Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Le Mutuz Naye Afunguka Kuhusu Rafiki Yake Dr Mwaka...Adai yeye Amejiridhisha Dr Mwaka Hana Kosa

$
0
0
EXTRA LIVE STRAIGHT TALK:- Ok guys kama nilivyosema ninarudia tena Dr.Mwaka ni rafiki yangu na ni my Client ni mtumzima mwenye akili timamu sijawahi kuwa na sababu ya kum doubt leo nimemtaka in private anihakikishie kwamba hizi tuhuma si za kweli na AMEFANYA HIVYO amenitumia kila kinachotakiwa Ku prove tofauti na kila anachotuhumiwa...nilitaka kujiridhisha na so far nimeridhika ana kila anachotakiwa kuwa nacho kufanya yote anayoyafanya...nilitaka kuweka wazi hilo tu NIMERIDHIKA unless nije niambiwe tofauti again nitasema...again sijawahi kumkimbia rafiki akiwa kwenye matatizo NEVER...in my life huwa sijibizani na yoyote anayemuhusu ndugu yangu wa damu NEVER maana nitakuwa namvunjia heshima anayemuhusu na siwezi kugombana na damu yangu kwa sababu ya MTU wa kupita hapana...nilipokuwa Baharia kuna wakati tulikuwa na safari ya Europe to Brazil ni lazima kupitia "BERMUDA TRIANGLE" mahali pa hatari sana ambapo hata kampuni yako ya Meli inakupa options za kubadili Meli usiende pale maana mkifika pale Meli inaweza kuzungushwa na Maji wiki nzima ndio mkaweza kupita na ukipita pale unaongezwa Mshahara binafsi nilipita Mara tatu in my Six years ya Ubaharia wangu. So sio mgeni wa kuchafuka bahari....my point is hakuna kazi isiyokuwa na "BERMUDA TRIANGLE" Social Media INA FAIDA na HASARA zake ila to me FAIDA ni kubwa kuliko HASARA so ni ya kawaida kusingiziwa singiziwa lakini in the end THE TRUTH WILL PREVAIL so again tayari nimejiridhisha na Dr. Mwaka sasa imebaki Naibu Waziri na again ninamtakia heri na niaamini UKWELI UTAJULIKANA WOTE TUTAKUWA HURU makosa ni kumuhukumu MTU bila FACTS just because Fulani kasema kama ushahidi WOTE alionipa Dr. Mwaka ni wa kweli basi TUTAKUWA na aibu ya the Century by leo jioni! JAMANI ASUBUHI NJEMA! - le Mutuz


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Disemba15, Ikiwemo ya JK Alivyoiumiza Nchi

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Disemba15, Ikiwemo ya JK Alivyoiumiza Nchi

Mbunge wa Ubungo Atiwa Mbaroni kwa Amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda

$
0
0
MBUNGE wa Ubungo, Saed Kubenea (Chadema) amekamatwa na polisi eneo la viwanda (EPZA) Mabibo kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Tukio hilo limetokea kukiwa na mgomo wa wafanyakazi zaidi ya 1800 wa kiwanda cha nguo cha TZ TOOKU ambao walimpigia mbunge wao aende kutatua mgogoro huo.

Kubenea alifika katika eneo hilo saa 6 mchana, akakutana na wafanyakazi kusikiliza kero zao za muda mrefu.

Kisha aliamua kuondoka na viongozi wa wafanyakazi hao na kufanya kikao na menejimenti ya kiwanda hicho kuanzia saa 7 hadi saa 9.

Ilipofika saa 10:30 Makonda alikuja na kupata taarifa kwa muafaka uliofikiwa kati ya Kubenea, menejimenti na viongozi wa wafanyakazi.

Alitoa amri wafanyakazi wakusanyike, akaawaambia kesho atafika huko na Waziri wa Viwanda na Biashara, Waziri wa Kazi na Ajira, na Waziri wa Afya Wanawake, Jinsia na Watoto.

Baada ya kutoa maagizo hayo, Makonda alimzuia Mbunge asihutubie kuaga wananchi aliokuwa nao tangu mchana, kutokana na hali hiyo Kubenea alisema ni vema aseme neno, ndipo mvutano ulipoanza.

Makonda alimuru mkutano ufungwe lakini wafanyakazi hawakutawanyika eneo hilo, alipoona hivyo aliamrisha Polisi wamkamate Kubenea, kwa madai alimwita yeye Kibaka.

Katika tukio hilo, Mwandishi wa habari wa Star Tv aliyekuwa anarekodi tukio hilo alinyang’anywa kamera na Polisi aliyejulikana kwa jina moja tu la Denis.

Mwandishi wa habari Mwanahalisi alijaribu kumsaidia mwenzake ili arejeshewe kamera lakini Polisi wa kituo cha Magomeni walimtisha, na kumtaka kuondoka haraka huku wakiondoka na aliyenyang’anywa kamera.

Bado Kubenea anaendelea kuhojiwa na polisi katika kituo cha Magomeni akiwa na mwanasheria wake, Fred Kihwelo.

Kivazi Kifupi Chamtokea Puani Shamsa Ford

$
0
0
Muigizaji wa filamu, Shamsa Ford ameonja joto la jiwe hivi karibuni baada ya kuambulia matusi katika mtandao wa Instagram kutokana na kuvaa kivazi kifupi akiwa mbele ya mtoto wake wa kiume.

Muigizaji huyo mahiri wa filamu ya Chausiku na Bado na Tafuta, ametoa ya moyoni kupitia mtandao huo baada ya kutukanwa na mashabiki.

Maisha yangu hayawahusu. Ukiona hufulahishwi na chochote toka kwangu ni unfollow. Hukulazimishwa kunifollow. Yaani kuniona kwenye movie ndo mnajifanya mnanijua mpaka mnipangie maisha ya kuishi.sikilizeni nitavaa nitavyojisikia mm hata nikiamua kukaa uchi kabisaa ni mm na wala hayakuhusu. Ww subili movie Itoke ndo unikosoe. Mnaboa sana. Hebu walekebisheni ndugu zenu wanaovaa madila mchana usiku ni vyangudoa,” aliandika Shamsa.

