Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Jay Z Caught On Camera Doing 'Things' To Beyoncé

0
0
Drunk in Love? Recent photos of superstar couple, Jay Z and Beyoncé, have surfaced online where they are seen getting a little too intimate while laying out by the pool.

The two pictures of what appears to be Beyoncé lying out in the sun in a gold bikini while Jay Z has his hands between her legs were allegedly leaked to Instagram.

We're not entirely sure that the pictures are of the couple, due to the extreme grainy nature of them but you be the judge!


Edward Lowassa Atimkia Monduli Kwenda Kuchanga Ng'ombe Kijijini Baada ya Kukosa Urais 2015

0
0


Picha za Lowassa Asubuhi ya Leo zimezagaa Mitandaoni zikionyesha akichunga ng'ombe kijijini kitendo ambacho kimezua gumzo kutokana na kauli yake aliyoitoa wakati wa uchaguzi kuwa akishindwa atarudi kijijini kwao kuchanga......

Je ndio ameamua kutimiza ahadi yake ama anatafuta kiki tu......

Nape Nnauye: Nchi ilifika Pagumu Sana, Tumuombee Rais Wetu Magufuli

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye amesema Watanzania wanapaswa kumuombea Rais John Magufuli ili aendelee kutumbua majipu kwani nchi ilifika pagumu baada ya wezi kuonekana wajanja.

Akizungumza wakati akizindua tamasha la Krismasi lililofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam Nape aliyemwakilisha Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan alisema haijalishi mafisadi nchini wamejenga mizizi kiasi gani, lazima majipu yote yatumbuliwe.

Alisema kila mmoja anatakiwa kuomba kwa imani yake kwani kazi aliyoifanya Rais Magufuli na anayotarajia kuendelea kuifanya sambamba na Baraza la Mawaziri na viongozi wengine ni kubwa.

Nape alisema kazi ya kutumbua majipu siyo ndogo, kwani Dk Magufuli na jopo lake wanaamini kwamba Watanzania wana haki ya kufaidi matunda ya nchi yao.

''Nchi ilifikia hatua ngumu asiyeiba alionekana mjinga na mshamba na wezi walionekana wajanja, waliostaafu wakiwa maskini walionekana wajinga, muombeni Rais Magufuli atumbue majipu ili Watanzania wafaidi matunda ya nchi yao'', alisema Nape.

Alisema hakuna sababu kwa nchi kuendelea kuwa maskini, mwenye haki atapata haki yake huku kila mmoja akila kwa jasho lake na si vinginevyo.

Waziri huyo ambaye aliimba pambio  liitwalo Yu Mwamba, alisema amani na utulivu wa nchi lazima viendelee na ili hayo yote yafanikiwe, Watanzania wanapaswa kuomba.

''Serikali tutahakikisha tunaitunza amani kwa gharama yoyote, hivyo viongozi wa Serikali na kidini wanapaswa kudumisha dhana hiyo ili nchi iendelee kuwa kisiwa cha amani, yapo mataifa yanatamani kuwa kama Tanzania lakini haiwezekani'', alisema Nape.

Nape alizindua albamu ya kwaya ya Wakorintho wa Pili kutoka Mafinga, Iringa na kuinunua kwa Sh1.5 milioni. Maaskofu na viongozi wa dini walifanya sala kwa dakika 15 iliyokuwa na lengo la kumwombea Rais Magufuli ili Mungu amlinde katika jitihada zake za kupambana na mafisadi.

Awali, Askofu David Mwasota alisema viongozi wa dini wanaunga mkono Serikali ya Awamu Tano kwa kutambua haki kwa Watanzania wote.

''Tunampongeza Rais Magufuli kwa jitihada zake ambazo kwa muda mfupi amefanya mambo makubwa yanayoonyesha nuru kwa nchi yetu miaka mitano ijayo'', alisema Askofu Mwasota.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Tarehe 26, Ikiwemo ya Fumanizi Krismas

0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Tarehe 26, Ikiwemo ya Fumanizi Krismas

Lady Jaydee Aikimbia Nchi Ahamia Ujerumani..Achoshwa na Maneno ya Wabongo....Mapenzi Kwake sasa Basi....

0
0
MOYONI nina majonzi, sina tofauti na mpofu! Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ au ‘Lady Jaydee’ kwa sasa hana makazi maalum Bongo, amehamishia makazi na shughuli zake katika ardhi ya ‘Kansela’ wa Ujerumani, Angelina Merkel kwenye Jiji la Born.

Katika mazungumzo yake na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Jumatatu ya wiki hii, Jide ambaye alidai kwa sasa yupo nchini kwa Sikukuu ya Krismasi (kesho), alisema sababu zilizomfanya akapige kambi nchini humo ni kuchoshwa na maneno ya watu ambao kazi zao ni kutazama nani kafikwa na baya ili waeneze sumu ya maneno.

Kwa sauti ya ‘kibabe’ na yenye mamlaka, Jide alisema: “Lakini ukiachana na Ujerumani, wakati mwingine natumia muda mwingi kuwa nchini Afrika Kusini (Sauzi) kwa mizunguko ya kimaisha na kupumzisha akili yangu.”

UJERUMANI ANA NYUMBA?

Jide: “Kwa sasa naishi hotelini, lakini kuna marafiki na jamaa zangu ambao wako kule. Kwa hiyo sina shida. Muhimu ni kukaa mbali na maneno ya watu wafurahiao matatizo ya wengine.

