Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Tarehe 31 Disemba, Ikiwemo ya Ray C Kurudia Unga...

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Tarehe 31 Disemba, Ikiwemo ya Ray C Kurudia Unga...


Kubenea Akana Kumtukana Dc Makonda

$
0
0
Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (44) amekana kumtukana Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda tarehe 14 Desemba 2015 walipokutana katika Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd. kilichopo eneo la External Mabibo kwa madhumuni ya kutatua mgogoro kati ya wafanyakazi na uongozi wa kiwanda hicho

Katika kesi inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Wakili wa Serikali mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa alimsomea mshtakiwa maelezo ya kesi hiyo ambapo baadhi  ya mashtakiwa aliyakana.

Akisomewa maelezo ya kesi, Saed Kubenea alikiri kuwa ni mbunge wa Ubungo na pia alikiri kuwa anamfahamu mlalamikaji katika kesi hiyo kuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Makonda na kwamba ni kweli kuwa tarehe 14 Desemba 2015 alifika katika Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd kulikokuwa na mgomo wa wafanyakazi.

Hata hivyo, alipoelezwa kuwa anashtakiwa kwa kosa la kumtolea lugha chafu Makonda ambapo alimwita kuwa ni kibaka, mpumbavu, mjinga na cheo chake ni cha kupewa kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani na utulivu; Saed Kubenea alikana.

Kufuatia Kubenea kukana mashitaka yanayomkabili, Hakimu mkazi mkuu wa mahakama hiyo , Thomas Simba alisema mashahidi sita wa upande wa mashtaka wataanza kutoa ushahidi wao Januari 20 na 21, 2016 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Nafasi za Kazi

Lipumba Amtwika Zigo Dr Shein Mgogoro Zanzibar....Asema Mgogoro Utakwisha Iwapo Dr Shein Atakubali ZEC Iendelee Kutangaza Matokeo

$
0
0
Mwenyekiti wa zamani wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ndiye mtu pekee mwenye uwezo wa kumaliza mgogoro wa Zanzibar.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Profesa Lipumba alisema mgogoro wa Zanzibar utamalizwa kwa Dk Shein kuiruhusu Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar (ZEC) kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.

Alisema pamoja na mazungumzo yanayoendelea kati ya CUF na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk Shein ndiye mwenye uwezo kuumaliza mgogoro huo.

Mazungumzo yanaendelea na hatujui yatafika mwisho lini, lakini Dk Shein ndiye anayeweza kuifanya Zanzibar iwe na amani au vurugu, ninashauri aruhusu kutangazwa kwa matokeo,” alisema.

Alisema amani na utulivu uliopo Zanzibar wakati wananchi wakisubiri hatima ya mgogoro huo, haiwezi kuwa ya kudumu kwani ikiamuliwa uchaguzi urudiwe wapo ambao hawatakubali.

Profesa Lipumba alisema uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa huru na haki na hata watazamaji wa kimataifa kutoka nchi mbalimbali walishangaa matokeo yake kufutwa.

Alisema wananchi wa Zanzibar walishapiga kura na kwamba wanachosubiri ni matokeo vinginevyo haki yao ya kidemokrasia itakuwa imechezewa.

Oktoba 28 mwaka huu, Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alifuta uchaguzi huo kwa kile alichosema kulikuwa na kasoro ndani ya tume yenyewe na kwenye vituo vya kupigia kura.

Profesa Lipumba alisema mgogoro huo ukiendelea, utakwamisha msaada wa Dola za Marekani 472.8 milioni uliokuwa utolewe na Shirika la Maendeleo ya Milenia (MCC) la Marekani.

Alisema Bodi ya MCC ilikutana Desemba 16 na kushindwa kupitisha msaada huo kwa Tanzania huku hoja kubwa ikiwa kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu Zanzibar.

Alisema miongoni mwa matumizi ya msaada huo ilikuwa kuunganisha wateja wapya 300,000 kupata umeme.

Hapa tunategemea busara za Dk Shein kuumaliza mgogoro ili tupate msaada huo wenye masilahi ya Taifa au kuendelea na mgogoro na kuukosa msaada huo,” alisema.

Akizungumzia suala hilo, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Magdalena Sakaya alisema huu ni muda mwafaka kwa Dk Shein kuweka masilahi ya Wazanzibari mbele.

Alisema atawekwa kwenye vitabu vya historia kama atafanya uamuzi wa kuruhusu kutangazwa kwa matokeo hata kama viongozi wenzake wa CCM hawatapenda uamuzi huo.

Lakini vurugu zikitokea, Shein atalaumiwa jumuiya za kimataifa yeye mwenyewe na atashangaa viongozi wenzake wa CCM watakapojiweka pembeni,” alisema.

Nafasi za Kazi
Bonyeza www.ajirayako.com

Kufakamia Pombe Kwamponza Baby Madaha...Aanguka Chooni na Kuvunjika Mguu....

$
0
0
MSANII wa filamu na Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha hivi karibuni alipata majanga baada ya kuanguka chooni na kuvunjika mguu wa kulia, Amani lina taarifa zote.

Tukio hilo lilitokea nyumbani kwake, Kijitonyama jijini Dar ambapo staa huyo alitoka kwenye matembezi yake usiku wa manane akiwa amepiga ‘mtungi’ wa kutosha.

Inadaiwa kuwa, alipofika kwake alihitaji kwenda bafuni kuoga. Hata hivyo, alianzia chooni kwanza na kutokana na miguu kukosa stamina kwa ‘ulabu’, alijikuta akiteleza na kudondoka chini kisha kuvunjika mguu huo.

