Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live

Mrembo Jack Wolper Afunguka Sababu za Kuacha Kuvaa Nguo za Kiume

$
0
0


Akiongea kwenye kipindi cha Nirvana, kinachoruka kupitia EATV, Wolper alisema ‘nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule, sasa hivi nimeshakuwa na mchumba’.

“Nilikuwa navaa vile kutokana na wakati ule ulivyokuwa. Kuna watu walikuwa wanapenda, lakini sasa hivi nimeshakuwa mchumba wa mtu. Ni kweli lazima nivae gauni, kwahiyo mtu unatakiwa ujibadilishe wewe mwenyewe usisubiri kubadilishwa,” aliongezea.

Wolper aliendelea kusema, “hata hivyo bado sijaacha kabisa, kidogo unakuwa unagusia mashabiki zako wanakuwa wanakupenda.”

Hata hivyo Wolper japo amekiri kuwa na mchumba mpya kwa sasa lakini hayupo tayari kuweka mahusiano yake hadharani kama mwanzo alivyokuwa anafanya.....



Namuona Mwanamuziki Harmonize Ndani ya Diamond Platnumz

$
0
0

Moyowe ya Afande Sele akiwa na Jay mo moja kati ya nyimbo zangu chache ambazo huzisikiliza mara nyingi kwa siku. Moja ya kati ya maneno yenye busara aliyosema Afande Sele ni “Hii ni fani na msanii na msanii siko mwenyewe ili nifanikiwe inahitaji nikosolewe na inapobidi nisifiwe”

Kwa wafuatiliaji wa muziki hakika Harmonize si jina jipya katika masikio yao, Aiyola ni wimbo wake uliomtambulisha kwenye ramani ya bongo fleva yani muziki wa kizazi kipya mwaka 2015. Aiyola ni wimbo ulifanyika katika studio za WCB ambazo zipo chini ya msanii Diamond Platnumz ambapo Rich Mavoko na Ray Vanny ni miongoni mwa wasanii waliopo chini ya Label hiyo ya WCB.

Inadhihirika katika maisha ya binadamu kabla ya kutokea chochote basi lazima kuwe na ishara yoyote ile, kabla ya kutoka kwa Harmonize hakika ishara zilikuwepo hasa kwa wale wanatumiaji mtandao wa picha Instagram. Tulipata kuona tambo za msanii Diamond pamoja na wapambe wake wakiwa wanampamba na kumnadi msanii huyu chipukizi Harmonize.

Sikuwa na shaka kabla ya kumsikia na hata baada ya kumsikia, licha ya kuona maoni mengi kutoka kwenye team zilizopo katika mtandao wa picha wa Instagram. Maoni mengi yalikuwa na kusema jamaa anamuiga Diamond Platnumz.

Haikuwa rahisi kukubali kile ambacho walikuwa wanasema, bali nilifikiri ni chuki zilizopo katika hizi team ambazo kiundani hazina maana yoyote zaidi ya kutumia muda mwingi katika msanii pinzania na kushindwa kujenga hoja kwa msanii wao ili aweze kufanikiwa zaidi. Lakini wao huwa kinyume na zaidi wamelala upande wa lugha chafu na kudharirishana tu.

Waswahili husema “Lisemwalo lipo na kama lipo laja” Sikuwa mbinafsi katika kujipa muda na kuendelea kusikiliza wimbo wa aiyola, si jambo la kupinga mfanano ulikuwa na mdogo, ila ambacho nilihisi ni labda kipindi anafanya wimbo huu ushauri wa msanii Diamond ulihusika kwa 100%. (Hisia)

Bado ni wimbo wake mpya msanii chipukizi Harmonize aliyomshirkisha Diamond Platnumz, ambapo kwa sasa ni wimbo wa bado ndiyo wimbo unaongoza kuchezwa kwenye vituo vya radio na runinga Tanzania. Hii ni kwa mujibu wa Copyrights Management East Africa (CMEA)

Ishara za Harmonize kuwa ndani ya Diamond zimeonekana dhahiri katika wimbo huu wa bado. Hakika ameshindwa kuwa yeye imenichukua muda kidogo kufikiri kwanini ameamua kuwa Diamond?. Mara kadhaa nilipata wasaa wa kumsikiliza katika mahojiano kadhaa ambapo alisema “Diamond ndiye msanii ninaye mkubali kuliko yoyote yule”. Hivyo katika hilo ni wazi yeye ni shabiki wa Diamond licha ya kuwa bosi wake. Si jambo baya hakika ni jambo jema kufanya kazi na mtu ambaye unamkubali na kumpenda.

Lakini jambo la kufanya kile anachofanya Diamond hakika si jambo jema, ni wazi kama ni mwandishi au mdau mwenye mapenzi na muziki wa kizazi kipya basi hutoacha kusema ili kusaidia muziki kwa ujumla au kumsaidia Harmonize. Ni wiki kadhaa zimepita tangu kumuona msanii chipukizi Harmonize katika mahojiano ya kipindi cha runinga. Hakika nilimuona Harmonize ndani ya Diamond kwa mara nyingine tena , ila hii ilikuwa katika muoenekano wake hususani katika uchezaji,maringo na hata katika uongeaji.Ni wazi alishindwa kujizuia katika ule upande wa kumuiga Diamond, pia hata katika tumbuizo fupi alilofanya pale kwenye kipindi ni wazi nilimuona Diamond ndani yake.

Kuiga ni kitu pekee kinachoanguasha walio wengi katika mambo mengi ya kidunia. Leo hii unapomuiga msanii Diamond ni ngumu kuwa kama yeye maana ni tayari yeye ameshakuwa yeye, pia si rahisi kupenya katika sehemu nyingi maana tayari yeye yupo. Hii si kwa Diamond pekee bali kwa msanii yoyote yule.

Wasanii walio wengi hawajui madhara ya kumuiga msanii mwingine, na makosa mengi yanafanyika sababu hawajui kuna mahala watakwama.

Nadhani huu ni muda mzuri wa msanii chipukizi Harmonize kuchukua nafasi ya kufanya marekebisho katika muziki wake, na kutengeneza mbinu zake kama si sauti tu pekee na hata kuwa yeye zaidi ni vyema kumuacha Diamond na muziki wake.

Pia tusione ukweli kama ni ubaya kwenye maisha yetu ya kila siku, hakika tukikubali ile kweli basi tutakuwa wakweli kwenye kile ambacho utakuwa unafanya kila leo.

SAKATA LA HATI FUNGANI: Kesi ya Aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya na wenzake 2 Imehairishwa

$
0
0
SAKATA LA HATI FUNGANI: Kesi ya aliyekuwa Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya na wenzake 2 imehairishwa tena mpaka Mwezi Mei tarehe 3.

Sababu ya kuhairishwa ni kutokana na jalada halisi la kesi kupelekwa Mahakama Kuu baada ya kukatwa kwa rufaa ya kufutiwa shtaka namba nane la utakatishaji fedha.

UVCCM Wamshukia Fredrick Sumaye ..Wamtaka Amwache Rais Magufuli Afanye Kazi Yake..Wadai yeye Alishindwa Alivyokuwa Waziri

$
0
0
Umoja wa vijana wa Chama cha mapinduzi umesema Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye hana vigezo wala sifa zozote zinazoweza kumfanya awe na uwezo wa kumkosoa Rais Dk John Magufuli katika uendeshaji wa serikali na masuala ya utawala.

Sumaye ametakiwa amuache Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Magufuli ili atimize majukumu yake kwa sababu alipewa dhamana ya kuwa Waziri mkuu lakini hakufikia hata theluthi ya utendaji unaofanyika sasa.

Msimamo huo umetolewa jana na Kaimu katibu mkuu wa uvccm shaka hamdu shaka alipokuwa akizungumza na wanachama wa ccm wa kata mbili za kwandele na mbichi jimbo la Rombo mkoani kilimanjaro.

Shaka alisema anachokifanya Sumaye na baadhi ya wanasiasa muflis wanaojaribu kukosoa utendaji katika utawala wa serikali ya awamu ya tano ni kutaka nao wasikike wakidhani yale walioyafanya wakati wakiwa madarakani wananchi wameyasahau.

Alisema kama yupo waziri mkuu ambaye ameonyesha udhaifu katika utendaji na usimamizi wa serikaki huku akishindwa kumsaidia Rais hakuna atakayempita Sumaye.

Aidha Kaimu huyo alimuonya Sumaye kuacha kumfuatafuata Dk Magufuli katika mikakati yake ya kutumikia nchi na juhudi anazozichukua dhidi ya mafisadi na wabadhirifu wa mali za umma nchini.

Alisema wakati Rais Magufuli akiwa katika dhamira njema na nia ya wazi kuwatumikia wananchi kwa uadilifu, uaminifu na heshima  kina sumaye na wenzake wafumbe midomo yao na waache mara moja kumbughudhi Rais kwa ajili ya kusaka umaarufu wa kisiasa.

Pia shaka aliwataka wananchi wa jimbo la Rombo kujitayarisha ili kumpiga chini mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya chadema Joseph Selasini kwa sabahu ni dhaifu na hatoshi kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo.

"Siku zake za kuitwa mbunge wa Rombo sasa zinahesabika, Selasimi hajui anachokifanya wala hajali shida na matatizo yaliopo katika jimbo lake,lazima adui huyo apigiwe mwaka 2020 "alisisitiza shaka

Akizungumza katika mkutano huo mwenyekiti wa uvccm mkoa wa kilimanjaro Juma Raib Juma aliwakanya wananchi wa kanda ya Kaskazini kuacha mara moja tabia ya kushiriki na kuchagua vyama na wagombea wa nafasi mbali mbali kwa ukabila, ujimbo au nasaba.

Raibu alisema ikiwa wananchi wa kaskazini sasa wanaishi katika Mikao yote ya Tanania, si jambo la maana wao wakahesabiwa kama ni wabaguzi kwa misingi ya asili au ujamaa.

"Tunachotaka kukisafanya baadhi ya wananchi wa Mikao ya Kaskazini ni kumuasi baba wa Taifa marehemu Mwalimu julius Nyerere, hakutuacha tukiwa tumegawanyika , tumeishi miaka yote hatukuongozwa kwa ukabila au udini, chadema acheni kwasabahu hilo ni balaa au janga katika jamii "alisema Raib.

Jumla ya wanachama wapya 103  walijiunga na chama cha mapinduzi pia shaka alipata nafasi ya kuangalia mechi ya soka kati ya timu za kata za makiidi na mahare wilaya ya Rombo.

Mauaji Nyumba ya Kulala Wageni..Mfanya Biashara Akutwa Kachomwa Kisu Shingoni

$
0
0
Mfanyabiashara wa mazao, Eliusta Peter(40),   amefariki dunia baada ya kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni akiwa katika  nyumba ya kulala wageni wilayani Kilombero.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Ulrich Matei alisema tukio hilo lilitokea   Aprili 22  baada ya  wahudumu wa nyumba  ya wageni ya  Sayari kubaini   maiti katika chumba namba mbili.

Inadawa Aprili 20 mwanamke huyo  akiwa na kijana mmoja ambaye  jina lake limehifadhiwa kwa ajili ya uchunguzi, walifika kwenye nyumba hiyo na kuchukua chumba kimoja wakisema  wao ni wafanyabiashara wa mazao.