Haya ni maoni ya mashabiki baada ya Shamsa Ford kuweka picha akiwa mevaa nguo fupi mbele ya mwanae.

Salumkiemba218: Angalia huyo mwanao asije akakutamani watoto wa sikuhizi ni shida.

Annmlokole: Tembea uchi bwana unamuogopa nani mbona unavaa?

Hapixlucas: Mmmh waja mwacheni dada wa watu jamani..dnt b so quick to judge her,after all u only see wat she choose to show u! Xo u better get a lyf u mofos…mnakera

Gmassam123Ila: Jaman kuna mambo ya kusifia jaman ila sio kwa uchii huo alio uvaa staa wetu ss hapo ndio unaelimisha nn? jamiii kukupenda tunakupenda sana ila kwa mavazii ya uchi kama hayo waachie wenyewe. Wenye tamadun zao.

Mlimboashura: Huo sio usafi Shamsa wewe ni kioo cha jangu unawafundisha nini wanaokuangalia

Happy.brown001: Duuu….hata kama ni ustaa dear c kwa kujiacha uchi hivyo…hata wazungu now days wana aibu kdg….but am yo fun na.

CHADEMA Wacharuka Baada ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda Kumweka Ndani Mbunge wao Saidi Kubenea..Watoa Tamko

$
0
0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kama ambavyo imeripotiwa kwenye vyombo vya habari na njia zingine za upashanaji habari tangu jana kuwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CHADEMA, Ndugu Saed Kubenea aliwekwa chini ya ulinzi na kuamriwa kwenda kituo cha polisi kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye inadaiwa hakutaka mbunge huyo azungumze na wananchi ambao ni Wafanyakazi wa Kiwanda cha Tanzania Took Garment, waliokuwa wamemuita mbunge huyo kwa ajili ya kumweleza matatizo wanayokumbana nayo kazini hapo, ikiwa ni pamoja na ujira kidogo na mazingira magumu ya kazi.

Aidha akitambua kuwa alichofanya matumizi mabaya ya dhamana ya uongozi, hivyo akakusudia kuficha umma usijue uovu huo, katika tukio hilo Makonda aliwaagiza polisi wakamate kamera za waandishi wa habari waliokuwa katika eneo hilo wakitimiza wajibu wao wa kikazi na kitaaluma kwa jamii.

Katika hatua ya sasa, tunaomba kusema ifuatavyo;
1. Tukitambua kuwa mamlaka ya DC kuamuru watu kukamatwa yamefafanuliwa kisheria na kuwekewa mipaka yake ambayo Makonda amedhihirisha kuivuka katika nyakati tofauti sasa, Mkuu huyo wa wilaya hana mamlaka ya kisheria wala ya kisiasa kuhalalisha amri aliyoitoa ya kumkamata mbunge, tena aliyekuwa anatekeleza wajibu wake, tunamtaka DC Makonda amwachie Ndugu Kubenea mara moja huku tukitoa wito kwa mamlaka zilizomteua kumwangalia kwa makini kama bado anazo sifa za kuwa kiongozi wa ngazi hiyo.

2. Kwa kuwa amri hiyo si halali kwa sababu haina msingi wowote wa kisheria, tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi kumuachia Ndugu Kubenea ili aendelee na uhuru wake huku akitekeleza wajibu wake wa kuwawakilisha wananchi wa Ubungo badala ya kumsumbua kwa mambo yasiyokuwa ya msingi.

3. Halikadhalika, Jeshi hilo liwarudishie waandishi wa habari vifaa vyao vya kazi vikiwa katika hali salama na bila athari yoyote ama ya vifaa vyenyewe au materials yaliyoko ndani yake.

4. Tunalitaka Jeshi la Polisi kutoa kauli ya kuwahakikishia usalama waandishi wa habari na vifaa vyao kila wanapotimiza wajibu wao kwenye matukio yanayomhusisha Makonda kwa sababu tayari ushahidi unaonesha anaweza kuwa tishio kwao binafsi na vitendea kazi vyao hususan pia wanapokuwepo polisi.

5. Kwa kitendo cha DC Makonda kuamuru kiongozi wa wananchi akamatwe bila kuwepo kosa lolote la kisheria, CHADEMA tutachukua hatua za kisheria dhidi ya DC huyo ili liwe fundisho kwake mwenyewe, wakuu wa wilaya wengine na utawala mzima wa Serikali ya CCM chini ya Rais John Magufuli, ili watambue kuwa suala la kuongoza nchi kwa kuzingatia Haki, Katiba, Sheria na taratibu si suala la kupenda bali ni lazima kuzingatiwa kwa ajili ya amani na utulivu wa kweli.

Tutachukua hatua hizo huku tayari kukiwa na kumbukumbu za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBU) ambayo hivi karibuni ilimuonya DC Makonda na wakuu wa wilaya wengine na wakuu wa mikoa ambao wameanza tabia ya kuendesha nchi kwa amri ambazo hazina uhalali wowote zikiwa nje ya mamlaka yao ya kisheria kufanya hivyo.

Tuliamini angalizo hilo la THUB ambacho ni chombo huru cha serikali, lingeweza kuwa mwongozo sahihi kwa viongozi wa serikali na kwamba kosa la awali la Makonda kuwaweka mahabusu watumishi wa Wilaya ya Kinondoni walioko chini yake lingechukuliwa kama fundisho kwake, lakini bahati mbaya watawala wanaweka nta masikioni linapofika suala la haki za binadamu na uongozi bora.

Imetolewa leo Jumanne, Nov. 15, 2015 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Waziri Mpya wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa Avamia DAWASCO Kwa Kushtukiza..Atoa Maagizo Haya

$
0
0
Profesa Makame Mbarawa 
Waziri mpya wa maji na umwagiliaji, Profesa Makame Mbarawa, ameiagiza mamlaka ya maji safi na maji taka jijini Dar es Salaam DAWASCO, kuongeza idadi ya watu wanaotumia maji safi kutoka 148,000 (idadi ya sasa) hadi watu 1,000,000 kufikia Juni mwaka ujao.

