Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli Amuapisha Balozi Eng. John William Kijazi Kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Eng. John William Herbert Kijazi kuwa Katibu Mkuu Kiongozi Ikulu jijini Dar es Salaam. Balozi Kijazi anachukua nafasi ya Balozi Ombeni Sefue ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Shabiki wa Ali Kiba Instagram Aponda Show ya Kiba Nigeria..Autupia Lawama Uogozi

$
0
0

Shabiki wa Kiba anayejiita @kiba_for_real Huko instagram mambo yamemfika shingoni na kuamua kusema haya:

"Leo naomba fans wenzangu wa alikiba mnisamehe nitaongea kinachoniuma,1.ivi king Kiba alipokuwa Nigeria alikuwa na uongozi wake? Na kama walikuwepo walihusika vip na maandalizi ya show ya king? Jamani wakati mwingine tuwe wakweli anapokosea sio tuwe tunasifia wakati kukosea alie iona ile show kama Ana mapenzi ya dhati na king Kiba Kuna mapungufu makubwa aliaona mfano sauti vyombo vilikuwa havisikiki vizuri Kiba mwenyewe alikuwa anaimba kama vile a naogopa yaaaani kama underground wakati ni msanii mkubwa Africa. Ndugu hapo ndio domo anatuzidi kwenye uongozi Hilo lilikuwa jukumuu Lao ivi wanageria watampa Tena shavu? Ilikuwa nafasi ya pekee kwa alikiba kuwa onyesha wa Nigeria kuwa Tanzania Kuna mtu muhimu kama yeye lakini show ikawa imedorora kama msanii mchanga, management ya king Kiba haifai kabisa wooote watolewe au Wana njama maaana show Za live Za king hapa bongo kila mtu anajua ni shidaaa hadi Domo anakimbia kiukweli show ya juzi tusimsifie ilikuwa mbovu mno wadau tueleze ukweli "

CHADEMA Warusha Kombora Kwa Rais John Magufuli...Wadai Wamechoka Sasa

$
0
0

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimerusha kombora kwa Rais Dk. John Magufuli na kusema kuwa sasa wamechoka na uonevu.

Chama hicho kimesema kuwa wanashangazwa na hatua ya kukamatwa kwa wabunge wao huku viongozi wa juu wa Serikali wakibaki kimya, hasa Rais Magufuli, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

Kimesema tangu ulipovurugika Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, wabunge na madiwani wao wamekuwa wakikamatwa na kudhalilishwa kwa madai ya kufanya fujo jambo ambalo si sahihi.

Akitoa tamko la Kamati Kuu kwa waandishi wa habari Dar es Salaam , Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema katika kipindi cha siku mbili watatoa tamko kwa wanachama wao ikiwamo kuchukua uamuzi mzito kutokana na vitendo hivyo vya udhalilishaji.

Alisema kuwa vitendo hivyo vya uonevu ambavyo vinafanywa na Jeshi la Polisi, vinatokana na shinikizo la viongozi hao wa Ikulu na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mbowe alisema wakati vitendo hivyo vinaendelea, Rais Magufuli, Waziri Mkuu Majaliwa pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue wamekaa kimya, jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa wanahusika kutoa amri ya kufanyika kwa vitendo hivyo.

Alisema hadi sasa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee wamezuiliwa na polisi kwa ajili ya kuhojiwa huku baadhi ya askari wakienda nyumbani kwao kwa ajili ya upekuzi.

Mbowe alisema wakati hali hiyo ikiendelea, hivi sasa Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea amekuwa akitafutwa na polisi kwa madai kama ya wenzake ya kuvuruga uchaguzi.

Alisema chama hicho hakitavumilia kuona vitendo vya wazi vya kuua demokrasia nchini vinafanyika, na kwamba kikao hicho kitakuja na uamuzi mzito wa kitaifa ambao utawasilishwa kwa wanachama ili kuchukua uamuzi.

Mbowe alisema hawawezi kuvumilia vitendo vya unyanyasaji, uonevu na dhuluma inayofanywa na Serikali ya CCM, hivyo basi watatangaza uamuzi mzito ambao utafanywa na wanachama wao nchi nzima.

“Tumechoka kunyanyasika, tutatoa tamko kali la kitaifa ambalo litawasha moto kwa wanachama wetu, kwa sababu wao wameandaa mkakati wa kuua demokrasia nchini, hatutakubali.

Poa Makonda Atoa Mpya...Atangaza Mpango wa Kuanzisha Mtaa wa Bar Kinondoni

$
0
0

PAUL Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ametangaza mpango mpya wa kuanzisha mtaa maalum utakaokuwa ukihusika na biashara ya uuzaji wa vinywaji vikali na baridi (Bar).

