Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live

Breaking News :Rais Magufuli Ateua Makatibu Tawala wa Mikoa 26

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.


Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kati ya Makatibu tawala hao 10 ni wapya, 2 wamebadilishiwa vituo vya kazi na 13 wamebakisha katika vituo vyao vya sasa.


Makatibu Tawala wapya walioteuliwa ni kama ifuatavyo;


    1.Arusha -    Richard Kwitega

    2.Geita -      Selestine Muhochi Gesimba

    3.Kagera -     Armatus C. Msole

    4.Kilimanjaro -     Eng. Aisha Amour

    5.Pwani -      Zuberi Mhina Samataba

    6.Shinyanga -   Albert Gabriel Msovela

    7.Singida -     Dr. Angelina Mageni Lutambi

    8.Simiyu -    Jumanne Abdallah Sagini

    9.Tabora -   Dkt. Thea Medard Ntara

   10.Tanga -    Eng. Zena Said


Makatibu Tawala waliobadilishwa vituo vya kazi ni kama ifuatavyo;


1.Kigoma -   Charles Amos Pallangyo (Kutoka Mkoa wa Geita)

2.Morogoro -  Dkt. John S. Ndunguru (Kutoka Mkoa wa Kigoma)


Makatibu Tawala waliobakishwa katika vituo vyao vya sasa vya kazi ni kama ifuatavyo;


    1.Dar es salaam -  Theresia Louis Mbando

    2.Dodoma -     Rehema Hussein Madenge

    3. Iringa -   Wamoja Ayubu Dickolagwa

    4.Katavi -    CP Paul Chagonja

    5.Lindi -   Ramadhan Habibu Kaswa

    6.Mara -   Benedict Richard Ole Kuyan

    7.Manyara -     Eliakimu Chacha Maswi

    8.Mbeya-    Mariam Amri Mjunguja

    9.Mtwara -    Alfred Cosmas Luanda

   10.Mwanza -  CP. Clodwing Mathew Mtweve

   11.Njombe -   Jackson Lesika Saitabau

   12.Rukwa -   Symthies Emmanuel Pangisa

   13.Ruvuma -   Hassan Mpali Bendeyeko


Makatibu Tawala wa Mikoa 10 ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza, wataapishwa siku ya Jumatano tarehe 27 Aprili, 2016 saa tatu asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam.


Gerson Msigwa

Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

Dar es salaam

25 Aprili, 2016

Aina Mpya ya Uwizi wa Magari Dar es Salaam...Soma Hapa Uwe Makini

$
0
0

Gari imeibiwa jana , 23/4/2016 Shopper plaza- Mikocheni, mida ya saa 9 mchana.Ni Volkswagen Tourge, Blue color... Kama umeiona au unajua ilipo au unajua chochote tafadhali piga number hii ‪+255 715 066 278‬ au toa ripoti polisi.
.
Hii story ntaiandika in full ili na wengine muwe makini mnapokuwa mnauza magari. Dada alieibiwa alitaka kushare ili isije kumtokea mtu mwingine. Na tafadhali kama unajua lolote kuhusu hili gari pls piga 0715 066 278‬
.
Story iko Hivi. Gari ilipostiwa www.kupatana.com . Jumamosi akapigiwa simu na muhindi Kuwa kaipendaKufika muhindi akampigia akasema yuko busy Ila Fundi wake ataangalia gari, basi Fundi akafika akaangalia gari akaongea na muhindi akaondoka. Baadae accountant akampigia wakutane waangalie contract. Accountant kufika akatoa mkataba feki then akamuuliza Fundi si alitest drive gari? Akasema Hapana aliangalia tu. Basi akajifanya kupanick Yani hajatest drive ?akampigia muhindi, muhindi akampigia huyo dada anajifanya kahamaki Fundi wake haki test drive wakati yeye anajua VW zina Tatizo la shock up . Basi wakapanga wakutane Kesho yake ambayo ndo jana Kwa ajili ya kutes5 drive na kulipana kabisa.
.
Kesho yake dada wa watu akaenda shoppers plaza. Accountant akaja wakaingia wote kwenye gari wakadrive kidogo. Basi wakapaki accountant akamrudishia dada funguo yake wakashuka, akamwambia muhindi nae keshafika shoppers anataka aone mwenyewe so yeye anaenda kumtafuta upande wa pili wa shoppers then anakuja nae so awasubiri pale juu Art Cafe. . Dada wa watu akawa amekaa anawasubiri. Kasubiri mpaka kachokaaaaaa, jamaa hajarudi. Kuchungulia chini gari yake haipo.
.
.
Sasa unajua kaibiwaje?siku ya kwanza Fundi wa gari alipokuja alikuwa kaja kuangalia funguo wa gari ukoje. Wakaenda kutengeneza similiar looking key. So siku alipoibiwa jamaa alivyosema anataka kutest drive gari ni kwamba alitaka tu funguo ya gari. Then akamrudishia funguo fake ambayo imefanana na yake, Then wao wakabaki na original
.
.
Number aliokuwa anatumia muhindi ni 069 271 3707 na imesajiliwa TIGo Kwa Jina la Aleej Khimji. Number ya accountant ambae ndo aliiba gari alisema anaitwa Omar ni +255 715 936 985 na number ya Fundi aliejiita Joseph ni +255 715 937 547

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Leo Katika Magazeti na Mitandao ya Kijamii

Raymond Asimulia Jinsi Alivyomshawishi Diamond Hadi Kumchukua WCB (Video)

$
0
0
Raymond amesimulia jinsi ambavyo alimshawishi Diamond hadi kuamua kumchukua kwenye label yake, WCB.

