Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Mbunge wa Zamani na Moshi Vijijini (CCM) Apandishwa Kizimbani

$
0
0
Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Thomas Ngawaiya amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na shtaka la kujenga hoteli kwa kutumia makandarasi wasiosajiliwa.

Ngawaiya ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Moshi Vijijini na pia Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Kilimanjaro, alipandishwa kizimbani jana na kusomewa shtaka hilo, siku moja baada ya kutiwa mbaroni na Polisi Kinondoni.

Kabla ya kumsomea shtaka, Mwendesha Mashtaka kutoka Bodi ya Usajili wa Makandarasi (ERB), Saddy Kambona alisema Ngawaiya amefikishwa mahakamani hapo kwa kukaidi amri ya Mahakama.

Pia, Wakili Kambona alimsomea mshtakiwa huyo shtaka linalomkabili, lakini Ngawaiya alikana na kuachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti.

Wakili Kambona alidai kuwa Machi 24, 2015 majira ya mchana, mshtakiwa alitenda kosa la kuagiza ujenzi wa jengo la hoteli, kwa watu ambao hawajasajiliwa na Bodi ya Usajili wa Makandarasi.

Alidai kuwa jengo hilo lipo Kiwanja Namba 32, makutano ya mitaa wa Dosi na Wazani, eneo la Magomeni Mapipa, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Aliendelea kudai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume cha kifungu namba 22 cha Sheria ya Bodi Usajili wa Makandarasi, Namba 17 ya Mwaka 1997.

Akitoa ufafanuzi nje ya Mahakama, Wakili Kambona alibainisha kuwa sheria hiyo inamtaka kila anayejenga jengo ambalo ni kwa matumizi ya umma lazima atumie makandarasi waliosajiliwa na ERB.

Baada ya kusomewa shtaka hilo, kisha kuulizwa na Hakimu Hellen Liwa iwapo ni kweli au la, Ngawaiya alianza kujitetea. Hakimu Liwa alimzuia na kumtaka ajibu shtaka kabla ya Wakili wake, Desidery Ndibalema kuingilia kati na kumuelekeza kwa kumnong’oneza cha kufanya, ndipo akakanusha shtaka.

Wakili Kambona baada ya kumsomea mshtakiwa shtaka hilo, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo unaendelea na kuomba Mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa. Hakimu Liwa aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili, 11.

Siku Mbili Tu Anadai ana Mimba yangu..Soma Kisa Kizima Hapa...

$
0
0
Wiki iliyopita ya Pasaka nilipewa taarifa na ndugu yangu sista alieolewa na muhindi, kwamba wanaomba msaada jumatatu saa6 usiku niwapeleke airport wanaelekea india, kwa sababu hawakua na gari, nikawakubalia, ilivyofika hjiyo cku nikawafuata saa 5 ucku, ili waandae mizgo yao kwanza.

Ghafla nashtuka namuona mtoto mrembo kavaa kanga ni mweupe akiwasaidia kubeba mabegi na kupakia kwenye gari, ikabidi nimuulize sista kwamba huyu dada ni nani, akanijibu ni dada wa nyumba ya pili hapo tumemuomba awe anakaa hapa kwa mda sisi tukiwa india, maana hapakua na mtu nyumba yote ile. nikamjibu OK, akili yote iliamia kwa yule mrembo.

Muda ukafika nikawapeleka airport nikakaa nao mpaka saa saba nikageuza kurudi zangu. nikasema hata lazima nirudi kulekule kwa sista nikamalizane nae yule mtoto, kwa kisingizio cha kusahau ufunguo. aisee nilikamua mafutaa mpaka mbez beach, ninakaa nao karbu umbali wa km3 toka kwao.

Nikafika nikapga hodi, mtoto akaja fasta akauliza nani, nikamjibu kaka rich hapa nimesahau funguo ya gheto kwangu, akasema wapi, nikamjibu kwenye kochi, akasema subiri nikuletee, nikamjibu poa, hapo bado hajafungua geti, na ufunguo nilikua ninao mwenyewe, akarud akisema hauoni, nikamwambia fungua nije niangalie mwenyewe, akafungua geti( KOSA) nikazama ndan nikijidai natafuta ufunguo, saa saba ya usiku hiyo, huku yeye kasimama ameshika kiuno ananiangalia ninavyohangaika kubidua masofa ya watu kama kweli vile.

Nikamwita anisaidie, akaja, nikasema hapana ngoja nivue shati maana naswet vbaya, uzalendo ukanishinda nikamfata kwa nyuma nikamkumbatia, lahaulaa akapiga kelele, nikamwambia usiogope, nikamweleza yaliyo moyoni yote mtoto akaelewa ila akawa mgumu kujirahisisha.

Akakimbilia chumban kwake na mlango kaacha wazi akisema nisimsumbue anataka kulala, nikacheka kimoyomoyo nikisema kwisha habari yako umeniachia mlango wazi pia umevaa kanga moja, nikamfata hukohuko nikaomba mzigo akawa anakataa mara ooh ndo tunaona mara ya kwanza, mara nipo danger maneno kibao, huku natomasa tu nikaona mtoto anapumua kwa kasi huku akiongea maneno yasiyoeleweka, nikasema tayariiii.

Mtoto akanipa ushirikiano vya kutosha mpaka saa 10 alfajir mwanaume naondoka kwa watu mku mtoto akinisindikiza mpaka getin, kesho yake nipo job akili yangu yote inamuwaza yeye nikasema hataa lazima niende tena, nikamwendea hewani nikaimbisha tena akakubali niende saa tano ila sio na gari maana ndugu watastukia ishu kwa sabab wapo karbu nao nawanajua muhndi kasepa na mimi saa 10.

