Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Mange Amjibu Faiza Ally 'Mimi Mpumbavu Inapokuja Issue ya Wema Ila Nadhani Nilionekana Mpumbavu Mara Mia Wakati Nakutetea Wewe'

$
0
0
Mangekimambi_ Sawa nakuwa mpumbavu kwenye swala la Wema Ila kumbuka hata wakati nakupigania wewe niliitwa mpumbavu vile vile.Nilitukanwa kona zote kwanini namtetea mwanamke anaevaa pampers na kutembea matako Wazi. Ila sikujali niliacha waniite mpumbavu Kwa ajili yako Na huku sikujui hata kukuona sikuwahi Ila Kwa sababu niliamini in my heart unaonewa niliacha waniite mpumbavu. Leo Na wewe unaniita mpumbavu sababu namtetea Wema Kwa kitu ambacho hata wewe unajua sio sawa? Na ukisoma sijamtetea nimekurekebisha tu kuwa hujakosea ni sawa team Wema ni wapumbavu je kwanini huwasemi hizo team zingine Kwa upumbavu huu? Umemsema Wema hawakanyi team yake je Mbona hujamsema Dai Au Zari kwanini hawakanyi team zao?Lazma tuwe watu wa haki. Hizi team zoooote ni ushuzi mtupu Na ni majipu. Sasa unapochagua team ya kutupia lawama unakosea..
.
.
Mimi mpumbavu inapokuja issue ya Wema Ila nadhani nilionekana mpumbavu Mara Mia wakati nakutetea wewe na sikujali so kaa ukijua huwa sijalimatusi, nishatukanwa matusi kibaooooooo Sasa wamebaki wanayarudia tu! As long as I feel Mtu anaonewa Hata Kama ni Malaya wa jollies ntamtetea tu.
.
.
After all Wema has been through as a woman Na wewe Kweli unaona huu ni mida wa kumu-attack? Wanawake walivyokupigania kipindi kile ushasahau?Au mpaka Mtu awe single mother ndo unaona anafaa kupewa support? 
.
Alafu muache kujiliza ovyo na huo usingle mother wenu. Utadhani mlibakwa jamani..... Seriously sawa Wanaume Wanakosea kuwatupieni Watoto Ila duh mmezidi kulalamika jamani! Yani Sasa Hivi nikisikia neno single-mother I just roll my eyes like 🙄🙄
.
.
PS- sijaweka Picha hizi ili utukanwe nimeweka ili tu nikukumbushe kuwa Mimi naweza kumtetea mtu Hata Kama akionekana hana thamani duniani. As long as I believe rights zake zimekuwa violated Au uonevu umezidi... I don't mind your dressing at all Ila usiite Mtu mpumbavu eti Kisa kumtetea mwanamke anae onewa , jikumbuke wewe ulivyoitwa mpumbavu , malaya, mshenzi, mama mbaya majina yote waliyamaliza and still watu tulikupigania. 
.
Although umeniita mpumbavu wala sitokutukuna au kukuita mpumbavu pia. Yawezekana nikawa mpumbavu Kweli ikija Kwa wanawake kama Faiza Ally na Wema Sepetu! Nakuwa sioni siambiwi
Read more at http://websta.me//n/mangekimambi_#XZ0wPpjK2xXS22UZ.99

Uchunguzi Usafirishaji wa Tumbili Wakamilika

$
0
0
Kikosi kazi maalumu cha kuchunguza makosa ya kihalifu kimekamilisha uchunguzi wa tuhuma za usafirishaji Tumbili 61 zinazowakabili raia wawili wa Uholanzi na Watanzania wawili.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, alilithibitishia gazeti hili jana kukamilika kwa uchunguzi huo na kusema jalada limepelekwa ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua zaidi.

Kauli ya Mutafungwa imekuja wakati kuna uvumi uliozagaa kuwa watuhumiwa hao wataachiwa huru wakati wowote kuanzia jana bila kufunguliwa mashtaka.

Kamanda Mutafungwa alisema kuwa wao kama chombo cha uchunguzi, wametimiza wajibu wao na mwenye uamuzi wa kushtaki au kutoshtaki ni Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) baada ya kupitia ushahidi.

Hata hivyo, alisema kuwa watuhumiwa hao wanne bado wanashikiliwa na polisi wakisubiri maelekezo ya kisheria ya DPP, hivyo siyo sahihi watu kuvumisha kuwa wameachiwa bila masharti.

Watuhumiwa hao ni Mkurugenzi wa Matumizi Endelevu ya Wanyamapori, Dk Charles Mulokozi na Ofisa Mfawidhi wa Kituo cha Uwindaji wa Kitalii, Utalii wa Picha na Sites cha jijini Arusha, Nyangabo Musika. Watuhumiwa wengine ni raia hao wa Uholanzi ambao ni ndugu wa familia moja, Artem Alik Vardanyian (52) na Eduard Alik Vardanyian (44).

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe alipoulizwa juzi kuhusu uvumi wa kutoshtakiwa kwa watuhumiwa, alisema yeye ametimiza wajibu wake.     


James Lembeli (Chadema ) Aangukia Pua Kesi ya Kupinga Ushindi wa Mbunge wa CCM Kahama

$
0
0
Mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Shinyanga leo imetupilia mbali maombi ya James Lembeli wa CHADEMA ya kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi wa mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini wa Oktoba 25 2015, kwa madai kwamba taratibu zilikiukwa.

Akisoma hukumu iliyochukua saa tatu Jaji wa Mahakama hiyo Moses Mzuna amesema ushahidi uliotolewa na upande wa Lembeli haukuwa na nguvu za kutosha kuishawishi mahakama hiyo kutengua matokeo ya uchaguzi kwani sehemu kubwa ni wa maneno.

Jaji Mzuna amesema kitendo cha Lembeli kulalamikia vitendo vya rushwa vidavyodaiwa kufanywa na mgombe wa kiti hicho kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jumanne Kishimba kushindwa kuvitolea taarifa kwenye vyombo vya dola kimedhoofisha ushahidi na kuuwekea mashaka. 

