Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live

Jipatie Dawa Asili za Kutengeneza Shepu, Kuondoa Michirizi Chunusi, Kurefusha Nywele Toka Markson Beauty Products

0
0
HABARI NJEMA MARKSON BEAUTY PRODUCTS
Baada ya kupata cheti cha bidhaa bora kwa mwaka 2015-2016, Sasa kampuni hii inasambaza huduma zake ndani na nje ya nchi kwa vibali maalum. Bidhaa zetu zimetengenezwa kwa mimea na matunda na kudhibitishwa. Hazina kemikali wala madhara. DAWA ZETU NI YA:-

  1. kurefusha nywele na kuzuia kukatika ovyo @100,000/=
  2. Kuongeza shepu (hips na makalio) kwa/= (a)Dawa ya kunywa au kupaka @150,000/=(b)Vidonge @170,000/=
  3. Kuwa mweupe na softi mwili mzima kwa:- (1)Mafuta @100,000/= (11)Vidonge @150,000/=
  4. Kupunguza unene na manyama uzembe @120,000/=
  5. Kuongeza uume pamoja na nguvu za kiume kwa:-(a) Gely ya kupaka @100,000/= (b) Vidonge maalum @120,000/= (c) Handsome up original @170,000
  6. Kuondoa mvi milele zisiludi tena @100,000/=
  7. Kuongeza unene wa mwili mzima na uzito @120,000/=
  8. Kupunguza tumbo (kitambi) na nyama za pembeni kwa:- (a) Dawa ya kunywa au kupaka @120,000/= (b) Mkanda wa kawaida @100,000/= (c) micro-computer belt unaovaibret @200,000/=
  9. Kupunguza maziwa na kuyasimamisha @90,000/=
  10. Kushepu miguu na kuwa minene @100,000/=
  11. Kuondoa mipasuko mwilini (michirizi) @90,000/=
  12. kubana uke na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa mwanamke @100,000/=
  13. Taiti za hips na makalio @150,000/=           
NB: Hakikisha unapata risiti yenye muhuri halisi wa MARKSON CO pamoja na garantii kwa bidhaa halisi. Wasiliana nasi :-(+255) 0767447444 na 0714335378 Google MARKSON BEAUTY.
Follow us
@Markson_beauty_pr
@Markson_beauty_pr

Afikishwa Mahakamani kwa Kumtisha Rais Magufuli Kupitia Mtandao wa Watsapp

0
0
Mfanyabiasha  Leonard Materu (31) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashitaka ya kutuma ujumbe wa kumtishia Rais John Magufuli kupitia mtandao wa WhatsApp.

Materu ambaye ni mkazi wa Moshi Bar Kwadiwani, alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka yake na Wakili wa Serikali, Diana Lukondo mbele ya Hakimu Mkazi Magreth Bankika.

Akisoma mashitaka Wakili Diana alidai, mshitakiwa huyo amefunguliwa kesi hiyo ya kuchapisha taarifa za uongo kwenye mtandao wa WhatsApp chini ya Sheria ya Mtandao ya mwaka 2015.

Ilidaiwa kuwa, Julai 17, mwaka huu jijini Dar es Salaam, Materu aliandika ujumbe wenye lengo la kudanganya umma kupitia WhatsApp ukisomeka; “Magu ajiandae tunaenda kupindua mpaka Ikulu.”

Inadaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo la kumtishia Rais John Magufuli. Baada ya kusomewa mashitaka, mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo, na upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Mshitakiwa aliachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja alisaini hati ya Sh milioni tano. Kesi itatajwa tena Septemba 20, mwaka huu.

Vyama vya Upinzani Tanzania Vijisahihishe Kwanza Vyenyewe

0
0
Ni wakati muafaka sasa vyama vyetu vya siasa vinavyojiita ni vya upinzani vijipime kama vinatosha kua vyama vya upinzani ama ni upinzani uchwara?

Vyama hivi ambavyo ndani yake haviishi migogoro na misukosuko,ambayo inaashiria ukandamizwaji na uminywaji wa demokrasia ndani yake leo vinatuaminisha utawala uliopo ni wa kidikteta..

Nani hakumbuki sakata la Zitto alivyodhubutu kutangaza kugombea urais kupitia chama chake cha Chadema,na baadae anatafutiwa zengwe na kufukuzwa chamani,leo hata yeye mwenyewe ameusahau Udikteta aliofanyiwa enzi zile na anaunga mkono harakati za Chadema kutuaminisha Magufuli ni Dikteta.

Nani hakumbuki kilichomkuta Dr. Slaa, au nani hakumbuki upinzani wa Dr. Slaa, ulikua ni upinzani imara wenye masilahi mapana kwa taifa letu,lakini Dr. Slaa alivopinga kuja kwa Lowassa chamani akaambiwa ni bora yeye aondoke ili Lowassa apate nafasi.

