Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

FOLENI ZA MAGARI ZAZUA GONJWA JIPYA

0
0
Dar es Salaam. Wakati kukiwa na ongezeko kubwa la ununuzi wa magari na kusababisha idadi kubwa ya vyombo hivyo vya usafiri, foleni za magari nchini, hasa jijini Dar es Salaam, imefikia hatua ya kutisha huku ikisababisha madhara makubwa kiuchumi, kijamii na kiafya, ikiwamo magonjwa ya akili.
Misululu ya magari ilikuwa ni ya kawaida kuonekana nyakati za asubuhi na jioni wakati watu wakielekea na kutoka kazini, lakini sasa foleni zimekuwa ni za kawaida katikati ya jiji na maeneo mengine ambayo ukarabati wa barabara unaendelea wakati wote.
Wakati kukiwa na kasi ndogo ya ukarabati wa miundombinu ya usafiri, kumekuwa na ongezeko kubwa la magari jijini Dar es Salaam. Pia kumekuwapo na ongezeko kubwa la idadi ya watu hadi kufikia milioni 4.3 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2002 huku vyombo vya usafiri wa umma (daladala) vikitumia njia zisizo sahihi (kutanua), kufanya foleni kuwa kubwa hali inayosababisha jiji kuwa kero kwa muda wote.
Licha ya jitihada za Serikali kutumia treni kusafirisha abiria ili kusaidia kupunguza msongamano wa magari nyakati za asubuhi na jioni, bado tatizo hilo ni kubwa. Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuri aliagiza Kampuni ya Strabag, inayojenga miundombinu ya mabasi yaendayo kasi, kufungua barabara zilizokamilika ili kupunguza msongamano.
Kutokana na tatizo hilo, wakazi wa Dar es Salaam na maeneo mengine yanayoathiriwa na foleni, wamekuwa wakilazimika ama kusitisha safari au kuchelewa kazini na kwenye shughuli nyingine, huku vyombo vya usafiri vikilazimisha kufanya safari chache na hivyo wamiliki kupata fedha kidogo kuliko matarajio yao.
“Madereva wanapata magonjwa ya akili kutokana na kero za barabarani,” alisema Dk. Innocent Godman, ambaye ni mmoja wa wataalamu wa nyanja tofauti aliyeongea na gazeti hili kuhusu tatizo hilo.
“Kwanza ni msongo wa mawazo kuhusu uchumi kutokana na mafuta mengi kupotea njiani; pili barabara mbovu; tatu hasira za kuchelewa anakokwenda; na nne wanakumbana na askari wa usalama barabarani ambao wanawakamua fedha,” alisema mtaalamu huyo wa magonjwa ya akili na mshauri nasaha kuhusu utumiaji wa madawa ya kulevya.
Tanzania inaelezwa ni nchi inayoongoza kwa kuwa na msongamano mkubwa wa magari katika nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Zatafuna mabilioni ya shilingi
Katika utafiti wake, Wakala wa Mradi wa Mabasi ya Kasi (DART), Jumbe Katala amebaini kuwa foleni husababisha ajali za barabarani, upotevu wa nishati (mafuta) na muda wa kukaa barabarani mambo ambayo husababisha hasara ya zaidi ya Sh655 bilioni kwa mwaka.
Katika utafiti huo, Katala alibaini kuwa foleni hizo husababisha kudorora kwa uchumi, huku bei ya mafuta ipanda kutokana na mahitaji ya nishati hiyo kuongezeka.
Alisema kuendesha na kuzima gari mara kwa mara kwa sababu ya foleni huongeza matumizi makubwa ya gari na kuongeza kasi ya uchakavu wake, hivyo kusababisha gharama kubwa za matengenezo ya mara kwa mara.
Madhara kiafya
Kiafya, foleni pia zinatajwa kusababisha maradhi lukuki yakiwamo magonjwa ya akili, pumu, maradhi ya mfumo wa hewa, mzio utokanao na mafuta na maradhi ya moyo.
Msongamano wa magari pia husababisha wasafiri hasa madereva kuvuta hewa chafu itokanayo na mafuta ya magari na maradhi ya mfumo wa hewa kutokana na kutovuta hewa safi. Dk. Godman alisema madereva wengi wa Tanzania wana magonjwa ya akili kutokana na sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na foleni.
“Madereva wanapata zaidi ya magonjwa ya akili hata mara mia moja zaidi,” alisema Dk. Godman. Dk. Godman alisema msongo wa mawazo unaotokana na adha za usafiri nchini umewaathiri watu wengi na kusababisha wawe na lugha chafu, hasira za mara kwa mara na uongo. “Foleni za magari kwa hapa nchini ni zaidi ya janga kwa sababu unaathiri kila sekta ya maisha,” alifafanua.
Kutokana na utafiti huo, madereva wengi wanaofanya kazi katika maeneo hayo, hasa katika mabasi ya mijini (daladala) kwa muda mrefu, wanatajwa kuwa katika hatari ya kupata maradhi ya akili kutokana na kuwa na msongo kwa kipindi kirefu.
“Wengi wao wanavuta bangi, halafu wakichanganya foleni ya barabarani na ugumu wa maisha, huo ni ugonjwa wa akili,” alisema. Wanasayansi wanautaja ugonjwa huo kwa kitaalamu kuwa ni ‘maradhi ya msongo wa foleni’ (Traffic Stress Syndrome).
Kuvunja ndoa
Wataalamu wa masuala ya kijamii wanaeleza kuwa madereva na abiria wamekuwa wakitumia muda mwingi kwenye foleni na kusababisha kupoteza muda ambao wangeutumia kwenye uzalishaji.
Kutokana na hali hiyo, bila takwimu wanasema abiria hao wengi hulazimika kusema uongo kwa kuchelewa katika mikutano ya kikazi, elimu, biashara na wakati mwingine watu kuadhibiwa kwa kuchelewa maofisini na majumbani, jambo linalosababisha kuyumba kwa ndoa.
Hasara zaidi
Mhadhiri wa Uchumi, kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haji Semboja anachanganua hasara ya msongamano katika mtazamo wa upotevu wa muda na mafuta.
Anasema, iwapo magari yatachukua muda mrefu kufika eneo moja, basi hata bidhaa zitapanda bei, kwa sababu mafuta mengi yanatumika njiani. “Chombo cha moto kilichotumia dakika kumi, si sawa na kilichotumia saa nzima, ukijumlisha hasara ya mafuta ni sawa na kujenga barabara zote hapa nchini,” 


