Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live

IMEBAINIKA Rihanna na Drake Wamekuwa Kwenye Mahusiano ya Siri Kwa zaidi ya Mwezi sasa

$
0
0
Jarida la PEOPLE limefumua bonge moja la siri kuwa staa Rihanna na rapa Drake wamekuwa na mahusiano ya siri kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.

Rihanna na Drake wamefanya collabo kama “Take Care” .“What’s My Name?” na “Work” ila pia wamekuwa wapenzi kwa muda sasa bila kutaka dunia ijue.

Rihanna ndio sababu ya Drake na Chris Brown kutoelewana ila kwa sasa inasemekana Kwa Rihanna pale Drake beki hazikabi.

Idadi ya Ajali zilizojitokeza wakati wa Majaribio Mabasi yaendayo Haraka

$
0
0
Wakala wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) umesema kutozingatia sheria za barabara za mradi wa mabasi hayo, kwa vyombo vingine vya moto vimesabisha ajali 14 wakati madereva wa mabasi hayo wakiendelea na mazoezi kwa ajili ya kuelekea kipindi cha mpito cha mradi kinachotarajia kuanza hivi karibuni.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala huo, Mhandisi Ronald Rwakatale amesema kuwa ajali hizo zimejitokeza wakati madereva wa mabasi ya mradi wakifanya mazoezi na kisha vyombo vingine vya moto viingilia barabara zake na kusabisha ajiali hizo.

Amesema ajali hizi ni matokea ya vyombo vingine vya usafiri kama magari madogo, daladala, bodaboda na waenda kwa miguu wamekuwa wakiingilia barabara za mabasi hayo na kusabisha ajali kutokana na kwamba barabara hizo haziruhusu mabasi hayo kupisha na vyombo vingine.

Mhandisi Rwakatale amesisitiza kuwa barabara za mabasi hayo ambazo ni za zege zimejengwa mahususi kwa ajili ya mabasi hayo hivyo madereva wa vyombo vingine wanahitajika kuheshimu sheria zinazoongoza mradi huo na kupita katika barabara walizotengewa na watakaokiuka sheria itachukua mkondo wake.

Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka unatarajiwa kuanza kipindi cha mpito mwezi huu wa Mei kutoa huduma ya usafiri kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam

Msanii Ray Kigosi Aibuka na Kutoa Soma Hili Kwa Vijana Kuhusu Viongozi wa Nchi na Siasa zao

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Ray Kigosi amefunguka na kusema kuwa yeye furaha yake ni kuona vijana wenzake wakifanikiwa na kupiga hatua kimaendeleo.

Ray Kigosi amewaasa vijana wenzake kuwa wasikae wakategemea kuwa viongozi wa siasa wanaweza kuja kuwabadilishia maisha yao bali amewataka kuwa na jitihada binafsi kwani huo ndiyo msingi mkubwa wa mustakabali wa maisha yao.

“Furaha yangu ni kuona kijana mwenzangu ukifanikiwa na kupiga hatua kimaendeleo, pambana achana na mambo yasiyo na msingi ukitaka kufanikiwa katika ndoto zako fanya vitu vigumu kufanyika. Fanya kitu ambacho mwingine hawezi kufanya, hakuna kiongozi yeyote wa nchi atakayekuja kuyabadilisha maisha yako isipokuwa ni jitihada zako mwenyewe huo ndio msingi mkubwa wa mustakabali wa maisha yako.”

