Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live

MTANGAZAJI MAARUFU GODWIN GONDWE KAHAMIA CLOUDS FM/TV ?

0
0
Nimekutana na Picha Mbali mbali za Mtangazaji Maarufu wa Redio One akiwa amepiga na watangazaji wa Clouds Fm Wakiwa Wanatoka Mapumziko/Semina Arusha ambapo walikuwa huko kwa Takribani Week moja...Anaye jua atujuze kama ninachoona ni sahihi......ama wamekutana tu uwanja wa ndege na kupiga picha nae....

MASHOGA WAZIDI KUONGEZEKA BONGO DSM....NINI HASA SABABU... AU WATEJA WAMEKUWA WENGI??

0
0
Nimepita pita huko mitaani hasa Kinondoni, kwenye mahotel ,ma bar na kumbi za starehe, Nimeshangaa sana kuona wakaka poa kibao, tena wamejiremba kama wadada vile, nao wakijiuza kama machangudoa, nini hasa tatizo ?? 

embu toeni comment zenu hapa na mwono wako juu ya swala hili labda tunaweza pata wazo jipya kuhusu hawa watu!!

HUU NDO UFUSKA WA MASTAA BONGO YANI HUWEZI AMINI KAMA WAO NDO WANAFANYA

0
0
Husna Idd 'Sajent' naye akionyesha machejo yake.



NI laana! Baadhi ya mastaa wamenaswa laivu wakifanya vitendo vilivyotafsiriwa kuwa vya kifuska, Tukio hilo lilijiri kwenye Ukumbi wa Letasi Lounge uliopo maeneo ya Victoria, Dar wikiendi iliyopita ambapo kulikuwa na Kibao Kata cha mtoto wa mjini, Rose Alphonce Nungu ‘Muna Love’.

"RAIS KIKWETE ALIKUWA SAHIHI HAKUKOSEA" KUNDI LA TANZANIA KWANZA

0
0
KITENDO cha baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, kukosoa hatua ya Rais Jakaya Kikwete kutoa maoni yake kuhusu rasimu ya Katiba, kimekosolewa.

Pia, imesisitizwa kuwa hakukosea kufanya hivyo na kwamba hotuba yake, haikuvuruga wala kuingilia mchakato ulio bungeni.

Kundi la Wajumbe wa Bunge Maalumu, linalojipambanua kama Tanzania Kwanza, limesema Rais alichofanya kama kiongozi wa nchi mwenye hekima na busara na uchungu kwa nchi yake ni kueleza faida na hasara ya mifumo ya serikali, iliyowasilishwa kwenye rasimu ya Katiba.

Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana, wajumbe wa kundi hilo linaloongozwa na Said Nkumba na Dk Emmanuel Nchimbi, walisema kitendo cha Rais kuchambua rasimu, si kumdhalilisha Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba na wajumbe wake.

Wajumbe wanaounda kundi hilo wako 400 na waliozungumza jana na waandishi wa habari jana ni Nkumba, Nchimbi, Evod Mmanda, Seleman Jaffo, Mahmoud Thabit Kombo, Asha Mtwangi, Amon Mpanji na Waride Jabu.

Akisoma tamko la wajumbe hao, Said Nkumba alisema Rais hakubadilisha sheria ya mabadiliko ya Katiba, hakupiga kura kwenye vifungu vya Katiba, bali alieleza faida na hasara ya mifumo ya serikali, iliyowasilishwa kwenye rasimu ya Katiba na kuachia wajumbe kazi yao.

Nkumba alisema Rais Kikwete kawapa wajumbe moyo na kuhimiza wamalize kazi haraka na waifanye kwa weledi huku wakiweka maslahi ya taifa mbele.

“Hata pale alipotoa maoni yake kuhusu vifungu vya rasimu hiyo, alisisitiza kuwa uamuzi wa mwisho ni wetu sisi wajumbe wa Bunge hili.”

Katika hotuba yake, Rais alisema msingi wa kutolewa kwa rasimu ni kuwezesha wananchi waichambue, waikosoe, wairekebishe, waiboreshe na hata ikibidi waibadilishe na mwisho wapige kura kwa pamoja.

Rais Kikwete alisema rasimu hiyo haikupelekwa bungeni kama Msahafu wala Biblia na ndiyo maana zimewekwa hatua mbili baada ya kazi ya Tume kukamilika.

Kundi hilo la wajumbe, limesema Rais akiwa Mkuu wa Nchi, pia ana nafasi yake katika mchakato wa Katiba “Sisi wana Tanzania Kwanza tunashukuru kwamba Rais alitutabanaisha kuhusu maeneo muhimu ya kuzingatia ambayo Tume haikuyaainisha kwa upana wake ikiwemo mipaka ya nchi yetu.”

