Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Zitto Kabwe Achekelea Utabiri Wake Kutimia Zanzibar....Majeshi Yaanza Kuondolewa

$
0
0
KIONGOZI wa chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe ameelezwa kufurahishwa na jitihada za kumaliza mzozo wa kisiasa visiwani Zanzibar,huku akitaja baadhi ya mbinu ambazo chama chake waliishauri Serikali ambazo zimeanza kuchukuliwa hatua.

Hii hapa chini ni post yake katika mtandao wa facebook juu ya suala hilo

Zanzibar tartiibu….

Disemba 20 mwaka huu 2015 Kamati ya Uongozi ya Chama cha ACT Wazalendo ilitoa tamko lake baada ya kufuatilia hali ya Zanzibar.

Moja ya mambo yaliyoelezwa katika tamko hilo ni uwepo wa askari wengi katika kisiwa hicho hali iliyokuwa inatishia amani kwa wananchi

Taarifa hiyo ya ACT mbali na masuala mengine, ikaeleza kuwa ni wakati muafaka kwa serikali kuhakikisha inawarudisha askari hao wa vikosi mbali mbali kuanzia jeshi la Polisi,JKU,KMKM JWTZ na Mafunzo katika makambi yao.

Lengo likiwa ni kuwaacha wananchi wakiwa katika uhuru wa kufanya shughuli zao wakati suala la mtanziko wa kisiasa kisiwani humo ukiwa unafanyiwa kazi

Kuanzia jana Disemba 22 na leo Disemba 23 majeshi hayo yameshaanza kuondoka katika maeneo mbali mbali ya mji wa Znz hali inayoashiria mwanzo wa mwisho mwema katika kadhia ya uchaguzi wa Zanzibar.

Ninaomba mamlaka husika ziendelee kufanyia kazi mapendekezo yetu mengine ili kulimaliza kabisa suala hili.

Jopo la Umoja wa Mataifa Linaloongozwa na Jakaya Mrisho Kikwete Lakamilisha kazi Yake New York, Marekani

$
0
0
Jopo la Watu Mashuhuri la Umoja wa Mataifa la Kupendekeza Namna Bora ya Dunia Kukabiliana na Majanga ya Afya limekamilisha kazi yake wiki iliyopita jijini New York.
 
Jopo hilo linaloongozwa na Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete lilikabidhiwa jukumu hilo na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki moon tarehe 2 Aprili, 2015 na kupewa muda wa kuanzia Mei hadi Desemba 2015 kukamilisha kazi yake.

Jopo limefanya mikutano minne na kukutana na wadau mbalimbali wa afya zikiwemo taasisi za Umoja wa Mataifa, wadau wa maendeleo, wataalam mbalimbali na kupokea maoni na uzoefu kutoka kwa nchi zilizoathirika na ugonjwa wa Ebola.

Watu mashuhuri wanaounda Jopo hilo ni Mheshimiwa Michelin Calm-Roy aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Uswisi; Mheshimiwa Marty Natelagawa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia; Mheshimiwa Joy Phumaphi, aliyekuwa Waziri wa Afya wa Botswana na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Mheshimiwa Celso Amorim aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Brazil na Rajiv Shah aliyekuwa Mkuu wa Shirika la Misaada na Maendeleo la Marekani (USAID).

Jopo hilo linatarajia kuwasilisha ripoti yake kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa mwezi January, 2016 na baadae kuwasilishwa kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 
Mwenyekiti wa Jopo, Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiendesha Mkutano wa Jopo.
Wajumbe wa Jopo katika Picha ya Pamoja na Wajumbe wa Sekretariati ya Jopo.
Wajumbe wa Jopo la Watu Mashuhuri la Umoja wa Mataifa la Kushauri Dunia Namna Bora ya Kukabiliana na Majanga

Nafasi za Kazi TRA, Application Deadline 12th January, 2016

$
0
0

TANZANIA REVENUE AUTHORITY (TRA)
EMPLOYMENT OPPORTUNITY

TRA would like to recruit dynamic and qualified personnel to fill vacant positions in the Human Resources & Administration Department. Applications are therefore invited from suitably qualified Tanzanians for the following positions:

Bonyeza HAPA Kusoma na Kuapply Kazi Hizo 

Serikali Yatangaza ‘Kuminya’ AJIRA za Wageni......Wanaoishi Nchini Bila Kibali Kukiona cha Moto

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ameagiza waajiri kote nchini kutowapa ajira wageni kwa kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania.

Pia, ameagiza maofisa wa Idara ya Uhamiaji kufanya operesheni maalumu kuwatimua raia wote wasio na vibali vya kuishi nchini ifikapo Januari 31, 2016.

Kitwanga ambaye alitembelea idara hiyo jana, alisema wizara yake kwa kushirikiana na Uhamiaji imeanzisha operesheni ya kuwakamata raia wote wa kigeni wanaoishi nchini kinyume cha sheria na kuwachukulia hatua stahiki.

Waziri huyo alisema kutokana na watu wengi kuishi nchini bila vibali, amewapa mwezi mmoja Idara ya Uhamiaji kufanya uchunguzi katika maeneo yote ya kazi na makazi, ili kuwaondoa walioingia nchini kinyemela.

“Katika operesheni hii, tutahakikisha tunawakamata wote na nimetoa maelekezo kwamba nitakuwa nikipewa ripoti kila Ijumaa kuanzia wiki ijayo, mpaka ifikapo Januari 31 tuwe tumesafisha nchi kabisa,” alisema Kitwanga.