Muonekano wa mguu huo uliovunjika.
Amani lilimsaka msnaii huyo ili kuzungumza naye kuhusu madai hayo ambapo alikiri kupata majanga.Baby Madaha alisema msala huo ulimfika majira ya saa 10 alfajiri (siku hakumbuki) akitoka kwenye kujirusha ambapo siku hiyo pombe zilimkoma kwa kufakamia kila aina.

Naamini kufakamia kwangu pombe nyingi ndiyo kuliniponza. Sijawahi kupata maumivu makali kama haya maana baada ya kudondoka chini nilijisikia sina nguvu wala sikuweza kusimama, nikalazimika kuukanyagia mguu wangu.

Ilipofika asubuhi nilijikaza kwenda Hospitali ya AAR iliyopo Kijitonyama (Dar) ambapo walinipiga X-Ray na kungundulika kuwa, mguu wa kulia ulivunjika, hivyo nikafungwa mhogo (P.O.P),” alisema Madaha.

Alisema kwa sasa (Jumanne iliyopita), anaendelea vizuri sana na anawashukuru madaktari wa AAR kwani awali yeye alijua mguu huo aliteguka tu na ungetengemaa muda wowote.

Da! Lakini yote maisha, leo tambarare, kesho mlima. Binadamu huwezi kuishi katika tambarare siku zote wala mlima siku zote. Najua hili hogo litatoka, nitadunda kama kawa,” alisema mrembo huyo.

Source:Global Publishers

Msanii Tekno Miles Kunogesha Tamasha JOHNNIE WALKER “Grown & Sexy The Gold Finale”

$
0
0

Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija (wa kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kumtambulisha rasmi Msanii Tekno Miles (Katikati) ambaye anatarajiwa kuporomosha burudani ya nguvu kwenye Tamasha la mwisho la “Grown and Sexy, the Gold finale” litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga karibu na Best Bite katika mkesha wa mwaka mpya. (wa pili kushoto) ni Dj rasmi wa Jay Z “Young Guru” toka Marekani na (wanne kulia) ni Mkurugenzi wa Straight up vibes Omary Abood.


Mkurugenzi wa Straight up Vibes Omary Abood (wa kwanza kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam ya kumtambulisha rasmi Msanii Tekno Miles (Katikati) ambaye anatarajiwa kuburudisha katika Tamasha la mwisho la “Grown and Sexy, the Gold finale” litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga karibu na Best Bite katika mkesha wa mwaka mpya.


Msanii Tekno Miles (wa kwanza kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla iliyomtambulisha rasmi kwa waandishi wa habari iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Msanii huyo anatarajiwa kuburudisha katika Tamasha la mwisho la “Grown and Sexy, the Gold finale” litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga karibu na Best Bite katika mkesha wa mwaka mpya ambapo pia atafunga rasmi mfululizo wa matamasha hayo ya Grown And Sexy tokea kuanzishwa kwake.


Meneja Chapa (pombe kali) wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Shomari Shija (Kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Msanii Tekno Miles (wa kwanza kushoto) na Dj rasmi wa msanii Jay Z wa Marekani al maarufu kama “Young Guru” wakati wa hafla iliyomtambulisha Msanii Tekno Miles kwa waandishi wa habari iliyofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam. Msanii huyo anatarajiwa kuburudisha katika Tamasha la mwisho la “Grown and Sexy, the Gold finale” litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga karibu na Best Bite katika mkesha wa mwaka mpya ambapo pia atafunga rasmi mfululizo wa matamasha hayo ya Grown And Sexy tokea kuanzishwa kwake.

Maandalizi ya Tamasha maarufu la Johnnie Walker “Grown and Sexy The Gold finale”  kwa ajili ya kuuaga mwaka na kuukaribisha mwaka mpya yanaendelea vizuri ambapo kwa mujibu wa waandaaji wa Tamasha hilo, “Capital events” kupitia wadhamini wao “Johnnie Walker” chapa maarufu ya pombe kali inayosambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti wamemleta Msanii Tekno Miles kutoka Nigeria kutumbuiza laivu katika Tamasha hilo ambalo litakua la mwisho kabisa katika historia ya matamasha ya Grown and Sexy nchini Tanzania.
Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam,Meneja chapa wa pombe kali SBL Shomari Shija alisema, “Tumeamua kulidhamini Tamasha hili kama njia mojawapo ya kujumuika na kufurahi kwa pamoja na wateja wetu wa chapa za Johnnie Walker katika kuuaga rasmi mwaka huu wa 2015.
Bw. Shija aliongeza kuwa katika Tamasha la mwaka huu ambalo ni la mwisho katika historia ya mfululizo wa matamasha ya Grown and Sexy waliona ni vema kumleta msanii maarufu toka Nigeria “Tekno Miles” ambaye aliwasili jana usiku mida ya saa nane akitokea Nigeria tayari kwa kulipamba Tamasha hilo. Msanii huyo ambaye anatamba na vibao mbalimbali kwenye anga ya muziki hivi sasa kama Shoki, Duro na Wash atatumbuiza laivu kwenye Tamasha hilo ambalo litafanyika siku ya mkesha wa mwaka mpya katika ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga, Msasani karibu na Best Bite.
Sambamba na uwepo wa msanii huyo wengine wataopamba Tamasha hilo ni Dj Maarufu “Young Guru” ambaye ni Dj rasmi wa msanii Jay Z toka Marekani ambaye ataisimamia shoo hiyo vilivyo pamoja na malkia wa uswazi mwanadada “Shaa” kisura wa Tamasha hilo ambaye atasherehesha shughuli nzima katika usiku wa tukio.