“Mwili wa marehemu uligundulika ukiwa kwenye nyumba ya kulala wageni iitwayo Sayari chumba namba mbili   saa 11 jioni na ulipochunguzwa ikagundulika kuwa kifo kilisababishwa maumivu ya jereha,”alisema Matei.

Mwanamke huyo  alikuwa na jeraha   kushoto mwa bega lake lililotokana na kuchomwa na kitu chenye ncha kali

Matei  alisema kwa taarifa walizozipata  bila shaka kijana aliyekuwa naye  anahusika na mauaji hayo.

Wakati huo huo, jeshi la polisi wilayani Kilosa limemkamata Rogasian Jeremia kwa tuhuma za kumshambulia mkewe,   Faustina Sizayi(25) kwa kumkatataka kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake.

Mtuhumiwa alikamatwa akiwa anajihusisha na kazi ya ulinzi wa maduka baada ya polisi kumsaka kwa muda mrefu na ndipo Aprili  24  alikamatwa  baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema.

Mashabiki wa Arsenal Wacharuka...Hawamtaki Arsene Weger Tena..Wanamtaka Kocha Huyu

$
0
0
Mashabiki wa Arsenal wamemshambilia meneja wa timu hiyo Arsene Weger katika mtandao wa twitter na kumtaka aondoke na nafasi yake ichukuliwa na raia wa Argentina, Diego Simeone.

Wamesisitiza kuwa timu ya Arsenal chini ya Wenger haijatwaa ubingwa wa Ulaya tangu mwaka 2004 na wala haijashinda UEFA Champions League hata mara moja.

Aidha mashabiki hao walimkubali zaidi Diego Simeone baada ya kuiongoza vyema klabu yake ya Hispania Atletico Madrid na kufanikiwa kuwafunga vigogo wa Ujerumani Bayern Munich 1-0 katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya UEFA.

Kambi ya Wenger msimu huu imetikisika kwa kias kikubwa kutokana na shinikizo kutoka kwa wadau wa klabu hiyo na kusababisha kuharibika kwa mbio zao za ubingwa walizoanza vyema.
Diego Simeone

Hizi ni Dalili za Mwanamke Anayekupenda Kwa Dhati Toka Moyoni, ila Hawezi Kukuambia

$
0
0

Kumekuwa na imani potofu kwa wanawake kwamba hawawezi kumwambia ukweli mwanaume anampenda kwanza mpaka mwanaume aanze lakini ukweli usiopingika ni kwamba wao pia hupendi na mara nyingi wao wakianza kupenda hupenda kweli kufikia stage hata ya kuhisi kuumwa. Hizi ni dalili za mwanamke anaekupenda ila anagoma kukwambia tu.

1. KUKUTEGA ILIKUJUA THAMANI YAKE KWAKO
Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda na kumthamini au la mfano wa mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia respond yako kwake ni kiasi gani unamjali na kiasi gani utahangaika kwa ajili yake.

2. KUPENDA KUCHEKA TENA MUDA MWINGINE KWA NGUVU
Kucheka kwa nguvu hata kwa kitu kisicho chekesha endapo wewe umezungumza. Mara nyingi ataonesha uso wa furaha hata kama si furaha ya kweli.

3. WIVU
Hujisikia wivu anapokuona na wasichana wengine. Ukiwa unachart nao na ukiwaita majina ya kimahaba. Hapendi na hupenda yale afanyiwe yeye tu hata kama sio mpenzi wako.

4.HUKUMBUKA MATUKIO MUHIMU YOTE KUHUSU WEWE
Anakumbuka siku zako muhimu. Hukumbuka kama vile siku yako ya kuzaliwa hatoweza kuisahau kufanya ipite bila kukutakia heri ya siku ya kuzaliwa kama sivyo ukifauli mtihani au chochote katika maisha yako atakuwa mbele kukupongeza.

5. HUPENDA KUANGALIANANA WEWE MUDA MWINGI
Eye contact hupendelea sana kukuangalia machon muda wote ambao mtakuwa mkizungumza pamoja akidhani kuwa utamuelewa ni kiasi gani anakupenda kupitia vile anavyokuangalia. Ila wengine huona aibu kuwatazama wavulana wanaowapenda hivyo huweka jicho la wizi na kukuvizia.

6. HUPENDA KUKAANA WEWE MUDA MWINGI NA KUKUJUAZAIDI
Hupenda kukaa muda mwingi na wewe. Hawezi kupoteza hata sekunde ukimuhitaji kwa mazungumzo. Anajisikia furaha kukaa na wewe muda mrefu bila kuchoka. Anaweza akaacha kila kitu anachokifanya ili ajumuike na wewe na akikaa na wewe hupendelea sana mwanzoni kukujua wewe zaidi na hukujengea mazingira ya wewe uwemuwazi ili umwambie mengi kuhusu wewe na pia akiwa na wewe atakuwa muwazi zaidi hadi mavazi aliyovaa hupenda sana kujua yako na kukuambia yake na hupenda kujua ni mavazi gani yeye akivaa anakuvutia zaidi na atajitahidi kuwa anavaa ya style hiyo kukufurahisha.

7.YUPO TAYARI KUJISACRIFICE
Kama msichana anakupenda yupo tayari kusacrifice. Ni kitu ambacho hakuna mtu ambaye anaweza akafanya kwa mtu mwingine. Utamuona vipi huyo msichana alivyo kwako na kwa wengine. Yaani yupo tayari akose lakini wewe upate na kwa mwingine anaweza akamwambia hana alichoombwa lakini akakupa wewe kama pesa na vitu vingine.

8. HUPENDA KUTATUA MIKWARUZANO YENU KWA AMANI
Mikwaruzano ikitokea katika urafiki wenu hayupo tayari kukupoteza kabla hajakwambia nakupenda.Kwa kuwa anakupenda endapo ikitokea mikwaruzano basi atafanya juu chini kuyaweka mambo sawa ili asikukose.

9. HUPENDA KUKUNUNULIA ZAWADI ZA MITEGO
Mwanamke anaekupenda hupenda kujua mengi sana kuhusu wewe na hapo inamsaiia kukununulia zawadi za mitego kama boxer , na mara nyingi hupenda rangi nyeupe, au kukununulia perfume , sabuni ya kuoge ya manukato,soksi, vest, bukta, saa,raba, t-shirt. Na kama mkitoka wote mkaenda shopping ataakutega kwa kukuonyesha vitu na wewe ukionekana umependa kitu hatonunua siku hiyo ila atanunua siku inayofuata na kukuletea kama suprise.

10. KUPENDA MLE WOTE
Mwanamke anaekupenda ili akujue zaidi hupendelea msosi mle sehemu mmoja na kama ikitokea mwanaume hawezi kuhama sehemu anayokula mwanamke yupo radhi kubadili na kumfuata mwanaume hatakama sehemu hiyo yeye haipendi na kama unakula kwako basi atakutega na kuja kupika kwako ili mle na atakuwa anapenda kununua vitu vya kupika ili tu akutekena uone upendo wake.

Ukiona Dalili kama Hizi Mwanaume Tafadhali Fanya mpango wa kumweka ndani (oa) Mwanamke huyo kabla ujachelewa alafu ukaja kuangukia kwa wale wanawake wenye sifa ya Pasua kichwa!!!!

Faiza Ally Awajibu Mashabiki Wanaomtag Kuhusu Sugu Kumnunulia Gari Mpenzi wake Mpya..

$
0
0

Instagram siku hizi kimekuwa ni kiota cha umbea wa mjini, Alhamisi hii akaunti moja maarufu ya umbea imeweka picha ya mwanadada anayedaiwa kuwa ni mpenzi mpya wa mbunge wa Mbeya, Mh Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ pamoja na gari ambalo anadaiwa kuzawadiwa siku yake ya kuzaliwa.

Akaunti hiyo ilipost picha (hapa juu) na kuandika:

Sugu shikamooo!ahsante kwa kutunyoosha sio kwa bday zetu zile za kiingilio na za kusaka wafadhiri miezi 3!kha hilo lizawadi toka kwa baby ni funga kazi..mtatoo umetulia hata ukiachwa huna haja ya kufuta bana raha si ulishazila bana?? jamani wagonjwa wanaendeleaje huko ICU??…Ukishindana na moto lazima ukuunguze dadeki

Post hiyo ina komenti tofauti tofauti ambapo baadhi ya mashabiki waliamua kumtag mpenzi wa zamani wa Sugu, Faiza Ally ambaye alizaa naye mtoto mmoja aitwae, ‘Sasha’.

Faiza Ally ambaye kwa sasa yupo nje ya nchi aliamua kujibu na kuandika:

Mmnanitag ili iweje ? watu wamenunuliwa magorofa kariokoo itakua harrier  people grow up!

Mafanikio ya Kituo Cha Uwekezaji Tanzania, TIC, Chini ya Julliet Kairuki

$
0
0
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni!, japo huyu mama ametumbuliwa, sababu za utumbuzi huo, ni kitu kinaitwa "personal matter", and has nothing to do na utendaji wake TIC, ifike mahali Watanzania tuwe na shukrani kwa mazuri aliyoyatenda.

Mimi kama mwanahabari huru ninayejitegemea, nimeifanyia TIC kazi za kihabari, tangu enzi za TIC ya Samuel Sitta, TIC ya Ole Naiko na hii TIC ya sasa ya Julliet Kairuki, mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 3 tuu ya Juliet Kairuki, ni mara mia ya mafanikio yote yaliyopatikana katika kipindi cha Samweli Sitta na Ole Naiko put together!, hivyo huyu mama pamoja na hilo tatizo lake "personal" la mshahara, amekifanyia makubwa Kituo cha Uwekezaji, na kulifanyia makubwa taifa hili, kiasi cha kuifanya Tanzania kuwa ndio nchi inayoongoza kwa kuvutia wawekezaji kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, kitendo ambacho ni cha kustahili pongezi na kuenziwa na sio kubezwa kama hivi anavyobezwa sasa as if she did nothing!.

Wiki hii nilialikwa katika kipindi cha 360 cha Clouds TV, kuzungumzia uhuru wa habari Tanzania. Swali la mwisho nililoulizwa niliulizwa nitoe maoni yangu kuhusu utendaji wa Rais Dr. John Pombe Magufuli, nilimpongeza Magufuli, na kuzipongeza hatua za utumbuaji majipu kuwa anafanya kitu sasa katika muda sahihi ila njia anayoitumia kutumbulia haya majipu, sio njia sahihi. (Magufuli is doing the right thing, at the right time but in a wrong way), nadhani kwa vile Magufuli ni rais, no ones tells him, kuwa that is not the right way!. Nikasema kwa vile Magufuli ni rais wetu, Watanzania na dunia wana very high regards on him na very high expectations on him, that he has to be perfect, not only on doing the right thing at the right time, but he got to do it right!. Kwa vile maamuzi yake ndio the highest, the king is always right hivyo haya na tuyaache turidi kwenye mada iliyopo mezani.