Muda ukafika nikachapa lapa mpaka kwa sista nikajilia vyangu mpaka saa 12.nilishiba aisee. Balaa linaanzia hapa baada kupga mara mbili na mara mwisho, mtoto akaanza kusumbua mara ooh sioni sku zangu na hii itakua mimba yako, nikamwambia acha ujinga wako yaani siku mbili tu cku huzioni, hiyo itakua ya watu wengine unataka kunisingzia, mi sihusiki, nikaanza kupokea matusi ya kutosha na pia akinitishia kuwa atamwambia sista kwamba cku ile nilivyowapeleka airport nilirudi kumbaka.

Aisee nilitaka kuanguka kwenye kiti ofisini, kuhusu kama akimwambia sista huu ujinga nilioufanya kwake. Ikabidi niwe mpole tu kukubali hali, akili inanituma nikamchoropoe bila ya yeye mwenyew kujua, maana baby wangu akijua hili nimekwisha.

Nataka nimpelekee zawad ya juice iliyo na vikorombwezo vya kuitoa hiyo mimba. Mimi ni pharmacist.

Imeandikwa na Richard77

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda Apiga Marufuku Kilevi Aina ya Kiroba

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda amepiga marufuku uuzwaji wa kilevi aina ya kiroba katika mkoa huo.

Alisema uamuzi huo unatokana na vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa kushindwa kufanya kazi na kulewa wakati wa kazi.

Aidha mkuu huyo wa mkoa alisema anafanyia kazi sakata la mkazi wa Kata ya Ngarenaro anayedaiwa kujihusisha na uuzaji na uingizaji wa dawa za kulevya ambaye baada ya kukamatwa na polisi aliachiwa katika mazingira ya kutatanisha.

Ntibenda alisema hayo jana Arusha wakati akizungumza na watendaji wa serikali za mitaa 154, maofisa watendaji kata 25 pamoja na wenyeviti wa serikali za mitaa.

Alisema suala la kilevi aina ya kiroba ni kero kwa vijana kufanya kazi wakiwa wamelewa au kuwa navyo mifukoni hasa madereva wa pikipiki, daladala na wapiga debe.

Alisema kutokana na vijana kunywa kinywaji hicho nyakati za kazi, amepiga marufuku uuzwaji wa kilevi hicho, atakayekiuka agizo hilo hatua za kisheria zitachukuliwa.

“Sitaki kuona viroba vikiuzwa katika Mkoa wa Arusha na atakayekiuka nitamchukulia hatua za kisheria, lakini huyu anayeuza dawa za kulevya halafu polisi wanamwachia na wananchi hawajui kwanini anaachiwa huku akiendelea kuuza dawa, sasa nasema mwisho wake umefika, nitafuatilia kwa makini suala hili.”

Baadhi ya wenyeviti wa serikali za mitaa walihoji sababu za kutokuwa na ofisi za kufanyia kazi badala yake wanalazimika kutumia nyumba zao au kukodisha ofisi ili kufanya kazi za jamii lakini pia hawana posho za vikao.

Wenyeviti hao akiwemo Amani Mwakalinga wa mtaa wa Darajani na Hilary Mkonyi wa mtaa wa Ngarenaro, walisema awali Mkurugenzi wa Jiji, Juma Idd aliahidi kuwajengea ofisi lakini hadi sasa hakuna utekelezaji.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Mwisho Mwampamba Kortini..Alala Mahabusu Siku Mbili Kisa Matusi ya Nguoni...

$
0
0
MOROGORO: Ikiwa takriban siku 40 tangu baba yao, Dk. Ephraim Njawala Mwampamba, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo Cha Sokoine (SUA) afariki dunia, mwanaye Mwisho Ephraim Mwampamba ameburuzwa mahakamani na kaka yake, Robert Ephraim Mwampamba, Jumatatu iliyopita.

Kesi hiyo namba 197/2016 ilisikilizwa katika  Mahakama ya Mwanzo Chamwino iliyopo Mazimbu mkoani hapa, ambapo Robert alimburuza mahakamani hapo mdogo wake huyo waliyechangia baba, akimtuhumu kumtukana matusi ya nguoni huku sehemu kubwa ya matusi hayo yakiwa ya kibaguzi.

Kabla ya kufikishwa mahakamani hapo, Mwisho alitokea mahabusu alikolala kwa siku moja ambapo baada ya kesi kusikilizwa, alipata dhamana huku ikidaiwa kuwa kesi hiyo imemkalia vibaya kutokana na ushahidi unadaiwa upo.

Akisoma kesi hiyo mahakamani hapo, Hakimu Amina Chungulu alidai Mwisho anatuhumiwa kumtukana matusi ya nguoni (hayaandikiki gazetini) kupitia namba za simu (tunazihifadhi) ambayo inaaminika inamilikiwa na Mwisho Mwampamba.

Mwisho alipoulizwa na hakimu huyo alikana kutenda kosa hilo na Robert alipoulizwa kama ana ushahidi ndipo aliposema anao wa meseji hizo kwenye simu yake.

Hakimu huyo aliahirisha kesi hiyo hadi Aprili 11, mwaka huu huku Robert akitakiwa kufika mahakamani hapo na meseji hizo kama ushahidi.
Aidha, Hakimu Amina alisema dhamana iko wazi kwa mshitakiwa; mdhamini mmoja na shilingi laki 4 ambapo kaka mwingine wa Mwisho aliyezaliwa naye baba mmoja na mama mmoja, lsambe alimdhamini mdogo wake huyo.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Babu Yake Wastara Aeleza kilichosababisha Ndoa ya Wastara Kuvunjika

$
0
0
Babu yake Wastara amefunguka na kueleza kilichosababisha kuvunjia kwa ndoa ya Wastara na Mbunge wa Donge kupitia CCM Sadifa Khamis Juma.


