Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live

Mwimbaji Mavoko Atoa ya Moyoni Kuhusu Watu Wanao Mtukana...

$
0
0
Rich Mavoko amesema ni rahisi sana kwa watu walio nje ya muziki kuanza kuongea maneno pasipo kujua ni mambo gani ambayo wao kama wasanii wanakutana nayo kuhusiana na muziki huo na tasnia nzima ya muziki, anadai anatamani wangejua ni kiasi gani wanakosa raha na kukosa usingizi sababu ya hizo kazi.

"Ukiwa nje inawezekana unaweza ona mchezo ni rahisi ila ukiwa ndani ya mchezo utajua ugumu wake kiukweli hatulali kwa ajili ya hii kitu, natamani hata wewe unaye tukanaga watu ungejua ugumu wa izi mambo ungeishia kuachia mdomo wazi sisi ni kati ya watu tunaosakamwa lakini bado tunajali uwepo wenu na kuwategemea, ningependa kusema haya ni maisha ya kioo ila baada ya hapa uzee hivyo lazima tulijue hilo... #tusidharuliane" Alisema Rich Mavoko

Breaking News..Rachel Mashishanga, Christowaja Mtinda wahama CHADEMA na kujiunga CCM

$
0
0
Leo mjini Singida katika kuadhimisha miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM, maazimisho hayo yanayofanyika mjini Singida pia yameambatana na tukio kubwa la kuwapokea waliopata kuwa wabunge wa CHADEMA ambao ni Bi Rachael Mashishanga na Christowaja Mtinda

Ni Nani Aliyekutuma Kuoa Mwanamke Flat Screen?

$
0
0
Naongea na wanaume wenzangu wale walio owa wanawake wenye makalio madogo halafu wakiona wa wenzao wenye makalio makubwa wanaanza kupiga mikelele.

Utakuta uko na mkeo matembezini uku kafungashia kidogo basi mijanaume isiyokuwa na akili inaanza kupiga mayowe oh wakubwa wanafaidi ohh marshallah.

Kwanini na wewe usioe au kutafuta mwanamke mwenye makalio na ukaacha kutamani vya wenzao. Kwanza unamkosea adabu mwanaume mwenzio kupiga miyowe utadhani umeona utupu wa mzazi wako.

Acheni ujinga tuacheni tuenjoy na wake zetu maana hatukuwatuma kuoa flat screen.

By Nitonye

Mwenyekiti wa CCM Jakaya Kikwete Asema CCM Ilisikitishwa Sana na Uamuzi wa ZEC Kufuta Uchaguzi Zanzibar

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza rasmi kuachia kiti hicho kabla ya mwezi Februari mwakani, huku akisema CCM imesikitishwa na uamuzi wa ZEC kufuta uchaguzi wa Zanzibar.

Dkt Kikwete ambaye pia ni Rais wa awamu ya nne wa serikali ya Jamhuri ya Tanzania, ametoa tamko hilo leo katika sherehe za miaka 39 ya chama hicho zilizofanyika katika uwanja wa Namfua mjini Singida, ambapo yeye ndiye aliyekuwa mgeni Rasmi.

Katika hotuba yake, Dkt Kikwete amewaeleza wana CCM waliofurika kiwanjani hapo kuwa hizo ndizo zitakuwa sherehe zake za mwisho kwake kuhudhuria huku akiwa mwenyekiti, kwa kuwa katika sherehe zijazo mwenyekiti wa chama hicho atakuwa ni Rais John Magufuli.

"Hii ni mara yangu ya mwisho kuhudhuria sherehe hizi kama mwenyekiti wenu, Katika sherehe za mwakani, mwenyekiti wenu atakuwa ni Rais John Magufuli"

Chama hicho kinataraji kufanya maadhimisho yake ya miaka 40 ya kuzaliwa kwake mwezi Februari mwaka 2017 mwaka ambao pia ni wa uchaguzi mkuu wa chama hicho kwa mujibu wa katiba yao.

Kuhusu Uchaguzi mkuu wa Zanzibar, Kikwete amesema wao kama CCM hawakupenda uchaguzi huo urudiwe kwa kuwa walikuwa wana uhakika wa ushindi, na tayari walikuwa wanajiandaa kusherehekea ushindi mnono, lakini wanalazimika kukubaliana na maamuzi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kwa kuwa hawana namna nyingine.

