Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Mkuu Mpya wa Wilaya Kinondoni Akataa Sherehe ya Pongezi na Kuomba Pesa Hizo zichangie Madawati

$
0
0
Mkuu wa Wilaya Mteule wa Kinondoni amekuwa na kikao na Mkurugenzi Mkuu wa Clouds Media Group Bw. Ruge Mutahaba.
Pia Alipewa nafasi ya kusalimia kwenye kikao cha Management ya Clouds.

Kikubwa Zaidi DC wa Kinondoni Ameandaliwa Sherehe ya kupongezwa na Akakataa Sherehe hiyo na kuwaomba Garama hizo za Sherehe kwa maana ya Chakula na Vinywaji Wachangie Madawani kwa wilaya ya Kinondoni.

Kisha alipata wasaa wakuzungumza ktk Kipindi cha Leo Tena.



Mchuano wa Waziri Kitwanga na Zitto Kabwe Wafika Pabaya..Zitto Adai Sio Size Yake na Aache Mchezo wa Kuwatuma Vijana wa UVCCM Kumchafua

$
0
0
Kiongozi Mkuuwa Chama cha Allience for Change and Transparency(ACT), Zitto Zuberi Kabwe, ameibuka na kujibu mashambulizi juu ya taarifa zinazoenezwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga kupitia Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) za kumhujumu Rais Dk. Magufuli katika utendaji wake.

Kiongozi huyo amesema anaushahidi wa moja kwa moja juu ya vitendo vinavyofanywa na Waziri huyo katika kueneza propaganda zinazolenga kuiyumbisha Serikali .

“Nina ushahidi usio na mashaka wa Kitwanga kupanga Vijana wanaojiita wa UVCCM kufanya mikutano na Waandishi wa Habari na anawalipa fedha kufanya hivyo, nataka ieleweke wazi kuwa nina muunga mkono Rais katika kazi ya kusafisha Nchi … nitakuwa mtu wa ajabu nisipo muunga mkono katika vita dhidi ya ufisadi” amesema Zitto Kabwe.

Zitto amemtaka Waziri Kitwanga kuepuka siasa za porojo na kusema waziri huyo si ‘size’ yake na hana mpango wa kumtoa katika nafasi ya uwaziri hivyo aache kulalamika na kueneza uzushi.

“Kimsingi nashangaa mtu kama yeye (Kitwanga) kuweza hata kuwa Waziri wa Wizara nyeti kama hiyo, zaidi ya yote Waziri Kitwanga sio ‘size yangu’. Naanzaje kuhangaika na Kitwanga? Ili iweje? Namsihi asijipandishe chati kwamba mimi nataka kumtoa (uwaziri) . Ningetaka kumtoa wala asingejua maana ningeshughulika na aliyemteua” Amesisitiza Kabwe.

Hata hivyo Kabwe amemtaka Waziri Kitwanga kujipima kama bado anastahili kuendelea kukaa katika nafasi yake ya uwaziri kutokana na kashfa ya kampuni anayo imiliki iitwayo Infosys kwa kushirikiana na Kampuni ya Lugumi kuiingizia Serikali hasara ya shilingi bilioni 34 kupitia Zabuni ya kununua vifaa vya kutekeleza mradi wa utambuzi wa vidole kwenye Vituo vya Polisi nchini.

“Nawasihi Watanzania wote kumdharau Waziri Kitwanga nakumtaka ajibu tuhuma zinazomkabili za kampuni yake binafsi kufanya kazi na Idara katika Wizara anayosimamia na kwamba ajipime kama anatosha kuendelea kumsaidia Rais kazi.” Aliongeza Kabwe.

MREMA Atoa Mpya..Aamua Kumfuata Magufuli Dar es Salaam ili Ampe Kazi..Adai Kuna Majipu Anayajua Akayasafishe

$
0
0
Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha TLP na aliyekuwa mgombea Ubunge wa jimbo la Vunjo, Agustino Mrema anatarajia kusafiri kuja jijini Dar es salaam kwa lengo la kumpongeza Rais Magufuli na kumkumbusha ahadi aliyompa mwaka jana ya kumpatia kazi Serikalini.

Akizungumza kupitia kipindi cha Sun Rise kinachoruka kupitia Times fm, Mrema amempongeza Rais kwa jitihada za ukusanyaji kodi na kupambana na Ufisadi kwa nguvu.

“Tuweke itikadi pembeni Rais wa sasa anaweka juhudi katika kukusanya kodi, na mimi nilikuwa napiga nalo sana kelele hili swala, ila akipewa ushirikiano baada ya miaka mitano tutasheherekea mafanikio yake.

“Wiki ijayo natarajia kuja Dar, na nafikiri nitaonana na Rais kwanza nimpongeze alafu nimsisitize anipe nafasi kuna sehemu nazijua tuzisafishe, siwezi kusema mpaka nionane nae ndio nitamueleza”.

Mrema pia alijivunia rekodi yake ya uongozi katika Serikali ya Tanzania, kama kigezo kimoja wapo cha kumpatia ‘Chambirecho’ ya kupewa nafasi katika Serikali ya Magufuli.