Ameiambia Bongo5 kuwa alipigiwa simu na mshkaji wake, Maromboso aende studio kuungana naye katika kusikiliza wimbo wa Diamond aliokuwa anataka mawazo ya watu wengi.

“Brother Diamond akifanya ngoma anapenda management yake, kuanzia madancer, mameneja wote waweze kusikiliza wimbo wake. Katika hiyo crew ya watu waliokuwepo Maromboso akapendekeza na mimi niwepo,” amesema.



Anasema baada ya kumshauri vitu kadhaa Diamond aligundua ana kitu cha ziada na kumuuliza kisa cha kutotoka hadi muda huo. Amedai kuwa Diamond alimuomba nyimbo zake azisikie na akawa anamshauri vitu vya kurekebisha. Aliendelea kurekodi nyimbo kwenye studio mbalimbali na kuwa anamtumia hadi alipofungua studio ya WCB.

Anasema kuwa kwenye studio hiyo alirekodi nyimbo nyingi kali zilimchanganya Diamond na uongozi wake hadi wakashindwa watoi upi.

Ray ameongeza kuwa Bado ilitoka kwa mbinde kwakuwa kulikuwa na nyimbo zingine kali sana. Mtazame hapo chini kumsikia akielezea.
Chanzo:Bongo5

Mirror Chini ya Management ya Wema Sepetu Umewaangusha Mashabiki Wako, Utawalipa Nini?

$
0
0
Marehemu Albert Mangwair alikuwa mtu wa mwanzo kutambua kipaji cha muziki alichokuwa nacho Mirror pamoja na Jordan.

Kwa mara ya kwanza watu walimtambua kwenye nyimbo yake ‘One and Only.’ Kiukweli huu ni wimbo mzuri ambao unaweza kuwarudisha karibu watu waliotengana kwenye mahusiano pindi watakapousikiliza wimbo huo.

Bahati ya mwenzio usiilalie mlango wazi, shukrani za dhati zimuendee Wema Sepetu aka Madam Sepetunga, aliyefanikiwa kumchukua Mirror na kuanza kusimamia kazi zake za muziki chini ya kampuni yake ya ‘The Endless Fame’.

Miaka inazidi kwenda lakini bado hatujamuona yule Mirror ambaye tulimtarajia atakuja kuwa ni miongoni kati ya wasanii watakao hit ndani hadi nje ya Tanzania.
Ni takribani miaka mitatu mpaka sasa tangu Mirror awe chini ya menejimenti hiyo na tayari ameshafanikiwa kuachia nyimbo kadhaa kama, ‘Hapo Ulipo’ na ‘Naogopa’.

Japo ameweza kuwa chini ya menejimenti yenye uwezo mkubwa wa kupata support na uwezekano wa kufanya vizuri lakini hali imekuwa ngumu kwa Mirror na kila siku anapoachia wimbo anazidi kuonekana ni kama msanii anayechipukia.

Nahisi inaweza ikawa kama hadithi ya sungura na kobe. Angalia alipotoka Baraka Da Prince mpaka leo amekukuta hapo hapo ulipo umelala usingizi mzito na amezidi kukuacha.

Sitaki kuamini kama ni kweli umeridhika na mafanikio ya huu muziki, hebu angalia wasanii wengine waliopata mafanikio zaidi lakini bado wanaendelea kupambana zaidi.

Ukiangalia mwanzo wakati anaanza, alifanikiwa kupata mashabiki wengi ambao walitarajia kuwa atakuja kufanya makubwa lakini kumbe’ Umdhaniaye ndiye kumbe siye’.

Muda bado upo bado hujachelewa, amka kwenye usingizi mzito uliolala acha kuridhika kwenye ndoto wakati hujapaona ulipotakiwa kufika

Watanzania Kwa Uchafu Tumeshindikana..Embu Ona Huyu Katupa Takataka Daraja Jipya

$
0
0

Pamoja na Jitihada za Paul Makonda Kuanzisha kampeni ya Usafi Jijini Dar es Salaam lakini kuna baadhi ya watu wanazikwamisha juhudi hizo kwa makusudi..hizi takataka zimetupwa daraja jipya la kigamboni ambalo limefunguliwa week iliyopita tu...

Una maoni gani kuhusu hili?

Afisa Mkuu wa Jeshi la Burundi Ameuawa Pamoja na Mkewe Baada ya Kushambuliwa na watu wasiojulika......

$
0
0

Afisa mkuu wa jeshi la Burundi ameuawa pamoja na mkewe baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana mjini Bujumbura.

Jenerali Athanase Kararuza na mkewe wameuawa wakiwapeleka watoto wao shuleni

Jenerali huyo ndiye afisa wa juu zaidi wa jeshi kuuawa katika mji huo mkuu wa Burundi tangu kufanyika kwa jaribio la kupindua serikali ya Rais Pierre Nkurunziza mwaka jana.

