Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

SAKATA la Bomoa Bomoa Nyumba ya Mchungaji Getrude Rwakatare Mapya yaibuka

0
0

Mvutano kati ya Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kutaka kubomoa nyumba anayoishi Mchungaji Getrude Rwakatare umezidi kushika kasi mahakamani.

Hali hiyo ilitokea jana, baada ya wakili wa familia ya Mchungaji Rwakatare, Emmanuel Agustino kupinga maombi ya NEMC ya kutaka kuongezewa muda wa kuwasilisha maombi ya mapitio ya hukumu ya maridhiano inayozuia baraza hilo kuchukua hatua yoyote dhidi ya nyumba hiyo.

Hukumu hiyo ya maridhiano ilitokana na kesi iliyofunguliwa 2012 katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi na Robert Brighton, ambaye ni mtoto wa Mchungaji Rwakatare aliyepinga kubomolewa kwa nyumba hiyo kwa madai kuwa imejengwa mahali pasiporuhusiwa.
Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Hamisa Kalombola Mei 11, 2015, pamoja na mambo mengine, alisema pande zote zilikubaliana kuwa, NEMC na wadau wake wasimbughudhi Brighton katika makazi hayo.

Hata hivyo, Desemba 29, 2015, NEMC ilifungua tena maombi ya kutaka kupatiwa kibali cha kuongezewa muda wa kuwasilisha maombi ya kufanya mapitio ya hukumu hiyo.

Katika maombi hayo namba 825 ya mwaka 2015, NEMC inadai kutoitambua hukumu hiyo na kwamba, uamuzi huo ulifikiwa na mwanasheria wake ambaye hakupatiwa idhini na NEMC.

Hata hivyo, wakati maombi hayo yalipotajwa mahakamani hapo Jumatatu wiki hii, Wakili Agustino kwa niaba ya mjibu maombi (Brighton), aliwasilisha hati ya kiapo kinzani dhidi ya hati ya kiapo cha NEMC kilichoapwa na Mkurugenzi wake Mtendaji, Bonaventure Baya akipinga maombi hayo ya NEMC.

Jaji John Mugeta anayesikiliza shauri hilo, aliamuru watoa maombi wawasilishe mahakamani hapo majibu ya kiapo kinzani cha mjibu maombi kabla ya Januari 20 na akapanga kusikiliza maombi hayo Januari 21, 2016.

Udaku Special Blog

ROSE NDAUKA Afunguka Kuhusu Nyumba yao Kubomolewa...Adai Hawezi Shikwa na Presha Kama Wastara

0
0
WAKATI mamia ya wakazi wa Dar es Salaam waishio mabondeni na pembezoni mwa bahari na mito wakihaha nyumba zao kuvunjwa, staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka amesema hajali kama nyumba yao itakutwa na bomoabomoa hiyo.

Badala yake, alimpongeza Rais John Magufuli kwa kusimamia zoezi hilo, kwani wengi wa wanaobomolewa walishapewa taarifa mapema na hawakutii agizo hilo la serikali, lakini akaitaka kuwaangalia kwa jicho la tatu watu ambao hawakupewa taarifa za zoezi hilo.

 “Wazazi wangu wakibomolewa nyumba naona kawaida tu, siwezi kuwa na presha maana kila kitu kinapangwa na Mungu, kama ni kubomoa wabomoe tu hatuna la kufanya,” alisema Rose.

Global Publishers

Udaku Special Blog

JE Umewahi Kusikia Tetesi Kuwa Mwigizaji Ray na Chuchu Hans Wamemwagana? Basi Chuchu Hans Kasema Haya

0
0
Chuchu Hans na Ray Mahabani
Msanii wa filamu nchini, Chuchu Hans amesema bado yupo kwenye uhusiano wa kimapenzi na Vicent Kigosi aka Ray licha ya hivi karibuni baadhi ya watu kudai wawili hao hawapo tena pamoja.

Akizungumza katika kipindi cha Take One cha Clouds TV Jumanne hii, Chuchu alisema toka aanze kutoka kimapenzi na staa huyo mengi yamezushwa juu yake.

Sasa hivi haya mambo ya mitandao yanapotosha sana jamii na watu wanataka ufanye kile wanachotaka,” alisema. “Sijaachana Ray na wala hatuna mpango huo sema kuna baadhi ya mashabiki kwenye mitandao ya kijamii wanataka tuishi maisha yao kitu ambacho hakiwezekani.

Pia Chuchu alisema madai ya kuachana na Ray yamekuja baada ya kufuta baadhi ya taarifa za mpenzi wake katika mtandao wa kijamii.
Chuchu Hans Katika Pozi

Sisi tulikuwa na utaratibu mimi nikipost kitu na Ray anapost kitu lakini baada ya kuacha watu wakajua si tumeachana lakini sisi tupo safi kabisa,” alisisitiza Chuchu.

Hata hivyo mwanadada huyo amewataka watu wa kwenye mitandao ya kijamii kuacha tabia za kumtukania wazazi wake pamoja na ndugu zake kwani wao hawahusiani na mambo yake binafsi.

