Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

Breaking News : Rais Magufuli Amteua Balozi John Wiliam Kijazi Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.......Ombeni Sefue Atapangiwa Kazi Nyingine

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.


Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India.


Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine.


Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi  wa Mawasiliano, IKULU

Dar es Salaam


06March,2016

Ikulu Yavunja Ukimya Sakata la Umeya Dar

$
0
0

Ikulu imevunja ukimya kuhusu ile sinema ya kuahirishwa mfululizo kwa uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam kwa kusema haitaona tatizo lolote iwapo Halmashauri hiyo itaongozwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).


Uchaguzi huo utakapofanyika na vyama hivyo kushinda na kuongoza Jiji, Ikulu imesema, hakutaathiri hata kidogo shughuli zake za kila siku hivyo haina mkono wake kwenye sarakasi za uchaguzi huo.


Hayo yalisemwa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue, alipoulizwa  ni kwanini Ikulu isiingilie kati na kuamuru kufanyika kwa uchaguzi huo ambao umeshapigwa danadana muda mrefu.


“Hilo la hisia kwamba Ikulu ina mkono wake kwa kuhofia Ikulu kuwa chini ya Ukawa si kweli hata kidogo,” alisema Balozi Sefue.


 "Sisi tuogope nini wakati wao hawataathiri shughuli zetu za kila siku? Nakuhakikishia hatuoni tatizo lolote."


Kumekuwa na tetesi kwamba serikali inahofia upinzani kuchukua Jiji, kwani Ikulu ni kama itakuwa ndani ya eneo linalotawaliwa na wapinzani hali itakayoleta mgongano wa kiutendaji na kimaslahi.


Balozi Sefue alisema Jiji kuongozwa na Ukawa hakuwezi kuwanyima usingizi hata kidogo kwasababu iko miji mingi mikuu duniani ambayo inaongozwa na vyama vya upinzani na shughuli za Ikulu kwenye miji hiyo zinaendelea kama kawaida.


“Sisi hatuhofii na wala hatuoni sababu ya kuingilia uchaguzi huo ati kwa kuhofia Ukawa kuongoza Jiji, mbona miji mbalimbali duniani inaongozwa na vyama vya upinzani na mambo yanakwenda kama kawaida?" Alihoji.


"Sisi hatutakuwa wa kwanza duniani na wala hakuna kitakachobadilika.”


Kuhusu zoezi hilo kutawaliwa na ubabaishaji, Balozi Sefue alisema kwa sasa Ikulu haiwezi kuingilia kati na kulazimisha siku ya uchaguzi huo kwasababu wahusika wapo na hawajasema kama wameshindwa.


“Waziri anayehusika na Tamisemi yupo na hasema kwamba ameshindwa. Sasa kwanini sisi tuingilie suala lao?


"Mimi naamini hawajashindwa na wakishindwa wenyewe wanajua waende wapi kwa ajili ya ufumbuzi.


Mvutano wa Umeya wa Jiji umetokana na vyama vinavyounda Ukawa kuvuna madiwani wengi kuliko CCM katika jiji la Dar es Salaam hivyo kuwa na uwezekano mkubwa wa kutwaa Halmashauri ya Jiji, ikiwa uchaguzi huo utafanyika kwa uhuru na haki.


Jiji lina madiwani 76 wa CCM wakati Ukawa ina 87.

Tayari Halmashauri mbili kati ya tatu za Dar es Salaam zinaongozwa na Ukawa: Ilala na Kinondoni wakati CCM ikiongoza Temeke pekee.


Hata idadi ya wabunge kwa Dar es Salaam, Ukawa imeizidi kwa mbali CCM ambayo imepata wabunge wanne tu ambao ni Faustine Ndungulile wa Kigamboni, Issa Mangungu (Mbagala), Bona Kaluwa (Segerea) na Mussa Azan Zungu (Ilala).


Katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana Ukawa ilichukua majimbo ya Kawe linaongozwa na Halima Mdee (Chadema), Ukonga la Mwita Waitara (Chadema), Ubungo la Saed Kubenea (Chadema), Kibamba la John Mnyika (Chadema) na Kinondoni la Maulid Mtulia (CUF).


Katika kuonyesha kuwa sakata hilo bado ni moto, madiwani na wabunge wanaotoka Ukawa, juzi walivamia ofisi za Jiji wakishinikiza waambiwe tarehe ya uchaguzi huo.


Wanachama hao wa Ukawa walikaa kwa saa nzima kwenye ofisi hizo bila kupata jibu kutoka kwa wahusika na walisikika wakilaumu uongozi wa Jiji kuwa umepanga kuwahujumu.


Ingawa Ikulu ilisema kuwa haiwezi kuingilia suala hilo kwa kuwa Waziri husika hajashindwa, kuna dalili kwamba waziri mwenye dhamana amenawa mikono na hajui namna ya kutatua tatizo hio


Jiji liko chini ya Tamisemi ambayo iko Ofisi ya Rais hivyo kumekuwa na hofu kwamba iwapo Ukawa watachukua kiti cha Meya, kutakuwa na mgongano mkubwa wa sera na utekekelezaji wa ilani ya upinzani na ya Ukawa.


Vyama vya Ukawa vilishatoa angalizo hivi karibuni kwamba serikali inajaribu kutengeneza mgogoro ili kumpa nafasi Rais John Magufuli kuvunja Halmashauri ya Jiji na kuunda tume ya jiji.


Sheria ya Tamisemi ya mwaka 1982 inampa mamlaka Rais kuvunja Halmashauri ya Jiji/Mji/Manispaa na kisha kuteua tume.


Mwaka 1996, Fredrick Sumaye, akiwa Waziri Mkuu, aliivunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuunda tume iliyoongozwa na Charles Keenja.


