Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Nisha Aongeza Utata Juu ya Mahusiano na Baraka da Prince...Adai Huwa Wanalala Pamoja

$
0
0
Nisha amesema kuwa, Baraka ni msanii ambaye ni mchapakazi na anaona mbali, tabia ambayo ni ya aina ya mwanaume ambaye anampenda, akidai kuwa ni marafiki wa karibu ambao hata kulala pamoja kwao ni kitu cha kawaida sana.

Wiki iliyopita, Baraka naye kwa upande wake alikana kuwepo kwa mahusiano ya kimapenzi na Nisha, akidai kuwa kusahau vitu vyake kwa mwigizaji huyo ikiwepo simu, ni vitu ambavyo hutokea na haimaanishi kuwa wana mahusiano.

Utafiti unaonesha kuwa, kuna hisia nzito na ukaribu mkubwa kati ya wasanii hawa wawili, kukiwa na dalili zote za mahusiano mazito ya kimapenzi, licha ya changamoto za hapa na pale, huku wasanii hawa wakikwepa kuweka wazi kinachoendelea kati yao na kuwapa mashabiki sintofahamu kwa makusudi.

Mtuhumiwa wa Mauaji ya Diwani wa CUF Muleba Apatikana..Adai Walitumwa Kumuua Kwa Sh Mil 1.5..Ataja Aliyemtuma

$
0
0
Kijana huyu anaitwa "Simon Shilage" ana umri wa miaka 22, Yeye kwa kushirikiana na mwenzie mmoja ambaye bado hajapatikana ndio waliomuua Diwani wa kata ya Kimwai huko Muleba Ndg.Faustine Muliga wa chama cha wananchi CUF.

Kijana huyu amekamatwa jioni ya jana na wananchi wa kijiji cha Kyota akijaribu kutoroka. Amekutwa na panga lenye damu alilotumia kumuua diwani Muliga. Alipohojiwa amekiri kwamba ni kweli yeye na mwenzie mmoja (hakumtaja jina) ndio waliomuua Mhe.Muliga kwa kumkata mapanga.

Amesema kazi hiyo walitumwa na aliyekua mgombea udiwani wa Kata hiyo kwa ticket ya CCM kwenye uchaguzi uliopita, ambaye alikua mpinzani wa Muliga lakini alishindwa kwenye uchaguzi.
Ameongeza kuwa Mgombea huyo aliwaahidi kiasi cha shilingi milioni 1.5 ikiwa watafanikiwa kumuua Muliga na aliwapa "advance" ya shilingi laki moja na nusu (150,000/=). Baada ya makubaliano hayo vijana hao walimvamia Muliga nyumbani kwake majira ya saa 2 usiku akiangalia "Taarifa ya Habari" ambapo walimkata mapanga maeneo mbalimbali mwilini mwake kabla ya kutokomea kusikojulikana.

Kijana huyu alikamatwa na wananchi wenye hasira kali ambao walitaka kumuua lakini akaokolewa na Polisi. Hata hivyo wananchi hao walifanikiwa kumkata sikio lake moja la kushoto kama anavyoonekana pichani.

Kwa sasa anashikiliwa kituo cha Polisi Muleba kwa upelelezi, kabla ya kupandishwa Mahakamani kujibu tuhuma za Mauaji.!

Diamond Platnumz Amwagia Sifa Mpenzi Wake Zari..Amwita Kadada Kabichi Kama Embe la Msimu

$
0
0
Picha za hivi karibuni za Zari zimezoa gumzo mitandaoni huku wengine wakisema japo ni mama wa watoto wa nne lakini bado analipa sana zaidi ya wanawake wengi ambao hata watoto hawana..Mpenzi wake nae Akapigilia Msumari kabisa kwa kuandika haya katika ukurasa wake wa Instagram;

"Diamondplatnumz; I swear i Can't get use to your Cuteness...Kadada kabichiii... kama Embe la Msimu! 🍋@zarithebosslady " 

Ushirikiano wa Zitto Kabwe na Mbowe Bungeni Waacha Maswali Mengi

$
0
0
Zitto Kabwe na Mbowe
 Kuna siri gani? Ushirikiano wa mahasimu wa kisiasa wa upinzani; Zitto Kabwe wa ACT Wazalendo (Kigoma Mjini) kwa upande mmoja na Freeman Mbowe wa Chadema (Hai) na Ukawa kwa upande mwingine kupinga uamuzi wa Serikali bungeni umevuta hisia za Watanzania na kuacha maswali iwapo ni urafiki wa mashaka au ni wa muda mfupi.

Uhusiano huo wa Zitto na viongozi mbalimbali wa Ukawa ambao umedumu kwa wiki moja sasa, umeibua maswali kama utadumu au ni kwa ajili ya kusimamia hoja zao bungeni.

