Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 6

0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 6
Publish

HATIMAYE Mwanamuziki Ray C Afunguka Siku Atakayo Maliza Kutumia Dawa za Methadone...Adai Mungu ni Mwema Kwake

0
0
Ameandika Haya Kupitia Ukurasa wake wa Instagram...

rayc1982 Mungu ni mwema siku zote ni takriban miaka mitatu sasa nameza dawa ambapo mwezi June mwaka huu namaliza dose,sambamba na hilo namshukuru mungu mpka Jana nimeambiwa vijana wote 80 nilio washawishi na ninaoendelea kuwashawishi kuachana na madawa wanaendelea na matibabu hapa Dar es Salaam ukiacha wale mikoa niliotembelea. Kwa mantiki hiyo nashukru taasisi ya ray c foundation Kwa mchango huo..Nimekaa na familia yangu,ndugu na jamaa pamoja na mashabiki wangu wamenishauli kuachana na binadamu wasio penda mafanikio yangu.Wanao Fanya juhudi za kuhakikisha wananiandama kwenye MEDIA bila kuangalia upande wa pili kwamba kachangia nini.Hasahasa Kwa manufaa yao binafsi Mimi kama Ray c namwachia mungu atawaliapa

Msanii Ali Kiba Amkana Tena Jokate Adai sio Wapenzi na Kufunguka Makubwa....

0
0
Msanii Ali Kiba amefunguka kuhusu suala la ndoa na mwanamitindo maarufu hapa Bongo Jokate Mwegelo, ambaye inasemekana yupo naye kwenye mahusiano ingawa mwenyewe anakanusha.

Akiongea kwenye kipindi cha eNews kinachorushwa na East Africa Television, Ali Kiba amesema siku hizi watu wanasahau na kudharau waliyokuwa wakiyafanya wazee wetu katika kuchagua mke wa kuoa.

“Unajua siku hizi watu wanasahau kuwa wazee wetu walikuwa wanachagua vipi msichana, siku hizi tunaoana tu, unaishi nae miaka mitatu, lazima muwe marafiki, hivyo ni vigumu kuachana na rafiki, ila ni rahsi kuachana na mpenzi wako”, alisema Ali Kiba.

Pia ameendelea kusisitiza kuwa yeye na Jokate ni marafiki tu na sio wapenzi kama watu wengi wanavyodhani na kuibua maswali yenye utata kuhusu kauli yake ya kwanza aliposema "Unapooa, lazima muwe marafiki na huyo mwandani wako, ili kudumisha ndoa yenu".

Mzazi Amlawiti Mtoto wa Mwaka Mmoja na Nusu, Serikali yatoa Tamko

0
0
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesikitishwa na kukemea vikali tukio la mzazi kumbaka na kumlawiti mtoto wake wa kufikia mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu, kitendo kilichofanywa na John Donald (35) mkazi wa Kiyangu, Manispaa ya Mikindani mkoani Mtwara. 

Tukio hili la kubaka na kulawitiwa ni ukatili wa hali ya juu dhidi ya mtoto maana husababisha maumivu makali ikiwa ni pamoja na kumdhuru mtoto kimwili, kisaikolojia, kijamii na kihisia. 

Aidha, vitendo hivi, vinaacha kovu la kudumu kimwilini, kiakili, kimaadili, kijamii, ulemavu, maumivu, na wakati mwingine husababisha kifo; jambo ambalo linahitaji ulinzi thabiti katika kuhakikisha watoto wanaishi mazingira salama na rafiki. 

Ukatili aliofanyiwa mtoto eneo la Kinyangu, manispaa ya Mikindani, ni ukiukwaji mkubwa wa haki za mtoto ambao huchangia kurudisha nyuma ustawi na maendeleo ya Mtoto na ni kinyume cha Sheria ya Mtoto Na. 21 ya mwaka 2009.

Wizara inatoa pongezi kwa Jeshi la Polisi mkoani Mtwara kwa kumkamata mtuhumiwa na kumfikisha mahakamani ili hatua za kisheria zichukuliwe. 

Vile vile, Wizara inaipongeza Mahakama ya Wilaya ya Ilala, mkoani Dar es salaam dhidi ya  Omary hamisi (25), mkazi wa Gongo la Mboto, Dar es salaam, ya kutumikia kifungo cha maisha jela, baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka tisa mwenye ulemavu wa kusikia na kuongea. 

Uamuzi huu ni kielelezo kuwa, wananchi wakitoa ushahidi wa matukio ya ukatili dhidi ya watoto, watuhumiwa watachukuliwa hatua kali ili kuwa fundisho kwa wananchi wanaowanyanysa watoto.

Wizara inamwelekeza Afisa Ustawi wa Jamii na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa wa Mtwara kuwasiliana na wadau wengine katika ngazi zote kuhakikisha mama na mtoto wanapata huduma ya afya na  ushauri na kufuatilia mwenendo wa shauri hili. 

Imetolewa na

Erasto Ching’oro
Msemaji wa Wizara
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

Ufisadi Waiponza NSSF... Yapigwa Marufuku Kuendelea na Ujenzi wa Miradi Mipya

0
0
Bunge limesimamisha utekelezaji wa miradi yote mipya ya Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) mpaka hapo Kamati na Wizara itakapopitia taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), sambamba na kuitisha taarifa za utekelezaji wa miradi yote iliyofanywa na mifuko ya hifadhi ya jamii nchini.