Kila mtu anageuka adui, ukiwa na mafanikio makubwa, watu wanajisogeza karibu, ukipungukiwa na jambo, haohao wanaanza maneno na kukusema vibaya, maisha hayatabiriki.”

HATAKI KUSIKIA MAPENZI!

Amani: “Vipi kuhusu mumeo, Gardner Habash, una mpango wa kurejeana naye?”

Jide: “Sitaki kusikia kabisa mambo ya mapenzi. Sitaki na usiendelee kuuliza upuuzi kama huo tafadhali. Si tu kwa huyo mtu (Gardner), hata kwa awaye yeyote, sitaki kusikia.”

ASIULIZWE KUHUSU MALI ZAKE!

Amani lilimuuliza Jide kuhusu ukweli juu ya madai kwamba amefilisika na kufikia hatua ya baadhi ya nyumba zake kuwa katika hatihati ya kupigwa mnada.

Jide: “Sitaki kugusia mambo hayo. Hata hivyo, umebahatika sana kupokelewa simu na kuzungumza na mimi, licha ya kuwa umejitambulisha unatoka Global. Sipendi mazungumzo na waandishi, hususan nyie wadaku.”

KUHUSU MUZIKI?

Jide: “Siwezi kusema nimeacha muziki, nipo maana ndiyo kazi pekee iliyonitambulisha.

Nawaasa mashabiki wangu waendelee kiniunga mkono, nawapenda sana na bila wao hakuna Jide. Lakini kwa sasa kuna mambo nayaweka sawa nje ya muziki.”

YUPO DAR AU KWINGINEKO?

Jide: “Kwa sasa niko Dar (Jumatatu), lakini keshokutwa (jana

Jumatano) nitakuwa nyumbani Musoma kwa ajili ya Krismasi. Niko kwenye mapumziko maalum ya sikukuu hiyo, lakini baada ya hapo, nitaendelea na mambo yangu mengine, ikiwemo kurejea Ujerumani.”

Chanzo: Global Publishers

Magufuli Awakuna Viongozi Wa Dini.....Maaskofu Wahimiza Aombewe Ili Aendelee Kutumbua Majipu

0
0
Viongozi wa makanisa mbalimbali nchini, wametoa salamu za Sikukuu ya Krismasi jana, wakielezea kufurahishwa na kasi ya utendaji kazi wa Rais John Magufuli.

Wamesisitiza waumini wao, kumuombea Rais na kuwataka wananchi kutii mamlaka, kwa kuwa yamewekwa na Mungu.

Viongozi hao pia, wamewataka watendaji wa Serikali na wananchi walioshiriki ukwepaji kodi, watubu dhambi zao na kurejesha vyote walivyochukua, ambavyo si halali yao.

Pia, wamempa moyo Rais Magufuli kuendelea kutumbua majipu, kwani hata Bibilia inatambua kazi hiyo.

Mbali na ujumbe huo wa viongozi wa dini kwa waumini wao na kwa Watanzania kwa ujumla, Rais Magufuli mwenyewe alishiriki katika ibada ya sikukuu hiyo katika Kanisa la Mtakatifu Petro, jijini Dar es Salaam, ambapo aliwatakia Watanzania wote Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya na kusisitiza waendelee kumuombea yeye na viongozi wengine.

Baada ya kuwatakia sikukuu njema Watanzania, Rais Magufuli aliwakumbusha wananchi kwamba ustawi wa nchi, unatokana na watu kufanya kazi, hivyo baada ya shamrashamra za msimu wa sikukuu, warejee kufanya kazi kwa bidii kwa ujenzi wa Taifa.

Dodoma wamuombea 
Mkoani Dodoma katika shamrashamra hizo, Askofu Amos Kinyunyu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Dodoma, aliwataka Watanzania kuzidi kumuombea Rais Magufuli kutokana na utendaji kazi unaowagusa Watanzania wa hali ya chini.

Alisema wao kama Kanisa, wataendelea kumuombea ili afanye kazi anayoendelea kufanya sasa hivi, kwani hata vitabu vitakatifu, vinataka usawa katika uchumi na kipato kwa kila mtu.

‘’Tunawaomba Watanzania wazidi kumuombea Rais wetu kasi aliyonayo aendelee kuwa nayo, kwani Mungu anapenda haki katika maisha pamoja na uchumi ulio sawa.

‘’Wakati mwingine hii kauli ya Hapa Kazi Tu, inakuwa hata sisi inatuogopesha, lakini Mungu ataendelea kumlinda na kumwongoza,’’ alisema.

Ni jibu la Kanisa 
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assembles of God la Miyuji Dodoma, Samson Mkuyi alisema utawala wa Rais Magufuli, unaonekana ni jibu la Watanzania wengi pamoja na Kanisa.

Mchungaji Mkuyi alisema wamefurahishwa na utendaji kazi wake hasa upande wa maadili, ikizingatiwa kuwa Kanisa linataka maadili ya kiroho na kimwili.

‘’Tulianza kuomba haya miaka mitano, sisi Kanisa tunamwambia asiogope kwani Mungu yupo pamoja na yeye, tunaendelea kumuombea ili Mungu aendelee kumpa ulinzi,’’ alisema.

