Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104427 articles
Browse latest View live

Marekani Kupitia Shirika la MCC Yainyima Mabilioni Ya Pesa Tanzania Kutokana na Mzozo wa Uchaguzi Zanzibar

0
0
Tamko kutoka kwa Balozi Mark B. Childress kuhusu uamuzi wa Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia kuahirisha kupigia kura mkataba wake na Tanzania
 *********

Tarehe 16 Disemba, Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) haikuichagua Tanzania kwa mkataba wa pili. Bodi iliahirisha kupigia kura mkataba wa pili, ikisubiri kutatuliwa kwa masuala ya kiutawala.

Bodi inaweza kuangalia upya ustahilifu wa Tanzania mwaka 2016. Ninatumaini kwamba Serikali ya Tanzania itachukua hatua hivi karibuni zitakazotatua masuala hayo ya kiutawala. Halafu, Bodi itaweza kupiga kura kuichagua tena Tanzania na kuidhinisha maendeleo ya mkataba.

Masuala ya kiutawala ya Bodi yanaakisi maadili ya muda mrefu ya MCC. Kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar kulisitisha mchakato wa uchaguzi uliokuwa unaenda vizuri na kwa amani.

Matumizi ya Sheria ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015 kuwakamata watu waliokuwa na kibali halali kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi yalikwaza uhuru wa msingi wa kujieleza na kukutana.

MCC imetiwa moyo na hatua zilizochukuliwa hivi karibuni na Rais Magufuli za kuimarisha vita dhidi ya ubadhilifu na rushwa. MCC inatumaini kuwa jitihada hizo zitaendelea na kuleta mabadiliko ya kimfumo.


Nafasi za Kazi 

TCRA imetoa miezi sita hadi June 16, 2016 kuzifunga simu zote feki Tanzania

0
0
TCRA imetoa miezi Sita hadi June 16, 2016 kuzifunga simu zote feki Tanzania.

Hakiki namba yako mapema (angalia video) ukigundua simu yako ni feki ibadilishe kabla ya June 2016! Chukua hatua usisubiri.

Utaratibu huu pia utasaidia kufunga simu iliyoibiwa Au kupotea. Ukiibiwa simu yako toa taarifa Polisi, chukua RB na toa taarifa kwa mtoa huduma wako. 

Simu itafungwa ndani ya saa 24! 

Haitaweza kutumika tena!

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi yaa Disemba 19, Ikiwemo ya Wahuni Kumpiga Chenga Magufuli

Aliyekuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dr Edward Hosea, Kutema Cheche

0
0
Aliyekuwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dr Edward Hosea, anatarajiwa kutapika cheche wakati wowote kuanzia sasa kwa lengo la kutumbua majipu ya vigogo wa serikali na makada waliokuwa wakimfunga mikono na miguu wakimzuia kufanya kazi yake kwa ufasaha na umakini unaotakiwa.

Katika cheche zake hizo, mtaalamu huyo wa masuala ya rushwa na ufisadi, ataweka hadharani majina ya vigogo na makada wa chama waliokuwa wakimchimba mkwara na kuwaachia wafanye yao ili kulinda kibarua chake tukufu.

Katika orodha hiyo ya Dr Hosea wamo watu wazito kutoka serikalini waliokuwa wakimuandikia vimemo mara kwa mara wakati wanapopitisha makontena yao bila kulipia ushuru na kuikosesha serikali mabilioni ya shilingi za mapato.

Aidha, inasakikiwa kwamba kwenye orodha pia wamo wauza unga na majangili wakubwa waliokuwa wakipitisha unga na vipusa mtawalia, kupitia banadari ya Dar es Salaam bila kuguswa na mtu yeyote. Pia wamo vigogo waliomshika mikono wakati anashugulikia skandali ya EPA, ESCROW na nyinginezo.

Mtakumbuka kwamba kuna kada mmoja wa ngazi ya juu anayetajwatajwa sana kuhusika katika biashara haramu ya meno ya tembo ambaye meno hayo yalipatikana yamepakiwa kwenye meli yake siku za nyuma yakiwa yamesafirishwa hadi nchi za mbali.

MAONI YANGU
Magufuli jiandae kwenda mbali zaidi kushughulikia waliotoa vimemo, kwa muktadha huo utakuwa umeiteketeza CCM nzima kuanzia juu mpaka chini.

Source:Jamii Forums

Kauli Ya Mwenyekiti Freeman Mbowe Kuhusu Uamuzi Wa Bodi Ya MCC Kuzuia Msaada Wake Wa Trilioni 1 Kwa Serikali Ya Tanzania

0
0
Muda mfupi baada ya Bodi ya MCC kutoa taarifa inayoonesha Tanzania haitapata msaada kutoka shirika hilo kama ilivyotarajiwa kwa ajili ya mwaka 2016, Mwenyekiti wa Chama (T), Freema Mbowe ametoa kauli nzito juu ya suala hilo akisema kuwa kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote iliyo chini ya ufadhili wa MCC.

MCC imeahirisha msada huo wa USD Mil. 472.8 ambazo ni takriban trilioni moja kwa fedha za Tanzania zilizolengwa kusaidia sekta ya nishati ya umeme hususan ule wa vijijini, katika kuunganisha wateja wapya, mabadiliko ya kimuundo ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO) ili lifanye kazi na kutoa huduma kwa ufanisi katika sehemu za uzalishaji, usafirishaji na usambazaji.

Fedha hizo pia zilikusudiwa kusaidia kuanza kwa mpango mkubwa wa kuboresha sekta ya umeme nchini.2014-2024.

Mbowe amemtaka Rais John Magufuli kuchukua hatua za haraka za kiuongozi kumaliza mtanziko wa kisiasa Zanzibar kwa mshindi wa nafasi ya urais kutangazwa kutokana na uchaguzi uliofanyika mwezi Oktoba, mwaka huu.