Alisema pamoja na kazi nzuri, iliyofanywa na Tume, rasimu hiyo inaweza kubadilishwa na kufanya hivyo siyo kuwadhalilisha wajumbe wa Tume hiyo.

Mwenyekiti huyo alisema wajumbe watimize wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kwa kuzingatia matarajio ya Watanzania.

Umoja huo ulitaka watu ambao hawakufurahishwa na hotuba ya Rais, waondoe hamaki, watulie na washirikiane kufanya kazi ya kuandika Katiba mpya.

Nkumba alisihi Watanzania kutoruhusu watu wachache, kuweka Bunge Maalumu rehani kwa malengo ya kutengeneza mtaji wa kisiasa.

“Tunataka Watanzania wawaone na kuwahukumu wale watakaotaka kuvuruga au kukwamisha mchakato adhimu wa kupata Katiba mpya kisa tu Rais kaenda kulihutubia Bunge hilo,” alisisitiza.

Juzi viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), walikutana na kushutumu kile walichodai hatua ya Rais kuhutubia Bunge hilo na kutoa maoni yake kwa kuichambua rasimu wakati yeye siyo mjumbe wa Bunge hilo.

Walisema walikerwa na kitendo hicho, wakidai kinaonesha wazi kwamba CCM haina utashi wa kuandika Katiba kwa maridhiano, bali kwa kutumia ubabe ukiwemo wa kuvuruga Katiba.

MWANDISHI UINGEREZA AIBUA MAPYA MENO YA TEMBO TANZANIA.

0
0
Licha ya Rais Jakaya Kikwete kutoa ahadi ya kuteketeza maelfu ya meno ya tembo yaliyo kwenye ghala la Serikali, imeelezwa kuwa uwezekano huo ni mdogo.

Mwandishi wa gazeti la Daily Mail la Uingereza, Martin Fletcher ameeleza kushtushwa na hali ya ulinzi kwenye ghala hilo lililosheheni meno 34,000 ya tembo ambayo kwa biashara ya magendo nchini China yanagharimu Pauni 150 milioni za Kiingereza (Sh403.5 bilioni)

Fletcher, ambaye aliandika habari ya kuhusika kwa wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa wa Tanzania katika biashara haramu ya meno hayo kiasi cha kuifanya nchi kuwa muuzaji mkuu wa nyara hizo, aliandika hayo kwenye taarifa kuhusu ziara yake nchini iliyochapishwa na gazeti hilo jana.

Habari ya awali ilitikisa ulimwengu ambao unapambana kulinda viumbe walio hatarini kutoweka ikiwatuhumu wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa nchini kuhusika, huku Serikali ikishindwa kuwadhibiti.

Habari hiyo iliifanya Serikali ya Tanzania kufungua milango kwa vyombo vya habari vya nje kuja nchini kupata habari sahihi kuhusu tatizo hilo, akiwamo Fletcher wa Daily Mail.

Katika ziara yake, Fletcher alipata nafasi ya kutembelea ghala la nyara hizo, kuzungumza na maofisa wanyama pori pamoja na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.

“Nyalandu pia aliweka bayana kuwa uteketezaji wa shehena ya Tanzania ni kitu ambacho kiko mbali na uhalisia, licha ya ahadi ya Kikwete jijini London,” Fletcher alimkariri Nyalandu kwenye habari hiyo ambayo imeambatana na picha alizozielezea kuwa za kushtua za ghala hilo, lenye idadi kubwa ya meno ya tembo kuliko maghala yote duniani.

“Alisema Rais alikuwa na nia ya kuteketeza (shehena hiyo), lakini Tanzania ilitaka ilipwe takriban Pauni 30 milioni za Uingereza kutoka Jumuiya ya Kimataifa kwa ajili ya Mfuko wa Hifadhi ya Tembo.”

Hata hivyo mwandishi huyo anaripoti kuwa; “Wahisani ambao wangeweza kutoa fedha hizo, walikejeli kiwango hicho wakisema hakina uhalisia.”

Alipoulizwa kuhusu kauli hiyo jana, Nyalandu alisema baadhi ya mambo kwenye habari ya mwandishi huyo yamekuzwa, lakini alisema uamuzi wa kuteketeza nyara hizo haujafikiwa.

Alisema Serikali ilichofanya hadi sasa ni kupiga marufuku biashara zote za meno ya tembo, hivyo haitauza yaliyopo na haitaomba kibali tena cha kufanya biashara hiyo na kwamba kinachoendelea sasa ni mazungumzo ya namna ya kushughulika na shehena iliyopo.