Profesa Mbarawa alitoa agizo hilo alipofanya ziara ya kushtukiza katika makao makuu ya DAWASCO. Mbarawa amesema serikali ya awamu ya tano imejizatiti kuhakikisha kunakuwa na maji salama na wanawake hawapati shida ya kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Kati ya mambo aliyoahidi Rais Magufuli wakati wa kampeni zake, ni kuweka mikakati ya kuhakikisha kunakuwepo na maji safi na salama ili kumaliza tatizo la ukosefu wake lililopo tangu nchi ipate uhuru.

Rais Magufuli pia alisisitiza kuwa Serikali yake haitavumilia mawaziri wavivu, hasa waliopewa wizara nyeti kama hii ya maji.

Mbawara pia ameagiza kuwepo na bei nafuu ili kila mwananchi aweze kupata maji safi na salama.

Tarehe 1, mwezi huu wa 12, DAWASCO ilipandisha bei ya maji kutoka shilingi 1, 098 kwa lita 1000 hadi shilingi 1,663 kwa kipimo hicho.

UPDATES..Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea Apandishwa Kizimbani..Asomewa Shitaka Hili...

$
0
0
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea anafikishwa mahakamani Kisutu muda huu.
Huku ni kuiongezea mahakama mrundikano wa kesi zisizo na kichwa wala miguu
Kwa mtindo huu lazima Makonda ajitafakari mara mbili mbili

=============

UPDATES;
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amesomewa shitaka la lugha ya matusi kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda. Kesi imehairishwa mpaka Des 29, ameachiwa kwa dhamana.

Nahreel Kasema ‘Nisieleweke Vibaya Kuhusu haya Niliyosema Kuhusu Mwanamuziki Diamond Platnumz’

$
0
0
Nahreel ni msanii wa kundi la Navy Kenzo lakini pia ni Producer ambaye mikono yake imehusika kuzisuka hits nyingi tu ikiwemo za WEUSI, Vanessa Mdee, Navy Kenzo, Shilole na hivi karibuni Nahreel ameingia kwenye headlines za Tanzania baada ya kusema hakupendezwa na maneno ya utambulisho wake kufutwa kwenye beat aliyoitengeneza ya wimbo wa ‘Nana‘ wa Diamond Platnumz ft. Mr Flavour

Nahreel anasema alikiweka hicho kibwagizo kikimtaja kwamba yeye ndio producer wa hiyo beat lakini wimbo ulipotoka hakukisikia sababu kiliondolewa, ikabidi aulize upande wa Diamond imekuaje…. kumsikia mwenyewe na alichoambiwa unaweza kubonyeza play kwenye hii video hapa chini.

Mbwana Samatta Katika Orodha ya Wachezaji Watatu Bora ya CAF

$
0
0
Mshambulizi matata wa Taifa Stars ya Tanzania na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mbwana Samatta ametajwa katika orodha ya wachezaji watatu bora na shirikisho la soka la Afrika CAF wanaocheza soka barani Afrika.

Samatta anawania hiyo na wachezaji wengine wawili Baghdad Boundjah wa Algeria na Etoile du Sahel na Kipa machachari wa TP Mazembe ya DR Congo Robert Kidiaba.
Mshindi atachaguliwa na makocha wa timu za taifa na kutangazwa katika dhifa maalum Januari tarehe 7 mwakani.

WABUNGE wanne wa CCM Wametajwa Kukataa Uteuzi wa Nafasi ya Uwaziri Wakihofia Kushindwa Kuendana na Kasi Magufuli

$
0
0
WABUNGE wanne wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wametajwa kukataa uteuzi wa nafasi ya uwaziri ili kujaza nafasi za wizara nne zilizokuwa wazi.

Hatua hiyo imetokana na kile kilichoelezwa kuwa ni hofu ya wabunge hao kushindwa kwenda na kasi ya Rais Dk. John Magufuli, ambaye aliwaapisha mawaziri wapya Desemba 12, mwaka huu.

Kwa mujibu wa gazeti la Mtanzania, wabunge wamedai kuwa kasi ya Rais Magufuli inawatia hofu.

“Kasi ya Rais Dk. John Magufuli ni nzito na kwangu ni ngumu na nilifikiri niko mimi peke yangu kumbe baada ya taarifa hizi nasikia na wenzangu wawili nao walikataa uteuzi.

“Niliarifiwa juu ya uteuzi lakini baada ya kupima nikaona hapana siwezi kazi ya uwaziri, bora ni baki na ubunge wangu,” alisema mbunge huyo ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Wizara 4 zilizokosa Mawaziri
Wakati akitangaza Baraza la Mawaziri, Desemba 10, mwaka huu, Rais Magufuli alisema kuna baadhi ya wizara hazina mawaziri kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo unyeti wa wizara hizo na kwamba anaendelea kuwatafuta.

Kutokana na hali hiyo Rais Magufuli aliteua manaibu waziri wa wizara hizo, huku akitoa ahadi kuwa atawatangaza mawaziri wake baadaye atakapomaliza mchakato.

Wizara hizo ni pamoja na Ujenzi, Uchukuzi na Miundombinu ambayo naibu wake ni Mhandisi Edwin Ngonyani na Wizara ya Fedha na Mipango, ambayo naibu wake ni Dk. Ashatu Kijaji.

Wizara nyingine ni Maliasili na Utalii, ambayo naibu wake ni Mhandisi Ramo Makani, Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ambayo naibu wake ni Mbunge wa Jimbo la Nyasa mkoani Ruvuma, Stella Manyanya.

Kinana atoboa siri
Mwishoni mwa wiki akiwa mkoani Arusha, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, alitoa siri ya wabunge wanne ambao walipigiwa simu za uteuzi wa uwaziri, lakini walikataa kwa hofu ya kushindwa kwenda na kasi ya Rais Magufuli.

