Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live

Shamsa Ford kufunga ndoa Ijumaa hii

$
0
0
Msanii wa filamu Shamsa Ford anatarajia kufunga ndoa Ijumaa hii na mfanyabiashara wa nguo aitwae ‘Chidi Mapenzi’.
Shamsa na Chidi Mapenzi

Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa ndoa hiyo itafanyika nyumbani kwa wazazi wake Sinza Africana jijini Dar es Salaam.

“Kweli bhana Ijumaa hii Mungu akipenda nafunga ndoa,” alisema Shamsa Ford.

Miezi mitatu iliyopita mfanyabiashara huyo alikiri kuwa kwenye mahusiano na malkia huyo wa filamu na kuweka wazi mpango ya ndoa.

Install Application ya SIASA HURU Kwenye Simu yako Kupata Habari za Siasa Kwa Urahisi

$
0
0
Kama wewe ni mpenzi wa Habari za Siasa basi hii ni habari njema kwako...Download Siasa Huru Application Kutoka Google Play Store Kwenye Simu yako itakurahisishia upataji wa Habari na Breaking News za Siasa kwa urahisi....

Bonyeza HAPA Kuinstall Kwenye Simu yako fasta....

Au Nenda Google Play Store Kwenye Simu yako Alafu Search 'Siasa Huru' Kisha Install


HATIMAYE Mbunge Godbless Lema Aachiwa Kwa Dhamana

$
0
0
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema amepandishwa mahakamani katika kesi mbili tofauti.

Kesi ya kwanza namba 351/2016 anatuhumiwa kumtumia ujumbe wa simu wa uchochezi Mkuu wa mkoa Arusha, Mrisho Gambo wenye maneno kuwa “Karibu tutakudhibiti kama mashoga walivyodhibitiwa Uarabuni”

Kesi ya pili namba 352/16 Lema anatuhumiwa kuhamasisha maandamano Septemba Mosi kinyume cha sheria.

Hakimu amepinga hoja za wakili wa Serikali,  Vincent Njau kuzuia dhamana kwa sababu za kiinterejensia kwa usalama wake.

Lema amekana mashitaka yote, na ameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ambapo kwa shitaka la kwanza alitakiwa kupata mdhamini na shilingi 10, na shitaka la pili dhama ni shilingi milioni 15.Kesi hiyo itatajwa tena Septemba

Hakimu anayesikiliza kesi ni Desderi Kamugisha wakati wakili wa serikali akiwa ni Innocent Njau.

Baadaye vurugu ziliibuka mahakamani wakati polisi wanataka kumpeleka Lema magereza kwa madai kuwa wadhamini wamechelewa, lakini mbunge huyo alipinga hatua hiyo kwa maelezo muda wa mahakama saa 9.30 ulikuwa bado.

Polisi Wamevamia Kikao cha Ndani cha Kamati Kuu ya CHADEMA

$
0
0
Kikao cha Kamati Kuu (CHADEMA) Kinachofanyika Dar es salaam kimevamiwa na polisi na viongozi walioko meza kuu wa natakiwa kwenda polisi.

Mtoto wa Shule Alivyofumaniwa na Mwanaume wa zaidi ya Miaka 60 Tanga

$
0
0
August 29 2016 Kupitia Hekaheka ya Clouds FM Geah Habib ametuletea Hekaheka iliyotokea Tanga ambapo mzee mmoja kafumaniwa na mkewe akiwa na mtoto wa shule wa miaka 14.

Mjomba wa mtoto ameeleza kuwa mtoto amekuwa akijiandaa asubuhi na mapema sana na anaaga anaenda shule lakini anapitia kwa huyo mzee na baadaye muda wa saa moja anaena shule……

Mahusiano yameanza tangia January, mpaka sasa hivi ni mwezi wa nane na sisi mpaka tumekuja kugundua ni baada ya kutokea ugomvi, mke wake yule mzee amempiga na kumng’ata mtoto ameumia na sisi ndio tukajua hilo suala.

