Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live

Mwanaume Kama Huna Hela Basi Ujue Mambo Kitandani la Sivyo....

$
0
0
Unaambiwa Sharti Mwanaume ujitume kunako sita kwa sita la sivyo basi kama huwezi kujituma uwe na hela za kumuhudumia kila kitu mwanamke hapo hutaachwa....la sivyo vitu vizuri utaviona tu kwa macho tu wanzako wakivinjari navyo...
Msikilize huyo dada akitoa makavu live....


Mahafali ya KKKT Chuo Kikuu Muhimbili Yapigwa Marufuku Baada ya Wanafunzi Hao Kumwalika Lowassa Kuwa Mgeni Rasmi

$
0
0
Uongozi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) umezuia mahafali ya wanafunzi  waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ) yaliyokuwa yamepangwa kufanyika jana mchana chuoni hapo jijini Dar es Salaam, ambapo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alikuwa amealikwa na wanafunzi kama mgeni rasmi.

Mahafali hayo yalizuiwa jana saa 6 mchana ikiwa ni saa mbili kabla ya muda kuanza

Tangazo lililobandikwa chuoni hapo na kushuhudiwa na wanahabari likiwa linamnukuu Kaimu Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Apollinary Kamuhabwa liliwataka wanafunzi hao kutoweka mikusanyiko ya aina yoyote chuoni hapo.

Profesa Kamuhabwa kupitia tangazo hilo aliwaonya wanafunzi hao kutojihusisha na masuala ya siasa wawapo chuoni kama ilivyo kwa watumishi wa umma.

Jitihada za waandishi wa habari kuzungumza na uongozi wa chuo hicho ili kupata ufafanuzi ziligonga mwamba baada ya kuelezwa kuwa hawakualika mkutano na waandishi wa habari.

Je Umesikia Kuwa Nahreel na Kundi la Weusi Haziivi? Nahreel Afunguka Ukweli Hapa

$
0
0
Producer wa The Industry, Nahreel ameukata mzizi wa fitina kwa kukanusha kuwa na tofauti na Weusi.

Amedai kuwa kubadilisha mfumo wa kurekodi muziki kwenye studio zake hakujavunja uhusiano na wasanii hao.

“Kusema ukweli hakuna mtu aliyekimbia, sisi bado ni washkaji, we are family, na kiukweli nimebadilisha utaratibu wa studio lakini si kwamba nilivyobadilisha ile ikaleta utata fulani, hakuna,” Nahreel ameiambia Bongo5.
“Hii ni biashara na mimi sasa hivi nataka niisukume biashara yangu iende mbali zaidi, kwahiyo nilibadilisha utaratibu kidogo lakini hiyo sio sababu yake kusema leo Weusi wamenikimbia au Jux au nani. Wale ni washkaji hata sasa hivi tumetoka tu kuongea nao vizuri tu na kuna projects ziko pale, kuna nyimbo ya Davido na Joh Makini, kuna nyimbo Joh Makini anayo na Khuli Chana iko pale, kuna nyimbo ya G-Nako ameimba na Vanessa ipo, Jux ana nyimbo zake kwahiyo zitatoka soon,” amesisitiza.

Nahreel amedai kuwa hivi karibuni amekuwa busy na tour na mambo mengi ya kundi la Navy Kenzo na hivyo kupishana ratiba na wasanii hao lakini amesisitiza kuwa hakuna tofauti yoyote iliyopo.

Chanzo:Bongo5

VIDEO: Edward Lowassa kaongea haya kuhusu wabunge wa upinzani kususia vikao

$
0
0
Vikao vya bunge la bajeti ya mwaka 2016/2017 ambalo limemalizika hivi karibuni huku ikishuhudiwa wabunge wanaounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, wakitoka nje na kutohudhuria vikao hivyo.

Leo July 31 2016 kupitia kipindi cha funguka kinachorushwa na kituo cha television cha Azam Tv, Waziri mkuu wa zamani na aliyekuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia CHADEMA, Edward Lowassa amezungumzia kuhusu wabunge wa upinzani kususia vikao vya bunge, Lowassa amesema…………..