Alisema kutokana na mpaka wa nchi kuwa mkubwa, Uhamiaji watawezeshwa ili kukabiliana na tatizo la upitishwaji wa wahamiaji haramu kutoka nchi mbalimbali, kama ilivyoripotiwa hivi karibuni.

Pia, alitoa agizo kwa wananchi wa kawaida kuhakikisha wanatoa taarifa kuhusu wahamiaji haramu walioweka makazi katika maghala, kampuni na viwanda bubu ili kumaliza tatizo la wahamiaji haramu nchini.

Wafanyakazi wageni
Mbali na maagizo hayo, Kitwanga pia aliagiza wamiliki wa kampuni mbalimbali kuhakikisha hawatoi ajira kwa raia wa nje kwa kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania.

“…Lakini kazi zote ambazo Watanzania wana utalaamu wa kuzifanya zitafanywa na wazawa na si wageni na zile ambazo inaonyesha wazi kwamba Watanzania hawana ujuzi huo, basi zifanywe na wageni,” alisema Kitwanga.

Kuhusu vibali, Waziri Kitwanga alisema hakuna raia yeyote wa kigeni atakayepata kibali cha kuishi nchini kama hajapata kibali cha kufanya kazi kama amekuja kwa ajili ya kazi. Lakini utaratibu mwingine kama mtu amekuja likizo utaendelea kama kawaida.

Kitwanga alisema kuanzia Jumatatu ijayo, viongozi wa wizara husika na uhamiaji, wakae wapange utaratibu mzuri utakaoonyesha kwamba hakuna usumbufu kwa raia wa kigeni ambaye anakuja kufanya kazi nchini kwa kuzingatia vigezo.

Pasi za kusafiria
Aidha, Waziri Kitwanga alisema mfumo wa uombaji wa pasi za kusafiria na vibali vya ukazi, hivi sasa utakamilishwa kwa njia ya Tehama.

Alisema mwombaji atatakiwa kufanyiwa mahojiano ya ana kwa ana pindi atakapokamilisha utaratibu wa kujaza na kuzilipia fomu hizo benki, na atapatiwa pasi ya kusafiria baada ya siku tatu huku kibali cha ukazi akikipata baada ya siku tano ili kupunguza urasimu.

“Tumeafikiana uboreshaji wa namna ya kufanya kazi na kwa mtazamo wa mbali,” alisema.

Angalia Picha za Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Ulipofikia Kwa Sasa....Siku si Nyingi Litaanza Kutumika

$
0
0


 Angalia Picha za Ujenzi wa Daraja la Kigamboni Ulipofikia Kwa Sasa....Siku si Nyingi Litaanza Kutumika Ambapo badala ya Kupanda Kivuko sasa unaweza kwenda kutoka kigamboni au kwenda kwa gari yako bila kupanda kivuko..

KIMENUKA..Serekali Kuvunja Nyumba ya Waziri Mkuu wa Zamani Sumaye....

$
0
0
WAZIRI Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye, ameingia matatani baada ya kudaiwa kuvamia eneo la wazi na kuanza kuzungushia uzio, bila kufuata sheria na utaratibu wa ujenzi.

Eneo hilo la kiwanja namba 719/1/3 lililopo Mkiocheni, mtaa wa TPDC, lilikuwa likitumika kwa ajili ya michezo, mikutano ya kisiasa, pamoja na mikusanyiko mbalimbali ya kijamii.

Kufuatia tuhuma hizo, timu ya maofisa ardhi inachunguza uhalali wa umiliki wake, hivyo wiki ijayo majengo yaliyojengwa kwenye eneo hilo yatavunjwa, endapo ikithibitika kufanya uvamizi huo.

Mbali na Sumaye, vigogo wengine wanaodaiwa wakuvamia kiwanja hicho ni aliyekuwa Katibu Mkuu Mstaafu Ofi si ya Rais, Philemon Luhanjo pamoja na Mbunge wa jimbo la Rungwe, Saul Amon, ambaye ni mfanyabiashara anayemiliki maduka ya S.H. Amon.

Awali kabla ya kuvamiwa kwa eneo hilo, ilielezwa kuwa iliyokuwa kampuni ya High Precision Technology Centre (HPTCMatsutisha), kulilinda lisivamiwe miaka ya 1970.

Hivyo mikusanyiko mbalimbali za kimichezo, pamoja na shughuli za kisiasa ilikuwa ikifanyika katika kiwanja hicho, ambako hata baada ya kampuni hiyo kufa, ililiendelea kutumika kwa shughuli za kijamii.

MAZITO YAIBUKA

Uchunguzi ulibaini kuwa, Sumaye anaendelea na ujenzi katika eneo hilo bila kuweka kibao chenye kuonyesha wakandarasi wanaohusika na ujenzi huo.

Lakini pia, licha baadhi ya nyaraka kudai kuwa kiongozi huyo mstaafu kulimiliki eneo hilo kuanzia mwaka 1998, hajawahi kulalamika kimaandishi kwenye uongozi wa mtaa kuhusu shughuli zilizokuwa zikiendelea kwenye eneo hilo.

Shughuli hizo ni pamoja na uongozi wa serikali ya mtaa kuweka kifusi, ili kusawazisha eneo hilo kuufanya uwanja utumike vizuri kwa ajili ya michezo.

Aidha wiki tatu zilizopita, Ofi sa Mtendaji wa Mtaa huo Mwanaidi Omary, aliongozana na mmoja ya maofi sa wa ardhi wa Manispaa ya Kinondoni hadi kwenye eneo hilo.

