Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Madawa ya Kulevya yamponza Mwanamuziki Ferooz...Mwenyewe Asema Haya

$
0
0
Baada ya ukimya wa muda mrefu sana wa wakongwe wa muziki wa Bongo Flava story zilizopo mtaani ni kuwa Ferooz ni miongoni mwa wasanii wanaotumia madawa ya kulevya na ndiyo sababu iliyompoteza kwenye reli ya muziki.

Kupitia Enewz Ferooz alikanusha tuhuma hizo na kudai kuwa misongo ya mawazo ndo huwa inawapelekea wasanii kuingia katika matumizi hayo ya madawa ya kulevya na kuwataka wengine wasifanye hivyo.

Ferooz amesema kuwa “Ni mara kumi upate UKIMWI kuliko uwe unatumia madawa ya kulevya” lakini pia akaongezea kwakusema “Nawashauri watu wengine pamoja na wasanii wenzangu wasije wakajaribu kufanya hivyo”.

Nafasi za Kazi Zilizotangazwa Mitandaoni leo Tarehe 30 April 2016

MSD Yaigeuzia Kibao Muhimbili Kuhusu Kuhusu Utata wa Dawa Uliobuliwa na CAG

$
0
0
Sakata la upotevu wa vifaatiba na dawa kutoka Bohari ya Dawa (MSD) kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kipindi cha miaka minne limeingia katika sura mpya baada ya MSD kuigeuzia kibao hospitali hiyo, huku ikitoa ushahidi wa ankara 23 zilizotumika kupelekea vifaa hivyo kwa kipindi cha miaka minne.

Ripoti iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad inaonyesha ukaguzi ulifanyika Muhimbili, huku rekodi zikionyesha kwamba hospitali hiyo ilikuwa ikiagiza mzigo kutoka MSD, lakini hazionyeshi kupokea vifaa hivyo tangu mwaka 2012/14.

Kwa kutumia vielelezo vya nyaraka hizo mbele ya vyombo vya habari jana, MSD ilitoa ufafanuzi kuwa haihusiki katika upotevu huo kwani iliwasilisha MNH vifaatiba na dawa zenye thamani ya Sh2.6 bilioni na kupokewa stoo kwa nyakati tofauti kwa kipindi cha miaka minne.

Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Lauren Bwanakunu alisema hati za CAG, zinaonyesha kuwa MSD haina tatizo lolote.

“Ankara hizo siyo kwamba dawa hazikufika hospitalini hapo, bali hazikuonekana kwenye vitabu vya kupokelea mali vya Hospitali ya Taifa Muhimbili,” alisema.

Alisema baada ya kupitia nyaraka zake, MSD imefanikiwa kupata uthibitisho wa hati za kupelekea mali za dawa na vifaatiba vyote vilivyopelekwa Muhimbili, ambavyo ni pamoja na dawa za figo na moyo.

Bwanakunu alisema pamoja na juhudi hizo, Bohari ya Dawa imewasiliana na Muhimbili ili kuainisha taarifa za kwenye ankara na shehena ya dawa na vifaatiba vilivyopelekwa hospitalini hapo, kwani utaratibu wa kupeleka na kukabidhi dawa hospitalini unamlazimu mpokeaji kusaini ankara inayoonyesha mzigo uliopelekwa kwa mteja (delivery notes) ambazo zote zipo Bohari ya Dawa.

“Vitabu vyetu kutoka kwa CAG vipo na tumepata hati safi, tumethibitisha kwamba mzigo wote wa ankara 23 ulipelekwa Muhimbili kwa kipindi cha miaka minne,” alisema.

 Alisema MSD ilikuwa ikiwasilisha dawa tangu mwaka 2012 kwa mujibu wa maombi kutoka MNH, hivyo hospitali hiyo inapaswa kujibu kwa kuwa imekuwa ikipokea dawa hizo kwa kipindi tofauti.

“Vifaa vyenye thamani ya zaidi ya Sh2.03 bilioni vilikuwa vikiagizwa kwa tarehe tofauti kwa miaka mitatu lakini havikuwahi kuingizwa katika rekodi.

"Kulingana na utaratibu wa usambazaji wa MSD, mteja hukiri kupokea mzigo kupitia Ankara ya mauzo (Sales Invoice), jukumu la kuandika hati ya mapokeo (GRN) ni la mteja husika ambaye ni Muhimbili,” alisema Bwanakunu huku akionyesha nakala hizo.

Ankara zilizotolewa jana na MSD zinaonyesha kuwa ilikuwa ikihudumia hospitali hiyo tangu Mei 14, 2012 hadi Desemba 4, 2014, lakini katika ankara hiyo, Muhimbili haikuonyesha kuwahi kupokea vifaa hivyo vyenye thamani ya Sh2,028,625,100.

 Alichosema CAG
Katika ukurasa wa 37, taarifa ya CAG, inaeleza kuwa ukaguzi huo ulibaini kuwa dawa na vifaatiba vyenye thamani ya Sh2.03 bilioni havijafika Muhimbili tangu Mei 2012 licha ya kuonekana kwenye ankara 23 za MSD.

Nakala hiyo ilieleza kuwa kwa hali ya kawaida, haikutarajiwa bidhaa hizo kuchukua zaidi ya wiki moja kufikishwa sehemu husika ukizingatia ofisi za MSD na MNH zote zipo Dar es Salaam.

