Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Idriss Sultan Amtusi Diamond, Ajitapa Mtaani Kuwa yeye ni Kidume Aliyeweza Kumpa Mimba Wema

$
0
0

 Hii dharau! Siku chache baada ya staa wa Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ kudaiwa kushika ujauzito ambao mhusika bado ni fumbo, balaa limezuka kufuatia Mshindi wa Big Brother Africa Hotshots 2015, Idris Sultan kudaiwa kumtusi zilipendwa wa mrembo huyo, Mbongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’, Risasi Jumamosi linakujuza.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, Idris amekuwa akijitapa mitaani kuwa yeye ndiye kidume aliyeweza kumpa mimba Wema na kwamba ni daktari bingwa wa magonjwa sugu, yakiwemo ya uzazi kwani kwake kunapatikana tiba mbadala.

Majigambo hayo yanadaiwa kuharibu urafiki uliokuwepo baina ya wawili hao, kwani Diamond anachukulia kama ni kumtusi kwa vile aliwahi kujihusisha kimapenzi na Wema kwa muda mrefu bila kupata ujauzito.

KAMA KUNA URAFIKI NI KIINI MACHO
“Kitu ambacho watu hawaelewi ni kwamba hivi sasa urafiki wa Diamond na Idris ni kiini macho tu, kwani majivuno ya Idris ya kutoka na Wema yameleta uhasama mkubwa, hasa baada ya kujigamba kuwa ameweza kumpa ujauzito.

“Inadaiwa juzikati Idris akiwa na Wema sehemu, rafiki zake wakawa wanampongeza kwa taarifa zilizosambaa kuwa yeye ndiyo amemdunga mimba mrembo huyo ambapo kijana huyo alisikika akisema hakuna mwanamke asiyezaa duniani, isipokuwa kinachotokea ni kuto-match (kuendana) kwa damu za wawili. Eti kwa kitendo hicho yeye ndiye kidume cha mbegu,” kilisema chanzo hicho.

OMMY DIMPOZ NAYE ATAJWA
Ommy Dimpoz ambaye ni rafiki wa karibu wa Diamond, naye anatajwa kuwemo katika watu wanaompiga vijembe kwa kufurahia kitendo cha Idris kumjaza mimba Wema kwa kile kinachosemwa kuwa wawili hao wana ka-bifu ka chini kwa chini, kisa kikiwa siri yao.

“Ommy Dimpoz naye ni miongoni mwa watu wanaosapoti kwa asilimia kubwa Idris kumpachika mimba Wema na kwamba anaonesha wazi kuunga mkono kila kitu kinachofanywa na kijana huyo katika kumuumiza Diamond kupitia mimba hiyo.”

DIAMOND ANASA UBUYU
Habari zinasema kuwa maneno yaliyokuwa yakitembea katika kundi la Idris yalimfikia staa huyo wa muziki wa kizazi kipya nchini, ambaye alisikitishwa na kitendo cha kuonekana kama hakuwa na uwezo wa kumpa mimba Wema, akitamka kuwa wanaomsema hivyo hawajui jinsi yeye na Wema walivyokuwa wakiishi kimapenzi.

IDRIS HUYU HAPA, MSIKIE
Baada ya kumegewa ubuyu huo, juzi paparazi wetu alimtafuta mshindi huyo wa BBA aliyejishindia dola 300,000 (zaidi ya shilingi milioni 500) na kubahatika kukutana naye ana kwa ana katika eneo moja, nje kidogo ya jiji.

Alipoulizwa kuhusu ukweli wa madai ya kumtusi rafiki yake huyo, huku akichekacheka, Idris alishindwa kufunguka moja kwa moja, badala yake akasema hategemei kuja kuwa na tatizo na Diamond kwa sababu ya ujauzito wa Wema, hasa kwa kuwa tayari ana mtoto (Tiffah) aliyempata kwa mpenzi wake, Zarinah Hassan ‘Zari’.

“Diamond hawezi kuwa na mawazo hayo kwani haoni tatizo lolote kwangu kuwa karibu na Wema, hata nikizaa naye, kwa sababu uhusiano wao ulishamalizika.

“Hata hivyo hayo yatabaki kama madai. Mimi kuitwa kidume itatokana na namna waitaji watakavyokuwa wamenichukulia. Ila kiukweli sidhani kama kuna mtu anaweza kuja kuninunia kisa Wema maana suala la uhusiano au kuwa karibu na mtu inategemea tu na watu wenyewe jinsi wanavyoweza kuchukuliana na kuwaziana.”