Ofi sa huyo wa ardhi alitoa notisi ya mdomo na sio ya maandishi ya kusitishwa ujenzi huo akidai mpaka mmiliki awasilishe nyaraka serikalini.

Licha ya ujenzi huo kufanyika bila kufuata taratibu za kisheria, ikiwemo kutokuwepo kwa kibao kinachoonyesha mkandarasi anayehusika na ujenzi, lakini ofi sa huyo hakuchukua hatua zozote za kisheria.

Katika kutaka kujua ukweli wa mzozo huo, gazeti la uhuru lilifanikiwa kupata barua iliyoandikwa na serikali ya mtaa kwa Halamashauri hiyo kuhoji ujenzi huo. Barua hiyo yenye kumbukumbunamba MKT/SER/MT/ TPDC/05/2015, iliyoandikwa Desemba 11, mwaka huu na kupokelewa Desemba 14, bado haijatolewa ufafanuzi na mkurugenzi kama ilivyokuwa ikielekeza.

LUKUVI KUTUMBUA JIPU


Kufuatia malalamiko hayo ya wananchi, Waziri Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, alisema serikali itavunja uzio na shughuli za ujenzi zinazoendelea kwenye eneo hilo itakapobaini ukweli, ifi kapo Jumatatu.

Katika kusisitiza hilo, Lukuvi alisema hatua hiyo itahusisha hadi vigogo wengine watakaobainika kuvamia eneo hilo.

Alisema baada ya serikali kupata taarifa, timu ya maofi sa ardhi itachunguza kwa kina eneo hilo ili kuthibitisha. Juzi gazeti hili lilishuhudia maofi sa hao wakiwa kwenye eneo hilo wakifanya uchunguzi.

Haya Hapa Ndio Majipu Yaliyotumbuliwa Kwa Mpiga na Mawaziri wa Rais John Pombe Magufuli

$
0
0
MAWAZIRI wawili jana ‘walitumbua majipu’ baada ya kutangaza kusimamishwa kazi kwa Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), Asteria Mlambo na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk Diwani Msemo, wote wakipisha uchunguzi dhidi yao.

Mlambo amesimamishwa kazi kuanzia jana ili kupisha uchunguzi baada ya serikali kubaini ukiukwaji wa wazi wa Sheria ya Manunuzi ya Umma katika kumpata mtoa huduma ya mpito wa mradi huo wenye nia ya kupunguza msongamano wa magari barabarani kwa madhumuni ya kurahisisha usafiri na usafirishaji jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Simbachawene alisema kutokana na kukamilika kwa sehemu ya ujenzi wa miundombinu ya Awamu ya Kwanza ya mradi, Serikali iliamua kuwa na mtoa huduma wa mpito kabla ya kumpata wa kudumu.

“Mtoa huduma wa mpito alipaswa kupatikana kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Hata hivyo, Serikali imebaini ukiukwaji wa wazi wa sheria hiyo wakati wa kumpata mtoa huduma wa kipindi cha mpito.

Kufuatia hali hiyo nimeamua kumsimamisha kazi kuanzia leo tarehe 23 Desemba, 2015, Mtendaji Mkuu wa DART, Bi. Asteria Mlambo ili kupisha uchunguzi,” alieleza Simbachawene.

Simbachawene alizitaja sababu za kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu huyo wa DART kuwa ni kushindwa kuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma wakati wa kumpata mtoa huduma katika kipindi cha mpito; kushindwa kuchukua hatua hata pale alipobaini kuwa mtoa huduma wa mpito amekiuka masharti ya mkataba wa kutoa huduma ya mpito; na kufanya maamuzi makubwa pasipo kuishirikisha Bodi ya Ushauri ya DART.

Aidha, alisema Serikali inatambua kuwa wapo watumishi wa DART ambao hawakumshauri vizuri Mtendaji Mkuu, hivyo watumishi hao watachunguzwa na kuchukuliwa hatua na Kaimu Mtendaji Mkuu atakayeteuliwa.

Nimemwagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tamisemi kuendelea na taratibu za kinidhamu dhidi ya Mtendaji Mkuu aliyesimamishwa kazi,” alisema Simbachawene. Aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua kwa haraka na uangalifu ili mradi huu uanze kutoa huduma bora ya usafiri kwa wakazi wa Dar es Salaam bila kuchelewa zaidi, huku akiwaomba kuitunza na kuithamini miundombinu ya DART kwa kuwa imegharimu fedha nyingi kwa manufaa yao.

Wiki iliyopita, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitembelea maeneo ya mradi huo wa DART na kuagiza kuwa uanze kazi Januari 10, mwakani baada ya kupigwa kalenda kwa muda sasa tangu mwaka jana.

Wakati Simbachawene akichukua hatua hiyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amemsimamisha Dk Msemo kwa kile kilichoelezwa ni kupisha uchunguzi unaolenga kubaini iwapo mgongano wa kimaslahi umeathiri utendaji wa taasisi hiyo.

Aidha, watendaji wote wa serikali katika sekta ya afya hususan wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya, wafamasia, wauguzi na waganga wafawidhi, wameagizwa kukiri kwa maandishi ndani ya siku 21 kuanzia sasa endapo wanamiliki hospitali, zahanati, kliniki na maduka ya dawa.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyosainiwa na Waziri Mwalimu, imefafanua uamuzi wa kumsimamisha Kaimu Mkurugenzi huyo wa Ocean Road, unatokana na ziara walizofanya kukagua utoaji wa huduma za afya katika maeneo mbalimbali ambako walibaini upungufu wa dawa umeendelea kujitokeza kwa wingi.

