Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Katibu TFF Akana Tuhuma za Upangaji Matokeo Ligi Daraja la Kwanza Baada ya Sauti Kuvuja...

$
0
0
Siku chache tangu kamati ya nidhamu ya TFF iwaadhibu baadhi ya viongozi wa vilabu vya ligi daraja la kwanza na kuvishusha vilabu hivyo kutokana na kupatikana na hatia ya kupanga matokeo ya michezo ya kundi C Katibu wa TFF aibuka baada ya kuhusishwa.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine amekanusha kuhusika na njama za upangaji matokeo ya michezo ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.

Licha ya kukanusha Mwesigwa ametishia kulifikisha mahakamani gazeti moja la kila siku nchini lililochapisha habari za kumuhusisha na mpango huo mchafu.

"Nimeshitushwa na kusikitishwa sana na habari hiyo juu yangu ambayo ni ya kutunga, yenye nia mbaya isiyokuwa ukweli wowote, kwani sijawahi kukaa na watu wowote kupanga njama yoyote iliyo kinyume na maadili ya mchezo wa mpira wa miguu,"amesema Mwesigwa.

Gazeti moja la leo nchini, limechapisha habari katika ukurasa wake wa 24 chini ya kichwa cha habari "Vigogo TFF wajikaanga" likisema katika ibara ya 7 kuwa kwenye mazungumzo yaliyochukua zaidi ya dakika 10 yalimhusisha pia Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa.

Yamkini hali bado si shwari TFF, baada ya kuvuja kwa sauti za maofisa wa shirikisho hilo wakiomba rushwa ya shilingi milioni kutoka kwa viongozi wa timu moja ya Daraja la Kwanza ili waisaidie kupanda Ligi Kuu.

Na jana TFF imetoa tamko la kusikitishwa na taarifa hizo na kuahidi kuwachukuliwa hatua kali maofisa wake waliohusika, ingawa imesema taarifa hizo hazihusiani na kesi ya kupanga matokeo iliyoamuliwa Aprili 3.

TFF imesema kwanza inachunguza kubaini uhalisia (authenticity) wa taarifa hizo na itachukua hatua kali sana kwa watumishi wa shirikisho na viongozi wa timu husika watakaobainika kushiriki vitendo vilivyo kinyume na maadili ya mpira wa miguu.

Tayari Kaimu Mkurugenzi wa Mashindano TFF, Martin Chacha, mmoja wa watuhumiwa ameacha kazi tangu juzi. Katika barua yake aliyomwandikia Katibu Mkuu wa TFF, Chacha amesema amepata majukumu mapya ya kikazi ambayo pamoja na majukumu ya kifamilia yatamfanya akose muda wa kutumika vema katika nafasi yake katika Shirikisho.

Chacha alijiunga na TFF Julai 2014 kama Ofisa Mashindano na baadaye kuteuliwa kukaimu nafasi ya Mkurugenzi wa Mashindano, kufuatia aliyekuwa anashikiria nafasi hiyo Boniface Wambura kuteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB).

Binti Mwenye Ulemavu Afungiwa Ndani Kwa Miaka Kumi na Sita Arumeru

$
0
0
Vitendo vya kuwafungia ndani watoto wenye ulemavu limeendelea kushamiri kwenye maeneo mengi nchini tukio la sasa likitokea katika kijiji cha njani wilayani Arumeru ambapo mtoto wa kike mweye ulemavu wa viungo amebainika kufungiwa ndani kwa kipindi cha umri wake wote wa  miaka kumi na sita.

Mtoto huyo Wine Ruth anayelelewa na bibi yake baada ya kutelekezwa na mama yake mzazi mara baada tu ya kugundua kuwa ana ulemavu amegundulika wakati wa zoezi la kuwaorodhesha watoto wenye ulemavu wilayani Arumeru ambapo bibi yake Veraelly Ndetaulo anakiri kumfungia kwa ajili ya usalama wake anapokwenda kuwatafutia rizi wajukuu zake.

Akizungumzia tukio hilo Mbunge wa Viti Maalum Walemavu Dk.Elly Macha aliyeongoza zoezi la kumtoa ndani mtoto huyo anasema imefika wakati sasa jamii ikatambua kuwa malezi ya watoto wa kundi hilo ni la kushirikishana hasa ikizingatiwa kuwa wengi wamekua wakitokea kwenye familia zenye kipato duni.

Maisha ya Bibi Ndetaulo anayemlea mtoto huyo mwenye ulemavu,pamoja na mdogo wake ni magumu kulingana na umri wake,wadau walioshiriki kwenye zoezi la kumtoa mtoto huyo likiwemo Jeshi la Polisi wilayani Arumeru wanashauri kuwa ipo haja kwa Serikali ya kijiji kuangalia uwezekano wa kumsaidia.

