Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live

CCM Yapinga Mpango wa Madiwani wa CHADEMA Kukopeshwa Magari Arusha...

$
0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimepinga mpango wa madiwani wa Halmashauri ya Meru inayoongozwa na Chadema kukopeshwa magari.

Akizungumza katika ziara ya Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo, Lekule Laizer wilayani humo, Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Langaeli Akyoo alisema wameshangazwa madiwani kukopeshwa Sh9 milioni kila mmoja, huku wananchi wakiendelea kuteseka kwa kero mbalimbali.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Bakari Sajini alipinga tuhuma hizo na kueleza kuwa hakuna kikao cha madiwani kilichopitisha uamuzi huo, lakini kinachofanyika ni madiwani kupitia posho ya Sh350,000 wanayolipwa kila mwezi kuitumia kukopa benki.

“Kama katibu wa baraza la madiwani sina hizo taarifa, ninachojua kuna madiwani wametumia posho zao kukopa benki za CRDB na NMB kulingana na mahitaji yao na jambo hili lipo nje ya halmashauri,” alisema mkurugenzi huyo.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alipinga madai ya CCM akieleza kuwa hataki siasa za malumbano na chama hicho katika jimbo hilo, huku akisisitiza aachwe afanye kazi za kutatua kero za wananchi.

Awali, akielezea kero zinazowakabili wananchi, katibu wa CCM wa wilaya hiyo alisema mojawapo ni kuwapo kwa barabara mbovu.

Alisema kabla ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana, halmashauri hiyo ilinunua tingatinga kwa ajili ya ukarabati wa barabara ambazo zimekuwa zikiharibika kila wakati.

Katibu huyo alisema baada ya uchaguzi huo Chadema ilishinda ubunge na pia kuongoza halmashauri, lakini ilibadili matumizi ya tingatinga na kuanza kulikodisha kwa watu binafsi.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo alisema wakati anahamia alikuta nyaraka ambazo ziliachwa na madiwani waliopita zinazotaka tingatinga hilo kujiendesha.

Baba yake Peter Manyika wa Simba Adai Mwanane Ameshuka Kiwango Kutokana na Kuendekeza Mapenzi

$
0
0
Baada ya kuona kipaji cha mwanae kikipotea wakati akiwa na kazi kubwa ya kulitumikia taifa lake, Baba mzazi wa kipa wa klabu ya Simba, Peter Manyika Jr, Manyika Peter ameibuka na kumkoromea mwanae.

Baba mzazi huyo alisema kinachomponza mwanae ni kukosa nidhamu na pia kutekwa na mahusiano ya kimapenzi aliyonayo kwa sasa.

Akizungumza kwa uchungu, nyota huyo wa zamani wa Sigara, Mtibwa Sugar, Yanga na Taifa Stars, alisema mwanaye anapotea kwa sababu ya kuendekeza starehe na huwa anajisikia vibaya anaposikia akiwajibu mbovu waanahabari na hata viongozi wake kuhusiana na sakata lake la mambo ya mapenzi.

“Amesajiliwa Simba afanye kazi siyo kula mshahara wa bure na kuishia kukaa benchi, viongozi hawana tatizo kama angekuwa msaada angepangwa lakini yeye ajiulize na hayo mahusiano aliyonayo kama yanamsaidia katika kazi yake?” Alihoji bila kumuweka hadharani binti huyo anayemzingua Manyika

“Akipata jibu na atarudi kwenye mstari, kama mzazi najisikia uchungu sana kwa yale anayoyafanya mtoto wangu kwa sababu najua maisha ni nini lakini yeye anaona mjanja ila nina shaka hapo mbele asije akaumizwa vibaya,” alisema Mzee Manyika.

Aliongeza, “Nimecheza nafasi kama yake kwa mafanikio makubwa, ndiyo maana nasema kwa uchungu kwamba jibu ni mwanangu wala siyo viongozi yeye ndiye chanzo kwa sababu wasingeweza kutupa pesa yao bure kumsajili kwa mkataba wa miaka mitatu kama pambo bali kwa ajili ya kufanya kazi yao,”

Pia alisema kuwa hawezi kumkataza mwanae kuendelea na mapenzi na mwanamke aliyenaye, isipokuwa ni vema kuangalia mustakabali wake kwa sababu mtaji wake ni kipaji cha soka na akizembea atakuja kujuta mbeleni.

“Kipindi nilichokuwa nacheza na staa katika jamii nilifuatwa na wanawake wa kila aina na wengine kutaka wagharamikie kwa kila hali lakini nilikuwa na msimamo na kupuuza mambo yao na sitaki mwanangu aangamie,” alisema Manyika.

Kipa Manyika aliposakwa kwa njia ya simu, hakupokea simu aliyopigiwa, lakini kocha wa makipa wa Simba Adam Abdallah, alisema kinachofanya Manyika Jr, asugue benchi ni kutokana na kukosa nafasi mbele ya Vincent Angban aliyepo juu kwa sasa lakini mchezaji huyo si mbaya

Atumbuliwa Jipu Kwa Kumdanganya Waziri Mkuu

$
0
0
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Machi 16, 2016) alipokuwa akiwahutubia mamia ya wakazi wa mji wa Chato waliojitokeza kumsikiliza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wilayani Chato, mkoani Geita.

Waziri Mkuu ambaye amewasili mkoani Geita kwa ziara ya siku mbili akitokea mkoani Kagera, alisimamishwa na wakazi wa kijiji cha Kalebezo, kata ya Nyamirembe, wilayani Chato na kukuta mabango yaliyokuwa yakidai maji safi na kuelezea uharibifu wa pampu ya maji.
Katika maelezo yao, wakazi hao walimweleza Waziri Mkuu kwamba mradi wa maji kwenye kata hiyo ulishakamilika lakini pampu yao imechukuliwa na kupelekwa Morogoro jambo lililosababisha wakose maji kwa muda mrefu.

