Quantcast
Channel: UDAKU SPECIAL
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live

Polisi Wamhoji Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob

$
0
0
Maofisa wa Polisi wamemhoji Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob kabla ya hajakutana na waandishi wa habari kwa madai kuwa wamepata taarifa mkutano wake huo ulilenga kumkashifu Rais John Magufuli.

Maofisa hao waliovalia kiraia walionana na Jacob ofisini kwake na walimruhusu kuendelea na mkutano huo baada ya meya huyo kuwahakikishia kwamba hana nia hiyo bali alitaka kutoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala baada ya ujio wa Rais, Kinondoni Jumanne iliyopita.

“Kwa mara ya kwanza meya anahojiwa, lakini niliwaambia wana usalama lengo langu ni nini na sipo kwa ajili ya kumkashifu Rais, ila nafahamu vita iliyopo kati yetu na baadhi ya viongozi,” alisema Jacob.

Pamoja na ufafanuzi huo, Jacob aliwataka baadhi yao (askari) kushiriki kwenye mkutano huo wa wanahabari kufuatilia alichotaka kuwaeleza wanahabari na polisi mmoja alibaki kusikiliza bila kutambulishwa.

Kamanda wa Polisi wa Kinondoni, Suzan Kaganda alisema hakukuwa na tatizo lolote polisi kuwapo eneo  hilo, kwani wanafanya shughuli zao za ulinzi na usalama wa raia na hasa ikizingatiwa kuwa kuna Ofisi ya Mkuu wa Wilaya.

Katika mkutano huo, meya Jacob alitoa ufafanuzi wa yaliyojiri Jumanne iliyopita wakati Rais Magufuli alipofanya ziara katika manispaa hiyo na kubatilisha umiliki wa eneo la Magomeni Kota lililokuwa mali ya halmashauri kuwa ya Serikali Kuu.

Meya Jacob aliwaambia wanahabari kuwa uamuzi wa Serikali kuchukua eneo hilo umeisababishia halmashauri yake hasara ya zaidi Sh4.5 bilioni kutokana na gharama walizoingia.

Katika eneo hilo, nyumba 644 zilivunjwa mwaka 2011 kwa miadi ya kwamba zikijengwa upya, wananchi waliokuwa wakiishi hapo wakiwa wapangaji wangerejeshwa, lakini mradi huo ulichelewa kuanza.

Akiwa ameambatana na baadhi ya madiwani, Jacob alisema hasara hiyo imetokana na halmashauri kutumia Sh2 bilioni kumlipa mkandarasi kwa ajili ya michoro ya eneo litakavyokuwa.

Alisema pia manispaa hiyo imetoa Sh1 bilioni kwa mkandarasi Gulf kwa ajili ya kuchora ramani ya ofisi mpya za halmashauri na kusimamia ujenzi wa mradi huo na kutumia Sh700 milioni kuwalipia kodi wapangaji hao baada ya kuwahamisha.

“Faida tuliyoipata ni kwamba wananchi tuliopanga kuwahudumia tayari Rais amewahudumia. Hatupingi maamuzi ya Serikali, lakini wananchi watambue kwamba manispaa haina chochote itakachokipata, bali kila kitu kitakuwa kinafanywa na Serikali Kuu,” alisema Jacob.

Meya alisisitiza kuwa madiwani wa Ukawa hawapingi uamuzi huo ila baadhi ya viongozi wanaomzunguka Rais hawamwambii ukweli wa mambo kuhusu mradi wa Magomeni Kota na kwamba baadhi ya watumishi wa Serikali ndiyo waliosababisha kufikia hatua hiyo.

“Siku ile ningepata nafasi hata dakika tatu, ningemweleza Rais Magufuli ukweli wa mambo wa mradi huu. Lakini kuna baadhi ya viongozi waliomzunguka waliamua kuninyima nafasi hiyo. "

Hata hivyo, Jacob alimwomba Rais Magufuli kukutana naye ili amweleze kwa undani jambo linalomuumiza kuhusiana na masuala ya ardhi yanayoikumbuka Kinondoni.

Alifafanua kwamba, Serikali iliyopita na manispaa hiyo ilishaingia mkataba na kampuni ya Blue Marine ya Romania kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa Magomeni Kota ambao ulifikia katika hatua nzuri lakini baadhi ya watumishi wa Serikali waliamua kuweka ‘kauzibe’ na kuipa sifa mbaya Kinondoni.

