Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Picha za Mwanamuziki Shilole Akiwa Mapumzikoni Ufaransa

$
0
0






Picha za Mwanamuziki Shilole Akiwa Mapumzikoni Ufaransa

Makamishna Wawili Kati Ya Sita Wa Tume Ya Uchaguzi Zanzibar Wamepinga Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar

$
0
0
Wakati wadau mbalimbali wa masuala ya kisiasa wakipinga kile kinachoendelea Zanzibar, nao makamishna wawili wa tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Nassor Khamis Mohamed na Ayoub Hamad wameibuka na kupinga uchaguzi huo wa marudio.


Wakizungumza na wandishi wa habari mjini Dar es salaam leo, makamishna hao wamesema kuwa sababu kubwa ya kupinga kufanyika kwa uchaguzi huo ni kutokana na kuvurugwa kwa katiba ya zanzibar tangu tukio la kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa oktoba 25, mwaka jana.


Makamishna hao wa ZEC, wakizungumza kwa hisia na kujiamini, wamesema kuwa mwenyekiti wa tume hiyo, Jecha Salim Jeche hakuwa na mamlaka ya kisheria kufuta uchaguzi huo bila kuwashirikisha makamishna wa tume hiyo.


Tayari, Jecha ametangaza kuwa uchaguzi wa marudio utafanyika siku ya Jumapili, Machi 20, mwaka huu. Lakini wajumbe hao wa ZEC, kwa pamoja wamesema wanapinga kufanyika kwa uchaguzi huo kutokana na ukiukwaji wa katiba:


“Tunapinga marudio ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi wa Machi. Uchaguzi huo si halali kulingana na matukio yaliyotokea tangu kufanyika kwa uchaguzi halali wa Oktoba 25, mwaka jana,” walisema makamishna hao wanaowakilisha CUF ndani ya ZEC.


Wamesema kuwa sababu nyingine inayowafanya kupinga uchaguzi wa marudio ni kutokana na kukamilika kwa uchaguzi wa mwaka jana ambapo uchaguzi huo ulikuwa umekamilika na baadhi ya washindi wa viti vya uwakilishi na udiwani walishakabidhiwa vyeti vyao.


Wamesema kurudiwa kwa uchaguzi huo ambao unatarajiwa kutumia zaidi ya shilingi billion saba hadi kukamilika kwake ni matumizi mabaya ya fedha za wananchi, kwani uchaguzi Zanzibar ulishafanyika na kinachoendelea ni mbinu za kuubatilisha.


Wamesema kuwa tukio la kufutwa kwa uchaguzi huo lilitanguliwa na matukio kadhaa ambayo yalionyesha wazi kuwa kuna kikundi cha watu ambacho kinamshauri Jecha, na sio maamuzi ya tume yote nzima.


“Tarehe 26 october mwaka jana CCM walileta barua ya malalamiko na kumtaka mwenyekiti na tume kufuta uchaguzi huo wakati tayari tulishaanza kutoa vyeti kwa washindi.


“Baada ya hapo mwenyekiti aliitisha kikao cha tume na tuliamua kwa pamoja kuwa maombi ya CCM hayakuwa na mashiko hivyo mchakato uliendelea.” amesema Nassor Khamis mmoja wa makamishna wa tume hiyo.


Amesema kwamba baada ya maamuzi hayo ya tume, ndipo siku iliyofuata Jecha (Mwenyekiti wa Tume), hakufika katika ujumuishaji wa matokeo kwa siku nzima na baadaye walisikia tu kuwa ametangaza kufuta uchaguzi bila kuwashirikisha wajumbe wengine wa tume.


Nassor amesema: “Baada ya hapo ndipo ofisi yetu ilianza kuzungukwa na wanajeshi na kuamuriwa tusifanye lolote huku Jaji wa mahakama kuu ya Zanzibar, naye akiwa amekamatwa na kupelekwa polisi.”


Wajumbe hao, wamesema kwa matukio kama hayo wanaamini kuwa tume hiyo imeacha kufanya kazi zake kisheria na sasa inafanya kazi kisiasa, jambo ambalo linampotezea sifa mwenyekiti wake kuendelea kuiongoza tume hiyo.


Aidha, wamesema kuwa hali iliyopo ndani ya tume kwa sasa sio hali ya kawaidia kuweza kusimamia uchaguzi wa haki kutokana na wajumbe wake kupingana hovyo hovyo:


“Wajumbe wamekuwa wakipingana kwa kila hoja inayoletwa…jambo ambalo linafanya uchaguzi wa marudio kutiliwa mashaka na wajumbe wengi wa tume hiyo,” amesema wajumbe hao.