Kwa upande wa mashahidi waliounga mkono kuwepo kwa vitendo vya rushwa Jaji Mzuna amesema wameshindwa kujenga hoja kwa mlolongo unaofanana kiasi kwamba wameonekana kana kwamba walikuwa na ushahidi wa kutengenezwa.

Akitoa hukumu hiyo, Jaji Mzuba amefafanua kuwa madai ya unyanyasaji wa wafuasi wake waliokamatwa na polisi katika hoteli ya Golden Rock na wengine katika kata ya Ngogwa yamekosa nguvu kufuatia kukosekana kwa kielelezo cha maandishi kinachoonesha kwamba walikuwa mawakala wake.

Mzuna amesisitiza, sababu ya Lembeli kushindwa kupeleka malalamiko kwenye kamati ya maadili ya uchaguzi iliyowekwa kisheria kwamba hakuwa na muda wa kutosha haikubaliki kwa kuwa mpiga kura yeyote anayemuunga mkono angeweza kulalamika.

Kufuatia uamuzi huo wa mahakama kutupilia mbali maombi ya kutengua matokeo hayo Lembeli amesema anaiheshimu mahakama, na kwamba atashauriana na wakili wake kuona kama haki haikutendeka ili kukata rufaa.

Naye Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini aliyekuwa mlalamikiwa namba moja katika shauri hilo Kishimba alipohojiwa amesema Jaji ametenda haki kama walivyotenda haki wananchi wa Kahama kwa kumpa kura za ushindi katika uchaguzi wa oktoba 25,2015.

Shauri hilo lilikuwa limevuta hisia za wananchi wa Kahama na kuhudhuria kwa wingi leo kwenye hukumu yake huku makundi ya kisiasa yaani wana-CCM na wana-CHADEMA yakijionesha wazi kwa kushangilia bila dalili zozote za uvunjifu wa amani.

Wanaume Wanne Wambaka Binti Mdogo Kwa Zamu na Kumuharibu Vibaya Sehemu za Siri.....

$
0
0
JESHI la Polisi katika Kanda Maalumu ya Tarime/Rorya mkoani Mara, linawasaka watuhumiwa watano wanaotajwa kuhusika kubaka wasichana wawili katika eneo hilo.

Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Andrew Satta alisema, watu hao wanatuhumiwa kuwabaka wasichana hao katika matukio mawili tofauti yaliyotendwa kwa nyakati tofauti Machi 26, mwaka huu katika wilaya za Rorya na Tarime.

Satta alisema kuwa, katika tukio la kwanza mwanafunzi wa shule ya msingi Kibasisi iliyopo kwenye kijiji cha Kangariani wilayani Tarime (Jina limehifadhiwa), alibakwa na watu wawili wakati akirejea nyumbani kutoka shuleni siku hiyo ya Machi 26.

Kamanda Satta alisema kuwa, mwanafunzi huyo alikutana njiani na watu wawili waliokuwa wamejifunga vitambaa vyeusi usoni, ambao walimkamata kwa nguvu, kumburuza vichakani na kumbaka kwa zamu. Alieleza zaidi kuwa, baada ya kumbaka, watu hao walimdhibiti asipige kelele kwa kumfunga kitambaa mdomoni.

“Walipomaliza kumbaka walitokomea kwenye vichaka na kutorokea mahali pasipojulikana, lakini Polisi inawasaka,” alisema na kuongeza kuwa, tukio hilo liliripotiwa Polisi na mwanafunzi huyo.

Katika tukio la pili, Kamanda Satta alisema kuwa, siku hiyo usiku kwenye kijiji cha Ruhu kwenye mwalo wa wavuvi wilayani Rorya, msichana mwenye umri wa miaka 21 (Jina limehifadhiwa), alidanganywa na vijana wanne kuwa aliitwa na rafiki yake wa kiume, jambo lililomfanya awaombe wamsindikize alipo na walitii.

Kamanda Satta alisema kuwa, bila kujua nia ya vijana hao kumdanganya hivyo, binti huyo ambaye hata hivyo anawatambua na kufahamu majina yao, alikubali na kuondoka nao. 

Alisema kuwa baada ya kufika kwenye eneo la mwalo wa wavuvi, karibu na vichaka, huku kukiwa na giza nene, waliamua kumkamata kwa nguvu na kumfunga mdomo kwa kitambaa asiweze kupiga kelele.

“Walipofanikiwa kudhibiti asipige kelele vijana hao wanne walimbaka kwa zamu na kumwacha akiwa hoi vichakani, ndipo binti huyo alipoamua kujikongoja hadi kwenye eneo alipopata msaada wa wasamaria waliomsindikiza kutoa taarifa kwenye kituo cha Polisi na kwenda hospitali kwa matibabu”, alisema.

Watu hao waliotajwa na binti huyo kuwa ndio waliombaka ni pamoja na Ophia Robert ambaye amekamatwa, Nchama Bureki, Robert Shija na mwingine aliyetajwa kwa jina moja, Mashije. 

Aliwaonya wanaoendeleza ubakaji katika kanda hiyo kuacha kwa sababu msako unaofanywa ni endelevu na jeshi hilo halitasita kuwachukulia hatua za kisheria.

Zitto Kabwe Afunguka 'Watumishi Hewa Kwenye Wizara Mbona Hatusikii? Najitolea Kutumbua wa Wizara ya Ujenzi'

$
0
0
Mbunge wa Kigoma mjini kupitia ACT wazalendo Zitto Kabwe, ameitaka serikali kuwabainisha wafanyakazi hewa kwenye wizara, baada ya agizo la Rais la kuhakiki watumishi hewa kwenye halmashauri kutekelezwa.

Zitto Kabwe ameandika ujumbe kwenye ukurasa wake facebook, na kuonesha kushangazwa kwa wizara kutoweka wazi wafanyakazi hewa waliomo humo, huku akijitolea kubainisha wale wa kwenye wizara ya ujenzi.

