Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104701 articles
Browse latest View live

Mbunge Sugu Awachana Wasanii Kufanya Show Ulaya....Adai Sio Kigezo Kwa Music Wetu Kukua

$
0
0
Kwenye stori tatu ya Planet Bongo ya East Africa Radio, Sugu amesema huwezi kutumia kigezo cha wasanii kufanya show nje ya Afrika yaani Ulaya, America na kwengineko kama kigezo kuwa game imekua, kwa sababu show kama hizo walishazifanya miaka zaidi ya 20 iliopita.
“Huwezi kutoa credit kwa kusema wasanii wanaenda kupiga show Ulaya, Sugu, X-plastars, tumekwenda tour Europe miaka 20 iliyopita 18 au 17, kwa hiyo mimi sichukulii hiyo kama credit kama tour tulizokuwa tunapiga sisi, I apriciate hustle za kila mtu lakini sisi tulikuwa tunaenda kwenye mafestival ya dunia unapiga mbele ya mtu laki moja, ukirudi nyumbani hakuna suport kwa hiyo ili watu laki moja waliokuona kule wakupe thamani wanakuja kuangalia huko kwenu huko vipi unakuta watu wanakuzingua tu”, alisema Sugu.

Sugu kwa sasa ameachia wimbo wake unaoitwa freedom, baada ya kimya kirefu kilichosababishwa na yeye kuingia kwenye siasa, mpaka kufanikiwa kutwaa jimbo la Mbeya mjini.

Waziri wa Mambo ya nje, Balozi Mahiga Asema Serikali imesikitishwa na Kusitishwa kwa Msaada wa Mabilioni ya Marekani

$
0
0
Serikali imeeleza kusikitishwa na uamuzi wa Marekani kusitisha uhusiano katika Shirika la Changamoto za Milenia (MCC), bila kuishirikisha wala kuisikiliza.

Kadhalika, imesema hakuna umuhimu wa misaada ya afya na elimu inayofadhiliwa na Marekani kwa dola za Marekani milioni 700 (Sh. trilioni 1.5), kama imejitoa katika kusaidia miradi ya umeme ambayo ni muhimu katika utekelezaji wa miradi inayofadhili, kwa kuwa ni sawa na kutoa kwa mkono wa kulia na kupora kwa mkono wa kushoto.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, baada ya kupokea taarifa ya uamuzi wa MCC, Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga, alisema uhusiano na Marekani utaendelea katika maeneo mengine, lakini kwa fedha hizo hakuna la kufanya ingawa milango iko wazi iwapo watafikiria upya.

“Fedha ni zao, uamuzi ni wao wameutoa Washington. Hatuwezi kulia kwa ajili ya hili, tutaendeleza ushirikiano katika maeneo mengine, lakini tunawaomba wafanye uchambuzi wa kigezo cha demokrasia kwa asilimia 100 kinachotumika katika misaada hiyo,” alibainisha na kuongeza:

“Wametusaidia kwa miaka mitano kwa vile tulikidhi vigezo, ila sasa tumeshindwa kimoja inafuta imani na uelewano ambao ulikuwapo kati yetu. Nishati ndiyo nyenzo ya maendeleo kwa Tanzania. Kwa sasa tunaelekeza umeme vijijini ili vijana wanaosoma bure wajisomee na hospitali zitoe huduma muda wote.”

Waziri Mahiga alisema Tanzania imetia saini mkataba wa malengo ya milenia ambayo yanakwenda sambamba na MCC, hivyo kufuta fedha hizo kwa sasa ni sawa na kuumiza mahali panapouma zaidi huku ikiwa (Marekani) kiongozi wa utawala bora, demokrasia na soko huria duniani.

Alifananisha kunyimwa fedha hizo sawa na kutoa adhabu kwa mkosaji bila kujali kuwa alipaswa kumwelimisha na kumwonya kabla ya adhabu kubwa.

“Ukichukua mizani na kuweka nyama upande huu na jiwe upande mwingine, ukapima mazuri ambayo Tanzania imekuwa ikifanya na kuonekana mtoto mzuri machoni mwa dunia, lakini upungufu wa sasa waliouona, utaona tuna mazuri mengi, hivyo  hatukustahili adhabu hii,” alisisitiza.

“Uamuzi wao hatuwezi kuwaingilia, nasi tukiamua yetu wasituingilie. Tumejitahidi tuwezavyo kulinda demokrasia na hatutarudi nyuma kwani katika uchaguzi wa Zanzibar vyama vilishirikishwa. Waelewe na kutambua mazuri yetu tunayofanya na tutaendelea kufanya,” afafanua.

Aidha, alisema suala la Zanzibar liliendeshwa vizuri kwa kuwa lilitoa nafasi ya mazunguzo kwa pande zote na kwamba hakuna mwenye uwezo wa kuingilia masuala ya uchaguzi, serikali na mambo ya ndani ya visiwa hivyo kwa kuwa wana katiba na sheria zao bali mambo machache tunashirikiana na hata Rais Dk. John Magufuli, alikuwa mwangalizi tu.

