Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live

Mwigulu Nchemba kuwakabidthi Yanga Kombe leo Taifa

$
0
0
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba Madelu leo Jumamosi Mei 14, 201 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kati ya Ndanda na Young Africans katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali ya Nchemba ambaye atakabidhi Kombe kwa Yanga ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2015/16, wageni wengi maalumu watakaokuwa kwenye mchezo huo ni Mkurugenzi wa Vodacom, Ian Ferrao sambamba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda pamoja na viongozi wengine wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi ya Kuu Tanzania Bara (TBLB).

Mchezo huo utafanyika kwa baraka za TPLB baada ya maombi ya Young Africans kukubaliwa na Ndanda ambao watakuwa wenyeji wa mchezo huo utakaoanza saa 10:00 jioni.

Mara baada ya mchezo huo, Mabingwa Young Africans watapewa Kombe la ubingwa, medali na fedha Sh 81,345,723; Mshindi wa Pili Sh 40,672,861; Mshindi wa Tatu Sh 29,052,044 na Mshindi wa Nne atazawadiwa Sh 23,241,635.

Mcehzaji Bora atapewa Sh 5,742,940 sawa na Mfungaji Bora wa Ligi na Kipa bora wa michuano hiyo inayodhaminiwa na Vodacom, Bia ya Kilimanjaro, Azam, Startimes na NHIF. Mwamuzi Bora atazawadiwa Sh 8,614,610 saw na Kocha Bora wakati timu yenye nidhamu itavuna Sh 17,228,820.

Young Africans ndiyo iliyoomba kwa Ndanda kadhalika TPLB kuomba ridhaa ya mchezo huo kufanyika Dar es Salaam kwa kuwa inatarajiwa kusafiri kwa ndege Jumapili kwenda Angola kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidia ya Sagrada Esperanca ya Angola utakaofanyika ama Mei 17 au 18, mwaka huu.

Barua ya Bodi ya Ligi kwa TFF imesema kwamba Young Africans watatumia mchezo huo ambao Ndanda itakuwa mwenyeji kupokea taji la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara litakalotolewa na Nchemba ambaye mara nyingi anaonekna uwanjani.

Kanuni ya pili ya Ligi Kuu Bara toleo la 2015/16 imeeleza wazi kuwa, “Katika mazingira maalumu, timu inaweza kucheza mchezo wake wa nyumbani katika uwanja mwingine endapo kuna sababu nzito na za msingi, utambulisho wa uwanja katika mazingira haya pia unawajibika kufanywa katika kipindi cha uthibitisho wa kushiriki ligi au kwa maombi maalumu kwa TPLB,” inasehemu kanuni hiyo. Kwa kuzingatia kanuni hiyo na sababu za yanga ambazo Ndanda na Bodi wameona kuwa ni nzito wamekubaliana kucheza mchezo huo Dar es Salaam.

Tayari Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameipongeza timu ya soka ya Young Africans kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa mara ya pili mfululizo baada ya kufanya hivyo msimu uliopita wa mwaka 2014/2015.

Hii ni mara ya 26 kwa Young Africans ambayo kwa sasa inacheza mashindano ya kuwania kutwaa Kombe la Shirikisho Barani Afrika, kutwaa taji hilo tangu kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka 1965. Simba inafuatia katika rekodi hiyo baada ya kulitwaa taji hilo kwa mara 18.

“Nichukue nafasi hii kuipongeza Young Africans kwa ubingwa. Pia nizipongeze timu zote za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kushiriki na kufanya msimu wa Ligi Kuu Bara ya Vodacom 2015/16 kuwa wenye mafanikio,” amesema Rais Malinzi baada ya Young Africans kufikisha pointi 71 ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine 15 zilizoshiriki ligi hiyo.


Wema Sepetu na Ommy Dimpoz Live Tena!

$
0
0
LICHA ya tetesi kuzagaa kuwa amerudiana na mpenzi wake, Idris Sultan, mtoto mzuri Bongo Muvi, Wema Sepetu kwa mara nyingine ametengeneza habari, amedaiwa bado anaendeleza uhusiano wa siri na staa wa Bongo Fleva, Omar Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, Risasi Jumamosi limepewa mchapo.

PICHA ZADHIHIRISHA
Hiyo imedhihirika hivi karibuni baada ya kuvuja kwa picha mpya za wawili hao wakiwa chumbani katika mapozi ya kimahaba huku wamevaa mavazi ya kulalia (angalia picha Uk. 1).
Picha moja wapo ilimuonesha Dimpoz akiwa amemwekea miguu Wema mgongoni huku nyingine akiwa ameegesha mkono kwenye kalio kitendo ambacho kinaleta tafsiri ya mtu na mtu wake.


TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini kilicho karibu na Dimpoz, kimepenyeza habari kuwa, licha ya Wema kupitia uhusiano tofauti, Dimpoz amekuwa akiendelea ‘kujiweka’ kwa siri jambo ambalo watu wengi hawalitambui.
“Mbona kitambo tu, Dimpoz amejiweka kwake kiulaini, sema wenyewe wanafanya mambo hayo kwa siri. Si mnajua Dimpoz si mtu wa kutangazatangaza mambo yake na ndiyo maana hadi Nay wa Mitego (Emmanuel Elibariki) akafikia hatua ya kumhisi vibaya hadi kumuimba kwenye wimbo wake,” kilisema chanzo.

MAZINGIRA YA TUKIO
Chanzo hicho kilimwaga ubuyu kuwa, picha hizo walipiga wenyewe chumbani, nyumbani kwa Dimpoz,  Kinondoni jijini Dar hivyo zilibaki katika simu ya Dimpoz ndipo chanzo hicho kilipozikwapua na kuzituma kwa paparazi wetu.
“Bwana nakupa lakini msinitaje huko, nyie kamilisheni mambo yenu lakini habari ndiyo hiyo; Dimpoz na Wema ni kapo ya kimyakimya maana wenyewe hawataki kuanika mambo yao,” kilisema chanzo hicho.

AKUMBUSHIA BIFU LA DIAMOND
Chanzo hicho kilizidi kuweka wazi kuwa, kutokana na Diamond kufahamu kuwa, wawili hao wanaendeleza uhusiano, ndiyo maana tangu picha zao za awali zilipovuja mwaka jana  wakiwa nchini Afrika Kusini,  Diamond na Dimpoz haziivi na hata uswahiba haupo tena kama zamani zile.
“Diamond hataki hata kumsikia Dimpoz katika maisha yake, anamuona ni mtu ambaye hakufanya uungwana kuwa na mtu ambaye yeye tayari ameshatembea naye,” kilisema chanzo hicho.

