Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda Atoa Siku Sita Kwa Ombamba Kuondoka Mabarabarani la Sivyo...

$
0
0

Mkuu wa Mkoa atoa siku 6 ombaomba kuondoka mabarabarani, awataka wamiliki wa majengo watengeneze sehemu za kuegeshea magari.

Pia awataka wamiliki wa bar wanaowapigia watu kelele wafuate sheria walizopewa kama ni mwisho saa sita kupiga muziki iwe hivyo..

Mange Kimambi Amshukia Lulu Michael...Ampa za Uso Kuhusu Kumtenga Mama Kanumba

$
0
0


Hali si nzuri kati ya Lulu Michael na Mama Kanumba Baada ya Madai ya Mama Kanumba kudai Lulu amemtenga hata salaam hampi siku hizi na hata siku ya kumbukumbu ya Marehemu Lulu Hakutokea Kanisani Wala makaburini...

Lulu leo ameandika about hiyo issue na kusema hivi:


Baada ya kusema maneno hayo Blogger maarufu alimshukia Lulu kwa kuandika haya kwenye ukurasa wake wa instagram:

"From @mangekimambi_ - Jibu la Lulu on this issue... Leo mama Kanumba anaitwa 'Muhusika Mwenyewe' we mtoto tema mate chini 🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽.... One quick question mama yako mzazi Huyo ulienae Sasa Hivi akikukosea utaacha mawasiliano nae? Au utaacha kumsaidia? Si utasamehe na kusahau yote. Basi na mama Kanumba ungemchukulia hivyo hivyo. Mama sio lazma akubebe tumboni 9 months mama Ni matendo. Alichokufanyia Yule mama Ana deserve msamaha wako Mara 70, hata Kama hutaki kuwa karibu nae msaidie tu.. Please usitafute excuses. Hatujui what happened but rudisha roho nyuma ukumbuke Tanzania nzima ilipokuchukia na kukuhukumu yule mama alikupenda weww mtu ambae ulishuhudia kifo Cha mwanae , hakuna mama duniani angeweza kufanya kitu kama kile Lulu. Mama Kanumba alitunyoooosha nchi nzima.. Mama yako mzazi mwenyewe alikuwa hana msaada na wewe zaidi ya kulia tu, huyu mama aisee laana yake itakupata tena bila chenga na hata haya mabalaaa makubwa yanayoendelea kukupata huwezi jua ndo laana zenyewe hizo! Seriously! Yani ungeweza hata kutumia maneno mazuri kujibu na siyo hivyo ulivyo jibu yani umejibu like you don't need her, hata time huna wakati mama wa watu analilia hata salamu yako tu..... Yule mama mpaka alifunguliwa page Facebook na fans wa Kanumba ya kuchambwa kwanini ana kusupport. Jinsi watu walivyo m-mind yani Yule mama aliharibu hata kesi kwa kweli. Maana Mara nyingi kesi za mauaji Ni familia ndo huwa zinasimamia kesi kuwaforce polisi wafatilie , kulilia haki itendeke Ila Kwa Kanumba it was the opposite mama wa Marehemu anamkumbatia anae tuhumiwa kumuua mwanae... That was shocker, Leo unamchukulia poa tu! Yani kama vile umekorofishana na rafiki.. .
.
Sijui mnakumbuka ile kesi ya Conrad alimuuaga Mlay , Conrad alishatoka jela kijanja janja yani mambo yalimwendea poa, weeee familia ya Marehemu walikinukisha mpaka kwa Rais Mbona mpaka Leo anaozea jela. Same thing na lulu kesi ya Kanumba ilikosa kilio Cha familia tu...
.
.
I hope I didnt come across as being rude kwako Lulu. But niliona tu kuwa hakuna aliekuwa anakwambia ukweli. I'm not saying this because I'm perfect , hata mie nna yangu na mtu akinishauri bila mitusi au michambo huwa sigombani"

FAIZA ALLY..Nampenda Sana Sugu Hata Akitaka Mtoto wa Pili na Watatu Nitampatia....

$
0
0
Baada ya Picha Kusambaa Mitandaoni Sugu Akiwa na Mpenzi wake mwingine, Mama wa Mtoto wake Faiza Ally ambae kwa sasa hawapo pamoja amefunguka mengi nimekuwekea hapa baadhi:


faizaally_ KUMPENDA MTU SIO ZAMBI  TUKANENI TU ! NAUMIA WALA SIKATAI LKN SIO KESI ! NINI HAWARA HATA AKIOA - ACHA MMBONGO HATA AKIOA MALKIA WA UK - BADO SIWEZI KUHUKUMIWA NDIO HIVYO TENA NAMPENDA - PEANENI HABARI - TUKANENI LKN NAMPENDA HIVYO HIVYO NDIO BABA WA MWANANGU HLF SIKUMUIBA....... NAJUA MNATAMANI HATA MWANANGU ASINGE KUWA HUYO NDIO BABA YAKE LKN NDIO BASI TENA MIPANGO YA MUNGU NA BY THE WAY AKITAKA MTOTO WA PILI NTAMPA NA WA TATU PIA.......

Faizaally_ PIGENI TU PICHA KWENYE NYUMBA YA MWANANGU LKN MWENYEWE AKIKUA ATAKUJA - KAMA HAJAWA AMBIA KILA KITU KIKO CHINI YA JINA LA DESDERIA-SASHA - HATA HOTEL MPYA INAITWA DESDERIA  #SHIKAMOO SASHA MBILINYI




Faizaally_ SIFAI NAFAA NDIO MAMA SASHA # THROW BACK MBEYA KWA BABA 🏻️ SEBLENI KWETU NA PAZIA CHAGUO LA MAMA  # KALIENI TU MAKOCHI YANGU #PIGENI PICHA KWENYE MAUA ALIO PANDA MAMA YANGU # NIKIKUA NARUDIIII KWETU #NA HIVI BABA YANGU ANA NIPENDA MTAJAMBIA HEWANI # IN SASHAS VOICE

Q-Chilla 'Nataka Kufanya Wimbo Mkubwa na Diamond Platnumz Ambao Haujawahi Tokea'

$
0
0
Q-Chief amedai kuwa anataka kufanya wimbo mkubwa na Diamond.

Ameiambia Bongo5 kuwa mazungumzo kwaajili ya kufanyika wimbo huo yapo sehemu nzuri.

“Diamond ana management yake, na he is big to his own way that huwezi tu kukurupuka ukasema tunafanya kazi,” anasema.
“Licha ya kwamba mimi ni mmoja kati ya wasanii ambao anawaadmire sana na mimi ni mmoja kati ya mashabiki wake, napenda kazi zake hasa this latest ambayo amefanya na AKA naona improvement na changes, mimi napenda mtu ambaye anabadilika ambaye habaki pale pale, napenda mtu ambaye anafunguka zaidi,” ameongeza.
“Nikimtumia message anarespond vizuri sana, kitu ambacho ananipa moyo zaidi. Lakini mimi na Diamond hatutakiwi kufanya kazi nyepesi, tunatakiwa kufanya kazi kubwa, kazi yenye uzito, kazi yenye ubora, kazi yenye kumbukumbu, kazi ambayo itaishi, itaingiza pesa na itamtoa Q-Chief kutoka hatua moja kumpeleka hatua nyingine. Kwahiyo tusubirie kwasababu nataka kuandika kitu kizuri.”