KUANIKA KUHUSU MIMBA YA WEMA
“Suala la mimba ya Wema nitakuja kuliweka vizuri baada ya mwezi mmoja. Kwa sasa niache kwanza maana nina mambo mengi ya kufanyia kazi, sitaki kabisa kuanza kuvuruga mudi za watu na ndiyo maana naona hakuna haja kwa muda huu kuongelea ishu hiyo ila yasemwayo yanaweza kuwa na maana kama yameelezewa vizuri,”

DIAMOND NAYE HUYU HAPA
Gazeti hili lilifanikiwa pia kumnasa mkali wa kibao cha Utanipenda? Diamond ambaye baada ya kuelezwa kilichopo alisema kwa sasa hana muda wa kusikiliza maneno ya watu wala kujibu kila anachosikia, zaidi anahangaikia maisha yake ili kuweza kufikia ndoto alizojipangia kwa vile maneno yapo kila siku na hayaepukiki.

“Dah! Mimi sioni kama kuna kitu cha ajabu wala kuzungumzia hapo, zaidi naweza kusema mimi sina muda tena wa kuanza kuzungumzia mtu ila kila mmoja atabeba mzigo wake.

“Kwa sasa nawaza kukuza muziki wangu kwa namna moja au nyingine, siwezi kuendelea kuwawazia watu wakati mwenyewe nina mambo mengi ya kujiwazia,” alisema Diamond.

Source:Global Publishers


Kajala Nae Adaiwa Kunasa Ujauzito wa Kigogo

$
0
0

Good news? Huenda mambo yanaweza yakawa yamejipa kwa mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’ kwani kuna taarifa zinadai kuwa mwigizaji huyo amenasa mimba ya kigogo serikalini.

Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo ambaye ana mtoto mmoja aliyezaa na prodyuza mkongwe Bongo, Paul Matthysse ‘P Funk’ (Paula), kimepenyeza ubuyu huo kuwa Kajala ana mimba ya zaidi ya miezi mitano na amegusiwa kuwa ni ya kigogo serikalini ambaye hataki kumtaja jina.

“Hivi hamna habari? Kajala mbona mjamzito. Tena yeye alianza kunasa kabla hata ya Wema, nashangaa mnakomalia kuripoti mimba ya Wema tu, Kay mmemuacha na kigogo wake,” kilimwaga ubuyu chanzo hicho.

Baada ya kupewa ubuyu huo, juzi Alhamisi, mwanahabari wetu wakati anaanza kuichimba habari hiyo, alitembelea kwenye ukurasa wa Instangram wa Kajala na kukutana na ujumbe ulionesha dhahiri kuwa mwigizaji huyo anajiandaa kuitwa mama kwa mara nyingine.

“Hey IG…do me a favor…help me to choose a name of my new baby coz Pau wants a name with P in the beginning and mimi sitaki..” aliandika Kajala akiwataka wafuasi wake katika mtandao huo wamsaidie kuchagua jina la mtoto wake ajaye kwani Pau (Paula) anataka jina linaloanza na herufi P lakini yeye hataki.

Alipopigiwa simu na mwanahabari wetu kuhusiana na ujumbe huo sanjari na taarifa za kuwa ni mjamzito wakati gazeti hili linakwenda mitamboni, Kajala alikata simu. (Huenda alikuwa sehemu ambayo hakuweza kuzungumza, bila shaka ataona habari hii na kutoa ufafanuzi zaidi kwani ni jambo la heri.

Source: Global Publishers

Bandarini Hapakaliki..Wakurugenzi Watatu Wapigwa Chini na Kuhamishiwa Wizarani, Vigogo TCAA Wasimamishwa Kwa Ufisadi

$
0
0

SERIKALI imeendelea kuisafisha Bandari kwa kuwaondoa watendaji wa ngazi za juu na kuwahamishia wizarani ili kuongeza ufanisi katika utendaji, sambamba na kuongeza ukusanyaji wa mapato.

Wakati hayo yakitokea Bandari, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) amesimamishwa kazi huku Mhasibu Mkuu na Meneja Manunuzi wa taasisi hiyo wakihamishwakwa tuhuma za kushindwa kusimamia ukusanyaji wa mapato katika taasisi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuhusu mabadiliko Bandarini, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (pichani) alisema serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha inasimamia mapato ya serikali na taasisi zinafanya kazi kwa ufanisi mkubwa.

Aliwataja watumishi walioondolewa Bandari kuwa ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Peter Gawile, Kaimu Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Killian Challe na Kaimu Mkurugenzi wa Manunuzi, Mashaka Kishanda.