Kifo cha Mwimbaji Papa Wemba Chawa Pigo Kubwa Kwa Diamond Platnumz...Azungumzia Collabo Waliyofanya Kabla ya Kifo Chake

$
0
0

Msanii wa bongo fleva Diamond Platnumz ameoneshwa kustushwa kwake na taarifa za kifo cha mwanamuziki mwenye asili ya Congo Papa Wemba, huku akielezea jinsi walivyokutana siku chache zilizopita na kufanya naye collabo.

Kwenye ukurasa wake wa Facebook Diamond ameelezea huzuni hiyo, huku akitoa taarifa kuwa kulikuwa na mipango mingi ya wao kufanya kazi, lakini mauti yameshafuta mipango hiyo.

“Wiki nne tu zilizopita tulikuwa Paris, akanishirikisha kwenye nyimbo yake, tukapanga mengi juu ya wimbo halafu ghafla naskia habari ya msiba…Dah! nimesikitika sana. Hakika binadamu ni wazungumzaji tu ila Mwenyez Mungu ndiyo mpangaji…Pumzika salama Kiongozi wetu daima tutakukumbuka” aliandika Diamond Plutnums kwenye ukurasa wake wa facebook

Msanii Papa Wemba amefariki dunia jana baada ya kuanguka akiwa jukwaani akiimba na kufariki papo hapo nchi Ivory Coast.

Kilichomfanya Siwema wa Nay wa Mitego Afungwe Miaka Miwili Gerezani ni Kutishia Kusambaza Picha za Uchi za Mpenzi Wake

$
0
0

Wiki iliyopita zilianza kusikika taarifa mbalimbali kuhusu kuhukumiwa kwa mpenzi wa zamani na mama mtoto wa msanii Nay wa Mitego aliyehukumiwa kwenda jela miaka miwili  jijini  Mwanza.
 

Pamoja na taarifa zote hizo kutoka hakukuwa na taarifa za kina kueleza ni nini hasa kilitokea mahakamani mpaka akahukumiwa jela miaka miwili  ila taarifa za awali  zilidai kwamba amehukumiwa kwa sababu ya kutukana mtu mtandaoni.


Wakili wa serikali Moris Mtoi ameongea kwenye exclusive interview na DStv  na kusema ukweli au chanzo cha Siwema kuhukumiwa hakikua kumtukana mtu mitandaoni bali kumtishia mtu.


Amesema kilichompeleka Siwema jela nikumtishia mpenzi wake wa zamani kutoa picha za uchi walizopiga, Siwema alikua akimtishia kwamba asingetoa pesa na kumnunulia gari au kufata maagizo yake angezisambaza picha hizo kwa mke wake na watu wengine.


Wakili huyu wa serikali na mwendesha mashtaka kwenye kesi hii amesema vitu vingine alivyokuwa akivitaka Siwema ni kununuliwa nyumba na boyfriend wake huyu wa zamani.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 26, Ikiwemo ya Nchi Kuliwa

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya April 26

CAG Aviumbua Vyama vya Siasa....Ni chama cha CUF Pekee Kilichopeleka Hesabu zake Kukaguliwa

$
0
0
Kati ya vyama 22 vya siasa vyenye usajili wa kudumu, ni chama kimoja tukilichopeleka hesabu zake kukaguliwa kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzoni mwaka 2015.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad, alikitaja chama hicho kuwa ni Chama cha Wananchi (CUF), kilichopeleka hesabu zake za kuanzia Januari mpaka Juni 2015, huku vyama vingine 21 vikishindwa kufanya hivyo, kitendo ambacho ni kinyume na kifungu cha 14 cha sheria ya vyama vya siasa namba 5 ya mwaka 1992.

“...na hili lifahamike kuwa, siyo katika kipindi hicho, hata leo (jana) nimeuliza wasaidizi wangu kama wameshaleta au bado lakini naambiwa ni chama kimoja,” alisema.

Alipendekeza ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, kufuatilia suala hilo ili uwasilishaji wa taarifa za fedha ufanywe kwa wakati kulingana na matakwa ya kisheria.

Askofu Dr Malasusa wa (KKK) Akamatwa Ugoni

$
0
0
MUME wa mwanamke anayedaiwa kumkamata ugoni Askofu Dk Alex Malasusa wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Tanzania (KKK) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, (DMP) anatafuta watoto waliotoroshwa kwa maelekezo ya Malasusa na Jeshi la Polisi, anandika Josephat Isango.

Akizungumza baada ya kuachiwa huru kutoka polisi kwa tuhuma za kushambulia, amesema watoto wake walichukuliwa na raia mmoja mjerumani aliyeolewa na mtanzania, anaitwa Caroline Shedafa.

Caroline Shedafa ametuhumiwa kuwa ametumia mwanya wa malalamiko ya Mwakilima na Malasusa kwa sababu ya urafiki alifanikiwa kuwatorosha watoto hao na kwamba ana mpango wa kuwasafirisha kwenda nje ya nchi wakati wowote.

MwanaHALISI limemtafuta Shedafa kwa tuhuma hizo, alipokea simu na baada ya kuambiwa kuwa anaongea na MwanaHALISI alikata simu na kukataa kuongea suala hili na mwandishi.

Malasusa anadaiwa kuwa anadaiwa kushirikiana na mfanyakazi wa hospitali ya Muhimbili anayeitwa Julieti, aliyewaambia ndugu wa mume anayenyang’anywa mke wake na malasusa kuwa atakiona.