Kwa upande wake Msanii Tekno alisema anafurahia kusherekea mkesha wa mwaka mpya akiwa Tanzania na kuahidi kuporomosha burudani ya nguvu kwa mashabiki wake watakaojitokeza kushuhudia Tamasha hilo la kufunga mwaka.

Naye Mwakilishi wa Capital events waandaaji wa Tamasha hilo Bw. Justin Massawe alisema “Tunawakaribisha wapenzi wote wa burudani na chapa ya Johnnie Walker kujitokeza kwa wingi kushuhudia Tamasha letu la mwisho la Grown & Sexy na kuahidi kuwa litakuwa la kufana zaidi kwani wamejipanga kutoa burudani ya nguvu na kuwafurahisha mashabiki mbalimbali.
“Ningependa kuwashukuru wadhamini wetu mbalimbali katika kipindi chote cha mfululizo wa matamasha haya tokea yalipoanzishwa rasmi kwa ushirikiano mzuri ambao wametupatia hadi hii leo tunapofunga rasmi tamasha hili la mwisho la Grown and Sexy the Gold finale.”
Bw. Justin hakusita pia kuwashukuru Johnnie Walker kwa kuhakikisha wanakamilisha mikataba yote ya kumleta msanii Tekno Miles pamoja na Dj Young Guru hapa nchini na kwa kuhakikisha kwamba tamasha la mwisho linakamilika kwa mafanikio” makubwa zaidi.
***MWISHO***

Jeshi La Polisi Lawatahadharisha Wananchi Kuhusu Mkesha Wa Mwaka Mpya.

$
0
0
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
KUHUSU TAHADHARI KATIKA MKESHA WA MWAKA MPYA   

Tunapoelekea kumaliza mwaka 2015 na kuukaribisha  mwaka mpya wa  2016, wananchi hutumia muda huo kwenda  katika nyumba za ibada ama kusherekea katika maeneo mbalimbali ya starehe, ambapo uzoefu unaonyesha kuwa baadhi ya watu hupenda kutumia fursa hiyo kufanya vitendo  vinavyohatarisha usalama wa raia mali zao.

Jeshi la Polisi nchini, limejipanga vizuri katika mikoa yote kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha kwamba vitendo vyovyote vya uhalifu vitakavyojitokeza  hususani katika kipindi hiki cha kuelekea mkesha wa mwaka mpya vinadhibitiwa. Ulinzi umeimarishwa kwenye maeneo yote ya kuabudia, fukwe za bahari, sehemu za starehe na maeneo mengine yote ambayo yatakuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu.

Aidha,  Jeshi la Polisi linatoa tahadhari kwa wananchi wote kuwa makini na kuchukua hatua stahiki za haraka kwa kutoa taarifa pindi wanapoona viashiria vyovyote vya uhalifu katika maeneo yao ya makazi ama maeneo ya biashara. Simu za polisi endapo mwananchi atakuwa na taarifa ni 111 au 112.

 Pia,  Jeshi la Polisi linawatahadharisha wale wote ambao watakuwa wakitumia barabara kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani na hasa kwa madereva wa magari na pikipiki, kuepuka kujaza watu kupita kiasi, kwenda mwendo kasi, kutumia vilevi pamoja na kupiga honi hovyo.

Vilevile, wananchi kuacha tabia ya kuchoma matairi barabani pamoja na kupiga mafataki. Aidha, yeyote atakayefanya vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Nawatakieni watanzania wote kheri ya mwaka mpya.
Imetolewa na:
Advera John Bulimba-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Makao Makuu ya Polisi. 

Taasisi za Dini Zatajwa Sakata la Ufisadi wa Makontena Bandarini.......

$
0
0
Mashirika ya dini ni miongoni mwa taasisi zilizotakiwa kuwasilisha nyaraka kwa ajili ya kuhakiki kama yalilipa ushuru wa bandari uliosababisha Serikali kupoteza Sh48 bilioni.

Uwapo wa taasisi hizo za kiimani kwenye sakata hilo ulibainishwa jana katika orodha ya iliyotangazwa jana na Mamlaka ya Bandari (TPA) ambayo ina kampuni na taasisi 40 zaidi ya orodha iliyotangazwa juzi yenye kampuni 243. Kwa tangazo la jana, kampuni na taasisi zinazotakiwa kuwasilisha nyaraka kuhusu malipo hayo sasa ni 283.

Tangazo la TPA lilitolewa jana likiwa na tarehe ya Desemba 24, linazitaka taasisi hizo ambazo ni Baraza la Kikristo Tanzania (CCT) na Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki, Caritas Tanzania na nyingine 281 kwenda kuchukua barua zao kwa ajili ya uhakiki wa malipo ya ushuru huo yaliyofanyika kuanzia Julai 2014 hadi Aprili, 2015.

Taasisi nyingine maarufu zilizopo katika orodha hiyo ni klabu maarufu ya mchezo wa soka ya Azam Football, kampuni maarufu ya Toyota Tanzania Ltd na Bakhresa Food Products.