“Tulikuwa tumejiandaa kushangilia, lakini Tume wakasema kuwa uchaguzi unafutwa kwa kuwa kulikuwa na dosari kubwa, tukasikitika sana lakini kwa kuwa tume wameamua, tukashauriana na wenzetu wa Zanzibar, tukaona ni bora kukubali kurudia uchaguzi huo, lakini hatukupenda”

Amewataka wana CCM wote visiwani Zanzibar kujiandaa na uchaguzi siku ya Machi 20, mwaka huu na kwamba wahakikishe wanatunza shahada zao kwa ajili ya kuchagua wagombea wa CCM.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete ametumia nafasi hiyo kuelezea mafanikio ya chama hicho katika kuwaletea watanzania maendeleo ambapo amesema katika miaka yake 39, chama hicho kimefanikisha mengi ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu ya barabara.

Pia amezungumzia mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ambapo licha ya kukiri kuwa chama hicho kilikuwa kwenye wakati mgumu, amesema bado kiko imara, na kitaendelea kuwa imara.

Amesema licha ya baadhi ya watu kukitabiria kifo chama hicho, watanzania bado wameendelea kukiamini na kukipa ushindi wa kishindo huku akitolea mfano ushindi ambao chama hicho kimeupata katika ngazi ya urais, udiwani, na ubunge mwaka 2015.

“Katika ubunge sisi tumepata asilimia 73 ya viti vyote vya ubunge wa majimbo, na hata katika udiwani tumeshinda asilimia zaidi ya 73 katika kata zote, nashangaa kuna watu wanadai kwamba eti CCM haipendwi, yaani hata hesabu zinawashinda..” Amesema Kikwete.

Akizungumzia utendaji kazi wa serikali ya awamu ya tano, Dkt Kikwete amempongeza Rais Magufuli kwa kufanya yale aliyotumwa katika Ilani ya CCM na kuahidi kumpa ushirikiano ili ayafanikishe yote yaliyomo katika ilani hiyo.

Amewakosoa watu wanaodai kuwa Magufuli hatekelezi Ilani ya CCM bali ya vyama vingine na kusisitiza kuwa kila jambo linalofanywa na serikali hiyo limo ndano ya ilani ya CCM.

Kikwete ametolea mfano suala la kuanzishwa kwa mahakama maalum ya kushughulikia rushwa na wahujumu uchumi na kusema kuwa suala hilo limo ndani ya ilani ya CCM, na wala sio jambo la kuzuka.

Amesema wanaodai Magufuli anatekeleza sera zao wameishiwa na hawana la kuzungumza tena.

"Watani zetu wanasema anatekeleza mambo yao, wamekosa ya kusema wanasubiri akija bungeni watoke, watu wazima hovyooo"

Pia amewataka wanachama wa CCM kuchagua viongozi bora na watakaoweza kukijenga upya chama hicho katika uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika mwakani , huku akiwataka wajiandae kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

“Mwisho wa uchaguzi mmoja ni mwanzo wa uchaguzi ujao, tumemaliza wa mwaka 2015 tuanze kujiandaa na uchaguzi wa 2020”

Diamond Ajisifia Baada ya Familia yake Kupata Deal la Vodacom..."Mimi, Tiffah na Zari ni Brand"

$
0
0

Familia ya Diamond Platnumz yote ni brand, kwa mujibu wake mwenyewe.
Yuko sahihi kwasababu si yeye tu anayenufaika na ubalozi wa mabilioni ya shilingi wa Vodacom Tanzania. Mchumba wake Zari, mtoto wao Tiffah na mama yake Sandra, wote wamepiga mpunga kutokana na ubalozi huo unaoshuhudia familia nzima ikishiriki kwenye tangazo la promotion mpya ya mtandao huo, Ongea Deilee.

Ni mtu mmoja tu muhimu aliyekosekana – Abdul, baba yake Diamond ambaye kwa wengi anaonekana kuwa ‘mcharuko’ kiaina kiasi cha mwanae kutopenda kujihusisha naye. Bila shaka itamchukua miaka mingi Diamond kumtengeneza naye kuwa brand.

“The Most Powerful and Impactful Family in Africa!!!… Bibi Brand, Baba Brand, Mama Brand Mtoto ndio Usiseme!!…. thanks for the Big Love our People… and get ready for another Big Thing,” ameandika Diamond kwenye Instagram.
Kweli hela huenda kwa wenye nazo tayari!

