Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live

Waziri Mbarawa Ampa Wiki Moja Mkandarasi wa Korea Kutoa Mikataba kwa Watanzania

$
0
0

Waziri wa ujenzi Makame Mbarawa ametoa wiki moja kwa mkandarasi anayetengeneza barabara ya njia nne kutoka Sakina hadi Tengeru mkoani Arusha kuhakikisha anatoa mikataba kwa wafanyakazi wa kitanzania wanaofanya kazi bila mikataka na akishindwa kufanya hivyo serikali itafuta mkabata wake kumshitaki na kumfukuza nchini.

Waziri Makame Mbarawa ametoa kauli hiyo wakati akikagua ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa kumi na nne nukuta moja inayo jengwa na kampuni ya Hanil-Jiangsu kutoka nchini Korea ambapo alipata malalamiko ya wafanyakazi wa kitanzania kufanyishwa kazi bila mikataba huku wakipata manyayaso kutoka kwa mkandarasi huyo.



Meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Arusha John Kalupale amesema ujenzi wa barabara hiyo unakabiliwa na changamoto nyingi zilizosababisha kuchelewa kwa utekelezaji wake kwani hadi sasa ni asilimia saba tu ya ujenzi uliyofanyika na imebaki miezi tisa muda uliyo pangwa kumaliza.



Meneja wa miradi kutoka Tanrods makao makuu Mhandisi Deusidedit Kakoko amesema katika shilingi bilioni ishirini za kulipa fidia kwa watu wanaondolewa kupisha ujenzi huo tayari bilioni nne zimeshapatikana na hakuna mtu atayeondoshwa kwenye eneo lake bila kulipwa fidia.

Dangote Yaanza Kusambaza Cement Tanzania...Bei ya Mfuko Mmoja wa Cement Hii Hapa...

$
0
0
Kile kiwanda kikubwa cha Africa mashariki na Africa kwa ujumla kwa mara ya kwanza kimeanza kuzalisha kusambaza cement jana tar 21/02/ 2016.

Kiwanda hicho ambacho ni tegemeo jipya kwa waakazi wa mikoa kusini Mtwara na Lindi kiliahidi ajira nyingi ya wakaanzi wa mikoa hiyo na watanzania kwa ujumla
Cement tayari iko maduka kwa bei nafuu ya sh 13,500 tofauti na cement ya viwanda vingine.

Tunawakaribisha wateja wa cement hiyo na wenye magari makubwa kufungua office mkoani Mtwara ili kuongeza ajira za madereva hapa mkoani.

Kweli Siasa si Uadui..Hawa Juzi Nusura Wazipige Laivu Laivu...Leo Mchana Hali ilikuwa Hivi Wakimsubiri Waziri Mkuu Airport..

$
0
0
Mbunge wa Iringa mjini akiwa na mkuu wa wilaya Kasesela wakimsubiri waziri mkuu Airport.. Unakumbuka juzi karibu wazichape laivu bila gloves?? Siasa ni..........

Nimechanganyikiwa Nimegundua Mke wangu na Dada wa Kazi Wanasagana

$
0
0
Yamenikuta Mie mwenzenu hata sijui nifanye nini ila kwa kifupi ni kuwa nimepata ushahidi bila chenga kuwa mke wangu na mfanyakazi wa ndani ama House Girl Wanasagana, Bado sijamwambia mke wangu kwamba najua kwa sababu hata sijui nianzie wapi ..ila ni kwamba juzi asubuhi nilipomaliza kujiandaa kwenda kazini nikatoka ndani ila nilisahau simu hivyo nikarudi kuichukua cha kushangaza nilimkuta mke wangu hayupo chumbani kwetu kwani nilimuacha amelala basi sikujali sana nikajua yupo chooni ila wakati nataka kutoka ndani nikawa nasikia makalele ya mihemeko ya mapenzi kwa mbali hapo ndipo nilipostuka na kunyemelea chumba cha house girl wetu na ambapo sauti zilikuwa zinatokea, 

Nilichosikia hata sina hamu ila nikelele za ku do kabisa wakihamasishana wakijua wapo wenyewe ndani ya nyumba…kiufupi kilinishuka nikashindwa nifanye nini …

Baada ya muda nilitoka nikaenda zangu kazini bila kufanya chochote huku nafikiria ni kitu gani nakosea mpaka mke wangu haridhiki na dozi yangu?? Isitoshe asubuhi hiyo hiyo nimetoka kumpa kimoja cha haja ….Embu nishaurini nifanye nini Jamani ??