Balozi Mahiga aliishangaa Marekani kwa kueleza kuwa uamuzi wa sasa unapingana na tamko la hivi karibuni lililosisitiza mazungumzo baada ya serikali mpya kuingia madarakani, kwa kuwa kabla ya utekelezaji, imetoa uamuzi wa kuvunja uhusiano na Tanzania katika MCC.

“Kitu kinachoitwa demokrasia kingekuwa kinafugwa kwenye bomba na kuona kinamiminika ingekuwa rahisi sana, lakini ni kitu cha kulea na kutengeneza. Tanzania imejulikana duniani kama mlezi na mjenzi wa demokrasia tangu kipindi cha chama kimoja hadi vyama vingi,” alisema.

Aidha, alisema kutokana na hali hiyo, serikali itafanya marekebisho katika bajeti yake na mpango wa maendeleo ambao ulijumuisha fedha hizo na kwamba kinachopaswa kufanyika kwa sasa ni kujikita kwenye ukusanyaji wa kodi kikamilifu.

“Ndani ya vikao vya Bunge la Marekani tuna marafiki zetu ambao tunaamini wataendelea kuihoji serikali yao juu ya uamuzi huu na hasa wakizingatia historia yetu katika kukuza na kuendeleza demokrasia nchini,” alibainisha.

Zitto Kabwe: Tanzania Kunyimwa Fedha ni Matokeo ya Ubabe wa CCM

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amesema MCC kuinyima fedha Tanzania ni kwa sababu ya ubabe wa CCM na kwamba, sasa watu wasivikwe koti la uzalendo kwa jambo hilo.


Kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Facebook, Zitto aliandika kuwa: “Uzalendo ni kutaka haki ya kidemokrasia Zanzibar. Haki ya Wananchi waliochagua viongozi wao Oktoba 25, 2015. 


“Sitakubali kuvishwa koti la uzalendo kwenye suala la MCC. Hilo ni suala la CCM, kukosa misaada ya Marekani ni matokeo ya ubabe wa CCM kuhusu Zanzibar.


“Haina mahusiano yeyote na uhuru wa nchi yangu. Nawasihi Wazanzibari wawe na subra Mola kamwe hatawatupa. Haki itapatikana tu. Nawasihi Watanzania kuelewa kwamba CCM ndio imetufikisha hapa na iubebe mzigo huu bila kuufanya ni mzigo wa nchi.”


Aliandika pia kwamba: “Zanzibar inatazamwa kama Zanzibar, kwa wenye maono mafupi. Nilipata kuwaambia viongozi wenzangu kwamba tishio kubwa zaidi la kutoshughulikia mtanziko wa Zanzibar ni upotoshaji. 


“Tutajikuta tunaacha kushughulika na masuala ya maendeleo kwa kipindi kirefu kidogo. Tabia ya kitanzania ya kupenda ‘shortcuts’ (njia za mkato) itatugharimu sana. You can’t just ignore Zanzibar and move on. You just can’t (huwezi ukaipuuzia Zanzibar na ukaendelea tu, huwezi).” 


Pia Mbunge huyo aliandika kuwa: “Serikali ya Marekani imesitisha mahusiano na Serikali ya Tanzania kwenye miradi ya MCC. 

“Hivyo Tanzania itakosa Sh. trilioni moja ambazo zilikuwa zimeelekezwa kwenye umeme na umeme vijijini. 

“Sababu? Zanzibar na Cybercrime Act. Siku si nyingi tutawasikia Umoja wa Ulaya nao. Nasubiri kusikia Serikali ya Rais Magufuli itasema nini. 


“Suala la Zanzibar likitazamwa kibabe kwa kuwa watawala wana maguvu nchi itaingia kwenye matatizo makubwa sana ya ndani bila kujali misaada inakatwa au la. Sipendi misaada. Sipendi mataifa ya kigeni kuingilia masuala yetu ya ndani. 


“Lakini Tanzania sio kisiwa, tunaishi ndani ya jamii ya kimataifa. Kuna mambo lazima tufanye kwa kuzingatia misingi ya kidunia. Zanzibar ni moja ya jambo hilo. Tusiweke kichwa kwenye mchanga kama mbuni.”


Naye Makamu Mwenyekiti, Kamati ya Katiba, Sheria na Mambo ya Nje wa Chama Cha ACT-Wazalendp, Theopister Kumwenda, alisema uamuzi huo wa MCC utawaumiza na kukwaza juhudi za wananchi wa vijijini katika kujikwamua na umaskini. 


Alisema ACT-Wazlendo inatambua kuwa katika kipindi hiki Tanzania inahitaji mahusiano mema na Jumuiya ya Kimataifa na wadau mbalimbali wa maendeleo duniani, likiwamo MCC, katika kuendeleza miradi  ya maendeleo. 


