Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104745 articles
Browse latest View live

Zari The Lady Boss Awakosha Mashabiki wa Penzi lake na Diamond Kwa Picha Hizi

$
0
0

Zari the Boss Lady ‘Mama Tiffah’ amewakosha mashabiki wa penzi lake na Diamond ‘Baba Tiffah’ baada ya kubandika picha zake akiwa kijijini kwao pamoja na watoto wake na kuonekana anafanya kazi zote zan nyumbani kitendo ambacho kimewafanya mashabiki kumwagia sifa kuwa ni mwanamke anayeyaweza maisha yote tofauti na wengi walivyokuwa wakimfikiria hapo zamani.

Katika kunogesha Zari ame-edit picha ya diamond na kujiweka , kisha kaiweka na kuandika;


Drug Dealer, Joaquin "El Chapo" Guzman captured in Mexico

$
0
0
Mexico's authorities have recaptured drug lord Joaquin "El Chapo" Guzman, six months after he escaped from a maximum-security jail.


In a post on Twitter, Mexican President Enrique Pena Nieto said: "Mission accomplished: We got him."

Guzman was one of the world's most-wanted drug lords, whose Sinaloa cartel smuggled cocaine, heroin and methamphetamines to the US.

He escaped from jail through a 1.5km (mile) long tunnel dug in the showers.

His escape sparked a huge manhunt, with flights suspended at the nearby airports. The US government had offered a $5m (£3.2m) reward for information leading to his capture.

Guzman was apprehended following a shoot-out with Mexican marines in Los Mochis, a coastal city in his home state of Sinaloa, north-west Mexico, an official told the Associated Press.

Authorities located him several days ago based on reports that he was in the area, he added.

Mr Pena Nieto said on Twitter: "I want to inform Mexicans that Joaquin Guzman Loera has been arrested."

Guzman's July escape was his second - he was first arrested in Guatemala in 1993 and escaped from Puente Grande jail in 2001, reportedly in a laundry basket after bribing officials.

He was on the run for 13 years before being held again in 2014. His recapture was hailed as a victory for Mexico's government.

In October 2015, Mexico officials said they had "broken up" and arrested the group responsible for helping him escape.

CCTV footage of his 11 July escape showed Guzman pacing his cell several times before heading into the shower area and disappearing at the maximum-security Altiplano jail.

His wealth is estimated at $1bn.

Despite being the leader of one of the world's most powerful and violent drug cartels, Guzman was seen by some in Sinaloa - where there are few job opportunities - as a modern-day Robin Hood figure who could offer more security to people than the government.

Following his escape, shopkeepers began selling souvenirs such as baseball caps branded with "El Chapo" (Guzman's nickname, meaning "Shorty").

Tundu Lissu Atofautisha Tuhuma za Ufisadi za Lowassa na Profesa Muhongo

$
0
0
Mwanasheria mkuu wa Chadema ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ametofautisha kilichomkuta Edward Lowassa kwenye sakata la Richmond na kilichomkuta Profesa Sospeter Muhongo kwenye sakata la Escrow bungeni.

Akiongea katika kipindi cha Mada moto cha Channel Ten, Lissu alieleza kuwa kwa kutumia ripoti za kamati za bunge zilizomhukumu Lowassa mwaka 2008 na ripoti za kamati ya bunge ilizomhukumu Profesa Muhongo mwaka 2014/2015 kuna utofauti mkubwa.

Alisema kuwa ripoti ya Mwakyembe ilieleza kuwa Lowassa anawajibika kwa makosa ya watu watano wa chini yake ambao aliwataja majina na kwamba hakuna sehemu ilimtaja Lowassa kuhusika moja kwa moja na sakata la Richmond.

Alisema kuwa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyokuwa chini ya Zitto Kabwe na Deo Filikunjombe, ilieleza wazi kuwa Profesa Muhongo alishiriki kudanganya kuwa fedha zile hazikuwa za umma na baadaye ikabainishwa na kamati hiyo kuwa zilikuwa fedha za umma.

Kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe, Lowassa aliwajibika kwa sababu ya makosa ya hawa watu… Sasa hayo ni ya Lowassa. Yanalingana kiasi gani na ya Profesa Muhongo, yanalingana kiasi gani na ya Profesa Muhongo aliyesema kuwa bilioni 300 na ushee zilizotolewa Benki Kuu zikagawanywa kama njugu ni hela binafsi.

“CAG akachunguza akasema kuna hela za Umma, Takukuru wakachunguza hawajatuletea taarifa bungeni mpaka leo. Bunge likachunguza likasema hizi ni fedha za umma na hawa watu wawajibike na wakawajibishwa. Kuna ulingano gani hapo? Na hapo nazungumzia taarifa za kamati hizi mbili za bunge,” alisema Lissu.

Alikosoa uteuzi wa Profesa Muhongo akidai kuwa Bunge liliazimia kumfukuza na leo serikali inamrudisha kama vile hakuna kilichotokea hata kabla mwaka mmoja haujapita.

Udaku Special Blog

Madereva wa Mabasi Ya 'Mwendo Kasi' Wapanga Kuigomea Serikali

$
0
0
Madereva wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es salaam wamesema watagoma kuendesha magari hayo kufuatia uongozi wa mabasi hayo kuwapa mkataba wa kazi usiokidhi mahitaji.

Baadhi ya mahitaji hayo ni mshahara mdogo wa shilingi laki 4 kwa mwezi tofauti na makubaliano ya awali ya shilingi laki 8.

