Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live

Kiama Cha Waliosafiri Nje Bila Ruhusa ya Rais Chaja....

0
0
Adhabu inawanyemelea watumishi wa serikali waliokaidi agizo la kutosafiri nje ya nchi bila kibali cha Rais John Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

Habari zilizopatikana kutoka baadhi ya wizara  zilieleza jana kuwa tayari baadhi ya Makatibu Wakuu wa Wizara wameshapewa orodha ya majina ya watumishi waliosafiri nje ya nchi kinyemela.

Chanzo kimoja cha habari kiliiambia Nipashe kuwa tayari majina hayo yamepatikana na kinachofanyika sasa ni kupitia taratibu, sheria na kanuni kabla ya kuwachukulia hatua.

Watumishi wanne wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) wamesimamishwa kazi kwa kwenda nje ya nchi licha ya maombi yao ya kusafiri kukataliwa na mamlaka.

Jana Nipashe ilifanya mahojiano na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee na Watoto, Dk. Donald Mmbando ili kufahamu ni watumishi wangapi kwenye wizara yake ambao wamesafiri nje ya nchi  bila kibali cha Rais.

Katika mazungumzo na gazeti hili Dk. Mmbando alikiri kukabidhiwa taarifa kuhusu watumishi waliosafiri nje ya nchi bila kibali cha Ikulu na kwamba kwa sasa kuna taratibu ambazo zinafanyiwa kazi na ngazi husika kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi.

“Ni kweli niliagiza nipatiwe taarifa ya watumishi hao na nimeshapewa ila kuna tataribu ambazo zinafanyiwa kazi na zitakapokamilika itatolewa taarifa ya wale wote waliosafiri na wamefanywa nini,” alisema Dk. Mmbando.

“Kwa sasa siwezi kulizungumzia ila likikamilika tutawajulisha.” Hivi karibuni Dk. Mmbando alitoa taarifa kwa wakuu wa Idara wizarani kwake akiwataka ifikapo Desemba 21 awe amepata taarifa ya wale wote waliokiuka agizo la Rais la kutosafiri nje ya nchi.

Dk. Mmbando aliandika dokezo kwenda kwa wakuu wa idara hiyo ambayo iliwataka kuwataja watumishi walio chini yao ambao walisafiri nje ya nchi baada ya katazo la Rais Dk. Magufuli.

Katika dokezo hilo walitakiwa kueleza watumishi hao wamesafiri kuelekea nchi gani, tarehe ya safari, madhumuni ya safari hizo, safari hizo zimegharamiwa na nani pamoja na kiasi cha fedha kilichotumika.

Waliosimamishwa kazi Takukuru ni Msemaji Doreen Kapwani, Mary Mosha, Ekwabi Mujungu na Rukia Nikitas. Awali, Ofisi ya Rais ilisambaza mwongozo kwa taasisi na mashirika ya umma unaoweka masharti ya ambayo watumishi wa umma wanaotaka kusafiri nje ya nchi watatakiwa kuyatimiza ili wapewe kibali cha kusafiri.

Masharti hayo ni kuomba kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi Sefue na maombi hayo yawasilishwe kwa Msajili wa Hazina kabla ya kwenda kwa Sefue ili mwombaji aweze kujenga hoja kwa kuzingatia umuhimu wa safari hiyo na tija itakayopatikana kutokana na safari hiyo.

Masharti hayo yanamtaka Mtendaji Mkuu wa Shirika ama taasisi apime aone kama safari hiyo ni muhimu  kuombewa kibali kwa Katibu Mkuu Kiongozi kabla ya kuwasilishwa Hazina.

Sharti lingine ni umuhimu wa safari hiyo na isipofanyika itaathiri vipi taifa na mwombaji  aeleze manufaa ya safari hiyo kwa taasisi na taifa kama imewahi kufanyika huko nyuma.

Ofisi za Umma zilipokea barua kutoka kwa Msajili wa Hazina Novemba 12 mwaka huu ikieleza kuwa Rais Magufuli ametoa zuio la jumla kwa safari za nje ya nchi katika utumishi wote wa umma na mihimili yake. Barua hiyo ya Hazina ilisema zuio hilo litadumu hadi pale itakavyoelekezwa vinginevyo.

Chama Cha CUF Wasisitiza Kutorudia Uchaguzi Mkuu....

0
0
Chama cha Wananchi CUF Zanzibar kimesema hakipo tayari kupokea maazimio ya mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa Uchaguzi Mkuu kama yatakuwa yanakwenda kinyume na maamuzi waliofanya wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 Mwaka huu.

Tamko hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mipango wa Chama hicho, Omar Ali Shehe katika mahojiano maalum na Nipashe Jumapili juu ya mazungumzo ya kutafuta mufaka wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.

Mazungumzo hayo yanaogozwa na Rais wa Zanzibar DK. Ali Mohamed Shein na kuwashirikisha Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar na Mgombea urais kupitia CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi pamoja na marais wastaafu wa Zanzibar. Alisema CUF kiko tayari kupokea maamuzi na kuyaheshimu kutoka katika Kamati hiyo ya mazungumzo kama yatakuwa yamezingatia maamuzi ya wananchi waliyoyafanya kupitia Uchaguzi Mkuu huo.

Inaaminika kuwa matokeo yaliyofutwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yalikuwa yakimpa ushindi Hamad. “Sisi tunasubiri matokeo ya mazungumzo yao tukiamini kwamba mazungumzo hayo hayatokwenda kinyume na maamuzi waliyofanya wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba Mwaka huu,” alisema Shehe.

Alisema kuwa Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salum Jecha hakuwa na mamlaka ya kikatiba na kisheria kufuta matokeo ya uchaguzi huo ambao tayari ulikuwa umekamilika kwa asilimia 70 na matokeo ya majimbo 31 yakiwa yametangazwa katika uchaguzi huo.

Shehe alisema siri ya kufutwa kwa matokeo ni baada ya Mwenyekiti kuona CCM wapo katika hatari ya kuanguka katika uchaguzi huo na hakuna sababu nyigine. “Mchezo wa kufuta matokeo kwa sababu tu chama tawala kiko katika hatari ya kuanguka utaendelea kufanyika kama  tukiacha hivi hivi,” alisema.

“Huku ni kuvuruga demokrasia ya nchi yetu.” Alisema miezi miwili sasa imemalizika lakini hakuna mtu yoyote aliyefikishwa Mahakamani kwa kuharibu uchaguzi au Mwenyekiti kuweka vielelezo na ushahidi wa kuharibika kwa uchaguzi huo.

Aidha, alisema msimamo wa Baraza Kuu la CUF ndiyo muongozo wa chama kuwa Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar warudi kazini wakamilishe ujumlishaji wa matokeo ya uchaguzi wa awali na kumtangaza mshindi wa uchaguzi huo.