Alisema MCC imekuwa mdau mkubwa katika miradi ya barabara na kusambaza umeme vijijini

Download Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

$
0
0

Good News! Sasa Blog yako ya Udaku Special Ipo Google Play Store.

Download Udaku Special Blog Android Application CLICK HERE From Play Store

Au Bonyeza hii picha hapa chini

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya March 31, Ikiwemo ya Nchi Inavyotafunwa na Wajanja Kila Kona

Soma Hapa Barua ya Binti Aliyoandika Kabla ya Kujiua Kwa Kujinyonga Kwa Kutumia Kamba Huku Longido

$
0
0
Binti mmoja anayejulikana kwa jina la Jesca ambaye ni mfanyakazi wa Longido Mountain Lodge amekutwa amejinyonga katika hotel ya Longido Mountain Lodge na kuacha ujumbe kuwa kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote 

Amesema amejinyonga kwa ridhaa yake mwenyewe.Katika ujumbe huo, ametaja majina ya watu anaowadai na kuagiza  walipe madeni yake kabla ya mwili wake kusafirishwa kwao pamoja na namba za Mama yake mzazi.

"Mimi Jesca Reinald Elisante Leo tarehe 29 , 03 , 2016 nimeamua kujinyonga kwa ridhaa yangu mwenyewe hakuna mtu yeyote anayehusika na kifo changu na hizi ni namba ya Mama  yangu,0672740439.

Ninao wadai
Mama Diana  33,000/=
John Memory card 4 GB
Boss Mshahara 60,000/=

wanao nidai
Zai 20,000/=alipwe na ninao wadai wahakikishe wanalipa kabla sijarudishwa kwetu.

NB:HAKUNA ANAYEHUSIKA NA KIFO CHANGU.
Ndugu zangu nawapenda sana
vitu vyangu vyote vipelekwe kwetu
Jau Kwenye Kuni."

Agizo la Paul Makonda la Kusalimisha Silaha Kuhakikiwa Laendelea Kutekelezwa..Watu 580 Wajitokeza

$
0
0
Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imesema watu 574 wamejitokeza kuhakiki wa silaha zao.

Mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda alitoa siku 90 kwa wakazi wa Dar es Salaam wawe wamehakiki silaha zao ifikapo Julai mosi, ikiwa ni miongoni mwa mikakati yake ya kupambana na uhalifu uliokithiri.

Hivi karibuni, Rais John Magufuli alihakiki silaha zake anazomiliki.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema wanaendelea kuwahimiza wananchi waendelee kujitokeza kuhakiki silaha zao kwa muda uliotolewa.

“Hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliokaidi kujitokeza kuhakiki silaha zao, baada ya siku 90 zilizopangwa kumalizika” alisema.

Wakati huohuo, Siro alisema wafanyabishara wanaouza vipuri vya magari vilivyotumika maeneo ya Kariakoo, wengi wanauza vilivyoibwa sehemu mbalimbali nchini.

 “Nimeshapata mtandao mzima wasipoacha kununua vitu vya wizi tutawakamata na wale wanaojifanya madalali wao, wanashirikiana na majambazi hivyo nataka waache mara moja,” alisema.

TETESI: Clouds FM Kuwatema Baadhi ya Watangazaji...PJ na Gerald Hando Watajwa

$
0
0
Habari zinasema kwamba PJ, Abel Onesmo na Gerald Hando watapigwa chini kuanzia mwezi April mwaka huu. Kwa kawaida, Clouds wana utaratibu wa kutoa mikataba mipya kila ifikapo April 1.

Katika zoezi hilo kuna wafanyakazi wapya wanaopewa mikataba na wale wa zamani ambao kituo kinawahitaji "hurenew" mikataba yao.

Imefahamika kwamba PJ , Abel Onesmo na Gerald Hando ambao wote wanatoka kipindi cha Power Breakfast (PB) watapigwa chini mwezi huu au kwa kauli ya mjini ni kwamba "Watatumbuliwa".

Sababu kubwa inayotajwa ya wakongwe hao kupigwa chini ni kushindwa kuendana na taratibu za kampuni hiyo kongwe na kinara katika sekta ya Burudani nchini kwani wanajiona wao wako juu ya watu wote.

Pia inasemekana suala la Rais Magufuli kupiga simu kwenye kipindi cha Clouds 360 limewauma sana kwani walikuwa wanaamini wao ndio kipindi bora zaidi cha asubuhi hivyo Suala la Magufuli kupiga simu 360 limeprove "otherwise".

Inadaiwa kuwa msuguano mkubwa ulianza wakati wa kipindi cha uchaguzi kutokana na kutumika kisiasa na kulipwa na baadhi ya wanasiasa ili watumie Power Breakfast kama jukwaa la kuwasafisha kinyume na maadili ya kazi yao yanayosisitiza "neutrality" katika kutoa habari.