Atumbue zaidi 
Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Central Tanganyika, Dk Dickson Chilongani alisema; ”Rais ameonekana kutumbua majipu yaliyokuwa yamejificha na katika hili tutaendelea kumuombea ili ayatumbue zaidi, pia na kuwafanya watendaji wafanye kazi kwa usahihi,’’ alisema.

Rais amepatikana
Kanisa la KKKT Dayosisi ya Morogoro mbali na kurejea umuhimu wa kumuombea Dk Magufuli, liliwataka viongozi wote walioteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali, wajitoe kikamilifu kuwatumikia na kuwahudumia wananchi wakiweka mbele maslahi ya taifa.

Askofu wa KKKT Dayosisi ya Morogoro, Jacob Paulo ole Mameo, wakati wa mahubiri yake alitaka vyama vyote vya siasa, kutanguliza maslahi ya Taifa mbele na kusema mwito wa Kanisa ni sasa tusonge mbele, uchaguzi umemalizika na Rais amepatikana.

“ Rais wetu ameanza kazi yake vizuri na sasa tumuunge mkono , tushirikiane kwa misingi ya umoja, upendo na amani katika kujenga Taifa na tuliombee lisonge mbele.

 “Wale viongozi waliozoea kutenda uovu sasa waache, wasijiingize tena huko, tunataka wawe mfano mzuri katika kuonesha uadilifu wao kwa kusimamia huduma bora mbele ya jamii,” alisema Askofu Mameo.


Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro, Telesphor Mkude, yeye alisisitiza waumini kuhubiri upendo na kudumisha amani iliyopo.

Alipongeza Serikali ya Awamu ya Tano, kwa hatua zake za kuwajali watu wanyonge, ili wapate huduma bora za kijamii ikiwa ni pamoja na kusimamia nidhamu, uadilifu na utendaji unaozingatia sheria za nchi.

Wakwepa kodi watubu 
Katika Kanisa la KKKT Usharika wa Maili Moja Kibaha, Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Isai Ntele, aliwataka watu waliokuwa wakijihusisha na ukwepaji kodi hapa nchini, kutubu mbele za Mungu na kurejesha kile walichokwepa na kuonesha utii kwa mamlaka iliyopo madarakani, kwani imewekwa na Mungu.

Mchungaji Ntele alisema Mungu alisikiliza kilio cha Watanzania kwa kuwapa kiongozi ambaye ana uchungu na wananchi wake, kwani ameonesha dhahiri kuwa hataki haki za wanyonge, zipotee kwa kudhulumiwa na wachache.

 “Hata Biblia inasema kila mtu aitii mamlaka iliyo Kuu kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na ile iliyopo nimeaminiwa na Mungu, hivyo asiye na mamlaka asipotii, anashindana na agizo la Mungu hivyo watapata hukumu,” alisema.

Wanatufananisha na mbinguni
 Mkoani Shinyanga, Askofu wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Mhashamu Liberatus Sangu, alisisitiza umuhimu wa kumwombea Rais Magufuli aliyeonesha nia ya kuwatumikia wananchi bila upendeleo, ambaye ameonesha wazi wazi kuwa anamtanguliza Mwenyezi Mungu.

"Kuna baadhi ya watu wanataka kutusadikisha kuwa Tanzania hakuna amani kwa nia zao wenyewe, labda wakilinganisha Tanzania na mbinguni ni sawa, kwa sababu mbinguni kuna utimilifu wake wote, lakini ukilinganisha Tanzania na mataifa mengine, ndugu zangu tuna amani ambayo tunapaswa kuilinda kwa nguvu zetu zote.

Wapo wengi wangetamani tuchinjane hapa nchini, wana wivu na chuki na nchi yetu na pengine wanaweza hata kutumia viongozi mbalimbali kupenyeza mambo yao, ili tuchukiane sisi kwa sisi, tuwakemee watu wanaodharau hii amani iliyopo,” alisema Askofu Sangu.

Alisema Tanzania hata bomu likilipuka, watu wanakimbia kwenda kutazama, lakini kwa nchi zenye machafuko, likilipuka bomu hakuna anayekwenda pale kwa kuhofia kifo na hiyo ni dalili tosha kuwa kuna amani.

Askofu Sangu aliwataka Watanzania kusherehekea sikukuu kwa upendo hususani katika ngazi ya familia na kuhamasisha watu kuishi kwa kupendana na kuepuka vitendo vya kupeana ujumbe wa kujengeana chuki, kwani ndiyo chanzo cha vurugu katika jamii na taifa kwa ujumla.

 Dar na mabadiliko ya kweli
 Mkoani Dar es Salaam, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam la Kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, alisema mabadiliko ya kweli yanaletwa na watu ambao wako tayari kufanya kazi kwa dhati usiku na mchana na si matajiri.

Akitoa mahubiri yake kwa waumini wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph lililoko Posta jijini Dar es Salaam, katika Ibada ya usiku wa Mkesha wa Sikukuu ya Krismasi, alisema katika fikra za mabadiliko, watu wa kawaida waliaminishwa kwamba hawana mchango wanaoweza kuutoa katika mabadiliko.

Mara nyingi sisi watu wa kawaida tulisadikishwa kwamba hakuna mchango tunaoweza kuutoa ili kuleta mabadiliko katika jumuia yetu, tulisadikishwa kwamba watu wanaokuwa na fedha na mali nyingi hao ndio wanaoweza kuleta mabadiliko katika jumuiya yetu,” alisema Pengo.