Alisema kuwa hali ya kisiasa ya Zanzibar ipo katika giza kutokana na wananchi kushindwa kufahamu lini watapata viongozi wa kidemokrasia huku wakiendelea kushuhudia kupanda kwa gharama za maisha Visiwani humo.

Hata hivyo alisema kuwa mazungumzo hayo yamesaidia kwa kiasi kikubwa kutuliza hali ya amani na kuondoa hofu wananchi lakini alitaka yakamilike kwa wakati ili wananchi wajue hatia yao ya kupata viongozi.

Aidha alisema kuwa CUF inatambua kuwepo kwa watu wanaotaka kupindisha uchaguzi uliyofanyika Oktoba 25 mwaka huu lakini alisema hawatafanikiwa kutokana na  ripoti za waangalizi wa ndani na nje kuweka wazi kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki Zanzibar.

“Wakati Mwenyekjiti wa ZEC anatangaza kufuta matokeo tayari matokeo katika Majimbo 54 yalikuwa yamekamilika na kubandikwa matokeo na Wagombea kupewa vyeti vyao vya ushindi hoja ya kufuta matokeo Mwenyekiti katoa wapi?” Aliuliza.

“Haiwezekani kufanyika uchaguzi wa marejeo kabla ya uchaguzi wa mwanzo kukamilika Zanzibar, sawa na kusherekea harusi kabla ya ndoa kufanyika.”

Alisema wakati Mwenyekiti Jecha anafuta matokeo hayo katika meza yake majimbo tisa yalikuwa yanamsubili kutangaza matokeo baada ya uhakiki kukamilika na kubakia Majimbo 14 ya Wilaya tatu za Kisiwani Pemba.

Aidha alisema kuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo alivunja kanuni na sheria kutokana na kitendo cha ZEC kuhakiki matokeo ya Urais mara mbili wakati tayari kazi kama hiyo ilikuwa imefanyika katika Majimbo na kumalizika na kumalizika  salama kabla ya kufutwa kwa matokeo hayo.

“Mwenyekiti arudi kazini atangaze marokeo na mshindi wa urais wa Zanzibar uchaguzi wa marudio hatutaki kusikia Zanzibar,” alisema Shehe.

Jecha alisema aliamua kufuta matokeo ya uchaguzi huo baada ya kutawaliwa na vitendo vya udaganyifu ikiwemo idadi ya wapiga kura kuzidi katika baadhi ya vituo kinyume na idadi ya watu waliosajiliwa katika daftari la wapiga kura Visiwani humo.

‘Mwakyembe Akianza Mchakato wa Katiba Tu, Nitafunguka’ Warioba

0
0
Urafiki wa Jaji Joseph wariona na chama chake cha CCM uliofufuka wakati wa Uchaguzi Mkuu, unaweza kuingia tena doa baada ya waziri huyo mkuu wa zamani kusema iwapo Serikali itaanza harakati za kumalizia mchakato wa Katiba, atatoa yake ya moyoni.

Jaji Warioba, aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alishambuliwa na makada wa chama hicho kutokana na kuwasilisha Rasimu ya Katiba iliyotofautiana na utashi wa CCM, hasa kwenye suala la muundo wa Muungano kuwa wa serikali tatu.

Lakini tofauti hizo zilipotea wakati wa Uchaguzi Mkuu alipoamua kusimama kidete kumtetea mgombea urais wa CCM bila ya kujali kilichomsibu kwenye Bunge la Katiba.

Baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe kueleza kuwa Rais John Magufuli amemuagiza aendelee na mchakato wa Katiba kuanzia pale alipoishia, Jaji Warioba amehifadhi maoni yake, lakini anasema ana yake ya moyoni.

“Kwa sasa siwezi kusema chochote kuhusu kauli ya Serikali kuendelea na mchakato wa Katiba,” alisema Jaji Warioba alipoulizwa na Mwananchi kuhusu kauli hiyo ya Dk Mwakyembe.

“Nasubiri nione. Pale watakapoanzia tu, ndiyo nitasema.”

Jaji Warioba alikuwa mmoja wa wadau mbalimbali walihojiwa na gazeti hili kuhusu mwenendo wa suala hilo lililogharimu mamilioni ya fedha za walipa kodi.

Wadau wengi walishauri mchakato huo kuanzia kwenye Rasimu ya Katiba na kutafutwa maridhiano kabla ya kuendelea na suala hilo la kuandika Katiba Mpya kuibadili ya sasa iliyoandikwa mwaka 1977.

Mchakato wa Katiba ulisitishwa mapema Aprili wakati ukisubiri hatua ya mwisho ya kupiga Kura ya Maoni kutokana na kutokamilika kwa uandikishaji wapigakura. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilisema imeamua kuahirisha Kura ya Maoni iliyokuwa ipigwe Aprili 30 kwa kuwa kazi hiyo ya kuandikisha wapigakura ilikuwa haijakamilika na haikusema mchakato huo utaendelea lini.

Lakini hivi karibuni, Dk Mwakyembe alisema Rais amempa kazi ya kumalizia mchakato wa Katiba kutoka pale ulipoishia, akimaanisha upigaji wa Kura ya Maoni, jambo ambalo limepingwa vikali na wadau hao.

Mmoja wa wadau hao, Deus Kibamba, ambaye ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba (Jukata), alisema iwapo mchakato huo utaendelea bila ya kutafuta maridhiano, hakutakuwa na Katiba Mpya.

“Mchakato wa Katiba Mpya ni jipu linalosubiri kutumbuka,” alisema Kibamba.

“Wakiendelea na mchakato huo bila kwanza kufanyika kwa maridhiano, watapata kashfa kubwa maana tutapata Katiba ambayo si mpya.”

Alisema busara inayotakiwa kufanyika sasa ni kuitishwa kwa jopo la watalaamu watakaoichambua Rasimu ya Katiba na Katiba Inayopendekezwa na kutoa ushauri wa kuendelea na mchakato huo.

“Tumetoa ushauri wa mambo mengi, lakini yalipuuzwa. Hili si jambo la kulazimisha. Huwezi kuendelea wakati kuna pande mbili zinapingana, hii ni hatari kwa kitu muhimu kama hiki ambacho ndicho kitakachotupa dira na mwelekeo wa taifa letu,” alisema.

Alisema kilichozungumzwa na Dk Mwakyembe ni mwendelezo wa “kutoambilika” kwa wale waliotakiwa kuutazama upya mchakato wa kupata Katiba Mpya baada ya kuonekana kuwa na kasoro nyingi.

Alikuwa akizungumzia kugawanyika kwa Bunge la Katiba baada ya wajumbe kutoka vyama vinne vya NCCR-Mageuzi, Chadema, NLD na CUF kususia vikao kwa madai kuwa Bunge liliacha kujadili maoni ya wananchi na kuingiza utashi wa chama tawala cha CCM. Vyama hivyo viliunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kushirikiana kulisukuma Bunge lirudie Rasimu ya Katiba.

Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha St Augustine, pia alizungumzia mgawanyiko uliojitokeza kwenye Bunge la Katiba akitaka kuwapo na maridhiano kwanza.

“Bunge la Katiba lilikwenda mrama na liliwagawa wananchi. Wajumbe wa Bunge hilo walipitisha mambo ambayo hayakutolewa maoni na wananchi. Walifumba macho wakadhani Katiba itapatikana lakini imeshindikana,” alisema Profesa Baregu.

“Rais Magufuli anapaswa kuwa na hekima na atambue wazi kuwa Katiba Inayopendekezwa si sahihi. Katiba sahihi ni ile iliyotolewa na Tume ya Warioba ambayo iliweka mabadiliko ya kiutawala, uongozi na maadili,” alisema.

Alisema kuwa mchakato huo unapaswa kuanzia pale ambako baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba waliposusia vikao vya Bunge hilo, kutokana na kuanza kuchakachuliwa kwa maoni ya wananchi yaliyokuwamo katika Rasimu ya Katiba.

Profesa Baregu alitaja mambo mawili yanayoweza kufanyika kuwa ni kutafuta watalaamu wa sheria na katiba ili kuwatumia kuandaa Katiba Mpya.

“Hawa watazungumza na wadau mbalimbali na kuja na Katiba hiyo. Jambo hili walilifanya wenzetu wa Kenya na walifanikiwa,” alisema.

“Pili, liundwe upya Bunge la Katiba na kuichambua Rasimu ya Katiba chini ya msaada na ushauri wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ndiyo iliyopita kwa wananchi na kukusanya maoni. Tutazame masilahi ya Taifa letu. Tutazame pale tulipojikwaa.”

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally pia alizungumzia kugawanyika kwa Bunge la Katiba.

“Mchakato mzima ulikumbwa na sintofahamu kubwa na kuligawa Taifa, sasa wanaposema wanaendelea walipoishia kivipi?” alihoji.

Alisema wengi wanadhani kinachopaswa kufanyika sasa ni Watanzania kupiga Kura ya Maoni, jambo ambalo alidai haliwezekani kufanyika bila kupatikana kwa muafaka wa pande mbili zinazovutana.

“Lazima umalize mvutano kwanza maana kasoro zilikuwa nyingi. Kila ngazi ya mchakato huo haikuwa na muafaka, kuanzia uundwaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Sasa hivi utaona (mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Katiba, Jaji Joseph) Warioba anasimama kwenye majukwaa ya CCM na kukiunga mkono chama chake.

“Pia aliyekuwa mjumbe wa tume hiyo, Profesa Mwesiga naye anasimama kwenye majukwaa ya Chadema na kukiunga mkono chama hicho,” alisema Bashiru, ambaye aliufananisha mchakato huo na kiporo chenye sumu.

“Kama wanataka kumaliza tatizo ni lazima watazame tangu mchakato huu ulipoanza na kujua tatizo lilikuwa nini na si kuendelea tu hivihivi.”

Profesa wa Chuo Kikuu Ruaha, Gaudence Mpangala alisema kupiga kura kupitisha Katiba Inayopendekezwa haitawezekana na badala yake akashauri kuundwa kwa Bunge jipya la katiba.

“Tuliona wajumbe 201 walioteuliwa na Rais walivyokuwa makada wa vyama vya siasa. Bunge la Katiba ni suala la kitaifa si vyama,” alisema.

Profesa huyo alisisitiza kwa hali ilivyo sasa, gharama haziepukiki ni lazima Bunge la Katiba liundwe upya kwa ajili ya kuichambua upya Rasimu ya Katiba ambayo ilitokana na maoni ya wananchi yaliyoondolewa katika Katiba Inayopendekezwa.

Kauli ya Sitta

Hata hivyo, Samuel Sitta, aliyekuwa mwenyekiti wa Bunge la Katiba, alipingana na maoni ya kuanza upya mchakato akisema tayari fedha nyingi zimetumika na kinachotakiwa kufanyika sasa ni mchakato kuendelea pale ulipoishia.

Kuhusu mvutano ulioibuka katika Bunge la Katiba, Sitta alisema: “Bunge lile lilikuwa na wajumbe 654. Ni wajumbe 114 tu ndiyo walitoka kwa kudai kwamba rasimu ya pili ya Warioba haifuatwi.

“Kusema kwamba hawa 114 ndiyo wanajua wananchi wanataka nini kuliko hawa 543 ni msimamo usio sahihi. Kwa nini watu 543 waonekane wote ni wajinga.”

Alisema hata wanaolalamikia kuwa suala la maadili limeondolewa katika Katiba Inayopendekezwa hawako sahihi, kwa maelezo kuwa katika Raismu ya Katiba jambo hilo liliwekwa katika Tunu za Taifa, katika Katiba Inayopendekezwa, maadili limewekwa katika utawala bora.

Alipoulizwa kuhusu mkanganyiko wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ili kuruhusu kuendelea kwa mchakato huo alisema: “Hayo ni juu ya Serikali. Watakwenda bungeni na watajua cha kufanya. Serikali ichague njia ambayo haiingizi gharama ya mabilioni kwa nchi.”

Diamond Wakomeshe Wanaosema Tiffah si Mtoto Wako, Wabandikie Matokeo ya DNA Kama Ulivyobandika ya Ujauzito

0
0

Pole Sana Diamond Platnumz  inasikitisha mtoto mdogo kusemwa midomoni mwa watu kuwa wewe sio Baba yake ,Wakomeshe wanaosema Tiffa si wako, wabandikie matokeo ya DNA Kama ulivyobandika ya ujauzito. Utawakata midomo kama alivyofanya Rafiki yako Ney wa Mitego.....

Mastaa wa Bongo Movies Walia na Tumbua Tumbua Majipu ya Rais Magufuli..Wadai Imewaletea Njaa.......

0
0
Jambo limezua jambo! Kufuatia tumbuatumbua inayoendeshwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa vigogo waliokuwa wanawapa jeuri mastaa wa kike mjini, wenyewe wameibuka na kusema kiongozi huyo ‘amewaua’ kwa njaa.

Chanzo makini kililiambia gazeti hili kuwa mastaa wengi wa kike wanalalamika njaa na ndiyo maana tangu alipoingia madarakani Rais Magufuli na kuanza kuwaondoa mafisadi, wasanii hao wamekuwa hawaonekani viwanja kama zamani kwa sababu hawana mkwanja.

Yaani wasanii wa kike wana hali mbaya sana ndiyo maana hamuoni wakiwa na mbwembwe kama zamani wamekuwa wakijifungia ndani tu hawataki kuonana na watu kwani hata hela za kwenda saluni kujiremba hamna maana wanasema waliokuwa wakiwapa jeuri wengi wao wamekumbwa na tumbua majipu,” kilisema chanzo hicho.

