Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Daaaamn!! Check Out Tanzania’s AGNES MASOGANGE’s Big Boo.ty…. Who ‘Eats’ This?

$
0
0

 Daaaamn!! Check Out Tanzania’s AGNES MASOGANGE’s Big Boo.ty…. Who ‘Eats’ This?



KIMENUKA Burundi....Waasi Wacharuka Waunda Umoja na Kutangaza Vita ya Kumg'oa Rais Pierre Nkurunziza

$
0
0
Waasi wanaompinga Rais Pierre Nkurunziza wameungana kuunda vuguvugu moja linalofahamika kama The Republican Force of Burundi, na limetangaza vita dhidi ya kiongozi huyo.
Kubuniwa kwa vuguvugu hilo kunatukia huku shinikizo kutoka kwa mataifa ya kanda hiyo, zikiongezeka.

Umoja wa Afrika unaitaka serikali ya Nkurunziza ikubalie walinda amani wa Umoja wa Afrika.
Hata hivyo serikali yake imekatalia mbali ombi hilo ikidai kuwa, haiko katika hali ya mapigano yawenyewe kwa wenyewe wala hakuna hatari ya kuibuka kwa mauaji ya kimbari kwa hivyo inaichukulia jeshi hilo la kulinda amani kama jeshi la kigeni na "kikosi cha uvamizi".

Umoja wa Afrika unaitaka serikali ya Nkurunziza ikubalie walinda amani wa Umoja wa Afrika.
Tanzania imejitokeza kupinga mpango huo wa AU wa kuwatuma wanajeshi elfu tano, wa kulinda amani wanaopangiwa kwenda Burundi, kusaidia kukomesha ghasia na umwagikaji zaidi wa damu.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Tanzania Augustine Mahiga, yuko katika ziara ya kidiplomasia nchini Uganda na kisha Burundi kuhusiana na mzozo huo katika taifa hilomojawepo ya kanda ya Afrika Mashariki.

Rais wa Uganda anatarajiwa kuongoza mchakato wa amani kuanzia jumatatu
Msemaji wa serikali ya Burundi Willy Nyamitwe amenukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa hofu ya kuibuka kwa kundi lipya la waasi sio tishio katika serikali ya Burundi.
Nyamitwe anasema kuwa Republican Forces of Burundi, ama "Forebu" haitadumu.
''sio mara ya kwanza kwa makundi ya waasi kuibuka hapa Burundi. Tutawakanyaga mara moja''
Nyamitwe anasema kuwa Burundi ina haki ya kimsingi ya kulinda maisha na usalama wa wananchi wake na kuwa haitachelewa kuwazima mara moja.

Vanessa Mdee Afunguka Sababu ya Kung’ara Kimataifa Kuliko Wasanii Wengine wa Kike wa Kibongo

$
0
0
Staa wa Bongo Fleva,Vanessa Mdee ‘V Money’ amefunguka sababu za kung’ara kwa mziki wake na kubahatika kupata tuzo kadhaa za Kimataifa kuliko wasanii wengine wa kike wa Kibongo.

Ujue kuna tuzo zingine zinatofautiana kuna zingine wapo wasanii wa Kitanzania ambao tuzo fulani wametajwa, na zingine hawakubahatika kuwepo,ukweli ni kuwa wale wanaoandaa tuzo pia wanaangalia ni msanii gani anafahamika zaidi kutoka nchi fulani yaani msanii anakuwa anajiuza mwenyewe zaidi Kimataifa,’’Alisema Vanessa Mdee.

Pia baadhi ya wasanii wa Kitanzania ambao wametajwa kwenye tuzo pengine wamepata soko(mashabiki) na nafasi ya kuafahamika zaidi kwenye nchi ambayo imetoa tuzo hizo,”alisema Vanessa Mdee.

Cloudsfm.com

Mama Lulu Michael Atia Ngumu Mwanae Kuondoka Nyumbani na Kwenda Kuishi Mwenyewe Geto...

$
0
0
Marufuku! Mama mzazi wa staa wa Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila ametia ngumu mwanaye huyo kuondoka nyumbani kwake na kwenda kuishi peke yake kwa kuwa bado anahitaji zaidi kufuata maadili yake.

Mama Lulu aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, hawezi kumruhusu Lulu kwenda kupanga na kuishi peke yake wakati bado ni mdogo na kwamba bado anahitaji aishi katika maadili ya mzazi.

Chanzo:Global Publishers

Serikali yapiga Marufuku Matangazo ya Tiba za Asili

$
0
0
Taarifa kwa vyombo vya habari

Ndugu mwanahabari

Wizara ya afya kuanzia leo 24 Desemba 2015 imepiga marufuku matangazo yote yanayohusu tiba asili na tiba mbadala kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Kwa wale wenye vibali wanatakiwa kuviwasilisha vibali na matangazo yao kwenye Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala ili vifanyiwe mapitio.

Utoaji wa elimu ya afya kwa umme unaofanywa na watoa huduma za tiba asili na tiba mbadala kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii umepigwa marufuku hadi hapo utaratibu mwingine utakapotangazwa.

Watoa huduma za tiba asili na tiba mbadala nchini kote wanaagizwa wawasilishe kwenye Baraza nyaraka zote muhimu ndani ya wiki mbili kuanzia leo Desemba 2015. Baadhi ya nyaraka hizo ni zile zinazohusu kuuza dawa za asili na tiba mbadala, nyaraka za kumiliki mashine zinazotumika katika kufanya uchunguzi katika tiba asili na tiba mbadala

Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala linaagizwa katika kipindi cha siku 14 kuanzia leo 24 Desemba 2015, lipitie nyaraka zote zikapowasilishwa zinazohusu usajili wa watoa huduma, usajili wa vituo vyao, ikiwa ni pamoja na maduka ya dawa za asili na dawa za tiba mbadala, usajili wa dawa zote zinazotumika katika huduma hizo na usajili wa mashine zote zinazotumika katika huduma za tiba asili na tiba mbadala.

Taarifa hiyo imetolewa na Dismas Lyassa kwa niaba ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Hamis Kigwangala na kusainiwa na M.O John, Kaimu Katibu.