Makamishna hao wamesema kuwa wametoa wito kwa wajumbe wengine wa ZEC, kuacha kufuata mkumbo na kuamua kusimamia sheria inavyosema, ili kuwapatia wazanzibar haki yao ya kikatiba..

Rais John Pombe Magufuli Atoa ya Moyoni Kuhusu Askari Watatu Waliofariki Jana Katika Ajali ya Gari

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali Ernest Mangu kufuatia vifo vya askari watatu waliopoteza maisha katika ajali ya gari iliyotokea jana tarehe 06 Februari, 2016 katika kijiji cha Isuna, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.


Askari waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni Inspekta Miraji Mwegelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerald Ntondo.


Katika salamu hizo Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa na vifo vya askari hao, ambao wamekutwa na mauti wakiwa wanatekeleza majukumu yao ya kikazi.


"Kupitia kwako Mkuu wa Jeshi la Polisi natoa pole nyingi kwa familia za Askari waliopoteza maisha, Ndugu, Jamaa na Marafiki pamoja na askari wote wa Jeshi la Polisi Tanzania ambao wameguswa kwa namna ya pekee na msiba huu" Amesema Rais Magufuli.


Ameongeza kuwa anaungana na wote walioguswa na vifo hivyo katika kipindi hiki kigumu, na amewaombea marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi, Amina.


Rais Magufuli pia amewatumia salamu za pole Askari walioumia katika ajali hiyo, akiwemo Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani katika Mkoa wa Singida Mrakibu wa Polisi Peter Magira na kuwaombea wapone haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao ya kila siku.


Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dodoma

07 Februari, 2016

Kauli ya Magufuli ya Kwamba Ataendelea Kufanya Kazi Aliyotumwa na CCM Yazua Utata..Wadau Wadai Atengue Kauli

$
0
0
Kauli aliyoitoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli, ya kwamba ataendelea kufanya walichomtuma chama cha CCM, imeibua mtafaruku miongoni mwa wananchi huku wakidai amewasaliti.

Wakitoa maoni yao katika ukurasa wa Facebook wa East Africa Television wananchi hao wamesema kauli hiyo ya Rais Magufuli haikuwa sahihi, na wengine kumtaka atengue kauli yake kwani walimchagua kama Magufuli na sio chama.

"Hahahaaa ni kweli katumwa na CCM na ndo wamempa mbinu zote za maigizo na scripts zote... sijapendezwa sana Rais wangu kwa kauli hiyo.... Atengue kauli please!! Wengine tulichagua yeye kama Magufuli ila sio yeye kama mgombea wa ccm... I hate CCM and all members wa hicho chama... Kama na yeye yuko kichama zaidi, hatutavutiwa naye pia”, alisema Revocatus Obote.
Mdau mwengine aliendelea na maoni haya...

“Ameshabadlisha kauli yake tayari,

ni kazi ambayo ametumwa na CCM sio wananchi tena, sasa kama ni kweli anataka kufanya kazi aliyotumwa na ccm inamaanisha kuja kumalizia pale alipoacha huyo wa Chalinze, kuja kuimalizia nchi yenyewe sasa”, alisema Kannole Kaisy.

Mdau mwengine alisema kutokana na kauli imeonyesha ni tatizo la kuchagua viongozi ambao sio vijana, na kushauri kuwapa nafasi vijana ili kupata fursa ya kuliongoza Taifa, ikiwemo na kubadili katiba ya nchi.

“Aseee yani hii nchi inaendeshwa kichama sio, kwahiyo CCM ndo anaiongoza na sio wananchi wa Tanzania, hili ndo tatizo la kuchagua wasio vijana siku hizi, kuna low expentance sasa hii katiba inabidi ibadilishwe ili vijana wapate fursa za kugombea urais, unajua sisi atuendelei kutokana kila secta unakuta mzee ndo anaongoza, tuwaige wenzetu basi yani Tanzania kila kitu bàdo tuko nyuma, dah yani bora kuzamia ulaya tu kwa mambo kama haya, we bado ufikilie jinsi ya upatikanaji wa ajira kwa vijana na mambo mengine ya nchi unaongoza chama sasa we unadhani na mtafaruku unao endelea nchini we unadhani vijana hawatojiunga kwenye makundi ya ajabu”, alisema mdau aliyejulikana kwa jina la Cannibal Man.

