Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live

Mtoto Aliyewekewa ‘mashine’ kwenye Moyo Aanza Mazoezi

$
0
0
Mtoto Happiness John Mkazi wa Seliani Arusha aliyefanyiwa upasuaji kwenye moyo na kupandikiziwa kifaa cha kusaidia kudhibiti mapigo ya moyo (pacemaker), ameanza mazoezi.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto, Sulender Kuboja aliyeshiriki upasuaji huyo alisema jana kuwa hali ya mtoto huyo inaendelea vizuri na wameanza kumfanyia mazoezi mepesi.


Dk Kuboja alisema kwa kawaida mgonjwa yeyote aliyefanyiwa upasuaji anapaswa kufanyiwa mazoezi mepesi na kwamba kwa mtoto, mazoezi anayofanyiwa ni ya kukaa, kusimama na kutembea kidogo.

“Hali yake inaonekana kuendelea vizuri sana... nimetoka kumfanyia vipimo muda mfupi uliopita kifaa kile kinafanya kazi vizuri na maendeleo yake yanaridhisha sana,” alisema Dk Kuboja.

Alisema mtoto huyo anaweza kuongea na hata kula chaku- la, hali aliyosema inaonyesha nafuu nzuri kwake.

Mama mzazi wa mtoto huyo, Elitruda Malley alisema anaridhishwa na maendeleo ya afya ya mwanaye kwa kuwa tangu afanyiwe upasuaji huo juzi, hali yake imeonekana kuimarika kwa haraka.

Mama huyo alisema tangu awekewe kifaa hicho, mwanaye amekuwa mchangamfu, hali aliyosema inamtia moyo na kumpa matumaini makubwa.

“Ingawa yupo kwenye oxygen, lakini namshukuru Mungu kwani anaonekana anapata nafuu nzuri, anatabasamu na kuongea vizuri kabisa na ana furaha sana, shauku yake ni apone ili aende shule kama watoto wengine,” alisema Malley.

 Aliongeza kuwa mtoto huyo amekuwa akila vizuri na kumpa moyo kwani mwili wake unaonekana kuwa na nguvu na afya nzuri.

“Madaktari wapo karibu wakifuatilia afya ya mtoto kwa ukaribu, wanampa chakula, wanamfanyia mazoezi ya kukaa na kushuka chini, anaonekana kuwa na nguvu na mwenye maendeleo mazuri. "

Alisema jambo linalompa faraja ni kuona jinsi madaktari wote wanaomuhudumia mtoto huyo wanavyofanya kazi hiyo kwa upendo na bidii.

Juzi, kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ilifanikiwa kumpandikiza mtoto huyo mwenye umri wa miaka mitano kifaa cha kusaidia kudhibiti mapigo ya moyo (pacemaker) kinachoendeshwa kwa betri.

Hayo ni mafanikio ya pili kwa taasisi hiyo ya kisasa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati baada ya Mei 24 na 25, mwaka huu kufanikisha operesheni kwa wagonjwa 18 bila kuusimamisha moyo.

Taarifa za Jerry Muro Kuteuliwa Kuwa Msemaji Msaidizi wa Ikulu, Jerry Asema Haya

$
0
0
Ule ujumbe wa Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga, Jerry Muro kuwa ameteuliwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa msemaji msaidizi wa Ikulu imezua gumzo kubwa.
Ujumbe huo umesambaa kwenye mitandao kibao ya kijamii hasa Whatsapp, Instagram na Facebook ukionyesha Muro atakuwa msaidizi wa Mkurugenzi Msaidizi wa Mawasiliano Ikulu chini ya Gerson Msigwa.

Hata hivyo, Muro amezungumza na SALEHJEMBE usiku huu na kuthibitisha kuwa taarifa hizo ni uzushi mtupu.

“Hakika ni uzushi, kwanza ile akaunti ya Twitter iliyoanza kusambaza si yangu,” alisema Muro ambaye tayari TFF imetangaza kumfungia huku ikiwa haijatoa hukumu.

UJUMBE ULIVYO…

USIEMPENDA KAJA!!!!!!!!
BREAKING NEWS
 Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemthibitisha Ndg Geryson Msigwa kuwa mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu huku msaidizi wake akiwa ni aliyekuwa msemaji wa Klabu ya soka ya Yanga Ndg Jerry Cornel Muro.

Mtanzania Awekwa Bondi na kaka yake kisa Madawa ya kulevya huko India. Sambaza Habari hii iwafikie ndugu zake

$
0
0
Mtanzania amuweka mdogo wake Bondi kwaajili ya Madawa ya kulevya huko INDIA sasa wenye mzigo wamecharuka wanataka pesa zao hali sio nzuri kabisa kwa mdogo mtu Haya ndio maneno yalio sikika akiyasema Mdogo mtu kwenye Video hii.

“Nakaa Magomeni  Mtaa chem Chem na Idrisa kwa hiyo Mwambieni  Juma, Mama yangu anaitwa Rukia Daudi Baba yangu anaitwa Akida anakaa idrisa na Chem Chem mwambieni  Juma amekula Hela za watu mimi kaniweka Gelenta huku ( Bondi ) mama yangu anaitwa Rukia Daudi mama yake mama yake Juma anaitwa Mariamu Rauwa kwaiyo juma afanye arudishe hela za watu Juma anakaa Kunduchi”. kama unamfahamu huyo Juma mama yake mfikishie ujumbe huu..

Sambaza Habari hii imfikie JUMA na ndugu zake kokote walipo..


 Angalia Video hii Hapa..

Babu Tale Afunguka..Niliitwa Mwizi Kuwa Nawaibia Wasanii Ninaowasimamia..Wakanikimbia

$
0
0
Meneja wa Diamond Platnumz na Tip top Connection, Babu Tale amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi waliondoka kwake kwa maneno ambayo walikuwa wakiambiwa mtaani na wananchi kuwa ana wasimamia huku akiwaibia pesa zao.

Babu Tale alisema haya kupitia kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio na kudai wasanii hao waliamua kuondoka chini ya uangalizi wake lakini kwa sasa wana maisha mabovu na yeye ana maisha mazuri.

“Unajua mtaa ndiyo uliwaambia wasanii waliondoka kwangu kuwa Babu Tale mwizi, na wakaaondoka Tip Top Connection lakini sasa hivi wasanii hao hao walioondoka kwangu wao wana maisha mabovu, wakati mimi na maisha mazuri. Wanakuja kwangu saizi wanataka niwasimamie kazi zao lakini mimi nasema sasa siwezi kwani wasanii nilio nao wananitosha” alisema Babu Tale.