Aidha, imeagiza ukaguzi wa kina wa ujenzi wa jengo jipya la Ofisi za Makamu wa Rais kwa kuangalia usalama wa jengo, hesabu zilizotumika kama zinaendana na thamani ya jengo na kama washauri walitoa ushauri wao ipasavyo.

Akizungumza katika kuhitimisha ukaguzi wa miradi mbalimbali ya serikali iliyofanywa na Kamati ya Katiba na Sheria, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohamed Mchengerwa alisema NSSF ilitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ikiwa haijitoshelezi kwa kutoonesha gharama zilizotumika mpaka sasa, bajeti iliyopangwa kutumiwa na kiasi kilichosalia ili kubaini kama fedha zilizotumika zinalingana na thamani ya ujenzi wenyewe.

Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria kwa takribani siku tano kuanzia Machi 29, mwaka huu, ilitembelea Wizara ya Katiba na Sheria, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu na Mahakama.

Akizungumzia taarifa za utekelezaji wa miradi iliyofanywa na mifuko yote ya hifadhi za jamii, Mchegerwa alisema kamati yake inataka kupitia taarifa zote za utekelezaji wa miradi sambamba na kupitia sera ya uwekezaji ili kuangalia kama yamefuata taratibu na hakuna upotoshaji.

“Kwanza kuna madeni makubwa ambayo mifuko hiyo inadai kwa wapangaji wao. Pia tunaangalia sera ya uwekezaji ili kujiridhisha kama ushauri wa kitaalamu uliotolewa unakidhi matakwa ya ujenzi unaoendelea.

Aliongeza: “Kuna majengo mengi yamejengwa hayana wapangaji lakini sera ya uwekezaji itatusaidia kujua kama inafuatwa. Pia itatusaidia kubaini mapungufu yaliyojiri, maana wajumbe wengi wana wasiwasi kuwa huenda ujenzi wa majengo unalenga kwa wahusika kupata asilimia 10 bila kuangalia mahitaji halisi, kwani majengo mengi yako wazi.”

Download Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

0
0

Good News! Sasa Blog yako ya Udaku Special Ipo Google Play Store.

Download Udaku Special Blog Android Application CLICK HERE From Play Store

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Vanessa Mdee analipwa kila muziki wake unapochezwa kwenye Radio na TV yoyote South Africa

0
0
Kwenye dunia ya sasa Wasanii wa muziki pia wanayo nafasi ya kulipwa au kujiingizia pesa kutokana na vyanzo mbalimbali na hiyo yote ni kutokana na muziki wao ndio maana sio kitu kigeni tena kuona msanii analipwa pale nyimbo zake zinapochezwa redioni.

Kama ulikua hujui, mwimbaji staa wa Tanzania Vanessa Mdee huwa anapokea pesa zake mara kwa mara kutokana na nyimbo zake kuchezwa kwenye Radio na TV za Afrika Kusini ambapo hii imekua ni kanuni inayofatwa kwa baadhi ya nchi, Radio na TV kuwalipa wasanii kutokana na jinsi nyimbo zao zilivyochezwa.

Sio kila msanii anaweza kulipwa kama hivyo, kwa Wasanii wanaotoka nje ya nchi kuna vigezo vinatazamwa kukuwezesha kusajiliwa na mamlaka husika na baada ya hapo unakua kwenye mzunguko wa kulipwa kama Wasanii wengine wa nchi hiyo wanavyolipwa.

Vanessa anasema ‘Kwanini Tanzania tusiende juu zaidi? ni kitu kizuri sana hiki…… kuanzia nilipotoa wimbo wa no body but me niliofanya na rapper K.O wa South Africa ndio nimeanza kulipwa sababu nilikua sijajiandikisha kabla ya hapo, South Africa msanii yeyote mziki wake ukichezwa kwenye Radio, TV au migahawani na sehemu nyingine analipwa‘

Sijajua kwa Uganda lakini Kenya kumekua na hii sheria kwa muda sasa hivi na nilikwenda wakati flani nikaambiwa mpaka Taxi, Saluni, Baa na sehemu nyingine za public kama club za usiku na hotelini wamiliki wake hulazimika kulipia ada ya kila mwaka na kupewa stika maalum kuwaruhusu kucheza muziki wa Kenya ambapo Diamond Platnumz wa Tanzania hulipwa kila mwezi maana ni miongoni mwa wasanii wa nje ya Kenya waliojisajili kwenye mamlaka inayosimamia malipo hayo.

FULL STORY: Mkuu wa wilaya Richard Kasesela Alivyowapeleka Polisi Watangazaji Waliomuigiza Redioni siku ya Wajinga

0
0
Siku ya kwanza ya mwezi April kila mwaka huwa ni siku ya Wajinga duniani na kila mmoja anaeifahamu hii siku huwa anazishtukia baadhi ya habari na wengine huwa wanaifanyia mzaha kweli hii siku kama Watangazaji wa Redio E-bony FM Iringa ambao hawakuwa na nia mbaya kwa kilichotokea sema ndio wakajikuta Polisi baada ya Mkuu wa wilaya kuchukua hatua.