Udaku Special Blog

NDOA ya Wastara na Mbunge wa CCM Nusura Itoe Uhai wa Bond Aliyekuwa Boyfriend wake

0
0
DAR ES SALAAM: Zikiwa zimepita siku chache tangu staa wa filamu, Wastara Juma kufunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge,  Zanzibar, Sadifa Juma aliyekuwa mpenzi wake, Bond Suleiman nusu afe, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili.

Wakizungumza na gazeti hili, ndugu wa karibu wa kijana huyo ambaye pia ni muigizaji (jina linahifadhiwa) alisema siku moja kabla ya ndoa ya Wastara, Bond alitaka kujiua kwa kunywa sumu, lakini kaka yake aliyeingia chumbani kwake ghafla, akamuwahi kabla hajaibugia.

Ni Mungu tu Bond kuwa hai mpaka sasa, japokuwa hayupo vizuri ni kama amepaniki kutokana na Wastara kuolewa, maana bado anampenda, ungekuta sasa hivi tunaongea mengine, kwani alikuwa ameshaweka sumu tayari anywe, lakini alisahau kufunga mlango ikawa ndiyo salama yake baada ya kaka yake kuingia chumbani kwake akiwa anahitaji kuzungumza naye ndipo akakutana na ishu hiyo na kufanikiwa kumuokoa.

Ukweli hata sisi tumeumia sana Wastara kuolewa na mtu mwingine kwani tulikuwa tukimfahamu kwamba atakuja kufunga ndoa na Bond maana aliwahi kuletwa kutambulishwa kwa ndugu,” alisema ndugu huyo.

Mwaka 2015, Wastara na Bond wakilishana keki kwenye birthday

Gazeti hili lilimtafuta Bond ili kupata ukweli wa habari hizo, ambapo alikiri kuokolewa na kaka yake baada ya kutaka kunywa sumu kutokana na Wastara kuolewa.

Nilikuwa nimeshaandaa sumu kabisa na Wastara nilimuaga kwa njia ya meseji na hii ni baada ya kuniambia siku inayofuata anaolewa, ukweli nilimpenda na najuta maana mimi ndiyo nilifanya makosa na kumkosea sana, lakini siku niliyoamua kuachana na mambo ya ufuska na kuwa mtu wa sala muda wote, naye naona ndiyo akasema basi hanitaki tena.

“Nilijitahidi sana kumuomba msamaha lakini akanikatalia na kusema amempata atakayempa faraja ya moyo, namtakia maisha mema ya ndoa na nitamsubiri kama ndoa itavunjika nitamuoa maana mwenyewe wakati anasubiri kufunga ndoa (Alhamisi iliyopita) aliniambia kwamba anaogopa ndoa hiyo,” alisema.

Chanzo: Global Publishers

Udaku Special Blog

DIAMOND Platnumz Ashutumiwa Kuwabania Wenzake Connection za nje...Mwenyewe Adai Anatumiwa na MTV Base Kupitisha Video za Kuchezwa Kwenye TV Hiyo

0
0
Kama Diamond akisema ‘Hapana’ huenda video ya msanii wa Bongo isipate mwanga wa siku kwenye playlist za kituo cha runinga cha MTV Base.

Hata hivyo amesema nafasi hiyo huitumia kuwabeba wasanii wengi wa Bongo Flava kwa kadri awezavyo.

Alisema anawashangaa wasanii wanaomtupia maneno kila kukicha kuwa anawabania wasanii wengine ‘connections’ za kung’ara kimataifa.
“Mimi nashangaa sana kusikia hayo maneno, wanasema hivyo wakati mi najitahidi kuwasaidia wenzangu tutoboe wote, kila kolabo ya msanii wa nyumbani na msanii wa Nigeria inayofanywa mi ndio huwa nasababisha,”alisema.

Nikiamua kubana mbona naweza tu, kwa sababu vituo vingi vya nje vinanisikiliza kwa mfano tu MTV wenyewe wakipokea video ya msanii yeyote kutoka hapa (Tanzania) wananipigia wananiuliza kwanza huyu vipi? Tuicheze ngoma yake au? Mimi huwa nasema tu anafanya vizuri huku, basi inapita wanaicheza nikiamua kubana si naweza tu?”

Pia Diamond alisema timu yake ya Wasafi ndiyo ilivishauri vituo vya runinga vya Sound City na MTV kuanzisha chati za Afrika Mashariki.

Source:Times FM website

 Udaku Special Blog

Waziri Muhongo Aahidi Kuongeza matumizi ya Umeme wa Makaa ya Mawe

0
0
Serikali imesema itahakikisha makaa ya mawe yanakua chanzo kingine kikubwa cha uzalishaji wa umeme nchini ili kupunguza gharama za umeme zilizopo hivi sasa.

Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameyasema hayo  alipotembelea mgodi wa makaa ya mawe wa Ngaka uliopo wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma na kuongeza kuwa serikali itahakikisha inafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na mgodi huo ili kuimarisha uchumi wa taifa kupitia makaa ya mawe.

