Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

SIMU Ziliingizwa Nchini Zikiwa Hazina Kiwango (Feki) Kuzimwa Rasmi Kesho,

$
0
0

SIMU ziliingizwa nchini zikiwa hazina kiwango kuzimwa rasmi kesho, katika kuhakikisha kila mtu anatumia simu kiwango kwa usalama  na ulinzi wa nchi.


Akizungumza na waandishi habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Mhandisi James Kilaba amesema kuwa katika uzimaji wa simu wameshatoa elimu juu ya simu hizo.


Kilaba amesema kuwa simu ambazo watu walibadilisha (Flash) nazo zitazimwa kutokana na kufanya hivyo ni kosa la kisheria na mtu anayefanya hivyo kifungo chake ni miaka 10.


Amesema hakuna kitu chochote kinachofanya simu zisiweze kuzimwa hivyo watu wajiandae kwa zoezi hilo na simu zitakazozimwa wametakiwa kuzihifadhi katika mazingira salama.


Aidha amesema wametoa elimu ya kutosha, hivyo kesho kutakuwa na mkutano wa wadau mbalimbali wa makampuni ya simu, na wamiliki wa maduka ya simu pamoja na mafundi katika kubadilishana mawazo wakati wa kuzima simu feki.


‘’Simu feki kesho zitazimwa, hatutakuwa na mabadiliko ya kuongeza muda au vinginevyo kutokana na elimu iliyotolewa juu ya simu ya  feki ambazo baada ya soko kushindikana mjini walipeleka vijijini’’amesema Kilaba  .

Peter Msechu Akiri Mwili Wake Umemshinda...Anatafuta Wakumpa Stress

$
0
0

Msanii Peter Msechu amefunguka na kusema kuwa yeye mwili wake umemshinda sasa maana amejaribu kila mbinu kupunguza lakini wapi upo pale pale na yeye mambo ya kusema afanye diet hawezi kwani hela ya kununu matunda ya elfu nne kila siku hana.

Peter Msechu amesema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio na kusema sasa amegundua kitu pekee kinachoweza kupunguza mwili wake si kufanya diet bali ni kupata stress tu, hivyo anatafuta mtu wa kumpa stress ili apungue.

"Mambo ya kusema nafanya diet mimi siwezi hizo hela za kununua matunda ya elfu nne kila siku mimi sina, sijui hela ya gym hamna, saizi mimi nataka stress tu ili nipungue maana kitambi hiki saizi kimekuwa na mazalia kama arobaini hivi" alisema Peter Msechu

Mbali na hilo Peter Msechu alisema kuwa katika wimbo wao mpya ambao wamefanya na Banana Zoro kwa asilimia kubwa umeandaliwa na Banana Zoro na kusema yeye yupo karibu na Banana Zoro kutokana na ukweli kwamba wanafanya muziki wa aina moja wa live, na kusema huo ndiyo muziki wa kweli na si muziki wa wasanii wengi wa bongo ambao wanabebwa bebwa na computer kwa kutengenezwa.

Utafiti: 8 Kati 10 Wanataka Bunge Lioneshwe Live

$
0
0

Watanzania walio wengi (79%) hawakubaliani na maamuzi ya serikali ya kusitisha matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge kupitia runinga na redio.

Karibu wananchi wote (92%) wanaamini kuwa ni muhimu vikao hivyo virushwe moja kwa moja.
Takwimu hizi zimetolewa na Twaweza kupitia muhtasari wa matokeo ya utafiti wake: #BungeLive.
Muhtasari huo unahusisha takwimu zilizokusanywa na Sautiza Wananchi, Utafiti wa kwanza barani Afrika unaotumia simu za mkononi na wenye uwakilishi wa kitaifa.

Matokeo haya yanatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,815 kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara (Zanzibar haihusiki kwenye matokeo haya) kati ya tarehe 29 Machi na tarehe 12 Aprili 2016.

Miongoni mwa watanzania waliokua wakitazama na kusikiliza vipindi vya Bunge asilimia 42 walikuwa
wakiangalia vikao vya Bunge vilivyokuwa vikirushwa moja kwa moja kupitia runinga na asilimia 60
walikuwa wakisikiliza vikao hivyo kupitia redio. Kati ya hawa, asilimia 59 waliangalia vipindi vya Bunge kupitia runinga miezi miwili kabla ya utafiti huu kufanyika, na asilimia 57% walisikiliza vipindi vya Bunge kupitia redio.

Takwimu hizi zinaonyesha kuwa wananchi walikuwa wafuatiliaji wazuri wa vikao vya Bunge vilivyokuwa
vikirushwa moja kwa moja. Sababu zao za msingi ni kama zifuatavyo:

• Asilimia 46 ya wananchi wanataka kuwafuatilia wabunge wao ili kuona kama wanawawakilisha
ipasavyo.

• Asilimia 44 ya wananchi wanasema ni haki yao kufahamu kile kinachoendelea bungeni

• Asilimia 29 ya wananchi wanaamini zaidi matangazo ya moja kwa moja kwa sababu wanawaona na
kuwasikia wabunge kwa macho na masikio yao wenyewe

Walipoulizwa na kama ni sahihi kutumia fedha za umma kugharamia matangazo ya moja kwa moja ya
vikao vya Bunge, asilimia 80 ya wananchi wamesisitiza kuwa matangazo hayo yana umuhimu sambamba
na huduma nyingine za jamii.

• Wananchi walio wengi (88%) wanasema matangazo ya vikao vya Bunge yarushwe moja kwa moja
bila kujali gharama.

• Watanzania wanaunga mkono kwa kiwango kikubwa (asimilia 75) suala la kuruhusiwa kwa
vyombo binafsi vya habari kurusha matangazo ya moja kwa moja ya viako vya Bunge iwapo serikali
imeshindwa kuyagharamaia.

Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, anasema: “Suala la kusitisha matangazo ya moja
kwa moja ya vikao vya Bunge la Tanzania limezua mjadala mzito miongoni mwa watanzania.

Kupitia
Sauti za Wananchi, tunaona wazi kabisa shauku kubwa ya wananchi ya kutaka kuwaona na kuwasikia
wawakilishi wao bungeni kwa macho na masikio yao wenyewe. Je, serikali iko tayari kuyapokea
matakwa ya watanzania walio wengi katika jambo hili? Ikibadilisha maamuzi yake na kurudisha
matangazo haya itakua ishara nzuri ya nia yake ya kuimarisha uhusiano wa karibu zaidi kati ya
wananchi na wabunge wao.”

Nukuu ya Maalim Seif ‘Lipumba asahau uenyekiti CUF’ yatolewa ufafanuzi

$
0
0

Baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii June 15 2016  vimeamka na habari yenye kichwa cha habari ambacho kimenukuu Katibu Mkuu wa chama cha CUF, Maalim Seif akisema ‘Prof. Lipumba asahau uenyekiti CUF’.

June 15 2016 chama cha wananchi CUF kupitia kwa kupitia kwa mkurugenzi wa habari na uenezi, Salim Bimani amekanusha taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari ambapo taarifa hiyo imesema kwamba Taarifa hii ni uongo na katibu hajaitoaa. Hii ni miongoni mwa propaganda zinazotengenezwa na watu wasio na malengo mema na chama, wakijua fika kwamba maamuzi ya chama hayafanywi na mtu bali vikao vya chama.

Taarifa imeongeza kuwa maoni na msimamo wa Katibu mkuu Maalim Seif ambaye yuko Marekani ni kwamba wanachama wanasubiri maamuzi ya vikao vya chama vitaamua mambo mbalimbali yanayoendelea na yanayotokea na vitatangaza maamuzi yake kwa wote.

Chama hicho kimetoa Rai kwa wanahabari kuwa makini sana na vyanzo vya taarifa mbalimbali wanavyotumia kupata taarifa hasa mitandao ya kijamii pia wafuate maadili ya uandishi wa habari na kuandika habari kutoka kwenye vyanzo vya uhakika visivyo na shaka.

Aidha CUF imetoa angalizo kwa wanachama wake wote kuwa makini na taarifa wanazopokea na wazithibitishe kwa umakini ili kuwa na uhakika na kuepuka kupotosh

Kauli ya Jenerali Ulimwengu Yakutaka Jakaya Ashtakiwe yageuka Mjadala Nchini

$
0
0
Hakyanani hakujatulia. Ile kauli iliyotolewa juzi na mwanahabari mkongwe nchini, Jenerali Ulimwengu kutaka Rais mstaafu Jakaya Kikwete ashtakiwe mahakamani inatesa mitaani.

Tayari baadhi ya wasomi wametia neno wakisema ipo haja ya kubadili Katiba ili mkuu wa nchi aweze kushtakiwa baada ya kuondoka madarakani.

Wakati wasomi hao wakitoa pia mifano ya wakuu wa ‘kaya’ katika baadhi ya nchi walioshtakiwa walipoondoka na walipokuwa madarakani…


Anna Makinda Akumbukwa kwa Hekima zake Bungeni...Tulia Akson Asababisha Mgawanyiko Mkubwa Bungeni

$
0
0
Kambi rasmi ya upinzani bungeni sasa inauona utawala wa Spika wa Bunge la 10, Anne Makinda kuwa ulikuwa na hekima ya uongozi kwa kumaliza tofauti na wabunge bila kushindana.

“Makinda alikuwa akiona mmeenda kinyume tu anawaandikia kimemo, mbunge mmoja mmoja akiwataka mkutane ofisini kwake na kumaliza. Hakukuwa na mwanya wa kushindana tofauti na Dk Tulia,” amesema Kaimu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, David Silinde.

 Amesema kukosekana kwa Spika Job Ndugai ambaye amekuwa bungeni kwa muda mrefu kumesababisha mgawanyiko kati ya wabunge wa upinzani na wa chama tawala.

Watuhumiwa wa Ubakaji na Waliosambaza Picha za Uchi za Msichana Morogoro Waendelea Kusota Rumande

$
0
0
Waendesha mashtaka wa serikali Morogoro wamepewa miezi miwili kuwasilisha cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili kuachia ama kuendelea kushikilia dhamana ya washtakiwa wanne wa kesi ya usambazaji wa picha chafu za ngono.

Washtakiwa hao ni wale waliopiga picha chafu za ngono dhidi ya mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Dakawa, Mvomero.

Mbele ya waendesha mashtaka wa serikali Gloria Rwakibalila, Edgar Bantulaki na Calistus Kapinga ilidaiwa mahakamani hapo na Ivan Msacky, Hakimu wa Mahakama hiyo kuwa, suala la dhamana chini ya Katiba ni haki ya kila mshtakiwa lakini akaonesha kushangazwa na upande wa mashtaka kutoeleza kwa uwazi sababu za kuendelea kuizuia dhamana hiyo.

Hakimu Msacky amewataka waendesha mashtaka hao kuhakikisha wanawasilisha mahakamani cheti kinachozuia dhamana kwa washtakiwa hao na sababu zake ili kesi hiyo iweze kuanza kusikilizwa.

Kesi hiyo ya jinai namba 54 ya mwaka 2016 inawakabili washtakiwa sita ambao ni Idd Adam Mabela, Zuberi Thabit, Rajab Salehe, Ramadhani Ally, Muksin Ng’ahy na John Peter ambao wanakabiliwa na shtaka la kusambaza picha chafu za ngono za msichana mwenye umri wa miaka 21 wilayani Mvomero mkoani humo. Washtakiwa wanaotaka dhamana ni mshtakiwa namba tatu hadi sita.

