Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Dkt. Kigwangala Amtembelea na Kumjulia hali Mwadhama Kardinali Pengo.

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamis Kigwangala jana alimtembelea na kumjulia hali Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Kadinali Polycarp Pengo aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliyopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Akiongelea kuhusu hali ya Kadinali Pengo, Mhe. Kigwangala alisema kuwa Kadinali Pengo yuko salama katika mikono ya madaktari wa taasisi hiyo na hali yake inaendelea vizuri ambapo ameweza kuongea nae ana kwa ana kiasi cha kuweza kukaa na kuongea.

‘’Mwanzoni alilazwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo hapa jijini Dar es Salaam, lakini ikaonekana ni vema akiletwa hapa kwenye Hospitali yetu hii ya juu kabisa ya matibabu ya moyo (Tasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete), hivyo napenda kuwapa taarifa Watanzania kwamba yuko salama kabisa katika mikono ya madaktari wetu na hali yake inaendelea vizuri.’’

Awali Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli akiongozana na Mkewe mama Janeth Magufuli walienda pia kumjulia hali Kadinali Pengo katika taasisi hiyo na kumtakia afya njema ili aweze kuendelea na shughuli zake za kiroho.

Kadinali Pengo alifikishwa katika taasisi hiyo ya moyo kwa ajili ya kuchunguzwa afya yake ambapo afya yake kwa sasa imezidi kuimarika.

Hapa  kuna  video  nzima ya Dr. Kigwangala  akimjulia hali


Bootylicious Socialite, Vera Sidika Flaunts Her Expensive Hotel Room in Las Vegas (PHOTOs)

$
0
0

Bootylicious socialite, Vera Sidika, is on a vacation in the US and just to prove that she is the true boss lady, she took to social media and flaunted the expensive hotel where she is spending her nights.

Vera has booked one of the high end hotels in Las Vegas but this is catered for by her wealthy sponsors.

This is how Vera is rolling in Las Vegas.


Bajeti ya Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar Yatengwa.......Kinachosubiriwa ni ZEC Kutangaza Tarehe Ya Uchaguzi

$
0
0
Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema bajeti ya uchaguzi wa marudio imeshatengwa na wanachosubiri ni Mwenyekiti wa Tume ya  Uhaguzi Zanzibar (ZEC) atangaze tarehe hiyo ya kufanya uchaguzi.

Amesema bajeti hiyo haitatofautiana na ile iliyotumika katika uchaguzi wa Novemba 2015 iliyofikia karibu ya shilingi bilioni saba.

Amekanusha kauli kuwa uchaguzi huo hautafanyika kwa vile matokeo yanayolazimisha kutangazwa na CUF yameshafutwa kwa mujibu wa sheria kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Miaka 52 ya Mapinduzi, Balozi Seif amesema mazungumzo yanayoendelea ni ya kuhakiksha amani inaimarika Zanzibar na si suala la uchaguzi uliofutwa.

Akizungumzia kuhusu maadhimisho ya miaka 52 sherehe za Mapinduzi Balozi Seif amewabeza wanaosusuia sherehe hizo kwa madia kuwa Rais Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein kuwa si halali ni upotoshwaji mkubwa.

Amefahamisha kuwa rais huyo yupo kihalali na hata mawaziri wake wote na watamaliza ukomo wao atakapoapishwa rais mwingine kama ilivyoanishwa katika kifungu cha 28 (1) a cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na si kama inavyeleezewa kuwa ukomo wake umeisha tangu tarehe 2 Novemba.

Tazama video hii kumsikia akiongea na kujibu maswali ya waandishi kuhusu marudio ya uchaguzi Zanzibar.

Is Navy Kenzo From Tanzania Taking Over The spotlight in The Music Industry

$
0
0
Navy Kenzo Music group which is composed of Aika and Nahreel have continued to shine in Tanzania and across Africa.

They have been the only Duo to represent Tanzania to Africa and the World,With their Video Game Featuring Vanessa Mdee Being announced as the Number Four in the list of  top 50 Best Videos that performed well in 2015 on the MTV Base Africa.

Diamond Platnumz and his song Nana was holding number 5 In the chat.Nana was also produced​ by non other than than the music Prodigy Nahreel Which still makes him the finest producer to ever exist in Tanzania in this era and East Africa in general.

The singer Wizkid of Nigeria Held No. 6 .

Congratulations goes to them @nahreel , @aikanavykenzo the heads of Navy kenzo

Expect Great Things From Them this year and The Industry Studios In General

Jee Mnatambua Kuwa Baadhi ya Maamuzi ya Magufuli, Yanaligharimu Taifa Kiuchumi?

$
0
0
Kuna watu wanashangilia sana kila kinachofanywa na Magufuli, wakidhani ndio the right thing!. Mfano alipoamua kuunda baraza dogo la mawaziri, na kuongeza idadi ya makatibu wakuu, badala ya kupunguza gharama, kutaongeza ghara za uendeshaji!, serikali ni makaribu wakuu ambao ndio waendeshaji, na sio mawaziri!.