“Meno mengine yaliyopo ni ya kihistoria. Ni marefu kuliko mengine na tembo wa aina hii hawapo tena, hivyo kuwa nayo pia ni kitu kizuri. Haya meno ni mali ya Watanzania wote, uamuzi wa kuyateketeza lazima uchukuliwe kwa busara,” alisema.
Kwa mujibu wa Fletcher meno mengine yana urefu wa futi 7, uzito wa tani 125 na moja linaweza kubebwa na watu kuanzia watatu, huku jino fupi likiwa na uzito wa kilo 0.4500 na kwa mujibu wa jangili aliyekiri kuua tembo 30 kwa siku, jino hilo dogo liling’olewa kutoka kwa tembo mtoto.

Mara tatu katika kipindi cha miaka minane, Tanzania imeomba bila mafanikio kibali cha kuuza shehena yake kutoka katika nchi 180 zilizosaini makubaliano ya kudhibiti biashara ya kimataifa ya viumbe walio hatarini kutoweka, Cites, licha ya ushahidi mkubwa kuwa kitendo cha kuuza mara moja tu, kitazidisha tamaa ya China kupata meno hayo.

Akizungumzia ziara yake nchini, mwandishi huyo anaelezea udhaifu katika ulinzi wa ghala hilo lililo nyuma ya jengo la Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam.

“Ghala hilo niligundua siyo kama ngome (yenye ulinzi mkali). Lina milango ya chuma ya kusukuma ikiwa na kufuli nzito tano ambazo funguo zake zimegawanywa kwa maboharia wawili, lakini milango ilifunguliwa yote nilipofika,” makala hiyo inaeleza. “Kila jino limewekwa alama na namba na ghala ina kamera za ulinzi wa ndani, lakini sikuona mlinzi mwenye silaha nje.”

Mwandishi huyo anaeleza kuwa habari yake ya kwanza iliyohoji kama mtoto wa Mfalme wa Wales na Waziri Mkuu wanaweza kushikana mkono na Rais Kikwete wakati alipotembelea Uingereza, ilizua kizaazaaa kiasi cha Rais Kikwete kuitisha kikao na maofisa waandamizi wa Maliasili na kutoa maelekezo kuwa wafanye kazi.

Mwandishi huyo alitembelea maghala ya meno ya tembo, Hifadhi ya Selous ambayo mwaka 2006 ilikuwa na tembo 70,000 lakini hadi sasa wamesalia 13,000 tu. Baadhi ya meno yalichukuliwa kutoka tembo waliokufa na mengi kukamatwa kutoka kwa majangili na hayawezi kuuzwa kwa sababu ya biashara hiyo kuzuiwa duniani.


NKAMIA "NTAYAFUNGIA NA KUFUTA MAGAZETI

0
0
VITISHO vya watendaji wa serikali kwa vyombo vya habari vimezidi kushika kasi, safari hii Naibu Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Juma Nkamia, akitishia kuvifungia au kuvifuta.

Nkamia amebainisha kuwa magazeti yanayowachafua watu, serikali na kuhatarisha usalama wa nchi yatakumbana na kifungo.

Itakumbukwa mwaka jana serikali ililifungia gazeti la Mtanzania kwa miezi mitatu na Mwananchi kwa wiki mbili, kwa madai ya kuandika habari za kichochezi.

Nkamia, alitoa vitisho hivyo  jana jijini hapa  kwenye tamasha la vijana lililoandaliwa na Taasisi ya Voice of Youth (VOYC) lililokuwa likijadili masuala mbalimbali yahusuyo vijana.

Miongoni mwa mambo yaliyokuwa yakijadiliwa ni ujira, uzalendo, ujasiriamali na ajira,
Nkamia alisema hatakubali siku moja asutwe kwa kutotimiza wajibu wake katika wizara anayoisimamia, kwa kuwaachia waandishi wasiofuata maadili ya taaluma yao.

“Mimi sitaki kufanya kazi na waaandishi wa habari makanjanja, ambao si makini na wanaofanya kazi kwa masilahi ya kundi fulani la watu.

“Tutakifuta, kukifungia chombo chochote cha habari pamoja na waandishi wake wanaokwenda kinyume cha maadili ya uandishi wa habari, sitaruhusu wanaoendekeza kuwachafua wengine, umbea,” alisema.

Alisema amefanya kazi hiyo kwa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo kabla ya kuingia kwenye siasa ambako sasa anasimamia wizara inayoshughulika na waandishi wa habari.

Nkamia pia alitumia fursa hiyo kuwasihi vijana waache kushiriki kwenye maandamano yanayoitishwa na vyama vya siasa alivyoviita havina malengo mema kwa taifa.

Alibainisha kuwa vijana hawawezi kupatiwa fedha kama hawafanyi kazi yoyote, kwani hata mataifa yaliyoendelea ambayo ni Marekani na Uingereza hawafanyi hivyo.

Hata hivyo katika mkutano huo, viongozi wa halmashauri na mkoa walikacha kuhudhuria na hawakutuma wawakilishi katika tamasha hilo licha ya kualikwa.

