Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Hivi ni Kweli Kuwa Wenye Herufi "M" Kwenye Kiganja Wana Bahati Sana?

$
0
0
Wengi Tumekuwa tukisikia kuwa watu wenye herufi M kiganjani mkononi ni watu wa bahati...Hapa nimekuwekea ukweli....


HERUFI ''M'' INA ASHIRIA WEWE MTU WA BAHATI KUBWA UNAWEZA KUWA NA PESA NYINGI AU KUWA KIONGOZI MKUU KATIKA MAMBO YA SIASA AU KUWA WEWE MTU MWENYE AFYA NZURI, AU KUWA NI MWANASHERIA AU HAKIMU AU KUWA MTU MAARUFU SANA. HERUFI ''M'' KWENYE KIGANJA CHAKO CHA MKONO WA KULIA INA ASHIRIA MAMBO MAZURI YA MAISHA YAKO YA BAADAE UTAFANIKIWA JITAHIDI.

Hali ni Mbaya Rais John Magufuli Awalaza Njaa Wapiga Dili Mjini na Madalali Waliokuwa Wamejazana Taasisi za Serikali...

$
0
0
Hali ni mbaya! Vita ya ufisadi aliyoitangaza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Pombe Magufuli ‘JPM’ inadaiwa kuwalaza njaa wapiga dili mjini na madalali waliokuwa wamejazana kwenye taasisi za serikali.

Uchunguzi wa gazeti hili kwenye taasisi kubwa zipatazo 20 zilizopo katika wizara mbalimbali zenye makao yake makuu jijini Dar, umebaini kuwa, wale ‘watu wa kati’ kwa sasa hawana dili kwani JPM ameziba mianya yote ya rushwa.

“Kama alivyosema Ludovick Utouh (aliyekuwa Mkaguzi wa Hesabu za Serikali) kuwa serikali na taasisi zake ilikuwa imejaa madalali na mafisadi ni ukweli mtupu.

“Ilikuwa ni vigumu kupatiwa huduma bila kujuana au kuwepo kwa mtu wa kati aliyekuwa pale kwa ajili ya kukamilisha dili, lakini sasa wanapiga tu miayo mitaani. Kweli JPM amenyoosha watu,” alisema mmoja wa wananchi waliojitokeza kupata huduma kwenye Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na kudakiwa na mwingine:

“Kwenye mashirika ya umma hali ilikuwa mbaya mno.
Ndiyo maana tunasema JPM aachwe akomeshe watu kwa sababu ameachiwa nchi iliyooza, yenye sera mbovu za kukumbatia na kuruhusu wapiga dili kuliibia taifa.”
Miezi kadhaa baada ya kuishika nchi, Rais Magufuli alikuwa na kazi kubwa ya kupanga mikakati ya kuijenga Tanzania mpya kwa kupiga vita ufisadi hivyo hata kama kuna wachache wanaolala njaa kwa mkakati wake huo ni heri walale njaa lakini Watanzania walio wengi wapate neema.

Waigizaji Wawili wa Series ya Empire Wafunga Ndoa

$
0
0
Waigizaji na mastaa wa tamthilia ya Empire, Grace Gealey ’31’ na mpenzi wake wa muda mrefu Trai Byers ’32’  wamefunga ndoa kwenye sherehe Alhamis hii, Gealey na Byers walichumbiana mwaka jana baad aya kukutana kwenye show ya Empire.

Mastaa na Wageni 50 tu walialikwa kwenye harusi hiyo kwa mujibu wa mitandao ua udaku nchini marekani.


PICHA:Makamu Wa Rais Mhe. Samia Azindua Mbio Za Mwenge Wa Uhuru Mkoani Morogoro Leo

$
0
0
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amezindua rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru kwenye Uwanja wa Jamhuri Mkoani Morogoro leo.

Katika uzinduzi huo, Makamu wa Rais alimnukuu Baba wa Taifa, Mwl Julius Nyerere akisema kuwa nia ya Mwenge wa Uhuru tangu mwanzo ni kumulika mipaka ya nchi yetu dhidi ya maadui, kuleta matumaini pale ambapo hakuna matumaini, kuondoa chuki pale ambapo kuna chuki na kuleta heshima pale ambapo kuna dharau.