Picha ya Siku..Pale Stori za Udaku Zinapokuweka Bize Kwenye App ya Udaku Blog

$
0
0
Mama ameona Isiwe tabu, mtoto anasumbua na Udaku umekolea kwenye App ya Udaku Special ikabidi amfungia mwanawe kama hivyo....

Mastaa Bongo Waanza Kuchunguzwa Msako wa Wauza Unga...Zari wa Diamond Naye Pia Achunguzwa

$
0
0
Imefahamika kuwa ule msako wa Wauza unga sasa umenoga hadi kufikia kuchunguzwa kwa mastaa mbali mbali wa bongo hasa wale wanaosafiri mara kwa mara nchi za nje...Habari zinasema uchunguzi huo sasa unamgusa mpaka mpenzi wa Diamond Platnumz ajulikanaye kama Zari Hassan ambae Safari za Bongo kwenda South Afrika na kurudi hazimuishi....

Siri ya Rais Magufuli Kuchagua Kutembelea Nchi ya Rwanda na Kusafiri Kwa Kutumia Usafiri wa Gari Hii Hapa

$
0
0
Tusihangaike Na Kwanini Magufuli Kachagua Rwanda Kama Nchi Ya Kwanza Kuzuru...
Tujiulize, Magufuli aliyekwenda kwa Kagame kwa barabara akirudi atakuwaje?
Ndugu zangu,

Wahenga walisema, tembea ujionee, ina maana tembea ukijifunza. John Magufuli anajenga ubia na Paul Kagame. Urafiki wa John na Paul, na atakayojifunza John kwa rafiki yake Paul, yumkini yataongeza maradufu kasi ya John Magufuli kutumbua majipu.

Kagame pamoja na kuitwa dikteta, lakini ameibadilisha Rwanda na inaelekea kuwa nchi ya kisasa zaidi. Siri kubwa ya mafanikio ya Rwanda ni kwa Kagame kuwafanya Wanyarwanda kuheshimu sheria, kanuni na taratibu za nchi. Kujenga misingi ya uadilifu na kuisimamia. Na wenye kukiuka kuadhibiwa. Ni kwa viongozi na raia.

John Magufuli ameanza kuijenga misingi hiyo hapa nyumbani, na kwa atakayoyaona kwa rafiki yake mpya Paul Kagame kule Kigali, basi, John Magufuli njiani akirudi nyumbani atakuwa akijisemea.
;" Yaani, kaanchi kadogo aka ka rwanda, hakina hata bandari wala migodi ya madini katupite hivi hivi kwa vile sisi tumekubali kuyafuga mafisadi...uwiii!"
Goodmorning.
Maggid.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 8, Ikiwemo ya Mtoto wa Rais Matatani Mikataba tata Jeshi la Polisi

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya April 8, Ikiwemo ya Mtoto wa Rais Matatani Mikataba tata Jeshi la Polisi

Lowassa Auponda Uongozi wa Rais Magufuli.......Asema Uongozi wake ni wa Hamasa na Umaarufu wa Muda Mfupi

$
0
0
Edward Lowassa
Siku 155 baada ya Dk John Magufuli kuapishwa kuwa Rais, aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema katika uchaguzi huo, Edward Lowassa ametaja mambo matano yanayomfanya autilie shaka mustakabali wa Taifa chini ya uongozi wa Rais huyo wa Awamu ya Tano.

Akizungumza na wanazuoni wa ndani na nje ya nchi wakiongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Profesa Rwekaza Mukandala nyumbani kwake Masaki Dar es Salaam, Lowassa alisema: “Hali ya siasa nchini ni ya hamasa lakini isiyo na msingi endelevu.”

Lowassa, ambaye alishika nafasi ya pili katika uchaguzi huo baada ya kupata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97 aliyataja mambo hayo kuwa ni Rais kugawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo, watumishi kuachishwa kazi, upitishaji mizigo Bandari ya Dar es Salaam kushuka, nchi kunyimwa misaada na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi hivi sasa.

Katika uchaguzi huo, Rais Magufuli alipata kura milioni 8.8 sawa na asilimia 58.47 na kumshinda Lowassa ambaye alikuwa amejiunga Chadema Julai mwaka jana akitokea CCM ambako jina lake lilikatwa katika mchakato wa chama hicho kupata mgombea urais.

Tangu aingie Ikulu, Rais Magufuli amekuwa akichukua hatua mbalimbali za kutengua uteuzi au kuwasimamisha kazi watendaji mbalimbali wa Serikali, kufuta maadhimisho ya sherehe mbalimbali na kuagiza fedha zitumike kutekeleza miradi mingine huku akiwabana wafanyabiashara kulipa kodi.