Baada ya kupata ubuyu huo, paparazi wetu aliwatafuta baadhi ya mastaa ambapo walikuwa na haya ya kusema;

ISABELA MPANDA

Kweli tumeathirika sana na hii tumbua majipu maana waliokuwa wakitupa fedha nyingi hata ukiomba milioni wanatoa kwa sasa wanaogopa hata ukiwapigia simu hawapokei huku wengine wakiwa ni wale vigogo waliokamatwa, Rais Magufuli ametunyoosha.

BABY MADAHA

Kiukweli lazima iathiri kwa sababu ilikuwa rahisi kwa mtu kudhamini hata katika muvi. Kipindi cha Kikwete (Jakaya, Rais wa awamu ya nne) mtu anakupa milioni 20 au 30 kwenye muvi lakini sasa hivi, thubutu.

MIRIAMU JOLWA ‘JINI KABULA’

Mimi sina kawaida ya kutoka na mapedeshee, bwana’ngu ni wa kawaida sana kwa hiyo sijui kama imeathiri vipi hiyo tumbua majipu.”

Chanzo: Global Publishers

Hivi Ndivyo Staa Diamond Akiwa na Mama Tiffah Pamoja na Dada Zake Walivyo Sherekea BOXING DAY

0
0
MAISHA YA KISTAA: Mkali wa Bongo Fleva, Diamond Platinum amesherekea siku ya Boxing Day kwa kupunga upepo baharini akiwa na mama mtoto wake, Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ pamoja na dada zake , Esma Platinum na Queen Darleen.

Vilevile meneja wa diamond Sallam na staa mkongwe AY walikuwepo kwenye boti ambayo Diamond aliltumia kumpeleka  fukwe za mbali.

Jionee Picha




Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Disemba 28, Ikiwemo ya Magufuli Kuwatesa Mawaziri

CCM Yajipanga Kurudia Uchaguzi Zanzibar.......Yawataka Wanachama Wake Kujitokeza Kwa Wingi

0
0
KAMATI Maalumu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar chini ya Mwenyekiti wake Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein imewataka wananchi na wanachama kujiweka tayari na hatimaye kujitokeza katika uchaguzi mkuu wa marudio.

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Itikadi na Uenezi Zanzibar, Waride Bakari Jabu, wananchi wametakiwa kujiandaa kwa uchaguzi wa marudio na kuachana na propaganda zinazotolewa na watu wachache kwa lengo la kupotosha ukweli.

“Kikao cha Kamati Maalumu ya CCM Zanzibar kilichokutana hapa chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar, Dk Shein kimewataka wananchi, wanachama na wafuasi wa CCM kujitayarisha kwa uchaguzi mkuu wa marudio ambao tarehe ya kufanyika kwake itatangazwa na taasisi husika,” imesema taarifa hiyo ya Waride.

Matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 25 ulifutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kwa kile alichoeleza ni kuwepo kwa ukiukwaji wa kanuni na sheria za uchaguzi huru wa kidemokrasia.

Katika kikao cha jana kilichohudhuria pia na viongozi kadhaa wa kitaifa akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kilijadili ajenda mbili ikiwemo hali ya kisiasa mara baada ya uchaguzi mkuu kwa upande wa CCM.

Katika taarifa hiyo, chama hicho kimesema kimeridhishwa na mwenendo wa hali ya kisiasa na kimewapongeza wanachama waliojitokeza kwa wingi kushiriki katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25.

Aidha chama kimepongeza na kutoa baraka kwa mazungumzo yanayoendelea ya viongozi wakuu wa kisiasa yakiwa na lengo la kuleta amani ya kudumu. Kamati ya mazungumzo ya hali ya kisiasa Zanzibar yenye lengo la kusaka amani ya kudumu iliyovurugika kutokana na kufutwa kwa uchaguzi mkuu inaundwa na viongozi wastaafu wakiwemo marais, Dk Salmin Amour, Amani Abeid Karume, Balozi Seif Ali Iddi ambaye ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Akizungumza juzi Ikulu, jijini Dar es Salaam, Rais wa Zanzibar, Dk Shein alisema mazungumzo hayo yanaendelea vizuri na taarifa kamili yatakapofikia tamati. Alipoulizwa kuhusu hatma ya CCM kama uchaguzi mkuu utarudiwa, Waride alisema chama bado kiko imara na hakijatetereka.

“Wapo wanaosema CCM imeyumba, si kweli wala CCM haijapoteza majimbo kwa sababu kura hazikumalizwa kuhesabiwa,” alisema.

I Am So Lonely.. I Need A Cute Guy That Knows Fun

0
0

Hello I am Becky by name; I relocated from Nairobi to Dar es Salaam recently but everywhere seems so boring for me, no friends to chat with, no fun, and nothing!

I'm the kind of party girl, I'm so tired of not seeing any friend or anybody to talk to here. I feel so lonely.. I'm in need of a cute looking guy, that knows how to party and catch some fun.

Please don't get it twisted I am not a sugar mummy, because I know most of you want sugar mummy.. I am just a girl who doesn't like dull moments, I might not be a sugar mummy or got so much money but one thing I can promise is you wont regret knowing me if you can keep me lively here in the city, I will satisfy you very well in bed, trust me I know the G – Spot of any guy..

Just leave your contact as a comment if you are a party guy then we connect.

Utajiri wa Madaktari wa Tiba Mbadala Kufuru...Ni Kutengeneza Utajiri Kirahisi, Lakini Kuhatarisha Maisha ya Watu

0
0
Ni kutengeneza utajiri kirahisi, lakini kuhatarisha maisha ya watu.

Madaktari waliosomea sayansi ya tiba hungaika kufanya vipimo mbalimbali kuchunguza chanzo cha ugonjwa kabla ya kutoa tiba, lakini waganga wa tiba mbadala hawahangaiki; wanachunguza kwa dakika zisizozidi mbili, kupata majibu na kutoa tiba.

waganga hao, ambao sasa wanatamba kwenye vituo mbalimbali vya redio na televisheni hasa nyakati za usiku, wanafanya uchunguzi huo kwa kutumia Kifaa kinachoitwa Quatum Magnetic Analyser, ambacho watengenezaji wake wanadai hufanya uchunguzi kwa nguvu ya sumaku, na kupata taarifa za mwili mzima ndani ya dakika moja na kutoa majibu.

Na si jambo la ajabu kwa mgonjwa, baada ya kuona maajabu ya kifaa hicho, kushawishika kulipia fedha nyingi kadri atakavyotakiwa kwa ajili ya kugharimia tiba yake hata bila ya kudadisi ufanisi wa kifaa hicho na uwezo wake wa kutoa taarifa sahihi. Wananchi sasa hawaendi tena Loliondo kunywa kikombe cha babu, bali kwenye kliniki za tiba mbadala zinazotumia kifaa hicho kufanya uchunguzi.