Kukacha kwao huko kulisababisha gumzo kubwa na Afisa Tarafa ya Nyamagana, Maximilian Kailanga, alibeba jukumu la kumkaribisha Nkamia.

KUAMBIANA: KIPIGO NILICHOWAPA WEMA SEPETU NA AUNT KIMEWAPA ADABU

0
0
Stori: Imelda Mtema

‘DAIREKTA’ na muigizaji wa filamu Bongo, Adamu Phillip Kuambiana amefunguka kuwa kitendo cha kuwatia makofi waigizaji Wema Spetu na Aunt Ezekiel kilikuwa cha kiungwana sababu amewafundisha.

Akipiga stori na paparazi wetu, Kuambiana alisema bila kuwa mkali wakati mwingine mambo huwa hayaendi kwenye uigizaji hivyo anapotembeza kichapo kidogo, mambo yanakwenda katika mstari.

“Kipigo kinasaidia, watoto wa kike hawa bila kuwatishia wanafanya wanavyotaka na ukiwaruhusu unaweza kuharibu kazi,  lakini nashukuru wamenielewa, tunapiga kazi,” alisema Kuambiana.
GPL

CHRIS BROWN AZIDI KUCHANGANYIKIWA HALI WALA HALALI HUKO JELA

0
0
Chris Brown baada ya kuvunja sheria za rehab alifukuzwa na baadae kukamatwa, hivi sasa amewekwa jela kwa muda wa mwezi mmoja.
Mtandao mmoja wa huko Marekani umeripoti kwamba Chris Brown yupo kwenye hali mbaya ndani ya gereza hilo kiasi kwamba hali chakula,usiku halali,anaongea peke yake na maisha ya humo ndani ni magumu kwake.
Wanaendelea kuripoti kwamba Chris anakunywa maji tu na wakati mwingine anapewa juisi ya machungwa.Huwa anapewa sandwich kwenye chombo kibovu na Chris Brown huwa anakataa hiyo sandwich.
Chris bado anakabiliwa na mashtaka mengine ambayo ni kumpiga kijana mmoja na kama kesi hiyo ikimuendea vibaya anaweza kwenda jela miaka 4.
Taarifa zinazotoka hivi sasa ni kwamba mwanasheria wa Chris Brown anafanya juhudi zote za kumlipa kijana huyo ili mteja wake akimaliza mwezi mmoja wa jela asiwe na kesi yoyote.
Mwezi huu mmoja anaotumikia Chris ni kutokana na jaji kumtaka akae rehab baada ya kuvunja sheria alizowekewa baada ya kesi ya Rihanna. Lakini pia akavunja sheria za Rehab na kujikuta anafungwa kwa mwezi mmoja.

MAUAJI MENGINE YA KIGAUDI YATOKEA KANISANI HUKO MOMBASA

0
0
Jana jumapili tarehe 23/3 watu kadhaa ambao wanasadikika kuwa ni magaidi wamevamia kanisa moja linalojulikana kwa jina la Joy Jesus Church huko Mombasa na kuanza kupiga risasi kanisani hapo.
Mashuhuda wa tukio hilo wanasema baada ya watu hao kutekeleza tukio hilo walikimbia kwa miguu kuelekea pasipo julikana.
Afisa wa polisi wa eneo hilo amesema hadi sasa wamefariki watu wawili na wengine kumi wamepata majeraha ya risasi nakukimbizwa hospitali.
Kikundi cha Al Shabaab kiliwahi kuhusishwa na tukio kama hili huko Nairobi lakini hivi sasa limetokea Mombasa.
Maafisa wa polisi wamesema wanaendelea kufanya uchunguzi wa kuwakamata watu hao japokuwa hadi sasa bado hawajapata tetesi yoyote juu ya watuhumiwa hao.
-Regina Iwole

STEVE NYERERE AMPATANISHA WOLPER NA MBAYA WAKE

0
0
Stori: Gladness Mallya

CHUKUA tano! Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amefanikiwa kumpatanisha Jacqueline Wolper Massawe na mbaya wake ambaye ni msanii mwenzake wa filamu (jina kapuni).

Akizungumza na gazeti hili, Steve alifunguka kuwa uongozi wake upo kwa ajili ya kuweka kundi hilo likae katika njia sahihi hivyo aliamua kumuita Wolper na huyo msanii mwenzake ambapo alifanya nao kikao cha saa kadhaa maeneo ya Mbezi Beach, Dar.

Alisema kuwa alifurahishwa kuona bifu hilo limekwisha kwani yeye anapenda watu wapendane na kundi liwe na amani, kusiwe na mifarakano ya hapa na pale ndiyo maana alichukua jukumu hilo na sasa wako vizuri.
Kwa sasa wawili hao wanazungumza tofauti na zamani ambapo walikuwa hawasalimiani hata wakikutana uso kwa uso.