UTAJIRI WA MTANGAZAJI DIDA GUMZO!....ATAJWA KUHUSIKA NA UUZAJI WA SEMBE

0
0
Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
AMINI usiamini lakini ndivyo ilivyo! Utajiri wa Mtangazaji wa Radio Times FM ya jijini Dar, Khadija Shaibu ‘Dida’ umeibua gumzo midomoni mwa watu wakidai kuna walakini juu ya upatikanaji wake.
Toyota Verossa ikiwa imepaki pembeni ya ghorofa analodaiwa kumiliki Dida.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Dida ana utajiri mnono lakini anafanya siri ili watu wasiulize alikoupatia kwa sababu si kwa njia halali.
NYUMBA MBILI, MOJA YA GHOROFA
Chanzo kiliendelea kudai kwamba mtangazaji huyo wa Kipindi cha Mitikisiko ya Pwani, ana nyumba mbili. Moja ipo Kigamboni na nyingine ipo Goba ambayo ni ya ghorofa  moja, zote jijini Dar.
“Ile ghorofa ya Goba ni kiboko. Ina uwanja mkubwa ndani kama wa mpira, kuna maegesho ya magari hata kumi. Kuanzia getini hadi mlango mkubwa kumesakafiwa,” kilisema chanzo.
Magari aina ya Toyota Carina na Verossa yote mali za Dida yakiwa yamepaki.
MAGARI MATANO YA KUTEMBELEA
Chanzo chetu kikazidi kwenda mbele kwa kudai kuwa mbali na umiliki wa nyumba, pia mwanadada huyo ana magari matano kwa ajili ya kutembelea tu.
“Mbali na nyumba hizo, Dida pia ana magari matano ambayo hubadili anavyotaka kwa ajili ya kutembelea tu kwenye mizunguko yake.
“Ana Toyota Verossa mbili, ana Toyota Noah rangi ya silva na nyeusi. Ana Toyota Vitz. Hivi karibuni ameanza mchakato wa kuingiza nchini gari lingine la sita aina ya Range Rover ‘Vogue’. Hebu fikirieni, Dida huyuhuyu mnayemjua, amepata wapi mali hizo?” kilihoji chanzo.
Khadija Shaibu ‘Dida’.
YADAIWA ANAUZA ‘UNGA’
Chanzo kilisonga mbele zaidi kwa kusema kuwa, habari za mitaani ni kwamba mtangazaji huyo anatuhumiwa kuuza madawa ya kulevya ndiyo maana ametajirika ghafla.
“Watu wamekuwa wakimsema kwamba fedha zake zinatokana na biashara ya kuuza unga. Si unajua wauza unga wana pesa sana?” kilisema chanzo hicho.
MADUKA MATATU YA NGUO
Katika tafutafuta, mapaparazi wetu waliwahi kuyanasa maduka matatu ya nguo za kike ambayo yapo Kinondoni, mmiliki wake akiwa ni Dida.
Katika mabango ya matangazo, maduka hayo yanasomeka; Dida Classic.
AMETOKA MBALI
Kabla ya kudaiwa kuwa na utajiri huo, wakati fulani Dida aliwahi kukumbana na misukosuko ya madeni ambapo benki moja maarufu jijini Dar es Salaam ilifilisi samani za sebuleni, nyumbani kwake Kinondoni, Dar baada ya kushindwa kulipa mkopo.
Dida akipozi jirani ya gari aina ya Range Rover Vogue alilopanga kulidondosha Bongo.
DIDA ASAKWA
Baada ya kuzinyaka habari hizo, mapaparazi wetu walimtafuta Dida ili kueleza ukweli ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Mimi sipendi kuanika vitu nilivyonavyo au ninavyomiliki ila ni kweli nina nyumba mbili, moja Kigamboni na nyingine Goba ya gorofa.
KUHUSU MAGARI
“Magari ninayo matatu na si matano, hilo Vogue mchakato unaendelea, ukikamilika nitaliingiza nchini.
MIRADI YA DUKA
“Kuhusu miradi yangu mingine siwezi kuianika hadharani kwa sababu, kwanza sipendi kabisa mambo hayo,” alisema Dida.
Toyota Noah kama anayomiliki Dida.
NI KWELI ANAUZA UNGA?
“Watu wamekuwa wakiongea sana kwamba nauza unga kitu ambacho si kweli, kwanza sijui hata huo unga unafananaje! Ila mimi ninajituma sana kwenye kazi pamoja na kufanya biashara mbalimbali.
“Sitasahau siku ambayo watu walikwenda kutoa taarifa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (Dar) kuwa siku hiyo nasafiri na mzigo wa madawa ya kulevya.
“Nilipofika uwanjani nikawekwa chini ya ulinzi na kupekuliwa. Kama haitoshi nilipelekwa Hospitali ya Temeke (Dar) nikafanyiwa X-ray, hawakuona kitu ndipo nikarudishwa uwanja wa ndege kuendelea na safari
“Mimi nawaacha tu waongee watachoka kwa sababu hawajui wanachokifanya, ila mimi najitambua na kile ninachokifanya,” alisema Dida.
Toyota Vitz kama ya Dida.
Akaendelea: “Nilichokuja kubaini ni kwamba kuna wabaya wangu ndiyo walipeleka taarifa za uongo pale uwanjani. Wote huo wivu tu hakuna lingine.
“Kuanzia hapo nikaamua kufanya mambo yangu kimya-kimya, hakuna sababu ya kutangaza kwani wabaya ni wengi, wazuri wachache na si kila anayeku-chekea ni mzuri kwako.”
Source:GPL

