Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Ujauzito wa Wema Sepetu Wambadilisha Tabia..Sasa Marafiki zake ni Watoto na Wamama Wenye Watoto Wachanga

$
0
0
Wema Sepetu Akiwa na Mtoto 
Habari ya mjini kwa sasa ni ujauzito wa Wema Isaac Sepetu ambapo inadaiwa kuwa ameanza mazoezi ya kumlea mtoto wake mtarajiwa.

Kwa mujibu wa shosti wake wa karibu, kwa sasa Wema ameongeza urafiki kwa akina mama wenye watoto wachanga ili kuchukua ‘maujuzi’ ya namna ya kuwa mama bora kwa mwanaye mtarajiwa.

Yaani ukitaka kujua Madam yupo bize na mazoezi ya kulea, kila tunapokwenda akimuona mama aliyemzoea mwenye mtoto basi ataomba ambebe mtoto acheze naye au hata amlishe.

Kweli Wema anapenda watoto lakini sasa hivi imekuwa too much (imepitiliza). Hata ukifuatilia kwenye akaunti zake kwenye mitandao ya kijamii utaona sasa hivi yupo bize kutupia picha akiwa amebeba watoto,” alisema shosti huyo wa karibu wa Wema na kuongeza:

Kiukweli bidada (Wema) yupo kwenye mazoezi makali ili awe mama bora kwa mwanaye mtarajiwa kwani alitamani kuwa na mtoto kwa muda mrefu.”

Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, gazeti lilimtafuta Wema ili kujua anaendeleaje na mazoezi ya kulea mwanaye mtarajiwa lakini simu yake iliita bila kupokelewa.

HATIMAYE Nuhu Mziwanda Akiri Tattoo ya Shilole Mwilini Mwake Yamtesa..Lakini Hata ifuta Mpaka Kieleweke

$
0
0
Nuhu Mziwanda na Shilole
Baada ya Shilole Kutamka wazi wazi kuwa hamtaki tena Nuhu Mziwanda kimapenzi na haoni faida yoyote ya kuwa na Nuh Mziwanda, Nuhu Amesikitika Sana na Kauli hiyo kiasi kwamba kila akiangalia Tattoo ya Shilole Mwilini mwaka anaumia roho lakini amesema hawezi kuifuta mpaka atakapopata mbadala wa Shilole

 “Ni kweli ila hii tatuu nitaifuta nitakapompata wa kuziba pengo la Shilole.” Nuhu Mziwanda

WIKI ya Baraka Kwa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete..Baada ya Kupewa Ukuu wa Chuo...Hili ni Jingine Zuri Kwake

$
0
0
Baada ya Kupewa Ukuu wa Chuo cha UDSM na Rais Magufuli Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ametunukiwa Shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa ya mahusiano ya kimataifa jana Jijini Dar es Salaam katika mahafaliya 30 ya Chuo Kikuu Huria Tanzania.

Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amesema amefarijika sana kutunukiwa Shahada hiyo ya heshima itolewayo na Chuo kikuu Huria Tanzania kwa watu ambao wametoa mchango katika maendeleo katika jamii kupitia nafasi zao kiutendaji.

Hapa Kazi tu ya Magufuli Yazaa Matunda..Haijawahi Tokea Nchini..Makusanyo ya Halmashauri Nchini Yaongezeka kwa 800%

$
0
0
Makusanyo ya mapato katika halmashauri nchini, yameongezeka kufikia asilimia 800 hadi 900 baada ya kuanza kutumika kwa mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki katika halmashauri 164.

Hayo yalibainishwa jana na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma

Jaffo alisema Serikali imesanifu na kutengeneza mfumo wa kukusanya na kutoa ankara na hati za madai kwa kodi na tozo mbalimbali katika mamlaka za Serikali za Mitaa ili kuachana na utaratibu wa kukusanya mapato kwa kutumia hati zinazoandikwa kwa mkono.

Alisema tangu halmashauri kuanza kutumia mfumo wa kukusanya mapato kwa njia ya kieletroniki, makusanyo yameongezeka kwa asilimia 800 hadi 900, hali ambayo inadhihirisha ukusanyaji mapato kwa njia ya stakabadhi za kuandikwa kwa mikono fedha nyingi zilikuwa zikipotea.

Alisema msingi wa kuanzishwa kwa matumizi ya mfumo huo ni kuanzisha matumizi ya benki ya TEHAMA katika kukusanya kodi na tozo mbalimbali na kuachana na utaratibu wa kukusanya mapato hayo kwa kutumia stakabadhi za kuandikwa kwa mkono, ambao hutengeneza mianya ya wizi na ubadhirifu wa fedha.

Alisema mfumo huo umekusudia kurahisisha utoaji wa stakabadhi na utunzaji kumbukumbu na kudhibiti upotevu wa mapato katika vyombo vinavyokusanya fedha za umma.

Alisema serikali iliagiza ifikapo Julai 1, 2015, halmashauri zote ziwe zimeanza matumizi ya ukusanyaji wa mapato kwa mfumo wa kielektroniki, lakini ilipofika tarehe hiyo halmashauri 51 sawa na asilimia 28.18 ya halmashauri zote nchini, ndizo zilikuwa zimetekeleza agizo hilo.

Aidha, hadi mwanzoni mwa Desemba 2015 ni halmashauri 86 pekee sawa na asilimia 47.78 ndizo zilikuwa zimeingia katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa agizo la serikali licha ya kupewa muda hadi Desemba 31, 2015.