Akizungumza na Times Fm, Babu huyo aliweka bayana kuwa Mbunge huyo mwenye cheo ndani ya umoja wa vijana CCM, alifikia hatua ya kuwatongoza wafanyakazi wa ndani ili awe nao kimapenzi.

“Wastara hataki kurudiana na Sadifa, kutokana na vitendo alivyokuwa akivifanya, imefikia wakati mpaka wale wafanyakazi wa ndani wananambia babu, babu, baba huku anatutongoza njoo uone na meseji tunazo kwenye simu,” alisema Babu.

Aliongeza, “Alafu hana adabu anafikia hatua ya kuniambia mimi nalala na mtoto wangu Wastara, aisee sijui atakuja kunieleza vipi kwa hilo”

Aidha ameweka bayana kuwa, kwa sheria za Dini ya Kiislamu ndoa hiyo siyo halali mara baada ya Mbunge huyo kutamka hadharani kwamba amemuacha Wastara.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Mtangazaji Sandu George Aka Kid Bway Atambulishwa Rasmi Radio Mpya Lake FM...Ala Shavu la Mtangazaji Mkuu wa Vipindi

$
0
0
Baada ya Watu wengi kujiuliza maswali mengi juu ya alipo Sandu George, maarufu kwa jina la Kid Bway (Pichani), ambae kwa muda mrefu amejizolea sifa kubwa katika tasnia ya utangazaji na uandaaji wa muziki, ukweli ni kwamba amejiunga na kituo kipya cha redio Jijini Mwanza kiitwacho Lake Fm, Raha Ya Rock City.

Katika kurasa za Mitandao ya Kijamii za redio hiyo, kuna post ya kumtambulisha Kid Bway iliyokuwa ikisomeka "Wananzengo tunayo Furaha Kumtambulisha Mwananzengo Kid Bway @kidboytz ambae ni Mtangazaji na Mkuu wa Vipindi 102.5 Lake Fm Mwanza. 

Raha yake ya Rock City ni Kuona Vipaji vya Wasanii wa Mwanza vinakua na Kutambulika hadi ngazi ya Kimataifa.
JE WEWE RAHA YAKO YA ROCK CITY NI NINI?

Follow ‪#‎LakeFm Instagram, Twitter & Facebook @lakefmmwanza

‪#‎RahaYaRockCity #‎RadioYaWananzengo".

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Hivi Ndivyo Irene Uwoya Alivyojifungua Kwa Upasuaji Bila Ganzi

$
0
0
Msanii wa filamu Irene Uwoya amesema hakupenda kabisa kujifungua kwa upasuaji lakini ilimbidi afanye hivyo ili kuokoa maisha yake pamoja naya mwanaye.

Muigizaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja aitwae Krish, amekiambia kipindi cha Uhondo cha EFM kuwa wakati anaelekea hospitali kucheki afya yake na maendeleo ya mimba yake, hakujua kama ndio siku ambayo angejifungua kwa kuwa hakuwa na dalili yoyote.

“Kwanza nilikuwa sipo Tanzania, nilikuwa na siku moja toka nirudi, so kesho yake nikaenda hospitali kuangalia mimba inaendeleaje. Kiukweli namshukuru Mungu sikuwahi kusikia maumivu ya uchungu, nikaenda pale Regency, kwa hiyo dokta kuniangalia tu akasema mtoto anachungulia wewe unatembeaje?, nikamwambia mimi sijui na hapo nimevaa kiatu kirefu kweli, akaniambia toa viatu mtoto anachungulia,” alisimulia Irene.

“Wakanifanyia vipimo, lakini baadaye wakaniambia huwezi kujifungua kawaida, njia ndogo kwa hiyo inabidi tukufanyie upasuaji. Kiukweli nilitamani kujifungua kawaida. Lakini nikikumbuka ile siku nakumbuka kile chumba kilivyotisha, kitu ambacho nakumbuka sana ni ganzi, walikuwa kila wakipiga inakataa, ikabidi nifanyiwe upasuaji hivyo hivyo, yaani nilipata maumivu makali mpaka nikawa naweweseka nahisi niko Paris kwa sababu kila walichokuwa wanakifanya nilikuwa nakisikia,” aliongeza Irene.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Wameanza Kubainika Mmoja Baada ya Mwingine Hawa Hapa Viongozi wa Juu wa TFF Waliokuwa Wakiomba Mil 25 ili Kupanga Matokeo..Audio

$
0
0
Mambo mapya yamezidi kuibuka kuhusu sakata la upangaji matokeo kwenye ligi daraja la kwanza ikiwa ni siku chache baada ya TFF kutoa hukumu kwa baadhi ya viongozi, wachezaji na waamuzi waliopatikana na hatia mbele ya kamati ya nidhamu ya Shirikisho hilo linalosimamia mpira wa miguu Tanzania.

Kubwa ambalo ndiyo habari ya ‘mujini’ kwa sasa ni kuvuja kwa sauti ambayo wanasikika baadhi ya maafisa wa ngazi za juu wa TFF pamoja na viongozi wa timu ya Geita Gold Sports wakipanga mikakati ya kupanga matokeo ambayo inahusisha rushwa ndani yake.

Sauti ya kigogo mmoja wa TFF inasikika akiomba rushwa ya shilingi milioni 25 kutoka kwa viongozi wa Geita ili aweze kuhakikisha anawasaidia katika baadhi ya matatizo ambayo miongoni mwayo ni pamoja na vibali vya wachezaji.