Boss wa Redio hiyo aitwae Edo Bashir aliiambia millardayo.com yafuatayo

‘Unajua ilikua siku ya Wajinga na vijana walichofanya ni ku-fake kama vyombo vya habari vingine vilivyofanya na nafikiri alivyoipokea Mheshimiwa ikawa tofauti, akawakamata na kuwatia ndani lakini nafikiri alielewa baadae ishu ikaisha‘
‘Walichofanya ni kuigiza sauti yake kwa kusema mkuu wa wilaya atakua sehemu flani kuwatembelea… sasa yeye akahisi  wametoa taarifa wakati yeye hakusema, haikuchukua muda Mkuu wa wilaya akawa ameshafika studio akiwa na Polisi‘ – Eddo
Kwenye mahojiano na millardayo.com Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alisema ‘nilikua nasikiliza Redio nikasikia mtu anahojiwa anajitangaza kwamba yeye ni mkuu wa wilaya na kujibu maswali na kutoa ahadi, walitangaza kuanzia jana yake kwamba mkuu wa wilaya atakuwepo, kitendo cha kutangaza jana yake tu yenyewe inaondoa ule usikukuu ya wajinga‘

‘Kisa cha mimi kuwaita wapelekwe Polisi ni ili waandike maelezo kiasi kwamba atakapotokea mtu yeyote atakaelalamika kwamba ilitokea ahadi ya mkuu wa wilaya tarehe moja haijatekelezwa au kuna kitu kimetokea, niwe na ushahidi wa kutosha kwamba wao ndio wamehusika kwahiyo wala sikuwaweka ndani, walikwenda tu kuandika maelezo zaidi‘ – Richard Kasesela
Kwenye sentensi nyingine Mkuu huyu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela ambaye picha zake zimekua zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii kumuonyesha jinsi anavyojitoa kwenye kazi za jamii amesema ‘Hawakukamatwa sababu sikukuu ya Wajinga siijui wala sielewi hapana…. nimewasamehe sababu hawakuelewa hilo ni kosa mi mwenyewe nilikwenda kuwatoa pale Polisi na kuongea nao wasirudie kutumia personality za watu au vyeo kuzungumza na jamii na ilichelewa sana kurekebishwa baada ya kupiga nyimbo tatu‘

Unataka kuipata hii stori kwa urefu na kuwasikia wahusika wote wakiiongelea? bonyeza play hapa chini

Afungwa Kifungo cha Maisha Jela Kwa Kumlawiti Mtoto Mlemavu wa kusikia na kuongea.

0
0
Mkazi wa Gongo la Mboto, Omary Hamis (25) amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka tisa ambaye ni mlemavu wa kusikia na kuongea.

Hakimu Mkazi, Flora Haule wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, alisema mahakama imeridhishwa na ushahidi wa mashahidi tisa ukiwamo wa daktari na fomu namba tatu ya polisi (PF3), iliyotolewa mahakamani hapo kama kielelezo dhidi ya mshtakiwa huyo.

“Mahakama imekukuta na hatia hivyo inakuhukumu kifungo cha maisha jela, baada ya kupatikana na kosa la kumlawiti mvulana wa miaka tisa ambaye ni mlemavu wa kusikia na kuzungumza, ili iwe fundisho kwa jamii,” alisema hakimu Haule.

Katika ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, ilidaiwa kuwa mtoto huyo siku ya tukio alifika kwenye banda la kuonyeshea video ambalo linamilikiwa na Hamisi saa za jioni, kwa ajili ya kuangalia video, lakini Hamis alimfukuza kutokana na kutokuwa na pesa ya kiingilio.

Baada ya kumfukuza mtoto huyo aliondoka, lakini baadaye alirudi bila ya Hamis kuwa na taarifa akakaa ndani ya banda na kisha kupitiwa na usingizi uliosababisha abaki kwenye banda hilo peke yake hadi usiku.

Hamis alitumia mwanya huo kumlawiti mtoto huyo kwenye jumba bovu lililopo jirani na ofisi yake hiyo.

Mashahidi waliieleza mahakama kuwa walisikia sauti ya mtu ambayo ilikuwa haisikiki vizuri akiomba msaada, ndipo waliposogea na kumkuta Hamis akitekeleza kitendi hicho huku akijua kuwa ni kosa kisheria.

Mashahidi walidai hata walipomkaribia, Hamis aliendelea kutekeleza kitendo hicho hadi walipolazimika kumpiga mateke. Hamis alikiri kuwa siku hiyo watoto walifika kwenye banda lake hilo.

Wakili wa Serikali, Ester Kyara aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mtuhumiwa ili iwe fundisho kwa wote wanaotumia mabanda ya kuonyesha video kufanya ukatili kwa watoto.

Katika utetezi wake, Hamisi alisema ana familia inayomtegemea hivyo apunguziwe adhabu, maombi ambayo yalitupiliwa mbali na mahakama hiyo na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela.

Hamisi anadaiwa kutenda kosa hilo Agost 26, 2014 eneo la Gongo la Mboto.

Fatuma Karume 'ALIPUKA': Zanzibar tunaishi kama wanyama!

0
0
Mwanadada jasri na aliyejizolea umaarufu hivi karibuni Fatuma Karume AMELIPUKA, unaweza kusema. Akihojiwa na DW amesema sasa Zanzibar wanaishi kama wanyama maana hawafuati katiba. "Kama wameamu kuondoa utaratibu tuliyojiwekea sasa tuna tofauti gani na wanyama?"