Afisa wa Intelijensia wa TANAPA Aliuawa na Mfanyakazi Wake Wa Ndani Kwa Kukatwa Panga Wakati Akinywa Uji.....

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani hapa limefanikiwa kumkamata mtu mmoja aitwaye Ismail Swalehe Sang’wa (20) ambaye ni mwenyeji wa kijiji cha Sepuka wilayani Ikungi katika Mkoa wa Singida kwa tuhuma za kumuua Afisa wa Intelijensia wa TANAPA aitwaye Emily Kisamo (52).

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana  asubuhi , Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas alisema tukio hilo la mauaji ya Afisa huyo wa TANAPA lilitokea tarehe 18.12.2015 muda kati ya saa 2:30 asubuhi hadi saa 4:00 asubuhi mtaa uitwao Corridor Area Uzunguni jijini  Arusha.

Kamanda Sabas alisema kwamba, siku ya tukio hilo marehemu alikuwa nyumbani kwake sebuleni akiwa anakunywa uji ndipo mtuhumiwa ambaye ni mfanyakazi wake wa ndani  alimvizia na kumkata shingo na kitu kinachoaminika kuwa ni panga na kisha kuchukua mwili wake na kuuweka kwenye gari la marehemu aina ya Nissan Mazda lenye namba za usajili T. 435 CSY.

“Baada ya kuuweka mwili wa marehemu kwenye buti alilisafisha gari hilo kwa nje na kisha kuliendesha mpaka eneo la kikwakwaru “B” kata ya Lemara ambapo alilitelekeza hapo na kisha yeye kuondoka”. Alifafanua Kamanda Sabas.

“Mara baada ya gari hilo kukaa mpaka saa 2:00 usiku ndipo baadhi ya wananchi wa eneo hilo walitoa taarifa kwetu ambapo askari wa doria walikwenda na kulichukua gari hilo kwa kulivuta mpaka kituoni. Kwa kuwa mke wa marehemu aitwaye Caroline Lukumay (38) alikuwa anamtafuta mume wake kwa njia ya simu bila mafanikio ndipo alipoamua kuja kituoni kutoa taarifa ambapo tulimuonyesha gari lililotelekezwa ambalo alillitambua mara moja”. Alisema Kamanda Sabas.

Aliongeza kwa kusema kwamba askari walimuomba mke wa marehemu funguo za akiba za gari hilo ambapo baada ya kulifungua ndipo walipouona mwili wa marehemu kwenye buti akiwa na vitu mbalimbali kama vile simu mbili aina ya Sony na Panasonic, pesa taslimu Tsh 300,000, Laptop aina ya Asus na kadi za benki tofauti tofauti.

Mara baada ya mtuhumiwa huyo kukamatwa alikiri kuhusika na mauaji hayo na kusema siku hiyo walikuwa wawili tu yaani yeye na mrehemu na alifanya hivyo kwa kuwa alikuwa na tamaa za fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya nyumba hiyo kiasi cha Tsh. Mil.5.

Upekuzi zaidi wa Jeshi la Polisi ulibaini kuwepo kwa fedha taslimu Tsh. 4,294,000, simu tatu aina ya Sumsang na vocha za mtandao wa vodacom za sh. Elfu tano tano zenye thamani ya Tsh. 70,000 ambapo vyote vilifukiwa kwenye banda la kuku.

Mbali na vitu hivyo pia mtuhumiwa Ismail Swalehe Sang’wa aliweza kuonyesha panga lenye damu ambalo alilihifadhi stoo pamoja na taulo nne kubwa, kitambaa cha mezani na suruali yake ambazo zilikuwa na damu na alizitumia yeye mwenyewe kupigia deki sebuleni baada ya tukio na kisha kuzificha kwenye migomba karibu na mabanda ya kuku.

Kamanda Sabas alimalizia kwa kusema kwamba Jeshi hilo linawashikilia watuhumiwa watatu wengine mbali na Ismail Swalehe Sang’wa akiwemo mke wa marehemu, rafiki wa mke wa marehemu ambaye ni mwanamke na dereva wa nyumbani wa marehemu kwa mahojiano zaidi.

Serikali Yawapiga STOP Akina Lowassa Na Wenzake Kufanya Mikutano ya Hadhara

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu hawaruhusiwi kuitisha mikutano ya hadhara kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa kuwa wanaweza kuvuruga shughuli za maendeleo.

Waziri Mkuu alisema hayo wakati akilishukuru Jeshi la Polisi wilayani Ruangwa kwa kufanya kazi ya kusimamia Uchaguzi Mkuu uliomalizika Oktoba 25 kwa CCM kushinda kiti cha urais na kuzoa takriban viti 180 vya ubunge.

Naendelea kuwashukuru kwa mchango wenu mkubwa kiulinzi, lakini pia usimamizi wa zoezi zima la uchaguzi na hatimaye hivi sasa watu wameshapatikana,” alisema Waziri Majaliwa nje ya ofisi za jeshi hilo.

Na tumesema, siasa tumeshazimaliza. Sasa tunataka tufanye kazi za maendeleo. Hatuhitaji tena watu kuja kutuvuruga. Mikutano ya shukrani itafanywa na wale tu walioshinda kwenye maeneo yao. Wengine watulie.

Vyama sasa viache wale tu waliochaguliwa kwenye maeneo yao washukuru, wengine hawa watakuja kuleta maneno ambayo yatatuvuruga. Mimi naamini mko imara.”

Wakati Waziri Majaliwa akisema hayo, tayari Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea urais wa Chadema na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alishapanga kuanza ziara ya kuzunguka nchi nzima kwa lengo la kuwashukuru wananchi waliompigia kura.

Hata hivyo, ilipofika siku ya kuanza ziara hiyo, Chadema ilitangaza kuwa imeahirisha hadi itakapotangazwa tena, ikiweka bayana kuwa uamuzi huo hautokani na vitisho vya makamanda wa polisi wa mikoa.