Bongo 5

Katibu Mkuu CHADEMA, Dr. Vincent Mashinji aripoti rasmi ofisini Kwake

$
0
0

Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), DR.Vincent Mashinji jana ameripoti rasmi kwenye ofisi yake mpya jijini Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi mbalimbali waandamizi wa chama hicho akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salumu Mwalimu.

Polisi Wakwama Kuuwasilisha Mkataba wa Lugumi.....Wabunge Watoa Siku 3 Mkataba Huo Upelekwe

$
0
0
BUNGE limetoa siku tatu kwa Jeshi la Polisi kuwasilisha kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) mkataba wa Kampuni Lugumi Enterprises wenye thamani ya Sh bilioni 37.

Hatua hii inakuja siku mbili baada ya jeshi hilo kudaiwa kukaidi agizo la kamati hiyo, iliyotaka likabidhi nyaraka za utekelezaji wa mkataba ufanyiwe tathmini kutokana na malalamiko yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG) katika hesabu za mwaka 2013/2014.

Akizungumza jana na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati ya PAC, Aeshi Hilaly alisema agizo la kamati la kutaka mkataba huo, lilitolewa wiki iliyopita kuwezesha wabunge kuangalia utekelezaji wake.

“Jana (juzi) ilikuwa siku ya mwisho kwa jeshi kuwasilisha mkataba huo ofisi za Bunge, lakini mpaka leo (jana) muda huu ninapozungumza nanyi (saa 7:30 mchana) walikuwa hawajawasilisha. “

"Siku zote tumekuwa tukitoa maagizo kwa mdomo na taasisi nyingi zimekuwa zikitekeleza, lakini hili la mkataba wa Lugumi naona kwa wenzetu limekuwa gumu, hivyo tumeamua kuwakumbusha kwa maandishi,” alisema.

Alisema kamati hiyo imetoa siku tatu tangu barua itakapopelekwa na ofisi za Bunge, kuhakikisha wanatekeleza agizo hilo ili kamati hiyo iweze kupitia utekelezaji wa mkataba huo na baadaye kupeleka mapendekezo kwenye Bunge.

“ Katika suala hili, Kamati haitarudi nyuma, hivyo tunawaomba wenzetu wa Jeshi la Polisi kutupa ushirikiano, si jambo la peke yangu kuamua, ni la Bunge, baada ya kupitia tunapeleka mapendekezo bungeni ambalo ndilo litakaloamua nini kifanyike,” alisisitiza.

Kamati ya PAC ilipokuwa ikipitia hesabu za Jeshi la Polisi, ilibaini kuwapo mkataba tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises .

Kupitia mkataba huo wa mwaka 2011, Kampuni ya Lugumi Enterprises ilipewa zabuni ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya polisi 108 nchini kwa gharama ya Sh bilioni 37.

Inadaiwa kampuni hiyo imekwishalipwa Sh bilioni 34 kati ya Sh bilioni 37 ikiwa ni sawa na asilimia 99 ya fedha zote, huku ikiwa imefunga mashine katika vituo 14 pekee katika jiji la Dar es Salaam, ambavyo pia inadaiwa havijulikani maeneo vilipo.

Gari la Serikali Lanaswa Baa Usiku.....

$
0
0
KIKOSI cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers, Ijumaa iliyopita kilimnasa dereva wa taasisi ya serikali akirandaranda na gari la serikali usiku na akaishia baa moja ambapo alikutwa akinywa pombe huku akila nyama choma.

OFM wakiwa kwenye hekaheka za kusaka matukio walishuhudia gari hilo (namba tunazihifadhi), likikata mitaa lakini likaishia maeneo ya Mji Mpya kwenye Baa ya Uswaa ambapo saa 4 usiku liliegeshwa na kudumu hapo kwa muda mrefu kinyume na maelekezo ya serikali yanayosema magari yake yote kutembea mwisho saa 12 jioni.

OFM ilimshuhudia dereva wa gari hilo akinywa pombe kinyume na sheria za usalama barabara zinazokataza kutumia kilevi kisha kuendesha chombo cha moto.
“Hii mbaya sana, mambo kama haya mpaka Magufuli (Rais Dk. John Magufuli) aseme? Viongozi wake wapo lakini hawasimamii ipasavyo sheria,” alilalamika mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Laudio Kabila.

Alisema maagizo yanapotolewa na rais hugeuka kuwa sheria hivyo haoni sababu polisi wanaosimamia sheria na maagizo ya viongozi tena wa nchi kuacha kusimamia ipasavyo.
0“Polisi ndiyo wanaosimamia sheria na maagizo ya viongozi wa serikali kama vile rais, waziri, mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya na kadhalika. Hili la magari kuzurura hovyo usiku wanalifumbia macho, waache kufanya hivyo,” alishauri Kabila.

Hadi OFM inaondoka kwenye baa hiyo saa sita usiku, ilimuacha dereva huyo akiendelea kupata kinywaji huku akiwa na mwanamke ambaye haikufahamika kama alikuwa mkewe au mpenzi.
Wakati anaingia maradakani mwaka jana, Rais Dk. Magufuli aliagiza magari yote ya serikali kutofanya kazi usiku isipokuwa yale ambayo viongozi wake watakuwa wako kazini.

Alisema magari yote yawe yanaegeshwa sehemu husika serikalini saa 12 jioni isipokuwa kama kuna viongozi au watendaji wa serikali ambao wapo kazini na akaelekeza kwamba yatakayokuwa na shughuli maalum za kiserikali, yawe na vibali.

Agizo kama hilo liliwahi kutolewa na serikali ya awamu ya nne iliyokuwa ikiongozwa na Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete lakini ilikuwa kama nguvu ya soda kwani baadaye lilipuuzwa.
Mbaya zaidi hata jeshi la polisi linalopaswa kusimamia agizo hilo limekuwa likifumbia macho jambo hilo ambalo lilitolewa kwa nia nzuri na kwa faida ya taifa.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, ACP Ulrich Matei (pichani) hakuweza kupatikana mara moja ili kueleza kwa nini hawayakamati magari yanayozurura usiku na kutumika kwa shughuli za starehe kama lilivyokutwa gari hilo mkoani hapa.

Chanzo:Global Publishers

TB Joshua Atajwa Kashfa ya Ukwepaji Kodi ya Panama...Mwenyewe Akana na Kuruka Kimanga

$
0
0
TB Joshua, muhubiri maarufu barani Afrika na raia wa Nigeria, ametajwa kwenye nyaraka za kashfa ya ukwepaji kodi za Panama, akidaiwa kuwa na hisa kwenye kampuni iliyosajiliwa visiwa vya British Virgin Islands.

Mwanzilishi huyo wa Kanisa la Sinagogi la Mataifa Yote (Synagogue Church of All Nations) na mkewe Evelyn wanadaiwa kuwa na hisa kwenye kampuni hewa ya Chillon Consultancy Limited iliyo kisiwa cha Tortola, ambacho ni kikubwa kuliko vyote vya British Virgin na ambacho hakuna watu wengi wanaoishi.