Zitto na Mbowe walionekana wakitabasamu pamoja Jumanne iliyopita baada ya kukutana kutoa tamko juu ya tangazo la Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye kuzuia kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Bunge kupitia TBC1 kwa madai ya kubana matumizi ya Serikali.

Tangu Zitto afukuzwe Chadema na kujiunga na ACT- Wazalendo Machi 21, mwaka 2015 kabla ya kuanza kutengwa na viongozi hao wa Ukawa kwa siku za karibuni ameonekana kuwa karibu na umoja huo wa katiba ya wananchi.

Kwa mara ya mwisho, viongozi hao waliunganisha uhusiano wao katika sakata la Escrow mwaka jana lakini baada ya hapo waliendelea kushambuliana hususani wakati wa kampeni za uchaguzi hatua iliyowachanganya zaidi wafuasi wa mabadiliko wa vyama vya upinzani.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema, huenda Zitto amebaini kuwa akiendelea kuwa mpinzani pekee asiyekuwa ndani ya Ukawa na asiyekuwa CCM, atakuwa mpweke kisiasa na huenda akaishia kule walikoishia Augustino Mrema aliyekuwa mbunge wa Vunjo na John Cheyo (Bariadi Mashariki) waliokaa bungeni bila kushirikiana na wapinzani wenzao na sasa wameanguka.

Zitto na baadhi ya viongozi wa Chadema na Ukawa wamekuwa wakivutana mitaani na mitandaoni kwa kauli za maudhi tangu Machi 9, mwaka jana, Chadema ilipotangaza kumvua rasmi uanachama kwa madai ya kuendesha mipango ya usaliti wa chama.

Aprili mwaka jana, akiwa wilayani Kyerwa, Mbowe alinukuliwa na gazeti moja la kila siku akisema hawatamruhusu Zitto kujiunga na Ukawa.

Mbowe alitoa kauli hiyo akijibu ombi la ACT la Aprili 15, 2015 kupitia Zitto kwamba, chama hicho kilikuwa tayari kujiunga na Ukawa kama walivyotaka baadhi ya viongozi wa umoja huo akiwamo aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Katika ufafanuzi wake, Mbowe alisema hawamwamini tena Zitto kwa madai kuwa akiingia Ukawa atakuwa akivujisha siri za umoja huo kwenda CCM lakini Zitto alisema Taifa limekuwa na shauku ya ACT kushirikiana na vyama vingine kama njia ya kufanikisha malengo ya kuitoa CCM madarakani.

Vilevile Aprili mwaka jana, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Bara, John Mnyika akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, alisema Chadema haiko tayari kuikaribisha ACT-Wazalendo ndani ya Ukawa kutokana na kile alichosema ‘ni adui kwao’.

Tofauti na hali hiyo, tangu mkutano wa pili wa Bunge kuanza, wanasiasa hao wameonekana kushirikiana katika kujenga hoja dhidi ya zile za wabunge wenzao wa CCM au Serikali.



Watu 6 Watiwa Mbaroni Kufuatia Kutunguliwa helikopta Katika Ranchi ya Wanyapori ya Mwiba, Meatu

$
0
0
Watu sita wanaodaiwa kuwa majangili, wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuitungua helikopta ya doria na kusababisha kifo cha rubani wake katika pori la akiba la Maswa.

Kukamatwa kwa watu hao kumekuja siku moja baada ya Rais, John Magufuli, kutoa agizo kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuwakamatwa waliohusika na tukio hilo na kufikishwa katika mkono ya sheria.

Kauli hiyo ya Rais iliyotolewa  na  Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa,  ilisema Rais Magufuli mbali na kusikitishwa na tukio hilo, pia aliuakikisha umma kuwa serikali itahakikisha inaendeleza mapambano dhidi ya ujangili kwa nguvu zote na kuwataka wananchi na wadau mbalimbali wa hifadhi ya wanyamapori kutokatishwa tama.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Gemini Mushy, jana alithibitisha  kukamatwa kwa watu hao.

Alisema awali walikamata watu wawili, juzi watatu na jana mmoja wote wakiwa wakazi wa Simiyu na uchunguzi bado unaendelea.

Ijumaa iliyopita, watu wasiojulikana, waliitungua helikopta hiyo  wakati ikifanya doria katika pori hilo baada ya kuwapo taarifa kwamba majangili walikuwa wameua tembo mmoja.

Katika tukio hilo, rubani wa helikopta hiyo raia wa Uingereza, Rodgers Gower (37) alikufa, huku mwenzake Nicky Bester wa Afrika Kusini akinusurika.