“Hali hii inaashiria uwezekano wa upotevu wa dawa na vifaatiba pasipo uongozi kuwa na taarifa. Menejimenti inashauriwa kuchunguza jambo hili ili kubaini kama kweli bidhaa hizo bado zipo safarini,” inasema taarifa ya CAG.

Msimamo wa Muhimbili
Akijibu hoja hiyo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma, Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha alisema MNH inazo hati za kupokelea ‘Develivery note’ za mizigo iliyopokea bila ankara, kinachohitajika ni MSD kuoanisha ankara walizozitaja na hati walizozifikisha hospitalini hapo.

Aligaesha alisema namba za ankara zilipatikana kwenye maelezo ya MSD yaliyowasilishwa MNH ikionyesha matumizi ya hospitali kwenye akaunti iliyopo MSD kutokana na fedha ambazo Serikali inapeleka huko.

“Ili kukamilisha utaratibu wa kupeleka mzigo mahali, mzigo huo unapaswa uambatane na nyaraka kama mkataba kati ya mnunuaji na muuzaji, ankara na hati ya kupokelea. Endapo mzigo ulioletwa ni wa msaada, mkataba hauhitajiki, kwenye msaada ni lazima hati ya kupokelea iwepo na nakala inayoonyesha thamani ya mzigo,” alisema.

Alisema kwa muda mrefu imekuwa ni kawaida MSD kupeleka baadhi ya mizigo Muhimbili au wazabuni walioagizwa na MSD ikiwa haina viambatanisho hivyo muhimu, kwani mpaka sasa Muhimbili ina orodha ya mali ambazo zilipelekwa kwa kutumia hati ya kupokelea katika kipindi husika.

 “Hata hivyo, tulifuatilia ankara za mizigo iliyokwishapokewa kutoka MSD ili tuweze kupewa ankara husika kwa mizigo tuliyopokea bila kiambatanisho hicho, lakini kwa bahati mbaya ankara zilizodurufiwa kutoka kwenye mfumo wa MSD hazionyeshi namba ya hati (customer reference) na hazijasainiwa na wao wala sisi,” alisema Aligaesha.

Nani Atashuka Daraja leo Coastal Union Au African Sports..Dakika Tisini Kusubiriwa

$
0
0

Dakika 90 za mchezo wa leo kati ya wapinzani wa jadi Coastal Union vs African Sports zitaamua ni timu gani itaanza kuipa mkono wa kwa heri ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara msimu huu. Timu itakayokubali kichapo ni wazi itakuwa imeiaga ligi huku matokeo ya sare yakiwa mabaya kwa timu zote.

Maandalizi kwa pande zote tayari yamekamilika, African Sports wao wakiwa wamejichimbia maeneo ya Mwakidila wakijifua vikali chini ya kocha wao Athumani Cairo kikosi chao kikiwa kimekamilika bila majeruhi.

Kwa upande wa Coastal Union kocha mkuu Ally Jangalu amesema, vijana wake wako vizuri na wanazidi kuimarika kadiri siku zinavyokwenda mbele.

Mimi ninashukuru kwasababu mpaka sasa hivi tumejiandaa vizuri kwa ajili ya mchezo wetu dhidi ya African Sports lakini kama sisi tumejiandaa vizuri basi na wapinzani wetu watakuwa wamejiandaa vizuri. Sisi tumejiandaa kushinda na wenzetu wamejiandaa kwa ajili ya kushinda, basi atakaecheza vizuri ashinde kwasababu timu zote ni za nyumbani.

“Kila mchezaji anaelewa matokeo ya sare au kufungwa yanamaanisha sisi ndiyo tumeiaga ligi kuu lakini tangu tumecheza na Simba kiwango chetu kimekwenda juu, tukacheza na JKT Ruvu tukashinda lakini hata mchezo wetu dhidi ya Yanga licha ya kufungwa, uwezo wa Coastal kila mtu kauona”, Ally Jangalu anasema kuelekea mchezo wa leo jioni.

Wakati huohuo mchezaji wa kimataifa wa Coastal Union Chidiebere Abasirim ameutaka uongozi wa klabu hiyo umkabidhi barua yake ya kumsimamisha huku akisisitiza kulipwa mshahara wake.

Chidiebere anaidai Coastal Union mshahara wa miezi mitatu madai ambayo yanatofautiana na kauli ya kaimu katibu mkuu wa Coastal Union Salim Bawazir kwamba wamemsimamisha nyota huyo na wanaendelea kumlipa mshahara wake.

“Chidiebere tumemsimamisha kwa michezo mitatu na tunaendelea kumlipa mshahara wake, bado ni mchezaji wetu halali na ataendelea kulipwa mshahara wake kama kawaida”, anasema Salim Bawazir.

Nay Aliachwa na Shamsa Ford Sababu ya Vibomu-Niva

$
0
0

Msanii wa filamu nchini Niva Super Mariyoo, ambaye alionja joto ya jiwe kwa muda fulani baada ya kutajwa kwenye wimbo wa Nay wa Mitego 'Shika adabu yako' na kusema "Huyo msanii huyo hana hata chumba cha kupanga ila anaishi kwenye gari".

Niva amefunguka na kusema kuwa Nay wa Mitego siku zote huwa anaimba watu maarufu ili apate kiki na kusema msanii huyo kutokana na kufanya nyimbo mbovu mbovu ndiyo maana hata siku moja hajawahi kupata tuzo.

