Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

PIGO LA PILI KWA LOWASSA, BADO LA TATU NA LA MWISHO

0
0
"Bwana Lowassa,

Nikupe pole nyingine baada ya ile ya juzi kati kukueleza vichomi ulivyotegeshewa na ambavyo vimeanza kukuchinjia baharini tena kuleeeee Nungwiiiii, Naam umepigwa kufuli kutojishughulisha na siasa za uongozi mpaka mwezi wa pili mwakani,

Sasa ulijiandaa kuteka siasa kwamgongo wa katiba mpya, ikawa usiku ikawa mchana, naaam leo Chenge kakulamba chenga ya kisigino, ndio kakutelekeza, tena alfajiri tu.

Chenge kaiona pepo japo ni ya masika tu na kaniki haifuliwi kwa maji ya mvua.

Chenge hatunae tena kwenye anga la ukuu wa katiba mpya, sasa ni yuleyule aliyekupeleka kibla mnamo 2007, si mwingine ni Samwel Sitta mbabe wako kutoka CCJ.

Wayajua mapigo mawili yaliyo mbele yako??

Haya tutaftane..."

By Yericko Nyerere From JF

SIKU TATU ZA CHADEMA WALIZOMPA RAIS KIKWETE ZIMEISHIA WAPI ?

0
0
Chadema kupitia kigaila walitoa siku tatu kwa rais afute kauli yake kuwa uvumilivu kwa wanaccm sasa basi. Leo ni zaidi ya wiki moja, aona kimya. Vipi, wamesahau? Hawana la kumfanya? Wamesalimu amri? Wamemuogopa? Tunaomba mrejesho wa kinachoendelea

HAYA NDIYO MADHARA YATOKANAYO NA NGUO ZA KUBANA (SKIN TIGHT)