Sakata la Bunge Kutokuonyeshwa Laivu..Mh Lazaro Nyalandu Naye Atia Neno

$
0
0
Sakata la Bunge Kutokuonyeshwa Laivu..Mh Lazaro Nyalandu Naye Atia Neno

Sasa Udaku Special Blog Ipo Play Store..Unaweza Download Kwenye Smart Phone yako Hapa

$
0
0

Good News! Sasa Blog yako ya Udaku Special Ipo Google Play Store.

Download Udaku Special Blog Android Application CLICK HERE From Play Store

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Aunt Ezekiel Afumwana na Gauni la Arusi..Yadaiwa Kafunga Ndoa Kwa Siri...

$
0
0

KUNASWA kwa msanii wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel akiwa ndani ya gauni la harusi (shela) kumezua maswali tata huku wadau wakiamini alikuwa safarini kwenda ukumbini kwa ajili ya harusi yake.

Aunt alinaswa hivi karibuni akitoka ndani ya saluni moja iitwayo Wedding  Dover, Sinza Afrikasana akitoka akiwa ndani ya shela hilo.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, baadhi ya watu waliamini Aunt alikuwa kwa ajili ya sherehe hizo kwani kuingia kwake saluni hapo mpaka kutoka akiwa amepambwa kulichukua saa moja.

AUNT EZEKIEL“Hizo picha mimi nimezipata akiwa ndani ya hoteli maarufu pale Sinza Afrikasana. Kila mtu alisema bibiye kafunga ndoa kwa siri na mzazi mwenzake, Iyobo (Moses) na harusi yake ni kwa siri,” kilisema chanzo.

Baada ya mwandishi kunasa habari hizo, alimtafuta Aunt ili aweze kuzungumzia kuhusu kuvaa gauni hilo ambapo alichenga na kusema kuwa muda utakapofika ataweka wazi kila kitu.

“Unajua kila mtu katika maisha yake na taratibu zake, sasa mimi bado sijapanga kulizungumzia hilo la kufunga ndoa ya siri mimi na Iyobo. Ila muda ukifika nitaweka wazi kila kitu. Hilo gauni lisikutishe ndugu yangu,” alisema Aunt.
Source-Global Publishers

Lubuva : Rais Magufuli Hana Mamlaka yoyote ya Kuingilia Uchaguzi wa Zanzibar Kama Watu Wanavyotaka

$
0
0

Mwenyekitu wa Tume ya Uchaguzi alikutana na Rais Magufulu jana na Amebainisha kuwa wanaosema Rais anapaswa kuingilia kati masuala ya uchaguzi iwe Tanzania bara ama Zanzibar wanafanya makosa, kwani kwa namna yoyote Rais hana mamlaka hayo na hivyo hawezi kuingilia maamuzi ya tume hizo

“Unaposikia kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano aingilie hilo suala la uchaguzi wa Zanzibar, yeye kwa kweli hana mamlaka kabisa. Pili ni kama kujikanganya, huku unasema tuwe na tume huru isiyoingiliwa halafu huku unasema aingilie kati maamuzi ya tume” alisema Jaji Lubuva.

Jaji Lubuva amesisitiza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kikatiba hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya tume ya uchaguzi ya Zanzibar na hata huku bara pia hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya tume.

Mwenyekiti huyo wa tume ya uchaguzi amewasihi watanzania kuwa uchaguzi umekwisha, na kuwaomba waungane na viongozi waliochaguliwa kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo.

Sugu Yamfika Hapaa Bungeni...Ni Kuhusu Rais Kutosafiri Nje ya Nchi

$
0
0
Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia CHADEMA Joseph Mbilinyi amemshangaa mh Rais John Magufuli kwa kitendo chake cha kutokusafiri nje ya nchi, akichangia bungeni mbunge huyo alisema haiwezekani Rais abaki amejifungia Dar badala yake anapaswa kusafiri nje ya nchi ili kwenda kujifunza kwa marais wenzie. 

Je, hii ni mwendelezo wa viongozi wa CHADEMA kubadili gia angani!?

CUF Waitaka ZEC Kuondoa Jina la Maalim Seif Kwenye Karatasi za Kura

$
0
0
Chama kikuu cha upinzani Zanzibar CUF, kimeitaka Tume ya Uchaguzi visiwani humo ZEC kuondoa na kutotumia karatasi za kupigia kura zenye kuonesha jina la mgombea wake wa urais pamoja na baraza la wawakilishi kwa lengo la kugomea uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20 visiwani humo.
Chanzo: DW Swahili

Baraza la Waislam BAKWATA Waunga Mkono Uchaguzi wa Marudio Zanzibar

$
0
0

WAKATI Chama  cha wananchi CUF ambacho ni chama kikuu cha Upinzani visiwani Zanzibar kikiwa kimesusia uchaguzi wa marudio ambao unafanyika Marchi 20 ya mwaka huu,Baraza la Waislam  (BAKWATA)  limesema marudio ya  uchaguzi huo ndo njia ya kipee ya kurudisha amani visiwani humo..