Chama kinaendeshwa na maamzi ya mtu mmoja mbona sisi wanachama hatukushirishwa kwenye mchakato wa kumpokea Lowassa ama kumkataa, na sisi ni wanachama? Si kweli kwamba kila mwanachama wa chadema alifurahishwa na kitendo hicho, chama kinaongozwa kama familia yenye mfumo dume.

Nani pia hakumbuki jinsi mchakato wa kumpata katibu mkuu wa sasa wa chama chetu?,mchakato uligubikww na mizengwe kibao,ilimradi tu mwenyekiti anaamua nani akae kwenye nafasi hiyo, na kwa nn mwenyekiti kang'ang'ania madaraka? Chama hakina utamaduni wa kuachiana uongozi?..hayo yote na mengine yanaonesha wazi upinzani wa Chadema ni Upinzani Uchwara, M/kiti anakanyaga katiba ya chama hivi leo akiingia ikulu atashindwa kukanyaga katiba ya nchi?

Nani hakumbuki kua hichi chama ndo chama kilichoanzisha vuguvugu la ufisadi pale bungeni miaka kadhaa iliyopita na waziwazi wakatuaminisha kua Lowassa ni mtuhumiwa namba moja wa Ufisadi,leo wanakuja na ngojera za kutuaminisha Lowassa ni mtukufu kwa kua wamekalia hizo nyaraka za ushahidi...hivi hapa napo panahitaji usomi kiasi gani kujua hawa ni wapinzani uchwara? Maana sio Slaa,sio Tundu Lissu, sio Peter Msigwa, sio Mnyika,na wala si Mbowe wote walimtuhumu Lowassa.

Kwa majirani zetu na penyewe kumenuka,Lipumba alijiuzuru tena kwa mbwembwe, kwa kuitisha press leo anatangaza yeye ndo mwenyekiti halali wa chama,kwani hivi vyama havina katiba? Sasa kama nyie wenyewe ni madikteta kwenye vyama vyenu, huo mnaotuaminisha ni udikteta uchwara mtaweza kupambana nao?

Ifike pahala watanzania tuamue kutokuwaunga mkono nyie upinzani uchwara, kama miaka kadhaa mlituaminisha kua Tanzania inahitaji rais mwenye maamuzi,rais asie chekacheka mwenye kusimama hadharani na kukemea ufisadi na ubadhairifu wa mali za umma, Mungu si kiziwi kasikia maombi yenu katupa kiongozi ambaye leo tuna sababu lukuki za kujivunia,kiongozi ambaye hajamaliza hata mwaka lakini tayari tumeshaona dira na mwelekeo wa wapi tunaenda.

Cha ajabu kila anachokifanya kizuri kwa watanzania nyie kwenu ni kuponda tu, hivi ni kweli hamuoni,Majipu yaliyotumbuliwa,hamuoni elimu bure?,hamuoni pesa zilizookolewa kupitia watumishi hewa?,hamuoni pesa zilizookolewa kwa kudhibiti ukusanyaji kodi?,hamuoni pesa zilizookolewa kwa kufutwa kwa maazimisho ya siku kuu za uhuru na muungano?,hamuoni ni sh ngapi zimeokolewa kwa kuzuia safari za nje?,hamuoni hata jitihada za serikali kubadili mfumo wa elimu ambao ulikia umechakaa?,hamuoni hata madawati? Mnachoona ni Udikteta uchwara..

Hivi ukuta utatumia sh ngapi? Kwa nini hiyo bajeti msiielekeze kutatua kero za wananchi kwenye maeneo ambayo hayajafikiwa na serikali? Kama kweli mna uchungu na sisi(watanzani) leo hii huu ukuta unamfaishaje mkulima,mama ntilie?mwanafunzi?wazee?,na watanzania wa kawaida hata wafanyabiashara,....lakini huo mnaouita udikteta uchwara ukimuuliza mtanzania wa kawaida atakuambia amepata elimu bure,shirika la ndege limefufuliwa,bomba la mafuta kutoka Uganda linajengwa ambalo litareta ajira na kukuza uchumi,reli itajengwa ndani ya miaka mitatu,elimu bure nk..

By Mashibes/JF

Hivi Ndivyo Nilivyofanikiwa Kujiajiri Baada ya Kumaliza Chuo Kikuu

0
0
Kwenye kitabu kimoja nilichowahi kusoma, kuna habari ya jeshi lilokwenda vitani. Baada ya wanajeshi wote kuvuka daraja kuwaelekea maadui jemedari mkuu akaamua kuchoma moto lile daraja, magari na kila kitu ambacho kingewawezesha kukimbia ikiwa vita ingewaelemea.

