Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live

Nay wa Mitego Anaimba Hip Hop Kama Taarab, Abadilike – Gigy Money

$
0
0
Video vixen machachari, Gigy Money amedai ni muda wa rapper Nay wa Mitego kubadilika kwasababu anachokisikia kwenye nyimbo zake ni taarab na sio hip hop ya ukweli.

image

Gigy ambaye hapo awali amewahi kuzinguana na hitmaker huyo wa ‘Nasaka Pesa’ baada ya kutumika kwenye video ya Shika Adabu Yako ya rapper huyo na kutolipwa ujira wake, amemuambia mtangazaji wa Jembe FM ya Mwanza, JJ kuwa hip hop ya Nay imejaa uswahili mwingi.

“Inabidi abadilishe uimbaji wake uwe wa kisasa zaidi. Nay anaimba hip hop as taarab, imekuwa ni lugha ya mafumbo wakati hip hop ni zamani ilikuwa inatritiwa nyimbo sexy ambazo anasikiliza mtu akiwa ametulia,maneno unayasikia,” amesema Gigy. “Lakini yeye anataka kuimba vitu vingi katika muda mmoja halafu anaponda, so he is bad to me kwa asilimia 00.0.”

Kwa upande mwingine Gigy amesema msanii wa hip hop anayemkubali Tanzania ni Joh Makini.

“Anajielewa, hana skendo, yaani ana nyota yake kali, msafi,” amesisitiza.

“Anaimba vizuri, unamsikia hata kama ni M-Arusha, yaani R na L zinatofautiana.”



Hamisa Mobetto Aumia Jinsi Mwanae Anavyohusishwa Kwenye Mambo yasiyomhusu, ‘Issue ya Majay na Lulu’

$
0
0

Mwanamitindo Hamisa Hassani Mobeto, amekataa kuzungumzia mgogoro unaodaiwa kuendelea kati yake na staa wa filamu Elizabeth Michael ‘Lulu’ huku akionyesha kuchukizwa na jinsi mwanae anavyohusishwa katika mambo yasiyo muhusu.
Hamisa Mobeto akiwa na mtoto wake aliyozaa na Majay
Hamisa Mobeto akiwa na mtoto wake

Akizungumza na Bongo5 Alhamisi hii, Mobeto amesema mtoto wake hana hatia yoyote katika mambo yanayoendelea katika mitandao ya kijamii.

“Issue ya Lulu sijui na Majay siwezi zungumzia, kitu ambacho kinaniumiza ni kumwingiza mwanangu kwenye haya mambo, na mtoto wangu anakuwa anajumlishwa katika mambo ambayo hayamuhusu kabisa na hakupaswa kuhusishwa,” alisema Mobeto. Kwa hiyo hakuna mzazi ambae angekubali mwanaye azungumziwe hivyo au aongelewe kwenye mambo yasio mazuri,”

Aliongeza,” Ningekuwa sina mtoto wala nisinge umia lakini kwa sababu kuna mtoto ambaye hana hatia wala hajui kinachoendelea, so sipendi hiki kitu,”

Katika mitandao ya kijamii mashabiki wa Lulu na Hamisa wamekuwa wakitupiana maneno huku chanzo kikidaiwa ni Majay, lakini Hamisa alikataa kuzungumzia chochote kuhusu mpenzi wake huyo wa zamani.

Kama Umepanga Nyumba au Kupangisha Taarifa Hii ikufikie Kutoka Jeshi la Polisi Dar es salaam

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kushirikiana na wenye nyumba kuhakikisha wapangaji katika nyumba wanaingia makubaliano ya mkataba na kuwa na picha zao.

Hatua hiyo imetokana na kuwepo kwa watu wanaofanya uhalifu katika maeneo mbalimbali na kushindwa kupatikana pindi polisi wafanyapo operesheni kutokana na kupanga kwenye nyumba hizo lakini wakati akiondoka hawaagi na wenye nyumba wanakosa kuwa na taarifa za watu katika nyumba zao.

Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishina (CP), Simon Sirro amesema kuwa wenye nyumba ambao watashindwa kufanya mkataba bila picha likitokea tukio dhidi ya mpangaji msalaba utamuangukia mwenye nyumba kuhusika katika uhalifu uliofanywa.

Wakati huohuo Jeshi la Polisi linamshirikia Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), MT 66807 SGT, George Kwisema kwa tuhuma za kukutwa na vipande kumi vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh. milioni 198 vikiwa katika gari yake yenye namba za usajili T.477 AXS aina ya Suzuki Vitara.

Katika tuhuma za vipande vya meno ya tembo wanaoshikiriwa wengine, ni Shafi Muhibu pamoja na Asha Hassan ambao walikutwa katika gari iliyokuwa imebeba meno ya tembo.

Wakati huo huo, Jeshi la Polisi linawashikiria watu watatu kwa tuhuma za kukutwa na sukari mifuko 35 ya Kilogram 50 ambao walikamatwa Chadibwa Mtaa wa Magogoni Kigamboni Mei 31 mwaka huu, ambayo ilikuwa haijalipiwa ushuru na waliokamatwa na tuhuma za sukari ni Said Bakari (25), Mkazi wa Mbagala , Hamadi Selemani pamoja na Bakari Masudi.

Jeshi la Polisi linafanya upelelezi pia wa mtuhumiwa wa aliyewaleta wahamiaji Haramu na kutoweka katika mazingira ya utatanishi akiwa chini ya ulinzi wa Polisi.

