Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104415 articles
Browse latest View live

Juma Abdul Mchezaji Bora Ligi Kuu Msimu Uliopita

0
0
Abdul ambaye pia ni mchezaji wa timu ya taifa, Taifa Stars amewashinda beki mwenzake, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ wa Simba na kiungo wa Mtibwa Sugar, Shizza Kichuya.

Na kwa ushindi huo, Abdul mbali na kukabidhiwa taji na mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba, pia atazawadiwa fedha Sh Milioni 9.2 wakati klabu yake, Yanga SC itazawadiwa Sh. Milioni 81.3 kwa kuwa bingwa, huku Sh. Milioni 40.6 zikienda kwa washindi wa pili, Azam FC, Sh Milioni 29 zikienda kwa washindi wa tatu, Simba SC na Sh. Milioni 23.2 zikienda kwa Prisons washindi wa nne.

Mlinda mlango wa Azam FC Aishi Salum Manula ameshinda tuzo ya kipa Bora akiwaangusha Deo Munishi ‘Dida’ wa Yanga na Benno Kakolanya wa Prisons na kuzawadiwa Sh. Milioni 5.7 huku mfungaji bora Amissi Tambwe wa Yanga akizawadiwa pia Sh. Milioni 5.7.

Thabani Michael Kamusoko ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Kigeni, akiwaangusha Mzimbabwe mwenzake anayecheza naye Yanga SC, Donald Ngoma na kipa Muivory Coast wa Simba, Vincent Agban hivyo kuzawadiwa Sh. Milioni 5.7 pia.

Mholanzi Hans van der Pluijm ameshinda tuzo ya Kocha Bora na kuzawadiwa Sh. Milioni 8, akiwaangusha Mecky Maxime wa Mtibwa Sugar na Salum Mayanga wa Prisons.
Tshabalala ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi akiwaangusha Farid Mussa wa Azam na Shizza Kichuya wa Mtibwa Sugar na kuzawadiwa Sh. Milioni 4.

Ibrahim Hajib wa Simba ameshinda tuzo ya Bao Bora la Msimu na kuzawadiwa Sh. Milioni 3 akimuangusha Tambwe wa Yanga, wakati Mtibwa Sugar imezibwaga JKT Ruvu na Mgambo Shooting katika tuzo ya Timu yenye Nidhamu na kuzawadiwa Sh. Milioni 17.2.
Ngole Mwangole ameshinda tuzo ya Refa Bora na kuzawadiwa Sh. Milioni 5.7 baada ya kuwaangusha Anthony Kayombo na Rajab Mrope.

Timu ya Mtibwa Sugar imeteuliwa kuwa timu yenye nidhamu Ligi Kuu Bara katika msimu uliopita wa 2015/16.

Nido za Kajala Zageuka Gumzo.....

0
0
Staa ‘the big name’ wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’ amegeuka gumzo ukumbini kufuatia kupita mbele ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akiwa amebusti nido (matiti) kiasi cha kuwafanya baadhi ya waalikwa ‘kumdiskasi’.

Tukio hilo la aina yake lilijiri usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita ndani ya ukumbi wa sinema uliyopo Jengo la Quality Centre Barabara ya Pugu jijini Dar ambapo staa huyo alikuwa akizindua filamu yake ya Sikitu huku mgeni rasmi akiwa Waziri Nape.

Katika shughuli hiyo ambayo Wikienda lilikuwa ndani ya nyumba, baadhi ya wapenyeza ubuyu walisikika wakinong’onezana juu ya matiti ya Kajala namna yalivyokuwa yametuna kwenye gauni tofauti na alivyozoeleka kiasi cha wengine kudai ameyabusti kwa kuyachoma sindano.
“Mh! Jamani mbona leo Kajala amebusti nido kiasi hiki? Si bure, kama hajachoma sindano ya kubusti itakuwa si bure. Yaani unaambiwa watu wanamkodolea mimacho hadi wanaduwaa,” alisikika mmoja wa mashabiki aliowaalika kwenye sinema hiyo ambayo itakuwa gumzo mtaani.

Shuhuda mwingine alisikika akisema kuwa, Kajala aliwafanya hata wasanii wenzake kumgeukia wakati anaingia ukumbini hasa wengi wao walikuwa wamemkodolea jicho kifuani kwake kwa lengo la kutaka kuona namna alivyokuwa amebusti nido.

Alipofuatwa Kajala kuulizwa kulikoni au nini kimetokea hadi akavimbisha matiti kiasi hicho, hakuwa na la kusema zaidi ya kushukuru kwa kufana kwa uzinduzi wa filamu yake hiyo.
“Hivi huna ‘engo’ nyingine? Huoni watu wanavyoifurahia filamu yangu? Hayo ndiyo mambo ya kuniuliza,” alisema Kajala akisisitiza kuwa hataki maswali zaidi.

Chanzo:Global Publishers

Chenge Akaidi Agizo la Jeshi la Polisi, Baada ya Kuendeleza Mikutano ya Hadhara

0
0
Agizo la Jeshi la Polisi nchini la kusitisha kufanyika kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa imeonekana kutoathiri ratiba za Mbunge wa Bariadi, John Chenge ambaye ameendelea na mikutano ya hadhara jimboni kwake.

Taarifa kutoka jimboni humo zimeeleza kuwa Chenge amekuwa akifanya mikutano ya hadhara katika vijiji mbalimbali na Alhamisi iliyopita alianza na eneo la Buchani, mkutano uliomalizika salama bila kuwepo kizuizi chochote.

Katika mikutano hiyo, Mtemi Chenge ameendelea kuwasisitiza wananchi wake kupuuza kauli za kisiasa zinazotolewa na wapinzani wake bali waangalie namna anavyotekeleza ahadi alizozitoa kwenye kampeni za uchaguzi mkuu.

Mikutano hiyo ya Chenge hutanguliwa na matangazo yanayofanywa kwa kutumia magari yenye vipaza sauti katika eneo husika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Onesmo Lyanga alipotafutwa kwa njia ya simu alisema kuwa yeye hahusiki kutoa vibali vya mikutano na kwamba mhusika ni Mkuu wa Polisi Wilaya (OCD). Hata hivyo, OCD hakupatikana kwa wakati.

Hali hiyo imedaiwa kuzua manung’uniko kwa vyama vya upinzani mkoani humo ambavyo vimeshindwa kufanya mikutano ya hadhara kutokana na kuwepo kwa zuio la Mikutano hiyo nchi nzima.

Mwezi uliopita, Kamishna wa Jeshi la Polisi, Operesheni ya Mafunzo, Nsato Msanzya alitangaza kupiga marufuku kufanyika kwa mikutano ya kisiasa kwa sababu za kiusalama.