Kituo cha Uwekezaji Rasilimali Tanzania (TIC) ni Idara inayojitegemea ya Serikali iliyoundwa kwa mujibu wa Sheria ya Uwekezaji Na. 26, ya mwaka 1997 kwa lengo la kuhamasisha na kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ili kukuza sekta binafsi na hatimaye kuinua uchumi wa Taifa na pia kuishauri serikali juu ya maswala yanayohusu uwekezaji. Kituo kinatekeleza majukumu yake kwa kuongozwa na Bodi ya Wakurugenzi yenye wajumbe sita wanaoongzwa na Mwenyekiti anayeteuliwa na Mhe. Rais. Wajumbe wa Bodi wanateuliwa na Waziri mwenye dhamana ya uwekezaji, aidha Mkurugenzi Mtendaji ambaye naye huteuliwa na Mheshimiwa Rais ni Katibu wa Bodi ya wakurugenzi na pia ni Mtendaji na Msimamizi Mkuu wa shughuli za TIC akisaidiwa na Wakuu wa Idara .

Kituo cha Uwekezaji rasilimali kina makao makuu yake Dar es Salaam na kina ofisi za kanda tatu ambazo zinaongozwa na Mameneja. Kanda hizo ni Kanda ya Kaskazini (Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga) ofisi ziko Kilimanjaro; Kanda ya Ziwa (Mwanza, Shinyanga, Kagera, Mara na Kigoma) ofisi siko Mwanza; na Kanda ya Nyanda za juu Kusini (Mbeya, Iringa, Rukwa, Katavi na Ruvuma) ofisi ziko Mbeya. Kituo kina Idara nne ambazo ni : Utafiti na Mfumo wa Habari, Uhamasishaji Uwekezaji, Huduma kwa wawekezaji, Fedha na Utawala, na masuala ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ambapo kwa sasa kitengo kimehamia Ofisi ya Waziri Mkuu.
MAJUKUMU YA TIC
TIC inatekeleza majukumu ya msingi yafuatayo:
Kubuni mbinu za kujenga mazingira bora ya uwekezaji nchini Kwa lengo la kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje.
Kuwasaidia wawekezaji kupata vibali na hati mbalimbali za kisheria ili waweze kuwekeza hapa nchini.
Kuandaa na kusambaza taarifa sahihi kwa wawekezaji kuhusu fursa za uwekezaji pamoja na upatikanaji wa mitaji na wabia.
Kushirikiana na Serikali kutafuta maeneo yenye ardhi inayofaa kuwekeza kwa ajili ya wawekezaji.
Kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wa kati kuibua fursa za uwekezaji kwa lengo la kukuza biashara zao na kuongeza kipato.
Kuwahamasisha wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza kwenye sekta muhimu zitakazokuza uchumi kwa haraka
Kuwajengea uwezo wafanyakazi wa Kituo ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

UHAMASISHAJI UWEKEZAJI
Kituo chetu cha Uwekezaji kwa kushirikiana na Ofisi zetu za Ubalozi zilizoko nje ya nchi, ziliweza kuandaa shughuli mbalimbali za Kuhamasisha uwekezaji katika nchini mbalimbali Duniani kama ifuatavyo;-

Makongamano ya Kuhamasisha Uwekezaji nje ya nchi
Serikali kupitia ofisi za Balozi zetu zilizoko nje ya nchi na kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji (TIC) tuliweza kushiriki kwenye Makongano yaliyofanyika nchi mbalimbali Duniani ambayo yalitoa nafasi kwa nchi yetu kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini. Baadhi ya nchi ambazo tuliweza kushiriki na kupata fursa ya kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo nchini ni kama vile Marekani, uingereza, China , Japan, Uturuki, India, Afrika ya Kusini, Ethiopia, Sweden, UAE, Thailanda, Singapore, Vietnum, Srilanka.

Kuitangaza nchi yetu nje (Country Branding)
Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji kwa kushirikiana na Shirika la Multichoice (Tanzania) Limited, tuliweza kuandaa sherehe za kutoa tuzo maalum ya CNN kwa mara ya kwanza hapa nchini inayoitwa ‘‘CNN African Journalist Award of the Year’’, kwenye ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam. Uwepo wa mashirika makubwa ya utangazaji Duniani kama ilivyokuwa kwa Shirika la utangazaji la CNN wakati wa sherehe hizo ,imewezesha nchi yetu iweze kufahamika Duniani kote kupitia sherehe hizo za utoaji tuzo maalum kwa waandishi wa habari.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa mgeni rasmi kwenye sherehe hizo ambazo ziliweza kuhudhuriwa na washiriki kutoka zaidi ya nchi 40.
Ziara za wafanyabiashara wa Tanzania nje ya nchi

Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji iliweza kuandaa ziara za wafanyabiashara wa ndani kwenda nje ya nchi ili kutafuta wabia wa kufanya nao biashara, kutafuta masoko ya kuuzia bidhaa zao, kutafuta teknolojia kwa ajili ya biashara za pamoja na mikopo.
Baadhi ya nchi ambazo ziara hizo zilifanyika ni kama vile Afrika ya Kusini, Kuwait, Bahrain, Oman, Saudi Arabia, Uingereza, Japani, Korea ya Kusini, Brazil, marekani, Canada, UAE, Ujerymani, Italia, China, na Kenya.

Ziara za wafanyabiashara wa nje nchini
Serikali kwa kupitia Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kiamataifa, Ofisi za Balozi za nje zilizoko nchini pamoja na Kituo cha kwekezaji, tuliweza kuandaa ziara za wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchi mbalimbali kuweza kuja nchini kwa ajili ya kujionea wenyewe fursa mbalimbali za uwekezaji zilizoko nchini.Wakiwa nchini, makundi hayo ya wawekezaji na wafanyabiashara waliweza kupata fursa ya kukutana na Kampuni za Kitanzania pamoja na taasisi mbalimbali za Serikali ambazo zilikuwa na miradi ya uwekezaji. Baadhi ya taasisi ambazo walipata fursa ya kukutana nazo ni pamoja na Mamlaka ya Bandari (TPA), Mamlaka ya Viwanja vya ndege (TAA), Shirika la Ndege Tanzania (AIR Tanzania Ltd), Shirika la Kusambaza Umeme nchini (TANESCO), Taasisi ya Umeme Vijijini (REA), Wizara ya Miundo Mbinu, SACOT Centre, n.k.
Makundi hayo ya wawekezaji yalitoka katika nchi mbalimbali Duniani kama vile Marekani, Uingereza, Ubelgiji, Italia, Afrika ya Kusini, India, China, Japani, Vietnum, Singapore, Canada, Brazil, Misri, Israel, Uturuki,Indonesia, , Ujerumani, Denmark, Syria, China, Finland.

Mikutano ya Kimataifa ya Kuhamasisha Uwekezaji iliyofanyika nje ya nchi.
Serikali pia iliweza kushiriki katika mikutano mikubwa ya Uwekezaji Duniani ambayo ilifanyika katika nchi mbalimbali ikiwa na lengo la kutangaza fursa mbalimbali za biashara na uwekezaji zilizoko nchini. Baadhi ya nchi ambazo Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji iliweza kushiriki ni kama vile Uswizi, Austaralia, Afrika ya Kusini ,Nigeria ambako mkutano wa World economic Forum ulifanyika, nchi zingine ni UAE, Japan, China,na Marekani

Mikutano ya Kuhamasisha Uwekezaji iliyofanyika nchini
Mikutano ,mikubwa ya kuhamasisha uwekezaji imekuwa ikifanyika nchini pia. Mikutano hiyo imekuwa na lengo la kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizoko nchini kwa wawekezaji wa nje na ndani. Serikali imekuwa na utaratibu wa kuandaa mikutano mikubwa ambayo inakuwa na tija kwa Taifa kwa kuzingatia sekta muhimu za uchumi kulingana na vipaumbembele ambavyo tumejiwekea.

Baadhi ya mikutano iliyoandaliwa ni kama vile mkutano uliolenga sekta ya kilimo, chini ya mpango wa ‘‘Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania’’, yaani SAGCOT, chini ya mpango huu wawekezaji wanahamasishwa kuwekeza kulima mashamba makubwa kwenye ukanda wa SAGCOT, mashamba ambayo yatazungukwa na mashamba ya wakulima wadogo wadogo yaani ‘‘outgrowers’’. Mpango huu unatarajiwa kupunguza umaskini kwenye maeneo ya ukanda wa SAGCOT kwa kuwa wakulima wataweza kulima mazao ambayo yatanunuliwa na wawekezaji wakubwa kwenye ukanda huo.

Mikutano mingine iliyoandaliwa ni ile iliyolenga kuhamasisha uwekezaji kwenye sekta ya utalii, sekta ya madini, sekta ya utafutaji mafuta na gesi.

Uhamasishaji Uwekezaji wa ndani
Serikali imekuwa na mkakati mahususi wa kuhakikisha kuwa watanzania wanafahamu fursa za uwekezaji zilizopo nchini na wanafahamu jinsi Serikali inavyosaidia kukuza uwekezaji kupitia taratibu mabalimbali ambazo zimerahisisha mchakato wa kuanzisha miradi ya uwekezaji nchini pia vivutio vya kodi ambavyo vinatolewa kwa wawekezaji wa ndani. Shughuli hizi za uhamasishaji uwekezaji wa ndani zimefanyika kupitia makongamano ya kimkoa, kikanda, mafunzo maalum ya uwekezaji na ujasiriamali kwa wajasiriamali wa ndani, pamoja na kushiriki maonyesho ambayo yamekuwa yakifanyika nchini.

Makongamano ya Uwekezaji yaliyofanyika nchini
Serikali kupia Mikoa na kwa kushirikiana na Kituo cha uwekezaji, imeweza kuandaa makongamano ya uwekezaji yaliyohudhuriwa na watu zaidi ya 2000 kwenye mikoa mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Mtwara, Ruvuma, Rukwa, Mara,Manyara, Mwanza,Tabora, na Kigoma. Pia makongamano hayo yaliandaliwa katika ngazi ya kanda kama ifuatavyo;-

Kanda ya Kaskazini ambayo inajumuisha mikoa ya Manyara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga - ambapo mkataba baina wa wakuu wa mikoa 4 waliingia makubaliano na Gavana wa Anjouan wa ushirikiano katika biashara na uwekezaji.

Kanda ya nyanda za juu Kusini ambayo inajumuisha mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa.
Kanda ya Ziwa Tanganyika ambayo inajumuisha mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma pamoja na

Kanda ya Ziwa ambayo inajumuisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara, Geita na Kagera - ambapo zaidi yawashiriki 1200 walihudhuria na TIC iliweza kusaini mikataba 6 na wakuu wa mikoa na mkataba mmoja na NARCO kuhusu kutangaza fursa za uwekezaji katika ukanda huo.

Mafunzo ya Uwekezaji na Ujasiriamali yaliyofanyika nchini

Serikali kupitia kituo cha Uwekezaji nchini, kiliweza kuendesha mafunzo kwa wajasiriamali na wafanyabiashara walioko katika mikoa mbalimbali nchini, ili kuweza kuwahamasisha kuanzisha miradi mbalimbali ya uwekezaji na pia kuwajulisha fursa mbalimbali za uwekezaji zilizoko katika maeneo yao na namna Serikali inavyoweza kuwasaidia katika uanzishaji wa kampuni hizo pamoja na unafuu wa kodi ambao Serikali utawapatia kupitia Kituo cha Uwekezaji.

Mafunzo haya ya Uwekezaji na Uwezeshaji yaliweza kuwasaidia sana wafanyabiashara wazawa kwa kuwapatia elimu juu ya maswala mabalimbali yanayohusu uwekezaji nchini, hivyo yamesaidia kuondoa dhana potovu kuwa Serikali imeunda Kituo cha uwekezaji kwa ajili ya kuwasaidia wawekezaji wan je.