Hata hivyo, Hakimu Msacky jana aliahirisha kesi hiyo hadi tarehe 29 Juni mwaka huu ambapo kesi hiyo itaendelea kujadili suala la dhamana kwa washtakiwa hao.

Katika kesi hiyo iliyosikilizwa kwa mara ya kwanza tarehe 18 Mei mshtakiwa namba 1 na 2 wanatuhumiwa kumbaka na kumuingilia kinyume na maumbile msichana huyo Aprili 27, saa 1 usiku katika nyumba ya kulala wageni ya TITII iliyopo katika Tarafa ya Dakawa, Mvomero.

Katika kesi ya kwanza ya kubaka na kulawiti inayowakabili washtakiwa Mabela na Thabiti, wakazi wa jijini Mbeya ilishindwa kusikilizwa jana  kutokana na wakili wa washtakiwa Mohamed Mkali kutokuwepo mahakamani.

Zari Anasa Ujauzito Tena!

$
0
0
Hii ni habari ya motomoto kabisa! Mama la mama, Zarinah Hassan ‘Zari The  Boss Lady’ amedaiwa kunasa ujauzito wa mpenzi wake, Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Risasi Mchanganyiko lina ubuyu ulionyooka.

Taarifa hizo za ndani ya familia zimevuja ikiwa ni takriban miezi nane tangu mrembo huyo ampe jeuri Diamond ya kutembea kifua mbele kwa kumzalia Tiffah ambapo inaelezwa kuwa, amefanya hivyo makusudi kuwakata ‘vilimilimi wabaya’ wake.Zarimond


TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo makini kutoka ndani ya familia ya Wasafi Classic Baby (WCB), juzikati kilinyetisha kuwa, gumzo la mjini kwa sasa ni wadau wa burudani kujadili ujauzito wa Zari, ambao unaonekana kuwatisha karibia wapambe wote wa timu pinzani.
“Naomba nikudokeze juu ya Zari kuwa mjamzito tena, habari hii ni ya uhakika na kila mtu WCB anajua, Zari amenyaka mimba na cha ajabu amekataa katakata kuichomoa kama Diamond alivyokuwa akimshawishi.

NDIYO CHANZO CHA UGOMVI
“Huwezi kuamini ugomvi wote ambao umekuwa ukidaiwa kuendelea kati ya Diamond na Zari umesababishwa na ujauzito huo ambapo Diamond amekuwa akitumia nguvu nyingi kumuomba Zari achomoe mimba hiyo lakini hakuna hata siku moja ambayo ameonesha dalili za kumuelewa.

MIMBA INA MIEZI MINNE
Chanzo hicho kilizidi kuweka bayana kuwa, kinachomsikitisha Diamond ni kwamba, mimba hiyo inazidi kukua jambo ambalo anaona si sahihi kwa sasa kwani ana mtoto (Tiffah) ambaye bado hajatimiza hata mwaka mmoja.
“Jamaa anaona soo, anaona kama jamii haitamuelewa hivi, jitihada zake za kumshawishi zinagonga ukuta na mbaya zaidi mimba kwa sasa ina kitu kama miezi minne,” kilisema chanzo hicho makini.

SAFARI ZA SAUZ ZATAJWA
Chanzo hicho kilizidi kutiririka kuwa, safari ambazo Diamond alikuwa akizifanya mara kwa mara kwenda Afrika Kusini  (Sauz), nyingi zilikuwa ni za kutatua mgogoro huo ambao umeikumba familia ya WCB, kiasi kwamba hadi wazazi wote wameshirikishwa lakini mwisho wa siku hakuna muafaka.
“Si unakumbuka kuna kipindi Diamond alikuwa anakwenda Sauz mara kwa mara, ishu hiyo ndiyo ilikuwa inampeleka lakini hazikuzaa matunda, mamaa kagoma,” kilisema chanzo hicho.

FAMILIA YAKE YAMSHANGAA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kuwa, familia yake imemshangaa Diamond kwa nini hakuwa makini wakati alijua kabisa Tiffah bado angali mdogo.
“Wamemshangaa sana kwa kushindwa kuwa makini wakati kwa sasa kuna mbinu nyingi sana za kuepuka ujauzito, sasa matokeo yake amesababisha hadi kuwe na mvutano unaokosa muafaka,” kilisema chanzo hicho.

NDUGU WA DIAMOND ATHIBITISHA
Mwanahabari wetu alipokuwa akiichimba habari hii, alizungumza na mmoja wa ndugu wa Diamond ambaye alikiri kuwa Zari ni mjamzito lakini akaombwa asitajwe jina maana suala hilo limegubikwa na usiri mzito.
“Ndiyo hivyo kama ulivyosikia. Zari hataki kutoa, nahisi kwa sababu ya kuwakomesha zile timu pinzani lakini anashindwa kujua upande wa pili familia inashindwa kukubaliana naye maana ni jambo la aibu kupata mimba kabla mtoto wa awali hajafikisha hata mwaka,” alisema ndugu huyo.

MSIKIE DIAMOND
Baada ya kupenyezewa ubuyu  huo wa motomoto, Risasi Mchanganyiko lilimtafuta Diamond mwenyewe ili aweze kuweka bayana habari hiyo ya heri, ambapo hakutaka kukataa wala kukubali licha ya kukiri kuzisikia habari hizo.
“Dah! Habari hizi sijui muda mwingine huwa mnazinyaka vipi, sijui hapa niseme nini zaidi ila unachotakiwa kufahamu mimi bado nahitaji kupata watoto zaidi ya mmoja na ifahamike kuwa ninapenda watoto sana, maana uwezo wa kuwahudumia ninao hata hivyo kushika mimba kwa Zari ni mapema sana,” alisema Diamond.