“Polisi kupitia vyanzo vyake mbalimbali, imebaini kuwea mikutano hiyo ina lengo la kuwahamasisha wananchi kutotii sheria za nchi,” alisema Kamishna Nsato.

Kufuatia agizo hilo, Jeshi la Polisi lilizuia kufanyika kwa mikutano iliyokuwa imepangwa na Chadema na ACT-Wazalendo kwa nyakati tofauti.

Wema Sepetu na Idris Sultam Wamwagana Rasmi

0
0
DAR ES SALAAM: Ubuyu wa motomoto wa mjini ni kwamba, zile mbwembwe zote za penzi la mastaa wawili Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Idris Sultan, zinadaiwa kufikia ukingoni na sasa imebaki stori kwani Wema, Idris wamwagana rasmi.

Wikienda limeng’atwa sikio kuwa, kitendo cha wawili hao ‘kushoo lavu’ kwenye ile Pati ya Black Tie iliyofanyika juzikati katika Ukumbi wa King Solomoni pale Namanga, Dar ilikuwa ni geresha tupu kwani walishamwagana kitambo.

Hata hivyo, kama utakumbuka au hukuipata ni kwamba iliwahi kuvujishwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wema na Idris wamemwagana lakini baadaye zilivunjwa picha zikiwaonesha wakiwa wameshikana mikono na mahaba tele ili kuua soo.

wema-na-idriss-insta Sasa ubuyu ulionyooka kutoka kwa chanzo cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao unadai kwamba, kilichotokea kwenye pati hiyo zilikuwa ni mbwembe za kuzuga zilizotokana na huruma ya Idris.

Ilidaiwa kwamba, Idris alilazimika kufika kwenye sherehe hiyo kwa sababu ilishatangazwa kuwa atakuwa ni miongoni mwa ‘ma-hosti’ lakini ukweli ni kwamba mambo yalishaharibika.

wema na idris 2“Unajua watu wengi hawakujua kuwa Wema na Idris walishaachana kitambo na pale (King Solomoni) walikuwa wanafanya maigizo tu, japokuwa haijulikani moja kwa moja sababu ya kuachana kwao lakini Wema anadaiwa kuwa tatizo kwa Idris kutokana na kutokea kwa migogoro ya kila kukicha,” alitonya sosi huyo.

Hata hivyo, katika kuonesha kwamba kuna kitu kinaendelea, wana-ubuyu wetu walifuatilia akaunti zote za mastaa hao katika mitandao ya kijamii kuona kama mbwembwe zao zinaendelea na kubaini kuwa hawako sawa baada ya kusoma ujumbe wa Wema unaoonesha kumbembeleza Idris huku jamaa huyo akionesha wazi kuwa hakuna mapenzi bali ni drama tu.

Ili kuleta ushahidi, tunakukaribisha hapa kusoma nukuu zao mtandaoni;

MANENO YA WEMA
“Having you as a friend, a brother, a lover and of course a shoulder to cry on every time, i’m at my worst has been the best feeling ever… I wouldn’t want to lose this feeling over anything…
“I realized without u then i ain’t complete…. You have stood by me in good times and bad and even when i messed up so bad you would look me in the eyes and tell me, “Baby, its okay, we gona fix this”…
“Idris you have been one of a kind and losing u is the last thing i want on this earth… I will love you until forever, until death do us part we will be together…
“I will hold on to you till da last minute because together we will get there…. I love you with my life…. For I believe you are my true love, my baby and inshallah! The Man that my kids will call daddy…” alimalizia kuandika Wema akimlilia Idris.

IDRIS NAYE ALIANDIKA:
“Kumbuka kurekebisha kiatu kila hatua ya maisha unayopiga kisije kuchomoka ukakanyaga mwiba ukapunguza spidi.”

WEMA ASAKWA
Wikienda halikuishia hapo kwani lilimsaka Wema anayedaiwa kubwagwa, alipopigiwa simu hakupokea, akaandikiwa ujumbe mfupi wa sms ambao pia hakuujibu.
Pia alitumiwa ujumbe kwa njia ya WhatsApp lakini pia hakujibu.

 UBUYU WAKAMILIKA KWA IDRIS MWENYEWE
Wikienda liligeuza dira yake na kuielekeza kwa Idris ambaye alifunguka bila kuacha lolote.
Kwa mujibu wa Idris, yeye na Wema walishasahau kuwa waliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kwani kwa sasa kila mtu ana ‘biashara’ zake.

“Mimi nilikwenda kwenye ile pati kwa sababu ya kuwaonea huruma tu kwani ndiyo kwanza wameanzisha kampuni na mbaya zaidi walikuwa wakiniweka kwenye matangazo. Unadhani watu wangewachukuliaje? Sikutaka kuwaharibia shoo lakini mimi nilishaachana naye na nina biashara zangu nyingine,” alifunguka Idris.

Idris alienda mbali zaidi na kusema kuwa kwa sasa ana mwanamke mwingine anayempenda na siku si nyingi mambo yakikaa sawa, atamuanika.
“Mwenzenu nina kifaa kingine soon nitawafahamisha,” alisema Idris.

WEMA NA IDRIS
Awali Wema na Idris walificha uhusiano wao lakini baadaye waliamua kujiachia ambapo mlimbwende huyo alidai kushika ujauzito lakini kwa bahati mbaya ukachoropoka.

Source:Global Publishers

'Ezylinc' A New Social Network To Promote Tourism

0
0

Tanzania, a county harboring a diversity of an unmatched fauna and flora, a unique destination
on the African continent yet to be discovered by foreigners.

Kilimanjaro, the highest free standing snow-capped mountain in Africa, the Islands of Zanzibar,
the national parks of Serengeti, Ngorongoro Crater, Tarangire, Lake Manyara, Ruaha, Selous and
the Marine Park of Mafia Island are few of the living examples.

Ezylinc is a new social network where individuals and companies can share tourists destination
sites’ photos and related activities, and at the same time connect with global travelers. Anyone
can join the social network freely by login to www.ezylinc.com, and post pictures, write articles
about destinations, form groups, add friends and much more.

Ezylinc connects two groups. On one side we have travelers and adventurists and on the other
side local businesses connected to travel and tourism.

Let’s take Tanzania as an example, where travel and tourism is one of the leading industries.
In 2014 The tourism sector in Tanzanian, contributed 17 per cent to the country’s GDP and
accounted for 25 per cent of all the foreign exchange earnings, with USD 2 billion in revenues.
According to the World Economic Forum (WEFORUM), Tanzania ranks 93rd out of 141 world's
tourist destinations rich in natural resources. Also, the country ranks 5th among African countries
with the highest growth in the hospitality industry with an average rate of 6.3 per cent per annum
in the last six years.