Kwa sababu alikuwa hajafika Chato mjini na hakuwa na taarifa sahihi za mradi huo wa maji, Waziri Mkuu aliwaeleza wakazi hao kwamba analibeba jambo hilo na atafuatilia hadi aelezwe ni kwa nini pampu hiyo imepelekwa Morogoro.
Akiwa kwenye mkutano wa hadhara, ndipo suala la maji likaibuka tena na Waziri Mkuu kuamua kuchukua hatua hiyo.

“It’s unethical (ni kinyume cha maadili) kumdanganya kiongozi wako. Nimekuuliza mara mbili mbili kama una uhakika kuwa pampu hiyo ipo ukasema una uhakika kuwa ipo. Nimemtuma diwani na vijana wangu wakacheki wakasema hakuna pampu,” alisema Waziri Mkuu na kumwita Diwani huyo jukwaani ili atoe majibu.

“Pale kulikuwa na pampu mbili; moja ni ya kuvuta maji kutoka kwenye kina kirefu na kuyapeleka kwenye pump house na nyingine ni ya kuvuta maji kutoka kwenye pump house na kuyapeleka kwenye tenki kubwa la kuhifadhia maji. Ile ya kutoa maji kwenye kina kirefu ndiyo haipo, wataalamu wanajua wameipeleka wapi,” alisema Bw. Charles Manoni ambaye ni diwani wa kata ya Nyamirembe ambayo kijiji cha Kalebezo kimo.

Waziri Mkuu alisema ahadi ya Serikali ya awamu ya Tano ni kuwatumikia wananchi kwa uadilifu.
“Lazima watumishi wa umma wabadilike na kuanza kuwatumikia wananchi kwa dhati. Hatuwezi kuwa na watumishi waongo ambao wanamdanganya hata Waziri Mkuu.”
“Kuanzia sasa, Engineer atakaa pembeni, polisi na TAKUKURU wamchunguze. Asitoke Chato hadi uchunguzi ukamilike. Nataka kujua nani alichukua hiyo pampu na kwa kibali gani. Tukijiridhisha atarudi lakini kwa sasa hivi akae kando,” alisema.

Mapema jana mchana, akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Geita na wilaya ya Chato mara baada ya kupokea taarifa zao kwenye ukumbi wa Halmashauri, Waziri Mkuu alimpa fursa Mhandisi huyo aeleze nini kimetokea kuhusu pampu inayodaiwa kupelekwa Morogoro lakini akakanusha na kudai kuwa ipo palepale kijijini.

“Una uhakika na hayo unayoyasema? Hiyo pampu ipo kweli kijijini? Nikienda nitaiona?” alihoji Waziri Mkuu na kujibiwa mara mbili na mhandisi huyo kwamba ana uhakika asilimia 100 kwamba pampu ipo na wala haijaenda Morogoro.

Alipotaka kujua ni kwa wananchi wa kijiji kile hawana maji kutokana na ubovu wa pampu hiyo, alijibiwa kwamba mradi ule ulikuwa chini ya mamlaka ya maji ya mji wa Bukoba (MBUWASA) ambako wilaya hiyo ilikuwepo zamani kabla ya kuhamishiwa kwenye mkoa mpya wa Geita mwaka 2012.

Mhandishi huyo alisema amekuwa akifuatilia fedha za matengenezo kutoka kwa Mkurugenzi wa MBUWASA bila mafanikio, ndipo Waziri Mkuu akamuagiza aende nje ya ukumbi huo akapige simu na kumletea majibu ni lini fedha hizo zitapatikana ili wananchi wa kijiji kile waendelee kupata maji.

CUF Watoa Tamko Jipya......Wampinga Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Aliyesema jana kuwa Kuna Amani ya Kutosha Zanzibar

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara) , Magdalena Sakaya akionyesha picha ya mhanga wa vipigo zanzibar.
****
WAKATI uchaguzi wa marudio ukitarajiwa kufanyika jumapili visiwani Zanzibar, Chama Cha Wananchi (CUF) kimesema kuwa haki za binadamu zimeendelea kuminywa kwa kiasi kikubwa visiwani humo huku wafuasi wa chama hicho wakilengwa zaidi.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara) , Magdalena Sakaya, ambaye pia ni mbunge wa viti maalum, ameyasema hayo leo wakati alipozungumza na waandishi wa habari kwenye Makao Makuu ya Ofisi za Chama hicho zilizopo Buguruni  jijini hapa.

Magdalena amesema kuwa Tanzania imeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu hivyo mambo yanayotokea Zanzibar ni ya kushangaza na hayapaswi kufumbiwa macho kwa ustawi wa Taifa.

Amesema kuwa baada ya CUF kutangaza kujitoa kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi wa marudio , wananchi wa Zanzibar wamekuwa wakiishi kwa hofu huku vikundi vya matukio ya uhalifu maarufu’mazombi’ yakipiga watu pasipo na kuchukuliwa hatua zozote na vyombo vya usalama.

“Mara kwa mara tumekuwa tukiwaambia jeshi la polisi kuhusiana na haya mazombi ila cha kushangaza hadi leo hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusiana na kukamatwa kwa makundi hayo ya mazombi,”alisema.

Chama hicho kimesema kuwa viongozi wao kadhaa wamekamatwa kwa nyakati tofauti ambapo jana Mkurugenzi wa Habari na Uenezi Taifa -Hamad Masoud, alikamatwa na kuwekwa kizuizini na Polisi baada ya kutoa taarifa ya matukio mbalimbali yanayoendelea visiwani humo ambayo ni ya kinyume na haki za binadamu.

“Jambo la kushangaza kila tukio baya likitokea wanasingiziwa wafuasi wetu, mara kwa mara wamekuwa wakikamatwa na tangu januari hadi sasa zaidi ya wafuasi 60 wamekamatwa kwa madai ya kuhusika na uvunjifu wa amani,”alisema.