Mfano wanaposikia maofisa wakuu fulani wa umma, wamesimamishwa kazi, na kuteuliwa wengine kukaimu nafasi zao!. Hatua hii kisiasa ni nzuri, maana ina mpa kick Magufuli kwa boost political mileage yake, ila kiuchumi, Magufuli analibebesha taifa hili mzigo kubwa kuliko hata serikali ya JK!.

Kwa mujibu wa sheria za kazi, kila mtumishi aliyesimamishwa kazi kwa tuhuma zozote, anaendelea kulipwa mshahara wake kamili, bali maupurupu ndio yanaondolewa!.

Mtumishi atalipwa nusu ya mshahara iwapo atasimamishwa kazi na kushitakiwa, na mtumishi hatalipwa lipwa mshahara iwapo atafukuzwa kazi!.

Tangu Magufuli aanze hii timua tumua, hakuna ofisa mkuu yoyote aliyefukuzwa, wala aliyeshitakiwa, wate wamesimamishwa tuu kusubiri kupangiwa kazi nyingine!, wote wanaendelea kulipwa mishahara yao ile ile!.

Hata upande wa uteuzi wa Makatibu Wakuu, wale makatibu wakuu wote ambao ukatibu wao mkuu haukutenguliwa, wanaendelea kulipwa mishahara ya makatibu wakuu kusubiri kupangiwa kazi nyingine!.

Hivyo baadhi ya hatua zinazochukuliwa na rrais wetu John Pombe Magufuli, japo ni hatua nzuri, na zimefanywa kwa nia njema, zitaligharimu sana taifa hili!, ni bora Magufuli angefuata ule mtindo wa Nyerere, ilikuwa hakuna kusimamisha kazi, ilikuwa ni kufukuza tuu!. Anapounda baraza jipya na kutea makatibu wakuu wapya, wale wote walioachwa, walikuwa wanastaafishwa kwa manifaa ya umma na mishahara yao inasimamishwa kuanzia hapo!.
Happy New Year

By Pasco-JF

Dk Makongoro Mahanga Amvaa Rais Magufuli Kwa Kuunda Serikali Kubwa Tofauti Na Ahadi Yake Aliyoitoa wakati wa Kampeni

$
0
0
Wakati watu mbalimbali wakimminia sifa Rais John Magufuli kwa kubana matumizi, aliyekuwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk Makongoro Mahanga amesema uwingi wa makatibu wakuu unakinzana na dhana ya yake ya kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri.

Dk Mahanga alikuwa Naibu Waziri wa Lazi na Ajira tangu mwaka 2008 na hakuwahi kuhamishwa wala kupandishwa hadi ngazi ya uwaziri hadi Serikali ya Rais Jakaya Kikwete ilipomaliza muda wake na baadaye kujiunga na Chadema.

Katika waraka wake alioutoa kwenye mitandao ya kijamii, Dk Mahanga alimkosoa Rais Magufuli akisema ameongeza ukubwa wa Baraza la Mawaziri baada ya kuteua makatibu wakuu 27 wakati anawaaminisha wananchi kwamba wizara ni 15 tu.

Dk Magufuli ameunda baraza lenye mawaziri 15, na manaibu waziri 19 na hivyo kufanya baraza lake kuwa na jumla ya mawaziri 34, tofauti na baraza lililopita lililokuwa na mawaziri 55.

Uamuzi wa kupunguza idadi ya wizara ulikumbana na changamoto ya nafasi za makatibu, ambao hata hivyo baadhi amewarudisha wizarani ambako watapangiwa kazi na kubakiwa na makatibu 27.

Si kweli kwamba kapunguza ukubwa wa Serikali, bali kaongeza ukubwa wake. Sina hakika kama wasaidizi wa Rais wamemshauri na kumweleza kwamba wizara si ofisi ya waziri bali wizara ni ofisi ya katibu mkuu,” alisema Dk Mahanga akifafanua kuwa katibu mkuu ndiye mtendaji mkuu wa wizara na afisa masuhuli.

Alisema katibu mkuu ndiye mwenye dhamana ya utendaji na ndiyo maana hata katika ngazi ya kata, ofisi inaitwa ofisi ya ofisa mtendaji wa kata na si ofisi ya diwani.

Kwa maana hiyo, Dk Mahanga, ambaye kitaaluma ni mhasibu, alisema Rais alipounda Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, ambazo awali zilikuwa mbili tofauti na kuteua makatibu wakuu watatu, kiuhalisia hakuunganisha wizara mbili kuwa moja bali ameunda wizara tatu kutoka mbili za awali.