Sauti hiyo imeifikia www.shaffihdauda.co.tz na kutokana na kutaka kuwajulisha wadau wa mchezo huu pendwa, mtandao huu unakuletea moja kwa moja sauti hiyo ili upate kuwasikia vigogo hao wa TFF wenye dhamana kubwa ya soka la Bongo wanavyolihujumu na kulisambaratisha soka kwa kutumia vibaya mamlaka yao.

Jana (April 5) Kaimu Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Martin Chacha alitangaza kujiuzulu nafasi yake katika utumishi wa TFF mara baada ya kuvuja kwa sauti ya mjadala wa kupanga matokeo pamoja na kuomba rushwa.

Katika barua yake aliyomwandikia Katibu Mkuu wa TFF, Chacha alieleza kuwa amepata majukumu mapya ya kikazi ambayo pamoja na majukumu ya kifamilia yatamfanya akose muda wa kutumika vema katika nafasi yake katika Shirikisho.

Martin alijiunga na TFF Julai 2014 akiwa Afisa wa Mashindano na baadaye kuteuliwa kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Mashindano, kufuatia aliyekuwa anashikiria nafasi hiyo Boniface Wambura kuteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB).

Hili ndiyo soka la Bongo sinema na mazingaombwe bado yanaendelea TFF, usiache kufatilia www.shaffihdauda.co.tz kujua mengi zaidi juu ya sakata hili, utaendelea kupata taarifa kadiri zinavyotufikia kutoka katika vyanzo mbalimbali.

Hii hapa ndiyo sauti iliyonaswa kwenye mjadala huo wa upangaji matokeo uliowahusisha maafisa wa ngazi za juu wa TFF pamoja na viongozi wa timu ya Geita Gold Sports ya mkoani Geita.   DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Kinachoendelea Afrika ya Kusini na Kiwe Funzo Kwa Nchi za Bara la Africa...Rais Afikishwa Mahakamani....

$
0
0
Kinachoendelea Africa ya Kusini na kiwe funzo kwa nchi za Bara la Africa,Huenda karata ya upinzani ya Nchi hiyo isifanikiwe kwasasa,ila Ilifanikiwa hapo awali baada ya kumpeleka Rais Mahakamani na Upinzani kuibuka kidedea.

Taifa langu Tanzanzia tunahitaji katiba mpya itakayoruhusu Rais kupandishwa kizimbani kwa kutumia mamlaka vibaya (Kufuja mali za umma) mambo ya kuwafanya marais kuwa ni watu wasiyogusika ni mambo ya kikoloni sana.
Tuitafuteni haki ya kupata katiba mpya itakayo wawajibisha Marais ama wakiwa madarakani ama nje ya Madaraka.

Vile vile tuwe na Katiba itakayomfanya Rais kuwepo bungeni na siyo utaratibu wa Sasa Wa Rais kulihutubia Bunge kisha mambo mengine yote anamuachia Waziri mkuu, Hapa hatuwafanyii Wananchi mazuri,Kumbuka Waziri huyu alichaguliwa na jimbo moja sasa anakuja kujibu Maswali ya nchi nzima....Tubadili muelekeo wa kisiasa kama tunataka kuwaletea Watanzania maendeleo na siyo maigizo ya kisiasa.

Kwasasa ni lazima waliyopo madarakani mkubali kupoteza vitu fulani na kuongeza vitu fulani vyenye manufaa kwa Wananchi....
TUITAFUTENI KATIBA MPYA

Written by Henry Kilewo

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Taswira Mbalimbali Za Rais Magufuli Na Rais Kagame Wakiwa Nchini Rwanda

$
0
0

Taswira Mbalimbali Za Rais Magufuli Na Rais Kagame Wakiwa Nchini Rwanda

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Miaka Minne ya Kifo cha Steven Charles Kanumba, Hii Ndiyo Hali Halisi

$
0
0
Hii ndiyo hali halisi! Ikiwa leo ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha aliyekuwa staa wa filamu Bongo, Steven Charles Kanumba ambapo ametimiza miaka minne kaburini, mambo mbalimbali yametokea tangu alipofariki dunia huku magari na kampuni aliyokuwa akimiliki vikiwa vimepukutika kama majani.

Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 maeneo ya Vatcan-Sinza jijini Dar nyumbani kwake alikokuwa akiishi ambapo aliyekuwa mpenzi wake kwa siri, staa wa filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ alishikiliwa na polisi na kusweka katika Gereza la Segerea kwa mwaka mmoja, akidaiwa kuhusika na kifo chake kwani ndiye aliyekuwa naye chumbani usiku huo.

TASNIA YA FILAMU
Tangu Kanumba aondoke, tasnia ya filamu imedorora na wasanii wengi wamekuwa wakikiri kwamba ni kutokana na kifo cha staa huyo kwani ndiye aliyekuwa chachu na changamoto kubwa ambayo ilikuwa ikisababisha wengine kufanya kazi kwa bidii ili wamfikie au pengine wapite kiwango alichokuwanacho.

TUZO ALIZO-NAZO
Kwa mujibu wa mama Kanumba, Flora Mtegoa hadi sasa marehemu anashikilia tuzo zaidi ya saba alizopewa na wadau wa sanaa hapa nchini kwa kutambua mchango wake tangu alipofariki dunia.
Kutokana na idadi hiyo ya tuzo, hadi sasa hakuna msanii yeyote wa filamu nchini ambaye ameweza kufikia rekodi hiyo.