Wiki iliyopita ziliibuka vurugu za kurushiana makonde kati ya wafuasi wa Ukawa na Polisi kufuatia kuahirishwa kwa uchaguzi huo kutokana na madai ya kuwepo zuio la muda Mahakama lilowekwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambalo baadaye ilibainika kwamba lilikuwa feki.


Kabla ya wiki iliyopita, uchaguzi wa Meya wa Jiji ulishaahirishwa mara moja kwa sababu za kiujanja ujanja kutokana na pingamizi la CCM.

Rais Magufuli Ampiga Chini Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue.....John Kijazi Kateuliwa Kuchukua Nafasi Yake

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amemteua Balozi Mhandisi John William Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. 

Kabla ya uteuzi huo Mhandisi Kijazi alikuwa Balozi wa Tanzania nchini India. Kufuatia uteuzi huo, aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi  wa Mawasiliano,
 IKULU-Dar es Salaam
06March,201
Katibu Mkuu Kiongozi Mpya, Balozi John William Kijazi

Serikali Yaanzisha Mfumo Mpya Wa Malipo Ya Mishahara Kwa Watumishi Wa Umma

$
0
0
SERIKALI imeanzisha mfumo wa Kielektroniki wa malipo ya mishahara kwa watumishi wa umma ambao unalenga kuondoa tatizo la madai ya malimbikizo ya stahili zao.

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa jana (Jumamosi, Machi 5, 2016) wakati akizungumza na watumishi wa sekta mbalimbali  katika wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu.

Waziri Mkuu alisema mfumo huo ujulikanao kama LAWSON, unatumika kwenye ajira za watumishi wote nchini, wa Serikali Kuu na wale wa Serikali za Mitaa

Waziri Mkuu alisema mfumo huo unasaidia kutunza, kutuma na kuhuisha  taarifa za watumishi kwa wakati na kwa ufanisi tangu mtu anapoajiriwa hadi inapofikia wakati wa kupandishwa madaraja na hadi anapostaafu.

Kabla ya kuanzishwa kwa mfumo huo, maafisa utumishi walipaswa kukusanya taarifa za watumishi wote walioajiriwa na kuzipeleka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma ili zikathibitishwe kabla ya kuzipeleka HAZINA kwa maandalizi ya mishahara.

Akitolea mfano wa kada ya ualimu, Waziri Mkuu alisema ajira za walimu zilikuwa zinaanzia Idara ya Utumishi wa Walimu  (TSD)  lakini anapaswa aende kuripoti kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  (DED) ambaye ni mwajiri wake chini ya TAMISEMI.

 "Hii ilileta ugumu wa malipo ya kupanda madaraja, uhamisho ama likizo kwa sababu mwajiri anakuwa hajatenga hizo fedha."

"Sasa hivi tuna Tume ya Utumishi wa Walimu  (TSC) ambayo iko chini ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri. Kwa hiyo ni rahisi wao kukaa pamoja na kuamua tuwapandishe daraja walimu 10 na wote hao wakalipwa bila bila kuchelewa," alisema.

Alisema mfumo huo umeanza kutumika tangu mwaka 2012 na ulianza kwa ajira mpya za walimu na hadi sasa umethibitisha kuwa inawezekana kumlipa mtumishi mshahara wake hata kama ameajiriwa ndani ya mwezi huohuo.

"Kama mtumishi anaripoti kwenye kituo kipya hata iwe wilaya ya wapi ili mradi amefika na barua zake zote na ziko sahihi mtu huyu ataingiziwa taarifa zake na wakati huohuo taarifa zitaonekana Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na pia zitapokelewa kwa maafisa wanaoshughikia mishahara kule HAZINA."

Alisema changamoto pekee waliyokutana nayo wakati mfumo huo umeanza ilikuwa ni kutoingizwa taarifa za wale ambao wameripoti baada ya tarehe 10 ya mwezi husika.

"Hii ni kwa sababu matayarisho ya mishahara yanakuwa yameshaanza. Kwa hiyo wengi walishauriwa kuripoti kati ya tarehe 25 hadi tarehe 9 ya mwezi uliofuata na wote hawa hawakupata matatizo ya kucheleweshewa mshahara," alisema.

Akifafanua kuhusu upandishaji madaraja ya watumishi, Waziri Mkuu alisema  Serikali imeondoa utaratibu wa mtumishi kulazimika kuandika barua ya kukiri kupandishwa daraja/cheo ndipo aanze kupata stahili zake mpya.

"Hii imeondoa ucheleweshaji wa kufanyika marekebisho ya mshahara  na pili imeondoa tofauti za mishahara kwa watumishi wenye ngazi moja (sifa sawa za kitaaluma, tarehe moja ya kuajiriwa) ambao walikuwa wakilipwa tofauti kwa sababu mmoja aliwahi kuandika barua ya kukiri na mwingine alichelewa kuandika barua hiyo hiyo " alisema

AKATISHA ZIARA KUTOKANA NA MSIBA
Wakati huohuo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amelazimika kukatisha ziara ya mkoa wa Simiyu ambayo ilikuwa imalizike kesho kutokana na msiba wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambayo alipangiwa kuitembelea leo.

Mkurugenzi huyo Bw. Traceas Kagenzi alifariki dunia usiku wa kuamkia jana kutokana na shinikizo la damu. Atasafirishwa kwenda Muleba  kwa mazishi.

Akitoa salamu za rambirambi kwenye ibada ya kumuombea marehemu Kagenzi iliyofanyika nyumbani kwake Maswa mjini, Waziri Mkuu alisema ameshtushwa na msiba huo uliotokea ghafla na kwamba Taifa limempoteza mtumishi mahiri ambaye bado Taifa lilikuwa likimtegemea.