Alisema watendaji hao wamerudishwa wizarani na itafanyika tathmini ili waangaliwe watapangiwa nafasi gani kwa kuwa inawezekana katika Bandari uwezo wao na ufanisi wao ulikuwa mdogo ila inawezekana maeneo mengine wakafanya vizuri zaidi.

Aidha alisema imewateua watendaji wengine kushika nafasi hizo akiwemo Anthony Mbilinyi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambaye anakwenda Bandari kushika nafasi ya Gawile, Benito Kalinga ambaye alikuwa Ofisa Manunuzi Mkuu wa TCRA anayeenda Bandari kushika nafasi ya Kishanda na Abdulrahaman Bamba ambae alikuwa TEHAMA Uchukuzi anayeenda kushika nafasi ya Challe.

“Tatizo kubwa lililokuwa linaonekana pale Bandari ni mfumo wa IT hivyo tumeamua hao waondoke… Tunaamini tukiwapa ushirikiano watendaji hawa wanaoingia watafanya vizuri zaidi na kufanikisha azma ya serikali ya kuongeza ukusanyaji wa mapato,” alisema.

Katika hatua nyingine, Profesa Mbarawa amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Charles Chacha na kutaka kuhamishwa mara moja kwa Mhasibu Mkuu Alhaji Said Mteule na Meneja manunuzi wa taasisi hiyo, Said Kaswela kwa kushindwa kusimamia ukusanyaji wa mapato katika taasisi hiyo.

Serikali pia imeona ifanye uchunguzi kuhusu ununuzi wa mtambo wa kufuatilia vyombo angani unaojulikana kama Automatic Data Surveillance-Broadcast (ADS-B) na mtambo wa kukusanya taarifa za usafiri wa anga (AMHS), ambayo imegharimu kiasi cha Euro milioni 1.5.

Mbarawa alitoa agizo hilo jana akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango pamoja na watendaji wa TCAA katika ziara aliyoizungumzia kuwa ni ya kuangalia uendeshaji na ukusanyaji wa mapato unavyofanyika katika taasisi hiyo.

Waziri huyo alisema kuna mambo yamejitokeza hivyo serikali imeona lazima ifanye uchunguzi kwenye ununuzi wa baadhi ya mitambo na pia imebaini kuna upotevu mkubwa wa ukusanyaji wa mapato ambao umechangiwa na uongozi wa taasisi kwa kutojipanga vizuri.

“Wizara imeamua Chacha kuanzia leo (jana), hataendelea na nafasi hiyo tena badala yake atatafutwa mwingine. Mhasibu Mkuu wa taasisi hii atahamishwa na ofisa wa manunuzi wa taasisi hii. Iko haja ya kumpeleka sehemu nyingine ili tupate mtu safi na makini,” alisema Waziri huyo.

Mitambo hiyo ilitakiwa kuanza kufanya kazi tangu Novemba mwaka jana, lakini mpaka sasa haijaanza kufanya kazi. 

“Bora ubaki na watu wawili kwenye kazi kuliko 10 ambao sio waadilifu,” alisema Mbarawa.

Kwa upande wake Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mpango alisema kikubwa wanachopigania ni kuhakikisha serikali inakusanya mapato yote ya kodi na yasiyo ya kodi na kuongeza kuwa taasisi hiyo ina vyanzo ambavyo vingeweza kuingizia serikali fedha nyingi.

“Mkaguzi Mkuu alikuja na kufanya utafiti lakini taarifa aliyoitoa haikufanyiwa kazi. Pia katika kudodosa inajulikana TCAA ina akaunti saba ambazo zinatia shaka,”alisema Waziri Mpango na kuagiza akaunti hizo kutokuguswa mpaka uchunguzi utakapofanyika.

“Nimeagiza ili fedha za taasisi hii zibaki salama isitoke hata senti, pia ndani ya wiki mbili ufanyike ukaguzi kubaini upotevu wote wa fedha za umma uliofanyika,”alisema na kuitaka Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA), ifanye uchunguzi wa mchakato mzima wa ununuzi wa mitambo hiyo miwili ya ADSB na AMHS, pamoja na kusisitiza kuwa watumishi waliosimamishwa watahamishwa mara moja.

Breaking News:UKAWA Washinda kiti ca Umeya Kinondoni, 16 January 2016

$
0
0

Vyama vinavyounda UKAWA vimeibuka na ushindi katika uchaguzi wa Umeya wa Manispaa ya Kinondoni baada ya kupata kura 38 dhidi ya CCM waliopata kura 20.