Wakiongea na Eatv leo, madereva hao wamesema pia wameshangazwa na kitendo cha uongozi wa mabasi hayo kuwapa mkataba wa kazi bila ya kuwapatia nakala yake jambo ambalo wamesema ni kinyume cha taratibu za ajira.

Madereva hao ambao leo walikusanyika katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo haraka kilichopo eneo la Kamata wamesema tayari walishatangaziwa malipo halisi kuwa ni shilingi laki 8 hivyo kitendo cha kusainishwa mkataba wa malipo ya shilingi laki 4 hawakubaliani nacho.

Udaku Special Blog

Video ya ‘Mbabe wa Unga El Chapo’ Alivyonaswa Huko Mexico na Polisi Miezi 6 Baada ya Kutoboa Gereza..

$
0
0
Jamaa aliteka sana vichwa vya habari kubwa duniani, jina lake halisi ni Joaquin Guzman a.k.a ‘El Chapo‘ ni jamaa ambaye ana kesi za kujihusisha na dawa za kulevya, kajikuta mikononi mwa Polisi miezi sita baada ya kutoroka gerezani alikokuwa amefungwa.

El Chapo ambaye anatajwa kuwa na mtandao mkubwa wa kusafirisha dawa za kulevya na kuziingiza Marekani, amekamatwa akiwa nyumbani kwake Los Mochis, mji wa Sinaloa uliopo Mexico.

Video:

Udaku Special Blog

Joh Makini,G-Nako na Vanessa Mdee Waingia Studio Kuandaa Kazi Mpya

$
0
0
Ni kazi baada ya kazi. Joh Makini na G-Nako pamoja na Vanessa Mdee wameingia studio ya The Industry na producer Nahreel kwa ajili ya maandalizi ya kazi mpya.

Kupitia Instagram, Joh Makini ameandika: Cooking #GoodMusicFamily #theindustrystudio unajua vile inakuaa G.Nako, Vanessa, Chinbees and Ahpha #January 2016.”

The Industry imekuwa na chemistry nzuri na wasanii hao baada ya kutengeneza hits zao kadhaa.


Udaku Special Blog

Nay wa Mitego Aoza Kwenye Penzi La Ex wa Prezzo Mrembo Chagga Barbie

$
0
0
Nay wa Mitego amedai amegundua mwanadada maarufu kwenye mitandao ya kijamii, Chagga Barbie aliyekuwa mpenzi wa rapper wa Kenya, Prezzo, ni mwanamke mwenye kila kigezo cha kuwa mama wa watoto wake.

Nay aliyekuwa akitoka kimapenzi na msanii wa filamu Shamsa Ford na baadaye kuachana, ameiambia Bongo5 kuwa mwaka huu atafanya surprise yoyote na mpenzi wake huyo.

Kusema kweli mimi na Chagga Barbie tunaendana sana,” amesema. “Mimi nina imani hata watoto wangu anaweza kuwalea. Suala la ndoa ni mpango wa Mungu lakini naweza kusema ndani ya mwaka huu kinaweza kutokea chochote kikubwa kwa sababu mimi natumia 966 kama codes zangu na huu mwaka ni 2016 vyote vinashabihiana. Kwahiyo naweza kusema huu mwaka utakuwa mzuri sana kwangu,” amesisitiza.

Chagga Barbie alijipatia umaarufu baada ya skendo ya kuachana na Prezzo kwa kuchafuana kwenye mitandao ya kijamii.

Ladies, Here Are 5 Places Men Want To Be Touched But They Won't Tell You

$
0
0

The most important step towards making a man extremely active in the bedroom is making him relax. Thus before you jump into action in the bedroom, indulge in foreplay to increase his drive.

If you are expecting a man to tell you where he wants to be touched then you are going wrong because he won't. It has been discovered that these are the 5 most common places that men want to be touched by their partners.

1. Face - A man's face is one of the most sensitive parts. Try and relax your partner's mood by running your fingers gently over his face. Start from gently pressing his temple to relieve his pressure and then gently go down to his cheek and then lips. You will see a marked difference in his mood instantly.

2. The Neckline - Neck region that holds thyroid gland is believed to get stimulated upon gentle caresses, which is responsible for body's metabolism, including his s*xual drive. Start with with a light touch round his neck to the Adam's apple with your hands in a circular motion. After a while, switch the action with your lips!

3. Ear Lobe - The ear lobe is a zone that has numerous nerve endings, so every time you touch his ear lobe, he will go crazy. Use imaginative ways to entice his senses by using your tongue, teeth or simply play with your fingers.

4. Behind the knees - The region behind his knees is very delicate and has many nerves to stimulate his senses. This sensitive volatile spot can be explored to drive him into pleasure villa. Scratch gently behind his knees to generate heat and ticklish sensations.

5. Hair - Like any other part of his body, his hair is very important. Run your fingers through his hair, very gently and sensually. Play with his locks, moving your fingers up and down his neck and ears. This would definitely prepare him for everything you have on your mind.

QUOTE: "Love is friendship that has caught fire. It is quiet understanding, mutual confidence, sharing and forgiving. It is loyalty through good and bad times. It settles for less than perfection and makes allowances for human weaknesses"– Ann Landers.



Kesi ya Mtanzania ( Rashidi Mberesero) Anayetuhumiwa Kwa Ugaidi Kenya Yaanza Kusikilizwa

$
0
0
Shahidi katika kesi ya shambulio la kigaidi lililofanyika mwaka jana katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kenya ameiambia mahakama kuwa Mtanzania Rashidi Mberesero anayetuhumiwa kushiriki, alikuwa akiswali katika msikiti ulio karibu na chuo hicho kwa siku tatu mfululizo.