Alisema anachoamini ni kwamba Rais John Magufuli, atakuwa aliwaeleza baadhi ya wabunge kuhusu nia yake ya kuwateua katika nafasi hizo, lakini wao wakamwomba asiwape majukumu hayo kwa kuwa hawana uhakika wa kwenda na kasi anayohitaji katika Serikali yake.

Kinana alisema kinachojitokeza sasa ni kama alivyoshauri Rais Magufuli kuwa si vema kwa waziri aliyeteuliwa kufanya sherehe nyumbani kwake na kuita marafiki kwa kuwa wana mzigo mzito katika kuwatumikia wananchi.

“Ni vema mawaziri hawa wakafanya maombi kwa kuwaita au kuwafuata viongozi wa dini kwani wana kazi ngumu kulingana na nia njema aliyonayo Rais Magufuli katika kupambana na masuala ya ufisadi.

“… kazi ya kupambana na ufisadi kamwe si rahisi hadi kushangilia uteuzi, lengo kubwa ni kuwaletea wananchi maendeleo kupitia ubinafsishaji wa viwanda kutoka kwa watu waliomilikishwa na kuviua,” alisema Kinana.

Katibu mkuu huyo wa CCM, alisema anaunga mkono uamuzi wa Rais Magufuli wa kufuta maadhimisho ya Siku ya Ukimwi dunaini, hali ya kuwa wagonjwa hawana dawa.

“Nyingine ni Wiki ya Maji, mnafanya maadhimisho huku watu hawana maji, Wiki ya Maziwa wakati wafugaji wamekonda na mifugo imekonda haitoi maziwa, fedha hizo zitumike kwa mambo mengine,” alisema Kinana.

Je..Fedha Zilizopigwa Stanbic Bank Ziligharimia Kampeni UKAWA?

$
0
0

Kinara Bashir Awale
UCHUNGUZI unaoendelea wa serikali kuhusu ufisadi wa takribani shilingi bilioni 13 katika mkopo uliochukuliwa kupitia Benki ya Stanbic unaonyesha kuwagusa watu ambao walikuwa mstari wa mbele kwenye kampeni za vyama vilivyo kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), imefahamika.

Ingawa kiwango halisi cha mkopo ambao serikali ilichukua kupitia benki hiyo ni dola milioni 600 (shilingi trilioni 1.3), ufisadi unaonekana katika kiwango cha dola milioni sita (shilingi bilioni 13) ambazo sasa imethibitika zilitumika kuwahonga viongozi wa serikali ili wauruhusu.

Kinara Bashir Awale
Huyu ndiye aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Stanbic wakati wa kutafuta na hatimaye kupatikana kwa fedha hizo. Kwa mujibu wa taarifa za kimahakama kutoka Uingereza, huyu ndiye alikuwa mtengenezaji wa mpango wote wa kupatikana kwa rushwa hiyo.

Mara baada ya kuondoka kutoka Stanbic mwaka 2013, kutokana na kukataa kutoa ushirikiano wakati wa uchunguzi wa sakata hilo, mara nyingi Awale alionekana akiwa na aliyekuwa mgombea urais wa Ukawa, Edward Lowassa.

Ndani ya kambi ya Lowassa haikuwa siri kwamba endapo angeshinda urais, Awale angeweza kupewa nafasi ya Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Yeye ni mmoja wa watu waliokuwa wakitajwa kama wasaka fedha wakuu wa Ukawa na Lowassa. Akiwa na uzoefu wa muda mrefu katika eneo la benki na fedha, Awale alikuwa miongoni mwa wana Ukawa walioweza kujigamba kwamba wako karibu na Lowassa.

Kwa sasa, Awale amefukuzwa nchini kwa madai ya kutokuwa raia wa Tanzania lakini ukaribu wake na Lowassa unaonekana katika baadhi ya picha zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonyesha akiwa katika mojawapo ya mikutano ya kisiasa ya Chadema, akiwa amekaa karibu na mtoto mkubwa wa Lowassa, Fred.

Uchunguzi wa vyombo vya usalama vya Uingereza unaonyesha kwamba wakati wa fedha hizo kulipwa kutoka Stanbic kwenda kwa kampuni ya EGMA, fedha zilikuwa zikitolewa kwenye akaunti na kwenda kwanza kugawiwa kwenye ofisi yake kabla ya kutoka nje ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Kinara Shose Sinare
Taarifa za kikachero kutoka Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Kijinai ya Uingereza (SFO), zinamtaja mfanyakazi huyu wa zamani wa Stanbic kama SS, na aliwahi kuwa Miss Tanzania mwaka 1996.

Katika ufisadi huu, Shose anatajwa kama msaidizi wa karibu wa Awale na mtu ambaye ukiondoa bosi wake huyo, alifanya kazi kubwa kuhakikisha mpango huo unafanikiwa. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja wa kumhusisha Shose na Ukawa zaidi ya hatua ya mama yake, Dk. Eve Sinare, aliyekuwa mwanachama wa muda mrefu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kutangaza kuhama chama hicho katika siku za mwisho za kampeni za Uchaguzi Mkuu.

Wakati Dk. Sinare akitangaza kuhama CCM, watu wengi walishangazwa na uamuzi wake huo kwa vile yeye si mmoja wa wanachama maarufu wa chama hicho na hatua yake hiyo haikuonekana kumsaidia yeyote. Mara baada ya kuibuka kwa kashfa hii ya Stanbic, maswali yameanza kuibuka kuhusu mwenendo wao katika wakati huo wa kuelekea Uchaguzi Mkuu. Inadaiwa kuwa kwa kawaida Dk. Sinare na Shose ni watu walio karibu sana.

Harry Kitilya
Huyu alipata kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Ushiriki wake katika kashfa hii umewashangaza wengi kwani kwenye jamii alijenga picha ya kiongozi msafi. Kitilya alikuwa mmoja wa wamiliki wa kampuni ya EGMA ambayo ndiyo ilipewa kiasi hicho cha shilingi bilioni 13 kwa ajili ya ?kulainisha viongozi wa serikali? kukubali kuchukua mkopo huo kutoka Stanbic.

Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, jina la Kitilya lilikuwa likitajwa kama mmoja wa watu waliokuwa wakichangisha fedha za kusaidia Lowassa ashinde uchaguzi.

Tofauti na watu kama Awale waliokuwa wakimuunga mkono Lowassa hadharani, Kitilya hakuwahi kutamka hadharani kumuunga mkono mwanasiasa huyo wala kuonekana kwenye mikutano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Kitilya, kwa nafasi aliyokuwa nayo TRA, ni mmoja wa watu waliokuwa wakiombwa ushauri na serikali iwapo ichukue mkopo au isichukue. Kwa maana hiyo, Kitilya alilipwa fedha hizo ili pia naye ?alainike? na ?kuishauri? serikali ichukue mkopo huo hata kama masharti yake hayakuwa muafaka.

Kwa mfano, wakati riba ya kawaida ya mikopo ilikuwa ni asilimia 1.4, mkopo huo ulichukuliwa kwa riba ya asilimia 2.4. Ongezeko hilo la asilimia moja ndilo lililoleta kiwango hicho cha shilingi bilioni 13. Ili kuhakikisha EGMA inapata fedha nyingi kupitia asilimia hiyo moja, badala ya serikali kukopa dola milioni 550 ilizotaka kukopa awali, ikakopa dola milioni 600. Kama ingekopa dola milioni 550, EGMA ingepata dola milioni 5.5 tu.

Kwa mujibu wa uchunguzi wa SFO, ingawa Kitilya ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya EGMA, hakuwahi kwenda kuchukua fedha hizo Stanbic na badala yake kazi hiyo ilifanywa na wabia wenzake, Dk. Fratern Mboya na Peter Nyabuti.

Peter Nyabuti
Uchunguzi wa SFO unamtaja Nyabuti kama raia wa Kenya na hakuna taarifa nyingi zinazomhusu. Hata hivyo, katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Tanzania, Nyabuti alikuwa mmoja wa wateja maarufu katika baa ya Kruz In iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Kwa kipindi kirefu, baa hiyo imefahamika kama kambi rasmi ya ?Marafiki wa Lowassa? ambapo ni kawaida kwa watu waliokuwa kwenye kambi yake; tangu akiwa CCM, kujumuika na kubadilishana mawazo katika eneo hilo. Kwa sababu hiyo, Nyabuti aliyekuwa akichanganyika na watu kama Awale na Fred Lowassa, alikuwa akifahamika kama mmoja wa wapanga mipango na mikakati wa Ukawa.

Ingawa Chadema na vyama vilivyo kwenye Ukawa vimekuwa vikifahamika kwa kupinga ufisadi, hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa kambi hiyo aliyetoa kauli ya karipio dhidi ya ufisadi huo wa Stanbic.

Kwa sasa serikali inafanya uchunguzi kuhusu suala hilo na tayari imeahidiwa kwamba itarejeshewa shilingi hizo bilioni 13 zilizotolewa kama hongo.

Kwa hisani ya RaiaMwema
by MsemajiUkweli/JF



Nafasi za Kazi

Madiva wa Mwanza Wajitokeza Kwa Wingi Kufunga Tamasha la Trust Divas Only

$
0
0
Baadhi ya madiva wa jiji la Mwanza wakiwa kwenye pozi la Red Carpet wakati wa Tamasha la “Trust Divas Only” ambalo lilifanyika katika hoteli ya Malaika Beach Resort jijini Mwanza mwishoni mwa wiki. Tamasha hilo ni maalum kwa ajili ya akina dada na ni mahususi kwa ajili ya utoaji elimu ya afya ya uzazi na maendeleo yao ya baadae.

Madiva mbalimbali wakijiandikisha wakati wa ufunguzi wa Tamasha la “Divas Only”ambalo lilikuwa maalum kwa ajili ya kuwaelimisha akina dada juu ya afya ya uzazi na maendeleo yao ya baadae. Tamasha hilo ambalo lilipambwa vilivyo na burudani toka kwa Msanii Vanessa Mdee lilifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza.



Moja ya Madiva wa jiji la Mwanza akiimba accapela kwenye tamasha la “Trust Divas only” lilofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza katika Ukumbi wa Malaika Beach Resort. Tamasha hilo ni maalum kwa ajili ya akina dada ambalo lilitoa elimu ya afya ya uzazi kwa madiva wa jiji hilo.


Msanii wa Bongo fleva Vanessa Mdee akitumbuiza kwenye Tamasha la “Trust Divas Only” lililofanyika katika hoteli ya Malaika Beach Resort jijini Mwanza mwishoni mwa wiki. Tamasha hilo ni maalum kwa ajili ya kina dada na limekua likitoa elimu juu ya afya ya uzazi na maendeleo ya baadae ya madiva hao tokea uzinduzi wa mfululizo wa matamasha hayo jijini Dodoma wiki mbili zilizopita.



Msanii wa Bongo fleva Vanessa Mdee, akipiga picha na baadhi ya mashabiki wake wakati wa Tamasha la “Divas only” ambalo ni mahusisi kwa ajili ya kuwaelimisha madiva mbalimbali kuhusu elimu ya afya ya uzazi. Tamasha hilo la mwisho lilifanyika katika ukumbi wa Malaika Beach Resort jijini Mwanza baada ya kuzunguka katika majiji ya Dodoma na Mbeya katika wiki zilizopita.