Baadhi ya wagonjwa walieleza kwa uchungu jinsi wanavyopata tabu ya kupata dawa hata zile ambazo wanatakiwa wazipate kwa bei ya ruzuku au zinazotakiwa kutolewa bure na serikali,” ilisema taarifa hiyo.

Kwa kuzingatia suala hili la mgongano wa kimaslahi, manung’uniko mengi kutoka kwa wapokea huduma, hususan katika Taasisi yetu ya Saratani ya Ocean Road, nimechukua hatua ya kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi,” iliongeza taarifa ya waziri huyo.

Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Latoa Kauli yake Kuhusu Shutuma za Kurusha Sherehe ya Harusi Laivu Kwa Masaa Mawili

$
0
0
Shirika la Utangazaji TANZANIA TBC limesema halijakiuka sheria za utangazaji kufuatia kipindi  maalumu cha chareko kilichorushwa na kituo hiki Desemba 19 siku ya jumamosi na kuwa kilichofanyika ni ubunifu wa vipindi.

Akizungumzia suala hilo Mkurugenzi Mkuu wa TBC, CLEMENT MSHANA amesema mteja wa kipindi hicho alitaka harusi yake irushwe moja kwa moja ambapo pia alipewa maelekezo ya kuzingatia wakati kipindi kitakapokuwa kikirushwa.

MSHANA amesema TBC ipo tayari kupokea maoni mbalimbali ya watazamaji wake ili kuboresha utendaji kazi wa chombo hicho, ambapo amewataka watazamaji kuendelea Kutazama TBC

Hii inakuja kufuatia hivi kitendo cha shirika hilo la umma kuamua kurusha ‘live’ harusi,kitu ambacho kililalamikiwa na wadau wengi hususani watazamaji wa kituo hicho,hali iliyompelekea Waziri wa Habari,sanaa na michezo Nnape Nnauye kumtaka Mkurugenzi huyo kujieleza ni kwa nini chombo hicho cha umma kinadiriki kufanya mambo hayo

Believe It or Not, This US Based Socialite Who Services Celebraties Is a Kenyan

$
0
0

Did you know that popular American socialite, Mercedes Morr, who is known for her services to celebrities, was born in Kenya?

Mercedes, who dropped out of school to be a socialite, was once a student at Braeburn School.

Check her out:



Samwel Sitta: Magufuli Anashauriwa Vibaya!

$
0
0

Katika ile dhana ya kusoma namba, ni wazi imeendelea kuwatafuna wanachama wa chama changu. Katika gazeti la leo, aliyekuwa spika wa bunge la tisa ametoa kali na kusema Rais Magufuli anashauriwa vibaya. Hasa baada ya kutumbua jipu la Reli. 

Samwel Sita, kasema Magufuli kachukua hatua hiyo baada ya kushauriwa vibaya, na vile vile ingemfaa achukue muda wa kujiridhisha kwanza!... 

Mtanzania, 24.12.2015

Ushauri kwa CHADEMA: Tumeshindwa Uchaguzi, Mbowe Beba Mzigo

$
0
0
Ni wazi kwamba CHADEMA ilianzishwa ili kuwa tofauti na CCM na vyama vingine. Tofauti hii lazima iwe dhahiri na ya kivitendo. CHADEMA iendeshwe kama vyama vya wenzetu kule Ulaya. Chama kikifanya vibaya ktk chaguzi kiongozi anawajibika. Uwajibikaji wa jumla " collective accountability".

Baada ya uchaguzi na michakato yake yote kukamilika chadema imepata nafasi ya pili, huku ikipata wabunge na madiwani kiduchu sana ukilinganisha na harakati, matarajio na nguvu iliyotumika.

Sasa nilitarajia na bado ninatarajia kuona vikao vya tathmini vikikaa na kufanya upembuzi wa kina kubaini sababu ya kushindwa kwenda ikulu na kuambulia wabunge na madiwani kidogo kiasi hiki.

Ni dhahiri kuwa kuna uzembe wa kupanga mikakati ya kupata ushindi mnono uliofanywa na viongozi wa ngazi zote. Hapa ndipo Kamanda Mbowe anabeba gunia la lawama kama kiongozi wa juu wa chama.

Alikuja na mbinu ya kubadili gia angani sawa Lakini je, mbinu hii ya kubadili gia angani imeleta athari gani chanya na hasi kwenye chama? Ukiziweka kwenye mizania athari hizi chanya na hasi, zipi zina uzito kuliko nyingine? Chama bado kina kasi ya kupendwa ama sasa kimefifishwa na mbinu ya kubadili gia angani?

Watu wengi huko mitaani wanaona CHADEMA ina wenyewe, na wenyewe ni akina Mbowe waliokaa Kitako wakamkaribisha Lowassa kisha mkutano mkuu ukaitishwa kama bosheni tu kuja "kuthibitisha" kilichoamriwa na "wakubwa".

Hii imepunguza ari ya kuibeba CHADEMA moyoni kama mwanzo. Maana wameona mpambanaji mwenzao Dr. Slaa aliyeumia ktk harakati za kukijenga chama na mkewe aliyevuja damu walivyopuuzwa na kutoswa kwa udhalili. Hii INA madhara makubwa kwa chama.

Sasa kamanda Mbowe jiuzuru ili aje mwingine na timu yake wafanye mikakati mipya ya kurudisha misingi ya chadema. Ikibidi hata kwa kuwafukuza waliokuja kufifisha nuru ya chama.

