Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Jux Asema Jack Clif Yupo ‘Okay’ Hana Tatizo

$
0
0
 
Ikiwa ni zaidi ya miaka kadhaa tangu mrembo Jack Clif kukamatwa china,kuna vitu vingi ambavyo bado havijajulikana, lakini kumbe jux huwa anafanya naye mawasiliano.

‘’Huwa tunafanya mawasiliano ingawa sio mara kwa mara ..she is okay..yuko sawa..nimewasiliana naye kama miezi miwili iliyopita ..siwezi kuongelea sana vitu vingine..hata hivyo yeye mwenyewe hapendi niwe naongea ongea na watu kuhusu maisha yake,’’Jux

Taarifa Muhimu Kuhusu Matokeo Ya Kidato Cha Nne 2015 (CSEE) 2015

$
0
0
Baraza la Mitihani la Tanzania limekuwa likipigiwa simu na watu mbalimbali wakiomba ufafanuzi kuhusu taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imetangaza kuwa matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2015 yamezuiwa kwa muda hadi tarehe 08/03/2016.

Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwajulisha watahiniwa na umma kwa ujumla kuwa taarifa hizo ni za UONGO na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki.

Hivyo, Baraza linaomba umma kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa Wizara haijasitisha utoaji wa matokeo hayo. Matokeo yatatangazwa mara tu mchakato utakapokamilika.

Imetolewa na,
AFISA HABARI NA UHUSIANO

Dada Aliyezaniwa Msukule wa Tajiri Kibamba Anaendelea Vizuri Baada ya Kupatikana Tena Bonde la Mto Msimbazi

$
0
0
Mariam Juma (25), maarufu kwa jina la Upa ambaye alidhaniwa na wananchi kuwa ni msukule baada ya kupatikana akiwa mtupu katika shimo lenye urefu wa futi kumi, nyumbani kwa tajiri aliyejulikana kwa jina moja la Mtei Januari 19, mwaka huu, Kibamba, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar, anaendelea vizuri kiafya katika Hospitali ya Taifa Muhimbili tofauti na alivyofikishwa hapo kwa mara ya kwanza.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii wiki iliyopita, Buguruni, Wilaya ya Ilala, Issa Mohamed, mume wa Upa alisema kwamba mkewe kwa sasa anaendelea vizuri ukilinganisha na mara ya kwanza alipofikishwa hospitalini hapo baada ya kupatikana katika bonde la Mto Msimbazi maeneo ya Tabata, Januari 23, mwaka huu.

‘Msukule’ wa tajiri aendelea vizuriAidha, Mohamed aliendelea kusema kwamba Upa yupo Muhimbili katika kitengo cha watu wenye matatizo ya akili anakofanyiwa uchunguzi na matibabu na kwamba amekuwa akienda kumjulia hali na kumpelekea chakula ambapo hata yeye amekuwa akijisikia vizuri anapomuona mumewe, jambo ambalo linamfanya wale naye pamoja, kuzungumza kisha kuagana.

“Kwa mara ya kwanza alipopatikana katika shimo nyumbani kwa tajiri na kutoweka akiwa mikononi mwa polisi kisha kupatikana tena kwenye bonde la Mto Msimbazi, kuna tofauti kubwa. Namuombea kwa Mungu apone haraka arudi nyumbani kwani watoto wamekuwa wakimlilia,” alisema Mohamed.
Upa aliaga nyumbani kwa dada yake mkubwa anayeishi Tabata Matumbi, Dar mwanzoni mwa mwezi Januari, mwaka huu akidai anakwenda kuwanunulia nguo wanaye katika Soko la Buguruni lakini hakurudi nyumbani ambapo baadaye alipatikana katika shimo, nyumbani kwa Mtei.

Global Publishers

Upangaji wa Matokeo Ligi Daraja la Kwanza Wamuweka Malinzi Pabaya..Kujiuzulu ama Kuchukua Hatua

$
0
0

Timu 3 za kijeshi kati ya nne zimehusika katika ‘tuhuma’ za upangaji wa matokeo ili kumpata mshindi atakayepanda ligi kuu msimu ujao kutoka kundi la 3 la ligi daraja la kwanza iliyomalizika wikendi-jana.

Ruvu Shooting ya Pwani ilikuwa timu ya kwanza kupanda VPL msimu ujao kutoka kundi la B, ubora wao uliwafanya wapande wakiwa na michezo mitatu mkononi. Hakika wamestahili pongezi kwa jitihada kubwa walizofanya mara baada ya kushuka msimu uliopita.

African Lyon pia imerejea ligi kuu baada ya kukamilika kwa mechi za kundi A siku ya Jumapili. Lakini timu ya tatu haijatangazwa na Shirikisho la mpira nchini, TFF lakini kwa asilimia mia moja itapaswa kuwa Mbao FC ya Mwanza ambayo hadi siku ya mwisho ya michezo ya kundi A ilikuwa katika nafasi ya nne.

Kwanini, Mbao FC wanapaswa kupanda kutoka kundi C badala ya timu za Geita Gold Sports, Polisi Tabora na JKT Oljoro ambazo zilimaliza katika nafasi 3 za juu katika kundi.

Katika ligi ambayo hakuna timu iliyowahi kushinda zaidi ya magoli 5-0 katika kundi si rahisi zipatikane ‘mechi mbili double’ zenye idadi kubwa ya magoli.  Geita imeishinda 8-0 JKT Kanembwa ya Kigoma katika uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma siku ya Jumamosi.