Tutazame tatizo katika ujumla, tatizo linatokea na Spika Ndugai kuwa na hali mbaya ya afya, namfahamu Ndugai ni mtu makini sana, angekuwa madarakani mambo hayo yasingefikiwa’
Kuna tatizo pale kwanza la psychology., naibu Spika ameletwa kwa njia ambazo watu wanaona pengine hazikuwa sahihi sana na amejichukulia madaraka na anachukua maamuzi ambayo ni magumu kidogo mimi ninawaelewa wabunge wetu’ 
VIDEO:

Irene Uwoya Asema Angeumudu ‘Ukuu’ wa Wilaya Kama Angepewa

$
0
0
Msanii wa filamu Irene Uwoya amefunguka kwa kusema kuwa kama angepata nafasi ya ukuu wa wilaya basi angefanya vizuri kwa kuwa ana uwezo mkubwa wa kuongoza.
Irene Uwoyo

Muigizaji huyo ameimbia Bongo5 kuwa hakuwa na matarajio yakuteuliwa lakini kama angeteuliwa angeitendea haki nafasi hiyo.

“Mimi sijaomba wala sijawai kusema kama nataka hiyo nafasi, lakini kama ikitokea naiweza sana, nipo vizuri sana ndio maana hata nikathutu kugombea ubunge kwa sababu nilijua naweza kuongoza,” alisema Irene Uwoya.

Muigizaji huyo mahiri aligombea ubunge wa viti maalum Tabora lakini akakosa na kuhaidi kujipanga katika uchaguzi ujao.

Samatta Uwanjani Leo Ligi Kuu Ubelgiji

$
0
0
Mbwana Samatta leo anatarajiwa kuonekana tena katika nyasi za Ulaya pale timu yake ya Genk itakapovaana na KV Oostende katika muendelezo wa mechi za ufunguzi katika Ligi Kuu ya Ubelgiji maarufu kama Jupiler Pro League.

Mchezo ambao utachezwa kunako dimba la Cristal Arena, nyumbani kwa Genk utaanza saa 1 kamili za usiku kwa majira ya Tanzania na Afrika Afrika Mashariki kwa ujumla.

Ikumbukwe tu, huu ndio msimu ambao Samatta anaanza kuanzia mwanzo mara baada ya msimu uliopita kuukuta mwishoni kufuatia ksajiliwa katika dirisha dogo akitokea TP Mazembe ya DRC.

Samatta, akiwa kama miongoni mwa washambuliaji tegemezi tayari alibainisha dhamira yake tangu mwanzo kwamba anataka kucheza Ligi ya Mabingwa msimu ujao, hivyo ni jukumu lake sasa kuhakikisha msimu huu timu yake inafanya vizuri ili kukamilisha ndoto zake.

Msimu uliopita, Samatta aliwafunga Oostende katika mchezo wa raundi ya pili ya ligi waliyokutana, hivyo kumbukumbu hii ni morali tosha ya kuhakikisha anaisaidia tena timu yake kuibuka na ushindi leo.

Genk na Oostende wamekutana mara kumi katika michuano tofauti-tofauti. Oostende anaonekana kuwa na rekodi nzuri zaidi baada ya kufanikiwa kushinda michezo 4, huku Genk wakishinda mara 3 na kutoka sare mara tatu.

Msimu uliopita Genk walimaliza nafasi ya tano baada ya kujikusanyia alama 48 huku Oostende wakimaliza nafasi ya nne baada ya kupata alama 49.

Lowassa: Nitaongea ikifika Novemba

$
0
0
Wiki moja baada ya kuwa gumzo kuu katika mkutano mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu ambaye aligombea urais katika uchaguzi mkuu mwaka jana, Jumapili 30 Novemba 2016 saa 3.00 asubuhi atafunguka juu ya mengi yanayosemwa juu yake.

Lowassa ambaye ni mjumbe wa Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) atazungumza kupitia kipindi cha “Funguka” kinachoendeshwa na mwandishi wa habari nguli Tido Mhando kupitia kituo cha televisheni cha Azam 2.

Katika taarifa iliyotolewa leo na Azam 2 inasema “Lowassa atafafanua na kueleza mengi kuhusu maisha yake marefu kisiasa”.

Aidha, Lowassa ambaye aligombea urais kwa tiketi ya Chadema, huku akiungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) amekuwa kimya kwa muda mrefu licha ya kuzungumzwa, kuandikwa kuelezwa na kutendewa mengi yanayomhusu bila yeye binafsi kujitokeza hadharani na kujibu.

Gumzo la Lowassa ndani ya mkutano mkuu wa CCM lililoenda sambamba na baadhi ya viongozi na wazungumzaji kumshambulia wazi wazi huku wakishidwa kujadili kwa kina mambo yanayohusu chama, linatajwa kuwa ni hofu ya CCM dhidi ya Lowassa.