“Sisi tumeamua kujitoa kwenye uchaguzi huo ili wananchi wetu wawe huru na kuwaepusha kwenye vurugu, kwa hiyo
Chama cha Mapinduzi kisiwalazishe wananchi kufanya mambo ambayo wenyewe hawako tayari kuyafanya na kuyaona ni kinyume na Katiba, kwa sababu uchaguzi huo wa marudio ni haramu.

“Asilazimishwe mbuzi kunywa maji wakati hana kiu,”alisema Magdalena na kuongeza kuwa wangetegemea uchaguzi huo kufanyika kwa amani baada ya kutangaza kujitoa mapema mwaka huu.

Magdalena alisema kuwa yapo maeneo kadhaa visiwani humo wananchi wamepigwa marufuku ya kutoonekana wakitembea kuanzia saa mbili usiku hatua inayosababisha hata wengine kushindwa kwenda kufanya ibada.

Akizungumzi kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, ya kusema kuwa hakuna watu wanaopigwa visiwani humo, Kiongozi huyo wa Chama alipinga madai hayo na kusema kuwa ni hatari kuudanganya umma kwa kuficha ukweli na kuacha watanzania wateswe.

Aliishauri Serikali kuhakikisha kuwa usalama wa wananchi visiwani humo unaimarishwa kwa kufuata misngi ya haki za binadamu na utawala bora, pia ichukue hatua dhidi ya ‘mazombi’ ambayo yamekuwa yakiripotiwa kupiga watu kwa nyakati tofauti. 

Akina Dada, Sio Kila Ex Wako Anayeomba Mrudiane Anamaanisha...

$
0
0

Sio Kila EX wako anayeomba Mrudiane anamaanisha! Wengine huomba kurudi ili wakutesti tu jinsi ulivyo Mbulula,jinsi usivyo na msimamo na jinsi ulivyo CHEAP na huna Misimamo wala Future.
Jitu mmeachana miezi 6,leo linakutesti lirudishe majeshi,na wewe ulivyo kiazi,upo-upo tu,ina maana miezi yote hii ulikuwa umeganda unasubiria rehema zake ama??


Kurudia Matapishi ya EX ukitegemea Amebadilika ni Sawa na Kupika Sufuria la Makande kwa Mshumaa,Utaambulia Masizi tu..
Kipi kipya kakiona kwako hadi arudi??Nini Kilimshinda huko nyuma ambacho leo anakiweza anataka kurudi??Akafie Mbele huko.


KUWA NA MSIMAMO,Ukisema Its Over umaanishe,sio unakuwa na hisia zinapepea tu kama Bendera ya Katibu Kata wa Kishumundu...Mtu kama Hajielewi achana nae,siku akijirudisha mwambie kwanza akapimwe Minyoo ya Kinyarwanda.
Umekazana kuwaambia marafiki zako 'Siku hizi hakuna Mapenzi ya dhati watu wote Majanga tu',nani amekwambia hayapo??Yapo sana ila wewe unatumia mbinu tofauti..Huwezi kusoma Degree ya Law halafu u-apply kazi ya Chief Accountant wa Bodi ya Tumbaku...Kila siku utasingizia Balance Sheet haina Jurisprudence..Lawyers mmenielewa!


Acha kudate watu wasiojielewa,Usidate kwa sababu uko lonely,Usiwe desperate kuingia Mahusiano kwa sababu shosti zako wanakusimulia walivyopelekwa Ruwenzori Waterfalls..Ingia kwenye Mahusiano pale Moyo wako ukiwa tayari na mtu uliyemfia kihisia na amekuwa approved na Veins,Auricles,na Aorta za Moyo wako kwamba He/She is really the One..
Unadate na mtu ambaye mustakabali wake mwenyewe haujui,ukimuuliza anataka kuwa wapi ndani ya miaka 5 ijayo anakwambia Mungu anajua dont worry,halafu BBM na Instagram unajiita Baby Ake Mie Iam in Love..Utaishia kufua boxer hadi kucha zinukie gololi!


Mbwa kamwe hashughuliki na kesi za Paka kufungiwa kabatini.Date the Right Person,With Right reasons,in a Right Time uone kama Mapenzi hayapo...

Ni Nani Aliyemtuma Balozi Juma Mwapachu Kurudi Katika Chama Cha Mapinduzi ili Kunusuru Biashara zake na Rafiki zake?

$
0
0
ALIYETUKANA na Kumdhalilisha Mama Maria Nyerere na Mh Mzee Alli Hassani Mwinyi.
Wahenga walisema kuwa ukimwona Mbwa juu ya mti ujue kapandishwa!

Balozi Juma Mwapachu ametangaza kurudi ndani ya Chama cha Mapinduzi. Amesema ameamua kurudi ndani ya chama hiki baada ya kuondoka na kukikana kikiwa katika uchaguzi mkuu tarehe 13.10.2015. Balozi anasema aliondoka kwa sababu alichukizwa na chama kumuondoa Mh. Lowassa katika kinyang'anyilo cha Urais.

Juma Mwapachu anachagiza sababu yake hiyo kwa kusema kuwa walikubaliana wao wiki mbili kabla ya kupiga kura waondoke ndani ya chama kwa mkupuo ili chama kiweweseke na kushindwa vibaya.

Kwa kauli yake hii Balozi Mwapachu anasema kuwa alidhamiria kukiangusha chama hiki ili kishindwe katika uchaguzi mkuu. Kwa maana nyingine anasema kuwa kama matarajio yake haya yangalitimia hakuwa na mpango na Chama cha Mapinduzi kwani angeteuliwa kuhudumu kama waziri wa mambo ya nje kupitia serikali ya upinzani.

Nani kamtuma Balozi Mwapachu kusema kuwa ameamua kurudi katika chama cha Mapinduzi ili kunusuru biashara zake na rafiki zake? Nini maana ya maneno haya?