"Nimeshtushwa sana na taarifa za msiba huu. Nimeambiwa hadi juzi usiku alikuwa akishirikiana na Mkuu wa Wilaya hii kuandika taarifa ya ziara ya wilaya hii. Kwa niaba ya Serikali, ninawapa pole sana wafiwa na Mungu awape uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi," alisema.

"Nimelazimika kukatisha ziara ya mkoa huu kwa sababu huyu ni mtumishi mwenzetu" alisema Waziri Mkuu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, MACHI 6, 2016.

Mzungu/Muitaliano Aliyehusishwa Kwenye Scandal ya Mwamvita na January Makamba Akanusha Adai January Ahusiki..

$
0
0
Mzungu/Muitaliano Aliyehusishwa Kwenye Scandal ya Mwamvita na January Makamba Akanusha Adai January Ahusiki..

Soma Alichoandika...... 

Mange Kimambi Afunguka Baada ya Mtaliano Kuandika Barua ya Kuwashafisha January na Mwamvita Makamba....

$
0
0



"Mangekimambi_ hii ndio Tanzania yetu. Mlalamikaji ambae a few hrs before aliingia Twitter Na kumtishia January Kuwa atae expose na Safari Yao ya Dubai amesainishwa na barua na wana sheria kabisaa ya kumsafisha January Makamba! . .

Have you guys seen anything like this before?? Does it make sense?? a few hrs before mlalamikaji anatoa vitisho hadharani then anafanya a complete 100% turn around , akili kichwani kwako Mtanzania! Wow! Anyways, like I said any reasonable average person anaelewa what happened, you don't need to be a genius. Yani hata Waziri Mkuu na Rais wakiamua kumwacha January ni vile waamue but from zile audio za Mwamvita, to interview ya January hata wao wanajua January is guilty as charged!

Barua yenyewe wamemuandikisha fasta Mpaka wamekosea date

Hata wasipomchukulia hatua Ila In 2020 we will not forget , voice note bado zitakuwepo, email bado zitakuwepo, interview ya January bado itskuwepo Na tutawakumbusha Watanzania " Mange

Ni Kipi Hasa Kilichomuondoa Balozi Ombeni Sefue Ikulu? Atapangiwa Kazi Gani Nyingine?

$
0
0
Tumekuwa tukipaza sauti kuwa mtu anayeondolewa kwenye nafasi yake ya utumishi basi ni lazima zitolewe sababu za msingi za kuondolewa kwake! Haiwezekani katibu mkuu kiongozi anaondolewa kimyakimya tu huku tukiwa hatupewi sababu za kuondolewa kwake!

Kiongozi huyu alikuwa akitoa matamko mbalimbali huku rais Magufuli mwenyewe akituaminisha kuwa ni mtu wa viwango na anayekidhi kile anachokiita "speed yake" Leo kulikoni?

Hatupingi kuondolewa kwa watu hawa kama wamefanya makosa! Lah! Tunapinga namna wanavyoondolewa huku kukiwa na sintofahamu ya hali ya juu!

Tulishuhudia Daktari Hoseah akitenguliwa uteuzi wake kimyakimya! Pia wapo watumishi wengine wengi huku mambo lukuki yakifichwa!

Sasa leo tunaambiwa kuwa Ombeni Sefue atapangiwa kazi nyingine? Ipi? Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo cha nne kwenye mhimili wa serikali! Atapangiwa kazi gani? Waziri mkuu? Makamu wa rais? Rais? Kutumbuliwa kwake kunaonyesha kuwa alikuwa na kasoro katika utendaji wake na si vinginevyo! Zipi?

Hali hii ya kufukuzana kimyakimya inaweza kuzua uhasama wa aina yake nchini! Kwanini mtu akifukuzwa na au kusimamishwa kazi zisitolewe sababu za msingi zilizopelekea kuondolewa? Nini tatizo? Tunajenga nini?

Angalizo kwa wana JF: Wakati Ombeni Sefue akitoa matangazo mbalimbali wengi wenu mlikuwa mkishangilia! Wengine mkadiriki kuandika kuwa Ombeni, Magufuli na Majaliwa wanatosha kuendesha nchi! Mkasema kuwa hakuna haja ya baraza la mawaziri! Leo Ombeni Sefue anatenguliwa mnashangilia kwa maandiko mbalimbali! Mmesimamia wapi? Hamuoni kasoro za wazi kwenye huu utenguaji wa watumishi (baadhi yao? ) Mimi ni miongoni mwa wale tunaoamini kuwa, kama ni kusafisha kwa kwelikweli! Hata Magufuli mwenyewe ni jipu!

Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya March 7, Ikiwemo ya Balozi Ombeni Sefue Kutumbuliwa Jibu

$
0
0
Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya March 7, Ikiwemo ya Balozi Ombeni Sefue Kutumbuliwa Jibu


Ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA 2016 utaziongezea pumzi filamu za Kibongo

$
0
0
Tuzo za Africa Magic Viewers Choice Awards, ni sawa na Oscars za Afrika. Ndiyo tuzo kubwa zaidi zinazoikutanisha tasnia ya filamu Afrika nzima pamoja.

Utofauti kati ya tuzo za Oscars na AMVCA ni kuwa tuzo za Oscar zinaikutanisha industry ya filamu ya Marekani iliyounganika pamoja, Hollywood bali AMVCA ni tuzo zinazokutanisha industry ndogo ndogo za nchi za Afrika.

Na kwa kiasi kikubwa tuzo za AMVCA ambazo mwaka huu zimetolewa kwa mwaka wa nne zimetawaliwa na Nollywood na kwa mbali tasnia ya filamu ya Afrika Kusini. Kwa kuona hivyo, waandaji walitengeneza tuzo za kikanda na za lugha maalum. Ndiyo maana kuna tuzo ya filamu ya Kiswahili na ya Afrika Mashariki.