“Huyu kaka anajidai mjuaji, hapti kitu, utaratibu uko tayari wa kuwasafirisha watoto kwenda nje ya nchi na hatawaona tena, ataishia kuwasikia tu, mimi ni mtu wa Karibu na Askofu Malasusa ndo nawaambia”. Alinukuliwa dada huyo akiongea kwa ujasiri.

Hadi sasa watoto wanaotafutwa na baba yao ambao Jeshi la Polisi linadaiwa kushirikiana na Malasusa licha ya taarifa zao kufika polisi kituo cha Wazo na kutochukuliwa hatua ni Sijenuni, Sephania, na Simon wote wanadaiwa kuwa watoto wa Venance Mwakilima.

Taarifa za leo usiku zilizofikiwa MwanaHALISI online zinadai kuwa baadhi ya Maaskofu Jijini Dar es Salaam wameamua kujitokea kulinda heshima ya uaskofu baada ya kudhalilishwa na Malasusa.

Maaskofu ambao hawakupenda kutajwa majina yao kwa kuwa si wasemaji wa vikao halali wamesema “hili suala tunalichukua,

Malasusa ana tuhuma nzito nchini, na baada ya gazeti kuandika watu wamejitolea kujieleza tunaomba muda kesho (Jumanne) tutaliongelea hadharani baada ya kukutana na mume wa me.
Aidha Malasusa hakupatikana kwenye simu zake wala kujibu ujumbe wa simu aliotumiwa tangu juzi wakati gazeti la MwanaHALISI likiendelea kufuatilia sakata hili.

Taarifa ambazo mwandishi anazo zinadai viongozi wakubwa wa serikali wanaingilia suala hili, zinafuatiliwa na zitaandikwa kwenye gazeti la MSETO…

Ripoti ya CAG Yaanika 'Madudu' Kibao Serikalini

$
0
0
Wakati Rais John Magufuli akipambana dhidi ya ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi na uovu mwingine dhidi ya mali za umma, ripoti mpya ya ukaguzi iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha ana kazi kubwa zaidi kupata ushindi kwenye vita hiyo.


Ripoti hiyo ya mwaka 2014/ 2015 iliyowasilishwa bungeni jana na CAG Mussa Juma Assad imeibua uozo zaidi kwenye halmashauri, taasisi za Serikali na mashirika ya umma, ikibainisha kuwa nchi ina tatizo kubwa zaidi ya watu ambao wamekuwa wakishughulikiwa na Serikali ya Awamu ya Tano.

Ripoti hiyo ya pili ya Professa Assad tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo mwaka juzi, imegusa taasisi zilizowahi kuwa chini ya Rais John Magufuli na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako na Balozi Asha Rose Migiro, ambaye alikuwa Waziri wa Sheria na Katiba.

Ripoti hiyo pia inaonyesha ufisadi katika ununuzi na uingiaji mikataba uliofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), matumizi yasiyo ya lazima kwenye Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Afya, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jeshi la Wananchi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na mkoa wa Tabora.

Pia ripoti hiyo imebainisha kuwa mapendekezo mengi ambayo CAG amekuwa akiyatoa kwa takribani miaka saba sasa, hayatekelezwi.

Katika ripoti hiyo, CAG anaonyesha dosari kwenye utendaji wa Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme (Temesa), na Wakala wa Barabara (Tanroads), taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi ambayo wakati huo ilikuwa ikioongozwa na Dk Magufuli.

Profesa Ndalichako alikuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), wakati NEC imeguswa na ripoti hiyo katika suala la mchakato wa kuandika Katiba upya ulioongozwa na Wizara ya Katiba na Sheria.

Ripoti hiyo ya Profesa Assad pia imebainisha kuwa Deni la Taifa, ambalo hutokana na fedha zinazopowa kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kugharimia matumizi ya Serikali, limekuwa kwa tofauti ya Sh7 trilioni.

Tangu aingie madarakani Novemba 5 mwaka jana, Dk Magufuli amekuwa akitumia ripoti zilizopita za CAG kusimamisha kazi au kutengua uteuzi wa watumishi wa umma wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi, lakini amekuwa akikosolewa kuwa hajaweka mfumo wa kukabiliana na hali hiyo.

Katika ripoti hiyo, CAG anasema Temesa ilinunua kivuko chenye kasi ndogo kuliko ilivyotarajiwa na hadi ulipokuwa unafanyika ukaguzi Agosti 2015, chombo hicho kilikuwa hakifanyi kazi kwa zaidi ya mwaka.

“Kuhusu dosari katika ununuzi wa kivuko chenye thamani ya Sh7,916,955,000, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Umeme, mitambo na ufundi (Temesa) iliingia mkatabana M/s Johs.Gram-Hanssen Bergensgade 10, DK 2100 Copenhagen Oe Denmark wa ununuzi wa kivuko cha Dar es Salaam –Bagamoyo chenye thamani ya Dola za Marekani 4,980,000 bila Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT),” anasema CAG.

“Dosari zifuatazo zilibainika katika manunuzi hayo. Kasi ya kivuko haikuzingatia matakwa ya mnunuzi.  Ripoti ya mtaalamu wa ukaguzi ilibainisha kwamba kiwango cha juu na chini cha kasi ya kivuko wakati wa majaribio kilikuwa na kiwango kati ya knots 19.45 na knots 17.25 kinyume na makubaliano yaliyoainishwa kwenye mkataba wa kasi ya kiwango cha 20,” anafafanua.