MAMA YAKE NAYE
Mama mzazi wa msanii huyo, Sanura alitafutwa ili kusikia maoni yake, lakini badala yake, aliishia kucheka na kumuomba mwandishi wa habari hizi kuachana na mambo hayo.

Chanzo:Global Publishers

Polisi Dar es Salaam Wamng’ang’ania Zitto Kabwe

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imesema inaendelea na upelelezi kuhusu tuhuma zinazomkabili Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Kabwe Zitto ambaye ni Mbunge Kigoma Mjini na watakapokamilisha atafikishwa Mahakamani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alisema, sababu za kumhoji Zitto ni kutokana na kauli za uchochezi alizozitoa katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Zakhem, Mbagala.

Alisema, tayari Zitto ameshahojiwa katika kituo hicho mara mbili, lakini bado jeshi hilo linaendelea na upelelezi ili kujiridhisha dhidi ya tuhuma zinazomkabili.

Sirro alisema jeshi hilo haliwezi kuruhusu siasa ambazo zinavunja amani, hivyo ameendelea kuwataka wanasiasa kufuata taratibu na endapo wamekataza kufanya mikutano basi watii.

“Kama hakuna amani hakuna siasa hatuwezi na hatutakubali kuruhusu amani tuliyonayo itoweke sababu ya wanasiasa lazima kutii ili kulinda amani yetu,” alisema Sirro.

Hivi karibuni Zitto alijisalimisha Kituo cha Polisi na kuhojiwa kwa zaidi ya saa tatu baada ya kuandikiwa barua ya kuitwa kituoni na Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Camilius Wambura.

Hatua ya Zitto kuhojiwa ilitokana na maudhui ya hotuba yake aliyoitoa Juni 5, mwaka huu kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Zakhem, Mbagala wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kutoka katika mahojiano hayo, Zitto alisema haoni kama hotuba aliyoitoa ina tatizo lolote, kwani hotuba hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya kisiasa.

Mume Kamtegesha Mke Kwa Njemba ili Avute Hela ya Ugoni..Kilichotokea Hata Kaa Asahau

$
0
0
Hii muvi ilianza kuna jamaa alikuwa anafkuzia mke wa mtu bila kuchoka.
Mke akamwambia mume.wakashauriana waweke mtego matata wa kufumania ili mgoni abananishwe atoe pesa maana anazo!

Siku ikawadia mke akakubaliana na jamaa wakutane gesti kama kawaida wako ndani washavua kila kitu mara mara mwenye mke akavamia na jamaa yake ili wamtaiti mgoni!kumbe mgoni mjanja bana akawatolea bastola akawaamuru wafunge mlango afu akawaweka chini ya ulinzi na kuwafunga kamba alafu akaendelea kula mzigo mbele yao hadi akamaliza afu akawafungia wote humo ndani akasepa ..Jamaa akajikuta kakosa ela na mkewe katafunwa mbele yake.....

Download Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

$
0
0

Download  Application ya Udaku Special Blog Kwenye Simu yako Kutoka Play Store Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi

Bonyeza Hapa CLICK HERE 

Au Bonyeza hii picha hapa chini

Kamanda Sirro: Tutamfungulia Zitto kesi ya uchochezi

$
0
0
Kamanda wa polisi wa jiji la Dar Simon Sirro amesema sasa hivi wanaendelea na kukusanya ushahidi wa makosa ya kichochezi aliyoyafanya Zitto Kabwe na upelelezi utakapokamilika watampeleka mahakamani.
Amesema hawatawavumilia watu kufanya uchochezi kwasababu ya siasa kwa kuwa bila utulivu hakuna siasa.

Picha/Video: Oscar Pistorius Atoa Miguu ya Bandia Mahakamani Kuonesha Udhaifu wake

$
0
0
Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius Jumatano hii amelazimika kutoa miguu yake ya bandia ili kumuonesha jaji jinsi alivyo dhaifu na kwamba asingeweza kumuua mpenzi wake makusudi.


Kwenye kesi hiyo iliyokuwa ikioneshwa live kwenye TV, mwanariadha huyo alijaribu kutembea kwa tabu bila miguu hiyo.


T-shirt yake ilikuwa imeloa kwa jasho na macho kuwa mekundu kutokana na kulia.
Video:

Mpaka Mwanamke Anaamua Kuchepuka Ujue Kuna Shida kwa Mumewe

$
0
0
Katika Utafiti wangu imegundua kuna tatizo kubwa katika mahusiano aidha ya kimapenzi au ya ndoa.Uaminifu umekuwa tatizo kubwa miongoni mwa jamii ya kizazi hiki! Kutoridhika imekuwa sehemu ya maisha ya sasa si kwa mwanaume au mwanamke kuchepuka ndiyo habari ya mujini kwa sasa hadi wale walioaminika kuwa viongozi wa dini maana hakuna mwenye kinga ya kutotenda dhambi hivyo imekuwa kujitwalia kadri tupendavyo nani atakuwa kiini cha mabadiliko katika wimbi hili linaoelekea kupoteza wengi.

Tatizo ni nini hasa kwa uzoefu wangu wa kuishi katika dunia hii na katika ndoa kwa muongo zaidi ya mmoja nimegundua mwanamke anaweza akatulizwa (walioko ndoani) tu endapo mume atakidhi mahitaji yote ya kiuchumi,zaidi kuwa na muda wa kutosha na mkewe bila kusahau kusaidiana kufikishana katika kilele cha maraha ambacho.Mungu aliona ni vema atupe wanadamu kama kitulizo ktk maisha yetu haya yenye adha nyingi.

Sasa cha ajabu kuna baadhi ya wanaume wamekuwa busy wakiamini magari,pesa na fahari ndiyo vitaziba uhitaji wa mke katika kukidhi haja ya upendo ndiyo maaana lawama haziishi watu wanachapiwa na kuishia kulalama eti wanawake hawaridhiki hata uwape nini mwanamke haswa alilyelewa vyema akihudumiwa bed na akapata mahitaji ya kiuchumi sina cha kufata nje hata kidogo.