“Nimefurahi sana kwa kuwa nimeweza kuwapatanisha, haikuwa kazi rahisi lakini nimefanikiwa, naamini wataendelea kuzungumza vizuri na kupendana maana mimi ni mtu wa amani, napenda na wasanii wangu wawe na amani na wapendane pia,” alisema Steve ambaye naye amepatana na Wema Sepetu baada ya kuwa Mwenyikiti wa Bongo Movie Unity.

Wolper na msanii huyo waliingia kwenye gogoro zito baada ya mbaya wake huyo kumkashifu Wolper laivu runingani na kumshambulia kwa maneno makali
GPL

KUMEKUCHA DODOMA"TAMKO LA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA WA KUNDI LA “TANZANIA KWANZA”

0
0
Sisi Wajumbe Wa Bunge Maalum la
Katiba tunaotoka makundi mbalimbali na pia tunaoamini katika kauli mbiu isemayo “TANZANIA KWANZA”, tunapenda kutoa tamko rasmi la kuunga mkono hotuba aliyoitoa Mheshimiwa Rais alipokuwa akihutubia Bunge Maalum la Katiba Tarehe 20/03/2014 kama ifuatavyo:

Kwanza, tunampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kwa hotuba yake aliyoitoa wakati akizundua Bunge Maalum la Katiba tarehe 20 Machi 2014.

Tunaamini Rais, kama Mkuu wa Nchi, alikuwa na haki na wajibu wa kutoa mwelekeo na maono yake kuhusu Rasimu ya Katiba na hatua hii tuliyonayo sasa ya kuipitia Rasimu kwenye Bunge la Katiba. 

Tunafarijika kwamba hotuba hiyo imepokelewa vizuri na Watanzania wengi kwenye kila kona ya nchi yetu na wengi wao wamekuwa wakitutumia ujumbe wakituhimiza kuizingatia hotuba hiyo katika kutimiza wajibu wetu.

Pili, tunamshukuru Rais kwa uchambuzi wake wa kina wa Rasimu na ushauri wake kwetu kuhusu haja ya kuweka taifa mbele, kushawishiana kwa hoja kuliko kulazimisha hoja na haja ya kutunga Katiba itakayoliimarisha taifa letu na kuendeleza umoja na ustawi wa
Watanzania. Sisi wana TANZANIA
KWANZA tutaendelea kushawishi kwa hoja na wala hatutalazimisha.

Tatu, tumeshangazwa na hamaki
iliyoonyeshwa na baadhi ya wajumbe wenzetu kuhusu hotuba ya Rais.

Tunasikitishwa na kauli zao zenye
mwelekeo wa kuhujumu mchakato wa kupata Katiba mpya. Viongozi
hawahawa wanaotoa kauli hizi
walionekana wakishangilia hotuba ya Rais pale aliposema yale waliyokuwa wanakubaliana nayo. Iweje watishie vurugu na kususia kisa tu Rais kasema baadhi ya mambo wasiyokubaliana nayo. 

Ustahamilivu wa kidemokrasia,
ustaarabu na hekima ya uongozi na utu uzima hautaki hivyo.Hotuba ya Rais imeweka wazi faida na hasara za mifumo yote ya Muungano wa Nchi yetu kwa hoja ili Watanzania wawe na fursa pana zaidi ya kutafakari na mwisho kuamua. 

Mheshimiwa Rais ametimiza kauli yake ya kushawishi kwa hoja na si kwa kulazimisha.

Nne, Hotuba ya Mheshimiwa Rais
haikuvuruga wala kuingilia mchakato uliopo mbele yetu. Rais hakuingilia kanuni za Bunge maalum
tulizozipitisha, Rais hakubadilisha
Sheria ya mabadiliko ya Katiba, Rais
hakupiga kura kwenye vifungu vya
Katiba, Rais ameanza kwa kuipongeza Tume ya Mh. Jaji Warioba na kuipongeza kuwasilishaji wake.

Alichokifanya Mheshimiwa Rais kama kiongozi mkuu wa Nchi mwenye hekima na busara na uchungu wa Nchi yake na kutambua dhamana aliyopewa na Watanzania wote bila kujali makundi ameelezea faida na hasara za mifumo ya Serikali iliyowasilishwa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Tume. Rais katupa moyo na kutuhimiza tumalize kazi haraka na
tuifanye kwa weledi huku tukiweka maslahi ya Taifa mbele. Hata pale
alipotoa maoni na ushauri kuhusu baadhi ya vifungu bado Mh.Rais
alisisitiza kwamba uamuzi wa mwisho ni wetu sisi Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba.