WEMA ASAKWA
Baada ya kupata ubuyu huo, mwanahabari wetu ‘alimvutia waya’ Wema ili kumsikia anazungumziaje picha hizo na uhusiano huo unaodaiwa ni wa siri, simu yake iliita bila kupokelewa lakini baadaye rafiki yake mmoja alisema huenda hakupokea kwa kuwa siku hiyo alikuwa safarini kuelekea Dodoma.
“Jana (Jumatano) aliniaga ana safari ya Dodoma so (hivyo) nafikiri yupo njiani na wenzake na pengine kelele za wasanii ndani ya gari si unajua tena na kaenda na wasanii wenzake wengi tu,” alisema rafiki huyo ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini.

DIMPOZ HUYU HAPA
Baada ya kumkosa Wema, mwanahabari wetu alimtafuta Dimpoz ambaye alikiri kuwa picha hizo zilikwapuliwa kutoka kwenye simu yake lakini akadai hawana uhusiano wa kimapenzi.
“Hizo picha nazijua, nakumbuka tulipiga hapahapa Dar. Ilikuwa ni hotelini na si nyumbani kama huyo mtu alivyowaambia lakini kitu cha msingi unachopaswa kujua, Wema ni mshikaji wangu wa karibu na hakuna kitu kingine zaidi ya ushikaji. Kuna mtu itakuwa kanifanyia umafia kwenye simu lakini nitadili naye lazima nitamjua tu,” alisema Dimpoz.

KUMBUKUMBU
Wema na Dimpoz walidaiwa kuanzisha uhusiano wa kimapenzi, Februari, mwaka jana walipokuwa wakirekodi video ya Ommy, Wanjera nchini Afrika Kusini.
Picha zao ‘tata’ wakiwa chumbani zilizagaa kwenye mitandao ya kijamii na kuripotiwa katika vyombo vya habari.
Baada ya hapo, Wema aliripotiwa kutembea na wanaume tofauti akiwemo Idris Sultan, mshindi wa Shindano la Big Brother Africa-Hot Shot (2014).

Chanzo:Global Publishers

Diamond Akanusha Kumsaliti Zari na Model wa Video ya Raymond ‘Kwetu’

$
0
0
Diamond Platnumz amekanusha tetesi zilizowahi kuvuma mtandaoni kuwa alimsaliti mpenzi wake Zari na mrembo aliyetumika kwenye video ya wimbo wa msanii wake Raymond, Kwetu.


“Sio kweli, wanahisi hivyo kwasababu ni binti mzuri, wanaamini kwamba kwasababu ni binti mzuri naweza kufanya chochote, kwasababu naonekana kuwa ni maarufu na nina uwezo, Raymon ndio msanii wetu so labda ningeonekana kuwa naweza kuchukua majukumu hayo,” Diamond aliiambia Fahamu TV.

Tetesi ambazo bado zinaendelea kuvuma zilisababisha msichana huyo aitwaye Irene atukanwe na baadhi ya mashabiki.

Yanga Yakabithiwa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jioni Hii....

$
0
0
Waziri na Kilimo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba (kushoto) akimkabidhi Kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' jioni ya leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam baada ya mchezo dhidi ya Ndanda FC uliomalizika kwa sare ya 2-2


Wachezaji wa Yanga wakifurahia na Kombe lao jioni ya leo Uwanja wa Taifa

Breaking News: Nyumba ya mama yake Sheikh Walidi Alhadi yateketea kwa moto

$
0
0
Nyumba ya mama yake Sheikh Walidi Alhadi imamu wa msikiti wa Kichangani yateketea kwa Moto jioni hii Nyumba hiyo ipo Mtaa wa Uwazani Magomeni Mapipa nyuma ya Bondeni Hotel.. Muungwana Blog inatoa pole kwa Familia ya Sheikh Walid Aihadi..

Nilikuwa Silipwi Kitu Top Band Kwa TID - Ommy Dimpoz Afunguka

$
0
0
Msanii Ommy Dimpoz amesema wakati anaanza muziki alipokuwa Top Band, alipitia magumu ambayo ndiyo yamemjenga.

Ommy Dimpoz ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, na kusema kuwa hajayajutia magumu hayo, kwani alikuwa anajifunza.

“Mwanzo wakati naanza nipo Top Band nilikuwa siko vizuri financially (kifedha), nilikuwa sina hela, nilikuwa naenda kwenye shoo kwenye bendi, ilikuwa some times (wakati mwingine) tunapata, unajua nilikuwa najifunza kama unaenda gereji, unaweza ukaitengeneza gari yote mwenye fundi anakuelekeza alafu hela yote anachukua, lakini kama unaelewa hapa nipo najifunza utaona kawaida utasema hapa nipo najifunza”, alisema Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz kwa sasa anamiliki lebo yake na kampuni yake ya Poz kwa Poz (PKP), na ameanza kwa kusaidia kuibua wasanii wachanga akiwemo Nedy Music, kitu ambacho alinukuliwa akisema kilikuwa ndoto yake ya siku nyingi

Waroho wa fedha kupewa mkono wa kwaheri Simba

$
0
0
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe, ametamka wazi kuwa wachezaji wote wanaoweka fedha mbele na wasiokuwa na mapenzi na timu hiyo hawatakuwa nao msimu ujao kwakuwa ndiyo wamechangia timu hiyo kukosa ubingwa wa msimu huu.

Hans Poppe ameyasema hayo baada ya hivi karibuni baadhi ya wachezaji wa Simba kugoma kwenda Songea kucheza mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Majimaji wakishinikiza kulipwa mishahara yao.
Wachezaji waliogoma ni wale wa kigeni ambao ni Hamisi Kiiza, Juuko Murshid, Emery Nimubona, Justice Majabvi, Vincent Angban, Brian Majwega na Paul Kiongera, lakini baadaye Majabvi na Angban waliungana na timu japo Angban akucheza kabisa huku Majabvi yeye akiingia kipindi cha pili.

Hans Poppe amesema: “Hatutaendelea kuwa na wachezaji wasiokuwa na mapenzi na timu, haiwezekani mshahara uchelewe kidogo halafu unagoma, mbona hata serikalini mishahara inachelewa na watu wanafanya kazi kama kawaida huku wakifuatilia haki yao kwa utaratibu lakini kwa wachezaji wa Simba imekuwa tofauti wamekuwa wakicheza ilimradi nakupelekea matokeo mabovu kwa timu hiyo na sasa imepoteza tena nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa kwa msimu wa nne.

Poppe ambaye kwa sasa ndiyo kama mhimili wa timu hiyo amesema “Hii haipo Simba tu, wanapaswa kutambua kwamba wapo kwa ajili ya kuipigania timu na masuala hayo yakitokea si sisi bali mazingira ndiyo husababisha, bora tubaki na wachezaji wenye mapenzi na timu kuliko wa aina hii awana uchungu na timu.”