Mwanza
Tamasha la “Trust Divas only” limefunga pazia lake rasmi usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Malaika Beach resort uliopo pembezoni mwa ziwa Victoria jijini Mwanza. Wakazi na madiva wa mkoa huo walijitokeza kwa wingi kushuhudia Tamasha hilo la mwisho na la aina yake lakini kikubwa zaidi kupata elimu na hamasa juu ya uzazi wa mpango na mambo yanayowahusu wakina dada katika kupanga maendeleo yao ya baadae.
Aliyelipamba Tamasha hilo si mwingine bali ni diva wa nguvu na msanii wa kizazi kipya Vanessa Mdee ambaye tokea awali amekua akishirikiana na Trust katika mfululizo wa matamasha hayo yaliyoanza rasmi wiki mbili zilizopita jijini Dodoma.
Mara baada ya kupanda jukwaani na kuporomosha burudani ya nguvu Vanessa alionekana kushangiliwa kila kona na madiva hao waliokuwa wakiimba sambamba na msanii huyo ambae alifanikiwa kukata kiu ya madiva wengi wa mkoa huo waliojitokeza kwa wingi kushuhudia burudani yake.
Mfululizo wa matamasha hayo ya Trust ambayo ni chapa ya njia za kisasa za uzazi wa mpango zenye kuaminika pamoja na bidhaa na huduma za maisha na urembo zinazotengenezwa kwa ajili ya wanawake yamefikia tamati baada ya kuzunguka kwa muda wa wiki tatu kwenye miji mitatu tofauti ili kuhamasisha madiva mbalimbali wajipange kwa ajili ya mafanikio yao ya baadae. Trust ipo katika kumsaidia diva wakati wote wa safari hii.
“Ni furaha yangu kubwa kuwa tumeweza kukamilisha zoezi hili kwa ufanisi mkubwa tangu tulipozindua matamasha haya jijini Dodoma”… alisema Meneja Masoko wa Trust Sialouise Shayo.
Bi. Shayo aliongeza kuwa katika zoezi zima wamefanikiwa kuwafikia madiva lukuki katika mikoa yote mitatu waliyoitembelea ambapo kwa pamoja wameweza kufurahi, kuelimishana na kujifunza kutoka kwa wataalamu mambo mbalimbali zikiwemo njia nyingi bora za uzazi wa mpango kama njia ya kitanzi ambayo ni bora sana  na ina ufanisi wa zaidi ya asilimia 99.9.
Kama wewe ni Diva wa Trust ama unataka kujua Trust inahusu nini, Tutafute kupitia ofisi zetu zinazopatikana Dodoma, Mbeya na Mwanza au kwa kupitia tovuti yetu (trustlife.co.tz) na ututembelee leo.

Ushindi wa Ubunge wa Godbless Lema Jimbo la Arusha Mjini Waingia Doa..Mgombea wa CCM Aibuka na Kupinga Ushindi Huo

$
0
0
Godbless Lema
Aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya CCM, Philemon Mollel amepinga matokeo ya uchaguzi huo yaliyompa ushindi wa kishindo, Godbless Lema wa Chadema.

Akiongea na waandishi wa habari baada ya msimamizi wa uchaguzi huo kutangaza matokeo, Mollel alidai kuwa kulikuwa na udanganyifu mkubwa ambao unafanya matokeo hayo kutokuwa halali.

Alisema kuwa wakati zoezi la kupiga kura likiendelea kuna gari lililokamatwa likiwa na kura bandia za kumpa ushindi Lema ingawa alidai gari hilo liliachiwa baadae.

Kulikuwa na Noah ya diwani wa Chadema ambayo ilipita katika baadhi ya vituo vya kupigia kura na kudai kupeleka vyakula. Lakini gari hiyo tumeambiwa ilikuwa na kura za bandia zilizofanikiwa kuingizwa kwenye masanduku,”alisema Mollel.


Kadhalika, alieleza kuwa kulikuwa na mapungufu makubwa kwenye fomu za matokeo kwa kuwa baadhi ya fomu hazikuonesha idadi ya kura zilizopigwa.

Mollel alilirushia lawama jeshi la polisi kwa madai kuwa liliwatisha akina mama na wazee kwenda kupiga kura.

Hakukuwa na vurugu zozote, kwanini kuwatishia wanachi kwa silaha na vifaa vya kivita,” alihoji Mollel.

Matokeo yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi huo uliofanyika Jumapili, Disemba 13 yalimpa ushindi Godlbess Lema kwa kupata kura 68,848 sawa na asilimia 65.9 huku Philemon Mollel akipata kura 35,607 sawa na asilimia 34 ya kura zote halali zilizopigwa na kuhesabiwa.

Rais John Magufuli, Majipu Yamekwisha? Ukimya wako Watia Shaka

$
0
0
Ulianza vizuri. Ulianza kwa mkwara imara hadi viongozi wakatamani wajiondoe wenyewe. Ukafanya ziara ya ghafla isiyo na hafla Wizara ya Fedha na Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kama hiyo haitoshi,ukaunguruma Bungeni ukiahidi kutumbua majipu ya ufisadi kwa wale waliofaidi zaidi. Ukajielekeza TRA na Bandari. Pakatokea yaliyotokea. Baada ya hapo,ukimya umetawala.

Ukimya wako umetanguliwa na kikao cha Kamati Kuu ya CCM. Kulikoni? Au TeamLowassa imekwisha kule TRA na Bandarini na haipo kwingineko? Nauliza tu kiutaniutani!

By Mzee Tupatupa wa Lumumba(kwasasa Arusha)

TAZAMA Picha Mbali Mbali za Maafa ya Mvua Dar Leo Disemba 15, 2015

$
0
0
 Maeneo ya Mbagala, Bonde la kuelekea Mission panahofiwa kutokea vifo; Nyumba zimebomoka kwa maji watu wakiwa ndani.

Mbunge wa Kawe Halima Mdee yupo Tegeta Kibo muda huu anakagua uharibifu uliofanywa na mvua na tayari na malori yanamimina vifusi.



Balaa jingine lamkumba mjumbe wa bodi TPA

$
0
0
Siku chache baada ya Rais John Magufuli kuvunja Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) kwa tuhuma za kushindwa kusimamia ipasayo shughuli za taasisi hiyo, mmoja wa wajumbe wake, Donata Mgassa amevuliwa uongozi wa kitengo cha manunuzi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Bodi ya TPA ilivunjwa Desemba 7 baada ya kugundulika kuwa zaidi ya makontena 2,670 yalipita Bandari ya Dar es Salaam bila kulipiwa kodi, hivyo kuikosesha Serikali mapato yake.