Mbali na hilo Babu Tale alitoa ufafanuzi juu ya ukimya wa msanii Tunda Man na kusema kuwa wakati wake bado haujafika ila ukifika atarudi tu kwenye game na kudai kuwa saizi wana mpango wa kuachia ngoma nyingine ya Dogo Janja.

Marufuku Watumishi wa Serikalini Kuwa na Tenda Serikalini

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene amesema serikali tayari imekataza watumishi wa umma kujiingiza katika kuomba tenda mbalimbali za serikali na hawaruhusiwi na kama mtu anajihusisha na jambo hilo basi anakiuka misingi ya sheria

Waziri Simbachawene ameyasema hayo kwenye mahojiano maalumu na East Africa Radio kuhusu baadhi ya watendaji wa umma ambao wanamiliki kampuni ambazo zinashiriki kufanya tenda ya serikali na zimekuwa zikifanya vibaya na kusababisha malumbano baina ya wanachi na halmashauri mbalimbali nchini.

Amesema wamezuia swala hilo kisheria ili kuepuka usumbufu ambao umekuwa ukijirudia mara kwa mara pindi serikali ifanyapo ukaguzi wa utekelezaji wa kampuni hizo sambamba na kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu utendaji kazi wa kampuni hizo, ambazo zinakuwa zimepewa tenda na halmashauri mbalimbali nchini.

Amewataka wakurugenzi na viongozi wa mikoa kuzingatia sheria ya manunuzi inavyoelekeza na tayari wameanza uchunguzi kuwabaini watendaji wasio waaminifu juu ya swala hilo na pindi watakapogundulika kuhusika na swala hilo serikali itachukua hatua za kisheria.

Ametoa wito kwa watumishi wote wa serikali kutokujihusisha na swala hilo na wazingatie katika kusimamia haki na usawa kwa watanzania ambao ndiyo walipa kodi na watumiaji wa huduma mbalimbali za serikali.

Rais Magufuli Anaishi Kwenye Maneno Yake Hana Longo Longo - Mrema Afunguka

$
0
0
Mwenyekiti wa TLP Dkt. Augustino Lyatonga Mrema amesema Rais Dkt. John Magufuli anaishi kwenye maneno yake kwa kuwa mwaka jana alipofika kwenye jimbo la Vunjo aliwaambia wananchi wamchague Mrema na wasipomchagua atampa kazi, jambo ambalo ametimiza

Mrema ameyasema hayo alipofanya mahojiano maalum na EATV kuhusu uwezo wake wa kusimamia Bodi ya Parole ambayo yeye ndiye mwenyekiti wake baada ya kuteuliwa na Rais Dkt. John Magufuli.

''Nafasi ambayo amenipa Rais Dkt. Magufuli nina uzoefu nayo kwa kuwa mwaka 1994 njia tuliyokuwa tunaitumia ni kutembelea magereza na kuongea na wafungwa hasa wanaotumia vyombo vya moto na wengine walikuwa wanataja walipoficha silaha, na wengine walikuwa wanataja wahalifu ndani ya jamii na nilipata ushirikiano wa kutosha.''

Aidha Dkt. Mrema amesema anachokitafuta Rais Dkt. John Magufuli ni mtu mzalendo na hatua ya Rais kumteua ni kuonesha imani yake kwake na si kwamba ana nia ya kuua upinzani bali ana lengo jema la kuchukua mtu mwenye uzoefu ili atumikie watanzania kwa sababu lengo la upinzani siyo kutaka wananchi wateseke.

''Watanzania wategemee ufanisi na kazi iliyotukuka ya kupunguza wafungwa magerezani ili waweze kupewa adhabu nyingine ndani ya jamii na wapewe watu wa kuwasimamia, kwa kuwa tatizo kubwa tulilonalo sasa hivi ni mlundikano wa wafungwa na serikali haiwezi kujitika kutanua magereza kwa kuwa sasa hivi inajikita kuboresha huduma za afya na elimu mfano suala la madawati'' Amesema Dkt. Mrema

Kuhusu yeye kuwa mzee na kama ataweza kumudu nafasi hiyo Dkt. Mrema amesema yeye ana miaka 72 na hana uzee wowote ambao utamfanya akwame kufanya kazi hiyo kwa ufanisi na hata kabla ya uteuzi Rais ana watu wa kumshauri na wameona anafaa nafasi hiyo

Taarifa Kamili Kuhusu Habari ya Rais Magufuli Kumteua Jerry Murro Kuwa Msaidizi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu

$
0
0
Baada ya taarifa kuenea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Rais John Pombe Magufuli amemteua Jerry Murro ambaye alikuwa afisa habari wa Yanga kuwa msaidizi wa mawasiliano ya Rais Ikulu, kurugenzi ya mawasiliano imekanusha habari hizo na kusema kuwa sio za kweli.

Barua iliyoandikwa kutoka Ikulu imesema ‘kuna taarifa zimesambazwa zikisema kuwa Rais Magufuli amemthibitisha Gerson Msigwa kuwa mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu huku msaidizi wake akiwa ni aliyekuwa msemaji wa klabu ya Yanga Jerry Murro, taarifa hizo sio za kweli na wananchi wazipuuze'


PICHA Zikionyesha Jinsi Raia wa Uturuki Walivyowachapa Wanajeshi Baada ya Kujaribu Kumpindua Rais wao Kipenzi

$
0
0
Furious civilians attack soldiers who were involved in the coup attempt after they surrendered on Istanbul's landmark Bosphorous Bridge
Soldiers involved in the coup attempt in Turkey surrender on Istanbul's Bosphorus Bridge with their hands raised on Saturday.
Soldiers cower from angry civilians after the apparently failed coup in Turkey.
.
People stand in front of a tank near the Fatih Sultan Mehmet Bridge during clashes with military forces in Istanbul early on July 16.
Turkish tanks move into position as Turkish people attempt to stop them in Ankara.
A man uses his belt to hit Turkish soldiers involved in the coup attempt.

Madaktari Waliogundua Vipandikizi vya Kansa Kwenye Chanjo Wameuliwa

$
0
0
Si mda mrefu kupita Neon Nettle walitoa taarifa jinsi madaktari wanavyouliwa, wengi wao wakitokea Florida,Marekani

Wataalamu hao waligundua kwamba nagalase enzymes protein iliongezwa katika chanjo. Nagalese inazuia uzalishwaji wa vitamin D mwilini, ambayo mwili unahitaji sana hivyo vitamin kujikinga na kuua seli za kansa.