Mwili Uliozama na Gari Baharini Jijini Dar es Salaam Wapatikana

$
0
0

Mnamo majira ya saa 10 alfajiri, gari aina ya Hiace  iliteleza toka kwenye kivuko na kutumbukia katika bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam.

Gari hiyo ilikuwa na abiria wawili. Mpaka majira ya asubuhi, jeshi la zimamoto na uokoaji lilifanikiwa kuupata mwili mmoja na likaendelea kuutafuta mwili wa pili.

Mchana  huu  umepatikana mwili wa pili  wa Nice Karagwe  huku zoezi la kuitoa gari likiendelea

Mwimbaji Ben Paul Apata Mtoto wa Kiume..Mwenyewe Aficha ila Mama Mtoto Aweka Picha Mtandaoni

$
0
0
Ni kwasababu tumebaini kuwa mfalme huyo wa R&B kama anavyojiita ni baba wa mtoto wa kiume mwenye miezi kadhaa sasa!

Muimbaji huyo wa ‘Ningefanyaje’ amepiga kimya lakini sio rahisi kwa mama aliyejifungua kuificha furaha ya kupata mtoto. Mchumba wa Ben Pol, Latifa Mohamed aka Queen Tipha aliyewahi kuwa mshindi wa pili kwenye Miss Tanzania 2013 ametusogeza karibu na mtoto wao. Tazama picha za Tipha na mwanae

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Atumbua Watumishi Watano Ilemela Kwa Tuhuma za ubadhirifu wa Fedha za Umma

$
0
0
Mkuu wa wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amewasimamisha kazi maofisa watano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma na matumizi mabaya ya madaraka.

Akiwa katika ziara ya siku moja ya kujitambulisha wilayani Ilemela leo, Mongella ameagiza kushushwa cheo kwa ofisa wa ardhi wa wilaya hiyo, Anicet Rweyemamu kwa tuhuma za kushindwa kusimamia watumishi walio chini yake wanaotuhumiwa kupokea Sh12 milioni kutoka kwa mwananchi mmoja aliyekuwa akitaka ardhi, lakini hajapewa hati hadi sasa.

Wengine walioangukiwa na rungu la mkuu huyo ni Debora Tongora ambaye pamoja na Alex Chigulu wanatuhumiwa kupokea fedha hizo kutoka kwa wananchi kwa ahadi ya kuwapatia viwanja.

Wakati Tongola tayari amefunguliwa mashtaka dhidi ya tuhuma hizo, Chigulu amehamishiwa mkoani Singida lakini Mongella ameagiza arejeshwe Mwanza ili afikishwe mahakamani.

“RPC wasiliana na mwenzako wa Singida ili huyo mtumishi atiwe mbaroni muda huu na kesho arejeshwe Mwanza kukabiliana na mashtaka dhidi yake. Hatuwezi kuwavumilia watumishi wanaoharibu sehemu moja halafu wanakimbia uhamisho kwenye maeneo mengine,” amesema Mongella

Ofisa uvuvi wa Kituo cha Kirumba, Ivon Maha ameshushwa cheo huku Peter Revelian akiondolewa kutoka nafasi ya mweka hazina.

Watumishi hao wa Idara ya Uvuvi wameondolewa madarakani baada ya kutuhumiwa kuhusika na upotevu wa zaidi Sh40 milioni zilizotokana na kodi na ushuru.

Awali, Mkuu wa wilaya ya Ilemela, Manju Msambya alimweleza Mongella kuwa wilaya hiyo tayari imetengeza madawati 7, 200 kati ya 29, 000 yanayohitajika.

“Wilaya yetu inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa walimu katika shule za umma na tayari tumewasilisha maombi ya walimu wapya,” amesema Msambya

Meya wa Manispaa ya Ilemela, Renatus Mulungi alimuahidi mkuu huyo wa mkoa kuwa baraza lake litaongeza juhudi katika usimamizi wa utendaji kwa watumishi wa halmashauri hiyo.

Wastara Afunguka, Asema kuvunjika kwa ndoa yake na mbunge Sadifa kumempa Amani

$
0
0
Msanii wa filamu Wastara Juma amefunguka na kuzungumzia kuvunjika kwa ndoa yake na Mbunge wa Donge kupitia CCM Sadifa Khamis Juma ambayo imeduku kwa kakribani miezi 3.

Akizungumza na Bongo5 hivi karibuni, Wastara amesema mahusiano ya mapenzi ni kama mtu anavyoishi na rafiki yake, mkizinguana maachana.

“Binafsi kwa sababu ni muda mchache naumia kuwakarahisha mashabiki wangu kwa sababu hawamchukulii Wastara katika stori hizo au katika muonekano huo,” alisema Wastara. Lakini kwa upande wangu naona ni bora zaidi nilivyotoka mapema kwa sababu pengine ingeniathiri nikashindwa kufanya kazi zangu na kulea wanangu,”

Wastara alisema hawezi kuzungumzia chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yake kwa kuwa yale ni maisha yake ya ndani.

Pia Wastara amesema bado umri wake unamruhusu kuingia tena kwenye mahusiano, ukifika wakati amempata mtu sahihi ataolewa tena.