Alisema kutokana na kusuasua kwa zoezi hilo la serikali, ndipo agizo la msisitizo lilitolewa na Ofisi ya Rais Tamisemi kuwa ifikapo Januari 10, mwaka huu halmashauri zote ziwe zimeingia katika mfumo huo; hivyo hadi Januari 12, halmashauri 164 sawa na asilimia 90.6 zimeingia katika hatua mbalimbali za ufungaji na matumizi ya mfumo.

Pia halmashauri 17 mpya sawa na asilimia 9.4, hazijaanza mchakato wa kufunga mfumo kwa sababu mbalimbali, zikiwemo kutokuwa na ofisi ya kudumu, kutofikiwa na Mkongo wa Taifa, umeme na zingine hazijagawana mali na halmashauri mama. Alizitaka zijipange kufunga mfumo huo.

Bernard Membe Afungua Mdomo na Kumkosoa Vikali Rais Magufuli Kuhusu Sera ya Kubana Matumizi na Safari za je

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Serikali iliyopita, Bernard Membe ameungana na waziri mwenzake wa zamani, Dk Makongoro Mahanga kukosoa sera ya kubana matumizi ya Rais John Magufuli ya kudhibiti safari za nje na kuteua baraza dogo la mawaziri.

Kama ilivyokuwa kwa Dk Mahanga, waziri huyo aliyedumu kwa miaka tisa kwenye Wizara ya Mambo ya Nje amesema kiuhalisia, Rais hajapunguza idadi ya wizara kama alivyosema bali amepunguza “idadi ya mifuko”, huku akisisitiza kuwa mkuu huyo wa nchi atalazimika kutoka nje “atake asitake”.

Membe amekuwa waziri wa pili wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kukosoa sera ya kubana matumizi ya Serikali ya Awamu ya Tano baada ya Dk Mahanga, ambaye sasa amehamia Chadema, kumkosoa akisema idadi ya wizara inapimwa kwa kuangalia makatibu wakuu na si wizara na hivyo ukubwa wa Baraza la Mawaziri bado uko palepale.

Katika mahojiano maalumu na Mwananchi mapema wiki hii, Membe alikuwa na maoni kama hayo na akaenda mbali zaidi kuzungumzia hata sera ya kudhibiti safari za nje na Rais kujizuia kusafiri, akisema “Tanzania haiwezi kuishi kama kisiwa” katika dunia ya leo.

Kubana matumizi

Membe, ambaye alikuwamo kwenye kinyang’airo cha urais na kufika hadi tano bora, alisema Rais hajabana matumizi yoyote kwa kupunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri, bali alichofanya ni kupunguza idadi ya mawaziri na siyo wizara.

“Alichofanya ni sawa na kuwa na mayai kumi halafu ukaamua kuyaweka kwenye mifuko kumi, maana yake ni kwamba utakuwa na mifuko kumi yenye mayai,” alisema Membe.

“Lakini unaweza kuwa na idadi hiyo hiyo ya mayai na ukaamua kuyagawanya; mayai matatu unayaweka kwenye mfuko mmoja, mawili kwenye mfuko mwingine na yaliyobaki kwenye mfuko mmoja. Maana yake ni kwamba utaendelea kuwa na mayai kumi lakini idadi ya mifuko imepungua. Hapa sasa utakuwa hujapunguza gharama za kuyatunza hayo mayai.”

Rais aliahidi kwenye kampeni na hotuba yake ya uzinduzi wa Bunge kuwa atapunguza ukubwa wa Baraza la Mawaziri ili kubana matumizi. Alitekeleza ahadi yake kwa kuunda baraza lenye mawaziri 34 tofauti na lililopita ambalo lilikuwa na mawaziri 55.

Upunguzaji huo wa baraza ulifanywa kwa kuunganisha wizara na hivyo kufanya makatibu wakuu, ambao ni maofisa masuhuli wa wizara kuwa zaidi ya mmoja kwenye baadhi ya wizara.

“Ameendeleza wizara zilezile, lakini akaamua kuzikusanya pamoja. Hiyo haimaanishi kuwa atakuwa amepunguza gharama za uendeshaji wake,” alisema Membe.

“Hilo tutaliona kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka huu. Tuone kama bajeti itaongezeka au itapungua? Kwa sababu kama wizara zimepungua kama tunavyoamini, lazima bajeti ipungue, sasa bajeti ikiongezeka au ikibaki vilevile maana yake hakuna kilichofanyika.”

Membe alitoa mfano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambayo sasa inaitwa “Wizara ya Mambo ya Nje, Kikanda na Ushirikiano wa Afrika Mashariki”, akisema itapaswa kuwa na bajeti mbili; ya Mambo ya Nje na Bajeti ya Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki kinyume chake ni vigumu kuiendesha.

Membe alikiri kuwa hata yeye angeingia kwenye mtego wa kupunguza idadi ya wizara kama angefanikiwa kuchaguliwa kuwa Rais kama ilivyokuwa nchini Namibia ambako wizara zilipunguzwa kutoka 32 hadi 20.

“Baadaye nikagundua kuwa hata Namibia yenyewe inajuta,” alisema.

Alisema siku ya kuapishwa Rais Magufuli, alikutana na Makamu wa Rais wa Namibia, Nickey Lyambo na baada ya kusalimiana na kumpongeza kwa hatua ya kupunguza wizara, kiongozi huyo wa Taifa hilo la kusini mwa Afrika alimweleza kuwa uamuzi huo umewasababishia matatizo makubwa bungeni

“Aliniambia katika Bunge la Namibia kuna mjadala mkali wa kutaka wizara ziongezwe,” alisema Membe akimnukuu makamu huyo wa rais wa Namibia.