Awali, amri ya kuzuia mikutano ya kisiasa ilikuwa ikitolewa kwenye mikoa na baadhi ya makamanda wa polisi, lakini tamko hilo la juzi la Waziri Majaliwa linatia msumari marufuku hiyo ya kuendesha shughuli za kisiasa kwa hoja ya kushukuru wananchi.

Lowassa, ambaye alihamia Chadema siku chache baada ya kukatwa jina lake na CCM mwezi Julai, aliweka rekodi ya kuwa mgombea wa upinzani aliyepata kura nyingi baada ya kupigiwa kura na watu milioni 6.07 ikiwa ni asilimia 39.9, huku mshindi akipata kura milioni 8.88 sawa na asilimia 58.46.

Tamko hilo la Waziri Majaliwa tayari limeanza kupingwa sehemu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kwenye mitandao ya jamii na vyama vya siasa kutoa matamko.

Hii ni kauli ya ajabu kutolewa na mtu anayesimamia utendaji wa shughuli za kila siku za Serikali inayotaka kuwaaminisha (wananchi) kuwa itakuwa tofauti na serikali nyingine zilizopita za CCM,” inasema Chadema katika tamko lake la jana jioni kujibu kauli ya Waziri Majaliwa.

Kama wao (CCM) ndiyo walioshinda kama ambavyo Waziri Mkuu Majaliwa amesema na kwamba wanaendelea kutekeleza wajibu waliokabidhiwa na wananchi, tunahoji hofu yao nini hasa wakiona au wakisikia Chadema wanapanga kwenda kuongea na wananchi? Wanaogopa nini?”

Taarifa hiyo iliyotolewa na Idara ya Mawasiliano, Chadema imesema kuwa waziri Majaliwa ametoa tamko hilo siku chache baada ya kufanya mkutano mjini Lindi uliowabagua wananchi kwa itikadi zao kwa kutoa nafasi kwa chama kimoja cha siasa ambacho ni CCM kuhutubia na kufanya siasa.

Matukio haya yanaanza kumdhihirisha Waziri Mkuu Majaliwa ni kiongozi mwenye uelekeo wa namna gani hivyo kuanza kuifunua Serikali ya Rais John Magufuli chini ya CCM kwa miaka mitano ijayo itawapeleka wapi Watanzania,” inaeleza taarifa hiyo.

Ni dalili za wazi za watu waliolewa madaraka na kuchoka kuwa viongozi na sasa wanataka kuwa watawala wenye kudhani kuwa fikra zao ndizo zinazongoza nchi badala ya misingi ya inayokubalika miongoni mwa jamii nzima kupitia Katiba, Sheria, Kanuni na taratibu mbalimbali.”

Naye makamu mwenyekiti wa Chadema, Profesa Abdallah Safari alisema uamuzi huo ni kinyume na Katiba na Sheria ya Vyama vya Siasa na kwamba Serikali inazuia wapinzani kufanya mikutano ya kushukuru wananchi kwa kuwa inajua watatoa ushahidi wa jinsi kura zilivyoibwa.

Wanatuzuia kwa sababu wanajua tutakwenda kutoa ushahidi wa jinsi CCM ilivyoiba kura za urais na ubunge,” alisema Profesa Safari.

Kiongozi anaweza kuzuia mkusanyiko iwapo tu nchi itakuwa katika hali ya hatari. Jambo hili hata Rais hawezi kulizua kienyejienyeji tu,” alisema Profesa Safari ambaye kitaaluma ni mwanasheria.

Alisema Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992 imeeleza wazi majukumu ya vyama vya siasa, kuwa ni pamoja na kufanya mikutano na maandamano.

Pamoja na tamko la Waziri Mkuu kumruhusu kufanya mikutano kutokana na ukweli kuwa alishinda uchaguzi wa ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alizungumzia marufuku hiyo kuwa ni kauli ya kisiasa isiyo na mantiki.

Mikutano inaratibiwa na Sheria ya Vyama vya Siasa. Hii kauli ya Majaliwa naona kama ilikuwa ya kisiasa zaidi. Jeshi la polisi ndilo lenye jukumu la kuzuia mikutano na litafanya hivyo kama kutakuwa na hali ya hatari na si vinginevyo,” alisema Zitto.

Mwanasheria wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia alimtaka Waziri Mkuu kujikita katika uwajibikaji badala ya kuingilia vyama vingine.

Sheria hairuhusu mtu yeyote kuzuia mikutano ya kisiasa isipokuwa kama kuna tishio la vita,” alisema Sungusia.

Kuruhusu baadhi ya watu kufanya mikutano na wengine kuwazuia ni kuwanyima haki watu.”  

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Disemba 25, Ikiwemo ya Zari na Ivan Warudiana

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Disemba 25, Ikiwemo ya Zari na Ivan Warudiana

Sipendi Watu Wanavyoniambia Nina Kalio Fake, Wakati Nimebarikiwa na Mungu

$
0
0
Admin , Sipendi Jinsi watu wanavyonisema kila nipitapo eti makalio yangu ya Mchina wakati mimi nimezaliwa hivyo hivyo toka nikiwa mdogo makalio yangu yalikuwa makubwa , kama unabisha uliza hata nilio soma nao shule ya msingi , Ki kweli sipendi hiyo tabia ya watu kila wakiona mtu amejaliwa basi eti ni fake wengine tumezaliwa hivyo jamani ..Khhaaaa Wabongo Acheni Ushamba

By Camila, Sinza

Kashfa ya Makontena yamuibua Ridhiwan Kikwete...Mwenyewe Afunguka Mazito..

$
0
0
Leo katika gazeti la Raia Tanzania Riz ameibuka na kusema wale wanaosema makotena ambayo mpaka sasa hayajalipiwa ushuru na hayajulikana mwenye nayo ni ya kwake ni watu wa siasa za maji taka na wenye nia ya kumchafua yeye na familia yao kwa ujumla.

Kijana huyo ambaye ni nadra kuzumgumza na vyombo vya habari ameibuka baada ya mitandao ya kijamii kwa muda mrefu kumhusisha na ukwepaji kodi na kudaiwa kujirundikia utajiri usioweza kuelezwa vyanzo vyake.