“Pili kivuko kilikabidhiwa bila hati ya makabidhiano Novemba 17, 2014 baada ya ucheleweshwaji wa siku 16; Pia nilibaini kwamba mpaka wakati wa ukaguzi, Agosti 2015, hati ya makabidhiano ilikuwa haijatolewa na mzabuni.”

Ununuzi wa feri hiyo uliwahi kuzua sakata bungeni huku wabunge wa upinzani wakilalamika kwamba kilikuwa bomu kwani kinatumia zaidi ya saa tatu kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo badala ya dakika 45 za gari.

Eneo jingine lililoguswa na CAG ni la malipo yaliyofanywa na Tanroads kwa makandarasi waliomaliza kazi zao. Kwamba moja ya matatizo makubwa ya taasisi hiyo ni udhaifu katika menejimenti.

“Wakala wa Barabara (Tanroads) iliingia mikataba mbalimbali ya ujenzi wa barabara na madaraja.

"Wakati wa ukaguzi nilibaini kwamba baadhi ya mikataba haikukamilika kwa muda uliopangwa kutokana na kuchelewa kwa ulipaji wa fedha.
 
"Pia, nilibaini kwamba ucheleweshwajiwa malipo ya kati ya mikataba 16 ulisababisha ulipaji wa riba kiasi cha Sh 5,616,652,022 na Dola za Marekani 686,174.86,” alisisitiza CAG.

Profesa Assad amezungumzia pia ukaguzi maalumu alioufanya kuhakiki fedha zilizowahi kutolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa taasisi mbalimbali zilizoko chini yake.

Ukaguzi huo ulifanywa kutokana na ombi lililowasilishwa na katibu wa Bunge kwa barua yenye Kumb. NaCBC.155/188/01/26 ya Desemba 19, 2013.

Bunge lilitaka kujua kama fedha zilizotolewa na wizara hiyo kwenda idara na taasisi zilizo chini yake zilipokewa na kutumiwa na wahusika kama ilivyopangwa.

Katika ukaguzi huo, CAG alibaini kasoro katika vitabu vya akaunti za fedha vya Necta mwaka 2010, Sekretarieti ya Elimu ya Jumuiya ya Madola, Chuo Kikuu Huria (OUT), na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (Adem).

“Udanganyifu wa malipo ya Sh185,350,000 yaliyolipwa Necta. Aprili 2010 kiasi cha 185,350,000 kilitumwa Necta kama matumizi ya kawaida. Wakati wa ukaguzi ilibainika kuwa kiasi hiki cha fedha hakikuandikwa kwenye vitabu vya uhasibu vya Necta. Hata hivyo, ilibainika kuwa stakabadhi ya mapokezi ya fedha hizo iliyotolewa na watumishi wasio waaminifu wa Necta ilikuwa ya kugushi,” anasema.

“Kuhusu fedha zilizopelekwa OUT ni kwamba kati ya mwaka 2009/2010 Wizara ilihamisha Sh90,000,000 kwenda Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, ni kiasi cha Sh40,734,000 ambacho kilipokewa huku Sh49,266,000 hakijulikani.

“Pia katika mwaka wa fedha 2010/2011 Wizara ilipeleka OUT Sh10,486,252,913 lakini ni Sh10,427,109,020 tu zinazoonekana kwenye vitabu huku Sh59,143,893 zikiwa hazimo kwenye vitabu.”

Vilevile, CAG amesema katika ukaguzi huo Sh188, 838,528 zilizopelekwa Adem mwaka 2009/2010 zimeyeyuka. Mwaka huo Wizara ilipeleka Sh712,798,788 kwa taasisi hiyo, lakini vitabu vinaonyesha Sh523,960,260 zilipokewa na kurekodiwa, huku Sh188, 838,528 zikikosekana kwenye vitabu.

Mbali ya CAG kuonyesha madudu katika matumizi ya fedha, pia ameonyesha matumizi mabaya ya Sh7,080 milioni katika mchakato wa uchapaji Katiba Inayopendekezwa.

“Katika ukaguzi wangu nilibaini kuwa Wizara ya Katiba na Sheria ilipokea fedha kiasi cha Sh7,125 milioni kwa ajili ya kulipia gharama za kuchapisha vitabu vya Katiba Inayopendekezwa.

"Kutokana na ufinyu wa muda, Wizara iliomba na kupewa kibali na Wakala wa Huduma za Manunuzi Serikalini kufanya manunuzi kwa njia ya dharura kupitia barua yenye kumbukumbu Na CAD.124/318/01/25 ya Desemba 11, 2014,” anasema CAG.

“Katika ukaguzi wangu nilibaini vitabu vya katiba vilipokelewa kabla ya kuingia mkataba. Nilibaini kuwa mkataba ulisainiwa Februari 2, 2015, lakini vitabu vya katiba vilipokelewa Januari 26, 2015.”

Ukaguzi uliofanywa Oktoba Mosi, 2015 umebaini kuwa nakala 158,003 za Katiba Inayopendekezwa zenye thamani ya Sh559,330,620 bado viko stoo au havijatumwa kwa wananchi ili vitumike kwa uhamasishaji.

“Kwa hiyo, haikuwa rahisi kujua kama thamani halisi ya fedha ilipatikana na lini vitabu hivi vitasambazwa kwa walengwa. Pia, ilibainika kuwa vitabu hivyo havikujumuishwa kwenye Taarifa za Fedha za Mwaka husika,” anasema.