Membe alibainisha kuwa kwa Tanzania, mfumo huo mpya wa wizara pia unaweza kuathiri uwasilishaji wa bajeti bungeni kwa kuwa mawaziri sasa watahitaji muda mwingi zaidi kuliko ilivyokuwa awali ili kuzungumzia wizara kadhaa zilizounganishwa, jambo ambalo lililalamikiwa pia na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Tundu Lissu. “Kila kitu kina form na content (muundo na maudhui). Alichofanya Rais Magufuli ni kubadili form na siyo content ya wizara, wizara ni zilezile na mzigo ni uleule,” alisema.

Safari za nje

Mbunge huyo wa zamani wa Mtama mkoani Lindi, pia alikosoa udhibiti wa safari za nje, akisema Tanzania si kisiwa.

Alikuwa akijibu swali lililomtaka aeleze uhalisia wa mpango wa Rais Magufuli kubana matumizi kwa kufuta safari za nje za mawaziri na watumishi wengine wa umma.

Mara tu baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli alifuta safari zote za nje ya nchi kwa watendaji na watumishi wa umma, isipokuwa zile tu ambazo zingepata kibali cha Ikulu, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kubana matumizi ya Serikali.

Rais Magufuli alisema katika hotuba yake ya kuzindua Bunge kuwa kuanzia mwaka 2013 hadi 2015, safari hizo ziliigharimu Serikali Sh356.3 bilioni na kwamba kati ya fedha hizo, Sh183.1 bilioni zilitumika kwa ajili ya tiketi za ndege, Sh68.6 bilioni kwa ajili ya mafunzo na Sh104.5 bilioni kwa ajili ya posho.

Bila kugusia madhara ya kufuta safari hizo, Rais Magufuli alijielekeza zaidi kwenye matumizi ya fedha ambazo angeokoa.

“Lakini tujiulize fedha hizo zingeweza kutengeneza zahanati ngapi? Zingeweza kutengeneza nyumba za walimu ngapi? Zingeweza kutengeneza madawati mangapi? Zingeweza kununua dawa hospitalini tani ngapi?” alihoji Rais Magufuli katika hotuba yake iliyotoa mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Lakini Membe, ambaye wizara yake iliwahi kutetea safari za Jakaya Kikwete nje ya nchi baada ya wapinzani kusema ziligharimu zaidi ya Sh4 trilioni, alisema safari za nje zina umuhimu kwa taifa lolote.

“Tanzania si kisiwa, hata ukiwa tajiri namna gani lazima utoke nje ya nchi yako,” alisema Membe ambaye ana shahada ya umahiri ya uhusiano wa kimataifa aliyoipata Marekani.

“Lazima utakwenda mwenyewe au mawaziri wako na hasa Waziri wa Mambo ya Nje kwa sababu kuna vikao nje ya nchi ambavyo mabalozi hawaruhusiwi kuingia.

“Ukijaribu kujifanya kisiwa utakuwa kama Zimbabwe. If you isolate yourself you will be isolated (ukijitenga, utatengwa).”

Membe alisema nchi ina mabalozi 36 tu duniani kote kati ya nchi 194 zinazohitaji uwakilishi huo na kibaya zaidi, mabalozi hawaruhusiwi kuingia kwenye baadhi ya vikao, na hata wakiingia wakifika kwenye hatua ya uamuzi watazuiwa kushiriki.

“Kwa mfano, Uturuki hatuna ubalozi, sasa unapoona ndege inaleta watalii kutoka Uturuki, unadhani Bunge la Uturuki liliketi kutuletea watalii Tanzania? Hapana. Tulitoka nje na kuwashawishi wakaja,” alisema Membe aliyewahi kueleza kuwa wakati wa awamu ya Rais Jakaya Kikwete mawaziri walikuwa wanapishana angani kana kwamba kuna moto ardhini.

“Pia, leo unaposikia gesi, gesi, gesi nayo imepatikana nje ya ubalozi. Mawaziri walitoka nje ya nchi wakatafuta wawekezaji. Ni kazi ya wizara kufanya yote hayo.”

Membe alirudia kauli aliyoitoa siku chache kabla ya kuanza mchakato wa Uchaguzi Mkuu mwaka jana kuwa lazima waziri wa mambo ya nje awe nje ya nchi kwa muda mwingi na ikitokea yuko ndani ya nchi kwa mwezi mmoja mfululizo, lazima ni mgonjwa.


PICHA ya Rais John Pombe Magufuli Akiwa Kwenye Nguo za Jeshi Zawakosha Wengi

$
0
0
Akiwa katika ziara Rais Magufuli Amevaa Gwanda za jeshi za Amiri mkuu wa Jeshi la Tanzania....

Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Arusha Mjini wakati akipita Barabarani kuelekea Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli ambako pamoja na mambo mengine kesho tarehe 23 Januari, anatarajiwa kutunuku Kamisheni kwa Maafisa wanafunzi wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi Monduli kundi la 57/15.

Kujichubua Kwa Wanaume ...Picha za EX wa Zari na Ray wa Bongo Movies Kabla na Baada ya Kujichubua

$
0
0
Aliyekuwa Mume wa Zari Ivan Kabla na Baada ya Kujichubua

Mwigizaji wa Movies za Kibongo Baada na Kabla ya Kujichubua.

Je Kuna Uzuri ama faida yoyote kwa Mwanaume kujichubua au ni ulimbukeni!!!

Kampuni ya UDA Yaibuka na Kusema Haya Kuhusu Familia ya Kikwete Kumiliki Kampuni Hiyo

$
0
0
Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena ameeleza kusikitishwa na taarifa zisizo za kweli zinazoihusisha familia ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete na umiliki wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na kusisitiza kuwa yeye ndiye mmiliki halali.