Baba yake Diamond: Nililia Sana Kutoalikwa Kwenye Arobaini ya Tiffah

$
0
0

Baba wa staa wa muziki Diamond Platnumz, Abdul Juma amesema hakuna siku alilia kwa uchungu kama siku ambayo mjukuu wake Tiffah alifanyiwa sherehe ya arobaini bila yeye kualikwa.

Akizungumza katika kipindi cha The Weekend Chat Show cha Clouds TV Jumamosi hii, Mzee Abdul alidai licha ya kuwa anawasiliana mara kwa mara na mama yake Diamond, lakini hakuwai kupewa taarifa yoyote kuhusu tukio hilo mpaka alivyoona picha kwenye magazeti.

“Hakuna kitu kiliniuma kama kufanyiwa shughuli kwa yule dogo bila kualikwa.” Alisema Mzee Abdul.

“Yaani nakumbuka nilipigiwa simu nikaambiwa baba mwanao amepata mtoto lakini sio siku ya arobaini, niliumia sana, nililia, nililia sana kutoalikwa kwenye arobaini. Mimi nachoomba (Mama Diamond) asinisahau, kuna kazi nilifanya mpaka akawa hapo,” aliongeza.

Katika hatua nyingine mzee huyo amemtaka Diamond kufanya kazi kwa bidii.

“Mimi nampenda sana, kama kuna baya niliwatendea wanisamehe, mzazi akosehi, pia aendelee kujituma zaidi,” alisema Mzee Abdul

Hatimaye Nuhu Mziwanda Akubali Yaishe Kwa Shilole..Atangaza Kufuta Tattoo ya Shishi Aliyoichora Mkononi

$
0
0

Msanii wa muziki Nuh Mziwanda, hatimaye ameamua na yeye kufuta tatoo ya Shilole aliyokuwa ameichora mkononi, akienda tofauti na nadhiri aliyojiwekea ya kwenda kaburini na tatoo hiyo.

Nuh amesema kuwa, ameamua kufanya hivyo alipogundua tabia halisi za Shilole baada ya kuachana naye, akidai kuwa ex wake huyo ameingilia ukurasa wake wa instagram (hacking), akimtukana katika mahojiano mbalimbali, kitu ambacho kimemfanya kugundua kuwa msanii huyo alikua si rafiki yake.

Nuh mbali na kuchora tatoo mpya juu ya ile ya Shishi Baby, ameongeza tatoo nyingine kadhaa mwilini kwake, ikiwepo usoni kama ambavyo inaonekana katika picha.

posted from Bloggeroid

Zitto Aanza Vita ya Wazi Dhidi ya Rais Magufuli

$
0
0

Sasa ni wazi kuwa Zitto kaanza rasmi kumshambulia Rais Magufuli, ukiangalia trend ya tweet zake za hivi karibuni ameaonekana kukosoa juhudi za Rais Magufuli tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma kidogo.

Mfano wa tweet zake na zingine ameaonekana kucopy kwa JK:

"@JrMalcolm88 @MariaSTsehai @Mkandara Rais ana historia ya kuingiza Taifa hasara. Mmesahau Meli ya Samaki? Mmesahau petrol station Mwanza?"

17m17 minutes ago
Zitto Kabwe Ruyagwa ‏@zittokabwe
@MariaSTsehai @jmkikwete Rais anasema watu ready handed wafungwe hapohapo? Hamjui nyie kuna watu hubambikiwa kesi mitaani? Tuwe makini sana

Mgonjwa wa Akili Aua Mganga Wake Kwa Jembe

$
0
0

Mganga wa jadi wa Kijiji cha Ididi, Kata ya Nyamilangano wilayani Kahama, Jilumba Mabula (70) ameuawa kwa kupigwa na jembe shavuni akiwa kwenye harakati za kumnywesha dawa mteja wake anayedaiwa kuwa mgonjwa wa akili.

Tukio hilo lilitokea juzi, nyumbani kwa mganga huyo wakati akijaribu kumpa dawa mgonjwa huyo aliyepelekwa kutibiwa ugonjwa huo akitokea Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Mika Nyange alisema baada ya mgonjwa huyo kugoma kunywa dawa, mganga huyo kwa kushirikiana na watu wengine walimshika kwa nguvu na kumwangusha chini, kisha kuanza kumnywesha kwa nguvu.

