Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Mwanaume Tambua Dawa ya Wanawake Wanaokukataa Kwa Sababu Huna Pesa....

$
0
0

Kuna tabia ambayo baadhi ya wanaume wamekuwa waki wa lalamikia wasichana kuwa hawana mapenzi ya Kweli wanapenda pesa tu,sasa minawapa dawa wanaume wenzangu ya kufanya wanapokataliwa na wanawake kwa sababu ya kipato chao kidogo,mwanamke akikuka taa kwa sababu huna pesa,usilalamike wala kusononeka,unachotakiwa kufanya tafuta pesa kwa nguvu zako zote"focus "kwenye malengo yako ya mafanikio mpaka ufanikiwe na wwe siku ukifanikiwa ukiwa tajiri,wanawake maskini wakikushobokea wakijifanya wanakupenda usiwakubalie na kamwe usikubali tena kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamke maskini au mwanamke njaa wao si walikukataa ulipokuwa huna kitu,na ukioa oa mwanamke tajiri usioe mwanamke maskini wasije wakakurudisha nyuma kwa sababu wanawake wengi wanaopenda wanaume matajiri hawajui "struggling" wanapenda short cut na hawana vision zao binafsi za kufanikiwa zaidi ya kutegemea wanaume ndio wawatoe kimaisha.

Fanya kama alivyofanya Diamond platinum alipokuwa hana kitu wanawake wazuri walimkwepa kama ukoma alipozipatatu akawa gumzo kwa wasichana mjini,kila msichana anajifanya anampenda Diamond platinum, alipokuwa hana kitu mbona walimtenga,ila nimemsifu amechukua mwanamke tajiri tena kutoka nchi za nje,zari the boss lady,na wewe ukizipata oa hata mtoto wa Obama,kwanza ukifanikiwa ukawa tajiri usioe kabisa mwanamke maskini wanawake wengine wana mikosi utafilisika bure,na Rudi kwa wasichana wanaopenda wanaume matajiri na kuwapiga chini wanaume wenye kipato cha chini.

Kama wwe ni msichana unapenda wanaume matajiri na kushauri tu uache hizo tamaa zako kwa sababu kwanza unatakiwa ujue wanaume matajiri wapo wa chache kwa hiyo sio rahisi kuwapata wakakuoa ni bora ukomae tu na maskini wenzio ipo siku mnaweza mkatoka,pili asilimia kubwa ya wanaume waliofanikiwa walikuwa na wapenzi wao Tangu zamani, kuna usemi unasema "kila mwanaume aliyefanikiwa nyuma yake kuna mwanamke shupavu" kwa hiyo wwe kama msichana sio rahisi kuwapata wanaume matajiri wakakuoa labda wakutumie tu kama chombo cha starehe,na choku washauri komaeni na maskini wenzenu mtatoka tu shida zina mwisho wake mkiji tuma.

Note: no short cut to process.

Nafasi za Kazi 

Baada ya Kuukosa Uspika wa Bunge...Samwel Sitta Atangaza Kuacha Siasa na Kuwa Mwandishi

$
0
0
Kwa mara ya kwanza tangu Kamati Kuu ya CCM ilipomuengua kwenye kinyang’anyiro cha uspika, Samuel Sita ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa, jana ameweka bayana mustakabali wake; ameamua kustaafu siasa.

Sitta aliongoza kwa mafanikio Bunge la Tisa kiasi cha kumfanya apewe kirahisi uenyekiti wa Bunge la Katiba na hivyo kujijengea jina miongoni mwa wana-CCM kiasi cha kujitumbukiza kwenye mbio za urais na baadaye kutaka kurudi tena kuliongoza Bunge la Kumi na Moja.

Lakini hakufanikiwa kupitishwa kuwania urais wala kugombea uspika, ambao aliahidi kuwa angeengulkiwa angefika hata mahakamani.
Lakini jana alikuwa na kauli tofauti.

“Mambo ya siasa kwa sasa basi,” alisema Sitta alipoulizwa na kuhusu mipango yake ya baadaye baada ya kutopitishwa na CCM kuwania uspika.

Sitta ambaye amewahi kuongoza wizara mbalimbali, alisema kwa sasa anajikita katika uandishi wa vitabu na kwamba kwa umri alionao na utumishi wake serikalini, umefika wakati kwake kupumzika na kutoa ushauri wa masuala mbalimbali kwa wale watakaohitaji mchango wake.

Novemba 15, Kamati Kuu ya CCM ilimtosa Sitta na wengine waliojitokeza kuwania uspika na badala yake ikateua majina matatu kwa ajili ya kupigiwa kura na wabunge wa CCM, ambao walimchagua mbunge wa Kongwa, Job Ndugai kuwa Spika.