Kisena alidai kwa muda mrefu watu wenye nia mbaya dhidi yake, wamekuwa wakihoji umiliki wa shirika hilo licha ya kuonyesha vielelezo vyote. Alisema taarifa zilizosambaa hivi karibuni zinazodai kuwa anaimiliki Uda kwa ushirikiano na Khalfan ambaye ni mtoto wa Kikwete hazina ukweli.

Alidai kuwa Kampuni ya Simon Group ambayo ilisajiliwa Mwanza 2007, inamilikiwa na watu wanane wa familia ya Kisena isipokuwa Profesa Juma Kapuya ambaye ana asilimia tano ya hisa kwenye kampuni hiyo.

“Kampuni hii inamilikiwa na watu wanane, hata mkisoma hizi nyaraka mtaona majina ya watu hao ambao ni mimi, wanangu; Simon, Gloria, Kulwa na George; mdogo wangu William Kisena, mama yangu Modesta Pole na Profesa Kapuya.

“Hakuna jina la Khalfan Kikwete hapa, sijui hizo taarifa watu wanazitoa wapi,” alihoji Kisena huku akionyesha vielelezo.

Alisema hata wakati kampuni hiyo inaanzishwa, Khalfan alikuwa mtoto mdogo ambaye asingeweza kumiliki kampuni hiyo ambayo inakua kwa kasi.

Kisena alidai taarifa hizo za uongo zinaenezwa na watu ambao ni washindani wake kibiashara na wengine ni maadui wa kisiasa wa Kikwete.

Alisema yeye ni kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na amekuwa hivyo siku zote, lakini hajihusishi na siasa bali anafanya biashara.

“Kama kuna wanaoichafua familia ya Kikwete waache kuniunganisha na mimi, sifanyi siasa.

"Na kama kuna wanaonichafua kibiashara basi waache kuiingiza familia ya Kikwete, wapambane na mimi kwenye biashara,” alisema Kisena.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo alisema kampuni yake ya Uda RT ndiyo itakayoendesha mradi wa mabasi yaendayo kasi na kuwa nauli zilizopendekezwa zilitokana na tathmini ya gharama halisi za uendeshaji wa mradi huo.

Alisema baadhi ya vitu vilivyowafanya wapendekeze nauli hizo kuanzia Sh700 mpaka Sh1,200 ni pamoja na kulipia barabara za Dart.

Pia, alisema mabasi hayo yatakuwa hayakai vituoni kwa hiyo huenda wakati mwingine yatakuwa yanatembea bila abiria.

“Sababu hizo ndiyo zimetufanya tupendekeze nauli hizo, lakini tuko kwenye mazungumzo na Serikali ili waondoe malipo ya barabara ili nauli ipungue.Mazungumzo yanaenda vizuri, ninaamini nauli zitapungua,” alisema.

Kisena alisema ifikapo Machi, mwaka huu, Kampuni ya Uda itaorodheshwa kwenye Soko la Hisa ili wananchi waweze kumiliki wenyewe kampuni hiyo.

Alisema wanaendelea kufanya mipango kwa ajili ya kuuza asilimia 70 ya hisa kwa wananchi wote.

Nay wa Mitego 'Mwanaume Niliyomfuma na Mwanamke Wangu Kitandani Alikuwa Amevaa Boxer Yangu

$
0
0
Nay wa Mitego na Siwema
Nay wa Mitego akihojiwa na kipindi cha Leo tena clouds radio kasema ni mengi sana yalitokea lakini hakuyaongea na alimpenda kwa dhati binti huyo na alikua na mipango nae mikubwa...
Amedai Siku Ambayo alimfumania Mchumba wake Kitandani akiwa na mwanaume mwingine huyo Mwanaume alikuwa amevaa Kaptula ya ndani (Boxer) yake...

Tukio hilo lilitokea Mwaka jana ambao kwa sasa wawili hao wameshaachana na kila mmoja akiwa na maisha yake...

Breaking News; Kamati Mpya ya Miss Tanzania ya Kina Jokate Yajitoa Kuandaa Mashindano Hayo

$
0
0
Kamati Mpya ya Miss Tanzania iliyokuwa na Kina Jokate na Juma Pinto imejitoa kuandaa mashindoni Hayo baada ya Kushindwa kuelewana mambo kadhaa..

UKAWA Walianzisha Tena Bungeni Wagomea Kamati za Bunge na Kususia Uchaguzi

$
0
0
Bungeni
Wakati vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge vikitarajiwa kuanza leo kwa uteuzi wa wajumbe, wabunge wa upinzani tayari wameanza kwa kumtikisa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Job Ndugai, baada ya kususia uchaguzi wa wenyeviti wa kamati hizo.

Dalili za mgawanyiko kwenye kamati hizo zilianza kuonekana juzi, baada ya wabunge hao wa Kambi ya Upinzani kufanya kikao na kuweka msimamo wa kutaka kushirikishwa kwenye uteuzi wa wajumbe.

Kambi ya Upinzani ilisema inataka kushirikishwa katika hatua hiyo ikidai kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM), imekuwa ikiwapangia watu wa kuongoza kamati zinazosimamia mapato ya serikali ambazo kikanuni zipo chini yao.

Viongozi hao wa kambi ya upinzani walidai kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakipangiwa watu wa kuongoza Kamati ya Hesabu za Serikali za (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ambazo kikanuni zinatakiwa kuongozwa na upinzani.

Baada ya Ofisi ya Bunge kutangaza majina ya wajumbe wa kamati, Kambi ya Upinzani Bungeni ilikutana na waandishi wa habari, lakini wakaahirisha kwa madai kuwa wamegundua kwamba orodha ya majina yaliyotoka, yana matatizo mengi zaidi.