Kupitia mafunzo haya, wafanyabiashara wa Tanzania waliweza kupata elimu juu ya kodi mbalimbali wanazopaswa kuzilipa kutokana na kuendesha shughuli zao, namna ya kupata fedha kutoka kwenye vyombo vya fedha n.k.

Mafunzo haya yamefanyika katika wilaya za Mbinga, Songea, Iringa mjini, Singida, Mbozi, Musoma (ikijumuisha Wilaya zote za Mkoa wa Mara),Kilombetro, Ifakara, Kilosa, Ruaha, Makambako pamoja na Njombe.

Kutoa elimu ya Uwekezaji kwa wananchi kupitia Maonyesho.
Kituo cha Uwekezaji kiliweza kushiriki kwenye maonyesho mbalimbali yaliyofanyika nchini kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu Kituo cha Uwekezaji kinavyofanya kazi zake na na namna mwananchi wa kawaida anavyoweza kunufaika na shughuli za Kituo cha Uwekezaji. Kituo cha Uwekezaji kiliweza kushiriki maonyesho yanayofanyika kila mwaka kama vile maonyesho ya Sherehe za Saba saba, Nane nane, Maonyesho ya utalii ya Karibu pamoja na maonyesho ya wiki ya Utumishi wa Umma.

Mafanikio ya ziara za Kuhamasisha Uwekezaji wa kutoka nje na ndani.
Juhudi za Serikali za kuhamasisha Uwekezaji nchini zimeweza kuzaa matunda kutokana na ongezeko kubwa la miradi ambayo imeanzishwa nchini kwenye sekta mbalimbali za uchumi wa nchi yetu, miradi hii imeweza kuleta ajira, kuongeza mapato ya Serikali, kuleta teknojia mpya, kuongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali za viwandani n.k . Miradi hii kwa kiasi kikubwa imeongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wan chi yetu.

Kulingana na takwimu za Ripoti za Uwekezaji Duniani (World Investment Report) zinazoandaliwa na shirika la UNCTAD, Tanzania imeweza kuvutia miradi mingi kutoka nje (FDI) kuliko nchi nyingine zilizo kwenye ukanda huu wa Afrika ya Mashariki. Mwaka 2005 Tanzania ilivutia mitaji kutoka nje yenye thamani ya Dola za kimarekani ziapatazo 447.6 Milioni. Kiasi hiki kiliweza kuongezeka kwa kasi hadi kufikia kiasi cha Dola za Kimarekani zipatazo 1,872.4 Milioni kwa mwaka 2013.

Uhamasishaji uwekezaji katika ukanda maalum wa SAGCOT
TIC imeendelea kushiriki vikao vya ubia vya SAGCOT ili kuongeza ufanisi katika kuhudumia wawekezaji katika ukanda wa juu kusini. Pia kituo kinaendelea kusimamia mchakato wa uhuishaji wa mashamba makubwa ya Mkulazi lenye ukubwa wa hekta 63,227 kwa ajili ya kupata wawekezaji mahiri wa Kilimo cha Miwa na Mpunga. Wawekezaji wakubwa wapatao kumi (10) walionyesha nia na kuandika michanganuo yao ya biashara katika kuendeleza mashamba. Kati ya hao 7 wameonysha nia kwenye Miwa, 2 katika mpunga na 1 katika mpunga na miwa. Baada ya mchakato wa zabuni kumalizika ni mzabuni mmjoja tu ndio aliyewakilisha mchanganuo wake na baada ya kamati kuipitia haukukuwa umefikia vigezo vinavyotakiwa.

HUDUMA KWA WAWEKEZAJI WA NDANI NA NJE
Usajili wa Miradi ya Uwekezaji (2005 -2014)
Kwa kipindi cha Mwaka 2005 hadi 2014, Kituo cha uwekezaji kimesajili jumla ya miradi 7159, miradi ilikadiriwa kuwa yenye thamani ya dola za Kimarekani zipatazo 154,274.5. Miradi hii ilikusudiwa kutoa fursa za ajira kwa watanzania wapatao 969,464
Sekta iliyoongoza kwa idadi ya miradi ni Uzalishaji/Usindikaji viwandani, ikifuatiwa na sekta ya Utalii na Usafirisha na Majengo ya Biashara. Angalia Kielezo namba 1 hapa chini
Katika kipindi cha mwaka 2005 hadi mwaka 2014 kati ya miradi 7159 iliyosajiliwa, miradi 3,535 sawa na asilimia 49.38 ni miradi ya wawekezaji wa ndani, miradi 1,676 sawa na asilimia 23.41 ni miradi ya Wawekezaji wa Kigeni, na miradi 1946 sawa na asilimia 27.18 in miradi ya ubia baina ya Watanzania na wageni kutoka nchi za kigeni. Usajili huu wa miradi mingi ya watanzania ni mafanikio makubwa kwa sababu:

Kwanza lengo serikali katika kukuza uwekezaji ni kutaka watanzania waingie na kumiliki uchumi wa nchi hii na hii ni dalili mojawapo.

Pili malengo serikali ni kuhamasisha uwekezaji wenye tija kwa watanzania hasa kwa kuwapa hajira zitakazowawezesha kukuza uzalishaji na kupata kipato.

Tatu Kuwekezwa kwa mitaji hiyo ni kichocheo katika uzalishaji wa bidhaa na huduma katika kiuchumi wa nchi na inaleta tija kwa taifa kwa kuongeza wigo wa kulipa kodi. Zikiunganishwa na ajira inakuwa na tija katika kuingiza technolojia na utaalamu ambavyo uboresha huduma na bidhaa kuweza kuingia kwenye masoko ya kisasa ndani na nje ya nchi na hivyo kubadilisha maisha ya watanzania kama Ilan ya chama cha mapinduzi inavyosema “MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA”.
Katika kipindi hiki chote cha mwaka 2005 – hadi mwka 2014 Kupungua kwa miradi katika kipindi chamwka 2009 – 2010 na mwaka mwaka 2014 kumesababishwa na mabadiliko ya sheria ya kodi kwa Wawekezaji katika bidhaa za mtaji(deemed capital goods) ambayo yalianza kutekelezwa kuanzia mwaka wa Fedha 2008/2009 mpaka miaka ya hivi karibuni

Utoaji huduma za vibali na leseni mbalimbali kwa wawekezaji chini ya mfumo wa “One Stop Shop”.
Katika kipindi cha cha 2005 hadi 2014 Kituo kimeendelea na maboresho katika kuhudumia wawekezaji ili kupata vibali mbalimbali kwa haraka wakati wa utekelezaji na uendeshaji wa miradi. Katika maboresho hayo Wizara ya Kazi na Idara ya Uhamiaji imeteua maofisa kuidhinisha vibali hivyo kwa niaba ya Makamishna wa Kazi na Uhamiaji. Mpango wa baadae ni kuhakikisha kuwa huduma nyingine zote zikiwepo za Kodi, ardhi, kufungua kampuni n.k zinatolewa ndani ya TIC kwa mfumo huo hapo juu nakuanza kutumia mitandao ili kurahisisha utoaji wa vibali.

Katika kipindi husika kitengo cha ardhi kiliendelea kutoa huduma za ushauri kwa wawekezaji katika masuala mbalimbali ya ardhi pamoja na kuainisha maeneo yenye ardhi kwa ajili ya uwekezaji katika maeneo mbalimbali ya Tanzania. Kitengo cha Ardhi Kilifanikiwa kilishughulikia jumla ya maombi 15,969 ya kumilikishwa ardhi, na jumla ya hati zisizo asili Derivatives /Leasehold title 39 zimekamilika na kukabidhiwa wawekezaji.

Katika kitengo usajili wa makampuni jumla ya maombi ya Makampuni 1246 ziliweza kuandikishwa kwa kutumia ofisa wa BRELA aliyepo hapa Kituoni.

Kitengo cha leseni za biashara kilifanikiwa kutoa jumla ya leseni za biashara 1034 kwa ajili ya ashughuli mbali mbali za wawekezaji.

Kitengo cha Kazi (Labour) na Uhamiaji walifanikiwa kuwapatia vibali vya daraja A kwa ajili ya wenye hisa na daraja B kwa ajili ya wafanyakazi, jumla ya vibali 26,535 vilitolewa katika kipindi hicho.

Kitengo cha TRA kilifanikiwa kuhudumia jumla ya wateja 35,783 kwa kuwasaidia kupata huduma kama vile, misamaha ya kodi, usajili wa mlipa kodi na VAT, na maswala mbalili yahusiyo kodi kwa ujumla.

Kuunganisha Wafanyabiashara Wadogo (SMEs) na Makumpuni Makubwa
Tangu programu ya kuwaunganisha wafanyabiashara wadogo na wa kati na wawekezaji wakubwa ianzishwe mwaka 2009 kituo kimeweza kutoa mafunzo ya wafanyabisahara (SMEs) 451 ambapo wanaume walikuwa 275 na wanawake 176. Mafunzo hayo yanayochukua siku sita (6) kwa kozi na yameweza kufanyika Dar es Salaam, Mbeya ikishirikisha mikoa ya ukanda wa juu Kusini, Moshi, Tanga ikishirikisha mikoa ya ukanda wa Kaskazini na Mwanza ikishirikisha mikoa ya Kanda ya Ziwa. Mafunzo hayo yana lengo la kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wajasiriamali wadogo kwa lengo la kuwajengea uwezo kwa jinsi ya kubadili mitazamo hasi, kuongeza utaalamu katika kutoa huduma au bidhaa, na kutunza mahesabu na kuboresha mahusiano ya kibiashara (Business Linkage) na makampuni makubwa katika sekta za mawasiliano, ujenzi, kilimo, saruji, madini, viwanda vya samaki, Viwanda vya Usindikaji Maziwa Viwanda vya bia, Viwanda vya vinywaji baridi na hoteli. Katika kipindi husika Jumla ya wafanyabiashara/ wasambazaji wa bidhaa na huduma wa ndani (local suppliers) 81 walihitimu mafunzo hayo.

Aidha tangu programu ya Business Linkages ianzishwe hapa Kituoni kwa kushirikiana na UNCTAD mafanikio mengi yamepatikana kwa kutoa mafunzo na kuwaunganisha wajasiriamali wapatao 150 kwa makampuni makubwa 20 kama kiambatanisho kinachofuata kinavyoonyesha
Huduma kwa Wawekezaji Waliopo (After-care Services)

Kituo kilitembelea miradi mbali mbali ya wawekezaji na kutoa huduma bora (Aftercare Services) ili kujenga mahusiano mazuri na wawekezaji, kutatua matatizo yao na kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji. Katika kipindi husika katika jitihada za kutoa huduma kwa wawekezaji kwa malengo ya kutatua kero zinazokabili miradi na pia kushauri wawekezaji kupanua miradi ili kuongeza mitaji na ajira kwa Watanzania. Changamoto zilizoainishwa katika kutembelea miradi hiyo ni pamoja na;
Uchelewezwaji wa vibali mbalimbali vya kuwasaidia wawekezaji kuendeleza miradi yao
Miundombinu ya barabara na bandari

Umeme usio wa uhakika
Gharama kubwa za mafuta ya kuendeshea mitambo
Mlolongo mrefu wa kupata Ardhi kwa ajlili ya upanuzi wa miradi
Mabadiliko ya mara kwa mara ya punguzo la kodi katika vifaa vya mtaji (deemed capital goods/ incentives)

Uagizwaji mazao ya kilimo na mbegu kutoka nje unaathiri soko la ndani
Ufanisi duni kutoka katika bodi za mazao

Uhamasishaji Miradi ya Wawekezaji Mahiri (Strategic Investors)
Katika jitihada za kuhamasisha uwekezaji wa kimkakati, TIC imesajili jumla ya miradi mikubwa ya kimkakati 45. Miradi hiyo inatarajia kuwekeza kiasi cha dola za Marekani bilioni 8.4
Miradi inayohusisha sekta mbalimbali, ambazo ni kilimo, viwanda, nishati, usafirishaji, utangazaji, miundombinu na mawasiliano.