SIMANZI: Msanii Bongo Muvi Afariki Dunia Akijifungua Hospitalini

$
0
0
Ni simanzi! Nyota ya msanii Leila Gabriel ‘Lissa’ ambayo ndiyo kwanza ilikuwa imeanza kuchomoza kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, ilizimika ghafla mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya msanii huyo kupoteza maisha muda mfupi baada ya kujifungua kwenye Hospitali ya St. Benard, Kariakoo jijini Dar es Salaam. 

Nafasi za Kazi Bonyeza: www.ajirayako.com

Shamsa Ford: Sina time na Nay wa Mitego, tukionana ni vikumbo tu

$
0
0
Shamsa Ford na Nay wa Mitego ni pua na moshi. Shamsa Ford amesema akikutana na Nay wa Mitego hawezi salimiana naye kutokana na mambo ambayo walifanyiana.

Mwigizaji huo wa filamu aliwahi kukiri kwamba hawezi toka tena kimapenzi na staa, ikiwa ni muda mchache toka aachane na Nay wa Mitego.

Akizungumza na Bongo5 hivi karibuni, Shamsa alisema Nay sio mshikaji wake tena na yaliyotokea kati yao anayachukulia kama ni sehemu ya maisha ambayo alitakiwa kuyapitia ili ajifunze.

“Hukana mkorofi tuliamua tu mahusiano yetu yafike mwisho. Hamna tena ushikaji tena wala ‘ucousin’ ulishaisha kila mtu ana maisha yake, tukionana vikumbo tu,” alisema Shamsa.

Katika hatua nyingine Shamsa amewatakama mashabiki wa filamu zake kuifuatilia filamu yake mpya iitwayo ‘Najuta Shamsa’.

Nafasi za Kazi Bonyeza: www.ajirayako.com

Chris Brown Akiri Alitaka Kujiua Kwa Sababu ya Penzi la Rihanna

$
0
0
Chris Brown amesema alitaka kujiua baada ya kumshambulia aliyekuwa mpenziwe Rihanna kabla ya tuzo za Grammy mwaka 2009.

Katika kipande kifupi cha makala yake ya ‘Karibu katika maisha yangu’,mwanamuziki huyo wa mtindo wa R & B amesema uhusiano wao ulikuwa kama ndoto lakini akajihisi kama hayawani.

“Nilikuwa katika kilele cha dunia,nyimbo zangu zikiongoza,nikapendwa na wengi nchini Marekani kabla ya kuanguka hadi kuwa adui wa umma,” alisema Chris Brown.

Kesi yake ilisitishwa mwaka jana baada ya jaji mmoja kusema kuwa nyota huyo amekamilisha mahitaji yake yote na kufunga kesi hiyo rasmi.

Pia kwenye makala hiyo inayowaonyesha Jennifer Lopez,Usher,Mike Tyson,Jamie Fox na Rita Ora, Chris Brown anasema, “Nilihisi kama nyota, lakini nilijiharibia. Nilikuwa nikilala.Sikuweza kula,nilijihisi maarufu,” alikiri.

Source: BBC

Atupwa Jela Miaka Saba Baada ya Kujerui Watu Wawili Kwa Kutumia Wembe..

$
0
0
 Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kifungo cha miaka saba jela fundi umeme, Lipyana Ndumbaro (29) baada ya kupatikana na hatia ya kujeruhi kwa kutumia wembe.

Mahakama pia imemtaka Ndumbaro kumlipa fidia ya Sh2 milioni mlalamikaji.

Ndumbaro ambaye ni mkazi wa Mvuti wilayani Ilala, hakuwapo mahakamani hapo wakati hukumu hiyo inatolewa baada ya kuruka dhamana.

Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, John Msafiri alisema Mahakama imemtia hatiani mshtakiwa huyo baada ya kuridhika na ushahidi wa mashahidi saba uliotolewa mahakamani hapo.

Hakimu Msafiri alisema Mahakama ilipokea vielelezo vitatu ambavyo ni picha, maelezo ya mgonjwa na fomu namba tatu ya Polisi (PF3).

“Kupitia ushahidi huu, Mahakama imeridhika na ushahidi wa upande wa mashtaka uliotolewa mahakamani hapa bila kuacha shaka,” alisema Hakimu Msafiri.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu, Wakili wa Serikali, Neema Moshi aliiomba Mahakama kutoa adhabu kali ili liwe fundisho kwa watu wengine wanaofanya vitendo kama hivyo.

Katika hati ya mashtaka, ilidaiwa mshtakiwa alitenda matukio hayo kwa watu wawili tofauti.

Ilidaiwa Machi 17, 2014 maeneo ya Mvuti wilayani Ilala, alimkata kwa wembe Watunde Abdallah sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia maumivu.

Pia, tarehe na mwaka huohuo, alimkata kwa wembe Shaban Kivanga na kumsababishia maumivu.  

Soma Nafasi za Ajira Hapa: www.ajirayako.com 


Rais Magufuli Azidi Kumng’ang’ania Kilango Baada ya Idadi ya Watumishi Hewa Shinyanga Kuongezeka Hadi 226

$
0
0
Rais John Magufuli ameendelea kumng’ang’ania aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango baada ya kusema idadi ya watumishi hewa katika mkoa huo imeongezeka kutoka 45 hadi 226.