Kimenuka...Wakili Awadh Ali Adai Uchaguzi wa Zanzibar Haupo Kisheria..Adai ZEC Inashurutisha Wasiasa na Wananchi Kushiriki Uchaguzi Batili

$
0
0
Wakili wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Wakili Msomi Awadh Ali amesema kuwa uchaguzi wa marudio wa Zanzibar haupo kisheria. Wakili Awadh,akihojiwa na ITV,amesema kuwa Katiba na Sheria ya Uchaguzi wa Zanzibar haitambui uchaguzi wa marudio.

Wakili Awadh amesema kinachofanywa na ZEC ni kuwashurutisha wanasiasa na wananchi kushiriki kwenye uchaguzi wa marudio hapo Machi 20. Wakili Awadh amesema kuwa washindi wa uchaguzi wa mwaka jana walishapewa vyeti vya ushindi na hivyo hawawezi kupokwa vyeti vyao.

Kuhusu pendekezo la kukimbilia mahakamani kupinga uchaguzi wa marudio,Wakili Awadh amesema kuwa Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar pamoja na Katiba haziruhusu kupingwa au kuchunguza ZEC kimahakama.

Collabo ya Shilole na Nicki Minaj yanukia

$
0
0
Siku chache baada ya kuachana na Nuh Mziwanda, mwanadada Shilole ‘Shishi Baby’, kupitia account yake ya Instagram ametoa tangazo la kuomba msaada. Tangazo hili linasema

“Anatafutwa mwalimu wa kingereza mzuri, jamani huu sio utani nipo sirias naona hali ishakuwa sio hali soon natakiwa kuonaa na Niki Minaji hivyo lazima nijinoeee, namba ya sm 0653883839“, aliandika Shilole kwenye ukurasa wake wa instagram

Shilole anafahamika kwa kutojua lugha ya kingereza, hivyo kuwa gumzo anapoongea lugha hiyo ambayo mara kwa mara huwa anachapia, lakini cha ajabu yeye mwenyewe huwa anafurahia na hajutii kuzungumza lugha hiyo ambayo haijui, kama alivyowahi kutamka neno la “I love is my country“, ambalo lilikuwa maarufu na watu kuvutiwa nalo.

Picha,Kanye West na Kim Kardashian wamuonyesha mtoto wao wa kiume ‘Saint West

$
0
0
Kanye West na mke wake Kim Kardashian wamemuonyesha mtoto wao wa kiume Saint West kwa picha waliyoweka mtandaoni February 22.

Kim Kardashian anasema post hii ya mtoto wao imewekwa kama ishara ya kumuenzi baba yao Robert Kardashian aliyefariki mwaka 2003.

“Today is my dad’s birthday,I know there’s nothing more in the world he would have wanted than to meet his grandchildren. So I wanted to share this pic of Saint with you all.”

Saint West ni mtoto wa pili wa Kim na Kanye, wakwanza ni North

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya Februari 23, Ikiwemo ya Wiki Mpya na Majibu Matano

$
0
0
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya Februari 23


Updates..Magufuli Alivyotinga Kivukoni na Magari Yenye Namba za Kawaida Bila Taarifa..

$
0
0
Rais John Magufuli ameendelea kufanya ziara za kushtukiza, baada ya kutembelea ofisi za Kivukoni Dar es Salaam kimyakimya juzi jioni kuangalia mwenendo wa utoaji huduma za vivuko.

Mashuhuda waliokuwepo eneo hilo Jumapili jioni wakati Rais anafanya ziara hiyo, walieleza mtindo alioingia nao Dk Magufuli ulikuwa ni wa kawaida na vigumu kwa mwananchi wa kawaida kung’amu uwapo wa Rais.

Mfanyabiashara wa eneo hilo, Sharif Mkamba alisema Rais Magufuli aliingia saa 11 jioni akiwa na msafara wa magari matatu ya kawaida yaliyokuwa na namba za kiraia.

“Hakukuwa na king’ora chochote kama tulivyozoea bali ulikuwa ni msafara wa kimya kimya. Aliingia moja kwa moja kwenye zile ofisi na alitumia kati ya dakika 10 hadi 15 kabla ya kutoka,” alisema Mkamba.