Vilevile habari za kuaminika kutoka ndani ya Clouds zinasema kwamba tayari Clouds Media Group imeajiri vichwa vipya ambavyo kuanzia tarehe 1 vitaanza kupiga kazi.

Wananchi Waanza Kugombania Kiti Alichokikalia Rais Magufuli Kwenye Mgahawa Jijini Mwanza

$
0
0
Mgahawa aliotumia Rais John Magufuli kupata mlo wa mchana na msafara wake juzi kwenye Uwanja wa Ndege wa Mwanza, umekuwa kivutio kwa wateja wengi wakinunua chakula na kutaka kukalia kiti na meza alivyotumia kiongozi huyo.

Meneja wa mghahawa huo wa Victoria, Elizabeth Maneno (pichani) alisema jana kwamba hali hiyo ilijitokeza mara baada ya Rais kuondoka hapo.

“Hata leo tumepokea wateja wengi kulinganisha na siku nyingine, baadhi yao wanaagiza chakula kwa sharti la kutaka kukikalia kiti na meza aliyotumia Rais Magufuli,” alisema Elizabeth.

Akizungumzia hali ilivyokuwa juzi kabla na wakati wa ugeni huo meneja huyo alisema: “Ilikuwa ni hofu na woga uliochanganyika na furaha kumwona Rais akiingia kwenye mgahawa wetu wa chai ya rangi ya Sh200 na ya maziwa Sh300.

“Mshtuko wetu uligeuka furaha baada ya kubaini kuwa oda ya sahani 28 za kubeba (takeaway), tulizoagizwa mapema asubuhi bila kuelezwa zinakoenda zilikuwa za ujumbe wa Rais,” alisema na kuongeza:

“Kabla Rais Magufuli hajaingia kwenye mgahawa wetu, alikuja mtu mmoja tusiyemfahamu na kuagiza sahani 28 za chakula kwa gharama ya Sh5,000 kila moja,”

Alisema baada ya kumtaarifu mteja wake kuwa chakula kiko tayari, alielekezwa kuandaa meza na viti kwa sababu wageni wake (wa mteja), sasa wameamua kula palepale mgahawani.

“Ghafla tulimwona Rais anaingia ndani ya mghahawa wetu; kwanza tulishikwa hofu, woga na kihoro tusijue tufanye nini hadi tulipogutushwa na aliyetoa oda kwa kutuagiza tugawe chakula alichoagiza,” alisema meneja huyo; “hapo ndipo tulipobaini kumbe chakula kile kilikuwa cha ugeni wa Rais.”

Pamoja na chai ya rangi na ya maziwa, mghahawa huo pia unauza vyakula vya aina mbalimbali kwa bei kati ya Sh1,500 hadi Sh5,000 kwa vyakula vya kubeba, huku soda ikiuzwa kwa Sh500 kwa chupa.

Ali Kiba na Gigy Money Mahaba Motomoto..Team Kiba Wapanick

$
0
0

Story ya town kwa celeb wa Tz n kuwepo kwa uhusiano wa kimya kimya kati ya ali kiba na gigy money bado haijathibika japo Gigy money alipohojiwa na clouds fm kasema hajapewa ruhusa na Ali kiba kuongelea uhusiano wao kwa sasa na hawezi kuongelea kwa sasa na uko insta amewarushia kijembe mashabiki wa kiba na kuwauliza kwan kiba sio mwanaume baada ya team kiba kupanick na mapovu kuwatoka.

Story hii inakuja miezi kadha baada ya Gigy kumlalamikia Jokate kumuibia Ali kiba na ikumbukwe ivi sasa Jokate hawapo kwny terms nzuri na King Kiba

JE Umeshawahi Kufikiria Mchezaji MBWANA SAMATTA Analipwa Mshahara Kiasi Gani Kwa Mwezi? Jibu Lipo Hapa

$
0
0
Klabu ya KRC Genk anayocheza nahodha wa Taifa Stars Mbwana Samatta inatajwa kuwa miongoni mwa vilabu tajiri ndani ya Ligi Kuu Ubelgiji, ila kwa mujibu wa www.xpats.com, wachezaji wengi wao Ubelgiji hulipwa kati ya euro 25000 hadi 50000 kwa mwezi.

EURO elfu ishirini na tano ni zaidi ya milioni sitini za Kitanzania kwa sasa wakati Euro elfu 50 ni zaidi ya milioni mia moja ishirini za Kitanzania.

Hivyo Samatta Mshahara wake unaanzia uero 25000 na kuendelea..

Nchi 10 kati ya 14 za Ulaya Zasitisha Misaada Tanzania

$
0
0
Tanzania tutegemee kuingia kwenye shida ya kiuchumi. Wale washirika wetu wa maendeleo yaan zile nchi za ulaya. Kwa kauli ya pamoja wamesitisha misaada katika nchi yetu. 