Aingie mtumbua majipu ndani ya chadema asafishe na kujenga matumaini mapya kwa wanachama. Vinginevyo chama kimekwama kwenye tope.

Wazohuru Toka Kwa G4N/Jamii Forums

Shamsa Ford: Sitaki Tena Kutoka Kimapenzi na Mastaa...Kisa na Mkasa?

$
0
0
Msanii wa filamu na mama wa mtoto mmoja, Shamsa Ford amesema amekoma kutoka kimapenzi na watu maarufu.

Muigizaji huyo ambaye miezi michache iliyopita alikiri kutoka kimapenzi na rapa Nay wa Mitego, ameiambia Bongo5 kuwa sasa hivi amepata mpenzi mpya ambaye atamweka wazi siku ya harusi yake.

“Mimi ni mwanamke mzuri nakosaje mwanaume? Nimetimia kila idara, nina mchumba ambaye tunapendana Mungu akijalia kiukweli natamani awe mume wangu,” amesema.
“Nimeshatangaza kabisa mastaa sitaki nimekoma, nimekoma kutoka kimapenzi na mastaa au kumtangaza mpenzi wangu kwenye mitandao. Mpenzi wangu watamjua siku ya harusi yangu. Unajua mastaa wana mambo mengi sana na kuendelea nao ni kupoteza muda tu” amesisitiza Shamsa Ford.

Hata hivyo Shamsa hakutaka kuzungumzia sababu ya kuachana na Nay.

Bongo5

Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kupiga Marufuku Mikutano ya Wapinzani Kushukuru Wananchi ni Sahihi?

$
0
0
Mh. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amepiga marufuku mikutano ya wapinzani ya kushukuru wananchi. Kasema mtu aliyeshindwa atashukuru nini kama siyo kuleta vurugu?

Kaonya wakuu wa mikoa na polisi watakaotoa vibali watashughulikiwa bila huruma

Wastara Juma Aamua Kufunguka na Kumtaja Mwanaume Anaye Mpenda Kwa Dhati...Adai Anafanana na Sajuki

$
0
0
"Mama na mwana mama na baba nimeipenda kama ilivyo ila kiukweli huyu jamaa nampenda mfano hakuna, mpole muelewa hana makuu anao ubinadaamu hana ugomvi na mtu, mpole ajui kufoka wala kugombana akikasirika dk 2 tu anarudi kuwa normal. Sichoki kufanya nae kazi namchukulia ni mdogo wangu wa tumbo moja namfananisha vitu vingi na Sajuki si mwingine ni      Yusuph Mlela au Mlelandro"

Hayo ni maneno ya mwigizaji Wastara Juma kwenye moja ya post zake kwenye mtandao picha wa instagram mara baada ya kuweka picha hiyo hapo juu akiwa Yusuph Mlela

She’s The Real Boss Lady! See What VERA SIDIKA Eats For Breakfast (PHOTOs)

$
0
0
As most of Kenyans live from hand to mouth due to harsh economic times, s3xy socialite, Vera Sidika, is rolling like a queen and tasting the finer things in life.

The money she spends on her heavy breakfast can be used to feed your family for several days and to prove this, Vera posted photos of what she eats for breakfast.

Check this out.






Rais Kagame Awapa Mbinu Viongozi wa Burundi Kutafuta Suluhu

$
0
0
Rais wa Rwanda Paul Kagame amewashauri raia wa Burundi kumaliza mgogoro unaoendelea nchini humo kwani hakuna mtu wa nje anayeweza kufanya hivyo.

Rais Kagame alisema kuwa, viongozi na nchi hiyo na raia hao wana wajibu wa kushughulika na mambo yao ya ndani kuliko kutegemea msaada wa watu wengine.

“Siyo kweli kwamba Rwanda inafurahia mgogoro wa kisiasa unaoendelea Burundi kwani athari zake zinatugusa hata huku. Wakimbizi wanazidi kuongezeka hivyo ni vyema wakatafuta ufumbuzi haraka iwezekanavyo kuyanusuru maisha ya watu,” alisema.

Kiongozi huyo alikanusha uvumi kwamba nchi yake imekuwa ikisaidia baadhi ya makundi ya wapiganaji yanayopingana na Serikali ya Burundi.

“Hayo ni madai ya yasiyo ya kweli na kama kuna mwenye ushahidi kuhusu hilo athibitishe. Huu siyo wakati wa lawama kwani jambo la muhimu ni suluhu itakayomaliza mgogoro huo,” alisema.



Amuunga mkono Museveni

Katika hatua nyingine, Kagame alionyesha kumuunga mkono Rais wa Uganda Yoweri Museveni anayewania madarakani kwa muhula wa tano.

“Ukiniuliza mtazamo wangu kuhusu Uganda jibu ni kwamba nimefanya kazi vizuri na viongozi waliopo madarakani hivyo nawatakia kila la heri kwenye uchaguzi ujao,” alisema na kuongeza kuwa:

“Naamini waganda ni watu wenye akili timamu na uelewa wa kutosha utakaowawezesha kufanya uchaguzi sahihi bila kuleta machafuko katika nchi yao.”

Kuhusu uamuzi ambao mataifa ya magharibi yanaweza kuchukua kutokana na kufanyika mabadiliko Katiba ya Rwanda, Kagame alisema Warwanda hawawezi kuishi kwa kufuata matakwa ya watu wengine.

“Wanyarwanda wataishi wanavyotaka. Hatuwezi kuwa waoga na watiifu kupita kiasi kwa vile tunategemea misaada kutoka kwa wahisani, binafsi sidhani kama kuna matatizo makubwa yanayoweza kutokea na yakawa zaidi ya yaliyowahi kutukuta,” alisema.