Akizungumza kwenye kipindi cha eNEWS Niva Super Marioo amedai kuwa ni kweli kwa sasa wanawake wengi wanafanya kazi na kutafuta riziki na wanakuwa wanawasaidia baadhi ya wanaume ambao kazi yao kukaa nyumbani kama Imma Chogo ambaye ni (Nay wa Mitego).

"Kimaisha mimi Imma Chogo hajanifikia sema sisi wengine huwa hatupendi kujiweka wazi sana, kama kweli mtu unamiliki nyumba, una kwako kwanini hutulii na familia? kama kweli wewe unajiona ni Gentle Man kwanini wanawake wanakukimbia? Star anakimbiwa? mimi najua Star anakimbiliwa. Mimi silelewi bali napewa mahaba ya dhati na mwandani wangu". Alisema Niva
"Mimi namkubali sana Shamsa Ford sababu aliona kabisa yeye ni classic sana kuliko Nay wa Mitego na ndiyo maana hajadumu naye akaachana naye, Nay wa Mitego tatizo haudumii na ndiyo kesi kubwa na Shamsa. Shamsa alikuwa akitoka kupiga movie lile bwana mkubwa linaanza kulialia oohh mara gari halina mafuta mara sijui nini, sasa yeye muziki wake yeye kweli kabisa kwanini anashindwa kumnunulia hata vitu anajinunulia mwenyewe" Niva aliongezea.

Rais Magufuli Anavyokubalika Kenya..Timu ya Mpira yaita Tawi lake jina la Magufuri

$
0
0

Jina la Rais wa Tanzania limekuwa gumzo sehemu nyingi duniani kutoka na staili yake ya kuongoza na kufatilia mambo, nchini kwenya mashabiki wa Timu ya mpira ya Gorimahia wameunda Tawi la timu hiyo na kujiita jina la magufuli kama inavyoosha hapo kwenye picha, hiyo ikiwa ni kuonyesha jinsi gani wanavyomkubali Rais huyo na kauli mbiu yake ya hapa kazi tu..

Aliyejifanya Ofisa usalama wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Atupwa jela Miaka 12

$
0
0

Mahakama ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, imemhukumu kwenda jela miaka 12, Qasama Machibya aliyejifanya ofisa usalama wa Taifa kwenye ziara ya Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete mwaka 2013.


Kabla ya hukumu, mshtakiwa alijitetea mahakamani hapo kuwa kitambulisho alichokutwa nacho siyo chake na anashangaa kuona kuna picha yake na jina lake.


Alidai kuwa hizo ni mbinu za polisi kumminya, hivyo aliiomba Mahakama kumpunguzia adhabu na kwamba ana ugonjwa wa Ukimwi.


Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Gabriel Kurwijila alisema utetezi wa mshtakiwa hauifanyi mahakama kutomtia hatiani kwa kuwa hana cheti cha ugonjwa.


Alisema kutokana na mahakama kuridhishwa na ushahidi wa upande wa mashtaka uliowasilishwa inamtia hatiani kwa makosa matatu.


Kurwijila alisema kosa la kwanza ni kughushi nyaraka ya Serikali hivyo, atakwenda jela miaka mitano na kosa la pili la kujifanya ofisa usalama wa Taifa kifungo chake ni miaka miwili.


Alisema katika kosa la tatu la kuudanganya umma kwa kutoa nyaraka iliyoghushiwa hivyo, atatumikia adhabu gerezani miaka mitano.


Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Elias Mgobela alisema mshtakiwa alikamatwa wakati Kikwete alipokuwa akitarajia kuhutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Rais mstaafu Jakaya Kikwete ametaja mali alizochuma alipokuwa madarakani kwa miaka 10.

$
0
0

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE.
Kamishna wa Tume ya Maadili, Jaji mstaafu Salome Kaganda ameiambia Nipashe katika mahojiano maalumu katikati ya wiki kuwa Kikwete ameshawasilisha tamko la mali zake tangu aondoke madarakani Novemba 5, mwaka jana.

Jaji Kaganda alisema Kikwete aliwasilisha fomu inayoonyesha mali alizozipata wakati akiwa madarakani kati ya 2005-2015, na alizozipata kabla hajangia madarakani kwa Sekretarieti yake.

Nipashe ilizungumza na Jaji Kaganda kujua kama Kikwete alishatoa tamko kama Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995 na kanuni zake zinavyoelekeza, lakini pia kufahamu idadi ya mali anazomiliki Rais huyo mstaafu na thamani yake.

Kaganda alisema ni kweli Kikwete aliorodhesha mali zake zote kwa tume lakini Jaji huyo alikataa katakata kumwonyesha mwandishi wa habari hizi tamko hilo.

Jaji Kaganda alisema sheria inazuia kumwonyesha mtu mwingine tamko la mali la mtu mwingine hadi kuwe na sababu ya maana ya anayehitaji, na pia kuwe na ulazima wa kufanya hivyo.

"Mwananchi anaweza kupata taarifa za mali za viongozi kwa kufuata utaratibu uliopo, lakini baada ya kupata taarifa hizo, haruhusiwi kuzitangaza au kuzichapisha kwenye vyombo vya habari,” alisema Jaji Kaganda.

Kwa mujibu wa kifungu kifunga 9(1) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, “Kila kiongozi wa umma atatakiwa katika kipindi cha miezi mitatu au katika kipindi cha siku thelathini baada ya kupata wadhifa, mwisho wa mwaka au mwisho wa kutumikia wadhifa wake kumpelekea Kamishna tamko la maandishi katika hati rasmi linaloorodhesha mali au rasilimali zake.”