 Kisha akawageukia wanajeshi wake akawaambia, "Chagueni kushinda vita ama kufa kwa sababu kukimbia ama kurudi nyuma haiwezekani tena". Jeshi lile lilishinda vita! Mbinu hii nimepata kuitumia nilipofanya rasmi maamuzi ya kujiajiri pindi nilipomaliza chuo kikuu.

 Nilijua kwenye kujiajiri kuna changamoto nyingi na kuna hatari nikakata tamaa na kutafuta ajira. Nikaamua kuchoma madaraja yote yanayoweza kunifanya nikimbie kujiajiri kwenda kuajiriwa! Kwanza kwa makusudi sikuchukua cheti cha matokeo wala cheti chochote wala barua inayothibitisha nimemaliza chuo kikuu; pili nilijiapiza kutoshughulika na matangazo, habari ama taarifa zozote kuhusu ajira. Nikabaki na option moja tu ya kuhakikisha napambana kufa na kupona kwenye kujiajiri mpaka kieleweke.

 Haikuwa kazi rahisi, lakini sikuwa na namna zaidi ya kutoka ama kufa. Nilikataa kufa na leo ninasonga mbele kwa mafanikio. Ninachokuhakikishia ni kuwa ukiamua kwa moyo mmoja kufanikiwa katika jambo lolote; ni lazima utafanikiwa, no matter what!! Kama stori nzima haijakuvutia, chukua sentensi moja ya mwisho!

 By SmartMind

UVCCM Wamtetea Rais Magufuli, Wasema Hotuba Yake Aliyoitoa Zanzibar Imezika upotoshaji wa siasa uchwara

0
0
UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umesema Rais John Magufuli, hana baya alilolitamka katika mikutano yake ya Unguja na Pemba, bali amezika upotoshaji wa siasa uchwara, kusafisha upepo mchafu na kufumba vinywa vya wanasiasa wakorofi na wazushi.

Pia umetoa mwito kwa Wazanzibari kwa nguvu zote kupinga siasa chafu au zenye lengo la kuwagawa, kuwatenganisha au kuwahasimisha badala yake watambue umuhimu wa kuendeleza umoja, amani na maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka alisema hayo ofisini kwake Makao Makuu ya CCM, Dodoma, alipotakiwa kueleza maoni yake kuhusu shutuma anazotupiwa Rais Magufuli ikidaiwa na baadhi ya wanasiasa kwamba alilenga kuamsha joto la mtafaruku wa kisiasa visiwani humo.

Shaka alisema hotuba ya Rais Dk Magufuli imezima siasa za uzushi na dhidi ya viongozi wanaowadanganya wafuasi wao kwamba utafanyika Uchaguzi Mkuu mwingine kabla ya mwaka 2020 na Rais Ali Mohamed Shein ataondoka madarakani ili kumpisha Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.

Shaka alisema hotuba ya Rais ilikuwa yenye mashiko na maudhui, makatazo, maonyo, maelezo na wosia uliojiegemeza katika kudumisha amani nchini.

“Kuhubiri amani ni dhamana yake kiutawala, kuwaonya wananchi wanaokata mikarafuu, kutoboa mitumbwi, kufyeka mazao mashambani na wengine kukataa kuwauzia bidhaa wenzao halikuwa kosa na si jambo baya kama inavyoelezwa na wazushi wa kisiasa,” alisema Shaka.

Aidha, alisema ikiwa kuna mwanasiasa asiyemtii Rais aliye madarakani Zanzibar na hata kukataa hata mkono wake, hakuna sababu kwa kiongozi huyo kutaka msaada kwenye serikali asiyoitambua.

“Iweje baniani mbaya kiatu chake dawa, unajigamba humtambui Rais aliyeshinda na kuunda serikali ila unadoea fedha zinazokusanywa na serikali usioitambua ili usaidiwe na kulipwa marupurupu. UVCCM inaunga mkono SMZ kumnyima stahili zote hadi atakaipomtambua Rais,” alisema Shaka.

Kaimu Katibu Mkuu huyo alisema wakati wa utawala wa Dk Salmin Amour Juma, Maalim Seif aliposema hamtambui kama mshindi halali hakuwa akilipwa chochote, Rais mstaafu Amani Abeid Karume hakumlipa kitu hadi alipojipeleka Ikulu Novemba 5, 2009 akatangaza kuitambua serikali yake.

Alisema matamshi ya Dk Magufuli katika hotuba zake zote, ameweka bayana kila kitu, amewakanya wanasiasa wachochezi na hatarishi kwa amani, amewaonya viongozi katika serikali zote huku akikataa uzembe, urasimu, ubadhirifu wa mali za umma na kusema wote wasiotosha, wajipime iwapo bado wanafaa au la.