Tukumbuke misaada yao inaingia moja kwa moja kwenye bajet!! Wanaojua hatujitoshelezi. Kimaneno tunajitosheleza kwa 60% kivitendo hatuzid 40%.Ni zaid ya ile MCC. Maamuzi hayo yamekubaliwa na nchi 10 kati ya 14 za Umoja wa ulaya.

Swali kwa watawala hata hizo milijua hamtapewa mlijiandaa kujitegemea??
Maana ya MCC nilimsikia msemaji wa wizara ya fedha anasema waljua haztakuja hawakuziweka kwenye bajet.
Je na za washirika wa maendeleo hamkuziweka???

Wananchi mnatwambia tufunge mikanda suruali zetu zinavyotupwaya wakati nyie mnashindwa Hata kufunga vifungo vya makotI kwa vitambi.

RASMI..Gerald Hando, Paul James Waondoka Clouds FM

$
0
0
Watangazaji Gerald Hando na Paul James, wanadaiwa kuachana na Clouds FM, kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.

Wawili hao wamekuwa watangazaji wa kipindi cha Power Breakfast cha kituo hicho kwa miaka mingi.

Gazeti la Mwananchi limedai kuwa watangazaji hao wamemaliza mkataba na kituo hicho na hakijapenda kuwaongezea.

Za Mwizi ni Arobaini..Wezi wa Nyaya za Kampuni ya TTCL Wakamatwa

$
0
0
WANANCHI  wa Mtaa  wa soko la sovya Wilayani Kasulu usiku wa kuamkia leo wamewakamata wezi waliokuwa wamekata nyaya za mawasiliano za kampuni ya TTCL. 

Akiongea juu ya tukio hilo Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya simu TTCL nchi Dk Kamugisha Kazaura alisema kuwa tukio hilo limetokea katika eneo la soko la sovya majura ya saa kumi na moja alfajiri. Alisema kuwa wananchi  wanaoishi karibu na eneo lililokatwa nyaya hizo ndiyo waliowakamata vijana hao baada ya kufanya uhslifu huo. Mkurugenzi huyo alisema kuwa hasara waliyoipatia kampuni kwa kukata nyaya hizo inakadiliwa ni zaidi ya milioni 20.

"Hasara waliyoingizia serekali ni kubwa sana hizo nyaya walizokata zinagharimu milioni 20,lakini kuitengeneza upya line hiyo inaweza kugharimu zaidi ya hiyo fedha''alisema Kazaura

Alisema kutokana na wezi huo umepelekea baadhi ya ofisi za serekali kukosa mawasiliano ikiwemo ofisi ya polisi Wilaya,Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Bank na Takukuru. Naye Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na mawasiliano profesa Makame Mbawala alivitaka vyombo vya dola kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wezi hao wanaohujumu mawasiliano. 

"Hawa muwapeleke kwenye sheria hiki walichofanya ni kosa kwa sheria ya mwaka 2015 wanatakiwa kulipa faini isiyopungua milioni 50 au kifungo jela ili iwe fundisho kwa wengine"alisema profesa Mbawala

Nape Nhauye Atema Cheche..TFF Inao Uwezo wa Kumlipa Kocha Mkuu wa Taifa Boniface Mkwasa...

$
0
0
Serikali ya awamu ya tano kupitia Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye imesema kwamba Shirikisho la Mpira wa miguu nchini TFF linapaswa kumlipa mshahara kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars,) kwa sababu uwezo wa kubeba majukumu hayo wanayo.

Charles Boniface Mkwasa alichukua nafasi ya M-holland, Marti Nooij, Juni 21 mwaka uliopita na ilisemwa kwamba serikali itaendelea kuisaidia TFF kumlipa kocha wa timu ya Taifa na Mkwasa (kocha wa kwanza mzawa tangu 2006) angeendelea kulipwa mshahara kama ule ambao makocha wa kigeni walikuwa wakilipwa.

Mbrazil, Marcio Maximo aliifundisha Stars kwa miaka minne kati ya 2006 hadi mwaka 2010, Mdenmark, Jan Borge Poulsen alichukua nafasi hadi mwaka 2012 tinu hiyo ilipochukuliwa na Mdenmark mwingine Kim Poulsen ambaye naye aliisimamia hadi mapema mwaka 2014 alipopewa majukumu hayo Nooij.

Makocha wote hao walikuwa wakilipwa mishahara yao na serikali iliyopita ya awamu ya nne chini ya rais mstaafu, Mh. Jakaya Mrisho Kikwete.

Licha ya TFF kusema kwamba Mkwasa ataendelea kulipwa kiasi cha Shililindi milioni 25 za kitanzania kama mshahara wake wa mwezi na serikali ya Kikwete kudai itaendelea kuwalipia, Mkwasa amelipwa mshahara huo mara moja tu (Mwezi Julai, 2015)

Kufikia mwezi huu katika mkataba wake imebainika kwamba kocha huyo anadai kiasi kisichopungua milioni 200 kama malimbikizo ya mishahara yake.