Ongezeko la gharama kwa kuongeza waziri mmoja ni ndogo sana kulinganisha na kuongeza katibu mkuu mmoja. Waziri anapoteuliwa tayari anakuwa ni mbunge mwenye mshahara wake wa ubunge na kinachoongezeka ni kama laki tano tu juu ya ule mshahara wa ubunge na gharama nyingine ndogo za gari, pia mishahara na gharama za katibu muhtasi, msaidizi na dereva,” alisema Dk Mahanga.

Alisema kwa ujumla ahadi ya Rais Magufuli aliyotoa kwenye kampeni kwamba ataunda Serikali ndogo, hakuitimiza badala yake ameongeza ukubwa wa Serikali.

Wakati wa kampeni na alipoapishwa, Rais Magufuli alisema ataunda baraza dogo la mawaziri, hiyo ilijenga shauku kwa wananchi kufahamu kiwango cha ukubwa au udogo wa baraza hilo ikilinganishwa na mabaraza yaliyoundwa na watangulizi wake, tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961.

Dk Magufuli pia alitoa ahadi hiyo alipozindua Bunge Novemba mwaka jana mjini Dodoma.

Ikulu Yaagiza Mtumishi Atakayefanya Kosa Aadhibiwe Hapohapo Alipo Badala Ya Kuhamishiwa Sehemu Nyingine ya Kazi

$
0
0
MAKATIBU Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu walioteuliwa na kuapishwa juzi wamekutana katika ukumbi wa mikutano wa Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya semina elekezi iliyoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

Akizungumza kabla ya kuanza kwa mada zilizoandaliwa katika semina hiyo  jana, Katibu Mkuu Kiongozi Sefue, alisema semina hiyo ni ya kikazi zaidi na kwamba lengo la serikali ni kuhakikisha viongozi hao waandamizi wanatekeleza wajibu wa kusimamia utendaji kazi wa serikali vizuri.

Balozi Sefue alisema kila Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu anapaswa kutambua kuwa nafasi yake ni ya maamuzi, hivyo serikali inatarajia kuona wanafanya maamuzi kwa usahihi na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazomuongoza kila mmoja katika majukumu yake.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano inawatarajia viongozi hao kuwa wasimamizi wazuri wa fedha za umma na kwamba haitarajii kuwepo kwa hati za ukaguzi wa mahesabu zenye kasoro.

Balozi Sefue aliongeza kuwa Makatibu Wakuu hao na Naibu Makatibu Wakuu ni mamlaka ya nidhamu katika wizara zao, hivyo serikali haitarajii kuona wanakuwa na kigugumizi katika kuchukua hatua dhidi ya watumishi watakaokuwa na makosa.

Aliwakumbusha pia kwamba haikubaliki kwa mtumishi aliyefanya makosa katika sehemu moja ya kazi, kuhamishiwa katika sehemu nyingine badala ya kuchukuliwa hatua palepale alipo.

Breaking News:Daraja la Flyover Limeanza Kujengwa Makutano ya Tazara...

$
0
0
Naam, ujenzi wa flyover pale TAZARA jijini Dar umeanza kama ilivyoahidiwa.

Tutarajie kupata kitu imara toka kwa wajapani?

Rais MAGUFULI AMPINGA Balozi Sefue Live!!

$
0
0
Katika hali inayoonyesha utendaji wa Rais Magufuli ni wa ufuatiliaji wa karibu, juzi alifuta utaratibu wa protokali uliokuwa umetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue na kuagiza itumike njia yake, wakati wa hafla ya kuapisha Makatibu Wakuu na Makatibu Wasaidizi wapya wa wizara mbalimbali aliowateua hivi karibuni.
Makatibu wakuu na manaibu wao walifika Ikulu kwa ajili ya shughuli ya kuapishwa kushika nafasi zao na baadaye kusaini kiapo cha uadilifu kilichoongozwa na Naibu Kamishna wa Maadili, Waziri Kipacha.

Mara baada ya Kamishna huyo kusoma kiapo hicho kwa niaba ya makatibu wakuu na manaibu hao, Katibu Mkuu Kiongozi aliwataka makatibu wakuu na manaibu hao kila mmoja asaini katika hati aliyopewa.

Utaratibu huo uliotangazwa na Balozi Sefue ulionekana kutomridhisha Rais Magufuli ambaye katika hali ambayo haikutarajiwa, aliinuka kutoka sehemu aliyokuwa amekaa na kutoa utaratibu tofauti.
Hapana huwezi kula kiapo kwa niaba ya mtu mwingine wakati wenyewe wote wapo hapa, kila mmoja aape kwa mdomo wake mwenyewe na kusaini," alisema Rais Magufuli na kutoa angalizo:
"Kama kuna mmoja wao hajakubalina na kifungu kwenye hati hii tutajuaje?

Kama yupo Katibu Mkuu au Naibu Katibu Mkuu anayeona kuwa hataweza kutekeleza mojawapo ya vifungu vilichopo katika hati hiyo ya maadili akae pembeni atuache wengine tuendelee.”