Said Likoko alisema kuwa baada ya kugundua kati ya magari matatu alikuwepo Rais, walisogea kufuatilia kwa kina kwa kuwa haijazoeleka na walitegemea huenda baadhi ya watumishi wangewajibishwa.

“Aliteremka na kumuuliza aliyemkusudia na taarifa tulizozipata jana zinadai hakumkuta huyo bosi, sijui ni meneja au ofisa sisi hatujui,” alisema Likoko ambaye hujishughulisha pia na biashara ndogondogo eneo la kivukoni.

Likoko alisema pamoja na kwamba aliingia kimya kimya, Rais Magufuli hakusita kuwasalimia wasafiri waliokuwa wakisubiri kivuko wakati alipofanya ziara hiyo.

Alieleza kuwa kama wananchi walifurahishwa na hatua hiyo ya Rais, kwa kuwa watendaji wengi hawafanyi kazi siku za wikiendi licha ya huduma zake kufanyika siku zote.

Tangu jana asubuhi kumekuwa na video inayosambaa ikimuonyesha Rais Magufuli akiwa Kivukoni akitembea kwa miguu ndani ya eneo hilo huku akishangiliwa na wasafiri waliokuwa wakingoja kivuko.

Hata hivyo, jitihada za kutafuta mamlaka husika kueleza kwa undani malengo ya ziara hiyo ziligonga mwamba baada ya Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kutopokea simu.

Ofisa habari wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) Theresia Mwami, alitaka utafutwe uongozi wa juu kueleza yaliyojiri kwenye ziara hiyo kwa kuwa yeye yupo likizo.

Profesa Ibrahim Lipumba Aibuka....Amtaka Rais Magufuli Atangaze Mshahara Na Marupurupu Yake

$
0
0
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amemtaka Rais John Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake, kwa kuwa amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge.

Profesa Lipumba amelieleza gazeti la Mwananchi kuwa Rais Magufuli amejipambanua kuwa kiongozi anayeguswa na matatizo ya wanyonge, hapendi makuu, anahimiza ukusanyaji wa mapato ya Serikali na matumizi mazuri ya fedha za umma, lakini watanzania hawajui mshahara wake ni kiasi gani

Profesa huyo aliyejikita katika masuala ya uchumi, alirejea mijadala mbalimbali iliyowahi kuibuliwa kuhusu mshahara wa Rais, ikiwamo ule uliyowahi kuibuliwa mwaka 2013 na Zitto Kabwe, wakati huo akiwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema kuwa Rais analipwa Sh32 milioni kwa mwezi.

Pia alirejea taarifa iliyochapishwa na Mwananchi, Julai 27, 2015, iliyoandikwa kutoka katika mtandao wa African Review kuwa Rais mstaafu Jakaya Kikwete ni wa nne miongoni mwa marais wa Afrika kwa kupata mshahara mkubwa wa dola za Marekani 192,000 kwa mwaka sawa na dola 16,000 kwa mwezi, ambayo ni sawa na Sh32 milioni kwa mwezi. Hadi jana jioni, dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na Sh2,187.

“Taarifa ya Ikulu ilikanusha vikali habari zilizochapishwa na Mwananchi. Ikulu ilieleza kuwa habari hizo siyo za kweli. Hata hivyo, haikueleza mshahara wa Rais na marupurupu yake ni kiasi gani?

Pia, katika mjadala wa mshahara wa Rais, Naibu Spika wa Bunge lililopita ambaye ndiye Spika wa sasa, Job Ndugai alinukuliwa akieleza kuwa mshahara wa mtu ni siri yake.

Waziri wa Nchi Katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa Umma wa wakati huo, Celina Kombani (kwa sasa ni marehemu) alisema kuwa ni kosa kutangaza mshahara wa Rais.

“…Kwa hivi sasa Rais Magufuli atangaze mshahara na marupurupu yake na kama mapato yake ni Sh32 milioni kwa mwezi, basi ajitolee alau nusu ya mapato hayo kuchangia elimu na afya ya wanyonge. Hatua hii itaimarisha taswira inayojengeka barani Afrika kuwa yeye ni Rais wa wanyonge,” amesema  Lipumba.

Wakati akizungumza na wazee wa Dar es Salaam wiki iliyopita, Rais Magufuli aliwataka mawaziri, naibu mawaziri na makatibu wakuu wachangie Sh1 milioni katika mishahara yao kuchangia elimu.