Mtoto wangu ana miaka kumi nne na mzee huyo ana kama 60 mpaka 70 maana ni babu kabisa, sisi halikuwa hatujui tulikuwa tunajua anaenda shule na alikuwa anamuaga bibi yake maana anakaa na bibi yake kwamba wanatakiwa kuwahi namba kumbe asubuhi anaanza kwanza kwa huyo baba.

Jumatano asubuhi walipokutana na huyo baba kupewa hela mara mke wa huyo baba akatoa akaanza kumshambulia na kumng’ata

Faiza Awataka Wasichana Kuwakimbia Wanaume wa Namna hii…

$
0
0
Msanii wa filamu Faiza Ally amewataka wasichana wenzake kuwakimbia wanaume ambao wanawataka wasichana ili kufanya nao mapenzi kinyume na maumbile.
Faiza Ally

Muigizaji huyo ambaye yupo mbioni kuachia filamu yake mpya ‘Baby Mama Drama’, amewataka wasichana wenzake kuwaepuka wanaume wa nanma hiyo.

“Mtu anayekutaka kinyume na maumbile ni mtu katili sana,” aliandika Faiza instagram “Wanawake wenzangu msikubali kufanyiwa hivyo, mwananume anaetaka kukufanyia hivyo ni adui na hana mapenzi zaidi ya kuiridhisha nafsi yake tu,”

“Na ukikubaliana nae anaona amepata boya, mifano nimeona mingi sana na wengi wanalia na wamebaki namaumivu na chuki, hata ukinunuliwa gari halita kuwa milele, hata ukiwa na nyumba hutakula matofali, ukipewa hela zitaisha, ukipewa kazi mkataba utaisha pia, ukiolewa baada ya muda utachoka kugeuzwa kila siku na ndoa itakua haina amani moyoni, maana kigezo sio cha kumpendeza Mungu lakini utu wako utabaki milele,” alifafanua.

“Pia siku zote usifike mwisho ukakosa plan b siku zote kuna plan nyingine maana wanawake tunatabia ya kujitolea tupate jambo fulani lakini si kweli kwamba bila kutoa nyuma utafeli kila sehemu, ukikutana na jambo kama hili basi acha tafuta kungine ! hakuna kisicho wezekana haijalishi una haso muda gani, usikubali kuna watu wame haso miaka 30 na akapata wa 31. Mungu anatoa kwa wakati sahihi,” aliongeza.
Aliongeza,

Diamond Ajibu Comment ya Shabiki Inayodai Anamuiga Ne-Yo

$
0
0
Baada ya mashabiki kumtuhumu Harmonize kumuiga Diamond – sasa imekuwa ni zamu ya hitmaker huyo wa ‘Kidogo’ kuambiwa anamuiga msanii wa Marekani Ne-Yo ambaye tayari ameshafanya naye collabo miezi kadhaa iliyopita.

Kupitia mtandao wa Instagram, mmoja wa mashabiki anayetumia jina la 41732043sandra amecomment moja ya picha ya Diamond aliyoiweka kwenye mtandao huo na kuandika, “You are good and talented in your own way n I love you n ur songs but u should stop copying @neyo… Be ueself boy @diamondplatnumz.”


“Not only copying him, and now in the flight heading to Los Angeles to shoot my new Video Ft. Him….,” amejibu Diamond comment ya shabiki huyo kwenye mtandao huo.

Baada ya kujibiwa comment yake, shabiki huyo aliandika tena, “Unfortunately av no time to argue with ppl….@diamondplatnumz n the rest.. Safe flight n am glad you read my comment n that’s my stand.. Haha be blessed.. I ain’t shaken boo.”

Mrema Awaombea 'Mateja' Kazi Kwa Magufuli

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Palore nchini, Dkt. Augustino Lyatonga Mrema, amemwomba Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuongeza maeneo ya kutoa tiba ya kuachana na matumizi ya dawa za kulevya.