Mkuu wa Mkoa Paul Makonda Amtembelea Diamond Ofisini Kwake..Diamond Asema Haya

$
0
0
From @diamondplatnumz - Shukran sana sana Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam @PaulMakonda kwa kututembelea katika Office zetu za @Wcb_Wasafi jana usiku.... ujio wako Umetutia nguvu na Moyo mkubwa katika ufanisi wa kazi zetu.... Hakika wewe ni kiongozi wa pekee....Tunashkuru kwa Ushauri, muongozo wako mzuri na Muda wako wa thamani ulioupendekeza kwetu Jana!... ijapokuwa kaofisi ketu ndio kanaanza ila naamini uliona tunavyo hakikisha kudhibiti na kuzingatia USAFI Kuanzia Ofisini hadi Maeneo yatuzungukayo kama Mh Rais John Pombe na wewe Mlivyoagiza

KOCHA Jamhuri Kihwelo 'Julio' Ajigamba..Lazima Tuifunge Simba

$
0
0
Kocha wa Mwadui FC, Jamhuri Kihwelo 'Julio' amesema atahakikisha anashinda mchezo huo ili Yanga iwe bingwa.

Mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya Simba dhidi ya Mwadui FC ni kesho Jumapili na inasubiriwa kwa hamu ile mbaya. Itapigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Yanga inaongoza ligi ikiwa na pointi 68 ikifuatiwa na Simba yenye pointi 58, wakati Azam ina pointi 57. Yanga na Azam zimebakiwa na michezo mitatu, huku Simba wakiwa nayo minne.

Simba ikishinda mechi zake zote ikiwemo hii na Mwadui, itafikisha pointi 70, hivyo Yanga na Azam zikipoteza mechi zake zilizobaki, Wekundu wa Msimbazi wanaweza kuwa mabingwa.

Julio ambaye amewahi kucheza na kufundisha Simba, alisema hataleta urafiki kwenye mchezo huo na amepanga kushinda ili Yanga ipate ubingwa rasmi.

Diamond na Kampuni yake ya Music WCB Yamzawadia Gari Jipya Harmonize

$
0
0
WCB imemzawadia gari jipya msanii wake, Harmonize.
Bosi wake, Diamond, ameandika kwenye Instagram: Kama nikusiivyo siku zote ni juhudi na nidhamu yako ndio itayokufanya upate matunda ya kazi yako….. Usiache unyenyekevu, kuheshimu mkubwa na mdogo, kumuomba na kumshukuru Mwenyez Mungu kwa kila hatua ndogo Uipigayo…. Congrats kwa your New Ride.”

Naye Harmonize hakuacha kuonesha furaha yake.

“Nichukue fursa fupi kuushukuru uongozi wangu mzima wa @wcb_wasafi @mkubwafella @babutale @sallam_sk @ricardomomo @diamondplatnumz kwa kunijali na kunithamini kijana wao wakanizawadia gari daaaaah furaha niliyo nayo haielezeki,” ameandika msanii huyo.

“Kwakweli nina furaha na ninashukuru sanaa nina mengi ya kuongea lakini sizani kama nikianza kuandika nitamaliza kubwa ni kwamba namshukuru m/mungu nashukuru kwa kurudia tena uongozi wangu @wcb_wasafi kwa zawadi lakini nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipo washukuru wazazi wangu walio nizaa na kunilea hadi nikafikia hapa na shukrani za dhati ziwafikie mashabiki zangu ambao wapo bega kwa bega kunisupport katika kazi zangu pia mama naseeb umekuwa ukinisistiza na kunisihi jinsi ya kuishi na watu @kendrah_michael.”

“Nimalize kwakusema ninashukuru sanaa na nina amini kuna mengi mazuri zaidi yapo mbele ila asieshukuru na kidogo kamwe hatoshukuru na kikubwa thanks #allah thanks #wcb #thanks #mashabiki.”

Mrembo Lulu La Diva Afanikiwa Kumteka Mrembo Wizkid....

$
0
0

Mrembo anayepanda kwa kasi Bongo, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ hivi karibuni amefunguka kuwa hatimaye ametimiza ndoto yake ya muda mrefu aliyokuwa nayo ya kujiweka karibu na mwanamuziki maarufu Afrika kutoka Nigeria, Ayodeji Balogun ‘Wizkid’.