“Nimeelezwa makaa ya Ngaka yana  ubora na kiwango cha hali ya juu na nimeelezwa  kwamba kuna baadhi ya viwanda vimeingia mkataba na Ngaka lakini  badala yake wananunua makaa kutoka nje. Hilo halikubaliki ikiwa makaa ya ndani ya nchi yana ubora lazima tutumie bidhaa za nyumbani,”amesisitiza Prof. Muhongo.

Kutokana na malalamiko ya Mgodi kuhusu hali ya Mkataba ya kuuziana makaa kutoafikiana, Waziri Muhongo ameutaka mgodi huo,Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC),EWURA, Kampuni za Saruji za Dangote, Tanga Cement na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) kukutana Makao Makuu ya Wizara tarehe 14 Januari,2016, ili kujadili  kuhusu suala hilo na pia kujadiliana juu ya  gharama za kuuziana umeme na TANESCO pindi mgodi huo utakapoanza kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Masoko wa mgodi wa Ngaka, Christopher Temba, mgodi huo unazalisha tani za makaa ya mawe laki tano kwa mwaka na tayari makaa hayo yanasafirishwa katika nchi za Kenya, Zambia, Malawi na vilevile katika viwanda kadhaa hapa nchini vikiwemo vya  Saruji, Mohamed Enterprises na viwanda vingine.

BREAKING NEWS:Jeshi la Polisi Latoa Kauli Kali Kwenda kwa Mabenki Kuhusu Ujambazi Dar

0
0
Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na Operasheni kali inayoendelea jijini Dar es Salaam Na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.

WAMILIKI wa Taasisi za Kifedha wanatakiwa kujiridhisha kama waajiliwa katika taasisi hizo kama wanahusika kwa njia moja ama nyingine katika uharifu unaohatarisha maisha ya wakazi wa jijini la Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa na  Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za makao makuu ya Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam leo.

Kamanda Sirro amesema kuwa hatua za makusudi zimechukuliwa katika maeneo mbalimbali hasa ya eneo la Kibiashara la Mlimani City kutokana na matukio mengi ya uporaji  wa fedha kwa kutumia pikipiki.

Pia amesema kuwa pamoja na sheria hizo kuchukuliwa watafanya operasheni maalumu katika eneo hilo na kutafuta namna nzuri ya kuondoa pikipiki katika maeneo hayo.

Katika Operasheni zilizofanywa na Jeshi hilo wamefanikiwa kuwakamata majambazi nane pamoja na kumamata Bunduki mbili aina ya Pump Action ambazo namba zake zilifutwa na kukatwa Mtutu.
Aidha Kamanda Sirro amesema kuwa katika Operasheni hiyo wamemkamata jambazi aliyekuwa akitafutwa kwa muda mrefu anayejulikana kama Mkama Hassan mkazi wa Gomgolamboto jijini Dar es Salaam na alipopekuliwa alikutwa na Bastola aina ya Chinese iliyofutwa

Udaku Special Blog
.

TETESI za Ujauzito wa Wema Sepetu Zawa Gumzo, Yadaiwa Hamjui Mwenye Mimba Hiyo Kama ni Idriss ama Mbunge

0
0
Habari zinazosambaa kwa kasi ya ajabu kama moto wa kifuu zinaeleza kuwa, mtoto mzuri ndani ya Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ mbali na taarifa za kuwa mjamzito, hadi sasa bado yupo kwenye wakati mgumu kuweza kutegua kitendawili cha nani mmiliki halali wa kiumbe kilichopo tumboni mwake, Risasi Mchanganyiko linakupa habari kamili.


Hivi karibuni, magazeti tofauti ya Global Publishers ndiyo yalikuwa ya kwanza kuripoti kuhusu uwepo wa mimba ya mlimbwende huyo asiyechuja Bongo, ambapo awali, vyanzo mbalimbali vilieleza kuwa mhusika ni mbunge mmoja machachari ambaye ndiye anayemuweka Wema mjini kwa sasa.


MAJIBU YA WEMA ALIPOBANWA
Kwenye habari ya awali iliyoripotiwa na gazeti la Ijumaa, Wema alipotafutwa kusomewa mashitaka yake kuwa ana ujauzito wa mbunge huyo, kupitia simu ya shosti wake, Aunt Ezekiel, staa huyo hakutaka kufunguka sana kuhusu mbunge huyo zaidi ya kusema; “ndiyo nina mimba, tena ya miezi sita.”

UBUYU MPYA SASA
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, Miss Tanzania  huyo wa mwaka 2006 amejiridhisha kuwa ni mjamzito baada ya kupima kwenye hospitali moja maarufu (jina tunalo) na kuondoka na furaha ya ajabu lakini kitendawili alichoondoka nacho ni kuwa hamjui mhusika wa kiumbe hicho.