Aidha amesema kuwa Sheria ya makosa ya mtandao (Cyber Crime Act 2015) ambayo ni mojawapo ya sababu zilizotumiwa na MCC kuahirisha msaada huo kwa Tanzania hadi itakapokuwa imefanyiwa kazi, ni sheria mbaya sana inayokinzana na kukua kwa technologia ya habari na mawasiliano na kuzuia upashanaji wa habari miongoni mwa jamii ambayo ililenga kuweka makosa ya kijinai ili kudhibiti wapinzani wa CCM katika uchaguzi mkuu na kukipatia mazingira ya ushindi chama hicho.

"Sasa imethibitika kuwa Bodi ya MCC iliyokaa tarehe 16 Dec 2015 imeahirisha rasmi kuidhinisha msaada wa Millenium Challenge uliokuwa umekusudiwa kwa Tanzania kwa mwaka wa fedha 2016. Sababu kuu mbili zilizosababisha uamuzi huo ni:

1. Mkwamo wa Uchaguzi wa Rais na Wawakilishi Zanzibar na
2.Matumizi mabaya ya she ria ya makosa ya mtandao hususan kuhusiana na uchaguzi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa 2015."

"Ubabe wa baadhi ya viongozi wa CCM ni janga la Taifa. Kuchelewa kupatikana kwa fedha za MCC si tu kunachafua jina la nchi na hadhi yake katika medani za kimataifa, bali kutaathiri kwa kiasi kikubwa miradi yote iliyo chini ya ufadhili wa MCC," amesema Mwenyekiti Mbowe na kuongeza;

"Sheria ya makosa ya mtandao (Cyber Crime Act 2015) ni sheria mbaya sana inayokinzana na kukua kwa technologia ya habari na mawasiliano. Aidha, kwa makusudi kabisa inafifisha uhuru wa kupashana habari na ni dhahiri ilitungwa kwa nia mbaya ya kuthibiti kijinai uchaguzi mkuu.

"Tuliipinga sheria hii Bungeni na ikapitishwa usiku wa manane kwa ubabe wa wabunge wa CCM na hata tulipomtaka rais Kikwete asiisaini aliisaini kibabe akijua anaandaa mazingira gani ya "kihalifu", " amesema Mwenyekiti Mbowe.

Ameongeza kusema kuwa sheria hiyo ilitumika kuvamia vituo vya CHADEMA vilivyokuwa vikitumika kukusanya matokeo ya kura za rais na wabunge na hadi leo vijana zaidi ya 161, wakiwemo wanafunzi, wana kesi za "kubumba" mahakamani.

Mwenyekiti Mbowe amesema kuwa Sheria hiyo hiyo ilitumika kuficha dhana ovu iliyotumika kuhalalisha kuvamia Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kilichokuwa kikiratibu watazamaji wa uchaguzi wa ndani kwa kibali cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

"Vile vile Sheria hii imetumika kuwakamata na kuwaweka ndani na hata kuwanyima dhamana vijana wetu ambao walituunga mkono katika uchaguzi mkuu.

"Namtaka rais Magufuli achukue hatua za kiuongozi na kiutawala kwa kufanya yafuatayo:

"Kwanza aumalize    mgogoro wa kisiasa Zanzibar kwa kuhakikisha kuwa mshindi halali anatangazwa.

"Pili achukue hatua ya kuifanyia marekebisho makubwa Sheria ya makosa ya mtandao katika bunge lijalo. Aidha wale wote waliobambikiwa kesi amuamuru DPP kuzifuta kesi hizo mara moja," amesema.

Mwenyekiti Mbowe amesisitiza kuwa Rais Magufuli hana budi kuchukua hatua hizo za haraka ili kulinusuru taifa na hasara ya kupoteza mabilioni hayo ya MCC na zaidi kuepusha kuporomoka zaidi kwa biashara ya utalii nchini Zanzibar.

Amesema katika taifa ambalo sekta ya umeme inakabiliwa na matatizo makubwa katika uzalishaji, usambazaji na usafirishaji huku wananchi wa kipato cha chini wakibebeshwa mzigo mkubwa wa kumudu nishati hiyo na wengine wakilazimika kutumia nishati mbadala kama mkaa unaotokana na miti hivyo kusababisha uharibifu wa mazingira, serikali inayojua wajibu wake yenye viongozi wanaothamini uwajibikaji, haikupaswa kushindwa kuchukua hatua stahiki kutimiza vigezo vya msaada huo ambao umeshaisaidia Tanzania katika miradi mingine kadhaa.

Imetolewa  Ijumaa, Desemba 18, 2015 na;

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Diamond Platnumz Aikacha Party ya Zari All White Ciroc Party, Ex wa Zari na Wapambe Wake Wahuzuria, Picha Hizi Hapa

0
0


Wana watoto watatu pamoja na wana biashara kibao za pamoja, hivyo ni ngumu kwa Zari na mume wake wake wa zamani, Ivan kupotezeana licha ya kila mmoja kuchukua njia yake kimahusiano.

Ivan na jamaa zake wa Rich Gang wakila bata kwenye Zari All White Party

Ndio maana Ivan na mpambe wake King Lawrenc walisafiri kutoka SA na kwenda kumuunga mkono Zari ambaye Alhamis hii aliandaa party yake ya kila mwaka ya mavazi meupe tu kwenye kiota cha Guvnor kilichopo Kampala Uganda.


Zari All White Ciroc Party
Zari All White Ciroc Party

ZARI8912ZARI834ZARI234ZARI734


ZARI0923


ZARI13

ZARI90

Majanga Yazidi Kukikumba Chuo cha IMTU, Yapewa Siku 14 Kuhama Majengo ya NDC

0
0
Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Teknolojia na Tiba (IMTU), kimeingia katika sakata jipya la kuamriwa kuhama ndani ya siku 14 kutokana na kushindwa kulipa kodi ya zaidi ya Sh3 bilioni.