WEMA UNATUUMIZA WENZIO ..MWEE NDIO MAANA DIAMOND KADATA KUMBE

0
0
Uwiiii jamani acheni Diamond adate na mtoto wema kwa mapozi yake...Wema Sepetu kwa kweli anamfanya ndugu yetu Diamond awe bubu kwa uzuri wake.

MWEEE....HILI TUKIO LILINIPITA...KWELI NAPE KAOA AMA NI KAMCHEZO KA PHOTOSHOP?

0
0
Nimekutana na hii picha Mtandaoni nikaona nishare na ninyi...Hivi kweli Nape Kaoa hivi karibuni ama ni Photoshop ..? Kama kweli hongera zake ....Maana na Upekuzi wangu hili tukio lilinipita mpaka nalikuta mtandaoni..

NAZIONA DALILI ZA KUMWACHA MKE WANGU..KWA HILI SIWEZI VUMILIA

0
0
Ndugu zangu mwenzenu yamenikuta makubwa. Mimi nimeoa nikiwa mtu mzima sana. Tofauti ya umri na mke wangu ni miaka kumi na kenda. Miezi sita ya kwanza ndoa yetu ilikuwa ya furaha sana na hakika nilionja raha majinuni ya ndoa. Baada ya hapo ni mateso makubwa sana.

". Hasikii la
mwadhini wala la
mtia maji msikitini"

Mke wangu kaanzisha tabia chafu sana na isiyo mpendeza MUNGU na walimwengu pia. Ilikuwa ni mwezi wa saba wa ndoa yetu usiku wa maanani ndipo kiini cha dukuduku langu lilipoanza. Baada ya kufanya tendo la ndoa kwa raundi ya kwanza ndipo mke wangu mpendwa aliponiomba "twende chooni" akimaanisha nimwingilie kinyume na maumbile.

Kwakweli ilibidi nifanye ili kumridhisha na kumuonya kwamba iwe ni siku ile pekee. Kuanzia hapo mke wangu kaweka msimamo kuwa hanipi haki yangu mpaka nimpe "kiu yake"

Nafikiria kumpa taraka mke wangu ukizingatia bado hatujazaa.

Naombeni ushauri wana mmu wapendwa.