Aidha, kifungu namba 9 (6) kinataka “Wakati wa kutoa tamko la rasilimali zake kwa mujibu wa fungu hili, kiongozi wa umma atatakiwa: (a) kutaja thamani ya mali aliyotamka na chanzo au namna alivyopata mali hiyo."

Kifungu namba 11 (2) cha sheria hiyo kinaeleza kuwa rasilimali zinazotakiwa kutajwa ni pamoja na (a) nyumba, mali ya starehe na mashamba yanayotumiwa au yanayotarajiwa kutumiwa na viongozi wa umma au familia zao.

Kifungu 2 (b) kinataka kutajwa kwa kazi za sanaa, mambo ya kale na vitu alivyonunua kidogokidogo; (c) magari na aina nyingine binafsi za usafiri kwa matumizi binafsi; (d) fedha taslimu na amana zilizowekwa benki au taasisi nyingine za fedha.

Kifungu 2 (e) kinataka taarifa za hawala za hazina na uwekezaji mwingine katika dhamana zenye thamani maalumu, zinazotolewa au kudhaminiwa na serikali au wakala wa serikali.

SH. MILIONI 25

Wakati viongozi wengi wa umma wakitaja mali zao kwa Tume ya Maadili tu ama kushindwa kutaja mali hizo huko kwa mujibu wa sheria, Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda ana historia ya peke yake.

Pinda alitaja mali anazomiliki ambazo miongoni mwake ni nyumba mbili pamoja na akaunti katika benki, zilizokuwa na fedha zisizozidi Sh. milioni 25 Januari 15, 2010.

Pinda alisema alikuwa akimiliki nyumba moja mjini Dodoma na nyingine Mpanda, mkoani Rukwa eneo la Makanyagio.
Aidha alisema alikuwa na kibanda shambani kwake Pugu, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

“Mimi kila mwaka nataja mali zangu kwa Tume (Sekretariati ya Maadili ya Viongozi wa Umma)," alisema Pinda wakati huo akiwa madarakani. "Sijaulizwa, sijagombana na Tume.

"Ukiniuliza ni masikini kiasi gani, nitakwambia nina property (nyumba) Dodoma, nimejenga kwa utaratibu wa serikali wa kuomba mkopo, ninayo nyingine kwetu Mpanda pale Makanyagio.

“Dar es Salaam sina nyumba, pale Pugu nina nyumba kidogo, inahitaji kazi ya ziada.

"Kijijini nilikuwa nafikia kwa babu, babu ana kanyumba kake ka ovyo ovyo… kile ambacho mlikiona, ana vyumba viwili nilikuwa nalala pale, lakini baada ya Uwaziri Mkuu, jamaa wakaniambia aah… haiwezekani pale.

"Nilijua nitaweza kulala pale na hawa jamaa (wasaidizi wake) watalala mjini humo, nikaambiwa hapafai.”

Pinda ambaye wakati huo alikuwa pia Mbunge wa Mpanda Mashariki, alisema hana gari lolote zaidi ya alilopewa kwa kuwa Mbunge, na kwamba katika akaunti zake zote, wakati huo alikuwa na Sh. milioni 22 hadi 25 tu.

Chanzo: Nipashe

MSAJILI WA HAZINA: Simon Group inamiliki 51% ya Hisa UDA na Serikali 49%, Jiji halina hisa

$
0
0

SERIKALI imetetea uuzwaji wa hisa za Shirika la Usafirishaji nchini (UDA) kwa Kampuni ya Simon Group na kwamba, kampuni hiyo inamilika hisa hizo kihalali.

Lawrance Mafuru, Msajiri wa Hazina akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam amesema, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliiuzia UDA hisa kihalali.

Utetezi huo unawapa pumzi Mama Salma Kikwete, Mke wa Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete na Ridhwan Kikwete, mtoto wa rais huyo na Prof. Juma Kapuya, aliyekuwa Mbunge wa Urambo Magharibi ambao wanatajwa kuwa miongoni mwa wana hisa kwenye kampuni hiyo.

“Bodi ya UDA iliyokuwepo muda ule ilikiuka taratibu za uuzaji wa hisa za serikali bila ya Baraza la Mawaziri ambalo lenye mamlaka ya kufanya maamuzi ya uuzwaji wa hisa kuamua kuuza hisa hizo,” amesema Mafuru.

Anaeleza kuwa, Bodi ya UDA iliamua kuuza hisa kwa Kampuni ya Simon Group baada ya kuona shirika hilo linayumba hivyo lilihitaji muwekezaji ili kulifufua.

“Baraza la Mawaziri chini ya mwenyekiti wake ambaye ni rais halikukaa kikao cha kufanya maamuzi ya kuuza hisa na kwamba, baada ya bodi kuona serikali inachelewa kutoa maamuzi ikaamua kuuza hisa za serikali,” anasema.

Amefafanua kuwa, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ndilo lililouza hisa zake kupitia Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji hilo kwa kushirikiana na wajumbe wenzake watatu akiwemo Mwanasheria wa Jiji.

“Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na jiji, lilipokea fedha kutoka Kampuni ya SGL kwa ajili ya manunuzi ya hisa zake na kwamba kwa sasa jiji halimiliki UDA, ” amesema.

Amedai, UDA linamilikiwa kihalali na Kampuni ya SGL ambayo inahisa asilimia 51 iliyouzwa na jiji pamoja na serikali ambayo ina hisa ya asilimia 49.

