Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

PICHA: Mkurugenzi wa H/Singida Akirejea Nyumbani kwa Miguu Baada ya Kusimamishwa Kazi

$
0
0
Huyu Mheshimiwa DED akirejea nyumbani kwake kwa miguu baada ya kusimamwishwa kazi na Mkuu wa Mkoa wa Singida kwa kudaiwa kulipa mishahara hewa kwa watumishi nane na kusbabishia Serikali hasara....

Picha: Wema Sepetu aja na mradi mpya ‘Wema na Jamii’

$
0
0
Wema Sepetu ameamua kurudisha kwa jamii.

Miss Tanzania huyo wa zamani na muigizaji wa filamu, ameanzisha mradi mpya alioupa jina ‘Wema na Jamii’ ambapo ameanza kuzunguka kwenye shule mbalimbali jijini Dar es Salaam kuongea na wanafunzi na kuwapa vitu mbalimbali.

Yeye mwenyewe anasema #WemaNaJamii #MkonoWaBaraka #MtotoWakoNiWangu. Tazama picha hizo chini.




Breaking News: Jengo la Ofisi za Kazi Mtaa wa Bibi Titi Dar Lawaka Moto

$
0
0

Moto umezuka jioni hii kwenye Jengo la ofisi za Kazi, Mtaa wa Bibi Titi Mohammed, Jijini Dar es salaam, na habari zilizotufikia magari ya Zimamoto yapo eneo la tukio na juhudi za kuuzima zinaendelea. Endelea kusikiliza

Idriss Sultan Afurahia Kazi ya Utangazaji, Adai Biashara zake Alizowekeza Nazo zimeanza Kumlipa...

$
0
0
Mshindi wa shindano la Big Brother Africa mwaka 2014 Idris Sultan amesema kwa sasa anafurahia sana kazi mpya ya utangazaji aliyopata katika kituo cha Radio cha Choice FM kilicho chini ya management moja na kile cha Clouds FM..
Idris Sultan pamoja na kufurahia kazi yake hiyo pia amesema kuwa sasa zile pesa zake alizowekeza kwenye biashara baada tu ya kushinda mtonyo wa Big Brother zimeanza kumlipa na si kweli kwamba amefulia kama watu walivyokuwa wanasema mitandaoni..

Walimu Wagoma, Kisa Mwenzao Kuzabwa Kofi darasani

$
0
0
WALIMU wa shule ya msingi Kianda wameanza mgomo wa siku mbili wa kutofundisha shuleni hapo huku wakilaani kitendo cha Ofisa Elimu (Shule za Msingi) wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Peter Fusi kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao akiwa darasani mbele ya wanafunzi wake.

Makamu Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Flora Kipesha alisema wameitisha mgomo huo wa siku mbili kupinga kitendo cha Fusi kumshambulia na kumpiga makofi mwalimu mwenzao Jacob Msengezi (25) ambaye anafundisha somo la Hisabati Darasa la Saba shuleni hapo.

“Licha ya kulaani vikali kitendo hiki cha udhalilishaji alichofanyiwa mwalimu mwenzetu na Ofisa Elimu (DEO) wetu (Peter Fusi) kumcharaza makofi mbele ya wanafunzi wake akiwa darasani ….

Ametudhalilisha sote yaani hata hamasa ya kufundisha imetoweka ….. “Sasa hatutaingia darasani kufundisha kwa siku mbili tukimshinikiza Mkurugenzi wa Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga (Adam Missana) achukue hatua dhidi ya ofisa huyo wa elimu ……yaani tunadhalilishwa hivi mbele ya wanafunzi wetu wenyewe wakati kazi hii tumeisomea na tuna vyeti halali ….

Tukiwa na sifa stahiki za taaluma ya ualimu,” alieleza Kipesha. Akifafanua, alisema walimu hawataingia kufundisha kwa siku hizo mbili na watakuwa ofisini wakiandaa mitihani huku wanafunzi wakiendelea kuhudhuria shuleni hapo kama kawaida.

Naye Mwalimu Msengezi alilieleza gazeti hili kwa njia ya simu akiwa shuleni Kianda kuwa juzi Jumatano Ofisa Elimu, Fusi alitembelea shuleni hapo saa tatu asubuhi akikagua mazingira ya shule.

“Mie wakati huo nilikuwa darasani na wanafunzi wa darasa la saba nikisahihisha madaftari yao kwani tayari kipindi changu kilianza saa 2:00 na kumalizika 2:40 asubuhi … Hivyo kwa kuwa mwalimu wa somo la Kiingereza alikuwa ‘busy’ akitunga mitihani niliamua niutumie muda huo kubaki darasani humo nikisahihisha madaftari,” alieleza Msengezi Kwa upande wake, Katibu wa CWT Wilaya ya Sumbawanga Vijijini, Vicent Ndewele akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alikiri kutokea kwa tukio hilo huku akisisitiza kuwa chama hicho kitatoa msimamo wake leo.