Aprili 11, Rais Magufuli alitengua uteuzi wa Kilango kwa kosa la kutangaza kuwa mkoa huo hauna watumishi hewa, lakini ikabainika baada ya Ikulu kufanya uchunguzi wake kuwa kulikuwa na watumishi hewa 45.

Akizungumza juzi wakati wa uzinduzi wa Daraja la Nyerere Kigamboni, Rais Magufuli alisema amekuwa habahatishi kila anapokuwa akichukua uamuzi wa kutumbua jipu.

Alitoa kauli hiyo dakika chache baada kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe na kusema hatakuwa na mzaha katika utumbuaji wa jipu.

Alisema Watanzania wameteseka sana hivyo wanatakiwa kutumikiwa.

Huku akishangiliwa na maelfu ya wakazi waliokuwa eneo hilo, Rais Magufuli alikumbushia msimamo wake kuhusu Shinyanga akieleza kuwa hadi leo (juzi) kuna wafanyakazi hewa 226, mahali ambako walisema wafanyakazi ni sifuri, hivyo kuwaomba viongozi ambao wanataka kufanya kazi na Serikali yake wajipange kuyaondoa mabaya yaliyo kwenye maeneo yao akisema wananchi wameteseka mno.

Makonda hajaridhika watumishi hewa 71 Dar

Jana, akizungumzia suala hilo la watumishi hewa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliwaagiza wakuu wa wilaya za Temeke, Kinondoni na Ilala kusimamisha shughuli zao kwa muda ili kulivalia njuga suala la watumishi hewa kwani bado hajaridhika na watu 71 waliopatikana hadi sasa.

Akizungumza wakati akizindua kampeni ya upasuaji watoto wenye tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), Makonda alisema tayari watumishi hewa 34 katika Wilaya ya Kinondoni wameshafunguliwa jalada.

“Nalipongeza jeshi la polisi kwa kumkamata mtu mmoja ambaye alikuwa anajipatia mshahara kwa njia ya udanganyifu, mpaka sasa yupo mikononi mwa vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua anazostahili kuchukuliwa,” alisema.

Makonda alisema Dar es Salaam ni miongoni mwa mikoa yenye watumishi wengi wajanja hivyo idadi ya walio hewa aliyonayo kwa sasa hawezi kuitangaza mpaka itakapokamilika, huku akitoa maagizo makuu matatu.

“Wengi wanaonekana wapo kazini, kumbe wanafanya shughuli nyingine, mwisho wa siku wanajiingizia kipato, nikaomba kuongezewa muda mbele ya Waziri (George) Simbachawene (Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi), kadri tunavyoendelea idadi inazidi kuongezeka, tumeona ni vyema kuujulisha umma hatua ambazo tumeanza kuzifanya,” alisema.

Alisema ameiomba Utumishi kumpatia utaalamu zaidi ili wajanja wanaopenya wapate nafasi ya kuwabaini mapema.  


Nafasi za Kazi Bonyeza: www.ajirayako.com

TUCTA Yapinga Mpango wa Rais Magufuli Kukata Mishahara ya Watumishi wa Umma Kutoka Milioni 40 hadi 15 Kwa Mwezi

$
0
0
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (Tucta) limepinga mpango wa Rais John Magufuli wa kukata malipo ya mishahara ya watumishi wa umma kutoka Sh40 milioni kwa mwezi hadi Sh15 milioni.

Akizungumza na viongozi wa vyama vya wafanyakazi Kanda ya Ziwa jijini Mwanza jana, Naibu Katibu Mkuu wa Tucta, Hezron Kaaya alisema uamuzi huo ni kinyume na sheria na utaligharimu Taifa iwapo wahusika wataamua kwenda mahakamani kupinga mishahara yao kupunguzwa.

“Watendaji hawa hawakujipangia mishahara wao wenyewe, bali malipo haya yalipangwa na bodi za mashirika na taasisi husika ambazo kisheria zimepewa mamlaka hayo. Malipo haya hayawezi kupunguzwa kwa kauli za kisiasa bila kuzingatia mahitaji ya kisheria,” alisema.

“Iwapo Serikali itatekeleza lengo hili bila kuwapo mjadala mpana na makubaliano ya kisheria kati ya wahusika, basi ijiandae kulipa mamilioni ya fedha kama fidia iwapo watakaokatwa mishahara yao watakwenda mahakamani.”

Akiwa mjini Chato wakati wa mapumziko ya wiki moja, Rais Magufuli alitangaza kupunguza mishahara ya juu kutoka Sh40 milioni hadi Sh15 milioni kwa mwezi, akisema wapo watumishi wa umma wanalipwa masilahi manono na kuishi kama wako peponi, huku wanaolipwa Sh300,000 wakiishi kama wako jehanamu.

Kaaya aliishauri Serikali kuendelea kuwalipa mishahara hiyo minono wahusika hadi mwisho wa mikataba yao, ndipo lengo la kuipunguza litekelezwe ama kwa kuwapa wahusika mikataba mipya au kuajiri watu wengine.