Na kutokana na ukubwa wa matatizo ya hedhi na ugumba kwa wanawake na kuishiwa nguvu za kiume kwa wanaume, waganga hao wamekuwa wakieleza jinsi dawa zao zinavyoweza kumaliza matatizo yao kwa kutumia tiba mbadala na kupata wateja kila kukicha.

Na kwa kuwa wengi sasa wanamiminika kwenye kliniki hizo na kulipia kuanzia Sh320,000 kwa tiba ndogo hadi Sh700,000 kwa mkupuo, waganga wa tiba mbadala sasa wamekuwa na utajiri wa ajabu, mwandishi wa gazeti la The Citizen anaandika.

Mashine hiyo, ambayo inatengenezwa China na Korea Kusini, imekuwa ikitumiwa na waganga hao ili kubaini ugonjwa kabla ya kumuandikia dawa za asili ambazo watatakiwa watumie kutibu tatizo lao.

Kwa dakika chache ambazo mgonjwa atakuwa ameshikilia kidude mfano wa mpini wa kisu kilicho na waya uliounganishwa kwenye mashine hiyo sambamba na kompyuta, watengenezaji wanasema muda huo hutosha kukiwezesha kifaa hicho kukusanya taarifa nyingi za mwili na kutoa matokeo ambayo hutumiwa na waganga hao kutoa tiba.

Hata hivyo, licha ya matumizi yake yenye ukakasi wa kuaminika kwa matokeo ya uchunguzi wake, bado hakuna ushahidi wa kitaalamu uliothibitisha ufanisi wa mashine hiyo.

Kutokana na hilo na hatua ya Serikali kuvalia njuga suala la waganga hao na tiba wanazotoa, mwandishi wa The Citizen, ambalo ni gazeti dada la Mwananchi, alihudhuria kliniki zinatozotoa huduma hizo ili kuchunguza tiba hiyo na jinsi Quatum Magnetic Analyser inavyofanya kazi.

Katika uchunguzi wake mwandishi huyo alithibitisha matumizi ya mashine hiyo ambayo pia matumizi yake yalishatiliwa shaka na Baraza la Utoaji wa Tiba Mbadala la Tanzania (AHPCT) na kuagiza uchunguzi wa haraka ufanywe.

Mwandishi huyo alibaini kuwa mashine hiyo imekuwa ikutumiwa na madaktari hao kama kivutio cha soko lao kwa kuwaaminisha wagonjwa kuwa ina uwezo wa kuchunguza mwili mzima wa binadamu bila ya kumtoboa au kuchukua sampuli za damu au mkojo na kubaini sehemu yenye tatizo.

Mmoja wa wakazi wa jijini aliyewahi kwenda kwenye moja ya kliniki hizo, Jerome Sungura alisema alimpeleka mchumba wake baada ya kusumbuliwa kwa muda na maumivu makali ya tumbo.

Sungura, ambaye ni mkazi wa Mwenge, aliiambia The Citizen kuwa daktari aliyekuwapo siku hiyo aliwaambia ni lazima mchumba wake achunguzwe kwa kutumia mashine hiyo.

Kwa kuwa jina la mashine hiyo lilikuwa geni kwake, Sungura alimhoji jinsi mashine itakavyotumika kumchunguza mchumba wake.

Daktari alimuambia ingesaidia kuchunguza mwili mzima na kubaini tatizo liliko, kama ni kwenye ini, ubongo au mfumo wake wa uzazi.

Mganga huyo alimuambiwa Sungura kwamba mashine hiyo inatumika kwa siri kwa sababu haikuwa na kibali cha kutumika, hivyo Serikali ikifahamu itakuwa shida.

Baada ya maelezo hayo, Sungura aliridhia mchumba wake kupimwa na majibu kutoka baada ya dakika moja, yakieleza alibainika kuwa na ukosefu wa vitamin E na kutokuwa na usawa wa homoni mwilini (hormonal imbalance).

Hapo ndipo wawili hao walipotilia shaka mashine hiyo.

Hali kama hiyo ilimkuta Allan Semzaba ambaye gazeti la The Citizen lilimchukua ajifanye mgonjwa kwenye kliniki hiyo ikiwa ni sehemu ya uchunguzi huu.

Semzaba, ambaye ni baba wa watoto wawili, alifika kwenye kliniki hiyo na kumueleza mganga kuwa yeye ni tasa.

Semzaba alitakiwa kutoa Sh40,000 kwa ajili ya kugharimia kipimo na ada ya kuonana na daktari.

Baada ya vipimo daktari huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la David, alimuambia Semzaba kuwa majibu yanaonyesha kuwa hana uwezo wa kupata mtoto.

Hivyo,i alimshauri atumie dawa za asili zenye thamani ya Sh 320,000 ambazo angempa akatumie kwa miezi mitatu na baada ya hapo tatizo la utasa lingeisha.

Hapo ndipo gazeti hili lilibaini kuwa mashine hizo hutumika kujipatia fedha si kusaidia wagonjwa.

Mapema mwaka huu Serikali mjini Dodoma iliwashikilia raia wawili wa Korea na kuwatoza faini ya Sh 500,000 kwa kutaka kutoa rushwa ili kliniki yao iliyokuwa inatoa huduma chini ya viwango isifungwe.

Licha ya juhudi za raia hao kugonga mwamba, Mwenyekiti wa AHPCT, Dk Edmund Kayombo alisema kushamiri kwa biashara hizo kunatokana na kutawala kwa vitendo vya rushwa katika uendeshaji wa kliniki hizo. Dk Kayombo alisema jambo hilo limekuwa kikwanzo kwa mamlaka husika kuchukua hatua stahiki dhidi ya wahusika ambao ni wamiliki wa kliniki mashuhuri nchini.

“Tunafahamu kwamba baadhi ya wamiliki wa kliniki hizo wamekuwa wakiingiza na kutumia mashine ambazo tumekuwa tukizitilia shaka,” alisema Dk Kayombo kwenye mahojiano na The Citizen.

Pia alisema anafahamu kwamba matumizi ya mashine hizo yamekuwa yakiendelea kwa muda sasa.

“Tutafuatilia kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) ili wachunguze kama mashine hizo zimesajiliwa na uhalali wa matumizi yake kwa sababu sisi tulifanya uchunguzi wetu tukabaini kwamba mashine hizo hazina msaada wowote kwa mgonjwa,” alisema Dk Kayombo.

Akizungumzia kuhusu tiba hizo, mtaalamu wa tiba asilia kutoka Hopitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Rogassian Mahunnah alitoa mfano wa tiba kwa mtu ambaye ni tasa akisema si rahisi kwa daktari wa tiba hizo kutibu ugonjwa huo kwa kutumia dawa hizo.