Inawezekana kabisa Geita walikuwa  na uwezo wa kupanda kutokana na mwenendo wao wa msimu mzima kuwa wenye  matokeo mazuri, ila njia ya mwisho waliyoitumia kutaka kupanda VPL ni  mbaya na huenda ikawapoteza kabisa katika ramani ya mpira ikiwa tu itagundulika walipanga matokeo kwa namna yo yote ile.

Siku hiyo hiyo katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi, Tabora wenyeji Polisi Tabora wakaichapa 7-0 JKT Oljoro ya Arusha. Oljoro ile iliyopiga mpira mwingi siku chache nyuma dhidi ya Geita Gold Sport isingeweza kufungwa 7-0 tena magoli 6 wakiruhusu katika dakika 45 za kipindi cha pili.

Katika baadhi ya vyombo vya habari baadhi ya mashuhuda walisema kulikuwa na asilimia nyingi kuashilia ulikuwapo upangaji wa matokeo huku jina la Jamal Malinzi (rais wa TFF) likihusika kama mtu aliyekuwa akitoa maelekezo ya nini kinapaswa kufanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika.

Hizi ni tuhuma za wazi amekuwa akitupiwa Malinzi kuhusu michezo hiyo ‘tata’ zinaweza kumfanya kuchukua maumuzi magumu ya kufuta matokeo ya timu hizo nne (Geita, Kanembwa, Polisi Tabora na Oljoro) kuzishusha daraja na kuwafungia wale wote ambao walihusika ikiwa itabainika matokeo yalipangwa.

Kushindwa kulisimamia hili na kulitolea maamuzi sahihi itamaanisha ameshindwa, na kama atashindwa katika hili atapaswa tu kujiuzulu. Hakuna sababu ya kuchezwa kwa ‘playoff’ kati ya Geita na Polisi kwa kuwa timu zote zimefungana kwa kila kitu.

Kama mechi zao zingemalizika wa matokeo yaliyokuwapo kipindi cha kwanza ( Polisi Tabora 1-0 JKT Oljoro, JKT Kanembwa 0-1 Geita Gold Sport) bila shaka sasa tungezifahamu timu zote 3 zilizopanda lakini kwa kile kilichojitokeza katika dakika 45 za mwisho, yakiwemo matukio ya mechi kusimama kwa muda mrefu bila sababu za msingi ni dalili ya za wazi kuwa matokeo yalipangwa.

Ikiwa matokeo ya timu hizo yatafutwa kama inavyotarajiwa na kushushwa daraja, timu ya Mbao FC itakuwa na nafasi ya kuongoza kundi na hivyo watacheza VPL msimu ujao. Malinzi hii ni nafasi yake ya kujimaliza kiuongozi au kufufua upya mtazamo wake alioingia nao madarakani miaka miwili iliyopita.

Kushindwa kuzishusha daraja na kuzifungia timu hizi atakuwa ameshindwa, maamuzi sahihi yatamsafisha na kumuweka katika viongozi wa mfano.

Tundu Lissu Matatani Ahojiwa na Polisi Lisaa Limoja Kisa Gazeti la Mawio lililofungiwa

$
0
0

TUNDU Lissu, Mwanasheria wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) pia Mbunge wa Singida Magharibi leo jijini Dar es Salaam amehojiwa na Jeshi la Polisi kuhusu hoja alizozitoa kwenye Gazeti la MAWIO, anaandika Faki Sosi.

Lissu amehojiwa kwa zaidi ya saa moja Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam baada ya kuhitajika kutoa maelezo kwa madai ya kutoa kauli za uchoelezwa zilizoandikwa kwenye Gazeti la MAWIO zilizohusu mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar.

Habari iliyoandikwa na gazeti hilo iliyobeba kichwa cha habari ‘Machafuko yaja Zanzibar’ inaelezwa kuwa sababu ya serikali kulifungia gazeti hilo tarehe 15 Januari mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kutoa maelezo Lissu amesema, serikali inajaribu kumziba mdomo asizungumzie kuhusu suluhu ya mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani Zanzibar wakati wahusika hawazingatii misingi ya demokrasia.

“Wale waliobebwa kwenye uchaguzi leo wanataka kutufumba midomo tusizungumzie masula ya uchaguzi wa Zanzibar kwani machafuko yanaweza kutokea visiwani humo kwa tahadhari hiyo wanatuita wachochezi,” amesema Lissu.

Amesema kuwa, wao wametoa tahadhari ili yasitokee machafuko na umwagikaji wa damu na kwamba, Rais John Magufuli atawajibika kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kama alivyowajibishwa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya.

Amesema, mahojiano yake na Gazeti la Mawio ndio yaliyosababisha yeye kuitwa na kuhojiwa na polisi na kwamba, mtazamo wake ulioandikwa kwenye gazeti hilo ndio umechangia kufutwa kwa gazeti hilo.

Amesema kuwa hatokubali kuzibwa mdomo hata kama watatumia nguvu ya polisi.
Amesema, hatua ya Rais Magufuli kukakataa kujihusisha na mgogoro wa Zanzibar haikubaliki kwa kuwa ndiye ndiye atakayepeleka jeshi pale vurugu zitakapotokea.

Lissu amefika polisi hapo akiwa na mawakili wa watatu wa Chadema ambao ni Peter Kibatala, Fedrick Kiwelo na Hekima Mwasibu.

Amesema, baada ya mahojiano hayo polisi watapeleka jalada lake kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kwa hatua zaidi.

Mawakala wa Forodha Wapinga Makampuni 210 Kufungiwa Bandarini.........Wasimulia Jinsi Wafanyakazi wa Bandari Wanavyoshirikiana na Benki Kuiba Kodi

$
0
0
Sakata la upotevu wa makontena katika bandari ya Dar es Salaam na kufungiwa kwa makampuni 210 ya forodha limechukua sura mpya baada ya Chama cha Mawakala wa Forodha (Taffa) kueleza kuwa kuna ushirikiano kati ya wafanyakazi wa taasisi hiyo na benki kuiba tozo za bandari.