Chanzo: Raia Tanzania

Waziri Mkuu Ataka Amani ya Nchi Ilindwe......Akemea Uvaaji wa Nguo Fupi na Matumizi Ya Dawa Za Kulevya

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wananchi waendelee kulinda amani ya nchi huku akikemea uvaaji wa nguo fupi na kuwasihi Watanzania kujenga tabia ya kuvaa mavazi yenye kumpendeza Mungu.

Pia, amekemea matumizi ya dawa za kulevya na mimba za utotoni akisema ni mambo ambayo yanaepukika kwa mtu yeyote aliyelelewa katika misingi ya kidini.

Waziri Majaliwa alisema hayo jana alipokuwa akihutubia Baraza la Maulid lililofanyika Karimjee jijini Dar es Salaam.

Alisema mambo yote hayo yanawezekana kama watu watamkimbilia Mungu huku akiwaomba viongozi wa dini kuwausia waumini wao kuvaa mavazi ambayo yanampendeza Mungu.

“Mtoto akilelewa kwenye mazingira ya dini itakuwa ngumu kuvaa mavazi ambayo hayampendezi Mungu,” alisema.

Amesema Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi za kidini zile ambazo ziko kisheria huku akizitaka ziendelee kuisaidia Serikali kwa kujenga shule na hospitali na kutoa huduma nyingine za kijamii.

Waziri Majaliwa alitumia fursa hiyo kuwapongeza Watanzania kwa kuwa watulivu katika kipindi chote cha uchaguzi hadi ulipofanyika Oktoba 25.

Akizungumza katika baraza hilo, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti, Abubakari Zuberi aliwaasa waumini wa Kiislamu kufanya mambo yote yanayompendeza Mwenyezi Mungu.

Aliwashukuru Waislamu wote nchini kwa kushirikiana na wananchi wenzao ambao siyo wa dini hiyo katika kudumisha amani.

My Son Caught Me Having S£X With a Pastor And Demanded a Round of s3x as Bribe - LADY

$
0
0

I don't even know where to start from.

My story is very embarrassing but because I desperately need an advice, I just have to eat the humble pie and let you know my story.

I have been married for the past 18 years and of late we have been having serious marital problems with my husband who is a truck driver. Half the times he is at home and half the times he is out of town on business duty. While he is away he sleeps around with pr@st!tutes and now we don't really love each other. Since I'm scared of contracting HIV due to his infidelity, I ended up not asking for s3x from him, instead I started dating a divorced pastor from our church.


We both love each other and we have been having protected s3x for quite some time. Over the weekend my 17-year-old son caught us having s3x and he demanded to have s3x with me as well as money from the pastor so that he won't tell his dad about it, or expose the pastor at church. Obviously I would never allow him to bonk me, if he was my step son maybe, but in this case he is my first born child, and I won't tolerate that.

I can't even explain to him that I stopped having s3x with his dad in 2013, neither can I tell him that his dad is doing even much more than what I did, only that he caught me and not his dad. I have no problem with him telling his dad about what he saw, but I want to protect my pastor at all costs. My son is still insisting that he must do what he saw our pastor doing, otherwise he will tell the whole church what he saw and also tell his father about it.

Please readers help me. 
How do I solve my dilemma?

Rais Magufuli Ashiriki Misa Ya Krismasi Kanisa La Mtakatifu Peter Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0

Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwasili kushiriki Ibada ya Krismas misa ya kwanza katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015. 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakishiriki Ibada ya Krismas katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015
Sehemu ya waumini katika Ibada ya Krismas misa ya kwanza katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakishiriki Ibada ya Krismas katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli, mkewe Mama Janeth Magufuli na Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa wakishiriki Ibada ya Krismas katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Muadhama Askofu Mkuu Polycarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam aliyemkaribisha kusalimia wananchi bada ya kumalizika kwa Ibada ya Krismas misa ya kwanza katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015.
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akitoa salamu zake za heri ya Krismasi mara baada ya kumalizika Ibada ya Krismas misa ya kwanza katika Kanisa la Mtakatifu Peter jijini Dar es salaam leo Desemba 25, 2015.

Upotevu wa makontena: Filamu iliyomaliziwa vibaya

$
0
0
Filamu ilianza vyema. Masteringi wawili walioneshwa wakipania kucheza filamu ya kusisimua. Wakaanza kwa ziara za kushtukiza zisizo na giza. Wakaibuka na hata orodha ya mambo ya forodha. Mkaratasi usio na wasiwasi ukiwa na idadi ya vyenye ukakasi ukaoneshwa.

Wapo waliosimamishwa. Wapo waliopoteza kazi. Wapo waliokamatwa na kushtakiwa. Wapo waliopanda vyeo. Wapo walioshushwa vyeo. Wapo waliotakiwa kulipa kwa siku kadhaa. Wapo wasioonwa na kubaki wakinona.

Makontena yakaongezeka kupotea. Masteringi wakapania zaidi. Ikasemwa kuwa sasa idadi ni ya kutisha. Maelfu ya makontena yakasemwa yamepotea au hayakulipiwa kodi. Masteringi wakapania. Wakaungwa mkono. Wakaaminiwa.

Halafu,ukimya ukatawala. Kwa yale ya mwanzo na hata ya mwisho. Ni kama Masteringi kumalizia filamu vibaya. Ni kama filamu kuisha kwa maadui kushangilia ushindi na Masteringi kutoonekana tena. Filamu ilikuwa tamu na ya kutia hamu. Ilichezwa kiufundi bila kumwaga damu. Mwisho wake umeharibu. Tuendelee kuamini?

Christmas njema!

By Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam/JF

Ridhiwan Kikwete Alikana Gazeti La Mawio.......Adai aliyekuwa Anamsaidia Kufunga Viatu Sio Paul Makonda,Ni Deogratias Kessy

$
0
0
Mbunge wa Chalinze, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete amekanusha aliyekuwa anamsaidia kufunga kamba za viatu katika picha iliyochapishwa kwenye gazeti la MAWIO (picha juu) si Paul Makonda Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

Akizungumza na waandishi wa habari , Ridhiwani Kikwete alisema anayeonekana akimsaidia kufunga viatu katika picha hiyo ni Deogratias Kessy, mfanyakazi katika kampuni ya ushonaji na mavazi ya Sheria Ngowi.