Tano, dhana ya kuichambua na
kuikosoa rasimu maana yake si
kumdhalilisha Mwenyekiti wa Tume na Wajumbe wake. Msingi mzima wa
kutolewa Rasimu hii ni kwamba
Wananchi tuichambue, tuikosoe,
tuirekebishe, tuiboreshe na hata ikibidi tuibadilishe na mwisho tutaipigia kura sote kwa pamoja. Rasimu haikuletwa kama Msahafu wala Biblia na ndiyo maana zimewekwa hatua mbili baada ya kazi ya tume kukamilika: 

BUNGE MAALUM LA KATIBA na KURA YA MAONI YA WANANCHI. 

Rais akiwa mkuu wa Nchi, naye ana nafasi yake katika mchakato wa Katiba. Sisi wana TANZANIA KWANZA, tunashukuru kwamba Mh. Rais alitutanabahisha kuhusu maeneo muhimu ya kuzingatia ambayo Tume haikuyaainisha kwa upana wake ikiwemo mipaka ya Nchi
yetu. Tunawapongeza Wajumbe wa tume kwa kazi waliyoifanya na kuikamilisha.

Kazi inayofuatia sasa ni uchambuzi wa Rasimu waliyoiwasilisha. Katika hatua hii ya sasa ya Bunge la Katiba, Rasimu hii inaweza ikakosolewa na hata inaweza kubadilishwa sana. 

Tunawasihi Wajumbe wa Tume waondokane na dhana kwamba kazi yao inapojadiliwa tofauti na mapendekezo yao siyo udhalilishaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Sita, Sisi Wajumbe wa Bunge Maalum, wana TANZANIA KWANZA ambao idadi yetu ni zaidi ya Wajumbe 400 na ambao orodha yetu tutaitoa hivi karibuni kwa
wingi wetu na umoja wetu tunayo
dhamira ya kutimiza wajibu wetu kwa mujibu wa Sheria na kwa kuzingatia matarajio ya Watanzania. 

Tunawasihi wale wenzetu ambao hawakuipenda hotuba ya Mheshimiwa Rais watulie, waondoe hamaki na sote tushirikiane kuifanya kazi hii, kama wapo ambao kitendo cha Rais kuja kuhutubia na kutoa uchambuzi wake kuhusu Rasimu, kinawafanya wasitake tena kushiriki
katika mchakato huu, basi uamuzi wao huo waufanye kwa namna ambayo haitatukwaza au kutuzuia sisi wengine tunaotaka kuendelea na shughuli hii ya mchakato wa Katiba. 

Tunawasihi viongozi wa Bunge Maalum wasivumilie wala kuendekeza vitendo vya vurugu za
makusudi vitakavyozuia uendeshaji wa Bunge. Tunawasihi msiruhusu watu wachache wakaliweka rehani Bunge Maalum ili kutengeneza mtaji wa kisiasa. 

Tunawasihi Watanzania wawaone na kuwahukumu wale watakaotaka kuvuruga au kukwamisha mchakato adhimu wa kupata Katiba mpya kisa tu Mh. Rais kaja kuhutubia Bungeni.

Mwisho, tunapenda kusisitiza kuhusu umuhimu mkubwa wa vyombo vya habari katika mchakato huu. Hiki ni kipindi muhimu sana katika uhai wa Taifa letu. Wananchi wengi wanafuatilia mchakato huu kupitia vyombo vya habari. 

Tunawasihi wamiliki, wahariri na waandishi wa habari wazingatie
weledi wa hali ya juu sana katika
kuripoti mchakato huu. Wananchi
wanapenda kusikia, kuona na kusoma yanayojiri wala sio propaganda za wanasiasa au makundi mbalimbali.

Tunapenda kuvisihi vyombo vya habari viwaunganishe Watanzania wote katika kipindi hiki muhimu na cha kihistoria.

Hata hivyo tunatoa shukrani zetu za
dhati kwa vyombo vya habari na wanahabari wote kwa ushiriki wao
katika mchakato huu wa Katiba. Tunazidi kuwasihi waendelee kufanya kazi zao kwa weledi mkubwa, kutokufanya kazi kwa kufuata propaganda za kisiasa au kufuata makundi, kutoa mizania sawa kwa maoni tofauti bila kuegemea maoni ya kundi moja au matakwa ya makundi fulani kwa kuwa mwisho wa siku sisi sote tuna jukumu kubwa la kuhakikisha tunakuwa na Tanzania moja.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu Libariki Bunge Maalum la Katiba

“TANZANIA KWANZA”

Tunawashukuru kwa kutusikiliza.