Alipoulizwa kama vitisho vya Ccm havimtishi na kama baba yake hamdhibiti, amesema. "Mimi siyo mbwa wala paka, nina haki yangu ya asili ya kujieleza na kutoa maoni" Amesema babake hawezi kuondoa uhuru wake kisa Ccm.
"Wanataka baba anidhibiti? (kicheko) "nina miaka 46, tena baba ananihimiza kufanya nachoamini ni haki"


Alipoulizwa maoni yake kuhusu MCC amesema anasikia watu wanasema wazanzibar wako tayari kufa njaa lakini serikali iachwe huru. "Hivi tunahitaji serikali huru au watu huru? hapa tuna wakoloni wengine" Ameuliza "yaani watu wa Zanzibar wafe njaa kisa Shein awe rais?" haiwezekani!

Hatimaye Utumishi Wafafanua Kuhusu Mshahara wa Rais Magufuli na Kikwete

0
0

Siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli, kutaja mshahara wake kuwa ni Sh. milioni 9.5 kwa mwezi, Wizara ya Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, imefafanua mshahara aliokuwa anapokea Rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete, kuwa unalingana na wa kiongozi huyo.


Katibu Mkuu Utumishi, Dk. Laurean Ndumbaro jana  alisema Kikwete aliondoka madarakani akiwa anapokea Sh. milioni 9.5, ikiwa ni kiwango sawa na cha Rais Magufuli.


“Hadi Kikwete anaondoka madarakani, mshahara wake kwa mwezi ulikuwa Sh. milioni 9.5, siyo kweli kuwa alikuwa akipokea Sh. milioni 34 kama ilivyowahi kuelezwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari,” alisema.


Mwishoni mwa wiki akiwa kwenye mapumziko nyumbani kwake Wilaya ya Chato mkoani Geita, Rais Magufuli alitaja mshahara wake, huku akiahidi kuweka hadharani stakabadhi za mshahara (salary slip) atakaporudi Dar es Salaam.


Rais alilazimika kufanya hivyo kufuatia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo), kumpa changamoto ya kutaja mshahara wake, baada ya kueleza nia ya serikali yake kupunguza mishahara ya watumishi wa mashirika na taasisi zake kutoka Sh. milioni 40 hadi milioni 15.


Iwapo Rais mstaafu Kikwete, alikuwa analipwa kiasi hicho, kwa mujibu wa sheria, kwa sasa analipwa asilimia 80 ya mshahara huo ambayo ni Sh. milioni 7.6 ya mshahara wa Rais aliyeko madarakani.


Hivi karibuni, baadhi ya vyombo vya habari vilinukuu taarifa iliyotolewa Julai, mwaka jana na mtandao wa Africa Review ulioandika kuwa Rais Kikwete wakati akiwa madarakani alikuwa akishika nafasi ya tano miongoni mwa marais 38 wa Afrika kwa kulipwa mshahara mnono wa Dola 16,000 za Marekani (sawa na Sh. milioni 34 wakati huo).


Taarifa hizo zilikanushwa vikali na Ikulu, lakini hakukuwa na ufafanuzi wa mshahara halisi anaopokea Rais kwa wakati huo.


Kwa mujibu wa Katiba ibara ya 43 (1), Rais atalipwa mshahara na malipo mengineyo na atakapostaafu, atapokea malipo ya uzeeni, kiinua mgongo, posho, kadiri itakavyoamuliwa na Bunge na mshahara, malipo hayo mengineyo, malipo ya uzeeni na kiinua mgongo hicho, vyote vitatokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya serikali na vitatolewa kwa mujibu wa masharti ya ibara hiyo.


Ibara ndogo ya pili inasema mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais havitapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba.

Mtu Aliyeungua na Moto Hadi Kufa Kwenye Gari Mbezi Ajulikana..Mi Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dar es Salaam

0
0

Mhadhiri  wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Idara ya Sayansi na Uhandisi wa Kompyuta (CoICT), Dk Richard Mgaya amefariki baada ya teketea ndani ya gari lake jijini Dar es Salaam juzi.


Gari la Dk Mgaya liliteketea baada ya kugongana na lori katika eneo la Mbezi Africana, Wilaya ya Kinondoni usiku wa kuamkia juzi na kuwaka moto uliosababisha kifo chake.


Juzi picha mbalimbali zilisambaa zikionesha gari aina ya Toyota Prado lililopata ajali eneo hilo la Africana baada ya kugongana na lori, baadaye ilibainika kuwa aliyekuwa katika gari hilo ni Dk Mgaya.


Akizungumza  kwa njia ya simu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Christopher Fuime alisema gari la Dk Mgaya liliteketea na hata kushindwa kujulikana dereva wa gari hilo.


Alisema baadaye ndugu wa marehemu ndio walithibitisha kuwa gari hilo lililoteketea na dereva aliyekuwemo ni Dk Mgaya ambaye hata hivyo naye aliteketea ndani ya gari hilo.


“Lile gari liliungua na hakuna kitu kilichopatikana, hata wakati polisi wanafika eneo la tukio walikuta tayari dereva amekuwa majivu kutokana na kuteketea kwa moto… labda baada ya kupima vinasaba ndio itathibitika kama ilikuwa ni yeye,” alisema Kamanda Fuime.


Alisema hata gari hilo hawakuweza kulitambua mara moja na baada ya kufuatilia Mamlaka ya Mapato (TRA) ilibainika kuwa mmiliki wake ni Dk Mgaya.


Alisema “ndugu wa marehemu ndio wamesema kuwa ni ndugu yao.” 