Kuenguliwa kwa Sitta kulikuwa ni pigo lake la pili katika nafasi ya hiyo baada ya kukatwa na kikao hicho mwaka 2010 alipokuwa akitetea nafasi yake. Wakati huo Anne Makinda alichaguliwa kuongoza Bunge la Kumi lililomaliza muda wake mwaka huu.

Sitta alijizolea sifa wakati akiwa Spika wa Bunge la Tisa kuanzia mwaka 2005 hadi 2010, baada ya kuliongoza kuibua mijadala mbalimbali dhidi ya Serikali na kashfa ya Richmond iliyomfanya Edward Lowasa kujiuzulu uwaziri mkuu.

Baada ya kung’atuka
Alipoulizwa atajishughulisha na nini baada ya kustaafu, Sitta ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba alisema: “Nipo tu nyumbani nimepumzika. Naridhika na niliyoyafanya kwa Taifa. Wale watakaotaka kupata ushauri wakinifuata nitawasikiliza.”

Alisema kwa sasa anaandika makala ambazo baadaye ataziweka katika kitabu chake kitakachoeleza hali ya nchi na historia za masuala mbalimbali.

“Ninachokiandika ni mtazamo wangu binafsi, ni jinsi ambavyo mimi ninaona kwa macho yangu,” alisema.

Alipoulizwa kama atakubali kuongoza wizara iwapo Rais John Magufuli atamteua kuwa mbunge na kisha waziri alisema: “Tusizungumze jambo ambalo halina mwelekeo huo.”

Hata hivyo, alisema kwa mtazamo wake hadhani kama anaweza kufikiriwa kuwamo katika baraza hilo.

Kupinga uspika kortini

Kuhusu sakata la uspika, Sitta alisema angekwenda mahakamani kupinga kuondolewa kwake, kama tu mchakato wa chama hicho ungefanyika bila kufuata taratibu na watu kuonewa.

Katika mazungumzo yake na Radio Uhuru FM wakati wa mchakato wa uspika, Sitta alisema kutokana na hali ya joto la kisiasa ilivyo, ambayo ilidhihirika zaidi wakati wa uchaguzi, wabunge walioshinda ni vijana na ni wazi spika anayehitajika ni mwenye uzoefu.

Alisema licha ya kwamba wapo waliojaribu kumshawishi asigombee nafasi hiyo tena, badala yake awe anatoa ushauri pale inapobidi, alisisitiza bado ana wito wa kuwatumikia wananchi kwa njia hiyo.

“Niliposema (nitakwenda mahakamani) kama nisipoteuliwa na CCM kuwania uspika nililenga kama kitatokea kitu kama uonevu. Yaani kama vingeletwa vigezo ambavyo havipo katika mchakato,” alisema.

“Kama unakumbuka mwaka 2010 kililetwa kigezo cha ‘spika mwanamke’. Hicho ndicho kitu ambacho nilikilenga kwamba kikijitokeza sitakikubali. Uzuri ni kuwa hakikuwapo na kumbuka kuwa jambo lile (la kupitishwa kuwania uspika) lilikuwa ni uamuzi wa chama si mtu,” alisema Sitta.

Jela kwa kupongeza majambazi yaliyovamia Polisi Stakishari

$
0
0


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu Bruno Kimaryo, kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya kusambaza ujumbe katika mtandao wa kijamii wa kuyapongeza majambazi yaliyovamia Kituo cha Polisi cha Stakishari na kuua polisi.  Aidha, mshtakiwa huyo ametakiwa ama kulipa faini ya Sh. 600,000 kwa kosa hilo.

Katika tukio la Stakishari lililotokea Julai 12, mwaka huu, majambazi yalivamia kituo hicho na kuua polisi wanne na raia watatu pamoja na kupora bunduki 20 aina ya Sub Machine Gun (SMG).

 

Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mkuu, Waliarwande Lema, baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka. Alisema vielelezo vitano na utetezi wa mshtakiwa vinaonyesha kuwa Bruno alifurahia kitendo kilichofanywa na majambazi hao na alitamani kila kituo cha polisi kivamiwe.

Alisema mshtakiwa huyo katika ujumbe wake huo alitumia viunganishi vya maneno yasiyokuwa ya kibinadamu ya auawe, avamiwe na kuwa utetezi wake unaungana na maelezo ya onyo aliyoyatoa polisi hayaonyeshi kusikitishwa wala kuhurumia polisi.