WASIKIE HAWA
“Kiukweli sanaa ya filamu imepoa sana na imekosa mwelekeo tangu alipofariki Kanumba, unajua alikuwa analeta changamoto ya kila mtu kufikiria atafanyaje ili amfunike Kanumba lakini sasa hivi watu wamebweteka, hakuna anayewaumiza kichwa tena, jambo ambalo limesababisha tasnia ya filamu kupoa na kukosa msisimko kama zamani,” anasema msanii wa filamu, Tiko Hassan.
Naye msanii mkongwe kwenye tasnia ya filamu, Hidaya Njaidi alisema:
“Kanumba alipofariki dunia tasnia ilikufa kabisa, sasa hivi ndiyo inaanza kufufuka kidogo baada ya serikali kuitambua na kuipa sapoti lakini vinginevyo hakuna ambaye ameonekana kuliziba pengo la Kanumba.”
Kanumba na Vincent Kigosi ‘Ray’ walikuwa ni washindani kwa kila kitu, iwe ni magari, blogu na hata katika filamu lakini Kanumba alipofariki dunia, hata Ray mwenyewe alipoa na manjonjo yake hayaonekani kama zamani.

MAGARI NA KAMPUNI
Miaka minne baada ya kifo cha Kanumba, magari yake matatu, Toyota Hiace, Toyota GX 110 na Toyota Lexus ambalo lilifanana na la Ray alilolinunua Sh. milioni 78. Toyota Hiace ambalo lilikuwa ni maalum kwa ajili ya kufanyia kazi za filamu ndani ya kampuni yake ya Kanumba The Great na Toyota Hiace yote hayaonekani. Yanadaiwa kuuzwa na sasa mama Kanumba anatumia usafiri wa daladala.

.
Isitoshe pia Kanumba alikuwa na ofisi maeneo ya Sinza-Mori, Dar lakini kwa sasa haipo tena na kwa mujibu wa mama yake, vifaa vyote wamehamishia nyumbani kutokana na kushindwa kulipia kodi ya pango.

MAMA KANUMBA ANASEMAJE?
Akizungumza kwa uchungu, mama Kanumba alisema kuwa kuhusu magari, hayapo na anaomba mwanaye aachwe apumzike salama huko alipo kwani anapoulizwa maswali mengi ndipo anazidishiwa uchungu zaidi.

Kuhusu kampuni alisema vifaa vyote vipo nyumbani (Kimara-Temboni) na ikitokea kama kuna kazi ya filamu basi wahusika waliokuwa wanafanya kazi na Kanumba huwa wanakwenda kufanyia hapohapo nyumbani.

VIPI KUHUSU BLOGU YAKE?
Mama huyo alisema kwamba hafahamu chochote kuhusiana na mambo ya mtandao hivyo hajui chochote kuhusu Blogu ya Kanumba the Great.

MDOGO WAKE KANUMBA YUKO WAPI?
Mdogo wa Kanumba anayejulikanakwa jina la Seth Bosco anasema baada ya Kanumba kufariki dunia mama yake ndiye aliyechukua nafasi ya mkurugenzi mkuu wa kampuni ya mwanaye hivyo hajui chochote kinachoendelea na ikitokea kuna kazi ya filamu huwa anaenda kufanya lakini kwa sasa anajishughulisha na mambo yake binafsi ya sanaa.

Kwa upande wa blogu ya Kanumba www.kanumbathegreat.blogspot.com ambayo picha ya mwisho kuwekwa ilikuwa Aprili 6, 2012 anasema kwamba walishindwa kuiendeleza kutokana na kuwa hawana namba ya siri ‘password’ yake kwani alikuwa nayo mwenyewe Kanumba na hakuna anayeifahamu hadi sasa.

MIRATHI VIPI?
Mama Kanumba anasema suala la mirathi halipo tena na bado yupo anasikilizia kama anavyosikilizia kesi ya Lulu kuanza kutajwa mahakamani ila kama Baba Kanumba, Charles Kanumba ataibuka na kuzungumzia tena mali za mwanaye, ataenda kufungua mirathi.

NINI HATMA YA LULU?
Baada ya kukaa gerezani kwa mwaka mmoja, Lulu aliachiwa huru kwa dhamana baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kusikiliza kesi hiyo na kukutwa na kesi ya kuua bila kukusudia, mpaka sasa haijaanza kusikilizwa.

Katika kumbukumbu ya kifo cha Kanumba leo, ibada ya kumuombea itafanyika Kanisa la KKKT, Temboni jijini Dar na baada ya hapo mama yake pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wataelekea Makaburi ya Kinondoni kulifanyia usafi kaburi lake.

Mama Kanumba anasema kwa mwaka huu utaratibu utakuwa ni huo tu lakini kwa mwaka kesho atakapotimiza miaka mitano atamfanyia kitu maalum, hakukiweka wazi.

DOWNLOAD APP YA UDAKU SPECIAL BLOG HAPA

Imeandikwa na Global Publishers

Taarifa Kwa Umma: Kufutwa Kwa Safari za Ndege za Fastjet April 02, 2016

$
0
0

TAARIFA KWA UMMA;KUFUTWA KWA SAFARI ZA NDEGE APRILI 2, 2016

Tunaomba radhi sana kwa taarifa kwamba idadi kadhaa ya abiria wetu walishindwa kufika kwenye maeneo waliyokusudia jioni ya Aprili 2, 2016.

Hii ilitokana na kushindwa kufanya kazi kwa mfumo wa taa kwenye njia ya kurukia kwenye uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro na hivyo kukosekana kwa usalama ambao ungewawezesha marubani wetu kutua.