Katika ripoti hiyo ya mwaka 2015/16, CAG Assad anasema ukaguzi wake umebaini matumizi ya mabilioni ya fedha katika ununuzi wa vitu visivyokuwa vya lazima au bila kuonyesha ushahidi wa malipo husika.

Alibainisha matumizi ya zaidi ya Sh53 bilioni zilizotumiwa na taasisi sita pamoja na Sekretarieti mbili za mikoa katika mambo ambayo hayakuwa ya lazima, kama faini za kuchelewa kulipa kodi ya pango.

Taasisi hizo ni Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Afya, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na Mkoa wa Tabora.

CAG Assad amebainisha matumizi ya ziada ya Sh109,722, 539 kwa ajili ya ununuzi wa gari aina ya Toyota Land Cruiser VX V8 kwa Sh297.5 milioni kutoka kampuni ya Toyota (T) badala ya kutumia mfumo wa ununuzi wa pamoja ambao ungefanya gari hilo lipatikane kwa Sh187.8 milioni.

Alisema katika kipindi hicho, wizara 17, balozi mbili na sekretarieti za mikoa 11 zilitumia zaidi ya Sh11.3 bilioni bila kuwapo vielelezo vyovyote, hivyo kusababisha ashindwe kujua uhalali wa malipo hayo.

Kwa taarifa zaidi, pitia  ripoti hizi za CAG
 




5. Ripoti ya Jumla ya Serikali za Mitaa 2014/2015

Zitto ‘Amchana Laivu’ Rais Magufuli..Adai Bado Hafanyi Inavyopaswa.......

$
0
0
ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT- Wazalendo amesema, Rais John Magufuli anapapasa suala la ufisadi, anaandika Pendo Omary.

Amesema, serikali yake bado haijachukua hatua madhubuti katika vita dhidi ya rushwa nchini licha ya ‘shangwe’ nyingi.
Ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa Halmashauri Kuu ya ACT- Wazalendo.

“Bado Rais hafanyi inavyopaswa, bado rais anapapasa suala la ufisadi. Kuna mambo ya muda mrefu ambayo tunaendelea kama nchi kuyalipua lakini arais ameyakalia kimya. Mfano ni suala la Tegeta Escrow,” amesema Zitto na kuongeza;

“Bado mtambo wa IPTL upo chini ya matapeli na kila mwezi serikali inawalipa matapeli hawa zaidi ya Sh. 8 bilioni wazalishe au wasizalishe umeme.
“Hivi ndio vikundi maslahi  katika sekta ya nishati ambavyo bila kuvibomoa, rais ataonekana anachagua katika vita hii.”

Zitto amesema, serikali imeficha inaowaita madalali wa rushwa katika suala la hati fungani ya Dola za Marekani 6 milioni.

Na kwamba, tayari kuna watu wamefikishwa mahakamani lakini  walioitoa rushwa hiyo ambao ni Benki ya Standard ya Uingereza na waliopokea ambao ni maofisa wa serikali, hawakupelekwa mahakamani.

“Hati fungani hii ambayo serikali imeanza kulipa riba yake ni ghali mno na imeongeza deni la taifa kwa kiwango cha Sh. 1.2 trilioni bila ya riba. Itakapofika mwaka 2020 ambapo tutakuwa tumemaliza kulipa deni hili, tutakuwa tumelipa zaidi ya Sh. 1.8 trilioni, shilingi bilioni 600 zaidi,” amesema Zitto.
Zitto amesema, Watanzania zaidi ya 2000 duniani kote wameweka saini kutaka Taasisi ya Rushwa kubwa nchini Uingereza ( SFO ) kufungua upya shauri hili na kuitaka Benki ya Standard iwajibike kwa ufisadi huu dhidi ya nchi masikini ya Tanzania.

Amesema Rais Magufuli angeongoza Watanzania kukataa mikopo ya namna hiyo ambayo inafukarisha nchi ingekuwa ni hatua kubwa lakini Taasisi ya Kupambana na Rushwa (Takukuru) wanaona sifa kuweka ndani watu kwa Sh. bilioni 12 bila kuwataja watu watakaofaidika na Sh. bilioni 600 zaidi zitakazolipwa katika deni hilo.

“Ndio maama tunasema rais na serikali yake bado hawafanyi ya kutosha katika vita dhidi ya rushwa. Sio suala la kutumbua majipu tu, ni suala la kuweka mfumo madhubuti ambao utazuia rushwa kabisa.

“Chama chetu cha ACT -Wazalendo ni lazima kiendelee kuunga mkono juhudi zozote za kuondoa ufisadi nchini kwetu. Hata hivyo chama chetu ni lazima kiendelee kukosoa serikali pale ambapo tunapoona mambo hayaendi sawa.

“Tusiogope kuikosoa serikali kwa hoja kwani kukosoa serikali ni tukio muhimu sana la kizalendo,” amesema Zitto.

Afisa Uchaguzi ahukumiwa kifungo cha Miaka 7 jela kwa Rushwa

$
0
0
Afisa uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara Bw.  Julius Bujabhi Makwasa amehukumiwa kifungo cha Miaka 7 jela baada ya kupatikana na hatia ya Makosa 34 yakiwepo ya Rushwa.