Meya mpya ni Boniface Jacob. Manispaa ya ilala zoezi bado linaendelea


Mume Wangu Ananinyima Unyumba

$
0
0


Mimi ni mwanamke mwenye watoto wawili na nipo kwenye ndoa kwa miaka nane sasa.Tumekuwa tukiishi maisha ya ugomvi kwa muda na mume wangu, ila nikaona ni vyema nijishushe na nisihoji chochote.Mimi ndiye ninahangaika na familia na mambo yote hakai kujadili jambo lolote la maana na mimi.

Binafsi niliona nijishushe na nisihoji chochote ila tatizo limekua ni kwenye unyumba. Kwa kweli navumilia sana tunalala pamoja najitahidi kujiweka safi, kubadili mazingira ya chumba, manukato na hata mavazi lakini wapi!

Naweza nikamfanyia vikorombwezo vyote ila atageukia upande wa pili na kukoroma nimemsihi sana yeye anasema anawaza maisha hawezi kuendekeza ngono.Tunaweza kukaa mpaka miezi mitatu hatujakutana,hili swala linanikondesha jamani.

Naombeni njia ya kujinasua katika hili janga.

 

Uchaguzi wa Meya Ilala: CCM wapata kura 0, UKAWA 31

$
0
0

Baada ya mvutano mkali unaoendelea wabunge wa CCM wa ilala wametoka nje kususia uchaguzi.

Matokeo ya Umeya Ilala,

1. Charless Kuyeko (UKAWA) kura 31,
2. Heri Kessy (CCM) kura 0.

Chanzo ITV

TCRA Yavifungia Vituo 27 Vya Radio Na Tv Kwa Kukwepa Kodi.......Miongoni Mwa Vituo Vilivyofungiwa ni Star Tv, Radio Free Africa na Kiss Fm

$
0
0


Mamlaka ya Mawasiliano TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya TV kikiwemo kituo cha Star TVRadio free AfrikaKiss Fm na Uhuru FM kwa kushindwa kulipa kodi ya lesseni kwa wakati ..

Akitangaza uamuzi huo, mkurugenzi wa habari na mawasiliano wa TCRA Innocent Mungy, amesema kuwa mitambo ya vituo hivyo itazimwa ifikapo kesho saa 6 usiku, na itawashwa baada ya vituo hivyo kulipa madeni yanayowakabili.

Mungy amesema mamlaka hiyo haiwezi kusema ni kiasi gani cha pesa ambacho vituo hivyo vinadaiwa kwa madai kuwa kanuni na taratibu haziwaruhusu kutaja kiasi hicho kwa kuwa ni siri kati ya TCRA na mteja.

Aidha Mungy amesema kuwa TCRA imewataka wadau wote wa mawasiliano nchini kutii sheria bila shuruti na kufuata taratibu, huku akisisitiza kuwa zoezi hilo la kuwasaka wanaokwepa kodi ni endelevu.

==> Vituo vingine vilivyofungiwa ni;
Sibuka FMBreez FMCountry FMEbony FMHot FMImpact FMIringa Municipal TVKiss FMKitulo FMKifimbo FMMbeya City Municipal TVRadio 5Radio Free Afrika (RFA)Musa Television NetworkPride FM radioRadio HurumaRadio UhuruStar TVRock FM RadioStandard FM radioSumbawanga Municipal TVTanga City TVTop Radio FM limitedUlanga FM 

Nape Nnauye Alifungia Milele Gazeti la Mawio

$
0
0

Serikali kupitia Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nauye, imelifungia kwa muda wote gazeti la kila wiki la MAWIO linalochapishwa na kampuni ya Victoria Media Services Ltd.

Katika tangazo lake lililotolewa kupitia gazeti la Serikali notisi namba 55 ya Januari 15, 2016 Serikali imebainisha kuwa imechukua uamuzi huo wa kulifungia gazeti la Mawio kwa muda wote kwa mujibu wa mamlaka iliyonayo kupitia sheria ya magazeti ya mwaka 1976 sura ya 229 kifungu cha 25(1).

“Mawio linatakiwa kusimamisha uchapishaji wake kwa kipindi chote ikiwemo pia katika vyombo vya mawasiliano vya kielektroniki kuanzia Januari 15, 2016”, ilisema sehemu ya tangazo hilo ambalo limetolewa katika gazeti la serikali, likisainiwa na waziri Nape Nauye.

Tangazo hilo halikuweza kufafanua zaidi ni makosa gani hasa yaliyosababisha gazeti kufungwa na kwanini adhabu iliyotolewa ni kubwa sana ukizingatia kuwa Mawio halikuwahi kufungiwa wala kuonywa kwa kosa lolote katika siku za wa awali.