Makonda ameweka wazi mpango huo mapema hii leo jijini Dar es Salaam ikiwa pia ndiyo siku ambayo utekelezwa wa mpango wa walimu wa shule za msingi na sekondari kusafiri bure kupitia usafiri wa umma (daladala) unaanza rasmi.

Mkuu huyo wa wilaya amesema mpango huo ni muendelezo wa ubunifu na uthubutu wa mipango ya maendeleo ambao kwa kiasi kikubwa umekuwa ukikosekana miongoni mwa Watanzania na hivyo kufanya kasi ya maendeleo hapa nchini kuwa ndogo tofauti na matarajio ya wananchi.

“Kinondoni nina mpango wa kutengeneza mtaa mmoja maalum wenye bar tu ili watu wakitaka kwenda kunywa pombe waende mtaa huo bila kubugudhi. Nasubiri muda tu ufike kwa sababu haiwezekani kila eneo liwe na bar mpaka nyuma ya misikiti na nyuma ya makanisa,” ameeleza Makonda.

Wilaya ya Kinondoni ndiyo wilaya yenye watu wengi zaidi hapa nchini ambapo kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 wilaya hiyo ina jumla ya watu milioni 1.7 na kwasasa ikikadiriwa kufikia watu milioni 1.9.

Katika hatua nyingine pia Makonda ameeleza kuridhishwa na zoezi la walimu wa jiji la Dar es Salaam kuanza kusafiri bure hii leo huku akibainisha changamoto mbalimbali alizozishuhudia hii leo wakati alipotembelea vituo mbalimbali za daladala kuangalia zoezi hilo.

Makonda amesema: “Changamoto zipo ikiwemo baadhi ya walimu kuficha vitambulisho vyao wakati nimewambia wavivae, lakini kiukweli makondakta wote katika vituo vya mawasiliano na Tegeta nilivyotembelea wana hamasa kubwa ya kuwasafirisha walimu kila mahali wanaita, walimu! walimu!”

Fella aeleza gharama anazotumia kuwatunza vijana 102 wa kituo chake cha Mkubwa na Wanae

$
0
0

Meneja wa kituo cha kusimamia wasanii ‘Mkubwa na Wanae’ Said Fella ameeleza gharama ambazo amekuwa akitumia katika kuendesha kituo chake.

Akizungumza na gazeti la Mwananchi Jumatatu hii Fella anasema kwa kuwa vijana wanaoishi kituoni hapo ni wengi, ameamua kuwa anawahudumia kwa wiki, hivyo anajua hesabu za wiki pekee kuwamudu kwa kila mlo na matumizi yao binafsi.

“Kwa ujumla huwa nachukua chakula kwa wiki na kwa bahati nzuri wanajipikia wenyewe,” alisema Fella.

Fella anasema aliamua kuwafunza kujitegemea hivyo akaona ni bora wajihudumie wenyewe, hesabu zake kwa wiki ni kiasi cha Sh360,000 ambazo hutumia kwa chakula, nauli za shule kwa wale wanaosoma na matumizi mengine pamoja na nauli kwa wale wanaotoka nyumbani kwao.

Pia alisema kwa kuwa huwa haingii jikoni, bado hajajua hesabu halisi, lakini jukumu la kupika hilo analifuatilia kuhakikisha kila kijana anajifunza kujitegemea na kuwa msaada kwa wengine

“Aslay mwenyewe anapika yaani ni kama watoto waliofiwa na mama yao, kila mmoja ana jukumu la kuingia jikoni na kupika chakula cha watu wote, leo Beka kesho atapika Getu. Yaani wote wanaweza kuamua kuingia jikoni watatu au vinginevyo,” alisema.

Linex Ataja Sababu ya Wasanii Kutopenda Kuwaweka Wazi Wapenzi wao Hadharani...Ipi Hiyo?

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva Linex amefunguka na kusema kuwa kuna sababu nyingi ambazo zinawafanya wasanii wengi washindwe kuwatambulisha wapenzi kwenye hadhara.

Linex ameweka wazi kuwa msanii anaangaliwa sana na jamii kitu ambacho kinampa hofu pengine anaweza mtu ambaye ana mambo ya kipuuzi na kumuharibia taswira yake.

“wanakuwa hawajakutana na watu wanaowez kuwaamini asilimia 100,unajua kumtambulisha mtu kwenye jamii na jamii nzima inakuangalia wewe halafu mtu mwenyewe labda ana mambo ya kipuuzi sio kitu kidogo” alifunguka Linex na kusisitiza kuwa huwezi ukakutana na mtu ambaye yuko perfect.

ZEC Yaibana Mbavu CUF Uchaguzi wa Marudio..Yaitaka Kuwakilisha Majina ya Mawakala Watakao Simamia Uchaguzi

$
0
0
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), imeiandikia barua CUF, kuitaka kuwasilisha majina ya mawakala watakaosimamia uchaguzi wa marudio uliopangwa kufanyika visiwani hapa Machi 20, mwaka huu.