“Watumishi hewa kwenye wizara mbona hatusikii? Wakuu wa mikoa wameagizwa kutambua watumishi hewa. Mawaziri hawakuagizwa. Ok ngoja nijitolee kutambua watumishi hewa wizara ya ujenzi kupitia ripoti za CAG 2010/2011 mpaka 2014/2015”, aliandika Zitto Kabwe.

Hivi karibuni mikoa yote nchini imetekeleza agizo la kuhakiki wafanyakazi hewa walioko kwenye halmashauri zao, huku mkoa wa Mwanza ukiongoza kwa kuwa na wafanyakazi hewa 334

Wenje Aiomba Mahakama Imkubalie Vielelezo Vyake...

$
0
0
Wakili anaemtetea Ezekiah Wenje katika kesi ya kupinga ubunge wa Jimbo la Nyamagana, Deya Outa, amewasilisha ombi dogo Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, akiomba fomu ya uchaguzi namba 21B zitumike kama ushahidi wao.

Kesi hiyo imefunguliwa na Wenje (Chadema) akipinga ushindi wa Mbunge wa jimbo hilo, Stanslaus Mabula (CCM) kupitia uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.

Akiwasilisha ombi hilo mahakamani hapo mbele ya Jaji Kakusulo Sambo wa mahakama hiyo jana, wakili Outa aliiomba mahakama iangalie jitihada zilizofanywa na mteja wake (Wenje), kuhakikisha kesi yake inasikilizwa, pia jitihada alizofanya za kukusanya fomu hizo na kuziambatanisha kama kielelezo na kuwaleta mashahidi wa fomu 646.

Alidai wajibu maombi (Mabula na wenzake wawili) wanafahamu mleta maombi anahitaji kuzitumia fomu hizo, pia walipewa taarifa mapema katika hatua za awali za uainishaji wa vielelezo vya ushahidi.

Upande huo uliwasilisha ombi hilo mahakamani hapo chini ya kifungu 13(4) cha Sheria ya Uchaguzi Sura ya 447 ya mwaka 2010, kifungu cha 13 cha mwenendo wa makosa ya madai, ukiomba kutolewa kwa fomu hizo mashahidi waweze kuzitolea ushahidi.

Hata hivyo, upande wa wajibu maombi ukiongozwa na Wakili Mwandamizi, Constatine Mutalemwa, pamoja na upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Vincent Tangoh, uliomba muda wa siku mbili kupitia kumbukumbu za mahakama pamoja na rekodi za kesi hiyo kwa ufasaha zaidi ili wajipange na kujiandaa kujibu maombi hayo.

Mahakama ilikubali ombi la kuongezewa muda kwa upande wa wajibu maombi na upande wa Jamhuri ili uweze kujipanga na  Jaji Sambo aliamuru upande wa wajibu maombi kwenda na majibu leo saa 3:00 asubuhi wakati kesi hiyo itakapoendelea kusikilizwa.

Soma Nafasi za Kazi Mbali Mbali Zilizotangazwa Magazetini Siku ya Leo...

$
0
0


Hapa nimekuwelea link ambayo unaweza kusoma nafasi za ajira zilizotangazwa katika magazeti ya leo tarehe 31 March 2016...
Bonyeza HAPA 

Mapumziko ya Rais Magufuli Nyumbani Kwake Geita Yawapasua Vichwa Viongozi

$
0
0
Mapumziko ya Rais John Magufuli nyumbani kwao, Chato mkoa wa Geita, yanaonekana kuwapasua vichwa viongozi wa serikali ya mkoa huo kutokana na kutoelewa ratiba yake kwa muda atakaokuwapo nyumbani hapo.

Rais Magufuli aliwasili juzi mjini Chato akitumia usafiri wa helikopta ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), iliyotanguliwa na helikopta ya polisi, kabla ya kuwahutubia wananchi wa wilaya hiyo.

Ujio huo ni wa kwanza tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Oktoba 25, mwaka jana.
Hata hivyo, Nipashe jana ililazimika kwenda ofisi ya mkuu wa wilaya ya Chato, Shaaban Ntarambe, ili kufahamu ratiba ya shughuli atakazofanya Rais Magufuli muda atakaokuwapo hapo.

Hata hivyo, hali hiyo imeonekana pasua kichwa kwa viongozi hao, baada ya mkuu wa wilaya kudai tangu Rais awasili nyumbani kwake, viongozi hao walielekezwa kuendelea na majukumu yao ya kawaida. 

"Ukweli viongozi hatuna ratiba yoyote zaidi ya mapumziko, maana tangu amewasili nyumbani tulielezwa kuendelea na kazi zetu za kawaida na Rais atakapotaka kufanya jambo atatujulisha kupitia kwa mkuu wa mkoa,” alisema Ntarambe.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli juzi aliwapongeza wananchi wa Chato kwa kujitokeza kumsikiliza kwenye mkutano wake wa hadhara, licha ya kuchelewa kutoa taarifa za ujio wake kwa kuwa hakupenda kupokewa kwa kishindo kwa sababu huko ni nyumbani kwao.

Nawapongeza kwa kunipokea. Najua wengi mmepata taarifa za ujio wangu kuanzia jana (juzi) saa 11. sikupenda kupokewa maana nakuja nyumbani, ndiyo maana kila napogeuka hapa nawaona wazee wangu mpo hapa wengi," alisema.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo April 1, 2016, Ikiwemo ya Bunge Kutikiswa...

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo April 1, 2016

Breaking News..Radio Clouds FM Yawarudisha Watangazaji Phina Mango na Masoud Kipanya Kazini

$
0
0
Jana kulikuwa na sinto fahamu baada ya tetesi kusemekana kuwa watangazaji maarufu wa kipindi cha Power Breakfirst cha Clouds FM Gerald Hando na PJ Wamefukuzwa kazi, leo tetesi hizo zimezidi kushika mizizi baada ya watangazaji wa zamani wa kipindi hicho Phina Mango na Masoud Kipanya walioacha kazi miaka kadhaa nyuma Kushika nafasi zao...Muda huu nao andika hii habari wako On Air wanatangaza Sambamba na Babra na Fredwaa

Mwenyekiti wa Kitongoji Auawa Kikatili Baada ya Kufumaniwa na Mke wa Mtu Akizini Kichakani....