“Aliyeuza hisa za UDA kwa SGL ni Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na wajumbe wengine watatu akiwemo Mwanasheria wa Jiji, sasa kama Masaburi hakuwa Meya halali wa jiji basi hisa hazikuuzwa kwa kampuni ya SGL,” ameeleza.

Akieleza mwanzo wa ugawaji wa hisa za UDA kutoka kwa serikali kwenda Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ambapo amesema, serikali iliona bora igawe hisa za asilimia 51 kwa jiji hilo ambalo UDA linapofanya kazi zake.

“Mnamo mwaka 1974 serikali ilianzisha shirika la UDA, mwaka mmoja baadaye serikali iliamua kugawa hisa ya asilimia 51 kwenda kwa jiji la Dar es Salaam na yenyewe kubaki na asilimia 49 ambazo inazo hadi sasa,” amesema.

Hivi karibuni Isaya Mwita, Meya wa Jiji la Dar es Salaam na Baraza la Halmashauri ya Jiji hilo lilikana kuitambua Kampuni ya SGL kuwa, mmiliki halali wa UDA.

Kwa mujibu wa maelezo yao, Masaburi alichukua jukumu la kuuza hisa za jiji kwa Kampuni ya SGL bila kulishirikisha baraza la madiwani la kipindi ambacho uuzaji ulipofanyika.

Siku tatu zilizopita, Saed Kubenea, Mbunge wa Jimbo la Ubungo alisema, halmashauri haikuuza UDA licha ya Simon Group Limited kudai kununua.

Kwenye mkutano huo ambao pia uliohudhuriwa na Isaya Mwita Charles, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Kubenea alisema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu.

“Kwanza tunataka mtambue halmashauri haikuuza UDA kwa kuwa, Simon Group Limited wametumia hati ya UDA – mali ya wananchi kufanya biashara. Haturudishi fedha hizi mpaka tufanye hesabu, tujue kampuni hii imepata faida kiasi gani.

“Hata katika mradi wenyewe wa UDA-TR, kumesheheni utapeli. Unaoitwa mkutano mkuu maalum wa wana-hisa wa tarehe 10 Juni 2011, uliosimamiwa na Didas Masaburi, aliyekuwa Meya wa Jiji kuidhinisha pamoja na mengine, uuzaji wa hisa za UDA, haukuwa halali,” amesema Kubenea.

Kubenea amesema, mkutano uliokabidha UDA kwa Simon Group uliitishwa bila baraka za wenye mali – Baraza la Madiwani la Jiji na Msajili wa Hazina na kwamba, ulihudhuriwa na watu wanne tu

“Watu hawa ni Dk. Didas Masaburi mwenyewe ambaye alikuwa mwenyekiti; Mkurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena ambaye alikuwa katibu; Mwanasheria wa jiji, Isaac Nassor Tasinga na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Phillip Mwakyusa,” amesema Kubenea.

Abiria Wanusurika Kufa Katika Ajali ya Ndege Mjini Bukoba Leo

$
0
0

Watu kadhaa wamenusurika  kufa baada ya ndege ya Shirika la Ndege la Auric Air waliyokuwa wakisafiria kupata ajali katika Uwanja wa Ndege wa Manispaa ya Bukoba ilipokuwa ikitua na rubani kupoteza uelekeo  kama inavyo onekana pichani.

Ndege hiyo ilikuwa ikisafiri kutoka Jijini Mwanza ,tukio limetokea majira ya saa nne asuhuhi ya leo Jumamosi April 30,2016.


Yanga Sasa Haikamatiki...Haya hapa Matokeo ya Leo Dhidi ya Toto Africans

$
0
0

Yanga imeendelea kushinda mechi zake za ligi kuu Tanzania bara baada ya kuifunga Toto Africans ya jijini Mwanza kwa magoli 2-1 kwenye uwanja wa CMM Kirumba, Mwanza.

Toto walianza kupata goli la kwenye mchezo huo lililofungwa na William Kimanzi dakika ya 39 kipindi cha kwanza lakini goli hilo likasawazishwa na Amis Tambwe dakika ya 50 kipindi cha pili.

Yanga walijihakikishia pointi tatu kwenye mchezo huo kupitia beki wao wa kulia Juma Abdul dakika ya 78 na kifanya Yanga kufikisha pointi 65 baada ya kucheza michezo 26 ya VPL.

Ajali: Mvua Zasababisha Jumba la Ghorofa Kuporomoka Kenya

$
0
0

Ijumaa ya March 29, 2013 Wakazi wa mtaa wa Hindhila gandhi, Kisutu Jijini Dar es salaam waligubikwa na majonzi na vilio, mara baada ya jengo llenye ghorofa 16 kuanguka na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 30 na majeruhi wapatao 17, ambapo sababu kubwa ilidaiwa kuwa lilikuwa linajengwa chini ya kiwango

Wakati ripoti ya Tanzania ikitanabaisha hayo, leo nchini Kenya imeripotiwa zaidi ya watu 7 wamefariki baada ya jumba moja kuporomoka mjini Nairobi
Watu zaidi ya 7 wameripotiwa kufariki na wengine zaidi 141 kujeruhiwa vikali baada ya jumba moja kuporoka kutokana na mvua kali zinazo endelea kunyesha nchini humo.

Watu 44 wamekwisha okolewa kutoka katika mabaki ya jumba hilo lililoporomoka.

Mvua kali zilinyesha mjini Nairobi na kusababisha mafuriko.