Pia Rais alieleza kuwa yeye mwenyewe, makamu wake na waziri mkuu watachangia Sh6 milioni kila mmoja, ili zifike Sh100 milioni kusaidia changamoto za elimu bure Mkoa wa Dar es Salaam.

Kutokana na tangazo hilo, Profesa Lipumba alisema, “Ikiwa Sh6 milioni zitakatwa katika mshahara wake wa mwezi mmoja ni wazi mshahara wake na ule wa makamu wake na waziri mkuu ni zaidi ya Sh6 milioni kwa mwezi.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi wa Tanzania hayako wazi. Watanzania hawajui kila mwezi Rais, Makamu wa Rais na viongozi wakuu wa Serikali wanalipwa kiasi gani? Malipo ya wabunge pia hayako wazi?” alihoji.

Profesa Lipumba ambaye amewahi kuwa msaidizi wa Rais katika masuala ya uchumi kati ya mwaka 1991 na 1993, alisema kwa kuwa Rais Magufuli amejivisha joho la kuwa Rais wa wanyonge, anawajibika kuwaeleza Watanzania mshahara na marupurupu yake.

“Ikiwa mshahara ni mkubwa sana achukue hatua za kuupunguza kama alivyofanya Mwalimu Nyerere mwaka 1965.”

Hata hivyo, alisema kifungu cha Katiba cha 43 (2) kinaeleza kuwa mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais havitapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba.

Profesa Lipumba alisema Rais Magufuli akitaka kupunguza mshahara wake itabidi kwanza abadilishe kifungu hicho cha Katiba.

“Anaweza kujitolea mchango wa kudumu utakaokatwa kutoka kwenye mshahara wake kusaidia sekta ya afya au elimu,”alisema.

Profesa Lipumba ambaye ni mshauri wa Benki ya Dunia (WB) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika masuala ya uchumi, alisema ili kuimarisha utawala bora ni muhimu uongozi ulio madarakani utumie mamlaka waliopewa kwa manufaa ya Taifa.

“Mishahara na marupurupu ya viongozi yawe wazi na yaamuliwe na kupangwa na taasisi iliyo huru. Kuweka utaratibu ulio wazi wa kuamua mishahara na marupurupu ya viongozi wa umma wakiwamo Rais na makamu wake, mawaziri, wabunge, majaji, makatibu wakuu na viongozi wengine,”alisema.

Alisema ni muhimu katika ujenzi wa utawala bora, uwajibikaji na uwazi wa viongozi wa umma kwa wananchi wanao waongoza.

“ Inasemekana mshahara wa mbunge katika Bunge lililopita ulikuwa Sh3.4 milioni kila mwezi.Pia mbunge alilipwa Sh8.2 milioni, nyingine kama posho ya jimbo, gharama za ofisi, mafuta, malipo ya wasaidizi wake na dereva.

“Vile Vile, mbunge anapohudhuria kikao cha Bunge alilipwa posho ya Sh80,000 za kujikimu, Sh50,000 za mafuta ya gari na Sh200,00 za kuhudhuria kikao cha Bunge, jumla ni Sh330,000 kwa siku.

“Posho ya siku moja ya mbunge ni zaidi ya mara mbili ya kima cha chini cha mshahara wa Serikali kwa mwezi mzima ambacho ni Sh150,000. Mishahara inakatwa kodi, marupurupu hayakatwi kodi,”alisema.

AY Awashangaa TCRA kwa Kuifungia Video ya zigo Remix..Alichosema Kiko Hapa.

$
0
0
Baada ya kuwepo taarifa kuwa video ya A.Y,Zigo aliyomshirikisha Diamond imefungiwa na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA kutokana na kutokuwa na maadili,msanii huyo amekiri kupokea barua kutoka kwa mamlaka hiyo.

Hata hivyo AY ameshangaa hatua hiyo na kuhoji ni maadili yapi ambayo hayajazingatiwa kwenye video hiyo,na pia mbona hawafungii video za nje ambazo zinakiuka maadili zaidi.