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Jijini Dar es Salaam, Sheikh Mkuu mkoani hapa,heikh alhadj Mussa Salum  amesema  Bakwata wanaunga mkono Tangazo la ZEC la kurudiwa kwa uchaguzi hu.

“Uchaguzi huu wa marudio  kwetu Bakwata tunaona ndio njia ya kipekee ya kukiweka kisiwa cha Zanzibar kuwa sehemu ya Amani na utulivu,natumia nafasi hii kuwaomba chama cha CUF kushiriki uchaguzi huu” Amesema Sheikh Salum.

Sheikh Salum ameongeza kwa kusema  kuwa hata kiongozi wa jumuiya ya Uamsho Visiwani Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmad amemwandikia barua na kumweleza kuwa kurudiwa kwa uchaguzi kutasaidia kurudisha Amani visiwani humo.

Afande Sele Aungana Na Mbunge Joseph Msukuma Kuitaka Serikali Ihalalishe Matumizi Ya Bhangi

$
0
0
Afande Sele
Msanii mkongwe wa hip hop nchini, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumizi ya bangi na si kukosoa juu ya hoja iliyotolewa na mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma.

Ikiwa imepita siku moja toka mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Msukuma (CCM), kusema haoni sababu ya serikali kuzuia bangi kuwa zao la biashara kwa maana haoni madhara yake huku akidai kwamba viroba vina madhara zaidi kuliko bangi, Afande Sele amefunguka na kusema serikali ihalalishe matumizi ya bangi na si kukosoa juu ya hoja hiyo ya Joseph Msukuma.

Afande Sele amedai kuwa kuna nchi ambazo tayari wao wamehalalisha matumizi ya bangi na kuthibitisha kuwa pombe ina madhara makubwa zaidi kuliko bangi.

"Legalize it, Don't criticize it. Korea Kaskazini, Marekani, Mexico Uruguay na mataifa mengine ya Ulaya yamethibitisha pombe ina madhara kuliko Cannabis Sativa" Amesema Afande Sele.

Hofu, Mashaka Uchaguzi wa Zanzibar

$
0
0
HOFU na mashaka vimeendelea kukomaa miongoni mwa wanataaluma pia wananchi kutokana na uamuzi wa Chama Cha Wananchi (CUF) kugoma kushiriki marudio ya uchaguzi visiwani Zanzibar.

Wakati CUF ikitangaza msimamo huo uliotokana na kikao chake cha Baraza Kuu tarehe 27 na 28 Januari mwaka huu ikiwa ni baada ya Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha kutangaza kufanyika tarehe 20 Machi mwaka, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye ni Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein amesisitiza chama chake kushiriki uchaguzi huo.

Hatua ya kutangazwa kurudiwa uchaguzi huo inaelezwa na Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavel Lwaitama kwamba ni haramu na ni uvunjifu wa sheria na kuwa hakuna kifungu cha kanuni kinaruhusu kufutwa kwa uchaguzi.

Dk. Lwaitama amesema kuwa, ZEC isijidanganye kwamba inaweza kufanya uchaguzi kwa amani bila kuwepo kwa CUF kwa kuwa nusu ya Wazanzibari ni wanachama wa chama hicho na pia CUF kuwa na wajumbe ndani ya ZEC.

“Tume iliyosimamia uchaguzi haiwezi kujikosoa yenyewe, awali Jecha alitangaza kuwa, watendaji ndio walioharibu uchaguzi, sasa je, hao watendaji wamebadilishwa? na kama wamebadilisha nani aliyefanya kazi hiyo?” amehoji Lwaitama na kuongeza;

“Wasione wananchi wapo kimya, hawawezi kujua wanafikiria nini au wamejipangaje kwani kitendo cha CUF kususia uchaguzi si kitendo kidogo. Na wala serikali isijidangaje kwa kupitia vyama vidogo, ijiulize vyama hivyo vina mchango gani ndani ya Zanzibar?”