Basi Moja Liendalo Haraka Limegongana na Pikipiki Shekilango Dar es Salaam

$
0
0
Ajali zimeendelea kutokea katika barabara za mabasi yaendayo haraka ambazo zimekuwa zikisababishwa na madereva wasiotaka kufuata sheria za barabarani ambapo leo katika mataa ya kuongozea magari Shekilango basi moja liendalo haraka limegongana na pikipiki.

Ajali hiyo ambayo haikusababisha vifo wala majeruhi imetokea majira ya saa sita ambapo kwa mujibu wa mashududa dereva wa boda boda akiwa na abiria mwanamke alikuwa akikatiza kwenye taa hizo akitokea upande wa soko la shekilango akielekea milleniam park huku taa zikiwa zimeruhusu basi hilo kupita na kusababisha kugongana na pikipiki kupinduka.

Askari wa usalama wakiwa katika harakati za kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo akatokea dereva
mwingine wa bodaboda kukatiza katika eneo hilo bila kufuata sheria ambaye nae alikamatwa na kuambatanishwa na waliosababisha ajali hiyo na kupelekwa kwenye vyombo vya dola kwa hatua zaidi.

Mambo 5 Tuliyoyaona Baada ya Rich Mavoko Kusainishwa na WCB

$
0
0

Jana ilikuwa siku kubwa kwa label ya WCB inayomilika na Diamond Platnumz. Kwa mara ya kwanza ilifanikiwa kumsainisha msanii mkubwa anayesifika kwa utunzi na uimbaji wa hali ya juu. Kwa kumsajili Rich Mavoko, WCB ilikuwa kama vile timu ya soka inapomsajili mchezaji maarufu na tena kwa dau kubwa.

Mavoko ameungana na Diamond mwenyewe pamoja na wasanii waliosainishwa awali, Harmonize na Raymond. Pia katika utambulisho wa label hiyo ulioendana sambamba na kumtangaza Mavoko kama msanii wake mpya, Queen Darleen, dada yake Diamond naye alitambulishwa rasmi kama sehemu ya roaster ya wasanii wa Wasafi Records.



Haya ni mambo matano ambayo nimeyabaini kwenye hatua hiyo:

1. NI ISHARA NYINGINE KUWA MUZIKI WETU UMEKUA

Pale tasnia ya muziki inapokuwa na record label za uhakika, ni ishara kuwa muziki umekua sana na unazidi kuwa rasmi. WCB wanaelekea kuanza kufanya mambo tuliyokuwa tukiyasikia kwenye nchi zilizoendelea tu. Nigeria ndipo wanapotupigia bao. Wana utitiri wa label zenye uwezo wa kugharamia mambo mengi kwa msanii na akafanikiwa kutengenezwa na kubwa mkubwa.

Utambulisho wa Mavoko uliandaliwa katika ukubwa ambao unaonesha kuwa WCB ipo serious na biashara ya muziki. Ndiyo maana, Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA, Godfrey Mngereza ameipongeza label hiyo.

“Ni vizuri sana tunapowaona wasanii watanzania wanawekeza katika industry ya muziki, kwa hatua hii inaondoa ile dhana kwamba wanaoweza kuwekeza kwenye muziki ni watu toka nje, kwahiyo ni hatua kubwa sana, ni hatua ya msingi sana ambayo Diamond na timu yake yote wameipiga katika kuonyesha dhahiri kwamba kila kitu kinawezekana,” alisema Mngereza Alhamis hii.

“Huu ni mfano kwamba ameingia hatua nyingine ya kuwa na label. Msanii kuwa na label ni hatua ya juu sana katika industry ya sanaa, kwahiyo kwa vyovyote vile tuweze kumpongeza Diamond, na serikali ipo na inatoa support kwa asilimia mia. Kwa Diamond na mameneja wake, lakini na team nzima ya Diamond, kwamba wanachokifanya, si kwa manufaa yao tu, lakini ni kwa manufaa ya maendeleo ya tasnia nzima ya sanaa na taifa kwa ujumla,” alisisitiza.

2. RICH MAVOKO AMECHUKUA UAMUZI MUHIMU MAISHANI MWAKE


January 29 niliandika makala kuhusu iwapo Rich Mavoko kusainishwa kwenye label ya Wasafi kunaweza kuwa kitu sahihi. Kwa mtazamo wangu, huu ni uamuzi muhimu zaidi ambao Rich Mavoko amewahi kuufanya kwenye maisha yake. Kwa kujiunga na label ya Diamond, hitmaker huyo ni sawa na mmea uliokuwa umeathirika na ukame na kisha kupata matone ya mvua na hivyo kuchipuka zaidi.

Mavoko sasa ana maisha mapya, uhakika zaidi katika muziki kwa kuwa kwenye label ya kwanza kubwa Tanzania inayofanya kazi zake kama label zilizopo kwenye nchi za wenzetu. WCB kupitia Diamond si label yenye wasiwasi wa vitu vidogo tena kama bajeti ya kufanya video nzuri, studio, photoshoot, wapiga picha na vitu vingine ambayo wasanii wengi vinawaumiza kichwa.

Mavoko anarudi tena kwenye chati, kwenye midomo ya watu, mtandaoni na kwenye vyombo vya habari, na muda si mrefu anarejea tena kuwa miongoni mwa wasanii wanaopiga show nyingi zaidi Tanzania. Hilo liko wazi hasa ukiangalia mabadiliko waliyonayo Harmonize na Raymond tangu wawe chini ya label hiyo ambao kwa sasa wana msululu wa show zinazolipa.