Alisema nia hiyo ya kuwepo kwa Mwenge wa Uhuru kama alivyomnukuu Baba wa Taifa, inaendana na dhana ya kutumbua majipu katika Serikali ya awamu ya tano. Alisema utumbuaji majipu unalenga kuleta matumaini kwa wananchi ambao wamekata tamaa na kuleta heshima kwa wananchi waliodharauliwa.

“Kaulimbiu ya mbio ya za mwenge mwaka huu ni hii: Vijana ni nguvu kazi ya taifa, washirikishwe na wawezeshwe,”alisema Makamu wa Rais na kuongeza kuwa vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa hawajatumika ipasavyo kutokana na sababu mbalimbali.

Alizitaja baadhi ya sababu au changamoto zinazowakabili vijana nchini kuwa ni ukosefu wa ajira, uwezo mdogo wa kuajiri kwenye soko la ajira, ukosefu wa mitaji rafiki kwa vijana, maeneo ya kufanyia kazi pamoja na mitazamo hasi kwa baadhi ya vijana kwa kuchagua kazi.

Makamu wa Rais pia amewataadharisha vijana kutokana na ongezeko kubwa la maambukizi ya ukimwi na matumizi ya madawa ya kulevya.

Amesema vijana wenye umri kati ya miaka 16-24 ndiyo wanaongoza kwa kuathiriwa na maambukizi ya ukimwi.

 Amesema athari za ukimwi na madawa ya kulevya kwa vijana ni kubwa lakini pia zinaongeza mzigo kwa jamii na serikali katika kuwatibu, kuwahudumia na kuongezeka kwa vifo.

Kwa upande wake, Waziri Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, amemtambulisha George Jackson Kijimba kuwa ndiye kiongozi wa mbio za mwenge mwaka huu akisaidiana na wakimbiza mwenge  wengine watano.

 Alisema sherehe za kuhitimisha mbio hizo za mwenge wa uhuru zitafanyika mkoani Simiyu tarehe 14 Oktoba mwaka huu.

Serikali Yakanusha Kuhusu Swala La Leseni Ya Madini Kutolewa Katika Hifadhi Ya Mwiba

$
0
0
Gazeti la Raia Tanzania Toleo Na.0615 la Tarehe 15 Aprili, 2016 liliandika taarifa  yenye kichwa cha habari “Mbunge apewa mgodi hifadhini” huku likieleza kuwa Mbunge wa Meatu, Salum Khamis Salum (CCM), ametumia ushawishi alionao kisiasa kufanikisha upatikanaji wa leseni ya kuchimba shaba katika eneo la Gururum lililomo ndani ya Hifadhi ya Mwiba, Meatu mkoani Simiyu.

Gazeti hilo lilieleza kuwa leseni hiyo ilitolewa na Ofisa Madini Kanda ya Ziwa, Mhandisi Juma Sementa, yenye uhai wa miaka Saba na kwamba upatikanaji wa leseni hiyo haujawaridhisha wadau kadhaa wa ardhi na mazingira kwani mbali na sheria ya kuzuia uchimbaji madini ndani ya maeneo ya hifadhi nchini, wadau wengine hawakuhusishwa katika upatikanaji wake.

Wizara inapenda kutoa taarifa kuwa, wilayani Meatu kuna hifadhi ya Maswa (Maswa Game Reserve) na Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika eneo la Makao (JUHIWAPOMA) ambapo Jumuiya hiyo ilipitisha Mpango wa Kanda za Matumizi ya Rasilimali kwa mwaka 2015-2017 na kutenga eneo la Gururum lenye ukubwa wa kilomita 16.5 sawa na asilimia 2 ya eneo lote, kama kanda ya uchimbaji madini baada ya madini ya shaba kugundulika katika eneo hilo.

Katika eneo hilo la Gururum mpaka sasa jumla ya viwanja 82 vya uchimbaji mdogo wa madini (PML) vimetolewa ambapo kwa sasa hakuna shughuli zozote za uchimbaji zinazoendelea hadi tathmini ya uharibifu wa mazingira (EIA) itakapokamilika ambayo ipo katika hatua ya uwasilishwaji.