Hata hivyo, CUF wameendelea na msimamo wao wa kutotambua uchaguzi huo na kuitaka ZEC  iache kutapatapa, wakati walishaijibu kuwa hawatashiriki uchaguzi huo.

Mwenyekiti wa makatibu wa CUF wa wilaya 10 za Zanzibar, Hamad Masoud Hamad  ambaye ndiye aliyeandikiwa barua hiyo na ZEC, alisema wanashindwa kuielewa tume hiyo kwa kitendo cha chao cha kukitaka chama hicho na vyama vingine vishiriki uchaguzi huo kwa madai kuwa ni batili.

“Tunashindwa kuwaelewa ZEC, hivi wanachokitaka kwetu sisi ni nini haswa, tuliwaambia na barua tuliwaandikia kuwa hatutashiriki uchaguzi wa batili.

“Isitoshe juzi Maalim Seif (Seif Shariff Hamad) alisisitiza kuwa hakuna mgombea wa CUF atakayegombea akiwamo yeye na kuitaka ZEC iondoe jina lake,” alisema Hamad .

Katibu wa CUF Wilaya ya Unguja Mjini, Fadhili Sijaamini ambaye pia ni mwenyekiti wa makatibu wa wilaya wa chama hicho Zanzibar alithibitisha kupokea  barua hizo Alhamisi ya wiki iliyopita kutoka kwa ofisa wa ZEC, ikimtaka apeleke orodha ya majina ya mawakala watakaosimamia uchaguzi huo, kisha nyingine asambaze kwa wenzake.

“Tunawashangaa sana ZEC ukweli upo wazi hawaeleweki na wamefikia pabaya na wanatapatapa,” alisema Sijaamini.

Aliongeza kuwa, yeye na makatibu wenzake wameshaiandikia barua ya kuijibu ZEC, kuwakumbusha msimamo wao kuwa hawashiriki  kwa sababu hawautambui uchaguzi huo wa marudio.

Alipotafutwa Ofisa Habari wa ZEC, Idrissa Hajji Jecha kuthibitisha taarifa hizo alidai kuwa yeye siyo msemaji wa tume hiyo na kumuelekeza mwandishi wa habari ampigie ofisa mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Muha.

Alipopigiwa Muha alikiri kupeleka barua hizo  kwa kiongozi huyo za kuwataka CUF kupeleka orodha ya majina ya mawakala watakaosimamia uchaguzi huo.

Maskani  CUF, CCM zachomwa

Hali ya hofu inazidi kutanda kila kukicha visiwani Zanzibar miongoni mwa wananchi kutokana  na matukio ya uchomaji moto.

Hali hiyo inakuja huku zikiwa zimebaki siku chache kufanyika uchaguzi huo.

Wakati juzi maskani ya Kisonge inayomilikiwa na CCM ikiwa imelipuliwa kwa bomu la kienyeji, jana matawi ya CUF, zaidi ya matano yamelipuliwa kisiwani Pemba.

Maeneo yaliyochomwa moto ni pamoja na tawi la Mkanyageni lililopo Mkoani, Kiwapwa (Ziwani), Kiuyu Miningwini (Kojani), Ofisi ya jimbo  la Wingwi na baraza la Konowe  la Micheweni).

Kamanda wa Polisi wa Mkoa Kaskazini Pemba, Shehani Mohammed Shehani, alithibitisha kutokea kwa matukio hayo na kusisitiza kuwa wanaendelea na uchunguzi.

“Mimi sikuwepo katika hayo maeneo kwa sababu nilikuwa nimesafiri, lakini bado tunaendelea kuchunguza matukio hayo, huenda ikawa ni mbinu ya watu kutishwa ili wasijitokeze kwenye uchaguzi,” alisema kamanda huyo.

Akizungumza matukio hayo ya kuchomewa maskani zao Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui alisema yametokea katika maeneo tofauti na kwamba wameripoti polisi.

“Kwa sisi hatuna la kufanya zaidi ya kwenda kuripoti polisi na kuwapa taarifa juu ya kuchomewa matawi yetu, na hilo tumelifanya asubuhi na mapema,” alisema Mazrui.

Mazuri alisema walitoa taarifa kwamba CUF imechoka   kufanyiwa vitendo hivyo  na kuwataka polisi wafanye kazi kwa maadili yao na siyo kufuata wanasiasa.

Mkurugenzi wa Haki za Binaadamu Wilaya ya Micheweni, Kombo Mwinyi Shehe alisema matawi hayo ya yamechomwa moto usiku wa manane na kuteketea vibaya.

Shehe alisema ofisi ya jimbo ya Wingwi na baraza la CUF la Kinowe zilizopo Mkoa wa Kaskazini Pemba zimeteketezwa.