“Tulikuwa tunasubiri utiaji wa saini kutoka Serikali Kuu, lakini baada ya kuona Kinondoni inaongozwa na Ukawa wameamua kuleta ‘figisufigisu’ za kuukwamisha,” alisema Jacob.

Katika ziara hiyo, Rais Magufuli alielezea kusikitishwa kwake na namna tatizo la wakazi hao lilivyoshughulikiwa na kuwaahidi kuwa Serikali yake itahakikisha hawasumbuliwi.

Mambo 10 Ambayo Mwanaume Hupenda Kusikia Toka Kwa Mpenzi Wake

$
0
0
10. Kukosolewa – “I think you are wrong”

Wanaume wanaweza kujikweza sana lakini daima hawachukii kurekebishwa. Wanachojali zaidi ni jinsi gani au njia gani imetumika kuwarekebisha. Mwanaume akikosea, anataka mpenzi wake amkosea lakini kwa mapenzi, sio kwa mikwaruzano au dharau au mbele ya kadamnasi. Mrekebishe au mkemee faragha, toa maoni yako na wala usimlazimishe, itamfanya aone unajali na unataka kumjenga.

9. Kujali – “How was your day?”

Wanawake wengi hutaka wao tu ndio waulizwe kuhusu jinsi siku zao zilivyoenda kila siku, wanasahau kabisa hata wanaume nao walikua kwenye mihangaiko. Mzoeshe kumuuliza mpenzi wako siku yake ilikuwaje? utaona hata nuru ya mapenzi yenu itang’aa na mtakua marafiki, japo mwanzoni atakua hakuambii kila kitu lakini baada ya muda atazoea. Kila mtu anataka wa kumsikiliza, mtu atakayezungumza nae chochote kilichotokea ndani ya siku yake, na pengine kukuuliza ushauri.

8. Ucha Mungu – “Can we pray?”

Mwanaume, anayesali au kutosali, lazima huwa ana imani kwamba Mungu yupo. Mwanamke mcha Mungu siku zote huwa ni wazo la kila mwanaume endapo ana mpango wa kuoa. Mwanaume huwa na amani kwa kiasi fulani akiongozwa na mwanamke wake kwa upande huo wa sala.

7.  Msamaha – “I forgive you”

Vikombe kwenye sahani havikosi kugongana, vivyo hivyo na kwa wapenzi, kuumizana hisia hakuepukiki, iwe kwa makusudi au bahati mbaya, mwenzio akikosea sasa isiwe ndo adhabu, akiomba msamaha ukamwambia nimekusamehe na kweli umemsamehe, funika kurasa endeleeni na maisha. Usililete tena mezani jambo ulilosema umesamehe.

6. Sifa – “That was great sex”

Kama amefanya kazi nzuri, mwambie. Wote tunajua sio kila siku watu hufanya kiwango che Maradona au Pele, siku akiwa kwenye kiwango hicho hata yeye anajua, usisite kumpa sifa zake. Wazungu wanasema, ‘Yes, you can kiss and tell some of the times’. Na kama unaona kuna sehemu anahitaji kujisogeza, mwambie pia, tena kimahaba. Hii itawasaida nyote.

5. Upekee  – “I admire you. No other man is like you”

Ni kweli kwamba kuna wanaume ambao ni wazuri na wenye uwezo mkubwa zaidi ya huyo ulienaye, lakini kwake hujisikia vyema zaidi ukimwona yeye ni zaidi ya wote hao. Sio mbele ya macho yake tu, matendo yako na hata nyuma yake msifie kwamba yeye ndio mwanaume pekee duniani unayempenda na hakuna mwingine zaidi yake.

4. Uaminifu – “I trust you”

Mwanaume akijua anaaminika sana kwa mwanamke, na yeye hujiachia. Na kwa hili huwa anaweza kugombana na watu kabisa kwa ajili ya mwanamke wake. Japo wengine hulitumia hili kwa uchafu wao lakini wengi wao ni kitu chema kwao.

3. Mapenzi –  “Make love to me”

Ni mtazamo wa wengi kwamba mwanaume ndio siku zote awe mwanzilishi wa tendo. Lakini mwanaume kwa wakati mwingine hupenda mwanamke wake ampe vishawishi na yeye vya kumleta kwenye mood. Sio kila siku aanze yeye tu, wakati tendo ni la kuwafurahisha wote. Hata kama ni ngumu kusema kwa mwanamke, ishara kibao zipo za kumuonyesha mwenzi wako akaona ‘Leo baby anataka na yeye’.