Zitto Kabwe Afunguka Kuhusu Upungufu wa Mizigo Bandarini..Adai Madereva 27,600 Wamepoteza Kazi

0
0
Takribani madereva na matingo wa malori 27,600 wamepoteza Kazi tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani

TATOA (Umoja wa Wamiliki wa Magari ya Kusafirisha Mizigo Nchini) unamiliki Wastani wa Malori 23,000 Kwa sasa. 60% ya Malori Husika Kwa sasa hayafanyi kazi Kabisa Kwa Sababu ya Uhaba wa Mizigo Bandarini.

Kila gari Moja hutumia Wastani wa Lita za Mafuta 2000 kutoka Bandari ya Dar es salaam Kwenda Burundi, Zambia ama DRC. Ambapo Magari yote 23,000 hutumia Lita Milioni 46 Kwa Safari Moja katika Nchi Tatu Hizo, Na Serikali hukusanya Shilingi 650/- Katika Kila Lita Moja ya Mafuta Kama Kodi.

Kwa Msingi Huo Ukifanya Mahesabu Utaona Athari Za kushuka Kwa Mizigo Katika Bandari ya Dar zinavyosambaa Kutoka Bandarini, Kwenda TRA, Kisha Kwa TAFFA (Umoja wa Mawakala wa Mizigo Nchini), kuja kwetu TATOA, Kwenda TASAA (Umoja wa Mawakala wa Meli Nchini) mpaka Kwa ICDs (Umoja wa Wamiliki wa Bandari Kavu Nchini)".

Mtumiaji wa Facebook Mwenye Umri Mkubwa Kuliko Wote Duniani

0
0
Ms Maria Seguar Metzgar mwenye umri wa miaka 105 inasemekana ndiye mtumiaji wa facebook mwenye umri mkubwa kuliko wote duniani
Ms Maria alisherehekea miaka 105 wiki moja iliyopita huku akiwa na marafiki 86 kutoka facebook

Nafasi za Kazi CVPeople Tanzania, Sales Executive


Adakwa Akiuza Wasichana Kama Njugu

0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia Julita Lucas (30), mkazi wa kijiji cha Masinki Wilaya ya Serengeti kwa tuhuma za kufanya biashara haramu ya  kusafirisha binadamu anaowauza kuanzia Sh150,000 hadi Sh300,000.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ramadhani Ng’anzi amesema Septemba 3, saa 9.00 alasiri, Lucas alikutwa akiwa na wasichana watano (majina yamehifadhiwa) aliokuwa amewaficha nyumbani kwake kwa lengo la kuwauza na wengine kuwaozesha kwa wanaume wenye kuhitaji.

Amesema baada ya mama huyo kuhojiwa alikiri kufanya biashara ya kuuza wasichana kwa bei ya kati ya Sh 150,000 hadi 300,000, kwa kuangalia ukubwa wa umbo na siyo umri.

“Baada ya kufanya mahojiano na wasichana hao wenye umri kati ya miaka 15 hadi 28, walisema wametokea katika kijiji cha Muhejangila Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera,” amesema.

Kamanda Ng’anzi  amesema polisi wanaendelea na uchunguzi dhidi ya mama huyo, ili kubaini mtandao wa biashara hiyo haramu ya binadamu.

 “Tunaendelea kumuhoji, tunataka kujua iwapo kituo cha mwisho cha biashara hiyo ni hapa ndani tu au ni hadi nje ya nchi , biashara hiyo ilianza lini na idadi ya wasichana waliokwisha uzwa na waliuzwa wapi,”

Kamanda Ng’anzi alisema baada ya upelelezi kukamilika, mama huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.

ACT – Wazalendo Yatabiri Uchumi Kuporomoka

0
0
CHAMA cha ACT – Wazalendo kimesema katika kipindi cha miezi sita tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, uchumi wa taifa umeporomoka kwa asilimia nne.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe, akinukuu taarifa ya Benki Kuu (BOT), alisema katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba mwaka jana, pato la taifa lilikua kwa asilimia tisa. Lakini kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu, limepungua na kufikia asilimia 5.5.

Alisema kulingana na mwenendo wa uchumi, Kamati Kuu ya chama hicho imeitaka Serikali izingatie sayansi ya uchumi katika kuendesha nchi.

Zitto alisema uamuzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa kuitelekeza Serikali kwa mwanasiasa mmoja na kudhani ndiye anayejua kila kitu na kuwa mshauri wa washauri wa uchumi, itasambaratisha uwekezaji nchini na kuua kabisa juhudi za miaka 20 za kuvutia uwekezaji na kujenga uchumi shirikishi.

“Tunawahimiza wananchi kuzingatia kuwa msingi wa uchumi wetu ni uwekezaji kutoka ndani na nje ya nchi, hivyo msingi wa kuvutia uwekezaji ni utawala bora. Serikali ya CCM inapaswa kujua kuwa kuua utawala wa sheria ni kuua uwekezaji pamoja na uchumi wa nchini.