Kwa mwaka huu tuzo hizo zote zimekuja Tanzania, ambapo Single Mtambalike maarufu kama Richie ameshinda kipengele cha filamu ya Kiswahili kupitia Kitendawili. Elizabeth ‘Lulu’ Michael alishinda kipengele cha filamu bora ya Afrika Mashariki, kupitia Mapenzi.

Na tumeshuhudia wenyewe kuwa ushindi huu umeshangiliwa zaidi na kurejesha imani katika filamu zetu. Ushindi wa Lulu na Richie unatupa moyo wa kuamini katika kazi za wasanii wetu. Ushindi huu umekuja katika kipindi ambacho tasnia ya filamu ya Tanzania imeshuka kwa kiasi kikubwa katika pande nyingi. Imeshuka kwenye mauzo na usambazaji kiasi ambacho wasambazaji wakubwa wamepunguza kasi ya kusambaza kazi kama zamani na kuwafanya waigizaji wengi kubaki na filamu zao mkononi wasijue namna ya kuzisambaza.

Ni kwasababu ni watanzania wachache wenye muamko wa kutoa fedha mfukoni na kununua filamu za nyumbani. Pengine kwasababu ya utandawazi ambapo tumekuwa ‘exposed’ na filamu bora kutoka Hollywood, imekuwa ngumu sana kuziamini filamu za nyumbani hasa tunapotaka kuzifananisha. Kuna sababu nyingi sana zinazochangia tuziweze kufikia hata asilimia 10 ya ubora wa filamu za wenzetu. Uchumi, teknolojia, ujuzi, elimu, utafutaji na unolewaji wa vipaji kwenye filamu na mambo mengine kibao yanaifanya tasnia yetu iendelee kudoda.

Lakini pengine kama tukiamua kuweka nguvu kwenye vitu vinavyowezekana kama vile kutengeneza filamu zenye story nzuri na zilizobeba uhalisia pamoja na uchaguzi mzuri wa wahusika watakaowasilisha maudhui kwa ufahasa, watanzania wanaweza kushawishika kuzinunua filamu za nyumbani. Inabidi filamu zianze kutengeneza mjadala kama ambavyo muziki wa Bongo Flava umefanikiwa. Kwamba Ray akitoa filamu yake, watu waijadili kwenye mitandao ya kijamii kama ambavyo Diamond au Alikiba na wasanii wengine wakiachia video zao.

Tukirudi kwenye ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA, naamini kuwa umepeleka ujumbe Afrika kuwa Tanzania ina kitu. Kama ambavyo kimuziki tunaonekana kuwa vizuri, ni kwa kushinda tuzo kama hizi kunawashtua watu wa pande zingine za Afrika kuwa kumbe nasi tumo.

Cha msingi ni wasanii wetu kuongeza spidi zaidi kwa kutengeneza filamu ambazo hata kama zitatajwa kuwania tuzo hizo, zisiishie tu kuwekwa kwenye vipengele maalum, bali pia kwenye vipengele vya jumla. Tunapenda kuona siku moja Lulu, Kajala, Wema Sepetu, Nisha au Shamsa Ford wanashindana kwenye tuzo moja na Genevieve Nnaji wa Nigeria au Yvonne Nelson wa Ghana.

Tunapenda kuona siku moja Ray, Richie, JB au Hemedy wanashindana kwenye tuzo moja na Ramsey Noah wa Nigeria au Van Vicker wa Ghana.

Mimi ninaamini kuwa ushindi wa Lulu na Richie kwenye AMVCA 2016 utaziongezea pumzi filamu za Kibongo

Wema, Kajala Acheni Utoto Bwana!

$
0
0
KWENU warembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ‘Madam’ na Kajala Masanja. Habari zenu binafsi? Bila shaka ni wazima wa afya na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku. Kitambo kidogo sijawaona lakini naamini pumzi ya bure mnaendelea kuivuta ndiyo maana nasikia matukio yenu kwenye vyombo vya habari.

Mkitaka kujua afya yangu, mimi ni mzima. Namshukuru Mungu naendelea na shughuli zangu kama kawaida. Mungu ni mwema sana, anaendelea kubariki kazi ya mikono yangu, namuomba yeye aendelee kunibariki zaidi na zaidi.

Dhumuni la kuwaandikia barua hii ni kutaka kuwakumbusha kwamba nyinyi kwa sasa ni watu wazima. Umri wenu unatosha kabisa kusema haufanani na yale matukio yasiyokuwa na kichwa wala miguu. Mara kadhaa nimewahi kuwaambia, hata yale mashindano yenu ya kumwaga fedha ukumbini, nyakati hizi si zake.

Mambo ya kuibiana mabwana kama yalishatokea, itoshe sasa kusema ulikuwa ni ujana. Kwa kuwa ilitokea, hakuna namna zaidi ya kuyasahau na kuchapakazi. Soko lenu la filamu bado haliridhishi, lakini mnapaswa kukomaa ili angalau mtengeneze fedha kupitia kazi zenu na si kuhongwa.

Binafsi sikufurahishwa na tukio lenu la kukutana ukumbini na kuzinguana mbele ya kadamnasi lililoripotiwa wiki iliyopita na magazeti Pendwa. Lilikuwa tukio linaloonesha kwamba bado hamjakua kitu ambacho sitaki kukiamini.

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, huu siyo wakati wa nyinyi kuoneshana ubabe wa fedha. Kwamba eti kwa kuwa mwenzako kaenda kutunza msanii jukwaani, na wewe lazima utunze nyingi zaidi ili uonekane wewe ni zaidi.

Ndugu zangu, bahati nzuri maisha  yetu tunajuana. Kwa kiasi kikubwa natambua maisha ya wasanii wetu nchini hususan warembo. Wengi wenu hamtegemei sanaa kuendesha maisha yenu. Wengi mnategemea  mapedeshee au ‘mabwana’ kutamba mjini.