Jana kwenye sherehe za kutimiza miaka 39 chama cha mapinduzi (CCM), Rais Magufuli alisema ataendelea kufanya kazi aliyoagizwa na CCM, kauli ambayo imeleta minong'ono mingi miongoni mwa Watanzania.

Jaji Lubuva Amshukia Edward Lowassa Kwa Anavyojitangaza Kuwa Alishinda Urais na Jina Lake Kukatwa

$
0
0

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Damian Lubuva amewataka wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu waache kujitangaza kuwa walishinda, akisema wanapotosha wananchi.


Kauli hiyo ya Jaji Lubuva imekuja siku chache baada ya aliyekuwa

mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa kudai kuwa kama si matokeo kuchakachuliwa, alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa sababu wananchi walishaichoka CCM na wakawa wanataka mabadiliko.


Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalum na waandishi wa habari ofisini kwake, akisema yeye na Ukawa walishinda kwa kishindo isipokuwa matokeo yalivurugwa makusudi ili CCM iendelee kubaki madarakani.


Jana, akiwa kwenye mkutano wa tathmini kati ya NEC na asasi za kiraia kuhusu utoaji elimu kwa mpigakura uliofanyika Dodoma, Jaji Lubuva alisema uchaguzi umeshapita na kilichobaki sasa ni kufanya kazi tu.


Bila ya kutaja jina la mwanasiasa huyo, Jaji Lubuva alisema kama kuna mtu alishindwa katika uchaguzi uliopita, ajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.


“Hata wananchi wanawashangaa kwa kuwa wao ndio walioamua ni nani anafaa kuwaongoza,” alisema Jaji Lubuva.


Alisema kuwa NEC ilikuwa inapokea matokeo ya uchaguzi kutoka majimboni na kuyasoma kama yalivyotumwa na katika hilo hakuna wakala hata mmoja wa chama ambaye aliyapinga matokeo hayo.


“Sasa nashangaa kuna baadhi ya wagombea wanaotaka Tume ifukuzwe kazi eti tu kwa sababu wao hawakushinda. Naomba ifahamike kwamba katika kila uchaguzi duniani kuna kushinda na kushindwa.


"Sasa kama kila atakayeshindwa atataka tume ifukuzwe kazi hapatakuwa na tume ya uchaguzi kwa sababu kila atakayekuwa anashindwa atakuwa anataka tume ifukuzwe kazi,” alisema Jaji Lubuva.

Pius Msekwa Amfungukia Jakaya Kikwete ...Amtaka Aondoke na Mifumo yake Kabla ya Kumkabithi Magufuli

$
0
0

Siku moja baada ya CCM kuadhimisha miaka 39 tangu kuzaliwa kwake, kada mkongwe na muasisi wa chama hicho, Pius Msekwa amesema kuna haja ya kufanya mabadiliko ndani ya chama hicho hasa muundo wa halmashauri kuu ya taifa. Amtaka Jakaya kikwete afanye mabadiliko kabla ya kumpa kijiti Rais Magufuli.

Wajane Wawili Wauawa Kwa Kukatwa Mapanga Wakidaiwa Kusambaza Kipindupindu Mkoani Mbeya

$
0
0

Wajane wawili wa Kitongoji cha Bulinda wilayani Kyela wameuawa kwa mapanga wakidaiwa kusambaza ugonjwa wa kipindupindu baada ya kufiwa na waume zao katika eneo hilo.


Waliouawa ni Geneli Kapwela (65) na Rahabu Bungulu (70) waliokuwa wakiishi peke yao.


Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Mbeya  Ahmed  Msangi  alisema  jana kuwa  wajane  hao  waliuawa  juzi  baada  ya  kipindupindu  kuhusishwa  na  imani za kishirikina.


Takwimu  za  mauaji toka polisi zinaonyesha  karibu watu wawili wanauawa  mkoani  Mbeya  kwa  imani  za  kishirikina

Tazama Hapa Video Mpya ya Wimbo Mpya wa ALI KIBA Unaoitwa Lupela

$
0
0
Ni siku mbili zimepita toka Alikiba alipoifanya party ya kuitambulisha video yake mpya kwa Watanzania wachache waliopewa kadi za mwaliko, ila sasa hivi ameiachia video kwenye Youtube ili kila mtu aitazame… ni video ambayo aliifanya Marekani wiki kadhaa zilizopita…. 