Breaking News: Fundi Seremala Auawa Kinyama na Kutumbukizwa Kwenye Shimo la Choo Mkoani Geita

$
0
0
Mwili wa marehemu John Mohammed baada ya kutolewa kwenye shimo la choo.
Mtu mmoja mkazi wa kata ya Nyankumbu wilayani na mkoani Geita ajulikanaye kwa jina la John Mohammed (33) kabila Mhangaza (fundi seremala) amekutwa akiwa ameuawa usiku wa kuamkia leo tarehe 01/01/2016 na watu wasiojulikana na kutupwa kwenye shimo la choo cha nyumba ya wageni iitwayo MWIBARA GUEST HOUSE iliyopo mtaa wa Elimu katika kata ya Nyankumbu Wilayani Geita.


Baba mzazi wa Marehemu Mohamed Ibrahimu akiongea na Blog hii amesema kuwa"kutokana na maelezo niliyoyapata kutoka kwa mtoto wa dada yangu ambaye alikuwa amekuja huku kwa lengo la kufundishwa kazi ya Useremala na mtoto wangu(marehemu) ni kwamba jana jioni walikuwa wanakunywa uji na watu wengine katika kijiwe kimoja jirani na mazingira yake ya kazi,mtoto wangu akamwambia huyu kijana mtoto wa dada yangu kuwa tangulia nyumbani,akabaki yeye akikusanya vifaa vyake sasa amekwenda nyumbani yule kijana hakumwona tena na kwa kuwa ilikuwa ni usiku na huku ni mgeni hakuweza kurudi kumtafuta,leo asubuhi amekuja amekuta hapa wanapofanyia kazi kuna kofia yake huyu binamu yake halafu kumetapakaa damu,sasa ndio akaanza kutoa taarifa,na pia akanipiagia simu nikawa nimekuja kwa hiyo kwa kweli siwezi kusema namhisi mtu fulani maana mi mwenyewe nipo kwenye mshangao."


Naye Bwana Hassan Malima ambaye ni mwenyekiti wa mtaa wa Elimu amesema kuwa"mimi nimekuja hapa saa moja asubuhi baada ya kupigiwa simu kuwa kuna damu nyingi sana hapo katika kijiwe cha fundi seremara inawezekana kuna tukio,ndipo tukafika pale tukaiona ile kofia ya fundi,basi tukaanza kufanya utafiti kwa kuzunguka baadae mimi niko upande wa kule juu wakanipigia simu wakaniambia njoo huku inaonekana mwili umo humu kwenye shimo la choo basi ndipo nikaja tukaona mguu na ndipo nikaondoka na kwenda kuripoti polisi."

Matukio ya mauaji mkoani Geita yamekuwa yakijirudia mara kwa mara,itakumbukwa Julai 23,2015 kuna mlinzi aliuawa maeneo ya Nyarugusu na watu wasiojulikana,mei 4,2014 mlinzi wa kampuni ya K.K SECURITY aliuawa kwa kuchinjwa akiwa eneo la kazi yake,Machi 17,2015 mlinzi mwingine aliuawa na mwili wake kufichwa ndani ya jokofu la bar,Novemba 14,2015 aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita Alphonce mawazo aliuawa mjini katoro kwa kukatwa mapanga na watu wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa CCM,mbali na orodha hiyo pia kumekuwapo na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi(albino).

PAULBAHEBE BLOG inaliomba jeshi la polisi mkoani Geita kufuatilia kwa makini ili kuweza kung'oa mzizi wa wahalifu

KIMENUKA Kwa Sumaye Wananchi Wavamia Shamba Lake na Kujimilikisha na Kufanya Haya

$
0
0
Wananchi zaidi ya 100, wakiwemo waliobomolewa maeneo ya mabondeni jijini Dar es Salaam, wamevamia shamba la Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye lenye ukubwa wa heka 33, lililopo Mji Mpya eneo la Mabwepande na kujikatia viwanja.

Sumaye ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa serikali ya awamu ya tano kati ya mwaka 1995 hadi 2005, amekiri wananchi kuvamia shamba hilo lakini alisema hana wasiwasi kwasababu ana hati za umiliki.
Aidha alisema atafuata mkondo wa sheria kuhakikisha wavamizi hao wanaondoka kwenye shamba lake.
Juzi Nipashe ilishuhudia wananchi kadhaa wakiendelea kujenga nyumba za miti na wengine za matofali baada ya kujigawia kila mmoja eneo lake kwenye shamba hilo.

Musa Juma, aliyekutwa kwenye shamba hilo akijenga nyumba, alisema yeye ni miongoni mwa waathirika wa bomoa bomoa iliyofanyika Kinondoni Mkwajuni na kwamba amefika hapo baada ya mwenzao aliyemtaja kwa jina moja la Ema kuwaeleza kuwa kuna pori la Sumaye alilolitelekeza.
“Mwenzetu Ema alikuja kule bondeni tulikobomolewa na kutupa habari hiyo hivyo watu kama 100 tukaamua kuja na tukawakuta wengine tuliliona shamba hili likiwa ni pori kubwa ndipo tukaanza kujigawia vipande vipande,” alisema.