Hakimu Lema alisema kama mshtakiwa angekuwa anapeleka ujumbe kwa polisi wachukue tahadhari, angeupeleka katika mamlaka husika, lakini kutokana na lugha aliyoitumia, mahakama hiyo inamtia hatiani.

Hata hivyo, mshtakiwa huyo alifanikiwa kulipa faini na kukwepa adhabu ya kifungo.

Awali, ilidaiwa kuwa Julai 13, mwaka huu, jijini Dar es Salaam, mshtakiwa huyo anadaiwa kusambaza machapisho ya uchochezi kinyume cha Sheria ya Magazeti kwa nia kuleta ushawishi na kueneza chuki katika mtandao wa kijamii wa facebook.

Wako Wapi Hawa Makamanda wa CHADEMA?

$
0
0
Mbona kimya sana. hawa Makamanda wako wapi?
1. Mabere Nyaucho Marando
2. Tundu Antipas Mgaiwa Lissu
3. Babu Juma duni Haji
4. Kingunge Ngombale Mwiru
5. Mch. Josephat Gwajima(Mshenga).
6. Lucy Philemon Owenya

Miss Colombia Atoa ya Moyoni Kuhusu Kuporwa Ushindi wa Miss Universe

$
0
0
Baada ya shindano la Miss Universe lililofanyika Jumapili iliyopita (Dec 20) kukumbwa na dosari ya MC kukosea kumtaja mshindi, Miss Colombia ambaye alitangazwa mshindi na dakika chache baadaye kupigwa na butwaa baada ya MC Steve Harvey kurudi na kutangaza kuwa alipewa ushindi kimakosa, hatimaye mrembo huyo ametoa ya moyoni na kumpongeza mshindi wa mwaka huu Miss Ufilipino.

Kupitia Instagram yake Miss Colombia , Ariadna Gutierrez aliandika ujumbe mrefu wa kugusa kuhusu kilichotokea, akieleza kuwa sasa moyo wake umetulia na maisha lazima yaendelee. Pia akagusia kwamba huko mbele ya safari itakuja kufahamika kwanini mambo yalitokea vile yalivyotokea, na akamaliza kwa kuwapongeza Wafilipino kwa kupata Miss Universe mpya Pia Alonzo Wurtzbach .

Huu ndio ujumbe wake:

“After the storm comes the calm. I want to thank each and everyone of you who have sent messages of support and strength. Every one of you has become an incredible human being in my book and I am the most fortunate and thankful for having the support not only from one country but from the whole entire world. Your destiny is written for you. And my destiny was this. I was able to bring happiness to my country after becoming Miss Universe for only a couple of minutes… Today because of that COLOMBIA and the LATIN COMMUNITY are being talked about in every corner of the world. I also want to congratulate the Philippines for their new Miss Universe . The happiness that you must be feeling must be incredible. Life continues and in the future we will find out why things happen the way they happen. Thank you all for your LOVE SUPPORT and KINDNESS.❤️”

Afande Sele Apasua Jibu...Wanaoenda Kushoot South Wana Boashara za Siri....

$
0
0
Afande Sele amedai kuwa anawashangaa wasanii wanaoenda kushoot video zao nje ya nchi wakati Tanzania ina kila kitu.

Rapa huyo mkongwe aliyekuwa kimya kutokana na shughuli za kampeni, ameiambia Bongo5 kuwa anaamini wasanii wanaosafiri kwaajili ya kushoot video nje, wana bishara zao za siri.

Kwenye kushoot video nje ni ulimbukeni,” amesema.

Tanzania tuna kila kitu kuliko hata huko wanakoenda. Mimi hii naitafsiri ni usaliti wa nchi, sisi tunakosa nini hapa nyumbani? Tuna milima, mbuga, maporomoko mazuri, yaani tuna kila kitu. Unajua wasanii wengi walikuwa wanatumia mwanya wa kwenda kushoot video nje ili kufanya biashara zao za siri. Wengi wameutumia sana huu mwanya, sasa Magufuli alivyoingia atawanyoosha tu,” amesisitiza Afande.

Katika hatua nyingine Afande Sele amesema anajipanga kuachia nyimbo mpya mbili ili kufidia ukimya mkubwa aliouacha kwa mashabiki wake.

Video: Davido Aongelea Sakata la BBA na Alivyowakera WaTZ, ‘Nilieleweka vibaya, Diamond ni Kaka Yangu Angenitetea’

$
0
0
Kwa mara ya kwanza na kwa urefu zaidi, Davido amelizungumzia sakata lilitotokea December mwaka jana la ushindi wa Idris Sultan kwenye Big Brother Africa na jinsi tweet yake ilivyowakera Watanzania.