Kolombo Adao ambaye ni imamu wa Msikiti wa Garissa alidai mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mlimani, Daniel Ogembo kuwa Mberesero aliondoka katika mazingira ya kutatanisha Aprili 2 mwaka jana huku akiacha begi lake msikitini.

“Alikuwa mwerevu mno na aliweza kuisoma Quran. Nilikutana naye mara ya kwanza asubuhi ya Machi 30, 2015 wakati nafungua msikiti,” alieleza shahidi huyo.

Kwa mujibu wa Adao, Mberesero alikuwa muumini wa kipekee kwani kila siku alikuwa akifika msikitini saa 10:35 alfajiri, wakati mwingine kabla ya adhana.

Shahidi huyo alidai kwamba Aprili Mosi mwaka jana alipofungua msikiti asubuhi alimkuta Mberesero akiwa ameshafika na alimpa kipaza sauti aweze kuwaita waumini wanaotakiwa kuswali asubuhi siku hiyo.

“Nilikuwa naumwa kifua siku hiyo. Kwa hiyo nilimpa kipaza sauti atangaze kwa sababu alikuwa anaijua vyema Quran,” shahidi huyo alidai.

Kuhusu sababu za Mberesero kuwapo Garissa, Adao aliiambia mahakama kuwa aliambiwa na kijana huyo kuwa alikwenda kumsalimia mjomba wake lakini alifukuzwa kwa kuwa ni Mwislamu.

“Alinieleza kuwa baba yake ni Mdigo wa Tanga na mama yake ni Mkamba wa Kenya,” alieleza Adao.

Kwa maelezo ya shahidi huyo, siku ya tukio Mberesero ambaye alizoea kuvaa kanzu alionekana amevaa mavazi ya kawaida na kofia kama mtu anayeficha uso.

Mahakama ilielezwa kuwa siku ya tukio aliingia msikitini na kuweka begi lake kwenye kona ya msikiti lakini hakusali na baadaye aliondoka na kuliacha.  

CCM: Lowassa Alitutikisa Haijawahi Tokea...

$
0
0
Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu, makada wa CCM walirusha kila neno baya na la kejeli kwa Edward Lowassa, lakini moyoni walikuwa wanajua kuwa mgombea huyo wa urais kwa tiketi ya Chadema alikuwa akiwasumbua, Mwananchi imeelezwa.

Lowassa, Waziri Mkuu wa kwanza wa Serikali ya Awamu ya Nne, alijiondoa CCM baada ya kumalizika kwa mchakato wa kumpata mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, jina lake likiwa limekatwa kabla ya kufikishwa kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa na Mkutano Mkuu, vyombo ambavyo hufanya uamuzi kwa kupiga kura.

Siku chache baadaye alijiunga na Chadema, ambayo iliingia kwenye Uchaguzi Mkuu chini ya mwamvuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliokuwa pia na vyama vya CYF, NCCR Mageuzi na NLD vilivyokubaliana kusimamisha mgombea mmoja wa urais, ubunge na udiwani. Hakuondoka peke yake. Waziri Mkuu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick Sumaye alimfuata pamoja na mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale-Mwiru, mawaziri wa zamani, wenyeviti wa mikoa, wabunge na madiwani na kufanya Uchaguzi Mkuu kuwa na ushindani wa aina yake.

Ukweli ni kwamba kuondoka kwa Lowassa kulitutikisa (sisi) CCM,” alisema Abdallah Bulembo aliyekuwa meneja wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli.

Hata hivyo, alidai kuwa athari za mtikisiko huo hazikuonekana kwa sababu chama hicho tawala kilijivunia ubora wa mgombea wake, utekelezaji wa ilani yake na kusimamia ukweli katika majukwaa ya siasa. Bulembo alisema hayo alipofanya mazungumzo maalumu na gazeti hili juzi jijini Dar es Salaam.

Nasema CCM ilitikisika kwa kuwa mbali na Lowassa tuliondokewa na mwenyeviti watatu wa mikoa; Shinyanga, Singida na Arusha,” alisema Bulembo.

Katika Idara ya Wazazi, mimi (mwenyekiti) niliondokewa na wajumbe wa baraza la mikoa ya Pwani, Njombe, Kagera na Rukwa. Lakini tukapata replacement (mbadala) na kusonga mbele.

Kwa mujibu wa Bulembo, pamoja na kuondokewa na viongozi hao ambao alisema ni nguzo muhimu ya chama, bado CCM iliweza kushinda viti tisa vya ubunge kati ya 10 mkoani Singida, viti vyote vya ubunge katika Mkoa wa Shinyanga na kiti kimoja katika Mkoa wa Arusha.

Maneno ya Bulembo yanaweza kuthibitishwa na jinsi kampeni za CCM zilivyojaa hotuba za kumrushia makombora mbunge huyo wa zamani wa Monduli karibu katika kila mkutano wa kampeni.

Wakati fulani akiwa mkoani Kagera, Bulembo aliwahi kuwatuhumu wana-CCM kuwa wamekuwa ndumilakuwili kwa kukiunga mkono chama hicho wakati wa mchana na baadaye kwenda Ukawa.

Bulembo alisema kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Bukoba Vijijini, ziara ya Lowassa mkoani Kagera iliratibiwa na wana-CCM na kwamba anawafahamu.

Msidhani hatuwafahamu. Mikakati yote na jinsi mnavyowafadhili Ukawa na Lowassa tunafahamu. Tena tunawafahamu kwa majina. nasema ole wenu. Msipoondoka wenyewe, tutawafukuza Dk Magufuli atakaposhinda uchaguzi,” alisema Bulembo wakati huo.

