Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104747 articles
Browse latest View live

Siku Moja Baada ya Kutolewa Kombe la Mapinduzi, Simba Wameamua Hivi Kuhusu Kocha wao Mzungu

$
0
0
 Uongozi wa klabu ya Simba usiku wa January 11 kuingia 12 unatajwa kufanya maamuzi magumu, kutokana na mwendo wa timu yao kwa sasa, stori kutoka mtandao wa mwandishi na mchambuzi wa soka Tanzania Salehjembe.blogspot.com, umeripoti uongozi wa klabu ya Simba kuamua kumfuta kazi kocha wake wa kiingereza Dylan Kerr.

Simba ambayo ilitolewa na Mtibwa Sugar katika hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi 2016 kwa goli 1-0, dalili za kuwa kocha Kerr yupo katika wakati mgumu, zilianza kuonekana baada ya afisa habari wa klabu hiyo Haji Manara kufunguka kwa jazba kuwa yeye kama shabiki ameshangazwa na maamuzi ya mwalimu ya kutopanga mapema kikosi cha kwanza. Kerr anatajwa kuitwa kwenye kikao cha dharura lakini kikao ambacho kinatajwa kuwa tayari kina maamuzi.
Jackson Mayanja akisalimiana na Kerr wakati ambao alikuwa kocha wa Coastal Union ya Tanga.


Haji alikuwa akiongea baada ya mchezo akijitaja kwa kiasi kikubwa kama shabiki na sio kiongozi wa Simba, ili apate nafasi ya kutoa ya moyoni, hiyo ni moja kati ya dalili za Kerr kuwa alikuwa anawashiwa taa nyekundu. salehjembe.blogspot.com umeripoti nukuu chache za chanzo cha siri kuwa Kerr amefutwa kazi, nafasi yake itachukuliwa na Jackson Mayanja ambaye hivi karibuni alisaini mkataba wa kuwa kocha msaidizi, lakini sasa ataava viatu vya Kerr.

Mtuhumiwa Anayesakwa na Polisi Awatumia Polisi Selfie ya Picha yake na Kusema Waliyotumia ni Mbaya

$
0
0
Mwanamume anayesakwa kwa makosa la kuteketeza na kuharibu mali ametuma picha ya selfie kwa maafisa wa polisi akisema picha iliyotumiwa na maafisa hao katika tangazo la kutafutwa kwake haikuwa ya kupendeza.

Donald "Chip" Pugh aliwatumia maafisa wa polisi picha aliyojipiga mwenyewe na kuandika ujumbe unaosema: "Hii hapa picha yangu nzuri, hiyo mliyotumia ni mbaya sana”.
Polise katika mji wa Lima, jimbo la Ohio, walikuwa wamepakia picha kwenye ukurasa wao wa Facebook wakiomba msaada wa kumtafuta Bw Pugh.
"Picha hii ilitumwa na Bw Pugh mwenyewe," kituo cha polisi cha Lima kiliandika kwenye ukurasa wa Facebook.

"Tunamshukuru kwa msaada wake lakini sasa tungeshukuru hata zaidi kama angejitokeza na kuzungumza nasi katika kituo cha polisi kuhusiana na mashtaka yanayomkabili."
Polisi walisema anatafutwa kwa mashtaka kadhaa na amri ya kukamatwa kwake inahusiana na kushindwa kufika kituo cha polisi kama ilivyoagizwa.

"Bwana, walinikosea,"Bw Pugh aliambia kituo cha Redio cha Ohio, akieleza ni kwa nini akawatumia polisi picha hiyo ya selfie.

Sikiliza Hapa Nyimbo Mpya ya Diamond Platnumz Inayosemekana Imevuja.....

$
0
0
Jamani huyu Diamond sasa ana sifa,tena hizi sifaa zimepitiliza!

Kuna nyimbo ake hapa naisikiliza inaitwa HELLOW jamaniiii nyimbo nzuri ,inachezekaa kila kitu poa 

Ni kama kamuimbia Wema Sepetu kwa haraka haraka!

Isikilize Hapa na Utoe Maoni yako:


Fatma Karume : Maana ya Mapinduzi Imepotea Zanzibar Madhumuni yake Hayaeleweki..

$
0
0
Mwanaharakati wa Marekani, Huey Newton alisema: “Mapinduzi siku zote yapo mikononi mwa damu changa. Ni vijana tu ndiyo huyarithi na kuyafaidi mapinduzi.”

Hakika maneno ya Newton yanasadifu kwa kiasi kikubwa kauli ya Fatma Karume, Wakili wa Kampuni ya Uwakili ya IMMMA, ambaye pia ni mtoto wa rais wa zamani wa Zanzibar, Abeid Aman Karume.