Niwashauri hizo fedha mnazozipata ni bora mngewekeza kwenye sanaa yenu. Mkajizatiti vizuri ili ziweze kuzaliana. Mnapigana ili iweje? Mnatambiana mbele za watu inawasaidia nini. Wenzenu wanapigana siku hizi wanaingiza fedha.

Nyinyi kazi yenu si ubondia. Kazi yenu ni uigizaji. Igizeni kwelikweli na Watanzania wawaunge mkono kwa kununua kazi zenu. Sanaa yenu ina changamoto nyingi, mnawezaje kuzishughulikia ikiwa hamna umoja.

Mtawezaje kutatua changamoto hizo ikiwa hamna upendo kati yenu? Si rahisi kutatua changamoto hizo wakati mna chuki. Ili mfanikiwe, mnahitaji kushirikiana. Shirikianeni ili muweze kuisogeza sanaa mbele, acheni vita ya kipuuzi mnayoendelea kuifanya.

Mkizingatia hayo niliyowaambia, hakika tutaona mabadiliko kwenu na sanaa kwa ujumla. Nina imani nyinyi ni watu wazima na mtajipanga upya na mtaanza kuchapa kazi kama kauli mbiu ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli, ‘Hapa Kazi Tu’.

Ni mimi mtu wenu,

Erick Evarist.

GPL

Mbwana Samatta Aonja Machungu Kwa Mara ya Kwanza Kwenye Timu yake Mpya ya Genk..

$
0
0
Nyota wa Tanzania Mbwana Samatta na klabu yake ya Genk walitoka vichwa chini baada ya timu yao kuchapwa bao 2-1 na klabu ya Standard Liege kwenye mchezo wa ligi kuu ya Belgium uliochezwa usiku wa Jumamosi March 5.

Genk wakiwa ugenini ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao dakika ya 42 kipindi cha kwanza likifungwa na Nikolaos Karelis na kuipeleka Genk mapumziko ikiwa kifua mbele kwa bao 1-0.

Dakika tatu baada ya kipindi cha pili kuanza, Ivan Santini akaisawazishia Standard Liege kabla ya Jean-Luc Diarra Dompe kuifungia Standard bao la ushindi na kupeleka msiba kwa Genk.

Kama kawaida Samatta iliingia uwanjani dakika ya 81 kuchukua nafasi Karelis lakini bado haikutosha kubalili matokeo.

Samatta anaishuhudia klabu yake ya Genk ikipoteza kwa mara ya kwanza tangu ajiunge nayo mwezi January akitokea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemrasia Kongo.

Video: Rais Magufuli Akimtangaza Katibu Mkuu Kiongozi Mpya Baada ya 'Kumtumbua' Ombeni Sefue

$
0
0
Video ya Rais Magufuli  akimtangaza John Kijazi Kuwa Katibu mkuu Kiongozi kuchukua nafasi ya Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine

Picha za Mwigizaji Rich Richie Alivyotua Airport Baada ya Kushinda Tuzo ya Filamu Nchini Nigeria

$
0
0
Usiku wa March 5 tasnia ya Bongo Movie iliingia kwenye headlines Lagos Nigeria, baada ya wasanii wawili kushinda tuzo za Africa Magic Viewer’s Choice Awards2016 zilizotolewa Lagos Nigeria, Single Mtambalike maarufu kama Rich Richie usiku wa March 6 kuamkia March 7 aliwasili Airport Dar na tuzo yake ya filamu bora yaKiswahili aliyoshinda Nigeria.


Aliyevaa kofia ni Prince na aliyeshika maua ni Darleen wote watoto wa Single Mtambalike.

Nafasi ya Mkurugenzi Mkuu NSSF ni Moto...Yakaa Siku 22 Bila Mkurugenzi wala Kaimu wake

$
0
0
Nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) inaonekana kuwa moto baada ya mfuko huo kumaliza siku ya 22 bila ya kuwa na mbadala wa Dk Ramadhan Dau au kaimu wake.

Jaribio la Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama kuziba nafasi hiyo kwa muda lilidumu kwa saa tano tu baada ya kulazimika kutengua uteuzi wa Carina Wangwe Alhamisi iliyopita.

Waziri Mhagama alilazimika kutengua uteuzi huo kwa maelezo kuwa taratibu zilikosewa huku Balozi Ombeni Sefue akieleza kuwa mkurugenzi huyo wa Tehama wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Jamii (SSRA) alitakiwa kuwa msimamizi tu na si kaimu mkurugenzi.

Jana, juhudi za gazeti hili kutaka kujua maendeleo ya uteuzi wa mtu mpya wa kushika nafasi hiyo ziligonga mwamba.

Balozi Sefue, ambaye hadi jana alasiri alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi, hakutaka kuzungumzia suala hilo akimuelekeza mwandishi kumtafuta Waziri Mhagama.

Lakini Waziri Mhagama hakuweza kupatikana licha ya kutafutwa mara kadhaa. Juhudi za kumpata kwa simu zilishindikana kwa kuwa hakuwa akipokea na hata alipotumiwa ujumbe hakujibu.

Pamoja na kuteuliwa kuwa balozi ambaye atapangiwa kituo baadaye, Dk Dau aliondoka NSSF kwa njia ambayo imewaacha wengi wakiwa midomo wazi.

Akiongoza kikao cha viongozi wa mikoa wa NSSF jijini Dar es Salaam, Dk Dau aliletewa taarifa kuwa alikuwa akihitajiwa na mtu muhimu na hivyo kulazimika kumuachia kikao mmoja wa wakurugenzi wake, kwa mujibu wa habari ambazo Mwananchi imezipata.

Dk Dau hakurejea tena kikaoni na baadaye habari zikitangazwa kutoka Ikulu kuwa ameteuliwa kuwa balozi pamoja na Asha Rose Migiro na Mathias Chikawe.