Hivyo tunautaarifu Umma kuwa mpaka sasa hakuna mgodi katika hifadhi ya Mwiba na kwamba leseni za uchimbaji mdogo wa madini zimetolewa katika eneo lililorusiwa tu kwa ridhaa ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika eneo la Makao (JUHIWAPOMA).

Tunawaasa waandishi wa habari kuhakiki taarifa wanazotoa katika vyombo vya habari kwa kuwasiliana na wahusika wanaotajwa katika habari husika ili kuepuka kutoa taarifa potofu kwa Umma.

IMETOLEWA NA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
18 APRILI, 2016

Rais Magufuli amteua Mathias Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI​

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua
Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan.

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 18 Aprili 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, imeeleza kuwa uteuzi wa Mheshimiwa Chikawe umeanza tarehe 13 Aprili, 2016.

Kabla ya kupangiwa kituo hicho cha kazi, Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe aliteuliwa kuwa Balozi mnamo tarehe 15 Februari, 2016.

Mheshimiwa Chikawe aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo Ia Nachingwea kati ya Mwaka 2005 na 2015, na kwa vipindi tofauti katika serikali ya awamu ya nne alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dares salaam
18 Aprili 2016

CCM Bunda Waanza Kumsaka Mchawi Aliyefanya Steven Wasira Kushindwa Uchaguzi

$
0
0
Jimbo hilo lilichukuliwa na Esther Bulaya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hivyo kumgalagaza mwanasiasa huyo mkongwe, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM.

Wapiga kura watatu walifunga kesi Mahakama Kuu kupinga ushindi wa Bulaya lakini hata hivyo walishindwa kuthibitisha udanganyifu wowote.

Kutokana na kushindwa huko kwenye sanduku la kura, wanachama wa CCM ‘wanakabana koo’ kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, na miongoni mwa wanaotajwa ni baadhi ya viongozi wake.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa kamati ya siasa ya CCM katika kata ya Nyasura na viongozi wa matawi yake wanakamilisha taratibu za kuwavua uanachama vigogo wanne wa wilaya. Mbali na vigogo hao, CCM pia inataraji kuwafukuza wanachama wanne maarufu.

Katibu Mwenezi wa CCM katika kata hiyo, Frank Mamba alisema wanachama hao wameitwa kuhudhuria kikao kitakachowajadili na kwamba endapo watakaidi wito huo, hatua zitachukuliwa na wao kufikishiwa taarifa rasmi.

"Tumeisha waandikia barua za kuja katika kikao kwa ajili ya kufanya mahojiano ya tuhuma zinazodaiwa na wanachama kupitia vikao vilivyokaa kwa wakati tofauti katika kutathmini matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Octoba 25 mwaka jana,” alisema.

“Kikao cha tawi la Nyasura B kilikaa Desemba 11 mwaka jana na kuazimia viongozi walioshiriki kukihujumu chama waitwe na kamati ya siasa. "Tawi la Nyasura A lilikaa Machi 21 mwaka huu na kupendekeza wafukuzwe uanachama.”

Source: Nipashe

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Katika Magazeti Siku ya Leo


Young Killer Aizungumzia Picha Yake na Diamond

$
0
0
Picha aliyoiweka rapa Young Killer kwenye ukurasa wake wa instagram akiwa na Diamond, imezua maswali kadhaa ya matumaini miongoni mwa mashabiki wake.

Young-Killer-na-Diamond

Rapa huyo wa Mwanza amepost picha akiwa na Diamond Plutnumz na kuandika:

Hakuna mtu aliye zaliwa ili aje awe maskini (ndiyo ) unaweza ukawa umezaliwa kwenye familia maskini ila ukweli ni kwamba hujazaliwa ili wew uje kua maskini….hivyo bas ::mafanikio uja kwa wale walio shindwa mara nyingi na wakajaribu tena kwa ujasiri.. (yes) mungu nisaidie yatimie .. with MSAFI @diamondplatnumz

Baada ya post hiyo iliyoibua maswali mengi, Bongo5 ilimtafuta Young Killer na kuzungumzia swala hilo.

“Hakuna kitu chochote kinachoendelea, nimepost tu,” alisema Young Killer. “Kama ikitokea nimesaini mtasikia. WCB ni label kubwa na kila mtu anatamani kufanya nayo kazi, kwa hiyo ikitokea nikajiunga pale ni jambo la heri sana,”

Bongo 5

Navy Kenzo ni mfano wa kuigwa kwa wasanii waliokata tamaa kwenye muziki

$
0
0
Navy Kenzo ni kundi linaloundwa na wasanii wawili, Aika na Nahreel.