Nina zaidi ya miaka 13 ya ndoa hivyo najua nisemacho sioni fahari wala sijawahi kufikiria kutoka na mtu nje ya mume wangu kwa muda wote huo ila kuna mazingira baadhi wanaume wanasababisha hadi mke unajiona mhitaji,mume hashikiki ndani kila siku kuja home late mvivu kitandani hayuko romantic nk unategemea mke afanyeje?

Ilihali naye ana damu inachemka(hapa siharalishi kuchepuka ila mke anakuwa katika upweke mkuu nani ampe faraja mpaka mke anaamua kutoka nje kuna tatizo kubwa hivyo chukueni tahadhari waume wenye tabia hizi zinajeruhi sana mioyo yetu (nasi tunapendwa sana huko nje uwezo wa kutoka kama mnavyotoka tunao sana..ila ni staha tu na hofu kwa Mungu muumbaji.Wanaume many sehemu yenu na wanawake pia ili tuishi kwa raha bila kuumizana.

Flora Mvungi Alidanganya Kuwa ana Mimba au Mimba iliyeyuka?

$
0
0
Baada ya H.Baba na mke wake Flora Mvungi kuweka wazi mapema mwaka huu kwamba wanatarajia kupata mtoto watatu, hivi karibuni Frola Mvungi ameonekana katika picha hana ujauzito hali ambayo imewafanya mashabiki wake katika mitandao ya kijamii kuhoji ilikuwaje.

Frebuari 8 mwaka huu, H.Baba ambaye ni baba wa watoto wawili, Tanzanite na Africa, alishare picha (hapo juu) katika mitandao ya kijamii zenye ujumbe kuhusu ugeni huo.

“Asante mungu kwa kila jambo #watoto nifaraja nakuombea muda ukifika ujifungue salama nakupenda mke wangu (1)tanzaniteone (2)Africa (???????) . Nitafutie jina la mwanangu Wa (3) nimuite nani?,” aliandika H.Baba.

Pia siku hiyo hiyo, mke wake Frola Mvungi alishere kwa mashabiki ujumbe mwingine kuhusu mimba hiyo.

“Hahahhahahahahhahaah nacheka kwa raha yaani nafuraha sana mana naona watu maneno yanawatoka kila kona..kwani kuzaa ni kosa?au kuna siku nimemuomba mtu hela ya kutunza wanangu??. Waja mna tabu sana,jamani hebu tusipangiane jinsi ya kuishi,,kingine siko nje ya ndoa na hata ingekuwa nje ya ndoa pia ni watoto wangu..mwakereka na nini??. Hhahaaaaaa yaani mtasema sana,” aliandika Frola Mvungi katika picha ambayo alipost instagram.

Baada ya mkanganyiko huyo, Bongo5 ilimtafuta H.Baba na kuzungumzia kauli hiyo ambayo iliwaacha mashabiki njia panda.

“Niliwauliza wananchi na mashabiki zetu kupitia insta wanichagulie jina la mtoto wa tatu 3 baada ya Africa na Tanzanite, watatu nimuite nani? . Tayari wao wamenipa majina yao kibao naendelea kuchagua jina moja. Mmesahau kabla ya mimba ya Tanzanite nilisema mwanangu ataitwa Tanzanite, kikubwa ndugu zangu endeleeni kunitafutia jina la mwanangu wa tatu kama ukitokea ujauzito,” alisema H.Baba.

Aliongeza, “Ni muda wakuwalea watoto wetu wawili wa kike na wakiume ashukuriwe Allah hii ni hatua kubwa sana kwangu kupata watoto wawili, nampenda sana mke wangu Flora Mvungi huyu ndiye malkia wangu wa nguvu kwangu mimi Tanzania nzima, hakuna kama malkia Florah Mvungi wengine malkia fake tuu. Bongo movie nzima ukitaja wadada wanao jiheshimu lazima jina la Mama Tanzanite linakuwemo kwa sababu anajiheshimu sana.


Sakata la Kumshitaki Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Laibua Mjadala Mzito

$
0
0
Kauli ya mwanahabari nguli nchini, Jenerali Ulimwengu kutaka Rais Mstaafu Jakaya Kikwete ashtakiwe mahakamani kwa kuitia hasara Serikali imeibua mjadala mzito, huku wasomi wakisema ipo haja ya kubadili Katiba ili mkuu wa nchi aweze kushtakiwa baada ya kuondoka madarakani.

Wasomi hao walisema ile kauli ya “hakuna aliye juu ya sheria” inapaswa kufuatwa na watu wote, wakitolea mfano Rais wa Brazil, Dilma Roussef aliyeng’olewa na Bunge baada ya kutuhumiwa kukiuka sheria za usimamizi wa akaunti ya bajeti ya nchi hiyo.

Kwa sasa nafasi yake inashikiliwa na aliyekuwa makamu wake, Michel Temer.

Hata hivyo, baadhi ya wasomi wamesema jukumu hilo la kumshtaki rais mstaafu inafaa liachwe mikononi mwa Bunge.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imempa kinga rais mstaafu ya kushtakiwa kwa jambo lolote alilofanya alipokuwa madarakani na imetoa mlolongo mrefu rais aliyeko madarakani kuondolewa.

Juzi wakati akizungumza katika Tamasha la Nane la Kigoda cha Mwalimu Nyerere, Jenerali ambaye pia ni mwanasheria wa kujitegemea alisema Kikwete anapaswa kushtakiwa kwa kuisababishia hasara Serikali kutokana na kuruhusu mabilioni ya shilingi kutumika katika mchakato wa Katiba ambayo haikupatikana.