“Unajua unavyo shoot una shoot kama maudhui ilivyo,huwezi ukavaa suti jangwani au ukavaa overall kwenye swimming pool..na mavazi ya swimming pool yako kila sehemu hata katika taarifa ya habari tunayoona kwenye vipindi vya michezo kama wao pia wanakiuka habari nitakubaliana nao..kama wanafungia wimbo wa zigo na kuacha za kina nick minaj ni sawa kama wanaona maadili ya kina Nick Minaj yako sawa na kina Ay ndo mabaya,inabidi kukubaliana nao” alifunguka Ay

Hata hivyo Innocent Mungi kutoka TCRA hakutaja moja kwa moja kuwa video hio umefungiwa bali wametoa barua kwenda kwa vituo vinavyorusha matangazo ya Tv kuwa wasimamie kanuni za maudhui ya utangazaji kusitisha kurusha nyimbo zote zinazokiuka kanuni hizo

Meneja wa Shirika la Posta Tanzania Afikishwa Mahakamani Kwa Matumizi Mabaya Ya Ofisi

$
0
0
Meneja wa Shirika la Posta Tanzania (TPC) Mkoa wa Dar es Salaam, Lawrence Mwalumwelo na wenzake wawili wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka ya matumizi mabaya ya madaraka.

Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Sophia Nyanda akishirikiana na Veronica Chimwanda mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage aliwataja washtakiwa wengine kuwa ni Ofisa Tawala, Modester Fumbuka na Ofisa Manunuzi, Radecunda Massawe, wafanyakazi wa TPC.

Chimwanda alidai kuwa kati ya Agosti Mosi na Oktoba 31, 2010 washtakiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kwa kuipa mkataba wa kutafuta vibarua kampuni ya Technical Merchantile Service bila kupata kibali kutoka bodi ya zabuni.

Vilevile ilidaiwa kuwa Septemba 26 ,2011 washtakiwa hao walitumia vibaya madaraka yao kwa kuiongezea kampuni hiyo mkataba wa kutafuta vibarua kutoka Septemba 30 hadi Desemba 31, 2011 bila ya kuishirikisha bodi hiyo.

Ilidaiwa kuwa Januari Mosi, 2012 washtakiwa hao waliiongezea tena kampuni hiyo mkataba wa kutafuta vibarua kutoka Januari Mosi, 2012 hadi Machi 30, 2014 bila ya kuishirikisha bodi hiyo. Washtakiwa hao walikana mashtaka.

Washtakiwa hao waliachiwa baada ya kutumiza masharti ya dhamana na kesi hiyo kuahirishwa hadi Machi 17.

Picha: Mrembo Huyu Ana Hips Kubwa na Umbo la Kuvutia Kuliko Wote Kenya?

$
0
0
Ana umbo namba nane anawachanganya… Ama kama alivyosema Diamond kwenye Zigo Remix – Usiombe akapita na khanga, nyuma figusu majanga, ana mwendo wa kung’onya, tena alivyoshona, umbo kama katuni wa kuchora – Ni Grace Sowairina Msalame.







Mwanamkakati wa Maalim Seif Aswekwa Ndani Na Jeshi La Polisi Zanzibar

$
0
0
Mwanamkakati  wa aliyekuwa mgombea urais wa Zanzibar, Mohamed Sultan Mugheiry, maarufu kwa jina la Eddy Riyami, amewekwa ndani na Jeshi la Polisi mjini Unguja kwa tuhuma za kumtukana Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.

Eddy Riyami ambaye ni mmoja wa wana mkakati wa timu ya ushindi wa aliyekuwa mgombea urais wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alikutwa na mkasa huo jana baada ya kuitwa polisi kutoa maelezo kutokana na tuhuma zinazomkabili.

Riyami ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Maridhiano Zanzibar, alikwenda Polisi Makao Makuu kuitikia wito wa Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, SSP Simon Pasua, huku akiandamana na Mwanasheria wa CUF, Masoud Faki Masoud.

Mwanasheria huyo jana alisema Riyami anatuhumiwa kwa kosa la matumizi mabaya ya kimtandao.

Alisema licha ya kuzikana tuhuma hizo, lakini Jeshi la Polisi bado lilimshikilia kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Ni kweli ameshikiliwa na polisi kwa ajili ya kupitisha uchunguzi na yupo Polisi Madema, eti Eddy kaambiwa kamtukana Dr. Shein kwenye ‘audio’ ambayo hata si sauti yake, lakini dhamana ipo wazi na tutamchukulia dhamana,” alisema Masoud.