2. Malengo -“What’s your dream?”

Mwanaume anaweza asionyeshe kama anahitaji msaada, lakini kwa kutumia njia za mapenzi, unakuta ni mwanaume tu anayehitaji uwepo  wa mwanamke anayempenda yeye. Mungu alimtengeneza mwanaume na kumpatia msaidizi kwa kumpatia mwanamke. Kuwa mwanamke mwenye msimamo na mpangilio mahiri usiotikisika, ambaye unauwezo wa kumuuliza anaenda wapi katika maisha yake, na akakukumbusha huko siko ni huku. Ndoto za mwanaume mara nyingi huendana na zile na mwenzi wake, na mwanamke huwa pale kuhakikisha ndoto za pamoja zinatimia.

1. Upendo wa dhati – “I love you”

Wanaume wengi hujiona wagumu kwenye kutamka neno ‘I love you’ kwa wanawake zao na hata akisema itakua ni mara chache chache hata kama kweli kutoka moyoni wanapenda, lakini haina maana hawataki kuambiwa na watu wanaowapenda, hii huwaaminishia nafasi yao kwenye moyo wa mwanamke.

Wilaya 43 ziko Hatarini Kukumbwa na Njaa

$
0
0
Serikali imesema kuwa nchi ina hifadhi kubwa ya chakula kutokana na mavuno ya msimu uliopita ingawa kuna wilaya 43 zenye upungufu wa chakula kutokana na mavuno yao kuwa chini hali iliyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha amesema hayo jana wakati akizindua tovuti ya wakala wa hifadhi ya chakula nchini (NFRA) mjini Dodoma.

Mhe. Ole Nasha amesema kuwa kwa sasa serikali ipo katika hatua za mwisho za kuratibu uuzaji wa chakula nje ya nchi bila kuathiri hifadhi ya chakula na kuwatoa hofu wananchi wenye wasiwasi wa kukumbwa na baa la njaa.

Naibu waziri huyo ameongeza kuwa kwa tathmini waliyoifanya imebaini kuwa nchi nyingi za ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula hivyo serikali itatengeneza mifumo mizuri ya kupeleka chakula hicho nje ya nchi.

Baada ya kuzindua tovuti hiyo ya wakala wa chakula nchini, uhifadhi wa nyaraka za serikali kwa njia ya makaratasi umepitwa na wakati lakini pia akaongeza kuwa hata wizara nyingine zimeanzisha tovuti lakini ni kama zimekufa kwa sababu haziweki taarifa za mara kwa mara.

Operesheni Dadapoa, Kakapoa Dar es Salaam Yashika Kasi

$
0
0
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema linafanya operesheni ya kuwakamata wamiliki wa nyumba za kulala wageni wanaofanya biashara kinyume cha sheria.

Taarifa iliyotolewa na Kamishna wa Kanda hiyo, Simon Sirro, ilisema wamebaini baadhi ya nyumba za kulala wageni zinatumika kuhifadhi magenge ya majambazi na wahalifu wengine.

Alisema nyumba hizo zimekuwa zikitumiwa na wanawake na wanaume wanaofanya biashara ya kuuza miili yao maarufu ‘dadapoa’ na ‘kakapoa’.

“Ni wajibu wa Polisi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye nyumba za kulala wageni, hoteli, migahawa, vilabu vya vileo, kumbi za starehe zinazokesha na zisizokesha na watakaobainika kuvunja sheria hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao,” alisema.

Katika hatua hiyo, Kamishna Sirro aliwatahadharisha wafanyabiashara wa nyumba hizo kufuata utaratibu wa kupokea wageni kwa kuandika majina yao kwenye vitabu, namba za vitambulisho vyao na sehemu wanapotoka na pale watakapomtilia shaka mteja yeyote watoe taarifa kituo chochote cha polisi.

Aidha wenyeviti wa Serikali za mitaa na wajumbe wa nyumba kumi wametakiwa kuwajibika na kuwatambua wageni wote wanaoingia kwenye himaya zao na kuwachukulia hatua stahiki  kwa lengo la kuimarisha ulinzi ndani ya jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo Kamanda huyo aliwataka wageni wanaotoka mikoani kupuuza taarifa zilizoenea katika mitandao ya kijamii kuwa polisi wanawakamata  watu wanaolala kwenye nyumba za kulala wageni mchana kwa kosa la uzembe na uzururaji.