Juzi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alizihusisha baadhi ya taasisi hizo 283 na upitishaji wa makontena 11,884 na magari 2,019 kwenye bandari bila kulipia ushuru wa bandari. Kubainika kwa ukwepaji huo ushuru, kunafanya idadi ya makontena yaliyohusika katika suala hilo kufikia 14,664. Awali makontena 349 yaligundulika kupitishwa kinyemela baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufanya ziara bandarini na mengine 2,431 kubainika baadaye.

Mbarawa aliwataka mawakala wa forodha na kampuni hizo 283 zinazotuhumiwa katika utoaji wa makotena na magari bila kulipia ushuru kupeleka vielelezo vya uthibitisho ndani ya siku saba kuanzia juzi.

Msemaji wa CCT, Mchungaji John Kamoyo alisema watafanya kama lilivyoagiza kwenda kuchukua barua zao.

Kama walivyoeleza sisi tutaenda kuchukua barua na kufahamu kilichopo ndani na tutafanya kama walivyoagiza,” alisema Kamoyo huku akikataa kuhusisha wito huo na suala lolote linalohusina na ukwepaji wa kodi.

Katibu mtendaji wa Caritas Tanzania, Laurent Masui alisema atashirikiana na mamlaka hiyo kutimiza agizo hilo.

Ni kweli tunahusika na utoaji mizigo bandarini lakini kwa wateja mahususi kutoka mashirika ya kidini ambayo husamehewa baadhi ya kodi na ushuru. Lakini tozo nyingine huwa tunalipa na kwa kuwa tangazo lenyewe linaonekana ni la kiutawala, basi nitawatuma maofisa wangu haraka wafuatilie ili tujue kama tulizidisha ushuru au tulitoa pungufu,” alisema Nasui.    


CUF Watangaza Kutoshiriki Sherehe za Mapinduzi Zanzibar....Tamko Zima Liko Hapa

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Tokea yalipofanyika Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964, tumekuwa tukiadhimisha tukio hilo kubwa katika historia ya Zanzibar kila mwaka inapofika siku hiyo. 

Tukio hilo kubwa ndilo lililopelekea kutangazwa kwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Rais wa kwanza wa Zanzibar, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume.

Chama Cha Wananchi (CUF) kimekuwa kikishiriki kikamilifu katika maadhimisho ya siku hiyo kila mwaka kwa kutambua kwamba Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964 ni Mapinduzi ya Wazanzibari wote. 

Malengo makuu ya Mapinduzi hayo yameelezwa na kufafanuliwa vyema kupitia Dikrii Nam. 6 ya mwaka 1964 iliyopitishwa na Baraza la Mapinduzi ambayo yanatajwa kwamba ni kuleta usawa, umoja na maridhiano baina ya Wazanzibari wote na kupiga vita aina zote za ubaguzi.

Tayari tumetangaziwa kwamba kuanzia tarehe 2 Januari, 2016 kutakuwa na shughuli mbali mbali zenye lengo la kuadhimisha Mapinduzi yetu na hatimaye, kama ilivyo ada na desturi, kufikia kilele tarehe 12 Januari, 2016 katika sherehe ambazo zitafanyika Uwanja wa Amaan, mjini Zanzibar.

CUF kama chama cha siasa kinawatakia kheri Wazanzibari wote katika kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi yao.

Hata hivyo, tunatambua kwamba sherehe za mara hii zinafanyika wakati ambapo nchi yetu na watu wake wema wamo katika mtihani mkubwa kufuatia kitendo cha mtu mmoja, Jecha Salim Jecha, kuamua kwa utashi wake na waliomtuma kuiingiza nchi yetu katika msukosuko na taharuki kwa kudai kwamba eti ameufuta uchaguzi mkuu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 na matokeo yake.

 Kwa kitendo hicho cha mtu mmoja ambaye amevunja Katiba, amevunja Sheria ya Uchaguzi na amevunja hata maadili ya kazi yake, mara hii nchi yetu itaadhimisha Mapinduzi huku Serikali ikiwa inaongozwa na viongozi ambao hawana uhalali na ridhaa ya wananchi.

CUF tumesisitiza mara zote kwamba hatukubaliani na uamuzi huo wa mtu mmoja kujinyakulia mamlaka ya wananchi wa Zanzibar yaliyowekwa kikatiba. 

Kwa msingi huo huo, tunapenda kutumia fursa hii kuwaeleza wananchi wa Zanzibar kwamba viongozi wetu hawatoshiriki katika shughuli walizopangiwa katika ratiba ya sherehe hizi kwa sababu zifuatazo:

1. Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 (Toleo la 2010), Ibara ya 28, Ibara ya 42(2), Ibara ya 48(b), Ibara ya 90(1) na Ibara ya 92(1) Serikali iliyokuwepo madarakani na Baraza la Wawakilishi lililokuwepo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita (2010 – 2015) vilimaliza muda wake wa uongozi tarehe 2 Novemba, 2015 kwa upande wa Serikali na tarehe 12 Novemba, 2015 kwa upande wa Baraza la Wawakilishi. Kwa sasa, hatuna viongozi wenye uhalali wa kikatiba kuweza kutekeleza majukumu ya kiserikali. Kwa hivyo, kushiriki katika ratiba hizo kwa kutumia nafasi ambazo hazina uhalali tena wa kikatiba ni kwenda kinyume na dhamira ya waasisi wa Mapinduzi, jambo ambalo hatuko tayari kulifanya.