Hayo yatajiri ikiwa ni siku tatu tangu aadhimishe mwaka mmoja tangu kuhama CCM na kuwataka wanaomuunga mkono wakiwa CCM waendelee kumpa siri za mambo yanayojiri CCM ikiwemo mikakati ya Rais Magufuli.

Chadema: Tutamalizia kwa Dk. Magufuli

$
0
0
Mbowe na Lowassa Wakiteta Jambo
SIKU moja baada ya Rais John Magufuli kuonya mikutano ya kisiasa ya hadhara, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeahidi kumalizia mikutano yake nyumbani kwake Chato, Geita, anaandika Moses Mseti.

Chadema Kanda ya Ziwa Victoria kimeeleza kuwa, kitahitimisha Operesheni ya Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) katika Wilaya ya Chato anakotokea Rais Magufuli.
Tarehe 27 Julai mwaka huu, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa alitangaza kuanza mikutano ya hadhara na maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu chini ya mwavuli wa Ukuta.

Licha ya Chadema chini ya Mbowe kutangaza mikutano na maadamano ya amani nchi nzima, bado kumekuwepo na zuio la polisi dhidi ya vyama vya siasa nchini kufanya mikutano ya hadhara kwa kile kinachoelezwa hali ya usalama kutokuwa nzuri.

Meshack Micus, Katibu wa Chadema, Kanda ya Ziwa Victoria amesema, baada ya Mbowe kutangaza kuanza kufanyika kwa mikutano nchini, wao kama kanda wanaunga mkono tamko hilo.
Amesema, maadamano na mikutano ya hadahara yataanzia mkoani Kagera na kuishia Chato nyumbani kwa Rais Magufuli ambako amedai “huko ndio itakuwa funga kazi”.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Micus amesema, maandamano hayo yatakayoanza Wilaya ya Kyerwa (Kagera) na kumalizikia Chato mkoani Geita, lengo lake ni kumtaka Rais Magufuli kuongoza nchi kwa kufuata Katiba ya Nchi.

Meshack amesema, mikutano ya vyama vya siasa nchini ipo kisheria ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzani lakini wanashangaa kuona Rais Magufuli akivunja sheria hiyo.
“Vyama vya siasa nchini haviwezi kuwaomba polisi kufanya mikutano yao, bali wajibu wao ni kuwataarifu kuhusu hilo, lakini kwa hofu ya kumuogopa Rais Magufuli, wanatumia nguvu zisizo na ziada kuzuia mikutano,” amesema Micus.

Amesema, tayari wamewapa taarifa wanachama wa chama hicho katika mikoa yote ya Kanda ya Ziwa, hivyo kuanzia Septemba Mosi mwaka huu, wataanza maandamano yatakayoanzia Kyerwa na kumalizikia Chato nyumbani kwa rais ili kumfikishia ujumbe.
Micus ameeleza kushangaa madai ya Rais Magufuli kudai wabunge wa upinzani waliondoka bungeni wakiwa wameziba midomo, huku akisahau Chadema ndiyo walioibua hoja ya ufisadi na rais kuamua kuunda Makahama ya Mafisadi.

Tungaraza Njugu, Mwenyekiti wa Operesheni Chadema Kanda Ziwa Victoria amesema, Taifa limeingiliwa na kirusi kutokana na viongozi kuacha misingi iliyokuwepo.

Njugu amesema, kiongozi mzuri anatokana na jamii iliyo bora, lakini yule asiye bora hutoka katika jamii iliyo mbovu na kwamba hali hiyo inajidhihirsha kwa Rais Magufuli anavyoendesha nchi.
Hata hivyo, Njugu amewaomba wapenda haki, waweze kuungana na Chadema kupinga unyanyasi unaofanywa kwa vyama vya siasa kuzuia mikutano na maandamano yaliyopo kisheria kwenye mujibu wa Katiba ya Nchi.

Mama Diamond Anywea Kwa Zari Hassan

$
0
0
Zari Hassan
DAR ES SALAAM: Imevuja! Baada ya muda mrefu kusambaa kwa habari kuwa mama wa msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kassim ‘Sandra’, ‘haivi’ na mwandani wa msanii huyo, Zarinnah Hassan ’Zari The Boss Lady’, imedaiwa kuwa kwa sasa bi mkubwa huyo amenywea kwa kumkubali Zari.