Alisema sasa mawazo hayo yamekwishatambuliwa kuwa hayakuwa sahihi, kwani watu wenye mali si wanaoweza kuleta mabadiliko yanayotakiwa katika jumuiya ya watu.

“Watakaoleta mabadiliko ni wale ambao haidhuru nafasi yao ni ipi katika jumuiya, lakini wako tayari kufanya kazi usiku na mchana, ili kuhakikisha kwamba hali ya kibinadamu inakuwa nzuri zaidi na huo ndio ujumbe unaopaswa kupokelewa kutoka kwa malaika aliowaendea wachungaji na kuwaambia msiogope,” alisema Pengo.

Askofu Pengo alisema na kupitia ujumbe huo wa malaika, Tanzania inaambiwa usiogope, kwani unayo habari njema, ambayo ni kuwa tayari kufanya kila linalokuwa ndani ya uwezo wake ili hiyo habari njema iifikie.

Aliwataka Watanzania wamuombe Mungu awajaalie neema ya kutambua kila mmoja anaweza kuwa chimbuko la habari njema na mabadiliko, si tu katika mazingira ya imani ya kidini, lakini katika mazingira hata ya kiuchumi na kisiasa.

Alisema watu hawapaswi kuogopa, bali kulinda makundi yao wakisubiri habari njema na habari hiyo si kwa ajili ya matajiri wanaoishi katika majumba ya kifahari, bali kwa ajili ya wote, habari ambayo ni ya furaha ambayo ni chimbuko la heri kwa wanadamu wote.

“Habari hii siyo kwa ajili ya matajiri, siyo kwa ajili ya wale wanaoishi katika majumba ya kifalme ni habari ya furaha ambayo itakuwa chimbuko la furaha na heri kwa wanadamu wote, Mwenyezi Mungu atujaaliye hilo katika Taifa letu,” alisema Pengo.

Magufuli asisitiza kazi 
Wakati viongozi wa dini wakihamasisha Watanzania kumuombea, Rais Magufuli mwenyewe alihudhuria ibada ya Sikukuu ya Krismasi katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro, lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika ibada hiyo, alipewa nafasi ya kutoa salamu, ambapo aliwatakiwa Watanzania wote sikukuu njema ya Krismasi na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani wakikumbuka kufanya kazi baada ya shamrashamra za sikukuu.

Rais Magufuli alisema watu wakumbuke kwamba ustawi wa nchi unatokana na watu kufanya kazi ndio maana anasimamia kaulimbiu yake ya Hapa Kazi Tu.

 “Tunaposherehekea sikukuu hizi, tukumbuke ya kwamba baada ya shamrashamra ni kufanya kazi kwa bidii kwa ujenzi wa Taifa letu,” alisema Rais Magufuli.

See These Youth In Action At The Beach on X-Mass Day, Our Camera Captured Everything!

0
0

People were watching but these fun-seekers were at a 'point of no return.' See for yourself...






Mwanamuziki Diamond Platnumz Aweka Historia Tena Dar Live...Angalia Alichofanya Hapa

0
0
Diamond Platnumz akisema na mashabiki wake waliofurika Dar Live usiku wa kuamkia leo
IMG_7989Diamond akicheza na mashabiki wake waliofurika Dar Live.
IMG_7359
Akicheza na wacheza shoo wake wa kike.
IMG_1416Nyomi ya kufa mtu ndani ya Dar Live wakiendelea kumshangilia Diamond.
IMG_7371Wacheza shoo wa kike wa Diamond wakifanya yao.
IMG_7324Diamond akiwachombeza mashabiki.
IMG_7325Diamond akicheza na wacheza shoo wake wa kiume.
IMG_7344Akiongea na mashabiki.
IMG_7377
IMG_7379IMG_7383Diamond akifanya yake na wacheza shoo wake.IMG_7390Diamond baada ya kuwakonga nyoyo mashabiki wake waliofurika Dar Live na wao kuridhika aliamua kupozi nao kwa picha hii.IMG_7432Nyomi ya kutisha ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live.IMG_7455
IMG_7973Diamond akizidi kuwapa raha mashabiki wake wa Dar Live.IMG_7927Mashabiki baada ya kupagawa na shoo.IMG_7975…Akiongea na mashabiki wake.IMG_7991Akiwasalimia mashabiki.
(PICHA: MUSA MATEJA, RICHARD BUKOS/GPL)

Bondia Mashali Amtwangia Cheka Nyumbani Kwao Morogoro

0
0
Bondia Thomas Mashari kutoka Dar amempiga Francis Cheka kwa pointi mjini Morogoro katika pambano la raundi 10, uzito wa Kg 77.

Majaji wamempa Mashari pointi 94, 96 na 97 wakati mwenyeji Cheka amepata pointi 96, 93 na 93

Mwanamuziki Bayo Atoa Wimbo Mkali wa Riddim Kama Zawadi ya New Year..Usikilize na Kudownload Hapa

0
0
Msanii Bayo amefanya riddim nyingine na this time ni kny beat ya Paper Loving ilofanywa na msanii wa Jamaica Chris Martin. Bayo ameiambia udaku specially kua huu ni wimbo ambao ameutoa kama bonus ya new year. Hivi karibuni Bayo the great ataachia video ya wimbo wa Kitimtim ambayo itatengenezwa chini ya director Nick Dizzo wa Focus Films.