Vilevile inasemekana Protein ya Nagalase inatumika kuunda viini vyote vya saratani.
Protini hii pia hupatikana katika viwango vya juu sana katika watoto wenye ugonjwa wa akili
Nagalase inazuia mwili kutumia vitamin D ambayo inasaidia kupambana na saratani na matatizo ya akili kwa watoto.

Kupunguza watu na kuweka sumu kwenye chanjo....ni kama sheria lazima mtoto achomwe hizo sindano. Jinsi wanavyoua wanavyotengeneza dawa za kuua taratibu, Wakidhani wao wataishi milele, Watu hawa hawana mioyo ya huruma.

Maalim Seif Kitanzini, Jeshi la Polisi Lasema Litamkamata na Kumshitaki kwa Uchochezi Zanzibar

$
0
0
MKUU wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Ernest Mangu amefunguka kuhusu mambo juu ya utendaji wa jeshi hilo na kueleza kuwa wakati wowote litamburuza mahakamani Katibu Mkuu wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad kwa kuhamasisha uchochezi visiwani Zanzibar.

Amebainisha kuwa jeshi hilo, kamwe halikandamizi wala kuonea chama chochote cha siasa, kwani limekuwa likitekeleza wajibu wake kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo.

Akizungumza katika mahojiano yaliyofanyika kwenye kipindi cha Funguka, kinachorushwa na Kituo cha Televisheni ya Azam jana, IGP Mangu alisema hali ya siasa Zanzibar ilikuwa shwari katika chaguzi zote mbili na kwamba machafuko na vurugu vilianza kutokea baada ya uchaguzi wa pili.

Alisema vurugu hizo zilianza baada ya kubainika kuwa Maalim Seif, alikuwa akifanya mikutano ya ndani na mingine ya chini kwa chini na wafuasi wake katika maeneo ya Kaskazini na Kusini.

“Kwa sababu ilikuwa ni mikutano ya ndani, Polisi hatukuona tatizo na wala hatukumzuia, tuliona ni mwananchi anataka kuzungumza na wafuasi wake, tukasema mwache aongee nao tu,” alisema IGP Mangu.

Alisema baadaye jeshi hilo liligundua kuwa kiongozi huyo wa CUF, alikuwa anawachochea wananchi waichukie serikali iliyopo madarakani na wapinzani wao ambao ni Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwafanyia uhalifu.

Alisema baada ya vikao hivyo vya Maalim Seif, visiwani humo kukaanza kuibuka matukio ya vurugu kama vile mashamba kuchomwa moto na mazao kung’olewa.

“Haya mambo hayakutokea kabla ya vikao vya Seif, yalitokea baada ya vikao vyake,” alifafanua mkuu wa polisi.

Alisema wafuasi hao walichochewa, kiasi cha kususa hadi shughuli za kijamii, kama vile misiba na wakati mwingine ilifikia hatua ya kususa kuwauzia bidhaa wafuasi wa CCM.

“Tukasema kama wameona kugeuza biashara zao siasa, basi waendelee tu. Biashara inadumu kwa sababu unatengeneza faida, sasa kama umeamua kuchagua wa kumuuzia ni shauri yako. Hawa tuliwaacha kwa sababu tuliona hawana makosa,” alisema.

Hata hivyo, alisema jeshi hilo kamwe halikuwanyamazia wahalifu waliochoma na kung’oa mazao kwenye mashamba ya wenzao, eti tu kwa kigezo cha ufuasi wa chama au siasa.

“Hawa tuliwakamata na wapo wengine tunaendelea kuwatafuta, watakapoacha ndio hatutawatafuta. Wale wahalifu ndio tunaowatafuta. Pengine kwa sababu ya siasa wanadhani Polisi tunawaonea wananchi tunawakamata bila sababu. Sasa hawa watu tunawaoneaje wakati tunawapeleka mahakamani?” Alihoji.

Maalim Seif kuhojiwa
Alisema kutokana na matukio hayo, tayari Maalim Seif amehojiwa na jalada lake halijaamuliwa, lipo kwa Mwendesha Mashtaka wa Serikali (DPP) Zanzibar. “Lakini pia tunataka tumpeleke mahakamani kumshitaki kwa makosa aliyofanya ya kuchochea fujo,” alieleza.

Alisema kazi kubwa ya Polisi kwa sasa si kujiingiza kwenye siasa au kupatanisha pande mbili zinapokwaruzana, bali kazi yake ni kuhakikisha inadhibiti na kuwakamata wahalifu.

Alisema endapo vyama viwili vinavyolumbana visiwani Zanzibar, vitaamua kuchukua hatua za kisheria kumaliza tofauti zao, polisi haina tatizo, lakini endapo vyama hivyo vitachukua hatua za kijinai au kukomoana, jeshi hilo halitokaa kimya.

“Kazi ya polisi iko wazi, tunakamata tunapeleleza na kupeleka mahakamani umma unatuona tunachofanya hatuna cha kuficha,” alisisitiza.

Maandamano na mikutano
Akizungumzia madai ya jeshi hilo kukandamiza demokrasia na wapinzani kwa kudhibiti shughuli za siasa nchini, IGP Mangu alisema hakuna mwanasiasa au chama chochote, kilichozuiwa kufanya shughuli zake, ikiwemo mikutano.

Alisema kinachotakiwa ni kwa mwanasiasa au chama hicho, kupeleka maombi yake Polisi kwa mujibu wa sheria na baada ya jeshi hilo kufanyia tathmini maombi hayo, endapo yataonekana hayana tatizo yataruhusiwa kuendelea.

Alisema endapo jeshi hilo linazuia shughuli za kisiasa, hutokana na uchunguzi au tathmini lililofanya na kujiridhisha kuwa shughuli husika si salama na inatishia usalama wa raia.

“Unajua unapozungumzia masuala hayo tuwe makini kidogo, kwa sababu hapa kuna watu wa aina mbili kuna wanaofanya siasa na sisi watendaji tunaotekeleza sheria. Ila sisi pia hatuko juu ya sheria, kama kuna mahali tunakiuka upo utaratibu wa kutushughulikia,” alisisitiza.

Alisema hata katika suala la kuzuia shughuli za kisiasa, kama vile mikutano na maandamano endapo, kuna chama au mwanasiasa anahisi kuwa jeshi hilo, halikutenda haki au limeenda nje ya mstari, taratibu zinamruhusu kukata rufaa kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais na Mahakama.