Sambamba hilo, Mrema amemuomba Rais kuwasaidia wahanga wa dawa za kulevya waliopatiwa tiba kurejea katika shuguli za kuzalisha uchumi.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo wahanga wa dawa za kulevya nchini, Dkt. Mrema amelitaka jeshi la polisi kuacha mara moja kuwanyanyasa waathirika wa madawa hayo huku akimtaka Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwapatia ajira pindi wanapoacha kutumia madawa hayo.

Naye Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili kutoka Hosptali ya Taifa Muhimbili Kitengo cha Madawa ya Kulevya Dkt. Cassian Nyandindi amesema ni vyema serikali ikajenga maeneo mengine nchini ya kutoa huduma ya matibabu kwani maeneo matano pekee yaliyopo nchini hayatoshi kuweza kuwahudumia waathirika hao ambao wanaongezeka kila siku.

EATV ilifanya mahojiano na baadhi ya waathirika wa dawa za kulevya ambao wamelilalamikia jeshi la polisi kuchukua fedha zao huku kila mara wakiwahusisha na kuuza dawa za kulevya ambazo tayari wameacha kutumia.

Taarifa Kwa Umma Kuaribika Kwa Mashine ya MRI Hospitali ya Taifa Muhimbili

$
0
0
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) inapenda kuujulisha umma kwamba mashine ya MRI itasimama kwa muda kufanya kazi baada ya kuharibiika. Mashine hii iliharibiika tarehe 24/08/2016 baada ya kutokea hitilafu ya umeme.


Baada ya kuharibiika, tarehe hiyo (24/08/2016) mafundi wa Philips kwa kushirikiana na mafundi wetu walianza kutafuta athari baada ya kutokea kwa hitilafu ya umeme.

Tarehe 26/08/2016, mafundi walibadilisha betri zote 31 na kufunga mpya ili kuongeza ufanisi katika mashine hii kwa kuwa betri za awali zilikuwa zimefungwa muda mrefu. Tarehe 28/08/2016 mafundi walibaini kwamba kifaa cha Gradient Module kilikuwa kimeharibiika na tayari hospitali kwa kushirikiana na Philips wameagiza kifaa hicho kutoka Uholanzi.

Hospitali ya Taifa Muhimbili inawaomba radhi wananchi kwa usumbufu wowote uliojitokeza.

Imetolewa na;
                                                                                         John Stephen, Ofisa Uhusiano,
                                                                                        
                                                                                         Hospitali ya Taifa Muhimbili

Mchezaji Mpira Avunjiwa Mkataba Baada ya Kugundulika Ana Virusi vya Ukimwi

$
0
0
Zikiwa zimepita siku nne tu tangu asajiliwe na klabu ya Al Ittihad inayoshiki ligi kuu ya Misri, Samuel Nlend, 21, mkataba wake umevunjwa baada ya klabu yake mpya kugundua mchezaji huyo anamaambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Jarid linalojulikana kwa jina la KingFut.com limeripoti kuwa, afisa habari wa klabu hiyo amethibitisha taarifa hiyo ya kusikitisha kwa vyombo vya habari.

Mshambuliaji huyo ameitumikia Cameroon katika michezo mitano, alifunga goli January kwenye michuano ya mataifa ya Afrika kabla ya kujiunga na Al Ittihad majira ya kiangazi.

Samuel Nlend alisaini mkataba wa miaka mitatu kuitumikia Al Ittihad tangu tarehe 24 August. Licha ya hayo yote kutokea bado amepata support ya kutosha kutoka kwa klabu yake mpya ya Misri.

SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Agosti 30, Ikiwemo ya Lowassa Aonja Joto la Polisi

$
0
0


SOMA Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya Agosti 30, Ikiwemo ya Lowassa Aonja Joto la Polisi

King Crazy GK Aamua Kuacha Muziki wa Rap..Sasa Kuimba Kama Diamond

$
0
0
Rapa kutoka kundi la East Coast, King Crazy GK ameamua kuingia Studio kwa Alonem ambapo amebadili maudhui ya uimbaji wake kutoka kurap na kufanya muziki wa kuimba huku video akiifanya na muongozaji Donald kutoka Uganda.