Serikali ilianza kulikabili rasmi gazeti la Mawio 31 Desemba, 2015 kwa barua iliyoandikwa na msajili wa magazeti ikimtaka mhariri wa gazeti hilo kutoa maelezo ya kwanini gazeti hilo lisifungiwe kufuatia makala zake mbili zenye vichwa vya habari “Hosea kortini” na “Seif Rais Zanzibar” ambazo zilidaiwa kuzua taharuki.

“Nakujulisha kwamba ofisi ya msajili wa magazeti haijaridhika na utetezi wako kwa kuwa hujatoa uthibitisho usio na shaka juu ya madai ya makala ulizochapisha,”ilitamka sehemu ya barua iliyosainiwa na Raphael Hokororo, kwa niaba ya msajili.

Gazeti la Mawio ambalo huandika habari za kiuchunguzi limefuata mkondo uleule ambao gazeti la MwanaHALISI liliufuata 30 Julai 2012 pale lilipofungiwa kwa muda usiojulikana kwa madai ya kuchapisha taarifa za uchochezi.

MwanaHALISI lilikaa kifungoni kwa zaidi ya miaka mitatu kabla ya kurejeshwa kwa amri ya Mahakama Kuu mwezi Agosti, 2015 kufuatia Mkurugenzi wa kampuni ya Hali Halisi Publishers, Saed Kubeneakufungua kesi, akipinga kufungiwa kwa gazeti hilo.


Alikiba Azungumzia Tuhuma Kuhusu Diamond Kuzuia Nyimbo MTV BASE

$
0
0

Baada taarifa kusambaa kwe ye mitandao ya kijamii ikisemekana Diamond Platnumz kuwa ndio anayehakiki kazi za wanamuziki wa Bongo ili ziweze kuchezwa MTV Base, sasa mwanamuziki Alikiba amefunguka hivi.

“Nitawaambia ukweli ambao unaohusu that it, kama ni kweli watakuwa wanakosea na sidhani kama ni sawa coz watakuwa hawapo fair.”Alikiba

“Hajabeba talent ya kila mtu, kila mtu ana talent yake, ana haki ya kuonyesha kazi yake coz kila mtu anafanya business ya muziki sasa hivi sio mtu anafanya masihara, na unapomuona mtu anafanya video yake anagharamikia so haipendezi n

CCM Chali Dar es Salaam, UKAWA Washinda Kiti ca Umeya Kinondoni na Ilala

$
0
0


Hatimaye baada ya danadana za muda mrefu, uchaguzi wa kuwachagua Mameya wa Manispaa za Kinondoni na Ilala, umefanyika na Umoja wa Vyama vinavyunda Katiba ya Wananchi (Ukawa) wamefanikiwa kuongoza Manispaa hizo.

Chaguzi hizo zilizhairishwa mara mbili kutokana na mvutano uliotokewa katika chaguzi za nyuma, ikiwa ni pamoja na kusimamishwa kwa amri za mahakama.

Kwa upande wa Manispaa ya Kinondoni,Diwani wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema, Boniface Jacob amefanikiwa kuwa Meya wa manispaa hiyo baada ya kushinda kwa kura 38 dhidi ya mpinzani wake, Benjamin Sitta wa CCM aliyepatakura 20. Naibu Meya ni Diwani wa Tandale kwa tiketi ya CUF, Jumanne Ameir Mbunju.

Uchaguzi wa Manispaa ya Ilala  leo pia uliingia katika mgogoro kati ya madiwani wa CCM na wale wa Ukawa, hali iliyosababisha CCM kususia uchaguzi huo na kuwaacha Ukawa kupiga kura peke yao na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kumtangaza Charles Kuyeko (Chadema)kuwa mshindi wa kiti cha Meya wa Ilala kwa ushindi wa  kura 31, wakati Naibu Meya ni Omary Kumbilyamoto (CUF) ambaye amepata kura 31.

Jumla ya madiwani waliotakiwa kupiga kura katika uchaguzi huo ni 54, hivyo madiwani 31 wa Ukawa waliobaki ndani walitimiza akidi ya uchaguzi huo kuendelea.

Lowassa: Utajiri Wangu Usitumike kwa Lengo la Kuchafuana Katika Siasa, Ndugu zangu Aliyepata Amepata

$
0
0

Mkubwa wa kazi ambaye amewahi kushika nafasi kubwa za uongozi katika taifa hili na mwenye kasi ya ajabu katika medani za siasa, uchumi katika chama chake, amekuwa akiwaonya wapinzani wake kutotumia kete ya mali zake kama njia ya kumchafua ki siasa.

Amesema hapendezwi na hilo, na jambo hilo halina tija kwa siasa zetu za Tanzania, kuna mijadala mingi ya ki taifa ya kujadili kwa maendeleo yetu na siyo mali zake kwani anazo mali za kawaida kuliko inavyozushwa.