Hata hivyo, alisema jeshi hilo halifanyi jambo lolote nje utaratibu wa kisheria, akifafanua, “lakini sisi hatuwezi kujiingiza kwenye siasa kwa sababu sisi sio wanasiasa, pia hatuwezi kuzuia wanasiasa kulumbana kwa sababu ni uwanja wao wa kulumbana. Sasa kama tulitoa maelekezo fulani basi ujue tulikuwa tunatekeleza sheria na utaratibu uliopo.”

“Sidhani kama sisi tunakandamiza upinzani, tunachofanya sisi ni kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na watu wako huru kama wanafikiri tumeenda nje ya mipaka yetu wakatuchukulie hatua,” alisisitiza.

Alitoa mfano wa matukio yaliyozuiwa na Polisi kwa sababu za kiusalama kuwa ni pamoja na mkutano wa mahafali wa Dodoma, ambao ulifanyika siku moja na mkutano wa mahafali uliofanyika Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam ambao wenyewe haukuzuiwa. Yote ilikuwa mikutano ya wanafunzi wafuasi wa Chadema.

“Kama sisi tuna sera ya kuzuia, mbona wa Karimjee hatukuuzuia? Dodoma kulikuwa na sababu na imeelezwa na viongozi wa Dodoma. Hii si sera yetu, usichukulie mkutano mmoja kuzuiwa basi ndio yote nchi nzima imezuiliwa. Haiwezekani,” alifafanua.

Alisema sheria inazungumzia wanaohitaji kufanya mkutano au kufanya maandamano, wanatoa taarifa kwa mkuu wa polisi wa hilo eneo, na mkuu huyo ataangalia kama mazingira yanaonesha hakuna tatizo, mkutano utaendelea, kama kuna tatizo atauzuia.

“Sasa ni wapi sisi tumefanya kitu ambacho ni kinyume na tunaonekana tunakandamiza upinzani? Na ikumbukwe kuwa kuna mikutano baadhi iliombwa tukaizuia kwa sababu kipindi hicho kulikuwa na kelele za mauaji Mwanza, Sengerema, Tanga mpaka tunahojiwa Polisi mko wapi,” alisema.

Alisema wakati Polisi ikihojiwa kuhusu dawa ya mauaji, baadhi ya vyama viliwasilisha maombi ya maandamano.

“Hivi kweli? Kwanza mauaji yenyewe mtindo wake ni mpya unajuaje kama wanaoomba wangeenda nao kuvamiwa? Lazima tuchukue tahadhari,” alisema na kuongeza kuwa Polisi imepewa jukumu la kisheria kuhakikisha panakuwepo na amani.

“Sasa tunapochukua hatua kuhakikisha kuna amani, naomba tuvumiliane. Msione kuna amani, basi mkajua ipo tu na ni ya kudumu, mjue kuna wengine wameumia kuhakikisha hiyo amani inakuwepo. Lazima iwe hivyo ndio utaratibu wa kuongoza nchi, sisi hatubagui wala kukandamiza chama chochote,” alieleza IGP Mangu.

Matumizi ya nguvu
IGP Mangu alisema si kweli jeshi hilo limekuwa likitumia zaidi nguvu katika kudhibiti vurugu na kubainisha kuwa nguvu hutumika, pale tu inapobainika kuwa upande wa pili unaodhibitiwa nao unatumia nguvu.

Hata hivyo, alisisitiza kuwa Polisi nchini imekuwa ikitekeleza wajibu wake vyema bila kukandamiza wala kutumia nguvu, kwani hata taasisi ya kimataifa iliyofanya tathmini juu ya utendaji wa jeshi hilo katika uchaguzi mkuu nchini ilibainisha kuwa jeshi hilo lilifanya vyema.

Polisi na rushwa
Akizungumzia tuhuma zinazorushiwa Jeshi la Polisi kwamba kuna baadhi ya askari wake, wanatuhumiwa kwa rushwa, alisema askari hawana mamlaka ya kula rushwa na kujilimbikizia mali halafu wasiguswe na mtu.

“Hili haliwezekani. Kwa hiyo nasema bado wananchi wanaweza wakasaidia kama kweli wanazo taarifa za Polisi na zitafanyiwa kazi. Kama hawaamini kama sisi wenyewe hatuwezi kudhibitiana, vipo vyombo vingine vinaweza kufanya hivyo,” alisema.

Hata hivyo, alisema wapo askari Polisi wenye maisha mzuri kwa maana ya nyumba na magari, ambao wamepata mali hizo kupitia taasisi mbalimbali za mikopo ikiwemo Saccos ya Polisi, ambayo ndio kubwa nchini.

“Askari polisi kumiliki gari nzuri si kosa, la msingi amepataje hilo gari, kama kuna polisi ana mali au gari isiyo na maelezo tuleeteni, polisi hazuiliwi kuwa na gari nzuri. Siku hizi kuna taasisi nyingi zinakopesha anaweza kukopa,” alisisitiza.

Kashfa ya Lugumi
Akizungumzia suala la kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises Ltd inayomilikiwa na mfanyabiashara Said Lugumi, IGP Mangu alisema suala hilo lilichukuliwa na Bunge na kufanyiwa uchunguzi hivyo, matokeo ya uchunguzi hawezi kuyazungumzia.

Alisema anachoweza kukizungumzia ni maelekezo ambayo jeshi hilo limepatiwa na Bunge, ambayo ni kukamilisha yale ambayo hayajakamilishwa.

“Tunaendelea kuchukua hatua za kukamilisha.Kuhusu uchunguzi kazi ilifanywa na Bunge kwa anayetaka anaweza kuwasiliana na Bunge na kupatiwa matokeo kwa kuwa naamini Bunge linawakilisha wananchi, taarifa zao ziko wazi,” alisema.

Kuwa Tajiri kwa Mtaji wa Laki 3 tu, Kupitia Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji

$
0
0
LEO TUANGALIE MCHANGANUO WA TSHS 300,000/= (LAKI TATU) KWA KUANZISHA MRADI WA UFUGAJI KUKU WA KIENYEJI.

Hapa tuta hitaji kuku 11 tu wakubwa wanao taga yani majike 10 na Jogoo 1 tu. Kwa kutumia kuku hao 11 baada ya miezi mitatu unaweza ukawa na kuku mia Tatu 300 au na zaidi kama unataka.
Nunua kuku wako katika chanzo cha kuaminika kuepuka magonjwa usinunue kuku sehemu za masokoni au kwenye mabanda ya njiani au kuku wanao safirishwa kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine.