“Taarifa hizo si za kweli na watu wanaotoka mikoani nawaomba waendelee na shughuli zao kama kawaida na wapuuzie taarifa hizo, “alisema Kamishna Sirro.

Alikiba Aelezea ‘King Kiba’ ilikotokea, Adai si Mtu wa Maringo

$
0
0
Alikiba ametoa ufafanuzi wa wapi #KingKiba ilitokea kiasi cha kuitumia katika sehemu nyingi.

Akiongea kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz kilichoruka Alhamis hii kupitia EATV, Kiba alisema ni mashabiki ndio waliombatiza.

“Wakati nimepumzika kwenye muziki kulikuwa kuna vitu vingi vinavyoendelea, kuna watu walikuwa wanaongea kwenye social media. Kuna watu walikuwa wananifikia sababu wanapajua nyumbani wakasema ‘au tuanzishe kampeni’ wakaanzisha mimi najua masihara,” alisema.

“Kiukweli walichokuwa wanacomplain, kwanini Ali hutoi nyimbo, uko wapi, kuna watu wakaanzisha Bring Back Our Alikiba. Ndio ikaanzia pale watu wakaanza kuniita King Kiba kwasababu hata kwenye show pale wakawa wananiita hivyo,” aliongeza.

“Nikaona sawa haina shida, kila kitu ikawa hashtag #KingKiba, lakini sikufikiria kujiita hivyo.”

Kwa upande mwingine muimbaji huyo wa Aje alisema kuwa kutomfollow mtu yeyote Instagram haimaanishi kuwa anaringa.“Nimeacha kufollow watu [Instagram] nikiwa na watu 50k,” alieleza.

“Nilikuwa nataka nione, nimekuja kwenye muziki, je nina fans wangapi watanifollow mimi nikiwa kama AliKiba na kuangalia kazi zangu. Nilikuwa nasikia watu wanasema naringa na nini, lakini nilisema kwamba nitawafollow watu baadaye.”

VIDEO: Mama Wema Aeleza Beef yake na Man Fongo Kisa……..

$
0
0
NI Mama Wema Sepetu ambae ameingia kwenye headlines mitandaoni baada ya kutofautiana na mkali wa nyimbo za singeli, Man Fongo.

Sasa hapa tumefanikiwa kuipata video ikionesha Mama Wema akieleza tofauti yake na msanii huyo na kusema..

Kwanza kama utakuwa umesoma SMS yangu niliyomtumia nilimwambia kwamba Amani nakuheshimu sana hasa baba yako ambae mpaka sasa namuheshimu ila matusi ambayo umeanza kunitukana huko ulipo nimeyapata sasa endelea’

Sasa mimi ndio wakumshtaki maana amenisema vibaya huko walipokuwa na watu wake ziarani nimeumia sana mimi kama mzazi, Manfongo bado  mtoto mdogo sana kwangu na mimi’-

‘Kwa upande wa Man Fongo alisema…‘Wamemtumia meseji mama yake na Wema kwamba ninaisema familia yake wakati mimi Manfongo muhuni na muhuni siku zote hatuna muda wa kumzungumzia mtu, riziki yangu naisaka tangu nipo kitaani sina muda wa kujibishana na watu sasa Mama Wema ananitumia meseji za matusi’

Unaweza ukabonyeza play kuitazama hii video Mama Wema Sepetu akieleza tofauti yake na Man Fongo

Mama Rwakatare awatoa wafungwa 12 gereza la Keko

$
0
0
Mchungaji wa kanisa la Mikocheni B Assemblies of God, Askofu Dr Getrude Rwakatare, amewatoa wafungwa 12 waliokuwa wamefungwa kwenye gereza la Keko jijini Dar es Salaam huku lengo ni kuwatoa wafungwa 78 waliofungwa kwa kukosa kulipa faini.

Akizungumza na wanahabari, Askofu Rwakatare alisema kuwa amewatoa wafungwa wanaodaiwa kiasi kidogo cha fedha na wenye makosa madogo ili waweze kurejea uraiani na kujenga taifa kwani kuendelea kuishi huko wanapoteza nguvu kazi ya kesho.