Amri hiyo imekuja baada ya mpangishaji wa IMTU ambaye ni Shirika la Maendeleo la Taifa(NDC) kupeleka notisi kupitia kwa kampuni ya mnada ya Fosters Auctioneers & General Traders, ya kuondoka katika ploti namba 2348 iliyopo Mbezi Beach jijini hapa.

Jerome Msemwa, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Uwakili ya Msemwa & Advocates inayoiwakilisha NDC, alisema jana kuwa IMTU ilisainiana mkataba wa upangishaji na shirika hilo kwa Sh100 kwa mwaka kuanzia mwaka 1996 kwa miaka 15 hadi Agosti, 2011 na tangu hapo chuo hicho hakikulipa kodi yoyote kwa mpangishaji wake.

“Hadi sasa NDC inadai jumla ya Sh3.06 bilioni kama deni la kodi ya kuanzia Agosti, 2011 hadi Septemba, 2015 kwa kodi ya Sh73 milioni kwa mwezi,” alisema Msemwa akieleza kuwa nakala za notisi hiyo imesambazwa katika taasisi mbalimbali zikiwemo Ikulu na vyombo vya habari.

Agizo hilo ni pigo jingine kwa uongozi wa IMTU ambao utalazimika kutafuta eneo mbadala kuendeleza masomo kwa wanafunzi wa chuo hicho, ambao tangu Julai mwaka jana wamejikuta wakisoma katika mazingira magumu.

Itakumbukwa kuwa Serikali iliwahi kuifungia hospitali ya chuo hicho Julai, 2015 kutokana na kutotimiza masharti na taratibu za uendeshaji.

Sakata hilo ilikuwa ni sehemu ya mfululizo wa balaa zilizokuwa zikiikumba IMTU, baada ya viungo vya binadamu ambavyo hutumika kufundishia madaktari kukutwa vimetupwa eneo la katika msitu uliopo Bunju wakati huo.

Notisi hiyo ilisema kuwa IMTU tangu Septemba 2012 ilikuwa ikipeleka mashauri mahakamani ya kupinga kuondolewa katika eneo hilo, lakini Septemba 2014 Mahakama Kuu ya Tanzania iliyotoa amri ya mpangaji huyo kuondoka, ambaye hata hivyo hakutekeleza.

“Unatakiwa kuondoka katika eneo hilo linalomilikiwa na NDC na kulipa madeni yote haraka iwezekanavyo.

“Zingatia kuwa ukishindwa kuhama ndani ya siku 14 kuanzia tarehe ya notisi hii, tumepatiwa maagizo ya kukuondoa kwa nguvu bila taarifa yoyote na kushikilia mali zako zote ili kuweza kulipia madeni hayo,” ilisomeka notisi hiyo.

Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU, Profesa Yassin Mgonda alisema hajapata notisi hiyo na kueleza kuwa huenda imeufikia uongozi wa juu hasa mmliki na mwenyekiti wa chuo hicho, Katuri Subbarao.

“Siwezi kusema nimejiandaeje kuondolewa wakati sina taarifa yoyote na mtu aliyeachiwa madaraka yupo likizo. Ila nafahamu kuwa kulikuwa na mgogoro wa muda mrefu wa masuala ya kulipana na mambo yalikuwa hayajakaa vizuri,” alisema Profesa Mgonda.

Nafasi za Kazi Real Insurance, Application Deadline: 31 Dec 2015

0
0

Kampuni ya Real Insurance Imetangaza Nafasi za Kazi
 Application Deadline: 31 Dec 2015

Bonyeza HAPAKusoma Na Kuapply


Majipu ya Tanesco Yaendelea Kutumbuliwa...Wengine 10 Wasimamishwa Kazi Kwa Upotevu wa Mapato zaidi ya Sh Mil 100

0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme (Tanesco), Felchesmi Mramba, amewasimamisha kazi maofisa 10 wakiwamo wahasibu waandamizi na mafundi kwa kusababisha upotevu wa mapato zaidi ya Sh.milioni 100.

Hasara hiyo ilitokea katika mfumo wa mita kupitia minara ya simu za mkononi na faini Sh. milioni 198.1 za wateja waliobainika kuiba umeme kwa kuchakachua mita zao.

Hata hivyo, shirika hilo limefanikiwa kuokoa fedha hizo zilizotokana na umeme wenye thamani ya Sh. 100,248,386.42 uliotumika bila kulipiwa pamoja na faini kutoka kwa wateja waliojihusisha na wizi wa umeme Sh.
198,105,928.68.

Kadhalika, shirika baada ya kufanya msako mkali limefanikiwa kukamata taasisi binafsi na za serikali pamoja na watu binafsi wakijihusisha na kuhujumu shirika hilo,ikiwemo Shule ya Sekondari ya Jangwani (Sh. 11,023,238.00), Diwani wa Kata ya Sinza C, Joseph Marandu (Sh. 3,443,555.00), Royal Oven Bakery Kawe, (Sh. 4,112,614.00), Havan Hotel, Mbezi Beach (Sh.1,847,913.00) na Kampuni ya Simu ya Viettel Mtwara (Sh. 524,554.76).

Wengine ni, Kampuni ya Saffa Petroleum ya Mkoani Pwani (Sh. 16,105,235.00), Msanii wa Filamu Nchini, Wema Sepetu (Sh. 8,200,496.20) na Kampuni ya Leadcom (Sh. 13,694,632.81).

“Zoezi hili ni endelevu kwa nchi nzima na tutaendelea kuwakamata, kuwatangaza na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale watakaobainikiwa kulihujumu shirika hatutaogopa wadhifa wala umaarufu wa mtu ama taasisi” alisema Mramba katika mkutano wake na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.