Akipiga stori mbili tatu na gazeti hili, Lulu Diva alisema tangu ajikute ‘in love’ na Wizkid kila mara alikuwa akimtumia ujumbe au ‘kumtag’ picha kwenye ukurasa wake wa Mtandao wa Kijamii wa Instagram hatimaye hivi karibuni mkali huyo wa Wimbo wa Ojuelegba alianza kujibu SMS zake jambo lililoanzisha safari ya kumnasa mkali huyo.

“Najihisi kuwa na bahati sana duniani maana Wizkid ni kipenzi cha wanawake wengi, huwezi amini mara ya mwisho nachati naye aliniambia anakwenda kwenye tamasha Zambia na akirudi Nigeria aliniambia nikutane naye Lagos, so kwa sasa niko katika maandalizi ya kuelekea huko na bila shaka naye ameshavutiwa na mimi,” alisema Lulu.

Diamond Platnumz Atokuja Kusoma Kwenye Simu ya Mpenzi Wake Kamwe...Hii Masege Ndio ilimuumiza Sana

$
0
0
Kwenye Exclusive Interview ya OnAIRwithMillardAyo mwimbaji staa wa bongofleva Diamond Platnumz hatosahau siku alipopekua simu ya mpenzi wake na kukuta msg ambazo zilimfanya mpaka leo asithubutu kushika simu ya mpenzi wake yeyote, mtazame mwenyewe akiongea hapa chini..


Coastal Union Chali Yafungashiwa Virago Vyake na Kushuka Ligi Daraja la Kwanza

$
0
0
Klabu ya Coasta Union ya jijini Tanga itahitaji miujiza pekee ili iweze kubaki katika ligi kuu ya Tanzania Bara msimu ujao kutokana na hesabu kuonesha kuwa tayari timu hiyo imeshuka daraja.

Miujiza hiyo inatokana matokeo iliyopata leo katika dimba la CCM Kambarage mjini Shinyanga kwa kuchapwa mabao 2-1 na wenyeji Stand United.

Mabao yote mawili ya Stand United katika mchezo wa leo yameupiwa wavuni na Elias Maguli katika dakika ya 29 kwa njia ya penati baada ya mchezaji wa Stand kuchezewa madhambi katika eneo la hatari, huku bao la pili akilipachika katika dakika ya 46, muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza, kabla ya Coastal kupata bao la kufutia machozi kupitia kwa said.

Kwa mabao hayo sasa mshambuliaji Elias Maguli amefikisha magoli 14 na anakamata nafasi ya 4 katika orodha ya wafungaji wanaoongoza kwa mabao mengi zaidi akitanguliwa na Amis Tambwe (20), Hamis Kiiza (19), Donald Ngoma (16) huku akimuacha Kipre Tcheche na John Bocco wenye mabao 10 kila mmoja.

Matokeo haya yanaifanya Coastal kutangulia ligi daraja la kwanza huku ikiwasubiri wenzake wawili kutokana na kuwa na point ambazo haziwezi kuinasua kutoka katika nafasi tatu za chini hata kama itashinda mchezo wake wa mwisho uliobaki.

Kwa upande wa mechi nyingine zilizopigwa leo, JKT Ruvu imeibwaga Ndanda FC kwa mabao 2-0, huku

Mgambo JKT ikiilazimisha sare ya bao 1-1 Mtibwa Sugar
Hesabu zinaonesha kuwa baada ya michezo ya leo Jumamosi, Coastal Union imeendelea kubaki mkiani na point zake 22, ikiwa nyuma ya Mgambo JKT iliyofikisha pointi 24 ikiwa na mechi 2 mkononi, Kagera Suga yenye point 25 na mechi 3 mkononi, na African Sports ikiwa na point 26 na mechi 2 mkononi.

Kwa upande wake JKT Ruvu kwa kiasi kikubwa imejinasua kutoka katika dimbwi hilo la kushuka daraja baada ya ushindi wake wa leo ulioifanya ifikishe pointi 29.

