Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live

TANZANIA INAWEZA KUZIPIKU NA KUONGOZA KIUCHUMI KATIKA NJE ZA AFRICA MASHARIKI

$
0
0
Licha ya nchi hizo kuwa chini ya mtawala mmoja wa kikoloni (mbali na Rwanda na Burundi), bado inaelezwa kuwa Tanzania ina nafasi kubwa ya kuendelea kiuchumi kuliko wanachama wengine wa Afrika Mashariki.
Akizungumza katika mjadala wa bajeti za Afrika Mashariki ulioandaliwa na taasisi ya utafiti wa jamii na uchumi (ESRF) juzi jijini Dar es Salaam, mwakilishi kutoka Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Abdulla Makame anasema Tanzania ina kila sababu ya kuendelea kupitia ushirikiano huo.

“Tunazo fursa nyingi tu za kuendelea; tunayo ardhi kubwa na yenye rutuba, tunazo rasilimali ingawa kwa sasa kuna janga la ujangili wa meno ya tembo. Tuko pia kwenye eneo zuri la kijiografia.

“Tofauti na nchi nyingine za Afrika Mashariki, Tanzania inapakana na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Zambia, Malawi na Msumbiji. Hakuna nchi nyingine ya Afrika Mashariki inayopakana na nchi wanachama wote kwa wakati mmoja,” Dk Abdulla.

Bajeti Jumuiya ya Afika Mashariki

Pamoja na kuwapo kwa fursa hiyo anasema bado bajeti ya Serikali hailingani na matakwa ya maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Bajeti ya Taifa hailingani na malengo na mipango ya maendeleo ya Afrika Mashariki. Tungetarajia kuwa bajeti za maendeleo ya jumuiya ziwekwe moja kwa moja kwenye wizara husika,” anasema Dk Makame.

Anashauri waandaaji wa bajeti kuangalia vipaumbele vya jumuiya hiyo na kukamilisha sera yake.

“Tunayo Reli ya Kati iliyojengwa na Wajerumani wakati wa ukoloni. Ilitakiwa reli hii itumike kuleta maendeleo ya uchumi kwa Tanzania, lakini bado haina viwango vya kimataifa,” anasema Dk Abdulla.

Akijibu hoja hizo, Kamishna Msaidizi wa bajeti kutoka Wizara ya Fedha, Emmanuel Tutuba anasema tayari bajeti ya Serikali imeanza kutekeleza mahitaji ya jumuiya hiyo.

“Nikiangalia kwenye bajeti yetu naona kuna mambo mengi yameanza kutekelezwa na mengine yako ngazi ya kimataifa. Kwa mfano, sekta ya umeme, ukiangalia takwimu na uwekezaji wa Serikali utaona lengo ni kuuza umeme kwa nchi za Afrika Mashariki. Maendeleo ni mazuri hasa kwa umeme wa gesi kutoka Mtwara. “Hata ukiangalia upande wa kilimo, wenzetu wa NRFA walinunua mahindi mengi na kuyauza nchini Kenya, wanategemea kupata Sh8 bilioni.

“Hata ukiangalia viwanja vya ndege kwa mfano, wa Kigoma, umejengwa mahsusi kwa ajili ya kuunganisha Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rwanda na Burundi. Kwa hiyo tayari kuna utekelezaji wa bajeti kwa maendeleo ya Afrika Mashariki.”

Biashara imeongezeka zaidi

aye Ofisa wa Shirikisho la Chama cha Wafanyakazi, Kilimo na wenye Viwanda (TCCIA), Adam Zuku anasema: “Tangu tumejiunga, ukubwa wa biashara umeongezeka tofauti na zamani, haijaridhisha, lakini inakwenda vizuri.

“Tunapozungumzia mtangamano huu wa sasa ni tofauti na wa zamani.

Mtangamano wa sasa ni wananchi zaidi kuliko zamani ambapo ilikuwa kwa viongozi pekee. Siku hizi mambo yanafanywa na wataalamu,” anasema. Anatoa mfano wa ukuaji wa biashara akisema hata mashirika ya viwango ya jumuiya hiyo sasa yanatambuana na kutoa maagizo yanayofanana.

BINTI ALAZIMISHA UMAARUFU KWA KUJIPIGA PICHA AKIKISS NA MSANII DAVIDO NA KUZISAMBAZA MTANDAONI

$
0
0
Umaarufu mwengine wa ajabu sana binti huyu inasemekana alifanya kila mbinu apate nafasi hata ya kumbusu tu davido , na alipoipata hakufanya makosa wakati wana kiss alijipiga picha nakusambaza picha hiyo kila kona kwenye mitandao. Daahhh hatari sana..!! 

JE NI KWELI UMAARUFU WA CHADEMA UNAPUNGUA? KAMA KWELI KWANINI?