This is why we have created a new social network. We want to support travel, local businesses,
and create more jobs in tourism along the way.

Welcome and join ezylinc at, www.ezylinc.com.

Rais Magufuli Aibua Ufisadi Mwingine wa Mabilioni ya Shilingi Ndani ya Jeshi la Polisi

0
0
Rais Magufuli amelitaka Jeshi la Polisi kujiepusha na vitendo vya rushwa ambavyo vilinafanya jeshi hilo kukosa heshima katika jamii huku akisema kuwa ana taarifa za jeshi hilo kuingia katika makubaliano ya kifisadi ya mabilioni ya shilingi kwa ajili ya kununua sare za jeshi hilo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa akiwaapisha makamishna wa Jeshi la Polisi waliopandishwa vyeo na kuongeza kuwa ni jambo la kusikitisha kwamba mabilioni hayo yalitolewa kwa siku moja lakini hadi leo hakuna hata sare moja ya iliyonuuliwa.

Ameshangazwa na jeshi hilo kutoa kiasi cha fedha kinachokadiriwa kuwa kati ya shilingi bilioni 40 hadi 60 kwa ajili ya sare za polisi ambazo hadi leo hakuna hata moja iliyonunuliwa na wakati huohuo jeshi hilo likikosa shilingi bilioni 4 tu za kukomboa magari yao zaidi ya 70 yanayoshikiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) huko bandarini.

Aidha, Rais Magufuli ameagiza uchunguzi ufanyike na wahusika wafikishwe mbele ya haki ila angalau hata nusu ya fedha hizo ziweze kurudishwa zikalipie magari ya polisi yaweze kutoka bandarini maramoja.

Amelitaka pia Jeshi la Polisi kuachana na utaratibu wa kuwa na watumishi ambao ni raia wa kawaida na badala yake polisi wenyewe ndio washike nafasi hizo kulingana na taaluma husika na kushangazwa na taarifa kuwa  Mhasibu Mkuu wa Polisi aliyetumbuliwa hivi karibuni kwa tuhuma za ubadhirifu alikuwa raia wa kawaida na sio polisi.

Nahreel Alinitengenezea Hit Yangu ya Kwanza Afrika, Siwezi Kuacha Kufanya Naye kazi – Jux

0
0
Hivi karibuni kumekuwepo na tetesi kuwa wasanii wengi waliokuwa wakifanya kazi na Nahreel wakiwemo Weusi wameikimbia studio yake ya The Industry baada ya kubadilisha utaratibu wa kurekodi nyimbo.

Jux kwa upande wake amekanusha na kudai kuwa Nahreel bado ni mshkaji wake mkubwa na mwishoni mwa wiki walikuwa pamoja. Anadai kuwa bado ana kazi nyingi kwa producer huyo na kwamba wakati mwingine huamua kubadilisha ladha ili kuogopa nyimbo zake kuzoeleka.

“Nahreel mimi amenitolea hit song, amenitolea ‘Looking For You, naweza kusema ndio wimbo ambao hata Kiafrika ndio ilifanya poa sana,” Jux ameimbia Bongo5.

“Hata kuna wasanii wakubwa wa Kiafrika wengine ambao siwezi kuwasema sasa hivi wameiskia na wameniona huku na tunakuja kufanya nao nyimbo baadaye, ni sababu ya Looking For You. Nisingetoka kwa Bob labda nisingepata kitu tofauti,” amesisitiza.

Kingine amedai kuwa muda wote huu hakuwepo alikuwa nchini China na pia Nahreel amekuwa na miradi yake mingine mingi ikiwemo kwenda Afrika Kusini kufanya video za Navy Kenzo na za wasanii wa The Industry.

“Karudi, tumekutana jana, bado mshkaji wangu na bado nafanya naye kazi pia, sababu ya yeye kubadilisha utaratibu wa studio mimi haijaniathiri chochote kwasababu ni program zake yeye mwenyewe alizotaka kufanya, kwahiyo mimi naona ni sawa. Kwanza mimi ni mmoja wa watu niliyeona hivyo yaani Nahreel alikuwa anadeserve hicho kitu pia kwasababu alikuwa anafanya kazi sana.”

Wiki iliyopita Jux aliachia wimbo wake mpya, Wivu aliorekodi kwenye studio za AM Records.

Bongo5

Baada ya Kufunga Goli Kwenye Mchezo wa Europa League Samatta Afunguka

0
0
Mtanzania Mbwana Samatta aliweka rekodi ya kufunga katika michuano ya Europa League baada ya timu yake ya Genk kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 mbele ya Budućnost ya Montenegro.

Clouds FM kupitia kipindi chake cha michezo cha Sports Extra kilifanya mahojiano maalu na Samatta kutaka kujua mambo mbalimbali. Mtandao huu ukaona haitakuwa vibaya kama utakuletea kile alichokisema nyota huyo hasa kama ulikosa kusikiliza show ya Sports Extra.

sportsextra: Mbwana Samatta unajisikiaje kuwa Mtanzania wa kwanza kufunga goli katika michuano ya Europa League?

Samatta: Nimejisikia vizuri kwasababu ndiyo kitu ambacho kila siku nakipigania kuweza kufanikiwa, mshambuliaji unaweza kufunga magoli, nimejisikia vizuri na inanipa morali zaidi ya kuendelea kujituma.

sportsextra: Ulianza katika kikosi cha kwanza mbele ya Nikola Karelis mshambuliaji wa kutumainiwa wa Genk, hii inamaanisha kuwa mwalimu Peter Maes anakuamini sana kuliko mshambuliaji huyo anayehusishwa na kujiunga na klabu ya Nottingham Forest ya nchini England?

Samatta: Nafikiri sasahivi mwalimu ananiamini na anapenda kunitumia, ni kitu ambacho kwakweli ni kizuri kwangu mwenyewe binafsi lakini pia nafikiri yeye kwake anaona namsaada mkubwa kwenye timu yake nikiwa naanza kwenye kikosi cha kwanza. Nafikiri ni jambo la kusubiri muda utakapofika kilakitu kitakuwa wazi lakini kwa sasahivi nafikiri mwalimu anapenda kunitumia zaidi.

sportsextra: Watu wengi walikuwa wanajaribu kujiuliza kuwa Mbwana yupo wapi wakati wa likizo yako baada ya kusimama kwa Ligi Kuu ya soka nchini Ubelgiji. Watu wanataka kujua ulikuwa wapi Mbwana wakati wa mapumziko?