WOTE AWAPA ASILIMIA 50
“Madam alifurahi kweli maana suala lililokuwa linamnyima usingizi siku zote ni kutopata mimba. Baada ya furaha hiyo, ishu ikawa ni kumtambua mhusika kwani kwa nyakati tofauti ameshabanjuka kimalavidavi na mshindi wa Big Brother Hot Shot 2014, Idris Sultan na mbunge yule anayempa jeuri ya pesa kwa sasa, wote amewapa asilimia hamsini hajajua nani hasa ndiyo mhusika,” kilisema chanzo hicho.

WOTE WAWILI KAWAMILIKISHA
Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, baada ya kuona ameshachanganya madawa, Madam aliamua kila mmoja kumwambia kuwa ‘mzigo’ huo ni wake hivyo wote kwa pamoja na nyakati tofauti wanahudumia na kumjali staa huyo, tena kwa nguvu zote.
“Yaani kila mmoja kamwambia mimba yake. Wote wawili wamezipokea taarifa za ujauzito kwa bashasha huku kila mmoja akijiamini kuwa ni mhusika pasipo kujua Madam hajui nani hasa ndiye halisi.

MBUNGE, IDRISS ‘FULL’ KUHUDUMIA
“Yani ni full kuhudumia. Mbunge kwa wakati wake amekuwa akimwaga chapaa kama hana akili nzuri. Amelipia nyumba ile ya Ununio jijini Dar na kama hiyo haitoshi, amekuwa akisimamia shopping za maana tu mjini na hata ile ndiga aliyojizawadia Wema katika sherehe yake ya kuzaliwa, mbunge huyo alihusika katika malipo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Idris naye si haba. Anajitutumua kwa upande wake, anaamini kwamba mzigo ni wake bila kujua mimba hiyo ina figisufigisu.”

IDRIS ASAKWA, AFUNGUKA
Gazeti hili lilimtafuta Idris kupitia simu yake ya mkononi ambapo alipopokea, alitiririka hivi:
Risasi: Mzee tumepata habari kwamba wewe ndiyo mhusika wa mimba ya Madam, vipi unazungumziaje taarifa hizo?

Idris: Kwenye hilo kwa sasa siwezi kuliongelea, labda unipe mwezi mmoja. Kichwa changu hakijatulia.
Risasi: Lakini inasemekana unagharamia kila kitu kwa sasa, ukiamini mzigo ni wako?
Idris: Aaa! Acha kuniingizia hayo mambo bwana. Wewe subiri huo mwezi mmoja ukipita nitakueleza kila kitu.

SHOGA ZAKE WAMSHANGAA!
Mashosti wake waliozungumza na Gazeti hili ambao hawakutaka kutajwa majina yao, walisema ni jambo la kushangaza kwa mwanamke kushindwa kumjua mwanaume aliyempa ujauzito.

WEMA ANASEMAJE?
Gazeti hili lilifanya jitihada za kutosha kumsaka Wema kwa kumpigia simu na kumtumia ujumbe mfupi lakini hakupokea wala kujibu ujumbe huo.

KUTOKA KWA MHARIRI
Mimba ni jambo la kheri hivyo kwa kuwa Wema ameziona simu za wanahabari wetu zikimuuliza juu ya mhusika wa kiumbe hicho, ni vyema akawapigia na kuanika kila kitu kuhusu habari hii.

CHANZO: Global Publishers (GPL)


Udaku Special Blog

Studio ya Music ya 'The Industry' Inayoongozwa na Producer Nahreel Yamtangaza Rasmi Msanii Mpya wa Kike Aliyejiunga Nao

0
0

THE INDUSTRY MUSIC LABEL

TAARIFA KWA UMMA

UTAMBULISHO WA MWANAMUZIKI MPYA WA STUDIO YA MUZIKI YA “THE INDUSTRY”


Uongozi wa Studio ya Muziki ya The Industry iliyoko chini ya Wanamuziki Producer Nahreel na Aika Marealle unapenda kuchukua Nafasi hii kuwatangazia Umma Kuwa kuanzia Tarehe 14 January 2016 Wamemuingiza Msanii mpya wa Kike aitwaye Rosa Ree, Rose Ree ni muimbaji wa Muziki aina ya Rap ambae kazi zake zitaanza kusikika/Kuonekana siku si nyingi kuanzia sasa katika Redio Mbali mbali na TV Stations za Tanzania na nje ya nchi.

Kama wasikilizaji na watazamani tunaomba Kumuunga mkono Msanii huyu mpya Kwani tuna uhakika hatawaangusha katika kuwaletea burudani Katika Masikio na macho yenu pindi kazi zake zitakapoanza kutolewa hivi karibuni.
Instagram anajulikana kwa jina la @rosa_ree

The Industry ni studio na kampuni ya muziki ambayo ipo chini ya kundi la music lenye Mafanikio makubwa la Navy Kenzo ikisimamiwa na Producer Nahreel na msaidizi wake Aika Marealle

Wasanii Baadhi Waliokwisha fanya kazi na Studio ya The Industry mpaka sasa toka kuanzishwa kwake hivi karibuni ni Diamond Platnumz na wimbo wake wa Nana, Nikki wa Pili na wimbo wa Baba Swalehe, Joh Makini na nyimbo zake kama Don’t Bother na nusu nusu.