"Hebu angalia sasa wamelipwa na walicheza kinazi na timu imepoteza nafasi ya ubingwa na uwakilishi wa michuano ya Kimataifa sasa hiyo mishahara wameifanyika kazi gani wakati wameharibu," alihoji Hans Poppe.

Kauli hiyo ya Hans Poppe inamaanisha kuwa, Kiiza na Juuko wana nafasi ndogo ya kubaki Simba kwani huwa hawataki kucheleweshewa mishahara yao.

Kiiza amekuwa akilaumiwa kwamba amekuwa chanzo cha migogoro ya chini chini ndani ya klabu hiyo hali inayosababisha mfarakano kati ya wachezaji na viongozi na kupelekea timu hiyo ambayo ilikuwa katika mbio za ubingwa kupoteza mwelekeo dakika za mwisho na kutoa mwanya wa mahasimu wao Yanga kuendelea kutamba.

Hivi karibuni, Kiiza aliwahi kufukuzwa kambini kutokana na utovu wa nidhamu na uamuzi huo ulichukuliwa na meneja wa Simba.

Simba sasa baada yakupoteza mwelekeo kutokana na kukosa mshikamano baina ya wachezaji, benchi la ufundi, viongozi na wanachama wamekuwa katika malumbano ya chini chini baina yao huku mashabiki na wanachama wakipiga kelele na kupaza sauti zao kuutaka uongozi wao ujiuzuru ama uitishe mkutano mkuu wa dharula kujadili mustakabali wa timu hiyo.

Mashine "iliyotumbuliwa" na JPM Uwanja wa Ndege Imepona na Inafanya kazi Kwa Ufasaha

$
0
0
Hatimaye mashine iliyotembelewa na Rais JPM jana na kukutwa ikiwa mbovu au haifanyi kazi kwa ufanisi sasa inapiga mzigo kama kawaida na ikiwa chini ya uangalizi wa Maafisa Usalama wa Mamalaka ya Viwanja vya Ndege,Polisi na Afisa wa TRA.

Mashine hiyo aina ya Rapscan inayotumika kukaguwa mizigo ya abiria wanaoingia Dsm kutoka Znz,na mikoa mingine ya Tanzania,mapori ya Utalii kama Selous,Mikumi,Sadani na Ruaha pamoja na wasafiri wa nje ya nchi.Ikumbukwe kuwa palikuwa na "uzembe" wa abiria wanaoingia nchini kupitia eneo la TB One,uwanja wa Terminal One una "Status" ya "General Aviation" kwa maana huruhusu kutua ndege za abiria,mizigo na kukodishwa,ambazo zinaweza kuwa za kutoka ndani ya nchi au nje ya nchi

Kwa maana hiyo,Arrival ya Terminal One ni tofauti na ile ya Terminal Two,sababu ya Teeminal Two imegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni "Domestic Arrival" na "International Arrival",hivyo ndege nyingi za domestic katika Terminal Two mizigo ya abiria haina haja kukaguliwa sababu watu wanatoka mkoa mmoja ndani ya nchi kwenda mkoa mwingine,na wale wanaotoka nje ya nchi hawachanganyikani na wa ndani ya nchi

Uwanja wa Terminal One "Arrival" hiyo hiyo moja hutumika na abiria wa kutoka Zanzibar,Mikoani,Mbuga za Wanyama(Porini) na nje ya nchi.Hivyo kuwa na Mashine mbovu eneo la Arrival ambayo inahudumia watu wanaopita toka Zanzibar(Wakiwa na mizigo ya kibiashara kwa nia ya kukwepa ushuru) na nje ya nchi ni "kosa" kiutendaji.Wapo watu kama Pasco wa JF wanaodhani JPM kakurupuka,wasijuwe kuwa "status" ya Terminal One Arrival sio kama ile ya "Domestic Terminal Two"

Vijana wa JPM,hatumpi vitu vya kukurupuka,anapewa data zilizoshiba,ndio maana akifika anaenda moja kwa moja.Jana baada ya kuongea tu kufika saa kumi mashine zikawa zimetengenezwa na mizigo inakaguliwa kwa ufanisi mkubwa.Simu nyingi zilizokuwa zinapitishwa kinyemela toka Dubai via Zanzibar kuja Dsm zimeanza kunaswa,mali pori zisizo na vibari zinaonekana na hivyo kuwa na uhakika wa kutambua nini na nini kinaingia nchini.

Kwa taarifa tu ni kuwa Wamiliki wengi wa ndege Terminal One ni wafanyabiashara wa uwindaji na utalii,matengenezo ya ndege zao hufanyika nje ya nchi,hivyo hufanya udanganyifu wa kwenda porini na kubeba mali pori,kurudi Dsm bila kuushusha mzigo,na baadae kusafiri kwenda nje ya nchi na mzigo "kimyakimya",na wakati ndege zikirudi toka nje huja na bidhaa ambazo ni "dutable",na baadae kuingia nchini bila kutozwa kodi

Ujanja mwingine uliokuwa unatumika na wafanyabiashara wengi ni kushusha mzigo Zanzibar na baadae kuuleta Dsm na ndege za Charter na hivyo kukwepa kosi,Ndege ya Qatar na Oman Air hutua Zanzibar,hivyo wafanyabiashara wengi huja na bidhaa na kuzishusha Znz na baadae wanakuja kama abiria kupitia Terminal One na hivyo kuingiza nchini bidhaa nyingi bila kulipa kodi,kwa mashine ile kutokutumika vizuri basi Taifa limepoteza mapato mengi kwa muda mrefu

JPM kwenda pale jana hajakurupuka,ni matokeo ya jitihada za kumuonyesha sehemu ambapo kuna mianya ya ukwepaji kodi.., Twende JPM ipo siku watakuelewa,hasa utakapoanza kuiachia hela unayoikusanya sasa,wacha tule ugali dagaa kwa muda..Msosi wa uhakika mezani unakuja

By Barafu

Haya Mambo Yafuatayo Huwafanya Wanawake Wengi Kushindwa Kuingia Katika Ndoa (Kuolewa)

$
0
0
Pamoja na kuwa kuna wanawake husita kuolewa, lakini jambo hili si kubwa sana kwa wanawake kama ilivyo kwa wanaume. Kwa kiasi kikubwa katika suala la kutaka kuingia ndani ya ndoa, wanawake ni wengi ambao hutaka kufunga ndoa kuliko ilivyo kwa wanaume. Hilo tunaliona wazi tokana na shamra shamra awazo nazo mwanamke wakati wa maandalizi ya shughuli za Ndoa na Harusi.