“Serikali inaweza kuwa na nia njema kupunguza tofauti kubwa ya mishahara kati ya kada ya juu na chini, lakini utekelezaji wake lazima usubiri muda mwafaka mikataba ya sasa itakapomalizika,” alisisitiza.

Katika hatua nyingine; Tucta imepinga hatua zinazochukuliwa na baadhi ya mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya ya kutangaza kuwasimamisha kazi watumishi wa umma ambao hawapo chini ya mamlaka zao kinidhamu.

Ushindi Mwingine Mnono wa Timu ya Genk Huu Hapa..Mbwana Samatta Acheza Dakika 75

$
0
0
Usiku wa April 20 2016 kocha wa KRC Genk Peter Maes kaendelea kumuamini na kumpa nafasi ya kuanza katika first eleven yake nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania anayeichezea klabu hiyo Mbwana Samatta, Maes amempa nafasi Samatta ya kuanza mchezo wa pili mfululizo.

Licha ya kuwa KRC Genk walikuwa nyumbani katika uwanja wao wa Cristal Arena kukabiliana na vinara wa Ligi hiyo Club Brugge, Maes kamuamini Samatta na kumpa nafasi katika mchezo huo mgumu ulio malizika kwa KRC Genk kuibuka na ushindi wa goli 4-2. Samatta amecheza kwa dakika 75 na dakika ya 76 alitoka akaingia Nikolaos Karelis.

Samatta anakuwa amefikisha jumla ya mechi tatu alizoanza akiwa na KRC Genk katika mechi hizo amefunga mechi mbili goli moja moja katika kila mchezo, magoli ya KRC Genk ya leo yamefungwa na Onyinye Ndindi dakika ya 15, Alejandro Melero dakika ya 42, Thomas Buffel dakika ya 45 na Jeren Uronen dakika ya 73.

Kwa Sasa Genk Inashikilia Nafasi ya Nne Katika Ligi hiyo


Nafasi za Kazi Tembelea www.ajirayako.com

Wanawake Kumbukeni na 'IKULU' Zenu Kinyume Chake Mtaachwa Kila Siku...

$
0
0
Kujiremba jirembeni na uzuri kuweni nao. Mashauzi tuleteeni na kutusumbua ongezeni. Saluni msikose na wa natural wasiishe. Vaeni vizuri na mtembee na muongee kwa maringo.Lakini msizisahau ikulu zenu. Wengi wenu huzisahau sana sehemu zao.

Inafikia wakati zinatoa harufu kama kafa panya au umezibua choo. Uzuri wa mwanamke ni huko ndani. Si vinginevyo mabinti nyinyi. Ziosheni ikulu zenu mara kwa mara hasa mnapokwenda haja au kufanya mapenzi. Msiingize chochote huko zaidi ya Abdala kichwawazi. Kinyume chake ni majanga. Na mtaachwa kila siku hadi mbadilike.

Nimewaacha watatu kwa sababu hiyo.Siwezi kukaa na mchafu tena wa sehemu muhimu kwake na kwangu. Afadhali leo nimewaambieni nami nitapata utulivu moyoni mwangu.
Ujumbe huu ni kwa wanawake wote

By Sonda

Tetesi ya Siri Nzito Kati ya Diamond na Mrembo Aliyecheza Kwenye Video ya Raymond Kwetu Hii Hapa

$
0
0
Kupitia Mtandao wa Instagram Siri Nzito nzito zinaendelea kuwekwa wazi kuwa kuna siri nzito kuwa Mwanamuziki Diamond Platnumz anatoka na mrembo Officiallyyn ambaye ameonekana kwenye video ya Msanii mpya wa WCB Raymond kwenye wimbo wake Kwetu....Chanzo cha habari hii kinasema Diamond na Msanii huyo walianza kutoka muda toka mwaka jana...Inasemekana imefikia mpaka mrembo huyo amejichora Tattoo ya Simba mgongoni kwake ambalo ni jina la analojiita Diamond..
Inasemekana Mrembo huyo Lyyn kwa Sasa anapokea michambo ya nguvu na Vitisho kutoka kwa Team Zari huku...Moja ya Kitisho ni Hichi hapa Chini kutoka Instagram

Wakati wengine wakirusha madongo kwa Diamond na Mrembo huyo Wengine wanampongeza Diamond kwa kuopoa kitu kizuri....
Soma Huyo Alichoandika:
Nataka_shari 
"UMEJUA KUCHAGUA
Asanteeeeeee @diamondplatnumz c kwa uchaguzi huu kabla hujampata huyu ndo MZURI uliyemmiss kwa hawarakikongwe unakuza tuu mtoto wa jirani yetu_ila mnambemenda mtoto we unapiga mama anachakazwa bila kukaedit katoto kanatia hurumasema video queen moyoni ashakutia DOA na hulitoi hata kwa jiki hahaa ila domo unaroho mbaya video queen umempangia mjengo katulia tuli Bibi nae ungempangia gheto south aache habari ya ntombe nilale huyu video queen wa msanii wako RAY n saluuuuutemtoto Hana makunyanzi usoni kama hawarakikongwe bila kuedit picha kuwa ya njano hapost @zarithebosslady unaswaga za kitoto unaedit picha kama upinde wa mvua tokea lini we Ukawa rangi sawa na majani yaliyopigwa juahahaha yamebaki mapenz ya insta moyoni network haisomi hureee wapi Lyn Mkali wako @zarithebossladyDOMO WE NI MFUNGWA ULIYESHINDIKANA UNAIBA MPK JELA SIJUI WATAKUFUNGA WAPI"

Tanzania ya Rais Magufuli na Kenya ya Rais Kenyata ziko Katika Vita Baridi?