Taffa, Wasafirishaji wa Nchi Kavu Wenye Magari (Tatoa), Mawakala wa Usafiri wa Majini (Tasaa) na Wamiliki wa Bandari Kavu (Cidat) wamesema hawahusiki na ukwepaji wa kodi.

Kwa muda sasa, kampuni za uwakala wa upakuaji na upakiaji wa mizigo zimekuwa zikituhumiwa kusaidia kukwepa kodi na kufikia hatua ambayo 210 zilitangazwa kufutiwa uwakala hivi karibuni.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar jana, mawakala hao walitaka uchunguzi ufanyike na endapo moja ya kampuni hizo itabainika kuhusika, hatua za kisheria zichukuliwe.

Mmoja wa wamiliki wa kampuni ya uwakala wa forodha, Ratish Kamanoor alisema alitoa mzigo bandarini 2013 na kulipa Sh40 milioni kupitia Benki ya CRDB Tawi la Water Front, lakini taarifa za TPA zilionyesha mzigo haujalipiwa. Baada ya kufanyika kwa utafiti ilibainika hundi yake imelipia kampuni nyingine 21.

Tony Swai wa Kampuni ya Wakala wa Forodha ya Transnotic alisema alifanya malipo ya Sh33 milioni kwa ankara yenye namba 11013092014, mwaka 2012, lakini malipo hayo hayakuonekana katika mfumo wa TPA licha ya kuwa na vielelezo vya benki na TPA vikionyesha kontena limeruhusiwa kutoka.

Mkurugenzi wa CRDB wa tawi hilo, Donath Shirima alipotafutwa kuhusiana na tuhuma hizo, alisema hawezi kuzungumza kwa kuwa siyo msemaji wa benki.

Mwenyekiti wa Taffa, Stephen Ngatunga alisema wamemwandikia barua Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa kumweleza jinsi wizi unavyofanywa na TPA pamoja na kumpa ushahidi.

“Tulimpelekea waziri sampuli ya kampuni 29 zinavyolipa tozo za bandari na kumweleza kuwa TPA wamechana ushahidi,” alisema.

Ngatunga aliilalamikia Serikali kutangaza kuwa kampuni 284 zinakwepa kodi na kuwa, kitendo hicho kinachafua taswira ya Tanzania kimataifa na utendaji wa bandari.

Tume yaundwa
Baada ya Taffa kukutana na Waziri Mbarawa iliundwa tume huru kuchunguza wizi huo iliyopewa siku 10 kutoa taarifa za uchunguzi.

Jinsi wizi unavyofanyika
Kwa maelezo ya wamiliki wa kampuni za uwakala wa forodha, wizi huo hufanyika kati ya wafanyakazi wa benki, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na TPA.

Mfumo wa malipo kwa njia ya benki ulianzishwa baada ya ule wa kawaida kuonekana unachangia wizi huo bandarini.

Taffa, Tatoa, Tasaa na Cidat walieleza kuwa wizi huo hufanyika kwa njia ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kupitia mfumo wa malipo wa IePS. Walielezwa kuwa baada ya mawakala kulipa, mfanyakazi wa TPA huingiza taarifa za malipo kama utaratibu unavyotaka.

Vyama hivyo vilisema baada ya TPA kumpa wakala risiti ya kuonyesha kuwa amelipa na kutoa mzigo wake, mtu wa kitengo cha Ieps cha TPA husubiri wakala anapotoa mzigo bandarini huwasiliana tena na mtu wa benki ambaye hurudisha malipo hayo.

Kuanzia hapo mfumo huonyesha kuwa mzigo huo haukulipiwa. Inaeleza kuwa mchezo huo huchezwa kati ya mtu wa benki kitengo cha Ieps cha TPA na anayeingiza taarifa za malipo kwenye mfumo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Februari 17, Ikiwemo ya Mawaziri wa Magufuli Kuanza Kuvuruga

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano Ya Februari 17, Ikiwemo ya Mawaziri wa Magufuli Kuanza Kuvuruga

Kwa Ujumbe Huu wa Idriss Sultani ni Uthibitisho Tosha Kuwa Mimba ya Wema Sepetu Imetoka Kama Inavyodhaniwa...

$
0
0
Mpenzi wa Wema Sepetu, Idris Sultan usiku wa kuamkia Jumatano hii amepost picha ya watoto mapacha huku akiandika ujumbe unao onyesha mimba ya mpenzi wake huyo imearibika.
Wema Sepetu

Kupitia instagram idris ameandika

"To my unborn twins,
So quickly you came into our lives,
So quickly torn away.
Never got the chance to meet you,
There’s so much I want to say. All these thoughts running through my head,
It’s enough to drive me insane.
Though you lived only 13 short weeks,
You were loved so very much.
I wish that I could hold you,
I long to feel your touch. I pray that in another life, We get the chance to meet. God brings and takes as he plans and we cannot complain but only pray that all that was for a better reason and a better plan in store for us. We have learnt lessons painfully but wont stop trying again and again and do swear by the time your brothers and sisters are made to come to this world we will be more than ready for them.
Sincerely Your Dad. ❤️" Idriss Sultan

Mwindi Afukuzwa Kazi Katika Hoteli ya Ramada Baada ya Kuwatukana Wafanyakazi Kwa Kuwaita Manyani....

$
0
0
Raia wa India, Dennis Smith ameachishwa kazi katika Hoteli ya Ramada kwa madai ya kuwatukana wafanyakazi wa ngazi za chini akiwaita nyani.