“Tunawajua mnaomng’ang’ania Lowassa. Lakini nawahakikishia kuwa mtalia baada ya uchaguzi wa mwaka huu. Mnajifanya CCM, lakini mnafadhili Ukawa. Mwisho wenu unakuja.”

Kabla ya mkutano huo, Dk Magufuli pia alifichua mipango ya wanachama ambao aliwaita wanakuwa upande wa CCM mchana na usiku wanahamia Ukawa wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Zimbiilo wilayani Muleba.

Kuna baadhi ya wana-CCM wanatujuhumu sana, wengine nawajua hata majina yao bahati nzuri huwa sisemi uongo bali ukweli. Kuna huyu Gasper mchana tunakuwa naye CCM lakini usiku anaungana na wapinzani,” alisema na kuacha mshangao kwenye mkutano huo. Kukiwa bado na mshangao, Bulembo alisimama na kwenda kumnong’oneza kitu Magufuli na baadaye mgombea huyo wa CCM akarekebisha kauli yake.

“Msaliti ni Gasper Anthony wala si Gasper Kileo,” alisema akimzungumzia mwanachama ambaye alijionyesha waziwazi kumuunga mkono Lowassa wakati wa mchakato wa kutafuta mgombea urais ndani ya CCM.

Siri ya ushindi

Pamoja na upinzani huo ambao CCM ilikumbana nao kutoka kwa Lowassa, Bulembo alisema siri ya ushindi wa chama hicho kikongwe kwenye uchaguzi uliopita ni pamoja na kukubalika kwa Dk Magufuli.

“Tulimteua mtu anayekubalika. Magufuli alijiuza mwenyewe na alikuwa mchapakazi. Tulikuwa tunafanya kati ya mikutano saba na kumi isiyo rasmi kila siku,” alisema Bulembo.

Alipoulizwa kingetokea nini endapo CCM isingemteua Dk Magufuli kugombea urais, alijibu “bado tungeshinda, lakini ingetulazimu kufanya kazi ya ziada”.

Katika uchaguzi huo, Dk Magufuli alipata kura milioni 8.8 na Lowassa alipata kura milioni 6.07, idadi ambayo ni zaidi ya mara mbili ambazo wapinzani wamekuwa wakipata kwenye chaguzi zilizopita. Bulembo pia, alieleza kuwa CCM ilijipanga vizuri ikitumia makada na viongozi wake waliotawanyika kuanzia ngazi ya tawi hadi taifa.

Chama kilikuwa baba na kilitegemea taasisi zake zote. Katika ngazi ya chama kulikuwa na timu ya watu 32 na mimi katika idara yangu ya wazazi niliteua watu 34, vilevile katika idara nyingine, ingawa siwezi kukumbuka idadi ya watu walioteuliwa kuongoza jahazi,” alisema.

Alisema mbali na timu hiyo iliyokuwa ikiandaa mazingira ya kampeni za mgombea urais, chama hicho kilitumia uongozi wake katika idara zote; vijana, wazazi na wanawake pamoja na kamati zake za uchumi na siasa kufanya kazi hiyo usiku na mchana.     

Udaku Special Blog


Magufuli na Edward Lowassa Wote Kwa Bwana Samatta

$
0
0
Si wanasiasa, si wanamichezo, wasanii na wengine wote walikuwa kitu kimoja wakati walipoungana kutoa salamu za pongezi kwa mshambuliaji nyota wa mpira wa miguu nchini, Mbwana Samatta kwa kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika.

Kundi hilo la wapeperusha salamu linaongozwa na Rais John Magufuli ambaye katika salamu zake za pongezi alizomtumia Waziri wa Michezo, Nape Nnauye, alisema; “tuzo hiyo imemjengea heshima Mbwana Samatta mwenyewe, wanasoka hapa nchini na Tanzania kwa ujumla katika medani ya soka la kimataifa”.

Pia, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alikuwa miongoni mwa waliotuma salamu za pongeza akisema: “Ushindi wa Samatta ni changamoto kubwa kwa wanasoka wa Tanzania, lakini zaidi kwa Serikali kuwekeza kwenye eneo hilo.”

Samatta, ambaye anatarajiwa kuihama klabu yake ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kujiunga na FC Genk ya Ubelgiji, alishinda tuzo hiyo ya Mwanasoka Bora wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa Wachezaji wa Barani Afrika juzi kwenye hafla iliyofanyika Lagos, Nigeria.

Mshambuliaji huyo, mwenye umri wa miaka 24, anakuwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika Mashariki kutwaa tuzo hiyo baada ya kuiongoza TP Mazembe kutwaa ubingwa wa Afrika akiwa amefunga mabao sita.

Pia, ndiye mfungaji tegemeo wa Taifa Stars, akiwa amefunga mabao mawili kwenye raundi mbili za michuano ya awali ya Kombe la Dunia dhidi ya Malawi na Algeria, ingawa Stars ilitolewa kwa jumla ya mabao 7-2 na wababe hao wa Afrika Kaskazini.

Jana ilikuwa siku ya shangwe kwa Watanzania baada ya Samatta kutwaa tuzo hiyo usiku, baadhi wakituma ujumbe kwenye mitandao ya kijamii na wengine taarifa kwenye vyombo vya habari kupongeza.

Taarifa iliyotolewa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa imeeleza kuwa Dk Magufuli amemtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amfikishie salamu zake kwa nyota huyo.

Katika salamu hizo, Dk Magufuli amewasihi wanasoka wote na wadau kuongeza juhudi za kuundeleza mchezo huo ili upige hatua zaidi za kimaendeleo.