WEMA, KAJALA KIMENUKA

$
0
0
Kimenuka upyaaa! Wale mashostito wawili katika kiwanda cha filamu za Kibongo, Wema Sepetu na Kajala Masanja ambao walikuwa marafiki wa kufa na kuzikana, wanadaiwa kuvunja rasmi ushosti wao, Ijumaa limenyetishiwa.

Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni rafiki wa mastaa hao, hivi sasa hali ni tete huku sababu mbalimbali zikidaiwa kuwa chanzo cha yote.

WEMA KARUDI KWA SNURA?
Chanzo hicho kilidai kuwa kila mmoja kwa sasa amechukua hamsini zake huku Wema akidaiwa kurudi kwa shostito wake wa zamani, mamaa wa Majanga, Snura Mushi.

KISA CHA SALUNI
Mpashaji wetu huyo alizidi kudai kuwa chanzo kikubwa ni kuwa mashosti hao walikutana katika saluni moja maarufu iliyopo Kinondoni, Dar ambapo Kajala alikuwa akitokea kwenye ‘shutingi’ ya filamu yake.
Ilidaiwa kuwa Kajala alifika saluni hapo akiendesha baiskeli iliyosababisha akaloa jasho sehemu kubwa ya mwili wake.

Ilisemekana kwamba Wema alipomuona Kajala alitaka kumkumbatia lakini Kajala alimkwepa kwa sababu mwili wake ulikuwa na jasho jingi, jambo lililomfedhehesha Wema na kununa.
“Yaani baada ya Kajala kukwepa kukumbatiwa, Wema aliumia sana.
“Alichokifanya Wema, alimrushia Kajala maneno makali akimhoji kwa nini alimfanyia hivyo wakati hawana tatizo lolote kati yao,” kilidai chanzo hicho.

KISA CHA NYUMBANI
Hata hivyo, chanzo kingine kilicholonga na Ijumaa kilidai kwamba kuna siku Kei alikwenda nyumbani kwa Wema, Kijitonyama Dar kwa lengo la kumchukua waende location (sehemu ya kurekodia sinema).

DIAMOND ANANYIMA FURSA?
Ikadaiwa kuwa Kajala alipofika nyumbani hapo aliambiwa ‘bimkubwa’ huyo amelala na Diamond na huwa hawaamshwi.

Chanzo hicho kilidai kwamba Kajala aliwasiliana na Wema kwa njia ya simu na akamwambia asubiri ambapo msanii huyo alisubiri kwa muda mrefu bila mafanikio hivyo hawakwenda kushuti siku hiyo.
Pia chanzo hicho kilitiririka kwamba ushosti wa Wema na Kajala ulianza kupepesuka muda mrefu lakini uzi wa mwisho umekuja kukatwa na Diamond mara baada ya kurudiana na Wema.

KIVIPI?
Chanzo hicho kilinyetisha madai kwamba eti Kajala hampendi Diamond kwani jamaa huyo amekuwa akitumia muda mwingi kuwa na Wema hivyo kubana fursa ya mashosti hao kujiachia.

“Unajua kabla Diamond hajarudiana na Wema, Kajala alikuwa anaweza kufika pale kwa Wema na kuingia hadi chumbani kwa shosti wake lakini sasa inashindikana kwa sababu anakuwepo Diamond,” kilidai chanzo hicho na kuongeza:

“Ndiyo maana Kajala ameona kama mbwai, mbwai tu! Kila mtu afe kivyake.”

HUYU HAPA KAJALA
Kwa upande wake Kajala alipopatikana, awali hakutaka kulizungumzia suala hilo lakini alipobanwa alidai kuwa hana tatizo na Wema na kwamba sasa yuko bize kutengeneza filamu zake.

BOFYA HAPA KUMSIKIA WEMA
Alipotafutwa Wema na kusimuliwa mkasa mzima alisema kwa kifupi: “Mimi niko sawa, hakuna kitu na muda si mrefu watu watatuona tena pamoja,” alisema Wema.

SI MARA YA KWANZA
Wema na Kajala wamekuwa mashosti wa muda tangu Wema alipomlipia mwenzake faini ya Shilingi Mil. 13 mahakamani na kumuepusha kwenda jela baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka saba.
Hata hivyo, si mara ya kwanza kutibuana kwani mwaka jana waligombana lakini baadaye wakapatana.
GPL

NAOMBA KUJUA..WANAWAKE WENYE PROFESSIONAL HIZI WANA TABIA GANI MAPENZINI?

$
0
0
Naombeni kufahamu wanawake wenye hizi profession wana tabia gani katika ndoa zao ama wanapokuwa uchumbani mwao..

1. Wanawake wanasheria..

2. Wanawake wenye profession za mambo ya fedha kama finance management na accounting..

3. Wanawake madaktari na waalimu..

Je, hawa wanatumiaje proffession zao katika cheating wakuu???

jamani tuangazieni na wanawake wengine katika profession mbali mbali..!

Je kazi anayofanya mwanamke inaweza kumbadilisha na kuwa na tabia fulani???

naombeni maoni yenu wadau!