$
0
0
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Bweya katika Kijiji cha Bweya mkoani Geita, Augustine Katemi (42) ameuawa baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu vichakani.

Mwenyekiti huyo alifariki dunia papohapo baada ya kudaiwa kushambuliwa kwa sime na mume wa mwanamke huyo, mkazi wa Kijiji cha Luchili, Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza.

Tukio hilo lilitokea saa nne usiku Machi 28 baada ya marehemu kudaiwa kukutwa akifanya tendo la ndoa na Chausiku Isangula (32).

Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Latson Mpojoli alisema hana za taarifa za tukio hilo na kuahidi kufuatilia.

Ilielezwa kuwa Katemi aliuawa baada ya kushambuliwa kwa sime na kufa papohapo na baada ya tukio hilo, mtuhumiwa anadaiwa kumshambulia mkewe kwa kutumia sime hiyohiyo na kumsababishia majeraha makubwa sehemu mbalimbali za mwili na amelazwa kwenye Kituo cha Afya cha Nzera.

Mtendaji wa Serikali ya Kijiji cha Bweya, Samson Walwa alisema baada ya kutokea tukio hilo wananchi waliendesha msako na kumtia mbaroni mtuhumiwa wakati akijaribu kutoroka kuelekea Sengerema.

Walwa alisema mtuhumiwa alikamatwa nyumbani kwa Edward Iswalala alipokuwa amefikia kwa siri kutoka Luchili ili kufuatilia mwenendo wa mkewe ambaye anadaiwa kuwa awali alimuaga kuwa anakwenda kumsalimia baba yake mzazi anayetibiwa kwa mganga wa kienyeji.

“Inavyosemekana alikuwa akifuatilia mienendo ya mke wake… sisi tulipomkamata tumemkabidhi Kituo cha Polisi cha Nzera pamoja na nguo za marehemu (mwenyekiti) na zile za mkewe kwani alipofanya mauaji hayo alizichukua nguzo zao hadi tulipomkata nazo,” alisema Walwa.

Mmoja wa wananchi walioshuhudia tukio hilo, Jumanne Tole alisema, Chausiku alimuaga mumewe kuwa alikuwa anakwenda kijiji cha Kalebezo kumsalimia baba yake mzazi kwa waganga wa tiba asilia alikokuwa anatibiwa lakini baada ya kufika na kumsalimia, alikwenda kwa kaka yake aitwaye Ndagabwene Isangula huko Bweya alikofikwa na mkasa huo.

Alisema kuna madai kuwa mtuhumiwa alifika kijijini hapo kwa siri akiwa amevaa nguo na kofia zilizochakaa ili asifahamike wakati akifuatilia nyendo za marehemu na mkewe na akafanikiwa ikidaiwa kwamba alikuwa na watu ambao walikuwa wakimpatia taarifa hizo.

Rais Magufuli Kwa Kupitia Clouds TV Ataja Mshahara Wake Anaolipwa Kwa Mwezi....

$
0
0
Nyota ya Radio ya Clouds FM inaendelea kung'aaa Baada ya leo tena wakati watangazaji wa Clouds TV wakijadili habari za magazeti Rais Magufuli alipiga simu na kusema mshahara wake anaolipwa kwa Mwezi ..Hii imekuja baaada ya magazeti ya leo kuandika habari ya Zitto na Lissu Kudai rais ataje mshahara wake na akatwe kodi..

Rais amewaambia Clouds TV kuwa analipwa Shilingi Milioni 9.5 amesema akimaliza mapumziko yake huko Geita atakuja kutoa mchanganuo wake pamoja na marupurupu anayopata...

Video ya Wabunge Saba Wakitolewa nje ya Bunge la Kenya Baada ya Kupiga Filimbi Rais Uhuru Akihutubia

$
0
0
Nchini Kenya ni Wabunge wa Upinzani kupiga filimbi sekunde chache tu baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuanza kulihutubia bunge la nchi hiyo ambapo KTN wamesema hizo filimbi zilisababisha hotuba ya rais ichelewe kusomwa kwa zaidi ya dakika 30.

kitendo cha Wabunge wa upinzani kukosa nidhamu hii kulimfanya spika wa bunge la Kenya Justin Muturi kuamuru kutolewa nje ya bunge kwa Wabunge saba ambao walitolewa na askari wa bunge kwa mabavu.. 

Tazama hizi video..

Mtazamo: Kuhusu MCC Kusitisha Msaada wa MCC 2 na Shughuli zake Tanzania

$
0
0
Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehemu.

“Democracy is not a bottle of Coca-Cola which you can import. Democracy should develop according to that particular country”. June 1991 in Rio De Janeiro, Brazil

"Demokrasia sio chupa ya Coca-Cola ambayo unaweza kuagiza. Demokrasia lazima ikue na kuendelezwa kulingana na nchi husika". Juni 1991 Rio De Janeiro, Brazil (Tafsiri ni yangu)

“No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people”. From ‘A Peaceful New Year’ speech, Tanzania, January 1968

"Hakuna Taifa lina haki ya kufanya maamuzi juu ya Taifa lingine; wala watu juu ya watu wengine ". Hotuba ya Amani ya Mwaka Mpya, Tanzania, Januari 1968 (Tafsiri ni yangu)

Hili la Marekani na uamuzi wa MCC ni jambo la mpito na haliwezi kuua mahusiano yetu na Marekani. Tanzania na Marekani zinashirikiana kwa mambo mengi na MCC ni sehemu tu tena ni eneo jipya la ushirikiano. Uamuzi huu ni jaribio kwa uhuru wa Taifa letu. Hakuna namna nyingine ila kushinda hili kama tulivyoshinda mengine huko nyuma. Kwa wale ambao wameuona umri watakumbuka namna tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi 1964 pale walipotaka kuwa na kauli hasi dhidi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi baada ya kutaka kuingilia Uhuru wa Mataifa Mawili huru yaliyoamua kuungana na kuunda Nchi Mpya ambayo leo tunajivunia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 1965 Tulivunja uhusiano na Uingereza kufuatia na kitendo cha wazungu wachache kujitangazia Uhuru (Unilateral Declaration of Independence) kule Rhodesia na uingereza kukaa kimya na kushindwa kuchukua hatua stahiki.