Ni kama vile kila anachokigusa Diamond hugeuka kuwa dhahabu. Hakuna shaka tutashuhudia Mavoko akigota vilele ambavyo kama angeamua kujaribu mwenyewe ingekuwa safari ndefu na yenye mitihani mingi.

3. KWA DIAMOND BIASHARA KWANZA, USHINDANI BAADAYE

Unapomuona msanii akichukua vijana wenzake kuwasaidia ilhali akiujua uwezo wao kuwa ni wa kuotea mbali, basi hapo ni wazi kuwa anafikiria biashara zaidi kuliko ushindani. Label ni biashara maarufu sana kwenye muziki – in fact ndicho kiini cha muziki wa Marekani. Kwa wenzetu, ni ndoto kwa msanii kutoka mwenyewe bila kupitia record label na wale waliofanikiwa hivyo ni wa kuwahesababu.

Label nyingi kama Def Jam, Warner Music, Universal Music, Sony Music, Atlantic Records ni makampuni yenye uwekezaji wa mabilioni ya dola za watu ambao hata hawatajwi kwenye vyombo vya habari. Kwahiyo pale ambapo msanii anayeendelea kustruggle kwenye muziki lakini akaamua kuwasaini wasanii wenzake, hahofii tena ushindani. Mawazo ya msanii kama huyu ni ya kiujasiriamali zaidi. Na kwa mkataba wa miaka kumi aliosaini Mavoko WCB, pande zote zitaneemeka na huo ni uwekezaji usio na shaka kabisa.

4. MAVOKO NA DIAMOND WANA CHEMISTRY


Mimi ni mmoja wa watu ambao nimeshangazwa na jinsi Rich Mavoko na Diamond wametengeneza chemistry halisi ndani ya muda mfupi. Sina uhakika, lakini sijawahi kusikia iwapo waliwahi kuwa marafiki huko nyuma. Na nakumbuka kuna wakati kulikuwepona ushindani mkubwa katika ya wawili hawa kiasi ambacho kulizaliwa hadi tension ambayo mara nyingi kwa wasanii wengi zimewahi hata kusababisha uadui.

Na hiyo ndiyo ilikuwa shaka kubwa ya watu wengi tangu tetesi za Mavoko kusainishwa WCB zilipoanza kuvuma. Wengi walikuwa na wasiwasi kuwa fahari huyu ataweza kuwa chini ya fahari mwenzake? Picha na video zinaongea jumbe maelfu kuwa wawili hao wana upendo halisi wao kwa wao na Diamond ni kama mzazi anayejivunia kuwa na Mavoko.

Video aliyoipost Diamond ya sherehe ya kumkaribisha staa huyo WCB ikimuonesha akiimba wimbo Ibaki Story, ni kithibitisho kuwa mastaa hao wana chemistry ya nguvu.

5. MAVOKO ANA FURAHA


Naamini moyo wa Rich Mavoko una furaha kubwa sasa. Hicho ni cha muhimu zaidi kuliko hata matarajio mengine makubwa aliyonayo. Tena, video zinaonesha jinsi alivyofurahia kujiunga na himaya hiyo. Support anayopewa na timu nzima ya WCB sasa ni ishara tosha kuwa yupo kwenye mikono salama.

PICHA: WASAFI CLASSIC INSTAGRAM

Imeandikwa na Fredrick Bundala

Hatuwaogopi Wamisri, Kesho Tutawafunga - Samatta

$
0
0
Samatta amesema, Misri ni timu ngumu na anaamini watakuwa wamejiandaa vizuri kwasababu wanajua mechi ya kesho ndiyo itawapa tiketi ya kuelekea fainali za mataifa ya Afrika mwakani lakini ni lazima watafugwa kwani Stars itakuwa inachezea Uwanja wa nyumbani.

Samatta amesema, hawaangalii kama wananafasi ya kupita au hawana nafasi lakini muhimu ni kuweza kupata ushindi wa aina yoyote haijalishi ni zaidi ya goli tatu au chini ya goli tatu wanachoangalia wao kama timu ni ushindi na kuweza kuwapa raha watanzania.

Samatta amesema, wachezaji wenzake wote wapo vizuri na kila mchezaji mawazo yake ni kuweza kufanya vizuri hapo kesho na wanategemea ushindi na sio sare wala kufungwa kwani watapambana kama timu ya Taifa na sio mchezaji mmoja mmoja.

Samatta amewataka watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa ili kuipa sapoti timu yao na watahakikisha wanawapa watanzania furaha kwa kuweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

Amissi Tambwe Aishauri Yanga

$
0
0
Mshambuliaji wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe ameushauri uongozi wa klabu hiyo kuhakikisha unasajili kiungo mkabaji (namba sita), wa nguvu katika kipindi hiki cha usajili ambaye atakuwa msaada mkubwa kwa timu hiyo.

Tambwe ambaye ndiye mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu akiwa na mabao 21, amesema Yanga inakabiliwa na tatizo kubwa la kiungo mkabaji mwenye uwezo kupambana muda wote wa mchezo.

Alisema hali hiyo ndiyo imekuwa ikiisumbua timu hiyo katika mechi zake za kimataifa jambo ambalo uongozi wa timu hiyo unapaswa kulifanyia kazi katika kipindi hiki cha usajili.