Dk Mgaya alijiunga na idara hiyo miaka kadhaa iliyopita akitokea masomoni nchini Marekani na alikuwa ni mtaalamu wa artificial intelligence.

Dk. Dau wa NSSF Sasa Matatani...Kufikishwa Mahakamani Muda Wowote

0
0
DK. Ramadhan Dau, aliyekuwa mkurugenzi wa Shirila la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), anatarajiwa kufikishwa mahakamani wakati wowote kutoka sasa. Anaandika Pendo Omary…(endelea).

Dk. Dau anatuhumiwa kuingiza NSSF hasara ya mabilioni ya shilingi, kutokana mikataba ya kinyonyaji. Amekuwa katika shirika hilo kwa miaka 15.
Taarifa kutoka serikalini na taasisi nyingine zinazoshughulikia uchunguzi zinasema, Dk. Dau ambaye aliong’olewa NSSF 15 Februari mwaka huu, atafikishwa kwa mahakamani, kujibu tuhuma za ufisadi zilizoibuliwa ndani ya shirika hilo.

Tuhuma nyingine ni matumizi mabaya ya madaraka, uzembe na ukiukwaji wa taratibu katika miradi ya uwekezaji na vitega uchumi mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Miongoni mwa miradi hiyo, ni ujenzi wa daraja la Kigamboni; hoteli ya kitalii jijini Mwanza, mradi wa ujenzi wa majengo katika mji mpya wa Kigamboni, uwekezaji kwenye jengo la biashara la Mzizima na mgodi wa mkaa wa mawe wa Kiwira, mkoani Mbeya.

Hii Ndiyo Mipango ya Diamond kwa Mwaka Huu

0
0
Pamoja na kuwa tumekuwa tukimshuhudia Diamond Platnumz akitangaza kolabo na wasanii wa kutoka Marekani lakini hakuna hata moja tuliyoona hata cover yake,mwaka jana rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete alimuunganisha Diamond na meneja wa Trey Song na ikasema kuwa kuna kolabo itafuta hiyo ni mbali na Swizz Beats,Alicia Keys,Alaine,Kanye West na wengine,na hivi karibuni tumeona picha ya Diamond akiwa na Awilo Longomba inawezekana kuna kolabo itafuata,sasa isue hua inaishia kwenye kupiga picha peke yake au inakuaje?

‘’Kuna kitu ‘sometimes’ tunasema wanamuziki wenzangu wa Tanzania tusikimbilie katika soko ikiwa kuna soko ambalo hatujalimaliza kwahiyo napiga hapa katikati kolabo nyingi za Waafrika ili niishike Afrika na nijizatiti zaidi usisahau kama mimi sijaanza ‘tour’ yangu rasmi Afrika bado kwasababu nishaona wanigeria wakipiga ‘tour’zao Gabon na sehemu zingine ,na ndio ‘target’ yangu kwa mwaka huu’’ Alisema Diamond.

‘’Na sio kwamba nilikuwa sipati ‘tour’ lakini nilikuwa sitaki kufanya shoo kiudogo ya watu elfu kumi kwenye ‘viklabu’ unaenda Ghana unapiga shoo klabu ni kujidharirisha watu wanakuona unaenda huko wanategemea upige uwanjani’’ Aliongeza Diamond.

cloudsfm.com

Aliyempachika Muna Love Ujauzito ni Kizungumkuti..Petit Man Ajing'ata ng'ata

0
0
Muna Love akiwa na Kalala Junior
Hali imezidi kuwa tete baada ya kuvuma kwa tetesi kuwa anayetajwa kama mke wa Kalala Junior mwanadada Muna Love ametundikwa mimba na Petit Man.

eNewz ilifanya mahojiano na Muna Love na alisema kuwa "Sina mimba ila nimeshiba tu". Lakini kutokana na muonekano wa tumbo lake kuwa kubwa fununu ziliendelea kuwa Muna ana ujauzito wa Petit Man.

Petit Man alipohojiwa na eNewz alijing'ata ng'ata kutoa maelezo ya kutosha na kusema "Acha watu waendelee kuhisi tu wanavyovihisi" huku akikataa kukanusha tuhuma hizo moja kwa moja au kuzikubali.

eNewz ilimtafuta Kalala Junior ambaye naye pia alisuasua kutolea maelezo juu ya mzozo huo, huku pia akikataa kuwa mume wa Muna Love na kusema kuwa Muna na yeye walikuwa ni wachumba tu!
Bado sekeseke hili halijapata majibu ya kueleweka kutokana na wahusika wote kupiga chenga kutoa majibu yanayofafanua ukweli wote.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Mwanamuziki DIAMOND Atoboa "PUA" na Haya ndio Maneno Aliyosema

0
0
Supa Staa wa Bongo Fleva DIAMOND PLATNUMZ ametupia Picha Kwenye Akaunt yake ya Instagram akiwa ametobua Pua na kuweka kipini..

Hata hivyo Hali sio nzuri juu ya Mashabiki wake wengine wakimponda na wengine wakimpongeza..

Hivi ndivyo Alivyo andika kwenye Page yake ya FACEBOO...