". Heri kufa macho
kuliko moyo"

DIVA AZIDI KUONYESHA MAPENZI YAKE KWA KING CRAYZ GK

0
0
Mapenzi yazidi kuchukua nafasi yake katika upande wa mwanadadiva Loveness Love "Diva" kwani ameshindwa kujizuia na kuzidi kuonyesha hisia zake kwa mpenzi wake aliyenaye kwa wakati huu King Crayz GK





SHUKA CHINI KUTOA MAONI YAKO

WOLPER "WAZAZI WANGU NI MATAJARI HAWAHITAJI MSAADA WANGU"

0
0

Staa wa sinema za Kibongo , Jacqueline Wolper amechomoa madai yaliyoibuka kuwa hawajali wazazi wake . Baada ya taarifa hizoza chini chini kuzagaa , Wolper aliibuka na kuzikanusha kama ifuatavyo: “ Wazazi wangu ni matajiri sana, kwa pesa gani nyingi nilizonazo za uwafikia wao kiasi cha kuwapa matunzo???, bado nawategemea hivyo wanaodai nimetelekeza wazazi ni waongo tu.” Aling’aka wolper

GAZETI LA MWANANCHI LAMUOMBA RADHI RAIS KIKWETE

0
0
Jana katika gazeti hili tulichapisha habari iliyokuwa ikielezea kuwa Rais Jakaya Kikwete aliwatembea wagonjwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) jijini Dar es Salaam.

Katika habari hiyo tuliwataja aliowatembelea kuwajulia hali kuwa ni Rajab Maranda, ambaye anatumikia kifungo cha miaka 18 jela kwa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), pamoja na mwandishi wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Salum Mkambala.

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais imeeleza kuwa Rais Kikwete hakwenda kumuona Maranda bali aliwatembelea wanahabari wawili ambao ni Salum Mkambala wa Channel Ten aliyelazwa wodi binafsi D, na Margaret Chambiri wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi aliyelazwa wodi binafsi .

Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa Rais Kikwete aliwajulia hali wagonjwa wengine wawili, John Mhina na Reuben Nyanga ambao wako chumba kimoja na Mkambala.

Tunachukua nafasi hii kuomba radhi kwa Rais Kikwete kwa usumbufu ambao ameupata kutokana na habari hiyo.

CHANZO: Mwananchi.

MASKINI TAMTHILIA YA SIRI YA MTUNGI YAAMBULIA PATUPU TUZO ZA MOVIE AFRICA

0
0
Watanzania tulifurahi kwa habari kuwa Tamthilia yetu ya Siri ya Mtungi imechaguliwa kuwania Tuzo Saba katika  tuzo za Africa Magic Movie Awards 2014’ Tuzo hizo zilifanyika jumamosi hii lakini kwa Bahati Mbaya Haikuweza kupata Tuzo hata Moja...

Kinachoumiza zaidi ni hata katika kipengele ambacho ilikuwa ni lazima Siri ya Mtungi ishinde cha Best Indigenous Language Movie/Series (Swahili) kilichukuliwa na Wakenya, Njoki Muhoho – Mama Duka.

Inatia wasiwasi kidogo kwakuwa hakuna fundi wa Kiswahili duniani kumzidi mswahili mwenyewe wa Tanzania. Inapofikia hadi Mkenya anachukua kile tunachokiweza zaidi, ni ishara kuwa tunahitaji kujitafakari tunakosea wapi. Ni kweli Wakenya ni mafundi wa Kiswahili kuliko sisi? Tatizo ni nini?

“Nadhani kilichopelekea Siri ya Mtungi kukosa tuzo ni vitu viwili, kwanza tabia ya Watanzania sisi kutopenda kupiga kura, hiyo ndio tatizo la kwanza, lakini pili crew ya Siri ya Mtungi yenyewe haikuwa na nguvu kubwa kwenye kushawishi wadau katika upigaji kura. All in all jamaa wako vizuri I hope next year tutafanya vizuri. Nadhani pia waandaaji wa Tuzo zozote Tanzania wamejifunza nini maana ya Tuzo,” anasema King David, mtangazaji wa Kings FM ya Njombe.

David yupo sahihi kwa mmoja. Ni kweli kabisa, lawama ije kwetu sisi wenyewe Watanzania tulioshindwa kuwa wazalendo kwa kuwapigia kura Siri ya Mtungi washinde, lakini mfumo wa tuzo hizo ulikuwa tofauti kidogo. Kulikuwa na jumla ya vipengele 27 na ni vipengele 9 tu kati ya hivyo ndivyo vilikuwa vya watazamaji kupiga kura na kuchagua mshindi.

Kwenye vipengele vilivyokuwa vikipigiwa kura (Votable Categories) Siri ya Mtungi ilikuwa imetajwa kwenye kipengele kimoja tu ambacho ni BEST ACTOR IN A DRAMA alichokuwa ametajwa ‘Juma Rajab Rashid’ aka Cheche.