Habari zinasema kuwa wiki iliyofuata, Dk Dau alianza kuonekana ofisini kabla ya kutaarifiwa kuwa uteuzi wake ulianza mara moja hivyo aachane na kazi za NSSF.

Kutokana na mazingira ya kuondoka kwake, hakuna mtu anayekaimu nafasi yake kati ya wakurugenzi nane walio chini ya Mkurugenzi Mkuu wa NSSF.

Habari zinasema kuwa mazingira hayo yamesababisha kuzorota kwa shughuli za shirika hilo kubwa kuliko yote yanayojihusisha na hifadhi ya jamii.

Miongoni mwa mambo hayo ni ufunguzi wa daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam ambalo lilitakiwa lianze rasmi kutumika Machi Mosi, ununuzi wa magari ya ofisi za mikoa, mkutano wa wanachama wa mwaka pamoja na wiki ya NSSF ambayo hujumuisha mambo mbalimbali, kama shughuli za kijamii, maonyesho ya huduma za NSSF na michezo.

Wiki iliyopita Balozi Sefue alisema maswali kuhusu uteuzi wa kaimu yaelekezwe kwa Mhagama, ambaye alieleza wakati huo kuwa utaratibu wa kumpata kaimu ulikuwa unaendelea.

Kwa mujibu wa ripoti ya fedha ya mwaka 2011, shirika hilo lilikuwa na wanachama 501, 218, kati yao wafanyakazi waliosajiliwa waliongezeka kutoka 17,666 hadi 18,779, sawa na ongezeko la asilimia 6, huku michango ikiongezeka kutoka Sh300.08 bilioni hadi Sh356.5 bilioni kwa mwaka, ikiwa ni ongezeko la asilimia 18.8.

Kwa mujibu wa muundo wa uongozi wa NSSF, Mkurugenzi Mkuu ndiye kiongozi mkuu wa shirika akiwa na wakurugenzi nane chini yake.

Wakurugenzi hao wanahusika na uendeshaji (DO); utawala na rasilimali watu (DHRA); mipango, uwekezaji na miradi (DPIP); fedha (DF); teknohama (DIT); ukaguzi wa ndani (DIA); uthibiti na usalama wa mali (DARM) na huduma za kisheria (DLS).

Dk Dau, ambaye amebobea katika taaluma ya masoko, ameliongoza shirika hilo kwa miaka 15, tangu mwaka 2001 alipoteuliwa na Rais wa Serikali ya Awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.

January Makamba Hatihati Kutumbuliwa Jipu Kwa Ufisadi......Mange Kimambi Aapa Kupeleka Ushahidi TAKUKURU

$
0
0
Sakata la Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), January Makamba na Mdogo wake Mwamvita kudaiwa kupokea rushwa kutoka kwa raia wa Italia, Vincenzo Cozzolino ili wamsaidie kupata zabuni ya ujenzi limechukua sura mpya.

Sauti na jumbe mbalimbali zilizosambazwa na kuwekwa kwenye mtandao na mtu maarufu kwenye mitandao ya kijamii na mmiliki wa tovuti ya U-Turn, Mange Kimambi, raia wa Tanzania aishie Marekani, zinaonesha mazungumzo kati ya watatu hao, mwaka 2011. Jana, Mwamvita na Makamba walikiri kuwa sauti hizo ni za kweli.

Muitaliano huyo ambaye anadaiwa kumpa Mange Kimambe ushahidi wote wa mawasiliano kati yake na Ndugu hao, amejitokeza na kuwasafisha akidai kuwa hakuwahi kuwapa rushwa wala kuhusiana na January kibiashara.

Cozzolino ameandika ujumbe akidai kuwa ingawa yeye na Mwamvita walikuwa na uhusiano wa mapenzi mwaka 2011 na baadae kujiingiza katika biashara binafsi ambayo ilipelekea kugombana kwao, hawakumhusisha January kwa aina yoyote katika biashara yao.

“Sikuwahi kumuomba [January] kunisaidia katika biashara zangu. Sikuwahi kumpa fedha. Mara chache nilizokutana naye ilikuwa ni mazungumzo ya kawaida ya kijamii. Nilikuwa na uhusiano na Mwamvita. Uhusiano wetu ulikuwa bomba mwanzoni lakini ukawa na mwisho mbaya,” ameandika Cozzolino.

Awali, sauti ya January na mwandishi wa habari iliyosambazwa, January anasikika akieleza kuwa aliwahi kukutana mara moja Dubai na Muitaliano huyo na kwamba alitambulishwa kama mpenzi wa dada yake.

Alisema baadae dada yake alimwambia wameanza kufanya biashara ya kahawa na Muitaliano huyo na baadae biashara hiyo kufa huku ikiwaacha katika mzozo.

Kwa mujibu wa Kamamba, Muitaliano aliyekuwa ameweka nusu ya mtaji ambayo ni dola milioni 50, alianza kudai kiasi hicho cha fedha na sio vinginevyo.

Alisema kuwa awali, muitaliano huyo alikuwa anajaribu kumshawishi Mwamvita amkutanishe na viongozi wakubwa wa serikali ikiwa ni pamoja na Katibu Mkuu.

Hata hivyo, Mange Kimambe ambaye ndiye anayeeleza kuwa na nyaraka zote za ushahidi aliokabidhiwa na Muitaliano huyo na kwamba hivi sasa Muitaliano amelipwa na kukubaliana kumsafisha Mbunge huyo wa Bumbuli.

Mange amesisitiza kuwa ana ushahidi wote wa January na dada yake kupokea rushwa kutoka kwa mfanyabiashara huyo na yuko tayari kuwakabidhi Takukuru.