HUDDAH MONROE"I DEAL WITH RICH MEN ON THE FORBES LIST NOT CHEAP ATTENTION SEEKERS LIKE MUSTAPHA"

$
0
0
It now seems that the public feud between care-free socialite, Huddah Monroe and Colonel Mustapha, will not end any-time soon as the two constantly engage in a war of words.

Earlier today, Huddah posted on facebook claiming that she deals with rich men on the Forbes List and not cheap attention seekers like Mustapha.

She further alleged that Mustapha only saw her half-nak3d body during a photo-shoot and she has never had s3x with him.

Huddah also claimed that Mustapha leaked the photos to look for publicity after realizing his career was dwindling.

“The class of men I date are busy out there looking to be on Forbes list not busy looking for social media fame!!!!! Hehe! Never seen a man so bitter over a woman he only saw half naked in a photo shoot…. Chill, at least u got to take to floss with!” Read the post.

Of late, the two controversial celebrities have been engaging in a war of words after they ended their infamous relationship late last week.

BEN POL "MIITO YA SIMU..UWIZI MTUPU ..NAJITOA RASMI"

$
0
0
Ben Pol hafurahii tena biashara ya miito ya simu (Ring Back Tone, RBT) kwakuwa ripoti ya miezi sita kutoka kwa moja makampuni yanayohusika na biashara hiyo nchini kumkatisha tamaa muimbaji huyo wa ‘Unanichora’.

Ripoti ya kipindi hicho iliyotolewa na kampuni hiyo, inaonesha kuwa ameingia shilingi 31,124 tu. “Mimi picha ninayoipata hapo naweza kusema kuna utapeli,” Ben Po ameiambia Bongo5.

Amesema ameshawahi kuishtaki kampuni nyingine tofauti inayohusika na biashara hiyo baada ya kupewa ripoti ya mapato isiyoridhisha na ndipo alipoufahamu ukweli. “Kwasababu na mtandao pia uliingia kwenye lile sakata na wenyewe wakatoa invoice ambayo walikuwa wanawalipa wale, ni tofauti na hizo ripoti wanazotoa hawa third part. Kwahiyo ni straight kama ni udhulumati,” amesema Ben.

“Mimi najitoa na kampuni zote labda kama mtu aseme ananunua copyright ya kumiliki huo wimbo jumla ambayo watashindwa kwakuwa itakuwa bei kubwa sana.”
-Bongo5

KAMA MABAKI YA NDEGE YALIO ONEKANA USTRALIA YATAKUWA YA AIR MALAYSIA BASI KUNA MKONO WA MTU

$
0
0
Australian security expert Neil Fergus says that if the two objects found ARE from flight MH370, it must have been flown there deliberately

A specialist has suggested that the location of the possible debris from missing flight MH370 means it COULD NOT have got there without human intervention.

Australian security expert Neil Fergus says there is no way the missing Malaysian Airlines plane could have got to the location now being searched of its own accord.

Speaking on Australia's Channel 9 he also ruled out a catastrophic malfunction, suggesting the plane couldn't have made it all the way to an area south west of Perth simply due to any kind of fault.

Mr Fergus told the channel the only way the plane could have made it that far from its original flight path was by human hand, be it by one or both of the pilots, or passengers.

"If this debris does turn out to be the missing MH370 then, given its location, we can definitely rule out technical malfunction," he said.

"There is no way with (some) sort of technical calamity or fire that it could have travelled to where it appears to be. It would - in the first instance confirm - human intervention."

The comments come in the wake of news earlier today that two objects have been spotted in a remote part of the the Indian Ocean - and that they could be debris from the missing Malaysia Airlines flight.

Four military search planes have now been dispatched to take a closer look at the objects, one of which had a dimension of 24 metres (82 feet).

There could be other objects in waters nearby in the area that is a four-hour flight from Australia's coast, said John Young, manager of Australian Maritime Safety Authority's emergency response division.

"This is a lead, it's probably the best lead we have right now," he said, while cautioning that the objects could also be seaborne debris along a key shipping route where containers periodically fall off cargo vessels.