NI juzi tu rais wa serikali ya awamu ya tano, Mh. John Magufuli alisema kuwa serikali yake itapunguza kima cha juu cha mishahara na kufikia milioni 15 kama mshahara wa mfanyakazi, na kiwango cha chini alisema kitakuwa milioni 1.5 kwa maana hiyo mshahara wa Mkwasa (milioni 25 kwa mwezi) hautakiwi pia katika serikali yake.

Kitendo cha serikali ya awamu ya tano kusema kwamba, TFF inapaswa kumlipa mshahara kocha wa timu ya Taifa kinaweza kuonekana ni pigo kwa Mkwasa lakini kwa namna yoyote ile Shirikisho linapaswa kufanya hivyo kwa kuwa Stars ni timu yenye udhamini mkubwa, pia TFF wanaweza kutumia njia nyingie za kujiingizia kipato chao kupata pesa za kumlipa mshahara kocha wa Stars.

Kila mtu ameona kazi iliyofanywa na Mkwassa kuanzia mchezo wake wa kwanza dhidi ya Uganda katika harakati za kufuzu kwa fainali zilizopita za CHAN. Mkwassa amesema kwamba amekubali kufanya kazi yake bila tatizo licha ya kutolipwa mshahara kwa miezi 8.

Ndiyo kama alivyosema mwenyewe kwamba yeye ni ‘mzalendo’ ndiyo maana ameendelea kufanya kazi yake lakini umefika wakati wa TFF kuwajibika yenyewe tena kikamilifu katika malipo ya mishahara ya timu za Taifa.

Hakuna uzalendo wa kufanya kazi miezi nane mfululizo bila kulipwa mshahara na Mkwasa anaweza kuzungumza hivi kwa uoga tu ama kulinda kibarua chake lakini katika uhalisi ni kitendo ambacho hakifurahii. Naungana na Waziri aliyesema kwamba, TFF inapaswa kumlipa kocha wa timu ya Taifa kwa kuwa uwezo huo wanao.

CCM Yatoa Tamko Baada ya Wabunge Wake Kufikishwa Mahakamani Leo Kwa Tuhuma za Rushwa

$
0
0
Kwa kipindi cha hivi karibunin kumekuwepo na tuhuma za baadhi ya wabunge kujihusisha na masuala ya rushwa.

Tuhuma hizo zimekuwa zikifanyiwa kazi na vyombo vya dola na kwamba tayari baadhi ya wabunge wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma hizo.

Chama cha Mapinduzi (CCM) kinasikitishwa sana na tuhuma hizo, hasa pale zinapowahusisha wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi  na kinaunga mkono jitihada za vyombo vya dola katika kutafuta ukweli wa tuhuma hizo.

Lazima ifahamike kuwa vitendo vya rushwa havina itikadi,dini, wala kabila na kwamba havikubaliki kwa namna yoyote kwani vina madhara makubwa kwa taifa.

CCM inavishauri vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina na kuwachukulia hatua stahiki wabunge wote watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa.

Chama cha mapinduzi kwa upande wake hakitasita kuwachukulia hatua kali za kinidhamu wabunge wake watakaobainika kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa.

Sakata la Wastara Kutoroshwa Hospitalini...Ndugu Wakwama Kumpata Alipo

$
0
0
Hali bado tete! Baada ya Gazeti la Ijumaa Wikienda ambalo ni dugu wa damu na hili toleo la Jumatatu iliyopita kutoka na habari yenye kichwa kisemacho; WASTARA ATOROSHWA HOSPITALINI, habari mpya ni kwamba, nduguze wameshindwa kujua wapi alipo mpaka sasa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Ijumaa iliyopita, baadhi ya ndugu wa Wastara, wakiwemo dada zake, waishio jijini Dar walikodi gari ndogo ili kwenda Morogoro kumfuata Wastara na kumrejesha Dar ambako ndiko kwenye makazi yake, lakini walidunda dakika za mwisho wakiwa Mwenge, tayari kwa safari.

HIKI HAPA CHANZO
“Jamani Wastara amezua balaa. Mnajua kwamba ndugu hatujui alipo mpaka sasa. Baada ya kuondoka nyumbani kwa mumewe (Mbunge wa Jimbo la Donge, Zanzibar, Sadifa Juma) hapa Dar, alikwenda Morogoro kwa huyo mtu aliyesema ni babu yake, Abdulaaziz Babu kwa lengo la kupumzisha akili.

“Sasa baada ya kusikia ameugua ghafla maradhi ya kisukari na moyo na amelazwa Hospitali ya St. Herry Health Centre , sisi ndugu tuliamua kumfuata. Sasa tukiwa ndani ya gari, tulipofika Mwenge, tukampigia simu Wastara ili kumjulisha kwamba tunakwenda.