Hata hivyo, kwa wale wanawake wachache ambao husuasua kuolewa hizi ni baadhi ya sababu zinazopelekea kusuasua huko. (Izingatiwe hii ni kwa wanawake ambao hawajawahi kuolewa kabisa)

Vigezo vilivyopitiliza viwango (hasa kwa muonekano)
Wanawake wengi hasa wa umri mdogo (lakini unatosha kuolewa) hutumia muda mwingi katika kuchagua aina ya mwanaume ambaye angependa awe mume wake. Wanawake hawa hujiamini zaidi na kusimamia sifa zile ambazo huamini ni muhimu mwanaume wa kumuoa awe nazo.  Vigezo hivyo huwa hata kwa misingi ya muonekano wa mwanaume huyo – kuna wale ambao hutaka mwanaume huyo wa kumuoa awe na sifa kama vile, mrefu, aliyejazia kifua, mtanashati, sauti nzuri n.k. Inaweza kuwa kama mzaha na ikaonekana ni kipengele kidogo sana lakini bado kuna wale ambao anaweza kuwa tayari kuolewa ila hataki sababu tu huyo mwanaume hafananii vile ambavyo yeye anataka mumewe awe.

Kutaka mwanaume tajiri
Kuna wanawake ambao tayari wameshajiwekea akilini kuwa hatakubali kuolewa na mwanaume yeyote yule ambaye hana pesa nyingi. Yupo tayari kuolewa ila si kwa mwanaume mwenye uwezo wa kawaida – hata ikitokea mwanaume ana uwezo kidogo wa kuweza kujitosheleza, yeye bado huona huyo mwanaume hamfai hadi pale tu atakapo pata yule ambaye anahisi ataishi maisha ya kifahari. Hivyo hukazana kusubiri na kujitahidi kuwinda aina ya mwanaume ambaye atakuwa na uwezo mkubwa, bila kujalisha kama huyo mwanaume kampita sana umri.

Kutompata Mwanaume Ampendae
Hili ni kama tu vile ilivyo kwa wanaume ambao huamini ndoa haiwezekani na haifai bali tu hadi pale umpatapo yule ambaye unampenda na unaamini anakupenda pia.  Wengi katika kundi hili huamini kuwa mafanikio ya ndoa kigezo kikubwa ni kupendana tu na mengine hufuata kwenye sababu ya upendo. Kuna wanawake vigezo vya mwanamme awe vipi havina umuhimu kabisa katika kutaka kuamua kuolewa. Yeye kikubwa anataka ampate mume ambaye atampenda kwa dhati na huku akiwa na matumaini kuwa huyo mume atampenda na yeye pia kwa dhati.  Huyu mwanamke anaamini msingi bora wa ndoa ni mapenzi ya dhati kati ya yeye na mmewe basi! Hana haraka hadi pale atakapompata mwanaume akampenda ndipo atakapokuwa tayari kuolewa.

Kuchagua mno Wanaume wa Kumuoa
Kuna wale wachache ambao akili hubadilika kama kinyonga; wasioridhika wala kujitambua ni nini wanataka ama mwanaume wa aina ipi wanataka. Akija wa mwenye uwezo atasema nataka wa kuchuma nae, akija asiye na uwezo atatoa sababu tu hata kama kumlaumu kuwa inaonyesha hajitumi kutafuta maendeleo. Akija wa kabila hii, atasema hapana hao wana tabia hii mimi siitaki! Yaani kwa ufupi ni mtu asiyeisha kutoa kasoro za wale ambao wanajitokeza kutaka kumuoa. Hatimaye inaweza tokea muda wa kuolewa ukapita na akaishia kupunguza uchunguzaji lakini ikiwa hata wanaume wa umri wa kufaa kumuoa kutokuwepo tena katika soko.

Kujiona ni mzuri sana
Kuna wanawake ambao ni kweli Mwenyezi Mungu kawajaalia uzuri hasa (uzuri wa muonekano), anakuwa ni mzuri kiasi kwamba wake kwa waume wote wanamkubali kwa uzuri huo na hata wote kumtamani. Hata hivyo hapo hapo kuna wale ambao huwa ni wazuri kawaida – ila kwa mtazamo wake hujiona ni mzuri mno hakuna mfano kama yeye; kitendo ambacho kwa wachache kwenye kundi hili hufanya kujiona yeye ni yeye na kuwa kwa yeyote kuwa na yeye huyo mtu anatakiwa atambue kuwa ana bahati sana. Kitendo hiki hukuza nyodo za hali ya juu ya mwanamke mwenye mtazamo huu, kiasi kwamba wanapojitokeza wanaume kutaka kuoa – anaweza onyesha tabia kama maringo, dharau na kiburi.

Kujiona ana Umri mdogo
Binti yeyote wa miaka 18 na kuendelea anaruhusiwa kuolewa endapo tu karidhia kuolewa. Wanawake wametofautiana mipangilio yao ya kimaisha, kuna wale akiwa katika umri wa kuolewa hutamani sana kuolewa na kuna wale ambao hupenda kuolewa wakiwa wakubwa zaidi. Katika kundi hili umri kuwa mdogo hutegemeana, kuna mwingine anakuwa na umri wa miaka 25 na bado akajiona mdogo na hali kuna mwingine anakuwa na miaka 20 na akajiona ni mkubwa na anafaa kuolewa. Hii pia ni kwa wanawake wale ambao huwa na malengo ya kutotaka kuharakisha katika ndoa. Anapokuwa na umri ambao anaweza kuolewa lakini yeye hayupo tayari kwa muda huo, huwa ni kikwazo kwake kuingia katika ndoa.

Maradhi hasa UKIMWI
Hili kama lilivyo kwa wanaume -  Pamoja na kuhamasishwa kwingi na wataalamu wa maradhi ya HIV/AIDS kuwa mtu hata ukiwa umeathirika unaweza kuwa na mahusiano na hata kuoa na kuwa na watoto; bado haisaidii sana kwa vijana wanaojitambua kuwa ni waathirika wakiwa bado ni wadogo, hawajaoa/olewa ama kuwahi kuwa na mtoto.  Wengi sana hukata tamaa na huona ni kheri kubaki walivyo kuliko kuingia katika ndoa, hasa tokana na imani kuwa wanawake wakizaa wakati ni waathirika; afya hudhoofika zaidi.

Kutaka maisha ya Tamthilia (Ndoa za kuishi kwa furaha milele)
Kutokana na kukua kwa idadi ya tamthilia nyingi ambazo huonyesha maisha ya kimagharibi zaidi; kumekuwa na dhana kwa baadhi ya wanawake kutaka hayo maisha ya tamthilia yawe na kwao pia. Hilo linafanya vigezo ambavyo mwanamke huyo anatumia kuchagua ama kukubali mwanaume kumuoa kutotimiza yale ambayo yeye binafsi anatarajia.  Wengi hushindwa kutambua kuwa hakuna maisha ya furaha milele, na hasa kuwa maisha ya maigizo yapaswa kuchanganya na zako kuweza kufanya maamuzi ya kipi kiigwe na kipi kiachwe kama kilivyo.