Chadema Walaani Kitendo cha Udhalilishaji Bungeni Walichofanyiwa Wabunge wa Wanawake wa Ukawa

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), mkoa wa Dar es Salaam kimelaani kauli iliyotolewa na Mbunge wa CCM, Goodluck Mlinga ya kuwa ili wanawake wapate nafasi ndani ya chama hicho lazima waitwe 'baby' neno linalo maanisha kutumiwa kimapenzi.

Hivi karibuni akichangia mjadala wa Wizara ya Katiba na Sheria Milinga alitoa kauli hiyo iliyoibua mtafaruku Bunge hadi kusababisha wabunge wa wanawake wa Ukawa kutoka nje ya ukumbi huo baada ya kunyimwa mwongozo na Naibu Spika Dk Tulia Ackson.

Akizungumza jana nje ya eneo la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), akiwa na viongozi wenzake walipokwenda kuchangia damu Katibu wa Chadema Dar es Salaam Henry Kilewo alisema wamesikitishwa na kauli hiyo ilitolewa na mbunge alipewa dhama na kuaminiwa wananchi.

Alifafanua kwamba, ili uwe mbunge wa viti maalumu ndani ya Chadema kuna hatua nne za kupitia ikiwamo wanawake wenyewe kuchaguana ngazi ya wilaya kupitia Baraza la Wanawake la Chadema hivyo siyo rahisi kuwa na kitu kama hicho cha uhusiano wa kimapenzi.

"Kauli kama hizi zinapaswa kukemewa na kukomeshwa kwani zinawadhalilisha wanawake wote Tanzania. Lakini cha ajabu nimeshangaa hata wenzetu upande wa pili CCM wamekaa kimya bila kutoa kauli ya kukaripia," alisema Kilewo.

Alisema Chadema mkoa wa Dar es Salaam, inaungana na wabunge wa wanawake wa Ukawa kupinga kauli hizo za kiuni zilizotolewa na mbunge huyo wa Ulanga Mashariki aliyepigiwa kura wananchi mbalimbali wakiwamo wanawake.

Kuhusu suala la damu Kilewo aliwataka Watanzania wote kujijengea tabia ya kuchangia damu ili kuokoa maisha ya Watanzania wengine waliolazwa katika hospitali na vituo vya afya mbalimbali nchini.

"Chadema Dar es Salaam, tumeonyesha mfano tunaviomba vyama vingine viige mfano huu ili tuwasaidie watu wenye mahitaji ya damu,"alisema Kilewo.

Kwa mujibu wa Kilewo zaidi ya wanachama 40 wakiwamo viongozi wa Chadema mkoa huo wamechangia damu na kwamba mchakato huo utakuwa kila baada ya miezi watakuwa wakitoa msaada huo wa damu.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalumu wa chama hicho, Ruth Molel alisema wabunge wa viti maalumu wa Chadema wanaoteuliwa wote na wanataalumu zao na hawabahatishi kupata nafasi hizo kama Mlinga anavyodhani.

"Nimeumia nilivyosikia kauli hii ikitolewa na kijana yule ambaye ni kama mwanangu, kiukweli hajatutendea kina mama. Inaonyesha jinsi gani bado ana fikra za mfumo dume" alisema Molel.

Ofisa Habari wa MNH,Neema Mwangomo alisema kwa siku hospitali hiyo inahitaji damu kwa wastani uniti 80 hadi 100 lakini zinazopatikana ni 40.

Hata hivyo, Mwangomo aliwashukuru viongozi Chadema kwa moyo wao na kuwataka Watanzania wengine kujitokeza kutoa damu katika hospitali hiyo.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Ahudhuria Mazishi ya Lucy Kibaki nchini Kenya.

$
0
0
Rais Mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania Jakaya Kikwete amekuwa miongoni mwa viongozi wa ngazi za juu katika ukanda wa Jumuia ya Afrika Mashariki kuhudhuria hafla ya mazishi ya aliyekuwa mama wa Taifa la Kenya Bi Lucy Kibaki aliyefariki akiwa na miaka 82.