Naye Lowassa, ambaye aligombea urais kwa tiketi ya Chadema, alisifu juhudi za Samatta.

Huyu kijana kufikia hapo ni kujituma, lakini zaidi ni malezi aliyoyapata katika timu yake ya TP Mazembe... ni lazima tuwe na utaratibu wa kujenga shule za kukuza vipaji vya soka (academy), tutawapata akina Samatta wengi,” alisema Lowassa.

Alisema Serikali isione shida kuchukua ilani ya Chadema iliyoridhiwa na Ukawa ambayo inataka kufutwa kodi kwa vifaa vyote vya michezo.

“Wasione haya kuchukua ilani yetu. Sisi tulitangaza kuwa tutafuta ushuru kwa vifaa vyote vya michezo pamoja na kuanzisha academy ili kuinua vipaji. Tunaamini kwa kufanya hivyo watapatikana akina Samatta wengi tu na si katika soka, bali hata michezo mingine kama riadha na ngumi.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Uvuvi, Mwigulu Nchemba, ambaye ni shabiki maarufu wa klabu ya Yanga, aliandika kwenye ukurasa wake wa Tweeter kumpongeza Samatta akisema ushindi wake umeipa heshima nchi.

Hongera sana, ufanikiwe zaidi ya hapa,” alisema Nchemba katika ujumbe wake.

Mbunge wa Kibamba, John Mnyika naye hakuwa nyuma kumwagia sifa Samatta, akisema mafanikio yake yanadhihirisha pasi na shaka uwepo wa vipaji lukuki hapa nchini ambavyo hupotea bila kufikia ukomo wa juu wa ndoto na uwezo wao.

Tunahitaji mikakati sahihi, utekelezaji na uwekezaji wa kutosha katika soka. Inawezekana! Tuiangalie hii kama fursa ya kuwakwamua vijana wetu kuzalisha ajira na wao kutimiza ndoto na matamanio yao,” alisema Mnyika katika salamu zake.

Kufeli mtihani si kufeli maisha

Nyumbani kwa wazazi wa Samatta na shuleni kwake ilikuwa ni kutafakari safari ya mshambuliaji huyo tangu utotoni.

“Haya ni mafanikio makubwa,” alisema mwalimu wa michezo wa Shule ya Sekondari ya Thaglan ya Mbagala, Mapesi Jamal ambaye hivi sasa amehamishiwa Kisiju wilayani Mkuranga.

Niligombana naye sana nikitaka apende vitu vyote viwili (shule na mpira) kutokana na kutokuwa vizuri darasani, ndiyo maana matokeo yake ya mwisho hayakuwa ya kuridhisha.

“Nakumbuka (baadaye) niliwahi kumwambia ajitahidi sana kupenda mpira na uwe ndiyo chaguo lake la kwanza baada ya kugundua kuwa darasani ameshindwa.

“Tangu ajiunge kidato cha kwanza alikuwa tayari ameanza kujifunza soka kwenye kituo cha Jamal Kisongo alikokuwa akichezea timu ya vijana ya klabu ya Mbagala Market.”

Mwalimu Mkuu wa Thlagan, Juma Nyenga ambaye kwa sasa ni mlezi na mshauri wa shule hiyo, alimwelezea Samatta kuwa ni kijana mpole ambaye hakukatishwa tamaa na matokeo mabaya ya kidato cha nne.

Alionyesha njia nyingine ya kupata mafanikio ambayo ni soka,” alisema Nyenga.

Nyange aliiambia Mwananchi kuwa wamefurahishwa na mafanikio ya Samatta kwa kuwa yanamtangaza yeye, shule na nchi yake.

Alisema kuna kipindi aliingia kwenye matatizo ya kitaaluma na walilazimika kumuita baba yake shuleni.

“Mzee Samatta ni muelewa pia, alituambia mfumo wa mwanaye na kutuomba tumsaidie jinsi ya kuendesha maisha yake kwa kuwa tayari ameonyesha kuwa alikuwa anapenda soka kuliko shule. Ingawa hata sisi tulitaka apende vitu vyote kwa pamoja, nililazimika kumpa adhabu ya kumchapa viboko vinne mbele ya mzazi wake,” alisema.

Nyenga anasema tangu siku hiyo alirudisha mapenzi ya kuhudhuria vipindi.

Walimu hao wanaona Samatta bado hajachelewa kujiendeleza kielimu.

Tunaposema arudi darasani si kwenda kusoma masomo yote upya, kwa vile amekuwa ni wa kimataifa na matokeo yake hayakuwa ya kuridhisha, anatakiwa kujiendeleza kwa kusoma lugha ya Kiingereza,” alisema

“Pia kama ameweza kufuata miiko ya soka, basi anatakiwa aendelee hivyohivyo maana hiyo pekee ndiyo itampa mafanikio zaidi huko mbele. Awe na nidhamu si uwanjani pekee, hata nje ya uwanja kama alivyo sasa, awekeze kwani mpira una muda wake,” alisema Mapesi.

Baba amwaga machozi

Baba yake mzazi, Ally Samatta alisema aliangua kilio mara baada ya mwanaye kutangazwa mshindi.

Nilifuatilia kuanzia mwanzo hadi mwisho. Walipotangaza sikuamini, nilijikuta naangua kilio mpaka majirani walishtuka,” alisema mzazi huyo.

Nimefurahi na ninampongeza sana kwa hilo, pia nawashukuru Watanzania wote waliowezesha hili kwa njia moja au nyingine.