Wakati leo tukisherehekea miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Fatma anasema: “Huu ni wakati sahihi kwa Serikali na Wazanzibari kujitathmini kama kweli tunaienzi mbegu ya mapinduzi.”

Anasema Wazanzibari wengi hawaijui Zanzibar ilivyokuwa kabla ya Mapinduzi,bali wanaifahamu baada ya Mapinduzi.


Hivyo hawaelewi madhumuni yake kwa sababu hawajaiona kabla na baada ya mabadiliko hayo.

“Nasimuliwa na wakubwa zangu tu kwamba mimi nimezaliwa baada ya Mapinduzi, lakini naambiwa hapo zamani Zanzibar ilikuwa na mchanganyiko wa watu wa makabila mbalimbali,” anasema.

Anasema zamani, kabla ya Mapinduzi kulikuwa na makundi mchanganyiko ya Waafrika, Waarabu, Wahindi, Washirazi, (asili yao ni Persia) kwa sababu Zanzibar ilikuwa ni kituo kikuu cha biashara.

Fatma anaeleza kuwa mchanganyiko huo ulisababisha kuwapo kwa ubaguzi na ilikuwa vigumu kuwapo kwa ndoa za muingiliano, hakikuwa kitu cha kawaida katika jamii hiyo.

“Ninayafahamu Mapinduzi ya Zanzibar kutokana na Amri namba 6 iliyotolewa Februari 25 mwaka 1964 na Baraza la Mapinduzi. Baada ya Mapinduzi Zanzibar iliendeshwa na Baraza la Mapinduzi, pamoja na waliohusika kumpindua Sultani,” anasema.

Anasema amri hiyo ilieleza kuwa madhumuni ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kuondoa ubaguzi wa aina yoyote masuala wa kiuchumi, kisiasa, kijamii na kisheria ambao hapo awali uliwagawa wananchi badala yake kuhimiza usawa, upatanisho.

Fatma anasema pia amri hiyo ilitaka kila mwananchi apate haki yake kama Mzanzibari.

“Ina maana kwamba, kutokana na amri hiyo madhumuni ya Mapinduzi yalikuwa ni kila Mzanzibari kupata haki sawa, Mswahili, Mwarabu, Mhadimu na Mshirazi,” anasema.

Fatma anasema madhumuni ya Mapinduzi yalikuwa kuhimiza umoja na mshikamo na kuchukua madaraka kutoka kwenye utawala wa kisultani na kuyaleta mikononi mwa wananchi.

“Tulihama kutoka kwenye uongozi wa kisultani na kuwa na Serikali yenye umoja na usawa kama yalivyo mapinduzi yoyote na ndiyo madhumuni yake hivyo ninavyoyaelewa,” anasema.



Malengo ya Mapinduzi yamefutika

Hata hivyo, Fatma anasema kwa sasa malengo ya Mapinduzi hayapo visiwani humo kutokana na sababu mbalimbali kubwa ikiwa ni pamoja na ubaguzi unaoendelea.

“Zanzibar hatuyasherehekei Mapinduzi na wala hatutimizi malengo yake kwa sababu kuna ubaguzi. Ubaguzi wa aina yoyote ni dhambi kubwa, hakuna kitu kibaya kama ubaguzi, ni kansa kwenye uongozi, ni kitu kibaya,” anasema.

Anasema mataifa yaliyoendelea yanakemea ubaguzi, lakini baadhi ya viongozi visiwani Zanzibar wameonekana kuupalilia ubaguzi ili waendelee kubaki madarakani.

Anasema ubaguzi huo unapaliliwa baina ya watu wa Unguja, Waarabu na Waafrika.

“Ubaguzi ukifanywa na Wazungu ni mbaya, lakini ukifanywa na Waafrika unaoenakana ni mzuri. Haiwezekani, hata ukiwa Mwafrika, ubaguzi ni mbaya, hiki ni kitu kibaya,” anasema.

Anasema ubaguzi ambao ulipingwa wakati wa Mapinduzi, unaonekana hata hapa Tanzania Bara. Anatoa mfano wa aliyekuwa mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania), Richa Adhia akisema alipingwa kwenda kwenye mashindano ya dunia na kuonekana hawezi kuiwakilisha Tanzania kwa kuwa ana asili ya India.

“Lengo la Mapinduzi ya Zanzibar ni kuondoa ubaguzi wa kila aina, lakini walio madarakani wanadhani wana haki ya kubagua kulingana na rangi,” anasema.

Fatma anasema: “Zanzibar ni sawa na chungu chenye kila kitu, kuna mchanganyiko mkubwa wa wahamiaji, kila mtu anakaribishwa. Kwa nini ubaguzi kuwapo.”