Hakuna asiyejua kuwa Aika na Nahreel ni wapenzi kwa muda mrefu kabla hawajaingia kwenye kiwanda cha muziki wa Bongo Fleva.

Mwanzo kabla ya kutengeneza kundi la Navy Kenzo walikuwa kwenye kundi la Pah One ambalo walifanikiwa kuachia nyimbo kadhaa kama, ‘Ghetto’ na ‘I Wanna Get Paid’.

Aika na Nahreel walifanikiwa kuachia nyimbo kadhaa wakati wanaanza ndani ya Navy Kenzo ambazo hazikufanikiwa kufanya vizuri na kupenya kwenye ngoma za masikio ya mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva.

Nawapongeza kwa uvumilivu wa muda mrefu, na sasa wanaanza kuona faida ya muziki wao. ‘Game’ ni nyimbo ambayo hawataisahau kwa maisha yao yote. Ujasiri wao wa kuwekeza hela nyingi kwenye video ya wimbo huo na kufanikiwa kufanya video nzuri chini ya Justin Campos ulivifanya vituo mbalimbali vya TV barani Afrika vicheze wimbo huo.

Mwaka mmoja kabla walionekana ni kama wasanii wa kawaida sana na hawatofika popote, lakini ‘no one knows tomorrow’ leo wamekuwa wakubwa na wameshaanza kupata jina Afrika kutokana na muziki wao wa tofauti na video nzuri zinazobamba kwenye TV.

‘Game’ ilikuwa ni direction nzuri iliyoisafishia njia ‘Kamatia Chini’ nayo ikiwa na video kali ambayo inafanya vizuri kwenye chati mbalimbali za TV kubwa Afrika. Mungu hamtupi mja wake, Aika na Nahreel kwa sasa ni mabalozi wa Airtel ambapo wamefanikiwa kuingiza mkwanja mrefu kutoka kwa kampuni hiyo ukiachana na lile dili alilolipata Nahreel ndani ya Coke Studio mwaka jana.

Wasanii wengi wanatamani kufanya kazi kwenye studio za The Industry Music kwa sasa kutokana na hit nyingi zilizotoka ndani ya studio hiyo.

Kama msanii hutakiwi kukata tamaa ukitaka kufanya vizuri na kama kweli una kipaji ukiwasoma Aika na Nahreel hakika utapata nguvu ya kufanya muziki na kuwa na imani utafika mbali. Japo hawajafika mbali sana na pale inapotakiwa lakini kwa hatua walioipiga Aika na Nahreel hakika wanahitaji pongezi. Ni nguvu zao binafsi wamezitumia hadi kufika hapo walipofika leo.

Hongereni Aika na Nahreel, hakika miaka kadhaa ijayo tunategemea kuwaona mkiwakilisha mbali zaidi muziki wetu wa Bongo Fleva.

Magufuli Atahadharishwa kwa Kauli yake ya Bora Kula Mihogo Kuliko Mkate wa Masimango

$
0
0
Baadhi ya wasomi na wanasiasa wamemtahadharisha Rais John Magufuli kuhusu kauli yake ya kupinga misaada yenye mashariti magumu aliyoifananisha na mkate wa masimango.

Akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya kwanza ya juu (flyover), inayojengwa katika makutano ya Barabara za Mandela na Nyerere, kwenye eneo la Tazara juzi, Rais Magufuli aliita misaada ya wahisani ‘mkate wa masimango’ na kusema kuliko kula mkate huo ni bora kushindia muhogo.

Hiyo ni mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kuzungumzia misaada yenye masharti tangu Shirika la Changamoto ya Milenia (MCC) la Marekani, kusitisha msaada wa Dola za Marekani milioni 472.8 karibu Sh1 trilioni, zilizokuwa zitumike kuongeza kasi ya usambazaji umeme.

MCC ilisitisha msaada huo ikilalamikia uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, ukisusiwa na Chama cha Wananchi (CUF).

Akizungumzia kauli hiyo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alisema ni jambo jema kwa Watanzania kujitegemea, lakini kwa sasa haijawezekana moja kwa moja.