Akiongea kwenye The Sporah Show, Davido alisema tweet ile hakuandika kuwalenga Watanzania bali kampuni ya Multi-Choice inayoanda shindano hilo ambayo pia ndio waandaaji wa tuzo za Channel O. Kabla ya hapo Davido alikuwa ametajwa kuwania tuzo tano lakini alikosa zote. Diamond alishinda tatu.

“Na nilitarajia Diamond angenitetea mimi kuliko kingine,” alisema.

Angenipigia na kuniambia ‘watu wangu wamekasirika nadhani ungeomba radhi au fanya hivi kuliko hivyo. Ingekuwa ni nchi yangu na najua jinsi ya kuwatuliza watu wangu ningesema Diamond ni kaka yangu hakumaanisha hivyo tuyaacha na tusonge mbele, hivyo ndivyo ilitakiwa kusuluhishwa,” alisema Davido.

Lakini tulikutana [na Diamond] kwenye MTV Awards na hakikuwa kitu kabisa, hata hatukuliongelea, tuko poa.”

ANGALIA VIDEO:

Ommy Dimpoz: Niko Tayari Kuoa Hata Sasa,Kama Nikipata…

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva,Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ amesema kuwa yuko tayari kuoa hata sasa hivi kama nikipata mtu sahihi katika maisha yake.

Ommy ameyazungumza hayo wakati akiitambulisha video ya ngoma yake mpya iitwayo ‘Achia Bodi’ kwenye kipindi cha Clouds360  cha Clouds Tv wakati alipoulizwa na mtangazaji kipindi hicho Hudson Kamoga kuwa anatarajia kuoa lini.

Niko tayari kuoa hata sasa hivi kama nikipata mtu sahihi katika maisha yangu” Ommy Dimpoz.

Miezi ya hivi karibuni msanii huyo alitupia picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na msichana ambapo picha hizo zilizua maswali kwa mashabiki wake na kuuuliza huenda alikuwa ndiye shemeji yao,lakini hawakupata jibu.

Cloudsfm.com

Watu 7 Wafariki Kwa Kuungua Moto Baada ya Gari Kupinduka na Kuwaka Moto

$
0
0
WATU saba wamefariki duniani na wengine kumi wamejeruhiwa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kulipuka na kuwaka moto.

Akiongea na mtandao huu ofisini kwake Mganga Mkuu wa hospitali ya Mkoa wa Kigoma Maweni Dkt. Leonard Subi amesema kuwa jana majira ya saa 12 jioni walipokea miili ya marehemu 6 na majeruhi 11 ilipofika saa 6 usiku majeruhi mmoja alifariki duniana na kupelekea idadi ya vifo kuwa saba.

Aliwataja waliofariki katika ajali hiyo ni Ashura Mussa, Kadogo Yusuph, Kabwe Iddy, Mwamvua Juma na Peter Sungura,maremu wawili miili yao bado haijatambulika sababu ya kuungua vibaya.

Dkt. Subi aliwataja pia majeruhi wa ajali hiyo kuwa ni Andrew Peter, Amos Thomas, Mutta Hamis, Shabaan Fadhil, Hassan Kasa, Esau Elias, Asha Kassim na Riziki Jaah.

"Majeruhi wote wamelazwa wodi namba saba na hali zao siyo nzuri wanaendelea na matibabu, mtoto aitwaye Riziki Jaah mwenye umri wa miezi nane ndiye aliyenusurika katika ajali hiyo hajaumia popote mama yake alimtupa dirishani baada ya moto kuwaka ila mama yake alifariki kwa kuungua kwenye ajali hiyo"alisema Dkt. Subi.

Naye Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Kigoma, Ferdnand Mtui amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya gari aina ya Toyota Hiace lenye  namba T.700 ADK lililokuwa likitoka Kigoma mjini kwenda katika kijiji cha Subankala kata ya Ilagala Wilayani Uvinza kilichopo mwambao mwa ziwa Tanganyika.

Kamanda Mtui alisema kuwa ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mwakizega na chanzo cha ajali hiyo ni dereva kuwakwepa watembea kwa miguu kisha kugonga gema iliyopelekea gari kupinduka na kuwaka moto.

Madereva Watakaozidisha Abiria Kwenye Vyombo Vya Usafiri Kukiona...Hii Inawahusu Hata Wale wa Daladala

$
0
0
JESHI la Polisi Nchini limewatahadharisha madereva  watakaozidisha  idadi ya abiria kuliko uwezo wa chombo cha usafari kwani ni kosa kisheria na watakaozidisha abiria kwenye vyombo vyao vya usafiri watachukuliwa hatua za kisheria.