CCM haitakiwi kukaa madarakani milele

Anasema wakati tunasherehekea miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar leo ni lazima walio madarakani watambue kuwa madhumuni yake hayakuwa kuiweka CCM madarakani milele.

“Najisikia kusalitiwa, Mapinduzi yalifanyika wakati CCM haikuwapo, ilikuwapo ASP, lakini ASP haikupanga iwe madarakani milele, mimi nasimuliwa kuwa babu yangu aliwahi kusema; “Utafika wakati Zanzibar itatakiwa kuwa tayari kwa mfumo wa vyama vingi.”

Anasema: “Babu yangu aliyeyafanya hayo Mapinduzi, alikuwa anajua kuwa ASP haitakaa madarakani milele. Alikuwa anafahamu kuna wakati watu watachagua nani abaki madarakani. Huyu ni mwanaume ambaye pia aliamini demokrasia ndiyo mfumo wa Serikali.”

Anasema ingawa Mzee Abeid Karume alikuwa na uwezo wa kuamrisha kwamba ni lazima Serikali ibaki madarakani milele, lakini alikadiria ndani ya miaka 50 kuwe na mfumo wa vyama vingi.

“Lakini leo hii kuna watu ambao hawakushiriki Mapinduzi ya Zanzibar, lakini wanajitaja kuwa ndiyo warithi wa Mapinduzi na wanasimama hadharani wakisema hawajaipata Serikali kwa karatasi hivyo hawataitoa kwa karatasi,” anasema.

Fatma anaenda mbali na kusema hayo si malengo ya Mapinduzi ya Zanzibar bali malengo yalikuwa ni kurejesha nguvu kwa wananchi.

“Ni hatari, ni hatari sana, Mapinduzi si kitu chepesi, nchi zilizopitia zinajua hili, utaona kuwa hiki si kitu cha kuchukuliwa kwa wepesi, taasisi zinabadilika, watu wanabadilika, ni mpasuko,” anasema.

Anasema ni jambo la ajabu kuona viongozi wa CCM, hata Mwenyekiti wake hajachukua hatua na kukanusha maneno yanayosemwa na wanachama wa chama hicho.

“Mtu anasema hatukuipata nchi kwa karatasi na hatuwezi kuitoa kwa karatasi, lakini viongozi wake wala hawajitokezi kukanusha. Si vizuri kusikia maneno kama haya,” anasema.


Uchaguzi Mkuu 2015, Zanzibar

Fatma anazungumzia uchaguzi uliofutwa na kutangazwa kurudiwa tena visiwani humo akisema CCM itaendelea kupoteza watu kwa sababu imeshindwa kuwashawishi.

“Siasa ni ushawishi, kama umeshindwa kuwashawishi badala yake unawapelekea jeshi, unawapiga virungu ni dhahiri utawapoteza,” anasema.

Anasema mwanasiasa yoyote huvuna kile alichokipanda baada ya miaka mitano akidai hicho ndicho alichovuna Dk Ali Mohamed Shein katika uchaguzi uliopita Oktoba 25, mwaka jana.
Chanzo:Mwananchi

Ndoa yangu Hatarini, Napewa Unyumba kwa Kulazimisha

$
0
0
Wadau,

Nimeoa kama miaka mitatu iliopita tatizo nalotoka tubadilishane mawazo ni mwenza wangu mke kuanzia mwaka jana amekua akinipa unyumba kwa mbinde kweli.Naweza fukuzia wiki nzima nikawa napewa jibu nimechoka nimechoka, siku nikilazimisha anasema fanya basi, nibake sasa na mimi nakua nahamu nafanya bila ushirikiano wowote kama vile nafanya na maiti, lakini kutokana na ukame wakati mwingine namuacha chumbani na kwenda kufanya mastabesheni sebuleni.

Nimejaribu kila namna kujua tatizo nimeshindwa wakati mwingine shetani ananiingia nitafute mchepuko wa kukataa kiu yangu ila moyo mzito nampenda mke wangu lakini pia madhara ya kuchepuka mengi. Nimejitahidi kufwatilia kama kapata mtu mwingine hakuna ushahidi kwa hilo pengine anaridhishwa sijapata dalili hizo. Nimejitathimini kama nilimkosea hakuna hivyo nimeleta hapa mnisadie wadau kunusuru ndoa yangu.

Maana kunyimwa tendo la ndoa bila sababu maalumu napata wakati mgumu msaada kwa wakubwa humu.

Tatizo nini...tubadilishane uzoefu...

Salaam...wote inauma saana kutongoza wife ndani ya ndoa ili upate mzigo


 By Juma


Udaku Special Blog

Breaking News:Zitto Kabwe Atoa Kauli Nzito Kuhusu Bango la CCM Lililoleta Utata wa Kibaguzi Zanzibar

$
0
0
"Siasa za Hatari sana hizi, Siasa za kibaguzi. Siasa zinazopaswa kulaaniwa na kila mpinga ubaguzi nchini. Nitashangaa sana kama wakubwa CCM hamtaomba radhi kwa siasa hizi hizi mbaya kabisa. What will be the stop?"