Kuona taasisi ya Ndoa kama Utumwa
Mtazamo huu kwa wanawake wenye msimamo huu, huchangiwa na baadhi kama haya:
- Usomi: Aina ya usomi ambao hupelekea kwa baadhi kuwa na tafsiri tofauti juu ya ndoa, haki, majukumu na mengine mengi.
- Kushuhudia ndoa mbovu: Hii inaweza kuwa ya wazazi/walezi wake wenyewe (pengine mama aliteswa sana), na hata ndugu wa karibu kama vile kushuhudia kila ndoa ya ndugu yake anayoijua mwanamke huishi kwa mateso, manyanyaso na maisha ya taabu na kuonewa.
- Kuwa na uwezo sana wa kujitosheleza ambao unaweza kumtimizia na kufanya lolote lile ambalo anataka katika maisha. Kwake kuwa na mwanaume kama mume kwake anaona kama ni utumwa.

Kutokuwa kabisa na mshipa wa hisia za kufanya mapenzi
Kuna wanawake wale wachache waliozaliwa hivyo. Hawana hisia yoyote ile ya kimwili ya kuweza kupata hisia za kuweza kujisikia ama kutamani kufanya mapenzi. Wengi wa aina hii ya wanawake huwa ni waoga sana wa kuwa karibu na mwanaume, na kwa wale ambao wamewahi hata jaribu baadhi huona kama kitendo cha ndoa ni kero, unyanyasaji na uchafu.  Hivyo wazo la kuwa akiolewa anatarajia kufanya kitendo cha ndoa mara kwa mara kinamvunja kabisa hamu ya kutaka kuolewa.


Source:Fikrapevu.com

Tulidanganywa Kutakuwa na Mabasi yanayoenda Kasi

$
0
0
Hili limeniuma sana. Serikal ilisema kutakuwa na mabasi yanayoenda kasi. Nmepanda haya mabasi zaidi ya mara 10 wala hayaendi kasi. Hayo ya kasi watatuletea lini?
Haya si haba hayasimami vituo ving sana kama daladala na hayana traffic jam but hayana kasi ambayo nlidhania yangekuwa nayo kama yanavyoitwa.
Kwa wale tulioenda nje ya nchi nadhan tunafaham train za kasi... Nlidhan at least hata kwa asilimia 40 tungekuwa na basi za namna hiyo. Kwa nini mlitudanganya?

Madee Akanusha Kufumaniwa Akiwa na Shilole Chumbani Wakiwa Watupu

$
0
0
Msanii wa muzuki wa bongo fleva Nuh Mziwanda ambaye alikuwa akitoka kimapenzi na Shilole alisema kuwa aliumia alipomfumania Madee na mpenzi wake huyo wa zamani katika sehemu ambayo si ya wazi yaani chumbani.

Lakini Madee kupitia kipindi cha Planet bongo amekana tuhuma hizo na kusema kuwa suala hilo halina ukweli wowote ule na kudai kuwa Shilole ni rafiki yake ambaye mara kadhaa walikuwa wakitembeleana kwa ajili ya kusalimiana na kupanga mipango mingine ila hakuwahi kutoka na naye kimapenzi na wala hajawahi kufumaniwa na Nuh Mziwanda kama ambavyo inasemekana.

” Siyo kweli Shilole ni rafiki yangu kama marafiki wengine, labda huyo Nuh Mziwanda angeleza vizuri aliwahi kunifumania wapi, lini na wakati gani labda naweza kukumbuka lakini ukweli ni kwamba yule na rafiki yangu kama walivyo rafiki wengine hivyo naomba ieleweke hivyo” alisema Madee

Mimi si Mali ya Mtu na Wala Sipo Kwa Ajili ya Kujiuza-Wastara Juma Afunguka

$
0
0
Staa wa Bongo Movie, Wastara Juma  ambaye siku za karibuni aliomba talaka kutoka kwa mume wake amefunguka na kusema yeye sio mtu wa kujiuza, bali ni mtu ambaye anajijali na kujitunza.

Wastara alisema hayo kupitia kipindi cha eNEWS ambapo inasemekana kwa sasa kuna wanaume kibao ambao wanajitokeza kumtaka baada ya kuachana na aliyekuwa mume wake Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa chama cha CCM (UVCCM) Taifa ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Donge, Sadifa Khamis Juma.

Msanii huyo amesema kuwa ni kweli wapo wanaume wengi wanaojitokeza kumtaka na wengine wakija na ahadi ya ndoa lakini bahati mbaya wanaume hao wanakuja wakati yeye haitaji kuwa na mtu kutokana na jinsi alivyoumizwa.

“Mimi si mali ya mtu na wala sipo kwa ajili ya kujiuza, lakini ukweli ni kwamba wapo wanaume wa aina nyingi ambao wanakuja na kunitaka wengine wanakuja wakitaka ndoa kabisa na wengine unakuta kweli wanania ya dhati kabisa lakini wanakuja wakati mimi sijisikii kuwa na mwanaume, maana kitu kwa kitendo alichonifanya Sadif hakijaniweka sehemu nzuri” alisema Wastara.

Najma: Sijali Mpenzi Wangu Baraka Da Price Ametoka na Wangapi Hapa Nahisi Nimefika

$
0
0
Mwanamuziki Najma Dattan ‘Naj’ ameibuka na kusema kuwa kwa msanii mwenzake Baraka Da Prince amefika wala hajali ametoka na wanawake wangapi kwa sababu hata yeye ana ‘pasti’ yake.

Akizungumza na Ijumaa, Najma alisema kuwa amekuwa akiwashangaa wasichana waliopita kwa Baraka ndiyo wanamuongelea kila siku wakidai anakula makombo lakini Baraka mwenyewe haongelei kabisa uhusiano wa watu wake wa zamani.

“Sijali ametoka na wangapi, hayo ni maisha ambayo kila mtu anapitia. Niseme tu kwamba sijawahi kumtambulisha mwanaume kwetu, hapa kwa Baraka nahisi nimefika kwa sababu ndiye mwenye penzi la kweli, kitakachofuata muda si mrefu ni ndoa tu kwani wazazi wetu wanaujua uhusiano wetu,” alisema Najma.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Awakemea Wafanyabiashara wa Sukari Wanaompigia Simu Usiku Kutaka Kumpooza

$
0
0
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi amefichua kuwa amekuwa akipigiwa simu na baadhi ya wafanyabiashara vigogo wenye nia ya kutaka kupunguza makali ya operesheni inayofanywa na wilaya yake dhidi ya waficha sukari.

Kwamba simu hizo amekuwa akipigiwa hadi usiku wa manane na huku wengine wakimtumia ujumbe mfupi wa simu wa maandishi (SMS). Amekemea wafanyabiashara hao na kutaka waache mara moja mchezo huo, kwani vyombo vya dola vinaendelea kuwafuatilia.