“Tumegundua kwamba matatizo hayapo kwenye kamati ya PAC na LAAC tu, kwenye kamati nyingi kuna matatizo kwa hiyo kwa sasa viongozi wa kambi wanakutana kujadili na kuchambua taarifa iliyotolewa baadaye tutakutana na wabunge wote kisha kesho tutatoa msimamo wetu,” alisema Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, John Mnyika.

Baada ya kauli hiyo, Mnyika aliulizwa inakuwaje wao wanaendelea na vikao wakati wenzao wa CCM wakiwa kwenye uchaguzi:

“Siwezi kujibu chochote, neno lolote nitakalosema, nitaingilia hicho kinachojadiliwa na viongozi. Wewe subiri kwanza tumalize kikao, tutoke na msimamo wa pamoja na kesho tutawaeleza msimamo wetu,” alisema Mnyika.

Awali, kabla ya kutolewa kwa majina hayo, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Magdalena Sakaya, alisema kwa muda sasa wamekuwa wakichaguliwa watu wa kuongoza kamati hizo na CCM.

“Ni sawa na mtu anakupa kitu kwa mkono wa kushoto na kukunyang'anya kwa mkono wa kulia. Ndiyo maana tukataka tushirikishwe kuanzia wajumbe watakaokuwa kwenye kamati hizo,” alisema Sakaya ambaye ni Mbunge wa Kaliua mkoani Tabora.

Kanuni za Kudumu za  Bunge Toleo la Aprili 2013, inasema: “Wenyeviti wa Kamati za Bunge zinazosimamia matumizi ya fedha za Umma ambazo ni Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, watachaguliwa kutoka miongoni mwa wajumbe wa kamati hizo ambao wanatoka katika Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.”

Diamond Platnumz Yamfika Hapaaa!...Afichua Jambo Kumbe ni Wasanii Wakubwa Ndio Wanao Ongoza Kumchafua Kuhusu Tifah

$
0
0
Diamond Platnumz amechukizwa na jinsi wasanii anaowaheshimu wanavyohaingaika kumchafua yeye na mwanae Tiffah mtandaoni na amesema tayari anawajua wasanii hao.

Akizungumza kwa hasia na Ayo TV Alhamisi hii, Diamond alisema anawashangaa wasanii wanaotumia muda mwingi kumponda mtoto wake kuliko kutafuta pesa.
“Watu wamekaa kwenye sanaa muda mrefu mimi nimewakuta, nawaona wameanza kuwa mastaa kabla ya mimi, hawana viwanja, hawana nyumba, hawana magari. Wangetumia muda huo kutengeneza maisha yao kuliko kukaa kumdis mtu mwingine. Halafu mimi sipendagi kusema lakini inavyofika hatua kwenye vitu kama hivi mimi naongea. Kwanza nilikuwa sijui uchungu wa mtoto sasa hivi naujua kwamba kweli mtoto anauma,” alisema Diamond.
“Halafu mtu anayezungumzia inawezekana mtoto akawa na pesa kuliko hata yeye, kwa sababu akaunti ya Tiffah inawezekana ikawa na hela hata kuliko huyo mtu anayemdiss huyo mtoto kama sio wangu mimi. Inawezekana akawa na hela kuliko hata wewe unayesema mtoto sio wangu au unasema mtoto mbaya. Kwa sababu mtoto alifunguliwa akaunti yake kwa mara ya kwanza ikaingia milioni 10. Ni mtoto inawezekana ni maarufu kuliko hata wewe kwa sababu nikifika Nigeria wanaanza kuuliza Tiffah hajambo? So inafikia time hata kwa mtoto unataka kiki?”
“Kwa ndugu zangu wasanii waache kidogo kumfuata fuata binti yangu, kila mtu anakuja sijui DNA sijui nini, waache hizi mambo mimi ndiye mwenye mtoto.”

Tazama mahojiano hayo hapo chini


Zitto Kabwe Afunguka ya Moyoni Kuhusu Kamati za Bunge...Awaponda Serekali na Ukawa Kwa Kuwaita Nyumbu

$
0
0
Kauli ya Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook
Kupitia ukurasa wake wa facebook, Zitto Kabwe ambaye bunge lililopita alikuwa mwenyekiti wa PAC ameandika;
 
"Kamati zote za Bunge zina hadhi sawa ndani ya Bunge. Kila mbunge ana haki ya kuwa kwenye kamati yeyote ile na hakuna mbunge bora zaidi ya mwingine.

"Kanuni zimeweka utaratibu wa uteuzi kwenye Kamati ikiwemo maombi ya mbunge, uzoefu na ujuzi wa eneo husika.

"Wanaolalamika leo upangaji wa Kamati ndio usiku wa kuamkia jana walimshinikiza Spika asiwapange mahasimu wao kisiasa kwenye Kamati wanazoona wao ni nyeti.

"Ni unafiki uliopitiliza unapojenga hoja ya uzoefu, chaguo la Mbunge na ujuzi wakati huo huo wenye vigezo vyote hivyo unawapiga vita kwa sababu za kisiasa

"Ni dhahiri kuwa mpangilio wa Kamati unajenga Bunge kibogoyo,  Nilitahadharisha toka Bunge la 11 lilipoanza kwamba, "kuna dalili za Serikali kutaka kulidhibiti Bunge ( kumbukeni sarakasi za Tulia Ackson ambaye sasa ni Naibu Spika) . "

"Kiongozi unapokwenda kwa Spika kusema 'fulani asipangwe Kamati fulani kwa sababu atapata sifa' halafu ukataka 'nyumbu' wako ndio wapangwe huko ujue unaisadia Serikali kudogosha Bunge.