“Tangu kuingia kwa awamu ya tano, Serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi imekumbana na changamoto ya uchumi kukua bila kuwanufaisha wananchi wa kawaida, wakati tulitegemea Serikali mpya ingeanza na kukuza uchumi wa taifa.

“Hali hiyo inamaanisha kuwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi katika kipindi cha miezi sita ya mwanzo wa  awamu ya tano umepungua kwa asilimia 4,” alisema Zitto.

Zitto ambaye alikuwa akitoa msimamo wa Kamati Kuu ya chama chake iliyoketi juzi Dar es Salaam, alisema katika sekta ya kilimo ambayo hutegemewa na wananchi kwa asilimia 70, pato la uchumi limezidi kushuka kutoka kasi ya ukuaji wa asilimia 10 kwa robo ya mwisho wa mwaka jana hadi kufikia asilimia 2.7 katika kipindi cha Januari hadi Machi, mwaka huu.

“Watu wameishiwa na imani kuendelea na shughuli za ujenzi, mfano nyumba zilizokuwa zikijengwa zimeachwa kujengwa,” alisema.

Habari hii imeandaliwa na Herieth Faustine, Johanes Respichius na Pauline Kebaki (Turdaco).

Bei ya Mafuta yashuka Maradufu

0
0
MAMLAKA ya Udhibiti wa Nishati na Maji na Mafuta (Ewura), imetangaza kushuka bei ya mafuta ya aina zote kwa jumla na rejareja.

Bei hizo mpya ya mafuta zimeshuka katika mikoa yote isipokuwa Mkoa wa Tanga, hasa kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa.

Taarifa ya Ewura jana ilisema bei hizo zimeshuka ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, mwaka huu.

Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi, alisema katika toleo hilo, bei ya rejareja kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa imepungua kwa viwango tofauti.

Alisema kwa petroli imeshuka kwa Sh 65, dizeli Sh 63 na mafuta ya taa Sh 86.

“Bei ya jumla imepungua ambako kwa petroli ni Sh 65.31, dizeli Sh 63.39 na mafuta ya taa Sh 85.93,” alisema.

Ngamlagosi alisema kushuka kwa bei ya petroli katika soko la dunia na kupungua kwa gharama za usafarishaji/uletaji wa   mafuta hayo nchini, ndizo sababu kuu zilizochangia  kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la ndani nchini.

“Bei ya jumla na rejareja kwa petroli na dizeli katika Mkoa wa Tanga imeongezeka kidogo ikilinganishwa na toleo la bei za mafuta hayo lililopita la Agosti 3, 2016.

“Katika toleo hili, bei ya rejareja kwa petroli na dizeli imeongezeka kwa viwango ambavyo petroli ni Sh 50 na  dizeli Sh 19. Kwa kulinganisha na matoleo haya mawili, bei ya jumla imeongezeka.

“Petroli Sh 49.61 kwa lita sawa na asilimia 2.80 na dizeli Sh 18.57 kwa lita sawa na asilimia 1.1.

“Ongezeko hili la bei limechangiwa kwa kiasi kikubwa na kupokea mafuta mapya (petroli na dizeli) ndani ya Agosti 2016, ambayo yalitarajiwa kupokewa Julai 2016 na pia kutokupokea mafuta mapya kutoka  katika meli ya MT. Nevaska Lady ndani ya Agosti mwaka huu,” alisema Ngamlagosi.

Hata hivyo, alisema mamlaka hiyo inawakumbusha wananchi kwamba bei kikomo ya mafuta kwa eneo husika, pia inapatikana kupitia simu zao za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kufuata maelekezo.

Alisema huduma hiyo hutolewa bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi nchini.

Sallam, Meneja wa Diamond Kuja na Kituo Chake Cha Redio

0
0
Meneja wa Diamond Platnumz, Sallam anatarajia kuanzisha redio yake ya mtandaoni (online radio).

Taarifa hiyo ilitolewa na Romy Jons, anayedai atakuwa mmoja wa watangazaji wa redio hiyo itakayojulikana kama DSM FM.