HABARI KUHUSU PICHA ZA SNURA ZILIZOMUONESHA AKIWA KWA MGANGA

$
0
0
Siku chache zilizopita kupitia blogs na website mbalimbali zilisambaa picha zilizokuwa zikimuonyesha Snura akiwa kwa Mganga wa Kienyeji akiwa kama anapatiwa maagizo na mganga,ambapo kwa picha hizo zipo baadhi kamshika jogoo zingine anaonekana yupo baharini anatupa kitu.
Maoni ya watu wengi na namna ya uandishi wa habari hiyo juu ya zile picha yalionesha Snura akifanya hivyo ili mambo yake yamnyookee,millardayo.com imepata picha hizo ambazo zilikua zimerekebishwa na kutolewa sehemu zinazoonyesha camera ambazo zilikua zikirekodi.
Hemed Kavu ‘Hk’ ambaye ndiye Meneja wa Snura amelisemea hilo>>’Kiukweli tumeshangazwa sana na picha hizo zilizosambazwa ambazo zime ‘editiwa’ na kutoa sehemu zinazoonyesha camera ili kumchafua msanii wangu aonekane anashiriki mambo ya kishirikina’
‘Ukweli wa zile picha ni baadhi ya vipande vya kwenye filamu ambayo Snura anaigiza sasa hivi na ni filamu ya Dotnata inaitwa Mlokole’.
Hizi ni baadhi ya picha zilizopo kwenye filamu hiyo.
IMG-20140320-WA0022
IMG-20140320-WA0020
IMG-20140320-WA0017
IMG-20140320-WA0016
IMG-20140320-WA0015

KWELI MAISHA MZUNGUKO DOGO JANJA AWAPIGIA MAGOTI TIP TOP NAKUOMBA MSAMAHA

$
0
0
Baada ya Kile Kinachoonekana Kujitambua na Kukua Kiakili ama Maisha kumwendea Kombo huko alipo Msanii Dogo Janja Amewaomba Msamaha Walezi wake wa Zamani ambao ndio walimtoa Katika Game Kundi la Tip Top la Manzese ...Dogo Janja Amesema kuwa Yeye anachotaka ni kumsamehe kwa kila kitu kilichotokea kati yake na hilo Kundi ....Ikumbukwe kuwa Dogo Janja Aliondoka kwenye kundi hilo miaka miwili iliyopita kwa kudai ananyanyaswa na kudhulumiwa kimaslahi aliondoka kwa mikogo mingi sana na Kuchukuliwa na Ostaz Juma na kuingizwa Mtanashati ..Ambao kwa sasa inaonekana wamefulia mbaya kwani hakuna kinachoendelea kwenye kundi hilo mpaka kufikia Dogo Janja kukumbuka Tip Top....Hili Liwe Funzo Kwa Wasaniiii 

BABA WA DOGO JANJA AONGEA BAADA YA DOGO JANJA KUOMBA MSAMAHA TIP-TOP

$
0
0
"Dogo Janja alishakua mtu mzima na tayari nilishawahi kumwambia achague mahali atakapoona kuna manufaa kwake, akishafanya maamuzi yake huwa ananishirikisha kwenye kujadiliana, tayari alishawahi kuniambia kuwa atafanya maamuzi baada ya kuona Mtanashati hakuna muelekeo wowote na hakuna anachopata ndipo akaniambia baba mimi mtu yoyote au kundi lolote nitakalokubaliana nalo basi nitafanya nao kazi’.
Hayo ni maelezo ya Baba mzazi wa Dogo Janja ambae ametoa baraka zote kwa Janja kurudi kujiunga na Tiptop Connection hivyo kazi imebaki kusikia kutoka upande wa Tiptop kufahamu kama wameukubali msamaha wa Dogo Janja" BABA DOGO JANJA

ANGALIA PICHA NDEGE SITA ZILIZOWAHI KUPOTEA DUNIANI HIZI HAPA

$
0
0

1. Amelia Earhart - 1937

Rubani wa Kimarekani, Amelia Earhart alikuwa mwanamke wa kwanza kuvuka Bahari ya Atlantic kuchunguza dunia, alipotea na ndege yake miongo saba iliyopita. Inahisiwa kuwa ndege yake iliishiwa mafuta na kuanguka. 
2. Airbus A330 - 2009
 Mwaka 2009 ndege ya Shirika la Ndege la Ufaransa, Airbus A330 iliyokuwa na abiria 228 ikitoka Rio de Janeiro, Brazil kwenda Paris, ilipotea kwa siku tano. Ilipatikana ikiwa imeanguka na kuungua. Hadi sasa maiti za abiria 74 bado hazijatambulika.

3. Flying Tiger 739 - 1962
 Mwaka 1962 ndege ya kijeshi ya Marekani ilipotea ikiwa na watu 90 waliokuwa wanakwenda Ufilipino. Rubani wa ndege hiyo hakuwahi kutoa taarifa yoyote ya dharura na hadi sasa haijaonekana licha ya wataalamu 1,300 kushiriki kuitafuta.
4. South American Airways - 1947
 Ilichukua miaka 50 kupata fununu za ndege ya Amerika ya Kusini iliyopotea mwaka 1947 ikiwa na abiria 11 na kupatikana mwaka 1998 katika Milima ya Andes. Ndege hiyo ilifunikwa kwenye barafu ya milima hiyo.
5. Bermuda Triangle - 1948 na 1949
 Ulikuwa ni mfuatano wa matukio ya kupotea kwa ndege mbili katika eneo la baharini linaloitwa Pembetatu ya Shetani (Devil’s Triangle) katika maeneo ya Florida, Puerto Rico na Bermuda ambalo limekuwa na matukio mengi ya kupotea kwa ndege na meli kimiujiza. Katika matukio hayo mawili, ndege hizo zikiwa na jumla ya abiria 51 zilipotea na hata wanaanga 13 waliotumwa kuitafuta pia walipotea.
6. Uruguay 571- 1972
 Ndege ya Shirika la Ndege la Uruguay, 571, ilipotea mwaka 1972 ikielekea Santiago, Chile. Ndege hiyo ambayo ilikuwa na abiria 45, ilianguka milimani na watu 12 walikufa. Walionusurika walitafutwa kwa zaidi ya siku 72. Kabla ya kuokolewa, majeruhi hao walilazimika kula nyama za wenzao waliokufa ili kuishi.