"Spika anapoamua Nyote, huyo usiyemtaka na nyumbu wako wasiende huko ujue amekudharau sana.

"Unapoona Viongozi wa Serikali wanahangaika kupanga Kamati za Bunge watakavyo wao ujue viongozi hao ni dhaifu, hawana nia njema na hawataki kuwajibishwa.

"Twendeni kwenye hizi hizi Kamati tulizopangiwa kuwafanyia kazi Watanzania. Twendeni tukaonyeshe kuwa Bunge litabaki Bunge tu na Wabunge tusikubali Bunge Kibogoyo. Ni lazima Bunge lidhibiti Serikali hata Serikali hiyo ikiwa inaongozwa na Malaika.

"Serikali ni chombo cha mabavu lazima idhibitiwe, na ndio kazi ya Bunge kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 63."

Diamond Platnumz Azidi Kulipalilia Bifu la Wema na Zari, Adai Zari Japo Ana Watoto Watatu Mwili wake Unadhamani zaidi wa Ambae Hana Mtoto Hata Mmoja

$
0
0
Zari Hassan
Wema Sepetu
Akihojiwa na Millard ayo Diamond Amesema kuwa Ukiangalia Japo Zari ana Watoto Watatu Kwa sasa lakini Mwili wake Bado una thamani kubwa zaidi ya ambao hawana hata mtoto mmoja...

Kwa kinachoendelea sasa kati ya Wema Sepetu na Zari Hassan hili ndogo moja kwa moja linamwendea Wema Sepetu ambae alishakuwa na Mahusiano naye na hana mtoto mpaka sasa..

Angalia Video Hapa Diamond Akiongelea hilo;


Mengine Yaibuka Kuhusu Mbwana Samatta Kwenda Kucheza Ulaya..Aamua Kurudi TP Mazembe

$
0
0
Mbwana Samatta Akianya yake
Baada ya dili la uhamisho wa mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta kusuasua kutoka klabu yake ya TP Mazembe kwenda klabu ya Genk ya Ubeligiji, star huyo ameamua kurejea kwenye klabu yake hiyo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwa ajili ya mazungumzo na tajiri wa Mazembe Moise Katumbi kuhakikisha dili hilo linakamilika.

Manager wa Samatta Jamal Kisongo amesema, mbali na mazungumzo, Samatta amerejea kwenye klabu yake ili aendelee kujifua hata kama ikitokea boss huyo akamfungulia mlango wa kutokea basi awe yuko fiti kuingia moja kwa moja kwenye timu kuliko kuendelea kukaa nyumbani.

“Tumeona ni vyema Samatta akarejea Mazembe katika kumpa presha na kumsukuma Katumbi, amerejea kwenye kituo chake cha kazi na kumpa taarifa Katumbi kuwa kama hato muuza kwenye klabu ya Genk basi yeye atamalizia mkataba wake TP Mazembe na ataondoka mwezi April. Jambo ambalo kwa hakika Katumbi hawezi kukubaliana nalo kwakuwa anajua Samatta akiondoka mwezi April ataondoka bure na yeye atakuwa ameingia hasara”, amesema Kisongo  leo asubuhi wakati akihojiwa kwenye kipindi cha michezo cha E-FM Radio.

“Lakini tumeona pia ni muhimu akaenda Mazembe ili awe anafanya mazoezi hata kama ikitokea ameuzwa basi anaweza kutumika moja kwa moja kwasababu atakuwa yuko fiti”.

“Mkataba wake na Genk unampa nafasi ya kujiunga mwezi January kama Katumbi atamuuza, kama Katumbi atagoma, mkataba wake huohuo unampa nafasi ya kuweza kujiunga katika majira ya joto (mwezi wa 7)”.

“Mbwana Samatta jina lake halijaingizwa kwenye orodha ya majina ya wachezaji watakaocheza michuano ya klabu bingwa Afrika mwaka kuu, Katumbi alishamuacha kwasababu anajua anamaliza mkataba mwaka huu na atamuuza January. Kwa maana hiyo Mbwana hana faida kwenye klabu ya TP Mazembe kwasababu ligi ya ndani ndiyo ligi pekee anaweza kucheza ambayo hata wachezaji wengine wanaweza wakacheza vizuri tu”.

Mara baada ya Samatta kupata timu ambayo imeonesha kumuhitaji, boss wa Mazembe amekuwa akitia ngumu kumuachia Samatta kutimkia Ubeligiji badala yake amekuwa akimtafutia timu yeye mwenyewe huku akiwa na sababu zake binafsi za kufanya hivyo lakini hana sababu za kimantiki za kumzuia mchezaji huyo kujiunga na Genk.

Ma-Video Queen wa Bongo Wanavyotumika Kama Big G na Kisha Kuishia Kutumiwa na Mapedeshee

$
0
0
Gigy Money
Wasanii wengi wa Muziki wa Bongo Fleva, kila wanapotoa nyimbo mpya hufikiria pia kuutengenezea video kali ili kuweza kuwashika vilivyo mashabiki zao. Katika video hizo, wapo wanaofikia hatua ya kwenda kuzifanyia nje ya nchi, hasa Afrika Kusini ambako wengi wanakimbilia huko.

Lakini sasa, kwenye uandaaji wa video hizo kuna watu muhimu sana ambao wamekuwa wakitumika kuzifanya ziwe na mvuto wa kutazamwa.

Watu hao ni wasichana wakali wanaofahamika kwa jina la Video Queens. Katika ulimwengu wa muziki wa sasa, wasichana hawa wana umuhimu mkubwa lakini sasa Kibongobongo inashangaza kuona baadhi yao wanatumika kama Big G.