By Zitto Kabwe

Udaku Special Blog

Wanawake Wavaa VIMINI Wacharazwa Bakora Hadharani Wilayani Sengerema, Mwanza

$
0
0
Viongozi wa Kitongoji cha Kasalazi, kilichoko katika Kijiji cha Kanyara, Kata ya Bulyaheke, wilayani Sengerema, Mkoa wa Mwanza, wanadaiwa kuwachapa fimbo hadharani wanawake wanaovaa nguo fupi zinazoonyesha baadhi ya sehemu zao za siri.

Pia, viongozi hao wanadaiwa kuwatoza faini ya Sh 20, 000 wanawake wanaokutwa na nguo hizo kama njia ya kuwafanya wasiendelee kuvaa nguo hizo.
Mmoja wa wasichana waliowahi kuchapwa na viongozi hao aliyejitambulisha kwa jina la Juliana Mafuru, alichapwa fimbo baada ya kufika kijijini hapo kwa lengo la kununua dagaa.

“Cha kushangaza ni kwamba, baada ya kufika katika kitongoji hicho, mgambo walinikamata na kunichalaza bakora mbele za watu nje ya boti niliyokuwa nimepanda.
“Pia waliamuru nivue suruali niliyokuwa nimeivaa na kuanza kuichana chana nyembe.
“Wakati wananifanyia hivyo, walitokea wasamalia wema ambao walinipatia shuka la kimasai ili niweze kujisitili, yaani waliniabisha kweli.
“Baadaye, walinipeleka kwenye ofisi ya kitongiji hicho na walinitoza faini ya shilingi 20,000, kisha wakaniachia,” alisema Juliana.\

Nao wakazi wa kijiji hicho, Lafael Bitulo na Mariamu Chacha, walisema mwenyekiti wa kitongiji hicho na katibu wake, ndiyo vinara wa tabia hiyo kwa kuwa wamekuwa wakinufaika nayo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, Andrea Mkama, alikiri kuwachapa fimbo wanawake wanaovaa nguo fupi na zinazobana kwa mavazi wanayovaa ni ya udharirishaji.
Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kanyara, Lazoro Mgonzo, alithibitisha wanawake kuchapwa fimbo ingawa alisema ni kitendo cha udharirishaji.
Mkuu wa Wilaya Sengerema, Zainabu Terack alipoulizwa juu ya tukio hilo, alisema hana taarifa ingawa aliahidi kulifuatilia

Udaku Special Blog

UVCCM yataka Rais mstaafu wa Zanzibar Dr Aman Abeid Karume Afukuzwe CCM

$
0
0
UMOJA wa vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), umekitaka chama hicho kumvua uanachama Rais mstaafu wa Zanzibar Dk  Aman Abeid Karume.

Kauli hiyo ilitolewa jana katika viwanja vya Maisara mjini Zanzibar na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Sadifa Juma Khamis wakati wa kilele cha matembezi ya vijana wa umoja huo kuadhimisha miaka 52 ya Mapinduzi.

Alimshushia tuhuma nzito mstaafu huyo kuwa anashirikiana na wapinzani kukihujumu chama hicho kikongwe nchini, na kwamba asipofukuzwa umoja huo utatumia njia zingine ambazo hakuziweka wazi.

Sadifa alionya kwamba Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar si mali wala miliki ya mtu kwani Wazanzibar wote wana haki ya kushiriki kuyaenzi kwa vitendo kutokana na historia yake.

Breaking News: CCM Yaomba Radhi Kutokana na Maneno ya Kibaguzi Kwenye Bango Katika Sherehe za Mapinduzi

$
0
0
CCM Yaomba Radhi Kutokana na Maneno ya Kibaguzi Kwenye Bango Katika Sherehe za Mapinduzi
Udaku Special Blog

Je ni Kweli Mwanamuziki Linex Ameoa Kama Picha Zinavyoonyesha Mtandaoni ?..Sikiliza Majibu yake Sasa Kupitia UHeARD)

$
0
0
Kama vile ambavyo huenda na wewe mtu wa nguvu umekutana na pichaz mitandaoni, Linex ndani ya suti yake kali kabisa, mrembo ndani ya gauni la nguvu !! Ilikuwa ndoa kabisa au ndio mambo ya cover ya mdundo njiani ?! Basi na Soudy Brown nae kazipata pichaz hivyohivyo..