Pia, amesema Serikali inatakiwa kutambua kwamba CUF na CCM zinauwiano , hivyo isichukulie rahisi kwamba uchaguzi utakuwa ni wa amani kwa kuwa wanavifaa vyote vya vita.
Dk. Lwaitama amesema kuwa CCM haina ubavu wa kuingia kwenye uchaguzi bila CUF, na kama wanadhania hivyo basi ni mzaha tu wanaoufanya.
Hata hivyo amesema kuwa, ameshangazwa na kitendo cha Serikali ya Tanzania Bara kuendelea kukaa kimya kuhusu Zanzibar akifananisha kitendo hicho ni sawa na Mbuni kujificha kwenye majani mafupi huku akizani haonekani kumbe anaonekana.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Benson Bana ameonesha hofu kutokana na hatua ya CUF kupuuza tangazo la ZEC la kurudia uchaguzi visiwani Zanzibar.
Bana ambaye ni Mhadhiri wa Sayansi ya Siasa na Jamii chuoni hapo ameeleza kuwa, kutoshiriki kwao kumeleta mshindo mkubwa na maswali mengi kwa viongozi wengi na kwamba “serikalia haipaswi kukaa kimya.”

“Hadi sasa bado watu wamebaki na butwaa na kutofahamu nini kinaweza kutokea baada ya CUF kutoshiriki uchaguzi,” amesema.
Wasiwasi uliooneshwa na Dk. Lwaitama pia Prof. Bana unawiana na ule wa Makame Ali Maalim ambaye ni Mkazi wa Bububu viziwani Zanzibar ambaye anasema kuwa, hali ya wasiwasi haiepukiki kwa kuwa, CUF kutoshiriki uchaguzi ni wazi kwamba hautafanyika.
“Huwezi kuingia kwenye uchaguzi hapa Zanzibar bila CUF, kama watalazimisha hivyo ni wazi hakuna atakayekubali. Haya yote yanajenga na uchaguzi uliopita na uliosifiwa na wasimamizi wa nje kwamba ulikuwa ni wa amani na haki,” ameeleza Makame.
Makame anawakilisha idadi kubwa ya Wazanzibari walio na wasiwasi kutokana na mvutano uliopo kati ya CUF na CCM ambapo anasema, kama CCM wangekuwa wameshinda basi mvutano huu usingekuwepo.

“Kinachoonekana hapa kuna wana CCM wamejazwa kiburi na wanasiasa kutoka bara, hawa ujanja wao ni msaada kutoka huko na wanapoambiwa iwe iwavyo watarudi madarakani basi hapa ndio wanajawa kiburi. Sina matumaini kama Zanzibar itabaki salama endapo uchaguzi utafanyika bila ya CUF,” amemema Makame.

Tayari wanasiasa, wanataaluma, jumuiya na wachambuzi mbalimbali wameeleza hofu kuhusu Zanzibar kutumbukia kwenye machafuko zaidi ya yale yaliyotokea mwishoni mwa mwaka 2000 chini ya uongozi wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.
Miongoni mwa walio na hofu ya vurugu ni pamoja na Jumuiya ya Maimamu Zanzibar (JUMAWAZA) kwa kushirikiana na taasisi za Kiislam Zanzibar ambao waliwataka wadau kushughulikia mgogoro wa Zanzibar kwa haraka.

Jumuiya hiyo pia imeonesha hofu ya kuwepo kwa kauli za kibaguzi, uchochezi na uhasama zinazoendelea na kumwomba Rais John Magufuli kushughulikia mgogoro jambo ambalo linaonekana kupuuzwa.

Novemba mwaka jana Asasi za Kiraia Tanzania (AZAKI) waliwataka wanasiasa visiwani humo kukaa na kutatua mgogoro wa kisiasa kwa kuwa, kutokuwepo kwa muafaka kunaweza kusababisha vurugu na hatiamye mauaji visiwani humo.

Hofu ya sintofahamu visiwani humo pia imemgusa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa katika Serikali ya Awamu ya Nne, Bernard Membe.
Membe ni miongoni mwa wanasiasa nguli waliojitokeza waziwazi na kupinga uamuzi wa kufutwa kwa matokeo yote ya uchaguzi visiwani Zanzibar akisema dunia inashangaa.
Kutokana na hali hiyo ya mashaka Zanzibar, Mwanasheria wa kujitegemea Fatma Karume amemshauri Dk. Shein kukaa pembeni ili kulinda katiba ya nchi hiyo ikiwa ndio msingi wa kuivusha Zanzibar salama.

“Dk. Shein lazima aondoke kwa kuwa kutofanya hivyo ni kuwanyang’anya Wazanzibari haku yao ya msingi,” amesema Fatma ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Aman Abeid Karume.

Source-Mwanahalisionline

Maandamano ya Vijana wa CHADEMA Kwenda Ikulu Kushinikiza TBC Ionyeshe Bunge LIVE Yapigwa Marufuku

$
0
0
Jeshi la Polisi kanda Maalumu Dar, limepiga marufuku maandamano ya Vijana wa CHADEMA kwenda Ikulu kwa lengo la kushinikiza TBC ionyeshe Bunge LIVE.

Kamanda Sirro amesema kuwa hakuna taarifa na pia hakuna uthibitisho kuwa maandamano hayo yatapokewa na Rais Magufuli.