Samatta: Likizo nilikuwa Tanzania japo likizo ilikuwa fupi lakini nilikuwa nyumbani nimepumzika ilikuwa ni kipindi cha mwezi wa Ramadhani kwahiyo nilikuwa kwenye mfungo. Ilikuwa haina sababu ya kuonekana kwasababu ilikuwa ni kipindi cha mapumziko.

Ukifata program ya mazoezi kutoka kwenye timu, ilikuwa ni muda wa kupumzika kwa wiki moja halafu wiki nyingine unatakiwa ufanye mazoezi wewe mwenyewe binafsi. Lakini kwa bahati mbaya mimi sikupata muda wa kupumzika kwasababu wakati likizo inaanza mimi nilitakiwa nijiunge na timu ya taifa kwa ajili ya mechi dhidi ya Misri na baada ya hapo niliendelea na program ambayo nilipewa mimi binafsi.

Mchezaji anapopewa likizo anatakiwa apumzike kabisa kwasababu ni kipindi ambacho mwili wake unatakiwa ujirudi na kutengeneza nguvu mpya. Haina maana kwamba ukipewa likizo basi ujifue na kujiweka nondo hapana, muda wa mapumziko ni kipindi ambacho anatakiwa apumzike kama amepewa program basi afanye lakini asijichoshe.

sportsextra: Mbwana nafasi ya timu yako ya Genk sasa unaionaje katika michuano ya Europa League baada ya jana kupata ushindi mbele ya klabu ya Budućnost?

Samatta: Nafikiri bado tunakibarua kwasababu ni mechi ya kwanza na tumeshinda kwa goli 2-0, mpinzani sasahivi kichwani kwake anajua kwamba amefungwa goli mbili na anahitaji kurudisha na kupata ushindi akiwa nyumbani, kwahiyo kibarua bado kipo siwezi kusema moja kwa moja kwamba tutakata tiketi ya kucheza kwenye makundi lakini nafikiri tuna timu nzuri na tunaweza kufika huko kwa hiyo kila kitu ni wakati.

sportsextra: Asante sana Mbwana Samatta.

MAGUFULI 'Ilifika Mahali Kuna Wafanyakazi Weekend zao Walikuwa Wakizifanyia Dubai na Kurudi Jumapili".

0
0
Mh Rais amewafikishia salaam wale wote wenye tafsiri hasi juu ya hali ya uchumi inayojitokeza sasa ya kufungwa na kugeuzwa kwa mahoteli kuwa hosteli kama mtikisiko wa kiuchumi kwamba fikra na mitizamo yao si sahihi.

Mh. Magufuli amesema na hapa namnukuu, "Hii ni tafsiri kwamba wapangaji wa nyumba hizi walikuwa ni wafanyakazi serikalini".

Mh Rais ameongeza na kusema kwamba, "Ilifika mahali kuna wafanyakazi weekend zao walikuwa wakizifanyia Dubai na kurudi Jumapili".

Mh. Rais nimemnukuu akisisitiza kwamba, "Hapo nyuma nchi hii kuna watu walikuwa wao wanaenjoy huku wengine wakiwa watizamaji, hii hapana lazima tu-enjoy wote".

Nimemsomesha, Nimegharamika, Leo Kaniacha Anaolewa na Mtu Mwingine

0
0
Wakuu nilikutana na huyu binti miaka kadhaa iliyopita mimi nikiwa nimepangiwa kazi mkoa fulani katika mihangaiko yangu nikakutana na huyu binti nilitokea kumpenda, mzuri kisura na kitabia very innocent niliamini kwake nimefika baada ya kash kash nilizopitia katika mahusiano ya nyuma.

Wanasema usiusemee moyo ila najua yule binti alinipenda kidhati tena moyoni kabisa na mimi kwangu she was a queen na niliapa kumuoa baada ya yeye kumaliza masomo yake. Binti huyu kwao ni familia maskini nikisema familia maskini ni familia maskini kisawasawa. Baba yake alifariki miaka kadhaa nyuma kabla sijaonana nae hivyo aliishi na mama yake na wadogo zake ni story ndefu kuhusu familia yao. Mimi nikawa ndio kama msaada katika familia yao, sikua na hiyana na nilisaidia niwezavyo kwani binti yule nilimpenda kutoka moyoni.

Yule binti alimaliza shule na kuhitajika kwenda chuo lakini familia ikawa haina uwezo wa kumsomesha na mkopo alikosa. Akakosa raha na ikawa kama jukumu ni langu. Mama yake aliniita tushauriane kwasababu kwao nilikua nafahamika. Kwakuwa mimi nilisema nitamuoa binti wakashauri nimsomeshe kama nina nia yakweli. Uwezo wa kumsomesha nilikua nao nikakubaliana na tukaandikishana kwamba namsomesha mimi lakini mwisho wa siku yeye atakuja kuwa mke wangu na hata mahari sintolipa kwani itakua imeingia huko.

Familia ilinishukuru sana kwani waliamini kusoma kwa binti itakua afadhali katika ukombozi wa maisha yao. Binti alikuwepo wakati maandikishano yanafanyika na mashahidi walikuwepo nakumbuka binti alilia yule akiapa kunipenda milele na mapenzi tuliyofanya siku hiyo siwezi kusahau ilikua best sex ever.

Wakuu nifupishe binti alianza chuo kila kitu nililipa nauli hosteli ada matumizi kila kitu ilikua mimi,mwaka wa kwanza ukaisha vizuri mapenzi yanachanua.Likizo naenda likizo zao anakuja, mama mtu alinishukuru sana. Mwaka. Mwaka wa pili matatizo yakaanza nikipiga simu naambiwa yuko library mara assignment nikiuliza zaidi anakua mkali nikasema labda labda kweli shule lakini hata mimi nilisoma muda wa kuongea na mwenzi wangu nilikua nao nikasema labda shule ya sasa ni ngumu. Binti akabadilika majibu ya jeuri nikaenda kuongea na mama yake amkanye naona akajirekebishe na kweli akatulia maisha yakaendelea. Upside zikiwa chache. Mahusiano yalitawaliwa na migororo

Kufupisha Miezi kadhaa imepita binti kaniandikia meseji eti "NAKUSHAURI UTAFUTE MWANAMKE MWINGINE MIMI SIKO TAYARI KUWA NA WEWE NIKUTAKIE MAISHA MEMA"

Naandika huu uzi wakuu acha nikipiga simu haipokelewi mara haipatikani. Nikampigia mama yake kumuuliza kama anajua lolote akasema hafahamu. Nikaomba likizo kazini nifatilie sikuamini siku naambiwa ana mimba na anaishi na mwanaume mwingine. Nilitamani ardhi ipasuke kumbe ndio maana niliandikiwa ule ujumbe nikajiuliza maswali bila majibu,basi angefanya nisijue na mimba juu kapata inauma sana. Kumuuliza mama yake hana analonijibu, kumbe chuo kapostpone sijui anaishi na huyo mwanaume moja ya mitaa Dar, yote hiyo nafatilia kwa baadhi ya marafiki zake na kibaya zaidi huyo mwanaume alishamlipa tena huyo mama pesa nyingine. Na ndio kamchukua binti yake.