Wote wawili wanamiliki hisa moja, ingawa kampuni hiyo yenye namba ya usajili 1033675, inaidhinishwa kutoa hisa zisizozidi “50,000 kwa thamani ya hisa ya daraja moja.” Haieleweki ni biashara gani TB Joshua alifanya na kampuni hiyo ambayo haina ofisi kwenye kisiwa hicho cha Tortola.

Lakini muhubiri huyo, ambaye alifuatwa na wagombea wawili wa urais wa Tanzania, John Magufuli na Edward Lowassa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, amekanusha vikali tuhuma hizo zilizoandikwa na gazeti la Premium Times la Nigeria, akisema zina lengo la kumchafua yeye na kanisa lake na kwamba aliyeandika habari hiyo, Nicolas Ibekwe aliwahi kumtuhumu kuwa alimpa rushwa wakati jengo la nyumba ya wageni la kanisa lake lilipoanguka.

“Mimi si mfanyabiashara na sina biashara. Kitu alichonipa Mungu si cha kawaida. Sihusiki na nyaraka za Panama,” alisema TB Joshua katika taarifa yake aliyoituma kwenye ukurasa wa facebook.

“Mimi na familia yangu tutaendelea kuwa kwenye shamba la Mungu. Premium Times – msiruhusu kampuni yenu kutumika. Msiruhusu kampuni yenu kupingana na Mungu. “Huu ni uongo! Zingatia – habari hii imeandikwa na mwandishi yule yule ambaye alinituhumu kuwa nilimuhonga wakati wa tukio la jengo kuanguka na alienda kwenye vyombo tofauti vya habari – vya ndani na vya kimataifa – kutangaza mambo hayo ya kutunga.

“Tangu wakati wa tukio la jengo, kumekuwa na mfululizo wa vitisho dhidi ya huduma yangu na mimi binafsi kutoka kwa mwandishi huyo, Nicholas Ibekwe, ambaye anawakilisha kikundi cha watu.”

Alisema: “Baada ya yote hayo yaliyofanywa kujaribu kuimaliza huduma hii, hiki ndicho alichoamua kukifanya. Hata picha iliyotumika kwenye habari ilipigwa kwenye mkutano wa injili nilioufanya Mexico. Nilikwenda kwenye mkutano wa injili, na si vinginevyo.”

Muhubiri huyo alitaka nyaraka za Panama zisitumike kushambulia watu ambao wamekuwa wakiwatafuta ili wawachafue kwa kuwa si kila mtu anayetuhumiwa na vyombo vya habari kuhusika kwenye sakata hilo, amehusika.

“Suala langu ni mfano mzuri,” alisema. TB Joshua amejizolea umaarufu kutokana na kutabiria watu matukio yanayotarajiwa kuwatokea na amekuwa akivuta waumini kutoka kila kona ya Afrika kwenda Nigeria kumsikiliza.

Kwa nyakati tofauti, Magufuli wakati akiwa waziri, na Lowassa walikwenda Nigeria kuhudhuria mahubiri yake na taarifa zinasema kuwa wote walitabiriwa urais.

Wawili wao walichangia kuufanya uchaguzi mkuu uliopita kuwa na msisimko na ushindani mkali, kabla ya Magufuli kuibuka mshindi kwa kupata kura milioni 8.8, akifuatiwa na Lowassa aliyepata kura milioni 6.07. Baada ya Uchaguzi Mkuu, TB Joshua alikuja nchini na kufanya mazungumzo na Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam na baadaye kutumia muda uliosalia kwa kuwa karibu na Lowassa kabla ya kurudi Nigeria. Nyaraka hizo zilivuja kutoka kampuni ya sheria ya Mossack Fonseca ya Panama iliyokuwa ikisaidia wanasiasa, wafanyabiashara na watu maarufu duniani kusajili kampuni hizo.

Nyaraka za Panama zimefichua watu maarufu 143 duniani wakiwamo wakuu 12 wa nchi walioko madarakani na waliostaafu pamoja na familia zao na marafiki wa karibu ambao wamenufaika na ukwepaji kodi. Miongoni mwao ni baba wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Davi Cameron, hayati Ian Cameron ambaye inadaiwa kila alipokuwa anakwenda kuhudhuria kikao cha bodi cha kampuni ya Blairmore Holdings, alianzia kwenda Uswisi au Bahamas.

Awali David Cameroon alikana kuhusika katika kashfa hiyo lakini juzi alikiri kumiliki hisa katika kampuni ya baba yake ambayo iliuzwa kabla hajawa Waziri Mkuu.

Wengine ni Sergei Roldugin, mshirika wa Rais Vladimir Putin wa Russia, shemeji wa Rais Xi Jinping wa China, Rais Mauricio Macri wa Argentina, na watoto watatu wa Waziri Mkuu wa Pakistan, Nawaz Sharif.

Pia yumo Ahmad Ali al-Mirghani, rais wa zamani wa Sudan, Kalpana Rawal (Naibu Jaji Mkuu wa Kenya), Koffi Annan (katibu mkuu wa zamani Umoja wa Mataifa), Mounir Majid (msaidizi wa karibu wa Mfalme wa Morocco) na Khulubuse Zuma (mpwa wa Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini).    


Hospitali ya Muhimbili Wachanganya Maiti..Ndugu Wasafirisha na Kuzika Maiti Isiyo yao...

$
0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imeingia katika mkasa baada ya kutoa mwili wa marehemu kwa watu tofauti ambao nao bila ya kujua, waliusafirisha na kuuzika Usangi, Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Kutokana na kosa hilo, hospitali hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, jana walilazimika kufukua maiti hiyo ya Janeth Bambalawe (65), kuirejesha Dar es Salaam ili ikabidhiwe kwa wahusika baada ya kusafirisha maiti ya Amina Msangi (79), ambayo iliachwa kwa makosa katika chumba cha kuhifadhia maiti hadi Usangi.

Ilivyokuwa

Sintofahamu hiyo ilitokea juzi asubuhi baada ya ndugu wa Janeth, kufika mochwari Muhimbili ili kuuchukua mwili wa marehemu huyo kwa ajili ya maziko katika makaburi ya Kipunguni, Ukonga na kuukosa.

Akizungumzia mkasao Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi MNH, Dk Praxeda Ogweyo alisema ndugu wa Amina ambaye alifariki Aprili 8 hawakuukagua mwili wa marehemu baada ya kupewa na badala yake waliondoka na mwili wa Janeth.

Alisema marehemu Amina aliyefikishwa hospitalini hapo kwa rufaa akitokea Temeke Aprili 6 na kulazwa wodi 12 katika jengo la Kibasila, alihifadhiwa jokofu moja na Janeth ambaye alifikishwa hapo kutokea Amana Aprili 4 na kulazwa wodi 2 jengo la Mwaisela. Naye pia alifariki Aprili 8.

“Wote walifariki siku moja, wakahifadhiwa katika jokofu moja kwa hiyo mtumishi wa mochwari alipokwenda kuutoa mwili alichanganya badala ya kuwapatia mwili wa Amina, akawapa ule wa Janet na ndugu nao hawakushiriki kikamilifu kukagua,” alisema Dk Ogweyo.