0
0
  Nguo za kubana

KADIRI siku zinavyokwenda kumekuwapo na ugunduzi wa vitu mbalimbali vinavyochangia kuleta mabadiliko katika jamii. Mabadiliko hayo yanaweza kuwa hasi au chanya kutegemea na aina ya  bidhaa iliyogunduliwa na matumizi yake. Zipo bidhaa zinazoonekana kuwa na matokeo ya haraka na mazuri baada ya kutumika, lakini wakati huo huo kuwa na madhara kiafya kwa mtumiaji.
Nchi nyingi zinazoendelea hasa zilizopo barani Afrika ikiwamo Tanzania zimekuwa ndizo waathirika wakubwa wa bidhaa zinaotajwa kuwa na madhara huku vijana wakiwa ndiyo kundi kubwa linaloathirika. Sababu za kundi hilo kuathirika zaidi ni kutaka kwenda na wakati kwa kujaribu kutumia kila bidhaa zinazotoka nje ya nchi bila kujua madhara yake.
Miongoni mwa bidhaa hizo ni nguo za ndani zilizoundwa maalumu kwa ajili ya kupunguza unene, pia kutengeneza umbile la mvaaji katika mwonekano wenye mvuto aupendao. Nguo hizo zimetengenezwa kwa mtindo wa mbano, (Skin tight)ambapo ikivaliwa hubana eneo la tumboni hadi kwenye mapaja na hufanya kazi ya kupunguza unene, zikiufanya mwili kuwa mwembamba kulingana na nguo husika ilivyo.
Licha ya kufanya kazi hiyo kwa ufanisi na kusaidia kwa kiasi kikubwa watu wengi kupunguza miili yao, utafiti wa kisayansi unaonyesha kuwa nguo hizo za ndani huchangia kwa kiwango kikubwa uwezekano wa mvaaji kupata matatizo ya kiafya.
Utafiti uliofanywa na wataalamu mbalimbali wa nchini Uingereza, unaonyesha kuwa uvaaji wa nguo hizo unaweza kumfanya mvaaji kupata maradhi ya mgongo, saratani na kiwango kikubwa cha asidi mwilini.
Mmoja wa wataalamu wa afya katika Hospitali ya The London Clinic, Dk Johnson Wilson, anasema kubana kwa nguo hizo katika eneo la tumbo huzuia mzunguko wa asidi inayozalishwa ndani ya mwili na kuisababisha kupanda juu, badala ya kushuka chini.
Anasema kuwa hali hiyo inatokana na msukomo unaotokea kwenye tumbo, hivyo kusababisha mlundikano wa asidi ndani ya mwili ambayo hupaswa kutoka baada ya kuzalishwa.
“Nguo hii inapovaliwa inatenganisha  eneo la kifuani na tumbo, hivyo asidi inayozalishwa inashindwa kushuka chini na matokeo yake inashia kwenya usawa wa  matiti na kurudi kwenye mrija unaopitisha chakula,”anasema DkWilson.
Kuhusu hatari ya saratani, Dk Wilson anasema kuwa kulundikana kwa asidi katika mrija wa chakula, kunamweka mhusika katika hatari ya kupata saratani ya koo na kinywa.
Anasema kwamba licha ya kuwa siyo watu wengi walioathirika na uvaaji wa nguo hizo, lakini matokea yake huonekana baada ya muda mrefu kutokana muda ambao mhusika atavaa nguo hizo.
“Hatari ipo zaidi kwa wanaovaa nguo hizi mara kwa mara, madhara yake hayawezi kuonekana kwa haraka zaidi, lakini kiafya kuna hatari ya kutengeneza saratani ya koo kutokana na kuzuia asidi na kusababishia irudi na kulundikana kwenye mrija unaosafirisha chakula,”anaonya.
Pamoja na hatari hiyo uvaaji wa nguo hizoi pia unachangia kusababisha ugonjwa wa ngozi unaotokana na mwili kubanwa kupita kiasi, hivyo hewa kushindwa kupita.
Dk Wilson anafafanua kuwa ikifikia hatua hiyo, kuna uwezekano wa kutengeneza mazingira ya bakteria na fangasi kujificha kwenye mwili hivyo kusababisha mvaaji kupata maradhi ya ngozi yaliyo magumu kutibika.
Mtaalamu wa ngozi Dk Sam Bunting anasema, kubanwa kwa ngozi pamoja na joto linalosababishwa na msuguano, vinachangia kuleta madhara makubwa katika mwili wa binadamu.
“Hali hii inasababisha ugonjwa unaofahamika kwa jina la kitaalamu kama Intertirgo, ambao huwatokea watu wanaovaa nguo maalumu za kubana kwa ajili ya kutengeneza maumbile,”anasema.
Nguo hizo pia huchangia kuifanya misuli ya tumbo kuwa dhaifu, kutokana na kubanwa muda mwingi, hata inapoachwa huru inashindwa kuwa na nguvu yake ya kawaida.
“Kwa asili misuli ya tumbo haina nguvu na unapoibana kwa muda mrefu unaisababishia kushindwa kufanya kazi yake kwa ufanisi, hivyo hulegea na kuwa  dhaifu zaidi hata inapofunguliwa au kutolewa nguo inayobana,”anasema.
Kwa upande mwingine, mtaalamu wa misuli Dk Robert Shanks anasema kuwa nguo hizo zinachangia pia kusababisha maumivu ya mgongo kwa mvaaji. Anasema nguo hiyo inapovaliwa, kunakuwapo na ugumu kwa viungo vya mgongo kujongea kwa urahisi, hivyo kusababisha maumivu ya mgongo mara kwa mara.
“Viungo na mifupa iliyopo kwenye mgongo inapaswa kujongea, lakini kuibana kupita kiasi kutasababisha kushindikana kwa hali hiyo hivyo mvaaji lazima atakumbana na maumivu ya mgongo mara kwa mara”
Pamoja na madhara hayo, nguo hizi pia huweza kusababisha kizuizi katika mzunguko wa damu kwani mishipa inayotakiwa kufanyakazi hiyo inashindwa, kutokana na maeneo ya tumbo hadi kwenye nyonga yanakuwa yamebanwa.
“Ni vigumu mzunguko wa damu kufanyika vizuri katika maeneo yaliyobanwa kupita kiasi; ni wazi kuwa nguo hizi siyo rafiki, huifanya damu isizunguke inavyopaswa,”anasema Dk Shanks na kuongeza:
“Ikifikia hatua hiyo, kuna dalili mvaaji kuweza kupata maimivu ya miguu kwa kuwa mishipa ya damu iliyopo katika maeneo hayo inashindwa kufanya kazi yake vizuri.”
Kwa upande wake mtaalamu wa masuala ya ngozi nchini Tanzania, Dk Isack Maro, anasema kuwa madhara yanayotokana na uvaaji huo siyo makubwa ikilinganishwa na ripoti ya utafiti unavyoeleza.
“Inawezekana kukawapo uwezekeno wa kupata maradhi ya ngozi kutokana na mwili kubanwa kwa muda mrefu, hivyo jasho kushindwa kutoka na kutengeneza mazingira ya fangasi,”anasema Dk Maro na kuongeza:
“Madhara yapo, lakini siyo kwa ukubwa huo. Inawezekana kuwakumba watu wachache mno kati ya wengi, lakini sidhani kama yanaweza kuwa kwa ukubwa huo.”

IF YOUR HUSBAND STRAYS, IT'S YOUR FAULT WOMAN

0
0
The recent wave of straying men is alarming. In fact, the issue of having ‘clandes’ otherwise known as ‘mpango wa kando’ has come to the attention of all such that debating about them in public and anywhere else people deem fit is no longer refutable.

In the recent years, married women or those in serious relationships have crafted a spirited fight against the so-called mushroom constituency of competitors. Present in this ‘constituency of competitors’ are certain types of women commonly referred to as ‘Clandes a.k.a Mpango wa kandos’ whom in other words can still be referred to as ‘the side kick’.