Ukimsikiliza vema Juma Mwapachu utaona kuwa swala la kuondoka ndani ya chama na kurudi ni uamuzi wao kwa maslahi binafsi kana kwamba CCM na serikali hii ni mali yake na rafiki zake.

Mwapachu amesema ameamua kurudi ndani ya Chama cha Mapinduzi leo. Kwa kauli yake ni kwamba hakuomba kurudi ndani ya chama isipokuwa ameamua tu kurudi na akapokelewa kama shujaa!

Kwa uamuzi huo Mwapachu anadhihirisha kuwa bado anao uwezo mkubwa yeye na washirika wake wa kuamua watakavyo ndani ya CCM.

Jambo muhimu kuliko yote katika filamu hii Mwapachu ni kuwa yeye ameamua kuwataja wasaliti wengine ambao alishirikiana kuhujumu chama wakati wa uchaguzi. Viongozi wa CCM Kata ya Mikocheni waliompokea katika kipindi ambacho Mwenyekiti wa Chama Taifa ametangaza kiama dhidi ya wasaliti wa chama. Wamempokea kwa kuvunja taratibu za chama, hawa wamedhihirisha kuwa wamekua na ushirikiano wa karibu na Balozi Mwapachu hata baada ya yeye kukihama chama.Balozi ametoa pesa sh. milioni moja ya ukarabati wa ofisi ya Kata ambayo waliitumia kupanga mipango ya kukihujumu chama cha Mapinduzi. Nitunze nikutunze!

Kwa mujibu wa kanuni ya UONGOZI NA MAADILI ya chama cha Mapinduzi toleo la 2012, katika FUNGU LA NNE, Ibara ya(8)Ibara ndogo ya (2) kipengele namba (ix) inalitambua kosa la Balozi Mwapachu,kosa la usaliti kama kosa kubwa kuliko yote ndani ya Chama cha Mapinduzi na adhabu yake ni kufukuzwa uanachama. Adhabu hiyo imefafanuliwa vizuri katika kipengelele hicho cha tisa sehemu ya (a-c).(Tafadhari rejea)

Balozi Juma Mwapachu alikisaliti chama wakati ambapo chama kilihitaji zaidi msaada wake,akakiacha kiangamie kwa bahati kikanusurika kwa mapenzi ya Mungu.

Kwa mujibu wa Katiba ya CCM Toleo la 2012,Juma Mwapachu alipoondoka CCM na kujiunga na chama kingine akawa amejifukuzisha mwenyewe uanachama wa CCM.

Mwapachu ameamua kurudi CCM kwa namna ya pekee! Amewaita waandishi wa habari,akatangaza kuwa ameamua kurudi CCM na Viongozi wa Kata ya Mikocheni wakampokea na kumkabidhi kadi ya Chama.

Kwa maneno mengine ni kuwa hakuna vikao vya chama vilivyoketi kumjadili Mwapachu pamoja na uzito wa jambo lenyewe. Mwapachu ana jeuri kubwa!

Kimsingi Mwapachu ameonesha jeuri kubwa,kiburi na dharau kubwa katika chama kikongwe na Imara kama CCM. Mtu mmoja aliwahi kuniambia kuwa Lowassa ana nguvu kubwa na jeuri ya ajabu,sikuelewa maana yake kwa wakati huo,baada ya tukio hili la Mwapachu naanza kuona maana ya maneno yale. Ni imani yangu kuwa Lowassa ameanza mikakati rasmi. Anajiandaa na ushindi kama alivyoahidi ktk balaza kuu la chama chao. Hii ndio tabia yake!

Ni nani aliemtuma Balozi Juma Mwapachu?
Sijaelewa ni kwa namna gani Mwapachu amekua na jeuri kubwa kiasi hiko dhidi ya chama tawala na hata apate nafasi kubwa ya kukidhihaki chama mbele ya waandishi wa habari. Zamani hapakua na michezo kama hii maana baada ya kauli yake hatua kali zingefuata nyuma yake.

Balozi Juma Mwapachu ametudhihaki vya kutosha!
Ametudharau vya kutosha!
Ametuonea vya kutosha.
Hivi ni nani aliemtuma Balozi Juma Mwapachu?

HAPA KAZI TU

Chanzo:Jamii Forums

Hii Ndio Sababu Iliyomfanya Diamond Amchukue Raymond Ajiunge WCB..Ipi Hiyo?

$
0
0
Msanii mpya kwenye lebo ya WCB,RayMond amefunguka na kusema kuwa alikutana na Diamond kupitia Maromboso ambaye alitaka atoe maoni yake kwenye wimbo mmoja wa Diamond.

RayMond amesema kuwa kadri alivyokuwa akifanya kazi na Diamond kwa kutoa mawazo yake ndipo Diamond alipoona kuwa yeye anaweza hivyo kumwomba Babu Tale amsadie kwa kuwa Tip Top kuna wasanii wengi.

“Diamond alimwambia Tale kwamba anataka kunisaidia,kwa sababu Tip Top kuna wasanii wengi,na WCB kuna msanii mmoja ambaye ni Harmonizer,kwa hiyo aliamua kunichukua kwa sababu aliona nina kitu”

Shindano la Miss Tanzania Kuanza Tena Rasmi Baada ya Kufungiwa....Tarehe ya Ufunguzi Yatajwa....

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika ufunguzi wa Mashindano ya Miss Tanzania mwaka 2016  yatakayofanyika Machi 19, 2016 jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia mashindano hayo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Lino International Agency Limited kampuni inayoandaa  mashindano hayo Bw. Hashim Lundenga amesema kuwa uzinduzi huo kwa mwaka 2016 utakuwa wa aina yake tofauti na miaka iliyopita.

“Tunatarajia kutangaza kamati mpya ya Miss Tanzania siku hiyo ya uzinduzi, kamati ya Miss Tanzania itakuwa na jukumu la kuusaidia uongozi wa Miss Tanzania katika shughuli nzima za kuratibu na kusimamia mashindano hayo.” alisema Lundenga.