Operesheni hiyo inaanza leo baada ya tamko la Jeshi la Polisi na kuanza kutekeleza kwa wale wote wataobeba abiria wengi tofauti na uwezo wa basi. Watakaochukuliwa hatua ni madereva wa daladala,mabasi ya mikoani pamoja na magari aina ya Noah.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba amesema kuwa Jeshi la polisi linaanza operesheni ambayo ni endelevu na kuwataka watu wafuate sharia ya ubebaji wa abiria.

Advera amesema kuwa katika kipindi hiki cha siku kuu Jeshi la polisi limejipanga katika kuwadhibiti waendesha bodaboda kwa wataopandisha watu zaidi  ya wawili (mishikaki) kukiona cha mtema kuni kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani.

Aidha amewataka wananchi kutoa taarifa za kihalifu katika msimu wa sikukuu ili  kuimarisha  ulinzi wa watu na mali zao ili maisha yaweze kuendelea baada ya sikukuu.

Breaking News:Rais Magufuli Akamilisha Uteuzi wa Baraza la Mawaziri, Makame Mbalawa Abadilishiwa Wizara

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza baraza la Mawaziri la kwanza katika awamu ya tano ya utawala wake, na hawa ndio waliopata nafasi hiyo.

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Profesa Jumanne Maghembe kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Dkt. Philip Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge) 15

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Mhandisi Gerson Lwenge kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Dkt. Joyce Ndalichako kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Hamad Masauni kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

#BREAKING: Rais Magufuli amemteua Prof. Makame Mbarawa kuwa Waziri wa Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano

Mtendaji Mkuu wa DART, Bi. Asteria Mlambo Asimamishwa KAZI Kupisha Uchunguzi

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mh. George Simbachawene amemsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wa DART, Bi. Asteria Mlambo kwa kushindwa kuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma wakati wa kumpata mtoa huduma katika kipindi cha mpito.

Simbachawene amesema mtendaji huyo alishindwa kuchukua hatua hata pale alipobaini kuwa mtoa huduma wa mpito amekiuka masharti ya mkataba wa kutoa huduma ya mpito na kufanya maamuzi makubwa pasipo kuishirikisha Bodi ya Ushauri ya DART.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Disemba 24, Ikiwemo ya Aunty Ezekiel Kumtia Umaskini Moses Iyobo

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya Disemba 24, Ikiwemo ya Aunty Ezekiel Kumtia Umaskini Moses Iyobo

Polisi Wauana Kwa Risasi Jijini Mwanza Wakiwa Lindoni

$
0
0
ASKARI Polisi wa Kituo cha Polisi Nyamagana jijini Mwanza, Konstebo Daud Masunga Elisha, amemuua askari mwenzake, Konstebo Petro Saimon Matiko kwa risasi na baadaye kujiua kwa risasi na kufa papo hapo.

Tukio hilo lilitokea jana saa 8.30 mchana jijini Mwanza katika eneo la Benki ya Posta Tawi la Pamba wilayani Nyamagana huku chanzo cha mauaji hayo kikiwa hakijulikani.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Justus Kamugisha alisema kitendo hicho si cha kawaida ndani ya jeshi hilo, na kufafanua jinsi mazingira ya tukio lilivyotokea na kusababisha taharuki kwa wananchi na wateja waliokuwa ndani na nje ya benki hiyo.

“Ni kweli kuna askari wawili wamefariki eneo la Benki ya Posta. Katika eneo la benki hiyo kulikuwa na askari wawili waliokuwa lindoni ambao ni PC Elisha na PC Remigius Alphonce mwenye namba H 4291, wakiwa wanaendelea na lindo alifika askari mwingine aliyekuwa amevaa kiraia PC Matiko na kuwasalimia kisha kuingia ndani ya benki kuchukua fedha,” alieleza Kamanda Kamugisha na kuongeza:

“Baada ya dakika tano, Matiko alitoka nje na kuwaeleza askari wenzake kwamba mtandao unasumbua, wakati akieleza hivyo, ghafla askari PC Elisha aliweka chemba risasi ambapo mwenzake PC Alphonce alimhoji mbona unaweka risasi katika hali ya utayari wa kutumika na alijibiwa kwa ufupi kwamba ‘achana na mimi.’

“Ghafla alimfyatulia risasi PC Matiko na kumpiga eneo la bega la kushoto na kutokeza mgongoni na kuanguka chini, kitendo hicho kilimfanya PC Alphonce kukimbilia Benki ya Barclays ili kuomba msaada kwa askari wenzake waliokuwapo lindoni hapo.