Ukishaitazama acha na comment yako hapo chini ili Alikiba akipita badae ajue mashabiki zake wanasemaje.

Kwa Mara ya Kwanza Kocha Jose Mourinho Aongelea Kuhusu Kurudi Uwanjani Kufundisha Baada ya Kufukuzwa Chelsea

$
0
0
Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu kwa kocha wa zamani wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho, February 7 karudi kwenye headlines na kauli mpya baada ya kutokuwa tayari kuzungumzia soka, Jose Mourinho ameamua kuzungumzia soka ikiwa ni wiki sita zimepita toka afukuzwe kazi na Chelsea.

Jose Mourinho ambaye amekuwa akihusishwa kujiunga na Man United ili arithi nafasi ya Louis van Gaal alikuwa hayupo tayari kuzungumzia soka, ila kwa sasa amekubali kulizungumzia hilo na kukiri kuwa yupo karibu kurudi kazini hivi karibuni, licha ya kuwa wengine huwa wanamtafsiri kama jeuri, lakini yeye anasema ni mtu wa kawaida na anajifunza popote.

“Siku zote nimekuwa nikijifunza hata katika sehemu ambayo najihisi ni mtaalam, siku zote mimi sio mkamilifu na nimekuwa nikijifunza kila siku, wakati mwingine katika kazi na hata maisha binafsi, narudi karibuni katika soka sehemu ambayo nahisi ni maisha yangu ya asili”  Jose Mourinho

Mwalimu Mkuu Ashushwa Cheo na Kukamatwa na Takukuru Kwa Rushwa ya KUKU

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Amani Mwenegoha amemvua wadhifa wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sinamila, Mashaka Lusotola na kumrudisha kuwa mwalimu wa kawaida.

Hatua hiyo ilikuja baada Mwenegoha kubaini kuwa walimu wa shule hiyo wamekuwa na tabia ya kuwaagiza kuku, wazazi wanaowaandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza.

Mwenegoha alichukua maamuzi hayo, baada ya kuthibitisha kuwa mwalimu huyo mkuu, ameshindwa kudhiti tabia hiyo ya walimu walio chini yake.

Akizungumzia kusimamishwa kwake, Mwalimu Lusotola alisema amefurahi na kufananisha adhabu hiyo na kumpiga teke chura.

Tayari mwalimu huyo amekamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupamaba na Rushwa (Takukuru), leo anatarajia kwenda kuandikisha maelezo, huku akisisitiza kuwa hajaomba kitu chochote kwa wazazi.

MEN ONLY: Here Are 13 Signs That you’re Chasing a Wild Goose When Seducing a LADY

$
0
0
If she exhibits one or more of the below, she is NOT playing hard to get, so cut your losses and move on.

1. She’s not returning your calls. She may not call you but not returning your calls is plain rude and a clear ‘I am not interested’ signal.

If she’s playing games, even worse, you should think twice whether this is the type of girl you want to be spending time with. Flashing red- light!

2. She’s giving you monotonous responses on the phone or text. Women like to talk especially to men they are interested in. One word answers mean ‘I am not interested in letting you know me and I am not interested in knowing you either.’ This is one signal I wish all guys would understand quicker. Double red- light!

3. She’s inflexible and too busy to fit you into her schedule. It is not unusual for a woman to clear her whole day’s schedule just to be available for one hour with a man she is clearly interested in. Red-light!

4. She declines gifts, never lets you do her any favors – or she repays them immediately. This is a sign she knows you’re into her, and she doesn’t want to feel indebted or obligated to you. Most women love receiving gifts and if she declines or doesn't acknowledge the gesture there isn’t a clearer signal that she is not interested. Proceed with caution!

5. She agrees to go out with you but cancels at the last minute. If she has cancelled on you a few times. Hint, hint, you are just back up.

6. You don’t hear from her for weeks or months at a time, and then she calls out of the blues to hang out. Chances are she is bored and you are the very last resort. You’re worse
than back up.

7. She’s trying to hook you up with her friends or talking about how attractive other women are. This is a sure sign she is trying to deflect your attention from herself to another woman. Not a good sign.

8. She’s talking to you about other men she is interested in. This is really a hopeless situation and if she’s doing this because she’s playing games, again I ask is this the kind of woman you really want to be with.

9. She says ‘maybe’ to a date scheduled 2 weeks in advance. She’s just being polite, she’s not interested.

10. She tells you that she just wants to be friends or that she thinks of you as a brother
(much worse). This means that she doesn’t find you attractive. She enjoys your company but she does not want to sleep with you. Sorry brother.