Akipiga story ndani ya eNewz, GK amesema kuwa ushindani uliopo kwenye game la muziki tofauti na zamani ikiwa ushindani ulikuwa wa hapa tu nchini, Ila kwa sasa wameongezeka wasanii mbalimbali wanaotoka hata nje ya nchi ya Tanzania.

“Nimeamua kuimba lakini ni kutokana na game la Tanzania kubadilika, zamani tulikuwa tukishindana sisi wa Tanzania kama Juma Nature, AY na wengine lakini kwa sasa muziki wa Bongo ume'change' na kuingia mpaka wakina Wizkind, so kubadilika muhimu” amesema GK.

Hata hivyo GK amebadilisha kabisa aina ya muziki wake na kutengeneza ngoma yenye mahadhi tofauti kabisa na muziki wake huku mwenyewe akisema anaandaa mashambulizi makali ili kupambana na game la sasa.

Safari Lager Kuliteka Soko na Bia Mpya ya Kopo Yenye Ujazo wa 500ml

$
0
0
Kampuniya Bia ya TBL kupitia bia yakeya Safari lager imezindua bia ya kopo ya kwanza yenye ujazo wamililita 500 kwa bia ya Kitanzania. Akizungumza katika uzinduzi uliofanyika jijini Dar, Meneja Bidhaa wa Safari Lager, Edith Bebwa Nasuwa alisema “Ni biaya kwanza ya Kitanzania ya kopo yenye ujazo wamililita 500 ambayo italeta urahisi, unafuu na ladha nzuri ya aina yake kwa wapenzi wote wa bia ya Safari Lager”

 Bia hii ya kopo tayari imeshaanza kupatikana maeneo yote nchini kuanzia tarehe 26 Agosti 2016 na imeelezewa kuwa ni bia ya wajanja wenye kujiamini.

“Bia mpya ya kopo ya Safari ni dhahiri kwamba imetengezwa kumpa umahiri Mtanzania katika safari ya maisha yake. Inapatikana kwa urahisi na kwa wakati muafaka hata wakati mtu anakwenda kwenye mihangaiko yake au kubeba akiwa anakwenda kwenye matembezi au safarini” alimalizia Edith Bebwa.

Fuatilia kurasaza Safari Lager kupataha barizaidi

Facebook: https://web.facebook.com/SafariLagerTz
Instagram: https://www.instagram.com/safarilager_tanzania/

Jokate: Wanawake Tusikatishwe Tamaa na vitu Vidogo

$
0
0
Kidoti kwa sasa anaendelea kupanua biashara zake kwenye nchi za Afrika Mashariki ambako kwa kuanzia wikiendi hii alikuwa jijini Kigali akiangalia fursa za kufanya biashara nchini humo.

“Wanawake tumeumbiwa kuwa na uvumilivu sana na upendo sana,” ameandika Jokate kwenye mtandao wake wa Instagram. Mungu atupe wepesi kwenye shughuli zetu, tusikatishwe tamaa na vitu vidogo. Tuseme Amen. Amen.”

Jokate ni miongoni mwa mastaa wachache wa hapa Bongo wanaoingiza fedha kutokana na biashara zao.

Multichoice Tanzania yampa mkataba wa mwaka aliyeshika nafasi ya tano olimpiki

$
0
0
Kampuni ya MultiChoice Tanzania imesaini mkataba wa mwaka mmoja na mwanariadha Alphonce Felix Simbu aliyeshiriki mashindano ya Olympic ya Rio 2016 yaliomalizika hivi karibuni huko nchini Brazil na kushika nafasi ya 5 kati ya wanariadha 157 kwenye mbio za Marathon za wanaume.