Smith, ambaye ni meneja wa chakula na vinywaji wa hoteli hiyo, aliwatukana na kuwadhalilisha wafanyakazi hao siku ya Sikukuu ya Wapendanao akiwatuhumu kushindwa kuandaa meza vizuri.

Kutokana na udhalilishaji huo, wafanyakazi wa hoteli hiyo jana waligoma wakishinikiza meneja huyo asimamishwe kazi au wao waache kazi.

Wakizungumza jana, baadhi ya wafanyakazi ambao waliomba majina yao yahifadhiwe walisema tabia ya meneja huyo imekuwa sugu na tukio la juzi lilikuwa halivumiliki. Walisema raia huyo wa India amekuwa mwenye majivuno na kutoa lugha chafu dhidi yao.

“Tumechoshwa, anatuitaje sisi nyani, hii tabia ni ya muda mrefu na sasa hatuwezi kuivumilia,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.

Mwakilishi wa wafanyakazi hao, Mathew Misalaba alisema bosi huyo amekuwa akiwarushia maneno ya kuwadhalilisha kila wanapofanya makosa hata kidogo.

Alisema licha ya uongozi wa hoteli kuahidi kumsimamisha kazi Smith, wamelipeleka suala hilo polisi ili hatua stahiki zichukuliwe.

Meneja Rasilimaliwatu wa hoteli hiyo, Sebastian Nchimbi alisema tayari Smith ameachishwa kazi kutokana na tukio hilo.

“Tulizungumza na wafanyakazi wakatuambia kuwa hawataki Smith awepo kazini na sisi tukafanya uamuzi ili kuwalinda wafanyakazi wetu,” alisema.

Alisema waliamua kumwachisha kazi Smith baada ya kupata malalamiko mengi kutoka kwa wafanyakazi hao.

“Si tukio la mara ya kwanza na ndiyo maana tulipoona yamezidi tuliamua kuchukua hatua,” alisema.

Hata hivyo, Nchimbi alimsifu Smith akisema ni mtendaji mzuri na alikuwa na tija kwa hoteli hiyo ya kitalii lakini hakuwa na kauli nzuri kwa wafanyakazi Waafrika.

“Kiutendaji ni mzuri mno… yaani kwetu sisi tunapoteza mtu hasa, tatizo ni mdomo tu,” alisema.

Walimu Watatu Wakatwakatwa Mapanga Huko Musoma, Mara

$
0
0
Walimu watatu wa shule ya Secondary Mara iliyopo katika manispaa ya mji wa Musoma Mkoani Mara,Vedastus Rwechungula ,Juma Amos Na Maccelo Ndege, Wamekatwa Mapanga sehemu mbali mbali ya miili yao walipokuwa wakirejea shuleni hapo Usiku wa Saa Nne toka matembezini.

Wakizungumza wakiwa wamelazwa katika hospital ya Rufaa ya Musoma,Walimu hao wamesema kuwa Vitendo vya Uhalifu jirani na Shule hiyo vimekuwa vikijitokeza mara kwa mara kutokana na vibaka waliopo katika eneo hilo kuwakata watu kwa mapanga.

Kariakoo: Wamachinga Msimbazi Waua Mtu Kwa Kukanyaga Nyanya

$
0
0
Mfanyabiashara mkubwa wa Kariakoo jijini Dar, Stephen Elija Silas (27) ameuawa kwa kupigwa mawe na wafanyabiashara wadogowadogo ‘Wamachinga’ kwa madai ya kukanyaga kwa gari lake nyanya walizopanga barabarani, Uwazi limefuatilia.

Tukio hilo lenye simulizi ya kusikitisha lilijiri usiku saa nne ya Februari 8, mwaka huu katika makutano ya Mtaa wa Msimbazi na Aggrey, Kariakoo jijini Dar es Salaam wakati marehemu huyo alipokuwa akilikwepa gari lililobeba maziwa. Marehemu Stephen alikuwa akiendesha gari lake aina ya Toyota Corolla lenye namba za usajili T 312 AZU ambalo pia lilipondwa kwa mawe na Wamachinga. Alikuwa njiani kuelekea nyumbani kwake, Kinondoni, Dar.

MBALI NA MAWE, ALICHOMWA KISU taarifa zaidi zinadai kuwa, mbali na marehemu huyo kupigwa mawe, pia Wamachinga hao walimchoma kisu kwenye kwapa la mkono wa kulia akiwa ndani ya gari. SHUHUDA ASIMULIA Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alisema marehemu alikuwa akitokea upande wa uliyokuwa mzunguko wa Shule ya Uhuru, akaingia Barabara ya Msimbazi.

Alipofika makutano ya mtaa huo na Aggrey, mbele yake kulikuwa na gari lililobeba maziwa ambalo liliyumba, hivyo ili asiligonge akalikwepa na hivyo kujikuta akikanyaga kwa bahati mbaya nyanya za Wamachinga hao ambao palepale walianza kumshambulia kwa maneno, baadaye mawe na kumalizia na kisu. WALICHANGANYIKA NA WAHUNI “Jitihada za wasamaria wema kumuokoa zilishindikana licha ya jamaa kuomba msaada.

Mimi naamini kuwa, mbali na wamachinga pia wahuni wa mitaani walikuwepo kwa lengo la kupora vitu vyake,” kilisema chanzo hicho. ALIOMBA MSAMAHA Chanzo: “Kwanza jamaa alipobaini amekanyaga nyanya za biashara ya Wamachinga hakufanya fujo kwa kunena mabaya, aliomba asamehewe au alipe fedha kulingana na nyanya zilizoharibika lakini Wamachinga na wahuni hao hawakumsikiliza, waliendelea kumwadhibu.