Linex kaanza kujibu hivi maswali ya Soudy Brown kuhusu picha hizo >>> ‘Kusoma hujui hata picha huoni? Kwani mimi nina kasoro kwamba siwezi kuoa au?‘

Unahisi ni cover ya wimbo anaotaka kutambulisha? Jibu lake hili hapa ‘Sina single yoyote kwanza muziki wenyewe nimepumzika… picha za kanisani coming soon’ kamaliza hivyohivyo.


Sauti ya U Heard yote ya Soudy Brown na majibu ya Linex hii hapa kama umepitwa mtu wangu.

Serikali Yakusudia Kuanza Kuzalisha Drip za Maji za IV Katika Hospitali zake zote Kubwa Nchini

$
0
0
SERIKALI inakusudia kuanza kuzalisha drip za maji za IV (Intravenous Fluids) katika hospitali zake zote kubwa nchini.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati alipotembelea mtambo wa kutengenezea drip hizo za majimaji katika hospitali ya Mtakatifu Joseph ya Peramiho, Mkoani Ruvuma.

Amesema haoni kwa nini hospitali hizo ziendelee kuagiza wakati uwezo na watalamu wa kufanya hivyo upo hapa hapa nchini.

Drip hizo zina manufaa makubwa kwa wagonjwa ikiwemo kuongeza maji kwa wagonjwa waliopungukiwa na maji mwilini na vilevile inatumika kwa ajili ya kutolea baadhi ya dawa ambapo huchanganywa.

Udaku Special Blog

Nafasi za Kazi Umoja wa Mataifa, Application Deadline 15 and 27 January 2016

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Afika Muhimbili Kumjulia Hali Waziri Mkuu Staafu Fredrick Sumaye

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Waziri Mkuu, Mstaafu Frederick Sumaye  ambaye amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu Januari 12, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wapili kushoto) wakizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amnaye amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa Matibabu Januari 12, 2016. Kushoto ni Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Esther Sumaye.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole Balozi Hassan 
Kibelloh ambaye naye  amelazwa katika hospitali ya taifa y Muhimbili kwa Matibabu Januari 12, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Lugha za kibaguzi, Uvaaji wa Sare za Chama Kwenye Shughuli za Kitaifa, Mambo Haya Yawe "Criminalized"

$
0
0
CCM kuomba radhi,pamoja na watu mbalimbali kuendelea kukemea kitendo kilichotokea Zanzibar leo hii kwenye sherehe za Mapinduzi,nafikiri haya yote hayatoshi na wala hayatasaidi kitu na kwahivyo tunapaswa kuchukua hatua zaidi katika kukabiliana na matukio ya aina hii katika siku za usoni.

Kwa mtazamo wangu,wakati umefika tuwe na sheria,tena sheria kali, itakayozuia watu kuvaa sare za vyama vya siasa katika shughuli au matukio ya kitaifa.

Vile vile tunapaswa kuwa na sheria itakayokataza au itakayopiga marufuku kauli,vitendo na aina yoyote ya matukio ya kibaguzi au yenye mwelekeo wowote ule wa kibaguzi. Ubaguzi huu uwe wa rangi,dini au kabila.

Hili ni wazo tu ila naamini kuna wataalamu wa sheria wanaoweza kulifanyika kazi wazo hili na kuliboresha zaidi.

Wabunge mnao uwezo pia wa kupeleka hoja binafsi Bungeni kuhusu swala hili na si kuisubiri serikali tu ambayo nayo inaweza isilifanyie kazi wazo hili au ikachukua muda mrefu kulitekeleza.

Tujifunze kutokana na makosa na tuchukue tahadhari pia.

Udaku Special Blog

Kwa Hili la Samatta, Serikali Inafanya Double Standards...Mbona Diamond Hajawahi Fanyiwa Sherehe wala Kupewa Zawadi na Serikali?

$
0
0
Wapendwa wanajukwaa na watanzania kwa ujumla, ni dhahiri kwamba sote tunapenda kuona nchi yetu ikisonga mbele kitaifa na kimataifa katika michezo na sanaa mbalimbali. Tumeshuhudia baadhi ya vijana wetu wakifanya vinzuri kimataifa na kuiletea heshima tele nchi yetu.

Sasa pamoja na heshima hii nina jambo ambalo naliona hakika halijakaa sawa na pengine linaleta picha mbaya kwa wananchi kuanza kudhani labda ni michezo au sanaa za aina fulani tu ndizo ambazo serikali inazithamini. Ni wiki iliyopita ambapo tumeshuhudia mchezaji wa soka Mbwana Samatta akitangazwa kuwa mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika. Tumeshuhudia namna serikali ilivyomtembeza mtaani kama kumpongeza kwa tuzo aliyopata. Leo hii muda huu Vodacom na serikali wameandaa hafla ya kumpongeza kwenye Hotel ya Hyat Regend. Kwa mujibu wa posts zinazowekwa na Vodacom katika mtandao wa instagram ni kwamba Samatta amepewa zawadi na serikali pesa taslim na kiwanja huko Kigamboni. Napongeza kwa hilo ni jambo jema hasa katika kutia moyo.