“Mimi nilishasema kwamba, jambo la kujitegemea ni jema, tunatakiwa kujifunza kujitegemea, lakini kwa sasa bado hatuna uwezo, tunatakiwa tujiandae,” alisema Msigwa na kuongeza:

“Hata bajeti iliyopita tulipunguza utegemezi kwa asilimia kadhaa. Hata mtoto mchanga anapozaliwa anaanza taratibu… kulikuwa na uzembe mwingi uliofanyika serikalini, unatakiwa kushughulikiwa.”

Alisema licha ya kuunga mkono dhana ya kujitegemea, Msigwa alionya tabia ya Serikali ya Magufuli kuwaghasi watumishi wa umma na watu wasio na hatia.

Naye mhadhiri wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Richard Mbunda alisema ni muhimu Rais Magufuli kuwa makini katika utekelezaji wa kauli yake hiyo.

“Inabidi awe makini sana jinsi anavyotekeleza mipango yake na jinsi anavyofanya kazi na wafadhili. Ni dhahiri kwamba kuna miradi bado inaendelea na hata hizo barabara nyingi alizosimamia yeye mwenyewe akiwa waziri zilikuwa zinafadhiliwa na wafadhili,” alisema Mbunda.

Alisema mbali na barabara, kuna miradi mingi inafadhiliwa na nchi wahisani ikiwamo ya umeme, hivyo inahitajika diplomasia ya uchumi ili kuendeleza uhusiano huo.

Kwa upande wake Profesa wa  Siasa wa Chuo Kikuu cha Iringa, Gaudence Mpangala aliunga mkono dhana ya kujitegemea, lakini amekubaliana na sababu za Marekani kukatisha msaada kutokana na utata wa uchaguzi wa marudio wa Zanzibar.

Alisema misaada haina shida kwa sababu inachochea maendeleo, lakini tukio la Zanzibar limechafua taswira ya Tanzania.

TFF Yalaani Kitendo cha Mashabiki wa Simba Kuwarushia Mawe Viongozi na Wachezaji wa Simba Baada Kufungwa na Toto

$
0
0
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limelaani kitendo cha baadhi ya mashabiki wa mpira wa miguu kufanya vurugu mara baada ya mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Toto Africans uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

TFF imesikitishwa na kitendo hicho cha mashabiki wa klabu ya Simba SC, na kusema inalaani kitendo hicho ambacho sio cha kiuana michezo, huku ikiwataka wanachama, washabiki kuheshimu viongozi wa klabu zao waliopo madarakani na kama kuna masuala ya kujadili wakayajadili katika vilabu vyao.

Mashabiki wa klabu ya Simba walifanya vurugu kwa kurusha mawe, wakilenga kuwadhuru viongozi wa klabu hiyo pamoja na wachezaji, magari waliyokuwa nayo baada ya timu yao kupoteza mchezo dhidi ya Toto Africans kwa bao 1- 0.

Jeshi la Polisi baada ya kuwasishi mashabiki kuondoka eneo la uwanja punde tu mchezo ulipomalizika, mashabiki hao walikaidi na kuendelea kurusha mawe hali iliyopelekea jeshi kutumia mabomu ya machozi kuwatanya katika eneo hilo.

Kufutia kitendo hicho, Jeshi la Polisi lilihakikisha bus la timu ya Simba SC na viongozi wake wanaondoka salama uwanjani baada ya kuwatawanya mashabiki hao, kwa kupitia mlango wa karakana ya wachina waliojenga uwanja huo.

Aidha TFF imeviomba vyombo vya Usalama na Ulinzi kuwachukulia hatua kali mashabiki waliohusika na kitendo hicho, kwani kufanya vurugu ni kosa la jinai na wanapaswa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Tanzia: Aliyekuwa Mkurugenzi wa BOT Amatus Liyumba afariki dunia

$
0
0
Aliyekuwa Mkurugenzi na Utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania ( BOT), Amatus Liyumba amefariki dunia, msiba uko nyumbani kwake maeneo ya Triple Seven, Mikocheni jijini Dar.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peoni

Rais Magufuli ateua Mkuu Mpya wa Wilaya ya Kinondoni kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Paul Makonda

$
0
0
Add caption
Rais Magufuli ateua Mkuu Mpya wa Wilaya ya Kinondoni kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Paul Makonda

Mwananchi Ampiga Jiwe Polisi Kwenye Paji la Uso Mpaka Kuzimia...