HIZI NI HOJA ZA ZITTO KABWE KUPINGA HOTUBA YA KIKWETE

$
0
0
Serikali 2 zitaendeleza hisia za Utanganyika kwa kasi 
Mkuu wa Nchi kamaliza kuhutubia Bunge la Katiba. Kimsingi kaegemea upande wa msimamo wa Serikali 2 ambao ndio msimamo wa CCM chama anachoongoza. Hata hivyo kasisitiza kuwa iwapo tunataka Serikali 3 basi tuzingatie hofu zilizopo ikiwemo masuala ya Uraia, uwezo wa kifedha wa Serikali ya Muungano nk. 
Ni dhahiri kero za Muungano zilizodumu kwa zaidi ya miaka 50 haziwezi kutatuliwa na muundo ule ule uliozitengeneza. 
Jawabu l...a muungano wa Tanzania ni muundo wa Serikali tatu wenye Serikali ya Muungano yenye nguvu na rasilimali. Tunaloweza kuongeza ni kuweka mfumo wa Tawala za Mikoa wenye kupanua demokrasia zaidi kwa kuchagua wakuu wa mikoa na kufuta wakuu wa wilaya. 
Ni dhahiri Uraia itakuwa ni 'deal breaker' kwenye suala la muundo wa Muungano. Hili litajibiwa kwa kuwa na Nchi moja, dola moja na Serikali tatu-Zitto

BAADA YA KIKWETE KUMALIZA HUTOBA YAKE...WEWE UNA HOJA GANI?

$
0
0
Kama umesikiliza Hutoba ya Rais leo katika Bunge la Katiba leo jioni Embu tupe Maoni yako, Je ametendea haki pande zote wa Serekali Mbili na Serekali tatu ?

NAPENDA KWENDA CLUB, LAKINI SIO NA MPENZI WANGU, ALONE TU..!! IMEKAAJE HII WADAU?

$
0
0
Huwa siko huru kabisa ninapokuwa na mpenzi wangu club, kwanza kuna wakati naona kama namkosea heshima vile nikisalimiana na wasichana wengine anakosa raha, mara ananiambia amechoka anataka kurudi nyumbani halafu hapo ndio kwanza club pamenoga, alafu sisikii raha nikicheza nae napenda kucheza na mtu simjui najiachia mpaka, naona Bora niwe nimuache tu kiroho safi. Au vipi wadau..!

LAZIMA AVUTE BANGI KABLA YA KUFANYA MAPENZI: USHAURI

$
0
0
Imekua tabia siku hizi yani kabla hatujaanza kufanya lolte lazima avute bangi kwanza , napia anipe na mimi nivute, huwa nafanya tu hivyo kwa sababu nampenda ila sasa imekuwa too much, mpaka inanitesa siku nyingine siwezi hata kuamka kichwa kinauma kutwa nzima. Naombeni ushauri.. wadau 

BABY SHILOLE PICS..."MIE KING'AMUZI KUNITAZAMA TU LAZIMA UWEKE VOCHA"

$
0
0
She is Mwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.........Our Hot Celeb Tonight...

KIKWETE AVURUGA MJADALA...AONYESHA ISIA ZAKE ZA KUTAKA SEREKALI MBILI

$
0
0
Rais Jakaya Kikwete jana alibadili upepo wa mchakato mzima wa Katiba baada ya kutoa maoni yake binafsi, akitaka muundo wa Serikali mbili badala ya tatu zilizopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Akizungumza katika ufunguzi wa Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma, Rais Kikwete alipangua hoja moja baada ya nyingine zilizotolewa na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba wakati akiwasilisha Rasimu ya Katiba bungeni Machi 18, mwaka huu.

Katika hotuba yake hiyo ya saa 2:49 iliyokuwa na maneno ya ‘kuuma na kupuliza’ kuhusu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba, Rais Kikwete alisema  suala la muundo wa Muungano ndiyo ajenda mama katika Rasimu ya Katiba na kwamba iwapo wajumbe watatoa uamuzi usio sahihi, nchi inaweza kujaa migogoro ambayo haikuwapo.

Huku akishangiliwa na wajumbe wa Bunge hilo, Kikwete alisema kuwa wanaotaka Serikali tatu waangalie changamoto zake na kuzitafutia majibu, kwa maelezo kuwa muundo huo unaweza kuvunjika kirahisi.