Imetolewa na,
The Industry PR
John Kiandika

Serikali Yamzawadia Samatta Kiwanja Na Fedha

0
0


Mchezaji Mbwana Samatta aliyejishindia Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wa Ndani nchini Nigeria amezawadiwa na serikali kiwanja kilichopo Kigamboni jijini Dar es salaam na fedha taslimu ambazo kiasi chake hakijafahamika. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh.Lukuvi anayeonekana katika picha  katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Hyyat Regency jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi kadhaa wa serikali.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria katika hafla hiyo ni Waziri wa Habari, Utamaduni,  Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Elisante Ole Gabriel na viongozi wengine wengi wa serikali na wanamichezo.

Nape Toa Mpya..Aitaka Chadema Kumfukuza Edward Lowassa

0
0

CCM imemjibu mwanasheria Mkuu wa Chadema ikisema ili chama hicho kikuu cha upinzani kionekane kinapambana na ufisadi kwa vitendo, kinatakiwa kumuunga mkono Rais John Magufuli na kumvua uanachama Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho tawala, Nape Nnauye alisema Chadema iliachana na ajenda ya kupambana na ufisadi baada ya kumpokea Lowassa  Julai mwaka jana baada ya jina lake kukatwa katika mchakato wa CCM kusaka mgombea wake wa urais.

“Sisi hatukumpitisha (Lowassa) awe mgombea wetu wa urais kwa sababu hiyo (ya ufisadi) na ndiyo maana yeye mwenyewe aliamua kuondoka na kwenda Chadema,” alisema Nape.

“Hata katika kampeni za uchaguzi mkuu, Chadema hawakuzungumzia ajenda ya ufisadi, ni kama Lowassa aliifunika tu.”

Alikuwa akimjibu Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu ambaye  juzi alisema ufisadi ni ajenda ya kudumu ya chama hicho kwa kuwa Rais Magufuli hataweza kuufumua wote katika kipindi cha miaka mitano.

Huku akichelea kueleza kiundani sababu za CCM kutomfukuza Lowassa kwa tuhuma za ufisadi mpaka alipoamua kujiondoa na kujiunga na Chadema, alisema kauli ya Lissu inalenga kuwahadaa Watanzania.

“Kauli ya Lissu ni ya kushangaza sana. Sisi tunajua jinsi ambavyo Chadema na washirika wake walivyojitenga na ajenda ya ufisadi. Kama kweli wanaupinga, basi wamuunge mkono Rais Magufuli ambaye kwa sasa anapambana na ufisadi kwa kasi,” alisema mbunge huyo wa Mchinga.

“Wakati mwingine kila jambo hufanyika kwa wakati wake. Suala la kupinga ufisadi CCM lilianza siku nyingi tangu enzi za kujivua gamba. Tumeendelea nalo mpaka watu wakajiondoa wenyewe,” alisema Nape.

Alisema hoja ya kupinga ufisadi ndani ya CCM ilikibeba chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kikapata ushindi mnono, huku Chadema iliyokuwa ikilia na ufisadi ikishindwa.

 “CCM tulieleza sababu za kutompitisha Lowassa kugombea urais na hilo lilikuwa wazi,” alisema.

Katika ufafanuzi wake wa juzi, Lissu alisema ili apambane na ufisadi, Rais Magufuli anapaswa kuacha tabia za CCM na kumtaka mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) amtangaze mshindi halali wa Uchaguzi Mkuu ambao Chadema wanaamini Maalim Seif Sharif Hamad alishinda.

Pia Lissu alimtaka Rais ataje majina ya waliokwepa kodi ili kama watajitokeza kuwania uongozi, wadhibitiwe kwa kuwa Katiba imezungumza kwa maneno makali dhidi ya vitendo hivyo viovu.

Aidha, aliponda uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo anayetajwa kuhusiska katika sakata la uchotwaji wa Sh3060 bilioni kutoka akaunti ya Tetega Escrow.

Miaka 39 ya CCM

Akizungumzia maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM, Nnauye alisema uzinduzi utafanyika Januari 31, visiwani Zanzibar na mgeni rasmi atakuwa makamu mwenyekiti wa chama hicho na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein.

Alisema kilele cha maadhimisho hayo kitakuwa Februari 6, mjini Singida na yataongozwa na mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete ambaye aliiongoza Serikali ya Awamu ya Nne.

“Viongozi wa kitaifa na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu watakaohudhuria maadhimisho haya watapangiwa shughuli za ujenzi wa chama na taifa katika wilaya zote za mkoa wa Singida, siku tatu kabla ya kilele cha maadhimisho,” alisema.

Alisema mikoa yote nchini inapaswa kuandaa shughuli hiyo wiki moja kabla ya maadhimisho, na kwamba lengo ni kufanya shughuli za ujenzi wa chama hicho katika maeneo yao.