Uamuzi wake huo unaofanywa pia na mawaziri wake umekuwa ukipongezwa na kukosolewa na watu wa kada mbalimbali na jana Lowassa alikuwa miongoni mwa wakosoaji hao ikiwa ni mara yake ya pili tangu Dk Magufuli aingie madarakani.

Mara ya kwanza, Lowassa alikosoa sera ya elimu bure, alipoitofautisha na ile aliyokuwa ameahidi ya kuanzia awali hadi chuo kikuu na kuhoji iwapo Rais Magufuli mbali na ada angefuta pia michango mingine, jambo ambalo lilifanyiwa kazi.

Alipoulizwa kuhusu mazungumzo hayo, Profesa Mukandala alisema: “Tunafanya utafiti kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, uchumi, utawala bora na ushindani wa siasa na tunazungumza na watu kutoka vyama mbalimbali na viongozi wa Serikali.”

Waziri wa Habari, Nape Nnauye alipoulizwa kuhusu kauli hiyo ya Lowassa alisema waziri mkuu huyo wa zamani anapingana na viongozi wa Chadema wanaokiri wazi kuwa Rais Magufuli anatekeleza sera na mikakati ya upinzani.

Kauli ya Lowassa
Taarifa iliyotolewa jana na ofisi ya Lowassa ilisema mwanasiasa huyo aliwaeleza wanazuoni hao kuwa; “hali ya siasa hivi sasa ni ya hamasa kutokana na Serikali mpya na ‘style’ mpya. Kwa kipindi kifupi atakuwa lakini hakuna mafanikio ya kiuchumi mbele ya safari.”

Alisema Rais amekuwa akigawa fedha wakati chombo cha kufanya hivyo kipo ambacho ni Bunge.

Rais Magufuli amekuwa na utaratibu kuidhinisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya sherehe mbalimbali kutumika katika shu ghuli nyingine. Juzi, aliagiza Sh2 bilioni zilizokuwa zitumike katika Siku ya Muungano zitumike kupanua barabara inayokwenda Uwanja wa Ndege wa Mwanza.

Pia, amewahi kuamuru Sh4 bilioni za Siku ya Uhuru kupanua Barabara ya Morocco – Mwenge, Dar es Salaam.

Aliagiza pia fedha za maadhimisho ya siku ya Ukimwi kutumika kununua vifaatiba na Sh225 milioni zilizotengwa kwa ajili ya hafla ya uzinduzi wa Bunge zilinunulia vitanda Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Lowassa pia alieleza kusononeshwa na hali ngumu ya maisha na idadi kubwa ya watu kuachishwa kazi.

“Nasononeshwa ninapoona watu wanaachishwa kazi na mashirika mbalimbali kwa sababu ya hali ngumu ya uendeshaji wa mashirika hayo.

“Bandarini sasa hivi nasikia uingizaji mizigo umeshuka kwa asilimia 50, kampuni nyingi za mizigo zimefunga shughuli zake na pale kulikuwa na vijana wetu wengi wana ajira, sasa hivi wako mitaani, hali inatisha maisha ya mwananchi yanazidi kuwa magumu,” alisema.

Lowassa aligusia uamuzi wa Marekani kupitia bodi yake ya Changamoto za Milenia (MCC) kusitisha msaada wa zaidi ya Sh1 trilioni.

“Ni pigo kwa mustakabali wa uchumi. Halafu tunasema tunataka nchi ya viwanda, hela tutatoa wapi kama si hawa wafadhili wa ndani na nje kusaidia katika hilo?” alihoji.

Lowassa ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alisema: “Hawa wafadhili siyo watu wa kuwabeza wataturudisha nyuma. Jakaya (Kikwete- Rais mstaafu wa Awamu ya Nne) kwa kiasi kidogo alijitahidi kuvutia wawekezaji, japo kulikuwa na uzembe na ufisadi katika kuwasimamia.

“Hapa kinachotakiwa ni kufanya mabadiliko katika mfumo na kuufanya kuwa endelevu,” alisema.

Alisema si kweli kuwa kila mtu katika Serikali ya Awamu ya Nne alikuwa mla rushwa huku akikiri kuwa mfumo wa Serikali hiyo ulikuwa mbovu na wa kifisadi.

Aliwaeleza wanazuoni hao kuwa: “Uchaguzi ule tulishinda (upinzani) na kila mtu anajua hivyo. Hata Magufuli anajua hilo...,” alisema.

Akizungumzia mikakati ya upinzani, Lowassa alisema wamejipanga kuhakikisha hawaporwi tena ushindi na kusisitiza kuwa joto la kutaka mabadiliko bado ni kubwa na Watanzania wameichoka CCM.