“Nipo gereza la Keko ambapo nina furaha kuwatoa wafungwa ambao wamefungwa mahali hapa kwasababu mbalimbali. Wengine wameshindwa faini ya shilingi elfu 40, wengine wameshindwa faini ya shilingi elfu 50 na wengine kukosa faini za laki moja,” alisema. “Mimi nimeguswa kama mtumishi wa Mungu na mchungaji wa mlima wa moto nikasema hapana haiwezekani wacha kile ambacho tunaweza kukifanya tukifanye kwahiyo katika gereza hili tunawatoa wafungwa 12 na tumewalipia na wamewekwa huru, mnarudi uraiani na mimi nimewaambia kwamba wawe raia wema, gerezani sio hoteli,” aliongeza.


“Wanaporudi wawe wananchi bora, mimi siwajui wengine wanatoka Mkuranga, wengine Kisarawe, wengine Temeke, wengine Ilala, kama vile tunavyoenda mahospitalini pia tuelekeze nguvu zetu magerezani kweli watu ni wahalifu lakini wanahitaji dawa vitu vidogo vidogo kama hivi watoto wadogo wapo pale wanahitaji dawa hata ya kikohozi. Tuje tusaidie sio mbaya. Unamtumikia Mungu na pia nawaasa ndugu, jamaa na ninyi wake mliorudishiwa waume zenu jamani watunzeni, watunzeni waangalieni na muwaonye,wazee kaeni na vijana waonyeni waache mambo mabaya,kwasababu wengine kweli wana makosa na wengine hawana makosa,wale wenye makosa waache uovu,hawatarudi tena mahali hapa, alisisitiza.

Baada ya Keke, Mama Rwakatare ataelekea katika gereza la Ukonga kwa ajili ya kuendelea na shughuli hiyo na amesema jumla ya kuwatoa wafungwa hao ni shilingi milioni 25 na kwamba ameguswa yeye kama mtumishi wa Mungu na kuwataka wanaotoka wawe wananchi bora na wakarudishe nguvu kazi zao nyumbani.

“Tunasema turudishe nguvu kazi inayoliliwa nyumbani wakakae na wake zao na watoto wao kwahiyo wakirudi watazalisha watafanya mambo yao, hatutetei maovu, kurudisha pia kupunguza mlolongo wa wafungwa magerezani.”

Hamisa Mobetto Hana Tatizo na Uhusiano wa Majay na Lulu, Soma Ujumbe Aliowaandikia

$
0
0
Hakuna tena bifu kati ya Lulu na Hamisa Mobetto – angalau kwa kile Hamisa amekiandika kumpongeza mzazi mwenzake.

Hamisa amezaa na CEO huyo wa EFM mwenye uhusiano na Elizabeth Michael ‘Lulu’ na kuna wakati warembo hao walidaiwa kurushiana vijembe.

Majay anasherehekea siku yake ya kuzaliwa na Hamisa amepost picha ya DJ huyo mkongwe akiwa na Lulu na kuandika:

Happiest birthday To BaBa Squad (Baba caesar, Baba Fantasy& Baba G ..akija in Shaa Allah). Thank You for being baba bora wa mtoto wangu that am sure any woman could ask for katika hii dunia .
Thank You for taking good care of me & wanetu Katika Siku yako hii i wanna wish you all the best kwa hii dunia M/Mungu akufungulie milango yote yenye kheri na Baraka teley.. in shaa Allah ………… Happy birthday best friend Happy birthday mchizi wangu Happy birthday baba Watoto❣ @majizzo


Majay Birthday: Lulu Amwambia Majay ‘I think Sisi ni Perfect Combo’

$
0
0
Leo ni siku ya kuzaliwa ya CEO wa EFM, Majay, ambapo wadau mbalimbali pamoja na watu wake wa karibu wanamtakia heri ya mafanikio katika maisha yake.

Elizabeth Michael ‘Lulu’ ambaye anadaiwa kuwa kwenye mahusiano na bosi huyo, amekuwa ni mmoja kati wa watu waliomtumia ujumbe wa heri ya mafanikio huku ujumbe wake ukionyesha ukaribu wa kimahusiano zaidi.

“Juhudi zako, uchapakazi na ukarimu ni vitu vichache tu kati ya vingi ninavyojivunia na nakujifunza kutoka kwako, I think sisi ni perfect Combo,” aliandika Lulu instagram.

Aliongeza, “Nikiwa mkubwa nataka kuwa kama wewe bosi wangu (I mean kuwa CEO na vitu kama hivyo) Juhudi zako tunaziona, tuko nyuma yako na tunakuombea mafanikio zaidi na zaidi. Yesu Wangu akutunze kwa ajili yangu na familia yetu kwa ujumla. Happy birthday baba G, My successful,”

Tetesi za mahusiano ya Majay na Lulu zilishika kasi zaidi baada ya wawili hao kuongozana kwenda Nigeria katika utoaji wa Tuzo ya Africa Magic Viewers Choice (MVCA) 2016.