“Tuna viungo wengi wazuri lakini bado tunahitaji kiungo mkabaji wa nguvu ambaye atakuwa anashirikiana vilivyo na mabeki wetu katika safu ya ulinzi.

“Uongozi wetu unatakiwa kuliona hilo na kulifanyia kazi katika kipindi hiki cha usajili kabla ya kuanza kushiriki michuano ya kimataifa ambayo itakuwa na ushindani mkubwa kutokana na aina ya timu tutakazokutana nazo,” alisema Tambwe.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Juni 4, Ikiwemo ya Kitwanga Kamwendea JPM Israel

$
0
0


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Juni 4

Tanzia; Bondia Mohamed Ally Afariki Dunia leo Asubuhi

$
0
0
Muhammad Ali has died aged 74 after a 32-year battle with Parkinson's disease. 
The legendary boxer - widely regarded as the best of all time - died with his family at his side on Friday evening, a day after he was rushed to hospital with difficulty breathing. 

'After a 32-year battle with Parkinson's disease, Muhammad Ali has passed away at the age of 74. The three-time World Heavyweight Champion boxer died this evening,' Ali's spokesman said.
Ali's family said his funeral would be held in his hometown of Louisville, Kentucky, and thanked the public for their outpouring of support. 

Ali had been on life support at a hospital outside Phoenix, Arizona, after he was found 'barely breathing' at his home on Thursday. 

He was taken to hospital with an 'unshakeable cough', a separate source said, with his fatal respiratory problems likely to have been complicated by his Parkinson's disease.

The Greatest was surrounded by his family, who rushed to be at his bedside on Friday after doctors warned his condition was 'rapidly deteriorating', a source said.

It was earlier reported that Ali's family had started making funeral arrangements after doctors warned that he was just hours from death. 

Zari ni Mjamzito tena!!! Mama Nasibu Athibitisha Kwa Maneno haya

$
0
0
Muda si mrefu sana toka Zari na Diamond Platnumz wamepata mtoto wao wa kwanza kwa jina

Kupitia mtandao wa Instagram Mama wa Diamond Platnumz amepost picha ya pamoja akiwa na Diamond Platnumzpamoja na Zari na kuandika "ETI MAMA .K...".


Video: Party iliyofanyika Nyumbani Kwa Diamond Platnumz ya Kumkaribisha Rich Mavoko

$
0
0
June 2 2016 Ndio siku rasmi ambayo Lebel ya WCB ilimtambulisha Rich Mavoko kama msanii wa lebel hiyo, mtu wangu baada ya utambulisho huo uongozi wa WCB uliamua kufanya party ya Kumkaribisha Rich Mavoko pamoja na mke wa Meneja wa Harmonize (Ricardo Momo) kwenye familia hiyo, party ambayo ilifanyika nyumbani kwa Diamond Platnumz

Mambo Mawili Yanayoibana Serikali Katika Mgogoro wa Wanafunzi 7000 Waliotimuliwa UDOM

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Kitilla Mkumbo amesema kuna mambo mawili yanayoibana Serikali katika mgogoro wa wanafunzi waliotimuliwa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Akizungumza jana kwenye kipindi cha ‘Kipima Joto’ kinachorushwa na kituo cha luninga cha ITV, Profesa Mkumbo alisema Serikali haiwezi kukwepa lawama, kwa sababu ndiyo iliyoanzisha utaratibu wa kudahili wanafunzi wa kidato cha nne kupitia mfumo maalumu kabla ya kuanza kusoma shahada ya chuo kikuu.

Pia, alisema Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), haiwezi kuhusika moja kwa moja kwenye udhaifu uliojitokeza katika udahili wa wanafunzi hao, bali Seneti ya Udom inapaswa kuwajibika katika hilo.

Alisema kuna udhaifu wa kiutendaji kwa seneti hiyo yenye mamlaka ya kudahili wanafunzi wenye sifa ambayo iliiacha kazi hiyo  mikononi mwa TCU.

Mkumbo alisema kazi ya TCU ni kuidhinisha majina ya wanafunzi waliokwisha dahiliwa na chuo husika na si kuchagua.

“Chuo chochote ndicho kinachagua wanafunzi wenye sifa wanazozihitaji, inashangaza kuona Udom imefanyiwa kazi hiyo, baraza na seneti wanapaswa  kuwajibika kwanza, TCU haiwezi kukichagulia chuo wanafunzi,” alisema Profesa Mkumbo.

Hata hivyo, alitoa angalizo kwa Serikali kutodharau mfumo huo wa udahili kwa wanafunzi ambao hawakuhitimu Kidato cha Sita kama ilivyoamriwa na Serikali ya Awamu ya Nne, kuwa upo na unatumika duniani kote.

“Ila kama Rais (John) Magufuli hautaki na ameona turudi kwenye mfumo wa zamani ambao mwanafunzi anapaswa kufaulu  kidato cha sita ndiyo ajiunge na chuo kikuu sawa,  lakini atambue kuwa kuna hasara na faida zake, vyuo vingi vinaweza kufungwa,” alisema Mkumbo

Mbali ya mfumo huo, profesa huyo alisema upo mfumo mwingine wa udahili kwa mtu yeyote mwenye umahili katika taaluma yake kusoma shahada kwa kuzingatia vigezo maalumu vilivyowekwa.