So if I were to ask, what has led to the emergency of this mushroom constituency? According to the Crazy Monday, married women are to be blamed for driving their men away from their homes which in turn increases their chances of finding comfort in the hands of the ‘side kick’.

But how is that? A pastor with one of the most popular worship sanctuaries in town opines,

“You see, it’s a battle out there for most men in their endeavors to provide for their families. So when they come home, this is the place he looks forward to get peace and comfort”.

Based on that argument, it is agreeable that home is the last place a man wants or expects to be bothered or better yet, subjected to any sort of battle. In essence, a man wants to have relative peace and comfort at home in addition to love and all that appertains to it.

As a wife, you may still ask yourself what happens if you have something critical you need discussed or addressed urgently. Wonder no more, the pastor says;

“My dear sister, even the Holy Scripture says there is time for everything. There is time to laugh and there is time to cry, there is time to work and there is time to play. It is upon you the woman to know your man and know when he is ready to be engaged in a draining conversation”.

When looked from such a vantage point, one must understand that simply because the wife is ready to discuss certain touching issues at certain times does not necessarily mean that the man is the mood to discuss them.

As noted in a number of considerable debates, women tend to let themselves down, ignore the small things that used to spark their relationships and reach to a point where they no longer bother wearing the negligees the man bought them. Instead, they choose to wear maternity-like dresses and ‘seng’eng’e ni ng’ombe’ or ‘Safaricom’ branded T-shirts which are, in my opinion, an absolute turn-off.

What they do not seem to understand is that, by doing so, they are simply preparing fertile grounds for their men to look for love somewhere else. With these facts on the table, if he seeks comfort in the hands of another woman and happen to be lucky or rather unlucky, for that matter, to find out about the ‘mpango wa kando’, blame no one but yourself woman.

WHY TANZANIA WILL SOON OVERTAKE KENYA IN CREATING MILLIONAIRES

0
0
Tanzania is creating dollar millionaires faster than any other East African country, a new report says.

This means that East Africa’s newest millionaires are likely to come from Tanzania, as opposed to Kenya, Uganda, Rwanda or Burundi.

According to the African 2013 Wealth Book, the country is ranked third in Africa, after Ethiopia and Angola, with its millionaires’ club growing at a rate of 51 per cent between 2007 and 2013.

While it had 3,700 millionaires in 2007, this number had risen to 5,600 by 2013. Tanzania is followed in the region by Kenya, the only other regional country that features among the top 10 in Africa. Kenya is reported to have had 8,300 millionaires in 2013 against 6,700 in 2007, a growth rate of 24 per cent.

The report, put together by New World Wealth, defines millionaires or high net worth individuals (HNWIs) as those with net assets worth $1 million or more, excluding the value of their primary residences. The survey includes only those countries that had over 800 millionaires in 2013.

On the scale of absolute numbers, Kenya is up there, mixing it up with Africa’s big boys, coming fourth after South Africa (48,700), Egypt (22,800) and Nigeria (15,700).

Tanzania’s faster acceleration must be understood in the context of a country that is coming from a low base.

After decades of a command economy in which the government controlled most of the wealth, the liberalised economy is just warming up and the risk-takers among the population are clearly cashing in. Tanzania is also more resource-rich than its EAC partners.

It is endowed with vast natural gas and oil deposits, besides substantial quantities of gold, diamond and tanzanite. It also has the region’s biggest water and forest resources and is often referred to as the “lungs of the region.”

Thus the newly created millionaires probably individuals who have bet their money on its rapidly developing oil, gas and minerals sector, where massive deposits of offshore gas have made Tanzania a leading investment destination for prospectors and developers. As of June 2013, 42.7 trillion cubic feet of natural gas (about 7.5 billion barrels of oil equivalent) has been discovered in Tanzania.

Tanzania’s gold sector has also witnessed a boom in the past few years, and it is now the country’s leading export, worth $2.2 billion in 2012, followed by tobacco exports at $223 million and coffee at $187 million.

It recorded a growth of 45 per cent between 2007 and 2012 against Kenya’s 20 per cent. Even then, Kenyans were generally richer than their Tanzanian counterparts at a per capita income of $862 against the latter’s $609 in 2012.

In average terms, the richest Africans are to be found in South Africa ($7,508 per capita income), Angola ($5,485), Algeria ($5,404), Tunisia ($4,237) and Egypt ($3,187). While South Africa is known to have a resource-rich and fairly sophisticated economy, Angola is the beneficiary of its oil. The Maghreb countries’ good fortune is a result of a mix of oil and “welfarist” public policies.

Uganda leads the pack in expanding individual wealth in the region. Closer home, Kenya is expected to have 21,200 dollar millionaires, compared with Tanzania’s 15,200.