Huu ni mfululizo wa matukio ambayo yalisababisha kufutwa kwa ndege mbili miongoni mwa ndege zetu kutua usiku ule:

• Ndege Na. FN157 iliondoka kwenye uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere saa 3.18 usiku ikitarajiwa kutua kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro kabla ya muda unaotakiwa saa 4.40 usiku. Wakati ndegte ikikaribia Uwanja wa Kilimanjaro marubani wetu walijulishwa na mnara wa kuongozea ndege kwamba taa zilizopo kwenye njia ya kurukia ndege zilikuwa hazifanyi kazi lakini hali ingetengemaa muda usiokuwa mrefu. Ndege ilizunguka uwanja wa Kilimanjaro ikisubiri ukarabati wa taa hizo kwa takribani dakika 30 kabla ya kurudi Dar es salaam kwa kuwa taa hizo zilikuwa bado hazifanyi kazi.

• Ndege iliwasili tena Dar es Salaam saa 5.20 usiku na abiria walibaki kwenye ukumbi wa kusubiria ndege wakati ndege ikijazwa mafuta tena na marubani wakiandaa mpango mpya wa kusafiri tayari kurudi Kilimanjaro mapema kadri iwezekanavyo pindi ukarabati wa taa kwenye njia ya kurukia ndege ukikamilika. Kwa bahati mbaya taa hizo zilikuwa hazifanyi kazi hadi kufikia saa saa 7.00 usiku wa kuamkia Aprili 3, 2016, ambapo muda sahihi na salama kwa marubani wa ndege ukiwa umemalizika kwa kuwa walishakuwa kazini kuanzia saa 12.30 jioni.

• Hii inamaanisha kwamba hatukuwa na mbadala wa kufuta safari, na hivyo ndege Na. FN158 ambayo ilikuwa irudi kutoka Kilimanjaro kuja Dar es Salaam.

• Abiria wetu waliopata usumbufu walipewa nafasi kwenye ndege iliyokuwa inafuatia na ilisafiri kutoka uwanja wa pili kurudi kule walikotoka. Baadhi ya abira walichukua mbadala huu lakini wengie waliamua kubaki katika uwanja wa ndege kusubiri ndege iliyofuata.

• Abiria wote walioomba kupatiwa usafiri kwenye ndege iliyofuata walisafiri nasi kwa kuelekea maeneo waliyokuwa wanakwenda Aprili 3, 2016.

• Tunaomba radhi kwa abiria wetu waliokuwa kwenye safari ile kwa usumbufu walioupata huku tukiwahakikishia kuwa tunaweka kipaumbele kikubwa kwenye usalama wa abiria wetu na marubani.

John Corse,
Meneja Mkuu, fastjet Tanzania
#FASTJETPRESSRELEASE @fastjetofficial

Rais Magufuli ashiriki katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 22 ya mauaji wa Kimbari nchini Rwanda

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakishuhudia  wenyeji wao Rais Paul Kagame na Mama Janeth Kagame pamoja na binti yao wakiweka shada la maua katika viwanja vya Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbali mjijini Kigali, Rwanda, leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa na wenyeji wao Rais Paul Kagame na Mama Janeth Kagame wakiwasili katika viwanja vya Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbali mjini Kigali, Rwanda, leo katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 22 ya mauaji hayo yaliyotokea mwaka 1994 ambapo watu takribani milioni 1,000,000 waliuawa.

Taarifa Za Uzushi Kuhusu Walimu Kushonewa Sare Inayosambazwa Katika Mitandao Ya Kijamii

$
0
0
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI
TAARIFA KWA UMMA

YAH: TAARIFA ZA UZUSHI KUHUSU WALIMU KUSHONEWA SARE INAYOSAMBAZWA KATIKA MITANDAO YA KIJAMII

Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi inakanusha taarifa inayosambazwa katika mitandao ya kijamii yenye kichwa cha habari “NDALICHAKO NA WALIMU TZ”.

Taarifa hiyo inadai kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa walimu wanaandaliwa sare watakazo vaa wakati wa kazi.

Tunapenda kuufahamisha umma kuwa Taarifa hizi si za kweli. Aidha, Wizara inawataka watu wanaoeneza taarifa za kizushi za aina hii waache kufanya hivyo ili kuepusha usumbufu unaojitokeza.

Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa watakaobainika kuanzisha na kueneza uzushi huu.

IMETOLEWA NA

KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
07/04/2016

Kikwete Akiri Kumkabidhi Rais John Pombe Magufuli Uenyekiti CCM

$
0
0
Katika mahojiano aliyoyafanya na BBC , Rais mstaafu Kikwete amekiri kuwa hivi karibuni atakabidhi Uenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kwa Rais Maguli na yeye kubaki kama mzee mstaafu lakini maarufu.

Hata hivyo Kiwete amekiri pia kuwa ataendelea kushughulika na maswala ya kimataifa kama sehemu ya kazi yake baada ya kustaafu.

Kile kitendawili cha Chama sasa kimeteguka.



Hiki Ndicho Alichokiandika Lulu Michael Miaka 4 ya Kifo cha Kanumba

$
0
0
TAREHE NA MWEZI KAMA HUU NDIPO ULITUACHA KIPENZI CHETU, MFALME WA BONGO MOVIE TANZANIA.
INATIA SANA SIMANZI KUENDELEZA TASNIA BILA WEWE, MTU WA KWANZA KUUMIA NI MIMI NA MASHABIKI WAKO...
MOLA AKUPUMZISHE MAHALA PEMA PEPONI, AMEN!
Tafadhali Tumuombee rehma za Mwenyezi Mungu ziwe kwake. ...