Makala haya yana dhamira ya kuonesha mazingira magumu wanayofanyia kazi wadada hao. WANAPATIKANAJE? Zipo kampuni zinatoa ‘Mavideo Queen’ lakini wengi wanatoka mtaani tu.
Kim Nana

Wanachokifanya wanamuziki ni kutafuta wadada wazuri, wenye maumbile tata na wasio na aibu. Ndiyo maana ukifuatilia utabaini kuwa ‘Mavideo Queen’ wengi ni micharuko. Kama siyo mcharuko kazi hii huwezi kuifanya na kama utaifanya, itakuwa kwa shida sana.

MALIPO Nimejaribu kuzungumza na baadhi ya ‘Mavideo Queen’ wakanieleza kuwa, hawalipwi pesa nyingi kivile.

“Unajua mimi niliwahi kulipwa shilingi laki moja tu tena kwa shida kucheza kwenye video ya….( anataja jina la mwanamuziki mkubwa). Nilikubali kwa sababu ya shida zangu.
Lakini kama hujui, Mavideo Queen wengine hawalipwi kabisa. Yaani wao ilimradi wauze sura na kupata umaarufu.
“Kwa mfano, wapo wadada ambao wako tayari kuonekana kwenye video za wasanii kama Ali Kiba, Dimpoz au Diamond bila hata malipo na wapo tayari kutumia gharama zao za mavazi, saluni ilimradi tu wauze nyago,” alisema mrembo mmoja aliyewahi kuonekana kwenye video nyingi za wa wasanii wakubwa aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Tunda
 IYO KAZI YA KUITEGEMEA Wengi niliozungumza nao wanaeleza kuwa, U-video Queen una faida pale tu utakapobahatika kupata msanii akayekulipa vizuri na ukapata umaarufu wa kuweza kupata dili nyingine.

 “Kwa hapa mjini ukisema mimi kazi yangu ni u-video queen tu, unajidanganya.
 Kwanza ukishaonekana kwenye video mbili tatu, tayari umechuja. Huwezi kupata dili    tena. Ndiyo maana nasema ili uweze kuwa na maisha mazuri, fanya u-video queen na  kazi nyingine siriasi.
Kinyume chake utapata umaarufu na mwisho wa siku utakuwa unabadili mapedeshee kwa kuwa watakupapatikia,” anasema Roseline John wa Kinondoni aliyewahi kufanya kazi hiyo miaka ya nyuma.
NINI CHA KUFANYA?
Kama nilivyosema kuwa, wadada hawa wana umuhimu mkubwa kwenye tasnia ya muziki lakini siyo kazi ya kuitegemea tu.

Niwashauri tu ‘Mavideo Queen’ kama vile Kidoa, Gigy Money, Gilla, Kim Nana, Cute Bhinna, Tunda, Zuhura Gora, Baby Nahiyyah na wengineo kwamba kama mmejaaliwa muonekano mzuri na mkapata dili la kuonekana kwenye video za wasanii, fanyeni lakini tafuteni kazi nyingine halali za kuwaweka mjini.
Kumbuka wasanii watakutumia kwa kipindi f’lani lakini itafika wakati utakuwa huna dili tena, watatafutwa wasichana wengine, wewe utawekwa pembeni. Je, utafanya kazi gani? Akili kumkichwa binti!

Source-Global Publishers 

Nafasi za Kazi Bank-Job On Training (120 Positions), Mwalimu Commercial Bank

$
0
0
Job Vacancy - Bank Job-Job On Training (120 Positions)
Location - Dar Es Salaam 
Position Type - Full Time
Organization Type - Company
Website - http://www.mcb.com
Mwalimu Commercial Bank

Bonyeza  HAPA Kusoma na Kuapply 

Au Tembelea www.ajirayako.com

Dk Magufuli: Arusha na Kilimanjaro Chapeni Kazi, Sitaki Kusikia Malalamiko ya njaa..Ikitokea Njaa Mkuu wa Mkoa Atawajibika

$
0
0
Rais John Magufuli jana, alitua kwa mara ya kwanza katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro tangu aingie madarakani na kuwataka wakazi wake kufanya kazi, kwani uchaguzi umekwisha.

Akizungumza na mamia ya watu waliojitokeza kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (Kia) na barabara kuu ya Arusha -Moshi, Dk Magufuli alishukuru kwa mapokezi aliyopata na kusema hatawaangusha wananchi hao.

“Uchaguzi umekwisha ndugu zangu sasa ni kazi tu na wananchi wa Arusha na Kilimanjaro sitawaangusha, ahadi zangu zote nilizotoa wakati wa kampeni nitazitekeleza,” alisema.

Alisema anajua matatizo ya Arusha na Kilimanjaro na kama alivyoahidi atatekeleza yote.

Pia  Mh John Magufuli amesema kuanzaia sasa hataki kusikia malalamiko ya wananchi juu ya suala la njaa na ikitokea akasikia vilio hivyo vikiendelea mkuu wa mkoa husika atachukuliwa hatua ikiwemo ya kufukuzwa kazi.

Mh. Magufuli ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani Arusha ameyasema hayo alipokuwa njiani kutoka jijini Arusha kwenda wilaya Monduli kwa ajili ya kufunga mazoezi ya kijeshi ya kuonyesha uwezo wa medani 2016 yaliyofanyika katika Briged ya 303 iliyoko Monduli

Kiingereza Tatizo Darasa la Nne, Wanafunzi 109,000 Kurudia Darasa Baada ya Matokeo Kutoka

$
0
0
Jumla ya wanafunzi 108,829 sawa na asilimia 11.13 kati ya 977,886 waliofanya mtihani wa kitaifa wa darasa la nne mwaka jana, wanatakiwa kukariri darasa baada ya kupata ufaulu usioridhisha.