“Tulipokwenda tumeona moto mkubwa na kama unavyojua kumeezekwa makuti, na makuti yote yameshika moto kwa hivyo hata watu walipofika wameshindwa kufanya lolote kwa kuwa yalishateketeza jengo zima,”  alisema Shehe.

Mbunge wa Wingwi, Kombo Juma Hamad alisema alipata taarifa katika jimbo lake kumetokea uchomaji moto huo na kuwasiliana na  wenzake.

Harmonize Asema Anaweza Kufanya Kazi na Ali Kiba, Amsifia

$
0
0
Msanii wa muziki kutoka ‘label’ ya WCB, Harmonize amesema yupo tayari kufanya kazi na Ali Kiba endapo ikitokea nafasi.
harmonize2

Akizungumza katika kipindi cha 360 cha Clouds FM Ijumaa hii, Harmonize aliulizwa kama anaweza kufanya kazi na Ali Kiba kama ikitokea nafasi.

“Unajua Ali Kiba ni msanii wa Kitanzania, ni msanii mzuri pia, so kolabo ikiwa na tija nitafanya naye kwanini nisifanye naye. Sio Ali Kiba tu, msanii yeyote wa Kitanzania,” alisema Harmozine.

Pia Harmonize alisema bado hajui kama kweli kuna beef kati ya Diamond na Ali Kiba.

“Mimi sijui kiukweli kama kuna beef, kwa sababu sijawai kukaa na Diamond siku moja akaanza kuongelea msanii mwingine tofauti. Diamond ni mmoja kati ya watu wanaosupport muziki wa Tanzania, ukiona kolabo nyingi za Tanzania na wasanii wa nje Diamond ana mchango wake,” alisema Harmonize.

Kwa sasa Harmonize anafanya vizuri na video yake mpya ya wimbo ‘Bado’ aliyomshirikisha bosi wake Diamond.

Millard Ayo 'Mimi ni Miongoni Mwa Wanafunzi Waliofeli Kidato cha Nne Lakini Niliinuka na Kuendelea'

$
0
0
Mtangazaji mahiri wa kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM Millard Ayo baada ya kufungua studio yake kubwa naya kisasa jijini Dar, ameanza kuuza vipindi vya burudani katika radio mbalimbali za Afrika Mashariki.
millard

Akizungumza Jumamosi hii katika mdahalo wa kuwatia moyo wanafunzi waliofeli kidato cha nne, ambao ulienda sambamba na uzinduzi wa video mpya ya Mrisho Mpoto, Millard alieleza mafanikio yake baada ya kupambana kwa muda mrefu.

“Nilijiuliza kwanini nisitumie uandishi wangu wa habari ili kusambaza habari Afrika?, ndipo nikaanza kujinyima ili nijenge studio yangu kwa pesa yangu mpaka imekamilika. Sasa hivi tayari nimeshaanza kuuza vipindi vyangu katika radio mbalimbali za Afrika, Kenya, Rwanda. Pia nimekuwa reporter wa radio mbalimbali za Afrika Mashariki, pia Nigeria kuna kazi maalum nimepata ambayo nimehifurahia sana,” alisema Millard.

Aliongeza, “Nimeona kama Rwanda na Kenya sasa hivi bongofleva ndiyo imetake over, hawa watu ingawa wanasikiliza muziki, pia wanataka stori mbalimbali za mastaa wa bongofleva. Kwa hiyo mimi nataka kuwaambia watu wangu tusikate tamaa kama ulianguka inuka endelea,”

Pia Millard Ayo alisema yeye ni miongoni mwa wanafunzi ambao walifeli kidato cha nne lakini aliinuka na kuendelea.

Upendo Kwa Wasanii Wetu Unapoanza Kuwa Kero Kwa Wasanii wa Nje!

$
0
0
Mitandao ya kijamii imesababisha mashabiki wawe na access ya moja kwa moja na wasanii wanaowapenda.

Imewasaidia kufuatilia maisha yao na kazi zao kwa ukaribu zaidi. Imewasaidia kuwapongeza wanapofanya vizuri, kuwashauri wanapoteleza, kuwakosoa wanapozingua na wengine kuitumia vibaya kwwa kuwatukana wale wasiowapenda. Kikubwa ni kwamba shabiki sasa ana full access katika career ya msanii.

Kupitia mitandao ya kijamii, vita vya kishabiki vimepata uwanja wa kupigania na hicho ni kitu kinachoendelea kila siku. Lakini vipi pale ambapo mapenzi kwa wasanii wetu kwenye mitandao hiyo yanapogeuka kuwa kero kwa wengine?

Mfano mzuri ni kile kinachoendelea kwa wasanii/mastaa aliopiga nao picha Diamond akiwa Marekani. Bahati tu ni kuwa Kanye West hayupo Instagram, kama angekuwepo, huenda sasa angekuwa ameshajua maneno machache ya Kiswahili kutokana na mvua ya comments kutoka kwa mashabiki wa Diamond.