Padri Amtolea Tamko Mrembo Jokate...Ni Kuhusu Kuwakera Waumini Kwa Kupiga Picha za Nusu Utupu

$
0
0
Baadhi ya watu waliodai kuwa wao ni waumini wa Kanisa la Mtakatifu Petro, Oysterbay jijini Dar es Salaam ambako anaabudu Mbongo Fleva na Miss Tanzania No. 2, 2006, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ wamesema nyota huyo hatakiwi kushiriki ibada kwa vile uhusiano wake na Mbongo Fleva, Ali Kiba upo wazi sana, sasa kanisa hilo limetoa tamko, tambaa na Amani.

Akizungumza na gazeti hili juzi kanisani hapo, padri aliyejitambulisha kwa jina moja la Edward ‘Faza Edward’ alisema wao kama kanisa wanamtambua Jokate kama muumini wao wa miaka mingi na kwamba mambo mengine hayawahusu.

“Jokate namtambua kama muumini wetu hapa ana anashiriki vizuri tu. Sisi hatuna tatizo naye. Kwanza sisi  mtu yeyote anaruhusiwa kuja kusali hapa, hata kama ni Mwislam ilimradi tu afuate taratibu zetu.

“Kwa hiyo Jokate tunaye hapa kanisani na anaendelea vizuri tu. Umemuulizia na paroko, yeye muda huu ana wageni,” alisema Faza Edward.


Awali waumini hao walisema kuwa, kitendo cha Jokate kuonekana kwenye vyombo mbalimbali vya habari akiwa na Kiba huku si mwanandoa wake jambo ambalo wao wanaliona si sawasawa kwa vile mrembo huyo hushiriki pia kuimba kwaya ya kanisa hilo.
Mwaka jana, gazeti dada na hili, Ijumaa liliandika habari yenye kichwa kisemacho; Waumini: Jokate anatutia aibu.

Katika habari hiyo, Jokate alidaiwa kuwakera waumini wenzake kufuatia kupiga picha za nusu utupu na kuzisambaza kwenye mitandao ya kijamii huku midume ikijirushia na kujifaidia kwa macho.
Pia, alilalamikiwa kwa tabia yake ya kupanda jukwani kwenye kumbi za muziki na kunengua huku yeye akiwa ni mwanakwaya wa kanisa hiyo.

Akijitetea kuhusu madai ya waumini wenzake katika habari hiyo, Jokate alisema kuwa, kanisa hilo halimzuii kuvaa nguo fupi wala kukata mauno jukwaani kama mwanamuziki kwani kazi ni kazi.
Alisema kanisani anakwenda kama kawaida na kwaya anaimba kama ‘kawa’.
Katika habari hii mpya, Jokaye alipoulizwa alisema: “Mimi sitaki mnifuatilie mambo yangu ya imani, sitaki kabisa, mnanikwaza.”

Waandishi Hamida Hassan na Imelda Mtema.
Global Publishers

Upinzani Waikubali Bajeti Pendelezo ya Magufuli, Waipongeza na Kusema Haya

$
0
0
BAADHI ya wabunge wamepongeza mapendekezo ya ukomo wa bajeti ya mwaka 2016/17, yaliyowasilishwa na Serikali kutokana na bajeti hiyo kwa mara ya kwanza, kupunguza kwa kiasi kikubwa utegemezi wa fedha za nje, lakini pia kuelekeza kiasi kikubwa cha fedha katika matumizi ya maendeleo.

Akizungumza baada ya Waziri wa Fedha na Mipango kuwasilisha mapendekezo ya ukomo wa bajeti hiyo pamoja na mpango wa maendeleo kwa mwaka huo, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), alisema mambo mema yamefanywa.

Alisema mambo matatu makubwa yakitekelezwa, itakuwa imetibu kiu ya watanzania ya muda mrefu, moja ni kupeleka fedha nyingi kwa maendeleo na kubana matumizi ya kawaida na pili imepunguza utegemezi wa wafadhili, kufadhili bajeti ya nchi. Alisema hilo ni jambo jema na kusisitiza kuwa msingi iwekwe ya kuimarisha.

“Ukomo wa bajeti ni kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, hili nalo katika serikali ya awamu ya tano wameliona na kweli tuwaunge mkono, sio kila kitu tuone kibaya, cha msingi tuwape nafasi tuone watamalizaje huko mbele kwenye utekelezaji”, aliongeza Mbowe.

Kwa upande wa Mbunge wa Kigoma Mjini, Kabwe Zitto (ACT-Wazalendo) alisema serikali imethubutu kupanga kiwango kikubwa cha bajeti na ni vyema kuwatia moyo na kuacha tabia ya kukosoa jambo kwa hatua ya awali.

Alisema kitendo cha kuweka asilimia 40 kwenye bajeti ya maendeleo ni hatua kubwa na kwamba mpango wa serikali kurasimisha sekta isiyo rasmi, wakiwemo wafanyabiashara ndogo na wengine ambao hawakuwa wakilipa kodi, utasaidia kuongeza mapato ya kodi.
“Ni hatua kubwa sana, cha msingi ni kuhakikisha bajeti ya maendeleo ambayo imetengewa asilimia 40 ya mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2016/17 inatekelezwa, ni vyema tuwatie moyo”, alisema Zitto .

Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), alisema mapendekezo hayo yametoa mwanga na unafuu kwa watanzania kwa kuwa kupitia Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17, ambao umegusa maeneo mengi nyeti yanayowagusa wananchi.

“Ni bajeti nzuri, kwa kweli imezingatia zaidi matakwa ya wananchi hasa katika eneo la matumizi ya maendeleo. Si kwamba bajeti za nyuma zilikuwa mbaya. La hasha. Lakini kutokana na utegemezi mkubwa wa fedha za nje, zilionekana kuwa hazitekelezeki,” alisema Ngeleja.