Sasa hoja yangu inakuja hapa, je serikali inayatambua mafanikio ya mpira wa miguu peke yake na si sanaa zingine pia? Nasema hivi nikichukulia mfano Diamond Platinumz. Hakuna mtu asiyetambua mafanikio aliyopata Diamond katika muziki kiasi cha kuiletea heshima kubwa nchi yetu katika Afrika na dunia nzima kwa ujumla. Mbali na tunzo nyingi alizopata Diamond katika Afrika hii, ameweka historia ya kuwa msanii wa kwanza Afrika kushinda tunzo ya dunia inayotolewa na MTV. Ni msanii aliyewafanya waafrika na dunia kwa ujumla waanze kujifunza na kukielewa kiswahili hasa kutoka na nyimbo zake kutumia kiswahili na hata katika nyimbo anazoshirikishwa nazo anaimba kwa kiswahili. Ni msanii aliyefanya soko la mziki wa Tanzania likabadilika hasa katika suala la malipo wanayopewa wasanii katika matamasha na shoo wanazoalikwa. Ni mwanamuziki pekee wa Tanzania aliweza kuzivuta media za kimataifa kama BBC, Aljazeera na CNN kuweza kufanya naye interview.

Pamoja na mafanikio yote hayo hakuna hata kiongozi mmoja aliyediriki kumpa hongera Diamond kwa tunzo kubwa ya Dunia aliyoipata. Nimejiuliza sana na kudhani labda michezo na sanaa zinazothaminika na serikali ni mpira wa miguu tu.


Udaku Special Blog

DPP Adhamiria Kumrudisha Shehe Ponda Issa Ponda Kizimbani... Akata Rufaa Mahakama Kuu Kupinga Kuachiwa Kwake

$
0
0


MKURUGENZI wa Mashitaka (DPP) ameamua kukata rufaa Mahakama Kuu dhidi ya kesi ya uchochezi inayomkabili mwanaharakati wa Kiislamu Shehe Ponda Issa Ponda.

Mwanasheria Mwandamizi katika ofisi ya DPP, Bernard Kongola amesema kuwa Serikali inapinga kuachiwa kwa Shehe Ponda ambaye alishitakiwa kwa makosa ya uchochezi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.

“Tayari tumeomba tupatiwe nakala ya hukumu pamoja na nyaraka za mwenendo wa shauri hilo ili upande wa mashitaka tuweze kuandaa rufaa yetu Mahakama Kuu,” alisema.

Kwa mujibu wa mwanasheria huyo, tangu waombe kupatiwa nakala ya hukumu hiyo katika mahakama hiyo ya hakimu mkazi, hakimu ambaye alikuwa anasikiliza kesi hiyo bado hajawapatia upande wa mashitaka hukumu ambayo imechapwa.

“Hatujui kuna tatizo gani, maana tunapoomba kupatiwa nakala ya hukumu, hakimu amekuwa anatuambia kwamba bado hawajamaliza kuichapa, kwa kweli hii inashangaza,” alisema.

Novemba 30 mwaka uliopita, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Morogoro, Mary Moyo alimwachia huru Shehe Ponda kwa maelezo kuwa upande wa mashitaka ulishindwa kuthibitisha pasi shaka yoyote mashitaka dhidi ya mwanaharakati huyo wa Kiislamu.

Wakati kesi hiyo ilipokuwa inasikilizwa, upande wa mashitaka uliita mashahidi wanane kwa lengo la kuthibitisha makosa dhidi ya Shehe Ponda ambaye alikuwa anatetewa na Mawakili wa kujitegemea Juma Nassoro na Abubakar Salum.

Shehe Ponda alifikishwa katika mahakama hiyo Agosti 19, 2013 akikabiliwa na mashitaka matatu likiwemo la kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu iliyomtaka awe mhubiri amani katika jamii likiwa ni sharti la kifungo cha mwaka mmoja nje baada ya kumtia hatiani katika kesi ya jinai.

Upande wa mashitaka ulidai kuwa Shehe Ponda alitenda kosa Agosti 10, 2013 katika eneo la Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege iliyoko katika Manispaa ya Morogoro.

Ilidaiwa kuwa siku hiyo kiongozi huyo wa kidini alidaiwa kutoa maneno ya uchochezi ya kuhamasisha jamii kinyume na maelekezo ya mahakama.