$
0
0
Ni ukweli kuwa uhusiano wetu na Kenya haujawahi kuwa wa "mahaba" (tukitumia msemo wa Lowassa). Tumekuwa tukivumiliana kwa maslahi ya kiuchumi tangu enzi za mwalimu. Hata hivyo tangu awamu ya tano ianze uhusiano wetu na Kenya unatia mashaka na ni vema tukaongelea jambo hili objectively.

Mambo yalianza na Magufuli kuchaguliwa kuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM. Ikaelezwa viongozi wa serikali ya Kenya walipata hofu kwa vile Magufuli ana urafiki na kiongozi wa upinzani.

Likaja suala la njia ya Bomba la Mafuta. Magufuli akaongea na Mseveni na kukawa na uwezekano mkubwa kuwa Uganda itachagua njia ya Tanzania badala ya Kenya. Suala hili halikuifurahisha Kenya hata kidogo. Kwa sababu ya ushindani wa njia ya bomba la mafuta wakati fulani waziri mmoja wa kenya na maafisa wake walizuiliwa uwanja wa ndege Tanga.

Jambo jingine la kuchekesha ambalo wakenya waliandika ni wakati wa mkutano wa marais wa EA ambapo Magufuli aliongea ki-luo mbele ya Kenyatta. Media ya Kenya ikachukulia ni kejeli kwa Kenyatta kwa vile rafiki wa Magufuli ni M-luo.

Tukio jingine dogo ni la binti wa rafiki mkubwa wa Magufuli kusema kuwa Olduvai Gorge iko Kenya. Media ya Tanzania ikalipuka kwa kulaani. Hii inatokana na historia ya Kenya kuitangaza Kilimanjaro kuwa iko kwao.

Katika mtazamo huohuo juzi wakati anafungua Daraja la Nyerere (Kigamboni) Rais Magufuli aliwasha moto mwingine kwenye media ya Kenya kwa kusema "wale wanodhani kila jambo jema liko kwao wameanza kuandika...walisema Kilimanjaro ni yao, Olduvai Gorge ni yao, n.k" . sasa hivi hii kauli iko katika headings za media za Kenya: "Magufuli fires shots...", "Magufuli hates Kenya with a passion"...n.k

Posts za wakenya kwenye blogs na online newspapers sio positive kama mwanzo wakati Magufuli kaingia madarakani. Watu wanatutukana. Wanauliza tuna nini zaidi ya Kiswahili na hili daraja la Kigamboni. Wanaona serikali ya Magufuli imedhamiria kuifanya Tanzania iwe Juu ya Kenya.

Kuna umuhimu viongozi wetu kwa makusudi wafanye bidii ya kuondoa hii hali ya vita ya maneno. Ile tabasamu Magufuli na Kenyatta wanaonyesha wakikutana iwe pia tabasamu kati ya watu wetu na media zetu.

Magufuli Calls Kenyans ‘Thieves and Liars’ While Opening Kigamboni Bridge (VIDEO)

$
0
0
From Nairobiwire.com

Tanzanian President John Magufuli yesterday officially opened Kigamboni Bridge, East Africa’s first cable-stayed bridge or as normal people call it – suspension bridge.

It was a great moment of pride for their country and rightly so as the piece of infrastructure will make life easier and improve business in Dar es Salaam.


On Monday, we published an article on the bridge opening.

 Kigamboni Bridge: Tanzania Has Just Built East Africa’s Longest Suspension Bridge

It received well over 100,000 hits with most of them from Tanzania. What followed was a bunch of sarcastic social media posts from Kenyans proclaiming the bridge to be in Kenya.



It seems Tanzania’s leadership took notice.

While unveiling the Kigamboni Bridge, now named Nyerere Bridge, President Magufuli just came short of calling Kenyans thieves.

“This is the only bridge of its kind in East and Central Africa. Go to Uganda, Kenya, DRC, there’s no bridge like this one,” he said.

“And that’s why those who think everything good is in their country have started writing. They said Mt. Kilimanjaro is theirs, Olduvai gorge etc.” he said, referring to a few isolated cases of Kenyans who have been ‘stealing’ their natural resources and lying to the world about it.

Raila Odinga’s daughter Rosemary Odinga was recently under fire from the Tanzanians for claiming Olduvai gorge is in Kenya at an international forum. Ironically, the Odingas’ are very close to the Magufulis’.

While most tweets from Kenyans about Kigamboni bridge were sarcastic or satirical, Tanzanians did not see it that way. They believed this was a coordinated effort to steal their shine and glory, like we’ve always done.