Uamuzi wa bunge

Juzi, Bunge la Burundi lilipinga mpango wa Umoja wa Afrika wa kutaka kutuma kikosi cha kusimamia amani katika nchi hiyo inayokabiliwa na mgogoro wa kisiasa.

Spika wa Bunge hilo, Pascal Nyabenda alisema hakuna dharura ya kutuma kikosi cha umoja huo nchini humo.

Kwa upande wake, Spika wa Baraza la Seneti la Burundi, Reverien Ndikuriyo alisisitiza kuhusu tofauti baina ya mauaji na mauaji ya kimbari.

Wabunge na wawakilishi wa baraza hilo wakiwa katika kikao chao, walikubaliana kwamba Serikali ifanye kila iwezalo kukomesha mauaji yanayohatarisha amani nchini humo.

Ijumaa iliyopita Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika llilipitisha uamuzi wa kupeleka kikosi cha askari 5,000 nchini humo.

Kabla ya hatua hiyo ya Bunge na Baraza la Seneti, Msemaji wa ofisi ya Rais alikuwa ametoa radiamali yake kuhusiana na uamuzi wa Umoja wa Afrika wa kutaka kutuma kikosi cha kusimamia amani Burundi na kutangaza kuwa, endapo AU itatuma kikosi hicho na kupuuza upinzani wa Serikali kwa hatua hiyo, vikosi hivyo vitahesabiwa kuwa ni majeshi vamizi.

Viongozi wa Serikali wanadai kuwa vitendo vya utumiaji mabavu vya vikosi vya usalama vinafanyika katika fremu ya kurejesha amani na usalama, wapinzani wanasema kuwa, hatua hizo ni za ulipizaji kisasi dhidi yao na lengo lake ni kuwauwa wapinzani wa serikali.

Katika hali ambayo, weledi wengi wa masuala ya kisiasa wanatahadharisha juu ya uwezekano wa kutokea vita vya ndani na kuanza mauaji mengine ya kimbari Burundi, Umoja wa Afrika umetangaza kuwa hautaruhusu kuanza vita na kutokea mauaji mengine ya kimbari barani humo.

Waziri wa Ulinzi wa Uganda, Crispus Kiyonga ambaye nchi yake ni mpatanishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mgogoro wa Burundi alitangaza hivi karibuni kwamba, njia bora kabisa katika mazingira ya hivi sasa na hali ya usalama inazidi kudorora nchini humo ni kuanza mazungumzo kwa minajili ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa nchi hiyo.

Kiyonga alisema, viongozi wana mambo 10 ambayo wanataka yatiwe katika ajenda ya mazungumzo ya tarehe 28 Desemba.

Miongoni mwa mambo hayo ni utawala wa awamu ya tatu ya uongozi wa Rais Pierre Nkurunziza, jedwali la uchaguzi, hali ya usalama pamoja na serikali ya umoja wa kitaifa.

Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha, zaidi ya watu 240 wameuawa na zaidi ya 200,000 wakilazimika kuyakimbia makazi yao, kutokana na machafuko hayo tangu Aprili mwaka huu.

Machafuko hayo yalitokea baada ya chama tawala CNDD-FDD kumwidhinisha Rais Pierre Nkurunziza kugombea urais kwa muhula wa tatu mfululizo.

Wapinzani Burundi walisema, hatua ya Nkurunziza kugombea kiti cha urais katika uchaguzi uliopita ilikuwa kinyume na katiba.

Mjengo Mpya wa Wema Sepetu ni Utata Mtupu..........

$
0
0
UTATA umegubika kuhusu umiliki wa mjengo aliohamia staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ambapo maswali yanayowasumbua wengi ni je, ameingia kwa kupanga au ameununua? Amani linakwenda sambamba na msomaji.
wema (2)
TUANZIE HAPA

Hivi karibuni, Wema aliyekuwa akiishi kwenye nyumba ya kupanga iliyopo Kijitonyama ya Makumbusho jijini Dar, alidaiwa kutimuliwa na mwenye nyumba baada ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (Dawasco) kumtumbua jipu la madai ya kuchakachua huduma hizo.
wema (2)Wema Isaac Sepetu
ATII AMRI, AHAMA
Wema aliihama nyumba hiyo usiku wa Ijumaa iliyopita lakini haikujulikana mara moja anakokwenda kuishi licha ya lori lililomhamisha, aina ya Toyota Canter kuandikwa nyuma, ‘Mtu Kwao’.
wema (3)
HABARI ZA JUMANNE SASA

Juzi Jumanne, chanzo kimoja kililipasha Amani kwamba Wema amehamia kwenye mjengo mkubwa na mzuri uliopo Ununio, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
“Jamani nilisoma habari kwenye Gazeti la Ijumaa Wikienda (ndugu na hili) la Jumatatu jana, zikisema kwamba Wema ametimuliwa kwenye ile nyumba ya Makumbusho lakini hamkusema amehamia wapi.
“Sasa mimi nawapa ubuyu. Wema amehamia hapa Ununio. Amepata nyumba nzima, kubwa. Lakini nisiwe msemaji wake mkuu, sijajua ni yake au amepanga,” kilisema chanzo hicho.
PAPARAZI WETU NYUMBANI KWA WEMA
Baada ya chanzo kuanika madai hayo, paparazi wetu alikanyaga mafuta akifuata maelezo ya chanzo mpaka kufanikiwa kufika kwenye nyumba hiyo.
wema (4)
SIFA ZA NYUMBA