Taarifa:Wenye Majina Haya Hapa Wanaitajika Mahakama Kuu ya Tanzania

0
0
Tunaomba kutoa taarifa kuwa, wenye majina na anuani hapo chini ambao ni watumishi/walikuwa watumishi wa  Mahakama ya Tanzania wanahitajika kupata taarifa muhimu na maalum juu ya masuala yahusuyo Utumishi wao: Wafike na kuonana na Bibi. Agatha Ng’ingo – Mkurugenzi Msaidizi- Idara ya Utawala na Utumishi, namba ya simu (0673 – 001 773) ndani ya siku kumi na nne (14) kuanzia tarehe ya tangazo hili.
S/N
JINA KAMILI
CHEO
KITUO CHA KAZI
C/N
1
BW. ROBERT WILLIAM CHAGAKA
DEREVA II
MAHAKAMA YA WILAYA IRAMBA
111824992
2
BW. GODLISTEN MOSES MWANRI
DEREVA II
MAHAKAMA YA WILAYA KISHAPU
111827839
3
BI. AGNES AUDAX RWEGOSHORA
HAKIMU MKAZI II
MAHAKAMA YA MWANZO UJIJI KIGOMA
111838464
4
BI. HAPPINESS ELIAS MISHWARO
HAKIMU WA MAHAKAMA YA MWANZO MWANDAMIZI
MAHAKAMA YA WILAYA MBARALI
10915901
5
BW. BARAKA JAFARI MUKAMA
MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II
MAHAKAMA YA WILAYA ILALA
9927780
6
BW. RAMADHANI MOHAMED KILYOUSUNGU
MLINZI
MAHAKAMA YA WILAYA RUFIJI
9496501
7
BI. REHEMA SAMWEL PANDAPANDA
HAKIMU MKAZI II
MAHAKAMA YA WILAYA MPWAPWA
9927919
8
BI. HAWA GODREY MKUMBO
MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II
MAHAKAMA YA WILAYA KASULU
8203232
9
BW.CHRISTINA JOHN MAYILA
MSAIDIZI WA OFISI MWANDAMIZIMAHAKAMA YA WILAYA KAHAMA
7758540
10
BW. YASSINI WAZIRI MASELE
MLINZIMAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI SINGIDA111400187
11
BW. JOSEPH FRANCIS BOMA
MLINZIMAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI SINGIDA
111397724
12
BW. BRUTON RABIEL KIMARO
MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU IIMAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI MANYARA7203497
13ABIHUDI GILLIARD MASEUMSAIDIZI WA KUMBUKUMBU IIMAHAKAMA KUU ARUSHA
5187924
14
HUSSEIN HASSAN BACHOO
AFISA UGAVI IDAR ES SALAAM
5529186
15
ASHA MAGOMBA ABDALLAHMSAIDIZI WA KUMBUKUMBU IIMAHAKAMA YA WILAYA MONDULI
111827925
16BW. AMRI MUSSA RASHIDIMLINZIMAHAKAMA YA WILA
YA TANDAHIMBA
9544435
Imetolewa na,
MTENDAJI MKUU.

Aliyetaka Kupindua Ikulu Afikishwa Mahakamani Kisutu

0
0
Aliyetaka Kupindua Ikulu Afikishwa Mahakamani Kisutu

Majina ya Watu 4 Matajiri zaidi Tanzania

0
0
Uchumi mkubwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unategemea zaidi kilimo kwa takriban asilimia 25 ya GDP na asilimia 85 Exports. Aidha, Tanzania ina madini kama dhahabu, almasi, makaa yam awe, uraniamu, chuma, shaba, Tanzanite n.k.

Tanzania imetengeneza matajiri wengi sana, na hawa ni wanne wakubwa kwa mujibu wa jarida la Forbes. Na mamilionea hawa wametudhihirishia kwamba kila kitu kinawezekana, na kila mtu ananafasi ya kuwa tajiri ili mradi tu aweke juhudi katika kazi yake na kwa makini

4) Reginald Mengi – Thamani: $560 Million

Bwana Reginald Mengi ni mmiliki wa wa moja ya kampuni kubwa inayomiliki vyombo vya habari ya IPP  Media Group, yenye magazeti 11, stesheni za redio na TV na mitandao ya intaneti.



3) Said Salim Bakhresa – Thamani: $575 Million

Umri wake ni miaka 65, nay eye alianza mwenyewe mpaka kufikia hapo. Mfanyabiashara huyu ameanzisha Azam TV, yenye mfumo wa kulipia chaneli za TV Afrika ya Mashariki. Aliacha shule akiwa na miaka 14 na kuanza kuunza Mix (Urojo) na baadae kufungua mgahawa mdogo na kisha kuhamia katika biashara ya mazao ya kilimo. Katika miongo mine iliyopita  ameongeza mauzo yake kwa dola za kimarekani milioni 750, na kuifanya Bakhresa Group kuwa moja ya kampuni kubwa Afrika ya Mashariki kwa kuwa na wafanyakazi zaidi ya 5,000 na kujikita zaidi kwenye bidhaa za vinywaji na chakula, Upakiaji wa bidhaa, huduma za feri na Mafuta ya Petroli na usafirishaji.