“Nilimpa maneno ya siri alipokuwa anakwenda huko na hata atakaporudi nitamwambia. Nashukuru huwa anazingatia. Samatta amekuwa mchezaji bora kama nilivyokuwa mimi mwaka 1964 nilipotwaa tuzo hiyo kwa Tanganyika ila yeye kanifunika kabisa.”

Mama mlezi wa Samatta, Khadija Abdallah naye alikuwa na furaha.

Mimi nilijikuta presha inapanda huku kichwa kikiniuma sana, hatujalala kabisa kwani bado hatuamini kwa kweli. Tumelala saa 11 alfajiri na tumeamka saa moja asubuhi,” alisema.

Mzee Samatta alitoa ahadi kwa mwanaye kuwa akitwaa tuzo hiyo basi watamfanyia sherehe kubwa.

Wazazi hao wameeleza kuwa mtoto wao anapokuwa likizo huwa anapendelea kufanya mambo kadhaa, hasa usafi wa nyumba, kuangalia televisheni, kucheza game, kusikiliza redio pamoja na kuchati.

Wazazi wake walisema Samatta alikuwa anamiliki nyumba saba, lakini moja ambayo ipo Saku, Maji Matitu ameibomoa na ana mpango wa kujenga msikiti, nyingine iliyokuwa Mbande aliiuza kwa sababu ilijengwa chini ya kiwango hivyo amebaki na nyumba tano.

Mbali na nyumba hizo anamiliki viwanja zaidi ya 10 pamoja na mashamba zaidi ya matatu na magari ya kifahari.


Source:Mwananchi

Udaku Special Blog

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Tarehe 10, Ikiwemo ya Majipu uchungu kwa Rais Magufuli

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Tarehe 10

WASTARA Atoa Neno Baada ya Harusi yake na Kudai Mke Mkubwa Aliyemkuta Kwa Mme Wake Kampokea Kwa Mikono Miwili

$
0
0

Wastara kapost picha kwenye account ya Instagram na kuandika haya :

Nilikuwa kwenye usingizi mzito nimeshtuka nikakumbuka ni vizuri kuwapa asante wale wote walipiga goti kuniombea siku moja nipate faraja au tulizo la moyo ama stara kwa mwanamke wa kiislam kama dini inavyosema.. Japo kwangu nilikuwa nimeweka nadhiri ya miaka 3 ikipita basi ridhki ya mume ikija milango iko wazi alhamdulilah imekuja wakati muafaka na siku muafaka baada nadhiri yangu kutimia. Mungu ni mwema sana namuamini sana na ananipenda sana ndio maana kaniumba anavyojua yeye tumshukuru mungu kwa hili, najiombea na wale wenye nia njema na mim tuwe pamoja, iwe yenye neema ndoa hii aliyoipanga mungu pekee yeye ndie mwenye mamlaka juu ya hili barka, rehma, stara, uvumilivu ridhiki, upendo uwe juu yetu na bi mkubwa niliyemkuta aliyenipokea kwa mikono miwili kma mke mwenziwe msiumize vichwa tunajuana tunaheshimiana.’- @wastara84

Udaku Special Blog

David Kafulila Majanga Matupu...Afunguliwa Kesi Nyingine Kigoma..Mwenyewe Adai ni Hujuma...

$
0
0
Taarifa ninayokusogezea ni ya David Kafulila aliyekuwa mbunge wa Kigoma Kusini, tunafahamu ana kesi Mahakamani ya kupinga matokeo ya ubunge 2015 jimbo la Kigoma Kusini kesi ipo Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, taarifa ikufikie kuwa Kafulila baada ya kufika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kigoma akasomewa kesi mpya ambayo anakiri hakuwa anaifahamu mwanzo kwenye sentensi zake;

Nilifikishwa mahakamani kwa kesi mpya ukiachilia kesi ya kwanza ya kupinga matokeo ya uchaguzi 2015 jimbo la Kigoma kusini, awali nilikuwa nikijua ninakesi moja katika mahakama ya hakimu mkazi kigoma kwa madai kwamba nilimdhalilisha aliyekuwa mkuu wa wilaya Khadija Nyembo tangu mwaka 2013….nikiwa mahakamani nikapewa tena kesi nyingine ni kesi ya kuhamasisha wananchi wasichangie mchango wa maabara;– David Kafulila

Bado msimamo wagu utabaki palepale kwamba nitaendelea kupigania nchi yangu, kesi hizi zote katika mahakama ya hakimu mkazi Kigoma ukitazama hati za mashitaka yote ya Kafulila hapa Kigoma zimeandaliwa na kusainia na DPP makao makuu Dar es salam inawezekanaje;- Kafulila

Udaku Special Blog

Mke wa Mtu Afia 'Gesti' Akiwa na Mchepuko Wake.....

$
0
0

"Polisi walipofungua chumba walikuta godoro liko chini lakini kitandani lilipopaswa kuwa kulikuwa na mwili wa mwanamke ukiwa umefunikwa shuka..."
 Mwanamke mmoja (jina linahifadhiwa)  anayedaiwa ni mke wa mtu, amefariki dunia katika nyumba ya kulala wageni katika Manispaa ya Bukoba, akiwa na mwanaume mwingine inayesemekana ni hawara yake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Augustine Ollomi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa, watu hao walienda katika nyumba hiyo ya kulala wageni iliyopo eneo la Hamugembe Januari 3, mwaka huu na kuchukua chumba namba nane.

Alisema siku iliyofuata saa 6:00 mchana, polisi walipokea taarifa kutoka kwa wahudumu wa nyumba hiyo ya kulala wageni kuwa katika chumba hicho kuna watu waliingia jana yake lakini hadi muda huo mlango wa chumba ulikuwa haujafunguliwa na kuna ukimya uliowatia hofu.