“Ila hakuna jinsi, nadhani  TCU wamemsikia Rais kuwa hataki njia za mkato tena.”

Mei 29, Udom iliwasimamisha masomo zaidi ya wanafunzi 7,000 wa kozi maalumu ya ualimu wa sayansi kwa ngazi ya stashahada na kuwataka waondoke chuoni mara moja.

Amri hiyo iliyotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, ilisema Serikali imeamua warejee kwao na wataelezwa mustakabali wao mapema iwezekanavyo.

Hata hivyo, Rais John Magufuli juzi alisema baadhi yao walikuwa vilaza, hivyo wajitafutie mahali pa kwenda huku wenye ufaulu wa daraja la kwanza na pili aliahaidi kuwa wataandaliwa utaratibu.

Pigania Ndoa Yako Si Michepuko ya Mumeo..

$
0
0
NIMEIKUTA MAHALI NIKAONA NI VIZURI KU-SHARE

Kuna dada mmoja nikikuwa namfahamu miaka mingi sana. Kama miama 15. Kipindi hicho tukiwa ni wasichana wa miaka 25. Dada huyo ghafla akawa na mahusiano na mume wa dada yangu. Nilimchukia sana. Dada yangu alimchukia sana. Wote tulimchukia. Alikuwa mlevi. Malaya na anayependa kuvaa uchi. Hakuwa anajijali hata kidogo.
Mimi na Dada yangu tulikuwa tunatamani hata afe ama akatike miguu kwa namna alivyokuwa malaya na mshenzi.

Miaka ikapita. Kila ninapokutana na dada yangu haishi kunikumbusha Dativa. Kila siku tulikuwa tunamuongelea. Na kutamani tusikie hata kuna msiba kwao na amefariki dunia.

Baada ya miaka mitano kupita. Mimi nikiwa nimeahamaliza masomo yangu. Na sasa na niko kazini nafanya kazi yangu nzuri tu. Kijana mmoja akaniambia ananipenda na anataka kunioa. Miaka yote hiyo sikuwa na mahusiano kwani nilijua na mimi kina Dativa wataharibu ndoa yangu. So sikupenda ndoa kabisa.
Hivyo kijana huyo nikamkataa. Ni kijana kama wa 10 hivi kumkataa.
Siku moja nikampigia dada yangu simu. Akanieleza mambo hayo kwamba hana raha na ndoa yake kwani anajua Dativa bado wana mahusiano na mumewe. Japo hawaoni ila anajua wanafanya siri. Dada yangu alikonda. Ni mwaka wa 7 sasa Dativa hajamtoka akilini.
Nilikuwa naumia pia.
Maisha yakasonga.

Nilipata safari ya mwenda mkoani Arusha.Jumapili Moja nikasema ngoja niende kanisani kuabudu Mungu. Ni kanisa la karibu tu lakini sio kanisa la imani yangu.
Siku hiyo nilipata msukumo hasa. Tena baada ya kujua muimbaji maarufu wa nyimbo za injili yuko hapo.Nilivaa vyema. Kisha nikajipeleka kanisani.
Ibada ilianza.
Ilikuwa nzuri sana.
Mh...Baada ya muda kidogo nikasikia mtangazaji akisema Familia ya Bwana na Bibi Juventus inataka kutoa shukrani.
Bwana Juventus na mkewe na watoto wao wawili. Wa kike mwenye 4 yrs na wa kiume mwenye 2 yrs.
Walisimama mbele.
Mwanaume alikuwa kavalia suti nzuri sana na kapendeza hasa. Mrefu. Bonge la handsome.
Watoto nao walipendeza sana. Walivalia vyema hasa.

Kisha huyo mwanamke alionekana mrembo. Aliyevalia nguo za thamani na kupendeza pia.
Nilimtazama sana mwanamke huyo. Ni kama niliyekuwa namfahamu. Nilijiuliza je ni mtangazaji ama nimemuona wapi?Sura yake ilinipotea kidogo. Pengine ni kwa namna alivuopendeza zaidi.
Nilipuuza. Ila ni familia iliyonivutia sana.
Kisha Mume akamshika mkewe bega na kumpa kipaza sauti na kumwambia ashukuru Mungu.
Mwanamke yule alianza kwakusema...

mimi na mume wangu na watoto wetu wapendwa. Tunazo kila sababu za kumahukuru Mungu kwa namna anavyitutunza na kutupigania kila mara. Na leo tuko mbele zenu kutoa shukrani zetu mbele ya Mungu na mbele ya kanisa kwa maombi yenu pia.
Mungu ametubariki na mwezi huu tarehe 10 tutasafiri kwa ajili ya huduma nje ya nchi. Maombi yenu ni ya Muhimu sana.

Mimi Dativa na Juventus tunawapenda sana. Mungu awabariki.
Moyo wangu ulifanya paaaaa... ulinipasuka paaaaaa...
Huyu ni Dativa?yule kahaba.. malaya... niliyekuwa natamani afe hata kesho?Leo ana ndoa na watoto na maisha mazuri?Nimebaki nakataa ndoa kwa sabau yake... kumbe yeye anasonga mbele?
Dada yangu naye analia kumbe Davuta ni wa viwango vingine?.Nilichukia... nikajikuta naumia zaidi na ninawaza kwamba Mungu hayuko fair.