Pia, Kamanda Sirro alieleza kuwa BAVICHA hawakuanisha barabara ambazo wanatarajia kutumia katika maandamano hayo.
 “Siku hiyo sio nzuri sana kwa sababu ni siku ambayo watu wanakuwa kazini. Ni siku ambayo wengi watataka kutumia barabara hizo kwa ajili ya huduma za kijamii. Na kwa sababu kuna option nyingine ya kuweza kupata suluhu hiyo, nisema tu kwamba maandamano hayo yamepigwa marufuku,” alisema.


Wabunge Wa CCM Waungana Na Upinzani Kuibana Serikali Kuhusu Ujenzi Wa Reli, Kuhamiashia Hela BoT Na Shirika la Ndege ATCL

$
0
0
Bungeni
Bila kujali itikadi za vyama vyao, wabunge wameukosoa mwongozo wa kuandaa mpango wa Bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha wa 2016/17, wakihoji suala la ujenzi wa reli ya kati kwa viwango vya kimataifa pamoja na mambo mbalimbali.

Pia, wamepinga mpango wa Serikali wa kutaka mapato yote ya halmashauri, taasisi na mashirika ya umma kuwekwa kwenye mfuko mkuu wa Serikali na kuitaka itafute vyanzo vipya vya mapato.

Katika kuonyesha msimamo wa pamoja, wabunge wote wanaotokea mikoa ambayo Reli ya Kati inapita wameunda umoja kuhakikisha Serikali katika mpango wake wa bajeti ya 2016/17, inakuja na mwelekeo wa ujenzi wa reli ili nchi ipate maendeleo ya kweli, si ya kwenye makabrasha.

Umoja huo uko chini ya uenyekiti wa Ezekiel Maige, mbunge wa Msalala (CCM), wakati Zitto Kabwe, ambaye ni mbunge wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo), anakuwa katibu wa wabunge hao walio katika mikoa inayoanzia Dar es Salaam kupitia Tabora hadi Mwanza na kutokea Tabora hadi Kigoma.

Mikoa mingine inayounganishwa na reli hiyo kongwe ni Shinyanga, Morogoro na Dodoma.

Akichangia mjadala kuhusu mwongozo huo, Zitto alitahadharisha dhidi ya siasa za kikanda.

“Tunapaswa kuwa makini sana kwenye siasa za kikanda. Tusikubali maslahi ya nchi nyingine yafunike maslahi ya nchi yetu. Ni lazima tuhakikishe mtandao wa reli ambao utaisaidia nchi yetu,” alisema kiongozi huyo wa chama cha ACT-Wazalendo.

“Juzi nilisikia kwamba tuna tatizo la fedha. Mwaka jana Bunge lilipitisha sheria ya Kodi ya Maendeleo ya Reli ambayo inataka kila mzigo unaoingia nchini, utozwe asilimia 1.5 kwa ajili ya reli. Tunacho chanzo cha uhakika cha fedha na tunachopaswa kufanya ni kuhakikisha kwamba chanzo hiki kinatumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa.

“Tupewe tafsiri ya Reli ya Kati. Kwetu sisi Reli ya Kati ni ile inayotoka Dar es Salaam, Tabora, Uvinza (kwenda msongati Burundi). Kutoka Kaliua kwenda Mpanda mpaka Kalema kwa ajili ya ujenzi wa Bandari ya Kalema. Kutoka Isaka kwenda Keza Ngara kwa ajili ya madini ya Nikel yaliyogundulika huko ili kusafirishwa kwenda Dar es Salaam.”

Mvutano kuhusu reli ulianza tangu wiki iliyopita katika mjadala wa hotuba ya Rais John Magufuli wakati mbunge wa Nzega Mjini (CCM), Hussein Bashe aliposema atawashawishi wenzake kuigomea bajeti ya 2016/17, iwapo Serikali haitatoa mwelekeo wa ujenzi wa reli hiyo ya kati.

Kuhusu Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Zitto alisema badala ya Serikali kukimbilia kununua ndege mbili, inapaswa kulifanyia shirika hilo marekebisho kwa kuzifanya taasisi za utalii kuwa na hisa ATCL.

“Kutokana na wingi wa watalii wanaoingia nchini, Tanapa na Ngorongoro wanapata mapato. Turuhusu wawe na hisa ATCL ili shirika hili lijiendeshe kibiashara,” alisema Zitto.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba aliungana na Zitto kumtaka Waziri wa Fedha, Dk Philip Mpango aeleze Reli ya Kati itajengwa kuanzia wapi kwenda wapi wakati atakapokuwa akiwasilisha mpango huo.