“Unajua mgonjwa wa akili anapogoma kunywa dawa huwa anashikwa kwa nguvu nyingi na kuanza kumbana mdomo ili ameze. Ndivyo ilivyofanyika kwa mgonjwa huyo ambaye alikuwa amegoma akidai wanampa dawa ya nini wakati haumwi,” alisema.

Nyange alisema mgonjwa huyo alifanikiwa kuwaponyoka na pembeni kulikuwa na jembe ambalo alilichukua na kumpiga nalo mganga huyo shavuni, hivyo kumvunja taya la kulia, hali iliyosababisha kifo chake papo hapo.

Kamanda huyo alisema wanamshikilia mtuhumiwa huyo na yuko mahabusu maalumu ya wagonjwa wa akili na kwamba, anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Baadhi ya wananchi wa Kata ya Nyamilangano, akiwamo Joseph Maziku walisikitishwa na kifo cha mganga huyo wakisema ni pigo kwa wananchi wengi kwa kuwa alikuwa msaada katika eneo hilo.

Maziku alisema hata yeye alifika kutibiwa kwa mganga huyo akitokea wilayani Kwimba mkoani Mwanza.

“Imeniumiza sana kwa kweli, maana huyu mzee alikuwa akitusaidia watu wengi katika eneo hili na baadhi ya watu walikuwa wanatoka mbali kuja huku kufuata huduma zake,” alisema.

Magreth Nkera alisema mgonjwa huyo hastahili kushitakiwa kwa kuwa anaumwa.

“Naamini kwamba asingekuwa mgonjwa asingeua,” alisema

Mamluki Waliobaki Ndani ya CCM Siku zao Zinahesabika..Jakaya Kikwete Aagiza Waanze Kushughulikiwa

$
0
0

MAMLUKI waliobaki ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), siku zao zinahesabika, baada ya Mwenyekiti wa chama hicho, Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete, kumuagiza Makamu Mwenyekiti, Tanzania Bara, Philip Mangula kuanza kuwashughulikia.

Akizungumza kwenye maadhimisho ya 39 ya kuzaliwa kwa chama hicho yaliyofanyika jana katika Uwanja wa Namfua, mkoani Singida, Kikwete alisema chama hicho kimevuka salama katika Uchaguzi Mkuu uliopita wa Oktoba mwaka jana, pamoja na baadhi ya wenzao kuondoka.

“Tunashukuru uchaguzi ulipita na Chama kimevuka salama katika mchakato mzito kinyume na watu walivyotutabiria kifo… haukuwa rahisi kwetu kwa sababu ulizidiwa na kelele na vitisho pamoja na kuwepo wenzetu waliotuhama na kudhani tutakufa lakini hatukutetereka.

“Tunajua wako wengine waliobaki kama mamluki, lakini wajue siku zao zinahesabika maana hatutakubali kuendelea kunyonywa damu, natumaini Mangula umeanza kuwashughulikia hawa mamluki,” alisema Mwenyekiti huyo anayemaliza muda wake.

Mama Diamond Platnumz Amsindikiza Zari Hassan Nairobi..Hizi Hap Picha Akifurahia Maisha

$
0
0

Mama Diamond Platnumz Amsindikiza Zari Hassan Nairobi..Hizi Hap Picha Akifurahia Maisha



Akiwa Salon

Mengine Yaibuka Taarifa ya Kocha Jose Mourinho Kujiunga Manchester United

$
0
0

Timu ya Manchester United imekataa kusema lolote juu ya madai kuwa ilifanya mashauriano na wawakilishi wa kocha mzoefu Jose Mourinho, aliyeachishwa kazi kutoka Chelsea Disemba, mwaka jana.

Habari za kuaminika hata hivyo zinasema kuwa mashauriano yamefanywa na Mourinho – ambaye ametajwa kama mmoja wapo wa makocha wanaowania kazi katika timu ya Manchester United ambayo imetapatapa kwa muda na ambayo kocha wake wa sasa, Lous Van Gaal, anatarajiwa kuondoka baadaye mwakani.

Hatua hiyo itampa fursa Mourinho ambaye anadaiwa kufurahia mapngo huo wakuifunza Manchester United.