“Kulikuwa na wananchi waliokuwa wakitokwa machozi walipomuona jamaa akipigwa mawe kwa kosa ambalo halina kichwa wala miguu.” WANANCHI WAPIGA SIMU POLISI Inaelezwa kuwa, baadhi ya wananchi waliamua kupiga simu Kituo cha Polisi Msimbazi ili wakamuokoe Stephen lakini licha ya kuwahi katika eneo la tukio, walimkuta akiwa hoi kutokana na kipigo na alifariki dunia wakati polisi wakimkimbiza Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa matibabu.

UWAZI LAFIKA MSIBANI Uwazi kama ada yake, lilifika kwenye msiba wa Stephen, kwa baba yake mkubwa marehemu aitwaye Charles Losaru, Mtoni Kijichi jijini Dar na kuzungumza na mdogo wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Rebeca Elija ambaye alisema alikuwa na marehemu muda mfupi kabla ya kifo chake. Alikuwa na haya ya kusema: “Marehemu kaka Stephen alikuwa mfanyabiashara mwenye maduka ya bidhaa mbalimbali, Kariakoo na Sinza. Huwa ana kawaida ya kutusindikiza na gari lake baada ya kufunga maduka. Mimi na ndugu zangu wengine tunaishi Kitunda yeye Kinondoni.

Amekuwa akitusindikiza hadi Banana na kutuacha tupande daladala. “Siku ya tukio, alitusindikiza na kutuacha Buguruni. Ilikuwa saa tatu usiku. Ni sisi tuliamua atuache hapo badala ya Banana. Yeye akarudi akipitia Kariakoo kwa vile kuna ndugu zetu wengine wana maduka maeneo hayo.” SIMU YAKE YAPIGWA, YAITA TU! Rebeca anaendelea: “Tuliposhuka kwenye daladala pale Banana, nilimpigia simu mara tatu ikawa inaita bila kupokelewa. Nikampigia simu mchumba wake, anaitwa Neema William ambaye ilikuwa wafunge ndoa hivi karibuni. Nilitaka kujua kama kaka alishafika nyumbani, Neema akasema hajafika.

TAARIFA ZA KIFO KWA NDUGU “Sasa wakati tunapanda daladala Banana kwenda Kitunda, nilipigiwa simu na marafiki zake na kuniambia kuwa Stephen amepata matatizo yupo Muhimbili. Niliposhuka Kitunda, alinipigia simu kaka yangu mkubwa, anaitwa Silas ambaye tulikuwa naye Kariakoo, akaniambia kaka amefariki dunia (machozi). “Kaka Stephen alikuwa mpole kupita kiasi! Hivi ni kwa nini walimuua kikatili vile? Kwanza pale walipompigia mawe, mbona ni sehemu ya magari na wala si pa kupanga nyanya wala bidhaa nyingine. Inaniuma sana (machozi tena).

” MAREHEMU AAGWA DAR, AZIKWA ARUSHA Mwili wa marehemu Stephen uliagwa Alhamisi ya wiki iliyopita katika Kanisa la Anglikana lililopo Muhimbili na kusafirishwa kwenda nyumbani kwao, Daraja Mbili mkoani Arusha kwa mazishi yaliyofanyika Ijumaa iliyopita.

POLISI WAZUNGUMZIA Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, ACP Ernest Matiku alipohojiwa na Uwazi ofisini kwake wiki iliyopita, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa, marehemu alipigwa na kundi la watu baada ya kugonga gari lililokuwa likiuza maziwa kisha kukanyaga bidhaa za Wamachinga zilizokuwa zimepangwa chini. Gari likiwa limehalibika vibaya.

“Mpaka sasa tunawashikilia watu kumi kutokana na tukio hilo na bado upelelezi unaendelea. Kwa sasa hakuna biashara ya Wamachinga inayoendelea maeneo yale ya Mtaa wa Msimbazi. “Nalaani kitendo kile cha mauaji kwani hata kama marehemu alifanya kosa lakini sheria zipo na siyo kuchukua maamuzi hayo mazito ya kukatisha maisha ya binadamu, wote waliofanya unyama ule watashughulikiwa kisheria upelelezi ukikamilika,” alisema kamanda huyo.

Chanzo: Uwazi

Serikali ya Magufuli Inajiandalia Anguko Kama Sio Aibu Siku zijazo

$
0
0
Dhana ya utumbua majibu inayoonekana kufanywa kwa nia njema na wakati mwingine kwa dhamira ya kisiasa zaidi bila kuchukua kwanza tahadhari ya kutosha,inaiweza kuja kuiweka serikali hii katika mtihani mgumu sana siku za usoni pale mambo yatakapoanza kuharibika na watu kuanza kukimbiana na wengine kugeukana.

Ziko sababu kadhaa zinazoweza kuja muifanya serikali iiumbuke ikiwa ni pamoja na kushindwa kesi pale itaposhitakiwa.

Makosa ya serikali yenyewe
Kuna baadhi ya shughuli za serikali katika Taasisi na Mashirika ya Umma zimefanywa chini ya kiwango au kutotekelezwa kabisa kutokana na serikali kupeleka fedha kidogo tena kwa mafungu mafungu na wakati mwingine kutopelekwa kabisa licha ya kuwa Taasisi husika ilitengewa bajeti. Hili linaweza kuja kujitokeza katika Taasisi kama Bodi ya Mikopo na nyinginezo ingawa ursasimu,uzembe na utendaji mbovu wa watumishi unaweza kuwa sehemu ya tatizo

Influence ya wanasiasa
Kuna sehemu watendaji wanawajibishwa lakini mwisho wa siku uchunguzi unaweza kuja kubainisha kuwa kulegalega au utendaji mbovu katika Mashirika / Taasisi hizi kumechangiwa na maamuzi ya wanasiasa kuingilia utendaji wa ma-CEO,manegement na hata Bodi zinazosimamia Mashirika haya na hivyo itafika wakati baadhi ya ma-CEO hawa watakuja kuonekana hawana hatia na kulazimika kurudishwa kazini au kupangiwa kazi nyingine.