Unapo nunua kuku wakubwa kwanza unapo wafikisha wape chanjo ya mdondo (Newcastle vaccine) ili kuweka rekodi yako ya chanjo maana chanjo hii hurudiwa kila baada ya miezi 3. Ukumbuke tarehe uliyo wachanja na tarehe utakayo wachanja tena baadae.

Usinunue kuku kabla hujaandaa banda na Chakula.
Katika sh. 300000 toa sh.69500 ambayo utanunua Chakula cha kuku, kuku hawa hawana formula ya Chakula hivyo unaweza kununua material ukachanganya Chakula mwenyewe ampapo utaokoa pesa nyingi pia.

Mchanganuo Wa 69500 ni:-
Pumba gunia 1. Shs.20000 gunia la pumba lina kilo 70.

Paraza kilo 25 = 700x25 =17500. Paraza ni mahindi yaliyo vunjwa vunjwa kwaajili ya Chakula cha kuku.
Mashudu ya alizeti kilo 15. 700x15=10500
layer's consetraite

Kilo 25 kifuko. = 21500.

Ukijumlisha utakuwa umepata kilo 135 kwa shs 69500. Ambapo kila kilo moja ya Chakula utakuwa umenunua kwa shiling 514.8.

Chakula hicho kichanganye kwa kutumia chepe kichanganye vizuri kichanganyike pumba lazima iwe kavu kabisa ikaushe usiwape kuku pumba mbichi.

Kumbuka kuku anayetaga anakula Gram 130 kwa siku
Hivyo kuku 10 watakula kilo 1.3 kwa siku ambayo ni gram 1300.
Hivyo tutaweza kuona Chakula chetu kitatupeleka zaidi ya siku 100 ya zaidi ya miezi mitatu.

TOA SHS 170000 AMBAYO UTANUNULIA KUKU.
Mchanganuo wake Kwa kila kuku mzuri ambaye ajazeeka anayetaga utampata kwa shilingi 15000 na Jogoo nzuri utampata kwa shilingi 20000.

Jogoo 1 = 20000
Majike 10 x15000= 150000 jumla 170000.
Itakuwa imebaki shs. 60500

-Hii pesa iliyobaki ni kwa ajili ya kununu material ya bei nafuu na kutengeneza banda la kuku 10 hadi 20. Kuku hawa hawaitaji banda Kubwa kwasababu hawashindi ndani wataingia ndani wakati Wa kulala jiaoni na mchana wakati wakutaga Kuku wachiwe eneo la kutosha na lenye mchanga watakao itumia kuoga kuondoa wadudu km papasi na utitiri sehemu wanayopenda kuoga nyunyizia Dawa ya utitiri.

Banda tengeneza la kuhamisha la futi 4x8x4 yani urefu kwenda juu futi 4 upana futi 8 kipenyo futi 4. Tumia materio yaliyo karibu nawe kama mirunda, mabanzi, Mabati reject au yaliyochakaa chicken wire au wire mesh, fito mbao 2x2 au 4x2 n.k. Kama ni sehemu za mjini litakugharimu kama Tsh 50,000-60,000.Vijijini au nje ya mji ambapo miti ni mingi litakugharimu Tsh 25,000 hadi 35,000.
Haya jinsi ya kuwaendeleza hao kuku ili kupata kuku wengi hadi utakao wataka. Hapa itabidi ukubali kupeleka Mayai sehemu ambapo wanatotolesha ambapo trey 1 ni shilingi 10000.

Hapa kuku hawa 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku ambapo kwa mwezi ni Mayai 240. Kila baada ya siku 7 peleka Mayai kwenye Mashine yakutotolea (incubator). Hivyo kwa mwezi utapeleka Mayai 240 utapata wastani Wa Vifaranga 200. Hivyo baada ya mwezi nakushauri usitotoleshe tena hao Vifaranga 200 ni wengi sana kwa kuanzia kwa kuwa tayari tunenunua Chakula cha kuku cha kutupeleka miezi mitatu basi Mayai utakayo endelea kuokota utayauza kwaajili ya kupata hela ya Chakula cha Vifaranga watakao toka hao zaidi ya 200. Hivyo mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe.

Nikiwa na maana kama kuku 10 watakupa wastani Wa Mayai 8 kwa siku na Mayai 240 kwa mwezi ni wazi kwamba kuku hao wanakuingizia 120000 kwa mwezi ambaya sasa hela Hii itatumika kununua Chakula cha kulea hao Vifaranga ambapo Mayai ya mwezi tu yataweza kununua Chakula ambacho Vifaranga 200 watakula mwezi pamoja na chanjo na Dawa zote.

Hivyo baada ya miezi mitatu utakuwa na Vifaranga wakubwa Wa miezi miwili na Chakula cha kuku wakubwa ndo kitakuwa kinaishia hapa utachanganya Chakula cha aina moja tu wale Vifaranga watakuwa wameshakuwa kiasi cha kula Chakula chochote.

Waziri Mkuu Apiga Marufuku wanafunzi kutumia viberit na mishumaa mabwenini

$
0
0
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku matumizi ya viberiti, mishumaa na hita za kuchemshia maji kwa wanafunzi wa bweni ili kuepusha majanga ya moto na atakayekutwa, atachukuliwa hatua kali.

“Kuna tabia ya baadhi ya wanafunzi hasa wa masomo ya fizikia kutengeneza vifaa vya kienyeji vya kuchemsha maji mabwenini, jambo hili ni la hatari kwani linaweza kusababisha ajali ya moto, hivyo ni marukufu kwa mwanafunzi kutumia vifaa hivyo,” alisema.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana katika harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa majengo ya Shule ya Sekondari Lindi, yaliyoungua moto usiku wa kuamkia Julai 10, mwaka huu.

Katika ajali hiyo shule imeathirika kwa asilimia 34 baada ya vyumba tisa vya madarasa, jengo lenye matundu 26 ya vyoo na jengo la maabara ya kemia na fizikia yameungua na kusababishia hasara ya Sh milioni 682.78.

Waziri Mkuu alisema kwa namna ambavyo majengo hayo yameungua, ni vema yakavunjwa na kujengwa upya. Aliwataka kutumia nafasi hiyo kujenga jengo la ghorofa ili kutumia eneo dogo kwa kujenga madarasa mengi.

Pia alimuagiza Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi kuhakikisha fedha zitakazopatikana katika harambee hiyo, zinatumika kama ilivyokusudiwa.