Maafisa wa juu wa Man United wanatarajiwa kutoa jibu lao baada ya majirani zao Manchester City kuchukua huduma za Pep Guradiola ,mapema wiki hii.

Kuwasili kwa Mourinho kunamaanisha kwamba upinzani mkali utaanza kati ya City na United kufuatia ule uliokuwepo kati ya Real Madrid na Barcelona wakati makocha hao walipokuwa katika timu hizo mbili.

Katika kipindi cha wiki mbili kazi ya Van Gaal imekuwa ikiyumba yumba.

Hatahivyo,kushindwa kwa timu hiyo dhidi ya Stoke na Southampton kumesababisha kuimarika kwa timu hiyo.

United ambao wako pointi tano nyuma katika nafasi ya kufuzu kwa michuano ya kilabu bingwa Ulaya itacheza dhidi ya Chelsea siku ya jumapili.

Diamond platnumz na Qeen Darling Baba ni Baba tu, Baba Yenu Kawaomba Msamaha Msameheni Kabla Hamjachelewa

$
0
0

Nimeona interview ya Clouds TV na Mzee Platnumz, kweli jamaa kachoka. Huyu ni Baba yake na mwanamuziki matata nchini Diamond Platnumz.
Kama alikukosea wewe na mama yako, mbona ameshasema mumsamehe? Bila ya yeye Diamond asingekuwa alivyo sasa. Hivyo inatakiwa Diamond awe na moyo mkubwa wa kusamehe mtu ambaye ameshaomba kusamehewa. Binadamu tuna mapungufu na ni ujasiri ulioje kukubali kuwa umekosa na kuomba kusamehewa.

Diamond ni kioo cha jamii, uwe na moyo wa kusamehe. Pia kwa Queen Darlin, Baba yenu kawaomba msamaha wote.
Msaidieni Baba Yenu ana Hali Mbaya

Dr. Slaa na Mpenzi Wake Kufunga Ndoa Nchini Canada

$
0
0

Aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA Dr. Wilbroad Slaa na Josephine Mushumbusi kubariki ndoa nchini Canada kabla ya sikukuu ya Pasaka itakayoadhimishwa mwishoni mwa mwezi wa tatu.

Sherehe za Miaka 39 ya CCM: Rais Magufuli Atuma Salamu Kwa Watendaji Wavivu Serikalini.

$
0
0

Rais John Magufuli amewataka watendaji wote wa serikali kuhakikisha kuwa wanatekeleza ipasavyo matakwa ya ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndicho kinachoongoza nchi kwa sasa.


Magufuli ametoa agizo hilo leo kwenye sherehe za miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi zilizofanyika katika uwanja wa Namfua mjini Singida.


Rais Magufuli ambaye alikuwa ni miongoni viongozi wakuu wa serikali waliohudhuria sherehe hizo akiambatana na makamu wake Samiah Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema yeye na serikali yake wamejipanga kutekeleza kikamilifu ilani ya CCM na kwamba hawezi kukiangusha chama hicho.


Akitoa salam zake katika sherehe hizo, Magufuli ametumia muda usiozidi dakika 10 kueleza mambo ambayo tayari serikali yake imeanza kuyafanya na ambayo itaendelea kuyafanya ikiwa ni pamoja na "kutumbua majipu" kwa ustawi wa maisha ya watanzania wote bila kujali vyama vyao.


Ametumia nafasi hiyo kuwaagiza wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya pamoja na watendaji wote serikalini kufanya kazi kwa nguvu, uadilifu na uzalendo ili kuwaletea watanzania maendeleo, na kwamba atakayeona hawezi atamuweka pembeni ili wengine wafanye kazi.


“Nawaeleza watendaji wote serikalini kuwa atakayeshindwa kufanya kazi, nitamueleza kwa upole sana maana mimi ni mtu mpole, nitamuambia akae pembeni apishe wengine”


Rais Magufuli pia ameupongeza uongozi wa CCM mkoa wa Singida kwa kuchangia madawati 1000 kwa shule za Singida na kuwaagiza wakuu wote wa mikoa na wilaya kuhakikisha wanafunzi hawakai chini.