Magufuli’s statement was just a continuation of the rivalry between the two nations in more than a few issues.

Watch him launch the thinly veiled attack on Kenya from around minute 5:20.

Deni la Taifa Laongezeka Mara Dufu, Upinzani Washtuka Wataka CAG Kufanya Ukaguzi

$
0
0
DENI la taifa limeongezeka maradufu, hali ambayo imeifanya kambi Rasmi ya Upinzani kushtuka na kumtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalum.

Ongezeko hilo, kwa mujibu wa kambi ya upinzani, deni hilo limeongezeka kwa kiasi hivyo, kutoka mwaka 2010 hadi mwaka jana.

Akiwasilisha maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu utekelezaji wa Mpango wa Kwanza wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2011/12 hadi 2015/16 na mwelekeo wa Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2015/16 hadi 2020/21, Naibu Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Wizara ya Fedha na Mipango, David Silinde, alisema hali ya deni la taifa inatisha na Bunge linapaswa kushituka.

Silinde alisema nchi itafilisika kama Ugiriki ikiwa Bunge halitachukua hatua madhubuti za kuisimamia serikali.

Alisema deni la taifa limekuwa na kufikia dola za Marekani bilioni 19.141 (Sh. trilioni 41.536). Alisema deni liliongezeka maradufu mwaka jana, baada ya serikali kukopa dola bilioni 3.846 (Sh. trilioni 8.347).

"Mwishoni mwa Juni, 2010, jumla ya deni la Tanzania lilifikia dola bilioni 9.9 (Sh. trilioni 13.6) kulingana na thamani ya dola kipindi hicho). Miaka mitano baadaye deni limefikia Sh. trilioni 41.5, lazima Bunge tushituke," alisema Silinde.

"Fedha zilizokopwa kuanzia 2010 hadi 2015 zilifanyia miradi ipi ya maendeleo? Mikopo hii ina riba kiasi gani, tumeweka nini kama dhamana ya kupatiwa mikopo au ile minong'ono mitaani ya vitalu vya gesi?

"Mkopo mkubwa wa mwaka 2010 ambao ni sawa na asilimia 5.9 ya deni lote ulitumika kufanyia jambo gani? Fedha hizi zimetumika kugharamia miradi gani au ndiyo EPA ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015?

"Majibu ya maswali haya yatapatikana tu kama itafanyika 'Special Audit' ya deni la taifa. Mkopo huu ni hatari zaidi kama hautalipwa kwa wakati kwani riba itaongezeka maradufu na kuifanya nchi ifilisike.

"Kwa sababu hiyo, Kambi Rasmi ya Upinzani inamtaka CAG kufanya ukaguzi maalum wa deni la taifa na kuleta taarifa ya ukaguzi huo bungeni kwa ajili ya kujadiliwa,” aliongeza.

Serikali yakubali

Akizunguma na Nipashe nje ya ukumbi wa Bunge jana mchana, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, alisema serikali iko tayari CAG afanye ukaguzi huo kwa kuwa fedha hizo zilitumika kwa miradi mbalimbali ya maendeleo.

"Wizara yangu haina kipingamizi, CAG aje atukague. Deni la taifa lipo tangu kipindi cha uongozi wa (Mwalimu Julius) Nyerere. Tunakopa fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Tutamwonyesha CAG miradi iliyotekelezwa," alisema.

Awali, akieleza kuhusu Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2015/16 hadi 2020/21, Silinde alilitaka Bunge kutunga sheria ya utekelezaji wa mpango huo kwa maelezo kuwa bila kufanya hivyo hautatekelezeka kama uliopita.

Mbunge huyo wa Mbozi Magharibi (CHADEMA), alisema mpango uliopita, ulikuwa na lengo la kujenga barabara kwa kiwango cha lami Km 5,204 (kila mwaka Km 1,040.8) ndani ya miaka mitano, lakini zilizojengwa ni Km 2,775 (kila mwaka Km 555), sawa na asilimia 53 ya lengo.

"Mwalimu Nyerere aliondoka (madarakani) mwaka 1985, aliliachia Shirika la Ndege (ATCL) ndege 11, lakini kwa sasa linamiliki ndege 'zero' (sifuri), ilhali likiwa na wafanyakazi wengi wanaolipwa kodi za wananchi," alisema.

Kuhusu reli, Silinde alisema serikali iliweka lengo la kukarabati Km 2,707 kwa kiwango cha 'standard gauge', lakini hadi sasa imekarabati Km 136 tu (wastani wa Km 27.2 kwa mwaka). Ili kutimiza malengo ya miaka mitano ya Km 2707, Silinde alisema serikali itatumia miaka 99.5.

Kweye kilimo, Silinde mpango uliopita ulikuwa na lengo la kukuza kilimo kwa asilimia sita kwa mwaka, lakini sekta hiyo imekuwa kwa asilimia 3.4 kwa kipindi chote cha miaka mitano, huku akidokeza kuwa mpango huo haukuleta matokeo chanya katika sekta ya elimu.