Alisema mapema Desemba 6, mwaka huu alitoa taarifa kwa wale wote wanaojihusisha na wizi wa umeme ama wenye mita zenye matatizo, lakini walijisalimisha ni watu 30 na kati ya watu 2,156 waliokaguliwa 138 walikutwa na dosari mbalimbali katika mita zao na walilipishwa faini.
 
Akifafanua, alisema fedha zinazotakiwa kulipwa ni Sh. milioni 198.1 na zilizokwishalipwa ni Sh. milioni 44.9 wakati waliofikishwa kwenye vyombo vya sheria ni watu 37 kwa makosa mbalimbali. Akizungumzia kuhusu hatua atakazowachukulia watumishi 10 aliowasimamisha kazi, Mramba alisema uchunguzi unaendelea na fedha wanazodaiwa kuzifanyia udanganyifu zitalipwa na kampuni ya simu husika.

Mramba alisema ili kuhakikisha kero za huduma zinamalizika, katika kila ofisi ya kitengo cha dharula kutakuwa na  Ofisa wa huduma kwa wateja na mhandisi ambao watasimamia muda na ubora wa huduma wanazopata wateja baada ya kutoa taarida za dharura.

“Kuanzia sasa kazi ya mafundi inapokamilika maofisa hawa niliowataja watawajibika kuwapigia simu wateja waliotoa taarifa kuhakiki kama kazi zimefanywa kwa wakati na mteja ameridhika … utaratibu huu utaanza leo (jana),” alisema Mramba.

Mbunge Peter Msigwa Amrushia Dongo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda..Ni Baada ya Picha Amkimfunga Kamba za Viatu Ridhiwani Kuzagaa

0
0
 Mbunge Peter Msigwa Amrushia Dogo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda..Ni Baada ya Picha Amkimfunga Kamba za Viatu Ridhiwani Kuzagaa

Ameposti picha hii hapa chini Paul Makonda akimfunga Ridhiwani Kamba za viatu
na Kuandika "Hivi Ndivyo U DC Unavyopatikana, Kujikomba Komba"


Taasisi 1,200 Duniani Zampa Tuzo ya Amani Edward Lowassa

0
0
Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya Amani kutokana na utulivu aliouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu.
Akizungumza kutoka Bukavu, DR Congo, mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Lowassa amechaguliwa jana mjini Bukavu na wajumbe 1,400 wa mkutano huo.

Mwamalanga alisema wajumbe wanaohudhuria kongamano la amani wanatoka mataifa ya Ulaya, Marekani, Asia na Afrika kwa kuwashindanisha wanasiasa 1,000 ili kumpata Kiongozi Bora wa Amani mwaka 2015, ambaye anajali na kuangalia maslahi ya jamii badala ya madaraka.
Hatua ya kumpatia tuzo Lowassa ni baada ya kuelezwa kuwa amedumisha amani hiyo hata baada ya kushindwa uchaguzi Mkuu wa Rais Oktoba 25.

Katika uchaguzi uliopita, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)ilimtangaza Dk John Magufuli kuwa mshindi kwa kupata kura 8,882,935 ikiwa ni asilimia 58.46 wakati Lowassa alipata kura 6,072,848 sawa na asilimia 39.97 ya kura zote.

Mchungaji Mwamalanga alisema katika kongamano hilo, wajumbe walijadili hali ya amani duniani na mchango wa wanasiasa katika kulinda amani hiyo.
Alisema kuwa wanasiasa barani Afrika wamekuwa vyanzo vya migogoro na mauaji ya raia wakati wa uchaguzi, kama ilivyo nchini Burundi. Hata hivyo, alisema kuwa wajumbe walipongeza ushindi wa Dk Magufuli, lakini wakasema umetiwa dosari na hali ya kisiasa Zanzibar baada ya matokeo kufutwa.

Alisema wajumbe wa kongamano hilo linaloshirikisha maaskofu, masheikh na vijana kutoka madhehebu mbalimbali ya dini barani Afrika, wamemuhimiza Rais Magufuli kumaliza utata wa uchaguzi wa Zanzibar.

Baada ya kupitishwa kugombea urais kwa tiketi ya Chadema, Lowassa alitangaza kuwa angefanya kampeni kistaarabu na kwa amani na baada ya matokeo aliwatuliza wafuasi wa chama hicho, akisema “hakuna anayeweza kuizuia bahati ya mtu” kwa hiyo kama amepangiwa kuwa rais, atakuwa.
Lowassa, ambaye ni Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, aliongeza upinzani kwenye uchaguzi wa mwaka huu baada ya kuihama CCM na kujiunga na Chadema iliyoukuwa na nguvu ya vyama vingine vitatu vya NLD, CUF na NCCR-Mageuzi.
Kama alivyoahidi, Lowassa hakutumia mikutano yake ya kampeni kushambulia mambo binafsi ya wagombea wengine, bali muda mfupi kuomba kura.

Picha za Shoo ya Diamond Platnumz Alivyowasha Moto Kwenye Concert Nchini Uganda..Zari Naye Alikuwepo

0
0
Usiku wa jana msanii Diamond Platinum alitumbuiza kwenye tamsasha kubwa ‘Born 2 Win Concert’ jijIni Kampala, Uganda.
Mbali na Diamond msanii Patoranking naye alitumbuiza kwenye tamasha hilo.