Lundenga ameongeza kuwa, katika uzinduzi huo wadau mbalimbali wa tasnia ya urembo wakiwemo wabunifu wa mavazi, mawakala wanaoandaa mashindano ya Miss Tanzania katika ngazi mbalimbali hapa nchini watakutana .

Aidha  amesema uzinduzi wa Miss Tanzania mwaka 2016 umedhaminiwa na makampuni ya Ramada Resorts Dar, Naf Beach Hotel Mtwara, Kitwe General Trader, CXC Africa, MMI Tanzania, Mwandago Invesment Ltd, Break Point na GSM Media.

Vilevile uzinduzi huo utahamia mkoa wa Arusha mara tu baada ya kufanyika  mkoa wa Dar es Salaam. Wasanii Linah Sanga anayeimba nyimbo za kizazi kipya na Wanne Star msanii wa ngoma za asili watatoa burudani katika uzinduzi huo.

Mashindano ya Miss Tanzania yalifungiwa kwa miaka miwili mfululizo na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Desemba 22, 2014 kutokana na kukiuka Sheria, Kanuni na Taratibu za uendeshaji matukio ya Sanaa nchini, kutokuwasilisha nyaraka mbalimbali za shindano lake hususan mikataba ya washiriki pamoja na kutumia mawakala wasiosajiliwa na kupewa vibali vya BASATA.

Mashindano hayo yamefunguliwa tena na BASATA Agosti, 2015 baada ya mwandaaji wake LINO International Agency Limited kufuata taratibu ikiwemo kuomba radhi  na kuyafanyia kazi baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza pamoja na kutekeleza masharti aliyopewa

Mahakama Yataka Upelelezi wa Kesi Ya Wabunge Halima Mdee, Mwita Waitara na Saed Kubenea Ukamilike Haraka

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi haraka ili kesi inayowakabili wabunge watatu wanaotokana na Ukawa na madiwani wao ianze kusikilizwa.

Washtakiwa hao ni pamoja na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee, Mwita Waitara (Ukonga) na Saed Kubenea (Ubungo).

Madiwani wanaoshtakiwa katika kesi hiyo ni Ephrein Kinyafu (Kimara), Manase Njema (Kimanga, Tabata) na kada wa chama hicho, Rafii Juma.

Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alitoa kauli hiyo jana baada ya Wakili wa Serikali, Mbunito Aloyce kudai kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa kwa kuwa upelelezi wake haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine.

Wakili Peter Kibatala anayewatetea washtakiwa hao, aliuomba upande wa mashtaka kuanza kuisikiliza kesi hiyo kwa sababu washtakiwa walikamatwa haraka haraka na usikilizaji wake uwe vivyo hivyo.

Washtakiwa hao wanaodaiwa kumjeruhi Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresa Mmbando katika vurugu zilizotokea Februari 27,2016 Ukumbi wa Karimjee kwenye Uchaguzi wa meya na naibu meya wa jiji la Dar es Salaam, wanatetewa na Mawakili Peter Kibatala na John Malya. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 18.

Picha: Sugu Aonyesha Maandalizi ya Ujenzi wa Hoteli yake ya Nyota Tatu Mbeya

$
0
0
Mkurugenzi wa Hotel Desderia Co Ltd, Mr Joseph Mbilinyi na Eng. Chao Nan wa kampuni ya ukandarasi Home Africa Investment Co Ltd ya China wakisaini mkataba wa ujenzi.

 Msanii mkongwe wa Hip Hop na mbunge wa Mbeya mjini, Mh Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ameachia wimbo wake mpya ‘Freedom’ ambapo ndani ya wimbo huo amezungumzia mambo mbalimbali yakiwemo mafanikio yake.


Katika kibao hicho kilichoandaliwa katika studio za MJ Record chini ya producer Marco Chali, Sugu ameelezea jinsi alivyoweza kupambana mpaka kufanikiwa huku alionyesha zaidi kumshukuru mama yake.

Katika ‘Verse’ ya pili ya wimbo huo, Sugu amesema “Mama Hemedy mwanao nimefika mbali, maisha yana afadhali nakomaa ili nisifeli, kiukweli hata mwenyewe najikubali najenga mpaka hoteli!,” .

Pia hivi karibuni kupitia ukurasa wake wa instagram alipost picha ya ujenzi wa hoteli hilo na kuandika: Mkurugenzi wa Hotel Desderia Co Ltd Mr Joseph Mbilinyi na Eng. Chao Nan wa kampuni ya ukandarasi Home Africa Investment Co Ltd ya China wakisaini mkataba wa ujenzi. Kampuni hiyo itajenga hotel ya nyota 3 itakayoitwa Hotel Desderia jijini Mbeya na ujenzi unaanza mara moja kwa mkopo wa bank ya CRDB.


Itakavyokuwa hoteli ya Sugu

Katika post nyingine ya hivi karibuni aliandika: Mkurugenzi wa Hotel Desderia Co. Ltd ya jijini Mbeya Joseph Mbilinyi akiwa kwenye makabidhiano ya site na wakandarasi wa Home Africa Investment Corp Ltd ya China… Mchakato wa ujenzi wa hotel hiyo ya nyota 3 umeanza rasmi leo… Mungu aendelee kubariki. Amen.

Ripoti: Kama Donald Trump Atashinda Urais Marekani ni Hatari Kwa Dunia...Soma Hapa Kwanini..

$
0
0
Shirika moja la kimataifa limesema ushindi wa Donald Trump unachukuliwa kuwa miongoni mwa hatari 10 kuu zaidi zinazokabili dunia.

Shirika hilo la Economist Intelligence Unit linaonya kuwa iwapo Bw Trump atashinda urais Marekani, hilo huenda likavuruga uchumi wa dunia na kuongeza hatari za kisiasa na kiusalama dhidi ya Marekani.