“Tumefanya kazi kubwa ya kulifyeka mpaka unaliona lipo katika hali hii, kazi haikuwa ndogo dada yangu, tumekutana na nyoka wakubwa, ukishuka kule bondeni kwenye kingo za shamba utajionea mwenyewe jinsi pori hili lilivyokuwa.” 
Juma alisema walivamia shamba hilo mwezi Oktoba mwaka jana, na wengine walikuja baadaye baada ya kupata taarifa kuwa kuna shamba la bure ambalo limetelekezwa akiongeza kuwa wako pia watumishi wa serikali waliovamia shamba hilo.

“Aliwahi kuja mwanamke mmoja ambaye hatumfahamu akidai kuwa yeye ni mke wa kiongozi huyo na kutueleza kuwa tunapaswa kuondoka eneo hili eti ni mali yao lakini juzi kaja mwenyewe Sumaye; akatusalimia na kuondoka bila kusema lolote,” alisema.
“Mwamamke yule alikuja na watu wengine akiwemo mtu ambaye alikuwa akipiga picha na baadaye aliondoka hadi Alhamisi ya wiki hii walivyokuja wote na Sumaye mwenyewe ingawa hakusema lolote mpaka anaondoka hapa.

“Sumaye alikuja kwa sababu Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, aliitisha mkutano na wananchi wa hapa, lakini tukiwa tumekusanyika tukimsubiria Makonda ghafla alifika Sumaye, ambaye hakushuka kwenye gari lake, alitusalimia kwa kutunyooshea mikono na kuondoka kwasababu Makonda hakuja siku hiyo.”
Alipoulizwa sababu za kuvamia shamba hilo, alisema walimsikia Rais John Magufuli kwenye kampeni akisema kuwa mashamba yote ambayo hayajaendelezwa yarudishwe serikalini na wapewe watu wenye uwezo wa kuyaendeleza.
Juma alisema wamejigawia shamba hilo na sasa wanasubiri serikali ije kuidhinisha kwa kuwamilikisha wao.

“Mtu anahodhi shamba kubwa kama hili halafu halijapimwa, tumetafuta alama za mipaka hakuna, wakati mashamba yote yaliyolizunguka shamba hili yamepimwa,” alisema.
Sumaye alisema anamiliki shamba hilo kihalali na ana hati zote na kwamba upo utaratibu wa kuchukua mashamba yaliyotelekezwa lakini sio huo walioutumia wananchi hao.
“Shamba hatujalitelekeza kama wanavyodai hao wananchi, tuna hati na ni letu kihalali, wanasema halina alama za mipaka je, waulize hati nilipataje? Shamba lina alama labda kama wamezing’oa kwa sababu ya jeuri.” 

Sumaye alisema juhudi za kuhakikisha shamba hilo linarudishwa mikononi mwake zimeanza kufanyika na mamlaka husika na kusisitiza kuwa hatatumia nguvu kuwaondoa zaidi ya kufuata sheria.
Kuhusu kuonekana eneo hilo siku ya Alhamisi, Sumaye alisema alienda huko kwa sababu Makonda aliitisha mkutano na wananchi ili kutafuta suluhu ya mgogoro huo lakini hakufika baada ya kupata udhuru.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Jastine Chiganga, alisema alipigiwa simu na Makonda akimweleza kuhusu mkutano huo lakini hakuweka bayana sababu za kuuitisha, ingawa aliuahirisha baada ya kupata dharura.

Makonda alilipoulizwa kuhusu lengo la mkutano aliouitisha na baadaye kuuairisha, alisema lilitokana na ofisi yake kupokea malalamiko ya uvamizi wa mashamba unaofanywa na wananchi eneo hilo.
Alisema baada ya kupokea malalamiko hayo aliomba kukutana na viongozi wa mitaa husika, wananchi, watu wa ardhi na wamiliki wa mashamba hayo ili kujua ukweli kuhusu mgogoro huo.
“Hilo shamba linalodaiwa kuwa ni la Sumaye, sijawahi kupokea malalamiko kutoka kwake dhidi ya uvamizi huo ila niliwahi kupigiwa simu na mmoja wa Makamanda wa Polisi Mkoa ambaye alinieleza kuhusu uvamizi huo,” alisema.

Aidha, Makonda alisema mbali ya shamba hilo la Sumaye yapo mengine likiwemo la Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), marehemu Daudi Ballali ambalo nalo limevamiwa.
Alisema mkutano wake aliouitisha ulilenga kwenda kupata taarifa kamili ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Makonda alitoa wito kwa watu wanaodai ni wamiliki halali wa mashamba yaliyovamiwa wajitokeze katika mkutano atakaouitisha wiki ijayo eneo hilo ili ufumbuzi uweze kupatikana.