Shilole Humfikii Vanessa Mdee Kwa Uzuri - Mashabiki Wagoma

$
0
0
Ikiwa zimepita siku kadhaa toka msanii Shilole afunguke kwenye kipindi cha 5Selekt kinachorushwa kwenye ting'a namba moja kwa vijana EATV kuwa hakuna msanii wa bongo fleva mzuri zaidi yake, mashabiki wameamua kutoa ya mioyoni.

Mashabiki wamemchana Shilole na kusema kuwa yeye si mwanamke mzuri katika wasanii wanaofanya bongo fleva huku wakisema kuwa uzuri wake hausofei kabisa kwa msanii Vanessa Mdee.

Baadhi ya mashabiki walikuwa wakimpa madongo kuwa mwanamke mzuri hawezi kujianika kama yeye, huku wengine wakisema kuwa mwanamke mzuri hawezi kuwa yeye kutokana na tabia yake ya kutojiheshimu na wengine wakisema kuwa yeye hana lolote na wa kawaida kabisa.

"Kuna manzi wakuitwa Vanessa cheki yule manzi alivyo mcute wewe nani wachakuji puraaaaaaaaaaa" Africanboihacker

Uliipata MSG ya sheria mpya DSM? Kabla ya kupewa chumba Guest mnapigwa picha? Meya kaongea

$
0
0
Ijumaa ya May 6 2016 kama ni mtumiaji wa mitandao ya kijamii hususani Whatsapp najua utakuwa ulipokea ujumbe ambao ulikuwa unaripotiwa kuwa umetoka kwa meya  wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita, ujumbe uliokuwa umeenea ulikuwa unahusisha kuwa meya wa Dar es Salaam Isaya Mwita ametangaza sheria mpya.

Meya Isaya Mwita ameeleza kuwa ujumbe unaoenea kuwa ametangaza sheria mpya Dar es Salaam sio wa kweli na umetungwa na watu ambao wanapanga kumchafulia jina lake.


Ujumbe wa uongo ambao ulisambazwa leo May 6 2016 na kudaiwa umetoka kwa meya wa Dar es Salaam

“Sio kweli kuwa kuna sehemu nimetoa statement ya namna hiyo ila huyo atakayekuwa ameandika atakuwa na lengo tofauti, kwa hiyo naomba wananchi wapuuze hiyo statement ambayo imekuwa ikisambaa, bahati mbaya sikuwahi kupata mtu akiuliza maoni yoyote kuhusiana na tukio hilo la Kimara ila kwa upande wangu sijatoa tamko lolote”

Serikali yakamata Tani 4,900 za Sukari iliyofichwa Mbagala na Tabata jijini Dar

$
0
0
Baada ya muda mfupi wa rais kusema kuwa kuna wafanyabiashara wameficha Sukari, muda huu imeripotiwa kuwa huko Mbagala kuna Sukari ya zaidi ya tani 4,900 kwenye ghala la mfanyabiashara mmoja na imeelezwa zitachukuliwa hatua stahiki.

Chanzo: TBC, habari mpasuko

Snura Atoboa Siri Alipojifunzia Mauno

$
0
0
Msanii Snura ambaye jana video ya wimbo wake wa ‘Chura’ ulifungiwa na serikali kutokana na kutokuwa na maadili na kukiuka utamaduni wa kitanzania amefunguka na kusema kuwa yeye kukata viuno amejifunzia kwenye ngoma za asili.

Snura ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ambapo alikuwa akitoa ufafanuzi na kuomba radhi kwa watanzania kutokana na video yake hiyo kutokuwa na maadili na kuwadhalilisha wanawake.

“Mimi ni mwanamke na niliwachukua wanawake wenzangu kucheza lakini haina maana kuwa niliwachukua ili niwadhalilishe hapana, ila nakiri kuwa nilichokosea ni kuwaingiza kwenye maji ndiyo maana ilionekana kama ni udhalilishaji kwao. Lakini kucheza hakumdhalilishi mtu na ndiyo maana kuwa bendi wachezaji show wake wanakatika hata kwenye ngoma zetu za asili tunakatika, mimi nimejifunza kukatika kwenye ngoma za asili kwani ndiyo kipaji changu cha kwanza na huko ndiyo nimejifunzia kiuno” alisema Snura

Jason Rweikiza Achaguliwa Kuwa Katibu wa Wabunge wa CCM

$
0
0
WABUNGE wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamemchagua Mbunge wa Bukoba Vijijini, Jason Rweikiza kuwa Katibu wao.

Rweikiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama, ambaye safari hii hakuwania nafasi hiyo.

Katika uchaguzi huo uliofanyika juzi usiku katika ukumbi wa Msekwa uliopo ndani ya viwanja vya Bunge, Katibu huyo mpya wa Wabunge wa CCM alikuwa akipambana na Mary Chatanda, Mariam Kisangi na Abdalah Ulega.

Wabunge wote wa CCM pia walipiga kura kuwachagua wabunge 10 kati ya 21 walioomba ujumbe wa NEC.

Waliochaguliwa ni Livingstone Lusinde, Dk Hamis Kigwangalla, Stanslaus Nyongo, Steven Ngonyani, Peter Serukamba, Faida Bakari, Agness Marwa, Munde Tambwe, Angella Kairuki na Jamal Kassim Ali.

Wabunge ambao kura hazikutosha ni Mbaraka Dau, Alex Gashaza, Hawa Ghasia, Ibrahim Raza, Profesa Norman Sigalla ‘King’, Almas Maige, Angelina Malembeka, Yahya Massare, Mattar Ali Salum na Hafidh Ali Tahir

Tazama Hapa Video Mpya ya Mwanamuziki Shetta ya Wimbo Unaoitwa Namjua

$
0
0
 Tazama Hapa Chini Video Mpya ya Mwanamuziki Shetta ya Wimbo Unaoitwa Namjua, Video Imefanywa South Africa...

VIDEO: Miaka 13 Baada ya Cameroon Kumpoteza Foe, leo Tena Wamempoteza staa Mwingine Uwanjani

$
0
0
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa mitandao ya soka barani Ulaya huenda utakuwa umekutana na taarifa za kusikitisha kwa taifa la Cameroon, usiku wa May 6 2016 Cameroon na Afrika  kwa ujumla ilipata taarifa za kushtusha, baada ya kupokea taarifa za kifo cha kiungo wa kimataifa wa Cameroon aliyekuwa anaicheze Dinamo Bucuresti Patrick Ekeng.

Ekeng amefariki baada ya kuanguka uwanja dakika ya 70 wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Romania uliokuwa unahusisha klabu yake ya Dinamo Bucuresti  dhidi ya Viitorul, mchezo ambao ulikuwa unarushwa live kwenye TV, tukio la Ekeng kuanguka limetokea wakati akiwa kasimama peke yake bila ya mpira.


Taarifa za kifo cha Ekeng ambaye zilithibitishwa masaa mawili baada ya kufikishwa hospitali, zinakuja baada ya miaka 13 toka Cameroon impoteze kiungo wake Marc-Vivien Foe kwa stahili kama hiyo, tukio ambalo lilitokea June 26 2003 wakati wa michuano ya Kombe la mabara iliyokuwa inafanyika Ufaransa na mchezo ulikuwa dhidi ya Colombia.


Ekeng alizaliwa March 26 1990 na amefariki akiwa na umri wa miaka 26 baada ya kuanguka uwanjani, Ekeng ndio alikuwa kaanza kupata nafasi katika kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon ya wakubwa, muda mchache baada ya taarifa za kifo chake kuthibitika, mastaa wa soka walianza kupost na kuonesha huzuni kwa taarifa hizo.

Video ya tukio la kuanguka kwake na kupoteza maisha

Ahukumiwa Miaka Mitatu Kwa Kosa la Kumtukana Mtandaoni Mwanamke Aliyedai Anatembea na Mumewe

$
0
0
Mfanyabiashara Naila Aminel (24) amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh milioni tano baada ya kukiri kutumia mtandao wa kompyuta kutuma ujumbe wa lugha ya matusi.

Aminel ambaye ni mkazi wa Kariakoo, alihukumiwa kifungo hicho jana katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Mfawidhi, Said Mkasiwa.

Awali, akisoma mashitaka, Wakili wa Serikali, Sylvia Mitanto alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari 13 mwaka huu, maeneo ya katikati ya jiji, wilayani Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam.

Mitanto alidai kuwa mshitakiwa alitumia lugha ya matusi dhidi ya Martha Sebarua kupitia mtandao wa kompyuta kinyume na kifungu namba 23 (1) na (3) cha Sheria ya Makosa ya Mtandao namba 14 ya mwaka 2015.

Hata hivyo, Mitanto aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo.