2) Rostam Azizi –Thamani: $1 Billion

Rostam Azizi ni tajiri wa kwanza kutokea Tanzania. Mnamo mwezi Mei mwaka 2014 aliuza hisa zake 17% alizokuwa akimiliki katika kampuni ya Vodacom. Vile vile ana miliki kampuni Caspian Mining, inayojihusisha na uchimbani wa madini kwenye kampuni kubwa kama BHP Billiton na Barrick Gold. Kampuni hiyo ya Caspian Mining pia inamiliki sehemu kubwa ya ardhi yenye uwezekano wa kuwa na madini kama dhabu, chuma na shaba hapa Tanzania. Aidha, Rostam ana hisa katika Bandari ya Dar es salaam ambapo yuko pamoja na Hutchison Whampoa na ana miliki sehemu ya ardhi kubwa hapa Tanzania, Dubai, Oman na Lebanon.



1) Mohammed Dewji – Net Worth: $1.3 Billion

Ana umri wa miaka 40, na ndio mdogo kuliko matajiri 50 wa Afrika yote kwa mfululizo wa miaka 3 sasa, ana miliki 75% ya kampuni ya METL Group, inayohusika na viwanda nchini humu iliyoanzishwa na Baba yake. Kizuri kuhusu Mohammed Dewji aliibadisha nyumba ya kufanyia manunuzi ya bidhaa za kilimo kuwa kiwanda cha uzalishaji.

Maoni ya Alberto Msando Juu ya Kauli Tata za Rais Magufuli

0
0
Sina tatizo na hatua za Raisi kuleta 'maendeleo' kwa wananchi na kutetea 'wanyonge'. ILA nina tatizo na kauli zake. Kuna jinsi ambavyo kama watanzania tumezoea kusemeshana na kuongeleshana. Sisemi kwamba tuishi kwa mazoea la hasha. Ila ni vyema mtu yeyote uangalie unasema nini na wapi kufanikiwa nini.

Mlimani City mpango wa kuijenga ulianza kipindi cha Mh. Mkapa na kumalizika kipindi cha Mh. Kikwete kama sikosei. Leo hii kusema kwamba mradi huo ni "magodown" ni kuwaonea waliokuwepo wakati unatekelezwa.

Mosi, maamuzi ya Serikali yeyote ni ya pamoja (collective responsibility). Kama mtu alikuwepo kwenye mabaraza yote ya mawaziri kipindi cha Mh. Mkapa na Mh. Kikwete kipindi ambacho magodown yamejengwa basi hawezi kuepuka ushiriki katika kudanganywa kwetu!! Pili, sijamsikia mtu akisema barabara ambazo zimebomoka (mfano maeneo ya Chalinze, barabara ya Mbeya, barabara za akachube nk) ni mitaro au mito kwa sababu zilijengwa chini ya kiwango!! Au ule mradi wa ferry kutoka Bagamoyo - Dar ni WHITE ELEPHANT. Au kukumbushia uuzaji wa nyumba za Serikali halafu kwenda kujenga nyingine!! Au kuhusu wale samaki wa wachina kwamba tuliingizwa chaka.

Tatu, uongozi ni endelevu. Zaidi pale ambapo bado ni CCM ndio kipo madarakani. Inatuchanganya wananchi tunapoambiwa tulichezewa na kudanganywa sana huko nyuma. Nyuma tunayoijua sisi ni ya NYERERE, MWINYI, MKAPA na KIKWETE. "Nyuma" ya CCM. Je ni yupi kati yao alikuwa mzembe na asiyejua kuongoza kiasi kwamba leo hii tuko hapa na magodown yetu???? Atuombe msamaha!! Kwa njia moja au nyingine ni ukweli kwamba sisi watanzania ni majuha. Tumechezewa wakati wa hao wote wala hatukujua. Leo angalau ametokea mtu kutuambia ukweli. Mzee Mkapa alikuwa sahihi kutuita malofa.

Lakini najaribu kujiamiaminisha kwamba Mh. Raisi ni mtu wa kauli za utani. Mfano, 1. Kufyatua watoto 2. Siasa mpaka 2020 3. Kuwapoteza nusu walioimba kwenye mkutano 4. Kumzamisha kisimani aliyezuia watu kuchota maji 5. Kutoa matairi kwenye magari yanayovunja sheria za barabarani 6. Polisi kutokuwa rafiki na raia 7. Kutokusaini pensheni mtu asipokupa mkono wa salamu nk nk.

Natamani sana niamini hivyo. Ni utani tu. Naomba sana iwe hivyo. #TatizoNiSisi

Alberto Msando

Msigwa 'Awatolea Uvivu' Mawaziri wa Magufuli!

0
0
Alichangia mswaada wa haki ya kupata taarifa mbunge wa Iringa mjini Mch Piter Msigwa amesema taifa limesinyaa kwa sababu mawaziri ni waoga wa kumkosoa hata kumshauri rais. " Huu mswaada mbovu ulipita kwenye baraza la mawaziri kwa sababu mnaogopa kumkosoa rais, huyu amekuwa kila kitu na kufungia kila kitu". Aliongeza "Mkileta mswaada kama huu sisi hatuogopigi kumkosoa, ukienda maabara ukaambiwa unaendesha haufungi maabara bali unatafuta tiba".