Wema Sepetu: Sina Mpango wa Kuzaa

$
0
0
Katika page yake ya instagram, staa mrembo Wema Sepetu aka Madame amewataka wote wanaompigia kelele kuhusu kuzaa mtoto wamkome, kwani hana mpango huo kwa sasa. Hiki ndicho alicho kiposti

“Okay… Lets get things straight here…. See dat doggie up there… Y’all see her….? Dat is my bebi…. since i dont have a bebi… Huyo ndo mtoto wng… Basi sasa nitapopost afu nisikie kuzaa nakublock fasta… Mshaniona sizai basi ndo mjue sizai… Akha…!! Zaa zaa… If u have a child im happy for u… Nd wish u da best… I dont… Ndo mungu alivyonipangia… So please hey…. Watakaozaa all da best… Walio na mipango ya kuzaa hongereni… Mimi sina … Im done… Vanilla ndo bebi wangu kipenzi na nampenda kuliko…. Na wale wa subhannah llah pia nisiwaone… This is getting too personal sasa…

Top 6 Major Celebrity Sex Scandals Of 2015 In Kenya. Number 3 Have Been Involved In Two Sex Scandals This Year (Photos)

$
0
0

2015 has had its share of gripping sex scandals that have kept Kenyans ‘entertained’ for the last 365 days.
As the year ends today, we decided to shed light on some of the hottest sex scandals that shook 2015 to its roots.


1.Creme De La Crème Sex Tape
This was the mother of all scandals, one of Kenya’s dopest mix masters was caught on camera smashing, oh sorry, being rode by Halima.

Most ladies who watched the tape agreed Crème needed to up his game, it was Halima who did most of the smashing while Crème was only moaning like an abandoned puppy.

 2. Waiguru
It was Machakos Senator, Johnson Muthama, who enlightened the country that former Devolution CS was the President’s side dish at the infamous CORD public rally held at Uhuru Park on September 23rd 2015.

The Senator said the only reason why the head of state had refused to sack Waiguru when all fingers were pointing at her in the NYS scam was because she was involved in all manner of debauchery with Uhuru.

Of course the President vehemently denied the rumor while addressing a political crowd in Narok County. He advised his detractors to go ahead and acquire themselves extra wives if at all they were dissatisfied with their current wives.




3. Nouhom Cheick Kone
This one has been implicated in two major sex scandals. It seems the Mali actor has blood that boils at an alarming rate at the sight of them ladies.

Kone was stupid enough to record himself devouring a little known girl in a public toilet at a popular Nairobi bar.


The video went viral and because we are not a porn site, we couldn’t embed it unfortunately.

4. Bro Ocholla


Does Embakasi Prayer Cell ring a bell?? A brother committed the blunder of the year by hitting on a female faithful on a Whatsapp prayer group.

Bro Ocholla, a married ninja, unleashed his Team Mafisi side and attacked a female faithful with sexually explicit imagination that caught the attention of the whole nation.

Corporates cashed in on Ocholla’s misfortunes making the brother trend for days.


5. Habida


Her case was the first major sex scandal in 2015 that involved a celebrity. The sultry songstress was caught pants down having illicit sex with actor, Nouhom Cheick Kone, at his house in Roysambu.

Kone’s girlfriend sounded the alarm the moment she walked in her boyfriend having sex with Habida in the living room.

The story went viral despite numerous attempts by Kone and his contacts trying to kill it. Then again you can’t bribe all blogs.



6. Hon. Joyce Lay And Hon. Elisha Busienei


It was the first incident of sexual advances in parliament in 2015. Members of the Defence and Foreign Affairs Committee accompanied President Uhuru to Tokyo, Japan and that’s when the Turbo MP used the opportunity to prey on the prettiest legislator.

The Taveta Woman Representative said they were booked on the same floor with Busienei and as she was talking to her Kitui counterpart, Nyiva Mwendwa, Busienei went and stood at her door, barring her way into her own room. That incident happened on March 18th.

Lay rejected Mr. Busienei advances and the Turbo MP reacted by attacking her with itchy words to prove he was a typical Kalenjin bull.

"When I tell him to move away from my door he tells me that ‘hujui mimi ni Kalenjin’, then he told me ‘you are so useless’," Lay was quoted as saying.





Ole Sendeka Amjibu Dk Makongoro Mahanga ....Asema Makatibu Wakuu na Manaibu wao Sio Wajumbe Wa Baraza La Mawaziri

$
0
0
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM na mbunge wa zamani wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka amewataka watanzania kuwa makini na kuzipuuza kauli zinazoenezwa na baadhi ya watu  kwenye mitandao kuwa serikali ya Dk John Magufuli imekuwa na baraza kubwa la mawaziri kuliko alivyo ahidi na kwamba serikali inaweza kuwa nagharama zaidi kwakuwa kauli hizo zinalengo la kufifisha juhudi za serikali ya awamu ya tano kufanya mabadiliko ya kiuchumi kwa watanzania.