Chid Benz alimfanyia unyama Ali Kiba wakati wakirekodi wimbo ‘Hasira za Nini’

$
0
0
Rapper Chid Benz amesema wakati wanarekodi wimbo ‘Hasira za Nini’ aliyomshirikisha Ali Kiba, alimfungia ndani msanii huyo katika chumba cha kuingizia sauti ambacho kilikuwa na joto kali.
Ali Kiba na Chiz Benz

Akizungumza katika kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, Chid Benz alisema wakati wapo Mj Records wakirekodi kazi hiyo, Ali Kiba alidondosha chozi sababu yeye alimfungia mlango ndani na kumwambia hawezi kutoka mpaka atakapo maliza kuweka vocal.

“Unajua mdogo wangu Ali Kiba alipoingia booth mimi nikamfungia mlango kabisa ili asitoke so akawa analalamika maana mle ndani kulikuwa na joto sana, lakini nikamwambia mdogo wangu huwezi kutoka mpaka umalize kazi baada ya hapo akalia kisha akakaa zake chini baadae aliinuka na kuendelea na kazi mpaka mzigo ulipoisha ndio nikamfungulia mlango na kutoka,” alisema Chid Benz

Katika hatua nyingine Chid Benz amesema licha ya yeye kufanya muziki wa Hip hop, lakini alikuwa na mashabiki wengi wakike kutokana na sauti yake pamoja aina ya nyimbo alizokuwa akiimba.

“Unajua kwangu mimi niliweza kuwa na mashabiki wa kike wengi kutokan na ukweli kwamba wanawake wanapenda sana sauti nzuri na nzito na mimi Mungu amenijalia sauti lakini pia nilikuwa naimba sana mapenzi lakini napochana kwenye mapenzi nilikuwa sifanyi zile ngumu lakini kingine nilikuwa naweza kuyaelezea vizuri mapenzi,” alisema Chid Benz

Lulu Hakurudi Tanzania Jana… Ninacho Alichoandika Leo Kuhusu Kurudi Kwake Nyumbani na Tuzo

$
0
0
Tunajua ni Watanzania wawili walishinda tuzo mbili kwenye usiku wa tuzo za Africa Magic Viewer’s Choice Awards, wa kwanza ni Single Mtambalike ‘Richie’ na Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambapo Richie tayari alisharudi nyumbani Tanzania usiku wa March 6 2016 ila Lulu hakutokea Airport japo baadhi ya watu walimtarajia.

March 7 2016 Lulu amewajulisha Watanzania kwamba anarudi nyumbani siku ya March 8 2016 na atatua uwanja wa ndege Dar es salaam na akayaandika haya
 ‘Tukijaaliwa uzima…kesho saa 8:30 (saa nane na nusu Mchana) nitaingia uwanja wa ndege Dar Es Salaam na mzigo wenu😂au acha niseme Tuzo Yenu..!!💋💋💋Can’t wait to see y’all😍
(I’m hungry and I’m ready 4 change….TODAY👊)

HALI ya Kisiasa Zanzibar Yazidi Kuwa Tete...Ofisi 5 za CUF Zachomwa Moto

$
0
0
HALI ya kisiasa visiwani Zanzibar, inazidi kuwa tete huku siasa za visasi, chuki na uhasama zikionekana kurejea kwa kasi.

Hali hiyo imejitokeza baada ya ofisi za matawi matano ya Chama cha Wananchi (CUF) zilizopo Pemba na moja  Unguja kuchomwa moto na watu wasiojulikana.

Matukio ya kuchomwa moto kwa ofisi hizo yamekuja siku mbili baada ya watu wasiojulikana kuchoma moto maskani ya CCM ya Sauti ya Kisonge iliyopo mjini Unguja.

Hata hivyo Jeshi la Polisi visiwani humo limetangaza kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini watu waliohusika na matukio hayo.

Uchomaji huo ulifanyika usiku wa kuamkia jana saa 8 usiku, ambapo watu hao walichoma moto na kuteketeza nyaraka za chama hicho.

Matawi yaliyochomwa moto ni Kilimahewa mjini Unguja Wilaya ya Magharibi, Mkanyageni, Kiwapwa, Kiuyu Minungwini, Wingwi na Kinowe yote ya Kisiwani Pemba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Hassan Nassir, amethibitisha kutokeo kwa matukio hayo.

Amesema kutokana na hali hiyo tayari ameagiza askari wake kuanza uchunguzi wa tukio hilo haraka ili waliohusika watiwe nguvuni na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

“Ni kweli kuna hilo tukio ingawa kwa sasa nipo safari kuelekea Unguja na tayari nimeagiza kuanza kwa uchunguzi wa matukio haya ili wahusika waweze kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

“…siwezi kusema kama matukio haya yana uhusiano wa masuala ya kisiasa ingawa huu ni uhalifu kama uhalifu mwingine,” alisema Kamanda Nassir.

Akizungumzia tukio hilo, Mbunge wa Wingwi, Juma Kombo Hamad (CUF), alilaani tukio hilo huku akiwatuhumu wafuasi wa CCM kuhusika nalo.

Alisema hatua ya CUF kutangaza kutoshiriki uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20, mwaka huu imekuwa ikiwaumiza CCM.

“Haya mambo yapo wazi tumeumizwa vya kutosha lakini katika hilo mimi binafsi wala sifichi hapa kuna mkono wa CCM  na sisi hatutarudi nyuma tunaendelea na msimamo wa chama,” alisema Hamad.

Kauli ya Maalim Seif
Machi 4, mwaka huu, Akizungumza na wafuasi wake waliomtembelea nyumbani kwake, Katibu Mkuu wa CUF,  Maalim Seif Sharif Hamad, alisema yuko tayari kukamatwa kutokana na msimamo wake wa kutotambua uchaguzi wa marudio.