Kwa niaba ya Wabunge wa Bunge la Katiba “WANATANZANIA
KWANZA”

AGANO LA DAMU KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI

0
0
Unapohusiana na mtu kimapenzi unafanya naye agano la damu. Agano hilo maana yake ni kwamba wewe unakubaliana na kufungamana na sifa na tabia pamoja na vifungo vingine vyote kama vile laana, mizimu, matatizo na majanga mbalimbali yanayomhusu huyo uliyefanya naye mapenzi, kadhalika na yeye anafungamana na wewe katika mambo hayo. Agano la namna hiyo humtaka aliyeingia katika hayo mapatano kukubaliana nayo "consistently". Iwapo mhusika hatatii au ataenda kinyume na agano, ndipo agano hilo "hutrigger malice" na kusababisha kutokuelewana, vurumai, kutokupendana na hata kuuana katika mahusiano na mara nyingi kupelekea kuachana!

Kimsingi, unapojamiana na mtu unakubaliana naye kuchangia kila kilicho chake, na yeye pia anakubaliana kuchangia na wewe kila kilicho chako, hasa laana na matatizo kama vile magonjwa na mizimu kwa sababu hivi vitu vimejengwa katika maagano ya damu.

Ndio maana wakati mnaoana na mwenzio mlipendana sana, lakini kwa sababu wewe au mwenzi wako alichepuka na kufanya maagano: ugomvi, mapigano, kutishiana, chuki na hata kutaka kuuana hakuishi kila leo! Swala sio wivu kwamba unahisi mwenzi wako anakusaliti au kuhitilafiana katika mambo tu ya kawaida, issue ni yale maagano ya damu ambayo "hudemand price"!

Mara nyingi unasikia watu wanalalamika kuhusu tabia za watoto "huyu mtoto tabia kaichukua wapi, mbona baba na mama yake au ukoo wao hawako hivyo?". Chanzo cha tabia za ajabuajabu za watoto ni matokeo ya michepuko iliyofanya maagano na watu/koo zingine zenye laana. Laana na matatizo yanayoletwa na agano la damu katika familia havihitaji mtu kuchepuka na kuzaa nje ya ndoa, bali tu kuhusiana katika mapenzi!

Mimi nilipoingia kwenye mahusiano na mke wangu nilivunja maagano yote kwa jina la Yesu. Lakini kumbuka kuwa huwezi kuvunja maagano kama vile ya michepuko kwa jina la Yesu ili "kufavor your own evil deeds"!

Maagano yanayofanywa na watu kwa njia ya mapenzi huenda vizazi hadi vizazi. Hii ni sawa kabisa kwa mjibu wa sayansi kwani "hereditary information" kutoka kizazi hadi kizazi hubebwa na viasili vilivyopo katika damu, mfano DNA. 
Pasco anaweza kuendeleza hii mada kwa uchambuzi zaidi.

Mie na mke wangu tuna furaha fulltime kwa sababu mapenzi yetu yananawiri kila kukicha, na huwa hatuelewi kabisa matatizo katika ndoa za watu yanatokana na nini! "We are the happiest couple" kwa sababu "we posses several life secrets" mojawapo ni siri kuhusu agano la damu!

Tambueni ya kwamba one of the great decisions a person can make in his/her life ni kuwa na uhusiano wa kimapenzi (hata kwa dakika moja) na mtu kwa sababu anafanya naye life covenant "blood covenant"!
We teach you things that matter most!
- LifeHacker

KWANINI UVAE NGUO FUPI MWENYEWE HALAFU UKOSE AMANI

0
0
Umevaa nguo fupi mwenyewe na ulivyotoka nyumbani ulijiona umependeza umefika njiani unaanza kuhangaika kuishusha kuziba mapaja au sehemu iliyo wazi, kwani ulivyo vaa hukulijua hili? Kama umea amua kuvaa vaa na ujiamini, ukianza kuhangaika nayo unaoneka muhuni , au mshamba. Vaa kitu kitacho kufanya uwe comfortable. mwili ni wako nguo ni zako pia maamuzi ni yako kwanini upate shida..??? 

MABAKI YA MIFUPA YA BINADAMU NA BINADAMU WANAO SUBIRIWA KUFA VYAGUNDULIKA KATIKA JUMBA

0
0
Human skeletons, body parts, decomposing bodies, skulls and bones on bloodstained floors were discovered at an abandoned building in Soka, Oluyole LGA of Oyo State yesterday March 22nd. The bodies are believed to be unfortunate victims of ritual killing. Police officers also rescued about seven people who were chained together in leg-irons and looked emaciated. (The old woman pictured above was one of those rescued yesterday).

Containers containing human parts were also discovered in the bush surrounding the building. It is believed that people go to the place in the dead of the night to buy human parts.

The abandoned house of horror was discovered after Okadamen in Ibadan discovered that some of their colleagues had gone missing...especially when they took passengers to that area. They decided to search the area and discovered skeletal remains...

The police said they have arrested a few people over the discovery and plan to 'investigate the crime in all its ramifications'. Continue to see very graphic pics from the House of Horror...