Mr Akumu writes for the Daily Nation, email – wakumu@ke.nationmedia.com

NIMEGONGWA NA BODA BODA NIKIMSHANGAA MDADA MWENYE WOWO KUBWA

0
0
Sasa nimekuwa kama mgonjwa ,nikiona mwanamke mwenye wowo kubwa akiri yangu inaruka kabisa. Leo katika pilika pilika za kutafuta maisha nikiwa kariakoo nimegongwa na boda boda nikiwa namshangaa mdada mwenye matako makubwa , bahati nzuri sikuumia sana, lakini sasa nawasi wasi kwamba inawezaikatokea nikagongwa nagari kabisa nakuumia sana au hata kufa kwa huu ugonjwa wangu wa kupenda kutamani wanawake wenye makalio makubwa . Sasa sijui nifanyaje, kuna rafiki yangu mmoja kanishauri nioe mwanamke mwenye makalio makubwa labda itakuwa nafuu kwangu. Majanga haya , yani leo baada ya kugongwa nilijiona jinga sana aisee...Naomba ushauri

UTEUZI WA MUME NA MKE BUNGE LA KATIBA WAKIVURUGA CHAMA

0
0
Zanzibar. Sakata la Mwenyekiti wa Chama cha National League for Democracy (NLD), Dk Emmanuel Makaidi kudaiwa kufanya njama zilizofanikisha yeye na mkewe kuteuliwa wajumbe wa Bunge la Katiba, limechukuwa sura mpya baada ya kiongozi wa chama hicho Zanzibar kujiuzulu na kujivua uanachama.

Akitangaza uamuzi wa kuachana na chama hicho juzi, Naibu Katibu Mkuu NLD Zanzibar, Khamis Haji Mussa alisema ameshindwa kuvumilia kitendo hicho alichodai kinadhalilisha chama.

“Kwa hiari yangu nimeamua kujiuzulu uanachama na kuacha wadhifa niliokuwa nao ndani ya NLD, jina zuri la tawi la Ustawi wa Kitaifa wa Demokrasia ni nadharia tu, vitendo vyake ni udikteta na ubabe... nashauriana na wanasheria kuona kama kuna kesi ya kufunguliwa,” alisema Mussa.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya NLD Zanzibar pia kutoa tamko la kumtaka Rais Jakaya Kikwete kufuta uteuzi huo, kwa madai walioteuliwa kutoka chama hicho ni mtu na mkewe hivyo kukosa sura ya Muungano.

Mussa alisema ameshindwa kuvumilia kwa sababu kitendo hicho kinadhalilisha chama na kinaashiria ukosefu wa misingi ya uwazi na uadilifu.

Alisema amefikia uamuzi huo kutokana na madai kwamba Dk Makaidi ameonyesha waziwazi anaiongoza NLD kwa ubinafsi, ubaguzi na kuitenga Zanzibar katika uwakilishi wa Bunge la Katiba. Mussa alisema Dk Makaidi amejidhihirisha ni mbaguzi na anaweza kuligawa taifa kwa misingi ya Uzanzibari na Utanganyika, ikiwa siku moja atabahatika kupewa dhamana.

Alisema utetezi uliotolewa na Dk Makaidi umekosa nguvu ya hoja, zaidi ametumia umwamba unaoweza kuvipaka matope vyama vingine vya siasa.

Katika utetezi wake, Dk Makaidi alisema NLD Zanzibar walichelewa kupeleka majina kwa Rais wa Zanziba na kwamba, kuteuliwa kwa mkewe hakuna matatizo kwa sababu ana sifa zinazotakiwa.

AKAMATWA AKIDAIWA KUUZA NYAMA YA BINADAMU

0
0
Mkazi wa Kijiji cha Kihinga, Kata ya Bugarama wilayani Ngara mkoani Kagera(jina tunalo), anashikiliwa katika kituo kidogo cha polisi cha kata hiyo baada ya kutuhumiwa kuuza kilo moja ya nyama ya binadamu kwa Sh100,000.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kihinga, Hassan Mohamed alisema kuwa jana saa mbili usiku, wananchi walipeleka fedha nyumbani kwake kununua nyama hiyo na alipowaona alikimbia na wananchi hao kwa hasira walimkimbiza ili kumuua na hapo hapo kuunguza nyumba yake.

“Mgambo ndio walimnusuru asiuawe na wananchi wenye hasira kali na alikimbizwa kituo kidogo cha polisi Kata ya Bugarama ili kuokoa maisha yake “.

Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa mgambo wa kijiji hicho, Emanuel Kaloli alisema wananchi waliandamana baada ya kusikia taarifa za kuwapo mtu anayeuza nyama ya binadamu na kutaka kuhakikisha ukweli huo.

Alisema baada ya wananchi kufika, walianza kumshambulia na kutaka kumuua, lakini wanamgambo wa kitongoji walifika kisha kumuokoa mtuhumiwa na hatimaye kumfikisha kituo cha polisi kwa ajili ya usalama wake.