Hapi alisema hayo jana wakati akizungumzia suala la Uadilifu kwenye Mkutano wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu nchini na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM wanaotokana na shirikisho hilo.

Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya alibainisha kwamba amekuwa hapokei simu hizo na SMS hizo za wafanyabiashara wakubwa kutokana na sababu mbalimbali.

“Sababu ya kwanza sina sababu ya kuzipokea, lakini pili nahofia nikizipokea nitarekodiwa na wafanyabiashara hao na sauti yangu itasambazwa kwenye mitandao, kuonesha nipo pamoja nao.

“Wakati mwingine mpaka usiku wa manane wanapiga simu na kutuma meseji na wengine wanajitambulisha. Lakini huwa namuonyesha mke wangu na kumwambia sina sababu ya kuzipokea, kwani naweza nikapokea lakini katika mazungumzo yetu nikasema neno ‘sawa’, kisha neno hilo linaweza kusambazwa katika mitandao kuonyesha kwamba nia yetu ni moja ya kuficha sukari”, alisema Hapi.

Alisema hao wafanyabiashara wanaoficha sukari, wanaleta madhara makubwa kwa jamii na uchumi wa nchi, kama vile kuua viwanda vya sukari nchini.

Alisema wafanyabiashara hao wamekuwa wakiweka ‘oda’ katika viwanda vya sukari kuchukua bidhaa hiyo, lakini hawaendi kuichukua kwa madai ya kwenda kuichukua siku za baadaye, lengo likiwa kuificha.

Hapi aliwaomba wakazi wa wilaya ya Kinondoni, kuendelea kuisaidia serikali kufichua watu wote walioficha sukari.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 15, Ikiwemo ya Majipu Mapya Tanesco na Tume ya Uchaguzi

$
0
0

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya May 15, Ikiwemo ya Majipu Mapya Tanesco na Tume ya Uchaguzi

VIDEO: Mtazame Mbunge Lichongwe Sanamu la Diamond Platnumz Liwekwe Badala la lile Sanamu la Askari Samora

$
0
0
 Ulanga Goodluck Mlinga
May 13 2016 ilikuwa ni zamu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwasilisha Bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2016/2017. Katika kipindi cha kupokea michango ya maoni kutoka kwa Wabunge, Mbunge wa Ulanga Goodluck Mlinga akaguswa na harakati za staa wa Bongo flava Diamond Platnumz…

’Ingekuwa amri yangu tungechonga sanamu la Diamond tukaliweka kwenye mnara wa Askari, ule mnara tumeuchoka. Ametufikisha mbali naameitangaza nchi yetu huko mbele‘

‘Serikali hatuna mpango wowote wa kuwasaidia wanamuziki, wanapenya wenyewe tunaenda kukutana nao mbele na sisi tunajifanya kuwasaidia. Yuko wapi Mr. Nice?,hatujawawekea mfumo mzuri, ninaongea haya nikiyamaanisha’

Unaweza kumcheki kwenye hii video hapa chini…

Gigy Money: Niko Kwenye Uhusiano wa Kimapenzi na Gardner Kwa Miezi 6 Sasa

$
0
0
Gigy Money na Mtangazaji Gadner G Habashi

MUUZA sura kwenye video za Kibongo, Gift Stanford ‘Giggy Money’ amefunguka kuwa mtangazaji maarufu Bongo wa Clouds FM, Gardner G. Habash hachomoki kwake na hadi sasa wako kwenye uhusiano wa mapenzi kwa muda wa miezi sita.

Gigy mefunguka haya baada ya picha zinazomuonesha akiwa kwenye mapozi ya kimahaba na Gardner kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Giggy alisema mtangazaji huyo amekuwa mtu wa muhimu kwake kwa sasa.

“Kwani kuna tatizo nikiwa na Gardner? Yule ni mtu muelewa na sahihi kwangu, ninafikiri kupitia yeye nitajifunza mambo mengi na kuzidi kufanikiwa kwa sababu yeye ni moja kati ya watu ambao wako kwenye tasnia ya burudani kwa muda mrefu,” alisema Giggy Money.

Gardner alipotafutwa ili aweze kueleza kuhusu ishu hii alisema:

“Nipo karibu na Giggy lakini hatuna uhusiano wa kimapenzi, kwa hiyo kama anasema hivyo si kweli lakini yeye ni shabiki wangu na mimi ni mshabiki wake, ninapenda pia kazi anazozifanya,”.

Source: Tanzania Today.

Wachumi Walia bei Elekezi ya Sukari, TFDA Wakana

$
0
0

Wakati wataalamu wa uchumi na sheria wamepinga utaratibu wa bei elekezi ya sukari, Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), imesema haina vibali vinavyosubiriwa na wafanyabiashara wa bidhaa hiyo.

Pia, wachumi hao wamekosoa kamatakamata ya wanaodaiwa kuficha sukari, baada ya Rais John Magufuli kuagiza vyombo vya dola viwakamate na kuigawa bure kwa wananchi sukari inayokatamwa .

Kuhusu bei elekezi, wachumi hao walipinga utaratibu uliotangazwa na Bodi ya Sukari (SBT), kwamba bei ya sukari itakuwa Sh1,800 kwa kilo moja.

Hoja ya bei elekezi pia, ilipingwa na Profesa wa Uchumi, Ibrahim Lipumba kwamba si kazi ya Serikali kupanga bei, na kuhoji hata bei iliyotangazwa haijulikani ni kwa mauzo ya jumla kutoka kiwandani au kwa wateja wa rejareja kwenye maduka ya mitaani.

Akizungumza katika kipindi cha Kipima Joto kinachorushwa na ITV juzi usiku, Mtafiti wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Haji Semboja aliitaka Serikali kuacha soko ndiyo liamue bei.

Dk Semboja alionya hatua ya Serikali kuweka bei elekezi, kwamba kutakimbiza wawekezaji katika sekta ya sukari na kuwaumiza wakulima wa chini, wanaotegemea miwa kupata kipato chao.

“Ili tutatue tatizo hilo, itabidi wadau washirikishwe. Jukumu la Bodi ya Sukari kwa sasa ni kuratibu tu mfumo, siyo kuweka bei elekezi. Ni kama Ewura (Mamlaka ya Kudhibiti Nishati na Maji) wanavyofanya, kama Tanesco hivi karibuni walipendekeza wenyewe, ikazungumziwa na wadau mpaka Ewura wakaipitisha,” alisema.

Dk Semboja alisema licha ya viwanda vilivyopo kuzalisha kiasi kidogo kuliko mahitaji, bado kodi ya bidhaa imechangia bei kupanda.

Hata hivyo Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Suleiman Nyakulingwa alimpinga Dk Semboja, akisema bei elekezi imetokana na utafiti uliofanywa na kwamba Serikali imeshusha kodi ya sukari.