Taarifa hizo zilizopenyezwa na chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya familia ya Diamond zimeeleza kuwa, hivi karibuni mama Diamond amesalimu amri na kutamka hadharani kuwa Zari ni kiboko kuliko wanawake wote ambao mwanaye amewahi kuwa nao.

“Mama Diamond kanywea kwa Zari na wala hana lolote la kusema, unajua Zari kamtuliza sana Diamond! Si kama alivyokuwa huko nyuma. Huwezi amini juzikati mama Diamond katamka kabisa kwamba hakuna mwanamke kama Zari maana amemtuliza Diamond vilivyo,” kilichonga chanzo hicho.

Baada ya kuunyaka ubuyu huo wa motomoto, Risasi Jumamosi lilimpandia hewani mama Diamond ili kumsikia anazungumziaje ubuyu huo ambapo baada kuelezwa kila kitu bi mkubwa huyo alijibu kwa kifupi na kukata simu:

“Eeeh mwanangu…eee..”

Risasi Jumamosi liliendelea kumpigia simu mama Diamond baada ya kukata lakini hakuweza kupokea tena.

Zari na mama Diamond wamedaiwa kuwa katika msuguano wa chinichini kutokana na kutoelewana tabia na kila mmoja kutomzungumzia mwenzake kwa mazuri hivyo kwa mama Diamond kudaiwa kusema anamkubali mkwewe huyo, ni dhahiri kwamba amekubali yaishe! Chanzo.GBP

Utajiri wa Dangote Washuka...Sasa Hayupo Katika List ya Matajiri Mia Duniani..

$
0
0
Dangote
Tajiri namba moja barani Afrika Aliko Dangote, sasa anashika nafasi ya 104 kati ya matajiri duniani. Dangote ameshuka kwa mara ya kwanza kati ya matajiri bora 100 chini ya jua kwa mujibu wa mtandao wa Bloomberg billionaires ranking.

Bloomberg wamesema kwamba Dangote ameshuka sababu kubwa ikiwa ni kuporomoka kwa thamani ya pesa ya nchi ya Nigeria, Naira. Ambayo imeshuka kutoka 198 hadi 300, na inakadiriwa kupunguza karibu robo ya utajiri wa Dangote ambaye bado anawekeza vitega uchumi mbalimbali katika nchi nyingi ikiwemo Tanzania.

Kulingana na ripoti hiyo ya Bloomberg billionaires, Dangote, aliyekuwa na utajiri wa dola za Marekani $15.4 billioni (Naira 3.05 trilioni) mwezi Machi mwaka huu mpaka sasa anamiliki utajiri unaofikia dola za Marekani bilioni 11.1 (Naira3.3 trillion), kwa maana tajiri kwa pesa za nchini kwao lakini maskini kwa pesa za dola ya Marekani.

Pamoja na kushuka kwake lakini bado kawazidi mabilionea wenye majina makubwa akiwemo mgombea uraisi wa Marekani, Donald Trump ($4.5) na msanii Oprah Winfrey ($3.1), anayetajwa kama mwanamke wa pili kwa utajiri duniani.

Kulingana na Jarida la Forbes la mwezi Juni 2015 ‘The World’s Billionaire’ rankings, mfanyabiashara huyo anamiliki utajiri unaokadiriwa kufikia $12.7 billion dollars na alikuwa akishika nafasi ya 51 miongoni mwa matajiri duniani na nafasi 71 ya watu wenye nguvu duniani.

Lowassa Atofautiana na Chadema, Ampa Sifa Rais Magufuli...

$
0
0
Lowassa 
KWA mara ya kwanza,mara baada ya uchaguzi mkuu kuisha mwaka jana ,Aliyekuwa Mgombea Urais wa CHADEMA,Edward Lowassa leo hii amefunguka na kukiri juu ya uwezo wa JPM katika kutenda kazi.

Lowassa ambaye leo asubuhi alikuwa katika mahojiano katika chombo kimoja cha Luninga,alisikika akimsifia Dr Magufuli huku akidai kuwa kama angelikuwa ni yeye ndio Rais angefanya zaidi ya JPM.