Vipengele vingine 6 ambavyo Siri ya Mtungi ilikuwa imetajwa, vilikuwa ni vile ambavyo jopo la wataalam limekaa na kuchagua mshindi linayemuona ni bora katika kipengele husika. Mara nyingi katika mfumo wa aina hii, yote yanaweza kutokea na upendeleo na mapenzi ya nchi fulani fulani yanaweza kuchukua nafasi.

Kipengele cha kupigiwa kura alichokuwa ametajwa Cheche, kilikuwa na ushindani mkubwa kutoka kwa Majid Michel ( Somewhere in Africa), Hlomla Dandala ( Contract), Majid Michel (House of Gold) na Tope Tedela (A Mile from Home). Ili Cheche ashinde, alitakiwa kupigiwa kura nyingi sana, na kwakweli haikuwa rahisi kuwazidi waigizaji wa Nigeria ama Afrika Kusini katika kipengele hiki japo yote yanawezekana.

JAY Z AKATAA KUA BEST MAN KATIKA HARUSI YA KANYE WEST

0
0
Kutoka kwenye mitandao tofauti ya Marekani kuna stori zimemake headline zinazowahusisha Jay Z na Kanye West ambao ni washkaji walioshirikiana kufanya album moja ya Watch the Throne ambayo ilitoka August 08 2011.
Story hiyo inasema kuwa Jay Z amegoma kuwa best man kwenye harusi ya Kanye west na mpenzi wake Kim Kardashian.
Miongoni mwa sababu zilizotajwa ni  kusemekana kuwa Jay Z hapendi na hayuko tayari kutokea na kuonekana kwenye Reality Tv show,Jiga ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 44 ni mume wa Beyonce na tayari ni baba wa mtoto wa miaka 2 aitwae Blue Ivy.
Kwa sababu hizo ni kwamba Jay Z hatapenda kutokea kwenye show ya maisha ya familia ya Kardashian maarufu kama The Kardashians,gazeti la Daily Star limeandika kuwa Jay Z ndiye msanii rafiki mkubwa wa Kanye West na anavigezo vyote kuwa msimamizi wake,
Masharti aliyoweka Jay Z amedai atakubali kuwa Best man wa Kanye West endapo kama hapatakuwa na mpiga picha yoyote wa kipindi hicho cha Kim K,mpaka sasa waongozaji wa kipindi cha Kim K na mabosi wa kituo cha E wako tayari kutoa hata dola milioni 1 ilikupata Picha za Jay z na Beyonce kwenye harusi hiyo.

UWEZI AMINI KUMBE DIAMOND NA ALLY KIBA NI NDUGU WA DAMU

0
0
Gossip Cop Soudy Brown leo anazo taarifa zinazomhusu dada wa kaka wawili ambao mara kadhaa imetoka taarifa kuwa hawapatani, sasa leo kupitia dada huyu anadai kumbe hao jamaa ni ndugu.
Clouds FM inapatikana Mbeya kupitia 87.8
Bonyeza play kusikiliza You heard yenyewe

LOWASSA AIKANA NOTI YA SH 500 YENYE PICHA YAKE BADALA YA RAIS

0
0
Kumekuwa na muendelezo wa matukio kadhaa kutoka kwa kikundi cha watu kumuhusisha Mhe. Edward Lowassa na matukio ya uongo na kumzushia vitu vya ajabu kabisa, hususani katika mitandao ya kijamii.

Kumesambazwa picha ya noti ya shilingi mia tano yenye picha ya Mhe. Lowassa. Kitendo hicho siyo utani, bali ni dhihaka na dharau kwa alama za Utaifa na Mamlaka ya nchi. Lowassa Amesema hajui na wala ahusiki na usambazaji wa Noti hiyo Mitandaoni

Mhe. Lowassa anaheshimu maoni ya watu na nguvu ya mitandao ya kijamii, lakini anasisitiza umuhimu kwa wananchi kutumia nguvu hiyo ya mitandao kwa kujadili maendeleo ya nchi yetu badala ya kuwa watu wa kuzusha mambo yasiyo na tija kwa nchi yetu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Mhe. Lowassa (MB)

POSTS ZA WASTARA JUMA INSTAGRAM ZAWAACHA WATU WAKIJIULIZA KUNANI...

0
0
Posts hizi 12 hapa chini zina maana gani ? Ni shukrani tu ama ? embu zisome ..zote ameandika mwigizaji Wastara...aliyekuwa mke wa Marehemu Sajuki












BUNGE MAALUMU LA KATIBA VULULU VULULU

0
0
Matarajio ya Bunge Maalumu la Katiba kukamilisha kanuni kwa maridhiano yaliyeyuka tena jana huku mambo ndani ya ukumbi yakionekana kuwa vululuvululu kwa baadhi ya wajumbe kuzungumza nje ya utaratibu na wengine kurushiana vijembe.