11. She finds every reason to argue with you and then puts the blame on you. She’s trying
to justify why you’re so wrong for her. Please help her leave you. Run!

12. She puts you down in public, shouts at you or rolls her eyes in contempt. Wow! She has no respect for you whatsoever so please just leave her alone.

13. She doesn't laugh at your jokes. She either doesn't get your sense of humor, which means you probably aren't compatible or you are really rubbing her the wrong way. When women are interested, everything about you is funny. She will laugh even when it isn’t funny.

Thank me later.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Februari 8, Ikiwemo ya Wema Kutapika Tembele Mbele za Watu

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Februari 8, Ikiwemo ya Wema Kutapika Tembele Mbele za Watu

Ubuyu Mpya....Jokate Amwangukia Mama Ali Kiba

$
0
0
Malovee tena! Siku chache baada mwanamitindo Jokate Urban Mwegelo ‘Kidoti’ na Mfalme wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’, kumwagana, hatimaye habari za chini ya kapeti zimevuja zikidai kwamba Jokate ameamua kumwangukia mama mzazi wa Kiba ili kunusuru penzi hilo na sasa mapenzi yamerudi upya.
Tukio hilo lililonaswa na vyanzo vyetu lilijiri usiku mnene wikiendi iliyopita katika Hoteli ya Slipway iliyopo Oysterbay, Dar mara tu baada ya Kiba kuzindua video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Lupela.8

Kwa mujibu wa watu wa karibu na wawili hao, mara tu baada ya kufika hotelini hapo, Jokate alimfuata mama Kiba na kumsalimia kwa heshima zote kabla ya kuelekea kwa ndugu wengine wa Kiba kisha kurejea kwenye meza ya mzazi huyo.

Mfuatiliaji makini wa tukio hilo aliliambia Ijumaa Wikienda kwamba, Jokate alilazimika kumwangukia mama Kiba ili anusuru hali ya hatari iliyokuwa tayari imeshatokea katika penzi hilo.26

“Wewe…(jina la mwandishi wetu) hukujua kinachoendelea, Jokate kamwangukia mama Kiba ndiyo maana umeona ndugu wengine wakiwa karibu kwa muda mrefu ndipo Kiba akaitwa ili akae na Jokate. Si unaona wanapiga stori na kucheka? Sasa hivi mambo safi na mapenzi ni kama zamani,” alisema mmoja wa watu wa karibu wa mastaa hao aliyejua mchongo mzima uliokuwa ukiendelea.

Mbali na maelezo ya mtu huyo, paparazi wetu alibahatika kujionea kwa jicho lake Jokate akiwa ‘klozi’ na mama Kiba na ndugu wengine.Pia mwanahabari wetu aliwashuhudia Jokate na Kiba wakiwa na nyuso za furaha wakifurahia mafanikio ya Video ya Lupela ambayo walisema itafika mbali kutokana na viwango vyake.

Jokate na mama Kiba wakiwa kwenye picha ya pamoja pamoja na dadaake kiba (kulia).
Wakati wa kuondoka eneo hilo, Jokate ndiye aliyetangulia kuondoka eneo hilo akiwa ameongozana na marafiki zake na muda kidogo baadaye Kiba alifuata naye akiwa na ndugu zake wengine na kuondoka kwa pamoja.

Mawaziri Yona na Mramba Waanza Kutumikia Kifungo cha nje...Wakabithiwa Vyombo vya Usafi

$
0
0

Yona, Mramba wakabidhiwa vifaa vya usafi hospitali ya Palestina.
Mawaziri wa zamani Basil Mramba na Daniel Yona wameripoti katika hospitali ya Sinza Palestina na kukabidhiwa vifaa kwa ajili ya kufanya usafi.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliridhia waliokuwa Mawaziri wastaafu Basil Mramba na Daniel Yona kutumikia adhabu ya kifungo cha nje kwa kufanya usafi katika maeneo ya kijamii ikiwemo Hospitali ya Sinza Palestina.

Wenye Mavogue na Mujumba ya Kifahari wote Sasa Waangaliwe Tax Paying Records

$
0
0
Kumekuwa na tabia nyingi za watu kujinasibu kwenye mitandao ya kijamii kama ni.matajiri mipicha ya nyumba za fahari, maisha ya fahari, magari ya kifahari sasa tunaomba TRA ifanye kama America IRS. Kuangalia background financial history na Tax payment compliance.