“Tutakachokifanya wiki hiyo ni kupokea wanachama wapya, kufanya mikutano ya kuwashukuru wananchi kwa kuiamini CCM na kuichagua iendelee kuongoza, kuhamasisha wananchi kufanya kazi ili kujiletea maendeleo,” alisema.

Hatimaye Lowassa Nae Amtambelea Kumjulia Hali Swahiba Wake Sumaye

0
0

Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa, amemtembelea Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye, katika taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Hosptitali ya Taifa Muhimbili alikolazwa.

Lowassa ambaye alifika hospitalini hapo jana saa 7:00 mchana akiwa na mke wake Regina, aliwapongeza viongozi wengine ambao wamekwisha kufika hospitalini hapo kumjulia hali Sumaye, wakiwamo Rais John Magufuli, Rais Mstaafu na Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Lowassa alisema hilo ni jambo jema la  kiungwana, la kuheshimiana na kutendeana mema.

Wengine waliomtembelea Sumaye hospitalini hapo ni Waziri Mkuu Mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema,  Prof. Mwesiga Baregu.

KASI ya Magufuli Yaingia Vyuoni..Sasa Vyuo Vyote Visivyo na Sifa Kufutwa

0
0

Serikali ina mpango wa kukagua vyuo vikuu vyote nchini na vile ambavyo vitakuwa havina sifa itavifunga bila kusita kwani haitaki watanzania wafanyiwe majaribio katika elimu.

Taarifa hiyo imetolewa na waziri wa Elimu,Prof. Ndalichako ambaye amesema vyuo vingi havina sifa licha ya vyuo hivyo kupewa ithibati.

Prof. Ndalichako amesema inatakiwa angalau asilimia 50 ya walimu katika kila chuko kikuu kimoja wawe na shahada ya uzamivu(Ph.D) na kwamba haitakiwi mwalimu mwenye shahada ya kwanza kufundisha wanafunzi wa shahada ya kwanza.

Prof. ameongeza kuwa uwepo wa vyuo vingi visivyo na sifa kunapelekea uwepo wa vijana wengi wasio na ajira mitaani na hivyo kuongeza hasira.

Chanzo: Nipashe

Lissu: Tunataka Rais Magufuli atuambie waliokwepa Kodi ni kina nani

0
0

Akihojiwa na gazeti la Mwananchi Mh Tundu Lissu amesema, tunataka Rais Magufuli atuambie, waliokaepa kodi bandarini ni kina nani na kwanini hatuwaoni Mahakamani.

Hatutakubali atuambie tu ameongeza makusanyo ya kodi. Atuambie waliokwepa wako wapi maana kukwepa kodi ni kosa kubwa kisheria"alisema Lissu"

Papa Francis (VATICAN), Ana Ushawishi Gani Zanzibar? Maalim Seif Amuomba Kusaidia Kupatikana Suluhuya Urais

0
0

Out of Curiosity!

Imeripotiwa katika vyombo vya habari leo kuwa Maalim Seif, anayedai kuwa alipokwa ushindi katika uchaguzi mkuu wa Zanzibar mwaka jana, amemuomba Papa Francis kusaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa mvutano unaoendelea visiwani humo.

Nimejiuliza tu Papa au Vatican ina uwezo au ushawishi wowote katika kuingilia siasa za Zanzibar?!


Jengo la Ghorofa 16 Mali ya NHC Lilojengwa Chini ya Kiwango Mikononi Mwa Lukuvi..Atoa Siku 18 Jengo Libomolewe

0
0


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ametoa siku 18 kwa uongozi wa Manispaa ya Ilala kuvunja jengo la ghorofa 16 lililopo katika Mtaa wa Indira Gandhi kabla halijaleta maafa.

Akizungumza jana katika jengo hilo, Lukuvi alisema anashangaa hadi sasa kazi ya kuvunja jengo hilo haijaanza licha ya manispaa kuelekezwa kulivunja.

Uamuzi wa Serikali  kulivunja ulikuja baada kuporomoka kwa jengo katika mtaa huo lililosababisha vifo vya watu 37 na wengine 18 kujeruhiwa mwaka 2013.

“Ni aibu, manispaa mnataka jengo hilo liporomoke na kuua watu tena! Tutachekwa kwa uzembe kama ikitokea tena ajali,” alisema.

Lukuvi alisema kuanzia Februari Mosi uvunjaji wa jengo hilo unatakiwa kuanza vinginevyo wahusika wajiandae kuchukuliwa hatua.

“Nataka nikipita hapa siku yoyote kuanzia mwezi ujao nikute mkandarasi anabomoa jengo hili vinginevyo hatutaelewana,” alisema.

“Hili ni eneo hatarishi hata tuliosimama hapa hatari yoyote inaweza kutukuta lakini Manispaa ya Ilala haioni kwamba hapa kuna tatizo,” alisema.

Waziri alisema uvunjaji wa jengo hilo utakapoanza, wananchi wanaoishi jirani watatakiwa kuhama kwa muda kwa tahadhari.