Vikosi vya uokozi bado

Makonda Asema hataki kuwaona wasanii nyumbani kwake.......Ni Baada ya Kumtosa kwenye uzinduzi wa kampeni ya usafi

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema hataki kuwaona nyumbani kwake wasanii ambao wamekacha kuhudhuria kampeni yake ya usafi ambayo imezinduliwa Jumamosi hii katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es salaam.


Akizungumza katika uzinduzi huo, Paul Makonda ameonesha kusikitishwa na idadi ndogo ya wasanii waliojitokeza kuunga mkogo kampeni hiyo.


“Lakini nashukuru wasanii wote ambao wamejumuika nasi, na kwa kweli hiki ni kipimo cha kuwatambua marafiki zangu wa kweli ni wapi. Na mimi niwaambie tu, sitaki kuona msanii yoyote nyumbani kwangu ambaye hawezi kuniunga mkono kwenye mambo yangu ya maendeleo,”alisema Makonda.


“Sitaki hiyo tabia, nimemuona Steve Nyerere hapa amekuja akiwa amechelewa hilo ni onyo, ukirudia tena nakushughulikia. Huwezi kuwa rafiki yangu alafu kwenye mambo kama haya huhangaiki, wengine wanataka waombwe, eti mbona hujanipigia simu kuniomba nipost, we nani?. Swala la usafi siyo la serikali ni swala la kila mtu,”aliongeza Makonda.


Wasanii ambao walihudhuria uzinduzi huo ni, Mchizi Mox, Yamoto Band, Diamond na team ya Wasafi, Mwasiti, Queen Darleen, Salam TMK pamoja na Steve Nyerere wa bongo movies.h


Katika hatua nyingine Makonda amevitaka vyombo vya usafiri jijini Dar es salaam kuwa na vifaa vya kuwekea uchafu.


Pia wamewataka wafanyabiashara siku ya jumamosi, kufungua maduka yao saa 3 asubuhi ili muda wa asubuhi wautumie kwa ajili ya kufanya usafi.

Ma Producer wa Muziki Bongo Wana Hali Mbaya Sana – Master J

$
0
0
Mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini Tanzania, Master J amesema watayarishaji wa muziki wa Bongo wana hali mbaya sana kwa sasa.

Master J amejiwekea heshima kubwa kwenye;muziki wa Bongo Fleva, pia amefanikiwa kuwatambulisha wakongwe kibao wa muziki wa Bongo Fleva na Hip Hop ambao wamejiwekea heshima kubwa kwa sasa nchini.

Akiongea kwenye kipindi cha FNL, kinachoruka kupitia EATV, Master J alisema ‘watayarishaji wa muziki Bongo wanahalimbaya sana’.

“Unajua maproducer wanahali mbaya sana sasa, madirector ndiyo wanamiliki magari na majumba. Kama inawezekana wasanii waende kufanya show mikoani na video zao halafu waone itakuwaje,” aliongezea.

Video: Idris Sultan Aeleza Jinsi Watu Walivyofuja Pesa zake na Kumsababishia Hasara

$
0
0
Mshindi wa shindano la Big Brother Africa 2014, Hotshots Idris Sultan, amevunja ukimya na kuzungumzia tetesi ambazo zilikuwa zinazagaa kwenye mitandao ya kijamii kwamba kuna mtu alimpatia pesa zake kwa ajili ya biashara lakini akazitumia vibaya kinyume na makubaliano.

Ikumbukwe mshindi huyo wa Big Brother Africa 2014, alipata zaidi ya milioni 500. Pesa ambayo alidai aliitumia kuwekeza katika biashara mbalimbali, na baadae aliweka wazi kwamba pesa hizo zilishaisha.

Akizungumza na Bongo5 Ijumaa hii, Idris amesema ni kweli kuna mtu alikuwa anafanye naye biashara lakini akamwingiza mkenge.

“Kuna watu ambao nimeweza kufanya nao kazi, lakini wakaaribu baadhi ya mambo, nisingependa kuliongelea kwa sababu kuna baadhi ya vitu ambavyo wameviharibu sana, na hawakuweza kuviweka sawa,” alisema Idris.

Aliongeza, “Yaani kama kupunyua, hivi vitu vinatokeaga katika sehemu yoyote, kwenye kampuni, kwenye nini. Kuna watu wanaweza wakafuja mali zako au wakafanya vitu vibaya kinyume na mlivyo kubaliana. Kwa hiyo siyo inshu kubwa sana kwangu, kwa sababu maisha yanaendelea na milango inafunguka,”

Stori ambazo zilikuwa katika mitandao ya kijamii zilikuwa zinadai kuwa meneja wa zamani wa Idris, ndiye ambaye alimwingiza mkenge Idris, kitu ambacho Idris hakupenda kukizungumzia zaidi.

Pia Idris amesema kwa sasa amepata menejimenti mpya ambayo itakuwa inamwongoka katika kazi mbalimbali.

Alinipenda Sana Kabla Hajapata Kazi, Sasa Kapata Kazi Ananiona Bwege

$
0
0
Najuta ni kiherehere cha moyo wangu kukupenda,kukuthamini na jukujali.