“Alichotujibu sasa. Alimwambia dada yetu mkubwa kwamba, kama tunataka kumkosa maisha yetu yote tumfuate, la sivyo tusiende Morogoro. Yaani alimaanisha kwamba, tukimfuata anaweza kujiua. Akasema atakuja mwenyewe na atafikia kwa huyo dada yetu mkubwa.

“Sasa ile ilikuwa Ijumaa iliyopita. Mpaka sasa tunavyoongea (juzi Jumanne), hajaja na mbaya zaidi tukipiga simu hapokei, hajibu meseji. Yule babu tumempigia simu akasema Wastara alimtoa hospitali na kwenda kumpangia chumba hotelini, sasa sisi hatujui anakoishi kule Morogoro na wala hiyo hoteli aliyompeleka ni ipi,” alisema ndugu huyo.

Baada ya maelezo hayo, juzi, Amani lilimwendea hewani Wastara ambapo simu yake iliita muda mrefu bila kupokelewa. Baadaye ikawa haipatikani.

Baadaye Amani lilimpigia babu huyo ambapo alisema;
“Wastara yupo fiti sasa, lakini huwezi kumpata kwenye simu kwa sababu ya mambo yaliyojitokeza hivi karibuni.”…

Ndoa ya Wastara na Sadifa ilidaiwa kuvunjika rasmi Machi 21, mwaka huu baada ya kuishi kwa siku 74 tangu kufungwa kwake, Januari 22, mwaka huu huko Tabata jijini Dar.

Hata hivyo, Sadifa akielezea kuhusu madai ya kuvunjika kwa ndoa yake alipozungumza na Magazeti Pendwa ya Global wiki iliyopita, alisema yeye hajatoa talaka huku akimshangaa mtu anayejiita ni babu wa Wastara kuzungumza kwenye vyombo vya habari kwamba, Wastara amepewa talaka mbili.
Kwa upande wake, Wastara alipozu- ngumza na Magazeti Pendwa alikiri kupewa talaka.

Chanzo: GPL

Tetesi: Kikwete Kumrith Ban Ki-Moon Umoja wa Mataifa

$
0
0
Dr. Jakaya Mrisho Kikwete Rais mstaafu wa Tanzania kwa awamu ya nne (2005 – 2015) ni miongoni mwa wanadiplomasia wakubwa duniani wenye ushawishi na uwezo wa utatuzi wa matatizo mbalimbali duniani, sio tu kwa sababu viongozi wa mataifa mbalimbali duniani wanamkubali bali kwa uwezo wake katika masuala ya kidiplomasia.

Alizaliwa mwaka 1950 Oct katika mkoa wa Pwani Wilaya ya Bagamoyo katika kijiji cha Msoga katika familia ya kisiasa na kilimo. Baba yake Mzee Mrisho Kikwete alikuwa ni Mkuu wa Wilaya (DC) ya Pangani na babu yake naye ambaye alikuwa ni Chief wa Wakwere, Chief Kikwete.


Alipata elimu ya Msingi Msoga kabla ya kujiunga na shule ya sekondari Kibaha akiwa pia ni mwenyekiti serikali ya wanafunzi na vijana wa TANU 1966 na Baadaye Tanga school. Ambapo alijiunga na chuo kikuu Dar es salaam, ambapo pia alikuwa mwenyekiti wa serikali ya wanafunzi na kuhitimu Shahada ya uchumi 1975 alipojiunga na Jeshi.

Aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Singida 1977 na baadae kuhamishiwa Zanzibar kwa kazi maalum baada ya muungano wa TANU na ASP mpaka kufikia mwaka 1980 aliporudishwa makao makuu ya chama (CCM).

Mwaka 1988 aliteuliwa kuwa mbunge na pia NaibuWaziri wa Nishati na Madini chini ya uongozi wa MH. Al Ahsan Mwinyi mpaka kufikia mwaka 1990 ambapo aliteuliwa kuwa Waziri kamili wa maji nishati na madini. 

Mwaka 1994 aliteuliwa kuwa waziri wa uchumi akiwa na umri wa miaka 44 ambapo alikuwa ni waziri mwenye umri mdogo kuwahi kuteuliwa. Kufika mwaka 1995 alitueliwa kuwa waziri wa mambo ya nje chini ya uongozi wa Rais Benjamin W. Mkapa na kuongoza wizara hiyo kwa miaka 10 mpaka kufikia mwaka 2005 ambapo alichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania.

Katika Nyanja za kimataifa Mh. Jakaya Kikwete ni miongoni mwa wanadiplomasia ambae amefanya mambo mengi katika bara la Afrika na Dunia, kama vile kutatua migogoro katika nchi za maziwa makuu, jumuiya ya Afrika Mashariki akiwa kama Mwenyekiti wake (EAC) baadhi ya mambo ambayo dunia inampongeza ni pamoja na Mwaka 2005 akiwa kama Mwenyekiti mwenza wa mikutano wa Helsinki (Helisinki process on Globalization and Democracy) aliweza kuongoza mikutano huo kwa mafanikio makubwa.