“Kodi ya Serikali ilikuwa asilimia 100, lakini Serikali imepunguza hadi asilimia 25 ili kupunguza gharama za uzalishaji na ununuzi wa sukari ili mwananchi wa kawaida aipate katika bei inayokubalika,” alisema Nyakulingwa.

Akifafanua jitihada za Serikali, Nyakulingwa alitoa mfano wa kontena 70 zilizotolewa bandarini kwa msaada wa kampuni binafsi ya Ticts iliyopunguza gharama za kutoa mzigo jumla ya Dola za Marekani 448,880.

Judith Kapinga kutoka Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) alikosoa operesheni ya ukamataji na utaifishaji wa sukari akisema ni kinyume cha sheria.

“Kuna sheria nyingi zinazodhibiti bidhaa kama sukari, kwa mfano Sheria ya Makosa ya Uhujumu uchumi ya mwaka 1984 inatoa mwongozo wa kushughulikia makosa hayo, siyo tu kutaifisha sukari,” alisema na kuongeza:

“Sheria hiyo inasema, baada ya mahakama kujiridhisha kwamba kuna mazingira ya kuhodhi sukari, Inspekta wa Polisi anaweza sasa kuendelea kuanzia hapo…

“Siyo tu unapotuhumiwa kuhodhi sukari, basi inaweza kutaifishwa hapo hapo na kusambazwa. Kuna taratibu za kisheria zinazoelezea mazingira ya kuhodhiwa sukari nini kifanyike.”

Mkuu wa Sheria na Mashtaka wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Donasian Kessy alisema kinaachofanyika ni kubainisha wafanyabiashara hao na kuwachunguza.

“Katika zoezi zima linaloendelea, tumeanza kubainisha kama kuna watu wanahodhi hiyo bidhaa. Kama unavyoona bidhaa imekutwa kwenye maghala na nyingine imekutwa bandarini ikisubiri taratibu za forodha ili itoke,” alisema.

TFDA yakana

TFDA imetoa tamko kwamba haina vibali vyovyote vinavyosubiriwa na wafanyabiashara waliodai kwamba sukari yao iko kwenye maghala kwakuwa inasubiri vibali toka kwao.

Akizungumza jana Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano wa Umma wa TFDA, Gaudensia Simwanza alisema utaratibu wa kutoa vibali huanzia bodi ya sukari ambayo huangalia uhaba katika soko na ndiyo inatoa ruhusa kwa wafanyabiashara kuingiza nchini.

Alisema muda wa kutolewa kwa vibali hivyo unategema na uchunguzi wa ‘parameter’ mbalimbali za kupimia, kwani kibali hakitolewi papo hapo, lakini kwa kipindi hiki hakukuwa na mtu aliyesubiri kibali.

“Kumbuka kulikuwa na tatizo la sukari na Rais Magufuli aliagiza watafutwe walioficha sukari, sisi tunahusika na vibali na hakukuwa na vibali vilivyokuwa vikisubiriwa, hata kama alishapatiwa kibali cha TFDA sisi hatukutoa ili afiche sukari,” alisema Simwanza.

Alisema TFDA inaendelea na uchunguzi wa sampuli za sukari iliyokamatwa kama wanavyopewa maelekezo kuzichunguza sukari hizo.

Timu ya Samatta Genk Yachapwa Goli 2 kwa 1, Samatta Acheza Dakika 45 Tuu

$
0
0

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amecheza kwa dakika 45 tu, timu yake KRC Genk ikifungwa mabao 2-1 na KV Oostende katika mchezo wa Ligi ya mchujo Ubelgiji kufuzu michuano ya Ulaya usiku wa Jumamosi Uwanja wa Schiervelde mjini Roeselare.

Samatta alitolewa baada ya kipindi cha kwanza na nafasi yake kuchukuliwa na Mgiriki Nikolaos Karelis, wakati huo Genk inaongoza 1-0 kwa bao la Mbelgiji Thomas Buffel aliyefunga dakika ya 25.

Lakini akiwa benchi, Samatta aliishuhudia Genk ikifungwa mabao mawili kipindi cha pili la kwanza na Mzimbabwe Knowledge Musona dakika ya 71 na la pili na Jordan Lukaku dakika ya 90 na ushei.

Samatta leo amecheza mechi ya 14 tangu ajiunge na Genk akitoka kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Afrika na TP Mazembe pamoja na kutwaa tuzo ya Mwanasoka Bora Anayecheza Afrika.

Katike mechi hizo, ambazo saba tu ndiyo ameanza, mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba SC ya Dar es Salaam, amefunga mabao nne, moja katika kila mechi Genk ikishindia 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji SV Zulte-Waregem, 4-0 na 4-1 dhidi ya KV Oostende na 3-2 dhidi ya Club Brugge mchezo wa kwanza.

Majipu Mapya Tume ya Uchaguzi naTanesco Yaibuliwa Bungeni

$
0
0

Ripoti ya mwaka ya Mamlaka ya Udhibiti wa Umma (PPRA) imewasilishwa bungeni mjini Dodoma ikibainisha majipu katika utoaji wa zabuni katika baadhi ya mashirika na taasisi za umma ikiwamo Tume ya Uchaguzi na Tanesco.

Ripoti hiyo ya tathimini kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 iliyotiwa saini na mwenyekiti wa bodi, Balozi Dk Martin Lumbanga iliwasilishwa juzi na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashantu Kijaji, ikibainisha ukiukaji wa taratibu za zabuni, harufu ya rushwa na kupuuzwa kwa ushauri wa mamlaka hiyo.

Ununuzi wa BVR

Katika ripoti hiyo mamlaka hiyo inabainisha majipu kwa kutofuatwa kwa kanuni katika zabuni ya ununuzi wa vifaa vya kuandikisha wapiga kura (BVR).

Imeelezwa kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilipotangaza zabuni hiyo ya Dola 78.9 milioni (Sh 169.6 bilioni) kampuni ya SCI Tanzania Limited ilishinda zabuni hiyo lakini ikalalamikiwa.

Katika malalamiko yake, kampuni ya Safran Morpho ambayo pia iliomba zabuni hiyo, ilikata rufaa ikisema haikuridhishwa na mchakato mzima ulivyoendeshwa na SCI Tanzania Limited kushinda.

Baada ya kushughulikia rufaa, Mamlaka ya Rufaa ya Manunuzi ya Umma (PPAA) ilibaini kuwa SCI Tanzania Ltd haikuwa na uzoefu uliotakiwa, fedha, ufundi wala uwezo wa kuzalisha na ikaiagiza NEC kuanza mchakato wa zabuni upya.

Badala ya kutekeleza uamuzi huo, NEC iliwakaribisha tena wazabuni wote ambao walishindana katika zabuni iliyofutwa na vifaa vya kampuni ya Lithotec Export vilionekana kufanya kazi vizuri.