Naombeni msaada,ni mpenzi wangu yapata 1&half year katika mahusiano ni binti ambaye tulifahamiana nae siku moja alipokuja na mama yake mdogo ofisini kwangu kupata huduma,

huyu mama yake mdogo ni mtu ninaefahamiana nae hivyo basi akaona haina budi kunitambulisha kwa mwanae nami nikaona ni vizuri kuanzia hapo binti yule alianza kunizoea na kuonesha dalili zote za kunitaka hata baadhi ya siku hufunga safari na kuja kunisalimia.

nami sikua na hiyana huwa sipendi kumkwaza mtu nikawa nampa ushirikiano tu mzur.

kutokana na ubize wa kazi yangu muda wa story huwa sina nikamwambia kama hutojali uwe unakuja saa 12jioni muda ambao nipo off ila sijui kama mama yako mdogo atakubali akasema hilo halina shida nikimwambia nakuja kwako hawezi kunikatalia kiukweli hilo jibu lake lilinipa ulakini!! 

Basi jioni tukawa tunaenda sehemu ya utulivu tunapiga story sana tunapata chakula then tunaondoka tuliendelea hivyo kwa muda mrefu huwa anakuwa kama na kitu cha kutaka kuniambia lakini anashindwa kila usiku lazima anipigie simu na asubuhi lazima aniulize umeamkaje.

kutokana na tabia zake nzuri alizozionesha kwangu nikaona pengine Mungu ndo kanionesha mke mwema nikamtongoza japo sikutumia nguvu hata kidogo alitabasam na kufurahi nakumbuka alinikumbatia na kunipiga busu hadi nilihisi kuwewesuka kwa joto lake.

Nikawa namhudumia kila alichokitaka nilimpatia na alinipenda na kuniheshimu kama mume wake.

Nakumbuka aligombana na mama yake mdogo akawa kahamia kwa dada yake ni mbali kidogo huko nadhani maisha yalikuwa ya shida,alikuwa akinipigia simu "leo baby sijala"nikawa namsaidia akiugua namtumia pesa za matibabu,

SASA basi miezi miwili imepita kapata kazi basi ni dharau mwanzo mwisho simu hapigi,text hanitumii hata nikimtext baada ya masaa mawili ndo anareply tena shortly wiki tatu zimepita kanipigia simu anaumwa bila hiyana nikaenda kumuona na nilimpa kila kitu anachohitaji mgonjwa sikutaka maongezi nikaondoka zangu hadi leo sijawasiliana nae sababu ninahasira nae sana na ninataka nimfanyie kitu ambacho hatakisahau ili iwe fundisho au nyie wanajamvi mnanishauri nini?

Watu 4 na wengine 29 Wajeruhiwa Baada ya Basi la HBS Walilokuwa Wakisafiria Kupinduka Jijini Mbeya

$
0
0
Watu wanne wamekufa papo  hapo na wengine 29 kujeruhiwa baada ya basi la HBS linalodaiwa kuwa ni mali ya kampuni ya Sabena walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mbeya kwenda Tabora kuacha njia na kupinduka katika eneo la maji mazuri, barabara kuu ya Mbeya – Chunya wilayani Mbeya.

Basi hilo likiwa limebeba abiria wengi kuliko uwezo wake, lilianza safari yake ya kuelekea Tabora likitokea jijini Mbeya, lakini inadaiwa kuwa likiwa kwenye mtelemko na kona kali za mlima Mbeya likafeli breki na ndipo dereva wake akaamua kuruka na kuliacha likijiendesha lenyewe hali ambayo ilisababisha lipoteze mwelekeo na kuanguka mtaroni.

Muuguzi wa zamu katika hospitali ya rufaa ya kanda ya nyanda za juu kusini, Jesca Kahangwa amethibitisha kupokea miili ya watu wanne na majeruhi 29 wa ajali hiyo, huku akidai kuwa hali za majeruhi wengi bado ni mbaya.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amewahi katika eneo la ajali na baada ya kupata maelezo ya chanzo cha ajali hiyo, akaliagiza jeshi la polisi kuwatafuta na kuwakamata haraka dereva, kondakta na mmiliki wa gari hilo kwa kosa la kuendesha gari bovu barabarani.

Dogo Janja: Tuwaombee Ali Kiba na Diamond Platnumz

$
0
0
Msanii Dogo janja amewataka watu kuwaombea wasanii Alikiba na Diamond, ili waendelee kuiwakilisha Tanzania vyema kimataifa kama wanavyofanya.

Dogo Janja ameyasema hayo alipokuwa akichati na mashabiki wake, alipotoa fursa hiyo kwa wale wanaomfuata kwenye mtandao wa instagram na kujibu moja ya swali la shabiki alipouliza ni msanii yupi kati ya hao anamkubali zaidi.

“Wote nawakubali na tuwaombee wazidi kututangaza zaidi sababu wana ‘Fan Base kubwa’, aliandika Dogo Janja.

Pia Dogo Janja amesema muziki umemfikisha mbali kutoka kuwa mpiga debe mpaka mpigiwa debe, pale alipoulizwa umefaidika nini tangu alipoanza kufanya muziki.

Mbali na hayo msanii huyo amegusia suala la matumizi ya madawa ya kulevya, alipoulizwa na shabiki wake anachukua hatua gani kupigana na matumizi ya madawa ya kulevya, hususan mtaani kwake alipotokea Ngarenaro Arusha, na kusema kuwa hata yeye anaumizwa na vitendo hivyo, na kutaka wahusika wachukuliwe hatua kwani wanajulikana.

“Mi nahitaji support ya mtaa kuongea na vijana wenzangu, unajua wengi ambao wamejikita humo ni wadogo zangu kaka zangu na baadhi pia ni ndugu zangu inaniuma hata mimi pia, na wanaouza wanajulikana wakamatwe”, alisema Dogo Janja.