Sikiliza na Download Hapa chini:

Vyeti Bandia Vinaweza Kuondoa Wafanyakazi Wengi Wizara ya Afya!

0
0
Inasemekana kwamba kuna idadi kubwa sana ya wauguzi na baadhi ya watumishi wa wizara ya Afya hasa mahospitali kwa kiasi kikubwa wamegushi vyeti vyao vya sekondari na wengine hawana kabisa vyeti hivyo, wengi ndani ya makazi yao wako matumbo moto wakisubiria fagio la Magufuli.

Inasemekana endapo fagio hilo litatua katika idara mbali mbali ndani ya wizara hiyo linaweza kuzoa watumishi wengi sana ambao kwa muda mrefu wamekua wafanyakazi wa umma ambapo hali hiyo inaweza kusababisha kupungua kwa wafanyakazi wengi sana.

Chanzo: Baadhi ya watumishi wa mahospitali.

Gwajima Amkana Edward Lowassa...Adai Yeye Hakuwahi Kumuunga Mkono Wakati Wa Kampeni

0
0
Mchungaji wa kanisa la ufufuo na uzima,Josephat Gwajima amejitokeza hadharani  na kukana kwamba hakuwahi kumuunga mkono Edward Lowassa wakati wa kampeni za Urais.

Akiongea katika mahojiano maalumu na kituo cha Azam Tv, Gwajima amesema yeye hakuwahi kuwa mshirika wa Lowassa wala chama chochote, bali aliitwa jijini Arusha na Jangwan Dar es Salaam  kwa ajili ya maombi tu na sivinginevyo....

Amesema kitendo cha kukubali wito huo wa maombi kimewafanya watanzania wahisi kwamba yeye alikuwa team Lowassa, kitu ambacho sio kweli.

Amedai yeye alikuwa mfuasi wa mabadiliko ya nchi, alikuwa akiunga mabadiliko ya nchi na SIO  personality ya mtu au chama cha mtu.

Wakati Gwajima akikana kumuunga mkono Lowasaa, kumbukumbu zinaonyesha kuwa mchungaji huyo alikuwa ni team Lowassa na  alikuwa mstari wa mbele kuhakikisha mheshimiwa Lowassa anashinda kiti cha Urais.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa Gwajima alitumia nguvu kubwa sana wakati wa kampeni kupambana na Dr Slaa ambaye wakati huo alikuwa akishusha makombora mazito kuhakikisha Lowassa hashindi huku akimtuhumu Gwajima kuwa mshenga wa Lowassa aliyemfuata kumpigia debe wampokee Chadema

Tazama Video hii Kumsikiliza Gwajima

Baada ya Mchangaji Gwajima Kumkana Lowassa, nimelezimika  kuitafuta Video ya Maombi ya Gwajima tarehe 29.08.2015 Jangwani, Dar es Salaam wakati UKAWA Walipokuwa wakizindua kampeni zao.

Miongoni mwa maneno aliyoyasema Gwajima siku hiyo ni kuwa Anayemlaani Lowassa  na Haji Duni, Laana iwarudie wenyewe kwa kuwa huu ni wakati wa Lowassa na hakuna wa kumzuia. Je, ni Kweli Gwajima hakuwa mshirika wa Lowassa kama alivyomkana leo?

Tazama video hapo chini

UTAFITI: Mimba Nyingi Hutungwa Siku ya Krismasi......

0
0
Utathmini wa takwimu kuhusu watoto wanaozaliwa Uingereza umebaini mimba nyingi hutungwa wakati wa Krismasi kuliko wakati mwingine wowote ule wa mwaka.

Takwimu hizo za kipindi cha miongo miwili kutoka Idara ya Taifa ya Takwimu zinaongeza watoto wanaozaliwa huongezeka sana wiki 40 (miezi 9) baada ya msimu wa sikukuu.

Hili huenda linatokana na wanandoa kutumia muda mwingi pamoja wakisherehekea, au kulenga makusudi mwanzo wa mwaka mpya wa shule ambao huanza mapema Septemba nchini humo.
“Ongezeko la watoto wanaozaliwa mwishoni mwa Septemba ni ishara kwamba mimba nyingi hutungwa wiki chache kabla ya Krismasi na kuendelea hadi siku chache baada Krismasi kuliko wakati mwingine wowote wa mwaka,” idara hiyo imesema.

Kawaida watoto 1,800 huzaliwa kila siku lakini idadi hii hupanda hadi 1,974 siku yenye kuzaliwa watoto wengi zaidi ambayo ni Septemba 26.
Siku zinazoshuhudia idadi ndogo zaidi ya watoto wanaozaliwa ni siku za Krismasi, Boxing Dei na siku ya Mwaka Mpya.

Hili sana huenda linatokana na idadi ndogo ya watu wanaopangiwa kujifungua kwa kufanyiwa upasuaji siku hizo, kwani huwa ni siku za mapumziko.
Profesa wa masuala ya uzazi kutoka Chuo Kikuu cha Sheffield Allan Pacey ameambia BBC: “Wazo kwamba mimba nyingi hutungwa wakati wa Krismasi lina msingi. Nina uhakika sherehe na shamra shamra za wakati huu huchangia.”

UHURU and MUSEVENI are jealous of MAGUFULI! See what they did to him on Whatsapp

0
0

Newly elected Tanzanian President, John Pombe Magufuli’s impressive performance has put him at loggerheads with President Uhuru Kenyatta and Uganda’s President Yoweri Kaguta Museveni.