Tulivunja Uhusiano na Uingereza kuieleza Dunia kwamba Uhuru wa nchi za Afrika ni kipaumbele muhimu kwa Tanzania. Jambo tunalopaswa kufahamu ni kuwa MCC 2 toka mwanzo imekuwa ni mtihani dhidi ya uhuru wetu. Napenda ieleweke kwamba kipindi hiki kilichotokea sio kuvunjika kwa uhusiano wetu na Marekani bali taasisi ya MCC ndio imesitisha msaada wao kwetu, lakini mahusiano yetu na marekani bado yako pale pale, na si Marekani au Tanzania inayoweza kuugharimu uhusiano wetu.

MCC 1 ilikuwa ni chambo cha kutuvuta na tulipewa bila masharti tena hela nyingi dola milioni 698 na ni fedha tulizopewa moja kwa moja na kupewa uhuru wa kuamua tuzitumieje. Tanzania ilitakiwa kuainisha maeneo kisha wao wanatoa hela. Ndio maana miradi kama ile barabara ambazo hazikuwa zikipata ufadhili kwa kuwa hazikuonekana ni za kiuchumi na miradi ya maji ya Morogoro na kwingineko iliingizwa humu na kupata ufadhili. MCC 2 sio hivyo. Kwenye MCC 2 walengwa wakubwa ni sekta binafsi ya Marekani, hapa kuna mtego hapa, hapa ni biashara hapa.

Mchakato wa MCC 2 ulipoanzishwa, wafanyabiashara kwa kushirikiana na Maseneta wakaanzisha hoja kuwa kwanini Marekani inatoa fedha kwa ufadhili katika nchi ambazo China ndio wenye kufaidika na fedha hizo? Wakaleta hoja ya kuwa Serikali ya Marekani ifanye jitihada ya kuweka fedha kwa kusaidia Sekta Binafsi ya Marekani kupenya Afrika.

Ukaitishwa mkutano wa US-Africa Summit na agenda kubwa ikawa Power Africa. Katika Power Africa, Marekani ikalichagua eneo la Nishati (si uzalishaji viwanda) kwa kutambua kuwa ndio eneo pekee wanaloweza kushindana na wachina. Wakasema wataelekeza fedha huko kuisaidia Afrika kutatua tatizo la nishati ambalo ndio pembejeo ya viwanda. Wakaweka sharti kuwa fedha hizo na miradi hiyo itatekelezwa na Sekta Binafsi ya Marekani.

Ndio sababu wengi wenu mtakumbuka hata Rais Obama alitangazia dhamira ile pale Ubungo kwenye Mitambo ya Symbion Power na sio kwamba alipenda kwenda kutembea Ubungo. Kuanzia hapo kumekuwepo na shinikizo kubwa sana na masharti magumu na yenye kuhamahama (shifting goal post) kutaka kuibaka sekta ya nishati nchini ikiwemo mageuzi ya TANESCO. Zikaainishwa hatua kadhaa,ambazo utekelezaji wake baadhi ni kisheria na kisera na hivyo haziwezi kwenda kwa deadline walizotaka. Kila bodi ikikutana wanaibua hiki na kile lakini wakisema hela watatoa. Hela hizi zikawa zimeshikiliwa kama chambo ukisogelea zinasogea, ni sawa na ule mchoro wa Mpanda Punde aliyeshika fimbo yenye majani na akiielekeza mbele ya punda, kwamba punda ataendelea kuyafuata majani akidhani atayafikia kumbe ndio anaupiga mwendo. Hatimaye wakasema wanasubiri uchaguzi mkuu jambo ambalo halihusiani na madai ya mwanzoni. Baada ya uchaguzi wakaibuka na suala la Zanzibar.

Hivyo, uamuzi wao wa leo ni uamuzi uliotarajiwa. Pia ni uamuzi wenye madhara kwa sekta binafsi ya Marekani pia ambayo ndio ilikuwa itekeleze miradi hiyo. Kama Taifa ni muhimu kulinda utu na uhuru wetu. Ndio msingi wa sera yetu ya nje toka mwanzo na hata sasa. Tumetofautiana na Marekani katika hili tutapatana katika mengine. Ndio uhai wa maisha ya diplomasia.

Wao nao wanayo hadhira ya wapiga kura wao wanayojaribu kuituliza huko nchini kwao kwa uamuzi huu. Tunapaswa kuheshimu uamuzi wao kama ambavyo wanapaswa kuuheshimu wetu. Hatimaye baadae tutapatana. Marekani inaihitaji Tanzania zaidi na Tanzania inaihitaji Marekani. Marekani inahitaji MCC 2 zaidi hali kadhalika Tanzania inahitaji MCC 2.

Mahusiano ya Tanzania na Marekani hayakuanza na hayataisha na MCC. MCC imeyakuta na itayaacha.

Kama marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ndio kigezo, basi Marekani isingekuwa inatoa zaidi ya Dola Bilioni 3 kila mwaka kwa Egypt iliyo chini ya utawala wa kijeshi kwa sababu ya kuununua ugomvi wa Egypt na Israel na isingetoa kiasi cha dola bilioni 6 kwa Israel kila mwaka kwa yale wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.

Huu ni wakati ambao Taifa linawaita Wazalendo wake. Wazalendo wasimame na kusema 'Nchi yangu KWANZA, iwe Sahihi au Imekosea" na Makuwadi watashangilia na kusema "si mnaona sasa kiko wapi?".

Huu ni wakati wa kujifunga mikanda na kulinda heshima yetu kama Taifa letu. Tuna vyanzo vya mapato vingi sana ambavyo hatujaanza kukusanya mapato, tuwe wabunifu na tusibweteke na kutegemea mapato yataongezeka maradufu kwa vyanzo vile vile.