Sheria za Utumishi wa Umma
Kuna watendaji leo hii wanaweza kusimamishwa kazi au kufukuzwa kazi lakini taratibu na sheria za utumishi zikifuatwa,huenda baadhi yao ikaja kuonekana kuwa waliadhibiwa kimakosa na Mahakama ya kazi inaweza kuagiza warudishwe kazini mara moja.Serikali inabidi na ilipaswa kutazama vizuri sheria hizi za utumishi wa umma na kuzirekebisha kwanza kabla ya kuendelea na fukuzafukuza hii au huku kusimamisha watu kazi kila kukicha.

Agenda za Kisiasa
Wakati unakuja siasa hazitakwepeka katika hili zoezi la utumbuaji majipu. Wanaotumbuliwa waliwekwa na wanasiasa na wanaowatumbua ni wana siasa ila nao wana ya kwao hivyo itafika hatu mmoja akimwaga ugali mwingine atamwaga mbogo kwani sidhani kama kuna msafi miongoni mwao na wataanza kutoleana siri.

Wanaotumbuliwa kuamua kutoa ya mayoni:
Kuna baadhi ya wanaotumbuliwa ambao mambo yao yanaweza kuja kuisha kiani iwapo wataamua kufunguka kiasi cha kutaja majina makubwa na pale itakapoonekana mambo yameisha kiujanjaujanja, ndio serikali itajikuta ikiinyooshewa kidole na pengine hata kusutwa.Hawa wanaotumbuliwa wanaweza hata kupenyeza siri kwa waandishi wa habari.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu
Kushinda kesi nyingi zitakazoibuka hapo baadae kufuatia maamuzi yanayofanywa sasa na serikali,itategemea na ufanisi na uwezo wa Ofisi hii kusimamia kesi ambazo serikali inaweza kushitakiwa.Kama watakuwa hawajajipanga vizuri kwa kuwa na wanasheria competent na wa kutosha huku serikali ikikabiliwa na kesi nyingi,kuna hatari ya serikali kuja kushindwa kesi nyingi zitakazifunguliwa na watumishi,watu binafsi ama makampuni.Katika kipindi hiki, Ofisi hii inatakiwa ipewe kipaumbele kuliko Taasisi nyingine yote ya umma.

Ukifukuza watumishi,ukinyang'anya watu mashamba,ukivunjia watu nyumba na ukanyang'anya watu leseni,ofisi pekee itakayobeba mzigo wa kesi zitakazofunguliwa ni hii ofisi ya AG labda kama kuna utaratibu wa serikali kuweza kukodi makampuni binafsi ya uwakili kuisadia kusimamia baadhi ya kesi zitakazofunguliwa.

Maamuzi ya bila umakini
Hivi sasa mawaziri wako busy kusimamisha watu kazi na sidhani kama wanachukua tahadhari ya kutosha kabla ya kufikia maamuzi haya.Mfano mzuri ni kusimamishwa yule mtumishi aliyekuwa kiongozi wa bomoaboma alafa baada ya siku chache ikitako taarifa kuwa amerejeshwa katika nafasi yake(kama sikosei Nipashe ndio iliripoti habari ya mtumishi huyu kurudishwa kazini).

Kusimamia nidhamu na uwajibikaji ndani ya serikali ni jambo jema na linalopaswa kuungwa mkono na kila mpenda maendeleo, lakini katika zama hizi za haki za binadamu na utwala wa sheria plus sheria zetu za utumishi wa umma, maamuzi haya ya leo yanaweza kuja kuwa "counterproductive " kwa serikali yenyewe yasipofanywa kwa umakini na kwa kutaka kujijenga kisiasa.

Katika kesi/mashauri kumi,serikali inatakiwa kushinda si chini ya saba au nane tofauti na hapo itakuja kuishi kubezwa kuwa ilikurupuka.

By Salary Slip/JF

Sikiliza Barua Aliyoiandika Mtanzania Jackline Cliff Kutoka Gerezani China...

$
0
0
Jackline Cliff ni Mtanzania ambaye alikamatwa kwenye uwanja wa ndege na kufungwa gerezani huko Macao China kwa kosa la kujaribu kuingiza dawa za kulevya miaka miwili iliyopita, sasa leo kamuandikia mwandishi wa habari na Mtangazaji Millard Ayo barua ili aisome kwa Watanzania, bonyeza play kwenye hii video hapa chini….

Baada ya Sinto Fahamu Wema Sepetu Mwenyewe Amedhibitisha Kuwa ni Kweli Ujauzito Wake Hana Tena...Aandika Maneno Haya Kwa Uchungu

$
0
0

Wema Sepetu Ameandika maneno haya kwenye page yake:

Wemasepetu - "Ni kweli. Na imeniuma sana lakini nimefika kwenye hatua maishani mwangu naweza kusema Alhamdulillah for everything.

Alhamdulillah kwa wote wanaojua uchungu nilionao na wameonyesha moyo wa kibinadamu. Nawashukuru kwa upendo wenu, MNANIPA NGUVU.

Alhamdulillah kwa wote wanaojua uchungu nilionao na wamefurahia kwasababu zao binafsi. Nawashukuru kwa uwepo wenu, MNANIPA UJASIRI.