According to an aide close to the Tanzanian new leader, Magufuli’s fight against corruption, laziness and wastage in his country has infuriated Uhuru and Museveni because ‘he is making them look bad to their citizens’.

The aide said that over the last one month, Magufuli has been trying to reach Uhuru and Museveni but he is always told by their aides that they are busy or in a meeting.


 “The most common excuse he has been getting is that they are in a meeting. But, surely, no one has meetings for a whole consecutive week that runs into the wee hours of the night,” said Magufuli’s aide.

The aide said that Magufuli has also found himself out of EA President’s WhatsApp group where they share about leadership and the state of their nations.

He also said that Uhuru and Museveni have been joined by Rwanda’s President, Paul Kagame who has ‘unfriended’ him on social media and stopped ‘following’ him.

Museveni and Uhuru are yet to respond to these accusations from Magufuli’s aide.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Disemba 27, Ikiwemo ya Dr Shein Kutinga Ikulu Kwa Magufuli

0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Disemba 27, Ikiwemo ya Dr Shein Kutinga Ikulu Kwa Magufuli


Dkt. Shein Atinga Ikulu Kwa Rais John Pombe Magufuli na Kumweleza Kinachoendelea Kwenye Mazungumzo Zanzibar

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein Ikulu Jijini Dar es salaam.

Akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya mazungumzo hayo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein amesema lengo la mazungumzo hayo ilikuwa ni kumpa taarifa Rais Magufuli juu ya hali ya mazungumzo ya kisiasa yanayoendelea huko Tanzania Zanzibar baada ya uchaguzi Mkuu.

Rais Shein amesema mazungumzo juu ya hali ya Zanzibar yanaendelea chini ya kamati maalum ambayo yeye ndiye mwenyekiti na wengine wakiwa ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Rais Mstaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungo wa Tanzania Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa awamu ya sita wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume na Rais Mstaafu wa awamu ya tano wa Zanzibar Dkt. Salmin Amour.

Amesema tayari kamati hiyo imeanza mazungumzo tangu tarehe 09 Novemba, 2015 na kwamba mazungumzo hayo yamelenga kujadili hatma ya Zanzibar baada ya uchaguzi Mkuu.

Rais Shein amebainisha kuwa mazungumzo hayo bado yanaendelea.

"Kwa hiyo nimekuja kumpa taarifa Mheshimiwa Rais Magufuli kuhusu maendeleo ya mazungumzo yetu ili aweze kujua kinachoendelea akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo Zanzibar ni sehemu yake, na sisi ni jukumu letu kumpa taarifa hiyo" Alisema Rais Shein.

Aidha Rais Shein ameongeza kuwa mazungumzo hayo yatakapokamilika wananchi watajulishwa.

Ridhiwan Aweka Mambo Hadharani, Soma Alichojibu Kuhusiana na Shutuma za Ufisadi Dhidi yake

0
0
Ndugu zangu waandishi wa habari, nimeamua kuwaita ili kuzungumza nanyi kuhusu baadhi ya mambo yaliyokuwa yanasemwa katika vyombo vya habari kuhusu mimi.

Awali ya yote napenda kusema kuwa habari hizo ni UONGO mtupu, ni mambo yanayozushwa na waandishi wa habari hizo kwa nia ya kuchafua jina langu kwa sababu wanazozijua wanaoandika. UKWELI ni kwamba haya ni mambo yenye kufanywa kwa nia na dhamira mbaya dhidi yangu na hata familia yangu.

Hivi karibuni, kwa mfano, lipo gazeti moja liliandika na kutoa picha yangu na mtu mmoja waliyedai ni Mhe. Paul Makonda eti akinifunga kamba za viatu. Katika maelezo yake mwandishi akadai kuwa Mhe. Makonda alipata uteuzi kuwa Mkuu wa wilaya ya Kinondoni kwa sababu hiyo. Huu ni uongo usiokuwa na hata chembe ya ukweli. Napenda watanzania wajue kuwa hakuna wakati wowote Baba yangu alipokuwa Rais wa nchi yetu alinihusisha kwa namna yeyote ile katika uteuzi wa mtu yeyote katika Serikali. Hivyo basi kujaribu kunihusisha na uteuzi wa Mhe. Paul Makonda kuwa Mkuu wa Wilaya wa Kinondoni ni jambo lisilokuwa na ukweli wowote.

Pili, Yule mtu anae onekana katika ile picha siyo Mhe. Paulo Makonda bali ni Bwana Deogratius Kessy anayefanya kazi katika kampuni ya ushonaji na mavazi ya Bwana Sheria Ngowi. Nilishona safari suti kwenye kampuni hiyo. Nilipokwenda kuchukua nguo yangu na nilipovaa ili kuona kama imeshonwa vizuri, Bwana Sheria Ngowi alitaka nivae viatu vya ngozi. Bahati mbaya nilikuwa nimevaa sandals hivyo akaamua kunipa viatu vya dukani kwake nivae. Wakati bwana Deogratius Kessy akinisaidia kuvaa viatu ndipo ile picha ikapigwa nampiga picha wa kampuni ya Bwana Sheria Ngowi , inashangaza na kusikitisha kuona picha hiyo inatumiwa kupotosha ukweli kwa kutoa maelezo ya uongo. Ni dhahiri kwamba mwandishi aliamua kufanya hivyo kwa maksudi mazima ya kutoa sifa mbaya kwangu na kwa Mheshimiwa Paul Makonda. Hivi ndivyo uhuru wa habari unavyostahili kutumika?