Alisema kwa kutambua kosa hilo, Muhimbili ilitoa gari la wagonjwa na wafanyakazi wawili kwa ajili ya kuupeleka mwili wa Amina, Usangi kwa ajili ya mazishi na kuurejesh Dar es Salaam ule wa Janeth. Pia iliwasiliana na jeshi la polisi kwa ajili ya taratibu za kufukua mwili huo. “Wawakilishi wetu wamekwenda Mahakama ya Mwanzo, Wilaya ya Mwanga kwa ajili ya viapo na baadaye jioni watafukua mwili tayari kwa safari ya kuurejesha kwa ndugu husika kwa mazishi,” alisema.

Alipopigiwa baadaye jioni Dk Ogweyo alisema: “Mwili unafukuliwa sasa na baada ya kukamilisha, watauandaa na wataanza safari usiku (jana) kuurudisha Dar es Salaam, tunatarajia watafika alfajiri au asubuhi (leo).”

Mbali na hatua hiyo, Dk Ogweyo alisema mtumishi aliyefanya kosa hilo amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi.

Akielezea hali ilivyokuwa mtoto wa marehemu Janeth, Peter Mkude alisema walipofika Muhimbili aliingia na kuonyeshwa mwili wa mama yake ambao hakuutambua, akatoka na aliporudi mara ya pili aliongozana na mama zake wadogo wawili na dada yake, lakini pia hawakuutambua.

Kuona hivyo walikwenda katika ofisi za utawala ambako waliongozwa kwa mwanasheria ambaye baada ya maelezo, waliongozana naye hadi mochwari na baada ya kuthibitisha kwamba mwili umekosekana, walikwenda Kituo Kikuu cha Polisi ambako waliandikisha maelezo na kupewa ahadi ya kurejeshewa mwili wa ndugu yao.

“Walituambia kwamba wataufukua na kufikia Aprili 13 (leo) tutakuwa tumeupata, tumepanga kuzika siku hiyohiyo katika makaburi ya Kipunguni Mashariki, Ukonga saa 10 jioni,” alisema Mkude.     

Wabunge Wadai TANAPA Ni JIPU....Washangaa Shirikia Hilo la Umma Kuwa na Matumzi Makubwa Kuzidi Makusanyo

$
0
0
SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limeingia kwenye orodha ya Taasisi za Serikali zenye matumizi makubwa ya fedha ukilinganisha na mapato wanayokusanya, jambo lililoishtua Kamati ya Bunge na kutaka shirika hilo lipunguze matumizi yake.

Hayo yalibainika jana Dar es Salaam wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC), ilipokutana na Tanapa kupitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2013/14.

Katika ripoti hiyo ilibainika kwamba Tanapa kwa mwaka huo wa fedha, ilitumia jumla ya zaidi ya Sh bilioni 151.7 ilhali mapato yao yalikuwa Sh bilioni 149.9 hivyo matumizi ya fedha yaliyozidi ni Sh bilioni 1.8.

Taasisi nyingine ya Serikali ambayo ilikuwa na matumizi makubwa ya fedha za Serikali ni Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ripoti ya CAG ya mwaka 2013/14 ilionesha kuwa ilitumia Sh bilioni 18.6 kwa ajili ya matumizi ya watumishi wake.

Wakichangia hoja mbalimbali wakati wa kupitia ripoti hiyo hapo jana, Wajumbe wa Kamati hiyo walisema kutokuwepo Bodi ya Shirika hilo, kunachangia watendaji wa shirika hilo kuliendesha ndivyo sivyo.

Mjumbe wa Kamati hiyo, Albert Obama, mbunge wa Muhigwe alisema shirika hilo ni jipu kwa sababu limejilimbikizia ulaji, kana kwamba ni chombo cha watu wachache, ilhali shirika hilo linatakiwa liwe kwa ajili ya ustawi wa uchumi wa nchi.

“Haiwezekani ripoti ya mwaka 2013/14 inaonesha kuwa mapato yenu yalikuwa Sh bilioni 149.9 halafu matumizi yenu ni Sh bilioni 151.8”, yaani mnatumia chote hadi mnadaiwa sasa hii sio sawa, hili ni shirika la umma?” Alihoji Obama.
“Hapa wanakuja na maneno matamu kwamba bajeti ya mwaka huu 2016/17 wamepanga kukusanya mapato ya Sh bilioni 188 lakini matumizi yenu pia mmeainisha yatakuwa Sh bilioni 270, hii ikoje? " Alihoji Obama.

Mjumbe mwingine, Joseph Kakunda mbunge wa Sikonge, alisema Tanapa haina changamoto kubwa, zinazoifanya ishindwe kukusanya mapato makubwa zaidi ya hayo ya sasa na kusema walipaswa kukusanya zaidi ya Sh trilioni moja na sio hizo bilioni 149

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 13, Ikiwemo ya Lugumi Kampuni ya Ikulu..?

TCRA yawapa Kibano Akina Lulu na Masogange Kwa Kuvaa Nguo Fupi na Kupost Mtandaoni

$
0
0
DAR ES SALAAM: Kufuatia tabia ya akina dada wengi kuweka picha za nusu utupu katika akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii, wakiwemo mastaa kama Lulu, Masogange na wengineo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewapa kibano kikali, Risasi Mchanganyiko lina stori kamili.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Innocent Mungi alisema ingawa jukumu la kuwakamata wote wanaoweka picha zinazokiuka maadili ni la jeshi la polisi kupitia kitengo cha makosa ya mtandao (Cyber Crime), taasisi hiyo inawasiliana na wamiliki wa mitandao ya kijamii ili kutafuta namna nzuri ya kuwadhibiti.

“Tunachofanya ni kuzungumza na hawa watu ili kuwafungia wote wanaokiuka maadili, tunajua baadhi yao wanajiunga katika mitandao kwa kutumia majina ya uongo, lakini sisi tutazifungia ‘line’ maana kila moja ina namba zake za siri na hazifanani na zingine, hivyo ukiondolewa kwa kufungiwa huwezi tena kujiunga kwa vile kule kwenye mitandao wanatambua namba,” alisema.
Akifafanua, Mungi alisema wakifikia makubaliano na mitandao hiyo ya kijamii aliyoitaja kuwa ni pamoja na Twitter, Facebook, Instagram, Badoo, Snapchat na mingineyo, mtu anayeweka picha zinazokiuka maadili atafungiwa na hataweza kujiunga tena hata abadili jina mara ngapi.


Katika mitandao hiyo, baadhi ya wasichana wakiwemo maarufu, wamekuwa wakiweka picha zinazokiuka maadili, kwa sababu mbalimbali wengine wakitajwa kuwa wanajiuza.
Baadhi wa wasichana wenye majina maarufu ambao wamekuwa wakitupia picha zenye utata mara kwa mara katika mitandao licha ya Lulu ni pamoja na Agnes Gerald ‘Masogange’, Gigy Money, Shilole, Kidoa, Anti Lulu, Isabela Mpanda na wengineo.

Chanzo:Global Publishers

Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Wamkana Anne Kilango Malecela.....Wadai Hata wao Walishangaa Sana Aliposema Shinyanga Haina Watumishi Hewa

$
0
0
Siku moja baada ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango kuvuliwa uongozi kwa kutosema ukweli, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Hawa Ng’humbi ameiruka taarifa ya kutokuwapo kwa watumishi hewa, ambayo amesema ilimshtua alipoiona kwenye televisheni.