Niseme kwa uchache, sababu walizotoa MCC, na ieleweke aliyetoa tamko ni MCC, heri lingetoka tamko hili Wizara ya Mambo ya Nje au Ikulu ya Marekani, moja ni Zanzibar na pili ni Sheria ya Makosa ya Mitandao (Cyber crimes Act).

Sasa hebu tujadili kidogo, hivi kule Zanzibar tulitaka kitokee nini pale ambapo wanasiasa walikuwa hawataki kujadiliana? Tume ile ile ya Uchaguzi ambayo bado ilikuwa na uhalali wa kikatiba na kisheria kuuitisha, kuufuta na kuuitisha tena uchaguzi ikachukua nafasi yake. Wanasiasa wasio makini wakaishia kuhamishia malumbano mitandaoni badala ya kuitafuta suluhu ya kisiasa na pale siasa iliposhindikana basi wangeitafuta suluhu katika mahakama za Zanzibar. Mezani wakashindwa, mahakamani hawakwenda. Tume ikachukua uongozi, uchaguzi ukaitishwa Wananchi wakapiga kura na sasa huko Zanzibar kuna serikali na baraza la wawakilishi. Hata mimi sifurahii sana njia waliyoichukua Zanzibar lakini ilibidi siasa za madaraka zisite ili tuanze kufanya siasa za maendeleo. Je wamarekani walitaka muujiza gani utokee huko.?

Kuhusu Sheria ya Mitandao, hata mimi siipendi, si twende mahakamani, bunge litaanza vikao muda si mrefu je wabunge si wapeleke hoja ya kuifanyia marekebisho sheria hii. Sasa Marekani (MCC) inapoweka shinikizo kwa suala la Sheria ambayo ni jambo la ndani na linaloweza kujadilika, sijaelewa. Mbona sie hatujapiga kelele Yule jamaa yao Trump alipotutusi waafrika na kusema sisi stahili yetu ni kuwekwa tena chini ya ukoloni (hapa nimechomekea tu).

INDHARI

Ni aibu kwa viongozi wa kisiasa kufurahia jambo hili, ni ishara ya ukuwadi wa kisiasa na ambao uko tayari kukumbatia mahusiano yanayotweza Uhuru wetu. It is now high time kufanya siasa safi za maendeleo (politics of development) na sio kujikita katika katika siasa za madaraka (Politics of Power).

Mwandishi, Ndg. Humphrey Polepole amenufaika na uelewa wa watu wenye uzoefu wa mahusiano ya Tanzania na nchi za Nje. Aidha, ni mnufaikaji (alumni) wa programu ya uongozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.

Muacheni Baba Diamond Akome Kidogo ....Diamond Atamsamehe Siku Akijisikia Kumsamehe na Sio Kwa Wananchi Kutaka-Faiza Ally

$
0
0
Faiza Ally Ameongelea Kuhusu Diamond na Baba yake, Ameandika haya hapa Kwenye Ukurasa wake wa Instagram

Faizaally_ Diamond ni inspiration kwa kina baba wote wanao terekeza watoto wao ! Diamond Ni inspiration kwa single mothers wote wanao lea watoto peke yao ! Diamond ni inspiration kwa watoto wote wanao lelewa na single mothers - single mama tunajua tunapitia mangapi kuwapa watoto wetu mahitaji - wkt mwingine unaweza ukalala hata na mtu mtoto wako apate mahitaji ! NI UHALISIA...... Kwa hiyo MUACHENI DIAMOND ATAMSAMEHE BABA YAKE SIKU AKIAMUA ! SIO WKT MEDIA NA WANANCHI MNATAKA AU KWA SABABU YEYE ANATAKA - MAMA NASIBU KWANZA !!!! AND I LOVE IT! MUACHE APONDE RAHA NA MWANAE MAANA WAO NDIO WANAJUA WAMEPITIA MAMGAPI.... Na Hawa kina baba Diamond wako wengi wakome! waache kuterekeza watoto wao na kukatia tamaa mama zao ! MUACHENI BABA DIAMOND AKOME KIDOGO - ATASAMEHEWA DIAOMOND AKIJISIKIA YUKO TAYARI KUSAMEHE ...... single mothers tunapitia mengi hata sisi tuna tamani kusaidiwa kulea watoto na baba zao ! SINGLE MOTHERS MAMA DIAMOND AWE INSPIRATION KWETU...... mwenye kumsomesha mwanae amsomeshe- mwenye kumuendeleza kipaji amuendeleze na haijalishi unawezo kiasi gani kila mmoja afanye kwa uwezo wake - kuwa single mother sio mkosi wale kilema ni maisha tu na ndio Kama hivyo mnaona MUNGU ANATUBARIKI KWA NJIA TOFAUTI - LEO NAAMINI KUNA WENGI WANGETAMANI WAWE MAMA DIAMOND HATA WALIO KUWEPO KWENYE NDOA  KUWA NA MTOTO KAMA DIAMOND SIO KITU KIDOGO - HONGERA MAMA NASIBU ! UKO JUU ! ...... sasa single mother watagini kina baba Diamond waambieni Kama hawa jirudi Na kutunza watoto baadae wakati tunakula bata Na watoto wetu ......! HATUTAKI KERO NDOGO NDOGO-Faiza Ally


Uamuzi wa MCC Wawagawa Watanzania..Wengi Wailaumu Serikali na Wengine Waunga Mkono

$
0
0
Uamuzi wa Bodi ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) kuinyima Tanzania msaada wa Sh1 trilioni kwa ajili ya kufadhili miradi ya umeme, umewagawa wananchi kutokana na baadhi kuilaumu Serikali na wengine kuunga mkono msimamo wa kujenga uchumi bila ya kutegemea misaada.

Katika kikao chake kilichofanyika Machi 28, Bodi ya Wakurugenzi wa MCC, shirika lililoundwa na Bunge la Marekani kusaidia nchi zinazoendelea, iliamriwa kuwa Tanzania iondolewe miongoni mwa nchi washirika watakaonufaika na misaada ya mfuko huo kutokana na kupoteza sifa.