Mshitakiwa huyo alidai hakumtukana mlalamikaji isipokuwa alifanya hivyo kwa kuwa alimchukulia mume wake na walipiga picha za utupu na kumtumia kwenye simu yake.

Aliiomba pia mahakama kumpunguzia adhabu kwa kuwa ana watoto wadogo ambao wanamtegemea.

Hakimu Mkasiwa alisema kuwa mshitakiwa amekiri kutumia lugha ya matusi hafai katika jamii na kwa sababu kosa lake ni la kwanza, atatakiwa kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh milioni tano.

Kajala Ahusishwa Undani wa Wimbo wa ‘Haya Yote ni Maisha’ ya P Funk

$
0
0
Msanii Madee amefunguka undani wa wimbo wa ‘Haya Yote Maisha’ wa Producer P Funk Majani ambao ameimba yeye, wimbo ambao ulishika chati na kugusa hisia za watu wengi.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Madee amesema wimbo huo ni historia ya kweli ya P Funk na mwanamke ambaye ndiye mama wa mtoto wake wa kwanza, Kajala Masanja.

“Haya yote maisha imetokea kipindi ambacho bado nipo na P Funk, alafu P Funk ana matatizo na mama mtoto wake Kajala, kwa hiyo wakati mi naenda pale kurekodi cheza kidogo, kabla sijamalizana na ile nakutana na beat ya yote maisha inaplay, alafu inaplay na chorus lakini hakuna verse, lakini the way ile beat inavyoplay majani anavyoiimba anaimba kwa feelings kinoma, nikamwambia bwana hii nyimbo mbona kali nigaie niimbe akasema hii na chana mwenyewe babu,” alisema Madee.

Madee aliendelea kusema baada ya mazungumzo P Funk alikubali kumpa beat na kwenda kuifanyia kazi, baada ya kukumbuka Madee mtindo alioutumia kwenye nyimbo zake.

“Sema wewe ulivyochana kwenye kazi yake mola kuna ryhmes fulani naona unapita pita, unaongea kimajonzi hebu chukua hii beat kaandike, kwa hiyo nikapewa ile beat, aliniambia kwamba hii nyimbo ina feeling zangu, nataka uandike kitu hiki na hiki, kwa hiyo idea iliyotoka mule ni idea ya P Funk,” alisema Madee akimuongelea P Funk Majani.


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Mei 7, Ikiwemo Neno Baby Lilivyochafua Hali ya Hewa Bungeni

$
0
0

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Mei 7, Ikiwemo Neno Baby Lilivyochafua Hali ya Hewa Bungeni

Afande Sele: WaTanzania Tuache Unafiki, Bhangi ihalalishwe (Video)

$
0
0
Afande sele: WaTanzania tuache unafiki, bhangi ihalalishwe (Video)
Mtazame Hapa Akielezea kwanini:

Shilole Akanwa Laivu Mchana Kweupe...Nedy Adai Hawana Mahusiano ya Kimapenzi

$
0
0
Bongo fleva super staa Nedy Music ambaye hivi karibuni amejiunga na lebel ya Ommy Dimopz ya Pozi Kwa Poz amekanusha uvumi kuwa Shilole ni Mpenzi wake...Akihojiwa Clouds FM amesema hana uhisiano wa Kimapenzi na Shilole

Awali Nedy alitajwa akuwa mpenzi wa Shilole baada ya staa huyu kuachana na Nuh Mziwanda.

Hii sauti ya Nedy akiongelea Issue Hii:

Nafasi za Ajira Zilizotangazwa Katika Magazeti na Mitandaoni leo

Nina Ugonjwa wa Kuiba Chupi za Wanawake..Nifanyaje Niache?

$
0
0
Kila nikilala na mwanamke kama kabeba chupi ya kubadili ile aliyovaa akiivua lazima nifanye manuva mpaka niondoke nayo, alafu nazitumia baadae kuvuta hisia kwenye mambo yetu ya kisabuni..
Sasa uvungu wangu chumbani umejaa chupi na nyingine zinanuka kweli...

Nafasi niweze kuacha?

Young Dee Aporomoshewa Matusi Baada ya Kupost Picha Akivuta Bang

$
0
0
Usiku wa kuamkia May 6 2016 Paka Rapa Young Dee alipost picha akiwa anavuta kitu ambacho mashabiki wake kwenye mtandao wa instagram walitafsiri ni bangi na kuanza kumporomosshea comments kuwa anaelekea kuwa kama Chidi Benz,

Je Young hapa alikuwa anavuta bangi ? na kama ni bangi ni sawa kwa msanii kufanya hivi bongo kama tunavyoona nje kwa kina Wiz Khalifa.
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images