Marehemu Lucy Kibaki ametajwa na wanaomjua kama kiongozi aliyetetea mazingira safi ya kifamilia na alikuwa tayari kufanya kila jambo kuhifadhi utu na wema katika familia.

Kikwete ambaye aliwasilisha ujumbe wa Rais John Pombe Magufuli alisema kifo cha mama Lucy kibaki kimetokea wakati mchango wake ukiwa bado unahitajika katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta na Naibu wake William Ruto waliohudhuria mazishi ya Bi Kibaki eneo la Bunge la Odhaya kaunti ya Njeri wamemtaja marehemu kama kiongozi aliyekuwa tayari kuhudumia taifa la Kenya.

Mimi Sifanyi Mapenzi, Hata Boyfriend Wangu Anajua Sipendi Kufanya Mapenzi – Gigy Money

$
0
0
Video queen ambaye haishiwi vituko, Gigy Money amefunguka kwa kusema kuwa yeye siyo mtu wa kupenda kufanya mapenzi kama watu wanavyodhani.


Akizungumza na Bongo5, Gigy amesema maisha aliyopitia yamemfanya awe ni mwanamke asiyependa kufanya mapenzi.

“Mimi nimepoteza ile ari ya kufanya mapenzi au kuwa na mpenzi mmoja au nijiachie na mwanaume kama mtu na mpenzi wake siwezi, sasa hivi natafuta maisha, pesa mbele,” alisema Gigy. “Kama yeye ana wivu na mimi, mimi sina wivu na mwanaume,”

Gigy amesema taarifa za kwenye mitandao ya kijamii kwamba anajiuza siyo za kweli, kwani yeye ana mwanaume ambaye anamuudumia kila kitu ingawa hawafanyi mapenzi.

“Nina mtu ambaye ananihudumia, ananipa mtaji ya biashara zangu. Pia hata kwenye muziki anawekeza pesa yake. Kwa hiyo waache wanifikie hivyo wanavyofikiria, mimi nafikiria navyojijua, mimi nipo tofauti sana na wanavyozungumza, ukijaribu kukaa na watu wangu wa karibu watakwambia,” alisema Gigy.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Mei 8, Ikiwemo ya Magufuli Kumtosa JK

$
0
0


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Mei 8, Ikiwemo ya Magufuli Kumtosa JK

Magufuli Afunguka 'Nitawatumbua Hadi Mwisho wa Dunia'

$
0
0
Rais Magufuli amerejea kauli yake kuwa serikali yake haitawavumilia viongozi na watumishi wa umma ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi, huku akisema ataendelea kutumbua majipu kwa yeyote atakayebainika kuchezea mali za umma ili kulinda maslai ya wengi, hususani watanzania wanyonge.

"Ninafanya kwa niaba yenu, ninafanya kwa niaba yenu, ningekuwa sifanyi kwa niaba yenu, na mimi ningeingia madarakani ningeanza kushirikiana na hao, na wengine walifikiria nitashirikiana nao, wamekwama mimi nitawatumbua kila siku ili Tanzania iwe ya neema iweze kwenda mbele, haiwezekani nchi kama hii tajiri, Tanzanite ipo, dhahabu ipo, wanyama mpaka nyani wameanza kuuzwa, wakimalizika nyani si tutauzwa na sisi ndugu zangu, ni lazima nisimamie hili" amesisitiza Dkt. Magufuli.

Aidha katika mazungumzo hayo, Rais Magufuli amewahakikishia kuwa serikali yake imeanza kuwashughulikia wafanyabiashara ambao wameficha sukari kwa makusudi na kusababisha upungufu wa bidhaa hiyo.

Rais Magufuli amesema tayari vyombo vya dola vimekamata tani 5,000 za sukari iliyofichwa na mfanyabiashara mmoja huko Tabata Jijini Dar es salaam na pia vimembaini mfanyabiashara mwingine aliyeficha sukari hiyo Jijini Arusha.