"Nilishona safari suti katika kampuni hiyo. Nilipokwenda kuchukua nguo yangu na nilipovaa ili kuona kama imeshonwa vizuri, Bwana Sheria Ngowi akanitaka nivae viatu vya ngozi.

"Bahati mbaya nilikuwa nimevaa sandals hivyo akaamua kunipa viatu vya dukani kwake nivae. Wakati Bwana Deogratias akinisaidia kuvaa viatu ndipo mpiga picha wa kampuni ya Sheria Ngowi akapiga picha hiyo kwa matumizi yao. Nashangaa kuona watu wanaitumia picha hiyo kwa makusudi yao yasiyo sahihi," alisema Ridhiwani Kikwete.

Sielewi kwanini waandishi wa habari wa MAWIO wanaamua kuandika taarifa za uzushi. MAWIO walikuwa na nafasi ya kuniuliza au kwenda kwa Sheria Ngowi kujua ukweli wa wanachoandika.

Ridhiwani alitahadharisha kuhusu vyombo vya habari kutumika kwa malengo ya kuwachafua watu.

Tuhuma za Mkurugenzi wa NHC Nehemiah Mchechu Kujilipa Mshahara wa Sh Mil 36 Kwa Mwezi....Mwenyewe Adai Watanzania ni Vigeugeu

$
0
0
Nehemiah Mchechu, moja ya majina maarufu katika nyanja za uongozi wa mashirika nchini, jina lake limeteka mitandao ya kijamii kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.

Ukiachana na umaarufu wa Rais John Magufuli mtandaoni kwa kazi yake ya ‘kutumbua’ majipu, Mchechu ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), anavuma kwa mema na ‘mabaya’.

Baadhi wanasifu mafanikio yake ya kuliimarisha shirika hilo kwa kipindi cha muda mfupi, lakini wengine wanamtuhumu kulitumia kujinufaisha ikiwamo kujilipa ‘mamilioni’ ya shilingi kama mshahara na posho za vikao.

Tuhuma zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii ni kwamba bosi huyo wa NHC, anajilipa mshahara Sh36 milioni kwa mwezi na kuhudhuria vikao vingi vya bodi vinampatia posho za kutisha.

“Kiwango hicho hakina ukweli,” anasema Mchechu, “mshahara wangu upo chini ya hapo,”anasema.

“Pia, huwezi kujilipa. Unalipwa kwa makubaliano maalumu tangu awali kabla ya kazi kulingana na kazi unayopewa,” anaongeza.

Mchechu anasema yupo NHC kulitumikia taifa kwa kuwa alipotoka sekta binafsi alikuwa akipata mshahara mkubwa, lakini alikubali kiwango kidogo serikalini kwa kuwa alikuwa akijua shirika hilo lilikuwa na hali mbaya kifedha na lilihitaji kuboreshwa.

Kuhusu vikao vya bodi na kamati mbalimbali anazotuhumiwa kushiriki na ‘kuvuna fedha’, Mchechu anasema kamati nyingi zinazorushwa mtandaoni siyo za kweli na hakuna fedha inayolipwa katika vikao hivyo.

“Watu wanapohoji mshahara wangu wanasahau kiwango ninachoingiza kwa Serikali. Jaribu kufikiri tumeirudisha ardhi ya Kawe Tanganyika Parkers yenye thamani ya zaidi ya Sh200 bilioni kutoka mikononi mwa aliyekuwa ameuziwa kipindi hicho, hivi ningekuwa mtu binafsi kwa kufanikisha majadiliano ya kurudisha kiwanja hicho, ningepata kiasi gani?” anasema.

Katika mahojiano maalumu yaliyofanyika hivi karibuni, Mchechu anaeleza kuwa Watanzania ni kigeugeu kwa kuwa wakati anaingia NHC mwaka 2010 akitokea Benki ya CBA, wengi walimuonea huruma wakieleza alikuwa anakwenda kupoteza weledi na mshahara, lakini sasa wanamzushia anapokea fedha nyingi zinazolifilisi shirika.

“Siku waajiri wangu wakigundua nalipwa mshahara mkubwa kuliko ninachofakifanya wataniondoa kwa sababu nawaletea hasara,” anasema.

Bosi huyo wa zamani wa Benki ya Standard Chartered alianza kazi mwaka 2010, wakati wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete, kwa kupatiwa mkataba wa miaka minne kuboresha shirika hilo lililokuwa likichechemea.

Mkataba wa awali ulimalizika mwaka jana na kusaini mwingine wa miaka mitano ambao unatarajia kumalizika mwaka 2018/2019.

Kama yalivyokuwa malengo ya Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1962, Mchechu, alikabidhiwa kazi ya kuendeleza sera ya kujenga makazi ya bei nafuu kwa Watanzania.

Kama ilivyokuwa kwa mashirika mengine ya umma, NHC halikuwa likipata faida kubwa ya kuwezesha kuendeleza miradi mikubwa na kwa mujibu ripoti za fedha za shirika hilo, mwaka 2010 lilikuwa limepata faida ya Sh3.1 bilioni.

Ili kulifanyia mabadiliko Shirika hilo, Mchechu anasema, ilihitajika akili na nguvu ya kutosha kwa sababu mambo yalikuwa yakiendeshwa kienyeji na kwamba baadhi ya vigogo walikuwa wakihusika kulifilisi NHC.

Mikataba ya vigogo

Anasema kuwa kuna baadhi ya vigogo serikalini na watumishi wa shirika hilo waliokuwa wakiendesha ukodishaji wa nyumba kwa mikataba ya kilaghai na NHC kwa kulipatia fedha kidogo wakati wanatoza fedha nyingi kwa wapangaji.

Kuna baadhi ya ‘madalali’ walikuwa wakililipa shirika kodi ya Sh700, 000 katika baadhi ya nyumba za biashara kwa mwezi wakati wao wanakusanya zaidi ya Sh5 milioni lakini mikataba hiyo ilivunjwa.