“Mkuu wa Wilaya ya Ilala, wakianza kuvunja jengo hilo tafadhali waondoeni wakazi wote kwa sababu eneo hili litakuwa hatarishi,” alisema.

Jengo hilo linamilikiwa kwa pamoja kati ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na Ali Raza Investment.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Isaya Mngulumi alisema kilichochelewesha ni makandarasi walioshinda zabuni hiyo kujitoa katika hatua za mwisho wakitoa sababu mbalimbali.

Alisema hivi sasa amepatikana mkandarasi Patty Interplan ambaye yuko katika hatua za mwisho za kupewa kazi hiyo.

“Tutaanza kazi kama ulivyoelekeza,” alisema Mngulumi.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi, alisema atatoa ushirikiano kwa manispaa hiyo ili kuhakikisha jengo hilo linabomolewa.

Mwanajeshi Amuua Mkewe Kwa Kumcharanga Mapanga..Ajipeleka Polisi Mwenyewe Polisi Washindwa Kumwamini na Kumwachia

0
0

Tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Jumatatu, wiki hii, katika eneo la Kwa Mpenda, Kata ya Kivule, Chanika wilayani Ilala. 
Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni mpangaji wa nyumba ya mtuhumiwa, Hellena Musa, aliiambia Nipashe kuwa wanandia hao walianza kugombana saa 5:45 usiku. 

Alisema Mahende alifunga mlango wa geti, walipokuwa wanagomabana chumbani, ambapo alikuwa akimpiga mkewe na kitu chenye ncha kali.

“Walikuwa wanagombana mara kwa mara. Baada ya kuona ugomvi huo umechukua muda mrefu, tulikwenda kuchungulia dirishani kwake ndipo tukamwona anachoma mwilini kwa kutumia kitu chenye ncha kali ambacho kipo kama chuma,” alisema.

Aliongezea kuwa: “Walikuwa wakitoka chumbani na kukimbilia sebuleni. Tulishindwa kumwokoa huyu mama kwa kuwa mlango ulifungwa na jambo lingine ni kwamba huyu baba ni mkali hivyo tukawa tunaogopa,” alisema.

Kwa mujibu wa shuhuda huyo, ugomvi huo ulidumu kwa zaidi ya saa mbili na baada ya muda, alifanikiwa kutoka nje ambapo aliweza kupiga hatua tano na kuanguka na ndipo mtuhumiwa huyo alipomfuata na kumpiga na kitu chenye ncha kali kwenye kisogo.

Baada ya kufanya hivyo, alisema mtuhumiwa alichukua panga na kuanza kumcharanga mkewe kisogoni na hatimaye kupoteza maisha majira ya saa nane usiku.

Alisema baada ya kufanya hivyo, mtuhumiwa alimfunika mkewe na kwenda kupiga deki chumbani kwake kuondoa damu zilizokuwa zimetapakaa. 

Shuhuda huyo alisema mtuhumiwa alikwenda kujisalimisha kituo cha polisi cha Sitakishari na baada ya muda mfupi, alirudi nyumbani na kuondoka tena ilipofika saa 12 asubuhi.

Gazeti hili lilizungumza na ndugu wa karibu wa mtuhumiwa ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, ambaye alisema tukio hilo limewasikitisha kwa kuwa alivyopatiwa taarifa hawakuamini kilichomkuta ndugu yao.

Alisema alipatiwa taarifa saa nane usiku wa kuamkia Jumatatu ambapo ilimbidi afike eneo la tukio kujionea hali ilivyokuwa.

Ndugu huyo alisema alipofika eneo la tukio, alikutana na kaka wa mtuhumiwa na mtuhumiwa mwenyewe ambapo walimwuliza ni kitu gani kilichomkuta na kueleza kuwa tayari ameshammaliza bila kutaka kutoa maelezo ya kile kilichosababishia.

Alisema anachoelewa ni kwamba watu hao wawili walikuwa na ugomvi wa muda mrefu, baada ya mtuhumiwa kuoa mke wa pili.

Kwa mujibu wa ndugu huyo, marehemu enzi za uhai wake alikuwa akidai apatiwe nyumba hali na baada ya kuona hatimiziwi matakwa yake, aliamua kufungua kesi mahakamani.

Hata hivyo, alisema mtuhumiwa alishakubali kutoa nyumba na kwamba kesi hiyo ambayo ilikuwa itolewe hukumu Januari 27, mwaka huu, alikuwa akabidhiwe hati ya nyumba kama aliyodai.

Licha ya kwamba suala hilo liko mahakamani, mkewe alikuwa akijitapa mtaani kuwa atahakikisha anamkomesha mumewe na kwamba akishapatiwa nyumba hiyo ataiuza.

“Huyu mkewe alishaambiwa anapatiwa nyumba lakini kila kukicha ni visa anaanzisha. Mara aende kazini kwa mumewe kumsemea maneno ya uongo. Pia kila mwezi mumewe alikuwa anakatwa Sh. 200,000 na kodi ya nyumba alikuwa anapokea lakini mumewe alipokuwa anarudi kutoka kazini, alikuwa hakuti chakula.