MSICHANA AMCHANA MWENZAKE NA KISU BAADA YA KUGUNDUA ANATOKA NA MWANAUME WAKE

0
0
Je Unaweza kufanya unyama kama huu ukisikia mtu wako anatoka kimapenzi na mtu mwingine? Basi hii imetokea hivi karibuni msichana mmoja baada ya kusikia boyfriend wake anatoka na msichana mwingine alitoka na kumtafuta huyu msichana na kumchana chana na kisu kama unavyoona hapo kwenye picha.......

ANGALIA VIDEO MPYA YA SHILOLE -CHUNA BUZI-(EXPLICIT-WAKUBWA TU)

0
0
Video hii imetoka ila hii ni kwa ajili ya Mitandao tu kwani humo ndani ni maono matupu ..yakuonekana kwenye Tv itafuata soon.....Angalia hapa ujionee mwenyewe Buzi linavyochunwa

AIR MALAYSIA PLAN IS LOST NOBODY SURVIVED-PM CONFIRMS THE AIRCRAFT CRASHED INTO SEA

0
0
The missing Malaysian Airlines flight MH370 must be assumed lost with everybody on board dead - Prime Minister Najib Razak said today.

At an emergency press conference, the Malaysian PM said that it is "with deep sadness and regret" that new data shows the flight "ended in the southern Indian Ocean".

After further tests of data British-based satellite company Inmarsat concluded that MH370 crashed into the sea, thousands of miles off course.

It wasn't close to any possible landing sites, said the PM, and was in the southern Indian Ocean to the west of Perth.

Investigators are still searching for any debris from wreckage and, crucially, the black box.

Razak said families had been informed of the latest developments by Malaysia Airlines.

He said: "The last two weeks have been heartbreaking. This news must be harder still."

There will be a further press conference tomorrow with more details, he added, from the press conference held in Kuala Lumpur.
The southern Indian Ocean is believed to be where the jet went down because Malaysian authorities have said pings sent by the Boeing 777-200 for several hours after it disappeared indicated that the plane ended up in one of two huge arcs: a northern corridor stretching from Malaysia to Central Asia, or a southern corridor that stretches towards Antarctica.

Malaysian authorities have not ruled out any possible explanation for what happened to the jet, but have said the evidence so far suggests it was deliberately turned back across Malaysia to the Strait of Malacca, with its communications systems disabled. They are unsure what happened next.

Authorities are considering the possibilities of hijacking, sabotage, terrorism or issues related to the mental health of the pilots or someone else on board.

Malaysia's police chief, Inspector General Khalid Abu Bakar, has reiterated that all the passengers had been cleared of suspicion.

But he said that the pilots and crew were still being investigated. He would not comment on whether investigators had recovered the files that were deleted a month earlier from the home flight simulator of the chief pilot.

In the US, Tony Blinken, President Barack Obama's deputy national security adviser, said on CNN: "There is no prevailing theory."

"Publicly or privately, we don't know," he said. "We're chasing down every theory."



UTABIRI WA TB JOSHUA WATIMIA-NI KWELI AIR MALAYSIA ILIANGUKA INDIAN OCEAN NA HAKUNA ALIYE PONA

0
0
Baada ya ndege ya Air Malaysia kupotea Mtabiri TB Joshua Alisema Kuwa Ndege hiyo itakuwa imeanguka Kwenye Bahari ya Hindi na Hakuna Aliyepona ,,,Utabiri huo kwa wengi ulichukuliwa kama mzaha lakini leo imedhihirika tena kwa mara nyingine kuwa utabiri wake ni wa Kweli , kwani imethibitika kuwa ndege hiyo ilianguka kwenye bahari hiyo na hakuna aliye pona...

WEMA SEPETU JIPANGE: DIAMOND PLATNUMZ KUPITIA UKURASA WAKE WA INSTAGRAM AFUNGUKA NA KUSEMA

0
0
Tunamtoa mtoto wetu mwingine toka kwa bwana #Moze_Iyobo na bi #Mwengi.... Eeh! Mwenyezi Mungu, wajaalie na hawa vijana wawili walio baki @emma_platnum na @tonser66wamalize haraka nao, ili Mtu mzima sasa nianze kufyatua copy zangu ��.. �������� au mda wangu Bado???

SHOPRITE IMEUZWA WAFANYA KAZI WAGOMA NA KUANDAMANA MLIMANI CITY

0
0
Leo mida ya Jioni pale mlimani City nimeshuhudia wafanya kazi wa Duka Kubwa la Shoprite wakiwa wamegoma wakizua watu wasiingie kwenye duka hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa duka hilo limeuzwa bila wao kupewa mafao yao ...Habari zilizopo ni kuwa duka hilo limenunuliwa na Super Market Ingine kubwa Nchini Kenya Ambayo inakuja kupanua biashara zake hapa Dar .....
Viewing all 104429 articles
Browse latest View live




Latest Images