Miradi katika sekta ya kilimo imechukua asilimia 39, viwanda vikubwa asilimia 26, miundombinu asilimia 16, nishati asilimia tano, usafirishaji asilimia tano, utangazaji asilimia tatu, maliasili asilimia tatu na mawasiliano asilimia tatu.

UTAFITI NA UBORESHWAJI WA MAZINGIRA YA BIASHARA
Tafiti za Uwekezaji
Tafiti za kiuwekezaji zilizofanyika zililenga kusahidia kufahamisha na kushauri serikali juu ya mambo yanayoendelea kwenye uwekezaji ili maamuzi sahihi yafanyike katika kuboresha mazingira ya uwekezaji na pia kuibua fursa za uwekezaji na kurahisisha kazi ya kuinadi nchi ndani na nje kiuwekezaji.

Utafiti wa mitaji ya kutoka Nje - Foreign Direct Investment
Katika vipindi vyote viwili, serikali iliwezesha,TIC kwa kushikiana na Benki Kuu ya Tanzania pamoja na Ofisi ya Takwimu ya Taifa kukamilisha tafiti ya tano (5) za ufuatiliaji wa wa uwekezaji wa miradi ya kigeni hapa nchini (makampuni yenye mitaji kutoka Nje) zijulikanazo kama Tanzania Investment Report (TIR)ambayo huonesha mwenendo wa uwekezaji wa kigeni hapa nchini. Taarifa hiyo huzalishwa karibu kila mwaka na takwimu zake huchangia pia katika ripoti ya uwekezaji ya dunia.

Lengo la tafiti hizo ni kufuatilia uwekezaji wa sekta binafsi unaofanya na mitaji iliyotoka nje ya nchi, hasa kwa kujua wanawekeza kutoka nchi gani, kiasi gani, sehemu gani, katika sekta gani, wanafanya nini na wanahusianaje na wenyeji (watanzania).Tafiti hizo zinafaida nyingi kwa taifa letu:
Kwa kujua nchi inakotokea mitaji hiyo, sera za mahusiano kati ya nchi yetu na nchi hizo hutengenezwa na kuimarishwa.

Kwa kuongea na wawekezaji wa mitaji hiyo serikali imeweza kugundua changamoto na vikwazo wanavyokumbana navyo na hivyo kuweka mikakati ya kuboresha mazingira ya uwekezaji.
Kujua sekta ambazo mitaji hiyo imewekezwa kumesahidia serikali kujuwa maeneo ya kuvutia wawekezaji na hivyo kuweka juhudi zaidi katika kuimarisha taarifa za fursa za uwekezaji na miundombinu ya maeneo hayo.

Baadhi ya matokeo ya utafiti unaonyesha kuwa;
Mitaji kutoka nje iliongezeka kwa wastani wa 10.3% (kutoka dola za kimarekani milioni 7,751.0 hadi 10,393.2)
Uwekezaji katika shughuli za umeme na gesi uliongezeka kwa kasi kubwa katika kipindi cha utafiti kwa mwaka 2008 hadi 2011 ambapo uwekezaji ulikuwa na thamani chini ya dola za kimarekani milioni 3.0 kwa mwaka 2008 na 2009, uliongezeka hadi kufikia dol aza kimarekani milioni 290.5 mwaka 2010 na dola za kimarekani milioni 209.4 mwaka 2011.

Sehemu kubwa ya faida iliyopatikana iliwekezwa nchini kwa wastani wa 82.5% (2008 hadi 2011) hii inaonyesha wawekezaji kuwa na imani na serikali na mazingira ya uwekezaji kwa kipindi cha utafiti.
Mtazamo wa wawekezaji na Uhusiano na Uchumi wa Ndani (Investors Perceptions) wakilinganisha walivyoanza biashara na wakati utafiti ulipofanyika ulionyesha kuwa;
Kulikuwa na uboreshwaji wa mazingira ya uwekezaji hasa katika huduma za benki, mawasiliano, uhamiaji, usafiri wa anga na nchi kavu.

Umeme usiokuwa wa uhakika ulibakia kuwa ni changamoto kwa wawekezaji
Shughuli za uzalishaji viwandani na kilimo ziliongoza katika utoaji wa ajira ambapo asilimia 94.1 ya waajiriwa ni wazawa na asilimia 5.9 ni wageni.

Makampuni mengi yalikuwa na mipango ya kuongeza uwekezaji hapa nchini ambapo 75.7% yalionyesha kuwa na mipango ya kuongeza uwekezaji kipindi cha miaka mitatu ijayo. Aidha 19.9% yalionyesha kutokuongeza uwekezaji na 4.4% yalionyesha yatapunguza kiwango cha uwekezaji. Mtazamo huu unaashiria kuwa wawekezaji wameridhishwa na jitihada za serikali za kuboresha mazingira ya uwekezaji hapa nchini.

Mtiririko wa mitaji kutoka Nje (Foreign Direct Investment)
Tanzania imeendelea kuongoza katika kuvutia wawekezaji kutoka nje ikilinganishwa na nchi nyingine katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa takriban miaka sita mfululizo kuanzia mwaka 2008. Takwimu zinaonyesha thamani ya FDI imeongezeka kutoka dola za kimarekani milioni 1,706 (2012) mpaka dola za kimarekani milioni 1,872 (2013) ambapo ni sawa na ongezeko la 9.7% Ongezeko hili limechangiwa zaidi na sekta ya mafuta na gesi katika miaka ya karibuni.

Soko la Ajira na madhara yake kwa fursa za uwekezaji nchini “A study of Labour Market and Impacts on Investment Opportunities in Tanzania” ambao ulilenga kupitia takwimu za ajira kupitia uwekezaji, kuchunguza mambo muhimu katika ajira ya Tanzania (ukubwa wa ajira, uwezo wake, utaalamu). Pia kuchunguza matatizo ya soko la ajira kwa kutoa picha halisi ya mwenendo wa ajira nchini na kushauri jinsi ya kuongeza ufanisi au kushauri juu ya njia mwafaka ya kuyatatua.
Madhara ya umeme kwa uwekezaji “A report on Power crisis in Tanzania and Its Impact on Investment” uliolenga kushauri juu ya changamoto za umeme kwenye uwekezaji hasa gharama na kutoaminika katika kupatikana (Tarriffs and unreliable supply)

Uwezo na Mlinganyo wa Tanzania kwa mataifa mengine juu ya uwekezaji “Tanzania’s Competitive and Comparative Advantages”. Utafiti huu ulilenga kuweka wazi uwezo wa Tanzania ukilinganishwa na nchi nyingine duniani ili kusaidia kuvutia uwekezaji zaidi.

Ukuwaji wa uwekezaji na matokea ya uwekezaji huo kwa nchi “Report on the Study of growth and Impact of Investment in Tanzania” ulilenga Kupima kazi zinazofanywa na kituo katika kukuza na kusaidia uwekezaji na; Kushauri juu ya jinsi ya kuongeza ufanisi wa uwekezaji katika uchumi
Utafiti juu ya madhara ya kufuta misamaha ya uwekezaji, huu ulilenga kutoa picha halisi ya jinsi kuondoa vivutio vya uwekezaji kunavyoathiri juhudi za kujenga uchumi kupitia uwekezaji na hivyo kuongeza madhara ya muda mrefu ya kutokuwa kwa vyanzo vya kodi.

Pia kituo kimekuwa kikifanya kazi na UNIDO katika kuandaa ripoti ya “Africa Investor Survey” na pia kuandaa ripoti ya “Tanzania investor Survey” inayotarajia kuzindulia siku za karibuni; kwa kushirikiana na UNCTAD na Benki ya Dunia kituo kimekuwa kikitoa michango mbalimbali ili kuwezesha kuandaliwa kwa ripoti nyingi za uwekezaji na kisera hasa katika sekta za kipaumbele
Maboresho na Utengenezaji wa Sera – kituo kimeendelea kuwa katika kikosi kazi cha kuboresha Sera ya uwekezaji na pia uandaaji wa Sera ya Sekta Binafsi ikishirikiana na wadau wa sekta binafsi na umma. Kazi hii imekuwa ikiratibiwa chini ya ofisi ya waziri Mkuu.

Uzinduzi wa Tovuti Mpya - Kituo cha Uwekezaji (TIC) kimezindua tovuti mpya www.tic.co.tz ambayo inatoa taarifa zote za muhimu kwa wawekezaji na wafanyabiashara. Na imekuwa ni tovuti ya kwanza kwa ukanda wa SADC kuwa na tovuti yenye maelezo ya kina kwa wawekezaji na wafanyabishara. Kanuni zipatazo 40 na taratibu 136 zimeainishwa kwenye tovuti hiyo na “link” ya tovuti ya TIC ipo katika mchakato wa kuonekana katika tovuti zote za balozi zetu za Tanzania.
Tovuti hiyo ina fomu 138 zinazosaidia maswala yote ya uanzwishwa wa biashara na uwekezaji, zikiambatana na sheria 38, ambapo zote kwa ujumla zinatoa muongozo rahisi wa jinsi ya kuwasilina na ofisi za umma zipatazo 20 na maafisa husika 88 wameainishwa kwa sura, simu zao na barua pepe kwa kumrahisishia mfanyabiashara / mwekezaji. Tovuti hii mpya inasomeka kwa lugha 80.
Muongozo mpya wa Wawekezaji “Investors Guide” inayoonyesha taarifa za uwekezaji zimegaiwa ndani na nje ya Tanzania na miongozo hiyo itaendelea kusambazwa kutokana na maombi maalum kutoka kwa wadau (physical copy) kwa uharaka “soft copy” ya muongozo unapatikana katika tovuti pia.
Tangu kuboreshwa kwa Taarifa katika tovuti Julai 2012 hadi Februari 2015 tovuti imetembelewa kwa mara 113,683 na watu kutoka katika nchi 210 duniani. Watu walioongoza kutembelea tovuti wanatoka katika nchi za Tanzania (51,519) ikifuatiwa na Marekani (6,864), India (6,408), na Uingereza (4,768). Kwa upande wa nchi Afrika inaongozwa na Kenya (3,058) na Afrika ni Afrika ya Kusini (2,640)
Mpango wa kusajili biashara na kujiunga na vivutio vya uwekezaji kwa njia ya Mtandao (Tanzania Investment Window)

Ushirikiano na taasisi za serikali kituo kimeweza kutengeneza programu ya pamoja kusajili miradi kwa njia ya mtandao ujulikanao kama TIW. Progamu hii ni endelevu na system ya kuhakikisha mwekezaji anaweza kusajili biashara, kupata Namba ya mlipa kodi na kujiunga moja kwa moja na mifuko ya hifathi jamii nchini imewezesha kupitia mtandao na mwekezaji hatatakiwa kusumbuka hata kama yupo mbali na Dar es salaam anaweza kuingia katika tovuti ya kituo na kupata maelezo na kujaza fomu moja na kuambatanisha nyaraka muhimu zinazotakiwa na kulipa kwa njia ya mtandao kwa kiwango kitakachokuwa kimeainishwa katika mtandao kutokana na aina ya huduma anayoitaka ( mobile payment au online benking) na kupangiwa siku ya kuja kuchukua cheti chake. Bado program hii haijazinduliwa rasmi ili kumalizia taratibu muhimu za taasisi zinazoshiriki. Mbeleni kituo cha uwekezaji kinaenedela na mchakato wa kumalizia vibali vingine vinavyotolewa hapa TIC viweze kupatikana pia kwa njia ya mtandao katika kujisali na hii itasaidia sana katika kupunguza urasimu katika ufanyaji biashara hapa Tanzania. Awamu ya kwanza ya program hii imefanyika chini ya ushirikiano baina ya serikali na UNDP na UNCTAD, awamu ya pili inatarajia kuanza Machi 2015 kwa ufadhili kutoka Investment Climate Facility (ICF)

Hitimisho.
Pamoja na yote haya huyu mama aliyoyafanya, yamemkuta ya kumkuta, wakati sisi tunanyanyapaa kwa mshahara wa milioni 5, sasa subirini wenzetu watakavyo mgombania!, japo hakutendewa vema, lakini you never know, everything happens for a reason, na kuna majanga mengine huwa ni blesing in disguise!.