Katika Mkataba huu, Kampuni ya Multichoice Tanzania imemzawadia Alphonce Simbu shilling za Kitanzania 1,000,0000 ambazo atalipwa kila mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja lengo likiwa ni kumsadia katika maandalizi yake ya mashindano yajayo ya IAAF WORLD CHAMPIONSHIP yanayotarajiwa kufanyika mjini London Uingereza August 2017.

Vile vile bwana Alphonce Simbu atapatiwa vifaa maalumu vya kuumuwezesha kufanya mazoezi yake vyema. Vifaa hivi ni kama vile, viatu na nguo za mchezo wa Riadha.

Si hivyo tu bali  Kampuni ya MultiChoice itamtengenezea makala yenye kuonyesha matukio mbalimbili aliyopitia ya Kimichezo na Familia siku za nyuma. Vile vile watarekodi mazoezi atakayo anafanya akiwa katika kambi ya riadha Chuo cha Wakala wa Mistu Fiti kilichopo West Kilimanjaro eneo la Ngarenairobi Wilaya ya Sia Mkoa Kilimanjaro.

Makala hii itarushwa kwenye DStv hapo baadae.
Katika Kipindi cha hicho cha mkataba huu Alphonce Felix Simbu atakuwa Balozi wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania ambapo atashiriki katika promosheni mbalimbali kutangaza huduma zake.

Alipokuwa akisaini mkataba huo Mkurugenzi Mkuu wa Multichoice Tanzania Maharage Chande mbele ya Rais wa Riadha Tanzania na mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka, mwalimu wa wake Alphonce Nd. Francis John Marcially pamoja na Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania Furaha Samalu, alisisitiza kuwa “huu ni mwanzo na kadri mafanikio yanavyo ongezeka Multichoice itakuwa tayari kuwa mstari wa mbele kushirikiana na chama cha riadha Tanzania katika kunyanyua riadha Tanznaia na kurudisha heshma ya taifa kwenye mchezo huo”.


UKUTA Wazidi Kuvunjika Hata Kabla ya Tarehe 1 Septemba, Katibu wa Chadema Ajiuzulu

$
0
0
Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza John Thobius Nzwalile amejiuzulu nafasi zake ndani ya chama hicho na kuhamia CCM kutokana na kukerwa na oparesheni UKUTA ambayo imelenga kuleta vurugu nchini. Amenukuliwa akisema "Nimejaribu sana kuwaonya wenzangu kuchana na huo ujinga lakini hawasikii"

Prof. Lipumba Adai Yeye Bado ni Mwenyekiti wa CUF Baada ya Kutengua Maamuzi ya Kujiuzulu

$
0
0
Prof. Lipumba amesema yeye bado ni Mwenyekiti wa CUF na alishatengua maamuzi ya kujiuzulu, hakitambui kikao kilichokaa Zanzibar na kusitisha uanachama wake.

Amesema kuwa Katibu Mkuu asipotaja tarehe ya yeye kurejea kazini kama Mwenyekiti, atasubiri barua ya Msajili wa Vyama ili aanze kazi tena kama Mwenyekiti wa Taifa wa CUF.

UVCCM Waahirisha Maandamano Yao,watii Agizo La Jeshi La Polisi

$
0
0
Agosti 22, 2016 Umoja wa Vijana wa CCM tuliutangazia umma na dunia kwamba ifikapo Agosti 31 mwaka huu tutaitisha maandamano ya amani nchi nzima yenye lengo la kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli kwa utendaji wenye tija, ufanisi na uliorudisha imani na matumaini kwa wananchi.


Msimamo na dhamira ya kufanya maandamano hayo ya amani yenye maudhui na kusudio hilo, bado uko pale pale ingawaje si kwa tarehe tuliopanga na kutangaza awali yaani Agosti 31 mwaka huu.


Jumuiya yetu kama mjuavyo ni ya Vijana wa CCM, (UVCCM) inapata malezi kwa karibu mno na Jumuiya ya Wazazi ya CCM. Wiki ya jana Mwenyekiti wa Wazazi Taifa Nd. Abdallah Bulembo alikutana na waandishi wa habari akitutaka UVCCM tuahirishe maandamano ya Agosti 31 mwaka huu hadi wakati mwingine.


Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi, Jumuiya ya Wazazi ndiyo Msimamizi wa Malezi, Maadili na Adabu kwa Vijana wote nchini, sisi UVCCM tunaamini kuwa sikio halishindani na kichwa, mtoto ni mtoto kwa Wazazi wake hakui, hana jeuri wala ubishi.


Mtoto au watoto wanaokaidi amri, ushauri au maelekezo ya Wazazi wao huitwa watukutu, wenye viburi, manunda na wasioambilika. UVCCM si watukutu, hatukufunzwa tuwe wabishi, wakaidi na wenye viburi. Tumezingatia kutii maelekezo, makatazo na maonyo , tumeambiwa tuahirishe maandamano yetu nasi tumekubali na kuheshimu mambo tuliyoaswa.


Sambamba na hilo tumepata majibu ya barua yetu tuliyomwandikia Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP Ernes Mangu) inayotutaka tuache kufanya maandamano yetu kwa sababu Polisi wamezuia mikutano ya hadhara ya Vyama vya Siasa na maandamano nchi nzima.


Jambo jingine ambalo limetufanya pia tuahirishe maandamano yetu ya Amani ni taarifa ya kintelejinsia iliowasilishwa na Kamati yetu ya Usalama na Maadili ya UVCCM mbele ya kikao cha Sekreteriet yetu, nayo ilipendekeza  suala hilo liahirishwe kwa wakati huu hadi muda mwingine.


Pia jambo jingine ambalo limefanya maandamano hayo tuyabatilishe ni kulipisha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ ) ambalo litakuwa katika shughuli za maadhimisho miaka 52 tokea kuanzishwa kwake.


Wanajeshi wetu watakuwa katika kazi mbalimbali za kijeshi kwenye kambi zao na mitaani kufanya usafi wa mazingira, hivyo isingependeza na wala si heshima wakati sisi tukiandamana, wao wakifanya kazi muhimu kila mmoja wetu zinazomgusa badala yake ni vyema kuwaunga mkono jambo wanalolifanya la usafi wa mazingira.


UVCCM tumekubali, hatutaki kuingia katika uvunjaji wa sheria hasa baaada ya kutakiwa kuahirisha na mamlaka za Kisheria hadi wakati mwingine muafaka na si wakati huu.


Tunaelewa kwamba uamuzi wetu wa awali wa kutaka kuandamana kwa amani hata kama tungenyimwa kibali ungetugharimu, ungetusababishia madhara na pengine hasara, kwa wakati huu na kuona jambo lenyewe ni la kuipa Ari serikali katika kuhimiza Uwajibikaji, Utendaji na Usimamizi bora wa Uendeshaji wa masuala ya kiutawala.


Tulishusha maagizo kwa Makatibu wetu wote wa Mikoa yote 32 na Wilaya 171 ya Kichama tukiwataka waandike barua katika Ofisi za Ma RPC na OCD, washirikiane ili kuratibu maandamano na kuyafanikisha kama tulivyokusudia.


Watendaji wetu wa ngazi husika wamefuata maelekezo, wametii taratibu zetu za kiutendaji na leo tumewajulisha tena wasitishe maandamano hadi tutakapowapa tena maelekezo mengine. Tunawahimiza na kuwataka ni vyema kutii mamlaka za Kikanuni na Kisheria.


UVCCM kwa wakati huu tumeamua kuachana na maandamano badala yake tunajikita katika matayarisho ya kuwapeleka Vijana wetu wakashiriki katika Mafunzo ya Siasa, Utawala, Uongozi, Ufundi na Ujasiriamali yatakayoanza kufanyika katika Chuo chetu kilichopo huko Ihemi Mkoani Iringa ambapo kitakuwa kielelezo na alama nzuri ya kumuunga mkono Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli kwa vitendo.