Nimechukia kuuziwa mbuzi kwa gunia.Love is blind inakuwaje sikuona yote hayo? Why me..Why.. Najiuliza sipati majibu, sikuwahi kupenda kama nilivyompenda huyo binti. Nilimpenda kutoka moyoni na kujitoa kwake sijawahi kumfanyia mwanamke yoyote niliyomfanyia leo ameniacha kwenye mataa na nyodo juu, kuna muda natamani ningekuwa na bastola nimsambaratishe ila that is not me. Juzi nimeona whatsup kaweka picha yake tumbo kule na namba yake nikafuta.

NILICHOFANYA;

Nimepeleka hii kesi Mahakamani kwasababu tuliandikishana kama mke nimekosa basi nilipwe gharama zangu najua haiwezi kuziba pengo kufuta maumivu naona is the least i can do for my self. Wakuu nifanyaje au nimekosea kupeleka shtaka polisi tumeshaitwa mara mbili hakuna mtu aliyetokea upande wao. Nimetokea kuwachukia wanawake sana. Kwanini mnatufanyia hivi jamani tuwapende vipi. Nimekaa hapa kitandani nimewaza mawazo mengi moyo wangu kama barafu naishia kusononeka.

Sijui nimfanyie kisasi gani aumie kama mimi nilivyoumia.

Adios.

JOKATE Aweka Silaha Chini na Kunyoosha Mikono Kwa Ex Wake Diamond Platnumz

0
0
Diamond Platnumz anazidi kuwa karibu tena na maex wake. Jacqueline Wolper, Wema Sepetu hawana noma naye tena – na sasa Jokate Mwegelo!

Ya Jokate ina nguvu zaidi kwakuwa kwa sasa ana uhusiano na hasimu wake kiburudani, Alikiba na hiyo ni ishara kuwa uadui kati ya Diamond na Kiba umebaki kwa mashabiki tu.

Mrembo huyo amempongeza Diamond kwa uwezo wake mkubwa wa uchezaji wa style mpya kwenye hit single yake, Kidogo.

Akipost kipande cha video Instagram kikimuonesha Diamond na dancers wake wakifanya mazoezi kwa wimbo huo, Jokate ameandika:
You just took choreography ya East African tracks to another sphere, inspirational is an understatement. Moves za kwenye huu wimbo. I can’t even hata.”
Jojo pia anatamani amuone Chibu na Kiba kwenye ngoma moja.
“Naendelea kusubiri siku utakayo fanya kazi na team kiba tho- kiroho safi 😊. Hongera kwa kazi nzuri dogo @diamondplatnumz.”

Mapokezi ya post hiyo yana mchanganyiko wa hisia. Ila wengi wamempongeza.

Mara ya mwisho Jokate anamuongelea Diamond ilikuwa ni malalamiko aliyommwagia kwa kumuita mswahili na mdhalilishaji wa wanawake.

DJ JOH wa 93.1 Marekani acheza Ngoma za Diamond!

0
0
Haya sasa naona taratibu ule ubishi wa kuwa nyimbo za Afrika hasa Tanzania hazichezwi kwenye vituo vya Radio za Marekani unaelekea kuisha!

Dj Joh wa 93.1 Marekani akihojiwa na Millard Ayo amezungumzia nafasi ya wasanii wa Afrika kusika katika vituo vya Radio vya marekani!! Amelezea Mengi lakini amekiri mara ya kwanza ili apate hiyo kazi ilibidi adanganye na alikataa kuwa yeye si mtanzania kutokana na ubaguzi lakini baadae alikuja kukubari kuwa ni mtanzania baada ya kazi zake kuanzwa kupendwa! Alienda Marekani kwa ajiri ya kusoma lakini alifika hatua akaanza kuwa Dj lakini hakuruhusiwa kuplay nyimbo za kiafrika kwani hakuwa anaruhusiwa!!

Anasema yeye ni anapenda Afro Pop na anaupenda sana mziki wa Diamond!!!! Kwa mara ya kwanza alijitosa na kuanza kuplay nyimbo za akina P-squre,Wizkid na Diamond!!! Anasema siku hiyo alipokea comments nyingi sanaaa zilizo mpongeza na kufanya yeye kuongeza juhudi ya kuplay nyimbo za kiafrika hasa Za diamond

Anasema siku ambayo hatoisahau ni siku Alio play nyimbo za Diamond na baada ya kipindi alipigiwa simu na Mtu ambae ni Mmarekani na alimuuliza kuwa Diamond kamfahamia wapi ndipo Dj Joh alipo sema yeye ni mtanzania na anamfahamu Diamond!!! Yule mmarekani alimwambia yeye Kwa Afrika Diamond ndo Msanii anaye mvutia na kwenye Gari yake muda mwingi huwa anasikiliza nyimbo za Diamond japo haelewi lugha!!! Dj Joh amesema kuwa Yule mmarekani alimwambia wiki ijayo nina harusi yangu na ninaomba uje Uwe Dj kwenye Harusi yangu na Nyimbo za Diamond uwe nazo nyingi!! Hapo Dj Joh anasema alifurahi nakuona kuwa mziki wetu sasa unakuwa!! Dj Joh amesema number don't lie kwani ni wengi walio mpigia simu na kumpongeza na kumtaka kumjua Diamond!!!

Mbali na hilo kuna siku Diamond alipost video ilionesha sehemu fulani Marekani watu wapo kwenye shuhuri wakisikiliza Nasema nawe!! Millard ayo ameongeza na kusema kuwa pia kuna kituo kingine cha Radio marekani kinachoitwa CSB nacho hucheza nyimbo Za Diamond!!!

Ni wazi sasa mziki wetu umefika mbali!!! Kuna siku niliwahi sema Diamond nyimbo yake na Neyo itachezwa sana kwenye Vituo vya Radio vya Marekani lakini watu walinipinga sana humu na sasa limeanza kujidhihirisha Kabla hata ya hiyo collabo

Breaking News Wakurugenzi wote wa NSSF wamesimamishwa kazi, kupisha uchunguzi wa idara zao katika shirika hilo.

0
0
BODI ya wakurugenzi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limewasimamisha kazi wakurugenzi sita na meneja watano na Mhandisi mmoja kufuatia matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata sheria na kanuni.