Alisema ingawa Jaji Warioba aliwatoa hofu wananchi kuwa Serikali tatu hazitakuwa na gharama kubwa, ukweli ni kwamba muundo huo una gharama na utekelezaji wake ni mgumu na kusisitiza kuwa CCM inaweza kuzimaliza kero za Muungano bila kuhitaji uwapo wa Serikali ya tatu.

Huku akichambua kile kilichoelezwa na Jaji Warioba sambamba na kuwapiga vijembe wenyeviti wa vyama vya upinzani akiwamo Christopher Mtikila (DP) na Freeman Mbowe (Chadema), Rais Kikwete alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa sababu mbili kubwa  za kupendekeza muundo wa Serikali tatu;

“Sababu ya kwanza ni kwamba muundo huo ndiyo matakwa ya Watanzania wengi Bara na Zanzibar.  Sababu ya pili muundo huo unatoa majibu ya uhakika na endelevu kwa changamoto za muundo wa sasa wa Serikali mbili zinazolalamikiwa na pande zote mbili.”

Aliongeza, “Wapo wanaokubaliana na tume na kwamba muundo wa Serikali tatu ni matakwa ya wengi na hauepukiki na kwa msemo wa Kiswahili wengi wape. Lakini wapo wanaopingana na takwimu za tume kwamba hazionyeshi ukweli huo. Mimi nasema maneno yanayosemwa na watu siyo yangu.” Huku akishangiliwa na wajumbe wa Bunge hilo alisema, “Watu wanasema Watanzania waliotoa  maoni kwa tume ni 351,664, kati yao 47,820 sawa na asilimia 13.6 ndiyo waliokerwa na muundo wa Muungano. Watu 303,844 sawa na asilimia 86.4 hawakuwa na tatizo na muundo wa Muungano na wala hawakuuzungumzia wakati wa kutoa maoni.”

Alisema hivi sasa watu wanahoji iweje asilimia 13.6 ndiyo wageuke Watanzania walio wengi ambao wametoa maoni ya kutaka Serikali tatu.

“Watu wanahoji mbona taarifa ya tume inayohusu takwimu (ukurasa 66,67), inaonyesha kati ya watu 47,820 waliotoa maoni kuhusu muungano watu 17,280 ndiyo waliotaka Serikali tatu ambao ni sawa na asilimia 37.2 na waliotaka muundo wa Serikali mbili ni asilimia 29.8, Serikali ya mkataba asilimia 25.3 na Serikali moja asilimia 7.7” alisema. Alisema taarifa ya tume inaonyesha kuwa watu 772,211 waliotoa maoni ni asilimia 10.4 ndiyo yaliyozungumzia muundo wa Muungano na asilimia 88.6 hawakuzungumzia Muungano, bali mambo mengine.

“Watu wanahoji kama Muungano ni jambo linalowakera sana Watanzania ingethibitika kwenye wingi wa wale waliotoa hoja. Usahihi wa hoja hii ni upi, nawaachie nyie (wajumbe) mjadili” alisema huku akishangiliwa kwa nguvu.

Akizungumzia sababu ya pili ya tume kwamba muundo wa Serikali tatu unajibu changamoto za muundo wa Serikali mbili, huku akifafanua kero zinazotolewa na kila upande wa Muungano alisema; “Nyinyi ndiyo waamuzi, sikilizeni vizuri hoja hizi mtafakari na kuamua. Tume yenyewe imekiri kuwa muundo wa Serikali wa Serikali tatu una changamoto zake ikiwa ni pamoja na gharama kubwa za uendeshaji wa shughuli za umma.”

WAPINZANI WAPINGA HOTUBA YA JK BUNGE LA KATIBA

$
0
0
Wenyeviti wa vyama vya Upinzani vya Chadema, Chama cha Wananchi (CUF) na Chama cha NCCR-Mageuzi, jana usiku walikutana ili kutoa kauli ya pamoja, kutokana na hotuba ya ufunguzi wa Bunge kwa maelezo kuwa tayari Rais amevuruga mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya.

Wakati viongozi hao wakikutana, Mwenyekiti wa Chama cha DP Mchungaji, Christopher Mtikila alisema, Rais ameingilia mchakato na kutoa maelezo jinsi ya  kuandika Katiba.

Wakizungumza na gazeti hili jana mara baada ya hotuba hiyo, Freeman Mbowe, James Mbatia na Profesa Ibrahim Lipumba, walisema wameipokea kwa masikitiko makubwa hotuba hiyo.

“Tunakwenda kujadili hotuba ya Rais na tutatoa msimamo wetu,” alisema Mbowe.

Awali Katibu wa muda wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Julius Mtatiro alisema Rais Jakaya Kikwete amevuruga mchakato wa Katiba, kwani walitarajia angetumia mamlaka yake kama Rais kuwaunganisha.