Hii inakuwa ni sawa na kwenda kinyume na Chama chake ambapo mara kadhaa wamekuwa wakiuponda utawala wa Rais Magufuli huku wengine wakimuita dikteta

Mwagizaji Jack Wolper Atoa Sababu zilizomfanya Kuisaliti Chadema na Kurudi CCM

$
0
0
"Nimefanya haya baada ya kuona kile nilichokuwa nakitaka kwenye nchi yangu Rais Magufuli anakifanya, kwanini niichukie CCM? naipenda CCM na CCM ndio nyumbani."– Jackline Wolper

Toa maoni yako

Mbunge Professor Jay Akibeza Kingereza..Adai Sio Muhimu Kukijua..

$
0
0
Msanii wa Hip Hop na Mbunge wa Mikumi, Professor Jay amesema kutokujua Kiingereza siyo dhambi. "Hii sijui kiingereza, Kiingereza ni Kushoboka tu. Viongozi wengi mbona tunaona wanakuja hapa Tanzania hawajui Kiingereza."

Kwa upande wako unadhani kuna umuhimu wowote wa kukijua kiingereza?

Lembeli Aibuka Mkutano wa Rais Magufuli

$
0
0
Mbunge wa zamani wa jimbo la Kahama, James Lembeli aliyehamia Chadema ameibuka leo katika mkutano wa na Rais John Magufuli uliofanyika mjini Kahama.

Akihutubia wananchi wa Kahama, Rais Magufuli amemkaribisha Lembeli na kumtaka kurudi  CCM akisema kwa Tanzania anayoijua yeye hatakuwa amepoteza mkia, kwani huko aliko ndiko mafisadi wamekimbilia.

Hivi karibuni akihutubia mkutano Mkuu wa CCM, Rais Magufuli akizungumzia waliotoka kwenye chama na kurejea tena, alitoa mfano wa ng’ombe aliyekatwa mkia, akisema huwezi kumzuia kurejea zizini lakini wenzake wanamkua kuwa hana mkia.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Lembeli amesema amekwenda kwenye mkutano huo kwa kuwa kazi anayoifanya Rais Magufuli ndiyo ambayo alikuwa anapigania wakati akiwa

mbunge kwa kuwa Shinyanga rushwa ilikuwa imekithiri.

Amesema na  hawezi kurudi CCM mpaka Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa chama hicho akisafishe.

"Kubadilisha msikiti siyo kuacha Uislamu, nyumba itaposafishika nitarudi," amesema Lembeli.

Rais Magufuli Asema Hatagawa Chakula cha Bure Kwa Watakaopatwa na Janga la Njaa Bila Sababu za Msingi.

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali yake haitagawa chakula cha bure kwa wananchi wanaopatwa na tatizo la njaa pasipo kuwa na sababu za msingi na badala yake amewataka watanzania wajikite kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ikiwa ni pamoja na kuzalisha chakula cha kutosha.

Rais Magufuli amesema hayo jana tarehe 31 Julai, 2016 wakati akihutubia mikutano ya hadhara na kuzungumza na wananchi waliosimamisha msafara wake akiwa njiani kutoka Mkoani Tabora kuelekea Shinyanga na baadaye Geita anakoendelea na ziara yake.

Pamoja na kuwahimiza wananchi kuzalisha chakula cha kutosha ili kuondokana na njaa Rais Magufuli alisema serikali yake itajikita kuhakikisha inashughulikia tatizo la uhaba wa maji, ujenzi wa miundombinu hususani barabara na reli, kuimarisha huduma za matibabu, elimu na kutengeneza ajira.

Akiwa Isaka Mkoani Shinyanga Rais Magufuli alisema serikali haitalipa fidia kwa wananchi waliopatwa na maafa ya mafuriko yaliyobomoa nyumba zao mwezi Machi mwaka 2015 na badala yake itajielekeza kutatua tatizo kubwa la uhaba wa maji katika mji huo ambao una makutano ya reli ya kati ya kutoka Dar es Salaam kwenda nchi za Burundi na Rwanda.

Katika Mji wa Kagongwa Rais Magufuli alipokea kilio cha wananchi dhidi ya vitendo vya ujambazi na ametoa siku tano kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha watu wanaojihusisha na ujambazi wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Mjini Kahama, Dkt. Magufuli aliiagiza Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana na Mbunge wa Kahama Mhe. Jumanne Kishimba kukokotoa mahesabu vizuri na kubaini kodi ambayo Serikali inastahili kulipwa baada ya Mbunge huyo kudai kuna kiasi kikubwa cha kodi hakijakusanywa kama ambavyo sheria inaelekeza.