Mkoa wa Shinyanga unaundwa na wilaya tatu ambazo ni Shinyanga, Kishapu na Kahama zinazoundwa na halmashauri sita ambazo ni Kishapu, Manispaa ya Shinyanga, Mji wa Kahama, Ushetu, Msalala na Shinyanga Vijijini.

Rais John Magufuli juzi alitengua uteuzi wa Kilango, ikiwa ni siku 30 tangu alipotangaza kumteua kwa maelezo kuwa alitoa taarifa isiyo ya kweli kuwa Shinyanga hakuna watumishi hewa kabla ya kujiridhisha.

 Pamoja na Kilango, Rais Magufuli pia alitengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Shinyanga, Abdul Dachi, kwa sababu hiyo ya kutoa taarifa za uongo.

 Dk Magufuli alichukua uamuzi huo baada ya kutuma timu mkoani Shinyanga kufanya uhakiki na kubaini kuwa kulikuwa na watumishi hewa 45 katika wilaya moja ya Shinyanga kabla ya kwenda wilaya nyingine za Kahama na Kishapu.

Akizungumzia sakata hilo jana baada ya uamuzi wa Dk Magufuli, Ng’humbi alisema taarifa za kukosekana watumishi hewa kwenye wilaya yake alizisikia kwenye taarifa ya habari ya televisheni Machi 30 na zilimshtua.

 “Binafsi nilishtuka sana nilipoona ikitangazwa kuwa mkoa mzima wa Shinyanga, hakuna mfanyakazi hewa wakati mimi sikuwa hata nimeona taarifa kutoka wilayani kwangu iliyoandaliwa na uongozi wa halmashauri,” alisema Ng’humbi.

“Nilijiuliza taarifa imefikaje kwa mkuu wa mkoa bila kupitia kwangu? Kusema kweli nilianza kuifanyia kazi taarifa hiyo na ninatarajia ifikapo Ijumaa nitakamilisha kazi hiyo.” 

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Alphonce Gagambobyaki alisema hadi sasa ofisi yake haijafahamu nani aliyempa mkuu wa mkoa taarifa ya ukaguzi wa wafanyakazi hewa kwa sababu taarifa aliyonayo mezani haijasainiwa.

 “Kuna tatizo la ofisi hii kukaimiwa na zaidi ya watu wanne tangu aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji, Dalikunda Kimulika alipostaafu Februari. Ni vigumu kujua nani alihusika nayo bila kuona saini,” alisema Bagambobyaki. 

Alisema taarifa hiyo inaonekana haikusainiwa kutokana na hofu baada ya watumishi waliobainika kutokuwapo kwenye vituo vyao vya kazi karibu wote kuonekana kuwa na ruhusa maalumu.

“Wakati bado tunajiridhisha kujua ni ruhusa ya aina gani na hawa watumishi wako wapi, ndipo taarifa ilipotangazwa kwamba mkoa hauna watumishi hewa,” alisema.

Hata hivyo, alisema anaamini taarifa sahihi itajulikana baada ya timu maalumu iliyotoka Tamisemi kukamilisha uhakiki wilayani humo jana.

“Timu ile ya Tamisemi imekwenda mbele zaidi katika uhakiki wake kwa kukagua mtumishi mmoja mmoja hadi vijijini na imekamilisha kazi yake jana,” alisema Bagambobyaki. 

Kuhusu iwapo aliyekuwa mkuu wa mkoa alitumia taarifa zao au la? kaimu mkurugenzi huyo alisema: “Iwapo RC alitumia taarifa zetu au la, hilo siwezi kulisemea kwa sasa.”

Kilango ambaye juzi alisema hakuwa amepata taarifa hivyo asingeweza kuzungumzia kutenguliwa kwake, jana alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kabisa na Dachi akaeleza kuwa ameupokea uamuzi huo kwa kuwa Rais ndiye mteule wake.

Taarifa ya kutenguliwa kwa watumishi hao wa umma sasa imekuwa kaa la moto kwa wakuu wa wilaya makatibu tawala wao, na wakurugenzi watendaji wa halmashauri za mkoa huo.

Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo za watumishi hewa, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro alisema hawezi kuzungumzia lolote.

“Sisemi lolote na wala sizungumziii mkoa,” alisema na kukata simu ambayo haikupokewa tena. 

Kama ilivyokuwa kwa mkuu wake wa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Shinyanga, Lewis Kalinjuna aligoma kuzungumzia uwezekano wa halmashauri yake kutoa taarifa zilizompotosha Kilango.

“Sitaki kulizungumzia hilo, nawaachia wanaolijua walizungumzie,” alisema Kalinjuna.

Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Vita Kawawa alikata simu yake mara kadhaa alipopigiwa na baadaye kutuma ujumbe mfupi wa maneno akisema yuko kwenye kikao na kuelekeza atumiwe ujumbe ambao hata alipotumiwa hakujibu.

Ombaomba Dar Wamjibu Makonda, Wasema Hawaondoki MJINI Ng'oo

$
0
0
OMBAOMBA katika jiji la Dar es Salaam wamemjibu Mkuu wa Mkoa, Paul Makonda wakisema hawawezi kuondoka kwa vile ‘mjini kila mtu ana kazi yake’.

Wamesisitiza kuwa hawawezi kuondoka Dar es Salaam kwa sababu wamekuja kutafuta kipato.

Baadhi ya ombaomba walitoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti jana, baada ya Gazeti hili kutaka maoni yao kuhusu tamko la Makonda kwamba atafanya operesheni ya kuwakamata Aprili 18 mwaka huu.

“Mimi siwezi kurudi Dodoma kwa sababu nauli ni kubwa. Nilikuja jana kwa kulipa Sh 20,000 sasa mimi nitapata wapi fedha nyingine? Kama anataka tuondoke atupatie nauli.

“Kama hawezi kutupatia nauli atupeleke popote sisi tutaendelea kuomba tuweze kujipatia kipato kwa ajili ya kujikimu maisha.

“Kama unavyoniona mimi na familia yangu nimekimbia Dodoma kutokana na mafuriko… sasa wakiniambia nirudi nitaenda wap?.

Pamoja na kunipatia nauli wanifanyie mpango wa nyumba ya kuishi,” alisema mmoja wa ombaomba hao, Amina Ramadhani aliyekuwa eneo la Mnazi Mmoja.

Mwingine aliyekuwa amekaa na watoto wake wanne na ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema: “Kila mmoja na kazi yake hapa mjini.

“Sisi tutaendelea kuomba kwa sababu ndiyo kazi yetu inayotupatia kipato cha kuendeshea familia zetu”.

Ombaomba mwingine ambaye naye alikuwa eneo la Mnazi Mmoja na pia hakutaka kutaja jina lake alisema viongozi wa Serikali nao ni wazazi kwa hiyo wanapaswa kuangalia namna ya kuwasaidia.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Makonda alisema muda wa ombaomba katika jiji umekwisha hivyo amewataka kufungasha virago vyao na kurudi makwao.

Alisema amefanya utafiti na kugundua kuwa asilimia 80 ya ombaomba wanatoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam na asilimia 20 ni wakazi wa jiji.

Makonda alieleza masikitiko yake kuwa ombaomba hao wamekuwa wakiwatumia watoto wao kuomba ili kujipatia kipato.