$
0
0
Jeshi la polisi Mkoani Manyara linamshikilia mkazi wa Kijiji cha Dongobesh Wilayani Mbulu, Mussa Selemani (28) akidaiwa kumpiga jiwe kwenye paji la uso askari polisi wa kituo cha polisi Dongobesh na kusababisha akapoteza fahamu.

Hadi hivi sasa askari polisi huyo ambaye alipigwa jiwe hilo wakati akiwa kituoni amelazwa kwenye hospitali ya rufaa ya Haydom, amepoteza fahamu na anaendelea kupatiwa matibabu huku akiwa na jeraha katika paji la uso wake.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Francis Massawe alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa kwenye kijiji hicho baada ya kumpiga jiwe askari huyo akiwa kituoni na kisha kukimbilia kusipojulikana.

Kamanda Massawe alimtaja askari polisi huyo kuwa ni PC Boniface mwenye G 8404 na tukio hilo lilitokea Aprili 15 mwaka huu saa 3 usiku wakati akiwa kwenye kituo cha polisi cha Dongobesh.

Alisema siku ya tukio hilo PC Boniface alikuwa anaandika maelezo ili awapatie fomu namba 3 (PF3) ya matibabu wazazi wawili waliofika na mtoto wao mwenye miaka 7 kituoni hapo kwa ajili ya kutibiwa wakidai kuwa alipigwa.

Alisema wakati akiandika maelezo hayo ndipo Selemani akatokea akiwa amelewa na kuingilia kati mahojiano hayo hivyo kusababisha usumbufu ndipo PC Boniface akamtoa nje kwa nguvu ili aweze kuendelea na kazi yake ipasavyo.

“Wakati PC Boniface anaendelea kuandika maelezo ya watu hao, ghafla Selemani alimpiga jiwe na kupoteza fahamu kisha akakimbizwa kwenye hospitali ya rufaa Haydom kwa matibabu,” alisema Kamanda Massawe.

Alisema baada ya tukio hilo Selemani alikimbia na wale watu wawili na mtoto wao nao wakakimbia ila polisi walifanikiwa kumkamata mhalifu huyo na askari huyo amelazwa hospitali ya rufaa ya Haydom na hali yake siyo nzuri bado hajitambui.


Rais Magufuli Azua Taaruki Jijini Leo..Aenda Bank ya CRDB na Gari Binafsi Bila Msafara...

$
0
0
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amezua taharuki mjini leo baada ya kufika katika Tawi la CRDB (Holland Branch), akiwa kwenye gari binafsi lenye namba T 182 DFQ huku likiwa halina nembo ya adamu na hawa wala bendera.

Tukio hilo lililochukuwa takribani dakika 25, limetokea majira ya saa nne asubuhi ya leo jijini Dar es Salaam katika tawi la benki hiyo ambalo liko katika makutano ya Barabara ya Ohio na Samora bila kutarajiwa.

Mara baada ya Rais Magufuli kufika katika eneo liliko tawi hilo makutano ya barabara hizo yalifungwa huku ndipo rais aliposhuka kwenye gari  na kuingia ndani ya benki hiyo.

Wakati akikaribia kuingia ndani ilibidi baadhi ya wateja waliokuwa wakijiandaa kuingia ndani ya benki hiyo  wazuiwe kuingia huku huduma ikiendelea tu kwa wale ambao walikwisha ingia.

Aidha, baada ya kuingia ndani baadhi ya wateja wa tawi hilo na wananchi wengine walibaki wakishangaa huku wengine wakijiuliza imekuwaje Rais kuingia benki kwa staili ile kwani baadhi ya wananchi walidai kuwa hawajaona tukio kama lile kwa marais wote waliopita.

James Charles, ambaye ni dereva wa Texi, alisema baadhi ya wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo baada ya kuona ulinzi unaimalishwa walishtuka huku wasijue ni nini kinaendelea, hadi pale walipomuona Rais Magufuli akishuka kwenye gari hali iliyowafanya wafikirie anakwenda kutembelea ofisi yake ya zamani.