Akizungumzia kukamatwa kwa Riyami, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Salum Msangi, alithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

“Kitu ninachoweza kuthibitisha ni kuwa tunamshikilia Riyami kwa ajili ya kupitisha uchunguzi,” alisema Naibu Kamishna Msangi.

Februari 15, mwaka huu Ofisi ya Mkurunzi na Makosa ya Jinai, ilimwandikia Riyami barua ya wito na kumtaka kufika ofisi ya upelelezi iliyopo Makao Makuu ya Polisi Zanzibar.

Riyami alitii wito huo ambapo wiki iliyopita alikwenda lakini mmoja wa maofisa wa Jeshi la Polisi aliyemwandikia barua alikuwa nje ya Zanzibar kwa shughuli za kikazi na kumtaka kwenda jana jumatatu

Riyami si mwanachama wa CUF, lakini mara kadhaa amekuwa akitumiwa na chama hicho kwa ajili ya mikakati mbalimbali pamoja na ushauri.

Ray C Aeleza Jinsi Magazeti ya Udaku yanavyo Mliza Mama yake

$
0
0
Rehema Chalamila ‘Ray C’ amesema mama yake amekuwa akipatwa na presha mara kwa mara kutokana na habari anazo ziona kwenye magazeti ya udaku kuwa mwanae amerudia matumizi ya madawa ya kulevya.

Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Television, Ray C amesema mama yake hana amani kutokana na mambo yanayo andikwa kwenye magazeti ya udaku.

“Mimi naweza nikasema nakushtaki, wewe una hela zaidi na unaweza ukanishinda, your powerful get a gun watu wanifyatue na wampige mama yangu, maana mama yangu yupo hospitali ana presha kwa sababu ya gazeti yake,” alisema Ray.

Wiki chache zilizopita gazeti la Ijumaa liliandika habari kuwa mwanadada huyo alionekama mazingira fulani ambayo yanadaiwa kupatikana madawa ya kulevya.

Jerry Muro Atoa Mpya ''Simba si Washindani Wetu Tena...Watabaki Kuwa Watani Wetu Kama Wagogo na Wasukuma"

$
0
0
Klabu ya soka ya Yanga imetangaza rasmi kuwa kuanzia leo wekundu wa Msimbazi Simba si washindani wao tena bali ni watani wa jadi kama walivyo wasukuma na wagogo.

Tamko hilo limetolewa hii leo na mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa wanajangwani hao Jerry Muro wakati akitoa salam za pongezi kwa wachezaji, benchi zima la ufundi na wanachama kwa kufanikisha kile walichokifanya Jumamosi iliyopita kwenye mtanange wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara walipoinyuka 2-0 Simba.

Aidha Muro ameongeza kuwa kwa sasa wanachotazama ni shughuli tatu zilizo mbele yao mechi ya kombe la shirikisho dhidi ya JKT Mlale, mchezo wa klabu bingwa barani Afrika dhidi ya Cercke de Joachim ya Mauritius na mechi dhidi ya Azam ikiwa ni ya ligi kuu Tanzania bara.

Aidha amesema kuwa kikosi cha Yanga kimeanza mazoezi katika uwanja wa chuo cha polisi Kurasini kwa ajili ya mchezo wa kombe la shirikisho dhidi ya JKT Mlale Jumatano na mara baada ya mchezo huo kitaendelea na maandalizi ya mechi ya marudiano dhidi ya Cercle de Joachim.

Mapenzi Ndio Basi Tena...Wema Sepetu Afuta Picha zote za Aliyekuwa Mpenzi wake Idris Sultan Kwenye Page yake ya Instagram

$
0
0
Looks like there is trouble in paradise.. Katika hatua ambayo wengi hawakuitarajia kama ingetokea mapema hivi, Wema Sepetu na Idris Sultan wanaonekana kuuvunja uhusiano wao.

Tetesi za kuwa uhusiano wao upo kwenye mawe zilianza baada ya ujauzito ambao Wema Sepetu alidaiwa kuwa nao kutoka.

Haijulikani ni nani kamkosea mwenzake lakini inaonekana kuwa ni Wema ndiye aliyechukia zaidi kiasi cha kuamua kufuta picha zote za Idris alizowahi kuzipost kwenye akaunti yake ya Instagram.

Wema aliwahi kueleza wazi jinsi ambavyo Idris alikuwa akimpenda Idris na namna alivyomfanya awe mtu mwema.