Alisema jambo hilo ni pana na kwamba dawa za asili zimethibitika kutibu magonjwa kama malaria na maumivu ya kawaida ya tumbo.


David Kafulila Aituhumu Tume ya Uchaguzi Kumchezea Rafu Kuhakikisha Anashindwa Uchaguzi....

0
0
Aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ameituhumu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kushirikiana na mtu aliyemwita kigogo kucheza mchezo wa kuhakikisha anashindwa katika kesi aliyofungua Mahakama Kuu kuiomba itengue ushindi wa Hasna Mwilima (CCM), na kumtangaza kada huyo wa NCCR-Mageuzi kuwa mbunge.

Matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa jimbo hilo yalikwama kutangazwa kwa siku kadhaa kutokana na kutokea mabishano kati ya Kafulila aliyekataa kura kuhesabiwa upya kwa madai kuwa maboksi yalilala polisi bila ya usimamizi, na Mwilima.

Baada ya mvutano huo, msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea huyo wa CCM kuwa mshindi kwa kupata kura 34,453, matokeo ambayo Kafulila, aliyetangazwa kupata kura 33,382, anayapinga mahakamani.

Jana, Kafulila amesema NEC inatupiana mpira kuhusu ombi lake la fomu za matokeo ya vituo vyote 382 vya kupigia kura vilivyopo katika jimbo hilo lenye kata 16 ili azitumie kama ushahidi mahakamani.

Kafulila, ambaye alijipatia umaarufu baada ya kuibua kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, alisema kwa nyakati tofauti ametoa malalamiko yake kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ramadhani Kailima na aliyekuwa msimamizi msaidizi wa uchaguzi katika jimbo hilo, Andrea Majaliwa lakini hajafanikiwa kupata chochote.

Kafulila alisema katika kesi hiyo anaitaka mahakama ifanye majumuisho na kumtangaza mshindi kwa madai kuwa fomu namba 21B za matokeo ya vituo vyote, zinaonyesha amepata kura 34,212 dhidi ya kura 33,390 za Mwilima.

Anavyozungushwa

Alisema Novemba 12, alimuandikia barua msimamizi wa uchaguzi wa jimbo, akitaka kupatiwa fomu ya majumuisho ya kura na kujibiwa kuwa tayari ilikuwa imetumwa makao makuu ya NEC jijini Dar es Salaam.

Alisema siku moja baadaye alimuandikia barua Kailima kuomba apatiwe fomu hizo kwa kuwa alijibiwa kuwa zimetumwa makao makuu ya tume hiyo.

“Zilipita siku 10 bila majibu. Novemba 24 nilionana na Kailima na alipewa maelekezo na (Jaji Damian Lubuva-Mwenyekiti Nec). Kailima alimpigia simu msimamizi msaidizi wa jimbo na kumtaka anipe fomu hizo kupitia kwa msaidizi wangu,” alisema Kafulila.

Alisema licha ya agizo hilo la Jaji Lubuva, mpaka sasa bado hajapewa fomu hizo na Mfune ambaye baada ya kuhamishwa halmashauri mpya, nafasi yake ilikaimiwa na Daniel Kamwela.

“Majaliwa yeye alishiriki mchakato mzima wa uchaguzi na Kamwela alikuwa mgeni tu pale. Nakumbuka Majaliwa alinijibu kuwa amepewa maelezo na Kailima ili anipatie zile fomu.”

“Alinieleza kuwa angenipatia baada ya siku tatu, majibu ambayo pia niliyapata kutoka kwa Kailima. Ilinishangaza, iweje waandae fomu wakati fomu hizo si za kuandaliwa na zipo tayari maana uchaguzi ushafanyika?” alihoji.

Alisema siku hizo zimepita na kila akikumbusha suala hilo kwa barua, hakuna majibu yoyote anayopewa na kudai kuwa kuna agizo limetolewa kwamba asipatiwe fomu za matokeo.

“Hivi sasa hata mikutano ya kushukuru wananchi nimezuiwa kufanya katika jimbo la Kigoma Kusini na hawataki kutoa fomu hizo kwa sababu wanajua kuwa matokeo yaliyotangazwa si sahihi,” alisema.

Alisema kuna “mchezo” umechezwa kuhakikisha anakwamishwa huku akitolea mfano kuhamishwa kwa Mfune, NEC kumzungusha na kupuuzwa kwa agizo la Kailima.

“Kinachonishangaza ni nguvu ya ushirikiano kupungua kutoka NEC. Kwa sasa hawataki kunisaidia na hawana ushirikiano kabisa,” alisema.


Kauli ya Nec

Akizungumzia suala hilo, Kailima alisema: “Kila mgombea au chama kiliweka wakala katika vituo vya kupigia kura, kuhesabia kura ambapo wakala au mgombea atapewa fomu namba 21B na katika kituo cha kujumlishia kura watapewa fomu namba 24B.

“Fomu hizo zina matokeo ya kila kituo na katika kituo cha kujumlisha kura zote. Mawakala wake (wa Kafulila) walipewa sasa anataka tumpe zipi? Kama amefungua kesi yeye awasilishe malalamiko yake na msimamizi atawasilisha huo ushahidi wake.”

Kailima alisema msimamizi wa uchaguzi hawezi kumpa ushahidi mlalamikaji na kama akifanya hivyo atakosa cha kuwasilisha mahakamani.

“Kama hakuweka mawakala siyo jukumu la NEC, lilikuwa jukumu lake yeye na chama chake,” alisema.

Kailima alisema suala hilo linaweza kufafanuliwa kwa kina na msimamizi wa uchaguzi aliyekuwepo katika uchaguzi huo, utangazaji wa matokeo.

Gazeti hili lilipowasiliana na Majaliwa hakukubali wala kukataa kuhusu suala hilo, akidai kuwa yeye si mhusika.


Diamond Amwaga Machozi Ukumbini....Kisa Kizima Hichi Hapa

0
0
Mbongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, amejikuta akiangua kilio kama mtoto mdogo na kuwashangaza watu kufuatia mashabiki wake kumtaka awaimbie ‘akapela’ ya wimbo wake mpya wa Utanipenda.

Tukio hilo ambao bado limo midomoni mwa mashabiki wake, lilijiri usiku wa kuamkia Boxing Day (Desemba 26, 2015) ndani ya ‘Uwanja wa Taifa wa Burudani’ Dar Live jijini Dar ambapo nyota huyo alikuwa akikamua jukwaani na shoo ya nguvu iliyopewa jina la Funga Mwaka Concert.

Dakika chache kabla Diamond hajamwaga chozi, mashabiki wake walimuomba aimbe ‘akapela’ ya wimbo huo mpya.

Wakati akiimba akapela hiyo, mashabiki wake, bila kificho, walimwambia anajitabiria ‘kufulia’ kwani wimbo huo una kila alama za yeye kumaliza gemu la Bongo Fleva vibaya.