Niliwaza mpaka watu wakanisikia. Mama mmoja akaniambia mbona unaongea mwenyewe?Nimasema kwanguvu..Mungu hayuko fair. Ana upendeleo.
Huyo mama akanimbia kwanini?
Nikamwambia Davita alikuwa malaya sana. Na kaitesa sana ndoa ya dada yangu.
Yule mama alinitazama na kutabasamu kisha akasema...
SIKIA MWANANGU... HUJUI KAMA MAKAHABA WATATUTANGULIA KWENYE UFALME WA MUNGU?

Mh.. akili ilinirudi.
Kisha nikatoka nje na kuiacha ibada ikiendelea. Na kumpigia dada yangu simu na kumwambia...
Dada nimemuona Davita. Ni mwanamke wa viwango vingime. Sio yule kahaba tena. Ni ana mume na watoto na ameokoka.
Hembu acha kumuwazia mabaya kabisa. Mungu amempendelea.

Kuanzia hapo nikajifunza jambo.
Hatupaswi kuwawazia watu mabaya wala kuwaombea mabaya.
Hembu na wewe nikusaidie leo.
Acha kuuwaza mchepuko wa mumeo. Waza maisha yako..songa mbele. Usisimame kuwaza mchepuko ambao saa yoyote utatubu dhambi mbele za Mungu na Mungu wetu ni Mungu wa Kusamehe. Badala yake kaza buti katika maisha yako Mungu akuinue.
......The End..........

Lulu DivA na Gigy Money Wapeana Makavu Live

$
0
0
WAUZA nyago kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ hivi karibuni wamechimbana mikwara na kupakana shombo kila mmoja akimuona mwenzake kituko kutokana na maneno anayoyasikia juu yake.

Ishu nzima ilianza baada ya mwandishi wetu kupata ubuyu kutoka kwa mmoja wa watu wa karibu wa Lulu Diva kuwa anamhofia Gigy Money kumfunika katika gemu wanalofanya.

Baada ya mwandishi wetu kupewa ubuyu huo alimwendea hewani Lulu, aliposomewa  madai hayo mwanadada huyo alisema;

“Nani kakwambia hivyo? Siwezi kumhofia Gigy kwenye kile ninachokifanya, hana kitu chochote cha kunifanya nimhofie maana ni mtu wa kawaida sana kwangu.”

Kwa upande wa Gigy alipotafutwa alisema; “Siwezi kupigizana kelele na huyo demu, anatafuta kiki kupitia kwangu lakini hawezi kuipata hata kwa dawa, haniwezi kwa kila kitu, akajipange sana na akae akijua simuogopi.”

Global Publishers

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Ya Nchi , Hamad Yussuf Masauni Alalamikiwa na Wabunge Kwa Kutoa Majibu ya Dharau na Kiburi Kwa Wabunge

$
0
0
SIKU chache baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga kutokana na ulevi, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Hamad Yussuf Masauni, ameshtakiwa kwa uongozi wa Bunge akidaiwa kutoa majibu ya dharau bungeni.

Wakati wizara hiyo bado haijapata Waziri tangu 'kutumbuliwa' kwa Kitwanga Mei 20, mwaka huu, katika Kikao cha 36 cha Mkutano wa Tatu wa Bunge la 11 mjini hapa, jana Mbunge wa Nkasi (CCM), Ally Keissy alisimama na kuomba mwongozo wa Spika akidai Mhandisi Masauni amekuwa akitoa majibu ya dharau kwa wabunge.
 
Keissy alidai Naibu Waziri huyo amekuwa akitoa majibu ya kejeli na kiburi na kwamba wabunge wengi hawaridhishwi na majibu yake.
 
"Nasimama kwa Kanuni ya 68(7), naomba mwongozo wako kuhusu majibu ya nyongeza aliyojibu Naibu Waziri, na tangu jana (juzi), amezoea kujibu kwamba wabunge watumie fedha za mfuko wa Jimbo kukarabati majengo ya polisi," Keissy alisema.
 
"Ndugu Mheshimiwa Naibu Spika, majengo ya Karando na Kabwe (jimbo la Nkasi) yamechakaa hata mfuko wa jimbo... nadhani Mheshimiwa Waziri hajui tunapata shilingi ngapi za mfuko wa jimbo kutosha kukarabati hayo majengo.
 
"Hayo majibu yanaridhisha? Anajibu kwa jeuri na kiburi. Kusema kweli wabunge haturidhishwi na majibu ya Naibu Waziri. Sikubalini na majibu ya aina hii.
 
"Katika majibu ya msingi ya swali langu, wamesema serikali itakarabati majengo ya Kabwe, lakini anasema baadaye (kwenye swali la nyongeza) Mbunge akarabati majengo ya Kabwe, si dharau hii? Anataka kunichionganisha mimi na wananchi. Hili jibu sijaridhika nalo. Mnanijibu nikakarabati mimi. Sina uwezo."
 
Baada ya maelezo hayo ya Keissy, Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson aliyekuwa anaongoza kikao hicho, alisema atatoa mwongozo wake baada ya kupitia taarifa za Bunge (Hansard) kuhusu suala hilo.
 
"Waheshimiwa wabunge, ili nijue swali liliulizwa kwa namna gani na Mheshimiwa Naibu Waziri amelijibu kwa namna gani, mpaka nipitie taarifa za Bunge, yaani Hansard," alisema Naibu Spika.
 
"Kwa hiyo, mwongozo huo nitautoa baada ya kupitia taarifa rasmi za Bunge kwamba swali liliulizwa vipi na majibu yametoka namna gani."
 