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa jana na Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania, Dk. Charles Msonde, somo lililofanya vibaya kwa kupata kiwango cha chini cha ufaulu ni Kiingereza.

Akitoa matokeo hayo jana, Dk. Msonde alisema kiwango cha ufaulu kwa somo la Kiingereza ni wa chini zaidi kwa asilimia 65.67 wakati Sayansi ufaulu wake ukiwa juu kwa asilimia 89.44.

Alisema jumla ya wanafunzi 1,037,305 waliosajiliwa kufanya upimaji huo kitaifa, wasichana walikuwa ni 535,273 sawa na asilimia 51.60 na wavulana walikuwa ni 502,032 sawa na asilimia 48.40.

Alisema wanafunzi 977,886 sawa na asilimia 94.27 ya waliosajiliwa, walifanya upimaji huo na kati yao wasichana walikuwa ni 510,211 sawa na asilimia 95.32 na wavulana walikuwa ni 467,675 sawa na asilimia 93.16.

Alisema wanafunzi 59,419 sawa na asilimia 5.73, hawakufanya upimaji huo ambapo wasichana ni 25,062 sawa na asilimia 4.68 na wavulana ni 34,357 sawa na asilimia 6.84.

UFAULU WA JUMLA
Dk. Msonde alisema jumla ya wanafunzi 869,057 kati ya 977,886, wamepata alama zenye daraja la ufaulu wa A, B,C na D.

Alisema wanafunzi 108,829 wamepata daraja la E lenye ufaulu  usioridhisha.

WANAFUNZI BORA KITAIFA
Aliwataja kuwa ni Frank Mgeta, kutoka Shule ya Msingi Twibhoki mkoani Mara, akifuatiwa na Salum Rashid, kutoka Shule ya Msingi Hazina, ya jijini Dar es Salaam.

Wengine na shule zao katika mabano ni Mussa Christian (Alliace Mwanza), Ezekiel Gilu (Waja Springs Geita), Martha Nkwimba (Tusiime, Dar es Salaam), Lameck Nsulwa na Rajabu Hamis (Rocken Hill, Shinganga), Charles Luhumbika (Kwema Shinyanga), Mathias Amos  na Idd Masoud ( Alliance Mwanza).

WASICHANA 10 WALIONG’ARA KITAIFA
Aliwataja na shule zao kwenye mabano kuwa ni Martha Nkwimba (Tusiime, Dar es Salaam), Sabina Athanas (Alliance English, Mwanza), Nervis Michael (Alliance English, Mwanza, Jenipher Nyachilo (Paradise English, Geita) na Vivian Lyimo (Imani Kilimanjaro).

Wengine ni Vaileth Emmanuel (Fort Ikoma, Mara), Beatrice Novatus (Kaizirege Kagera), Ayamu Ayoub (Kaizirege Kagera), Ashura Juma (Kaizirege Kagera) na Alinda Byamungu (St. Peter Claver Kagera).

WAVULANA 10 BORA KITAIFA
Dk. Msonde aliwataja kuwa ni Frank (Twibhoki Mara, Salim Rashid (Hazina Dar es Salaam), Mussa Christian (Alliance English Mwanza), Ezekliel Gilu (Waja Springs Geita) na  Lameck Nsulwa (Rocken Hill Shinyanga).

Wengine ni Rajabu Hamis ( Rocken Hill Shinyanga), Charles Ndaki (Kwema Shinyanga), Mathias Amos (Alliance English Mwanza), Idd Masoud (Alliance English Mwanza) na Godfrey Manazi (Alliance English Mwanza).

SHULE 10 BORA KITAIFA
Katibu huyo alisema iliyoongoza ni Shule ya Msingi Alliance ikifuatiwa na Waja Springs, St. Peter, Tumaini, Furaha, Acacia Land, Tusiime, Imani, Kaizirege na Evenezer.

MIKOA 10 ILIYOFANYA VIZURI
Aliitaja kuwa ni  Dar es Salaam ambayo imeongoza ikifuatiwa na Iringa, Kilimanjaro, Njombe, Arusha, Tanga, Geita, Kagera, Mwanza na Shinyanga.

Halmashauri 10 zilizofanya vizuri alizitaja kuwa ni Ilala, Moshi, Mji Njombe, Arusha, Mji Makambako, Tanga Mjini, Arusha, Mufindi, Hai na Bukoba Manispaa.

Dk. Msonde alitaka zifanyike juhudi za makusudi ili kuinua kiwango cha ufaulu kwa masomo ambayo wanafunzi wamefaulu kwa kiwango cha chini.

Alisema Baraza linafanya uchambuzi wa kina wa matokeo hayo kwa kila somo ili kubainisha mada mbalimbali zilizowatatiza wanafunzi na baadaye kutoa machapisho ya uchambuzi yatakayowasilishwa kwa wadau wa elimu.

Alisema lengo ni kuwawezesha walimu kutumia taarifa hizo katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji shuleni.

Dk. Msonde alisema baraza linawahimiza maofisa elimu wa mikoa na wilaya kufuatilia katika kuhakikisha kuwa ufundishaji na ujifunzaji wa maeneo yaliyohitaji mkazo unafanyika ipasavyo.

Breaking News;Uchaguzi wa Marudio Zanzibar Kufanyika Mwezi Machi 2016

$
0
0
Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC ametangaza siku ya uchaguzi wa marejeo kwa upande wa Zanzibar ambayo itakua ni March 20 2016.

Je una Maoni Gani!
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images