Maproducer wa MJ Records Wamtetea Sugu Kupitia Kipindi Cha Friday Night..Wadai Wimbo wa Freedom ni Halali yake....

$
0
0
Utata uliokuwa umeghubika umiliki wa ngoma mpya ya Mr Two a.k.a Sugu inayokwenda kwa jina la Freedom umemalizwa katika show ya FNL baada ya producer wa ngoma hiyo Daxo Chali kuthibitisha rasmi kuwa ni ngoma halali ya Sugu.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa msanii Mr Blue aliyekuwa akidai kuwa Sugu amebadilisha ngoma yake aliyokuwa amemshirikisha, na kuondoa mashairi yake bila ya ruhusa yake, na kasha kuitoa kwenye media.

Akiwa katika kipindi cha FNL kinachoruka kupitia EATV usiku wa Ijumaa, producer wa ngoma hiyo kutoka MJ Records Daxo ambaye pia ndiye aliyekuwa ametengeneza ngoma ya Mr Blue na Sugu, alisema kuwa alichokifanya ni kuchukua ‘beat’ ileile na kumpa Sugu kwa ajili ya ngoma nyingine.
Daxo amesema alifanya uamuzi huo kwa kuwa ‘beat’ ile ni mali yake, na pia aliona kuwa ngoma aliyokuwa amefanya Mr. Blue haikuwa “serious” hivyo baada ya kupata wazo la kutoa ngoma ambayo ni serious kutoka kwa Sugu akaamua kufanya hivyo.

Akiwa ameongozana na Sugu mwenyewe pamoja na mmiliki wa studio za MJ Record, Master J, Daxo amesema kuwa alichokifanya ni halali kwa kuwa katika muziki, ‘beat’ ni mali ya producer.
“Mwanzo kabisa Blue aliongea na Marco Chali, baadaye mimi nikamsikilizisha hii beat ikiwa pamoja na chorus yake, hiyo chorus nimefanya mimi, Blue akaipenda, akaja kufanya ngoma na Sugu lakini ngoma ile haikutoka official, baadaye Sugu akaja, tukampa, kile ambacho ni mali yetu, mashairi ya blue tukayatoa kwa kuwa ni mali yake” Alisema Daxo.

Katika kipindi hicho kilichoanza saa 3:00 hadi saa 5:00 usiku, Daxo aliongozana na Sugu pamoja na Master J ambao wote walionesha kushangazwa na kitendo cha wasanii wa kitanzania kutoelewa masuala ya haki miliki za muziki na kwamba ‘beat’ yoyote inayotengenezwa na producer ni mali ya producer na ndiye mwenye haki zote.

“Kibongobongo msanii akishakulipa pesa ya kumtengenezea ngoma, basi anaona yeye ndiyo kila kitu, anaona anaweza kuifanyia chochote ile beat ambayo producer umemtengenezea, kitu ambacho siyo sahihi, siku zote ‘beat’ ni mali ya producer” Alisema Master J.

“Sina cha kusema na ningependa huo mjadala sasa ufungwe na tutumie fursa hii kujifunza masuala ya copy rights, tatizo wasanii wengi wakiitwa kwenye semina za masuala kama haya hawatokei” Alimalizia Sugu

Muungwana Blog Yasherehekea Kufikisha Mwaka Mmoja Toka Kuanzishwa Kwake Rasmi

$
0
0
nf
Kushoto ni RASHID MALIK ambaye ni Mmiliki wa Blog ya MUUNGWANA BLOG akishirikiana na JOHN KIANDIKA ambaye ni mmiliki wa Blog ya UDAKU SPECIAL katika zoezi la kukata keki ya kuadhimisha mwaka mmoja tangu MUUNGWANA BLOG kuanzishwa rasmi..

MUUNGWANA BLOG imefikisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake rasim, pia Muungwana Blog inapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wadau wote wanaotumia Blog yetu ya MUUNGWANA BLOG.. Tunasema Asanteni sana kwa kuichagua MUUNGWANA BLOG.

Keki maalumu yenye nembo ya MUUNGWANA BLOG..

Hapa kulia ni RASHID MALIK ( mmiliki wa Muungwana Blog ) anayefata aliyevaa T shet ya zebra ni mmiliki wa Blog ya BONGO CLAN na anayefata ni JOHN KIANDIKA mmiliki wa Blog ya UDAKU SPECIAL akiwa na mkewe pembeni...

Hapa aliyevaa shati jekundu ni FADHILI KAYANDA Team Muungwana ambaye anahusika na Habari za michezo..

Wageni waalikwa..

 Wageni waalikwa..

 Kushoto ni JAMAL MALIK ni Team Muungwana Blog anahusika na Habari za MAKALA..

Mmiliki wa MUUNGWANA BLOG akiongoza wageni katika kupakua chakula..


 Wageni rasmi wakiwa wanapata chakula..


 Wageni wakipata chakula..

  Wageni wakipata chakula..

 Wakati wa kutaka Keki..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki Jonh Kiandika..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki Mohamed Dala..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki Mmiliki wa Blog ya Bongo Clan..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki HALID..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki JASTIN..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki SAID..


 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki ISSA NCHIMBI..

 Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki ABED..

Boss wa Muungwana Blog akimlisha keki FADHIL KAYANDA mwana habari za michezo katika Blog ya Muungwana.

Sherehe hizi zilifanyika katika Hotel ya Mikumi inn..  Shukrani kwa mote waliohudhuria...
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images