Not everyone is going to like, want, accept or know how to receive your Energy...Make peace with that and keep Moving....👍
(Siku zote kumbuka: Sio kila mtu atapendezewa, Atafuraishwa ama kuridhika na ulifanyalo jifunze kulipokea Hilo na uendelee kupambana.... 👍) thank you @zarithebosslady for the Outfit💞 ‪#‎FromTandaleToTheWorldTour‬

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Kinywaji Cha Red Bull ni Hatari Sana Kwa Afya Yako..Chakua Tahadhari

0
0
RED BULL Huuzwa katika maduka makubwa (Supermarkets) na madogo (Retail Shops) katika nchi ya Tanzania, watu wazima na watoto wengi wana mazoea ya kunywa kinywaji hiki ambacho kinaweza kusababisha kifo. Kemikali zinazopatikana katika kinywaji cha RED BULL zilitengenezwa maalum katika maabara za kijeshi za Marekani kwa ajili ya kutuliza mzuka wa maaskari wao wakati wakitekeleza mauaji ya kikatili sana dhidi ya wananchi wa Vietnam miaka ya sitini na sabini. Kemikali hizo zilitumika pia kama dawa ya kuwazindua watu waliozirai (“stress coma”).

Hazikukusudiwa kutumiwa kama kinywaji au kilevi cha kawaida! Duniani kinywaji hiki
(RED BULL) huuzwa kama kitu cha kuleta msismko (Energizer Drink) na matangazo
yake yanataja sifa zake kama ifwatavyo. “Ni kinywaji kinachompa mtu nguvu ya kustahimili na umakini. Humpa mtu kasi ya vitendo” na kadhalika.

RED BULL imesambaa katika nchi 100 kwa mpigo (nchi masikini!). Na matangazo yake huwalenga vijana na watoto, hasa wanamichezo. Hawa ni rahisi kushabikia kinywaji hiki kibaya na kudhurika kiafya baadaye. Katika hali yake ya matumizi ya sasa kinywaji hiki kiligunduliwa na Mjerumani Dietrich Mateschitz ambaye alikikuta huko Hong Kong kikiwa ni mojawapo ya madawa yaliyotumika katika kutengeneza dawa ya mswaki wa meno.
Dawa hiyo ilitengenezwa kwa kemikali ambazo zina kafeni na taurini (“caffeine and “taurine).

Mjerumani huyo aliona vijana wajinga wa huko wakishabikia unywaji wake akaona mwanya wa kufanya biashara na akafanikiwa kukileta ulaya. ATHARI ZA KUNYWA RED BULL Kinywaji kinachotengenezwa na kusambazwa leo hii kina kemikali mbaya iitwayo “Glucuronolactone”, kemikali hatari ambayo ilitengenezwa na idara ya jeshi la Marekani wakati wa vita na Vietnam kwa ajili ya kutuliza mvurugiko wa mawazo wa maaskari wake uliotokana na mauaji ya kinyama waliokuwa wanafanya huko Vietnam.

Kwa sababu ya madhara makubwa ya kinywaji hiki nchi za FRANCE na DENMARK zimepiga marufuku kinywaji hiki na kibatiza jina la “MKOROGO WA UMAUTI”. Katika nchi hizi, utafiti uligundua kuwa maaskari wa Marekani waliotumia kinywaji chenye
kemikali ya “GLUCURONOLACTONE” waliishia kupata madhara ya maumivu makali ya kichwa, uvimbe wa ubongo na hata ugonjwa wa ini (Migraines, Cerebral tumours and liver diseases).

Na kwa sababu hiyo wamarekani waliacha kuwapa maaskari wao hicho kinywaji katika miaka ya sitini na sabini. Jambo la kushangaza ni kuwa lebo ya RED BULL inaonyesha wazi kuwa kinwaji hiki kimetengenezwa kwa kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE”! Ni kwa sababu hiyo serikali za Denmark na Ufaransa nazo zikapiga marufuku unywaji wa RED BULL. Pamoja na wauzaji wa RED BULL kuweka bayana kuwa ndani mwake mna hiyo kemikali hatari ya “GLUCURONOLACTONE” lebo ya RED BULL hailezi madhara makubwa yanayoletwa na kemikali hiyo.

Madhara ambayo hayakuwekwa bayana kwa mnywaji ni kama yafuatayo:

1. Ni hatari kwa mtu ambaye hafanyi kazi au mazoezi mazito sana kukitumia kwani kina tabia ya kuongeza msukumo wa damu na kasi ya mapigo ya moyo kiasi kwamba mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa moyo.

2. Mtumiaji anaweza kupatwa na ugonjwa wa damu kuvuja ubongoni kwani RED BULL ina kemikali zinazoifanya damu iwe nyembamba ili moyo upate kusukuma damu nyingi bila kutumia nguvu nyingi.

3. Ni hatari kuchanganya RED BULL na pombe ya aina yoyote kwani mchanganyiko wake huwa ni sumu (“Deadly Bomb”) inayoathiri musuli za ini la mtumiaji na kuiacha katika hali ambayo haitapona kamwe.

4. RED BULL Ina vitamini B12 kwa wingi, vitamini ambayo hutumiwa kama dawa ya kuwazindua wagonjwa mahututi. Matumizi ya vitamini hii katika watu wazima ina athari za kuleta shinikizo la damu na humfanya mtu ajisikie kama mlevi.

5. Unywaji wa RED BULL mara kwa mara huvuruga mfumo ya neva za fahamu na husababisha maradhi mithili ya mfadhaiko wa akili usioponyeka.