Hizi ni baadhi ya picha za Diamond akitumbuiza kwenye tamasha hilo.
DIAMOND13
Diamond1341DIAMOND134DIAMOND288DIAMOND186

Kilichomponza Dk. Mwaka Chafichuka..Nimekuwekea Hapa A to Z

0
0
Stori: Deogratius Mongela na Chande Abdallah
SIRI nje! Sakata la mmiliki wa Kliniki ya Tiba Asilia ya Fore Plan iliyopo Ilala Bungoni, Dar, Dk. Juma Mwaka ‘JJ Mwaka’ kufanyiwa ziara ya kushtukiza na baadaye kudaiwa kumkimbia Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Hamis Kigwangalla limechukua sura mpya huku mambo mengi yaliyomponza yakifichuka, Risasi Jumamosi limechimba.
DSC_0004Dk. Kigwangalla akiingia kwenye Kliniki ya Tiba Asilia ya Fore Plan.
SOO LILIVYOKUWA
Siku chache baada ya kuteuliwa kuwa naibu waziri, Dk. Kigwangalla alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho kinachosifika kwa kutoa tiba ya asili badala ya hospitali (tiba mbadala), hasa kwa wanawake wanaosumbuliwa na matatizo ya uzazi.
Katika hali ya kushangaza, matatibu na manesi waliokuwa kazini walitokomea kusikojulikana na kuwatelekeza wagonjwa, wakikwepa kuonana na waziri huyo ambaye akiwa na msafara wake, walifanya ukaguzi wa kina kwenye kituo hicho.
Kufuatia kitendo cha Dk. Mwaka na wenzake kuingia mitini, Waziri Kigwangalla alitoa amri ya kufungwa kwa muda kwa kituo hicho mpaka uchunguzi wa kina utakapokamilika ili kuona kama huduma zinazotolewa zinakidhi vigezo na ni salama kwa wagonjwa.
MWAKA (1)Nyumba ya Dokta Mwaka JJ 
MITANDAO YAMCHOMA
Simulizi ya jinsi tabibu huyo alivyosimamishwa kutoa huduma ili kupisha uchunguzi na ukaguzi wa kina, inaanzia mbali ambapo kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya kuaminika, chokochoko kuhusu huduma zake zilianzia kwenye mitandao ya kijamii.
“Kwa kipindi kirefu kulikuwa na makundi mawili yanayoshindana kwenye mitandao ya kijamii. Kundi la kwanza ni wale waliowahi kutibiwa katika kliniki hiyo na kufanikiwa kupona matatizo yao.
MWAKA (2)
“Hawa walikuwa wakimtetea kwamba anatoa huduma sahihi lakini kundi jingine ni wale waliotibiwa na kupoteza fedha nyingi bila kupona matatizo yaliyokuwa yakiwasumbua.

“Hawa ndiyo waliochangia kwa kiasi kikubwa kuifumbua macho Serikali ya Rais John Pombe Magufuli kwani walitaka dawa na huduma za Dk. Mwaka zichunguzwe kwa vile walishapoteza imani naye,” kilisema chanzo chetu makini kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.
MWAKA (4)Gari lake, ania ya Range Rover-Sport SE
KUANIKA MAISHA YAKE MTANDAONI
Kwa mujibu wa chanzo kingine, tabia ya Dk. Mwaka kupenda kuanika maisha yake kwenye mitandao ya kijamii ni suala jingine lililomponza na kufanya watu waanze kutilia shaka utajiri wake.
“Unajua Dk. Mwaka na mkewe wamekuwa wakiposti kwenye mitandao ya kijamii, hasa Instagram picha za magari yao ya kifahari anayomiliki likiwemo Range Rover-Sport SE na hekalu (jumba kubwa la ghorofa) analoishi, lipo Mbezi (Dar).
“Pia walikuwa na kawaida ya kujisifia wanaposafiri kwenda nje ya nchi kufanya shopping, hasa Dubai. Hicho pia kimemponza sana maana watu walianza kufuatilia utajiri wao na pengine ndiyo waliomchongea serikalini,” kilisema chanzo hicho kilicho karibu na familia hiyo.
1
VIPINDI RUNINGANI

Sababu nyingine inayotajwa na vyanzo vyetu kwamba imemponza tabibu huyo, ni ile kawaida yake ya kuendesha vipindi kwenye runinga, akieleza huduma anazozitoa kwa lengo la kupata wateja wengi.
“Unajua Dokta Mwaka ndiye anayeongoza kwa kuwa na vipindi vingi vya runinga kwenye televisheni mbalimbali nchini. Kama unavyojua kipindi kimoja cha runinga kulipia kinagharimu fedha nyingi sana. Sasa watu wakawa wanajiuliza anapata wapi fedha za kulipia gharama hizo? Ni kutoka kwa wateja wake kweli?” kilisema chanzo chetu.
DSC_0089
KUPUUZA AGIZO LA WIZARA

Pia, habari za ndani zinadai kuwa, mwaka jana wizara husika iliwaita wataalam wote wanaotoa tiba mbadala na kuwapa masharti.
Masharti hayo ni kutovaa koti jeupe, kutoning’iniza shingoni chombo cha kusikilizia mapafu/mapigo ya moyo (stethoscope) na kutojiita madaktari wakitakiwa kutumia utambulisho wa tabibu masharti ambayo karibu wote wameyapuuza.
dk mwaka na diamond
KUNA KOSA KUJITANGAZA?

Katika utafiti uliofanywa na gazeti hili na kutiliwa nguvu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu imebainika kwamba, kwa mujibu wa viapo wanavyokula madaktari na matabibu ni makosa kujitangaza kwenye redio, runinga au mitandao kwa lengo la kuwavuta wagonjwa.
“Changamoto iliyopo kwetu ni kwamba matangazo wanayoyatoa ni kinyume na kanuni lakini tumebaini kwamba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo inasimamia sekta ya mawasiliano na utangazaji nchini ndiyo inayoruhusu. Tumejipanga kukutana nao ili kujadili jambo hili,” alisema Mwalimu.
SIYO MARA YA KWANZA KUFUNGIWA
Tukio hili la kusimamishwa kutoa huduma, si la kwanza kumtokea Dk. Mwaka ambapo mwaka jana, maafisa kutoka wizara ya afya walifika kwenye kliniki hiyo kwa kushtukiza, wakiwa wameongozana na waandishi wa habari na kufanya ukaguzi ambapo kutokana na kutoridhishwa na mazingira waliyoyakuta, walilazimika kuifunga kliniki hiyo kwa muda usiojulikana.
Hata hivyo, wiki kadhaa baadaye, Dk. Mwaka alifungua kesi mahakamani kupinga kufungiwa huko na kushinda kesi.
GPL

Exclusive: Ben Pol Aeleza Kwanini Alimuandikia Alikiba Tweet iliyozua Utata Mkubwa!