Nilikunywa Pombe Kutoa Aibu Kwenye Video ya ‘Natafuta kiki’-Shilole

$
0
0
Msanii wa muziki wa bongo fleva Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kusema ilikuwa ni jambo gumu kwake kufanya video ya ‘Natafuta kiki’ ya msanii Raymond.

Msanii Raymond akiwa na Shilole wakati wa utengenezaji wa video ya ‘Natafuta kiki’
Amesema ugumu huo ni kutokana na ukweli kwamba ‘scene’ ambazo alipaswa kucheza zilikuwa ngumu kwake jambo ambalo lilimfanya atumie kwanza kilevi kuondoa aibu.
Shilole alisema hayo kupitia kipindi cha eNewz kinachorushwa na EATV na kudai alikuwa anashindwa kufanya mambo kwenye video hiyo kutokana na vile anavyomuheshimu Raymond kama mdogo wake.

“Mimi niliweka upendo na kuona nimsaidie mdogo wangu Raymond katika kazi yake ili iweze kutazamwa na watu wengi zaidi, ila kiukweli ilikuwa ni kazi mbaya sana kwangu na ngumu lakini nikaona maji nishayavulia nguo hivyo sina budi kuyaoga, nikamwambia Raymond wewe ni mdogo wangu sasa naanzaje kufanya haya mambo? Ilikuwa ni ngumu ikanibidi ninywe pombe kidogo ili niweze kuchangamka, kwani watu walikuwepo wengi nikawa naona aibu. Akaniambia hamna usijali hii kazi tu nisaidie tu, ikabidi nivae ile night dress na kuingia kazini” alisema Shilole.

Mbali na hilo Shilole alisema kuwa amekuwa akitumika kwenye baadhi ya video mbalimbali kutokana na wasanii hao kumuomba ashiriki kwenye video zao ili kuwasaidia video zao kuangaliwa na watu wengi zaidi.

“Nilifanya video ya Man Fongo haina ushemeji, video ya Darasa ‘Too much’ hii ya Raymond ‘Natafuta kiki’ na ile ya Dully Skyes na Harmonize ‘Inde’ wao wamekuwa wakiniomba na kusema uwepo wangu kwenye video zao unaleta ‘impact’ kwa watu kwani watu wanakuwa wanazitazama sana video zao hivyo mimi naamua kuwapa ‘support’.

Sijamuimba Siwema wa Nay wa Mitego – Dogo Janja

$
0
0
Msanii Dogo Janja ameachia ngoma mpya inayokwenda kwa jina la ‘Kidebe’ na kuwa gumzo mtaani kutokana na kuwasifia baadhi ya wasanii huku wengine akiwaponda, ambapo ndani yake amemtaja mtu anayeitwa ‘Siwema’.

Dogo janja ametoa ngoma hiyo wakati wimbo wake wa ‘My Life’ ukiwa badi ni miongoni mwa ngoma ambazo mashabiki wengi wanazikubali huku wengi wao awali wakidhani kuwa asingeweza kufanya wimbo mwingine zaidi ya huo,

eNewz ilitaka kufahamu kuhusiana na chanzo cha Dogo janja kumsema Siwema ambaye anajulikana alikuwa ni mpenzi wa rapa Nay Wa Mitego na kubahatika kuzaa naye mototo mmoja kwa kusema “Siyo kiburi siyo mchafu kama Siwema” katika ngoma hiyo.

Dogo Janja aliamua kujitetea kuwa Siwema aliyemtaja katika ngoma hiyo siyo Siwema wa Nay wa Mitego bali ni msichana mwingine kutoka Arusha mtaa wa Ngarenaro.

Pia alifafanua zaidi kuwa wapo wengi wanaoitwa Dogo Janja lakini sio Dogo janja yeye.

“Mimi sijamzungumzia Siwema wa Nay wa Mitego, Siwema pale mtaani kwetu Ngarenaro kuna mwanamke anaitwa Siwema anatabia za kimiyeyusho yaani siyo mchoyo watu wengi wanapaa sana” Alisema Dogo Janja kufafanua mstari wake.

eatv.tv

Zari Awaponda Wanawake Nyaku Nyaku...Atupa Jiwe Gizani na Kujibiwa Hivi

$
0
0

Zari Hassan amechukizwa na wanawake wanaopenda kunyakua nyakuwa wanaume wa wenzio na hapa ameamua kutupa jiwe gizani....