Lakini mtu mwenye experience hii, ni staa wa Empire, Bryshere Y. Gray maarufu kama Hakeem kwenye tamthilia hiyo. Kimuziki pia dogo huyo anajulikana kwa jina la Yazz. Tangu Diamond apost akiwa naye, page yake imevamiwa na waswahili waliokesha wakipiga soga za hapa na pale.

Wametengeneza makao ya muda kwenye page ya Mmarekani huyu ambaye huenda akalazimika kutafuta mkarimani wa Kiswahili ili kumsaidia kung’amua mawili matatu yanayojadiliwa na mashabiki wa kibongo. Wakati mwingine nahisi upendo huu tulionao kwa wasanii wetu unaanza kuwa kero kwa wasanii wa nje.

Nafahamu kuwa hivi bado ni vitu vigeni na itachukua muda kuvizoea (wasanii wa Bongo kufanya collabo na wasanii wakubwa wa Marekani), lakini nadhani ni muhimu tukaendelea kuonesha upendo kwa wasanii wetu, lakini kutowaharibia siku wengine.

Sidhani kama comments zaidi ya 1,000 za Kiswahili ni kitu kinachomfurahisha staa asiyekielewa. Nimesoma baadhi ya comments zinadai kuwa Yazz alimfollow Diamond lakini baadaye akamunfollow tena na wengine wanadhani ni sababu ya fujo alizofanyiwa na mashabiki wake.

Kama ni kweli hiyo ni sababu, basi kumbe mapenzi yetu kwa wasanii wetu yakizidi sana kiasi cha kuzivamia page za wasanii wa nje tukidhani tunataka wajue tunavyowapenda, yanaweza kuwaharibia uhusiano wao.

Wao wataogopa tu kuwaambia mashabiki ukweli huu lakini sometimes wangependa kuona mashabiki wao wana behave kidogo! Sijasahau pia kuwa Jesse “Corparal” Wilson, co-producer wa collabo ya Diamond na Ne-Yo, naye anachezea mvua ya comments za Kiswahili.

Tupunguze mzuka kidogo

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya March 8, Ikiwemo Siri ya Balozi Sefue Kung'oka Ikulu

$
0
0
SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya March 8, Ikiwemo Siri ya Balozi Sefue Kung'oka Ikulu

Maalim Seif Alazwa Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam

$
0
0
Siku tatu baada ya kutoka India alikokwenda kwa ajili ya kupata matibabu, Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad jana alilazwa katika hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassoro Mazrui amesema kuwa chanzo cha Maalim Seif kulazwa katika hospitali hiyo jana asubuhi ni uchovu wa safari yake ya India ambayo alienda kwa ajili ya kufanyiwa upasuaji wa mgongo.

Mazrui alikanusha taarifa zilizokuwa zinaenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa kiongozi huyo wa CUF alilazwa kutokana na matatizo ya moyo. Alisema kuwa hakuna kumbukumbu yoyote ya ripoti ya daktari inayoonesha kuwa Maalim Seif ana tatizo la moyo.

Naibu Katibu Mkuu huyo wa CUF alisema kuwa kiongozi huyo anaendelea vizuri kiafya na kwamba hayuko katika hali mahututi kama ilivyokuwa ikielezwa.

“Anakula na kufanya kila kitu mwenyewe na hata jioni hii nimeongea naye, anakula kila kitu, hivyo Watanzania wasiwe na wasiwasi juu ya afya ya Maalim Seif,” alisema Mazrui.

Viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa waliwasili katika hospitali hiyo kumjulia hali akiwemo aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.

Madaktari wa Hospitali ya Butimba Mwanza Wagoma Baada ya Madaktari Wenzao Kutumbuliwa Majipu

$
0
0
Siku chache baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo kuwasimamisha kazi wauguzi watano wa Hospitali ya Butimba wilayani Nyamagana Mkoani Mwanza kufuatia uzembe uliopelekea vifo vya watoto mapacha, madaktari wa hospitali hiyo jana waligoma kwa saa kadhaa.

Madaktari hao waligoma kutoa huduma kwa zaidi ya saa sita na kusababisha usumbufu mkubwa, wakidai kuwa wamekuwa wakinyanyaswa na kutishwa na watu wanaofika hospitalini hapo kupata huduma. Pia  wanadai watumishi wenzao waliosimamishwa kazi hawakupewa nafasi ya kujitetea

Akieleza sababu ya mgomo huo, Bi. Rechungula ambaye ni mmoja kati ya watoa huduma ya afya katika hospitali hiyo alisema kuwa wagonjwa wamekuwa wakikiuka taratibu za kupata huduma huku wakiwatishia na kuwasukuma kufanya kazi zao.