Alisema bila kuwa na reli ya uhakika ni ndoto nchi kupata maendeleo inayoyatarajia.

Serukamba alisema kuna taasisi zilizoanzishwa kwa sheria hivyo kuzitaka zianze kupeleka fedha katika mfuko mkuu wa Serikali, italazimika sheria kubadilishwa.

Mbunge huyo alihusisha suala hilo na uvivu wa watendaji wa hazina kutopenda kufikiria vyanzo vipya vya mapato.

“Mtazifanya halmashauri zishindwe kujiendesha jamani mbona hamfikirii suala hili. Waziri hii kitu si sawa kabisa iondoeni,” alisema.

“Viwango vya kodi mnavyoviweka ni vikubwa sana. Hivi (Mamlaka ya Mapato) TRA haijifunzi kwa nchi kama Mauritius ambayo viwango vyake vya kodi ni vidogo lakini inakusanya fedha nyingi?” alihoji.

Naye mbunge wa Kigamboni (CCM), Dk Faustine Ndugulile alisisitiza umuhimu wa kuwa na reli.

“Tukitaka kupaisha uchumi, lazima tuwe na Reli ya Kati ya kiwango cha kisasa. Ni lazima serikali mje na mpango wa kueleweka,” alisema akizungumzia reli hiyo ambayo ujenzi wake ulianza mwaka 1905 wakati nchi ikiwa chini ya wakoloni wa Kijerumani.

Mbunge wa viti maalum (CCM), Mwanne Nchemba alisema suala la reli ya kati si la mzaha kwa maelezo kuwa wapigakura wengi wanaitegemea reli hiyo, pia ni njia nzuri ya kusafirisha mizigo, hivyo lazima Serikali ihakikishe inaijenga kwa kiwango cha kisasa.

Kwa upande wake mbunge wa Kasulu Mjini (CCM), Daniel Nsanzugwako alisema sera ya uchumi wa viwanda ya Serikali ya Awamu ya Tano haiwezi kufanikiwa vyema bila nchi kuwa na reli ya uhakika.

“Mizigo lazima ipite katika reli ili kuokoa barabara zetu. Msipokuja na mkakati hatutawaelewa katika bunge hili. Haiwezekani miaka 20 sasa tunazungumzie reli tu,” alisema huku akisisitiza kuwa uwepo wa reli utaongeza kasi ya mapato bandarini.

Mbunge wa Babati Mjini (Chadema), Pauline Gekul naye aliungana na Serukamba kuhoji uamuzi huo wa Serikali kuweka fedha zote za mapato kwenye mfuko wa Serikali, akisema utaua halmashauri.

“Tukumbuke historia ya ugatuaji wa madaraka, kumbukeni jinsi Mwalimu (Julius)Nyerere alivyourudisha baada ya kuona faida zake. Serikali za mitaa zina mamlaka ya kukusanya mapato na kutumia, sasa hayo mamlaka mnayaondoa mnategemea nini,” alisema.

“Mkipitisha suala hili, haya mapato hayatakusanywa ipasavyo na pia mtatengeneza mianya mingine ya ajabu ajabu.Tumekuwa tukiona jinsi ambavyo Serikali inashindwa kutoa fedha za maendeleo, sasa mnapotaka fedha zote zipelekwe katika mfuko mkuu wa Serikali, je zitatoka zote wakati zitakapohitajika?” alihoji.

Gekul alisema kama tatizo ni sheria za halmashauri na taasisi, ni vyema zinakabadilishwa ila si kuziondolea mapato.

Mbunge wa Nsimbo (CCM), Richard Mbogo alizungumzia Shirika la Ndege (ATCL) akitaka lipunguze wafanyakazi wake ili kuweza kujiendesha kibiashara.

Alisema kwa sasa shirika hilo linasuasua kutokana na kutokuwa na mapato ya kutosha.

Director Adamu Juma Afunguka..Akerwa na Wanamuziki Kwenda Kufanya Video nje..

$
0
0
Kupitia instagram, Adam Juma ameandika:

Katika hizi siku za karibuni kumekua na mwaswali mengi kuhusu wasanii kufanya kazi nje ya nchi, kila napopita swali ni hilo. Je kufanya kazi njee ya nchi ni sawa au si sawa? Jibu lake si rahisi na kiukweli linahitaji fikra kwa anayelijibu kulingana na nafasi yake. Industry ya mziki ni pana sana, katika upana wake imewapa fursa vijana wengi kufanya kazi na kujikomboa kimaisha, katika video kuna vionjo vingi sana ambavyo ni ajira kwa wengi, kwa mfano dancer na mavazi nk. Jambo hili kama nilivyosema awali usipo litafakari unaweza ukajibu kikawaida tu, ili industry ikue ushirikiano huu wa fani tafauti tafuti unahitajika sana.