“Lakini kufumba na kufumbua tukamuona anaelekea kwenye benki ya CRDB tukajiuliza vipi rais leo kaamua kuwa kama mteja hata hivyo hatujui kama hiyo ilikuwa inawezekana. Lazima kutakuwa na kitu haiwezekani aende akachukue fedha kwa utaratibu ule ngoja tusubiri tutasikia amefuata nini,” alisema Charles.

Joyce Godwin ambaye ni mwanafunzi wa chuo kimojawapo cha elimu ya juu, alisema kuja kwake kumewashtua wafanyakazi wa tawi la benki hiyo kwani walidhani alikwenda pale kwa ajili ya kutumbua majipu.

“Mimi wakati Rais Magufuli anaingia nilikuwepo ndani kwenye foleni nikisubiri huduma kwa ujumla kila mmoja wetu alishtuka lakini hatukujua kilichomleta,”alisema.

Baada ya Rais Magufuli kumaliza kazi yake iliyompeleka alitoka na kuingia kwenye gari huku akiwapungia mkono wananchi.

Taarifa Kuhusu Daraja Jipya la Kigomboni Kufungwa Kesho Kwa Muda

$
0
0
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inapenda kutaarifu Umma kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe ya ufunguzi wa Daraja la Kigamboni kesho, Jumanne tarehe 19 Aprili, 2016.

Kutokana na ufunguzi huo, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inawataarifu watumiaji barabara na Wananchi wote wanaotumia daraja hilo kuwa huduma ya magari kutumia daraja hilo itafungwa kwa muda kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana ili kuwezesha kufanyika kwa sherehe hiyo ya ufunguzi wa daraja. Aidha, huduma katika Daraja la Kigamboni itarejea kama kawaida kuanzia saa 8:00.

Daraja la Kigamboni lililoanza kutumika tarehe 16 Aprili, 2016 lina urefu wa mita 680 na barabara unganishi (approach roads) upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilometa 2.5.

Imetolewa na;
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
18 Aprili, 2016.

Oparesheni ya Kuwaondoa Ombaomba Jijini Dar es Salaam Yagonga Mwamba..... Polisi Wapanga Mikakati Mipya

$
0
0
OPERESHENI ya kuondoa ombaomba katika jiji la Dar es Salaam imegonga mwamba kutokana na kukinzana na baadhi ya mamlaka katika kuwaondoa watu hao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam leo , Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam (CP),Simon Sirro amesema kuwa operesheni ya kuondoa omba omba imeshindikana kutokana na baadhi ya mamlaka kushindwa kuhusishwa.

Amesema kuwa wanaendelea kujipanga kwa kuhusisha mamlaka zote ili kuweza kutekeleza operesheni hiyo kwa ufanisi.

Amesema kuwa kuna omba omba wengine wameweza kuondoka baada ya tangazo kutolewa hivyo waliobaki waondoke kwa savabu operesheni itakayoanza haitaangalia uso wa mtu.

Jeshi Polisi limeweza kukusanya zaidi ya sh. Milioni 911 ambazo zimekusanywa kutokana na makosa mbalimbali ya magari  pamoja na pikipiki katika jiji la Dar es Salaam.

Kamanda Sirro amesema kuwa hawajisifii kukusanya fedha hizo, nia yao ni kuona watu hawafanyi makosa ya usalama barabarani.

Wakati huohuo Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata jambazi sugu, Shaban Ramadhan (35) ambaye alikuwa anamiliki bunduki mbili za kivita SMG na risasi nane.

Kamishina Sirro amesema kuwa walipata taarifa kutoka kwa watu juu ya mtu huyo kumiliki silaha ambapo alikutwa na silaha moja huku moja ikiwa kwa rafiki yake wa kike, Fatuma Salehe (20).

Aidha jeshi la polisi limeonya wananchi kununua gari katika sehemu zinazotambulika  kutokana na kuibuka uhalifu wa watu kuuza gari zisizo kuwa zao.

Ali Kiba na Diamond Wazipige Ngumi ili Tujue Kama Kweli Wana Beef – Mzee Yussuf

$
0
0
Mzee Yussuf ni miongoni mwa wasanii ambao hawaamini kama Diamond na Ali Kiba wana beef kutokana na wawili hao kutokutana pamoja na kuonyesha tofauti zao.