“Tumekirejesha alichokuwa akikitaka Baba wa Taifa kwa sababu kwa sasa karibu kila mkoa una nyumba za bei nafuu zilizojengwa na shirika,” anasema Mchechu akieleza kuwa hadi sasa wamejenga nyumba zaidi ya 3,000 za bei ya chini.

Katika mtandao wa nyumba hizo, zilizokuwa zikiuzwa bei ya chini kuliko zote nchini ni zile zilizopo mkoani Katavi ambazo zilikuwa Sh32 milioni kwa sababu huduma za umeme na barabara zilikuwa zimesogezwa.

Anaeleza kuwa wastani wa bei ya makazi ya bei nafuu ni Sh34 milioni kwa nyumba ya vyumba viwili na Sh43 milioni kwa nyumba ya vyumba vitatu na bei hupanda kutokana na gharama za ujenzi zikiwamo kuandaa miundombinu na kodi ya ongezeko la thamani.

Pia, gharama hizo anasema zinatokana na riba kubwa ya mikopo iliyopo sokoni na kupanda kwa thamani ya Dola ya Marekani mara kwa mara.

Hata hivyo, baadhi ya wakosoaji wanasema nyumba hizo zinauzwa ghali na kununuliwa na mabepari pekee badala ya walengwa ambao ni watu wa kipato cha chini na sehemu kubwa zinadoda kwa kukosa wateja.

Kwa Mchechu, tuhuma hizo hazimnyimi usingizi. Na kabla ya kujibu hoja hiyo, anatasabasamu kidogo.

“Kila mradi tunaoufanya huwa tunalenga watu wa kundi fulani. Hatukurupuki. Tunaangalia wa kipato cha chini, kati na cha juu. Sina sababu ya kuficha.

“Lakini nyumba zetu ni za bei ya chini kulinganisha na kampuni binafsi hivyo naomba fananisha embe kwa embe na chungwa na chungwa na si vinginevyo,” anasema.

Mchechu anasema kuna baadhi ya miradi mikubwa kama ya Kawe na Morocco ni ya kibiashara zaidi na nyumba zake zinauzwa bei kubwa kwa kuwa zililenga kundi la watu ambao hukimbilia nje ya nchi kununua makazi lakini sasa wanataka wabaki nchini.

“Kama mtu ni wa malengo ya Sh50 milioni halafu anakosoa bei za mradi wa Kawe yupo sahihi kuona bei ile ni kichaa kwa sababu inaenda mara tatu hadi 10 ya kipato chake. Lakini mimi sikulenga kule,” anasema.

Nyumba za bei nafuu

Hata hivyo, anaeleza kwa kuwa NHC malengo yake ni kujenga nyumba za bei nafuu katika halmashauri zote nchini ambako tayari wamenunua ekari 5,600 huku nyingine 22,000 wapo kwenye mazungumzo ya kuuziana na wamiliki.

Kuhusu kudoda kwa nyumba, bosi huyo anapinga kidogo.

Anasema makazi mengi waliyoyajenga kwa bei nafuu yalinunuliwa yote na mengine kabla ya miradi yake kukamilika kupitia mikopo ambayo wananchi wanakopa benki za biashara kununua nyumba za NHC.

“Kibada, Kigamboni (Dar es Salaam) tuliuza ndani ya saa 48, mradi wa Eco Housing na Mchikichini zote zimeuzwa hata hizo za mikoani zina soko…hakuna zilizododa,” anasema Mchechu.

NHC inafahamika kwa muda mrefu kuwa na nyumba za kupangisha za bei nafuu nchini lakini kwa sasa miradi yake ya kupangisha haisikiki kwa kiasi kikubwa.

Hata hivyo, majibu ya kiongozi huyo yanashitua kidogo kwa wanasubiri kiwango kikubwa cha nyumba za kupangisha.

Anasema kuwa katika mikakati yao walipanga kujenga nyumba asilimia 70 kwa ajili ya kuuza na asilimia 30 ya kupangisha kwa watu wa hali ya chini.

Matangazo ya ukodishaji hayawi makubwa sana kama ilivyo katika uuzaji kwa kuwa wananchi wengi wanahitaji nyumba hizo, anaeleza.

“Tanzania ina upungufu mkubwa wa nyumba takriban 3.5 milioni hivyo iwapo nikisema nijenge nyumba moja kwa Sh100 milioni na kuikodisha ile fedha itasaidia familia moja tu lakini nikiuza nyumba mtaji ule nikauzungusha tunaweza kujenga zaidi ya nyumba nane za familia,” anasema Mchechu.

Tangu Rais John Magufuli aingie madarakani ameanza kubadilisha utendaji kwenye utumishi wa umma na moja ya njia ya kufanikisha hilo ni ziara za kushtukiza katika taasisi na mashirika ya umma.

Mchechu amejiandaje na ujio wa kushtukiza wa Rais?

“Sisi tayari tulikuwa tunaendesha mambo yetu kwa mwendokasi na baadaye tutaongeza zaidi kasi,” anasema.

Katika uongozi wake, anaeleza aliyoyapata NHC yakiwamo kuongeza uwekezaji wa ujenzi nyumba nchini na kukuza mapato ya shirika ambayo mwaka jana yalifikia Sh130 bilioni kutoka Sh36.6 bilioni mwaka 2010 baada ya kubana matumizi na kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi.

“Pesa tumeikuza lakini haitosheelezi miradi hata ukichanganya na mikopo hivyo tunaendelea kutafuta fedha zaidi ili kufanikisha malengo yetu.

“Na pia niwe muwazi kabisa kama nitashindwa kutimiza malengo kwa miaka tisa niliyokaa NHC sidhani kama nitaleta kipya nikipatiwa miaka 20 hivyo baada ya hapa nitarudi sekta binafsi,” anasema.    