Kwa mujibu wa taafia iliyotolewa leo na Mkurugnezi Mkuu wa NSSF,  Profesa Godius Kahyarara imesema hatua ya kuwasimamisha kazi wakurugenzi na mamenja hao inafuatia kikao cha bodi chini ya uenyekiti wa  Prefesa Samweli Wangwe kilichokaa kuanzia Ijumaa iliyopita.

“Bodi imeagiza  kusimamishwa kazi Wakurugenzi , Mameneja watano na Mhandishi mmoja ili kupisha uchunguzi ili kubaini wahusika katika tuhuma za ubadhirifu, matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata kanuni, sheria na utatibu katika uwekezaji,  usimamizi wa miradi na manunuzi ya ardhi na ajira,” alisema Profesa Kahyarara.

Aliwataja wakurugenzi hao ni Mkurugenzi wa mipango, Uwekezaji na Miradi, Yakub Kidura, Mkurugenzi wa fedha, Ludovick Mrosso, Mkurugenzi wa rasilimali watu na utawala, Chiku Matessa, Mkurugenzi wa Udhibiti,Hadhara na Majanga, Sadi Shemliwa, Mkurugenzi Mahesabu ya ndani, Pauline Mtunda na Mkurugenzi wa Uendeshaji,  Crescentius Magori.

Aidha Aliwataja mameneja waliosimamishwa ni pamoja na Meneja wa utawala, Amina Abdallah, Meneja wa Uwekezaji, Abdallah Mseli, Meneja Miradi, Mhadisi,John Msemo, Mhasibu Mkuu, Davis Kalanje, Meneja kiongozi mkoa wa Temeke, Wakili,  Chedrick Komba na Mhadisi John Ndazi.

Awali amedaiwa kuwa baadhi ya wakurugenzi na mameneja waliosimamishwa, leo wamefikishwa katika kituo cha polisi cha kati Dar es Salaam kwa mahojiano kufuatia tuhuma hizi zinazowakabili.

a wakurugenzi wote wa NSSF wamepigwa chini leo na wanne kati yao wako chini ya ulinzi.

Ugonjwa wa Kisukari ni Nini? Chanzo, Dalili na tiba yake

0
0
Magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni magonjwa ambayo hayasambazwi kwa mtu mwingine kwa kuwa hakuna vimelea mwilini vinavyohusiana na magonjwa hayo. Magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni kama ya moyo na mishipa ya damu, figo, saratani, kifua sugu, kisukari, magonjwa ya akili na mengine ya kurithi kama vile ugonjwa wa selimundu (Sickle Cell Disease).

Ripoti ya Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) ya 2013, inadai magonjwa yasiyo ya kuambukiza ndio chanzo kikubwa cha vifo ulimwenguni, yakifanya asilimia 63 ya vifo vyote kwa mwaka. Magonjwa yasiyo ya kuambukiza huua watu zaidi ya milioni 36 kila mwaka. Asilimia 80 ya vifo vinasababishwa na magonjwa hayo hutokea nchi zinazoendelea, Tanzania ikiwa miongoni mwa nchi hizo. Inakisiwa kuwa mwaka 2020 magonjwa haya yasiyo ya kuambukiza yatasababisha asilimia 73 ya vifo vyote duniani na asilimia 60 ya ukubwa wa tatizo la magonjwa duniani.

Nchini Tanzania, katika mpango wa upimaji wa afya kwa magonjwa yasiyoambukiza jijini Dar es Salaam, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umebaini kuwa idadi kubwa ya wanaume wanapatwa na magonjwa hayo kuliko wanawake. Uchambuzi huo umeonyesha magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari, shinikizo la damu na saratani zote ambazo zimekuwa chanzo cha vifo hivyo, huku serikali ikisema imeamua kuongeza juhudi za makusudi kupambana nayo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mfuko wa Bima ya Afya, athari ya magonjwa yasiyoambukiza ni mara nne zaidi ya watu waliopo mijini kuliko vijijini, huku asilimia 12.8 ya wanaougua wakiwa wako mijini na asilimia 3.1 wako vijijini kutokana na mfumo wa maisha.

Uchunguzi mwingine uliofanywa na jopo la madaktari bingwa kuanzia mwaka 2011 hadi 2014 ulibaini asilimia 79 ya watanzania wazee waligundulika kuugua magonjwa ya kisukari, macho na shinikizo la damu. Pia walidai magonjwa hayo yamekuwa kikwazo cha maendeleo kutokana na kuwasumbua wazee na hata wenye umri wa kati ya miaka 40 na 50.

Kisukari ikiwa ni moja ya muuaji wa kimya kimya katika kundi hili la magonjwa yasiyo ya kuambukiza. Watu milioni 285 duniani kote wameathiriwa na kisukari ambayo ni sawa na asilimia 6.6 ya idadi ya watu wote ulimwenguni pia ikishika nafasi ya 5 kwa kusababisha vifo duniani.

Nchi zinazoongoza kwa idadi kubwa ya watu wenye kisukari ni China wagonjwa milioni 43.2, India wagonjwa milioni 40.9, Marekani wagonjwa milioni 25.8, Urusi wagonjwa milioni 9.6 na Brazil wagonjwa milioni 6. Nchi zenye idadi kubwa ya watu wazima wenye kisukari ni Nauru kwa asilimia 30, Bahrain kwa asilimia 25.5, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa asilimia 25, Saudi Arabia kwa asilimia 23.7 na Mauritius kwa asilimia 20.

KISUKARI NI NINI HASWA?

Sukari mwilini hutokana na vyakula pamoja na vinywaji tunavyotumia kila siku na hutumika kuupa mwili nguvu. Glukosi ni aina ya sukari ambayo huzipa chembe za mwili nishati. Hata hivyo ili glukosi iingie ndani ya chembe hizo inahitaji insulini. Insulini ni kemikali (Homoni) ambayo hutokezwa na kongosho (Pancrease).

Kisukari ni ugonjwa unaotokana na mtu kuwa na sukari nyingi kupita kiasi kwenye damu. Ugonjwa huo huvuruga utaratibu wa kuingiza sukari ndani ya chembe kutoka kwenye damu kwa kuwa chembe huhitaji sukari ili kupata nishati.

Ugonjwa wa Kisukari hutokea pale ambapo tezi ya kongosho inaposhindwa kutengeneza kichocheo (Homoni) aina ya insulin au pale mwili unaposhindwa kutumia vizuri kichocheo hicho na kusababisha kuongezeka kwa sukari (Hyperglycemia) au kushuka kwa kiwango cha sukari (Hypoglycemia). Ugonjwa wa kisukari unaweza kusababishwa na kuwa na kiwango kidogo cha insulin mwilini, mwili kutosikia kichocheo hicho au yote mawili.