Hata hivyo, shirika hilo halimtarajii Bw Trump, anayeongoza kwenye kinyang’anyiro cha kumchagua atakayepeperusha bendera ya chama cha Republican, kumshinda Bi Hillary Clinton ambaye shirika hilo linasema "ana uwezekano mkubwa sana kuwa mgombea wa chama cha Democratic".

Ushindi wa Trump unaorodheshwa kuwa hatari zaidi kwa dunia kushinda hata Uingereza kuondoka kutoka kwa Umoja wa Ulaya au hata makabiliano ya kivita katika bahari ya South China Sea.
Kuyumba kwa uchumi wa Uchina au Urusi kuingilia kivita Ukraine na Syria na kusababisha “vita baridi” vipya ni miongoni mwa mambo ambayo yanachukuliwa kuwa hatari zaidi ya ushindi wa Bw Trump.

"Kufikia sasa, Bw Trump ametoa maelezo machache sana kuhusu sera zake, na huwa anabadilisha sana msimamo wake,” EIU wanasema kwenye ripoti yao ya utathmini wa hatari zinazokabili dunia.
Utathmini huo huangazia pia athari za jambo fulani na uwezekano wa jambo hilo kutokea.
Al-Shabab wamtumia Trump wakitafuta wafuasi

EIU hutumia kipimo cha moja hadi 25, na Bw Trump ana alama 12, sawa na hatari ya "kuongezeka kwa ugaidi wa kijihadi kuathiri uchumi wa dunia”.

"Amekuwa na msimamo mkali sana dhidi ya biashara huria, pamoja na Nafta, na ameituhumu Uchina mara nyingi kuwa taifa linalofanyia mchezo sarafu,” EIU inasema.

Shirika hilo limeonya kuwa matamshi yake makali dhidi ya Mexico na Uchina hasa yanaweza kusababisha vita vya kibiashara.

Bw Trump amependekeza ua ujengwe kati ya Marekani na Mexico kuzuia wahamiaji na pia ametetea kuuawa kwa jamaa za magaidi. Aidha, amependekeza kuvamiwa kwa Syria ili kuangamiza kundi la Islamic State.

EIU wanasema pendekezo msimamo wake kuhusu mzozo Mashariki ya Kati pamoja na pendekezo kwamba Waislamu wazuiwe kuingia Marekani vinaweza kutumiwa na makundi ya itikadi kali za Kiislamu kuwatafuta wafuasi zaidi.

Zaidi ya nyumba 50 Zilizojengwa Kinyume cha Sheria Kubomolewa Mkoani Kilimanjaro

$
0
0
Zaidi ya nyumba 50 ikiwemo ya mkuu wa jeshi la polisi mstaafu katika manispaa ya moshi mkoani Kilimanjaro zipo hatarini kubomolewa wakati wowote baada ya kujengwa kinyume cha sheria ya mipango miji na sheria ya hifadhi ya mazingira ambayo ni kando ya mto Karanga.

Mkuu wa wilaya ya Moshi Bw.Novatus Makunga amesema hayo baada ya kukagua baadhi ya nyumba akiwa na kamati ya ulinzi na usalama na kujiridhisha juu ya ujenzi wa nyumba hizo kinyume cha sheria..

Bw.Makunga  ambaye ameipa siku saba manispaa hiyo kutoa taarifa rasmi juu ya ujenzi holela amesema,serikali inafanya uchunguzi wa kuwabaini baadhi ya maafisa ardhi wa manispaa hiyo  waliotoa vibali vya ujenzi wa nyumba hizo ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Kaimu mkurugenzi wa manispaa hiyo Bw.Danford Kamenya amesema, kamati hiyo pia  imeyatembelea baadhi ya maeneo ambayo wafanyabiashara ndogondogo  wamepanga bidhaa zao chini na kuangalia namna ya kuwatafuia maeneo mengine ya biashara.

CEO wa Shirika la Ndege FastJet Afukuzwa Kazi, Kampuni Hatarini Kuishiwa Fedha

$
0
0
CEO wa FastJet kuacha kazi wiki hii baada ya wawekezaji kulalamika kuwa shirika lina gharama nyingi, ikiwa ni pamoja na kuwa na makao makuu London Gatwick pamoja na kwamba shirika linafanya kazi zake Tanzania.

Mwekezaji mkubwa Haji Ioannou amesema kuna hatari kampuni hiyo kuishiwa hela mwaka huu ndani ya miezi sita.

Maalim Seif Aiondoa Familia yake Zanzibar na Kuipeleka Muscat Oman

$
0
0
Pichani ni mkewe Seif Shariff Hamad, Bi Awena Sinani Masoud akiwa chumba cha VIP uwanja wa ndege na tiketi yake ya Oman Air, muda mfupi kabla ya kuondoka.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad ameondosha familia yake katika Kisiwa cha Unguja na kuipeleka Muscat-Oman.

Familia hiyo ya Maalim Seif Shariff Hamad wameondoka jioni hii kwa kutumia ndege ya Shirika la ndege la Oman (Omar Air). Familia hiyo ya Maalim Seif wameondoka katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport saa 5:50 jioni hii.

Haikuweza kufahamika mara moja sababu hasa za Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Seif Shariff Hamad kuiondoa familia yake Zanzibar. Kwa sasa Makamu huyo wa Kwanza wa Rais yupo katika mapumziko katika Hoteli ya Kitalii ya Dar es Salaam Serena.

Chanzo: ZanzibarNews.net

Umoja wa Rufaa za Wananchi Tanzania Wapingana na UKAWA..Waomba Wazanzibari Wajitokeze Kwa Wingi Kupiga Kura Tarehe 20

$
0
0
Viongozi wa muungano wa vyama vya siasa uitwao Umoja wa Rufaa za Wananchi Tanzania wamewaomba Wazanzibari kukamilisha haki yao ya kupiga kura katika uchaguzi wa marudio ili wapate viongozi wa kuwaletea maendeleo

Ujumbe wa watu saba wa umoja huo ukiongozwa na John Shibuda wa Ada Tadea, ulitoa kauli hiyo jana ulipokutana kwa mazungumzo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, ilisema ujumbe huo ni kutoka vyama visivyokuwa na wabunge ambavyo ni UPDP, Sau, UDP na Ada-Tadea.