“Msidhani kuwa mtatupiga shavu la kulia tukawageuzia la kushoto. Kila mara tunaibiwa, tunapigwa, tunafanywa kila kitu. Tukisema kuwa watu wajilinde, inakuwa nongwa.

“…basi tunawaambia kuwa kuitwa polisi, kuwekwa ndani, kufunguliwa mashtaka ya bandia, hata kuteswa, hayo ni mambo yamekuwa yakitutokea tangu 1992 tumeshayazoea,” alisema Maalim Seif.

Alisema udhalilishwaji kama huo haujawahi kukirudisha nyuma chama chake, zaidi ya kukiongezea umashuhuri na ufuasi mkubwa visiwani Zanzibar, huku akilituhumu Jeshi la Polisi kwa kuwa ‘tawi la CCM’ ambalo litakuwa dhamana wa machafuko yoyote yatakayotokea.

Katika hatua nyengine, Maalim Seif ambaye alikuwa mgombea urais katika Uchaguzi wa Oktoba 25, mwaka jana  alirudia msimamo wa chama chake wa kutoshiriki kile alichodai uchaguzi wa marudio ulioitishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salim Jecha, Machi 20, mwaka huu.

Alisema yeye alishashiriki uchaguzi na kushinda na hahusiki kabisa na uchaguzi mwengine. “Ninamwambia Jecha kuwa uchaguzi huo ni wenu peke yenu,” alisema Maalim Seif.

Mrembo Sabby Angel Adaiwa Kumpindua Jokate kwa Ali Kiba

$
0
0
Mwigizaji wa sinema za Kibongo anayefanya vyema pia kwenye Muziki wa Mduara, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ amedaiwa kumpindua mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ kwa mpenzi wake, Ali Kiba ‘King Kiba’, Ijumaa Wikienda limenasa vielelezo vya ubuyu kamili.

Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa, Sabby amevamia penzi la Jokate na kuhakikisha anampa ‘vitu adimu’ Kiba kiasi ambacho mkali huyo wa Wimbo wa Lupela kuhamishia majeshi rasmi kwa mrembo huyo ambaye jina lake linazidi kushamiri siku hadi siku mjini.

“Huwezi amini mtoto wa kike kampa mambo adimu Kiba kachanganyikiwa. Amehamishia kabisa majeshi kwa Sabby. Hana habari tena na Jokate kwa sasa, akili yake yote ipo kwa Sabby,” kilisema chanzo hicho.

Wakati chanzo hicho kikivujisha ubuyu huo, chanzo kingine kilikwenda mbele zaidi kwa kuanika mawasiliano ya kimahaba kati ya Kiba na Sabby.

Kwenye meseji hizo zilizoonekana kupigwa picha kutoka katika meseji halisi katika simu (screen shot), inaonesha namba iliyoseviwa jina la Kiba ikichati na ya Sabby wakiitana baby baby kwa sana huku wakichombezana na maneno matamu kuashiria ni ‘mtu na mtuwe’.

Kuna seheme Sabby anaonekana kumchombeza Kiba kwa maneno matamu; “be free, jiamini ati. Mimi si kama hawa malaya wa mjini. Ni mpenzi wako, napenda mwanaume anayenijali…”

Baada ya kunasa meseji hizo, mwanahabari wetu alimtafuta Kiba bila mafanikio lakini bahati nzuri Sabby alipatikana na kukiri kuwa na uhusiano na Kiba lakini akaomba habari isiandikwe kwani hataki vitu hivyo vijulikane sababu haikuwa kusudio lake.

“Niliibiwa simu sasa nafikiri aliyeniibia ndiyo kawapa hayo mawasiliano yangu na Kiba. Please naomba msiandike hiyo habari, mtaniharibia,” alisema Sabby.

Chanzo:GPL

Huwa Napata Shida sana Nikikutana na Wanawake Wenye Hii Tabia

$
0
0
Huwa napata shida sana nikikutana na Wanawake wenye hii tabia...Unampenda Mwanamke kabisa from ur heart,unajipanga unampiga saundi..anakujibu,''How old are you kaka'' unamwambia am 29 years..utamsikia,''Oh my Ghosh,ur still a kid,mi nadate guys who are 45 years above...Wanajua kupenda,they are so caring,yaani nyie vijana mnasumbua sana''.Sio tunasumbua,anajua kabisa miaka 29 bado ndo unasaka hela,ndo umeanza maisha huna cha kumhonga,ukijitahidi sanaaa utampeleka shopping Karume na hiyo hela itakuuma kishenzi!

Anakuita Kid bila aibu wakati yeye ana miaka 23 tu halafu eti ana mahaba na jitu la miaka 47..Uongo mtupu!Ina maana mtu hawezi kupenda na kucare hadi afike miaka 45??Nyie semeni tu mnawalia timing coz mnajua mtu mwenye miaka 45 anakuwa ameshajipanga,amefanya kazi ana hela,unajifanya unampenda kumbe Parasite tu unataka kumnyonyoa mafao yake ya uzeeni,hamna hata aibu..Mnapenda sana vitu ready made,tengenezeni vya kwenu,ukiona mtu ana miaka 45 jua kuna Mwanamke mwenzio amefanya kazi kumfikisha hapo alipo,we unakuja unadandia tu,,,Kama kweli una mahaba tafuta mwanaume wako,panda nae daladala za Buguruni mrukie wote dirishani,msotee maisha kwa kutembelea TZ 11 hadi siku apate gari mfaidi wote halafu akifika miaka 45 uone kimwanamke cha IFM kinamsogelea eti hes caring uone inavyouma,utatamani umpige patasi ya kisogo...Gold diggers,waone kwanza,msione gesi mtwara mshaanza kuandamana!45years guy waiting for u student of 23 years,ina maana miaka yote hiyo alikuwa Stevie Wonder au??

By  Seth De Jesus Giovanni
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images