Kutokana na uzembe huyo, Rais aliivunja na kutengua uteuzi wa mwenyekiti wake, Profesa Joseph Msambichaka na katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dk Shaaban Mwinjaka huku mkurugenzi mkuu wa TPA, Awadh Massawe akisimamishwa kazi.

Licha ya Mgassa kuwa mjumbe wa bodi hiyo, pia alikuwa meneja wa idara ya manunuzi ya UDSM.

Alipotafutwa kuzungunzia sakata hilo, kwa ufupi Mgassa alisema: “Samahani, siwezi kulizungumzia hilo.”

Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala alithibitisha kuenguliwa kwa mjumbe huyo. “Ni mabadiliko ya kawaida ambayo yanalenga kuimarisha utendaji uliotukuka wa chuo kikuu hicho,” alisema na kuongeza kuwa:

Alishamaliza muda wake ndiyo maana tukaona ni vema tubadili damu. Tumeingiza damu mpya ili kuendana na kasi ya miradi tunayotarajia kuwa nayo.”

Bila kuhusisha kilichotokea TPA, Profesa Mukandala alisema mabadiliko hayo yamefanywa kuanzia Desemba 7, siku ambayo bodi ya TPA ilivunjwa na Rais Magufuli.

Taarifa zilizopatikana kutoka vyanzo vingine chuoni hapo vinaeleza kuwa huo ni utaratibu wa siku nyingi miongoni mwa watendaji wake waandamizi na kwamba yeyote ‘anayeharibu’ sehemu moja anakotumika akiwa mjumbe wa bodi chuo pia humwajibisha.

“Ni kanuni za chuo. Asingeweza kubaki. Mara tu baada ya Rais kuvunja bodi ya Bandari chuo nacho kilitangaza kumuondoa kwenye nafasi yake. Mtu mpya ameshapatikana na ameanza kuisimamia ofisi hiyo,” kilisema chanzo hicho. Mbali na Mgassa, wajumbe wengine waliokuwa kwenye bodi hiyo ni Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson, Dk Francis Michael, Crescentius Magori, Flavian Kinunda, Haruna Masebu, Gema Modu na Musa Nyamsibwa.

Prof. Lipumba Afunguka.....CHADEMA Wamepoteza Dira Baada ya Kumpokea Lowassa

$
0
0
Wakati akiongea kupitia AzamTwo Television, Prof. Lipumba amesikika akisema, CHADEMA kimepoteza dira ya kisiasa kutokana na mtafaruku uliojitokeza ndani ya UKAWA baada ya kumpokea Lowassa na kumfanya mgombea Urais wa Tanzania.

Prof. Lipumba amesema, ''Sisi ndani ya CUF tunaweza kukijenga vizuri chama chetu kwa sababu msingi wetu ni kusimamia haki kwa wote lakini wenzetu wa CHADEMA wamepoteza dira kwa sababu itakuwa ni vigumu kuzungumzia suala la mapambano dhidi ya ufisadi''.

''Msingi wa sera zetu ni Haki Sawa Kwa Wote, Rais Magufuli anasema HapaKaziTu na sisi tunasema Hapa ni Haki Tu'' Alisema.

Aliendelea kusema, ''Tuna mahala pazuri pa kuanzia, kutazama namna ya kuikosoa serikali katika kutekeleza hizi sera za HapaKaziTu, Je tunalinda haki za kila mmoja wetu, tunafuata utaratibu mzuri wa sheria''

Alimalizia kwa kusema, ''wenzetu CHADEMA wamepoteza dira''.


VIDEO

Marekani Yamuweka Rais Magufuli Njiapanda......MCC inakutana Kesho Huku Suala La Zanzibar Likiwa Bado Ni Kitendawili

$
0
0
Marekani imeiweka njiapanda Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, baada ya Bodi ya shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) kuamua kukutana kesho kujadili masuala kadhaa ya utoaji wa misaada kwa nchi zinazoendelea huku angalizo lake kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi.

Kwa mujibu wa ratiba ya MCC, kikao chao cha Bodi kitakutana kesho (Jumatano) na kupitia mapendekezo ya kupeleka misaada kwa nchi mbalimbali zinazoendelea.

Inaelezwa kuwa kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbi wa Holbrooke, saa 4:00 asubuhi kwa saa za Marekani.

Inatarajiwa kuwa kupitia kikao hicho, nchi zitakazokidhi vigezo zitakuwa na fursa ya kuidhinishiwa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyojipangia yenyewe kabla ya kupata fedha hizo.

Tanzania inasubiri kuidhinishiwa fedha za awamu ya pili za MCC Dola za Marekani milioni 472 (takribani trilioni moja).

Hata hivyo, kutokana na ratiba hiyo, Serikali ya Rais Magufuli inatarajiwa kuwa njiapanda kwani suala la Zanzibar lililokumbushiwa na MCC kupitia maelekezo yake yaliyoripotiwa mwezi uliopita, bado linaonekana kuwa kuendelea kuwa tete.

Hadi sasa, licha ya vikao mbalimbali vinavyoendelea kufanyika na kuwakutanisha wagombea waliokuwa wakichuana kwa karibu kabla ya uchaguzi huo kufutwa, Dk. Ali Mohamed Shein wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Maalim Seif Shariff Hamad wa Chama cha Wananchi (CUF), bado ufumbuzi haujapatikana.

CCM wanaamini kuwa uchaguzi huo ni lazima urudiwe baada ya kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, huku CUF wakisisitiza kuwa uchaguzi huo haukuwa na kasoro kubwa kiasi cha kufutwa wote na hivyo kutaka matokeo yatolewe na mshindi atangazwe kuwa Rais wa visiwa hivyo.

Awali, katika angalizo lake kwa serikali ya Magufuli iliyoingia madarakani Novemba 5, 2015, MCC ilitaka kupatiwa ufumbuzi kwa suala la Zanzibar na pia kuwapo kwa ufafanuzi juu ya watuhumiwa waliokamatwa kwa makosa ya mtandao wakati wa Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25.