Aidha, Rais Magufuli alisema serikali itahakikisha wawekezaji wanaochimba madini wanaacha kusafirisha mchanga wenye madini kwa lengo la kwenda kuchakata nje ya nchi na badala yake ametaka uchakataji huo ufanyike hapa hapa nchini.

Dkt. Magufuli alizungumza na wananchi vijiji vya Segese na Bukoli na kuwahakikishia kuwa Barabara ya Kahama, Segese, Kakola hadi Geita yenye urefu wa kilometa 146 itajengwa kwa kiwango cha lami kama alivyoahidi.

Mjini Geita, Rais Magufuli alipokea kilio cha wananchi wanaodai kuwekewa zuio la kutumia mawe yenye mabaki ya madini ya dhahabu (Magwangala) kwa lengo la kusaga na kuchenjua ili kupata dhahabu, na ametoa wiki tatu kwa Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya tathimini na kuwaruhusu wachimbaji wadogo kutumia Magwangala.

Rais Magufuli pia ameiagiza Bodi ya Pamba hapa nchini kuhamisha ofisi zake zilizopo Jijini Dar es salaam na kuzileta katika Mikoa ya kanda ya ziwa ambako uzalishaji wa zao la pamba unafanyika.

Dkt. Magufuli amewaonya viongozi na watendaji wa bodi hiyo dhidi ya vitendo vya usambazaji wa mbegu za pamba zisizoota na amesema ikitokea tena watachukuliwa hatua.

Tarehe 01 Agosti, 2016 Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli anatarajia kukamilisha ziara yake ya siku nne katika Mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Geita

31 Julai, 2016

Mbwana Samatta Afanya Mambo Tena Genk...Tazama Goli lake la Ushindi Alilofunga Jana

$
0
0
Mbwana Samatta anazidi kuonyesha uwezo mzuri wa kupachika mabao baada ya jana kupachika bao lililoipa ushindi Genk wa bao mbili kwa moja dhidi ya Oostende.,
Mbwana Samatta aliingia uwanjani dakika ya 80 na katika dakika 91 akapachika bao

Tazama Video Hapa jinsi alivyopachika bao safi:

Nay wa Mitego Apiga Magoti Nakuwaomba Msamaha Watanzania

$
0
0
“Wakati naandika wimbo “Pale Kati” nilikua nimeangalia nyimbo zilizowahi kutoka nyuma na zilizoko sokoni sasa, sikuona kama mistari yake ina matatizo. Lakini baada ya kukaa pamoja na kusikiliza mstari kwa mstari tumegundua kwamba kuna baadhi ya mistari ilikua ina maneno makali. Hivyo basi naomba radhi kwa mtu yeyote aliyeumizwa na mistari hiyo." - Nay wa Mitego

Tupia neno kwake

Nay wa Mitego Aanza Kuuza Mkaa Baada ya Kufungiwa Muziki...Tazama Video Hapa

$
0
0
Mchekeshaji Stan Bakora ameendelea na utani wake ambapo Ijumaa hii ameachia video ya kumdhihaki rafiki yake Nay wa Mitego baada ya kufungiwa na BASATA.
TAZAMA VIDEO:

Serikali haitagawa chakula cha msaada - Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali yake haitagawa chakula cha bure kwa wananchi wanaopatwa na tatizo la njaa pasipo kuwa na sababu za msingi

Rais Magufuli akimtambulisha aliyekuwa mbunge wa Kahama James Lembeli, wakati wa mkutano wake wilayani humo, leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema serikali yake haitagawa chakula cha bure kwa wananchi wanaopatwa na tatizo la njaa pasipo kuwa na sababu za msingi na badala yake amewataka watanzania wajikite kufanya kazi kwa juhudi na maarifa ikiwa ni pamoja na kuzalisha chakula cha kutosha.

Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 31 Julai, 2016 wakati akihutubia mikutano ya hadhara na kuzungumza na wananchi waliosimamisha msafara wake akiwa njiani kutoka Mkoani Tabora kuelekea Shinyanga na baadaye Geita anakoendelea na ziara yake.