“Ombaomba wote wafahamu kwamba mji unapaswa kuwa safi na wale wanaokaa katika makutano ya barabara au nje ya maduka ya watu kwa ajili ya kuomba, watambue kwamba muda huo umekwisha, wanapaswa kurudi katika mikoa yao.

“ Wafanyabiashara wengi wamekuwa wakiwalalamikia ombaomba wanaolala kwenye milango ya biashara zao kwamba hujisaidia hapo hapo hali inayochafua mazingira na kusababisha usumbufu mkubwa.

“Sasa ninasema ombaomba hawa wamekuja kwa nauli zao hivyo wataondoka kwa nauli zao… nitakayemkamata katika operesheni yangu nitakayoifanya Jumatatu nitamchukulia hatua za sheria ikiwa ni pamoja na kumfikisha mahakamani,” alisema Makonda.

Naye Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es Salaam, Simon Sirro, alisema ombaomba ni wengi katika jiji na wanaopaswa kufuatilia watu hao ni viongozi wa Serikali za mitaa lakini wamekaa kimya.

“Wenyeviti wa Serikali za mitaa ni wajibu wao kuwashauri watu hawa hivyo tunawaomba wafanye hivyo kabla mkuu wa mkoa hajaanza kufanya operesheni hiyo,” alisema.

Wakati huo huo, Makonda amewataka wote waliojenga maghorofa bila kutenga maeneo ya kuegesha magari, wayabomoe la sivyo watafute maeneo mengine kwa ajili ya maegesho.

“Majengo makubwa yanapaswa kuwa na maegesho. Ninashangaa kuona magari yameegeshwa ovyo ndani ya jiji hasa pembezoni mwa barabara hali inayosababisha watembea kwa miguu kukosa maeneo ya kupita kutokana na magari hayo.

“Hii ni hatari kwa sababu mtu anaweza kugongwa kutokana na uzembe wa watu wasiozingatia sheria,” alisema Makonda.

Pia aliwataka wamiliki wa baa kufuata sheria za leseni zao na kufunga muda waliopangiwa.

Source: Mtanzania

Utajiri wa Sh. Bilioni Nane wa Mwanamuziki Diamond Wazua Maswali...

$
0
0
Hivi karibuni, Mtandao wa The Net Worth (www.the-net-worth.com) umetangaza utajiri wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ (26) ambapo kwa mujibu wa jarida hilo, nyota huyo ana utajiri wa dola milioni 4 za Kimarekani (sawa na zaidi ya shilingi bilioni 8.75), jambo lililozua maswali yapatayo 6 miongoni mwa Wabongo.

Mtandao huo umekuwa ukijipambanua kwa kuanika utajiri wa watu maarufu barani Afrika wakiwemo David Adedeji Adeleke ‘Davido’ (shilingi bilioni 32), Ayodeji Balogun ‘Wizkid’ (bilioni 24) na wengineo kibao.

Baadhi ya wasomaji wa gazeti hili wameuliza maswali hayo wakisema mwenye uwezo wa kuyajibu ni Diamond mwenyewe na si jarida hilo huku wakitia shaka kwamba, huenda waandaaji wa jarida hilio wamepewa taarifa za uongo na Diamond mwenyewe.

AMEPATA WAPI UTAJIRI HUO WA HARAKA?
Swali la kwanza ambalo wengi waliosikia taarifa za mtandao huo walihoji, nini chanzo cha utajiri huo kwani wengi wanaamini kwamba hata kama soko la muziki  wa kizazi kipya linalipa, haliwezi kuwa katika kiwango cha kumfikisha Diamond au Dangote katika utajiri huo.

“Kwanza nyie waandishi mjue mtandao unaposema Diamond ana utajiri wa kufikia shilingi bilioni nane ina maana anaingiza bilioni moja na ushee kila mwaka, maana Diamond kushika soko la muziki hasahasa kwa maana ya kuitwa kufanya shoo za pesa nyingi ni kuanzia mwaka 2010.

“Haiwezekani! Hata kama ni huo muziki ndiyo pesa zote hizo? Kwani anafanya shoo ngapi kwa mwaka mzima? Lazima kuna namna hapa. Anaweza kuwa jipu huyu, tunamuomba Magufuli amchunguze,” alisema msomaji mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.

MTANDAO WAMCHANGANUA
Kwa mujibu wa mtandao huo, Diamond anatajwa kwamba analipwa wastani wa shilingi milioni saba na nusu kwa kila shoo. Japokuwa mwenyewe amekuwa mgumu wa kueleza kiwango anacholipwa kwa kila shoo, lakini uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa, huwa inategemea aina ya shoo anayotumbuiza.

KAMA NDIYO HIVYO
Msomaji huyo akaendelea: “Kama utafiti wa mtandao huo ni wa kweli, Diamond kila wikiendi anaingiza shilingi 7, 500,000 si ndiyo? Na mwezi mmoja una wikiendi nne, hivyo anaingiza shilingi 30,000,000 kwa mwezi mmoja yaani 7,500,000 mara wiki nne.

“Sasa mwaka una wikiendi ngapi? Chukua mwezi mmoja milioni 30, mara miezi 12 ni sawa na shilingi milioni 360. Na yeye yuko kwenye gemu tangu 2010. Kwa hiyo kwa miaka hii sita tu ametengeneza vipi pesa za kufikia bilioni moja na zaidi kila mwaka mpaka kuwa na bilioni 8 na kadhaa?


“Unaweza kusema kuna pesa za mikataba ya kampuni za simu, lakini pia mjue hapo kuna kununua magari yake yale, kujenga nyumba Madale. Kujiachia na akina Wema (Sepetu), kumuuguza mama yake na kufanya mambo kadha wa kadha! Hapo tunadanganyana jamani.”

ANALIPA KODI KIHALALI?
Baadhi ya wasomaji pia waliuliza swali jingine ambalo wengi wameendelea kutaka kujua je, kama utajiri wake anaupata kwa njia halali, analipa kodi ya mapato (TRA) kama sheria inavyotaka? Ni kawaida kwa wasanii wakubwa hasa kwa nchi zilizoendelea, kulipa kodi katika kila shughuli za kuingiza kipato wanazozifanya.

Kwa mfano, katika kila shoo anayopiga, Diamond anapaswa kulipia kiwango cha kodi kulingana na kiasi cha fedha alichoingiza.

“Kama kweli hakuna figisufigisu kwenye utajiri wake, atuambie huwa analipa kodi? Mara ya mwisho alilipa lini na alilipa kiwango gani? Huyu jamaa anatakiwa kumulikwa, huenda kuna dili nyingine zinazomuingizia fedha kwa njia zisizo halali halafu anasingizia muziki,” alichangia mchangiaji mmoja kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.

ANAUZA MADAWA YA KULEVYA?
Wapo waliokwenda mbele zaidi na kumhusisha Diamond na biashara haramu ya madawa ya kulevya ‘unga’ kwamba huenda anajishughulisha na biashara hiyo ndiyo maana ‘ametusua’ haraka wakitolea mfano wa Juni mwaka jana alipotaitiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar ambapo walinzi wa uwanja huo walimtilia shaka na kumpekua kutokana na safari zake za mara kwa mara nje ya nchi lakini hakukutwa na unga.