2. Kiuataratibu, kilele cha sherehe huongozwa na Rais ambaye yupo kikatiba. Kwa mara ya kwanza tokea tarehe 12 Januari 1964, sherehe za miaka 52 zitaongozwa na Rais ambaye ameshamaliza muda wake wa uongozi kikatiba na ambaye hana uhalali na ridhaa ya wananchi wa Zanzibar. Kushiriki katika sherehe hizo ni kuhalalisha kipindi cha uongozi ambacho hakipo tena kikatiba. Maalim Seif Sharif Hamad na viongozi wenziwe ndani ya Chama waliokuweko Serikalini hadi tarehe 2 Novemba, 2015 hawako tayari kuhalalisha uvunjaji wa Katiba ya Zanzibar ambayo ndiyo sheria kuu ya nchi.

3. Viongozi wa CUF wakiongozwa na Maalim Seif Sharif Hamad wanaamini katika msingi mkuu wa Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964 chini ya uongozi wa Baba wa Taifa la Zanzibar, Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume, ambao ni kuleta utawala wenye ridhaa ya wananchi walio wengi. 

Msingi huo umewekwa wazi na kutiliwa nguvu na Katiba ya Zanzibar ya 1984 (Toleo la 2010) kupitia Ibara ya 9(2)(a) ambapo inaelezwa kwamba, “Mamlaka ya kuendesha nchi ni ya wananchi wenyewe ambapo nguvu na uwezo wote wa Serikali kufuatana na Katiba utatoka kwa wananchi wenyewe.” 

Mamlaka hayo ya wananchi yalitekelezwa tarehe 25 Oktoba, 2015 kwa kuwachagua viongozi watakaoongoza Serikali yao kwa miaka mitano ijayo.

 Kitendo chochote cha kupindua mamlaka hayo ya wananchi ni kwenda kinyume na misingi ya Mapinduzi na misingi iliyowekwa na Baba wa Taifa la Zanzibar, Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume. CUF hatuko tayari kushiriki katika kuisaliti misingi hiyo na kuisaliti dhamira ya Mzee Karume.

4. Sherehe za kuadhimisha Mapinduzi ya tarehe 12 Januari, 1964 zina lengo la kukumbuka malengo ya Mapinduzi hayo na dhamira ya waasisi wake wakiongozwa na Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume katika kusimamia utawala wenye ridhaa ya wananchi walio wengi.

 Kuzitumia sherehe za Mapinduzi kuhalalisha utawala usio na ridhaa ya wananchi wa Zanzibar na ambao haupo kikatiba ni usaliti mkubwa wa dhamira ya kuwepo kumbukumbu hiyo. CUF hatuko tayari kuwa sehemu ya usaliti huo.

Kwa sababu hizo zilizoelezwa hapo juu, viongozi wa CUF hawatoshiriki katika ratiba walizopangiwa mpaka pale chaguo la wananchi wa Zanzibar walilolifanya tarehe 25 Oktoba, 2015 litakapoheshimiwa.

Tuweke wazi kwamba tulichoamua ni viongozi wetu kutoshiriki katika ratiba zinazohusisha viongozi wa Serikali ambao wamemaliza muda wao wa uongozi. Kwa hivyo, bado tunachukua nafasi hii kuwatakia wananchi wa Zanzibar maadhimisho mema ya miaka 52 ya Mapinduzi na kuwataka waendeleze umoja, mshikamano na amani katika nchi.

Mwisho kabisa, tunamuomba Mwenyezi Mungu awalaze mahala pema Peponi muasisi wa Mapinduzi yetu, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, na waasisi wenzake wote na awasamehe makosa yao.

Tunawaomba Wazanzibari wote kila mmoja kwa dini yake wamuombe Mwenyezi Mungu kuijaalia kheri na salama nchi yetu na kuyasimamisha yaliyo ya haki. Tukiishika kamba ya Mwenyezi Mungu hatutoanguka.

Tunawatakia wote kheri ya mwaka mpya wa 2016 na tunaamini unakuja na kheri kubwa kwa Zanzibar na watu wake. Ni mwaka ambao safari ya ujenzi wa Zanzibar Mpya itaanza.

MAPINDUZI DAIMA!
HAKI SAWA KWA WOTE
MANSOOR YUSSUF HIMID
MSHAURI WA KATIBU MKUU – CUF
31 DESEMBA, 2015

Wema Sepetu Amdiss Diamond kwa Namna Isiyo Rahisi Kuijua! Nimekunyambulia Hapa

$
0
0
Si unajua kuna lile sakata la jina Simba ambalo Diamond amekuwa akilitumia na Mr Blue hivi karibuni kudai alilianzisha yeye?

Na sasa issue hiyo inaenda mbali zaidi. Wema ametumia Instagram kuingia pia kwenye issue hiyo katika njia ambayo inaishia kuwa dongo kwa ex wake.

Watu walikuwa wanasubiria na mimi nitaje jina langu la mnyama… Mi ni Mnyama Ndio na Jina Langu ni WEMA SEPETU…. Gnyt Y’all…. Langu mwenyewe hilo…. Ila Balozi Kasema…. hihihihihi,” aliandika Wema.

Bila shaka bado hujaiona diss! Acha tukusanue. Diss ipo kwenye mstari huu ‘Ila balozi kasema.’

Kivipi? Siku ya show ya Alikiba kwenye boxing day, hitmaker huyo alijinadi kuwa yeye ni balozi wa wanyama – akimaanisha ubalozi wake wa Wild Aid, taasisi inayopigia debe haki za wanyama.

Wengi waliistafiri kauli hiyo kama dongo kwa wote wenye majina ya wanyama!