Nampongeza kwa kazi nzuri TIC, Mungu ambariki.

Imeandikwa na Paskali.

Soma Hapa Taarifa Kwa Vyombo vya Habari Kutoka Chadema

$
0
0
CHADEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vincent Mashinji amesema kuwa Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi ndiyo msingi imara pekee unaoweza kuweka mifumo na taasisi kwa ajili ya maendeleo ya kweli yatakayogusa maslahi ya Watanzania wote badala ya nchi kuongozwa na kauli za viongozi.

Kutokana na umuhimu huo wa kuzingatia maoni ya wananchi yanayobeba matakwa yao katika mchakato wa Katiba Mpya, amesema kuwa CHADEMA hakitashiriki Kura ya Maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa ambayo ilipitishwa na Bunge Maalum la Katiba baada ya kubadili na kuondoa mapendekezo yaliyotolewa na wananchi kwenye Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya.
Badala yake, CHADEMA kitaendelea kuweka agenda ya kupigania Katiba Mpya na bora katika vipaumbele vyake, kwa sababu itatibu vidonda na kumaliza makovu yaliyoko katika jamii kutokana na matatizo mbalimbali kama vile ukosefu wa haki, migogoro ya ardhi, wananchi kukosa huduma za msingi za kijamii zikiwemo elimu, maji na afya.

Dkt. Mashinji ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipoukaribisha ujumbe wa Chama cha Centre Party cha Norway uliofika ofisini kwake jijini Dar es Salaam kutia saini makubaliano ya ushirikiano kati ya vyama hivyo kwenye Mradi wa Elimu ya Demokrasia awamu ya pili unaofanyika Wilaya ya Mtwara Vijijini.

Dkt. Mashinji pia amekishukuru chama hicho kwa kusaidia kutoa elimu ya uraia kwa Watanzania hususani maeneo ya vijijini katika mradi ambao unahusisha vyama vyote vya siasa vyenye uwakilishi ndani ya Bunge, huku akisisitiza kuwa CHADEMA kiko tayari kwa ushirikiano unaozingatia maslahi na matakwa ya wananchi hasa katika kukuza uelewa wa kudai haki, demokrasia na uongozi bora ndani ya nchi.

“Suala la Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi kama ilivyowasilishwa kwenye rasimu ya pili na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya ni agenda muhimu kwa Watanzania wapenda nchi yao na sisi ni kipaumbele kwa mwaka huu na kuendelea hadi hapo nchi yetu itakapopata Katiba Mpya ya Wananchi.

“Jana na leo tumewasikia baadhi ya viongozi wa serikali wakisema kuwa wanajiandaa kuitisha kura ya maoni…hatutashiriki kura ya maoni ya Katiba Mpya Inayopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba. Tunajua Watanzania wengi wanataka Katiba Mpya iliyotokana na maoni yao, si ile iliyochakachuliwa bungeni.

“Katiba Mpya iliweka masuala kuhusu haki za wananchi, kuimarisha misingi na kuweka mifumo ya demokrasia na uongozi bora, walau kwa kuanzia. Hatuwezi kusema sasa tutatumia mikakati gani kuwahamasisha Watanzania kuidai Katiba Mpya…tutajua namna ya kuvuka tukishafika mtoni,” amesema Katibu Mkuu Dkt. Mashinji.

Aidha, Katibu Mkuu Dkt. Mashinji amesisitiza kuwa suala la nchi kuwa na misingi na mifumo imara ya demokrasia na uongozi bora ni muhimu kwa Tanzania, katika wakati ambapo nchi inaelekea kwenye uchumi mkubwa wa nishati ya gesi na mafuta, akisema vinginevyo ni hatari iwapo taifa lenye utajiri mkubwa wa rasilimali, litaendelea kuwa na wananchi waliokata tamaa kutokana na mfumo mbovu uliopo.

Akisisitiza umuhimu wananchi kuwa Katiba inayotokana na wananchi, Dkt. Mashinji alitolea mfano wa nchi ya Norway ambayo miaka mingi nyuma ilikuwa sawa na Tanzania, lakini ilifanikiwa kuondokana kuwa taifa maskini kutokana na uwepo wa uongozi bora, mifumo na taasisi imara za kidemokrasia ambazo ziliweza kusimamia ustawi wa taifa hilo kutokana na uchumi wa gesi na mafuta na sasa ni kati ya mataifa yaliyoendelea barani Ulaya na duniani kwa ujumla.

Kwa upande wake ujumbe huo uliokuwa ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Centre Party, Knut Olsen, umesema kuwa chama hicho kinashukuru kwa mradi huo kuingia katika hatua ya pili kuanzia mwaka 2016-2019 huku hatua ya kwanza ikiwa na mafanikio makubwa katika jamii ya wananchi wa maeneo ya pembezoni.

“Kama unavyojua, mradi huu kupitia TCD unahusisha vyama vyote vyenye uwakilishi ndani ya bunge, na lengo letu ni kuwajengea uwezo viongozi wa vyama hasa wanawake na vijana katika ngazi ya jamii kwenye vitongoji, vijiji, kata na bunge ili waweze kushiriki mchakato wa maamuzi. Tunatarajia kuendelea kupata ushirikiano katika hatua ya pili,” amesema Inger Bigum, ambaye ni Meneja wa Mradi hapa nchini.

Wengine waliokuwa katika ujumbe huo wa Centre Party ni pamoja ni Katibu Mkuu wa Vijana Sara Hamre, Katibu Mkuu wa Wanawake, Eline Stokstad-Oslan na Katibu Mkuu wa Wazee, Kristin Madsen.

Mradi huo wa Elimu ya Demokrasia katika Wilaya ya Mtwara Vijijini unaohusisha vyama vyenye uwakilishi bungeni kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) chini ya ufadhili wa chama hicho, katika awamu ya kwanza ulihusisha kata za Msangamkuu, Nanyamba, Ziwani na Mbembaleo na katika sasa awamu ya pili utakuwa katika kata za Mkunwa, Tangazo, Mayanga na Madimbwa.

Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA

Zitto Kabwe Aibua Mazito Bungeni: Ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti, Ufisadi wa Hati Fungani ya Sh1.2 Trilioni

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe jana aliibua mambo mazito bungeni wakati akichangia mjadala wa Bajeti ya Ofisi ya Rais –Tamisemi na Utawala Bora, likiwamo la ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti kutokana Bunge kupitisha bajeti Sh23.7 trilioni huku Serikali ikija na bajeti ya Sh29 trilioni.

Mambo mengine yaliyobainishwa na mbunge huyo ni sakata la ufisadi wa hati fungani ya Sh1.2 trilioni katika Benki ya Standard ya Uingereza na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kushindwa kutoa majibu ya uchunguzi wa miamala kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow kwenda Benki ya Stanbic.

Tazama Video Hapa Zitto Akimwaga Cheche:


Kuhusu bajeti, Zitto alisema kuna ukiukwaji wa Sheria ya Bajeti namba 11 ya mwaka 2015 katika mchakato wa bajeti ya mwaka 2016/17 kwamba kifungu cha 8 cha sheria hiyo kinaeleza namna ambavyo mfumo wa bajeti ya Serikali unapaswa kuwa.

“Vifungu cha 8(1)(b) na 9(1)(a) na 19(1) vinataka ‘mpango na miongozo ya bajeti’ ipitishwe na Bunge katika mkutano wake wa Februari kila mwaka. Bunge lilikaa kama Kamati ya Mipango na kupitisha Mpango wa Bajeti uliokuwa na Bajeti ya Sh23.7 trilioni,” alisema.

Alisema kiasi hicho ni tofauti na bajeti inayojadiliwa sasa ya Sh29.5 trilioni na kubainisha kuwa jambo hilo si utawala bora kwa maelezo kuwa utungaji wa bajeti umeainishwa kisheria na kama sheria hazifuatwi, ni vigumu hata Bajeti yenyewe kutekelezwa.

“Ili kurekebisha hali hii ni lazima Bunge likae tena kama kamati ya mipango na kupitisha upya viwango vya juu vya bajeti kabla ya mjadala wa bajeti kuendelea au angalau kabla ya kupitisha bajeti kuu, Juni 2016,” alisema na kwamba bajeti za taasisi hazimo kwenye vitabu vya bajeti ya Serikali kinyume na sheria ya bajeti.

Kuhusu ufisadi wa Sh1.2 trilioni, mbunge huyo alisema mwaka 2013, Serikali ilikopa fedha hizo kutoka nje kwa msaada wa Benki ya Standard ya Uingereza ambayo sasa inaitwa Standard Bank, kwamba mkopo huo wenye riba inayoweza kupanda umeanza kulipwa Machi mwaka huu.

Alisema mkopo huo utalipwa mpaka mwaka 2020 kwa mikupuo tisa inayolingana na kuongeza kuwa mkopo huo umegubikwa na ufisadi huku baadhi ya Watanzania wakiwa tayari wamefikishwa mahakamani wakihusishwa na sehemu ya mkopo huo.

“Jambo la kushangaza ni kwamba wanaosemekana kula rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Vilevile, waliotoa rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Waliopo mahakamani ni wanaosemekana kutumika kupeleka rushwa. “Mjumbe kashtakiwa, lakini aliyemtuma hajashtakiwa na aliyepelekewa kilichotumwa hajashtakiwa. Hapa kuna tatizo la msingi ambalo tukilitatua Serikali yetu itaepuka masuala kama haya siku za usoni.”

Alisema ana barua ya kundi la Watanzania zaidi ya 2,000 wakitaka benki hiyo ya Uingereza ichunguzwe katika suala hilo la hati fungani huku Takukuru ikitumia taarifa ya Taasisi ya Uingereza ya (SFO) katika kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya Watanzania wanaotajwa katika sakata hilo.

Alisema SFO haikufanya uchunguzi dhidi ya benki hiyo ya Uingereza na kushangazwa na Tanzania kusaidiwa kesi hiyo na wataalamu kutoka nchi hiyo.