Ni nyumba kubwa kuliko aliyokuwa akiishi Makumbusho. Ina eneo kubwa linalokaribiakaribia ukubwa wa uwanja wa mpira. Magari makubwa matano na madogo kumi yanaweza kuegeshwa eneo la wazi la ndani.
Pia Wema anaweza kufanyia ndani kwenye uwazi huo zile sherehe zake. Na kuna madai kwamba anaandaa sherehe kubwa kwa ajili ya kuumaliza mwaka 2015 akiwa mzima wa afya njema.
PAPARAZI AZUIWA KUINGIA NDANI
Hata hivyo, paparazi wetu alipotaka kufanya utalii wa ndani, alipigwa stop na msichana mmoja aliyejitambulisha kuwa ni ndugu wa Wema pia akimhoji paparazi wetu alifikaje ndani ya ukuta wa nyumba hiyo na kusema Wema hakuwepo.
Lakini kwa macho ya haraka, paparazi wetu alibaini kuwa nyumba hiyo ina vyumba vya kulala vinne, stoo, jiko, bafu na choo kwa ajili ya jumuiya, sehemu ya kulia chakula na sebule kubwa.
AMANI LAFANYIA KAZI UTATA
Licha ya msichana huyo kumkataza paparazi wetu kuzama ndani na kujionea kwa macho yake yaliyomo, alimuuliza kama anajua Wema ni mpangaji au mmliki. “Wema amejenga hii nyumba.
We huoni kuwa ni mpya! Watu wanadhani Wema hawezi kujenga nyumba siyo! Loo! Wataisoma namba mwaka huu,” alisema msichana huyo.
PETIT MAN
Katika kuchochea utata huo, paparazi wetu alibahatika kukutana uso kwa uso na mpambe mkubwa wa Wema, Petit Man ambaye jina lake halisi ni Ahmed Hasheem na kuzungumza naye kuhusu kutolewa Makumbusho na kuhamia huko kwa sasa.
Alisema: “Tena sasa tunahamia kwenye nyumba aliyonunua Wema mwenyewe. Bonge la nyumba, mtaipata habari yake. Iko Mbezi Beach.” (Ununio huhesabika kuwa ipo Mbezi Beach).
NANI MKWELI?
Madai ya msichana aliyekutwa nyumbani, anasema Wema amejenga nyumba hiyo. Ina maana alipata kiwanja, akatafuta mafundi, wakaanza ujenzi. Madai ya Petit Man ni kwamba Wema ameinunua! Kwamba, nyumba hiyo ilijengwa na mtu mwingine, akaamua kuiuza, akanunua Wema.
WEMA HAYUPO HEWANI
Juzi, paparazi wetu alimsaka Wema kwa simu ya mkononi ili kumsikia anasemaje lakini hakuwa akipatikana hewani.
MENEJA WA WEMA
Paparazi wetu alimpigia simu meneja wa Wema, Martin Kadinda na kumuuliza kuhusu umiliki au upangaji wa nyota huyo kwenye nyumba hiyo ya Ununio.
“Kusema kweli nilisafiri, ndiyo nimerudi usiku wa jana. Muda huu najiandaa kwenda kukutana naye. Nitakuwa na majibu baadaye,” alisema Kadinda.

Source:Global Publishers

Mchungaji Kiongozi Kanisa la KKKT Jela Kwa Wizi.......

$
0
0
Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Rauya, Zawadiel Maruchu amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la wizi wa kuaminiwa.

Usharika aliokuwa anahudumu mchungaji huyo upo Mambo katika Jimbo la Kilimanjaro Mashariki la Dayosisi ya Kaskazini.

Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Himo – Moshi, Shaban Mkude baada ya kuridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka.

Kesi hiyo ya jinai namba 417/2015, ilifunguliwa na mlalamikaji Judith Matemba, akimtuhumu mchungaji Maruchu kwa kujipatia Sh8.3 milioni kwa njia ya udanganyifu.

Kosa hilo ni kinyume na Kifungu namba 304, Sura ya 16 ya Kanuni ya Adhabu kama ilivyofanyiwa marejeo na Bunge mwaka 2002, kosa ambalo adhabu ni kifungo cha miaka mitatu. Awali, mwendesha mashtaka, Koplo Patrick Mgiriama alidai mahakamani kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Septemba 16, 2011 akimshawishi Judith anunue kiwanja eneo la Njiapanda ya Himo.

Siku hiyo mshtakiwa alimfuata mlalamikaji dukani kwake na kumshawishi kuwa kuna kiwanja kinauzwa karibu na Sekondari ya Muungano kwa Sh8.3 milioni.Hakimu alisema mshtakiwa ndiye aliyewachukua mlalamikaji na mumewe na kwenda kuwaonyesha kiwanja hicho na kwa vile mshtakiwa ni kiongozi wa kiroho alimwamini na kukubali kukinunua. Makubaliano ya mauzo hayo yalifanyika nyumbani kwa mchungaji na baada ya kukabidhiwa fedha hizo, alizifanyia sala fupi na kuahidi kumpelekea muuzaji ambaye alimtaja kuwa ni Boniventura Kilawe.

Hata hivyo, ilibainika baadaye kuwa kiwanja hicho kilikuwa kinamilikiwa na mtu mwingine aliyekuwa na hati za umiliki na jitihada za mlalamikaji kutaka arudishiwe fedha zake hazikuzaa matunda. Hakimu Mkude alisema baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili na kuuchambua, alimtia hatiani mshtakiwa huyo kwa kosa hilo na kumhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela. Hata hivyo, kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mshtakiwa aliomba apunguziwe adhabu kwa maelezo kuwa anategemewa na familia, ana matatizo ya kiafya na ni kiongozi wa kiroho.