Kwa upande wa Mbunge wa Mbinga Mjini, Sixtus Mapunda (CCM) alisema mapendekezo hayo, yametoa matumaini na mwanga mpya kwa watanzania, kwani kwa mara ya kwanza Serikali inaonyesha nia ya dhati ya kuachana na utegemezi.

“Bajeti imeweka wazi utegemezi wa wahisani uko asilimia 12 tu ya bajeti yote, miradi mingi ilikuwa haitekelezeki au kumaliza kutokana na wahisani wengi kutotimiza ahadi zao, lakini sasa Serikali imeamua kujikita katika ukusanyaji wa mapato yake na kutegemea zaidi fedha za ndani,” alisisitiza Mapunda.

Mbunge huyo alipongeza hatua za Serikali ya awamu ya tano za kuhakikisha matumizi yote ya fedha za Serikali yanafuatiliwa, ikiwa ni pamoja na kuweka mfumo wa kuhakiki matumizi na mapato yake kila mwezi ili kuona kama yanawiana.

Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) alisema kwa sasa yapo matumaini ya miradi ya maendeleo kukamilika kutokana na bajeti nzima kujikita katika fedha za ndani, kwani kiasi kinachotarajiwa kutoka kwa wahisani, hata kisipotolewa, upo uwezekano wa fedha hizo kupatikana kupitia mapato ya ndani.

“Hata hao wahisani mara nyingi wamekuwa wakitoa ahadi, lakini utekelezaji wao unaambatana na masharti mengine ambayo hayana hata msingi. Na upatikanaji wa hela yao umekuwa mgumu. Sio hata hizi Shilingi trilioni tatu hata wasipoleta tuna uwezo wa kuzikusanya kutoka humu ndani,” alisema.

Aliongeza kuwa, “Mimi naunga mkono jitihada za serikali ambazo zimefanya na kutuondoa katika utegemezi wa misaada sana. Mimi naamini kuwa nchi yetu ni tajiri ina vitu vingi sana, ambavyo vinaweza kutufikisha mahala tukajitegemea”.

Kwa upande wake, mbunge wa Vunjo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), alisema mapendekezo ya bajeti hiyo, hayana uhalisia na huenda yasitekelezeke, kwa kuwa yameegemea zaidi katika mafanikio ya muda mfupi yaliyopatikana katika ukusanyaji wa kodi na faini za wakwepa kodi.

Kuhusu ushauri wake wa namna ya kukabiliana na changamoto zinazoweza kukwamisha utekelezaji wa mapendekezo ya bajeti hiyo, mbunge huyo alisema “waulizeni CCM, hiyo si kazi yangu”.

Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya (CUF) alisema baada ya kumaliza habari ya faini za kodi na wale waliokwepa kulipa kodi, makusanyo yatashuka kwa kiasi kikubwa. Alishauri kuibuliwa kwa maeneo mengi, yaliyotekelezwa yanayoweza kulipishwa kodi, ikiwemo eneo la bahari ambalo kwa mujibu wake kwa sasa limegeuzwa kama shamba la bibi.

Mbunge wa Sumbawanga Mjini, Aeshi Hilaly (CCM), alisema mpango na mapendekezo ya bajeti ni mzuri, kwa kuwa vitu vingi vimelenga mahitaji ya wananchi na sasa kiu ni kuona utekelezaji wake.

TANZIA: Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Christina Lissu Afariki Dunia Jijini Dar

$
0
0
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum toka Singida, Christina Mughwai Lissu(CHADEMA) amefariki dunia kwa ugonjwa wa kansa.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa cancer tangu mwaka jana.

Tundu Lissu Ameandika Hivi:



Waheshimiwa nawasalimu kutoka Kibondo.

Nina habari zisizokuwa njema. Dada yangu na aliyekuwa Mbunge wetu wa Viti Maalu m Mh. Christina Lissu Mughwai amefariki dunia muda mfupi uliopita katika hospitali ya Aga Khan Dar.

Marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa cancer tangu mwaka jana.

Kwa sasa niko nje ya Dar na ndio kwanza taarifa hizi zimenifikia, sina taarifa zaidi juu ya mipango ya mazishi, etc. Tutawataarifu baada ya familia kuwa tumeshauriana.

Tundu Lissu.

Muda Mwingine Wanaume Kuchapiwa Wake zetu Tunatakaga Wenyewe

$
0
0
Hili suala nimelifikiria kwa kipindi kirefu sana., naona mifano mingi kupitia kwa marafiki zangu na hata ndugu zangu na watu wangu wa karibu. Unakuta mwanaume upo kwenye mahusiano ya kawaida na msichana bado hamjafunga ndoa alafu migogoro na kuachana mara kwa mara, tena unakuta wewe ndo unaachwa na huyo mwanamke alafu unambembeleza mnarudiana. Mwanamke haonyeshi upendo wowote kwako lakini wewe unaendelea kumpenda na kumjali sana. Hayo yote haujifunzi unaamua kumng'ang'ania na mwisho wa siku mnafunga ndoa.

Hivi mwanamke kama huyo akiwa anakusaliti katika ndoa utamlaumu nani.?

Kuna rafiki yangu wa karibu aliwahi kuoa mwanamke wa aina hiyo, ndoa yao ilidumu kwa miaka 5 tu na mimi nilikuwa best man wake, maana mwisho wa siku ikaja kugundulika hata watoto wawili ambao walikuwa wameshazaa hawakuwa wa kwake.

Wanaume tujifunze jamani tunapochagua mwanamke wa kuishi naye kwa maisha yote, tusiziendekeze akili za nyege wakati wa kuchagua wenzi wa maisha.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images