"Kweli nitawakomesha hawa, wasije wakanilaumu, haiwezekani ukaficha sukari wakati viwanda vyetu vinatengeneza sukari, kuna mmoja mwingine yupo Arusha hapa, nae ameficha sukari, alienda akanunua kwenye viwanda vya sukari vya hapa akaificha yote, leo ninamshughulikia.

"Kuna mwingine alinunua sukari pale Kilombero zaidi ya tani 3,000 akaficha, na mwingine ameshikwa pale Tabata alikuwa ameficha tani 5,000, na wanasubiri katika mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili ndugu zetu Waislamu wapate shida, haya ni mashetani makubwa, unawafichia watu chakula ambacho wanatakiwa kula, lakini nataka niwahakikishie ndugu zangu, hili ni tatizo la muda Tanzania, sukari itapatikana kwa wingi, na itanunuliwa na serikali, tumeshaagiza sukari lakini hatutawapa vibali hawa wafanyabiashara ambao wanatunyonya, tutanunua wenyewe na tutauza bei ya chini, hilo ndio lengo la serikali" Amesema Rais Magufuli

Hawa ndio Wafanyabiashara Wakubwa wa Sukari Nchini

$
0
0
Rais Magufuli ana vita pevu kuhusu mstakabali wa sukari na hatima ya viwanda vya sukari nchini.

Sukari yote nchini inayoagizwa kutoka nje kwa kiasi kikubwa ilikuwa inaagizwa na hawa matajiri wakubwa nchini kama wanavyoonekana kwenye picha.

Hawa ni baadhi ya matajiri ambao wanamiliki soko la sukari nchini ambalo wakati wa utawala wa Rais Kikwete, hakuweza kuwadhibiti ili kuvilinda viwanda vya sukari nchini na afya za walaji.

Hawa kwenye picha hapo chini ni aina ya watu wanaoitwa sugar industries movers and shakers katika jumuiya ya wafanyabiashara nchini.

Kutoka kushoto ni Harun Daudi Zakaria ambaye juzi vikosi vya usalama nchini vilikuta kwenye magodauni yake huko Mbagala na Tabata tani zaidi ya 4,600 ambazo inasemakana zilikuwa zimefichwa, kwa lugha ya kisheria wanasema hoarding commodities. Huyu wakati mwingine alikuwa anapewa vibali ambavyo waingereza wanasema special/exclusive permit kununua au kuagiza sukari kwa ajili ya soko la Zanzibar.

Anayefuatia ni Said Salim Bakhresa ambaye hununua sukari nchini au kuagiza nje ya nchi maelfu ya tani za sukari kama malighafi kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa kwenye viwanda vyake.

Anayefuatia ni Reginald Mengi ambaye ana viwanda vya vinywaji. Hununua sukari nchini au kuagiza nje ya nchi maelfu ya tani kama malighafi kwa ajili ya viwanda vyake mbali mbali.

Anayefuata ni Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete ambaye baada ya kushindwa vita ya sukari kutokana na nguvu kubwa waliyonayo hawa wafanyabiashara, akaamua kuacha mbuzi ale kulingana na urefu wa kamba yake. Huu ulikuwa ni mwanzo kwa serikali kushindwa kufahamu kiwango cha sukari kilichoko ndani ya nchi na pia kiwango kinachohitajika kwa mwaka.

Anayefuata ni Gulam Dewji ambaye ni Baba yake na Mohammed Dewji (Mo Dewji). Huyu ni Mwenyekiti wa MeTL Group na Mnunuzi na mwagizaji mkuu wa sukari kama malighafi kwa ajili ya viwanda vyake na pia kuuza kwenye soko laTanzania Bara. Huyu pia alikuwa anapewa special/exclusive permit ya kuagiza sukari

Wa mwisho ni Balozi wa Jamhuri ya Djibouti-Tanzania, Saidi Amin Shamo ambaye ni mmoja wa inner circle ya Sir Andy Chande (Mtanzania wa kwanza kukiri kuwa Mwanachama wa Freemasons). Kwenye inner circle ya Sir Andy Chande huwezi kumkosa Edward Lowassa, Rostam Aziz na Balozi Juma Mwapachu.