“Kijana aliyefahamika kwa jina la Man Balyamwabo mkazi wa Shina la Kalenge katika kitongoji hicho, ndiye aliyeambiwa kuwa angeuziwa nyama hiyo ya binadamu na kuleta taarifa katika uongozi wa kijiji ili uweze kuchukua hatua zaidia”.Alisema Kaloli.

Alisema nyumba aliyounguziwa pamoja na mali iliyokuwamo ndani hasa maharage, mavazi na vitu vinginevyo inakadiriwa kuwa na thamani ya Sh2.6milioni. Pamoja na kuwepo kwa tukio hilo, baadhi ya wananchi walisema mtuhumiwa inasemekana ni raia wa nchi jirani ya Burundi na alianza kuishi katika kitongoji hicho tangu mwaka 1981 kama kibarua wa kilimo kwenye mashamba.

Taarifa zinasema kuwa katika kuishi kwake na ndugu yake aliyefahamika kwa jina la Kahungu walikuwa wakituhumiana kwa uchawi na ilifikia mahala wakatofautiana na kaka yake ambaye alirejea kwao.

Polisi wilayani Ngara imethibitisha kumpokea mtuhumiwa huyo na kwamba linafanya mahojiano ya kina kwa kushirikiana na viongozi wa kijiji ili kubaini ukweli wa tukio hilo.

HATARI:KAJALI ALISHWA SUMU, AKIMBIZWA HOSPITALINI

0
0
Mwanadada mwigizaji Kajala juzi alikumbwa na dhahama ya kusikitisha baada ya kulishwa kitu kinachosadikiwa kuwa ni sumu alipokuwa kwenye show ya msanii wa muziki kizazi kipya Izzo Business huko.

Akielezea Zaidi kajala alisema…

‘’Jana (juzi) nilivyokuwa kwenye shoo ya izzo ghafla nikaanza kuumwa nikapelekwa home halafu nikaenda hospitali. Nilivyo pimwa nikakutwa nimekunywa kitu chenye sumu lakini namshukuru mungu naendelea vizuri asante mungu kwa kila jambo...

Hali ya kajala ni nzuri na ameruhusiwa kutoka hospitalini sasa. Pole sana Kajala

MREMBO AFIA GESTI ARUSHA

0
0
Stori: Joseph Ngilisho, Arusha
MREMBO mmoja ambaye alihu-dumu kwenye nyumba ya kulala wageni na baa (jina tunalo) iliyopo Tengeru, wilayani Arumeru, mkoani Arusha, Blandina Michael (33) amekutwa amekufa kwenye moja ya vyumba vya nyumba hiyo huku chanzo cha tukio hilo kikihusishwa na vitendo vya ushirikiana.

Taarifa za awali zilimtuhumu mmiliki wa nyumba ya wageni moja ambaye pia anajihusisha na biashara za madini (jina tunalo) kwamba alimtoa kafara mhudumu huyo. Ilidaiwa kuwa, kila mwaka mtu mmoja katika biashara zake hupoteza maisha ghafla.

Hata hivyo, mfanyabiashara huyo alipoongea na Uwazi juzikati alikanusha vikali tuhuma hizo na kueleza kuwa yeye ni muumini mzuri wa imani yake.

‘’Hao watu wanapotosha sana, unajua kuna mwaka mwanaume mmoja alikufa ghafla kwenye nyumba yangu ya kulala wageni, alikuja na mpenzi wake ila alimeza Viagra ambazo hata polisi walizikuta mezani.
“Sasa watu wasio na nia njema na mimi tukio hilo wanaliunganisha na hili kwamba nawatoa kafara,” alisema.

Kifo cha Blandina kilitokea ndani ya chumba huku mtu mmoja anayedaiwa kuwa mpenzi wake aliyejulikana kwa jina moja la Timo, mkazi wa eneo hilo akihojiwa na polisi.

Marehemu Blandina ambaye ni mzaliwa wa mkoa wa Tanga, anaelezwa na bosi wake huyo kwamba alikuwa kama mtoto wa familia yake kwa vile alimwamini sana. Alifanya kazi hapo kwa miaka 8 na hakuwa na tatilo la kiafya.

Bosi huyo alisema mwili wa marehemu uligundulika baada ya mfanyakazi mwenzake wa kiume kumpigia simu saa 2 asubuhi ambapo simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa ndipo alipoamua kwenda kumgongea katika chumba hicho.

Alisema baada ya kufika alishangaa kukuta mlango wa chumba chake uko wazi na alipochungulia alibaini kwamba Blandina alikuwa amefariki dunia.

Hata hivyo, polisi baada ya kufika na kuufanyia uchunguzi wa awali mwili huo hawakugundua kuwepo kwa jeraha lolote linaloashiria kuuawa, ingawa mwili huo ulipelekwa kufanyiwa uchunguzi wa kitaalam katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.

Jeshi la Polisi mkoani Arusha limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali hiyo.
GPL

ASKOFU BILIONEA ATIKISA BONGO

0
0
Stori: Jelard Lucas
ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchi  kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa’ iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake, Uwazi lina ushuhuda wa kutosha.

Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea.

Mbali ya kuwa na chopa iliyokuwa ikiimarisha ulinzi ambayo ameinunua hivi karibuni, askofu huyo alikuwa na msururu wa magari yenye thamani kubwa yanayomfanya kutajwa kuwa tajiri kuliko maaskofu wengine wanatoa huduma katika makanisa ya kiroho Tanzania.

Akiwa Karatu, mbali na ulinzi binafsi, Geordavie alikuwa akilindwa na askari wa jeshi la polisi, askari kanzu, Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na wale wa usalama barabarani.

Mbali na askari hao wa serikali ambao wamekuwa wakimlinda kila anapofanya mikutano yake, pia Geordavie analindwa na askari wake binafsi hali iliyowafanya baadhi ya watu kuamini kuwa ulinzi wake ni kama ule wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’.

“Sijawahi kumuona JK akilindwa na chopa lakini mtumishi wa Mungu Geordavie analindwa na ndege katika msafara wake! Hii ni mara yangu ya kwanza kuona,” alisema muumini mmoja ambaye hakupenda kutajwa gazetini.

Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji utajiri wa askofu huyo kutokana na fedha nyingi anazozitumia anapofanya mikutano katika sehemu mbalimbali jijini Arusha.

“Tunajua kuwa ni tajiri, lakini anapata wapi fedha za kutumia hivi?” alihoji muumini aliyejitambulisha kwa jina moja la Julius ambaye naye alihudhuria mkutano wa askofu huyo anayetumia kaulimbiu ya Ngurumo ya Upako katika kutoa huduma yake.

Pia, waumini wengine walilalamikia ugumu wanaoupata wanapotaka  kumuona mtumishi huyo wa Mungu kutokana na ulinzi mkali anaopewa.

“Kila mtu alitamani kumuona mtumishi wa Mungu lakini haikuwezekana kutokana na ulinzi wake kuwa mkali, utajiri wake hakuna mfano, hata kule nyumbani kwake Arusha, anaishi kama Mfalme Daud,” alisema Fred Mushi.

Gazeti hili lilimsaka Askofu na Nabii Geordavie kwa lengo la kutaka kujua sababu ya kuwa na ulinzi mkali na kutumia magari ya kifahari ikiwemo chopa katika mikutano anayoifanya lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Credits:Global Publishers

ANAYEONA POSHO YA BUNGE LA KATIBA HAITOSHI AFUNGASHE VIRAGO VYAKE

0
0
Dodoma. Wizara ya Fedha imepigilia msumari maombi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba ya kutaka waongezewe posho na kusema anayeona ameacha kazi inayomlipa zaidi kwenda bungeni afungashe virago na kuondoka.

Msimamo huo umekuja siku moja tu baada ya gazeti hili kudokeza kuwa madai ya wajumbe wa bunge hilo kutaka waongezewe posho kutoka Sh300,000 za sasa kwa siku, yamegonga mwamba baada ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza uhalali wake kusema kiwango hicho kinatosha.

Mwenyekiti wa muda wa bunge hilo, Pandu Kificho alisema jana bila kutaja viwango, kuwa ripoti ya kamati hiyo imewasilishwa kwa Rais Jakaya Kikwete kwa uamuzi.

Madai ya wajumbe kutaka waongezewe posho, yamechafua hali ya hewa ndani na nje ya Bunge, huku baadhi ya wananchi wakipaza sauti zao na kumsihi Rais Kikwete alivunje bunge hilo iwapo wajumbe watashikilia msimamo wa kutaka nyongeza ya posho.

Jana, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alisema wanaoshiriki kutunga Katiba ni Watanzania na siyo wataalamu washauri waliokodiwa kutoka nje.

Alisema kwa msingi huo, Serikali ilitarajia kuwaona watu hao wakitanguliza uzalendo zaidi badala ya kudai malipo manono.

“Katika kutengeneza Katiba hii, hatujakodi consultants (wataalamu washauri) kutoka Uingereza, Marekani, Kenya, Uganda wala nchi nyingine yoyote… Hawa ni Watanzania na kazi wanayoifanya ni yao,” alisema.

“Wangekuwa wataalamu wa kukodi wangeweza kudai malipo hayo, lakini hapa ni tofauti... wanafanya kazi yao na kila mtu anafanya kazi yake na anapaswa kujivunia kushiriki katika tendo hili la kihistoria kwa kutanguliza uzalendo,” alisema.

Nchemba alisema anazielewa hoja za baadhi ya wajumbe walioibua suala la posho, lakini kwa mtazamo wake, hoja hiyo hata kama ingekuwa na mashiko kiasi gani, imewasilishwa wakati usiokuwa mwafaka. Alisema wapo makandarasi na wazabuni waliotoa huduma kwenye taasisi mbalimbali za umma lakini hawajalipwa.