2013 akiwa ndiye kiongozi pekee kutoka Afrika aliyeshiriki katika mkutano nchi za umoja wa Ulaya EU wa Alpbach Austria aliliwakilisha bara la Afrika vyema katika kutafuta fursa za maendeleo na ushirikiano kimataifa.

Dr. Jakaya Kikwete pia amekuwa Mjumbe tume ya Elimu Duniani ikiongozwa na waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown katika kutafuta namna ya kugharamia Elimu duniani (TICFGEO) kwa mwaka 2015.

Kwa mwaka huu 2016 Dr. Jakaya Kikwete ameteuliwa kuwa Mjumbe wa kamati ya Amani nchini Libya katika kusaidia kurudisha amani nchini Libya
Pia amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mwenza kwa tume ya kusaidia afya ya Mama na motto duniani kwa mwaka huu 2016 ikiwa ni katika jitihada zake kuhakikisha Afya na mama na motto duniani kote zinalindwa.

Kwa mtazamo huo nina imani kubwa kwa kipindi ambacho Mh. Ban Ki-Moon ataachia ofisi, Mwanadiplomasia huyu ndiye atakayechukua viatu vyake .

Hizi ni baadhi ya tuzo za heshima alizowahi kupata toka nchi mbalimbali...

2007: Sullivan Honor
2007: The AAI African National Achievement Award (on behalf of Tanzania).
2009: US Doctors for Africa Award.
2011: Social Good Award from the United Nations Foundation
2011: South-South Award for Global Health, Technology and Development
2012: FANRPAN Policy Leadership Award from the Food, Agriculture and Natural Resources Policy Analysis Network.
2013: Africa's Most Impactful Leader of the Year by the Africa Leadership Magazine
2013: ICCF Mengha Award by the International Conservation Caucus Foundation
2014: Icon of Democracy Award, from The Voice Magazine (Netherlands)
2015: Leadership Excellence Award by the Pan-African Youth Union.
2015: African Achievers Award by the Institute for Good Governance in Africa.
2015: African Statesman of the Year by the The African Sun Times.

Magufuli amponza 'Mlevi', Apandishwa kizimbani kwa tuhuma za kumtishia kifo Rais Magufuli

$
0
0
HAMIMU Seif, mkazi wa Mwananyamala Ujiji, Dar es Salaam, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kumtishia kifo Rais John Magufuli, anaandika Faki Sosi.

Mbele ya Hakimu Mkazi Helleni Liwa, Keneth Sekwao, Wakili wa Serikali, aliiambia mahakama kuwa kijana huyo alitishia kumuua rais Machi 10 mwaka huu, alipokuwa katika baa ya Soweto maeneo ya Makumbusho, Jijini Dar es Salaam.

Sekwao ameeleza mahakama kuwa kijana huyo alitamka kuwa amechoshwa na mambo anayofanya rais, na kwamba yupo tayari kujitoa mhanga kwa kujilipua na bomu.

Mshitakiwa amekana mashitaka, na mahakama imeweka wazi dhamana yake.

Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo tarehe 14 Aprili mwaka huu.

Faiza Ally Awatukana Team Wema.."Team Wema Wengi Wapumbavu - Mimi Siwezi Kupenda Kuwa na Team za Kipumbavu"

$
0
0
Mrembo wenye Vituko vya kila leo Faiza Ally ameamua kuwafungukia team Wema Sepetu kwa Kuandika Haya:

Faizaally_ Team Wema wengi wapumbavu - mimi siwezi kupenda kuwa na team za kipumbavu ! Pumbavu zenu wote ....... Mnaponda watu bila mnazalilisha huyo Malkia wenu nae anaonekana Kama nyinyi ! Kweli mshamba mshamba - mshamba belongs uswahilini bora mngekuwaga hata mna point basi #ujinga mtupu..... Hivi account za kina Malkia Malkia wote wajinga sijui wanatafuta followers kutumia picha za Wema ? But i swear to god nisinge penda kuwa na stupid team at all - Ndio Maana mnafanya anatukanwa - mmeanza kuchokonoa matako ya zari sasa mwisho wameanza na watu kuchunguza yake and u know why ? Because of the stupid team that she has - Kama mm ningewaambia yoyote ana taka kuwa team yangu awe na adabu za kuheshimu wengine Na maisha Yao ! Na yoyote mwenye account ya kutukana watu asitumie picha zangu ! And there for kidogo ange kuwa hata na watu wa manna kabisa hata wa kumwambia ya Maana zaidi ya Hawa wajinga wa Insta wanao jiita team Wema ......

Viewing all 104701 articles
Browse latest View live




Latest Images