Nakumbuka shows zamani zilikata zikaja Dar live mwaka mzima, ghafla ikawa bills na maisha, mpaka sasa jiii hamna kitu. Mdomo ukizoe mnofu mwishowe meno hugeuka kitoweo, show sikuhizi za kutafuta na haya yote ni madhara ya pupa. Wasanii wanaofanya video nje naamini wengi wanasababu za msingi ila bila fikra hawajui kinachotokea nyumbani, leo hii hakuna sababu mtu awekeze kwenye vifaa vya music video crew zinavunjika kila siku, models imekua story ndefu na mengine mengi yanajitokeza kila siku. Kinachosikitisha nipale unaposhot video ya $10000 alafu ukirudi nyumbani unalia na mil3 alafu watu wakiingia youtube director unanyewa kama mtoto wa kambo huku wakikulinganisha na director flani. Kweli kuna vitu wametuzidi lakini ubunifu nasie km watanzania tupo, tusitengeze mazingira siku moja tuje kushindwa kufanya kazi hapa nyumbani. Kuna faida nyingi za kushot njee tusijisahau, wanaija wameshtuka GOD anajua. Regards to all

HATIMAYE..Dr Slaa Aibuka..Ajibu Tuhuma za Nyumba yao Kupigwa Mnada Kutokana Kushindwa Kulipa Mkopo wa Sh Million 300

$
0
0
Katibu Mkuu wa Zamani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa ametoa majibu kuhusu taarifa zinazoandikwa kwenye baadhi ya magazeti nchini pamoja na mitandao kuwa nyumba yake iliyoko Mbezi jijini Dar es Salaam inauzwa baada ya kushindwa kulipa mkopo wa Benki ikidaiwa kuwa mkewe aliuchukua na kumpa mwanaume mwingine.

Taarifa hizo zilieleza kuwa Mke wa Dk. Slaa, Josephine alichukua mkopo wa shilingi milioni 300 katika moja kati mabenki nchini na kushindwa kuirudisha fedha hiyo.

Dk. Slaa ambaye yuko nchini Canada akijiendeleza kimasomo, amekanusha taarifa hizo na kueleleza kuwa yeye na mkewe Josephine hawajawahi kuchukua mkopo katika benki yoyote nchini.

“Nataka nikuambie na uwajulishe Watanzania kwamba wala si mimi Dk. Slaa wala mke wangu, Josephine kwa wakati wowote ule hatujawahi kuchukua mkopo benki,” Dk. Slaa aliliambia gazeti la Mtanzania kwa njia ya simu.

“Tangu nitoke Bungeni sijawahi kuchukua hata senti moja benki, achilia mbali propaganda ya shilingi milioni 300.

" Hivyo, ni vizuri waliokupa taarifa wakupe undani ni benki ipi nilikopa au Josephine alikopa na ni shilingi ngapi na kwa nyaraka zipi. 

"Na ni vema ukafuatilia benki husika pia kama walikuwambia ni benki gani,” Mwanasiasa huyo mkongwe alieleza.

Dk. Slaa ambaye alitangaza mwaka jana kustaafu siasa, alisema kuwa anapanga kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wote walioandika habari hizo.

TFF yampongeza Kikwete Kwa Kuteuliwa na CAF

$
0
0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanznaia (TFF), Jamal Malinzi amempongeza Rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa kukubali uteuzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF) na GAVI utakaomfanya kuwa bingwa wa chanjo na balozi wa mradi wa Africa United Duniani.

“Familia ya mpira wa miguu inajua umuhimu wa chanjo na hasa katika maendeleo ya vipaji na wanamichezo kwa ujumla na jinisi chanjo inavyoweza kuwapa watoto siyo tu fursa ya maendeleo bali pia haki ya kuishi” ilisema sehemu ya barua hiyo iliyosainiwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.
Katika barua hiyo, Malinzi ameelezea furaha ya TFF kuona kiongozi wa Tanzania akiongoza mapambano ya kuokoa afya na uhai wa kizazi cha sasa na kijacho katika Afrika na dunia kwa ujumla.

“TFF itaunga mkono juhudi zako ili kufanikisha malengo yaliyowekwa na ushirika wa chanjo” ilimalizia barua hiyo ambayo nakala yake imetumwa kwa Rais wa CAF, Issa Hayatou.

Bungeni...Halima Mdee Adai Chama cha Mapinduzi Kimechoka....

$
0
0
Wakati Bunge lilipokuwa likipamba moto kwa mabishano hapo jana, Mbunge wa Kawe Halima Mdee (CHADEMA) alisikika akisema kuwa Chama Cha Mapinduzi CCM kimechoka.

Je unakubaliana na kauli hii ya Halima?
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images