“Unajua hawa wasanii siku hizi wanashiriki sana kwenye biashara ya unga. Wengi wakiwa wanasafirisha madawa wanasingizia kwamba wanakwenda kufanya shoo, mara Afrika Kusini, mara Dubai, Marekani na nchi za Ulaya.

“Diamond siku hizi amekuwa na ‘ruti’ nyingi sana za nje ya nchi, huenda anauza ‘ngada’. Haiwezekani mtoto mdogo awe na fedha nyingi kiasi hicho,” Michael Sabuni, mkazi wa Ubungo- Maziwa, Dar aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu.

ANAHUSIKA NA FREEMASON?
Yapo madai mengine kwamba msanii huyo ni mwanachama wa jamii ya siri ya Freemason inayotajwa kuwapatia utajiri wafuasi wake kwa njia ya makafara na nguvu za giza madai ambayo baadhi ya wasomaji wameyaibua tena kufuatia mtandao huo kumtaja Diamond kwamba anamiliki bilioni 8 kibindoni.

“Mbona kitambo tu watu wanamhisi jamaa kwamba ni Freemason? Unajua ukishajiunga na hawa watu halafu ukafuata masharti yao ya kutoa kafara, kuua watu na kumuabudu shetani, utajiri upo nje nje. Inawezekana hao ndiyo wanaompa jeuri kwa sababu mimi siamini kama fedha zote hizo amezipata kwa sababu ya muziki tu,” alichangia msomaji wetu aliyepiga simu chumba cha habari baada ya kuona taarifa hizo za utajiri wa Diamond mtandaoni.

ANAMTUMIA MWANAYE KAMA KITEGA UCHUMI?
Yapo madai mengine kwamba utajiri wa Diamond unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mwanaye aliyezaa na mwanamama Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’, Latiffa ‘Tiffa’, kwamba tangu kuzaliwa kwa mtoto huyo, makampuni mengi, hasa yanayohusika na biashara ya bidhaa za watoto na mitandao ya simu, yamekuwa yakimlipa mamilioni ya fedha kwa sababu ya kumtumia mtoto huyo kwenye matangazo ya bidhaa zao.



ANAHONGWA NA ZARI?
Swali jingine ambalo wengi wanajiuliza ni kama msanii huyo anahongwa fedha na mpenzi wake, Zari ambaye kabla ya kuanzisha naye uhusiano wa kimapenzi, alikuwa mke wa tajiri wa Kiganda, Ivan Ssemwanga mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini.

“Hakuna cha muziki wala nini, unajua Ivan amemuachia utajiri mkubwa sana mkewe kule Sauzi (Afrika Kusini), anamiliki vyuo mbalimbali, maduka ya urembo na magari mengi ya kifahari. Yeye ndiye anayempa jeuri Diamond, mbona ipo wazi kabisa?” alisema mchangiaji mwingine aliyeomba hifadhi ya jina lake.

MAMA YAKE ANAJUA KILA KITU
Baadhi ya wasomaji walisema kuwa, mama wa Diamond ndiye anayejua utajiri wa mwanaye unatokana na nini kwani inadaiwa kuwa ndiye mwongozaji wake mkubwa.

“Mimi naamini mama Diamond anajua mengi sana. Hawa wamama wa mastaa wamekuwa ndiyo nguzo ya watoto wao kupata pesa. Tunaweza kuumiza vichwa anapata wapi utajiri kumbe mama yake anajua,” alisema msomaji, Isaya Mwarami wa Mabibo, Dar.

DIAMOND ANASEMAJE?
Baada ya kusikia madai hayo ya watu mbalimbali waliokuwa wakiuzungumzia utajiri wa Diamond, gazeti hili lilimtafuta Dangote mwenyewe na kumsomea maswali yote sita ambapo aliguna na kuanza kuyajibu kwa kifupi:

“Sikia braza, hayo wanayoyasema Wabongo hayana ukweli wowote lakini kwa sababu ni kawaida ya Waswahili kuongea mimi nafikiri waache waendelee kuongea lakini ukweli ni kwamba muziki wangu ndiyo ulionifikisha hapa nilipo.

“Nafanya kazi kwa bidii, narekodi ngoma kali, nafanya video zilizokwenda shule, namtanguliza Mungu kwa kila jambo, nina nidhamu ya fedha na sihusiki kwa namna yoyote ile na kujiingizia kipato kwa njia zisizo halali.

“Mimi nafuata sana sheria, ishu ya kulipa kodi, unajua promota anayeandaa shoo ndiye anayetakiwa kusimamia kila kitu. Kwa hiyo mimi akinipa changu, anakuwa tayari ameshakata kodi na mambo ya vibali na kila kitu.

“Ishu ya Freemason siyo kweli bwana, unajua baadhi ya Wabongo wanapenda sana kunizushia mambo. Kuna kipindi walikuwa wanasema natumia uchawi, wameona haitoshi wananizushia Ufreemason na mengine mengi, hakuna kitu kama hicho.

“Nina hofu ya Mungu na yeye ndiye anayeniongoza katika kila ninachokifanya. Mama yangu anajua napata fedha kwa sababu ya kujituma kwangu na si vinginevyo.”

UTAJIRI WAKE MWAKA 2013
Mwaka 2013, alipohojiwa na mtangazaji Zamaradi Mketema wa Clouds TV kwenye Kipindi cha Take One, Diamond alisema utajiri wake, ikiwa ni pamoja na vitega uchumi vyote na fedha zilizopo benki ni zaidi ya shilingi bilioni moja (ikaandikwa kwenye Magazeti Pendwa ya Global Publishers), lakini miaka mitatu baadaye (2016), kwa mujibu wa mtandao huo, utajiri wake umepaa hadi kufikia shilingi bilioni 8.

MALI ZAKE ZA MACHONI
Mpaka sasa, Diamond anamiliki nyumba kubwa ya kifahari iliyopo Madale ambayo inakadiriwa kuwa na gharama ya shilingi bilioni moja. Pia ametumia kiasi kinachoaminiwa kufikia shilingi milioni mia moja kukarabati nyumba ya familia iliyopo Tandale, Dar. Inaelezwa pia kuwa anazo nyumba nyingine mbili zilizopo Kijitonyama na nyingine iliyopo Mwananyamala.

Ana magari matatu, BMW, Toyota Land Cruiser Prado na Toyota Harrier. Anamiliki daladala kadhaa zinazofanya safari zake ndani ya Jiji la Dar na Bajaj. Pia ana mikataba na Kampuni za Vodacom, Samsung, Cocacola na nyinginezo.

Chanzo:Global Publishers

Mrema Ajitokeza Kwa Mara Nyingine Tena Kumkumbusha Rais Magufuli Ampe Kazi Yoyote

$
0
0
Mwenyekiti wa TLP taifa Dkt. Augustino Lyatonga Mrema amesisistiza ombi lake la kazi kwa kumkumbusha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwamba ampe kazi yoyote amsaidie kibarua kigumu alichonacho cha kuwahudumia wananchi

Dkt. Mrema ameyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na EATV kuhusu miaka 32 ya kifo cha aliyekuwa waziri mkuu wa Tanzania Edward Moringe Sokoine ambaye alihudumu kwenye awamu ya kwanza ya Mwl. Julius Nyerere ambapo alifariki akiwa na cheo cha waziri mkuu tarehe 12.04.1984 kwa ajali ya gari.