“Mh mwenyekiti inasikitisha sana kuona sisi tunajifungia kwenye maofisi makubwa yenye viyoyozi, na maviti ya kuzunguka lakini tukitoka tu nje tunakuta wanafunzi wamekaa chini kwenye mavumbi, sasa nawaagiza wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa hakikisheni wanafunzi hawakai chini”


Rais Magufuli pia ametumia nafasi hiyo kukishukuru Chama cha Mapinduzi kufanikisha yeye kuwa Rais kwa kuwa bila chama hicho yeye asingekuwa Rais.


“Nataka watanzania wote wajue kuwa bila CCM mimi nisingekuwa Rais wao, kwa hiyo huwezi kunitenganisha mimi na CCM, ndiyo maana leo nimekuja nimevaa kijani yangu hapa”


Pia amesema haoni kama kuna chama kingine chochote kitakachokuja kutawala Tanzania zaidi ya CCM


"Nataka ifikie hatua watanzanie wote wasiwaze wala kuota vyama vingine, tutafanya yale ambayo wao wanataka kuyafanya, ... Hakuna mtawala anayetaka kutawaliwa, tena kwa bahati mbaya atawaliwe na vyama vya hovyohovyo, CCM itaendelea kutawala"

Mbowe Afunguka Sababu Zilizopelekea Zitto Kabwe Kutochaguliwa Baraza la Mawaziri Kivuli

$
0
0

Maswali mengi yameibuka hivi karibuni baada ya wadau mbalimbali wa masuala ya siasa kutolisikia jina la mbunge wa kigoma mjini Zitto Kabwe kwa tiketi ya ACT katika Baraza Kivuli la Mawaziri

Mbowe ametoa Ufafanuzi kwanini Zitto Hakuchaguliwa Kama ifuatavyo:

“Ukawa tulisaini tamko la pamoja la ushirikiano na hiyo ilikuwa katika Bunge la Katiba. Kumbuka tumeshirikiana katika Uchaguzi Mkuu na kupata madiwani na wabunge ambao ndiyo hawa wamezaa baraza hili, Ushirikiano wetu upo katika halmashauri na majiji. Kutokana na jambo hilo huwezi kuiingiza ACT maana haikuwapo katika makubaliano ya Ukawa,”


Hata hivyo, baada ya Mbowe kutangaza baraza hilo kivuli, Zitto aliwapongeza na kuahidi kushirikiana nao.

Maalim Seif Afunguka Mazito Atoa Siri na Kusema Dr Shein Amemzunguka

$
0
0

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema katika vikao vya kutafuta ufumbuzi wa mkwamo wa kisiasa Zanzibar, walivyofanya na Rais Ali Mohamed Shein, walikubaliana kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) haifai tena kusimamia uchaguzi na kujadiliana kuhusu namna ya kupata tume nyingine inayoweza kufanya kazi hiyo.

Hivyo, ameelezea kushangazwa na kitendo cha Serikali ya CCM kuukubali uamuzi aliouita batili wa ZEC kutaka kufanya uchaguzi wa marudio.

Akizungumza na viongozi wa CUF Mkoa wa Dar es Salaam katika ofisi za chama hicho Buguruni, Maalim Seif alisema hatua hiyo imedhihirisha kuwa viongozi hao hawakuwa na nia njema kwenye mazungumzo hayo yaliyofanyika mara tisa na baadaye kuvunjika bila mwafaka.

Maalim Seif alitoa kauli hiyo katika mfululizo wa vikao vyake na viongozi wa chama hicho ngazi ya wilaya na majimbo, yenye lengo la kuwaeleza kuhusu uamuzi uliofanywa na Baraza Kuu la Uongozi la CUF wa kutoshiriki uchaguzi wa marudio.

Alisisitiza kuwa kitendo cha kufuta uchaguzi uliokamilika na kutangaza tarehe nyingine ya marudio ni batili na kwamba hakuna msingi wowote wa kutangaza kurudiwa.

Alisema waangalizi wote wa uchaguzi wa ndani na nje ya nchi waliridhishwa na uchaguzi huo kwamba ulifanyika kwa amani, ulikuwa huru na haki na kwamba ana matumaini kuwa wataendelea na msimamo wao huo hadi haki ya wananchi wa Zanzibar itakapopatikana.

“Msimamo wa CUF ni kwamba hakitambui kufutwa kwa uchaguzi na kurejea wito wake kwa Tume ya Uchaguzi kukamilisha mchakato wa kujumlisha kura kwa majimbo yaliyobakia na hatimaye kumtangaza mshindi wa uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, 2015.