0
0
Ali Kiba na Ben Pol
Ben Pol amesema tweet ya utata aliyomuandikia Alikiba, alikusudia kumtumia kwenye ujumbe wa siri wa mtandao wa Twitter (DM) lakini akakosea na kuiweka wazi!

Juzi kupitia mtandao huo, Ben Pol alimuuliza Alikiba swali, “Bro @OfficialAliKiba mi naona kama unakuwa overrated halafu inakugharimu.. au Haikugharimu?”

Ben Pol ameiambia Bongo5 kuwa wasanii wamekuwa wakiambiana ukweli kuhusu muziki na maisha yao ili kuwekana sawa.

Ile tweet kwanza nilikuwa nataka iende DM,” alisema.
“Unajua sisi wasanii tunaongeaga tu, mtu anaweza akakwambia ‘mwanangu mbona hauna kiki.’ Kwahiyo mimi nilikuwa naipeleka ile tweet DM, lakini nikaipost kimakosa ikaenda public,” alifafanua.

“Mimi pale kitu kimoja kimenichanganya, watu wengine wamesema poa, wengine wanasema hapana, wengine wanatukana kwahiyo kwa kifupi hali imekuwa tafrani.

Sasa Ali alivyoona labda na yeye amelipokea vibaya baada ya kuona nimeweka public ndio maana akajibu namna ile. Kwa sababu hajanipigia akaniuliza mbona mwanangu umeandika hivi? Ila yeye aliona kama noma na iwe noma. Mimi haijanigharimu, labda kwa sababu watu wanaandika vibaya kwenye mitandao ya kijamii lakini hii ni kawaida lakini nachotaka watu wajue nilitaka tweet iende DM. Sijawahi kugombana naye, hatupo pamoja mara nyingi lakini tupo pamoja,” aliongeza.

Katika hatua nyingine Ben Pol amewataka mashabiki wake kuitazama video ya wimbo wake ‘Ningefanyaje’ aliyoiachia wikiendi hii.

Source:Bongo5

Nafasi za Kazi 

Jeshi Lawasaka Watu Walioeneza Uzushi Mtandaoni Kuhusu Vyeti Feki Vya Polisi

0
0
Katika siku za hivi karibuni, kumeibuka tabia ya baadhi ya watu kutoa taarifa za uzushi na uongo kutumia majina ya taasisi, mashirika ya umma na ofisi za Serikali na kueneza taarifa hizo  katika mitandao ya kijamii kwa lengo la kupotosha wananchi.

Miongoni mwa taarifa hizo ni pamoja na taarifa kuhusu Jeshi la Polisi iliyosambazwa jana katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari  ‘chujio Jesho la polisi, vyeti feki vyawaonndoa askari kazini’  Taarifa hiyo ni uzushi na haijatolewa na Jeshi la Polisi.

Kufutia hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini linapenda kukanusha taarifa hiyo  ya uzushi ambayo haina ukweli wowote  na inalengo la kuchafua taswira ya Jeshi la Polisi kwa jamii.

Jeshi la Polisi nchini limeanza upelelezi wa kuwatafuta watu wote waliohusika kueneza taarifa hiyo na kujifanya wao ni Jeshi la Polisi.

Aidha, Tunatoa onyo kali kwa watu  wote kuacha kutumia mitandao ya kijamii vibaya  kwa kufanya uposhaji na badala yake watumie mitandao hiyo kwa ajili ya ustawi wa jamii.

Imetolewa na:
Advera John  Bulimba – SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.

Mimba ya Jokate Aliyopewa na Mwimbaji Ali Kiba Yadaiwa Kuchoropoka

0
0
IMEFICHUKA! Ile mimba ya mwanamitindo maarufu Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ iliyokuwa ikisemekana ni ya Mbongo-Fleva, Ali Saleh Kiba inadaiwa kuharibika kwa kuchoropoka kisa kikiwa ni mazoezi makali aliyoyafanya hivi karibuni.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kwamba, Jokate kwa sasa hana ujauzito tena kwani ulichoropoka kufuatia mazoezi makali ya kujiandaa na shoo aliyofanya ya Nyama Choma Festival kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar iliyosapotiwa na mpenzi wake huyo.

Kama mlikuwa hamjui kitumbo cha Jojo (Jokate) kilichoropoka kutokana na mazoezi makali ya shoo aliyoifanya hivi karibuni ambapo kwa sasa anaendelea vizuri na anafanya kazi zake kama kawaida bila ujauzito,” kilinyetisha chanzo hicho.

Baada ya kupata habari hizo, paparazi wetu alimtafuta Jokate na kumuuliza kuhusu ujauzito wake ambapo alijibu kwa ufupi: “Kwa sasa mimi sina mimba.”

Hata hivyo, chanzo hicho kiliendelea kueleza kwamba, kwa sasa Kiba anajipanga upya katika masuala hayo ya kupata mtoto na mrembo huyo.

Chanzo: Global Publishers

Tanesco Wataja Kiasi Wanachomdai Wema Sepetu Kufuatia Kuiba Umeme! Nimekuwekea Hapa Uone

0
0
Tanesco wako shingoni kwa Wema Sepetu!