Msimamo wa vyama hivyo unakinzana na ule wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) uliotoa tamko la kususia uchaguzi huo wa marudio.

Kwa upande wake John Cheyo alisema upigaji kura ndiyo njia pekee itakayotoa mwanga kwa wananchi wa Zanzibar kuamua wapi wanataka kuelekea katika mustakabali wa maisha yao ya baadaye.

Wakati huohuo, vyama 12 visivyo na uwakilishi bungeni vimetoa tamko la kushiriki uchaguzi huo vikisema hoja za kugomea uchaguzi huo hazina mashiko.

 Vyama vilivyotoa tamko hilo ni CCK, Sau, Ada-Tadea, TLP, AFP, UPDP, Demokrasia Makini, NRA, UMD, Chausta, DP na ADC ambacho mgombea urais Zanzibar ni Hamad Rashid aliyejiengua CUF miaka miwili iliyopita. 

Ommy Dimpoz Afunguka Kuhusu Bifu yake na Mwanamuziki Diamond...Adai Hawapo Karibu Kama Zamani....

$
0
0
Ommy Dimpoz aliwahi kuwa rafiki mkubwa wa Diamond lakini urafiki wao kwa sasa umeonekana kupungua au haupo kabisa.

Hitmaker huyp wa ‘Achia Body’ ametueleza hali ilivyo sasa.

Amesema hana ukaribu sana na Diamond kwa sasa lakini hana tatizo naye.


“Hapa hakuna mambo ya kufichaficha, kwamba haina noma hata jana nilikuwa naye. Vitu viko wazi vinaonekana hatuko karibu kama zamani, hilo liko wazi. Lakini itakapotokea huko mbele mimi sina tatizo kabisa,” amesema.
Kwa upande mwingine Ommy amedai kuwa anachofanya kwa sasa ni kujikita kwenye mambo yake zaidi.

Msikilize zaidi hapo chini.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 18, Ikiwemo ya CUF Kumshtukia Maalim Seif

$
0
0
SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya March 18, Ikiwemo ya CUF Kumshtukia Maalim Seif

Ukiendelea Na Tabia Hizi Mafanikio Kwako Yatakuwa Ni Ndoto....

$
0
0
Hasira za mafanikio zinatofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine. Kama kweli unahitaji mafanikio ya kweli ni lazima uwe na hasira ya njaa kama aliyonayo simba. Miongoni mwetu ni watu wachache sana wanatambua hasira hii ya mafanikio, wengi wetu huchukulia mafanikio kwa sura ya kawaida sana na mwisho wa siku tunaishia kuwa maskini.

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana, nasema hivi ni kiwa na maana ya kwamba binadamu anapenda sana maisha ya kufanyiwa kila kitu, kwa mfano mtu anapenda umpikie chai, umuwekee kwenye chupa, umuwekee chai kwenye kikombe na umgorogee  na sukari katika chai na ukishamfanyia yote hayo subiri anywe hiyo chai uone atakavoanza kulaamu utamskia anasema sukari imezidi au sukari hajikolea na lawama zingine nyingi,  kitu cha kujiuliza je, mtu huyo alishindwa kuweka sukari mwenyewe kwenye chai yake ili jambo lolote likitokea akose wa kumlamu.

Mtu huyo huyo ukimuuliza unafanya biashara gani? Utamsikia anasema sifanyi biashara yeyote ile mi nipo tu, ukimuuliza kwanini haufanyi biashara yeyote  tatizo nini? Atamsikia anakujibu tatizo mtaji huku akiamini kuwa mataji pekee katika biashara ni fedha. Ndugu msomaji wa makala hii hata uwe na fedha kiasi gani kama huna wazo kwa ajili ya matumizi ya fedha, hata ukipewa milioni mia moja leo  hizo pesa zitaisha utajikuta mwisho wa siku huna hata mia mbovu. Watu wengi tunatazama mitaji kama fedha peke yake ukitazama katika msingi huo utazidi kulamu mpaka mwisho huku maisha yakiendelea kuwa magaumu.

Ngoja nikuibie siri mtaji unaweza ukaupata kwa kutumia ujuzi pamoja nguvu ulizonazo ili kutengeneza bidhaa au huduma zitazokufanya upate fedha.  Kwa mfano Wewe mwenye elimu juu tekinologia ya habari na mawasiliano unaweza ukabili ujuzi wako kuwa bidhaa kwa kuwa fundi wa computer na kutengeza progamu mbalimbali. Swali la kujiuliza unaweza vipi kubadili ujuzi ulio nao kuwa bidhaa au huduma hapo ndipo wengi tunapofeli kwa sababu ni wavivu wa kufikiri.

Naendelea kumchambua binadamu ili uone ni jinsi gani tulivyokuwa na tabia za lawama. Binadamu huyo huyo utamkuta  anaishi mazingira machafu ambayo yatasababisha muda wowote magonjwa ya mlipuko kutokea, ukimfuta binadamu huyo na kumuuliza unafikiri ni kwanini  mazingira haya ni machafu, utamsikia jibu atakalokupa atakwambia tatizo ni serikali, binadamu huyohuyo utamkuta hana ajira ila ukimuuliza kwanini  hauna ajira? Atakujibu tatizo ni serikali.