Maalim Seif alisema, CCM na viongozi wake wamepoteza dira baada ya kutoungwa mkono na jumuiya ya kimataifa kutokana na kubakwa kwa demokrasia Tanzania na hasa Zanzibar.

Alisema kauli ya Serikali ya kutaka mabalozi wa nchini za nje na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa wasizungumze na viongozi wa vyama vya upinzani isipokuwa kwa ruhusa ya Wizara ya Mambo ya Nje ni kitendo cha aibu.

Amshukia Jaji Lubuva
Maalim Seif alimshutumu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kwa kuunga mkono “hoja dhaifu ya ZEC” ya kutaka kurudiwa kwa uchaguzi wa Zanzibar.

Alisema Jaji Lubuva kama anaweza kutenda haki asingekubali matokeo ya urais na wabunge kwa upande wa Zanzibar, kwa vile uchaguzi huo ulifanyika sanjari na ule wa Zanzibar kwa kuwashirikisha wapigakura haohao, daftari hilohilo na vituo vilevile vya kupigia kura.

Akijibu madai hayo, Jaji Lubuva alisema: “Huyu Maalim na (Edward) Lowassa wanataka kutuchanganya, wasimamizi hawakuona dosari katika uchaguzi wa Tanzania Bara, licha ya kwamba kura zilipigwa katika chumba kimoja.”

Aliongeza: “Maalim namheshimu, sipendi kubishana naye, uchaguzi umekwisha, kinachofuata ni watu kufanya kazi ili watu waone matokeo yake mbeleni na kutoa hukumu.” Alisisitiza kuwa Rais Magufuli hawezi kuiingilia ZEC, bali anaweza kuiingilia Zanzibar kama kutakuwa na machafuko kwa kuwa ni Amiri Jeshi Mkuu.

Alisema ni lazima CCM ikubaliane na misingi ya demokrasia ya vyama vingi na kama haiwezi ni bora kurejesha mfumo wa chama kimoja.

Gari la Mafuta Laanguka na Kulipuka Moto Mkoani Dodoma

$
0
0

Ripoti kutoka Dodoma leo asubuhi ni hii ya ajali ya gari la mafuta lililodondoka na kulipuka katika eneo la Kibaigwa ambapo hazikupatikana taarifa rasmi kuhusu ajali yenyewe kwenye upande wa Majeruhi au vifo 

Kimenuka Tena Uchaguzi Zanzibar..Chama Kingine Chajitoa Uchaguzi wa Marudio

$
0
0

Chama cha APPT Maendeleo, kimetangaza rasimi kwamba hakitashiriki Uchaguzi Mkuu wa marudio kutokana na kupoteza imani na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), baada ya kufuta kibabe matokeo ya

uchaguzi wa Oktoba 25 mwaka jana.

Msimamo wa APPT ulitolewa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Peter Kuga Mziray katika barua yake kwa  (ZEC), ambayo nakala yake ilisambazwa kwa vyombo vya habari Zanzibar.

APPT kinakuwa chama cha pili kutangaza kutoshiriki uchaguzi huo wa Machi 20 baada ya Chama kikuu cha upinzani Zanzibar, CUF kutoa tamko lake kama hilo mwezi uliopita.

Mziray alisema njia iliyotumiwa na Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha kufuta matokeo ya uchaguzi haikuwa ya kisheria hivyo APPT Maendeleo haitambui kufutwa kwa uchaguzi huo.

Mbwana Samatta Acheza Kwa Mara ya Kwanza Kwenye Team Mpya Genk...Washinda 1

$
0
0

Jana Mbwana Samatta alipata nafasi ya kucheza kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha kwanza cha KRC Genk ambayo inashiriki ligi kuu ya Ubelgiji iliyomsajili hivi karibuni kutoka klabu ya TP Mazembe ya DR Congo.

Nahodha huyo mpya wa Stars aliingia uwanjani dakika ya 73 kipindi cha pili wakati timu yake tayari ikiwa inaongoza kwa bao 1-0 kwenye mchezo wa ligi ya nchini humo.

Genk itashuka dimbani Jumamosi ijayo February 13, dhidi ya Waasland kwenye uwanja wa Cristal Arena ambao ndiyo uwanja wa nyumbani wa Genk. Mechi hiyo itachezwa saa 4:30 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Viewing all 104670 articles
Browse latest View live




Latest Images