri

Hata hivyo,Rais Magufuli anatarajiwa kutangaza baraza lake la mawaziri muda wowote kuanzia sasa. 

Kwa mujibu wa katiba, rais anapaswa kutangaza baraza lake kabla ya kuanza kwa vikao vya bunge vya mwezi Januari.
Viewing all 104690 articles
Browse latest View live




Latest Images