Familia Ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Yatoa TAMKO Zito....Yasisitiza Haihusiki na Utoroshaji wa Makontena Bandarini.Mwenye Ushahidi Autoe

$
0
0
Mbunge wa Chalinze, Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete,  ambaye ni mtoto wa Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete ,kwa niaba ya familia yake ametoa tamko zito kupinga tuhuma mbalimbali zinaozoelekezwa kwake na familia yake.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Jana,Ridhiwani alisema baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wa miaka 10  madarakani, baadhi ya watu wamekuwa wakiiandama familia yao kwa tuhuma mbalimbali.

Alisema baadhi ya tuhuma zinamhusisha yeye mwenyewe kwa lengo la kuupotosha uuma.

Alizitaja tuhuma hizo kuwa ni utoroshaji wa makontena kwenye bandari ya Dar es Salaam na kusisitiza kwamba tuhuma zote zinazotolewa hazina ukweli wowote bali zimelenga kumchafua yeye na familia yake.

Ridhiwani alisema tangu serikali ya awamu ya tano ianze kuwabana  watu wanaokwepa kulipa kodi za serikali,baadhi ya watu wanafanya jitihada za kumhusisha  na  watuhumiwa  hao.

Alisema hajawahi kuagiza bidhaa yoyote kutoka nje,kuwa na kontena la kulipiwa ushuru,kukwepa au kumuombea msamaha wa kupunguziwa kodi mfanyabiashara yeyote aliyeagiza kontena kutoka nje, hivyo mwenye ushahidi juu ya hilo autoe.

"Kama kuna mtu mwenye ushahidi autoe hadharani mimi niuone,dunia iuone, nawahakikishia ushahidi huo haupo na hautokuwepo labda uwe wa kughushi na wakifanya hivyo wataumbuka.

"Sina na sijawahi kumiliki lori au basi katika maisha yangu.Sina hisa wala ubia na mtu yeyote  au kampuni ya malori au mabasi." Alisema Ridhiwani na kuongeza;

"Naambiwa hapa nchini siku hizi kila jengo jipya linalojengwa inasemekana ni langu na vituo vipya vya mafuta naambiwa ni vyangu.Huo ni uongo mtupu.

"Naomba nimalizie kama nilivyoanza,yanasemwa mengi lakini ni maneno ya uzandiki na uzushi mtupu usio na chembe ya ukweli.

"Wanaosema, kuandika na kueneza maneno hayo wanajua wanasema uongo isipokuwa wanafanya hivyo kwa nia mbaya dhidi yangu na familia yangu.Nawaomba watanzania muwapuuze."

Nafasi za Kazi Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Application Deadline 02 January 2016

$
0
0
TANZANIA BUREAU OF STANDARDS (TBS)
EMPLOYMENT OPPORTUNITIES
RE- ADVERTISED POSTS

Bonyeza HAPA Kusoma Nafasi zilizotangazwa

Au Tembelea www.ajirayako.com

Nimerekodiwa Video ya Ngono Bila Kujijua. Nifanyeje?

$
0
0
Wadau natumaini mu wazima Mi ni mjasiriamali toka Arusha but huwa nakuja Dar kwa ajili ya kuchukua bidhaa, nikiwa Dar napenda kujibururdisha ama MEEDA au KONA BAA/AMBIANCE AFRIKA SANA huwa nikipata demu wa kupiga nampelekaga Guest/hotel niliyofikia tunafurahia "game" asb namlipa chake anatambaa.

    Sasa katika kuingia guest kadhaa za hapa Dar nimegundua hawa jamaa wa guest wanaweka SECURITY CAMERAS kuanzia kwenye parking, kwenye korido, karibu na milango, vyumbani hadi bafuni. Je, ni haki kuweka security camera hadi vyumbani/bafuni?

    Jana nikiwa kwenye foleni Magomeni Mapipa dogo mmoja akaja na DVD kibao za dini, chini yake ameweka DVD ya X ina picha ya WEMA nikainunua ile kufika hotelini nikaweka kwenye laptop najiona mimi na demu niliyemchukua wk 2 zilizopita.

    Hakika nilichoka, sijui cha kufanya nishaurini wadau.

Mapya Yaibuka Mauaji ya Wafanyabiashara Walio Pigwa Risasi Kwa Kukusudia na Polisi Dar

$
0
0
Mapya yameibuka kuhusiana na tukio la kuuawa kwa wafanyabiashara Yasin Rashid na Samson Michael ‘Ngosha’ wanaodaiwa kupigwa risasi jijini Dar es Salaam na askari wa kikosi maalum cha kudhibiti ujangili kufuatia taarifa zinazodai kuwa mmoja wa marehemu hao alikuwa akitumiwa na askari kuwapa taarifa za mauziano ya meno ya tembo kwenye hoteli moja maeneo ya Sinza saa chache kabla ya kifo chake.

Kwa mujibu wa Polisi, mauaji ya wafanyabiashara hao yalitokea Jumamosi iliyopita (Desemba 19), huku baadhi ya watu wanaodai kushuhudia tukio la kuuawa kwa Michael ‘Ngosha’ wakieleza kuwa lilitokea Sinza majira ya saa 7:45, karibu na Shule ya Msingi Reginald Mengi.

Hata hivyo,  chanzo kimoja kiliiambia Nipashe katika taarifa ya jana kuwa Rashid aliuawa katika eneo jingine, maeneo ya fukwe ya Bahari ya Hindi na siyo Sinza kama ilivyokuwa kwa mwenzake (Ngosha).

Chanzo kimoja kiliiambia Nipashe kuwa sababu kubwa ya kuuawa kwa wafanyabiashara hao ni fedha kiasi cha Sh. milioni 168 alizokuwa nazo Ngosha (Michael), ambaye aliuza meno kadhaa ya tembo aliyoyafikisha jijini Dar akitoka nayo kwenye mkoa usiotajwa, lakini safari yake ikihusisha Mikumi mkoani Morogoro.    

Hata hivyo, taarifa mpya ambazo Nipashe imezipata zinaeleza kuwa kabla ya kuuawa, Rashid alikuwa mtu wa karibu na baadhi ya askari wa kikosi cha kuzuia ujangili na kwamba, kama siyo yeye (Rashid) kuwaeleza kuhusu mauzo ya meno ya tembo aliyofanya Ngosha katika hoteli moja iliyopo Sinza, isingekuwa rahisi kwa askari hao kufika eneo la tukio.