Tumewataka Makatibu wetu wa Mikoa na Wilaya kuendelea na zoezi la Uratibu na Uhakiki kwa Vijana ambao watateuliwa kushiriki Mafunzo hayo huko Ihemi.


UVCCM tunarejea kusema tena kwamba dhamira ya maandamano yetu ya kusifu Utendaji wa Serikali ya awamu ya tano iko pale pale ila tutapanga tarehe nyingine katika wakati ujao badala ya kufanyika Agosti 31 mwaka huu kama tulivyotangaza hapo awali.


UVCCM tunawataka Vijana wote kuendelea kuheshimu Tunu ya Amani Umoja na Mshikamo wetu kwa Taifa.



KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Shaka Hamdu Shaka (MNEC)

KAIMU KATIBU MKUU.

Wema Sepetu: Sirudi Tena Dar

$
0
0
Malkia wa filamu Wema Sepetu amelikimbia jiji la Dar es salaam na kuamua kuanzisha makazi mapya mkoani Arusha kama alivyodai mwenyewe.

Mwigizaji huyo ambaye kwa sasa yupo mkoani Arusha ameonyeshwa kuvutiwa na jiji la Arusha na kuamua kuwarusha roho mashabiki wake kwa kuwaambia kwamba hatarudi tena Dar es salaam.

“My shouger nikimpenda hovyooo, kweli watu tumetoka mbali, huyu ndiye atakayenifanya nihamie Arusha kwakweli,” aliandika Wema katika picha hiyo hapo juu akiwa na rafiki yake.

Kadhi siku zinavyozidi kwenda mrembo huyo anaonyesha kuendelea kuvutiwa mji wa Arusha.

“Nirudie nini Dar mie, kurudi Dar majaliwa, na sirudi Dar ng’o,” aliandika Wema katika ujumbe wake wa pili.

Hata hivyo uwamuzi huyo umepokewa tofauti na baadhi ya mashabiki wake katika mitandao ya kijamii.

Haya ni maoni ya baadhi ya mashabiki wake.

Hopeolivier24
Dar bila Wema Itawezekana kweli? Itakuwa manispaa maana jiji unaliamishia Arusha😀😀

Zai_miss
Kwaiyo ushahamia arusha jamani khaaaa vigoma vyako itakuwaje My mmmh ila umefanya lamaana maana bongo kwa moto arusha Baridi kishezi😂😂😂😂😂

Theonerealdully
Utarudi tuu. Watu wa dar miji mingine hamuiwezi hekaheka zenu na mafoleni mwayapenda hivyohivyo

Andymsalali
jamn kwann, rudi bhana, tumekuzoea wenyew kukuona dar

Zeyaabdallah
Wema Rudi home coz matatizo hayakimbiwi dadaangu mpenz Wang.sawa Bali unatakiwa uyakabi

Bongo5

Comments

Lowassa Atoa Waraka Kuhusu Kukamatwa Kwake

$
0
0
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametoa waraka akisema kitendo cha askari wa Jeshi la Polisi kuwakamata wakati wakiwa kwenye kikao cha ndani cha Chadema jana  kimemuimarisha na kumpa nguvu zaidi ya kudai demokrasia.

Katika waraka wake kwa vyombo vya habari leo, Lowassa amesema anafurahishwa na kutiwa moyo na jinsi Watanzania walivyoipokea operesheni yao ya Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta) iliyopangwa kuanza kesho kwa maandamano na mikutano, lakini vitendo vya polisi vinawapa wasiwasi wananchi.

Lowassa, akiwa na Freeman Mbowe, ambaye ni mwenyekiti wa Chadema, John Mnyika (naibu katibu mkuu-Bara) na viongozi wengine wa chama hicho kikuu cha upinzani walikamatwa jana wakiwa kwenye kikao cha ndani kilichofanyika Hoteli ya Girrafe na baadaye kwenda kituo kikuu cha polisi kwa mahojiano kabla ya kuachiwa na kutakiwa kwenda kituo hapo kesho.
Viewing all 104709 articles
Browse latest View live


Latest Images