Kadhalika, katika mpango uliopita, Silinde alisema lengo lilikuwa kuzalisha Megawati 2,780 za umeme ndani ya miaka mitano, lakini katika kipindi chote zimeongezeka MW 496.24, hivyo Tanzania itahitaji miaka 13 kufikia malengo ya mpango wa kwanza.

Source: Nipashe

Umoja wa Vijana CCM Wamjibu Zitto Kabwe Baada ya Kuwatuhumu Kumchamfua Kwa Kutumwa na Waziri Kitwanga

$
0
0
UVCCM NI TAASISI IMARA HAIWEZI KUTUMIKA NA MTU KINYUME NA MASLAHI YA CHAMA AMBAYO PIA NI MASLAHI YA  NCHI.

Nimeona taarifa ya Kaka Zitto kabwe akielezea hoja zake kwa msingi wa kukana kumhujumu Rais Magufuli na kuwa waliotoa taarifa hizo wanatumiwa na mmoja wa Mawaziri ( ) wa Serikali ya awamu ya tano.

Kaka Zitto ameenda mbali zaidi akiandika,namnukuu
 “maneno hayo yanaenezwa na watu wanaotumwa na Waziri(anamtaja jina) nina ushahidi usio na mashaka wa waziri( ) kupanga vijana wanaojiita wa UVCCM kufanya Mikutano  na waandishi wa habari na anawalipa fedha kufanya hivyo” mwisho wa nukuu.

Mosi, nimpongeze Mh. Zitto Kabwe kukana kwa sauti ya juu kabisa kuwa hampingi Rais Magufuli na anamuunga mkono katika Ujenzi wa Nchi kama alivyofanya kwa Serikali ya awamu ya nne.Kama ni kweli na lipo kwa matendo Ni jambo jema sana kwa maslahi ya nchi yetu ambalo wapinzani wengine wanapaswa kuliiga.

Pili,Nimthibitishie pasi na shaka ndugu Zitto Kabwe kuwa Vijana hao kama alivyosema (wanajiita wa UVCCM) ni wanajiita tu. Vijana wa CCM kama Jumuiya imara ya Vijana wa Tanzania haiwezi kutumika na kulipwa pesa na mtu ili kutumika kwa maslahi binafsi. Na kwa kuwa ndugu Zitto amelisema jambo hili kwenye umma na kuwa anao ushahidi wa hao wanaojiita wa UVCCM, tupo tayari kushirikiana nae na ikithibitika kuchukua hatua zaidi kwa mujibu wa Kanuni yetu, vinginevyo tunaona jina la Jumuiya yetu linatumika kama Nyanya kwenye mboga za watu,na hatutakubali hilo.

Tatu. UVCCM inaimani kubwa na Rais Magufuli kuwa hawezi kuwa mtetezi wa Majipu ata kama mwenyejipu kwa madai yako ni rafiki yake, na UVCCM ni kisu cha kumsaidia Rais kutumbua majipu hayo. Lakini tunajua kuwa Rais Magufuli ni Rais makini katika atua anazochukua pasi na kumuonea mtu, kwa kuwa  kutumbuliwa jipu kunamaumivu makali sana yanayoweza kuvumiliwa tu na mwenye jipu, asiekuwa na jipu hawezi kutumbuliwa.

Hivyo kama kweli tuhuma hizo zinazotolewa kwa Waziri huyo zina ukweli na zinahusu rushwa na ufisadi Rais angeshamtumbua waziri ama atakuja kumtumbua tu ikishathibitika, tusiwe na haraka,"haraka haraka haina baraka"

MWISHO.
Ushauri kwa kaka Zitto Kabwe, kwa kuwa yeye ni Mbunge na Waziri anaemtuhumu anaingia Bungeni basi ni vizuri akatumia jukwaa hilo kuweka ushahidi wa hoja zake ili zipate majibu ya kina na anaetuhumiwa, kwani nae atakuwa na fursa ya kujibu kwa hoja na ushahidi. UVCCM tunachotaka ni mazingatio ya maslahi ya watanzania hasa wengi ambao bado ni masikini.

Tumeendelea mara zote kuwaomba kupata habari sahihi za jumuiya na kuepuka uzushi unaofanywa mara kwa mara kuichafua jumuiya yetu,

UVCCM utoa taarifa zake kwa utaratibu wake wa kanuni chini ya Mwenyekiti SADIFA JUMA HAMIS kama msemaji Mkuu ama Makamo Mwenyekiti wake Bi.MBONI MHITA ama Kaimu Katibu mkuu SHAKA HAMDU SHAKA

au Kaimu katibu wa Idara ya Uhamasishaji, Sera, Utafiti na Mawasiliano MR Abubakar Asenga,pia
Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu MFAUME KIZIGO

Kaimu Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Ndugu ABDUGHAFAR IDRISSA
ama itakavyoelekezwa vinginevyo

Kwa lolote wasiliana nasi kwa
email.uvccm1978@gmail.com
simu - 0627 968 722 AU 0222150743.
imetolewa na.
Abubakar D. Asenga
Kaimu Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji,Sera,Utafiti na Mawasiliano
UVCCM MAKAO MAKUU
S.L.P 19989
DAR ES SALAAM.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live




Latest Images