Haiingii akilini mtu ana kiduka cha.nguo za china sinza ana range rover na Tax paying history yake ni void. Huyu ana maswali ya kujibu kipato chake kikoje na shughuli ipi halali inampatia kipato.

Kuna wimbi la vijana wanaendesha magari ya bei ghali lakini ukiuliza biashara au ofisi au hata bank account hawana. Ni lazima tubadilike wote kwa ujumla tulipe kodi

Wingu Zito Laendelea Kutawala Ufisadi Wa Mabilioni NIDA....Yadaiwa Kitambulisho Kimoja Kimegharimu Sh 89,800

$
0
0
Wingu  zito limetanda ndani ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuhusu matumizi ya  Sh bilioni 179.6 ambako kila kitambulisho  cha taifa kimegharimu Sh 89,800 zikiwamo gharama za utawala

Hayo yamebainika  siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kushangazwa na watendaji wa mamlaka hiyo ikizingatiwa vitambulisho vilivyokwisha kutengenezwa hadi sasa havifiki   milioni mbili na havina saini.

“Utaona ugumu wa kuongoza, nchi inatawaliwa na madudu ya kila aina.  Wapo watu wanacheza na fedha wanavyotaka wakati wapo watu masikini sana  wengine wanataka bodi zao wakakae Ulaya.

“Hapo ndipo tulipofikia, wengine wanalipwa mshahara wa Sh milioni 35 kwa mwezi…naomba mniombee kabla ya kunihukumu, toeni hukumu kwa haki kwa hawa wanaotaka kuifikisha nchi pabaya, toeni hukumu zao haraka,” alisema.

Rais Dk. Magufuli, licha ya kushangazwa na hali hiyo, alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilipewa Sh bilioni 70 lakini iliweza kutengeneza vitambulisho   23,253,982 ambavyo vilikuwa na saini ya kila mpiga kura na kila kimoja kimegharimu Sh 3,010.

Kutokana na hali hiyo, tofauti ya gharama kati ya kitambulisho kimoja cha NIDA na cha NEC ni Sh 86,790.

Pamoja na hayo, hivi sasa Watanzania wanasuburi   ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Juma Assad, kuhusu  matumizi ya fedha hizo za NIDA.

Januari 26 mwaka huu, Rais Magufuli alitangaza kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake, Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu.

Maimu alisimamishwa kazi pamoja na maofisa wengine wanne, kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za Serikali.

Maofisa hao ni Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Joseph Makani, Ofisa Ugavi Mkuu, Rahel Mapande, Mkurugenzi wa Sheria, Sabrina Nyoni na Ofisa Usafirishaji, George Ntalima.

Akitangaza uamuzi huo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue, alisema taarifa zilizomfikia Rais zinaonyesha kuwa NIDA hadi wakati huo ilikuwa imetumia Sh bilioni 179.6, kiasi ambacho ni kikubwa.

Alisema Rais angependa ufanyike uchunguzi na ukaguzi kujua jinsi fedha hizo zilivyotumika, maana amekuwa akipokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na kasi ndogo ya utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.

Licha ya kumuelekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, afanye ukaguzi maalumu wa hesabu za NIDA  ukiwamo ukaguzi wa “value for money” baada ya kuthibitisha idadi halisi ya vitambulisho vilivyotolewa hadi sasa, pia aliitaka Takukuru ifanye uchunguzi kujiridhisha kama kulikuwa na vitendo vya rushwa au la.

Credit: Mtanzania

Mwanamuziki Peter wa P-Square Atuhumiwa Kumsaliti Mke wake na Mchepuko wa Marekani

$
0
0
POP staa, Peter Okoye ametuhumiwa kumsaliti mkewe, Lora Omotayo baada ya kuripotiwa kuwa ametoka na modo anayefahamika zaidi kupitia Instagram, Aimee ambaye makazi yake yapo Marekani.
Awali,mrembo huyo aliposti picha kwenye Instagram akiwa na Samuel Eto’o na kusema kuwa yupo kwenye maandalizi ya kurejea London akidai kuwa ndiyo sehemu pekee ukitoa Marekani ambayo anapenda kuishi na wakati huo alikuwa akitokea Paris, Ufaransa kwenye mishe zake.
Peter na Mchepuko wake 

Kilichoharibu; baada ya kutupia picha hiyo ambayo ilipigwa na Peter kisha staa huyo naye ‘akashare’ hapo ndipo ishu ikaibuka baada ya mfuasi wao mmoja kukomenti kuwa nyota huyo kutokaKundi la P Square anatoka na modo huyo na amekuwa akizunguka naye miji kama Paris, Antalya na London na kumuacha mkewe nyumbani.