Harambee ilihudhuriwa na mke wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa, mke wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Mama Salma Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendego na wadau wa maendeleo na wanafunzi waliosoma shule hiyo akiwemo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amezitaka taasisi mbalimbali nchini kufunga vifaa vya kuzimia moto katika majengo yao kwa ajili ya kuvitumia pindi ajali za moto zinapotokea.

Auawa Kwa Kukatwa Kichwa..Kiwiliwili Chatelekezwa Bila Kichwa

$
0
0
Mtu mmoja amefariki dunia kwa kukatwa kichwa na kiwiliwili chake kutelekezwa kichakani katika Kijiji cha Rushwa, Kata ya Mushabago, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Buyango, Gasper Joseph amesema wamelazimika kuita wananchi ili kuutambua mwili wa marehemu.

Amesema licha ya kiwiliwili kutelekezwa kwenye eneo la kichaka, kichwa cha marehemu huyo wa kiume hakikuwapo kwenye eneo hilo jambo ambalo alilosema limeleta hofu kwa wananchi.

“Nimeita watu na walikusanyika, hata hivyo walishindwa kuubaini mwili huo kwa kuwa kichwa chake hakikuonekana. Mwenyekiti wa Kijiji cha Rushwa alitoa taarifa polisi kwa ajili ya hatua zaidi ili turuhusiwe kuzika,” amesema Joseph.


FAIDA za Wana Ndoa Kufanya Tendo la Ndoa Angalau Mara Tatu Kwa Wiki Hizi Hapa

$
0
0

Utafiti umebainisha kwamba kufanya mapenzi angalau mara tatu kwa wiki kunapunguza uwezekano wa kupatwa Heart Attack (Shambulio la Moyo) kwa 50% ukilinganishwa na yule ambaye anapitisha wiki nzima bila kupiga mambo yetu. Pia utafiti huo unasisitiza ya kwamba mwenye Kufanya Mapenzi killa siku anaondoa uwezekano wa kupata Heart Attack kwa Asilimia 100%

ZIJUE FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI

Kiafya
Tendo la ndoa ni moja kati ya mazoezi ya mwili. Wataalamu wanasema kwamba, unapofanya tendo hilo mara tatu kwa wiki husaidia kupunguza kiasi cha mafuta mwilini na pia endapo mtu
atafanya tendo mara tatu kwa wiki kwa kipindi cha mwaka mzima ni sawa na kukimbia maili 75.

Tendo la ndoa huongeza takriban vizalisha nguvu 150 kwa nusu saa ambayo ni sawa na kukimbia dakika 15 kiwanjani.

Kuongeza mwendo wa damu
Tendo la ndoa husaidia kuongeza kasi ya mtiririko wa damu kwenye ubongo na sehemu nyingine ya viungo vya mwili, hii huchangia kuongeza kasi ya mapigo ya moyo na kuboresha mfumo wa upumuaji. Msukumo thabiti wa damu mpya yenye oxygen na homoni zenye chembe chembe hai zinapopenya kwenye mishipa ya damu husaidia katika uunguzaji wa chakula, pia huondoa kiasi cha uchafu ambao ungesababisha mishipa na kushindwa kufanya kazi na kumfanya mwanadamu apate maumivu ya mwili.

Hupunguza mafuta yenye kileo (Cholesterol)
Tendo la ndoa huweka sawa uwiano wa mafuta yenye kileo (Cholesterol) nzuri na cholesterol mbaya na wakati huo hupunguza kwa ujumla kiasi cha mafuta yenye kileo mwilini.

Kupunguza maumivu
Wakati wa kufanya mapenzi, homoni iitwayo oxytosin huzalishwa mwilini ambayo husababisha kuzalishwa kwa homoni iitwayo endorphin ambazo hupunguza maumivu kama vile kuvimba sehemu za viungo (arthritis) maumivu ya shingo (Whiplash) na maumivu ya kichwa.

Ulinzi wa tezi ya kibofu (mwanaume)Majimaji yanayozalishwa katika tezi ya kibofu (prostate) yakizidi husababisha kuleta matatizo mwilini. Tendo la ndoa la mpangilio huondoa uzalishaji wa majimaji hayo yenye madhara.

Mabadiliko ya ghafla ya tendo la ndoa huelekea kuleta matatizo yahusianayo na tezi ya prostate.

Kupunguza mfadhaiko wa moyo
Kujitosheleza na kupumzisha mwili baada ya tendo la ndoa ni muhimu kwa kutuliza akili na kurekebisha mzunguko wa damu mwilini. Watu wenye kushiriki tendo la ndoa wanatajwa kushinda mfadhaiko na kupata usingizi mnono hasa mara baada ya kumaliza kufanya mapenzi.

Huongeza uzalishaji wa homoni za kiume(testosterone) na za kike (Oestogen)
Faida nyingine inayopatika ni kuongeza uzalishaji wa homoni za kiume na za kike likiwemo suala zima la msukumo wa kufanya tendo hilo ambapo mhusika hutosheka zaidi ya yule ambaye hana mazoea ya kufanya mapenzi. Hata hivyo, baadhi ya madaktari wamegundua kwamba ongezeko la homoni za kiume/ kike huweza kuwakinga wanadamu na magonjwa ya moyo.

Kuishi muda mrefu huku ukionekana kijana
Wakati wa tendo la ndoa homoni iitwayo DHEA huzalishwa mwili mzima. Hii husaidia msisimko wa mapenzi kuongezeka.

Kutokana na elimu hiyo DHEA ni kemikali yenye nguvu duniani ambayo husaidia kuweka sawa kinga ya mwili, huongeza ufahamu, kuimarisha mifupa, kutengeneza na kuimarisha afya na kuimarisha mishipa ya moyo (Cardiovascular).

Hupunguza baridi na mafua
Elimu inaonesha kuwa wanaofanya tendo la ndoa mara moja au mbili kwa wiki huongeza 30% ya uzalishaji wa chembe chembe hai za mwili ziitwazo Immunogloulin A ambazo huwa na kazi ya kuulinda mwili dhidi ya magonjwa.

Hizo ni faida chache tu za kufanya tendo la ndoa.
NB: Jambo kubwa la kuzingatia ni kuwa faida hizi hupatikana kwa ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na hofu ya kufumaniwa au kuumbuliwa

HAYA KWA WANA NDOA FANYENI MAPENZI JAPO KWA WIK MARA 3 MUPATE FAIDA ZA TENDO LA MAPENZI NDANI YA NDOA. KWA WALE WASIOWA HAWAPATI HIZI FAIDA SHAURI YENU MSIE OWA OWENI MUPATE FAIDA ZA TENDO LA NDOA

​Staa wa Pakistan Auawa na Kaka yake Aliyechukia Picha Alizokuwa Akiweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

$
0
0
Qandeel Baloch, aliyekuwa miongoni mwa mastaa wa mitandao ya kijamii nchini Pakistan, ameuawa na kaka yake katika mji wa Multan uliopo kwenye jimbo la Punjab. Alidai amemuua dada yake kwa heshima.