Alhamdulillah kwa siku ya kesho. Ilimradi nina pumzi, SITACHOKA KUJARIBU TENA.

Hata ukikosa, ukakosa, ukokosa eeeeeeh...sema ASANTE, KWELI YEYE NI MUNGU.

Alhamdulillah for EVERYTHING! " Wema Sepet

Dada wa Diamond..Esma Platnumz Apewa Talaka Tatu na Mpambe wa Wema Sepetu Petit Man

$
0
0
Petit Man ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi pendwa cha burudani Afrika Mashariki cha Planet Bongo, na kusema kuwa yeye na mke wake huyo wameachana kwa mapenzi yao, ingawa hajafurahishwa na kitendo cha mama yake kuingilia suala lao.

"Mimi mwenyewe sikusikia interview ya mama yangu, nilisikia tu ameongea lakini sikujua ameongea hivyo kwa madhumuni gani lakini mi sipendi sana vitu vyangu na familia yangu kuviweka wazi, nadhani ni matatizo tu ya ndani ya familia, sisi wenyewe na mapenzi yetu ndo imefanya ifikie mwisho na Mwenyezi Mungu pia amependa iwe mwisho wetu, kwa hiyo hatuna jinsi.

Petit Man amesema kwa sasa yeye na mkewe Bi Esma ambaye wamezaa mtoto mmoja wanaishi sehemu tofauti, huku kila mmoja akiendelea na maisha yake binafsi.

"Mimi siko tena nae nishaachana naye, ye anaishi kwake na mimi naishi nyumbani kwangu, ninaposema mtu nimeachana nae nimemaanisha, nimetoa talaka tatu yani siko nae tena yani", alisema Petit Man.

Majipu Yaendelea Kutumbuliwa....Wakurugenzi Wanne wa Halmashauri Mkoani Kagera,Mtwara,Geita na Tunduma Wasimamishwa Kazi

$
0
0
WAZIRI nchi ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mtaa,George Simbachawane amewasimamisha kazi wakurugenzi wa nne  kwa  tuhuma  za  kuwahonga wakaguzi wa fedha  kutoka katika ofisi ya Mkaguzi mkuu wa  Hesabu za  serikali (CAG) ili wapewe hati  safi huku Halmashauri hizi zikiwa na ufisadi .

Wakurugenzi  waliosimamishwa  kazi  ni   Elizabeth Chitundu wa Halmashauri za Misenyi mkaoni Kagera, Ally Kisengi wa Halmashauri ya Nanyumbu mkaoni Mtwara  na  Abdalla Mfaume wa Halmashauri ya Mbogwe mkoani Geita.

Pia,Waziri Simbachawene   amemsimamisha kazi  mkurugenzi Halmashauri ya  Tunduma Mkoani  Mbeya Bi Halima Ajali  ili kupisha uchunguzi kutokana matumizi mabaya ya madaraka ikiwa ni pamoja na kuwatumia watoto wake katika shuguli za halmashauri na kuwalipa posho na kusababisha upotevu wa mapato.

Aidha, Waziri Simbachawane pia ameziagiza mamlaka husika kuwasimisha kazi watendaji wa ofisi ya mkaguzi wa Hesabu za Serikali nchini,CAG  waliohusika kupokea rushwa kutoka kwa wakurugenzi hao ili watoe  hati safi kwenye Halmashauri hizo huku zikiwa na ubadilifu wa fedha za Umma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana Jijini Dar es Salaam,Waziri Simbachawene amesema Wakurugenzi hao wamegundulika  baada ya uchunguzi wa kina uliofanywa na wizara yake

Akibainisha makosa ya kila mkurugenzi,Waziri Simbachawene amesema Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misenyi, Bi Chitundu  alimwagiza  mweka hazina wake Majaliwa Bikwato atoe rushwa ya Milioni tatu kwa maafisa wa  ofisi ya CAG kwa lengo la kuficha kasoro walizoziabini katika ukaguzi huo  huku akijua ni kosa kisheria. Watumishi wa  wa ofisi ya CAG  waliopokea pesa hizo ni Stevin Buawa,John Elias pamoja na Kilembi Mkole

Katika Halmashauri ya Nanyumbu, Simbachawene amesema  kuwa  tarehe 26 Juni 2015, mkurugenzi wake bwana Kasengi pamoja na mweka hazina Pasco Malowo na mwasibu Emmanuel Mugesa walimkabidhi fedha Milioni 3 na laki tano  afisa wa ofisi ya  CAG  kwa lengo la kutoa hati safi

Waziri Simbachawene amesema mwezi Novemba mwaka jana , Mkurugenzi wa Halmashauri  ya  Mbogwe mkoani Geita Abdalla Mfaume na mweka hazina wake waliwapatia milioni 16  maafisa wakaguzi wa ofisi ya CAG  ili wafiche ufisadi walioubaini

Amesema katika Halmashauri hiyo pia kumegundulika kuwepo na ufisadi mkubwa ikiwemo malipo ya mishahara hewa pamoja na malipo ya milioni 200 yaliotolewa pasipo kuwa na Stakabadhi

Huddah Monroe Declares Herself Kenya's Range Rover Ambassador After Doing This To Her Range Rover (Photos)

$
0
0

Just when you thought Huddah Monroe, arguably everyone’s favorite socialite was keeping it low, she comes up with quite an act that has people talking for days.

The petite socialite cum entrepreneur has long shown she s the proud owner of a sleek Ranger Rover. However, despite being seen with it in public, many have accused her of posing. Well, she just proved she is the rightful owner in one move that saw he paint the powerful SUV pink and have her name engraved on it. Here is how an elated Huddah celebrated the customizing work

RANGE ROVERS chose me..... Call me the Range Rover Brand ambassador in Kenya Abeg!!! 
I'm a BRAND!