Kauli na Nape 
Akijibu hoja zilizotolewa na Lowassa, Nape alisema, “Anajichanganya tu, maana Mbowe (Freeman – Mwenyekiti wa Chadema) amenukuliwa akisema Rais Magufuli anaiga kila kitu cha Chadema, sasa yeye (Lowassa) anaposema hayo maana yake haelewani na Mbowe.”

Alisema litakuwa jambo la ajabu kama Lowassa atakubali kila jambo linalofanywa na Serikali iliyopo madarakani kwa kuwa ndivyo alivyo.

“Katika Uchaguzi Mkuu Lowassa hakuchaguliwa na wananchi ila Magufuli alichaguliwa kwa sababu wananchi walifurahishwa na sera zake, hivyo amuache mwenzake atekeleze ahadi zake kwa wananchi,” alisema Nape.

“Kwanza Lowassa amekuwa mtetezi wa wezi, mafisadi na wala rushwa. Unawateteaje watu wa aina hii wanapofukuzwa kazi. Amebanwa tu na kwake kazi inayofanywa na Magufuli inampa maumivu.”

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven Awaagiza Polisi Kuwakamata Watumishi HEWA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Zelothe Steven amemwagiza Kamanda wa Polisi mkoa huo, Jacob Mwaruanda kuwasaka na kuwakamata watumishi hewa 18 waliobainika katika uhakiki uliofanyika katika halmashauri zote mkoani humo hivi karibuni.

Pia ameagiza fedha hizo zilizolipwa kwa watumishi hao hewa na kuiingizia hasara kubwa Serikali zirudishwe mara moja.

Akifafanua alisema katika uhakiki huo, watumishi hewa tisa walibainika katika wilaya ya Nkasi, wanane katika Manispaa ya Sumbawanga na mmoja wilaya ya Sumbawanga wakati Kalambo ikiwa haina mtumishi hewa.

Uhakiki huo unatokana na maagizo aliyotoa Rais John Magufuli baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa aliowateua, aliwaambia wakafanye kazi ya kutatua kero za wananchi na sio kwenda kufanya siasa.

Pia Rais Magufuli aliwapa wakurugenzi wa halmashauri siku 15 wawatoe katika orodha ya malipo ya mshahara wafanyakazi hewa wote katika halmashauri zote nchini.

Zelothe alitoa agizo hilo jana katika kikao maalumu cha kufahamiana kilichojumuisha wazee , viongozi wa dini , watendaji wa umma na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo kilichofanyika mjini hapa.

Alisisitiza kuwa hajaridhishwa na uhakiki huo, hivyo akaagiza halmashuri zote kurudia upya uhakiki wa watumishi.

“Siku ile ile nilipoapishwa kabla sijavuka geti kutoka nje ya Ikulu nilipiga simu na kuagiza halmashauri zote (Manispaa, Nkasi, Kalambo na Sumbawanga) kuanza uhakiki mara moja wasinisubiri hadi niripoti mkoani hapa,” alieleza.

Aliongeza kuwa aliporudi mkoani humo na kuripoti kazini katika siku yake ya kwanza ofisini alikabidhiwa kitabu chenye orodha ya watumishi wa umma wa halmashauri zote akielezwa kuwa hakuna mtumishi hewa katika mkoa wa Rukwa.

“Sikukubaliana nao nilikataa, nikaagiza ufanyike uhakiki mara moja ndipo wamepatikana watumishi hewa 18 na watumishi wengine 137 wapowapo tu wakiwa na taarifa zinazotia mashaka. Wote wamebainika kwenye hicho kitabu nilichokabidhiwa kikionesha hakuna mtumishi hewa,” alisisitiza.

Staa wa Bongo Movies Cloud Amkacha Mkewe Bongo Akimbilia Sweeden na Kufunga Ndoa na Mwanamke Mwingine

$
0
0
NYOTA wa sinema za Bongo, Issa Mussa ‘Cloud’ amefunga ndoa  tena, lakini safari hii ni kwa siri huko nchini Sweden na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mina ambaye amekuwa akimposti kila kukicha mitandaoni kwa kumuita pacha.
Chanzo kilicho karibu na staa huyo kililiambia gazeti hili kuwa, Cloud amemfanyia mbaya mkewe, Cynthia kwa kuamua kuoa kwa siri wakati imani yake inamruhusu kuwa muwazi.
Chanzo kilisema kuwa, awali Cloud alimwambia mkewe wa Bongo kuwa, amepata mfadhili hivyo anakwenda nchini Comoro kupata matibabu ya moyo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu, kumbe haikuwa hivyo bali alikwenda Sweeden ambapo yupo na mwanamke huyu anaedaiwa kufanya kazi ya uuguzi huko...mkwewe Cloud baada ya kusikia nyeti hizo kwa sasa amerudi nyumbani kwao.....