''Namkumbuka Sokoine kama mtu wa watu aliyehudumia watu, aliyepambana na ufisadi na magendo .Alikuwa anatenda haki kwa wananchi wote .

"Hata mimi nilipokuwa waziri wa mambo ya ndani na naibu waziri mkuu nilijaribu kufanya kama yeye bahati mbaya sikufanikiwa kama yeye kwa sababu sikuwa waziri mkuu au Rais''- Alisisistiza Mrema.

Kuhusu Mrema kuomba kazi kwa Dkt. Magufuli
Mrema alisema kwa kutambua rekodi yake ya utendaji kazi wa  Rais Dkt. Magufuli, aliwahimiza wananchi wa Vunjo wamchague kipindi cha kampeni na yeye akampigia kampeni na Rais akawaambia wananchi wa Vunjo kwamba Mrema akikosa ubunge atapangiwa kazi nyingine ndiyo hiyo wananchi wanaulizia.

Aidha Mrema alisema kuna maeneo ambayo yeye anafiti siyo lazima apewe madaraka makubwa

"Mimi sihitaji ukuu wa mkoa au uwaziri, anipe kazi yoyote na nikionana naye nitamkonyeza maeneo ambayo ninafiti ili nimsaidie kutumbua majipu." Alisema Mrema

Hata hivyo Dkt. Mrema alimpongeza Dkt. Magufuli kwamba ni mtendaji ambaye ameamua bila kusukumwa kupambana na mafisadi na kwamba yeye ni alfa na omega na kazi hiyo ameonyesha kwamba atafanya vizuri kuliko Sokoine na Mrema.

'Sikupendi wala Sikuzimii Marekani..Nimenunua Nyumba South Africa'- Diamond Platnumz

$
0
0
Msanii Diamond Platnumz amefunguka kuhusu suala la yeye kutonunua nyumba nchini Marekani kama wasanii wenzake wakubwa wa Afrika wanavyofanya.

Diamonda amefunguka hilo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na kusema kuwa haoni umuhimu wa yeye kununua nyumba Marekani, tofauti na alivyonunua Afrika Kusini, kwani kule ilimlazimu.

“Nna nyumba South Africa kwa sababu nina familia South Africa kwa hiyo ni lazima ninunue nyumba south Africa, lakini sina sababu ya kusema ninunue nyumba Marekani, ninunue nyumba Marekani kwa sababu gani, kwanza sipapendi, uongozi unajua kabisa”, alisema Diamond.
Pia Diamond aliweka wazi kuwa kununua nyumba Marekani kwake hakuna faida, ni heri awe na kijiji cha nyumba Tandale au Mwananyamala, lakini si Marekani.

“Nyumba sio hela nyingi dola laki mbili kama milioni mia nne unanunua nyumba, so ni matakwa ya mtu mwenyewe, sasa usitake kununua nyumba Marekani wakati trip zako za kwenda Marekani ni chache, usitake kuonekana tu una mashauzi, mara kumi milioni 500 ukanunua nyumba pale Tandale karibuni 10 ukapost nna kijiji Tandale ukazipangisha ukaingiza hela kuliko Marekani”, alisema Diamond.

Muimbaji wa Zamani wa Blue 3 Jackie Chandiru Hoi Kwa Madawa ya Kulevya

$
0
0
Madawa ya kulevya si janga linaloviumizwa vichwa vya wadau wa muziki wa Bongo Flava, bali Uganda pia mambo si mambo.

Muimbaji wa zamani wa kundi la Blue 3, Jackie Chandiru yupo kwenye hali mbaya baada ya kuathirika na utumiaji wa unga. Amekuwa kwenye wakati mgumu zaidi baada ya ndoa yake kuvunjika na sasa yupo rehab huku afya yake ikiwasononesha wengi.

Yupo kwenye kituo cha Bunamwaya ambako madaktari na washauri nasaha wanamsaidia arudi kwenye hali yake ya kawaida. Waliomuona wanadai kuwa hata ngozi yake imeanza kubabuka. Amekuwa akitumia cocaine na madawa mengine.

Askofu Josephat Gwajima Apinga kauli ya mkuu wa Mkoa wa Arusha ya Kutaka kuyadhibiti Makanisa ya kilokole katika Makazi ya watu.

$
0
0
April 5 mwaka huu, mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Daud Felix Ntibenda alitoa amri ya kuyadhibiti makanisa ya kilokole jijini Arusha kwa madai kuwa yanawasumbua wananchi kwa kupiga vinanda na kuimba usiku kucha.

Ntibenda alitoa  amri  hiyo  ofisini kwake   wakati akizungumza na wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji wa mitaa yote ya jiji la Arusha.

Alisema hataweza kuvumilia makanisa hayo kuzinduliwa kila mahali katika makazi ya watu na kufanya ibada usiku kucha.

"Mimi ni mkristo, sikatazi waumini kusali, lakini nataka kuwe na utaratibu maalumu, sio kila kukicha unakuta kanisa jipya na kibaya zaidi yanasumbua hata wageni wanaoingia jijini hapa." Alisema Ntibenda.

Kutokana na kauli hiyo ya mkuu wa mkoa, Askofu Mkuu wa Kanisa na Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima  amejitokeza hadharani kupinga kauli hiyo.

Gwajima amesema Tanzania ni nchi huru, na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, kila mtu ana haki ya kuabudu muda wowote na wakati wowote atakao bila kuingiliwa na mtu yeyote.

Amesema waumini wa makanisa ya kilokole Tanzania wako zaidi ya milioni 11, hivyo kuwazuia kuabudu ni sawa na kutafuta matatizo mengine

Gwajima  amesema waumini wa Kiislam huamka saa kumi usiku kuswali kwa sauti kubwa na hakuna mtu huwaingilia kwa kuwa hiyo ni haki yao kikatiba.

Mwigizaji Ray Atuhumiwa Uchawi, Afunguka

$
0
0
Staa wa filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameingia kwenye kashfa nzito baada ya kudaiwa kutumia ndumba kwenye sanaa ili kuwa juu ya wenzake, Risasi Mchanganyiko limetonywa.

Chanzo kutoka Bongo Muvi kilieleza madai kwamba msanii huyo mwenye jina kubwa, amekuwa ‘akiwachezea’ wenzake ili wasifanye vizuri kwenye soko la sanaa na sasa hivi ndiye anayeongoza kwa mauzo katika Kampuni ya Steps Entertainments baada ya Steven Kanumba kufariki dunia akifuatiwa kwa karibu sana na Stephen Jacob ‘JB’.

Inadaiwa kuwa moja ya viashiria vya ‘ulozi’ huo ni tukio la hivi karibuni lililotokea huko Kigamboni, ambapo tangazo lililowekwa ili kutangaza ujio wa filamu mpya ya JB, kupasuka muda mfupi tu baada ya kuwekwa.

“JB alienda kuweka bango la filamu yake ya Chungu cha Tatu maeneo ya Kigamboni lakini muda mfupi tu likapasuka katikati, lakini alipokuja kuweka Ray la kwake la Tajiri Mfupi lipo mpaka leo, hali imetutisha sana sisi wasanii,” kilisema chanzo hicho.

Chanzo:GPL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images