Bodi hiyo ilisema kufutwa kwa matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana, na kuendesha uchaguzi wa marudio Machi 20 bila ushirikishwaji wa wadau na utekelezaji wa Sheria ya Mtandao ni sababu zilizofanya Tanzania ipoteze sifa za kuwa mnufaika wa miradi hiyo.

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salim Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi wa rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani Oktoba 28, 2015 siku ambayo alitakiwa amtangaze mshindi wa kiti cha rais. Uamuzi huo ulipingwa na chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar, CUF lakini Jecha akatangaza tarehe mpya ya uchaguzi ambao ulirudiwa Machi 20.

Pia, kwa kutumia Sheria ya Mtandao, watu kadhaa walikamatwa kwa tuhuma za kusambaza habari za upotoshaji, huku Chadema ikilalamika kuwa vijana wake waliokuwa wakijumlisha matokeo ya uchaguzi walikamatwa na kunyang’anywa kompyuta zao.

Akizungumzia hatua hiyo, Waziri Kivuli wa Mambo ya Nje, Peter Msigwa alisema wakati tukijenga uwezo wa kujitegemea, bado tunahitaji kuutumia ushirikiano uliopo na nchi marafiki ya mashirika ya kimataifa ili Tanzania isiishi kama kisiwa.

“Nimesikitishwa na Tanzania kukosa fedha za MCC ambazo zilikuwa ni muhimu sana katika kuharakisha upatikanaji wa umeme kwa Watanzania wa vijijini. Hata hivyo, ningependa kuweka wazi kuwa Tanzania haijaonewa hata kidogo kunyimwa msaada wa Sh1 trilioni na Shirika la Misaada la Marekani la MCC kama ilivyopotoshwa na Serikali,” alisema Msigwa katika taarifa yake kwa vyombo vya habari.

“Ni vema ikazingatiwa kuwa MCC inazingatia vigezo 17 katika kuchagua nchi inayostahili kupata msaada na miongoni mwa vigezo vya msingi kabisa ni nchi husika kuwa na dhamira ya dhati ya kuimarisha demokrasia na kuendesha chaguzi zilizo huru na haki.

“Na katika taarifa yake MCC ilieleza maeneo ambayo Tanzania imekiuka vigezo kuwa ni marudio ya uchaguzi wa urais Zanzibar na kupitisha Sheria ya Makosa ya Mawasiliano ya Mitandaoni –“Cyber Crime.”

Mchungaji Msigwa ameelezwa kushangazwa na kauli ya Waziri wa Mambo ya Nje, Dk Augustine Mahiga kuwa amestushwa na uamuzi wa MCC, badala ya kukiri makosa yaliyofanywa na Serikali na chama tawala katika suala la Zanzibar na mtumizi ya Sheria ya Mtandao, ambayo amesema yananyima uhuru wa habari na kujumuika.

Makamu Mkuu wa Chuo Kiku Kishiriki cha Ruaha (Ruco), Profesa Gaudence Mpangala aliungana na Mchungaji Msigwa kuhusu uamuzi wa MCC.

“Uroho wa madaraka wa kundi dogo la Watanzania umesababisha dhahama hiyo itakayoligharimu Taifa kwa muda mrefu wakati mikakati ya kusaka mbadala ikiandaliwa,” alisema.

“Pamoja na jitihada za serikali kubana matumizi na kuongeza ukusanyaji wa mapato hatuwezi kuziba pengo lililopo. Itachukua muda.”

Naye mkurugenzi mtendaji wa Shirika lisilokuwa la Kiserikali inalojihusisha na Masuala ya Kijamii (Fordia), Buberwa Kaiza ameandika katika ukurasa wake wa facebook kuwa Tanzania inapaswa kuwa makini zaidi.

“Tunachotakiwa kufahamu ni kuwa Tanzania isipokuwa makini itaelekea njia ile ile na kuishia iliko Zimbabwe ya sasa. Si muda mrefu tutasikia Eurozone (nchi za barani Ulaya) nao wameamua hivi au vile dhidi ya Tanzania. Haitachukua muda tutasikia G7 wameamua kuunga mkono Serikali ya Marekani dhidi ya Tanzania. Baadaye watafuata Paris Club, WTO na kadhalika,” ameandika mwanaharakati huyo.

Lakini wachambuzi wengine waliilaumu Marekani kwa kutaka kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania.

Mhadhiri mwanadamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Francis Michael alisema MCC wana haki ya kufanya kile walichoamua, lakini wanapaswa kutambua kuwa Tanzania pia ina haki kama hiyo katika kuendesha mambo yake.

“Hatuwezi kuamuliwa au kupangiwa masuala yetu ya ndani kwa mgongo wa misaada. Huu ni ukoloni mamboleo. Wakae na misaada yao. Jambo muhimu ni kwa Rais (John) Magufuli kusimamia uzalishaji nchini,” alisema Dk Michael.

“Viwanda vilivyokufa vifufuliwe na kilimo kipewe mkazo unaohitajika ili kutosheleza mahitaji ya ndani na ziada isafirishwe nje. Marekani ni wazuri kwenye kuhubiri demokrasia. Ni wao ndio wanaoifadhili Israel wakati wanafahamu kuwa inaikalia Palestina kwa mabavu. Demokrasia hainunulwi.”

Mtaalamu wa masuala ya fedha na utawala jijini hapa, Asanterabi Barakaeli alisema: “Kwa kipindi kirefu tumekuwa tukitegemea misaada hiyo, lakini haijatufikisha popote. Tuanze kufikiri uchumi bila misaada.”     

Instagram Wamwongezea Diamond Dakika za Kuposti Video

$
0
0
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva nchini, Nassib Abdul ‘Diamond’ pamoja na watumiaji wengine wa mtandao wa Instagram wameonekana kufurahia kuongezewa nafasi ya kuweka video katika mtandao huo kutoka sekunde 15 hadi 60.