“Rais tulitarajia angeongea kama mkuu wa nchi, lakini amezungumza kama Mwenyekiti wa CCM na kutoa msimamo juu ya muundo wa Muungano jambo ambalo hatukulitegemea,” alisema Mtatiro.

Alisema kwa Rais kutoa msimamo ni sawa na mwongozo jambo ambalo limevuruga mchakato mzima.

Hofu ya kuvunjika Bunge

Wakizungumza nje ya Bunge, baadhi ya wajumbe wameeleza kuwa hotuba ya Rais Kikwete kama ikitekelezwa uwezekano wa kupata Katiba Mpya utakuwa mgumu.

Mjumbe Luhaga Mpina alisema kwa jinsi rasimu ilivyoandikiwa na kama muundo wa serikali mbili ukipita basi rasimu ya Katiba itabidi iandikwe upya.

“Rasimu yote imetengenezwa kwa mfumo wa serikali tatu sasa hapa kuna hatari ya Bunge kukwama ,” alisema.

Mtatiro kwa upande wake alisema sasa kuna hofu ya kushindwa kupatikana Katiba Mpya kwani Rais amewachanganya wajumbe na kama watapitisha maoni yake itabidi rasimu kuandikwa upya.

Mjumbe Mustapha Akoonay, alisema upatikanaji wa katiba upo shakani kwani sasa upinzani utakuwa mkubwa juu ya muundo wa muungano.

“Kwa sasa nadhani itabidi turudi upya kwa wananchi kupata kura ya maoni juu ya muundo wa muungano,” alisema.

Lucy Owenya alisema  Rais amegeuza mkutano wa Bunge kuwa ni mkutano wa Chama Cha Mapinduzi, kwani ameshindwa kabisa kutoa mwelekeo wa nchi na badala yake ametoa msimamo wa CCM.

“Kutokana na hili, naamini kabisa Bunge halitakuwapo na ni bora iwe hivyo kwa kuwa amejibu hotuba ya Warioba na kwa maana hiyo amepingana na mawazo ya wananchi.”

Godbles Lema alisema kuwa Rais hakuja kuhutubia taifa bali alikuja kufanya semina na kujibu hotuba ya Warioba.

Mjumbe huyo ambaye ni mbunge wa Arusha Mjini alionyesha shaka kuwa baada ya muda wa wiki tatu hakutakuwa na Bunge la Katiba kwa kuwa wako baadhi ya watu ambao hawatakubali kilichofanywa na Rais Kikwete.

“Waliochukua fedha ni vyema wakaenda kumalizia nyumba zao kwa kuwa kiongozi wetu amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwafurahisha wanaCCM lakini kwa Watanzania hatutakubali,” alisema Lema.

John Cheyo alisema, “Mimi ninachokiona ni maridhiano tu, suala la kufumua rasimu halinipi shida kwa kuwa vitu vyote vinavyoletwa bungeni huwa ni mali ya Bunge na hivyo tutafanya tunavyoona sisi inafaa.”

Mchungaji Peter Msigwa, alisema kuwa kosa kubwa ambalo lilifanywa na upinzani ni kukubali na kuruhusu Jaji Warioba atangulie kuwasilisha rasimu yake akasema hilo ndilo lililowagharimu.

Alitaka Bunge livunjwe mara moja ili warudi kwa wananchi wakaamue na kuwahukumu kutokana na kile ambacho walikifanya katika Bunge ambalo kwa maoni yake wamekula fedha za walipa kodi bure.

Naye Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa aliipongeza hutuba ya Rais Jakaya Kikwete ya uzinduzi wa Bunge la Katiba.

Lowassa ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge la Katiba, alisema kwa kifupi hotuba ya Rais Kikwete ni nzuri. Lowassa alitoa kauli hiyo, wakati akitoka nje ya Bunge, muda mfupi baada ya Rais Jakaya Kikwete kumaliza hotuba ya uzinduzi wa Bunge hilo.

HENRY KILEWO"SIKUTEGEMEA HOTUBA NZURI...HAKIKA MAHESABU YA SEREKALI MBILI YAMESHAPANGWA"

$
0
0
Katika Ukurasa Wa Henry Kilewo wa Chadema Ametoa hisia zake kuhusu Hotuba ya Jana ya Raisi katika Bunge la Katiba....Jisomee Hapo chini:

"Pole Watanzania, maana wahenga wanasema kibovu huja na kibovu, kimsingi sikutegemee hutuba nzuri ya kiuongozi bali nilitegemea hutuba mbovu kwa aina ya anayehutubia.
Kimsingi kiongozi mbovu huongea hutuba mbovu na ndicho kilichotokea, kwa maana hiyo kwa hali halisi mliyoiona msitegemee katiba ya wananchi.

Kwani tayari na mahesabu wamekwisha fanya yakuwa ilinserikali 2 zipite wanahitaji wajumbe 16 kutoka zanzibar, huku akinanga maoni ya wananchi ya serikali 3 ili yapite yanahitaji wajumbe 80 kutoka zanzibar kuyaunga mkono.