Mwimbaji Linah Amnyakuwa Idriss Sultan Kutoka Kwa Wema Sepetu...Yadaiwa Amelipiza Kisasi

$
0
0
Kipindi cha Nyuma Linah sanga aliingia Bifu zito baada ya Kuibiwa Bwana na Wema Sepetu ambapo alilalamika sana kwenye vyombo vya habari hasa Radioni... Hivi karibuni Linah na Mpenzi wa Wema Sepetu Idriss Sultan wanaonekana kuwa na ukaribu usio wa kawaida kiasa kwamba inasemekati eti ni wapenzi wanapika na kupakuwa kitendo ambacho kinaonyesha ni kama kulipa kisasi kwa Wema....!! Haya Tuache Movie liendeleeee tutawajuza zaidi kinachoendelea.......



Mtangazaji wa Clouds Tv ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Wilaya

$
0
0
Hii sio mara ya kwanza kwa Rais Magufuli kuteua watangazaji kushika nyadhifa mbalimbali kwani alimteua aliyekuwa Mtangazaji wa ITV, Godwin Gondwe kuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni.

Leo Septemba 10, Rais Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya 11, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji 1 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa 1 ili kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika Halmashauri hizo.

Miongoni mwa Wakurugenzi wa Halmashauri walioteuliwa, yumo pia mtangazaji wa kipindi cha Clouds 360 cha Clouds Tv kinachorushwa kila siku kuanzia jumatatu hadi Ijumaa.

Hudson Stanley Kamoga ameteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mkoani Manyara.

Mambo 10 Usiyoyafahamu Kuhusu Watu Wanaotumia Mkono wa Kushoto

$
0
0
Kila tarehe 13 mwezi Agosti ya kila mwaka ni siku ya watu wanaotumia mkono wa kushoto. Watu wanaoandika na kufanya vitu vingine kwa kutumia mkono wa kushoto si wengi sana dunia. Hivi hapa ni baadhi ya vitu ambavyo huenda huvifahamu kuhusu watu wanaotumia mkono wa kushoto kwenye shughuli zao.

1.) Takribani asilimia 10 ya watu wote duniani hutumia mkono wa kushoto, na idadi hii imebaki hapo hapo kwa miaka mingi sana. Wanaume ndio wengi hutumia mkono wa kushoto.

2.) Kihistoria, watu wanaotumia mkono wa kushoto huchukuliwa kama ni wanyonge ambapo baadhi ya maeneo kutumia mkono wa kushoto kunahusishwa na imani za kishirikina.

3.) Kumsalimia mtu kwa kutumia mkono wa kushoto ni ishara ya kukosa maadili. Hii ilitokana na kipindi cha miaka mingi ya nyuma watu walianza kutumia mkono wa kushoto kutawaza wanapokwenda chooni.

4.) Pete ya ndoa ambayo  huvaliwa katika kidole cha tatu cha mkono wa kushoto, ilianza kuvaliwa Ugiriki na Roma ili kujikinga na mabaya yaliyokuwa yakihusishwa na mkono matumizi ya kushoto.

5.) Bingwa wa mchezo wa Tenesi, Rafael Nadal alijibadilisha na kuanza kutumia mkono wa kushoto, na kuna imani kuwa kocha wake aliamini ingemsaidia akienda mahakamani.

6.) Neno ‘mrengo wa kushoto’ lilivumbuliwa miaka ya 1790 wakati mwakilishi wa kijamaa katika bunge la Ufaransa alipokaa upande wa kushoto.

7.) Wakristo wanahusisha upande wa kushoto na upande wenye mambo mabaya kama wanavyosema siku ya mwisho wanaokwenda jehanamu watakaa mkono wa kushoto.

8.) Katika filamu ya  The Simpsons, Ned Flander alitengeneza duka lililokuwa likiuza vifaa vya watu wanaotumia mkoa wa kushoto pekee.

9.) Katika mchezo wa masumbwi au kikapu, watu wanaoutumiwa mkono wa kushoto hufahamika kama ‘Southpaws’ likimaanisha mtu anayetumia mkono wa kushoto.

10.) Kati ya marais 7 wa mwisho wa Marekani, 5 wanatumia mkono wa kushoto Gerald Ford, Ronald Reagan, George H.W. Bush, Bill Clinton, na Barack Obama.