Ripoti hiyo inasema NEC iliamua kutumia utaratibu wa chanzo kimoja (single source) na kusaini mkataba na kampuni hiyo ya Afrika Kusini ya kusambaza BVR 10,500 zenye thamani ya Dola za Marekani 89 milioni (Sh191.3 bilioni), ikiwa ni ongezeko la Sh21.7 bilioni za awali.

Mbali na hilo, baadhi ya maofisa wa NEC walishiriki katika timu ya uthamini kwenye bodi ya zabuni na vikao vya majadiliano, hali iliyosababisha mgongano wa maslahi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Kailima Ramadhan alipoulizwa alisema sheria ya manunuzi ya umma inaruhusu kupatikana mzabuni kwa njia ya ‘single source’ na kwamba hawakuwa wamevunja sheria yoyote na BVR 8,000 zilinunuliwa na watu wakapiga kura.

“Ni kweli PPAA walipoona mapungufu walitwambia turudie mchakato upya na sheria inaruhusu mzabuni mmoja kulingana na mazingira, hatukuwa kinyume cha sheria,” alisema Kailima.

Majipu Rahco

Katika hatua nyingine, PPRA imebaini madudu katika zabuni ya kuboresha Reli ya Kati iliyofanywa na kampuni ya Rahco, ambayo haikuwa katika mpango wa manunuzi kwa mwaka 2014/2015.

Mamlaka hiyo inadai mkurugenzi mkuu wa Rahco alijitwalia madaraka yote ya kuwa mamlaka ya uidhinishaji wa bajeti na yale ya bodi ya zabuni na kuidhinisha matumizi ya fedha.

Meneja mkuu wa manunuzi wa Rahco, alitoa ushauri sahihi kwa mkurugenzi huyo mwendeshaji lakini ushauri wake haukuzingatiwa na matokeo yake alibanwa na mkurugenzi huyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, bodi ya zabuni ya Rahco haikushirikishwa kabisa katika mchakato huo wa zabuni ambapo kampuni ya CRCC and Integreted Communication zilipewa zabuni.

Jukumu la kuita wazabuni na kuwapa zabuni hiyo lilifanywa na mkurugenzi mwendeshaji wa Rahco pekee bila kushirikisha bodi ya zabuni, taarifa hiyo inabainisha.

PPRA imeeleza katika taarifa hiyo kuwa hakuna ushahidi wowote wa nyaraka kuonyesha ni kwanini mkurugenzi huyo aliivunja bodi ya zabuni iliyokuwepo na kuteua nyingine kabla ya muda wake kwisha.

Mamlaka hiyo imependekeza mkurugenzi huyo, Benhadard Tito afike mbele ya Bodi ya wakurugenzi ya Rahco kujieleza ni kwanini alikiuka kwa makusudi sheria ya manunuzi ya umma.

Vilevile mamlaka hiyo inaagiza bodi ya wakurugenzi kumchukulia hatua mkurugenzi huyo huku ikipendekeza suala hilo lipelekwe Takukuru ili kuchunguza uwepo wa mazingira ya rushwa.

Mamlaka hiyo ilipendekeza Rahco ijulishwe kuwa zabuni kati yake na makampuni hayo ni batili na ianzishe mchakato upya na pia kulipeleka suala hilo kwa mkurugenzi wa upelelezi (DCI) kwa uchunguzi zaidi.

Hata hivyo, Tito na mwanasheria wa Rahco, Emmanuel Massawe na mwakilishi wa kampuni ya RothChild Proprietary Ltd ya Afrika Kusini, Kanji Mwinyijuma wameshtakiwa kwa makosa tofauti na hilo la PPRA.

Tito ameshtakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi, matumizi mabaya ya madaraka na kula njama na kuisababishia Serikali hasara ya Dola 527,540 za Marekani.

NHIF na kampuni ya China

PPRA inabainisha kuwa zabuni ya Sh8.1 bilioni ilitolewa kinyume cha taratibu na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kampuni ya China Wuyi Co. Ltd.

PPRA inasema NHIF kupitia barua yake ya Agosti 28,2014, iliitaka mamlaka hiyo kufanya uchunguzi katika mchakato wa zabuni hiyo ikishuku kuwapo kwa mchezo mchafu.

Baada ya uchunguzi, PPRA ilibaini kuwa timu ya wathamini ya NHIF ilikosea kwa kupendekeza kampuni hiyo ipewe zabuni kwa sababu ilikuwa imefungiwa na Benki ya Dunia kufanya shughuli za manunuzi kuanzia mwaka 2009 hadi 2017.

Kutokana na makosa hayo, PPRA imemtaka ofisa aliyehusika kusaini zabuni hiyo kujieleza kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kukiuka sheria kwa kuipa zabuni kampuni iliyozuliwa kushiriki manunuzi ya umma.

Pia mamlaka hiyo imependekeza kuchukuliwa kwa hatua kwa timu ya uthamini kwa kushindwa kubaini mapungufu hayo na hatua kama hizo pia zichukuliwe kwa bodi ya zabuni ya NHIF.

Tanesco na zabuni ya mafuta

Mbali na suala hilo, mamlaka hiyo pia imemtaka mwenyekiti wa bodi ya zabuni ya Tanesco kujieleza kwanini asichukuliwe hatua kwa kuiingiza kampuni ya Camel Oil (T) Ltd katika zabuni wakati iliondolewa kwa kukosa sifa.

Kampuni hiyo pamoja na Oryx Oil Company Limited ziliingizwa katika zabuni ya ununuzi wa mafuta mazito (HFO) kwa ajili ya mashine za kuzalisha umeme za kampuni ya IPTL.

Ripoti hiyo inafafanua kwamba shehena ya kwanza ya lita milioni 9 zenye thamani ya Sh12.4 bilioni zilinunuliwa kutoka kampuni ya BP na shehena ya pili ya lita milioni 16 yenye thamani ya Sh21.2 bilioni ikanunuliwa kutoka Puma.

Hata hivyo, PPRA imebaini mapungufu ikiwamo kutokuwapo kwa barua ya ushindi wa zabuni iliyotumwa kwa BP na pia hapa kuwa na hati ya makabidhiano (delivery note) kama ushahidi.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa kampuni ya BP ililipwa kwa kuegemea mzigo uliopakiwa wa lita 8,979,000 lakini shehena iliyoshushwa katika mitambo ya IPTL ilikuwa lita 9,970,106, ikiwa ni lita 991,106 zaidi.

Mamlaka hiyo ilibaini kuwa kutokana na zabuni hiyo, BP ililipwa Sh12.4 bilioni kwa hati ya malipo namba 58 VC 1100081 ambayo ilionyesha malipo hayo yalizidishwa kwa Sh42.4 milioni
Viewing all 104756 articles
Browse latest View live




Latest Images