TAKWIMU MBALIMBALI ZA UGONJWA  WA KISUKARI

Kulingana na ripoti mbalimbali karibu watu milioni 316 ulimwenguni pote wana kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu, ingawa wengi wao hawajui wana kiwango hicho. Kwa mfano, nchini Marekani pekee asilimia 90 ya watu wenye sukari nyingi kwenye damu hawatambui kama wana tatizo hilo. Ingawa asilimia 8.3 ya watu watu wa Marekani wana Kisukari ambayo ni sawa na watu milioni 25.8 na kufanya Kisukari cha 7 kusababisha vifo vya watu Marekani.

Mamilioni ya watu wana ugonjwa huo lakini hawana habari! Ni ngumu zaidi kutibu ugonjwa wa kisukari kwa kuwa mtu anaweza kuishi nao kwa muda mrefu kabla haujagunduliwa. Hiyo ndiyo sababu watu husema kwamba ugonjwa huo huua kimyakimya.

NINI CHANZO HASA CHA KISUKARI?

Ili kuelewa vyema ugonjwa wa kisukari ni muhimu kwanza kuelewa namna chakula kinavyovunjwa vunjwa na kutumiwa na mwili ili kuzalisha nguvu. Wakati chakula kinapoyeyushwa matukio kadhaa hutokea. Moja ni sukari inayoitwa glucosi ambayo ni chanzo cha nishati/nguvu mwilini huingia katika damu. Tukio la pili ni kiungo kinachoitwa kongosho (Pancrease) kutengeneza kichocheo cha insulini. Kazi ya insulini ni kuondoa glucosi katika damu na kuingiza katika misuli, seli za mafuta na ini, ambako hutumika kama nishati.

Watu wenye kisukari huwa na kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu kuliko inavyotakiwa kwa sababu miili yao haiwezi kupeleka sukari kwenye seli za mafuta, ini na misuli ili ihifadhiwe kwa ajili ya kuzalisha nguvu. Hii ni kutokana na moja ya sababu zifuatazo, huenda kongosho zao haziwezi kutengeneza insulini ya kutosha au seli za mwili wao haziathiriwi na insini kama inavyotakiwa au sababu zote hizo mbili.

Main Symptoms of Diabetes FikraPevu.com
Kama wewe ni mnene kupita kiasi, hufanyi mazoezi kwa ukawaida au una watu wa ukoo walio na kisukari, huenda tayari una kiwango cha juu cha sukari kwenye damu. Ongezeko la sukari kwenye damu mbali na kuwa kisababishi cha kisukari, hali hiyo inahusianishwa na hatari ya kupatwa na ugonjwa wa akili uitwao 'DEMENTIA'.

Kula sukari nyingi sio sababu ya ugonjwa wa kisukari. Lakini lazima tuseme kwamba kula sukari nyingi si nzuri kwa afya yako kwani utaongeza uzito wa kuweza kuathiri uwezo wa mwili wako kujikinga na maradhi tofauti. Ugonjwa wa kisukari umeitwa kwa kufaa "ugonjwa unaoathiri kiini cha nishati ya mwili". Mwili unaposhindwa kutumia glukosi, mifumo mbalimbali ya mwili inaweza kuacha kufanya kazi au hata kusababisha kifo.

Ugonjwa wa Kisukari kitaalamu hujulikana kama 'DIABETES MELLITUS'. Jina 'Diabetes Mellitus' linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha 'kunyonya' na neno la Kilatini linalomaanisha 'tamu kama asali'. Maneno hayo yanafafanua vizuri sana ugonjwa huo, kwani maji hupita mwilini mwa mtu aliye na ugonjwa wa kisukari kana kwamba yananyonywa na mdomo na kupitia kwenye njia ya mkojo kisha kutoka nje ya mwili. Isitoshe mkojo huwa na ladha tamu kwa kuwa una sukari. Ndiyo sababu kabla ya kuvumbua njia bora za kupima ugonjwa huo, mbinu moja ya kutambua kama mtu ana ugonjwa wa kisukari ilikuwa kumwaga mkojo wa mgonjwa karibu na kichuguu cha sisimizi. Ikiwa sisimizi wangevutiwa na mkojo huo basi hilo lilimaanisha kwamba mkojo una sukari.

NI NANI ANAWEZA KUWA NA UGONJWA WA KISUKARI?

Watu walio katika makundi yafuatayo wana uwezekano mkubwa wa kupata ugonjwa wa kisukari:-

– Wenye uzito uliozidi,

– Wenye historia ya kuwa na wagonjwa wa kisukari katika familia zao,

– Wanawake waliozaa watoto wenye kilo 4 au zaidi,

– Watu wasiojishughirisha au wasiofanya mazoezi,

– Wenye shinikizo la damu,

– Wenye msongo wa mawazo na

– Wenye matumizi makubwa ya pombe na sigara.

Watu hawa wanashauriwa kupima sukari yao kila mwaka wakiwa na umri wa miaka 45 na kuendelea.

Kuna hatari kubwa ya kuugua ugonjwa huo ikiwa mtu ana mafuta mengi katika tumbo na kiuno chake kuliko katika mapaja yake. Mafuta katika kongosho na ini huvuruga uwezo wa mwili wa kudhibiti kiasi cha sukari kwenye damu.

Wavutaji wa sigara wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi kwani zoea hilo hudhuru moyo na mfumo wa mzunguko wa damu na kubana mishipa ya damu. Kitabu kimoja kinasema kwamba asilimia 95 ya watu wanaougua kisukari ambao hulazimika kukatwa viungo ni wavutaji wa sigara.

DALILI ZA UGONJWA WA KISUKARI

~ Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati.
~ Kwenda haja ndogo mara kwa mara. Watoto kukojoa kitandani.
~ Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.
~ Kupungua uzito au kukonda licha ya kula vizuri.
~ Kusikia njaa kila wakati na kula sana.
~ Wanawake kuwashwa ukeni.
~ Kutoona vizuri.
~ Kupungua nguvu za kiume au hamu ya kujamiiana kwa wanawake.
~ Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole.
~ Miguu kuoza na hata kupata gangrini.
~ Kukaukwa na ngozi na pia kupata aina ya ngazi katika miguu.
~ Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka.
~ Majipu mwilini.

Wenye dalili hizi wanashauriwa kupima sukari ili kubaini kama wana kisukari.

Uhusiano Uliopo Kati ya Punyeto na Upungufu wa Nguvu za Kiume Kwa Mwanaume......

0
0
 UKOSEFU  ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.

 Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.
Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:


  1. Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema
  2. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )
  3. Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )
  4. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini
  5. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema
  6. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.


Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume. Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka.

Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

  • Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.
  • Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA)


Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

  • Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume
  • Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :


  1. Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.
  2. Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana.  Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.



  • Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

  • Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.
  • Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame
  • Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa
  • Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume


DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO

Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

  • Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
  • Uume kurudi  ndani
  • Uume  kusimama  ukiwa  legelege
  • Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

Sare ya TP Mazembe v Mo Bejaia yazidi kuishindilia Yanga mkiani

0
0
TP Mazembe imejiongezea pointi moja baada ya kupata sare ya bila kufungana dhidi ya wenyeji wake Mo Bejaia katika mechi ya Kombe la Shirikisho.

TP Mazembe walikuwa wageni wa Bejaia katika mechi ngumu usiku wa kuamkia leo na watakuwa na furaha baada ya kupata pointi hiyo moja muhimu.

Sare hiyo imeihakikishia TP Mazembe kufuzu hatua ya nusu fainali kwa asilimia 90 kwa kuwa kama itashinda mechi moja katika mechi tatu zilizobaki basi itakuwa ina uhakika wa asilimia 100.

Lakini sare hiyo, imezidi kudidimiza matumaini ya Yanga kuamka angalau na kupata pointi zitakazoiwezesha kubadili mambo kwa kuwa ina pointi moja tu baada ya kucheza mechi tatu ikipoteza mbili na kupata sare moja tu dhidi ya Medeama.


TP Mazembe inaendelea kuongoza kundi hilo ikiwa na pointi saba ikifuatiwa na Bejaia yenye tano, Medeama ina mbili na Yanga inaburuza mkia na pointi hiyo moja.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 19, Ikiwemo ya Mtikisiko Mkubwa NSSF

0
0


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 19, Ikiwemo ya Mtikisiko Mkubwa NSSF

PAUL Makonda Adai Mashoga Dar es Salaam Wanafanya Mpango wa Kumwangamiza

0
0
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema tangu alipotangaza kuanza kukamatwa kwa mashoga, amebaini kuna mkakati unawaohusisha watu hao zaidi ya 150 kutaka kumwangamiza.

Kauli hiyo aliitoa jana Dar es Salaam baada ya kumaliza mahojiano katika kituo cha redio Clouds FM, ambako alikuwa akifafanua hoja na changamoto mbalimbali za mkoa wake.

Alisema kuwa baada ya kubainika kwa mipango hiyo, mashoga wanane wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa hatua zaidi.

“Lazima watu wajue jitihada na harakati za kusimamia katiba na usawa hapa nchini. Hakuna anayezipenda, vita inakuwa kubwa… Nimebaini kuwa mashoga zaidi ya 150 waliketi katika baa moja Kinondoni wakipanga njama za kunimaliza kwa namna moja ama nyingine, lakini kutokana  na taarifa za kiintelijensia, watu kadhaa, wengi wao wakiwa ni mashoga wameshakamatwa,” alisema Makonda.

Katika hatua nyingine, Makonda aliwatolea uvivu watu wanaosambaza ujumbe wa tofauti juu ya maagizo yake katika mitandao ya kijamii, ikiwamo kutengeneza akaunti feki.

“Kwanza wanapaswa kujua kuwa sina akaunti ambayo inaanza na cheo changu, hivyo akaunti zote zangu zimeandikwa kwa jina langu Paul Makonda si vinginevyo, hivyo kila mtu anapaswa kuwa makini na hilo,” alisema Makonda.

Aliweka wazi kuwa kuna agizo batili lililowekwa katika mitandao ya kijamii, akidaiwa kusema kuwa watu wasiokuwa na kazi watakwenda jela, lakini ukweli ni kwamba ameagiza wenyeviti wa Serikali za mtaa kuhakikisha kuwa wanafanya uhakiki wa wakazi wao nyumba kwa nyumba kwa ajili ya usalama wa maeneo wanayoishi.

Aidha Makonda alisisitiza kuwa kutokana na matatizo yaliyopo, kamwe Hatoacha kupambana na mafisadi katika halmashauri zote tatu za mkoa wake, pamoja na wauza unga, wafanyabiashara wa shisha na mashoga.

FAIZA Ally Amfungukia Mchumba Mpya wa Mh Sugu..Adai Anahonga Mashemeji na Mama Mkwe

0
0
Faiza Ally Kamfungukia Mrembo anayesemekana ndio mchumba wa Mh Mr Sugu Kwa Sasa Anaitwa Happy...
Soma Hapa:
Simpati Kwa lipi huyo happy - makengeza? Au Kwa sababu Ana Fany kazi biuro Au Kwa sababu Na baba Sasha wamefanana sura ? Simpati Kwa sababu kila wiki anatuma Mbeya Samaki? Simpati Kwa sababu Ana mfupi mweusi mbaya Au simpati Kwa sababu Ana tumia nguvu Na hela KWENYE mapenzi ? Au simpati Kwa sababu mweusi Ana vidole Kama tangawizi? Mkisema simpati mna maanisha nn hasa ? Au simpati Kwa sababu hazai ? Simpati kivipi labda tuwekane Sawa ! Siwaelewi ....? Nielewesheni? Au simpati Kwa sababu Ana honga mashemeji Na mama mkwe yaani kivipi sielewi? Haha nyie mnao SEMA simpati naombeni majibu simpati kivipi ? Au simpati Kwa sababu amenuna gari kasema kanunuliwa ? Siwaelewi simpati kivipi ? 

MREMA Ataka Watanzania Waupime Utendaji Kazi wake Baada ya Siku 100

0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Msamaha kwa Wafungwa (Parole), Augustine Mrema amemmwagia sifa Rais John Magufuli huku akiwataka Watanzania kumpa siku 100 aonyeshe mabadiliko katika magereza nchini.

Mrema aliyasema hayo jana alipohojiwa katika kipindi cha Amka Tuongee kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha Star tv.

“Ni Rais mzuri tuliyempata, ni mchapa kazi, tumpe muda kwa sababu ndiyo kwanza ana miezi minane, lakini ni mchapa kazi kiasi kwamba marais wenzake wanatembea yeye anakimbia,” alisema.

Julai 16, Rais Magufuli alimteua Mrema ambaye ni Mwenyekiti TLP baada ya kumkumbusha ahadi aliyompa wakati wa kampeni eneo la Himo Kilimanjaro kuwa wasipomchagua kuwa Mbunge wa Vunjo atampatia kazi.

“Nina uhakika nitafanikiwa kwa sababu nilipokuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nilifanya mambo makubwa hadi nikapewa cheo cha Naibu Waziri Mkuu,” alisema.

Viewing all 104415 articles
Browse latest View live




Latest Images