Ikiwa Kiti cha Spika kitabaini majibu ya Naibu Waziri hayakusadifu swali la Keissy, kitaagiza swali hilo lirudiwe kujibiwa kwenye kipindi cha maswali na majibu bungeni.
 
Uteuzi wa Kitwanga ulitenguliwa na Rais Magufuli ikiwa ni muda mfupi baada ya Mbunge huyo wa Misungwi (CCM) kuingia bungeni akiwa amelewa na kijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Devotha Minja lililoelekezwa kwenye Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 
Kiti cha Spika kiliagiza swali hilo lirudiwe kujibiwa katika kipindi cha maswali na majibu bungeni Mei 23, baada ya Kitwanga kutoa majibu ambayo hayakuridhisha.

Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 5, Ikiwemo ya Ripoti ya Watoto wa Vigogo BOT Mezani Kwa Magufuli

$
0
0


Soma Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya June 5, Ikiwemo ya Ripoti ya Watoto wa Vigogo BOT Mezani Kwa Magufuli

CHADEMA Kuishitaki Serikali Kwa Wananchi

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kuanza ziara ya kuishtaki Serikali kwa wananchi kuhusiana na utumbuaji majipu usiofuata maadili ya kazi na kutoonyeshwa kwa matangazo ya moja kwa moja ya televisheni ya vikao vya Bunge.

Mratibu wa ziara hiyo, Singo Benson alisema ziara itaanza Juni 7 katika Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga na kuendelea mikoa mingine, lengo ni kuelimisha wananchi juu ya ubakwaji wa demokrasia.

“Wananchi wananyimwa haki ya msingi ya kutoona matangazo ya Bunge moja kwa moja na hakuna sababu ya msingi iliyotolewa, hivyo lazima tuwaelimishe na tuwatetee wananchi haki zao,” alisema Benson.

Aliongeza kuwa katika utumbuaji majipu unaofanyika, umekuwa kwa asilimia kubwa ukilenga majipu madogo (viongozi wa chini) na kuacha viongozi wakubwa mafisadi bila kuchukuliwa hatua yoyote.

Benson alitoa mfano wa ubakwaji wa demokrasia akisema ni kitendo cha Serikali kuingilia mihimili mingine, Bunge na Mahakama, ambapo kwa Bunge Serikali ina daiwa kuingilia uchaguzi wa mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC) ambaye anatakiwa kutoka kambi ya upinzani.

Alisema ziara hiyo itakayojumuisha Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji itakuwa na awamu nne nchi nzima huku wabunge wote na wajumbe wakuu wa chama watashiriki, akiwamo aliyekuwa mgombea urais 2015, Edward Lowassa.

Awamu ya kwanza itakayochukua siku 14 itaendelea kwa kugawana maeneo na kundi moja la viongozi wa Chadema litaenda maeneo ya Chato, Katoro, Busanda, Biharamulo, Muleba, Bukoba Mjini, Karagwe, Ngara na Geita; Kundi la pili Shinyanga mjini, Meatu, Maswa, Bariadi, Lamadi, Musoma Mjini, Bunda, Tarime na kuhitimisha Mwanza Mjini.

Benson ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uratibu na Mafunzo wa Chadema, alieleza kuwa awamu ya pili itahusisha nyanda za juu kusini na kati, awamu ya tatu itakuwa mikoa ya kaskazini na kusini na kuhitimisha jijini Dar es Salaam.

“Ziara hizi zinawakaribishwa wabunge na wanasiasa wa vyama vyote wenye lengo la kutetea haki za wananchi kwa viongozi waliowachagua,” alieleza Benson.

Shilole na Nuh Mziwanda Wakutana Tena Zamu hii Hawajapigana ila Hiki Kikubwa ndo Kimetokea.

$
0
0
Kwa sasa Shilole na Nuh mziwanda washatemana na kila mtu ana mpenzi wake, huku Nuh akiwa kattutambulisha mrembo mpya na kukiwa na skendo kua Shilole katemana na Nedy. Basi kama mtakumbuka vizuri siku chache baada ya Shishi na Nuh kutemana walikutana katika Interview Clouds Tv na mwisho wa siku waliishia kupigana.

Imepita miezi mingi sasa wawili hawa hawajakutana tena mpaka juzi hapa walipokutana tena Clouds Fm katika kipindi cha XXL. Kizuri ni zamu hii hawajagombana ila kumetokea jambo moja lakushangaza zaidi pale walipokua wakiulizwa maswali na BDozen. Hebu cheki video hii kisha niambie ni nani muungwana zaidi kati ya Shilole na Nuh??

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yawashukia Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU)

$
0
0
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa ufafanuzi kuhusu ripoti ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwaka jana, iliyowasilishwa na Ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi wa Umoja wa Ulaya (EU).

NEC imesisitiza kwamba ripoti hiyo imebainisha mapungufu ambayo hayapo kwenye sheria na taratibu, zinazoiongoza tume hiyo.

Miongoni mwa mapungufu waliyoyatoa waangalizi hao ni Suala la Uchaguzi wa Zanzibar, Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 na haki ya wagombea binafsi kugombea nafasi katika uchaguzi wowote wa Tanzania Bara na Zanzibar, mgawanyo wa majimbo na uwazi wa kuhesabu kura.