Mnamo mwaka 2013 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Mara ilimfikisha katika Mahakama ya Wilaya ya Serengeti Afisa uchaguzi wa Halmashauri hiyo Bwana Julius Bujabhi Makwasa na wenzake wawili wakishitakiwa kwa makosa thelathini na manne yakiwemo ya matumizi mabaya ya fedha za umma, kuisababishia hasara Halmashauri ya Serengeti, kusaidia kutenda kosa, kughushi na kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri wao.

Washitakiwa wengine katika shauri hilo la uhujumu Uchumi E.C.C 130/2013 lililokuwa likisikilizwa na Hakimu wa Mahakama hiyo Mheshimiwa Ismail Emanuel Ngaile,  walikuwa  Bi Scola Daudi Mosi ambaye ni mtunza kumbukumbu wa Halmashauri hiyo na Bwana Dickson Julius Makwasa ambaye ni mtoto wa mshitakiwa wa kwanza.

Ilidaiwa na mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Wakili Martin Makani mbele ya mheshimiwa Ngaile kwamba mshitakiwa wa kwanza Julius Makwasa  ambaye majukumu yake yalikuwa pamoja na kuviteketeza vifaa vya uchaguzi muda wa uchaguzi unapopita na mshitakiwa wa pili Scola Mossy ambaye  majukumu yake ni pamoja kusimamia kumbukumbu zinazoingia na zinazotoka nje ya Halmashauri hiyo,  kwa nafasi zao hizo,  walikuwa na jukumu la kuharibu nyaraka za uchaguzi mkuu wa Octoba 2010 kama ilivyokuwa imeelekezwa na Tume ya Taifa ya uchaguzi.

Katika kutekeleza jukumu hilo ilielezwa kwamba, waliandaa majina ya vibarua na kuingiza majina hewa ishirini na tano (25) kuonyesha kwamba majina hayo hewa pia yalishiriki  kuchimba mashimo, kusomba nyaraka hizo za uchaguzi na kuzipeleka kwenye mashimo kisha kuziteketeza kwa moto hivyo kustahili malipo.

Katika udanganyifu huo ilielezwa kwamba, mshitakiwa wa kwanza na wa pili waliweza kuandaa nyaraka za kuipotosha Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na kuwawezesha kujipatia jumla ya shilingi million tatu laki nane na elfu hamsini (Tsh 3,850,000/=) kwa kutumia nyaraka kumdanganya mwajiri .

Hizi Hapa Aina Nne za Wanawake Michepuko.....

$
0
0

1.MCHEPUKO LAMI: Huu ni ule ambao hauombi pesa, katulia hana mapepe, uwe naye au usiwe naye maisha yake yanaendelea tu.

2. MCHEPUKO VUMBI: Huu ni ule wa vibomu!! mara ooohhh sina pesa, naomba vocha, sijui simu imekufa, oooh mara nipo saluni nadaiwa elf thelathin, naomba nauli.....n.k! Na hii ndio noma maana njia kuu lazima washtuke mana mchepuko vumbi unachafua na unasumbua full time.

3. MCHEPUKO KOKOTO: Huu ni mkali zaidi ya njia kuu maana kila mara huuliza upo wapi, Uko na nani, why hupokei simu yangu? Kama uko kwako naomba utoke nje tuongee kidogo na leo uwe na mimi tu...Yaani tabu tupu!

4: MCHEPUKO MATOPE: Yaani huu usiombe hata kukutana nao maana wenyewe ndio funga kazi.. Huu bana unajua kuchuna hasa ila pale unapoupa pesa na wenyewe unaenda kuzihonga zote kwa mchepuko wake mwingine yaani hatari tupu

Uhuru Unfollows Everyone on Twitter Except These 11...Magufuli Included

$
0
0
President Uhuru Kenyatta has unfollowed most of the people he had been following on Twitter leaving only 11, mainly famous Heads of State.

Kenyatta who has been the most popular Twitter personality in Kenya based on the number of followers, was following more than 140 people but his following has suddenly shrinked.

The President has only retained United States President Barrack Obama, François Hollande of France, Indian Prime Minister Narendra Modi and Japan's Abe Shinzo.

Among the African Presidents, Mr Kenyatta now only follows Tanzania's John Magufuli, Uganda's Yoweri Museveni, President of Nigeria Muhammadu Buhari and head of the African Development Bank Akinwumi A. Adesina.

In Kenya, the President unfollowed everyone except First Lady Margaret Kenyatta, Deputy President William Ruto and State House Spokesman Manoah Esipisu. What informed the decision remains unclear as Kenyans.co.ke unsuccessfully tried to reach Director of Digital Communications in the President's office, Dennis Itumbi.

Some of the people the President unfollowed include: Safaricom CEO Bob Collymore, Police Inspector Joseph Boinnet, State House official account, Water Cabinet Secretary (CS) Eugene Wamalwa, former CS Charity Ngilu, blogger Ory Okolloh, South African President Jacob Zuma and former Tanzanian Head of State Jakaya Kikwete.

In 2015, Kenyatta became the first person in the country to hit one million followers and also became the second most followed African President behind Rwanda's Paul Kagame.

The President has, however, overtaken Kagame and is currently followed by over 1.4 million people owing to his active interactions on social media.