SHAMSA FORD Ashtukia Kuwa Sio Deal Kuwa na Mahusiano ya Kimapenzi na Mastaa wa Bongo..Asema Haya

$
0
0
Msanii wa filamu nchini, Shamsa Ford hivi karibuni alifunguka kupitia mtandao wa Instagram kuwa mahusiano na mastaa wa Bongo hayadumu kwa miezi mitatu na amemuomba Mungu amuepushe mbali nayo.

Akiweka picha ya Beyonce na Jay Z, Shamsa alidai ni uhusiano wao tu ndiyo anaouelewa miongoni mwa mastaa.

Aliandika: Haya ndio mahusiano ninayoyakubali dunia nzima.unaweza kuona mapenzi ,mafanikio na kazi katika nyuso zao….lakini mahusiano ya mastar wetu wa hapa bongo yakidumu sana ni miezi 3..Mimi huwa naona mapenzi ya mastar wa bongo ni kutafuta kick tu but si mahusiano ya kweli. …Mungu niepushe mimi kuwa na mahusiano na star yoyote. Happy anniversary Mr and Mrs JAZZ. ..”

Gari Aina ya Toyota Prado Inauzwa Kwa Bei Nafuu Kabisa...

$
0
0

Toyota prado 2000 model,
Km 110,000
Imetunzwa vizuri sana kama inavoonekana,
Comprehensive insurance,
Petrol fùel,
Engine 3RZ
CC 2690
Price 25 Million
Contacts 0768570703/0657266777




Riyama Awapa Makavu Wanaoponda Mahusianio Yake na Kijana Huyu

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Riyama Ally ambaye siku za karibuni ametolewa mahali na msanii wa muziki wa kizazi kipya Leo Mysterio amevunja ukimya kwa watu ambao wamekuwa wakisema kuwa anatoka na dogodogo huyo.

Riyama amesema kuwa wanataka atoke na mzee ndiyo wamuone kuwa ana heshima.

Kupitia kipindi cha eNEWS kinachorushwa na EATV Riyama amesema kuwa Leo Mystereo ndiyo furaha yake, na ujio wake katikia maisha yake umemuongezea changamoto kwenye maisha yake na kumfanya awe na furaha muda wote.

” Watu wanatakiwa wajue penzi haliingiliwi wewe ukicheka au ukinuna mimi hainisaidii kwani mimi natafuta furaha yangu na huyu ndiye furaha yangu, wewe unataka mimi niondoe furaha yangu nitaipata wapi. Unataka niwe na babu wa miaka mingapi ili uone Riyama ana heshima huyo babu unayetaka niwe naye asiponiheshimu pia mtasema. Jamani binadamu kweli maneno yapo kwa ajili ya kusema ila inabidi tuwe tunachagua vitu vya kusema” alisema Riyama Ally.

Riyama alisema kuwa wapo baadhi ya watu wamekuwa wakiongea vibaya sana juu ya mahusiano yake lakini amewataka kutambua kuwa wao wamependana na wana mipango na wameridhiana wao hivyo kuwatenganisha kwa maneno si jambo jepesi.

Rais Magufuli Kaeleza Kwanini Hapendi Sana Kusafiri Nje ya Nchi

$
0
0
Tunajua Rais Magufuli amekuwepo nchini Rwanda kwa ziara ya siku mbili kuanzia April 6 2016 mpaka April 7 jioni aliporudi Tanzania, kwenye moja ya maongezi yake mbele ya Wananchi wa Rwanda ameongea pia kuhusu kwanini hapendi kusafiri nje ya nchi na toka achaguliwe October 2015, amesafiri nje ya nchi kwa mara ya kwanza April 2016.

‘Nataka niwaeleze ndugu zangu, mimi sipendi sana kusafiri kwasababu ninapenda kubana matumizi… nimealikwa sehemu nyingi nimealikwa Ulaya lakini na sehemu nyingine bado sijaenda, nilipoalikwa na Muheshimiwa Kagame nimekuja na ninataka niwaeleze ndugu zangu wa Rwanda hii ndio safari yangu ya kwanza kutoka nje ya Tanzania‘ – Rais Magufuli.

Masanja Mkandamizaji na Wenzako..Vengu Yupo Wapi na Anaendeleaje Kiafya?

$
0
0
Leo Nimesoma Makala moja katika Gazeti fulani wakimuongelea Msanii Vengu Ambae alikuwa Original Comedy kabla ya kuanza kuugua Mwaka 2009 kiasi cha kupelekwa India kupata matibabu, Gazeti hilo wamesimulia jinsi walivyofanya juhudi za kumtafuta kijana huyo ili kujua anaendeleaje baada ya miaka mitano sasa ya ukimya..lakini bila mafanikio hawakuweza kupata lolote la maana kuhusu alipo ama afya yake.....