“Kabla ya askari hao kufika, ilisikika sauti ya mlio wa risasi na baada ya kurudi alimkuta PC Elisha akiwa amejipiga risasi kwenye paji la uso na kutokea nyuma ya kisogo, tayari akiwa amepoteza maisha.”

Sakata Dk. Mwaka Lawa Pasua Kichwa kwa Dk. Kigwangalla

$
0
0
Utata kuhusiana na uhalali wa tiba zinazotolewa na Dk. Juma Mwaka wa kituo cha tiba mbadala cha Foreplan Clinic kilichopo Ilala jijini Dar es Salaam unaelekea kuwa ‘pasua kichwa’ kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk. Hamis Kigwangalla, baada ya majibu ya uchunguzi wa vyeti vya mganga huyo kushindwa kutolewa kwa umma kama ilivyoahidiwa.

Awali, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Waziri Kigwangalla aliahidi kutoa taarifa kwa umma kuhusiana na Dk. Mwaka juzi (Jumatatu). Alieleza hayo baada ya kufanya ziara ya ghafla kwenye kituo cha Dk. Mwaka Desemba 14, 2015 na kutomkuta yeye na baadhi ya watoa huduma wake kabla ya kumtaka (Dk. Mwaka) awasilishe vyeti vyake wizarani kwa ajili ya ukaguzi.

Hata hivyo, licha ya Dk. Mwaka kutekeleza agizo alilopewa Desemba 16 na waziri kukiri kuwa kweli vyeti hivyo vimefikishwa kwao na kuhakikiwa, bado suala lake linaelekea kusumbua kwani hadi kufikia jana, hakukuwa na ufafanuzi zaidi kama ilivyoahidiwa wiki iliyopita huku Dk. Kigwangalla akiutaka umma utulie na kusubiri taarifa ya ukaguzi kwani hivi sasa kuna masuala mengine ya kushughulikia.

 “Tutawapa taarifa mara tutakapomaliza kuipitia ripoti hiyo, subirini tu kwa kuwa kuna kazi nyingi za kufanya wizarani,” Dk. Kigwangalla wakati alipoulizwa na mwandishi wa Nipashe jana kuhusiana na matokeo ya ukaguzi wav yeti mwaka kama alivyoahidi wiki iliyopita.

Akieleza zaidi, Dk. Kigwangalla alisema bado anaipitia ripoti hiyo na akishamaliza, atashauriana na viongozi wengine wa wizara yao akiwamo Waziri mwenye dhamana, Ummy Mwalimu, na kisha ndipo ataitisha mkutano na waandishi wa habari kwa ajili ya kutoa taarifa.

ILIVYOKUWA
Desemba 14 ya wiki iliyopita, Dk. Kigwangalla alifanya ziara ya kustukiza kwenye kituo cha Dk. Mwaka ambaye amekuwa maarufu kutokana na matangazo mbalimbali anayotoa kila mara kuhusiana na tiba anazotoa.

Hata hivyo, baada ya Dk. Kigwangalla kufika kwenye kituo hicho, hakumkuta Dk. Mwaka na wenzake na ndipo (Dk. Kigwangalla) alipotoa amri ya kufungwa kwa muda kituo hicho akimtuhumu Dk. Mwaka na wenzake kumkimbia na kisha akaamuru apeleke vyeti vyake ili vichunguzwe na kuona kama huduma wanazotoa zinakidhi vigezo na ni salama kwa wagonjwa.

Desemba 20, Kigwangalla aliiambia Nipashe kuwa ameshapokea ripoti yenye maelezo ya vyeti vya Dk. Mwaka na kwamba, angetoa ufafanuzi kwa vyombo vya habari Jumatatu au Jumanne (juzi au jana).

KIMENUKA Somalia...Serikali Yapiga Marufuku Sikukuu za Christmass Nchini Humo

$
0
0
Serikali ya Somalia imepiga marufuku sherehe za kuadhimisha Sikukuu ya Krismasi katika mji mkuu wa Mogadishu.

Mkurugenzi mkuu katika wizara ya masuala ya dini, Sheikh Mohamed Khayrow, ameonya kuwa maadhimisho kama hayo yasiyofungamana na dini ya Kiislamu yanaweza kusababisha mashambulizi kutoka kundi la wanamgambo wa Al Shabab.

Maofisa wote wa kulinda usalama wanapaswa kusimamisha ama kuvunja mikutano ya aina yoyote yenye nia ya kuadhimisha sikukuu hiyo isiyofungamana na dini ya Kiislamu.” alisema Sheikh Mohamed

Mwaka uliopita wapiganaji wa Al shabab walishambulia kambi ya majeshi ya muungano wa Afrika (AU) iliyopo Mogadishu wakati wanajeshi hao walikuwa wakisherehekea sikukuu ya Krismasi.
Wanajeshi 5 waliuawa katika shambulizi hilo la kuvizia.
Asilimia kubwa ya raia wa Somalia ni wasilamu.