Mtukaneni tu Tiffah Lakini Siku Moja Atakuja Kuwa Rais Wenu – Zari

$
0
0
Watu hawana haya – Kwa mujibu wa Zari the Bosslady, baadhi yao wamekuwa wakimporomoshea matusi mtoto wake aliyezaa na Diamond, Tiffah tangu alipozaliwa.

Lakini Zari ana habari kwa haters! Mrembo huyo wa Uganda anaamini kuwa siku moja watamheshimu mtoto wake sababu anamlea aje kuwa rais kama Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia!

“Matusi from day one even before she was born,” ameandika Zari kwenye Instagram.

“But she is here and strong enough to handle. Boss ladies use bricks thrown at them to build empires. And this right here is my future president in the making #IronLady #EllenJohnsonSirleaf #Kichuna @princess_tiffah.”

Martin Kadinda Ataja Mipango Mipya kwa Wema Sepetu 2016...Adai Skendo Sasa Basiiiii

$
0
0
Meneja Wema Sepetu, Martin Kadinda amesema mpango alionao ni kumtoa mwanadada huyo katika drama na kumfanya awe mfanyabiashara mkubwa mwaka 2016.

wemaa na kadinda

Kadinda ambaye pia ni mbunifu wa mavazi, ameiambia Bongo5 kama Wema akiweza kubadilika na kuacha drama, atakuwa na mafanikio makubwa.

Wema is a business woman, kitu ambacho nitakifanya ni kuhakikisha anasimama kama mfanyabiashara,” alisema.

Kuna kipindi tulikuwa tayari tumeondoka kwenye drama na mimi nikasimama na kazi zangu nyingine akarudi tena kule kule. Lakini cha umuhimu ninachomuomba Mungu tuweze kurudi katika hali ya kawaida na kikubwa tunachopigania ni kuwa nje ya drama na tuwe watu ambao tunafanya biashara,” aliongeza.

Rais Magufuli Hataniii....Hatimaye Jumba la Kifahari la Mchungaji Getrude Rwakatare Lawekwa Alama ya Kubomolewa

$
0
0
Baada ya nyumba ya Dr. Reginald Mengi kudaiwa kuwa itabomolewa... Nyumba ya Mchungaji Getrude Rwakatare (aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum CCM Bunge lililopita) nayo kubomolewa!


Shilole Aporomosha Matusi Hewani Akihojiwa Redioni Baada ya Kuulizwa Kuhusu Kuachana na Nuhu Mziwanda..Mashabiki Wadai Amefanyiwa Interview Akiwa Mlevi

$
0
0
MWIGIZAJI na mwanamuziki wa kizazi kipya Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amemzingua Dj Tass mtangazaji wa kipindi cha Kwetu Fleva baada ya kushusha matusi hewani akihojiwa na mtangazaji huyo na kumfanya aombe msamaha kwa wasikilizaji kwa kutamka Sorry for That mara mia.

Tass alikatiza matangazo baada ya Shilole kuulizwa swali kuhusu mpenzi wake Shilole ambaye ametangaza kutengena naye hivi karibuni Mziwanda ambaye alitamba naye kwa muda mrefu na hata msanii huyu wa kiume kujichora picha ya Shilole mwilini mwake.

Wapenzi wa kipindi cha Kwetu Fleva nawaomba radhi kwa kilichotokea Shilole waombe msamaha, na nimekukanya mara ngapi? Nitakuzingua upo hewani unatukana una maananisha nini? Sorry for that, sorry for that,”anasema Dj Tass.

Baada ya kuagana na Shilole wapenzi wa kipindi hicho wamelaumu Dj Tass kwa kumleta Shilole akiwa kalewa studio na kuharibu interview , msanii huyu alikuwa akimponda sana Nuhu Mziwanda akimtangaza msanii kutoka Uganda E Kenzo kama mchumba wake mpya kwa sasa.


Askari Mwenye Kitambi Akutana Laivu na Magufuli.....Haya Ndio Maongezi yao......

$
0
0

.Rais John Magufuli Katika Katuni laivu na Askari Mwenye Kitambi......

Sheria Ya Kuzuia Kelele Yaanza Kutumika....Kufanya Sherehe Mtaani, Kupiga Mziki, Kufanya Ibada Kwa Kelele ni Milioni 10

$
0
0
BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limeanza kung’ata kwa kutumia kanuni ili kudhibiti uchafuzi wa mazingira kwa kelele na mitetemo.

Kwa sasa mtu akitaka kufanya sherehe mtaani, kupiga muziki kwa kelele, kuendesha ngoma za kukesha za nusu uchi (vigodoro) au ‘bai koko’ au kufanya ibada kwa kelele mitaani, atapaswa kulipa Sh milioni 10.

Pia, baa na kumbi za starehe za usiku zitakazopiga kelele, zitapaswa kulipa kiasi hicho.

Aidha, NEMC imesema pia kuwa wale watakaohusika na kelele za migodini za kutumia baruti, kupasua miamba zilizo zaidi ya matakwa ya sheria ya mazingira ya kelele na mitetemo, watapaswa kulipa Sh milioni tano ili kupata kibali.

NEMC imetaka watu kuheshimu kanuni za viwango vya kelele na mitetemo katika maeneo mbalimbali nchini. Imeonya kuwa watakaokiuka, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao. Kanuni hizo zimeanza kutumika mwaka jana (2015).

Mkurugenzi Mtendaji wa NEMC, Bonaventure Baya alisema hayo Dar es Salaam jana. Alisisitiza kuwa uchafuzi wa mazingira, unaosababishwa na kelele na mitetemo, umekuwa ukifanyika bila kujali sheria za nchi na sasa watashughulikia suala hilo ipasavyo.