Masanja na Wenzako wa Original Comedy sisi Washabiki wa Vengu tunataka kujua alipo na hali ya yake kiafya kwa sasa...Tumemmiss.......

Kipini Cha Pua Cha Diamond Chawatoa ‘Povu’ Mashabiki

$
0
0
Watu wanahofia kipini cha pua cha Diamond kuliko hata kesho yao.

Kinachowaumiza zaidi mashabiki wake ni kuwa haoneshi kujali kilio chao. Aliwashtua sana juzi pale alipoweka picha ikimuonesha akiwa na kipini hicho na wengi walihisi amejitoga.

“Bro hapo umezingua mm nmekuwa shabik yako tangu mwaka 2010 mpaka now nakubali kila ufanyacho bt kwahil nme kushusha vyeooo coz tambua ww ni mtot kisilam hapo ume feel bro nitaendelea kusapoti mziki wako ila tambua ume wakwaza wengi,” ameandika shabiki mmoja.


Baadaye alipost picha nyingine inayomuoesha hana kipino hicho kitendo kilichowafanya mashabiki wake wapumue. Lakini amekuja kuwatoa povu tena baada ya kupost video mbili zinazomuonesha akiwa amekirudisha kipini hicho.

“Bro sorry sana tunaokuelewa niwengi mno ila dah kwahiyo ishu unatupambanisha na maadui mana tunakosa majibu, kma kuna uwezekano m nahisi fanya utoe,” amemuomba shabiki mmoja kwenye video hiyo.

Seems like kipini cha pua bkwa mwanaume si kitu mtanzania anaweza kukielewa! Good news lakini ni kwamba reality TV show yake inakuja soon!

Bosi wa Zamani wa TRA Harry Kitillya, Shose Sinare na Sioi Solomoni Wanyimwa Dhamana

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imepuuza ombi la dhamana ya kesi inayowakabili Harry Kitillya, Shose Sinare na Sioi Solomoni ambapo wamerejeshwa rumande.

Kitillya, alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA); Sinare, Mkuu wa Idara ya Ushirikiano na Uwekezaji katika Benki ya Stanbic na Sioi Solomoni, Mwanasheria wa Benki ya Stanbic.

Dhamana yao imesikilizwa mbele ya Amilis Mchaura, Hakimu Mkazi Kisutu ambapo mawakili wa pande zote mbili waliwasilisha hoja zao.

Dk. Lingo Tenga ndiye aliyeongoza jopo la mawakili upande wa watetezi ambapo upande wa serikali umesimamiwa na Oswadi Tibabyekonya, Wakili Mkuu wa Serikali Mahakama ya Kisutu.

Upande wa utetezi uliomba mahakama kubatilisha mashitaka ya utakatishaji pesa haramu uliosababisha watuhumiwa hao kukosa dhamana. Tibabyekonya ameieleza mahakama kuwa, shitaka la utakatishaji fedha halina dhamana.

Upande wa utetezi ulifanya mapitio ya kesi mbalimbali zinazofanana na kesi hizo ikiwemo kesi namba 314 ya mwaka 2015 kwenye Mahakama ya Rufaa ya Mwanza iliyokuwa ikimkabili Kigunda Francis aliyeshitakiwa kwa kosa kama hilo lakini alipewa dhamana.

Christopher Msigwa, wakili wa serikali amesema kuwa kesi hiyo haina dhamana kwa sababu, kosa hilo linaathiri uchumi wa taifa.

Washitakiwa wamekosa dhamana na wamerudishwa rumande hadi tarehe 22 Aprili mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Taarifa Ya CCM Kuhusu Kauli Ya Mhe Lowassa Kubeza Utendaji Wa Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli

$
0
0
Aliyekuwa mgombea Urais wa UKAWA kupitia CHADEMA, Ndugu Edward Lowassa, Aprili 7, 2016 alifanya mazungumzo na Wanazuoni kutoka katika vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi.

Katika mazungumzo hayo, Ndugu Lowasa aligusia masuala mbalimbali ya Kitaifa yakiwemo hali ya siasa nchini, kuachisha kazi watumishi wenye tuhuma mbalimbali, na kile alichokiita tatizo la mfumo nchini.

Alichokifanya Ndugu Lowassa ni kutaka kuwaaminisha Watanzania masuala yasiyo sahihi kwa maslahi ya kisiasa, kwani ukweli ni kwamba; Mosi, Rais John Pombe Magufuli hatafuti umaarufu, badala yake yeye na Serikali yake wanachapa kazi ili kuwaletea maendeleo Watanzania kwa ujumla.