By Msemakweli
Jamii Forums

Picha: Msichana Asiye na Mikono Ashinda tuzo la Muandiko Bora

$
0
0
Anaya Ellick kutoka Chesapeake, Virginia hatumii viungo vya kumsaidia wakati anapoandika.

Wakati anapoandika yeye husimama huku akishikilia kalamu yake katika mikono.

Mwalimu wake mkuu Tracy Cox kutoka shule ya Greenbrier Christian amemtaja kuwa mtu wa mfano mwema.

“Yeye uhakikisha kuwa hakuna kitu kinachomzuia kufanya atakalo”, alisema Cox.”Ni mkakamavu na ana muandiko mzuri katika darasa lake”.

Msichana huyo anadaiwa kuwashinda washindani wengine 50 ili kushinda taji hilo la kitaifa.

Orodha hiyo ya tuzo huwazawadi wanafunzi wenye akili, matatizo ya kimwili, au ulemavu endelevu



Taasisi ya Takururu Walivalia Njuga Sakata la Walioficha Sukari..Hichi ndo Kinaendelea sasa

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa inafanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowahusu  wafanyabiashara wa sukari nchini kwa kuficha bidhaa hiyo ili  kusababisha upungufu katika soko na hivyo kuleta usumbufu kwa jamii ya watanzania wanaohitaji bidhaa hiyo kwa matumizi jambo ambalo limesababisha kupanda kwa bei hadi kufikia shilingi elfu nne kwa kilo moja ya sukari.

 Taasisi imeanza uchunguzi dhidi ya Tuhuma hizi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi na tayari tumeweza kutembelea Maghala ya mfanyabiasha Haruni Daudi Zacharia ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Al-Naeem yaliyoko Mbagala na Tabata ambaye ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa nchini wa sukari na anayetuhumiwa kuficha bidhaa hii.

Mnamo tarehe 05 Mei, 2016 timu ya uchunguzi ilitembelea maghala ya Tabata na kubaini uwepo wa sukari yenye jumla ya tani 4,579.2 iliyonunuliwa toka Kiwanda cha Kilombero Sugar Company.
Aidha uchunguzi ulibaini kuwepo kwa njama za dhati za kutouza kwa sukari kulikofanywa na mfanyabiashara huyu kwani hata sehemu ya Maghala ilipo sukari hapa kuwepo dalili za upakiaji wa sukari na baada ya kufika Kitumbini tulibaini uwepo wa wananchi wengi waliokuwa wakihitaji bidhaa hiyo na wachache sana waliweza kuuziwa tena kwa kiwango kidogo sana kuliko mahitaji yao.

Wananchi wengi walikosa huduma hiyo licha ya ukweli kwamba sukari ilikuwepo.
Uchunguzi uliofanyika umebaini kuwepo kwa mikakati ya dhati iliyokuwa ikifanywa na mfanyabiasha huyu kwa kununua sukari yote toka viwanda vya ndani na kisha kuihifadhi na kuuza bidhaa hiyo kidogo kidogo kwa wastani wa tani 250 kwa siku wakati alikuwa na uwezo wa kuuza zaidi jambo lililochangia uhaba wa sukari katika soko. Kuficha bidhaa ni kosa la uhujumu uchumi na ni  kinyume na Aya ya 3 Jedwali la kwanza Sheria ya Uhujumu Uchumi Sura ya 200 [Chapisho la Mwaka 2002]. Serikali haitavumilia hujuma za namna hii na itachukua hatua kali dhidi ya mfanyabiashara yeyote ataekwenda kinyume na sheria hii.

Kuanzia sasa TAKUKURU inatoa wito kwa wafanyabiashara wote wa sukari kuacha vitendo vya kuficha sukari na vyombo vya uchunguzi vinafuatilia kote nchini na yeyote atakayebainika kufanya hujuma hizo atakabiliwa na mkondo wa Sheria.