Alisema hivi sasa kanuni za kudhibiti suala hilo, zimekamilika na zimeanza kutumika kikamilifu. Mtu yeyote atakayekwenda kinyume cha kanuni na sheria, atachukuliwa hatua kali. Baya alitoa ufafanuzi kuwa yapo maeneo yenye kelele zaidi ya viwango vinavyoruhusiwa kisheria, ikiwamo maeneo ya migodini.

Alieleza kwamba kanuni zimeweka vigezo na tozo maalumu la kuanzia Sh milioni tano hadi Sh milioni 10, kulingana na eneo na aina ya kelele na mtetemo. Alisema mambo mengine ambayo kanuni zimeweka ni faini kwa kila kanuni itakayovunjwa na kusisitiza kuwa hatua hizo zitachukuliwa ipasavyo.

Kulingana na hatua hiyo ya NEMC, sasa mtu mwenye kutaka kufanya sherehe mtaani, itakayohuisha kelele zitakazosumbua jamii pamoja na majirani zake, ikiwamo muziki maarufu wa ‘kigodoro’, ibada za makanisani zinazozidi matakwa ya kisheria ya uanzishwaji wa makanisa hayo katika jamii, atapaswa kulipa Sh milioni 10 ndipo aruhusiwe kuendelea na shughuli yake.

Kwa mujibu wa NEMC, ruhusa hiyo inayo lipiwa, pia ina muda na viwango vyake, ambapo kila muda husika unapoisha, kelele zinapaswa kupunguzwa ama kuzimwa. Hii inahusisha pia baa na kumbi za starehe za usiku.

Baya aliitaka jamii kuepuka uchafuzi huo wa mazingira wa kelele na mitetemo, ambao watu wengi wamekuwa wakidhani si tatizo. Alitaka watu kuheshimu matakwa ya sheria na kanuni kwa nyakati za mchana na usiku.

Tumekuwa tukipokea malalamiko kutoka kwa watu wengi, wakilalamikia usumbufu wa kelele na mitetemo kutoka kwa watu wanaoendesha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii katika jamii,” alifafanua Baya.

Alitoa angalizo kwa wanaotumia vyombo vya muziki na sauti katika maeneo ya makazi, ambavyo vimeleta madhara kwa afya za watu. Alisema matumizi ya vipaza sauti na vyombo vya sauti kubwa, wanapaswa kuwa na kibali maalumu.

Alieleza kuwa kanuni za kelele na mitetemo, zimeweka vigezo na viwango vya sauti kwa ajili ya kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya hospitali, makazi, migodini, kumbi za kijamii, kumbi za usiku za starehe, matangazo, baa na maeneo mengine.

Baya alisema baraza limepata changamoto kadhaa, ikiwamo uelewa mdogo wa jamii kuhusu kiwango cha sauti kinachotakiwa na kisichoruhusiwa na baadhi ya watu kwa makusudi huvunja sheria.

Kuhusu faini, alisema sheria ya mazingira imeweka wazi faini kwa wanaokiuka na kuchafua mazingira kwa kelele na mitetemo. Faini hiyo haiingiliani na tozo la Sh milioni tano hadi Sh milioni 10 lililoelezwa, ambapo mtu anapaswa kulipa si chini ya Sh milioni 50 na si zaidi ya Sh milioni 50 ama kifungo jela.

Kaimu Mkurugenzi wa Usimamizi wa Sheria za Mazingira wa NEMC, Ruth Lugwisha alisema tatizo la kelele na mitetemo, limekuwapo kwa muda mrefu. Alisema tangu kupitishwa kwa kanuni, tayari watu kadhaa wamewajibishwa.

Alisema miongoni mwa waliowajibishwa ni makanisa, kumbi za starehe na baa. Hata hivyo, hakuwa tayari kuwataja wahusika wala maeneo. Alisema uwajibishwaji huo ulihusisha faini, kufungiwa na onyo.

Jumba la Mchungaji Mama Rwakatare, Hoteli za Double Tree na Slip Way Kubomolewa

$
0
0
Wakati operesheni ya kuweka alama ya X kwenye nyumba zilizojengwa mabondeni, maeneo ya wazi na kinyume na taratibu ikiendelea, Hoteli za Double Tree na Slip Way nazo zimekumbwa na pigo hilo.

Hoteli hizo pamoja na nyumba ya Maheshbhai Patel na baadhi ya wamiliki wengine wa nyumba ambao kuta zake zimejengwa karibu na barabara ya Slip Way eneo la Msasani Peninsula, wamepewa siku saba kuzibomoa.

Jana, uongozi wa Manispaa ya Kinondoni uliweka alama za X na kuwaonya wamiliki hao kwamba, wasipobomoa manispaa itazibomoa na kudai gharama za ubomoaji.

Akizungumza kwa simu jana, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alisema Serikali haitaurudi nyuma katika kutekeleza sheria hata kama kuna watu wana jeuri ya pesa.

Alisema Manispaa ya Kinondoni iliwapatia vibali vya kupendezesha maeneo ya pembezoni mwa barabara ikiwamo kupanda maua, lakini wao badala ya kutimiza masharti ya vibali walizungushia kuta jambo ambalo hawatalivumilia.

Wangependezesha na kufunga minyonyoro kuzuia kuharibiwa mazingira yao kama walihisi wananchi wangeharibu, lakini siyo kujenga kuta.