IDRIS SULTAN: NILIKUWA NAWAPENDA WEMA NA SAMANTHA KWA WAKATI MMOJA, ‘I WAS A VERY BAD GUY

Hata hivyo Idris anaonekana bado moyo wake haujamkatia tamaa Miss Tanzania huyo wa zamani. Jumapili alipost picha akiwa naya na kuandika: Only you know how much i love you, the rest doesn’t matter. #BeingAMan.”

Wengi walikuwa wameanza kuvutiwa na uhusiano wao na waliamini kuwa wawili hao wangekuja kuwa miongoni mwa couple zenye nguvu zaidi. Walikuwa wamepanga pia kuja na reality TV show yao.

Mengi yazidi Kuibuka Kuhusu Nyalandu na Kampuni ya Uwindaji Ambayo Majangili Walitungua Helkopta yao na Kuuwa Mzungu...

$
0
0
Mambo mapya yameibuka kuhusu kampuni ya Kimarekani ya Friedkin Conservation Fund (FCF) ambayo majangili walidungua helikopta yake mwezi uliopita na kusababisha kifo cha rubani raia wa Uingereza, Roger Gower.
FCF inamiliki kampuni tanzu za uwindaji wa kitalii za Mwiba Holdings Ltd, Tanzania Game Trackers Safaris (TGTS) Ltd na Wengert Windrose Safaris.

Wakati helikopta hiyo ikidunguliwa kwa kile kinachoelezwa kwamba ilikuwa kwenye doria dhidi ya majangili, kumbukumbu zilizopo Wizara ya Maliasili na Utalii zinaonesha kuwa kampuni ya Mwiba Holdings Ltd ni miongoni mwa watuhumiwa wa ujangili
Uchunguzi unaonesha kumekuwapo matukio kadhaa ya wafanyakazi wa Mwiba kukamatwa wakiwa wameua wanyamapori na kukutwa na nyara za Serikali.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii vimesema mara zote kesi zinazoihusu kampuni hizo zimekwama kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni urafiki wao wa karibu na aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Nyalandu.

Urafiki wa Nyalandu na wamiliki wa kampuni hizo ulikuwa mkubwa kiasi cha kumpatia moja ya helikopta zake aitumie kwenye mbio za kuwania urais, kabla ya kushindwa na kujielekeza kwenye ubunge. Helikopta iliyodunguliwa na majangili ndiyo aliyoitumia wakati wote wa kampeni zake za ubunge

Nyalandu alimwamuru Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori wa wakati huo, Paul Sarakikya, kutoa Leseni ya Rais kwa familia ya Tom Friedkin (mmiliki wa kampuni hizi) kuwinda wanyamapori 700 katika vitalu vinane na eneo la wazi la Makao. Leseni hizo zilitolewa bure bila kulipiwa hata senti.
Miongoni mwa wanyamapori waliokuwa kwenye orodha ya kuuawa ni tembo walio katika hatari ya kutoweka.

Pia Nyalandu alikiuka sheria kwa kupuuza ukomo wa idadi ya vitalu vitano kwa kampuni moja. TGTS imemilikishwa vitalu vinane pamoja na eneo la wazi; hali ambayo ni ukiukwaji wa kifungu cha 38(7) cha Sheria ya Wanyamapori.
Kampuni hiyo pia ilipewa vitalu na Nyalandu kinyemela, ilhali sheria ikiagiza kuwa kitalu kinapobaki wazi sharti kitangazwe kwanza na waombaji washindanishwe katika mfumo na utaratibu ulio wa haki na uwazi [Kanuni ya Uwindaji wa Kitalii 18(1).

Pamoja na kutoa Leseni ya Rais, Wamarekani hao walileta watoto wadogo, chini ya umri wa miaka 18 kuwinda; jambo ambalo ni kinyume cha kifungu cha 43(3) cha Sheria ya Wanyamapori Namba 5 ya mwaka 2009.
FCF na kampuni tanzu imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makao kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama (Makao Ranch).