MREMBO Lulu Michael Amwagia Mabusu Hadharani Majay

$
0
0
CEO wa EFM, Majay amepokea mabusu yakutosha kutoka kwa mpenzi wake Elizabeth Micheal ‘Lulu’ katika tafrija ya sherehe ya siku yake ya kuzaliwa. Malkia huyo wa filamu Ijumaa hii alimwandikia ujumbe mzuri wa kumtakia heri ya mafanikio huku ndani kukiwa na ujumbe ‘I think sisi ni perfect combo’. Video:

Ruby amjibu Diva baada ya kudai kuwa hamfahamu

$
0
0
Muimbaji wa ‘Na Yule’ Ruby amefunguka baada ya mtangazaji wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Diva kudai kuwa hamfahamu msanii huyo.


Ruby ameiambia Bongo5 kuwa kauli aliyoitoa mtangazaji huyo anaiona ni kama utoto. “Naona ni ujinga, I don’t want to talk about it, naona ni utoto sidhani kama ninaweza kuliongelea hilo.”

“Everybody knows me, so nahisi huo ni utoto tu labda wa kukosa majibu kwenye maswali ya interview aliyohojiwa. I don’t to talk about her,” ameongeza.

Pia Ruby amedai kuwa licha ya kuzinguana na uongozi wa THT, bado mambo yanaenda mswano.

“Kutokuwa na mawasiliano mazuri na uongozi wangu wa zamani sijaathirika kwakweli, sitaki kuliongelea hilo kwa sababu mimi naona kwangu ni kitu ambacho kimeshapita nataka niongelee vitu ambavyo vinaendelea mbele. Sidhani kama nina tofauti na wao mimi sijui ila, I don’t talk about them, at all.”

Inawezekana Diva alitoa kauli hiyo kutokana na Ruby kutokuwa na mawasiliano mazuri na Clouds Media baada ya kushindwa kuhudhuria kwenye tamasha la Fiesta lililofanyika Mwanza, August 20 ya mwaka huu.

Zari Hassan na Huddah Katika Bifu la Kumgombania Diamond Baada ya Zari Kutupa Jiwe Gizani Kwa Manyaku Nyaku

$
0
0

Baada ya Zari Hassan kupost Kwenye Page yake ujumbe tata ambao unawagusa wanawake wanao nyakua nyakua waume za watu kwa siri siri , Ujumbe huo inaonekana umewagusu baadhi ya wadada wa mjini na kuhisi moja kwa moja kuwa wanasemwa wao...Mmoja wapo aliyepatwa na dogo la zari ni Mrembo Huddah Monroe Kutoka Kenya Ambae ameamua kujibu kwa Kuandika haya hapa Chini:

Huddahthebosschick
Kuna mtu anatafuta Kiki Kwa Nguvu na Kwangu hapati ngo' huna jipya😂' ...... I'm busy Building my HUDDAH BUSINESS EMPIRE ... I don't fight with people the age of my mom on social media . I'm better than that and I don't want to end up a broke cougar dating young boys for money and fame! Stop letting your mid-life crisis out in the public, unajiaibisha. .... Act your AGE grandma! #MistressOfAllTrades



Wakenya Wasimama Kidete Kumtetea Huddah Baada ya Kuingia Kwenye Bifu na Zari, Wema Sepetu Atajwa

$
0
0
Wakenya wamekuja juu baada ya Dongo la Zari Kumpata Huddah Kuwa ni Nyaku Nyaku, Inasemekana Diamond yupo nchini Kenya ambapo ameenda kupiga Show Mombasa, sasa wadaku wa Kenya wanasema hiyo ndio sababu Zari Huko alipo hapakaliki kwani anahisi Mrembo Huddah atachukua nafasi hiyo Kumnyakuwa Diamond.....

Hivi Ndiyo Wasemevyo Wakenya Wakimtetea Mtu wao Huddah Monroe na kuwaponda Wabongo ambae huwa kazi yao Kuponda tu wakimtaja na Wema Sepetu kuwa Wabongo Wamegive Up Kwake:


LOWASSA Azungumzia Uzee Wake..Adai si Dhambi

$
0
0
"Uzee si tatizo, uzee si dhambi, uzee ni kitu kinachokuja wakati fulani muda ukifika, mzee anaweza kusaidia jamii katika mambo mengi." - Edward Lowassa

Toa maoni yako
Viewing all 104785 articles
Browse latest View live




Latest Images