Diamond na watu wengine walituma baadhi ya video zenye urefu wa muda ulioongezwa kama ishara ya kufurahia ukubwa huo ulioongezwa kwenye mtandao huo wenye watumiaji zaidi ya milioni 400 duniani kote.

“From 15 seconds to 1 minute’ mwee! Asante instagram kwa kutuongezea urefu wa hizi ‘clip’ tujinafasi,” aliandika Diamond kwenye video aliyoituma akiwa na mtoto wake kwenye kifaa cha kubeba mtoto akiwa anavutwa

Wifi wa Zari , Esma Platnumz Adaiwa Kutimuliwa Madale kwa Diamond Platnumz

$
0
0
Hivi karibuni yalitua madai kwenye meza ya gazeti hili yakieleza kuwa, eti yule wifi nambari moja wa Zarinah Hassan ‘Zari’ anayefahamika kwa jina la Esma Platnumz (pichani) ametimuliwa pale nyumbani kwa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’, Madale jijini Dar na sasa anaishi Tandale.

Chanzo chetu ambacho kiliomba jina lake lisiandikwe gazetini kilidai kuwa, baada ya Zari kutua Bongo kabla ya kwenda Ulaya, Esma alitakiwa kufungasha kila kilicho chake na kwenda kuishi kwenye ile nyumba ya familia iliyokuwa ikikarabatiwa pale Tandale.


“Nyie mbona mnapitwa na ubuyu? Esma katimuliwa pale kwa Diamond, sasa hivi anaishi kule Tandale kisa ni zile figisufigisu zilizokuwa zikitokea kati yake na Zari.
“Diamond ameona ili mzazi mwenzake awe na amani, anayeweza kuondolewa kwenye ule mjengo aondolewe ili amani itawale na kusiwepo manenomaneno,” kilidai chanzo hicho.
Siku chanche baada ya ubuyu huo kunaswa, paparazzi wetu akiwa kwenye mishe zake alimuona Esma nje ya nyumba ya akina Diamond iliyopo Tandale huku akionekana kuwa, yupo maskani yake mapya.

Ili kupata ukweli wa madai ya kutimuliwa, paparazi wetu alimvutia waya Esma na alipopatikana alisema: “Nyie bwana, mimi ni wa kutimuliwa pale kwa Diamond? Huwa naishi pale na nikipenda ndiyo nakwenda Tandale lakini hayo mambo ya kwamba nimetimuliwa ili kumpisha Zari ajiachie na Diamond ni vijineno tu vya watu.”

Garissa University Survivor Marries KDF Soldier Who Saved Her

$
0
0
A former Garissa University student married a soldier who came to her rescue during the Al Shabaab attack on the campus that killed 148 people. 

21-year-old Maureen Mayengo had been hidding in a closet for 12 hours when a contigent of the Kenya Defence Forces troops found her.

Among the soldiers was 25-year-old Ivan Okello based at Lanet, who married Ms Mayengo four months after the attack. 

The two had met before but decided to tie the knot after the horrifying incident. Manyengo revealed to the Standard that she lovingly refers to her husband as her 'shield and defender'. 

The Garissa survivor has since transferred to Moi University alongside other affected students and hopes to formalise their marriage after her graduation in a church wedding.

Mayengo lives in Lanet with her husband who is currently deployed in Somalia where KDF is battling the Al shabaab militants under AMISOM.  

In the interview, Mayengo divuldged that she was still traumatized by the events of that fateful Thursday morning and vowed never to step foot in Garissa University college. 

On April 2nd 2015 armed gunmen stormed Garissa University College shooting randomly at students before members of the elite RECCE squad neutralised the attackers. 

On Saturday, Kenyans marked one year since the attack which was the deadliest since the 1998 Unites States Embassy bombing in Nairobi.  

MREMA amtaja kortini mwakilishi wa Papa ilivyotumika kusambaza vipeperushi vya kumfanyia kampeni Mbatia

$
0
0
Shahidi wa kwanza katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge Jimbo la Vunjo, Augustine Mrema (TLP), ameieleza Mahakama jinsi siku ya ziara ya Balozi wa Baba Mtakatifu nchini, Askofu Mkuu Fransisco Padilla ilivyotumika kusambaza vipeperushi vya kumfanyia kampeni mbunge wa sasa, James Mbatia.

Mrema ambaye anapinga ushindi wa Mbatia, alitoa ushahidi wake mbele ya Jaji Lugano Mwandambo wakati akijibu maswali ya Wakili Mohamed Tibanyendera anayemtetea Mbatia.

Mwanasiasa huyo aliyegombea ubunge katika jimbo hilo alikana taarifa ya gazeti la Mwananchi la Februari 15, mwaka huu, lililomnukuu akisema kwamba hajutii kumpigia debe Rais John Magufuli wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Katika gazeti hilo, Mrema alinukuliwa akisema pamoja na kutoswa ubunge bado anasimamia kwamba Rais Magufuli ndiye mtu aliyestahili kuongoza Tanzania.

Alidai Oktoba 24, mwaka jana, katika eneo la Mandaka, Kata ya Kilema Kusini, Msaidizi wa Baba Mtakatifu Padri Msafiri alikuwa kwenye ibada iliyofanyika kanisani hapo na alikuwa akigawa vipeperushi vya Mbatia kwa waumini.

Mrema alidai siku ya ibada yeye na Mbatia hakuwakupo kanisani, lakini salamu za mbunge huyo zilisomwa mbele ya waumini na taarifa ya yaliyojiri alipelekewa na watu waliokuwapo pamoja na kipeperushi mojawapo.

Alidai katika jimbo hilo lina makanisa zaidi ya 100 na yote yalipata vipeperushi, isipokuwa moja ambalo huwa anasali lililopo katika Kijiji cha Kiraracha, Kata ya Marangu Magharibi na ndilo eneo ambalo Mbatia alipata kura chache kuliko zote.

Katika kesi hiyo, Mrema anamlalamikia Mbatia, msimamizi wa uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali akidai uchaguzi haukuwa huru na wa haki.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images