Kuna msanii mmoja wa hapa nchini aliwahi kuimba kwenye wimbo huku akiuliza serikali ni nini? Maana imekukuwa ikutupiwa lawama kwa kila kitu. Ndugu msomaji wa makala haya nakusihi na kukushauri pia kwa kile ambacho unaweza kukifanya usisubiri serikali ndio ukifanyie, kama unauwezo wa kufanya usafi katika eneo lako fanya usisubiri kuambiwa, maana tabia za bianadamu kwa asilimia kubwa wanasubiri kuambiwa fanya hiki fanya kile . UKisubiri kuambiwa maisha ya mafanikio kwa upande wako yatakuja kwa asilimia chache sana.

Kitu cha msingi ya kuzingatia ni kwamba tuache lawama sizisokuwa na msingi wowote, kwani lawama ulizonazo leo hata yule unayemlalamikia hakusikii na unazidi kuwa maskini tu. Jambo la msingi fanya kila kitu kwa moyo mmoja bila kusubiri mtu fulani akwambie ufanye. Daima tukumbuke usemi huu “kila uonapo nyundo usifikiri kila tatizo ni msumari’’

Mafanikio ya kweli huja kwa mtu kujitambua yeye ni nani? Na ni kwanini upo hapo ulipo. Kuna usemi mmoja hivi wa kiswahili unasema kila binadamu ni mchungaji ,kama ndivo hivyo basi kama mimi leo nikiulizwa nimechunga nini, jibu langu litakuwa lipo wazi ya kwamba natumia muda mwingi kuwafunza watu ili kujua mbinu za kufanikiwa, je wewe mwenzangu unasoma makala hii endapo utaulizwa swali kama hilo utajibu nini? Tafakari kisha uone una thamani gani mbele ya watu wengine?

Kuchapiwa Mke Wanaume Saa Nyingine Mnajitafutia..Soma Hapa

$
0
0

WIFE....Honey plz lets come and help
me in the garden to clean these
flowers??
MME.......Are you mad ,do I look like a
gardener?
WIFE.....Ok sory babie,...but
sweetheart please go and fix that
door to the bathroom,Junior broke it
last night??
MME.....I hate your nosense
requests,,do I look like a Carpenter??
..
At night MME came back from town
and found that the garden is clean
and the door if fixed well..he was
surprised and decided to ask his wife..
..
MME.....Honey I can see the garden is
clean and the Door is well fixed,who
fixed the door for you??
WIFE.....Its our neighbour ofcourse..
MME.....Woow thats great,,did he fixed
it for you free of charge?
WIFE........NO he gave me two options
to choose,,,He said I must give him
BREAD OR SE..X..
MME.....I hope you gave him BREAD??
WIFE....What???....Do I look like
BAKERY???

Shahidi wa Lembeli Atinga Kortini na Mzigo wa Masufuria ......Mawakili Wajitoa Kesi ya Kupinga Matokeo ya Ubunge Jimbo la Kyerwa

$
0
0
Shahidi wa tatu wa mlalamikaji, James Lembeli katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini, Jumanne Kishimba (CCM) jana alitinga Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga akiwa na mzigo wa masufuria, akidai alipewa kwa ajili ya kumpigia mgombea ubunge wa CCM. 

Mbele ya Jaji Moses Mzuna anayesikiliza shauri hilo, Cesilia Gregory wa Nyahanga mjini Kahama alikiri kupokea zawadi ya masufuria hayo kutoka kwa Wakala wa Kishimba ili ampigie kura. 

Gregory alidai Oktoba 19, 2015, Kikundi cha Amani waliitwa nyumbani kwa Hamad Hilal na kumkuta Ezra Machogu, ambaye alikuwa ni Wakala wa Kishimba akigawa masufuria yalitolewa kwa ajili ya kumuombea kura mgombea ubunge wa CCM. 

Hata hivyo, kulitokea mvutano baada ya Wakili wa Kishimba, Antony Nansimire kumtaka shahidi kuwataja wanakikundi 20 ambao walipewa masufuria hayo, hivyo kuwataja 22 na kwamba ongezeko hilo lilisababishwa na baadhi ya wanaume waliojiunga kuhamasisha utafutaji wapiga kura wa Kishimba. 

Wakati huohuo, mawakili wa mdai katika shauri la kupinga matokeo ya ubunge Jimbo la Kyerwa mkoani Kagera, Benedicto Mutungirehi wamejitoa. 

Hatua hiyo ilifuatia makosa ya kisheria yaliyobainishwa katika hati ya kiapo cha shahidi wa pili, Pastory Bagambila ambaye tayari alikuwa mbele ya Mahakama kutoa ushahidi wake. 

Baada ya kubaini makosa hayo, Wakili Erasto aliiomba Mahakama kumuondoa shahidi huyo kutoka kwenye orodha ya mashahidi kabla ya kutoa ombi la kujadiliana kwa muda na mteja wake. 

Hata shahidi wa tatu, Alistides Boniface alipoitwa naye hati yake ya kiapo ilibainika kuwa na kasoro za kisheria, hali iliyomtia hofu Wakili Erasto kuwa yawezekana viapo vya mashahidi wote 36 vilivyowasilishwa vina kasoro. 

Kabla ya kujitoa, wakili Erasto alimuomba Jaji Maisario Munisi anayesikiliza shauri hilo, kuahirisha kwa muda ili wajadiliane na mteja wao. 

Waliporejea mahakamani baada ya dakika 30, Wakili Erasto alimweleza Jaji Munisi kuwa wanaomba kujitoa kwa maelekezo ya mteja wao. 

Kutokana na hali hiyo, Mutungirehi aliiomba Mahakama kumpa muda kutafuta wakili, ombi lililokubaliwa na Jaji Munisi na kuiahirisha hadi Machi 22.

Mbunge wa sasa wa jimbo hilo kupitia CCM, Innocent Bilakwate anawakilishwa na Wakili Peter Matete.

Baadhi ya maombi yake ya msingi, Mutungurehi anadai kulikuwapo na ukiukwaji sheria, taratibu na kanuni katika kuhesabu kura na kudai kulitawaliwa na usiri bila kumhusisha.
Viewing all 104702 articles
Browse latest View live




Latest Images