Alisema wahudumu hao waliambatana na polisi na walipofika eneo la nyumba hiyo walimkuta mmiliki wake ambaye alitoa funguo za akiba na kufungua chumba hicho.

Polisi walipofungua chumba walikuta godoro liko chini lakini kitandani lilipopaswa kuwa kulikuwa na mwili wa mwanamke ukiwa umefunikwa shuka na kuuchukua kwenda kuuhifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera,” alisema.

Kamanda huyo wa polisi mkoa wa Kagera, alisema mtu aliyekuwa pamoja na mwanamke huyo (jina linahifadhiwa) ambaye ni dereva wa basi la abiria linalofanya safari zake kati ya Bukoba na Mwanza, hakukutwa katika chumba hicho na alifunga mlango kwa nje na kuondoka na funguo.Hata hiyo, alisema chanzo cha kifo hicho hakijajulikana lakini kutokana na taarifa walizopata kutoka kwa msaidizi wa dereva huyo wamefanikiwa kumpata mtu aliyejitambulisha kuwa ni mume wa marehemu.

Kamanda Ollomi aliongeza kusema kuwa,  mume wa marehemu mkazi wa Butimba, jijini Mwanza, amepatikana na kukabidhiwa mwili wa mkewe, huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea na kwamba wafanyakazi wawili wa nyumba hiyo ya kulala wageni wanashikiliwa na polisi kwa upelelezi zaidi lakini pia kwa kitendo cha kuficha taarifa za wageni wanaolala katika nyumba hiyo.

Muswada wa Habari Kurejeshwa Tena Bungeni

$
0
0
MUSWADA wa Sheria ya Habari ambao uliwahi kupelekwa bungeni kisha kuondolewa kimya kimya, sasa unatarajiwa kurejeshwa tena bungeni mwezi huu.

Uwezekano wa kurejeshwa tena bungeni kwa muswada huo, kunatokana na kuundwa kwa kamati ya wanahabari sita, itakayoshirikiana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (pichani) kupitia muswada huo kabla ya haujawasilishwa bungeni baadaye mwezi huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana na wahariri wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari nchini, Nnauye alisema serikali inathamini mchango mkubwa wa vyombo vya habari na watendaji wake, na kwamba itashirikiana nao kuhakikisha sheria bora ya habari inapatikana.

Kamati hiyo imeundwa baada ya mapendekezo ya Waziri Nnauye ambaye alitaka kamati hiyo iundwe na ikutane naye Januari 13 mwaka huu, kwa ajili ya kuanza kupitia muswada huo wa sheria ya habari.

Wanaounda kamati hiyo ni Naibu Mhariri Mtendaji wa kampuni ya TSN, Tuma Abdallah, Mhariri Mkuu wa gazeti la Nipashe, Jesse Kwayu na Mhariri Mtendaji wa gazeti la Jamhuri, Deodatus Balile.

Wengine ni Mhariri wa Upendo Media, Mengda Johanes, Prudence Constantine wa Shirika la Taifa la Utangazaji(TBC1) na Joyce Shebe wa Clouds Media.

Awali, akizungumza na wahariri hao, Nnauye alisema vyombo vya habari nchini vina mchango mkubwa katika taifa na vinapaswa kuwa na sheria inayowasimamia, ili kuhakikisha uhuru wa habari unakuwepo na pia kuwa kuwa na mipaka yake.

Nape aliongeza kuwa yeye ni muumini mzuri wa uhuru wa habari nchini, hivyo atahakikisha anatekeleza wajibu wake kwa kuharakisha mchakato wa muswada wa sheria hiyo, kwa kuhusisha wadau watoe mapendekezo kabla ya kuupeleka bungeni.

Alisema nia ya serikali kutunga sheria hiyo ni nzuri kwa kuwa inaweka utaratibu wa kurahisisha utekelezaji wa majukumu ya vyombo vya habari ili kuwa na mazingira mazuri na yenye tija.

Akizungumzia masuala ya vitambulisho vya waandishi (press card), Nnauye alitoa wiki moja kwa Idara ya Habari (Maelezo) kuangalia kanuni na utaratibu mzuri wa jambo hilo na kutoa mwongozo utakaotumika kwa ajili ya utoaji vitambulisho hivyo na kwa muda gani.

“Nawapa siku saba Maelezo, mkakae, muangalie kanuni na taratibu zikoje, ili mniletee ripoti juu ya jambo hili,” alisema Waziri Nnauye.

Kuhusu Muswada wenyewe
Katika Bunge la Juni mwaka jana, serikali iliuondoa Muswada wa Sheria ya Haki ya Upatikanaji Habari wa mwaka 2015, uliokuwa usomwe kwa mara ya pili.

Ilieleza kuwa muswada huo utasubiri bunge jipya litakapokaa, baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka 2015.

Akitoa taarifa ya kuondolewa kwa muswada huo bungeni mbele ya Naibu Spika, Job Ndugai (wakati huo), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), kwa wakati huo, Profesa Mark Mwandosya alisema, “Uamuzi wa kuuondoa umeafikiwa na Serikali baada ya Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Huduma za Jamii kuishauri hivyo.”