HITIMISHO:
RED BULL ni kinywaji HATARI SANA ambacho hapana budi kipigwe marufuku katika nchi zote zinazoendelea kwani ni dhahiri kimetengenezwa na kusambazwa ili kiathiri afya za wananchi wasiojiweza wa nchi hizi masikini. Kwa kuwa wengi katika nchi hizi hutumia pombe za kila aina ni wazi kuwa kinywaji hiki kinalenga kuwamaliza watu watu wetu– kana kwamba ukimwi uliobuniwa na hao wabaya wetu hautoshi!

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 7, Ikiwemo Wabunge Wajipanga Kumtishia Magufuli

0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya April 7

Nimemuomba Radhi Shetta Kwa Kumtukania Wazazi Wake...Nilikuwa Nimelewa Sana -Dudu Baya

0
0
Msanii Dudu baya ambaye alikuwa na ugomvi na msanii mwenzake Sheta, na kumtolea maneno machafu kwenye kipande cha video kilichosambaa kwenye mitandao ya kijamii, amemuomba msamaha msanii huyo na kumtaka kuwe na amani kati yao.

Kwenye ukurasa wake wa instagram Dudu Baya amepost picha ya Sheta huku akiandika ujumbe mrefu wa kumuomba radhi msanii huyo.

“Habari zenu mashabiki zangu? Ningependa kuchukua nafasi hii leo maalumu kwa ajili ya kukuomba samahani mdogo wangu Nurdin Bilal (Sheta) kwa ajili maneno machafu na matusi niliyowahi kukutukana kwenye kipande cha video kilichosambaa sana kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo facebook,instagram,youtube n.k. So ningependa kuchukua nafasi hii adhimu kuweza kukuomba msamaha kwa lile jambo lilitokea kwani kusema ukweli kabisa sikuwa kwenye hali yangu ya kawaida kwani nilikuwa nimelewa sana pombe”, aliandika Dudu baya.

Baada ya hapo Planet Bongo ya East Africa Radio ilimtafuta Dudu Baya na kusema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa sababu anampenda sana Mungu, hivyo akimkosea mtu lazima atamuomba msamaha na kwa kuwa alimsikia akilalamika kuwa ameumia (Sheta) kutukaniwa wazazi wake.
“ Mi nampenda sana Mwenyezi Mungu na kama unampenda Mungu huwezi ukapenda sana maugomvi na mtu, na ndio maana mi naweza nikamkosea mtu alafu nikamuomba msamaha, na mi mtu akinikosea natakiwa kumsamehe hata kama hajaniomba msamaha, yani mi nimeapology kwa sababu nilimsikia kwenye radio moja akisema mi nimeumia tu kutukaniwa wazazi wangu, na nilitukana hayo matusi, kwa hiyo nimeapology kwa yale matusi”, alisema Dudu Baya.

Bajeti ya Serikali 2016/ 2017 ni Trilioni 29.5.....Matumizi ya Kawaida ni Trilioni 17.7, Mikopo ni Trilioni 11.1. Bofya Hapa Kuona Vipaumbele Vilivyotajwa

0
0
Bajeti ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano itaizidi ya Serikali ya Awamu ya Nne kwa Sh7.1 trilioni baada ya Waziri wa Fedha kutangaza sura ya bajeti ya mwaka 2016/17 inayoonyesha kutakuwa na makusanyo na matumizi ya Sh29.5 trilioni.

Sura hiyo ya bajeti ya mwaka 2016/17 inatofautiana na iliyopita iliyokuwa ya Sh22.45 trilioni katika maeneo mengi, ikiwa ni pamoja na kiwango cha fedha kitakachotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo, ambacho ni zaidi ya mara mbili ya fedha za eneo hilo katika bajeti iliyopita.

Waziri wa Fedha, Dk Phillip Mpango alisema wakati akiwasilisha mapendekezo ya kiwango cha ukomo wa bajeti jijini Dar es Salaam jana kuwa kati ya fedha hizo, Sh18.46 trilioni, ambazo ni sawa na asilimia 62.5 ya bajeti yote, zitatokana na jumla ya mapato ya ndani yanayohusisha na halmashauri.

Kiwango hicho kimezidi Sh3.64 trilioni ya bajeti iliyopita ambayo ililenga kukusanya Sh14.82 trilioni.

“Kati ya mapato hayo, Serikali inalenga kukusanya mapato ya kodi ya jumla ya Sh15,105 bilioni, sawa na asilimia 82 ya mapato ya ndani,”alisema Dk Mpango.

Alisema makisio ya mapato ya kodi na yasiyo ya kodi yameongezeka kwa kuwa kuna viashiria vingi vinavyoonyesha kwamba Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa kushirikiana na wizara na taasisi zinazokusanya maduhuli, zina uwezo wa kukusanya kiasi hicho.

Alisema: “Kipaumbele cha kwanza cha Serikali kitakuwa ni kujizatiti katika ukusanyaji wa mapato kwa kubuni vyanzo vipya na kuendelea kudhibiti mianya mbalimbali ya ukwepaji wa kodi. Suala hili linahitaji ushirikiano wa karibu na wananchi ili tujiletee maendeleo ya haraka kwa kushiriki kulipa kodi na kuwafichua wakwepa kodi kwa kuwaona kama maadui wa maendeleo yetu.”

Kwa mujibu wa Dk Mpango, Sh17.72 trilioni zitakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida, wakati Sh11.82 trilioni, sawa na asilimia 40 ya bajeti nzima, zimetengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Katika bajeti iliyopita, matumizi ya kawaida yalitengewa Sh16.7 trilioni, sawa na asilimia 74.3 wakati shughuli za maendeleo zilipangiwa Sh5.76 sawa na asilimia 25.9.