Baada ya kusikiliza maombi ya mchungaji huyo, hakimu alisema ameyazingatia hivyo anamhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela na atakapomaliza alipe fedha hizo.

Jana, mlalamikaji katika kesi hiyo alisema baada ya kutolewa kwa hukumu, ndugu wa mfungwa huyo walitafuta fedha hizo na tayari amelipwa hivyo yatakayoendelea yeye hayamhusu tena.


Madee Amdiss Afande Sele, ni Baada ya Kuwaponda Wanaoshoot Video South

$
0
0
Kauli ya Afande Sele kuwa wasanii wanaoenda kushoot video zao Afrika Kusini wanafanya biashara za siri, haijamuingia vyema hasimu wake wa muda mrefu, Madee.

Bongo5 iliongea na msanii huyo mkongwe wiki hii na kudai kuwa haoni sababu ya maana wasanii wa Tanzania kwenda kufanya video zao nje ya nchi.

Kwenye kushoot video nje ni ulimbukeni,” alisema.

Tanzania tuna kila kitu kuliko hata huko wanakoenda. Mimi hii naitafsiri ni usaliti wa nchi, sisi tunakosa nini hapa nyumbani? Tuna milima, mbuga, maporomoko mazuri, yaani tuna kila kitu. Unajua wasanii wengi walikuwa wanatumia mwanya wa kwenda kushoot video nje ili kufanya biashara zao za siri. Wengi wameutumia sana huu mwanya, sasa Magufuli alivyoingia atawanyoosha tu,” alisisitiza Afande.

Kupitia Twitter, Madee aliandika: Kadri unavozidi kuzeeka na akili nazo zinarudi utotoni na kuambatanisha screeshot ya kichwa cha habari cha habari ya Afande.


Hata hivyo Madee amefafanua zaidi kupitia website ya Millard Ayo ambapo amemtaka Afande aombe radhi kwa kauli hiyo:

Unajua yale ni matusi kwenye muziki kwenye Bongo Fleva halafu watu kama Afande Sele ndio waanzilishi wa huu muziki sasa muziki unapoelekea sasa ni kwenye level ya kimataifa muziki unakua kwahyo vitu alivyokuwa anafanya yeye mwanzo..kwasasa anaviona vipya anaona kama maajabu watu kumiliki hela nyingi…astaajabu na kuhisi labda wasanii wanafanya ishu nyingi.

Anazungumzia suala la wasanii kushoot nje ya nchi Labda tuchukulie mfano John Legend alipotoka kwao Marekani ambapo kuna vitu vingi na kuja Zanzibar kushoot video yake Je alikuja kufanya vitu vya siri eeeh! Hii ni katika harakati za kutanua wigo wa muziki, watu wanataka kufanya vile vitu ambavyo hatukuwahi kufanya ili twende sawa na soko la kimataifa.

Sasa wewe Baba au Babu yetu ambaye unastaajabu kuona watu wanatoka kwenda kushoot sehemu nyingine wewe unasema wanaenda kufanya vitu vya ajabu unakuwa unatukatisha tamaa sisi ambao tumeachiwa hii nafasi kwahiyo nikiwa kama msanii namuomba Afande Sele awaombe radhi wasanii wote kwa ujumla kutokana na kauli yake aliyoizungumza sio nzuri.

Afande na Madee wamewahi kuwa na beef.

Ben Pol Ampigia Magoti Alikiba, Wayamaliza, Huenda Wakafanya Collabo

$
0
0
Wagombanao ndio wapatanao. Baada ya wiki nzima ya kuoga matusi kutoka kwa mashabiki wa Alikiba kutokana na kauli yake ya utata kwenye Twitter, Ben Pol amekiri kuwa aliteleza na kumuomba radhi muimbaji huyo wa Nagharamia.

Akiongea kwa simu kupitia kipindi cha Jahazi cha Clouds FM Alhamis hii ambako Kiba alikuwepo studio, Ben Pol alisema yeye ni shabiki mkubwa wa Kiba na anamchukulia kama kaka yake na amekiri kuwa tweet ile haikuwa sawa.

Mimi shabiki wa Kiba, moyoni mwangu nina furaha kubwa kuona kwamba tuko sawa kwa sasa,” alisema Ben ambaye aliimba wimbo ‘Njiwa’ wwa muimbaji huyo wakati wa mahojiano hayo.

Kwa upande wa Alikiba, alisema alishamsamehe muimbaji huyo wa ‘Ningefanyeje’ kitambo.

Ben Pol mimi bana kiukweli nilikuwa nimekusamehe toka nilivyokuwa nimeona ile lakini kwasababu nilishtushwa kama watu wengine walivyoshtuka nikajua labda utakuwa umeghafilika, lakini kiukweli mimi nilishtuka nilivyoona vile,” alisema Kiba.

Najua ulikosea ndio maana nikaona basi yaishe kwasababu binadamu tunakuwaga na makosa hayo.”

Ben Pol alimalizia kwa kusema, “Mwenyezi Mungu anakuwga na mipango yake, hatuwezi jua, pengine hapo mbele kunaweza kuwa na bonge ya collabo.”

UNAHISI COLLABO YA ALIKIBA NA BENPOL ITAKUWA MOTO?


Viewing all 104684 articles
Browse latest View live


Latest Images