Baadhi ya wajumbe waliamua kutoleana lugha chafu na kuweka kando hoja za msingi zinazowafanya watofautiane na kuchelewesha kazi ya kuandika Katiba Mpya.

Hali ilichafuka mchana wakati wajumbe walipokutana kupitisha kanuni baada ya mmoja wao, Felix Mkosamali kuomba mwongozo kwa Mwenyekiti wa muda, Pandu Ameir Kificho. Hata hivyo, Kificho alimtaka kukaa chini kwa muda kwa maelezo kuwa wajumbe waliofika katika kikao hicho walikuwa wachache, hivyo mwongozo wake kama ulikuwa unahitaji majibu ingekuwa vigumu kutolewa.

Baada ya muda alisimama, James Mbatia na kuomba mwongozo, akihoji sababu za kutaka kuanza kikao cha kupitisha kanuni hizo wakati wajumbe hawajapewa vitabu vya rasimu ya kanuni zenyewe.

“Mwenyekiti ulitangaza asubuhi kuwa tutagawiwa kanuni kabla ya saa tisa lakini hadi sasa tunataka kusomewa kanuni wakati hatujagawiwa kanuni hizo,” alihoji Mbatia.

Kificho alitoa ufafanuzi kuwa kanuni hizo zilikuwa bado zinadurufiwa na kuwataka wajumbe wawe na nidhamu kwani anapotangaza wanapiga kelele.

Ghafla alisimama Mkosamali tena na kuwasha kipaza sauti na kuhoji kitendo cha mwenyekiti huyo kumpa Mbatia nafasi ya kutoa mwongozo wakati yeye amenyimwa... “Mwenyekiti hivi unaongozaje kikao, inakuwaje mimi nikuombe mwongozo uninyime na mwenzangu umpe? Mwenyekiti nakuheshimu sana, lakini sijui unatumia kanuni ipi kutoa nafasi kwa mjumbe wakati mimi ulinizuia nisiseme,” alihoji Mkosamali.

Baada ya kauli hiyo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Hawa Ghasia aliwasha kipaza sauti na kwa sauti ya juu alisema “Mtoto mdogo hana adabu.” Kauli hiyo iliibua hasira za Mjumbe mwingine, Moses Machali ambaye naye aliwasha kipaza sauti na kumjibu: “Kubwa jinga halina adabu,” kauli iliyoibua miguno ndani ya Bunge.

Hata hivyo, licha ya Mwenyekiti kutoa onyo kwa kauli hizo kwamba hazifai, Mkosamali alisimama katika sehemu yake na kusema kuwa hakuna mtoto mdogo na kwamba tangu lini mtoto aliishinda CCM.

Chanzo cha tatizo

Chanzo cha mvurugano huo ambao wiki iliyopita kidogo usababishe ngumi kurushwa bungeni, ni mfumo wa upigaji kura katika kupitisha ibara za rasimu, ambao jana uliendelea kuwagawa wajumbe na kufanya ukumbi huo kuonekana kama eneo la mzaha.

Kauli za ‘ndiyoooo’, ‘hapanaaaa’ na vitendo vya kugonga meza viliongezeka katika kipindi cha asubuhi baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kuandaa Kanuni, Profesa Costa Mahalu kuwaleza wajumbe kuwa kamati yake haijafikia mwafaka wa ama iwe kura za siri au wazi na kwamba suala hilo limerejeshwa kwa wajumbe wenyewe.

Profesa Mahalu alisema uamuzi unaachwa mikononi mwa Kamati ya Kudumu ya Bunge itakayoundwa baadaye. Alisema ili Bunge lisonge mbele baada ya kukwama kwa takribani wiki nzima, vifungu namba 37 na 38 vilivyozua utata vimerekebishwa.

“Tulizungumzia kanuni ya 37 na 38 zinazoelezea utaratibu kufanya uamuzi. Kanuni hizo sasa zitaeleza tu kwamba utaratibu wa uamuzi utakuwa ni wa kura, bila kusema ni ya siri ama ya wazi,” alisema na kuongeza: “Lakini tumeona ni vizuri tukaweka fasili nyingine katika kifungu cha 38 ambayo itaeleza waziwazi kwamba ni aina gani ya kura itakayotumika na kwamba hiyo itategemea itakavyoamuliwa na Bunge hili.

Wajumbe wapinga

Mjumbe Profesa Ibrahim Lipumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa CUF, alisema walichokubaliana katika Kamati ya Mashauriano ni kinyume na kilichoelezwa na Kamati ya Profesa Mahalu.

Alisema walikubaliana kuwa kifungu cha 37 na 38 visomeke kuwa mambo nyeti yaliyomo katika rasimu ya Katiba, yapigiwe kura ya siri na ya kawaida yapigiwe kura ya wazi.

“Tulichokubaliana ni tofauti kabisa na hiki ambacho kamati imekiwasilisha. Hatuwezi kufanya uamuzi wakati hatujafikia mwafaka,” alisema Profesa Lipumba.