Shabiki huyo ambaye anatumia jina la Mihlany kwenye Instagram,alimwaga mboga kuwa nyota huyo amekuwa akimsaliti mkewe kwa kutoka na modo huyona wiki iliyopita walikuwa pamoja Paris kabla ya kwenda kukutana tena Marekani.

Baada ya komenti hiyo, Peter na modo huyo waliifuta na kumblock kabisaMihlany kwani alishachafua hali ya hewa. Modo huyo alisema: “Tetesi ni burudani lakini wakati mwingine zinawaharibia wahusika.

Kila mmoj ana familia yake na siyo vizuri kunihusisha na mtu mwingine kwani ni rafiki tu na hakuna cha zaidi.”

Jack Wolper Aambulia Matusi Mtandaoni Baada ya Kupost Picha ya Mazishi ya Kalosh, Mwenyewe Atoa ya Moyoni na Kusema Haya

$
0
0

Jack Wolper amejikuta katika wakati mgumu baada ya kupost mtandaoni picha ya maiti ya Marehemu Kaloosh ikiwa katika jeneza...Baada ya tukio hilo watu mbali mbali walianza kumkosoa na wengine kumrushia matusi kwenye page yake kwa kusema sio sahihi kipost picha kama hizo..

Mwenyewe leo amefunguka kama ifuataavyo:

"Jamani insta NAOMBENI muwe na mipaka kwanza mnatakiwa mjue hii ni acc yangu sishei na mtu yoyote..pili nimekosea nimewaelewa kwann mnitukane jamani wakati nilielewa sikilizeni mm ni dada na ni mchumba wa mtu na vilevile sio bora dada ni dada bora naheshimika kwangu mpk kwetu sawa kwahiyo mnapoandika matusi YENU wadogo zangu wanaumia mbali na mm naombeni sana Mkome na msinizoee kunitukana kwasababu naumia na mnawaumiza ndugu zangu na wengine ambao wamenifollow sitaki sitaki huwezi kunishauri mpk unitikane unfollow sina nguvu ya superglue kusema nimewagandisha tafadhari...sipendi nasema tena sipendi mbona mm siwafati kwenye acc zenu kuwatukana from no where jamani MNIACHE plz" Jack Wolper

Lulu Michael Afunguka Bei yake Kama Ukitaka Kufanya Nae Movie..Adai Hatumiki Bure

$
0
0
Staa wa filamu Diana Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kama unamtaka kumshirikisha katika filamu yako, andaa milioni 15 kwani anaogopa kuendelea kutumika bila faida.

Akizungumza katika kipindi cha Take One cha Clouds TV Jumapili hii, Lulu alisema tayari alishatengeneza jina kwa miaka mingi na sasa anahitaji pesa.

“Kufanya filamu kwa milioni 15 sio hela nyingi, watu wanaongea tu kwa sababu hawajui nini kipo ndani yake. Mimi nikipewa milioni 15, mavazi pamoja na kila kitu najitegemea.” Alisema Lulu

Aliongeza, “Kwa hii milioni 15 ni kweli kuna faida, faida moja ni kwamba naepuka kutumika bila faida, kwamba mtu unakuwa na jina sawa, umefanya movie hii, umefanya movie hii nini unacho?. Mwisho wa siku tunajikuta tunaanza kufanya vitu vingine ili kumaintain ile status yako kwa sababu umeshatengeneza jina na unahitaji kulimaintain.” alimalizia Lulu.

Wema Sepetu Atapika Tembele Mbele za Watu.....

$
0
0
Hii pia ni habari njema! Kisa mimba, Miss Tanzania 2006 aliye pia staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu amejikuta akiteswa na kitumbo hicho kila kukicha na habari mpya ni yeye kutapika huku wapambe wakisema mbali ya chakula kingine, pia mboga ya majani aina ya matembele ‘tembele’ ilikuwepo, nenda na Ijumaa Wikienda.
Tukio hilo la kiujauzito lilimkuta Wema mwishoni mwa wiki iliyopita alipokuwa akiwasili kwenye Hoteli ya Slipway iliyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam ambako staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba alikuwa akizindua video yake inayokwenda kwa jina la Lupela. Wema alikuwa na wapambe wake.