Hata hivyo, licha ya mashabiki kumpasulia hivyo, baadhi yao walianza kulia wakionekana kuguswa na mashairi ya wimbo huo hali iliyosababisha Diamond naye aanze kulia na kushindwa kuendelea kuuimba wimbo huo.

Kufuatia hali hiyo, dada yake kwa upande wa baba yake, Abdul Jumaa, Mwanahawa Abdul ‘Queen Darleen’ alimfuata jukwaani na kumtoa huku akimfunika na kitambaa cha bendera ya taifa ambacho pia dada huyo alikitumia kumfutia machozi kaka yake huyo.

Diamond alipelekwa nyuma ya jukwaa ambako ukiachia mbali yeye Queen Darleen, meneja wake, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ naye alitumia nguvu ya ziada kumbembeleza staa huyo huku akimwambia anawapa wasiwasi mashabiki wake. Kwa hiyo anyamaze.

Licha ya Babu Tale kutumia hekima ya kibabubabu, bado Diamond aliendelea kulia, safari hii kwa uchungu zaidi na kujiinamia huku akikataa kutulizwa wala kuambiwa maneno yoyote yanayoonekana ‘kama’ yana busara ndani yake.

Huna sababu ya kuendelea kulia ndugu yangu kwani kufulia au kuendelea kuwa na mali ni neema na msimamo wa Mungu. Hakuna binadamu anayeweza kumshusha mwenzake kama Mungu hajapanga kuwa hivyo,” alisema Babu Tale lakini Diamond hakumsikiliza.

Diamond alinyamaza mwenyewe baadaye kufuatia mawasiliano ndani ya ubongo wake kumwambia ‘umelia sana kijana, imetosha sasa’!

Kilio hicho, kilimaliza shoo hiyo kwani Diamond hakurudi tena jukwaani baada ya kukamua nyimbo zake kibao na kuwafanya mashabiki wake kuiweka siku hiyo katika kumbukumbu.

Zaidi ya Watu 1500 Wajitangaza Kuwa MASHOGA Mkoani Iringa

0
0
Kukithiri  kwa biashara haramu ya ngono pamoja na tabia ya ushoga mkoani Iringa kunadaiwa kusababishwa na baadhi ya vijana wa vyuo vikuu waonafika mkoani humo kwa ajili ya masomo ya elimu ya juu, huku miongoni mwao wakitaka starehe zilizo nje ya uwezo wao.

Tamaa ya kumiliki vitu vya thamani – ni miongoni mwa mambo yanayotajwa  kuwahadaa baadhi ya wasomi hao wa vyuo vikuu, jambo linalosababisha wengi wao kuangukia katika wimbi la biashara ya ngono na ushoga na kuufanya  ongezeko la maambukzi ya vvu.

Kwa mkoa wa iringa inadaiwa kuwa zaidi ya mashoga 1500 wamejitangaza wenyewe kuendesha  biashara haramu ya ngono, jambo ambalo kiafya linadaiwa kuwa ni hatari  kwa maambukizi ya virus vya ukimwi.

Baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu  mkoani iringa ndiyo wanaonyooshewa kidole kuhusika na biashara hiyo ya ngono na tabia ya ushoga- ambapo shirika la restless development linalojihusisha na masuala ya afya ya uzazi na makuzi kwa vijana- kupitia mradi wa dance for life- limewakutanisha viongozi hawa wa serikali ya wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani iringa- ili  kujadili namna ya kujinasua katika wimbi hilo la ushoga na biashara haramu ya ngono.

Serikali inaona  tatizo hilo la ushoga na biashara ya ngono litamalizwa na jamii yenyewe, endapo tu wazazi na  walezi watakemea mapema mienendo hatarishi ya vijana wao.

Ushoga ni tabia inayofanywa na baadhi ya wanaume, kwa  kujihusisha kimapenzi na wanaume wenzao, suala  ambalo kwa kiwango kikubwa linatajwa kuchochewa na mambo ya utandawazi, ambao unaibua mitindo mbalimbali na tabia mpya kila uchwao.

Chanzo :Star tv

Waziri Nape Akanusha Wizara Yake Kukataza Wanawake Kuvaa Mavazi ya Kubana

0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni Wasanii na Michezo Nape Nnauye, amekanusha taarifa iliyosambaa mitandaoni inayohusu wizara yake kukataza baadhi ya mavazi hasa sehemu za mikusanyiko ya umma.

Amesema Taarifa hizo ni za uzushi na uongo, na kuwataka mamlaka husika kuwachukulia hatua watu waliotoa taarifa za uongo.

Hizo taarifa ni uzushi mtupu na uongo, mamlaka husika wachukue hatua, watimize wajibu wao, watumie sheria iliyopo kuwachukulia hatua”, amesema Mh. Nape Nnauye.

Mwishoni mwa wiki hii kuna taarifa ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikionyesha ni taarifa kwa vyombo habari juu ya katazo la mavazi yasiyofaa kwenye mikusanyiko ya watu, hususan hospitali, maofisini, sokoni, na vyuoni.

Dr. Mwakyembe Kuendelea na Ubunge wake. Rufaa Dhidi Yake Yatupwa

0
0
Rufaa ya kutengua ubunge wa mh. Mwakyembe imetupiliwa mbali baada ya mgombea wa CHADEMA jimbo la Kyela kushindwa kulipa tshs. MILIONI 3 tu, hiyo ndiyo habari kuu mjini Mbeya.

Poleni sana mlioguswa na habari hii, hongera sana mh. Mwakyembe

Zanzibar: Dr. Shein yuko Tayari kwa Lolote; Maalim Seif Anataka Moja tu

0
0
Alipokuwa akizungumzia kufutwa kwa uchaguzi mzima wa Zanzibar, aliyekuwa mgombea wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad alisema safari hii 'No compromise'. Ingawa ni sentensi fupi, ina ujumbe mzito. Ujumbe wa Maalim Seif ni kuwa safari hii hatakubali kuombwa na hatimaye kukubali matokeo kama ilivyokuwa miaka ya 2005 na 2010. Kauli ya kuwepo kwa 'compromise' inathibitisha kauli ya Mzee Moyo aliyosema kuwa ilifika wakati aliombwa akamshawishi Maalim Seif akubali matokeo.

Maalim Seif ametuma ujumbe mmoja mkubwa. Ujumbe wa kutotakiwa tena mashauriano ya kumfanya abadili msimamo wake wa kutangazwa mshindoi wa uchaguzi wa mwaka huu ambao umefutwa na Mwenyrkiti wa ZEC, Ndugu Jecha. Maalim Seif, pamoja na kufanya mazungumzo ya hapa na pale; ya huyu na yule, anataka jambo moja tu: mshindi atangazwe na mambo mengine yaendelee.