Pili, kuhusu suala la mfumo, Tanzania haina tatizo la kimfumo, kwani iliyopo, iliyowekwa tangu awali na waasisi wa Taifa letu, Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Abeid Aman Karume ni imara na imekuwa ikiboreshwa kulingana na mahitaji.

Ifahamike hakuna mahali popote duniani ambako mfumo wa nchi unajiendesha wenyewe, siku zote mfumo huongozwa na kuendeshwa na binadamu ambao kwa udhaifu wa ama kibinadamu au wa kukusudia, hufanya makosa yanayohitaji kusahihishwa kwa taratibu zilizowekwa.

Tatu, Hakuna mtumishi aliyeachishwa au kusimamishwa kazi kwa sababu ya hali ngumu ya uendeshaji wa Shirika lolote, isipokuwa hatua hiyo imechukuliwa ili kupisha uchunguzi kutokana na tuhuma mbalimbali za ukiukaji na matumizi mabaya ya ofisi na madaraka, ubadhirifu, uhujumu uchumi na ufisadi.

Chama Cha Mapinduzi kina ushahidi wa utendaji wa Ndugu Lowasa akiwa Waziri Mkuu namna alivyoendesha zoezi la kusimamisha na kufukuza kazi na kuwadhalilisha watumishi bila kufuata taratibu, hali hiyo ni tafauti sana na hii ya sasa, kwani kila anayesimamishwa kazi, anasimamishwa kwa kufuata taratibu zote, ili kuhakikisha kila mtumishi anatendewa haki ya kusikilizwa.

Na katika hili la kuwasimamisha kazi watumishi wa umma wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wizi na matumizi mabaya ya ofisi, Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuunga mkono, kutokana na baadhi yao kuwa kikwazo cha shughuli za maendeleo nchini.

Kiongozi au mwanasiasa anayemkosoa Rais Magufuli katika hatua anazozichukua hivi sasa, ikiwa ni pamoja na kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma, ni wa kutiliwa shaka kwani kufanya hivyo ni sawa na kutetea wizi, ufisadi na uporaji wa rasilimali za nchi.

Ndugu Christopher Ole Sendeka
MSEMAJI WA CCM
MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
08/04/2016

Mabula Ambwaga Ezekiel Wenje Kesi Ya Ubunge Jijini Mwaza Leo

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Nyamagama,jijini Mwanza pichani akifurahia mara baada ya kutangazwa mshindi wa jimbo hilo na Mahakama kuu ya jijini Mwanza dhidi ya aliyekuwa Mgombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia chama cha CHADEMA,Mh.Ezekiel Wenje.
****
EZEKIEL Wenje, mbunge wa zamani wa Jimbo la Nyamagana, Mwanza ameshindwa kwenye kesi aliyoifungua katika Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga dhidi ya Stanslaus Mabula.
 
Mahakama hiyo leo imempa ushindi Mabula (CCM) baada ya kujiridhisha kuwa, upande wa madai hauna ushahidi unaokidhi, kuithibitishia mahakama.

Wenje alifungua kesi hiyo akipinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo hilo mwaka jana yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na kumpa ushindi Mabula.

Katika kesi hiyo namba tatu ya mwaka 2015, ambayo ilionekana kugusa hisia za wakazi wa Nyamagana imehudhuriwa na idadi kubwa ya wafuasi wa upinzani na CCM.

Akitupilia mbali shauri hilo leo Kakusulo Sambo, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Sumbawanga amesema kuwa, amefikia hatua hiyo baada ya upande wa mpeleka maombi kuiomba mahakama kuifunga kesi hiyo.

Amesema upande wa mpeleka maombi, ulidai kwamba kutokana na ombi lao la kupokelewa kwa fomu namba 21B kukataliwa kortini hapo, ulidai hakuna umuhimu wa kuendelea kwa kesi hiyo.

Jaji Sambo amesema, upande wa mpeleka maombi, licha ya kupewa muda wa siku 10 kupeleka fomu namba 21B lakini hawakufanya hivyo.

Amesema, pamoja na kuchelewa kupeleka fomu hiyo pia walipopewa muda wa kujieleza katika ombi lao la kuiomba mahakama kupokea fomu hizo, hawakueleza sababu za msingi.

Hata hivyo amesema baada ya kuwasilishwa kwa ombi hilo kortini, mahakama ilikaa na kutafakari kwa kina juu ya ombi hilo ambapo imeamua kutupilia mbali kesi hiyo.

“Mleta maombi aliomba kufunga kesi mahakamani na mahakama sasa imepitia ombi lao, hivyo na kuona kesi hii haina msingi wowote ule na tunakubaliana nao,” amesema Jaji Sambo.

Hata hivyo wakati shauri hilo likitupiliwa mbali kortini hapo, Wenje pamoja na wakili wake, Deya Outa hakuwepo mahakamani hapo bila taarifa yoyote.