Hivi karibuni walifanya ziara ya kushtukiza kwenye nyumba yake na kubaini kuwa muigizaji huyo anatumia umeme wao bure!

Jana Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Eng. Felichesmi Mrambaalizungumza na waandishi wa habari na kutaja kiasi cha fedha kitakachopatikana kutokana na faini waliyowapiga wezi mbalimbali wa umeme.



Imebainika kuwa Wema Sepetu anadaiwa shilingi 8,200,496.20.

Nafasi za Kazi 
Bonyeza www.ajirayako.com

Huyu Jerry Muro Ana Matatizo Gani Jamani? Angalia Video Jinsi Alivyoropoka Maneno Yaliyowasikitisha Wengi...

0
0
Jerry Muro
Jana katika Press Conference pale Jangwani msemaji wa klabu ya yanga jerry muro hakika alitufanya watu wenye akili zetu tena zilizotukuka tuwe na mashaka nae ya kitaaluma na kiuweledi kutokana na kile alichokifanya ambacho nashukuru hakikumfurahisha kila mtu aliyekuwepo pale na hasa hasa wana Yanga wenzake wale wenye uwezo wa kuchambua masuala.

Hivi ni kweli Jerry Muro anajua majukumu hasa ya afisa habari au afisa uhusiano au meneja mahusiano au kurugenzi ya habari, uhusiano na mawasiliano?

Yaliyonifanya hadi nikaamua kuanzisha huu uzi ni kitendo chake ambacho binafsi naweza kukiita ni kama vile ameibaka taaluma na ikiwezekana upesi na haraka sana atuombe radhi wana taaluma na hapa ndipo tutapima uimara wa uongozi wa klabu ya Yanga kama utamwajibisha au na wenyewe utaungana nae Jerry Muro.

Jana pale mkutanoni Jerry Muro wakati akijibu maswali ya wanahabari, ghafla akapotoka katika hoja ya msingi na kuanza kumjibu hovyo msemaji wa klabu ya Simba, Hajji Manara.

Na ili muyaamini haya niyasemayo naomba kama una mwandishi yoyote wa habari ambaye jana alikuwepo pale ukumbini, muulize maneno machafu, ya kejeli, kudhalilisha, ya kishamba na sifa ambayo Muro alikuwa akiyasema pale.

Hapa nitayasema kisha nitawaombeni nanyi humu mnisaidie kuniambia, je msemaji wa timu au taasisi hivi ndivyo anavyotakiwa kutekeleza wajibu wake?

Maneno yenyewe ni kama haya yafuatayo:

" Kwanza huyo Manara ni mpuuzi kabisa na wa hovyo "
" Mtu anakaa uswahilini ataweza kushindana na mimi niishie Mbezi beach? "
" Mimi namiliki gari la kifahari ambalo yeye hana na hatoweza kuwa nalo "
" Isitoshe nina elimu kubwa ya masters degree ambapo yeye hata diploma tu tatizo "
" Nina uwezo sasa hata wa kuoa mwanamke wa kizungu kwa kuwa mimi ni wa kimataifa zaidi "
" Afisa habari gani kutwa anashinidia mihogo pale Magomeni Kagera? "

Hayo hapo juu ndiyo maneno ya msemaji wa Yanga aliyoyasema jana ktk press conference, ila kutokana na pengine hao waandishi kumwogopa au kumpotezea hakuna aliyeyasema au hata kuyazungumzia isipokuwa chombo kimoja tu cha Magic Fm kipindi cha jana usiku. Na nimeamka leo asubuhi hii nikijua kuwa wale waandishi niliowaona jana pale wangeandika hii kitu na kukemea kwa maslahi na maendeleo ya mpira wetu. Cha kushangaza, hakuna print media yoyote iliyoandika hivyo!

Kidume nimeamua kujilipua kama kawaida yangu. Na kwa wale mtakaodhani hizo kauli nilizoziweka hapo juu Jerry Muro hakuzisema, nawaombeni Muangalie Video Hapo chini

Na cha kuchekesha zaidi, hizo kauli chafu zote alizitoa baada tu ya kuulizwa kuwa je, anasemaje kuhusu malalamiko ya timu za Simba na Azam kuwa Yanga inapendelewa na TFF, baada ya TFF kuyafanyia haraka sana marekebisho ya wachezaji wa kigeni, yaliyowaruhusu wachezaji wote wageni waliokuwa na matatizo na taratibu za vibali vya kucheza ligi kuu kuanzia leo, wakati kabla ya mechi ya Simba na Azam klabu ya Simba ilihangaika huko huko TFF ili wachezaji wake Paul Kiongera na Brian Majwega wacheze lakini TFF ikaikatalia Simba tena hadi kwa vitisho?

Nimetema nyongo rasmi na nawaachieni intellectuals na academicians mliopo humu muweze kujadili zaidi, ila naiomba klabu ya Yanga iliangalie suala hili kwa umakini mkubwa mno hasa kwa huyu msemaji wao kwani akiachwa aendelee kuwa na hizi lugha zisizo na staha kuna siku mpira wetu utachafuka na hata kusababisha machafuko makubwa na hadi vifo.

Binafsi nimesikitika mno!​

Angalia Video Hapa


CHADEMA Yaionya CCM Umeya Dar es Salaam

0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimemteua diwani wa Ubungo, Isaya Charles kugombea nafasi ya Meya wa jiji la Dar es Salaam, na kuitahadharisha CCM hakitakubali kuchezewa rafu katika uchaguzi huo.

Aidha, Chadema imemtangaza diwani wa Ubungo, Boniface Jakob kuwa mgombea wa nafasi ya Meya wa Kinondoni na diwani wa kata ya Bonyokwa, Charles Kuyeko kugombea umeya wa Ilala.