Akitoa ufafanuzi huo, Mkurugenzi wa NEC, Ramadhan Kailima alisema kuwa kwa mujibu wa sheria, waliwapa nafasi hiyo waangalizi wa ndani na nje kuangalia uchaguzi wa Tanzania Bara , kama unaenda kulingana na Katiba, sheria na taratibu za uchaguzi huo.

Alisema kuwa katika ripoti hiyo, waangalizi hao wamezungumzia uchaguzi wa Zanzibar, ambao NEC hawahusiki nao na kwamba wamefanya makosa, kwa kuwa wao walikuwa waangalizi wa uchaguzi wa Tanzania Bara na sio Zanzibar.

‘’Waangalizi wowote wa uchaguzi wanapoomba kibali kuangalia uchaguzi, wanatakiwa kufuata taratibu kwa kutambua kwamba kuna NEC na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC). Sisi tulitoa kibali kwa waangalizi hawa kuangalia uchaguzi wetu na sio wa Zanzibar,’’ alisema.

Aliongeza kuwa, ‘’hawakupaswa kuingiza katika ripoti yao masuala ya uchaguzi wa Zanzibar ulivyokuwa, badala yake wangeeleza kama NEC hatukufuata sheria na taratibu kwenye uchaguzi huu wa Tanzania Bara.”

Alisema pia kuwa waangalizi walitakiwa kuangalia uchaguzi huo na sio kupendekeza kwamba uchaguzi ulitakiwa kuwa vipi.

Kuhusu suala la mgombea binafsi, alisema Katiba iliyopo sasa haijaruhusu, hivyo wasingeweza kuweka wagombea hao, kwani Katiba ingewabana.

Kailima alisema kuwa endapo Katiba Inayopendekezwa ingepitishwa, waangalizi hao wangeweza kuhoji kwa nini hakukuwepo na mgombea binafsi, kwani ndiyo inaeleza kuhusu mambo hayo.

Akizungumzia mgawanyo wa majimbo, Kailima alisema kuwa kila halmashauri ya mji na wilaya ni jimbo na kwamba hawapaswi kulinganisha kati ya Halmashauri ya Temeke yenye watu 419,612 na jimbo la Madaba lenye watu 27,502, kuwa mgawanyo wake haukufuata uwiano.

Alisema kuwa mgawanyo wa majimbo, huzingatia mambo mengi, ikiwemo jiografia ya eneo lenyewe. Alieleza pia kuwa NEC haijawanyima haki Wazanzibari kwa kutoongeza idadi ya majimbo, kwa kuwa Bunge ambalo lilitakiwa kujadili, lilikuwa limekamilisha kazi yake.

Alisema kwamba ZEC yenyewe ilichelewa kutangaza mabadiliko hayo ya majimbo kutoka 50 hadi 54.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kwa mara ya kwanza Tanzania matokeo ya uchaguzi wa Madiwani na Wabunge yalikuwa yanabandikwa kwenye vituo vya kupigia kura pamoja na matokeo ya awali ya Rais.

Alisisitiza kuwa matokeo yote, yalikuwa yanasainiwa na wawakilishi kutoka vyama mbalimbali vya siasa na kutangazwa kwa wananchi.

Aidha, alisema kuwa hawakuweza kutangaza wabunge wa viti maalumu kabla ya uchaguzi, kwani kisheria wanachagua wagombea hao baada ya kujua idadi ya kura ya asilimia tano zilizopata chama, hivyo wasingeweza kutangaza kabla ya uchaguzi.

Hata hivyo, alisema kuwa Tume hiyo imepokea mapendekezo yao na itayafanyia kazi ikiwemo kuwa na watumishi kwa ngazi zote. Kailima alisema kuwa hali hiyo, itawasaidia kujua namna ya kuwaadhibu watumishi ambao watakiuka utaratibu wa NEC.

‘’Pia tutaongeza muda wa daftari la kupiga kura kuhakikisha kwamba kwa mwaka linakuwepo mara mbili ili wapiga kura wote waangalie. Lakini suala la Sheria ya Makosa ya Mtandao wanatakiwa kulipeleka kwa wahusika na mengine kwa serikali kwani sisi kama NEC hatuhusiki nayo,’’ alisema.

Video : Nay Wa Mitego Kujizawadia Gari Hili la zaidi ya Milioni 170 Katika Siku yake ya Kuzaliwa

$
0
0
Katika kusherehekea birthday yake mwaka jana, msanii Nay Wa Mitego alihamia katika nyumba yake mpya ya Kimara huku akijizawadia gari mpyaaaa. Habari hiyo ilikua gumzo sana magazetini na mitandaoni kwani nyumba hiyo ilikua ya kisasa kabisa.


Tarehe 9 mwezi huu Nay Wa Mitego atasherehekea siku yake ya kuzaliwa na moja kati ya maswali yaliyokua yakimuumiza zaidi ni zawadi gani ajipatie kati ya kujinunulia gari au kuhamia katika nyumba yake kubwa ya ghorofa ambayo haijaisha vizuri???

Na baada ya kujiuliza sana msanii huyo ameamua kujizawadia gari aina ya Range Rover Vogue ambayo kwa maelezo yake anasema ni moja ya gari alizokua akitamani kumiliki. Lakini Nay kaunguka kua anaogopa kutangaza gari hiyo kwa sababu anamwogopa kiongozi huyu wa Serikali. Unataka kumjua ni nani??? Basi cheki video hii hapa chini Nay akifunguka...
 
Viewing all 104789 articles
Browse latest View live




Latest Images