“Iwapo tutafanikiwa kuonyesha kuwa Benki ya Standard ilihonga kupata biashara nchini kwetu, Tanzania itakuwa fundisho kwa kampuni ya kimataifa kwamba Afrika siyo mahala pa kuhonga na Tanzania haitalipa mkopo huu na riba zake na tutaokoa zaidi ya Sh2 trilioni katika deni la Taifa,” alisema.


Chanzo: Mwananchi

Hii Tumbua Tumbua ya Rais Magufuli, Hivi Kikwete Anajisikiaje?...Anajisikia Sifa Au Anajuta?

$
0
0
Hii tumbua tumbua majipu ya Rais John Pombe Magufuli, japo inafanyika kwa nia njema, swali la kujiuliza ni Jee mtangulizi wake, Jakaya Mrisho Kikwete anajisikiaje?!.

Kwa jinsi Magufuli anavyotumbua baadhi ya majipu, kunamuabisha sana mtangulizi wake, Jakaya Kikwete kumfanya Kikwete kuonekana kuwa alikuwa ni rais dhaifu sana, kiasi cha kulea madudu kibao, as if awamu ya JK kulikuwa hakuna lolote la maana lililokuwa likifanyika zaidi ya kulea uzembe, as if serikali ya JK ilikuwa ni serikali goi goi, kazi yake ilikuwa ni kulala tuu usingizi, lakini sasa awamu hii ya Magufuli, "hapa kazi", ndio serikali sasa inafanya kazi!.

Just imagine kama wewe ndio JK, unaposafiri unakutana na ma diasfora wa Tanzania kwenye nafasi nzuri ughaibuni, huku wanalipwa vizuri, unawaomba warudi nyumbani kuja kuutumia ujuzi wao kuijenga nchi, baadhi ya wana diaphora hawa wanaguswa na uzalendo, wanakubali kurudi nyumbani na kuukubali umasikini wetu, lakini wanakuwa wakweli kuwa mishahara ya seikali ni midogo mno kuwavutia kurejea nyumbani, JK unawabembeleza na kuwaahidi utajitahidi kuwaongezea kidogo katika kugawana umasikini, japo hautawalipa kama wanavyolipwa huko ughaibuni, lakini utaboresha boresha zaidi angalau kufikia kiwango cha kumfanya asurvive comfortably, hivyo baadhi yao wanakubali wanarejea nyumbani.

Kwa vile wamekuja kwa promise, wanaamua kutopokea any less than the promised amount, wewe unamuahidhi kufuata taratibu za kufikia kiwango kilichoahidiwa, sasa hata kabla muafaka haujafikiwa, mtu aliyekufuatia uliyemkabidhi kijiti kwa upendo wote, kazi yake ya kwanza ni kuwakomoa baadhi ya wateule hawa!, Magufuli alianza na Bade pale TRA, wakafutia wengine, na jana ndio ilikuwa zamu ya Juliet wa TIC, jee ungekuwa ni wewe JK, utajisikiaje?!.

Anachokifanya Magufuli, is it fair kwa JK, kuwatimua watu wake kwa kuwakomoa, jee anawakomoa hao anaowatumbua, au anamkomoa JK na kumuaibisha kuwa JK alikuwa dhaifu mno, hadi kushindwa kuyatumbua hayo anayoyaita majipu?!.

Jee kuna uwezekano kuna baadhi ambao hawakumchagua Magufuli, (walimchagua yule 'jamaa yetu') lakini sasa wanamfurahia Magufuli kutokana na huu utumbuaji wa majipu, lakini kuna waliomchagua Magufuli, akiwemo Kikwete na wote waliotumbuliwa, ambao kutokana na nyadhifa zao, lazima walimchagua Magufuli, lakini sasa wanajuta?!.

Hii tumbua tumbua ya majipu, imekuwa popular hadi kubadili majina ya watu, wale wote waliotumbuliwa, hawatajwi tena kwa majina yao, bali sasa wanaitwa "jipu", hata majirani zao wanawaona kama ni majibu!, mtu unajitolea kuacha maslahi bora ughaibuni kwa kusukumwa na uzalendo, na kuamua kurejea nyumbani, kuitumikia nchi yako kwa moyo wa kujitolea tuu, mara ghafla unatumbuliwa!, hata jina unabadilishwa unaitwa "jipu", is this fair kweli?!.

Kama JK bado anajisikia proud kumkabidhi nchi Magufuli, kwa haya anayoyafanya na kwa stahili hii, ikiwemo uonevu na kuaibishana, then JK ndio mwenye matatizo!.

Imeandikwa na Pasco

Video ya Chura Yawa Gumzo Mtandaoni..Hivi Ndivyo Inavyozungumziwa nje na Ndani ya Tanzania

$
0
0
Video ya Mwanamuziki Snura iliyotoka hivi Karibuni imekuwa gumzo mtandani kwa jinsi wadada wanavyotingisha makalio kwa mtindi wa Chura kama jina la wimbo huo unavyoitwa..Japo video hiyo mpaka sasa haijachezwa na kituo chochote cha Tv Tanzania lakini huko Youtube inaonekana imeshakuwa maarufu kwani watu nje ya nchi na ndani wamekuwa wakiijadili kwa maoni tofauti tofauti

Hapa nimekuwekea maoni mbali mbali ya Wadau:


Boss Hogg2 
Thats it am going to TZ... Hey tanzanians, place gani poa ya kupata madem wana mizigo huko kwenu... Area gani na club gani.. Mtu anijibu

Ado Ashu1
Astaghfirullah!! Mna laana wote mliojidhalilisha ktk hii nyimbo. Ama kweli thamani ya mwanamke inapotezwa na watu wachache kama nyie.


Niyongabo Idrissa
Mnaosema video haina maadili mnatafuta nini youtube?

La Shay Glenn2 
Wanaosema hii tradition mjiulize kwa nini snura asijiweke hapo,halaf hao wanawake wamevaa mask....obvious its wrong in many ways

emanuel kilima10 
Oooops ladies and gentlemen nimeipenda hii video...its a nys twirking style....kiukwel watu wanaonesha umahiri waoh....katika kudance...kipaji hicho ww unaweza? Dont say dat kwamba video haina maadili kwako tuu ndo itakuwa haina maadili......big up sana snura....tumeipenda hiyoo..

Ali Khamis
Mhu  snura  na  hao  madada  mnajiuza?

Thomas Noel23 
mnaojifanya kukejeli Hii video wenyewe mna madhambi kibao

Jerry Pharel20 
You guys mnaokuja with maadili comments here I think hamjawahi tembele ngoma za uswahilini.
This song is mchiriku (singeli) style, did u expect a video to be in love story type of way?
If u dont like it dont watch it.
Snura u done it right girl!

La Shay Glenn2
Aliekuambia kurusha mitako ni tamaduni ni nani.....Snura mwenyewe hajaweka sura yake hapo plus hao wadada wana mask kuficha id zao....obviously its wrong khaaa....get in ur senses bro

lvyl bby dol17
Ameshaxema yy mwnywe basata kaifungia YouTube xaxa ww mweny maadili unatafta nini uku kwa chura

Kedrick Ross15
Jamani jamani jamani, aisee.Hii wimbo inachangamsha kinouma sana. nimeipenda beat inavyokakamua na  hao wanawake kucheza kwa uchangamfu. Yaani utamaduni uenee.Yaani bora hivi kuliko kucheza nusu uchi kama marekani.Full respect of our ngoma dances. Wanaosema si maadili kwani ngoma za vijijini vilichezwaje? Khaa,mkiendelea na mambo kama hayo mnadhani tutafika mbali? Nyimbo za kuchangamka kama hizi na video vinaoheshimu uchangamfu huo ndo itabeba kucheza huko


Itazame Video Hapa:

Hatimaye Lulu Michael Avishwa Pete ya Uchumba na Dj Majay...Tazama Picha Hapa

$
0
0
 Lulu Amepost Picha Kadhaa Akionyesha Pete yale aliyovalishwa na kuandika maneno haya:

Simplicity z the key.
Kwenye picha nyingine ameandika: Pale unaposikia Kwa…Kwa…Kwa…Kwa Ya Rihanna wakati WA kupiga picha #simplicityisthe


Bosi TIC Juliet Kairuki Katikati ya Jakaya Kikwete na Rais Magufuli

$
0
0
Baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa Juliet Kairuki, mjadala umeibuka kuhusu kitendo cha mkurugenzi huyo mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kutochukua mshahara tangu mwaka 2013 alipoteuliwa na Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete.

Kitendo hicho kimetajwa kuwa moja ya sababu za kutimuliwa kwake.

Swali hilo na sababu tofauti za uamuzi huo ndizo zilizotawala mijadala mbalimbali kwa siku nzima ya jana, ikiongozwa na mitandao ya kijamii.

Rais Magufuli alitangaza uamuzi wa kutengua uteuzi wa Kairuki Alhamisi ya jana akisema uamuzi huo ulifanywa tangu Aprili 24 na kwamba moja ya sababu za kuondolewa kwake ni kutochukua mshahara tangu Aprili, 2013.

“Pamoja na mambo mengine, hatua hii imechukuliwa baada ya Mheshimiwa Rais kupata taarifa kuwa Bibi Kairuki amekuwa hachukui mshahara wa Serikali tangu alipoajiriwa Aprili 2013 mpaka sasa, jambo linalozua maswali mengi,” inasema taarifa ya Profesa Adolf Mkenda, katibu mkuu wa Biashara na Uwekezaji wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Tofauti na watumishi wengine waandamizi ambao baada ya uteuzi wao kutenguliwa Ikulu ilisema watapangiwa kazi nyingine, kwa Kairuki atapangiwa kazi nyingine iwapo atataka kuendelea kufanya kazi serikalini.

Awali ilishawahi kuripotiwa katika vyombo vya habari kuwa Kairuki alikuwa hachukui mshahara uliotajwa kuwa Sh5 milioni (ambao Mwananchi haijaweza kuthibitisha) unaotolewa na TIC kwa kuwa ni mdogo kulinganisha na aliokuwa akipata nchini Afrika Kusini kabla ya kuombwa na Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kuja nchini kusaidia kusukuma gurudumu la maendeleo.

Kabla ya kuteuliwa na Kikwete kushika nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Emmanuel Ole Naiko kustaafu, Kairuki alikuwa akifanya kazi Afrika Kusini katika chama cha benki cha Afrika Kusini, akiwa meneja mkuu wa Idara ya Benki na Huduma za Fedha.

Inadaiwa kuwa akiwa TIC, Kairuki, ambaye ni mwanasheria alikuwa akipendekeza apewe mshahara wa Sh18 milioni kwa mwezi kiwango ambacho kinadaiwa kingeendana na stahiki alizokuwa akipata Afrika Kusini. Madai hayo yalipingwa na Kairuki mwaka jana.

Katika mjadala mwingine, inaelezwa kuwa pamoja na kutolipwa mishahara, Kairuki aliweza kumudu maisha kutokana na kuwa na safari nyingi zinazoendana na nafasi yake ya kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na hivyo kupata posho nzuri.

Kundi jingine lilieleza kwenye mijadala hiyo kuwa Kairuki alikuwa akilipwa posho zinazofikia Sh25 milioni na hivyo kuweza kumudu maisha bila ya kuchukua mshahara.