Polisi wamedai kuwa Baloch aliuawa na kaka yake kwenye nyumba ya familia yao baada ya kuchukizwa kwa muda mrefu na picha ambazo dada yake alikuwa akizipost mtandaoni.

Mwili wa mrembo huyo ukipelekwa kuzikwa

Baada ya kutekeleza mauaji hayo kaka yake alikimbia japo baadaye alikamatwa na polisi na kukiri kuhusika mbele ya waandishi wa habari.
Msichana huyo alikuwa akiweka picha za kawaida ambazo mastaa wengine duniani hupenda kuziweka kuonesha urembo wao.


Hata hivyo kwa maisha ya Pakistan na sheria zake, Baloch alionekana kuwa ‘controversial’ japo alipendwa sana.

Alikuwa na karibu wafuasi 750,000 kwenye mtandao wa Facebook ambako video zake zilikuwa maarufu na kuzalisha mijadala nchini humo.


Alijipatia umaarufu zaidi nchini humo baada ya kuahidi kuwa angevua nguo online kama timu ya Pakistan ingeshinda kwenye mchezo wa  cricket dhidi ya mahasimu wao India.

Baloch alitengeneza pia vichwa vya habari baada ya kupost selfie kwenye Instagram akiwa na Mufti Abdul Qavi, moja ya viongozi wa dini nchini humo na kupelekea kusimamishwa wadhifa huo.
Kaka yake alidai kuwa skendo zake ndizo zilimfanya achukue uamuzi wa kumuua.

Bongo5

UVCCM wawasaka BAVICHA Dodoma....Waandaa vijana 3000 Kuimarisha Ulinzi

$
0
0
Umoja wa Vijana CCM, wametua mjini Dodoma ambapo Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unatarajiwa kufanyika wiki hii huku wakiwatafuta wajumbe wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA) ambao awali walipanga kuzuia kufanyika kwa mkutano huo.

Akiwa katika Ofisi za UVCCM – Dodoma jana, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu aliwaambia waandishi wa habari kuwa amefika mjini hapo pamoja na mambo mengine kusimamia ulinzi wa chama na viongozi wa chama hicho lakini hawaoni BAVICHA.

“Nipo hapa kwa muda mrefu kwa ajili ya kuongoza shughuli za ulinzi wa chama na viongozi wetu, kama Mtendaji Mkuu na mtoa maelezo ya itifaki. Kwa bahati mbaya kwa muda wote sijaona dalili wala harufu ya BAVICHA. Hii inadhihirisha kwamba kusema na kutenda ni vitu tofauti,” alisema Shaka.

Aliongeza kuwa wamejipanga vizuri na wameandaa vijana 3,000 maalum watakaofanya kazi ya kulinda mkutano huo uliolenga kufanikisha kumkabidhi Uenyekiti wa chama hicho, Rais John Magufuli kwa mujibu wa katika ya chama hicho tawala.

Aliwahakikishia usalama wajumbe wa Kamati Kuu akiwataka kuwa na amani kwani wataingia na kuondoka mjini humo wakiwa salama.

Juzi, BAVICHA walitangaza kurudi mjini Dododoma kwa lengo la kufanya Mkutano wao wa Kamati ya Kiutendaji baada ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kuwataka kusitisha adhma ya kutaka kuzuia kufanyika kwa mkutano wa CCM.

Aliyeongoza Jaribio la Mapinduzi Nchini Uturuki Akamatwa

$
0
0
Jenerali Erdal Ozturk (katikati) aliyekuwa kinara wa jaribio akiwa mikononi mwa wananchi.

Jenerali Erdal Ozturk aliyekuwa kinara wa jaribio lililoshindikana la mapinduzi ya rais nchini Uturuki amekamatwa, huku viongozi wengine wa mapinduzi hayo, saba wakifanikiwa kutoroka na kukimbilia nchi jirani ya Uturuki kwa kutumia Helikopta.


Jenerali Erdal Ozturk (kulia) enzi akiwa kazini.

Hata hivyo viongozi hao waliokimbilia nchini Uturuki wakiwemo mameja wawili, makapteni watano na raia mmoja wamekamatwa nchini humo kwa kile kilichoripotiwa kuingia nchini humo bila kibali.Jenerali Erdal Ozturk aliyekuwa kamanda mkuu wa kikosi namba tatu tayari amekamatwa na kuwekwa mahabusu wakati akisubiri hatma yake na huenda akanyongwa ikiwa atapatikana na hatia hiyo.

Mapinduzi hayo yalishindikana baada ya wananchi wengi kujitokeza kumsapoti Rais Recep Erdogan, ambaye ametamka bayana kwamba wote waliohusika na jaribio hilo lililoshindikana watakabiliwa na adhabu ya kifo.

Askofu Gwajima Aibuka, Azungumzia Sakata lake Kanisani, Msaidizi wake Akanusha Kanisa Hilo Kufungiwa

$
0
0
KIONGOZI wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima, amefunguka kwa kuelezea safari yake aliyoifanya nje ya nchi hivi karibuni, baada ya taarifa mbalimbali kudai kuwa alilikimbia Jeshi la Polisi.

Akiongoza ibada kanisani kwake, Ubungo, jijini Dar es Salaam jana, Askofu Gwajima alisema aliondoka nchini kwenda Japan Juni 15, mwaka huu, kwa ndege ya Emirates.

Akitoa mahubiri katika ibada jana, Gwajima alisema alifika mjini Osaka Juni 16 na kuanza mkutano wa kuhubiri injili na siku zilizofuata alikwenda katika miji mbalimbali.

Askofu Gwajima ambaye aliingia kanisani hapo saa 5:00 asubuhi na kuanza kuhubiri dakika 15 baadaye, asubuhi alitumia muda wa saa tatu hadi saa 8:20 kumaliza mahubiri yake.

Baada ya kuanza kuhubiri, alielezea safari hiyo kwa kutaja miji aliyekwenda ikiwamo Nagoya alikohubiri kwa siku mbili, Karuizawa, Ibaraki, Hiloshima na Yanakochi.