Katika mkutano huo Shehe Ponda anadaiwa kusema maneno haya, “Ndugu Waislamu msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti, kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa CCM na Serikali na kama watajitokeza kwenu watu hao na kujitambulisha kwamba wao ni kamati za ulinzi na usalama za msikiti, fungeni milango na madirisha ya misikiti yenu na muwapige sana.”

Kauli hiyo inadaiwa kwenda kinyume cha amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Dar es Salaam, iliyotolewa mahakamani hapo na Hakimu Victoria Nongwa, Mei 9, 2013 ambayo ilimtaka ndani ya mwaka mmoja kuhubiri amani na asifanye jambo lolote la uvunjifu wa amani na badala yake ahubiri suala la amani, ambayo ni kinyume cha Kifungu cha Sheria Namba 124 cha Mwaka 2002.

Shitaka la pili lililokuwa likimkabili Shehe Ponda ni uvunjifu wa sheria Kifungu cha 129 cha Makosa ya Jinai kuwa siku hiyo, alitoa maneno ya uchochezi yaliyohatarisha kuathiri imani za watu wengine.

Katika hati ya shitaka hilo, ilinukuu kauli ya Ponda kuwa “Serikali ilipeleka Jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana na gesi kwa kuwaua, kuwabaka na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni Waislamu. Lakini Serikali haikufanya hivyo kwa wananchi wa Loliondo walipokataa Mwarabu asipewe kipande cha ardhi ya uwindaji baada ya kudai ni mali yao kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wake ni Wakristo.”

Shitaka la tatu anadaiwa kutenda kosa kinyume cha sheria kifungu cha 390 na 35 kwa kuchochea maneno dhidi ya wananchi wakati wa kongamano lililofanyika Agosti 10, 2013 Uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege.

Jecha wa ZEC Atoka Mafichoni.....Dk. Shein Asisitiza Uchaguzi Lazima Urudiwe Zanzibar

$
0
0

Hatimaye  Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, jana ameonekana hadharani katika maadhimisho ya sherehe za miaka 52 ya Mapinduzi zilizofanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.

Jecha ambaye inaaminika alikuwa mafichoni tangu alipotangaza kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar Oktoba 28, mwaka jana, alionekana ameketi kwenye jukwaa kuu la viongozi, jirani na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk. John Magufuli na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Kuonekana kwa Jecha hadharani kumezua mijadala mitaani na hata katika mitandao ya kijamii, huku wengi wakihoji alikuwa wapi mara baada ya kufuta matokeo ya uchaguzi.

Watu mbalimbali wamekuwa wakihoji kuonekana kwa Jecha hadharani jana, siku ambayo Dk. Shein alitumia maadhimisho ya Mapinduzi kutangaza kwamba uchaguzi wa marudio Zanzibar iwe isiwe utafanyika.

Oktoba 28, mwaka jana majira ya saa sita mchana kwenye Ofisi za Tume ya Uchaguzi Zanzibar zilizopo Kilimani mjini Unguja, ilikuwa ndiyo siku ya mwisho kuonekana Jecha hadharani.

Siku hiyo huku akiwa chini ya ulinzi wa vijana wawili wanaoaminika kuwa ni makomandoo wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania (JWTZ) waliovaa kiraia, Jecha alitangaza kuufuta uchaguzi wa Zanzibar mbele ya vyombo vichache vya habari.

Alitumia dakika mbili tu kuvitangazia vyombo hivyo vya habari juu ya adhima yake ya kuufuta uchaguzi na kutoa sababu zilizomfanya kufanya hivyo ikiwamo kuharibiwa kwa uchaguzi kisiwani Pemba.

Hata hivyo, baada ya kumaliza kutoa taarifa yake kwa vyombo hivyo, Jecha hakutaka kuulizwa maswali.

Oktoba 27, mwaka jana ikiwa ni siku moja kabla ya kutangaza kufuta matokeo ya uchaguzi, Jecha pia hakuonekana kwenye kituo cha kutangaza matokeo kilichokuwa katika Hoteli ya Bwawani kwa kile kilichodaiwa alipata matatizo ya kiafya na hivyo kumwachia kazi hiyo Makamu Mwenyekiti wa ZEC, Jaji Abdulhakim Ameir Issa.

Siku hiyo majira ya saa kumi jioni, askari wa JWTZ walizingira kituo cha Bwawani na kuwaamuru watu waliokuwa ndani kutotoka nje na hata wale walioko nje ya kituo hicho kutosogea.

Watu waliokuwa ndani ya kituo hicho wengi wao walikuwa waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi pamoja na baadhi ya wawakilishi wa vyama vya siasa waliofika kusikiliza matokeo ya uchaguzi.

Dr. Shein asisitiza Uchaguzi lazima urudiwe

Kutokana na kile kinachoonekana kuendelea kupasuka kwa hali ya kisiasa visiwani Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, amesisitiza uchaguzi utarudiwa baada ya awali matokeo yake kufutwa na ZEC.