Mbali na fedha zilizotumiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati wa kukusanya maoni, kununulia magari, kulipia pango la ofisi, nyingine zilitumika kurekebisha ukumbi wa Bunge uweze kubeba wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, na kulipa posho ya Sh300,000 kwa siku kwa wajumbe 620 kwa muda wa siku 130.

“Itabidi (Kigoda cha Mwalimu) mumuite (Kikwete) mwaka ujao, aje aeleze fedha za wananchi zilizotumika katika mchakato ule zilikuwa na sababu gani,” alisema huku akishangiliwa na umati wa watu.

Jenerali aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya za Hai na Ilala na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, alisema kama mawaziri wa zamani wamepandishwa kizimbani kwa kusababisha hasara, hata Kikwete anapaswa kupelekwa mahakamani kwa kusababisha hasara kwa Serikali na kuzima matumaini ya wananchi, jambo linaloweza kusababisha machafuko nchini.

Ibara ya 46 sehemu ya (1) ya Katiba inasema wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii, itakuwa ni marufuku kumshitaki au kuendesha mashataka ya aina yoyote juu yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

Sehemu ya (3) inasema isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais kwa mujibu wa Katiba hii.

Ibara ya 46A sehemu ya (1) inasema bila ya kujali masharti ya ibara ya 46 ya Katiba hii, Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa mujibu wa masharti ya ibara hii.

Sehemu ya (2) imeweka masharti kwamba bila ya kuathiri masharti mengineyo ya ibara hii, hoja yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama inadaiwa kwamba Rais; (a) ametenda vitendo ambavyo kwa jumla vinaivunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma; (b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadili yanayohusu uandikishwaji wa vyama vya siasa yaliyotajwa katika ibara ya 20 (2) ya Katiba.

Mbali ya Katiba ya sasa kumwekea kinga Rais mstaafu, Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Jaji Joseph Warioba na Katiba Inayopendekezwa zilinakiri kipengele hicho kinachompa Rais mstaafu kinga ya kutoshtakiwa bila kubadili chochote.

Maoni ya wasomi
Mhadhiri wa Shule ya Siasa ya Chuo Kikuu  Dar es Salaam (UDSM), Dk James Jesse alisema ili kuondoa kile alichokiita ‘kusumbuliwa’, jukumu la kumshtaki Rais mstaafu au aliyepo madarakani linapaswa kuachwa mikononi mwa Bunge.

“Katiba imeeleza wazi kwamba ataondolewa madarakani kwa azimio la Bunge. Binafsi nadhani utaratibu huo ndiyo mzuri hata kama atakuwa amemaliza muda wake, hoja ya kumshtaki ianzie bungeni,” alisema .

Naye Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia, Innocent Shoo alisema, “Tukizingatia demokrasia za kisasa, rais akitoka madarakani hapaswi kuwa na kinga ya kushtakiwa. Hii inatakiwa iwezekane hata akiwa madarakani ili kuzingatia utawala wa sheria.”

Katika ufafanuzi wake, Shoo alisema kuwa kutokuwajibika na utamaduni wa kutokujali ni utambulisho wa viongozi wengi barani Afrika huku akinukuu kauli ya Rais wa Marekani, Barack Obama, kwamba “Afrika inatakiwa kuwa na taasisi imara siyo mwanaume mwenye nguvu.”

Shoo alisema nchi nyingi barani Afrika hazina chaguzi huru, haziheshimu haki za binadamu na uhuru wa watu na taasisi mbalimbali, mambo aliyodai kuwa yanafaa kumfanya Rais kushtakiwa.

“Umeona kilichotokea Brazil? Ule ni mfano hai kuwa rais anaposhindwa kufuata sheria na taratibu ashtakiwe tena ashtakiwe hata akiwa madarakani,” alisisitiza.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua), Profesa Damian Gabagambi alisema, “Anapaswa kushtakiwa anapomaliza utawala wake na hasa kama wakati akiwa rais alikuwa akifanya mambo ya kulihujumu taifa.”

Profesa Gabagambi ambaye alikuwa mmoja wa wataalamu walioandaa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN), alisema kushtakiwa siyo kufungwa kwa kuwa mtuhumiwa atakwenda mahakamani na kujitetea.

“Hii itasaidia viongozi wakati wa utawala wao kuheshimu utawala bora na kufuata sheria na Katiba ili kukwepa kushtakiwa, mara wamalizapo kipindi chao cha kuongoza,” alisema.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Ezekiah Oluoch alisema Katiba inampa Rais kinga ya maisha, jambo ambalo si sahihi huku akieleza kuwa wazo la Kikwete la kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya lilikuwa zuri ila liliharibiwa na wanasiasa.

“Kinga aliyonayo rais ndiyo inayompa kiburi na ndiyo sababu akiwa madarakani akishauriwa hataki, ila akimaliza muda wake anajuta kwa uamuzi aliouchukua,” alisema Olouch huku akisisitiza kuwa hayo ni maoni yake binafsi si ya CWT.

Akitolea mfano wa kilichomkumba Rais wa Brazil, Oluoch ambaye alikuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, alisema hata kama nchi nyingine nazo zina kinga kwa marais wao, si lazima Tanzania kubaki na kinga hiyo kwa kuwa kila nchi ina utamaduni na ustaarabu wake.

“Rais wa Tanzania yupo juu ya sheria. Mfano Benjamin (MkapaRais wa Awamu ya Tatu) amesema anajutia uamuzi wake wa ubinafsishaji na kutowekeza katika elimu. Hayo ni baadhi tu ya makosa wanayoyafanya viongozi wetu,” alisema Oluoch.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandala alisema kuondoa kinga ya Rais baada ya utawala wake ni hatari kwa usalama na demokrasia ya nchi.

Alisema kwa kuwa kila kiongozi hufanya maamuzi ya kisiasa ambayo wakati mwingine hayatimii, kuondolewa kwa kinga hiyo kunaweza kukaleta matatizo ya kisiasa kwa siku za mbele.