“Huku ni kukwepa uwajibikaji na haiwezekani tupitishe kanuni wakati baadhi ya vifungu havijakamilika. Kamati imepinga makubaliano yetu,” alisema.

Mjumbe David Kafulila alisema: “Kwa namna tunavyokwenda, hakuna kinachoendelea, bado pande mbili zinavutana na kusababisha masuala yakwame. Tukikutana jioni (jana) na bado hali ni hii ya kupata taarifa nusunusu ambazo hazina mwafaka kuhusu jambo hili, tukubaliane kwamba semina hii isimame kwa muda, watu warudi majumbani kwao ili wafanye makubaliano huko nje.”

Mwenyekiti Kificho alimjibu akisema Rais Kikwete ndiye aliyeitisha Bunge hilo na kwamba hata uamuzi wa kulivunja utafanywa na yeye.

Mjumbe Ezekiah Oluoch alisema iwapo Kamati ya Maridhiano iliyoanza kuketi Ijumaa imeshindwa kukubaliana, kilichopo sasa ni sekretarieti kuandaa karatasi za kura.

“Kwamba sisi tulikuchagua kwa kutumia kura ya siri, sasa tupige kura ya siri ambayo itaamua kura ambayo tunaitaka. Ikiwa tunakuja hapa jioni ukatuletea rasimu ya kanuni ambayo haina vifungu hivi 37 na 38 vya namna ya kufanya maamuzi, sidhani kama umetutendea haki kupitisha vitu nusu,” alisema.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alijikuta katika wakati mgumu baada ya kuzomewa na baadhi ya wajumbe kwa madai ya kuwapotosha.

MWEEE! ETI YESU KAONEKANA MAENEO YA SINZA JANA....JIONEE

0
0
Habari ndio hiyo ..Jamaa Kaonekana Mitaa ya Sinza Kijiweni Jana....Mwee Ndio Yesu karudi Ama?

MCHUNGAJI ANAYE HUBIRI AKIWA NA NYOKA SHINGONI AFARIKI DUNIA BAADA YA NYOKA HUYO KUMG'ATA

0
0
Pasta anayejulikana kuhubiri akiwa amemweka nyoka shingoni ameaga dunia. Pasta Jamie Coots anayeamini kuwa kinga hutoka kwa mungu aliweza kupoteza maisha yake baada nyoka huyo wa sumu kumuuma akiwa akihubiria mbele ya maumini.

Ilikuwaje hadi pasta huyo kuhubiri na nyoka mgongoni?

Kupitia andiko la Marko 16:15-18, pasta huyo anaamini kuwa Yesu aliweza kuwaambia wakristo wote kuwa wanaweza kushika nyoka na hatawaumiza wala kuwadhuru bora tu uwe umebarikiwa na mungu mwenyewe.

Pasta huyo wa kanisa la Full Gospel Tabernacle in Jesus Name aliumwa na nyoka huyo mbele ya kanisa lake na ilimbidi kukimbizwa hadi nyumbani kwake bila kupelekwa hospitalini.

Wauguzi walipowasili nyumbani kwake waliweza kufukuzwa huku pasta huyo akiwa na imani kuwa mungu atamtibu ugonjwa wake, jambo ambalo halikufanyika

MAMBO SITA USIYOYAFAHAMU KUHUSU NDEGE YA MALAYSIA ILIYOPOTEA

0
0
Ndege ya shirika la ndege la Malaysia (Malaysia Airlines).
Kuna mambo ambayo watu hawajafahamishwa kuhusu ndege ya shirika la ndege la Malaysia (Malaysia Airlines) safari namba Flight 370 ambayo imepotea ikiwa eneo la juu ya bahari katika Ghuba ya Thailand na watu 239.
Ndege hiyo aina ya Boeing 777 iliyopotea Jumamosi asubuhi wiki iliyopita na kutoonekana mpaka leo imewababaisha wataalam wengi duniani wa mambo ya usalama wa vyombo vya anga.

Hata hivyo, pamoja na mkanganyiko huo, gazeti la Wall Street Journal limeorodhesha mambo ambayo watu wengi hawayafahamu kuhusiana na kupotea kwa ndege hiyo. SOMA ZAIDI
Mambo hayo ni yafuatayo:
Ndege zote za Boeing 777 zina kisanduku maalum cha kutunza kumbukumbu za mawasiliano ya marubani wa ndege na waongoza ndege walioko ardhini (black box) ambacho hakiwezi kuharibika katika mlipuko wowote unaoweza kutokea kwenye ndege.
Kijisanduku hicho (black box) kina nguvu za kurusha mawimbi kuonyesha kilipo kwa siku zisizopungua 30 baada ya kuanguka baharini.