“Asilimia 40 kwenda kwenye mipango ya maendeleo, hili ni jambo jema,” alisema Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, alipoongea na waandishi.

“Kwamba tumepunguza matumizi ya kawaida ya Serikali na kuelekeza fedha zaidi kwenye mipango ya maendeleo, nasema hili ni jambo jema kama litatekelezeka.”

Vipaumbele 
Kwa mujibu wa Dk Mpango, shughuli zitakazopewa kipaumbele kwenye mipango hiyo ya maendeleo zimegawanywa katika maeneo manne ambayo ni viwanda vya kukuza uchumi na ujenzi wa msingi wa uchumi wa viwanda, kufungamanisha maendeleo ya uchumi na rasilimali watu, mazingira wezeshi kwa uendeshaji biashara na uwekezaji na pia usimamizi wa utekelezaji wa mpango.

Dk Mpango alisema washirika wa maendeleo wanatarajiwa kuchangia Sh3.6 trilioni, ikiwa ni ongezeko la Sh1.7 trilioni kulinganisha na Sh1.88 trilioni zilizokuwa zinategemewa kwenye bajeti iliyopita.

Fedha hizo zitakuwa za misaada na mikopo nafuu kutoka nje ambayo ni pamoja na GBS, Basket Fund na miradi ya maendeleo.

Aidha Serikali inatarajia kukopa Sh5,374.3 bilioni kutoka soko la ndani kwa ajili ya kulipia hati fungani na dhamana za Serikali zinazoiva pamoja, wakati kutoka kwenye soko la nje kwa masharti ya kibiashara inatarajia kukopa Sh2.1 trilioni.

Awali Spika Job Ndugai alisema kwa mujibu wa utaratibu mapendezo hayo yalipaswa kuwasilishwa tangu Machi 11, lakini kutokana na ratiba za wabunge wengi kuwa kwenye majimbo yao, aliamua kuongeza siku.

“ Sasa ninawashauri wabunge wote kwenda kuyasoma mapendekezo hayo vyema ili mpate nafasi ya kuchangia fedha bajeti itakapowasilishwa bungeni. Pia mhudhurie kwenye vikao vya kamati zenu ili kujipanga vyema. Wale watakaokuwa hawaonekani kwenye vikao, tutawasilisha majina yao kwenye vyama vyao ili wachukuliwe hatua zinazostahili.”

Miradi ya maendeleo
Katika kuongeza wigo wa makusanyo ya kodi, Dk Mpango alisema sera za mapato kwa mwaka 2016/2017 itajielekeza kufanya tathimini ya mkupuo ya majengo ili kuongeza mapato.

Katika mpango wa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda, Dk Mpango alisema kipaumbele kitakuwa ni mradi wa magadi soda ulioko kwenye Bonde la Engaruka ambako utafiti umebaini kuna magadi ya mita za ujazo bilioni 4.68 ambazo huongezeka kila mwaka kwa mita milioni 1.9 za ujazo.

“Mradi utahusisha kiwanda cha kuzalisha tani milioni moja za magadi kwa mwaka kwa ajili ya matumizi ya viwanda, hususan madawa, vioo na sabuni,” alisema.

Mradi huo utakapokamilika utaliingizia taifa Sh 400 bilioni kwa mwaka.

Eneo jingine ni kufufua kiwanda cha General Tyre cha Arusha, ambacho kimetengewa Sh2 bilioni kwa kazi hiyo. Pia kiwanda cha viuadudu kilichopo Kibaha mkoani Pwani ambacho mradi wake utatekelezwa kwa awamu tatu, mbili za mwisho zikihusisha ujenzi wa kiwanda cha mbolea na cha virutubisho.

Pia mpango huo utahusisha uendelezaji wa viwanda vidogo mkoani Morogoro, Dar es Salaam, Mbeya na Mwanza.

Katika kufunganisha maendeleo ya uchumi na rasilimali watu, Serikali itaweka nguvu kwenye elimu na mafunzo ya ufundi, ikihusisha kuimarisha mifumo, majengo na miundombinu katika shule za awali, msingi na sekondari.

Pia itahusisha ukarabati, upanuzi na ujenzi wa vyuo vikuu, mradi wa upanuzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (Mkwawa, Duce, Udom na OUT, Ardhi, Mzumbe, Sokoine, Muhimbili, Ushirika, Chuo Kikuu cha Sayansi cha Mwalimu Nyerere na pia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.

Eneo hilo litahusisha uendelezaji ustawi wa jamii kwa kuangalia huduma za afya, maji, kazi na ajira, na uwezeshaji wananchi kwa kutoa Sh50 milioni kwa kila kijiji.

Mazingira wezeshi 
Katika kujenga mazingira wezeshi, Serikali itaongeza uwezo wa uzalishaji umeme, usambazaji umeme mijini na vijijini, ujenzi wa kiwanda cha kupokea, kuchakata na kubadilisha gesi asilia kuwa katika kimiminika kwa ajili ya kusafirisha nje, ujenzi wa miundombinu ya kusafirisha gesi asilia, ujenzi wa miundombinu ya usafiri, teknolojia ya habari na mawasiliano, miradi ya makaa ya mawe na mradi wa chuma wa Liganga.
Viewing all 104432 articles
Browse latest View live




Latest Images