“Nimewaagiza Kinondoni wawapatie notisi ya siku saba kubomoa kwa hiari. Wasisubiri Serikali ivunje.

"Tutabomoa hadi lile jengo lililopo karibu na Hospitali ya Ami lililovunja sheria, yule hawezi kuonyesha jeuri ya fedha,” alisema Lukuvi.

Alisema Serikali ina mpango maalumu wa kubomoa majengo yote yaliyojengwa kinyume na sheria Masaki na Oysterbay na wameanza na Barabara ya Slip Way.

Katika hatua nyingine, sakata la bomoabomoa pia limewakumba waliojenga katika hifadhi za mikoko baada ya watumishi wa Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na maofisa misitu wa Manispaa ya Kinondoni kuweka alama ‘X’ katika nyumba zaidi ya 30 ikiwamo ya kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God, Dk Getrude Rwakatare.

Kazi hiyo ilianza jana mchana katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam ikiwamo, katika Mtaa wa Ally Sykes, Kawe na Jangwani Beach eneo la Mbezi Beach. Ofisa Misitu Msaidizi wa Manispaa ya Kinondoni, Issa Juma aliwaambia wanahabari kuwa kazi hiyo ni endelevu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Tarehe 1 Januari 2016, Ikiwemo ya Wema Sepetu Kukoleza Bifu Kwa Diamond

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Tarehe 1 Januari 2016, Ikiwemo ya Wema Sepetu Kukoleza Bifu Kwa Diamond

Osama Bin Laden Is Still Alive...Former CIA Employee Revealed

$
0
0

Former CIA employee, Edward Snowden has said that he has evidence showing that Osama bin Laden, who was supposedly killed in Pakistan in 2011 by U.S. special forces, is still alive and well.

In an interview with the Moscow Tribune, Snowden said Osama was living in the Bahamas, on the payroll of the CIA.

He told the newspaper, "I have documents showing that Bin Laden is still on the CIA's payroll. He is still receiving more than $100,000 a month, which is being transferred through some front businesses and organizations, directly to his Nassau bank account. I am not certain where he is now, but in 2013, he was living quietly in his villa with five of his wives and many children."

Snowden, who now lives as a fugitive in Russia, fled the U.S. after leaking documents about the NSA's mass surveillance programs to the media in 2013.

The report also said that Snowden previously too made some unreported allegations about Osama bin Laden.

Snowden goes on to say that the CIA orchestrated the fake death of the former leader of Al-Qaeda.

He claims that Osama was transported with his family to an undisclosed location in the Bahamas.

The report further quotes him as follows – "Osama bin Laden was one of the CIA's most efficient operatives for a long time. What kind of message would it send their other operatives if they were to let the SEALs kill him? They organized his fake death with the collaboration of the Pakistani Secret Services, and he simply abandoned his cover. Since everyone believes he is dead, nobody's looking for him, so it was pretty easy to disappear. Without the beard and the military jacket, nobody recognizes him."

Not only this, Snowden categorically states that he will talk about the documents which prove Bin Laden is alive in his soon-to-be-released book.

However, Snowden's claims have not been substantiated or confirmed by any other source.

The US government has filed espionage charges against Snowden for revealing classified NSA documents to journalists.

Hivi Escrow ni Ufisadi au Promotion? Wahusika Bado Wanapeta na Kukabidhiwa Vyeo....

$
0
0
Tumeshuhudia watuhumiwa wa Escrow wakikabidhiwa Wizara na Idara Muhimu za Umma na wengine kupitishwa kugombea Ubunge wa kwenye Serikali ya awamu wa Tano kana kwamba hawakufanya Ufisadi wa aina yoyote, kwenye Serikali ya awamu wa nne. Pengine mimi naweza kuwa sina Ufahamu wa kutosha juu ya maana ya neno Ufisadi.

Hebu tujiulize, unawezaje kufumbia macho Ufisadi wa Escrow zaidi ya bilioni 300, na wakati huo huo ukasema unatumbua jipu kwa ufisadi bilioni 59? Namaanisha bilioni 12 za makontena TRA na 47 za makontena bandarini. Na usimpeleke mtu hata mmoja mahakamani, na wakati huo huo ukamkabidhi uongozi, Wizara na Idara muhimu za Umma.

Kwa uelewa wangu hapa kuna double standard na maana halisi ya Kutumbua jipu inageuka kuwa uonevu na kuoneana haya.

Je, ni lini watuhumiwa hawa wa Escrow walifikishwa mahakamani kujibu tuhuma za Ufisadi wa Escrow na Mahakama ikawasafisha, na wakastahili Promotion hii?

Prof. Muhongo - Waziri Nishati na Madini

Maswi - Ag D. Commissioner TRA.

Chenge - Mbunge.

Tibaijuka - Mbunge.

Ngeleja - Mbunge.


Je, Escrow ni Ufisadi au Promotion?

" Injustice anywhere is a threat to justice everywhere" M.L. King Junior.

Mwaka Mpya 2016 Ulivyokaribishwa Usiku wa Jana Escape 1, Mikocheni ...Picha

$
0
0
Watu mbalimbali waliofika Escape 1 kuukaribisha mwaka Mpya 2016.
Msanii Chemical ndiye aliyefungua pazia la burudani pande za Escape 1 kuukaribisha mwaka Mpya 2016.
Msanii Matonya akiwapa burudani mashabiki waliofika Escape 1 kuukaribisha mwaka Mpya 2016.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images