Awali, akizungumza na waandishi wa habari Jumatatu wiki hii, Kamanda wa Polisi katika Kanda Malaum ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Suleiman Kova, alisema jeshi lake linawashikilia askari sita wakiwamo wanne kutoka katika kikosi maalum cha Kukabiliana na Ujangili nchini kuhusiana na utata uliojitokeza kuhusiana na vifo vya wafanyabiashara hao.

Kamanda Kova alisema kuwa taarifa zilizofikishwa awali zilidai kuwa Rashid na Ngosha wanaodaiwa kuwa ni majangili, waliuawa wakati wakirushiana risasi na askari hao wa kikosi maalum cha kukabiliana na ujangili kwenye maeneo ya Sinza.

Alisema wanaoshikiliwa ni askari sita wakiwamo polisi wa kawaida wawili na wengine wanne wa idara ya wanyamapori. Polisi wa kawaida wanaoshikiliwa kwa tuhuma hizo ni Bonny Mbange na Philibert huku wale wa wanyamapori wakiwa ni Emmanuel Mbaga, Deogratias Mwageni, Joseph Jimmy na Asbile Mwakyusa. Mwingine aitwaye Issa Kazimoto bado anatafutwa na polisi baada ya kukimbilia kusikojulikana.


KUHUSU RASHID
Chanzo kimoja kiliiambia Nipashe kuwa licha ya Rashid kuwa rafiki wa Ngosha (Michael), ndiye pia aliyekuwa akiwasiliana na baadhi ya askari wa kikosi cha kudhibiti ujangili na kuwaleza kila hatua aliyokuwa akipita kutoka mkoani alikokuwa hadi Sinza ambako ndiko biashara ilifanyika na Ngosha kulipwa kiasi kikubwa cha fedha kinachotajwa kuwa ni Sh. milioni 168.

Inaelezwa kuwa mpango uliokuwapo ni kwa askari kutumia taarifa walizokuwa wakizipata kutoka kwa Rashid tangu Ngosha alipokuwa Mikumi kuelekea Dar es Salaam hadi Sinza ili wavamie eneo la mauziano na kuwakamata wahusika (Ngosha na mnunuzi wa meno yake) pamoja na vielelezo vingine kama ushahidi.

“Licha ya Rashid kuwapa maelezo yote kuhusu biashara hiyo, bado askari hawakufika kwa wakati. Na hili halikufanyika kwa bahati mbaya, ni kwa sababu kinachoonekana ni kwamba walijichelewesha kwa nia ya kusubiri biashara ikamilike ili wakute fedha zikiwa tayari,” chanzo kiliiambia Nipashe.  

Aliongezea kuwa, “Rashid aliendelea kuwasiliana na askari hao na kuwajulisha wafanye haraka kwa kuwa wameanza kuhesabiana fedha, lakini bado hawakuwahi eneo hilo.”

Chanzo kinaeleza kuwa baada ya askari kufika kwenye hoteli hiyo huku wakijua kuwa tayari biashara imeshafanyika, ndipo palipoibuka malumbano yaliyomlazimu Rashid kujaribu kukimbia eneo hilo, kama ilivyokuwa kwa Ngosha (Michael) ambaye naye aliiwahi gari yake aina ya Toyota Platz na kuondoka.

Hata hivyo, ilielezwa zaidi kuwa Rashid hakufika mbali baada ya kupigwa risasi ya mguu na kukamatwa akiwa majeruhi, hiyo ikiwa ni baada ya wananchi waliokuwa jirani kutoa msaada wakidhani kuwa ni jambazi.

Kadhalika, jitihada za Ngosha ziligonga mwamba pia kwani watu wanaodaiwa kuwa ni askari waliokuwa kwenye gari linalotajwa kuwa ni Toyota GX 110 (likiwa halina namba rasmi bali za ‘cheses’), walilipiga risasi gari lake na yeye kumjeruhi kwa risasi iliyompata maeneo ya bega.  

Ilielezwa na baadhi ya watu waliodai kushuhudia tukio hilo kuwa baada ya kuona amezidiwa, Ngosha alisimamisha gari, akateremka na kujaribu kunyoosha juu mikono yake kuashiria kujisalimisha. Ni hapo ndipo mmoja wa watu wanaodaiwa kuwa askari alimfuata na kummiminia risasi za kifuani zilizomuangusha chini na kufariki dunia.

Taarifa zaidi kutoka kwa waliojitambulisha kama mashuhuda zilidai kuwa baadaye, waliomuua walitwaa mfuko mkubwa wa rangi ya khaki na bahasha kubwa, vyote vikidaiwa kuwa na fedha ambazo chanzo kingine kiliiambia Nipashe kuwa ni Sh. milioni 168.

Ilielezwa zaidi kuwa watu hao wanaodaiwa kuwa askari walikabidhi mifuko hiyo inayodaiwa kuwa na fedha kwa mtu aliyefika mahala pa tukio na bodaboda, kisha akaondoka nazo.

Chanzo kingine kiliiambia Nipashe kuwa Rashid aliuawa na watu hao wanaodaiwa kuwa askari ili kufanikisha mpango wa kugawana fedha zilizotwaliwa kutoka kwa Ngosha.

Chanzo kingine kiliiambia Nipashe kuwa kabla ya kuwa mtu wa karibu na askari wa kikosi cha kupambana na ujangili, Rashid alikuwa akijihusisha na biashara zinazohusiana na ujangili kabla ya kuacha na kujiunga katika vita hiyo.

KOVA ASEMA UCHUNGUZI UNAENDELEA
Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Kamanda Kova alisema uchunguzi unaendelea na wakati muafaka ukifika wataeleza kila kitu kwa umma.

"Uchunguzi unaendelea. Hatuwezi kuzungumza kila siku na mwandishi mmoja… nitafanya kikao na waandishi wote pindi upelelezi utakapokamilika," alisema.
CHANZO: NIPASHE
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images