Ilifahamika kuwa maelekezo ya MCC kwenda kwa mamlaka mbalimbali za serikali ya Tanzania, yalionyesha kuwa lipo tishio la kufutwa kwa msaada huo (trilioni moja) iwapo mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar hautapatiwa ufumbuzi na pia kutolewa ufafanuzi wa sheria ya makosa ya mtandaoni kabla ya kikao cha bodi ya MCC mwezi huu (Desemba, 2015).

 “MCC inafuatilia kwa karibu hatua zitakazochukuliwa na serikali ya Magufuli katika suala la utawala bora, katika kipindi hiki tunapokaribia kufanya kikao cha bodi ya MCC Desemba. Utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar kwa kuridhisha pande zote zinazohusika,” ilielezwa katika kile kilichodaiwa kuwa ni sehemu ya angalizo la MCC kwa serikali ya Tanzania na kuripotiwa Novemba, 2015.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, aliwahi kulitolea ufafanuzi suala hilo  Novemba 29, 2015, akisema kuwa Serikali haina wasiwasi kuhusu mashariti ya MCC juu ya Zanzibar kwani yatafanyiwa kazi kabla ya bodi ya MCC kukutana tena (Desemba).

Hata hivyo, hadi sasa hakuna muafaka uliotangazwa rasmi kuwa umefikiwa kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar huku pande zote zikiendelea kutoa msimamo tofauti; hali hiyo ikielezwa kuwa inaiweka njia panda serikali ya Magufuli kwani fedha za MCC ni muhimu katika utekelezaji wa ahadi zake mbalimbali, hasa juu ya dhamira ya kusambaza umeme na kuwaunganisha wananchi wengi katika gridi ya taifa.

Kadhalika, fedha za awamu ya pili za MCC ni muhimu pia katika uimarishaji wa taasisi zinazohusika na sekta ya nishati.

Akizungumzia hatari iliyopo sasa ya kukosa fedha za MCC baada ya suala la uchaguzi wa Zanzibar kutopatiwa ufumbuzi, Balozi Sefue alisema hakuna hofu yoyote (ya kukosa fedha) kwa sababu tayari kuna hatua kadhaa zimechukuliwa na Serikali ya Tanzania kushughulikia mambo yaliyohojiwa na MCC.

Akieleza zaidi, Balozi Sefue alisema taarifa ya MCC haikusema masuala hayo mawili yaishe vipi, bali walieleza yashughulikiwe; na kwamba hivi sasa yanaendelea kushughulikiwa na yanaendelea vizuri.

Alisisitiza kuwa Tanzania imefuata mashariti yote ya kupata fedha hizo kutoka MCC.

“MCC walituambia sisi kama serikali kuwa yaangalieni masuala haya, na siyo kwamba walituambia tuyashughulikie hadi tuyamalize ndipo watatupatia fedha … hilo siyo kweli,” alisema Balozi Sefue.

Aliongeza kuwa hadi sasa, hatua zilizofikiwa katika kutatua mgogoro wa Zanzibar na pia suala la wahalifu wa makosa ya mtandao, yote hayawezi kuikosesha sifa Tanzania kupata fedha hizo.

Taarifa: Ziara ya Edward Lowassa Kuwashukuru Watanzania kwa Kura Walizompigia

$
0
0
Taarifa inatolewa kwa vyombo vya habari na umma wa Watanzania kwa ujumla kuwa aliyekuwa Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Ndugu Edward Lowassa atazungumza na wananchi wa Tanga katika mkutano wa hadhara utakaofanyika mjini Tanga, siku ya Alhamis, Desemba 17, 2015.

Mkutano huo ni sehemu ya ziara ya viongozi waandamizi wa Chama na UKAWA kwa ujumla ambao watakwenda maeneo mbalimbali nchi nzima kuwashukuru wananchi kwa namna walivyounga mkono upinzani na agenda nzima ya MABADILIKO katika uchaguzi mkuu uliopita na wanavyoendelea kuweka matumaini yao kwa upinzani kuwa ndiyo nguzo imara wanayoweza kuitegemea kuwaletea mabadiliko ya kweli kwa ajili ya maendeleo yao na ustawi wa taifa kwa ujumla.

Itakumbukwa kuwa mbali ya Watanzania kupiga kura za ushindi katika nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu uliopita, wananchi waliwachagua wabunge wengi wa upinzani wanaotokana na UKAWA na kuongeza nguvu kubwa ndani ya bunge hususan kupitia Kambi ya Upinzani Bungeni ambayo itakuwa serikali yao mbadala huku wakiviamini vyama hivyo kusimamia na kuongoza halmashauri zipatazo 34 nchi nzima, ikiwa moja ya misingi imara katika kupigania mabadiliko ambayo Watanzania wanayataka.

Wananchi wanastahili shukrani kwa imani hiyo kubwa ambayo ni ishara ya wazi kuwa matumaini yao kwa miaka mingine mitano yatasimamiwa na kuongozwa na upinzani imara kupitia UKAWA.

Katika ziara hiyo ya Tanga, Ndugu Lowassa ataambatana na viongozi wengine waandamizi wa UKAWA ukiwa ni mwanzo tu wa ziara kubwa itakayokwenda nchi maeneo mbalimbali nchi nzima.

Imetolewa leo Jumanne, Desemba 15, 2015 na;

Tumaini Makene

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Nimekonda Sababu Nafanya Sana Mapenzi– Huddah Monroe

$
0
0
Huddah Monroe ni mwanamke anayetumia muda mwingi kusafiri katika nchi mbalimbali na kula bata.

Lakini kingine ambacho anakifanya mara kwa mara ni kula uroda… mara tano, mara sita kwa siku? Jibu analo mwenyewe lakini amekiri kuwa mwili wake umepungua sababu anavunja amri ya sita mara nyingi mno!

Mrembo huyo alipost picha ya kitambo na kuandika:

#TBT! I miss my body like this ! Sema kukonda these past months? Been up and down like an athlete, paper chasin see_no_evil and maybe too much SEX??”
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images