 “Kuna mtu atakuja kung’ang’ania ikulu endapo atatambua kuwa yupo kwenye hatari ya kufikishwa mahakamani,” alisema Profesa Mukandala na akashauri zianzishwe taasisi makini na imara zitakazokuwa zinamshauri Rais juu ya maamuzi mbalimbali anayoyafanya akiwa madarakani.

Alisema hakuna haja ya kuwafikisha mahakamani viongozi wa ngazi hiyo, kama makosa yao yalitokana na mtazamo wa kisiasa na kukumbusha kuwa hata Rais wa awamu ya kwanza, Mwalimu Julius Nyerere alishindwa kutekeleza mkakati wa kuanzisha Vijiji vya Ujamaa kama ulivyoratibiwa sawa na ilivyotokea kwenye Katiba Mpya kipindi cha Rais Kikwete.

Chama cha Wananchi (CUF) Zanzibar, kimeunga mkono kauli ya Jenerali kuhusu Kikwete kushtakiwa kuhusiana na mchakato wa Katiba ambayo haikupatikana.

Mkurugenzi wa Haki za Binadamu, Habari, Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salim Bimani alisema CUF inaunga mkono kwa asilimia 100 kauli hiyo, kwa sababu sehemu kubwa ya matatizo yaliyojitokeza na yanayojitokeza Zanzibar yamesababishwa na kutopatikana kwa Katiba Mpya.

“CUF tungekuwa na uwezo hata leo tungetaka ashtakiwe haraka iwezekanavyo. Kwa sababu Kikwete ni mmoja wa watu aliyevuruga uchaguzi Oktoba 25, mwaka jana,” alisema Bimani.

Lakini Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vua Ali Vuai alisema maoni ya Jenerali si sahihi na si ya kiungwana kwa kuwa yana lengo la kuleta uchochezi kwa wananchi dhidi ya Kikwete.

“Huu ni upotoshaji kwa wananchi, kwa sababu Kikwete amefanya mambo makubwa nchini. Sioni sababu ya kusema fedha nyingi zimetumika wakati mchakato huu bado unaendelea, ukisubiri kupiga kura za maoni.

Hasheem Thabeet Afikiria Uwekezaji Michezoni

$
0
0
Mchezaji wa kikapu wa Tanzania aliyetamba katika  ya mchezo huo  kwenye Ligi ya Marekani (NBA) miaka michache iliyopita, Hasheem Thabeet  amesema madhumuni ya kuwapo nchini ni  kukutana na viongozi wa Serikali na kufanya mazungumzo nao kwa ajili ya kuangalia jinsi ya kusaidiana kuinua michezo nchini.

Akiwa NBA, Hasheem alizichezea klabu za Memphis Grizzlies, Houston Rockets, Portland Trail Blazers na Oklahona City Thunder.

 “Haiwezekani, Watanzania zaidi ya milioni 45 tushindwe kuwa na wachezaji wanaocheza nje ya nchi, ni kitu cha kushangaza,” alisema Thabeet.

Picha: Utaupenda Muonekano Mpya wa Chidi Benz, Mashabiki Wampongeza Babu Tale

$
0
0
Rapper Chidi Benz amefanikiwa kuirudisha afya yake baada ya kuachana na matumizi ya Madawa ya kulevya.

Mapema mwaka huu katika kituo kimoja cha runinga Chidi Benz alikiri kutumia Madawa ya kulevya na kuomba msaada ambapo meneja Diamond na Tip Top Connection, Babu Tale akishirikiana na Kalapina walimsaidia na kumpeleka katika kituo cha Bagamoyo Sober House ambacho kilimsaidia kuachana na Matumizi ya madawa ya kulevya.

Jumatano hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa picha mpya za rapper huyo zikimuonyesha jinsi alivyopendeza hali ambayo imewafanya mashabiki kumpongeza Tabu Tale.

Haya ni maoni ya baadhi ya mashabiki.

Sharifujuma00
Babu tale tunakushukuru sana mweyezimungu akulinde chidy kazaliwa upya kawa mtoto mchanga aendelee namsimamo huohuo wakuacha ngada

Abduly_iddy
Katik mameneja wote tz cjaon km ww @babutale mungu awe nawe nashangaa xn wanaokutuc labd hawajui umuhm wk ila umenifurahish kweny interview eeet matuc km vil wanakup juice 😂😂big up mzee


Official_thuwebseif
Wenimtu wapekee atakwamacho tu mtu akikutizama we nimtu safi watu km nyie mpo wachache allah akujalie kher na afya njema @babutale

Stambulya
Asante Babtale kutuludishia jembeletu na kuanzia sasa tunamuita Chiditele, si Chidbebenzi

Fauzinho1
May God bless you @babutale for what you did for Chidi Benz

Gendi3054
Thanks @babutale kwa hili… Mungu aendelee kukutumia na kwa wengine,,,, pls talk to ray c too.. I real believe it can work.

Manji Aendelea Kusubiri Majibu ya Barua Yake Aliyomwandikia Rais Magufuli Kuhusu Sakata la Coco Beach

$
0
0

Mwenyekiti wa Kampuni za Quality Group Limited (QGL), Yusuf Manji amesema bado anasubiria majibu kutoka kwa Rais John Magufuli juu ya sakata la kuendeleza ufukwe wa Coco, maarufu Coco Beach uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam baada ya kumwandikia barua Desemba mwaka jana.

Manji alisema anatamani suala hilo limalizike kabla ya kuondoka rasmi katika kampuni hiyo mwezi ujao, na kwamba tayari alishamwandikia barua kiongozi huyo wa nchi juu ya usahihi wa mchakato wa zabuni wa kuendeleza eneo hilo la ufukwe wa Bahari ya Hindi.