“Wagonjwa wanakuja hawataki kufuata utaratibu, wakifika mlangoni wanataka kuandikiwa kadi mara moja bila kufuata utaratibu. Na wakifika kwa daktari vivyo hivyo." Alisema Bi. Rechungula

Alisema kuwa wagonjwa wamekuwa wakiwatishia kuwapiga endapo hawatawahudumia kwa muda wanaoutaka.

Kufuatia sakata hilo, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga alifika hospitalini hapo na kuwahakikishia usalama wauguzi hao, huku akitahadharisha watu wanaotaka kuhatarisha usalama.

Alisema kuwa hakutakuwa na sababu ya kuweka ulinzi wa polisi kusimamia huduma hospitalini hapo bali hali ya amani inapaswa kuzingatiwa.

Baada ya kufanya kikao na wauguzi hao pamoja na Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, huduma zilirejea hospitalini hapo majira ya saa saba mchana.


Balozi Ombeni Sefue Afunguka Kilichomtoa Ikulu...Kijazi Asema Utumbuaji Majipu Upo Pale Pale

$
0
0
Baada ya kudumu Ikulu kwa takribani siku 127 zikiwamo 67 tangu aongezewe muda wa mwaka moja akiwa na Serikali ya Awamu ya Tano, Balozi Ombeni Sefue ameshukuru heshima aliyopewa na Rais John Magufuli kwa muda wote aliomsaidia kutekeleza majukumu yake ya ukatibu mkuu kiongozi na kueleza kuwa Serikali ya sasa ni ya mabadiliko.

Wakati Sefue akiondoka, mhandisi John Kijazi amepokea kijiti cha ukuu wa utumishi serikalini na kuahidi kuwa atafuatilia mazingira ya watumishi wote pamoja na mazingira yao, ili kurekebisha panapohitajika kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na tija kwa wananchi.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuapishwa kwa mrithi wake, licha ya kumshukuru Rais, Balozi Sefue aliwataka watendaji wote serikalini kumpa ushirikiano wa kutosha Balozi Kijazi ili kuleta ufanisi kwenye huduma za umma.

“Namshukuru Rais kwa kuniamini kwa kipindi chote nilichodumu naye. Ni heshima kubwa kuwatumikia Watanzania pamoja naye. Nitampa ushirikiano wowote atakaouhitaji katibu mkuu kiongozi mpya kwenye utekelezaji wa majukumu yake,” alisema Sefue.

Rais Magufuli, ameahidi na mara zote amekuwa akisisitiza adhma yake ya kutumbua majipu kwa watumishi wote ambao hawaendani na kasi yake.

Tangu taarifa za mabadilio hayo zilipotangazwa jana, kumekuwepo na tetesi nyingi kuwa huenda Sefue naye ni jipu lilikuwepo ikulu, suala ambalo halikupata maelezo ya kutosha kutoka kwa balozi huyo.

Alipoulizwa juu ya tetesi hizo alijibu kwa ufupi: “Hii ni Serikali ya mabadiliko.”

Kwa upande wake Kijazi, alisema atafanya kazi kwa kuzingatia vipaumbele vya Rais huku akimshauri namna sahihi za kuboresha mazingira ya utumishi serikalini.

Akieleza juu ya majukumu yake mapya, alionyesha kuyatambua ipasavyo na kubainisha kuwa atashirikiana na Baraza la Mawaziri kwenye vikao vyao, bila kusahau kuzifuatilia wizara husika na kuona endapo kila kitu kinaenda kama inavyotakiwa.

“Nitakutana na mawaziri kwenye vikao vyao nitakavyoviandaa. Nitawasiliana na kuwafuatilia watendaji wa wizara husika juu ya masuala yatakayokuwa yamejitokeza ndani ya maeneo yao ya uwajibikaji. Kila mmoja atimize wajibu wake ili Taifa lisonge mbele,” alisema Kijazi.

Ili kuitendea haki hadhi ya utumishi wa umma, Kijazi ameahidi kuhakikisha kila kitu kinasimamiwa kwa ukaribu huku akitoa msisitizo kwenye vipaumbele vya Rais.

 “Kwenye suala la mapato na rushwa, nitafuatilia kwa nguvu ili kuongeza uwajibikaji kwa watumishi wa Serikali,” alisisitiza Kijazi.

Balozi Kijazi aliteuliwa juzi kushika nafasi inayoachwa na Balozi Sefue. Kabla ya uteuzi huo, Kijazi alikuwa mwakilishi wa Tanzania kwa nchi za India, Singapore, Sri Lanka, Bangladesh na Nepal huku makazi yake yakiwa jijini New Delhi, India kuanzia mwaka 2007.

Katika wadhifa huo, alikuwa mkuu wa mabalozi wote wanaowakilisha Tanzania nje ya nchi pamoja na mkuu wa mabalozi wa Afrika nchini India.