VALENTINO MLOWOLA
 MKURUGENZI MKUU WA TAASISI 
YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA
7 MEI, 2016

Bado Sijajua watu Wanaupendea nini Muziki wa Diamond Platnumz

$
0
0
Bongo ina wasanii wengi sana, kati yao 90% hawajui muziki kifupi ni wabovu akiwemo Diamond ila wanapendwa kupita maelezo, na 10% wanajua muziki kifupi ni wakali akiwemo Rama dee na Steve wa RnB ila cha kushangaza hawapendwi(muziki wao).

Sasa nashindwa kuelewa inakuwaje?? Mfano huyu Diamond miziki yake ni ya kawaida tu lakini raia wanamshobokea vibaya sana, kila ngoma anayotoa inakuwa ni national anthem lakini nikisikiliza mi naona ni miziki tu ya kawaida ambayo hata kwenye flash au laptop au memory card yangu siwezi kuweka.

Sijajua watu ni kwamba hawajui muziki au ni nini tatizo au ni ufreemason na uganga wa kupumbaza watu?? Kama ni mganga basi ni kiboko aisee, nasema ukweli ngoma za jamaa ninazozikubali ni Nitarejea na kesho, basi!

Pesa Tulizowekeza Kwenye Muziki zimeanza Kurudi- Navy Kenzo

$
0
0
Kundi la muziki, Navy Kenzo ambalo linaundwa na wasanii wawili, Nahreal pamoja na Aika, ni moja kati ya makundi machache ya muziki nchini ambayo yanawekeza pesa nyingi katika kuandaa kazi zao.
Navykenzo

Akizungumza na Bongo5 hivi karibuni, Nahreal amesema tayari wameshaanza kurudisha pesa zao ambazo wamekuwa wakiwekeza kwenye muziki kwa muda mrefu.

“Gharama ambazo tumetumia ni kubwa na tunajua muziki ni uwekezaji, lazima uwekeze, kwa hiyo mwanzo tulikuwa tunaweka pesa nyingi lakini hazikuwa zinarudi, so tumefika wakati pesa imeanza kuingia. Kama tour yetu imetupatia pesa fulani, pia wimbo wetu ‘Kamatia Chini’ umetupatia deal kubwa. Kwa hiyo pesa ambayo tuliwekeza inarudi kwa njia nyingi, makampuni, show, na issue nyingine,” alisema Nahreal.

Pia katika hatua nyingine Nahreal amewataka mashabiki wake kusubiria kazi mpya pamoja na kolabo za kimataifa.

Mme Amkata Mke Wake Sehemu za Siri Akauze Shilingi Milion Tano ili Apate Mtaji

$
0
0
Mwanamke mwenye umri wa miaka 60 (pichani jina linahifadhiwa), anadai kukatwa sehemu zake za siri (nyeti) na mumewe aliyemtaja kwa jina moja la Mashaka ili akauze Sh. milioni tano za Kitanzania akauze kwa mganga wa kienyeji ili apate mtaji.Mwanamke mwenye umri wa miaka 60 aliyekatwa sehemu zake za siri (nyeti) na mumewe anayefahamika kwa jina moja la Mashaka. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo baya,

Mwanamke huyo anadai kujeruhiwa na mumewe usiku wakati wakiwa wamelala nyumbani kwao
Akizungumza na mwanahabari wetu kwa tabu akiwa wodini kwenye hospitali hiyo akiwa na maumivu makali, mama huyo alikuwa na haya ya kusema:
“Siku ya tukio, nakumbuka mume wangu alikwenda kutembea, aliporejea nyumbani alifuatana na mtu mmoja ambaye ni mganga wa kienyeji.“ Walipofika nyumbani aliniambia yupo na mganga wa kienyeji ambaye alikuwa akitafuta viungo vya sehemu za siri za mwanamke akiwa na fedha milioni tano
Viewing all 104698 articles
Browse latest View live




Latest Images