Alisema kwa kawaida, Februari ni mwezi mbaya kwa kuwa baadhi ya wilaya zina historia ya kukumbwa na uhaba wa chakula hivyo kuhitaji fedha nyingi za Serikali ili kuokoa maisha ya watu katika maeneo hayo.

Pia alisema si wakati mwafaka wa kudai nyongeza hiyo hasa ikizingatiwa kuwa kuna walimu wapya 30,000 nchini kote ambao hawajapangiwa vituo kutokana na kukosekana kwa fedha za kulipa stahiki zao.

Nchemba alisema mbali na walimu hao wapya kutokupangiwa vituo, walimu wengine wanadai malimbikizo ya fedha zao na kwamba hawajalipwa kutokana na ufinyu wa bajeti serikalini.

“Siku zote ukweli unauma. Nasema kama kuna mjumbe ambaye anaona huko alikokuwa kabla ya kuteuliwa alikuwa anapata pesa zaidi kuliko hii, basi kwa heshima afungashe virago na kuondoka,” alisema.

JE ULISHAWAHI KUWA KWENYE MAHUSIANO NA MTU ALIYEKOSEA NUMBER YA SIMU?

0
0
Kwa kawaida binadamu tumekuwa tukiingia kwenye mahusiano ya kimapenzi katika mazingira tofauti tofauti mfano kwenye daladala,kwenye mkusanyiko wa sherehe,kwenye mazingira ya kutafuta elimu n.k.

Nia na madhumuni kutaka kufahamu je ushawahi kuwa na mahusiano na mvulana/msichana aliekosea namba kwenye simu yako ?

Na kama ushawahi je mahusiano yenu bado yapo hai au mmekwisha achana na mwenzi wako ?

Karibuni wadau tuweze ku share experience

MWEE...WADAU HIVI ZILE SHULE ZA VIPAJI MAALUMU BADO ZIPO ?

0
0
Enzi mie nasoma palikuwa na shule za vipaji maalumu yaani tulikuwa tunasoma ili tuingie shule kama Tabora Boys,Mzumbe,Kibaha,Ilboru na Kilakala enzi izo zilikuwa ni shule maalumu kwa wanafunzi wenye akili ..aka vipaji maalumu .....na kweli yaani zilikuwa zinafaulisha balaaa....lakini siku hizi nasikia tu Marian Boys/Girls Sijui St nini mara Feza eti ndio zinaongoza kwa ufaulishaji , sasa swali langu je izo shule za vipaji maalumu bado zipo ??

SINTAH "NASHUKURU LE MUTUZ UMENISIKILIZA..ACHANA NA VINUKA MKOJO"

0
0

"Nashukuru umenisikiliza my ndugu Le Big show Le Mutuz nilikwambia na kila siku nikiongea na wewe nakwambia, achana na vinuka mkojo wa mitaani , unakaa na watu wasiongea mambo ya maana  kuanzia asubuhi wakiongea la maana ni ku snitch mtu, wewe ongea na matajiri wakuambukize harufu nzuri ya ankara sasa nakuona jinsi unavyo shine, mie tangu nijue hiyo kanuni sipati shida na mtu nni mwendo wa salamu, unacheka nao wabaya ni haohao, usnitch umetawala kila sehemu kazini, majumbani, kwenye familia seriously u dont know who to trust , ila umeniuzi mbona hukunichukua kwa Ken na mie nikatoe maada zangu si unajua beauty plus brain, usingekuwa disappointed, next trip usiniache....

Big up na endelea kunisikiliza utapata mengi ......"SINTAH

MASOGANGE BORA UKATE MAONO KAMA HIVI KULIKO KUUZA SEMBE

0
0
Week hii Mitandaoni zimetawala picha za Agness Masogange Mitandaoni Akicheza jukwaani huku akionehsa kiuno chake kwa chati kwenye ufunguzi wa Pub Moja huko Dodoma Its Obvious Alilipwa kwa kufanya hivyo tena si hela ndogo ...Mimi ki  ukweli kanifurahisha ni bora atumie kipaji chake na umbo lake kujipatia hela kwenye matamasha ama video mbali mbali kuliko ile ya kuuza Sembe aka Ungaz....Hongera Masogange......Au unasemaje mdau ?