Pamoja na kuwahimiza wananchi kuzalisha chakula cha kutosha ili kuondokana na njaa Rais Magufuli amesema serikali yake itajikita kuhakikisha inashughulikia tatizo la uhaba wa maji, ujenzi wa miundombinu hususani barabara na reli, kuimarisha huduma za matibabu, elimu na kutengeneza ajira.
Akiwa Isaka Mkoani Shinyanga Rais Magufuli amesema serikali haitalipa fidia kwa wananchi waliopatwa na maafa ya mafuriko yaliyobomoa nyumba zao mwezi Machi mwaka 2015 na badala yake itajielekeza kutatua tatizo kubwa la uhaba wa maji katika mji huo ambao una makutano ya reli ya kati ya kutoka Dar es Salaam kwenda nchi za Burundi na Rwanda.

Katika Mji wa Kagongwa Rais Magufuli amepokea kilio cha wananchi dhidi ya vitendo vya ujambazi na ametoa siku tano kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha watu wanaojihusisha na ujambazi wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Mjini Kahama, Dkt. Magufuli ameiagiza Wizara ya Nishati na Madini kushirikiana na Mbunge wa Kahama Mhe. Jumanne Kishimba kukokotoa mahesabu vizuri na kubaini kodi ambayo Serikali inastahili kulipwa baada ya Mbunge huyo kudai kuna kiasi kikubwa cha kodi hakijakusanywa kama ambavyo sheria inaelekeza.

Aidha, Rais Magufuli amesema serikali itahakikisha wawekezaji wanaochimba madini wanaacha kusafirisha mchanga wenye madini kwa lengo la kwenda kuchakata nje ya nchi na badala yake ametaka uchakataji huo ufanyike hapa hapa nchini.
Dkt. Magufuli amezungumza na wananchi vijiji vya Segese na Bukoli na kuwahakikishia kuwa Barabara ya Kahama, Segese, Kakola hadi Geita yenye urefu wa kilometa 146 itajengwa kwa kiwango cha lami kama alivyoahidi.

Mjini Geita, Rais Magufuli amepokea kilio cha wananchi wanaodai kuwekewa zuio la kutumia mawe yenye mabaki ya madini ya dhahabu (Magwangala) kwa lengo la kusaga na kuchenjua ili kupata dhahabu, na ametoa wiki tatu kwa Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya tathimini na kuwaruhusu wachimbaji wadogo kutumia Magwangala.

Rais Magufuli pia ameiagiza Bodi ya Pamba hapa nchini kuhamisha ofisi zake zilizopo Jijini Dar es salaam na kuzileta katika Mikoa ya kanda ya ziwa ambako uzalishaji wa zao la pamba unafanyika.
Dkt. Magufuli amewaonya viongozi na watendaji wa bodi hiyo dhidi ya vitendo vya usambazaji wa mbegu za pamba zisizoota na amesema ikitokea tena watachukuliwa hatua.

Kesho tarehe 01 Agosti, 2016 Rais Magufuli ambaye ameongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli anatarajia kukamilisha ziara yake ya siku nne katika Mikoa ya Singida, Tabora, Shinyanga na Geita.

Kiki zinawapa Taabu Wasanii Wengi Sasa - Prof Jay

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Mikumi na msanii ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake wa 'Kazi Kazi' Professor Jay amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi hivi sasa wanapata taabu na kitu kinachoitwa kiki.

Professor Jay akizungumza kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) ya EATV amedai kuwa wasanii wengi wa kipindi hiki kazi zao za muziki zimekuwa zikizidiwa na kiki wanazofanya jambo ambalo linapelekea wasanii hao kushindwa kufanya vizuri kwenye sanaa, na kuachia nyimbo mara kwa mara kwa kuwa kazi hizo zinakuwa hazina nguvu, wala ubora kutokana na wasanii hao kutegemea kiki ili kufanya vizuri.

"Wasanii wengi wa sasa wanasumbuliwa na hizi kiki, unakuta msanii ana wimbo lakini kiki zake ni kubwa kuliko hata hizo nyimbo zake, yaani ni sawa na mtu anakimbia mpaka anapitiliza kwake. Hizi kiki za wasanii hawa ni jambo ambalo linapelekea wasanii hao kujikuta wanatakiwa kutoa kazi mpya kila siku maana kazi zao zinakuwa hazina nguvu kama kiki zao" alisema Professor Jay

Mbali na hilo Professor Jay alisema kuwa yeye mpaka sasa anazaidi ya 'Hits song' 100 lakini hata sikumoja hajawahi kutegemea kiki katika kufanya kazi zake zaidi ya kutengeneza ngoma kali.
Viewing all 104768 articles
Browse latest View live




Latest Images