Kabla hajateuliwa kuwa mwakilishi wa nchi, Kijazi amekuwa mtumishi serikalini kwa nafasi mbalimbali ikiwamo Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi kuanzia mwaka 2002 mpaka 2006.

Kabla ya hapo alikuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu kati ya mwaka 1996 hadi 2002.

Ndani ya Wizara ya Ujenzi, kabla hajawa katibu mkuu, alikuwa mhandisi mwandamizi wa ujenzi wa barabara kisha kupandishwa cheo na kuwa mkurugenzi wa barabara za mikoa.

Kumbukumbu za taaluma yake zinaonyesha kuwa alipata Sha hada yake ya kwanza ya Sayansi ya Uhandisi wa Umma mwaka 1982 kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na baadaye Shahada ya Uzamili katika Uhandisi wa Barabara kutoka Chuo Kikuu cha Birmingham, Uingereza mwaka 1992.

Jana wakati anaapishwa, saa 4:15 asubuhi, Kijazi alikuwa sambamba na mke wake, Fransiscar Kijazi na kwa pamoja wamejaliwa watoto watatu, David, Emmanuel na Richard.

Kwa heshima ya familia hiyo, baada ya kukamilisha protokali, Rais Magufuli alipiga picha ya pamoja na familia ya mteule huyo mpya atakayehudumu ikulu kuanzia sasa.

Hata hivyo kwa mara ya mwisho, Sefue aliendelea na kazi yake mpaka jana asubuhi na ndiye aliyemkabidhi Kijazi kitabu kitakatifu cha Biblia, Katiba na kiapo cha uongozi ambacho alisaini.

Mgombea Urais wa Marekani Donald Trump Amshukia Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.Amwita Tapeli wa Matapeli....

$
0
0
Just a month after endorsing former Kenyan Prime Minister Raila Odinga for President, Donald Trump has this time expressed his hate for Uhuru regime, terming it ‘A fellowship of con-men’ of con-men.

Speaking to an ABC News pressman after his meeting with black pastors, the GOP said that Uhuru Kenyatta, Kenyan President has failed to lead by example.

“You see I have been right all along. Uhuru Kenyatta is a dangerous conman that cannot be entrusted with the leadership of a country let alone the chairmanship of even a funeral committee. How can this man carry 23 of his relatives to Paris at the detriment of poor Kenyans? How can he take with him his daughter to a forum she has idea about? What does Guinea as – he struggled to mention Ngina – know about climate change? Can she even define the term climate? This man is simply a tourist who loves to holiday around the world. Since he went to the “white House”, he has made more trips to foreign countries compared to his own country. I don’t know Kenya well and I have never stepped foot there but my intelligence tells me that ever since he was elected, Mr. ‘Keniatta’ has never stepped foot in the North Eastern Province. People say that I hate these Africans, no it is the ridiculous things they do that I hate. How do you carry the entire community to a climate Change forum at the expense of poor denizens? Is this not a fellowship of con-men?I hear he sends to jail bloggers from the opposition side and whoever criticizes him. Freedom of Press must be espoused by all leaders including Mr. Keniatta” Answered Mr. Trump as he confirmed he loves Kenya and would one day love to visit.

Mwanafunzi Aliyeongoza Kitaifa Matokeo Kidato cha Nne Aahidiwa Ajira Na Benki ya CRDB

$
0
0
Benki  ya  CRDB  imemfungulia  Akaunti  ya  Scholarship  na  kumwekea  sh. Milioni 5  mwanafunzi  aliyefanya  vizuri  katika  mtihani  wa  kumaliza  kidato  cha nne  mwaka  2015,  Butogwa Shija  na  kumwahidi  ajira  pindi  amalizapo  masomo.

Hafla  hiyo  ilifanyika  jana  jijini  Dar  es  Salaam  ikiwa  ni  kuelekea   kilele  cha maadhimisho  ya  siku  ya  wanawake  duniani  leo, ambapo Butogwa  alipewa  zawadi  ili  kuwahamasisha  watoto  wa  kike  kwamba  wanaweza.

Pia  Mamlaka  ya  Elimu Tanzania (TEA)  ilimuongezea  mwanafunzi  huyo  kiasi  cha  shilingi 500,000  lengo  likiwa  ni  kuwahamasisha  watoto  wa  kike  ili  kuleta  haki  sawa  kwa  wote.

Naye Butogwa  aliahidi  kutumia  fursa  hiyo  vizuri  kwa  kusoma  kwa  bidii  bila  kubweteka  na  kuwataka  wanafunzi  wengine  kuweka  bidii  kwenye  masomo  yao.

Katika hatua  nyingine, Naibu Mkurugenzi Mtendaji  wa  CRDB, Esther Kitoka  alisema   wametoa  sh. milioni 20  zitakazosaidia  katika  ujenzi  wa  mabweni  kwa  watoto  wa  kike  ili  kuongeza  kasi ya  ufaulu  kwa  wanafunzi

Rais Magufuli Aanza Kuhujumiwa....