Wakati Maalim Seif akisema na kubaki na msimamo huo, Dr. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na aliyekuwa mgombea wa CCM, yuko tayari kwa jambo lolote. Yuko tayari kutangazwa kwa mshindi; yuko tayari kurudiwa kwa uchaguzi na kadhalika. Msimamo huo unachagizwa na heshima ya Dr. Shein katika kufuata na kutii makubaliano ya Muafaka uliopelekea kuundwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Pia, 'upemba' wa Dr. Shein na Maalim Seif unakoleza msimamo wa lolote-lije wa Dr. Shein. Dr. Shein anamuona Maalim kama ndugu na Mwalimu wake wa kisiasa na hata kaka wa kisiasa. Lakini, external forces from party members and party leaders make things harder for Dr. Shein. He is afraid of being named a party traitor!

Source: Jamii Forums/Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Sentensi za Wema Sepetu kwa Mashabiki baada ya Kuimba Wimbo wa Diamond Platnumz…

0
0
Dec 27 mashabiki wa Diamond Platnumz walipost video ya msanii wa Bongo Movies, Wema Sepetu katika mtandao wa instagam ambayo ikionesha akiimba wimbo wa Diamond uitwao ‘Utanipenda’.

Baada ya kusambaa kwa video hiyo yenye dakika 15 Wema akuchukua muda kuwajibu mashabiki hao na kuandika’Mwenzangu niache na kisauti changu ila swali la kizushi kwa hao wanaojiita NAT Team Wema mnanipa tabu sana kwahiyo nikiimba nyimbo ya Diamond kaninyoosha nikimpost nimemmiss au mara kanimwaga?, oooh mara hanitaki..mara nimefulia kiukweli maisha mnayonifanya niishi maisha magumu sana Diamond and I are over..We have over karibu mwaka na sasa kila mtu ka move on na sinaga tabia za kiswahili mtoto wa watu basi hata nyimbo nisisikilize‘..Wema Sepetu



Pamoja Kuwa na Kashfa ya Escrow Huyu Ndio Waziri Anayefanya Kazi Kuliko Mawaziri Wote wa John Pombe Magufuli....

0
0
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto mbele) akimsikiliza Mhandisi wa kituo cha kufua umeme wa dharura cha Kibeta- Bukoba mjini, Mhandisi Filbert Mlaki wakati wa ziara yake kituoni hapo leo (27 Desemba, 2015). Kituo hicho chenye mitambo minne kinao uwezo wa kuzalisha megawati 2.1 ambacho hutumiwa pale umeme wa kutoka Uganda unapokatika.

Serikali imesema ifikapo mwaka 2018 Mfumo wa umeme katika Mkoa wa Kagera utakua umeingizwa kwenye Gridi ya Taifa.
Hayo yalisemwa jana tarehe 27 Desemba na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipofanya ziara mjini Bukoba, Mkoani Kagera ili kukagua miundombinu ya umeme.
Ilielezwa kwamba Mkoa huo kwa sasa unapata umeme kutoka nchini Uganda ambao umekuwa ukikatika mara kwa mara na hivyo kulilazimu Shirika la TANESCO kutumia mitambo yake inayotumia mafuta ambayo hata hivyo haikidhi mahitaji ya umeme ya Mkoa.
Profesa Muhongo aliliagiza shirika hilo kuhakikisha linaharakisha taratibu za kuunganisha mkoa wa Kagera kwenye umeme wa Gridi ya Taifa.
"TANESCO ni lazima muharakishe mipango ya kuunganisha mkoa huu kwenye gridi ya taifa ili kuwapatia wananchi huduma ya umeme wa uhakika," aliagiza.

Aidha, Profesa Muhongo aliiagiza TANESCO kuhakikisha mafuta kwa ajili ya kuendeshea mitambo hiyo yanakuwepo yakutosha kwa muda wote.
Alisema ifikapo mwaka 2025, Tanzania itaingia kwenye uchumi wa kati ambao utatokana na uwekezaji mkubwa kwenye viwanda ambavyo vitahitaji umeme wa kutosha na uhakika.

Mbali na hilo, Profesa Muhongo aliliagiza Shirika la Tanesco mara baada ya mkataba uliopo wa kuuziana umeme kati ya Tanzania na Uganda kuisha, wahakikishe wanaingia mkataba wa muda mfupi mfupi lengo likiwa ni kuepusha kuwa ndani ya mkataba wakati tayari mkoa huo utakua kwenye gridi ya taifa.
Akielezea hali ya umeme mkoani humo, Meneja wa Tanesco Kanda ya Ziwa, Mhandisi Amos Maganga alisema kwa sasa Tanzania inanunua umeme kwa gharama ya senti za Marekani 8.4 kwa kila unit.

Alisema Tanzania inao mkataba wa kununua umeme kutoka Uganda kiasi cha megawati 10 ambao unahudumia wilaya za Bukoba Mjini na Vijijini, Karagwe, Muleba na Misenyi.(P.T)

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kushoto) akimsikiliza Mhandisi Filbert Mlaki.

Waziri wa nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akikagua moja ya mtambo wa kuzalisha umeme wa Kituo cha Kibeta

Moja ya mtambo wa kuzalisha umeme katika kituo cha kufua umeme wa dharura cha Kibeta- Bukoba Mjini.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kagera, John Mongella kabla ya kuanza ziara ya kukagua miundombinu ya umeme mkoani humo.

Money Can Buy Everything! ZARI Flaunts Her Car Park Full of Expensive Cars (PHOTOs)

0
0
Diamond’s lover, Zari Hassan, is among the East African female celebrities who are eating life with a big spoon and living the life that many people dream of.

Money to her is not a problem and she can afford all the finer things in life thanks to her fat wallet.

Just to prove her worth, Zari flaunted her parking lot that is full of expensive guzzlers which most of you only see in high budget music videos.


Check out the photos below and see how Zari rolls.








Beef Jipya....Mr Blue Aibuka na Kudai Mwanamuziki Diamond Amemuibia Jina la Simba Analotumia Kwa Sasa

0
0
Mr Blue anadai chake.. kwa mujibu wa Kabayser, jina ‘Simba’ analotumia Diamond sasa kwenye post zake kwenye mitandao ya kijamii alilianzisha yeye wiki kadhaa zililopita baada ya kupewa na mashabiki wake.

Naikumbuka hii post niliipost miezi saba iliyopita pale watu waliponiita jina la simba…ila inanishangaza kuona baada ya muda watu wengi wakijiita jina hili …hiii inanionesha kuwa mi ni mbunifu wa hali ya juu..na watu husubiri mimi nifanye ili waige….#mfanowakuigwa$,” Blue ameandika kwenye Instagram.

Cha kufurahisha zaidi mashabiki wanadai picha aliyopost Blue haikuwa ya Simba bali ni Tiger!!

Unayaonaje madai ya Blue?
Viewing all 104417 articles
Browse latest View live




Latest Images