Mfanyabiashara huyo anasema anashangazwa na baadhi ya viongozi wa Serikali kurudiarudia suala hilo na kusababisha kuwa maarufu kuliko hata Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kwa mujibu wa mfanyabiashara huyo, suala la Coco Beach ilikuwa ni sehemu ya biashara na kwamba zabuni hiyo walishinda baada ya kutimiza masharti yaliyokuwa yamependekezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni, lakini cha kushangaza hali imekuwa tofauti.

Mfanyabiashara huyo alifikia hatua hiyo kufuatia Rais John Magufuli kutangaza eneo hilo liendelee kutumika na watu wa kawaida kwa kile alichosema kuwa kuna mfanyabiashara ambaye anatumia fedha kuwahonga baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo ili kumiliki eneo hilo.

Rais Magufuli ambaye alikuwa akihutubia mkutano wa wafanyabiashara alisema; “Inanifadhaisha sana kuona mfanyabiashara tajiri akihonga maofisa kutumia vibaya fedha za umma kwa manufaa yake binafsi na wakazi kutoka mazingira duni wakishindwa kutumia ufukwe huo kuogelea na kuburudika.”

Hata hivyo, Manji alisema kuwa kampuni yake ilikuwa ikilihitaji eneo hilo kuliendeleza kwa ajili ya biashara na kuhudumia wananchi hivyo iwapo Rais ataridhia linyang’anywe licha ya kushinda zabuni na mahakamani, hawatakuwa na hatua nyingine ya kufanya.

Alisema Rais aliyasema yake na Mahakama ilishafanikisha ushindi wa awamu ya kwanza na Serikali baadaye ilikata rufaa na kwamba mtu yoyote akitaka kusoma kwa nini walishinda kesi ya awali, hukumu iliyotolewa inajieleza.

Manji alieleza kuwa ingekuwa eneo lile linahitajika kwa matumizi binafsi hata wangemwambia aliachie na achukue Jangwani angekubali, lakini kampuni isingekubali kwa sababu eneo lile lilitafutwa kwa ajili ya biashara na mbadala wowote huenda usiwavutie wanahisa.

 “Coco Beach siyo nyumbani kwangu na wala siyo sehemu ambayo lazima niwe nayo au nisiwe nayo. Ni sehemu ambayo kampuni ilihitaji kwa ajili ya uwekezaji,” alisema Manji.

“Wanahisa walitaka kuwekeza lakini iwapo halitapatikana, hawajatufungia milango ya kiuwekezaji kwa kuwa Coco Beach siyo sehemu moja tu duniani ya kuwekeza.”

Tayari QGL ilishaingia ubia na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) mwishoni mwa mwaka jana kutekeleza mradi wa Dola 250 milioni za Marekani (Sh537.5 bilioni) kuendeleza eneo la Bwawani, kwa kuikarabati hoteli hiyo na kujenga mji wa kisasa ambao utakuwa na huduma zote za kisasa katika visiwa hivyo.

Tunafanyaje Hili la Naibu Spika Tulia Ackson Kukataliwa na Upinzani?

$
0
0
Ndugu zangu,
Swali hili lilipaswa wajiulize Wabunge wa upinzani wenye kutoka Bungeni kila baada ya dua ya asubuhi.

Kwa kufuatilia kwangu siasa za nchi hii na dunia, na kwa kuyaangaalia mahitaji ya wananchi kwa sasa, naona mkakati huu wa wabunge wa upinzani ni wa kimakosa.
Ni mkakati utakaokuwa na gharama zaidi kwa wapinzani huko tunakokwenda kuliko Chama cha Mapinduzi chenye wabunge wengi Bungeni.

Unapopanga kulifanya jambo ni vema ukatafakari pia matokeo ya jambo husika. Kwa sababu za kibinadamu, ikiwamo kupandwa na jazba na mengineyo, wapinzani kutoka Bungeni siku ile ya kwanza baada ya mtafaruku kuanza ingeeleweka kwa wapiga kura.
Lakini, kwa kuendelea kwao kutoka kila asubuhi ya siku ya kazi za Bunge walizotumwa na wapiga kura kwenda kuzifanya inaanza kujenga hisia miongoni mwa Watanzania, mimi mmojawapo, kuwa huko ni kukosekana kwa umakini.

Niliangalia Bunge lilipoanza jana asubuhi na hakika nilisikitika moyoni. Naamini, siko peke yangu, maana, hayo si matarajio ya Watanzania kuwa na wabunge watakaokuwa wakichaguliwa na kufanya mambo kama yale.

Kama nchi, hakuna namna yeyote ya kuikimbia mifumo na kanuni tulizojiwekea. Haina mashiko, hoja ya kumkataa mtu katika nafasi yake na ambaye hajafanya lolote linalomtaka ang'atuke kwa mujibu wa kanuni, sheria na taratibu zetu kimfumo.

Yanapotokea mapungufu ya kimfumo ndani ya kanuni, sheria na taratibu zetu mahali pekee kwa kuanzisha jitihada za kuyabadili hayo ni ndani ya Bunge au Mahakamani. Si kwenye viwanja vya Bunge. Na kwa ilivyo sasa hakuna namna, Wabunge wanaotoka itafika siku itawalazimu wabaki tu ndani ya Bunge na Naibu Spika huyo huyo. Tatizo hapa watakuwa wamepoteza muda mwingi nje ya Bunge badala ya kuwa ndani na kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi kupitia Bunge.
Hii ni Nchi Yetu sote. Iko siku wapinzani ndio watakaounda Serikali na Spika au Naibu Spika atatoka miongoni mwa wapinzani wa sasa.

Kama wabunge wa CCM watafanya haya ya kutoka bungeni kwa vile tu hawatampenda au kumtaka Spika, basi, kwa namna hii hii, tutawashutumu wabunge hao wa CCM kwa wakati huo.
Maggid Mjengwa,
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images