Kakazia kwamba wapinzani wake wasijikite katika mali zake kwani "ALIYEPATA AMEPATA".

Haya wadau hizi ndiyo siasa za bongo watu wamewekeza kwenye kuchafuana tu. Chama cha CCM kazi ipo.

Toa Maoni yako....

Udaku Special Blog

Mtoto wa Diamond (Tiffah), Apata Dili Jipya la Kusoma Bure

$
0
0

Nyota njema uonekana asubuhi,mtoto wa rais mwenye Ikulu yake Madale pembeni kidogo ya jiji la Dar es salaam Tiffah au mtoto Tee amepata dili la kusoma bure kutoka shule ya ushuani wanakokula burger saa nne na kutumia kengere za umeme kwenda mapumziko ,Tanganyika international school (TIS) kwa kipindi chote na huku kumfanya awe balozi wa shule hiyo lkn ubalozi huo kuwa siri mpaka mtoto atakapoanza shule.

Mtoto Tee anakuwa moja ya watoto wachache wasiotokana na familia za kifisadi kusoma shule yenye swimming pool lenye kiwango cha olympic.

Lkn habari zinadai wakina dada wanaopenda attention mjini Wema na Jokate baada ya kusikia habari hizi walijaribu kuzunguka shule kadhaa hapa town kuona kama na wao wanaweza kupata dili kama hilo kwa watoto wa king Kiba ili kwenda sambamba huku baadhi ya shule zikidai ubalozi wa Tembo unamtosha kabisa King huyo wa coke studio.

Inadaiwa pia Diamond ataenda Uganda next month kushoot video ya wimbo mpya ambao Zari ameimba kiitikio na dada yake Diamond amefanya intro

Chanzo: Msaga Sumu/Jamii forums

Toa Maoni yako

Msaniii AT Atoa ya Moyoni Kuhusu Mwanamuziki Ali Kiba..Awashangaa Watu Wanaosema Anaringa

$
0
0

Mfalme wa miondoko ya mduara nchini AT, ambaye amewahi kutamba na nyimbo yake ya Bao la Kete na nyingine nyingi zilizo wakuna wadau wa muziki na kuamua kuongeza ushabiki mkubwa kwenye aina ya mziki huAT ameuamua kusema ukweli ambao alikuwa ameuhifadhi moyoni kwa muda mrefu juu ya mahusiano yake na msanii nyota kwa sasa nchini Tanzania, mwenye mashabiki wengi kutokana na tungo zake kuwagusa wengi ajulikanaye kama Alikiba hitmaker wa Nagharamia aliyofanya na Chrstian Bela.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram AT amemzungumzia Alikiba kama msanii mwenye kufanya jitihada katika kazi zake na mwenye kusaidia watu tofauti wa watu wanavyomdhania kuwa anaringa, jambo ambalo AT analipinga kwa asilimia mia moja kwa sababu kama angekuwa anaringa asingeweza kumsaidia yeye, kipindi hicho hana kitu.

Nuh Mziwanda: Nilishaficha Mambo Mengi Sana Mabaya ya Shilole kwa Maslahi ya Penzi Letu

$
0
0

Nuh Mziwanda amedai kuwa aliyofanyiwa na Shilole ni mengi na mazito ambayo ilibidi ayafiche kwa maslahi ya penzi lao na heshima kwake

Akiongea kwenye kipindi cha D’Weekend Chat Show cha Clouds TV Ijumaa hii mbele ya Shilole aliyekuwa amejikunyata pembeni kwa kukasirishwa na uwepo wa ex wake studioni hapo bila kutaarifiwa mwanzoni, Nuh alisema Shilole hakuwa mwanamke wa kutawaliwa.

“Yeye anajua mambo gani alikuwa anafanya kwangu mambo ambayo yalikuwa hayastahili anifanyie. Alikuwa anafanya kwa kunichukulia poa kwamba nitafanya nini lakini at end of the day kila kitu kina mwanzo na mwisho,” alisema.

Nuh alisema ni ngumu tena kurudisha imani kwa mpenzi wako huyo licha ya kukiri kuwa bado hajaweza kuwa tayari kuwa na mwanamke mwingine kwa sasa.

Kwa Hili la Uchaguzi wa Mameya Dar es Salaam, CCM Mmetutia Aibu!

$
0
0

Kwa hili lazima tuseme, kwamba kama mwanachama halikunifurahisha hata chembe.
Ni jambo lililo wazi kuwa baada ya uchaguzi mkuu, CCM tumepigwa bao hasa hapa jijini Dsm.