Mbunge Joseph Msukuma ni "Zero" Brain! Ona Anavyozungumzia Faida ya Bunge Kutokurushwa "Live"

$
0
0
Tumekuwa tukilalamikia uwezo wa wabunge wengi wa CCM kifikra. Bungeni ndipo mahala ambapo wahusika wanatakiwa kutuliza akili na kutoa mawazo chanya ya kulijenga taifa na kusimamia serikali katika majukumu yake ya kila siku. Mimi binafsi nimekuwa siioni faida ya wabunge zaidi ya asilimia 98 ya wabunge wa CCM kwa taifa! Ni mzigo ambao watanzania tunaubeba huku ukiwa hauna faida yoyote ile kwetu.

Mbunge wa Geita vijijini ndugu Joseph Kasheku Msukuma (CCM) amesema kuwa amefurahi sana bunge kutokuonyeshwa "live" kwa madai kuwa jimbo lake halina umeme hivyo watu wa jimbo hilo walikuwa wakilazimika kununua mafuta ya petrol kwa ajili ya jenereta ili kuangalia bunge "live". Aidha amesema kuwa kwa sasa wananchi hao hawatalazimika tena kuingia gharama ya mafuta hayo ya petrol na badala yake watajikita kwenye kilimo.

"Jimbo langu halina umeme, wananchi wangu walikuwa wakilazimika kununua mafuta yapetrol kwa ajili ya kuendesha jenereta ili waone bunge "live" hivyo walikuwa wanaingia hasara. Kwa sasa nimefurahi sana bunge kutokuonyeshwa "live" kwa kuwa hawatalazimika tena kuingia gharama ya kununua mafuta ya petrol! Watajikita zaidi kulima mashamba yao" alisema mbunge Msukuma.

Hao ndiyo wabunge wetu watukufu wa CCM wanaotakiwa kumshauri rais Magufuli anayetokana na chama chao.

Source:G Sam/JF

Watu Watatu Wakamatwa na Madawa ya Kulevya Aina ya Mirungi Mkoani Kilimanjaro

$
0
0
Watu watatu akiwemo raia wa Kenya wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya Mirungi na Bangi kilo 54 na misokoto ya Bangi 4,500 ikisafirishwa kutoka nchini Kenya kwenda mkoani Arusha.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Bw.Wilbrod Mutafungwa amesema watuhumiwa hao wamekamatwa katika maeneo ya njia panda Himo wilaya ya Moshi na Sanya juu wilaya ya Siha wakiwa wameficha madawa hayo ya kulevya kwenye miili yao kuanzia maeneo ya tumboni hadi miguuni.

Amewataja waliokamatwa ni Vitalis Victor mfanyabiashara mkoani Arusha, Naftal Mvoyi mkazi wa Voi nchini Kenya, Maulid Maulis mkazi wa Arusha ambao walikuwa wakisafirisha Mirungi kilo 44 kwa kutumia magazeti na gundi ya karatasi na kisha kuifunika kwenye nguo walizokuwa wamevaa wakitokea nchini Kenya kuelekea jiji la Arusha.

Ripota wetu amefanikiwa kuzungumza na baadhi ya vijana wanaojihusisha na matumizi ya madawa ya kulevya katika manispaa ya Moshi na kueleza kwamba changamoto kubwa inayowabaili ni ukosefu wa ajira hali inayowasababisha baadhi yao kujihusisha na matukio ya uhalifu.

Matumizi ya madawa ya kulevya yameathiri vijana wengi kiafya kutokana na baadhi yao kushindwa kufanya shughuli za maendeleo na hivyo kulazimika kujihusisha na matukio ya wizi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji Amemtaka Rais Magufuli Apunguze Utumbuaji Majipu

$
0
0

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Vincent Mashinji amemtaka Rais Magufuli apunguze utumbuaji majipu. Adai inadhalilisha Watumishi wa Serikali

Alisema pamoja na kuwa CHADEMA wanaunga mkono kitendo cha kuwashughulikia mafisadi pamoja na watumishi wasio timiza majukumu yao ipasavyo lakini hawako tayari kuendelea kushuhudia ambavyo amekua akivunja sheria za nchi. “Watumishi wengi wamedhalilishwa na serikali hii ambayo imekuwa ikitumia mabavu kuwawajibisha watu bila kufuata sheria za nchi,” alisema Dk, Mashinji. “Suala la rushwa katika nchi ni jambo la kimfumo ambapo kila unapoona kunamtu katumbuliwa kwaajili ya rushwa basi kuna idadi kubwa ya watu ambao wanashiriki katika rushwa hiyo,” aliongeza Dk Mashinji.

Aidha, alisema kuwa utaratibu wa Rais kuwatumbua watumishi kwenye mikutano ya hadhara kwa kutumia ushabiki wa wananchi hauwezi kulisaidia taifa kufanikiwa katika kuwaletea mabadiliko ya kweli wananchi wake. “Magufuli ametumbua watumishi wengi sana tangu aingie madarakani lakini niwaulize sukari imeshuka bei au mchele umeshuka bei lakini kila siku tunasikia watu wametumbuliwa bila kuwa na tija kwa taifa,” alisema.

Aliwataka vijana wa vyuo vikuu nchini kuungana na CHADEMA katika kuhakikisha serikali inaruhusu kuonyeshwa kwa vipindi vya Bunge moja kwa mpja kama ilivyo kuwa hapo awali.
Viewing all 104712 articles
Browse latest View live




Latest Images