Kwa maana nyingi wanaweza kununua hawo wajumbe 16 ili kutimiza matakwa yao ya serikali2

Hofu kubwa ya chama tawala ni kuondoka madarakani iwapo kutapatikanika serikali 3 na kama mnavyofahamu ccm haijawahi kuishinda cuf zanzibar na huwo ndiyo ukweli, Na hofu nyingine ni ccm kufa, yaani ASP Itarudi kwa upande wa Zanzibar na Tanu kwa upande wa Tanganyika, so hapa ccm wanaangalia maslahi ya chama chao na siyo nchi.

Ila hatutakubali kupitishwa kwa katiba ya ccm bali katiba ya wananchi waliyopendekeza, ikishindikana ni bora kurudi bila katiba mpaka hapo tutakapo pata serikali makini itakayoweza kusimamia mchakato huwo.

Kwa wale ambao hamkupitia post yangu ya jana naomba mrejee nilichopost, pili Nchimbi aliniita mimi ni muogo ila leo yeye ndiye kawa muongo kwa wale mliyokuwa mnafuatilia.

Hongera Warioba ulitoa hutuba ya kiuongozi na Kimamlaka kuliko hii ya vijembe na ngonjera, Nina uhakika Watanzania tuliyowengi tupo nyuma yako pamoja na tume yako kusimamia walichotaka Watanzania, Ikishindikana wakataka kulazimisha kuipata katiba waitakayo ccm njia zipo nyingi za kudai katiba ya Wananchi.

WATAKAO PONDA TUTAENDELEA KUWAELIMISHA NA KUWA NAO KITU KIMOJA SIKU MOJA.

HOTUBA YA RAIS NAISIKILIZA NAPATA HOMA, INANISIHI KULIA NA KUNIPA MAUMIVU YA TANZ TUITAKAYO WANANCHI & WAITAKAYO VIONGOZI:

Kama Kiongozi ameona hoja mama ni Muungano wa Serikali.
Muhimu ni kuzingatia na kuhakikisha tunapata Muungano bora unaotakwa na wananchi na si Viongozi wa upande mmoja. Ikishindikana hapo iwe ruksa kwa watz kuitafuta Katiba waitakayo na wenye Imani nayo kwa nguvu ya sauti yao na si kwa njia ya sauti ya viongozi wa upande mmja kuwasemea. Inawezekana watanzania tukiamua, Viongozi waache masihara.
“Haya ni maneno yangu na Bunge hl ndo lenye maamuzi” yatakuwaje maamuzi ya Bunge ikiwa miongoni mwa wajumbe kuna mkakati maalum wa kichama kila kukicha. Na wewe upo upande huo!
Nikizaliwa simjui baba hainizuii kumtafuta na kumjua baba yng mzazi..Nimezaliwa nje ya Tanganyika lkn hainizuii kuitafuta Tanganyika.. Kutumia hoja ya tuliozaliwa miaka 64 na kuendelea tusitafute Tang ni point lesss.
Ni kweli kutunga Katiba ni suala zito na kubwa sana nakubaliana na wewe Kiongozi. Maneno haya naya dediketi kwa wajumbe wa CCM sana sana kwa kuwa naona yanawahusu.
Huu haukuwa uzinduzi bali darasa la kubadili upepo wa Jaji J. S. WARIOBA. Mh Warioba aliyoyazungumza hayakuwa maneno yk binafsi au Tume bali yalikuwa maneno, mawazo na msimamo wa wananchi ambapo nguvu ya kukusanya maoni aliipata baada ya wewe kumuamini na kumteua kuwa Mwenyekiti wa Tume. Swali lng ni Je, uliyozungumza wewe ni maneno na msimamo wa nani?? Je kabla ujaja kuzungumza na wajumbe hukupata nafasi ya kuzungumza na wabunge wa CCM? Na kama ulikutana nao mlipanga nn?
Wakati ukianza kuhutubia niliamini unaanza kwa nasaha na ujumbe mwema. Mwishoni nikagundua unapinga maoni ya wananchi yaliyowasilishwa na Warioba na kujibu hoja za Warioba ukisahau ni maoni ya wananchi na kudhani ni msimamo wa Jaji mstaafu S. WARIOBA. Ktk hilo tumepoteza mabilioni ya pesa ktk mchakato unaominywa ukweli na usahihi na baadhi ya wajumbe wa chama fulani.
Katika hili mmeonyesha dharau kwa Mtu mzito na mwenye historia ya Awamu nzito ya kwanza JAJI J. S. WARIOBA. NA HAKIKA HATA NYERERE ANGEKUWEPO ASINGEPENDEZWA KWA KUWA ALIKUWA MUUMINI WA MATAKWA YA WANANCHI NA MABADILIKO"
Source:Henry Kilewo Facebook Profile
Viewing all 104776 articles
Browse latest View live




Latest Images