Najuta Kuachana na Mke Wangu wa Kwanza – Gardiner

$
0
0
Mtangazaji wa Clouds FM, Gardiner G Habash amesema miongoni mwa vitu anavyojutia katika maisha yake ni kuachana na mke wa kwanza aliyezaa naye mtoto wa kike, Karen, ambaye kwa sasa yupo mwaka wa pili chuoni.

Akiongea kwenye kipindi cha Take One cha Clouds TV, Gardiner alisema kutokana na kubadilisha kazi ya awali na kuwa mfanyabiashara kipindi anaishi Mwanza, alijikuta akiiweka kwenye mawe ndoa yake kwa kukosa muda nayo.

“Yale mazingira niliyokutana nayo Mwanza ya kibiashara yalisababisha nikaachana na mke wangu wa kwanza, ni kitu ambacho najuta,”alisema staa huyo. “Nisije nikasema sana mwisho nikalia hapa bure,” alisisitiza.

Amesema mke wake huyo kwa sasa aliolewa japo wana mawasiliano mazuri sababu ya mtoto wao. Kuhusu kama anajuta kuachana na Lady Jaydee, Gardiner alisema: Siwezi kusema najuta kwamba alitokea kwenye maisha yangu na siwezi kusema kwamba najuta tuliachana. Lakini ninachoweza kusema tu kwamba kwa suala la Jaydee ni suala ambalo nilichagua sana lisiwe ni jambo ambalo nalizungumzia au kulitolea comment kwasababu yule ni public figure unaposema kitu kuhusu yeye tafsiri zinakuwa ni tofauti na vile unavyotarajia.”

“Kwahiyo sina majuto yoyote, na sina aina yoyote ya chuki au uadui na nategemea hata yeye atakuwa anafeel the same,” alisisitiza.

Alidai kuwa yeye na Lady Jaydee hawana mawasiliano ya aina yoyote kwa sasa na mara ya mwisho walikutana kipindi wanakamilisha taratibu za talaka.

Kwa upande mwingine Gardiner amedai kuwa maisha aliyonayo sasa ni ya furaha tele. Mtangazaji huyo amejiunga tena na Clouds FM akitokea EFM.

Bongo5

Haya Ndio Maamuzi ya Mgodi wa Geita Gold Mine Baada ya Timu yake Kujihusisha Katika Upangaji wa Matokeo

$
0
0
Mgodi wa dhahabu wa Geita ambao ndiyo wadhamini wakuu wa Geita Gold Sports umesitisha udhamini wake kwa muda kwa klabu hiyo inayotuhumiwa kupanga matokeo ya ligi daraja la kwanza.

Msemaji wa mgoni huo Tenga bin Tenga amesema licha ya Geita Gold Sports kuwaandikia barua ya kujitetea kwamba haihusiki na kashfa hiyo, mgodi kwa sasa hautahusika na udhamini wowote hadi pale ukweli halisi wa tuhuma hizo utakapobainika.

“Baada ya tu ya timu kutuhumiwa kwamba imetumia rushwa na kupanga matokeo, haraka uongozi wa mgodi wa Geita ukaiandikia timu barua kwamba iwezekutoa ufafanuzi wa jambo hili ambalo linazunguzwa”, amesema Tenga.

“Timu ilichofanya, ilijibu na kusema hawana hatia yoyote na hawajafanya kitendo kama hicho lakini kama uongozi unahakikisha sheria na taratibu zinafuatwa, mgodi ulichofanya ni kusitisha udhamini tukisubiri upelelezi na uchunguzi wa TFF pamoja na chunguzi nyingine ili ziweze kutoa majibu yanayofaa katika kufanya maamuzi”.

“ Kwahiyo kwasasa mgodi umesitisha udhamini ukitegemea kutoa maamuzi sahihi pale ambabo taratibu zote za uchunguzi zimeshapata majibu”.

Msemaji huyo pia akazungumzia namna mgodi huo ulivyopokea taarifa za hukumu ya shirikisho la soka nchini (TFF) hivi karibuni.

“Kuhusiana na hukumu iliyotolewa na TFF ilitushtua sana kwasababu jamii na watu wote ambao ni wadau tunaojishughulisha nao tunaamini kwamba watafanya vitu sawasawa na mgodi vile ambavyo unafanya. Mgodi unatii taratibu na sheria za nchi, mambo ya rushwa na upangaji wa matokeo ni vitu ambavyo mgodi unapinga sana”.

“Kwahiyo TFF kusema kwamba timu ya Geita imejihusisha na rushwa imetushtua na imetusikitisha kwahiyo uongozi utakaa na utatuambia tunafanya nini”.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images