Mwanasiasa huyo mkongwe aliyekuwa mjumbe wa kamati ya kampeni ya CCM katika uchaguzi mkuu uliopita amesema kimsingi Raisi Magufuli anatembea kwenye ahadi alizo zitoa za kuifanya Tanzania kuwa mpya na kikatiba makatibu wakuu na manaibu wao siyo wajumbe wa baraza la mawaziri kama inavyo potoshwa na baadhi ya watu.

Hivi karibuni,aliyekuwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira katika serikali ya awamu ya nne , Dk Makongoro Mahanga alisema uwingi wa makatibu wakuu unakinzana na dhana ya Rais Magufuli  ya kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri.

Mahanga alimkosoa Rais Magufuli akisema ameongeza ukubwa wa Baraza la Mawaziri baada ya kuteua makatibu wakuu 27 wakati anawaaminisha wananchi kwamba wizara ni 15 tu.

Ni Nani Anayemdanganya Edward Lowassa? Mwacheni Basi Akachunge Ng'ombe wake Monduli!

$
0
0
Dunia inatambua Lowassa ana utajiri wa kifikra kuhusu njia ya kuwa fisadi nchini Tanzania. Kinachoendelea kwa sasa kinadhihirisha Lowassa anahitaji huruma za kisiasa kutokana na mwenendo wake kisiasa. Anahitaji sana ushauri usio wa kinafiki kuhusu hatima yake kisiasa nchini.

Nilivyomsikia kwa mara ya kwanza akitoa madai kuwa ukimya wake baada ya Uchaguzi Mkuu umesababisha kuwepo amani nchini, nilidhani kinachomsumbua ni mihemko ya kisiasa.

Nilipomsikia pia kwa mara ya pili akitamka maneno hayo Mkoani Arusha wakati akishiriki katika kampeni za Uchaguzi wa Jimbo la Arusha ambao uliahirishwa katika siku ya Uchaguzi Mkuu baada ya kifo cha mgombea wa ACT-wazalendo Estomih Mallah sikushangaa sana.

Kilichonishangaza zaidi ni pale nilipomuona tena kwa mara ya tatu ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Usharika wa Monduli akisema kunyamaza kwake baada ya wananchi kupiga kura kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 kumewafanya wananchi wasiuane. Eti anadai wananchi walikuwa wanasubiri neno lake ili waingie barabarani na kuanza kuuana.

Lowassa anataka kutuambia watanzania wengi ni kama nyumbu kwamba kila atakalolisema watalifuata au kulitenda. Anataka kutuambia watanzania wengi wanafanya mambo yao kwa kutegemea kauli zake. Anadhani yale aliyokuwa anayaita mahaba kwenye mikutano yake ni unyumbu.

Hawa watu wanaomshauri Lowassa waache kumdanganya. Kuna baadhi ya watu wanamjaza ujinga ili adhani ana hekima na busara zaidi ya Watanzania wengi.

Lowassa na wapambe wake hawafahamu kama watanzania wengi wana haiba ya kutopenda vurugu. Hafahamu kama kuna chaguzi kuu nne zimefanyika na Tanzania imeendelea kuwa nchi ya amani na kuheshimiana. Hafahamu utawala wa machifu uliokuwa na nguvu kubwa (powerful influence)katika jamii nchini ulipigwa marufuku na Tanzania ikaendelea kuwa na amani na kuheshimiana. Hafahamu tuna makabila zaidi ya 120 yenye imani za kidini tofauti lakini yanaishi katika msingi wa kuheshimiana na undugu.

Lowassa na wapambe wake wangetafuta kwanza uzoefu kuhusu haiba ya Watanzania kutoka wapinzani ambao wamekuwa katika uwanja wa upinzani kabla yeye hajawaza/kufikiria kama kuna siku atakuja kuwa mpinzani wa serikali ya CCM.

Kinachoonekana kwa sasa Lowassa yuko katika safari ya kisiasa ambayo Augustino Mrema amepitia! Lowassa has gone from hero to zero! As a politician, he is finished. There is no way back for him.

Ni nani anamshauri Edward Lowassa? Mwacheni akachunge ng'ombe wake Monduli!

By MsemajiUkweli-JF

Gigy Money Adaiwa Kulala na Msanii Kutoka Nigeria, Tekno Miles na Kufanya yao Hotel ya Serena, Mwenyewe Adai Hajali....

$
0
0
Siri imefichuka! Muuza nyago kwenye video za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ ameibua gumzo baada ya ukweli kuanikwa kwamba alilala kwenye Hoteli ya Serena iliyopo Posta jijini Dar akijiachia na msanii kutoka Nigeria, Tekno Miles.

Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika, usiku wa kuamkia Ijumaa, mrembo huyo alionekana akijiachia na jamaa huyo ambaye alitua Bongo kwa ajili ya kutumbuiza kwenye Ukumbi wa King Solomon uliopo Namanga jijini Dar.

Kama hiyo haitoshi, ilidaiwa kwamba, katika kudhihirisha hilo, Gigy alitupia picha kadhaa kwenye mitandao ya kijamii akiwa na Tekno hivyo kupewa makavu laivu na mashabiki wakionesha kwamba kitendo hicho ni kujidhalilisha kwa kumshobokea staa huyo wa Ngoma ya Duro.

Kufuatia ishu hiyo, gazeti hili lilimsaka Gigy ili afunguke juu ya tukio hilo ambapo alikiri kukutana na kulala na jamaa huyo hotelini hapo. “Wanaoponda waache waongee tu, mimi sirembi hata kidogo pale ninapotaka jambo langu litimie, ingekuwa nimegharamia kulipia hoteli sawa, lakini sijahusika hata kidogo na hilo, wamelipa wenyewe,” alisema

Nafasi za Kazi 

Waziri Mbarawa Atoa Siku Tatu Ukarabati Reli Ya Kati Iliyosombwa na Mafuriko

$
0
0
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka watendaji wa Shirika la Reli nchini (TRL) na Kampuni Hodhi ya Mali za Reli (RAHCO) kuhakikisha sehemu ya reli iliyosombwa na mafuriko wilayani Kilosa mkoani Morogoro inaunganishwa ndani ya siku tatu na huduma za treni kurejea.

Prof. Mbarawa amesema hayo baada ya kukagua sehemu ya reli hiyo kutoka Kilosa hadi Magulu- Kidete kuona athari zilizosababishwa na mafuriko yaliotokana na mvua zilizonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma.

“ Fanyeni kazi usiku na mchana ili ikifika alhamisi mawasiliano ya reli kati ya mkoa wa Morogoro na Dodoma yawe yamerejea na abiria waendelee kupata huduma ya treni ,” amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Amewahakikishia wananchi wa vijiji vya Munisagara, Mkadage, Mzaganza, Magulu na Kidete ambao usafiri wao pekee wa uhakiki ni wa kutumia reli watoe ushirikiano kwa serikali ili ukarabati na ujenzi wa reli hiyo ukamilike kwa haraka.

Amewataka wananchi waishio pembezoni mwa reli katika wilaya ya Kilosa kupanda miti ili kuzuia mmomonyoko wa udongo unaosababisha mafuriko kwa urahisi wakati wa mvua na kubomoa reli kila wakati.

“Pandeni miti, lindeni miundombinu ya reli na acheni vitendo vya uharibifu wa mazingira ili ujenzi wa mwaka huu uwe wa kudumu na reli isiathiriwe kirahisi na kuwasababishia kero wananchi,” amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Naye Diwani wa kata ya Kidete Bw. Mohamed Seleman Mbunda amemhakikishia Waziri Mbarawa kuwa wananchi wake watashirikiana na serikali kulinda mazingira ili kudhibiti mafuriko yanayoharibu miundombinu ya reli kila wakati wilayani humo.

Mafuriko wilayani Kilosa ni matokeo ya mvua zinazonyesha katika mikoa ya Iringa na Dodoma ambayo husababisha maji ya mto mkondoa kuacha mkondo wake na kubomoa tuta la reli katika eneo la Msagali hadi Kilosa kila wakati.

Mvua za hivi karibuni zilizonyesha mkoani Iringa na Dodoma zimesomba reli katika eneo la Magulu-Kidete kilomita 315 kutoka Dar es Salaam na kukata mawasiliano ya reli kwa siku tatu sasa.

Katika hatua nyingine Waziri Prof. Mbarawa amewataka watendaji wa TRL na RAHCO kutafuta suluhisho  la kudumu katika madaraja 32 yaliyo katika mtandao wa reli ya kati ili yasiathiriwe na mvua wakati wote.

Esha Buheti: Nikipata Tatizo Team Diamond Itahusika

$
0
0
Chokochoko! Msanii wa filamu za Kibongo, Esha Buhet amefunguka kuwa endapo atakumbwa na tatizo lolote basi timu ya Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Team Diamond itahusika.

Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Esha alisema kuwa chokochoko zilianza alipoposti picha za Ali Kiba mtandaoni ambapo Team Diamond walianza kumtukana na kumwambia watamfanyia kitu mbaya.

Chanzo: Global Publishers Limited

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Jaunuari 4, Ikiwemo ya CCM Kumjia Juu Lowassa

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Jaunuari 4, Ikiwemo ya CCM Kumjia Juu Lowassa

Nafasi za Kazi Shirika la Ndege Qatar Airways, Application Deadline: 10 Jan 2016

$
0
0
Qatar Airways
Job Vacancy 

Position Type : Full Time
Organization Type : Company

Application Deadline: 10 Jan 2016

Bonyeza=>HAPA



Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images