$
0
0
SERIKALI ya Rais John Magufuli imeanza kuhujumiwa, wanaotajwa kuihujumu ni wafanyabiashara.

Wafanyabiashara wa sukari nchini wameanza kujenga utaratibu wa kuficha sukari ili kuibua malalamiko kutoka kwa wananchi lengo likiwa ni kushinikiza vibabali vya kuingiza sukari kutoka nje vinatolewa.

Hatua hiyo imemwibua Charles Mwijage, Waziri wa Viwanda na Biashara ambaye anakiri kuwepo kwa hujuma hizo na kudai, serikali haitalala.

Amesema, kuna wafanyabiashara wanaficha sukari kwenye maghala yao ili kuchochea mfumko wa bei na kisha waiuze kwa bei ya juu na hatimaye kupata faida kubwa.

Hivi karibuni Rais Magufuli alizuia kutolewa vibali holela vya uingizaji sukari nchini na kumwagiza Kasim Majaliwa, Waziri Mkuu kusimamia hilo.

Taarifa zilizopatikana zinaeleza kwamba, wafanyabiashara waliokuwa wananufaika na uingizaji wa sukari nchini wameanza kuhujumu kwa kushirikiana na wenye maghala ya sukari.

Mwijage amesema, wafanyabiashara hao wamekuwa wakificha sukari ghalani ikiwa pamoja na kufungia maghala yao ili kuzuia mfumuko wa bei na hatimaye kupata faida kubwa.

Amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam ambapo amewataka wananchi kutoa taarifa sahihi za baadhi ya watu wanaoendelea kuficha sukari kwa makusudi.

“Kama kuna taarifa sahihi za baadhi ya watu wanaoficha sukari ghalani kwa makusudi ili kuiaminisha jamii kuwa sukari ya ndani haikidhi na kupandisha bei holela ya sukari kwa masilahi yao binafsi muwataje,” alisema Mwijage.

Mwijage alisema kuwa, kwa dhamana aliyokuwa nayo katika Sekta ya Viwanda na Biashara anauwezo wa kufungia maghala yatakayobainika kuficha sukari kwa makusudi.

“Niwahakikishieni kuwa hakuna mfumuko wa bei ya sukari, mambo ni mazuri na utaratibu uko vizuri, niwasihi wawekezaji wa ndani wajitokeze kuwekeza katika viwanda vya sukari ili kuiendeleza nchi yetu,” alisema.

Alisema, Serikali inampango wa kujenga viwanda vya sukari vidogo na vikubwa ikiwemo ujenzi wa kiwanda kikubwa cha sukari kinachotarajiwa kujengwa hivi karibuni katika mkoa wa Kigoma.

“Viwanda vya sukari vinakuja,nchi yetu si ya kupokea bidhaa hafifu, sukari isiyokidhi ubora haitaingia nchini wala kuuzwa na kutumiwa na watanzania,” alisema Mwijage.

Diamond Aingia Studio Kumaliza Wimbo na Ne-Yo, Akutana na Hakeem wa Empire

$
0
0
Diamond hakwenda Las Vegas kutumbuiza tu bali pia ameitumia fursa hiyo kumalizia kiporo cha wimbo wake na Ne-Yo. Wawili hao walirekodi kwa mara ya kwanza wimbo wao mwaka jana jijini Nairobi lakini kuna vitu hawakumalizia.

Akiwa Las Vegas, staa huyo aliingia studio na Ne-Yo pamoja na producer, Jesse Corporal Wilson aliyeshiriki kutayarisha nyimbi nyingi za Ne-Yo.

Huenda pia akatumia fursa hiyo kufanya video ya wimbo huo.

Pia staa huyo alikutana na rapper na muigizaji wa Empire, Bryshere Y. Gray aka Yazz The Greatest anayejulikana kwenye tamthilia hiyo kwa jina la Hakeem.

Baada ya Kutemana na Nisha Huyu Hapa Ndio Mpenzi Mpya wa Baraka De Prince

$
0
0
Penzi ni kikohozi kulificha huliwezi!

Seems like Barakah Da Prince ana ngekewa na watoto wazuri wa mjini. Baada ya Meninah, Linah, Masogange, Nisha na wengine tusiowajua, hitmaker huyo wa ‘Siachani Nawe’ ameangukia kwenye penzi la mtoto wa kihindi, Naj

Sasa Udaku Special Blog Ipo Play Store..Unaweza Kuinstall Kwenye Smart Phone yako Hapa

$
0
0

Good News! Sasa Blog yako ya Udaku Special Ipo Google Play Store.

Download Udaku Special Blog Android Application CLICK HERE From Play Store

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images