Akihutubia katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 52 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Uwanja wa Amaan jana, Dk. Shein alisema uchaguzi huo utarudiwa kwa mujibu wa katiba na sheria.

“Kila mmoja anajua kilichotokea katika uchaguzi Zanzibar baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta uchaguzi kutokana na kasoro zilizogundulika kutokea wakati wa uchaguzi huo,” alisema Dk. Shein na kuongeza:

“Suala la kurudiwa kwa uchaguzi liko palepale na utarudiwa kwa mujibu wa katiba na sheria, hivyo nawaomba wananchi muwe na uvumilivu na upendo wakati tukisubiri kutangazwa kwa tarehe ya kurudiwa uchaguzi.”

Licha ya kwamba kila upande umeshaweka msimamo wake, lakini Dk. Shein alisema mazungumzo ya kusaka suluhu yanaendelea baina ya pande hizo na kwamba taarifa ya mazungumzo hayo itatolewa punde yatakapokamilika.

“Tangu kutokea kwa mgogoro huu tulishauriana kukutana viongozi sita waliopo madarakani na waliostaafu ili kufanya mazungumzo ya kusaka suluhu na taarifa itatolewa pindi mazungumzo yatakapokamilika,” alisema Dk. Shein.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya January 13, Ikiwemo ya Wema Sepetu Kuwa ni Mjamzito

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya January 13, Ikiwemo ya Wema Sepetu Kuwa ni Mjamzito

Karueche Amchokonoa Chris Brown....Atangaza Kuhitaji Penzi Sasa

$
0
0
ALIYEKUWA mpenzi wa staa wa pop, Chris Brown, mwanamitindo na muigizaji, Karreuche Tran amefunguka kwenye mtandao wa Twitter akisema kuwa kwa sasa amefungua milango ya uhusiano na kwamba yupo tayari kumpokea mpenzi baada ya kukaa mpweke kwa muda mrefu japo amedai itakuwa vigumu kumpata mpenzi wa kweli ambaye ataweza kumpa mapenzi ya dhati.

Udaku Special Blog

Mapya Kuhusu Chama cha Mapinduzi CCM Kuazimisha Kumbukumbu ya Kuzaliwa ya Miaka 39

$
0
0

Chama Cha Mapinduzi kila mwaka huadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwake Februari 05, 1977. Mwaka huu kitakuwa kinatimiza miaka 39.

UZINDUZI
Uzinduzi wa maadhimisho ya kumbukumbu ya hiyo utafanyika tarehe 31 Januari, 2016 Unguja, Zanzibar ambapo Mgeni rasmi atakuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Zanzibar, Dokta Ali Mohammed Shein.

KILELE CHA SHEREHE
Kilele cha maadhimisho hayo Februari 06, 2016 mjini Singida ambapo Mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dokta Jakaya Mrisho Kikwete.

Viongozi wa kitaifa na baadhi ya Wajumbe wa Kamati Kuu watakaohudhuria watapangiwa shughuli za ujenzi wa Chama na Taifa kwa ujumla katika wilaya zote za mkoa wa Singida siku tatu kabla ya kilele cha maadhimisho hayo.

Mikoa yote iandae shughuli mahsusi kwa wiki nzima ya maadhimisho hayo, mkazo ukiwa ni kufanya shughuli za ujenzi wa Chama na Taifa katika maeneo yao, Mambo ya kuzingatia katika wiki hiyo ni kama ifuatavyo:-

i. Kuingiza wanachama wapya wa CCM na Jumuiya zake na kufanya shughuli nyingine za kuimarisha Chama.

ii. Kufanya mikutano ya kuwashukuru wana CCM na wananchi kwa kuiamini CCM kuendelea kuongoza Nchi yetu kwa kushiriki na kukamilisha Uchaguzi Mkuu wa 2015 ambapo CCM ilipata ushindi wa kishindo wa Rais, Wabunge na Madiwani.

iii. Kuhamasisha wananchi kufanya kazi ili kujiletea maendeleo yao binafsi na ya Taifa.

iv. Kushiriki shughuli za maendeleo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa madarasa, zahanati, vituo vya afya, upandaji miti, uchimbaji wa mitaro ya maji, kufanya USAFI wa mazingira pamoja na shughuli nyingine za kijamii.

KAULIMBIU
Kaulimbiu ya sherehe hizo ni “Sasa Kazi, Kujenga Nchi na Kukijenga Chama”.

Nape Moses Nnauye (Mb.), 
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
ITIKADI NA UENEZI
13/01/2016

Udaku Special Blog

Viewing all 104747 articles
Browse latest View live




Latest Images