Naye Mjumbe wa Shina Na. 17 la mtaa huo, Jackson Mathayo, alisema kuwa tukio hilo limewaumiza na kwamba tatizo lililojitokeza ni kukosa taarifa kwa wakati.

Alisema alifika eneo la tukio na kushuhudia mwili huo ukiwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili huku maeneo ya kichwani yakiwa yamepasuliwa kwa panga.

Mathayo alisema mtuhumiwa baada ya kufika kituo cha polisi alirudishwa na kutakiwa kupeleka barua ya mjumbe inayothibitisha kuwa kafanya tukio hilo.

“Nimesikia kuwa alisema nimeua. Wale askari hawakuamini kwa kile alichokizungumza maana alikuwa anazungumza kama ni jambo jepesi na hakuwa na hofu ndiyo maana akaambiwa apeleke barua ya mjumbe,” alisema.

Baada ya kuambiwa hivyo, alisema alikwenda kwa balozi na kumweleza kuwa: “Mimi nimeshaua. Alipoulizwa tatizo ni nini alisema tayari ameua,” alisisitiza.

Mathayo alisema balozi hakuamini ikabidi amjulishe na mjumbe mwingine kwa ajili ya kwenda eneo la tukio kushuhudia suala hilo.

Alisema baada ya kushuhudia tukio hilo alipatiwa barua na kuipeleka kituo cha polisi ambapo wamemshikilia hadi sasa.

Naye Amina Sulemain ambaye ni jirani wa mtuhumiwa, mtuhumiwa huwa ana hasira za haraka, hivyo huenda mkewe alimpa majibu mabaya hali iliyosababishia kutokea kwa mauaji.

Mwili wa marehemu uliagwa jana saa sita mchana kwa ajili ya mazishi ambayo yatafanyika mkoani Mara. Familia ya mtuhumiwa haikusafiri na mwili wa marehemu kwa kuhofia huenda watalipiziwa kisasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya, alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alikiri kutokea bila kulitolea ufafanuzi.

CHANZO: NIPASHE

Tiffah Dangote Anawasumbua Wengi-Wolper

0
0

Hapa na Pale: Staa wa Bongo movies, Jacqueline Woper ambaye siku za hivi karibuni ameonekana kuwa karibu na falimila ya staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz amefunguka hayo kupiytia ukurasa wke myandaone mara baada ya kubandika picha ya mtoto Tiffah.

Tiffah Dangote..mtoto anawasumbua wengi huyu…!Naona mpk kuna wengine wanahisi wanalingana na Tiffah maana sio kwa mineno inayowatoka…Mchambo wa leo naomba unifikie mpk nilipo nilikuwa naomba mchambo upande ndege leo unifikie…Usiponifikia nilikua naomba niukatie ticket…Vyote vikishindika muende chooni mkachambe wenyewe vizuriiii…


Ujumbe umefika.

Baada ya Bond Kutaka Kujiua Kisa Penzi la Wastara... Wastara Aibuka na Kumpa Masharti Mazito

0
0

Staa wa filamu Bongo, Wastara Juma amempa wakati mgumu aliyekuwa mwandani wake ambaye pia ni meneja wake, Bond Bin Suleiman kuwa kama bado anataka waendelee kufanya kazi pamoja asiendekeze wivu baada ya yeye kuolewa.

Wastara aliyeolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Khamis alisema kuwa ni ukweli usiopinga kwamba yeye na Bond walikuwa wapenzi, kwa kuwa sasa ameolewa na mkataba wake na Bond bado haujaisha imempasa ampe masharti.

“Ninachotaka tuendelee kufanya kazi na azingatie kuniheshimu na kusahau kabisa kama tuliwahi kuwa wapenzi, pia muamuzi wa mwisho ni yeye kama ataona hawezi basi maana nimeshaandaa mtu mwingine,” alisema Wastara.

Chanzo: GPL

Mapya Yaibuka Baada ya Shilole Kufuta Tattoo ya Nuhu..Kumbe Picha za Mademu Wengine wa Nuhu Ndio Chanzo

0
0

Shilole ameifuta ‘tattoo’ ya aliyekuwa mpenzi wake Nuh Mziwanda baada ya kuachana,lakini Nuh hajaifuta na hana mpango kwa sasa wa kuzifuta ‘tattoo’ hizo.

‘’Kiukweli nimesikitika sana hata kama tumeachana mimi mbona sijafuta tattoo zake na sina mpango wa kuzifuta kwa sasa,’’Alisema Nuh.

Hata hivyo Shilole alipoulizwa kuhusiana na alichokisema Nuh alisema kuwa mbona Nuh aliwahi kuwapost mademu zake wapya mara tu baada ya kuachana.

‘’Mimi nimewahi kufuta tattoo kwa sababu yeye alianza kuwapost mademu zake wapya Instagram baada ya kuachana,’’Alisema Shilole.

Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images