Akizungumza  Jumamosi hii, Mzee Yussuf amesema beef ya Diamond na Ali Kiba zinakuzwa na mashabiki lakini sio beef kweli.

“Mimi Ali Kiba na Diamond sidhani kama wana beef kweli,” alisema Mzee Yussuf. “Bado siamini kwa sababu ni watu ambao hawakutani tukaona kama kweli ni beef kweli zikapigwa ngumi watu tukaona,”

Aliongeza, “Kwenye taarab kuna beef za kweli, watu wanazipiga kweli. Mimi naamini wanaume hawanuniani,”

Katika hatua nyingine Mzee Yussuf amesema anajipanga na wasanii wenzake kuanzisha umoja wa wasanii wa taarab ili na wao waweze kupeleka kero zao kwa pamoja.

Mwanaume Shoga Aamua Kukiri Redioni Kufanya Biashara Hiyo...Aangua Kilio na Kuelezea A to Z Jinsi Alivyoanza....Ataka Kuacha

$
0
0
Morogoro: My confession! Katika hali isiyo ya kawaida, kijana Karimu Said (25) almaarufu Anti Karimu aliyekiri kufanya biashara haramu ya kuuza mwili (ushoga), ameangua kilio redioni wakati akiutangazia umma wa Watanzania kuachana na dhambi hiyo aliyodumu nayo kwa miaka saba.

Ilikuwa Alhamisi iliyopita, Karimu alifika katika ofisi ndogo za gazeti hili za mkoani hapa na baadaye alitinga kwenye Kipindi cha Mcharuko wa Pwani cha Radio Planet FM kinachoendeshwa na mtangazaji mahiri, Warda Makongwa akishirikiana na Farham Abraham.

Lengo la Karimu lilikuwa ni kutubu dhambi yake hiyo sambamba na kumuomba msamaha Mwenyezi Mungu na Watanzania kwa jumla.

Akiwa hewani laivu kwenye kipindi hicho na watangazaji hao na mwandishi wetu, Karimu alisimulia kilichomwingiza kwenye ushoga kuwa ni umaskini uliotokana na vifo vya wazazi wake.

“Baada ya wazazi wangu kufariki dunia na mimi kumaliza darasa la saba hapa Morogoro, nilikwenda Dar kutafuta kazi. Nilipofika nilipata kazi ya ndani (house boy) kwa bosi mmoja.

“Nikiwa hapo, bosi wangu wa kike na wanaye walikwenda likizo kijijini, mimi nilibaki na bosi wa kiume.

“Siku moja huyo mwanaume alinirubuni akanipeleka beach (ufukweni) na baadaye Mlimani City ambako alinilazimisha kunywa pombe.

“Tuliporudi nyumbani aliniingilia, tangu hapo kila siku akawa akinifanyia hivyo. Mkewe aliporudi alinikanya nisimwambie, nikajikuta namuonea wivu huyo mwanaume hata akiwa na mkewe.

“Hali hiyo ilisababisha mkewe kujua na kunitimua,” alisema Karimu.
Alisema kuwa baada ya kutimuliwa alirejea kwao Morogoro na kuendelea na ushoga akijiuza kwenye madanguro yaliyopo ltingi na Kahumba mjini hapa.

Alipoulizwa wateja wake wakubwa ni watu gani, Karimu alifunguka kuwa ni waume za watu wakiwemo baadhi ya vigogo wa serikali.

Mwandishi wetu alipomtaka kuelezea changamoto alizokumbana nazo, alifunguka huku akiangua kilio studio: “Changamoto ni nyingi zikiwemo za kupigwa, kupata bwana akakulipa elfu arobaini lakini ukifika geto kwake, ukishamhudumia, anakugeuka na kukunyang’anya fedha.

“Nimeyatafakari matukio yote hayo, ndipo nikaungana na rafiki yangu aliyenipeleka kanisani ambako niliombewa hadi nikaanguka, nikapoteza fahamu, nilipozinduka nikajiona niko kwenye ulimwengu mwingine na kujutia dhambi hiyo ya ushonga, hivyo naomba Mungu na Watanzania wanisamehe,” alisema Karimu huku akilia.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images