"Sasa ninyi mmekuwa waoga mpaka mnatia huruma, na rais wenu hana urafiki atawafurumua huko mje huku back bencher kukutana na sheria mbovu mlizopitisha wenyewe, hamuoni wenzenu mliokuwa nao tumekaa nao huku?" alisema. Amesema anashamshangaa Dr Mwakyembe na usomi wake kutumwa kupotosha sheria ya vyama vya siasa. Hivi wewe Mwakyembe na usomi wako kweli ile ndiyo tafsiri ya sheria ya vyama vya siasa? Kweli? "Eti kuna watu mnachangia eti mnalinganisha Tanzania na nchi za Ulaya kwa demokrasia, sisi tulinganishe na Rwanda"

Amewataka wabunge wa Ccm kuacha kuamini watatawala milele kwani hata Roma Empire ilianguka. "Hata Lowassa alikuwa huko kwenu, leo tunapigwa naye, tunafungwa naye na maji ya washa washa tunamwagiwa naye"

AUDIO: Sikiliza Bifu la Wema Sepetu na Man Fongo...Mama Wema Atoa Mapovu

0
0
Linapokuja suala la muziki mzuri hakuna mtu anaweza kutia neno akapingana na ukweli amabao wengi wameamua kuunga mkono,

 Muziki wa Singeli umekuepo kwa kipindi kirefu lakini design kama wabongo tulio wengi tumeanza kuuelewa kupitia waimbaji watu kama Man Fongo na Sholo Mwamba.
 ManFongo ni mshikaji ambae anazidi kujitengenezea Fanbase hasa kupitia shows za Fiesta ambazo zinaendelea mikoani.

 Mkali huyo wa Ngoma ya "Hainaga Ushemeji" amejikuta akiingia kwenye bifu zito na mama wa mrembo Wema Sepetu baada ya kuongea kile kilichotajwa kuwa hakimuhusu huku mpinzani wake Sholo Mwamba akitajwa kuwa chanzo cha beef hilo.

 Ubuyu uliozagaa unadai kuwa ManFongo aliongea vibaya kuhusu Mama Wema kilichopelekea Mam huyo kutokwa na povu lisilo la polepole.

 GossipCop Soudy Brown hakusita kuwatafuta wawili hao ili watuweke sawa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Septemba 8, Mbunge CCM Amshukia Magufuli

0
0


Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Septemba 8, Mbunge CCM Amshukia Magufuli

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Akagua makazi yake mapya Dodoma.

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kukagua ujenzi wa makazi mapya ya Waziri Mkuu katika eneo la Mlimwa na kuagiza umalizike kwa wakati ili aweze kuhamia kama alivyoahidi.

Katika ziara hiyo aliyoifanya jana mchana (Jumatano, Septemba 7, 2016) Waziri Mkuu alisema ameridhishwa na namna kazi ya ujenzi inavyofanyika.

“Nimekuja kukagua makazi mapya na mahali pa kufanyia kazi. Kazi ya ujenzi inaendelea vizuri, nimejionea mwenyewe na naamini katika kipindi kifupi watakuwa wamekamilisha,” alisema.

Alisema kutokamilika kwa ujenzi huo hauwezi kukwamisha azma yake ya kuhamia Dodoma kwa sababu tayari inafahamika kuwa Makao Makuu ya Ofisi ya Waziri Mkuu yako Dodoma.

Alisema uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma hautokani na shinikizo la kisiasa bali ni utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao chimbuko lake ni agizo lililotolewa Oktoba Mosi, 1973 kwenye Mkutano Mkuu wa 16 wa chama cha TANU.

“Tangu wakati huo Serikali zote ziliendelea kufanya juhudi mbalimbali za kuandaa miundombinu na hata awamu ya nne ilisimamia kwa kiwango kikubwa uwekaji wa miundombinu hiyo,” alisema.

“Pia tukumbuke kauli ya Mheshimiwa Rais aliyotoa kwenye hotuba yake ya Julai 23, 2016 alipochaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM, na akairudia tena Julai 25, kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya Mashujaa na mimi siku hiyo hiyo nikaweka msisitizo,” alisema.

Alisema uamuzi wa Serikali ya awamu ya tano wa kuhamia Dodoma unakuja baada ya kuridhishwa na ujenzi wa miundombinu na maeneo ya kutolea huduma za kijamii kwa wageni na wenyeji ikiwemo Hospitali ya Benjamini Mkapa iliyopo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yenye uwezo wa kutibu magonjwa makubwa kama ya moyo na figo.

Waziri Mkuu alisema tayari Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) ina mpango kamambe (master plan) na ina viwanja vya kutosha kujenga makazi na ofisi mbalimbali.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Viewing all 104414 articles
Browse latest View live




Latest Images