Nay Wa Mitego Fires At Wema Sepetu Again With Fake Baby Bump Amidst Miscarriage News.

$
0
0
Controversial Rapper Nay Wa Mitego slammed Wema Sepetu in his recent released single Shika Adabu Yako. In the song the rapper asks whether Wema's pregnancy is real or it is fake just for seasonal kicks. Wema kept silent, however Team Wema stormed Nay's instagram page with negative comments. But it seems Nay hadn't enough of Wema as he has come for her yet again. Today Nay posted a fake baby bump asking how much it is sold, and many believed the post is for Wema Sepetu who is said to have miscarriage. Look belowa what he posted...


Ray Kigosi Akana Katu Katu Kuwa Anajichubua Ngozi...Adai Anafanya Mambo yafuatayo Mpaka Ngozi yake Inakuwa Nyeupe

$
0
0
Mwigizaji maarufu wa Bongo Movie hapa nchini Ray Kigosi amesema kwamba yeye hajawahi kujichubua bali huwa anakunywa maji mengi pamoja na kufanya mazoezi .

Ray ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano katika kipindi cha ENews kinachorushwa na EATV na kusema kwamba hua anakwenda salon mara moja kwa wiki kwa ajili ya kusafisha uso wake (Scrub) ili akiwa anafanya kazi zake watu waweze kumwona vizuri na kupenda kazi zake.

Naye Mpenzi wake Chuchu Hans amesema kwamba Mpenzi wake hajichubui bali ni maisha yamemkubali tofauti na hapo nyuma alivyokuwa anahangaika kuinua sanaa na kipaji chake.

Katika kipengele cha ''Cheche'' ambacho majirani hupewa nafasi ya kumzungumzia msanii au mgeni wa siku kwenye show wamesema kwamba Ray apunguze kutumia vipodozi kwani anakuwa kama mchina.

Pia wamemtaka mwigizaji huyo kuwa na moyo wa kusaidia wasanii chipukizi ilikukuza tasnia ya uigizaji hapa nchini.

Will Wema Sepetu’s fans trust her again?

$
0
0

Reality TV star, actress and former Miss Tanzania, Wema Sepetu has captured all her fans by her beauty and her interesting drama. Yes is the drama queen!

Now you will agree with me, there was a time she made us all proud by launching her own lipstick. Of late Wema has been double speaking and this may trigger her fans feel a little bit misguided.

Firstly, when she gifted herself with a brand new Range Rover on her birthday and the story later came to be that she didn’t clear the custom papers that the car wasn’t registered under the Tanzania Revenue Authority.

Secondly and perhaps the most interesting incident was when she was caught stealing electricity. As a celebrity what does it cost to pay electricity like any other ordinary citizen? Nothing, you only need to have personal discipline to assure that you do follow what the country expects of you.

Then, her scandal with Zari The Bosslady left us all speechless. Truth is, it was childish to poke herself into Zari’s business and demand for a DNA yet she does not even have her own child. Sorry if I may sound a little but harsh. The insults she posted on Zari Instagram page made her soon implied that she was pregnant.

It was good news to her fans because it made them feel like she was soon going to settle down and focus on her family. People were also happy for her because they know how she has struggled to conceive. Too bad because it is now a wish that can never make beggars ride on a horse.

Though she hasn’t confirmed the news yet, but it’s sad now that she has had a miscarriage and maybe this may open her eyes and teach her a lesson that she should let God do his work. Perhaps it was too early for her and Idris to start talk and brag about it. Her fans are disappointed, confused and some of them like Precious Sada are very angry!

“I used to love u kwakweli but now nimekuchoka na drama zako, laiti kama ungekua mjamzito kweli na bahati mbaya imetoka usinge act normal hivyo pia tusingeona video zako unavuta shisha,” says Precious.

She adds,” wewe ni mdada mzuri sana ila njia uliyo changu kupita inakuharibia heshima yako na urembo wako unapenda kick za kip*mbavu,unapenda mashindano yasio na mpangilio, kwa mwanamke aliokuwa anatafuta mimba kama wewe usinge hata anza tangaza ikiwa bado ndogo na kuanza kufanya maonyeshonila sababu unapenda mashindano na kick na umaarufu usio na mpango ukaanza jionyesha kila mtu akawa anashika tumbo do u think ivyo ni sahihi?ungekaaa kimya ungepoteza nini?”

“Au huwa unapenda sana watu wakutukane kila siku je unafahamu kuwa kutajwa jina lako vibaya kila siku lina halibu nyota ulio nayo?am so tired of u and very dissapointed well kama mimba yako imetoka am sorry to tell u this ur responsible kwani uliifanyia maonyesho na kama hukua na hata huo ujauzito mungu akusamehe bure, wewe ni mdada mzuri usio kuwa na akili wala usiopenda kushauriwa unadhani kina aunty na hamisa mobeto walivyoficha mimba zao walikua hawana akili.”

Again, I am sorry if I may sound harsh. If she has had a miscarriage as her boyfriend Idris Sultan implied on his Instagram page, I assume she might be in a very depressing state. But her recent Instagram posts seem not to communicate that message. Everything seems to be okay! Was she pregnant after all? Was it a publicity stunt? She has posed so many questions right now.

We really do not know if we can trust her anymore. Most of her stories happen to contradict from what she says. It is about time that she realizes that she cannot run away from reality. The next time she announces or implies something serious like that; shall we have the guts to trust this beauty queen?

All in all, she will always remain our Wema, the drama queen.

By Pauline Bohela

Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images