“Safari yangu ilikuwa ya mafanikio sana. Tulisafiri salama na kuzunguka miji mbalimbali na tulirudi Jumatatu ya wiki iliyopita,” alisema Askofu Gwajima.

Kadhalika, katika mahubiri hayo, Gwajima aliwakumbusha waumini wa kanisa hilo kuhusu kuhama kwa kanisa hilo, kwa kuwatajia siku ya mwisho ya kumalizia michango kwa ajili ya ujenzi wa kanisa jipya kuwa ni Julai 30, bila ya kutaja sehemu ambayo kanisa hilo litahamia.

Hata hivyo, Askofu Gwajima wakati wote wa mahubiri, hakuzungumzia suala la kuhojiwa kwake na Jeshi la Polisi.

Wakati huo huo, mwandishi alizungumza na Msaidizi wa Askofu Gwajima, Yekonia Bihagaze, kuhusu tetesi za kufungiwa kwa kanisa hilo na kusema taarifa hizo si za kweli bali ni maneno ya mitaani.

“Hayo maneno si ya kweli. Si umeona ibada imeendelea kama kawaida na Askofu amehubiri? Maneno ya mtaani usiyalete kanisani,” alisema Bihagaze.

Julai 12, mwaka huu, Kikosi cha Polisi cha Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) kilimkamata Askofu Gwajima wakati akitokea Japan kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege la Kenya.

Baada ya kukamatwa, alipelekwa moja kwa moja Kituo Kikuu cha Polisi kwa ajili ya kuhojiwa, akidaiwa alitoa maneno ya uchochezi mwezi uliopita.

Jeshi la Polisi lilikuwa likimtafuta Askofu Gwajima baada ya kusambazwa mkanda kwenye mitandao ya kijamii unaodhaniwa una sauti yake.

Katika mkanda huo, Gwajima anapendekeza Rais mstaafu Jakaya Kikwete afikishwe mahakamani kwa yote yaliyofanyika wakati wa utawala wake, ambayo kwa sasa Rais Magufuli anayashughulika kwa staili ya utumbuaji majipu.

Pia Gwajima alisikika akimshauri Rais John Magufuli, kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM) iwapo watakataa kumkabidhi uenyekiti na kwamba apeleke muswada bungeni, kuondoa kinga ili rais ashtakiwe kwa makosa aliyoyafanya akiwa madarakani.

Tangu kusambaa kwa mkanda huo, Jeshi la Polisi lilikuwa likipiga kambi katika moja ya nyumba za Askofu Gwajima, iliyoko Mbezi Salasala jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kupiga kambi, jeshi hilo halikufanikiwa kumkamata na baadaye ilielezwa kuwa amekwenda nje ya nchi kuhubiri.

Mwaimbaji Shaa Aikacha MJ Records, Adai Hayupo Tena Katika Lebo Hiyo Inayomilikiwa na Master Jay

$
0
0
Malikia wa uswazi kama mwenyewe anavyopenda kujiita Shaa ameweka wazi zile tetesi zilizokuwa zimezagaa kwamba ameondoka Mj Record na kesema ni kweli hayupo chini ya lebo hiyo lakini haimaanishi kwa hafanyi kazi na studio za Mj .

Hata hivyo Shaa amesema ameanzisha kampuni yake inayoitwa SK ambayo ni matokeo ya kazi za sugua gaga,toba na nyingine ambazo zilirudisha gharama za Mj na kumuwezesha kufungua kampuni hake hiyo binafsi ambayo anatarajia kusajili wasanii hata wa tano ila kwa sasa yupo yeye peke yake.

Hata hivyo Shaa ameachia wimbo wake mpya unaoitwa Sawa kupitia kampuni yake hiyo ila unaambiwa Shaa hayupo taari kuyazungumzia mahusiano yake kama ailivyo mpenzi wake Master J ambaye akiulizwa na huwa anajibu lakini kwa Shaa nitofauti kabisaa

PAUL Makonda Afunguka na Kutolea Ufafanunuzi Kauli yake ya Kukamata Watu Wasio na Kazi Maalumu

$
0
0
Jukumu la Ulinzi na Usalama kwa ngazi ya chini lipo chini ya Serikali za Mitaa baada ya Serikali Kuu kuhamishia madaraka yake huko likiratibiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ambaye kimsingi  kwa ngazi hiyo ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa husika.

Moja ya suala ambalo lilipata upotoshaji mkubwa kwenye mitandao ya kijamii ni kauli aliyotoa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ya kutaka kuwatambua wakazi wa Dar es Salaam ambapo taarifa za kwenye mitandao ya kijamii zilizusha kwamba lengo lilikuwa ni kuwakamata watu wasio na kazi maalumu.

Kupitia Power Breakfast ya Clouds Fm Makonda amesema “Sikusema wasio na kazi maalumu wakamatwe kwa kuwa hatuna sehemu za kuwahifadhi hao wote watakaotiwa nguvuni, kimsingi huu ni upotoshwaji mkubwa uliofanyika kwenye mitandao ya kijamii, mimi nilitoa maelekezo kwa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa wawafahamu na kuwatambua watu wao na shughuli wanazozifanya”.

Makonda amesema jukumu la ulinzi na usalama kwa ngazi ya Mkoa lipo chini ya Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa ambaye kimsingi ni Mkuu wa Mkoa na sio Meya wala mtu mwingine yeyote; ndiyo maana jukumu hilo ameamua kushirikiana na ngazi ya serikali ya mtaa kwani suala la ulinzi liliachiwa Jeshi la Polisi pekee na ndio maana lilionekana kulemewa.


“Hakuna mwenye uwezo wa kumzuia Mwenyekiti wangu wa Serikali ya Mtaa kwenda nyumba hadi nyumba akiwa na askari ili kuwatambua wakazi, suala la ulinzi ni jukumu letu sote … tukishindwa kuwatambua watu maana yake hata milioni 50 zitakazotolewa na Rais Magufuli ambapo Dar es Salaam itapata bilioni 28 na milioni 650 zitashindwa kuwafikia walengwa”. Alisema Makonda.

Kuhusu swala la ombaomba

Makonda amesema jumla ya ombaomba 687 walibainika kuwepo jijini Dar es Salaam huku asilimia 70 kati yao sio wakazi wa Dar es Salaam, na kusisitiza bado operesheni ya kuwaondoa inaendelea kwa kipindi cha miezi mitatu ambapo hadi kufikia Agosti mwaka huu zoezi hilo litakamilika ili watoto ambao wanazurura wakiomba waweze kurejeshwa shuleni.
Viewing all 104775 articles
Browse latest View live




Latest Images