Halmashauri nyingi waliochaguliwa ni wanachama wa vyama vya upinzani kwa wingi zaidi kuliko wa chama tawala.
Hivyo ndivyo ilivyokuwa kiuhalisia.

Dhambi kubwa na ya kutia aibu, ni kuleta mamluki toka Zanzibar, watuamulie mambo ambayo kwanza hawayajui ya DSM, na pili si wawakilishi wa wananchi wa DSM.
Katika kata yangu, diwani alichaguliwa wa CHADEMA, mimi nilimpa kura yangu(wa CCM) alishindwa vibaya.
Kushindwa kwa huyo mwana CCM mwenzangu kunatokana na kutoshughulikia kero , hasa za barabara huku Mbezi.

Sasa leo huyu mwana CHADEMA TUTAMPIMA KWA KIGEZO HICHO HICHO.

Sasa leo tunaletewa mamluki wa kutusaidia kuamua mambo yetu?
Mbaya zaidi ni kususia uchaguzi.
Hii ni AIBU KUBWA!

Toa maoni yako


Sakata la Bwana Samatta Kucheza Ulaya..Bosi wa TP Mazembe Akubali Yaishe

$
0
0

Mshambuliaji wa TP Mazembe na Taifa Stars, Mbwana Samatta amepaa usiku wa kumkia leo kuelekea Ubelgiji kukamilisha usajili wake wa kujiunga na klabu ya KRC Genk inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo.

Kuondoka kwa Samatta ni kama kunamaliza sintofahamu iliyogubika hatima ya wapi atakapoelekea baada ya mkataba wake na Mazembe kumalizika, huku mmiliki wa timu hiyo akiweka ngumu kumruhusu kujiunga na Genk akitaka aende     Ufaransa kwenye klabu ya Nantes.

Safari ya Samatta kuelekea Ubelgiji, imethibitishwa na familia yake ambayo imelazimika kuahirisha sherehe iliyoandaliwa kwa ajili ya kumpongeza.

Baba mzazi wa mshambuliaji huyo, Ally Samatta alisema sherehe hiyo ambayo ilikuwa ifanyike leo, haitokuwapo kutokana na safari ya Mbwana kwenda Ubelgiji.

“Sherehe haitafanyika kesho (leo), kwani Samatta anaondoka usiku wa leo (jana) kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kujiunga na Genk ya Ubelgiji na sisi kama familia tumepanga kuifanya siku nyingine,” alisema      

Ukawa, Tayari Jiji la Dar Lipo Chini yetu Pambanane na Changamoto Zilizopo

$
0
0

Jiji la Dar es Salaam kuwa sasa lipo chini ya Ukawa ni muda sasa wa Ukawa kupambana na changamoto nyingi za Jiji hilo baada ya kupata mameya na manaibu meya Kinondoni na Ilala.
Tatizo kubwa la foleni kwenye jiji la Dar esa Salaam pamoja uchafu mwingi unaozalishwa ni muda wa Ukawa kutatua ili tatizo.
Pia changamoto ingine ni mfumo wa leseni za biashara maeneo ya Ilala na Kinondoni imekuwa kero kubwa kwa wafanyabiashara ni wakati sasa wa Ukawa kupambana na ili suala la leseni.
Changamoto ingine hii mifumo ya ulipaji uhuru wa masoko kama Tandale, Kariakoo, Buguruni na maeneo mengine ni wakati sasa wa Ukawa kulisimamia ili suala hili wananchi wafanye biashara zao bila usumbufu.
Suala la parking kwenye Jiji la Dar es Salaam ni kero kubwa ni wakati sasa wa Ukawa kulitatua wananchi pamoja na malipo ya parking. 
Usumbufu mkubwa wa ukamataji ovyo wa boda boda na bajaji hii ni miradi ya watu ni wakati sasa wa Ukawa kulisimamia hili.
Toa Maoni yako

Mke Wangu wa Ndoa Ame-Hack Simu Yangu

$
0
0

Katika hali isiyo ya kawaida nimegundua kuwa mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu na kuweza ku-access mawasiliano yangu yote hasa ya sms tokea mwezi wa 10 mwaka jana 2015 na kuzihifadhi kwenye simu yake. 

Sina uhakika kama aliweza kupata mawasiliano mengine tofauti na sms. 

Ninasema ku-hack kwa sababu tunaishi mikoa tofauti na hivyo hakuwa na namna yoyote ya ku-access simu yangu physically toka wakati huo, pia simu yangu ambayo ni smart phone ina security (password) in case angetumia mtu aliye karibu yangu. 