Hakuna mjadala ulioweza kuthibitisha madai hayo, lakini imeelezwa kwenye mitandao hiyo kuwa hali iligeuka baada ya Serikali kukubaliana naye mshahara na mtendaji huyo kudai malimbikizo yote ya mishahara ambayo hakulipwa.

Jitihada za kumpata Kariuki jana ziligonga mwamba.

Profesa Mkenda hakutaka kuzungumzia kwa undani suala hilo la mshahara na mtumishi wake wa zamani.

“Mshahara wa nafasi hiyo upo na umekuwepo siku zote. Kabla yake kulikuwa na mtangulizi wake alikuwa anapokea mshahara,” alisema Profesa Mkenda kupitia ujumbe mfupi wa simu.

Alipoulizwa ni jambo gani lilitokea hadi Kairuki asichukue mshahara huo na Serikali ilichukua hatua gani za awali kumalizana naye mapema kabla ya kumalizika miaka mitatu, Profesa Mkenda hakujibu ujumbe wa swali hilo.

Lakini alisisitiza kuwa ngazi ya mshahara ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIC ipo na haijawahi kubadilishwa tangu taasisi hiyo ianzishwe.

Hata hivyo, mwandishi wetu alipotaka ufafanuzi kutoka kwa katibu mkuu huyo iwapo mshahara ulikuwa ukiingia katika akaunti ya Kariuki halafu hautumii au haukupelekwa kabisa katika akaunti yake, hakujibu.

Katibu Mkuu Wizara ya Utumishi, Dk Laurian Ndumbaro alisema jambo hilo alikuwa amelisikia kwa mara ya kwanza mchana na kueleza kuwa Profesa Mkenda ana majibu zaidi.

Alipoombwa kuelezea iwapo kanuni au taratibu za utumishi zinambana mtu asiyechukua mshahara, aliahidi kumtafuta mwandishi kwa kuwa alikuwa bungeni lakini baadaye hakupokea tena simu.

Watu waliohojiwa na Mwananchi walikuwa na maoni tofauti.

Mhadhiri wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Damian Shumbusho alisema iwapo alitenguliwa bila uchunguzi wa kina, uamuzi huo si wa busara.

Alisema kuwa iwapo kukubali kufanya kazi pasipo kuchukua mshahara ni kosa kwake na Serikali nayo inawajibika kwa kuwa Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya Mwaka 2004 hairuhusu mtu kufanya kazi kabla ya makubaliano. “Hapa tatizo linaonekana lipo kwenye mkataba. Pasipo makubaliano ya mshahara mtu hawezi kufanya kazi,” alisema Shumbusho.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wafanyakazi Tanzania (Tucta) Nicholas Mgaya alionyesha wasiwasi wa mwajiriwa kutochukua mshahara.

“Unakula nini siku zote kama huchukui mshahara? Kwanini huchukui mshahara wako na kuutumia. Una kula rushwa au una chanzo kingine cha mapato kisichojulikana?” alihoji.

Alisema Tucta hawawezi kuzungumzia jambo lolote linalohusu wateule wa Rais kwa kuwa ana mamlaka kikatiba kutengua uteuzi wao, lakini wana uhakika Dk Magufuli alifanya uchunguzi wa kina na kushauriwa na wataalamu kabla ya hatua ya jana.

Mtaalamu wa masuala ya rasilimali watu, Elias Baraka kama wengine alihoji Kairuki alikuwa akiishi vipi bila kuchukua mshahara na kama uchunguzi umebaini hivyo ana tatizo la kukwepa uwazi.

“Kama uchunguzi umefanyika na ukabaini hivyo, ana kosa la kutokuwa mwaminifu. Hakuwa muwazi. Alikuwa anaishije bila mshahara? Hivyo adhabu hiyo itakuwa sahihi vinginevyo alitakiwa asimamishwe kwa uchunguzi zaidi,” alisema Baraka.

Wakati Profesa Mkenda akitangaza utenguzi huo, Kairuki alitakiwa kuwa mmoja wa waongozaji wa mkutano wa wawekezaji kutoka Urusi uliokuwa ukiendelea jana kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere.

Kairuki, ambaye taasisi yake ilikuwa moja ya waandaji wa mkutano huo, hakuonekana tangu asubuhi hata kabla ya tangazo la kutumbuliwa. Ratiba ya mkutano huo inaonyesha kuwa alitakiwa kuongoza mkutano huo muhimu sambamba na mwanzilishi wa kampuni ya b2b-export.com kutoka Urusi, Ekaterina Dyachenko na kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya Uendelezaji Biashara Tanzania (Tantrade), Edwin Rutageruka.

Waziri wa Biashara, Viwanda na Uwekezaji, Charles Mwijage a aliyekuwepo katika mkutano huo, alipoulizwa kuhusu sababu ya Kairuki kutopokea mshahara na sababu za Serikali kutochukua hatua kwa miaka aliyotumikia TIC, alisema hakuwa na taarifa za kutimuliwa kwa Kairuki.

“Hii ni habari (mpya) kwangu. Nimefika kutoka bungeni asubuhi hii,” alisema.


Wananchi Wamelielewa Soma la TCRA...Simu Feki Nchini zazidi Kupungua....

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema idadi ya namba tambulishi ambazo zilikuwa hazina viwango zimeendelea kupungua kutoka asilimia 30 mwezi Desemba hadi kufikia asilimia 13, Machi mwaka huu.

Kutokana na kupungua huko, inamaanisha kwamba simu feki nchini zinazidi kupungua.

Akizungumza na vyombo vya habari leo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TCRA James Kiraba amesema katika uchambuzi na matokeo ya awali ambacho pia kilishirikisha kampuni za mawasiliano kimeonyesha kuwa mwezi Februari ilishuka mpaka asilimia 18.

Amesema uchambuzi wa Februari ulionyesha idadi ya namba tambulishi ambazo hazikuwa na viwango zilikuwa asilimia tatu, vilevile idadi ya namba tambulishi ambazo zimenakiliwa zilikuwa na asilimia 18, huku simu halisi zikiwa asilimia 79.

"Uchambuzi wa Machi unaonyesha idadi ya namba tambulishi ambazo hazina viwango zilikuwa sawa na asilimia mme, huku idadi ya namba tambulishi ambazo zimenakiliwa zilikuwa asilimia 13. Uchambuzi huu unahusisha kampuni zote za simu nchini," amesema Kiraba.

Ahadi ya Rais Magufuli Kuonyesha Salary Slip ya Mshahara Wake Akitoka Likizo yakumbushiwa....

$
0
0
Mdau mmoja wa ACT Wazalendo  kutoka Kibaha ajulikanae kama Habib Mchange ameandika yafuatayo kwenye ukurasa wake wa Facebook kuhusu ahadi ya Rais Magufuli kuonyesha Salary Slip ya Msahara wake:


"Hivi Rais ‪#‎MAGUFULI‬ bado yupo likizo au amesharudi kazini Magogoni?.
Mbona alituahidi kutuonyesha ‪#‎SALARY‬-‪#‎SLIP‬ yake anayolipwa 9.5ml. Kila mwezi kama mshahara na Mpaka leo Kimya?.
#Magufuli Baba ahadi ni deni. Tuwekee wazi kale ka salary Slip kako ili tuone unavyoyaishi maneno yako.
Yawezekana umesahau na wanaokuzunguka wanaogopa kukukumbusha wanahofu utawatumbua.
Kwetu sisi ‪#‎ACtWAZALENDO‬ ni Kusema ukweli tu bila kumung'unya Maneno.
‪#‎AuNaloJipu‬?" By Habib Mchange

Tanzania Yapata Dili mpya Uganda La Kujenga Bomba Jingine la Gesi

$
0
0
Baada ya Tanzania na Uganda kukubaliana mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta utekelezwe kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, matumaini mengine mapya yameonekana kutokana na Uganda kuweka wazi azma yake ya kujenga bomba jingine la gesi katika njia hiyohiyo kwa ajili ya biashara na Tanzania.

Licha ya kutofafanua kwa kina juu ya mpango huo, Waziri wa Maendeleo ya Nishati na Madini wa Uganda, Irene Muloni aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Serikali ya Uganda na Tanzania bado ziko kwenye majadiliano ya kuanzisha mradi mwingine wa bomba hilo la gesi.

“Ni mpango mpya bado tunajadiliana, kuna uwezekano mkubwa wa kujenga bomba hilo lakini utekelezaji wake utaanza baada ya mradi huo wa bomba la mafuta wa sasa kukamilika,” alisema. 

Waziri Muloni aliyekuwa ameongozana na mwenyeji wake Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alitoa kauli hiyo katika mkutano wa kwanza wa jopo la watalaamu wa sekta mbalimbali waliokutana kwa mara ya kwanza kuandaa mpango wa utekelezaji wa mradi huo.

Mkutano huo unafanyika ikiwa ni siku sita tangu azungumze na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili nchini akitokea Kampala ambako Rais wa Uganda, Yoweri Museveni alitangaza kuwa bomba hilo la mafuta ghafi kutoka Hoima, Ziwa Albert litapita katika ardhi ya Tanzania kwenda Bandari ya Tanga.

Waziri Muhongo alisema mbali na bomba hilo, nchi nyingine za Afrika Mashariki pia zimekubali kununua gesi ya Tanzania.

Kuhusu mradi wa bomba, Profesa Muhongo alisema nchi hizo zimekubaliana kukamilisha Kazi hiyo kabla ya makubaliano ya awali ya 2020.

Makubaliano mengine ya nchi hizo ni kuchangia ujenzi wa mtambo wa kuchakata mafuta ghafi utakaojengwa Uganda ambao alisema utasaidia kuweka akiba ya mafuta kwa ajili ya biashara kwa nchi wanachama.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 30, Ikiwemo ya Magufuli Amvaa Lugumi

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya April 30, Ikiwemo ya Magufuli Amvaa Lugumi

Breaking News: Jambazi Sugu la Tigo Pesa Lakamatwa Dar es Salaam , Wenzake Wawili Watoroka

$
0
0
MTU MMOJA ANAYE SAKIKIKA KUWA JAMBAZI AMEKAMATWA JIJINI DAR MAENEO YA POSTA BAADA YA KUTAKA KUMTAPELI MAMA MMOJA ANAYE FANYA KAZI YA TIGO PESA …

MASHAHIDI WALIO KUWEPO ENEO HILO WANASEMA HUYO KIJANA ALIFIKA KWA DADA HUYO KWA LENGO LA KUTAKA KUWEPA PESA KIASI CHA TSH.ELFU TANO ..

WAKATI YULE DADA ALIKUWA ANAHESABU PESA ZAKE KWANZA NDIPO HUYO JAMBAZI AKAKWAPUA NA KUKIMBILIA NDANI YA GARI AINA YA NOAH..NA KUMRUSHIA MTU ALIYEKUWA NYUMA YA HILO GARI….

WAKATI HUO MCHEZO UKIENDELEA NDIPO DEREVA AKAWA ANAJIANDAA KUWASHA GARI NA KUONDOKA NDIPO RAIA WAKAMDAKA DEREVA NA KUMTOA KWENYE GARI

 …LAKINI DEREVA NA YULE ALIYEPOKEA PESA AKACHOROPOKA ..ILA YULE ALIYEIBA AKANASWA NDO HUYO KWENYE PICHA
Viewing all 104684 articles
Browse latest View live




Latest Images