Uteuzi huo ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu Chadema (Zanzibar), Salim Mwalimu wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Majina hayo yaliteuliwa kwa ushirikiano ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema.

Mwalimu alisema wanatarajia kuona uchaguzi huo ukifanyika kwa amani na utulivu bila kuwepo na ubadilishwaji wa matokeo, kwa kuwa kuna mbinu chafu zinazofanywa na CCM sasa.

Alisema katika Halmashauri za Ilala na Kinondoni Chadema inaongoza kuwa na madiwani wengi lakini cha kushangaza CCM imekuwa haitaki kuyakubali matokeo hayo na kutaka kuyabadilisha.

"Kwa mujibu wa taratibu zilivyo ni kwamba Hamashauri yenye madiwani wengi ni kuwa chama hicho huchukua ushindi lakini hawa wenzetu CCM wamekuwa hawataki," alisema.

"Mfano mzuri katika Wilaya ya Temeke madiwani ni wengi wa CCM tumekubali huo ushindi kwa kuwa ni kweli wametuzidi.

"Kinondoni na Ilala hawataki umeya uchukuliwe na Chadema licha ya kuwa na madiwani wengi na sisi hatuwezi kukubali njama za wazi zinazofanywa na CCM.
"Na hata meya wa jiji lazima atoke Chadema kwa kuwa katika mkoa wa Dar es Salaam tunaongoza kuwa na madiwani wengi."

Mwalimu alisema ameshangazwa na kitendo cha CCM kwenda Zanzibar kuchukua wabunge kwa ajili ya kupigia kura Kinondoni.

Alisema kitendo cha wabunge hao kukubali jambo hilo ambalo ni la aibu katika jamii inayowazunguka ni sawa na kuwazalilisha Wazanzibari kuwa hawajasoma.

"Unakubalije kubebwa kutoka Zanzibar kuja kupigia kura meya wa Kinondoni! Hivi kabisa mwenyekiti wa chama cha CCM anakubali hii aibu ya wazi wazi isiyohitaji propaganda ya kuleta majeshi Zanzibar""Hilo jambo tutalipinga kwa nguvu zote."

Pia Mwalimu ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kuhakikisha inamaliza changamoto zote zilizojitokeza katika viti maalum vya udiwani.

"Huko Kelwa tumeshinda viti vya udiwani 13 na CCM wameshinda 11 katika mgawanyo wa viti maalum Chadema wamepatiwa viti vinne na CCM imepatiwa vitano,? alisema.

"Hapa tumeitaka NEC itueleze huo mgawanyo umegawanywa vipi" Tumeenda kuwauliza wanatueleza Mkurugenzi hawampati kwenye simu ili athibitishe ni nani mwenye madiwani wengi. Eti mkurugenzi hapatikani na mwezi umeshapita."

CHANZO: NIPASHE

Mwanamuziki Ali Kiba Anaenda Kuzimika Kama Mshumaa Katikati ya Pepo Kali.....

0
0
Leo nimetembelea Account ya Sporahshow insta nikakuta kapost kua leo atakua na show na alikiba hivo watu wafunguke nini wanachotaka kumuliza kiba

Chakushangaza nimeona Mashabiki wa Kiba Wakimtumbua majipu ile mbayaaaa... Sikujua kama kiba ana majipu yaliyoiva kiasi icho.... Wengine wamediriki kumwambia kama asipo jirekebisha wanahamisha nguvu kwa Rich Mavoko na wasanii wengine maana anayesukumwa hataki kwenda ana madharau na nyodo zakujiona ata akikaa kimyaa atabaki kuonekana juu siku zote kutokana na fans alonao

Asa nachoona apo Kiba itamcost maana vilio vile havitaenda bure atakumbuka shuka kumekucha

Lakini kama vile kiba alikua kashaa staafu Mziki ila analazimishwa na pampu za mashabiki na kwasaabu ataki kukubali defeat inamgarimu kuendana na kasi iliyopo ilihali hana pesa wala uwezo so anapata pressure za mashabiki pamoja na kejeli za haters wake, ukijumlisha stress zauchumi pamoja na mahitaji ya watoto shule na shida za familia, namuona jamaa kwingine...

Kama Namuona Anataman kutangaza kastaafu Mziki ila anaogopa kejeli

Baadhi ya Comments za Mashabiki wa Ali Kiba

Jnayma
mm naomba umulize mbona anazembea saana kwenda na kasi ya mziki ulivyo?mm kama shabik ake naumia saana @thesporahshow

Steve_octotz
Jamani mwambie alikiba aachie ngoma video ya nagharamia haiwezi kuzima moto unaoendelea bongo kwa sasa aachie bonge la ngoma Pamoja na video yake alaf namuomba ajalibu kuwa na njaa kwenye muziki

bern_bizzy
Tumechoka mashabiki hatusikilizwi why mimi atakula siwezi


Waishucom55_jr
Muulize Kwa nini alipaniki sana swali aliyo ulizwa na Ben pol kwenye Twitter ?


paulgenious
@thesporahshow mwambie aache uongo mungu hapend kutwa kutuahidi uongo tu mara bampa to bampa mara cjui nn wakat hewa tupu...!! @officialalikiba kama umefika ukingoni funguka jamaa tujue 1

officialfestomumba
Tatizo la Alikiba ni kwenda na wakati, kuchelewa kutoa nyimbo, ubora Wa video, na ubunifu ktk kazi zake . Akijirekebisha hayo basi Kiba atakuwa next level 100%


duwly_abdwly
Anachiaa lin nyimboo,,Ebu tusaidiee kumuliza...Koz tUNAKARIBIA Kukata tamaa..Wenzake kina diamond,ommy dimpoz,mwana fa, wanachia nyimo kalii yy mzgo unakuja lin..Au kalogwa.


Viewing all 104427 articles
Browse latest View live


Latest Images