Nimegundua hii hacking baada ya kuwa na hali ya kutoelewana kati yetu kwa muda sasa ambapo pamoja na mambo mengine niligundua kuna taarifa zangu za siri anazozifahamu ndipo nilipoanza uchunguzi na kugundua kuwa ana hizo sms. 

Miongoni mwa sms anazoshikia bango ni zile zinazohusiana na miamala ya Mpesa ambapo nimewatumia pesa ndg, jamaa na marafiki ambao sikuona umuhimu wa kumtaaifu hivyo akazijengea hoja mbali mbali ikiwemo ya uhusiano wa kimapenzi wakati si kweli!

Nimejaribu kumbana aseme amewezaje ku-access "private communications" zangu ila amegoma kabisa kuweka wazi.

Cha kushangaza zaidi ni kuwa hana utaalam wowote wa masuala ya mawasiliano!

Kwa kuzingatia usumbufu uliojitokeza kwa kuingilia mawasiliano yangu ya siri hasa kupitia mis-perception ya taarifa alizokutana nazo, nimepata wazo la kumshtaki kwa mujibu wa ile SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015 ila nikaona kabla sijafanya hivyo nililete suala hili hapa ili nipate michango yenu ya mawazo hasa juu ya nini cha kufanya.

Suala hili limenichanganya sana hasa ukizingatia kuwa tumekuwa kwenye ndoa takribani miaka 8 sasa na tuna watoto 2. 

Naombeni michango yenu ya mawazo.

Ahsante!

By Mpigania Uhuru/JF

Breaking News: Habari Mpya Kuhusu Bifu la Yanga na Mchezaji Haruna Niyonzima..

$
0
0

Baada ya uongozi wa klabu ya Dar Es Salaam Young African kutangaza kuwa imevunja mkataba na kiungo wake wa kimataifa wa Rwanda Haruna Niyonzima, January 17 kiungo huyo akiwa katika makao makuu ya klabu hiyo, pamoja na afisa habari wa Yanga Jerry Muro, alitangaza kuomba radhi wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yangambele ya waandishi wa habari kutokana na kosa alilolifanya.

Licha ya kuwa afisa habari wa Yanga Jerry Muro kutotangaza rasmi kuwa klabu imemsamehe, na kusema kuwa isubiriwe taarifa rasmi, dalili zinaonesha kuwa uongozi wa Yanga na Niyonzima umeyamaliza.

Yanga walitoa barua kwa umma ya kuvunja mkataba na Niyonzima December 28 2015, barua ambayo inaeleza makosa ya Niyonzimaambayo yamepelekea haya yote kutokea. Unaweza pitia barua ya Yanga iliyotolewa December 28 2015 na mkuu wa idara ya habari wa klabu hiyo.

Tamko la Star Tv, RFA Na Kiss Fm Baada Ya Kufungiwa Na Serikali Kwa Miezi Mitatu

$
0
0

Manejimenti ya sahara media group ambao ni wamiliki wa Star Tv, RFA naKiss Fm  imesema haijapata barua au taarifa rasmi yeyote kutoka mamlaka ya mawasilano Tanzania TCRA  ya kutakiwa kufunga vyombo vyake.

Imesema wameshtushwa na taarifa hiyo ikizingatiwa kwamba wamekuwa wakilipia leseni ada zake na ada za masafa kwa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 500 hadi kufikia mwezi October 2015.

Wamesema yamekuwapo mawasiliano ya mara kwa mara kati ya TCRA kanda ya Mwanza, makao makuu na sahara media group limited nakukubaliana juu ya utaratibu wa malipo ya ada husika.

Lakini menejimenti imeshangazwa na hatua hiyo ya TCRA kutangaza kuvifungia vituo vyake kupitia mkutano wa  vyombo vya habari bila kujali athari zakufungia vyombo vya kitaifa kwa walaji na watoa huduma.

Sahara media group limited imekuwa ikilalamikia utozwaji wa ada kwa dola za kimarekani jambo ambalo limekuwa likipandisha ada hizo kila mara na kufanya ulipwaji wa ada hizo kibajeti kukwama kwama.

Menejimenti pia imelaani taarifa hiyo kutolewa mwishoni wa wiki nakuvipa vituo husika siku mbili tu kukamilisha ulipaji ada wakijua dhahiri jumamosi na jumapili sio siku za kazi.

Menejimenti ya star tv  inawaondoa wasiwasi watazamaji na wasikilizaji wake,  hatua  thabiti zitachukuliwa ili kumaliza tatizo hili kwa sahara media group limited  na TCRA Kwa Kufuata Misingi Ya Sheria, Kanuni Na Maridhiano.

Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images