Siku za nyuma gazeti lingine liliandika eti kuwa nilihojiwa kuhusu sakata la makontena bandarini. Napenda kuwaambia ndugu waandishi wa habari kuwa sijawahi kuhojiwa na mtu yeyote, chombo chochote au kamati yeyote kuhusu madai hayo. Ni uongo usiokuwa na ukweli wowote. Ni mambo ya kugushi na uzushi kabisa, Ninayasema maneno haya kwa kujiamini na kama mwandishi ana uthibitisho wa madai yake autoe hadharani watu wauone. Aidha, nasema kama yupo mtu aliyenihoji ajitokeze kukanusha ninayoyasema, Namtaka aseme wazi. Nawahakikishia kuwa mtu huyo hayupo na wala hatakuwepo.

Ndugu waandishi na watanzania wenzangu, inaelekea kuna mtu au genge la watu mahali fulani ambao wameamua na kudhamiria kuchafua jina langu na la familia yangu kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Tangu Serikali ya awamu ya tano ianze jitihada za kuwabana watu wanaokwepa kulipa kodi za Serikali bandarini wapo watu wamekuwa wakifanya jitihada za kunihusisha na watu Fulani wanaotuhumiwa kuhusika na ukwepaji huo. Wapo baadhi ya watu wamekuwa wakidai eti baadhi ya makontena hayo ni yangu. Na, wapo waliodai eti kuwa nimekuwa nawasaidia baadhi ya wafanyabiashara hao kukwepa kodi kwa kutoa maagizo kwa maofisa wa forodha wasiwatoze kodi inayostahili kulipwa.

Napenda kuwafahamisha kuwa sijawahi kuagiza bidhaa zozote kutoka nje hivyo sijawahi kuwa na kontena lolote ambalo nililowahi kutakiwa kulipia ushuru nikakwepa. Aidha, sijawahi kumuombea msamaha wa kutokulipa au hata kupunguziwa kodi mfanyabiashara yeyote au mtu yeyote aliyeingiza kontena nchini kutoka nchi za nje. Kama mtu ana ushahidi autoe hadharani mimi niuone na dunia iuone. Nawahakikishia ushahidi huo haupo na wala hautokuwepo. Labda uwe wa kugushi na wakifanya hivyo wataumbuka.

Napenda pia kutumia nafasi hii kusema kuwa sina na wala sijawahi kumiliki lori au basi wakati wowote katika maisha yangu. Aidha, sina hisa au ubia na mtu yeyote au kampuni yeyote ya malori au mabasi. Nayasema haya kwa sababu wapo wabaya wangu wanaoeneza maneno ya kunihusisha na kumiliki malori na mabasi. Pia kunihusisha na baadhi ya makampuni yanayomiliki na kuendesha biashara ya malori na mabasi.

Ndugu wanahabari, napenda kusema kwa kurudia na kusisitiza kuwa sina lori wala basi hata moja na sina ubia na wafanyabiashara ama makampuni yoyote yanayofanya shughuli hizo. kama yupo mtu yeyote ana ushahidi wa kuhusika kwangu auweke hadharani watu wauone. Napenda ieleweke kuwa kama ningekuwa na ubia wa namna hiyo nisingekuwa na sababu ya kuficha. Niogope kitu gani ? Ukweli ni kwamba sizuiliwi kufanya biashara kama nikipenda kufanya hivyo , Hata kwa nafasi yangu ya sasa ya uongozi yaani mbunge bado sina kizuizi. Mbona Bungeni wapo wafanyabiashara wakubwa kwa wadogo. Isingekuwa ajabu kwangu kufanya biashara hivi sasa mimi pamoja na kuwa mbunge ni mwanasheria wa kujitegemea na nimeiweka katika TAMKO langu la mali na madeni la viongozi kwa mujibu wa sheria ya maadili ya viongozi.

Nimewavumilia sana lakini sasa nimechoka, nimeona leo nivunje ukimya. Nimeona niseme kidogo kwani bila ya kufanya hivyo nitaliacha genge la watu wenye nia mbaya na mimi waonekane wanasema kweli. Wahenga wanasema msema pweke hushinda! Nikiendelea kukaa kimya uongo wao utageuka kuwa ukweli dhidi yangu.

Naambiwa hapa nchini siku hizi kila jengo jipya linalojengwa linasemekana ni la Ridhiwani, kituo kipya cha petrol ni cha Ridhiwan.
Nimeanza kuona athari za uongo huo, Siku moja kuna mtu alikuja kuniomba nimpangishe katika lile jengo la PSPF pale stesheni. Nilipomuuliza nitampangishaje akasema mbona watu wamemwambia ni jengo langu!? Siku nyingine nikakutana na jamaa mmoja mwenye asili ya kiasia akiwa anahema. Akasema ananiomba sana niache kutaka kupora kampuni yake,nikamuuliza kampuni gani hiyo? Na kwanini anasema hivyo?