Credit: BBC

MREMBO Gigy Money Amtambia Wema Sepetu Kwa Kumzidi Kalio

$
0
0
MSANII anayechipukia kwenye ulimwengu wa filamu Bongo, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ‘amejivua’ akili kwa kumtambia staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu kuwa si chochote kwake kwani hawezi kumfikia kwa umbo lake hususan kalio.

Akipiga stori na kona ya Bongo Movies, Gigy ambaye pia ni ‘muuza nyago’ kwenye video za Kibongo alisema kuwa ana kila sababu inayomfanya kujitambia kwa umbo lake ambalo linawateka hasa wanaume wakware.

Kuna siku kwenye kipindi kimoja cha runinga tulishindanishwa kati yangu na Wema nani mwenye kalio kubwa nikamfunika, hicho ni kigezo cha kwanza kuwa nina uwezo wa kumpoteza na sehemu nyingine,” alisema Gigy. Source:Global Publishers

Ugandan sentenced to 5 years in jail for getting pregnant in Kuwait

$
0
0
A Ugandan woman named Nambi Fatumah has been sentenced to 5 years in prison together with her baby in Kuwait for getting pregnant outside marriage.

According to the chairperson of the Association of Ugandans living in Asian and Arab countries, Ali Nusbuga, Fatumah was produced to court a few months ago and would have been saved from the verdict had the government and Human Rights bodies intervened.

He said that much it breaks the law in Kuwait for a woman that is not married to get pregnant or to have a baby and under such instances, the offenders, regardless of nationality or religion, face jail,not alot of help has been offered by the Ugandan authorities despite the endless calls for intervention.

Nsubuga calls upon the government use it’s diplomatic ties with Kuwait so as to save Fatumah and have her deported or even have her sentence reduced.

He also decried the little help and protection given to Ugandans abroad and said that many Ugandan who leave the country for greener pastures go through alot and mentioned instances of them being exploited,having their visas confiscated.

Fatumah suffers the same fate another lady called Mastula did,both are now to serve cases in Kuwait.

Mlangua Tiketi Stand ya Mabasi Ubungo Ajihami Kwa Kinyesi Polisi Wasimkate

$
0
0
Mtu mmoja anayetuhumiwa kuuza tiketi za ulanguzi kwenye Kituo cha Mabasi cha Ubungo (UBT), jana alitumia kinyesi cha binadamu kujilinda dhidi ya polisi waliokuwa wakitaka kumkamata baada ya kubaini alikuwa akifanya biashara hiyo haramu.

Pamoja na kutumia mbinu hiyo ya kipekee, mtu huyo aliyejulikana kwa jina la Nuhu Matumla (26), alikamatwa na askari hao ambao jana waliweka kambi UBT ambako ulanguzi wa tiketi za mabasi yaendayo mikoani umepamba moto wakati huu wa kuelekea siku kuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

Tukio hilo lililovuta hisia za watu na kusababisha msongamano wa magari, lilitokea saa 1.30 asubuhi nje ya kituo hicho wakati wa operesheni hiyo ya kukamata walanguzi wa tiketi na matapeli.

Askari wapatao wanne waliokuwa na silaha walikuwa wakimfukuza Matumla na walipomkaribia, alivua suruali yake iliyokuwa na kinyesi na kisha na kukichota kwa mkono na kuwarushia.

Wakati akirusha alikuwa akisema “niachieni, nitawapaka kinyesi”, lakini juhudi zake hazikufua dafu.

“Kamata huyo hakuna kumwachia, unarusha kinyesi unafikiri sisi tunaogopa,” alisema mmoja wa askari hao.

Kinyesi alichokuwa akirusha kilichafua sare za askari hao na magari madogo yaliyokuwa yameegeshwa katika eneo hilo.

Wananchi walioshuhudia tukio hilo tangu asubuhi, walidai kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa na zaidi ya tiketi 20 ambazo alianza kuziuza kwa watu waliokuwa wakitaka kusafiri.

“Sisi tulikuwa tumekaa hapa tukamuona huyo jamaa (Matumla) akiuza tiketi, hatukujua kama ni za ulanguzi. Baada ya muda tukaona askari wanakuja wakamkamata.” alisema Hassan Issa.

Juma Idd, aliyekuwapo eneo la tukio, aliwamwagia sifa askari kwa kumkamata.