Kampuni ya Mwiba Holdings Ltd chini ya TGTS Ltd ambazo zinamilikiwa na Friedkin Conservation Fund (FCF) imekuwa ikiendesha shughuli za utalii kwenye eneo la Makao WMA tangu 2011 baada ya Mwiba Holdings Ltd kumilikishwa eneo jirani na WMA ya Makoa kwa ajili ya shamba la mifugo na wanyama.
Hata baada ya kumalizika Mkataba wake na JUHIWAPOMA, kampuni ya Mwiba Holdings Ltd iling’ang’ania na kuendelea kukalia eneo la Makao WMA kwa mabavu na kinyume cha sheria.

Source:Jamhuri/Jamii Forums

Waziri Nape Nnahuye Awashukia Startimes..Ataka Mkataba Wake na TBC Upitiwe Upya.

$
0
0
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ameitaka Bodi mpya ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kupitia upya mkataba wa StarTimes na shirika hilo.

Amesema kumekuwa na maneno kuhusu mkataba huo, hivyo bodi inapaswa kubainisha vifungu vya sheria ambavyo vitahitaji kufanyiwa marekebisho.

Akizungumza katika uzinduzi wa bodi mpya chini ya Mwenyekiti wake, Balozi Herbert Mrango, Nape alisema mapitio hayo yanaweza kufanyika ndani ya mwezi mmoja, kubaini mapungufu yaliyopo.

“Bodi hii inapokea majukumu yaliyoachwa na bodi iliyopita. Majukumu hayo ni pamoja na kupitia upya mkataba wa StarTimes na TBC kwani mkataba uliopo utaisha na utatakiwa kuwa na mkataba mpya,’’ alisema Nape.

Pia aliitaka bodi hiyo kuhakikisha kwamba baada ya miaka minne, TBC inajiendesha yenyewe kiuchumi kwa kuzingatia uwekezaji katika viwanja vyao.

Alisisitiza kuwa ni vyema bodi hiyo ikaangalia upya muundo wa shirika hilo na kwamba wawashirikishe wafanyakazi ili wajue nafasi zao.

Updates: Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Akana Kutoa Amri ya Kufuta Matokeo ya Uchaguzi Zanzibar

$
0
0
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete amesema hajahusika kufutwa kwa uchaguzi Zanzibar kwa kumpigia simu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.

Aliyasema hayo juzi mjini Kibaha wakati wa uzinduzi wa jengo la Ofisi ya Chama ya Kibaha Mjini mkoani Pwani na kusema maneno hayo ni ya uongo, hayana ukweli wowote na watu hawapaswi kutoa shutuma hizo juu yake.

Rais huyo wa Awamu ya Nne alisema maneno hayo hayana kichwa wala miguu wala hajawahi kumpigia simu Jecha kwa ajili ya kuzungumzia masuala ya kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kwani tume hiyo inajitegemea.

“Wasitoe lawama zisizohusika, wapuuzeni sikuwahi kufanya hivyo hata kwa Damian Lubuva wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania hivyo nashangaa watu wanavyosema kuwa nimehusika kufutwa uchaguzi huo,” alisema Kikwete.

“Tume ya Zanzibar ni tume huru na inajitegemea kwani ina mambo yake hata Dk Ali Mohamed Shein (Rais wa Zanzibar) hana uwezo wa kuingilia na kuahirisha uchaguzi huo, watu hao wasipake watu matope wasio husika kwani kila mtu ana nafasi yake,” alifafanua Kikwete.

Alisema kikubwa kinachotakiwa ni kuwaombea Wazanzibari wafanye uchaguzi wao mkuu wa marudio kwa amani na utulivu ili wapate viongozi wao wa kuiongoza Zanzibar na wawaombee wagombea wa CCM washinde.

Aidha, alisema chama hicho kinapaswa kuwaadhibu watu waliokihujumu chama wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kwa kutomwonea mwanachama, bali watende haki na si kwa kwa uonevu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Mwinshehe Mlao alisema Mbunge wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka ameonesha njia ya kiongozi kutumia fursa kuboresha mazingira ya utendaji kazi Awali, Koka ambaye ndiye aliyejenga ofisi hiyo yenye thamani ya Sh milioni 100, alisema aliamua kujitolea kujenga ofisi hiyo kwa lengo la kukisaidia chama kiendeshe shughuli zake.

Koka alisema aliamua kujenga kama kumbukumbu kwa wanaKibaha ili iwe kielelezo cha uongozi wake kama mbunge wa Jimbo hilo kwa ajili ya kufanya shughuli za chama badala ya kufanyia sehemu zisizo na hadhi yao
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live




Latest Images