Hata hivyo, wataalam wameshindwa kunasa mawimbi ya chombo hicho na hivyo kuwa na wasiwasi kwamba huenda kimeharibiwa na nguvu kubwa isyokuwa ya kawaida.
Sehemu nyingi zilizoharibika za ndege huwa zinaelea juu ya maji baada ya ndege kuanguka baharini au majini.
Katika tukio hili hakuna kilichoonekana, na hivyo kuzua hofu kwamba ndege hiyo huenda imetoweka katika eneo la Dunia.
Iwapo kombora lingeipiga ndege hiyo, basi kombora hilo lingeonekana katika vyombo vya uchunguzi vya kijeshi na vya usalama wa safari za anga. Hii ni pamoja na kwamba huenda imepigwa na kombora na kuikatakata ndege hiyo katika vipande vidogo-vidogo.
Katika nadharia hii, hakuna dalili zozote zilizonaswa na vyombo vya ulinzi na usalama kuonyesha kulikuwa na kombora lililohusika.
Pamoja na eneo ambalo ndege hiyo ilikata mawasiliano na kupotea kufahamika, bado wataalam wameshindwa kujua iko wapi.
Kufahamu eneo la tukio, mwelekeo na kasi ya ndege hiyo, bado hakujasaidia kupatikana kwa ndege hiyo, hivyo kuzidisha hofu inayowachanganya wataalam.
Iwapo Flight 370 ilitekwa, isingeacha kuonekana kwenye vyombo vya kudadisia nyendo za vyombo vya angani (radar).
Nadharia ya kutekwa haina msingi wowote, kwani ndege zinazotekwa huwa hazitoweki katika radar.


HITIMISHO: Ndege hiyo ya Boeing 777 haikulipuka angani, bali imetoweka!

NGUO FUPI YAMTOKEA PUANI DADA HUYU ..AFUATWA NA MIDUME YENYE UCHU KAMA NYUKI

0
0
Jamani Wadada Tuweni Makini na Mavazi hasa tunapoenda sehemu zenye mkusanyiko wa watu mbali mbali ..Kama kariakoo na mjini City Center Kwa hapa Dar si Sehemu nzuri ya kuvaa mavazi mafupi yenye kuonesha viungo adimu katika mwili...Huyu Dada alimfika baada ya kuvaa kimini na kukatiza mitaaa bila woga ....Ona kundi ka wanaume wenye uchi wakimfuata nyuma huku mate yakiwadondoka.....Mweeeee

OLE SENDEKA ATOKA KWENYE UKUMBI WA BUNGE HUKU AKIFUTA MACHOZI

0
0
Mara baada ya mbunge mmoja kusimama na kumuomba Mwenyekiti wa Bunge Pandu Ameir Kificho awatake watendaji wake wagawe vikaratasi vya kura ili ipigwe kura ya siri wachaguwe aidha siri au wazi na kuondokana na kanuni hizo zilizodumumu takriban siku kadhaa bila ya kupatiwa ufumbuzi na wajumbe wengi kuunga mkono.


Mh Ole Sendeka ameonyeshwa na kamera za bungeni akiwa amebeba mafail yake na kutoka nje ya ukumbi wa bunge huku akifuta futa machoz.

MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA ACHAFUA HALI YA HEWA BUNGE LA KATIBA

0
0
Dodoma, Tanzania. Mchungaji Christopher Mtikila amechafua hali ya hewa bungeni, hivi punde kwa kumtaka Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Pandu Kificho amueleze ni kwanini tangu jana amekuw akimnyima nafasi ya kuzungumza bungeni.

Mchungaji Mtikila alisimama ghafla na kusema: Mwenyekiti kwanini unaninyima haki yangu ya kuzungumza, nataka kujua kwanini unaninyima haki ya kuzungumza. Kuzungumza ni haki yangu."


Mchungaji Mtikila amezungumza kwa jazba huku wajumbe wengine wakimzomea, lakini bila uwoga aliendelea kuzungumza na kusema yanayofanyika Mungu anapenda na yeye ana amini katika Mungu, lakini "Wewe Mwenyekiti inaonekana kuwa hupendi Mungu."

Wakati Mchungaji Mtikila akimwakia Kificho, Felix Mkosamali alilipuka na kumwambia mwenyekiti kuwa tangu jana pia anamnyima nafasi.
"Ninyi mmejipanga, kupitisha kanuni mbovu, alafu sisi wengine hamtupi nafasi," amesema Mkosamali.

Mwenyekiti Kificho aliwajibu kuwa kwa bahati mbaya wamekosa nafasi na hivyo wawe wavumilivu.

Kificho anatangaza utaratibu wa kumchagua Mwenyekiti wa kudumu wa Bunge na wajumbe wanaotaka kugombea nafasi hiyo wametakiwa kuchukua fomu ya kugombea.

Bunge hilo limeahirishwa mpaka kesho na kanuni zitaanza kufanya kazi rasmi.
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images