“Tunawasifu hawa askari. kitendo cha kumkamata huyu jamaa aliyekuwa akiwarushia kinyesi ni cha kishujaa,” alisema.

“Kwanza kinyesi chenyewe kilikuwa kinatoa harufu kali ambacho kwa mtu wa kawaida huwezi hata kumsogelea.”

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Mohamed Mpinga alisema mpaka sasa watu wawili wamekamatwa kwa kuuza tiketi za ulanguzi huku wengine 20 wakikamatwa kwa makosa ya kutapeli na kusumbua abiria.

“Tumefanikiwa katika hilo japo ulanguzi wa tiketi unafanyika kwa kiwango kikubwa,” alisema.

Alisema wote waliokamatwa watafikishwa mahakamani na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.     

Dk Magufuli Akamilisha Baraza la Mawaziri, Amteua na Boss wa TRA

$
0
0
Rais John Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa mawaziri na naibu waziri alizobakiza wakati akitangaza Baraza la Mawaziri la kwanza la Serikali ya Awamu ya Tano.

Katika taarifa iliyotolewa jana usiku na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, walioteuliwa ni Profesa Jumanne Maghembe ambaye anakuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Philip Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Mhandisi Gerson Lwenge kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji na Dk Joyce Ndalichako kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi.

Katika uteuzi huo, Rais Magufuli amefanya mabadiliko madogo ya Baraza hilo kwa kumhamisha Profesa Makame Mbarawa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwenda Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Pia, amemteua Hamad Masauni kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.


Mawaziri wapya

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Maghembe ambaye ni Mbunge wa Mwanga, alikuwa Waziri wa Maji katika Serikali iliyopita akiwa pia amewahi kuongoza wizara hiyo ya maliasili. Nyingine alizowahi kuongoza ni Kazi na Ajira na Elimu.

Mhandisi Lwenge ambaye pia ni Mbunge wa Njombe Magharibi, alikuwa Naibu Waziri wa Ujenzi akifanya kazi chini ya Dk Magufuli katika Serikali iliyopita.

Dk Mpango ambaye pia ameteuliwa kuwa mbunge, hivi karibuni aliteuliwa na Dk Magufuli kuwa kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), baada ya kumsimamisha kazi, Rished Bade kutokana na kashfa ya upotevu wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam.

Kama ilivyokuwa kwa Dk Mpango, Dk Ndalichako ambaye pia ameteuliwa kuwa mbunge aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta).



Maoni ya wadau

Akizungumzia uteuzi huo, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema kitendo cha Rais Magufuli kumhamishia wizara nyingine Profesa Mbarawa kunadhihirisha jinsi alivyokosa utulivu katika uteuzi.

Alisema ili nchi iweze kusonga mbele, inahitaji iwe na mfumo imara wa utawala ambao hauwezi kupatikana kama nchi haitakuwa na Katiba Mpya, kanuni na taratibu nzuri.

“Mawaziri wameteuliwa Desemba 10 na kuapishwa siku mbili baadaye. Leo (jana) ni siku ya 13 tangu wateuliwe tayari waziri mmoja amehamishwa wizara.”

“Dk Magufuli akitaka kuongoza nchi arudi katika msingi wa kubadili mfumo. Kasi ya mabadiliko ya dunia hatuwezi kwenda nayo sambamba kama tutaendelea kuwa na mfumo mbovu,” alisema Mbatia.

Profesa wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Kitila Mkumbo alisema kama kuna jambo Dk Magufuli amepatia, ni kumteua Dk Ndalichako.

“Ndalichako ni mzoefu na amekuwa katika sekta ya elimu kwa muda mrefu sana. Wizara hii imepata mtu sahihi na mwerevu maana kwa muda mrefu imekuwa ikipata watu ambao hawakuwa makini,” alisema.

Mhadhiri wa UDSM, Richard Mbunda aliungana na Mbatia, lakini akisisitiza kuwa uteuzi wa Rais unaonyesha jinsi CCM inavyokosa watu anaoweza kwenda na kasi yake.

“Ukitizama utabaini kuwa ameteua watu kuwa wabunge na kuwapa wizara nyeti. Hii inaonyesha kuwa ndani ya CCM kwa sasa wanakosekana watu ambao Dk Magufuli anawahitaji, kwa maana ya wachapakazi na watakaokwenda na kasi yake,” alisema.

Mbunda alipongeza uteuzi wa Dk Ndalichako kutokana na uzoefu wake katika sekta ya elimu.


Bosi mpya TRA

Kutokana na uteuzi wa Dk Mpango, Rais Magufuli amemteua Alphayo Kidata kuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA. Kabla ya uteuzi huo, Kidata alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.


Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images