Akanijibu, anasikia wakisema kampuni yake ni ya ridhiwani wakati kampuni hiyo hata yeye kairithi kwa baba yake na yeye alirithi kwa baba yake zaidi ya miaka hamsini iliyopita, Nikamwambia kuwa habari hiyo si kweli, sina mpango huo na wala sina sababu ya kufanya hivyo. Hayo ni maneno yanayoenezwa na wabaya wangu walioamua kunipakazia kwa sababu wazijuazo wao. Tukaachana ,sijui kama ameamini kama sina mpango wa kumpora kampuni yake. Siku moja Mzee wangu mmoja wa kwetu kijijini alinilalamikia kuwa nina roho mbaya kwa vile sitaki kumpa kazi mwanae kwenye kampuni yangu ya malori wakati yeye ni dereva mzuri, Nilipomueleza Yule mzee kuwa sina lori hata moja akashangaa na kusema mbona watu wanasema nina malori mengi. Ndugu zangu mnaiona fitina kubwa inavyotengenezwa katika jamii kuhusu maneno haya, Wapo wanaoniona mimi FISADI, Wapo wanaoniana mimi nina Roho mbaya, Wapo wanao niona mie nataka kupora mali zao. Baada ya Baba kustaafu maneno yamekuwa mengi na yanazidi kupata kasi. kila kukicha wanazua jambo jipya. Nimeoa niyaseme haya ili watu wajue ukweli wa upande wangu.

Naomba nimalize kama nilivyoanza kwamba yanasemwa mengi lakini ni maneno ya uzandiki, uzushi na ni uongo mtupu usiokuwa na chembe ya ukweli. Wale wanaosema, kuandika, na kueneza maneno hayo wanajua kuwa wanasema UONGO, ila wanafanya hivyo kwa vile wana nia mbaya dhidi yangu na familia yangu , Naomba watanzania muyapuuze maneno hayo, naomba watanzania wenzangu muupuuze uongo huo.
siko hivyo, sina mali hizo na wala sifanyi hayo wanayodai nafanya na wala sina mpango wa kuyafanya.

Imetolewa na:-
Ridhiwan J. Kikwete
Mbunge wa Jimbo la Chalinze.

Baada ya Askofu Gwajima Kumkana Lowassa Laivu, Dkt. Slaa Amtaka Gwajima Awaombe Radhi Maaskofu Pamoja na Watanzania.

0
0
Baada ya Askofu Gwajima kusema kuwa hakuwa akimuunga mkono Lowassa, Dkt. Slaa amtaka awaombe radhi Maaskofu pamoja na Watanzania.

Asema hakutegemea Askofu Gwajima kumkana hadharani Lowassa

My Boyfriend Just Told Me I'm Boring In Bed... What Should I Do?

0
0

I caught my boyfriend searching on Google "My girlfriend is so boring in bed. How do I tell her?" So I asked him what's up and he, pomp and plain, told me he is not satisfied with our s*x life.

I can't even tell you how much of a blow that was to me. I was absolutely gutted. I didn't even know whether to cry or beg him.

I know I'm not the prettiest girl in town and I don't feel comfortable flirting around, or things like that. But I know I'm a very good girl, I try! What the hell can make someone not boring in bed?

What can I do now?

Mrithi wa Dk Slaa CHADEMA Kujulikana Mwezi Ujao

0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema mchakato wa kumpata katibu mkuu wake utaanza mwezi ujao.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho, ndiye mwenye jukumu la kupendekeza jina la Katibu Mkuu na kulipeleka katika Baraza Kuu kupigiwa kura, kisha kupitishwa.

Tangu Agosti 3, Katibu Mkuu wa chama hicho Dk Willibrod Slaa alipumzishwa na Baraza Kuu baada ya kutofautiana na Kamati Kuu baada ya chama hicho kumkaribisha waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu ndiyo anakaimu nafasi iliyoachwa wazi na Dk Slaa.

Mchakato wa kumpata Katibu Mkuu umeanza kuibua hali ya sintofahamu, huku majina mbalimbali ya vigogo wa chama hicho yakitajwa, likiwemo la Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye ambaye hivi karibuni alitangaza rasmi kujiunga na Chadema.

Kwa mujibu wa Katiba ya Chadema Ibara ya 6.3.5 inasema; (b) nafasi wazi za uongozi walioteuliwa zitazibwa na vikao husika kwa kufanya uteuzi mpya katika muda usiozidi miezi mitatu tangu nafasi kuwa wazi, (c) muda wa uongozi wa muda kwa mujibu wa kifungu 6.3.5 (b) hautazidi mwaka mmoja (d) bila kujali sharti la kifungu 6.3.5 (c) hakutafanyika uchaguzi rasmi wa kuziba nafasi kama kumebakia miezi sita tu au chini ya hapo kabla ya uchaguzi mkuu wa kawaida wa Chama unaofuata kufanyika.

Akizungumzia mchakato huo, Mwalimu alisema Baraza Kuu litakutana mapema Januari mwakani, kujadili masuala mbalimbali, likiwamo la kumpata Katibu Mkuu.

“Si kama chama kimekaa muda mrefu bila Katibu Mkuu. Yupo anayekaimu na kinachofanyika sasa ni kumpata Katibu kamili.”

“Baraza Kuu lilikutana litajadili suala hilo kwa kina na kuja na mapendekezo mbalimbali,” alisema Mwalimu na kusisitiza kuwa kila jambo litafanyika kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho.

Alisema uongozi wa muda ndani ya chama hicho hauwezi kuzidi mwaka mmoja na nafasi ya kuteuliwa muda wa kukaa wazi hauzidi miezi mitatu kabla ya kuteuliwa kiongozi mwingine.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images