Mwandosya alisema sheria hiyo ya upatikanaji habari ilichapishwa Februari 20 mwaka 2015 na kusomwa bungeni kwa mara ya kwanza Machi 12 hadi Aprili mosi mwaka huo.
Alisema muswada huo si wa dharura, kwa kuwa umepitia hatua mbalimbali, ikiwemo kujadiliwa na kamati hiyo Juni 22

Wafanyakazi 360 wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote Wakamatwa Kwa Kufanyakazi Nchini Bila Kibali

$
0
0
Wafanyakazi zaidi ya 360 wa kiwanda cha saruji cha Dangote mkoani Mtwara, wamekamatwa kwa kufanya kazi nchini bila kuwa na vibali vya Uhamiaji.

Kamatakamata hiyo imekuja baada ya agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga la kuwakamata wahamiaji haramu na wageni wanaofanya kazi bila vibali.

Jana, ofisi ya Uhamiaji ya mkoa ilifanya operesheni katika kiwanda hicho, lakini haikupewa ushirikiano na uongozi.

Ofisa Uhamiaji wa mkoa, Zakayo Mchele alisema walifika kiwandani hapo kufanya ukaguzi, lakini walikosa ushirikiano kutoka kwa Meneja Mkuu aliyefahamika kwa jina la Vidya Digixt.

Mchele alisema kutokana na meneja huyo kutotoa ushirikiano, wanamshikilia ili kusaidiana na Uhamiaji kuwabaini wafanyakazi wanaoishi bila uhalali na pia watamfikisha mahakamani.

Alisema licha ya kukosa ushirikiano, wafanyakazi 117 wa kiwanda hicho walipeleka maombi ya kutaka kupewa vibali vya kazi.

Mchele alisema walifanya msako katika mpaka wa Kilambo na Wilaya ya Tandahimba na kuwakamata watu 48 raia wa Ethiopia ambao walisafirishwa kwa malori kutoka Kenya.

“ Pia, tuliwakamata raia wengine wawili wa Msumbiji wakiwa na kadi za kupigia kura (za Tanzania) na kukamatwa siyo kwamba msako ulikuwa haufanyiki siku za nyuma,” alisema.
Alisema mwaka jana idadi ya watu walioingia nchini bila kibali kwa Mkoa wa Mtwara walikuwa 121.

Ofisa huyo alisema katika operesheni hiyo kesi zilizopelekwa mahakamani ni 36 ambazo zilikamilika na wahusika kutiwa hatiani na kutozwa faini, huku wengine wakipewa adhabu ya kutumikia kifungo.

Simba Yapakatwa na Mtibwa Sugar....Ibrahim Jeba kaipeleka Mtibwa Sugar fainali

$
0
0
Baada ya mapumziko ya siku moja kutokana na kukamilisha hatua ya Makundi ya michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa mwaka 2016, January 10 michuano ya Kombe la Mapinduzi iliendelea katika hatua ya nusu fainali. January 10  saa 16:15 ulipigwa mchezo wa kwanza wa nusu fainali kati ya Simba dhidi ya Mtibwa Sugar, wakati nusu fainali ya pili ikipigwa saa 20:15 usiku.

Mchezo wa nusu fainali ya kwanza kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Simba ulikuwa ni mchezo wa kuvutia kwa kiasi kikubwa na ulianza kwa timu zote kucheza mpira wa taratibu na kuusoma mchezo, Mtibwa walipata goli la ushindi dakika ya 45 baada ya Chiza Kichuya kupiga shuti kali lililomfanya Peter Manyika kutema na Ibrahim Jeba kupachika goli la ushindi.

Hadi dakika 90 zinamalizika Simba hawakufanikiwa kusawazisha goli, na kufanya mchezo kumalizika kwa Mtibwa Sugar kutinga fainali kwa ushindi wa goli 1-0. Kwa matokeo hayo Mtibwa Sugar wametangulia fainali na sasa wanasubiri mshindi wa mchezo wa nusu fainali ya pili kati ya Yanga dhidi ya URA ya Uganda.

Ukimkosa Prezzo Kwenye Muziki Ujue yuko Huku na Anaitwa Doctor Prezzo !!

$
0
0
Star wa muziki kutoka area code ya +254 kwa watu wa nguvu Kenya, rapper Prezzo japo hasikiki mara kwa mara lakini jina lake lipo kwenye majina ya wakali walioubeba muziki wa Kenya kwa kipindi kirefu toka ‘Genge’ yao ilivyopasua anga na kufahamika kimataifa.

Nimeipata Interview aliyofanyiwa siku chache zilizopita na mrembo Betty Kyallo Okari wa TV ya KTN ya Kenya… kaongelea mengi ikiwemo ishu ya kusomea udaktari.

‘Baba yangu alifungua Makini Herbal Clinic na mimi ni mtoto wa pekee wa kiume nyumbani, imenibidi nisome kuhusu masuala ya utabibu ili nisimamie shughuli za clinic… nitakuwa natoa huduma kwa watu na majaaliwa nitaitwa Dr. Jackson Makini. Nahitaji kuendeleza urithi wa kitu kizuri alichokijenga baba yangu‘- Prezzo.

Sentensi nyingine za Prezzo hizi hapa >>’Namkumbuka sana mzee wangu, angekuwa hai najua angejisikia fahari kuwa na mtoto kama mimi… nadhani angekuwa hata Rais wa Kenya‘- Prezzo.

Tazama Video Hapa:

RISPER FAITH Owns A Small Shop And This is How She Dresses For Her Customers, Eish (PHOTOs)

$
0
0

Besides servicing old rich men who empty their bank accounts to have a taste of her juicy derriere, popular city socialite, Risper Faith, also owns a small beer, wines and spirits shop in one of the up-market malls.

When she has no client to service, Risper goes to serve customers at her small shop and this is how she dresses.



Viewing all 104745 articles
Browse latest View live




Latest Images