MAPENZI YAPO WAPI SIKU HIZI? EMBU JIONEE MWENYWE HUYU ALIVYOPIGWA NA BOYFRIEND WAKE

0
0

Her name is Gabriella. Says she's an aspiring Victoria Secret model and actress. Not sure where she's from though. Gabriella, via her instagram account @bambiiiii_ shared her recent sad experience of domestic violence from her boyfriend of eight months. She was badly beaten, thrown from a moving vehicle and dragged. She shared this photo of her injury above on her instagram page and wrote:
"This might be a little graphic but I just want to let everyone know that I am okay. I am a survivor of domestic violence with a boy I dated for 8 months. I really thought everything was fine but he constantly questioned me about cheating and flirting. Nonsense. I never looked at someone the way he looked at me. Thought I loved this boy. How can someone that 'loves' me do this to me? The scars on my chest are way worse and extend down to my right nipple, completely scarred. The skin on my shoulder has been completely skinned. And I have bruising on my rib cage, neck, and my muscles. I was kicked out of a moving vehicle, then beaten and dragged, as I blacked out and was left lying there in my own puddle of blood. Doctors said I could have died if not made it when I did. I am so blessed and beyond lucky to be alive and have so much support from friends, family, and strangers. As I try to recover I ask to please keep me in your prayers. I have to wear a neck brace for 3-4 weeks, an arm cast and I can barely walk for now. Thank you for all the love. I hope to be an inspiration to women and anyone involved in domestic violence.
She didn't say what happened to the guy that did this. See pics of Gabby before the brutal attack after the cut ...

SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO MPYA WA WALTER CHILAMBO-MAVELA

0
0
Mshindi wa BSS wa Mwaka Juzi Walter Chilambo Ametoa Wimbo Mpya ...Embu Usikilize hapa Ukiupenda unaweza Udownload pia...

KOCHA WA AL AHLY AICHAMBUA YANGA KAMA KARANGA

0
0
Dar es Salaam. Kocha Msaidizi wa Al Ahly, Ahmed Ayoub ameichambua Yanga kwa kusema ni timu bora katika kushambulia, lakini si nzuri kwenye safu ya ulinzi.

Yanga itaivaa Al -Ahly Jumamosi hii katika pambano la raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika litakalopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mahojiano na mtandao wa klabu hiyo, Ayoub alisema, ushindi wa jumla ya mabao 12-2 ilioupata Yanga dhidi ya Komorozine ni uthibitisho kwamba safu yake ya ushambuliaji ni moto wa kuotea mbali.

Katika michezo 17 ya Ligi Kuu Tanzania Bara safu ya ushambuliaji wa Yanga imefunga mabao 41 na kuruhusu mabao 12 hadi sasa.

“Yanga ina safu ya ushambuliaji yenye nguvu kwani imefunga mabao 12 katika raundi ya awali ya Ligi ya Mabingwa ilipocheza na Komorozine ambayo matokeo ya jumla ni 12-2,” alisema Ayoub.

Aliongeza: “Ina kikosi chenye nyota watano wa kulipwa kutoka Congo, Rwanda, Burundi na Uganda ambao wana mchango mkubwa katika safu ya ushambuliaji.”

Pamoja na kusifia safu ya ushambuliaji ya Yanga, kocha Ayoub alisema atatumia udhaifu wa ngome ya ulinzi kupata matokeo mazuri.

Alisema beki ya Yanga si imara kwani haina ushirikiano wa kutosha miongoni mwa wachezaji wake husika.

“Timu ya Tanzania ina udhaifu katika eneo la ulinzi ambako kimsingi hakuna muunganiko mzuri wa wachezaji wanaocheza eneo hilo,” alisema Ayoub.

Kocha huyo alishuhudia pambano la kwanza kati ya Yanga na Komoriozine lililopigwa kwenye Uwanja wa Taifa.

Kauli ya kocha huyo ni changamoto kwa Kocha wa Yanga, Hans Van Der Pluijm kwani ni wazi anatakiwa kuisuka kikamilifu ngome yake ya ulinzi kabla ya mchezo kati yake na vigogo hao wa Misri.

Safu ya ulinzi ya Yanga inaundwa na mabeki wa kati Kelvin Yondani na Nadir Haroub pamoja na mabeki wa pembeni Oscar Joshua anayecheza kushoto na Mbuyu Twite kulia.

HIVI HAWA WATU WAPO DODOMA KUCHUKUA POSHO AMA KUANDIKA KATIBA?

0
0

Nina wasiwasi na uwakilishi wa baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, ninajiuliza je, wataweza kutimiza jukumu walilopewa na Watanzania na Rais Jakaya Kikwete la kusimamia mchakato wa kupata Katiba Mpya au la?

Wasiwasi wangu unasababishwa na jambo moja, kauli za baadhi ya wajumbe hasa ile ya kuanza kufikiria masilahi yao na kusimama kidete kutaka yatekelezwe bila kujali endapo yana athari kwa taifa. Wakiwa katika siku yao ya tatu, baadhi ya wajumbe walianza kuwatia kichefuchefu Watanzania kwa kulalamikia kiwango cha posho ya Sh300,000 na kutaka kiongezwe ili walau kifikie Sh500,000.

Ikumbukwe kuwa kila mjumbe wa bunge hilo anapokea Sh300,000 kama posho kwa siku awapo katika kikao cha bunge hilo.

Jambo baya zaidi ni kuwa wakati baadhi ya wajumbe wa bunge hilo wakidai nyongeza ya posho, tayari Watanzania walishaanza kuhoji iweje wapewe kiasi kikubwa hicho cha pesa.
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images