MPAMBE AMWAGA SIRI
Mpambe mmoja (jina tunalo) ndiye aliyelipenyezea Wikienda tukio la staa huyo kutapika mbele ya kampani bila kujali mazingira.
“Jamani mimba inamtesa sana madam (Wema). Muda huu tunakuja hapa Slipway wametapika. Yaani ametapika mpaka mboga ya matembele,” alisema mpambe huyo akimwambia paparazi wetu mara baada ya kuingia ndani ya hoteli hiyo.

SASA WEMA ANACHUNGWA
Mbali na wapambe wengine, kuna mwanaume alikuwa sambamba na Wema akihakikisha usalama wake na wa kitumbo huku akiwa karibu kwa lolote.
Mtoboa siri wa Wema alimwambia paparazi wetu kuwa, jamaa huyo ndiye anayemshika mkono Wema kama ataonesha dalili ya kutetereka wakati wa kutembea.
“Huyu mwanaume ndiye mlinzi wa Wema kwa sasa. Kazi yake ni kuangalia kama Wema anaweza kuanguka wakati akitembea au kufanyiwa jambo lolote ambalo linaweza kuumiza makuzi ya mtoto tumboni,” alisema mpambe huyo.
WEMA NA WIKIENDA
Baada ya maelezo hayo, Wikienda lilimfuata Wema na kuzungumza naye mambo makuu mawili. Moja ni kumwomba akubali kupigwa picha akiwa na kitumbo hicho. Pili ni kumuuliza kuhusu kutapika.
Wikienda:“Mambo madam?”
Wema: “Poa, vipi?”
Wikienda:“Poa. Leo naomba nikupige picha.”
Wema:“Mmh! Haya!”

PICHA NA MALALAMIKO
Hata hivyo, wakati Wema akipigwa picha hizo alikuwa akilalama kwamba, hakuwa tayari kupigwa picha akiwa ndani ya gauni la kumbana hivyo kitumbo chake kuonekana.
“Leo ni historia. Sikuwa na mpango wa kupiga picha tumbo langu. Sijui wewe (paparazi wetu) umeninogesha na nini mpaka nimekubali,” alisema Wema.

KUHUSU KUTAPIKA
Wikienda lilimuuliza Wema kuhusu taarifa za kutapika ambapo alikiri:
“Yeah! Nimetapika wakati nakuja hapa hotelini. Ilibidi nishuke kwenye gari (akiendeshwa) ili nitapike vizuri! Kwa kweli tumbo linanitesa sana…huwa natapika.”
Wakati Wema anaulizwa kama alitapika tembele, kuna mtu alimuita hivyo kumuondoa kwenye umakini na paparazi wetu na kuondoka.

ASHINDWA KUTULIA
Baada ya kuachana na paparazi wetu, Wema hakuweza kutulia sehemu moja kwani pitapita yake kila kona huku akiwa amevaa viatu vya mchuchumio (virefu) na kumfanya kila mtu ajue yupo ndani ya nyumba.
MVUTO WAKE
Hata hivyo, katika hali isiyokuwa ya kawaida, Wema baada ya kuingia kwenye ukumbi huo, alibadili mazingira ambapo yeye akawa kama ndiyo mwenye shughuli hiyo ya kuzindua video na si Ali Kiba.
Baadhi ya watu walipobaini Wema ameingia, walilipuka kwa nderemo huku kila mtu akitaka kumwona.
Baadhi ya watu walisema: “Jamani kumbe Wema ana mimba kweli?! Si mnaona kitumbo kile! Dah! Aisee! Kweli Mungu mkubwa…mwacheni aitwe Mungu.
“Halafu si alipachikwa kila aina ya jina huyu…wengine walimwita mgumba, wengine tasa, yaani jamani, Wabongo wanaongea sana,” alisikika akisema mmoja wa watu waliohudhuria shughuli hiyo.
WEMA ACHOKA, AONDOKA
Ilipofika saa nane usiku, Wema aliondoka hotelini hapo akiwa na wapambe wake huku akigoma kuongea na paparazi wetu licha ya kupigwa picha nyingine akiwa anasepa.
MAHESABU YA HARAKA
Kwa mujibu wa watu wake wa karibu, mimba ya Wema sasa inagonga mwezi wa nne huku akiwa anaendelea kuhudhuria ‘viwanja’ mbalimbali kwa ajili ya kujirusha jambo ambalo wengi hawakubaliani naye wakisema anajichosha pasipo sababu.

Source:Global Publishers
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images